Search This Blog

Wednesday, November 2, 2022

NI SHIIDA! - 5

 





    Chombezo : Ni Shiida!

    Sehemu Ya Tano (5)





    ?Baba Juliana? Haiwezekani hata kidogo kuuvunja mlango, haiwezekani?



    Mama Juliana alishindwa kumdhibiti baba Latifa. Akaamua aache baba Latifa auvunje kisha wakaingia ndani na kufikia sebuleni moja kwa moja huku wakimsubiri Juliana.

    ***

    ?Sweet! Sweet! Embu amka!? alisikika Bitungu akimwamsha Juliana. Juliana ambaye usingizi ulikuwa umemchukua baada ya kupigishwa gwaride la kufa mtu.

    ?Hee! Kwani saa ngapi sasa hivi??



    ?Saa tatu kasoro usiku, ujue tumepitiwa na usingizi halafu mlio nilioutegesha kwenye simu kumbe nilikosea kurekebisha muda!?

    ?Unasemaje Bitu!?

    ?Simu sweet!?



    ?Simu eeh! Umenifanyia makusudi Bitungu mpenzi wangu, ona sasa na funguo za nyumbani ninazo, mama hawezi kunielewa!??Funguo! Ina maana umeondoka na funguo za nyumbani kwenu? Lakini si atakuwa nazo nyingine!?

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ?Wee humjui tu mama yangu, siku moja utamuona! Mama aliniachia nyumba na miye nikajifanya mbishi kwa ajili ya mapenzi yako, nikafunga na kuja na ufunguo, hizo hapo kwenye kimkoba changu.?



    Juliana aliongea kimtego huku Bitungu asijue mama yupi anayezungumziwa. Aliinama chini kisha akakiinua kichwa na kuangaza kwenye kile kimkoba na kuanza kuuangalia ufunguo wa nyumbani kwao. Akahamia kwenye simu ambapo aliichukua na kukutana na missed call zaidi ya nne zote zikiwa zimetoka kwa mama yake.



    ?Nimekwisha mimi, nimekwisha leo!?

    ?Umekwisha kwa kipi???Ona sasa! Kumbe alikuwa akinitafuta kwenye simu!?

    ?Fanya basi uvae, uende fasta!?



    Juliana hakutaka cha kusikiliza tena, hata kuingia bafuni kujimwagia maji aliona ni kazi kubwa zaidi ya kuchukua nguo zake na kuvaa haraka-haraka, akaitumbukiza ile simu kwenye kimkoba chake kisha akatoka nduki bila hata ya kumuaga Bitungu vizuri.



    Mpaka inafika saa nne na nusu Juliana alikuwa nje ya nyumba yao. Taa zote za ndani zilikuwa zimewashwa na hakuelewa vizuri imekuwaje wakati funguo anazo.

    ?Au mama alikumbuka kuchukua funguo zake??



    Alijiongelesha Juliana huku akipiga hatua mdogomdogo kuelekea mlango wa mbele. Akiwa katika mwendo wa kunyata, wazo likamjia. Wazo la kuelekea dirishani kwa wazazi wake na kusikilizia kujua kinachoendelea. Alipofika kimya kilikuwa kimetanda na wala taa hazikuwa zimewashwa hivyo akabadili wazo na kuelekea sebuleni moja kwa moja. Kabla hajafika kwa mbali akasikia sauti za wazazi wake wakiteta!http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ?Hadi sasa, hakuna cha huyo Juliana wako wala nani? Kwa hiyo mlitaka kunilaza nje hadi sasa hivi, kama nisingepata wazo la kumchukua baba Latifa avunje ingekuwaje??

    ?Baba Juliana jamani si yameshakwisha!?



    ?Hayawezi kuisha hadi nijue Juliana yupo wapi hadi sasa hivi? Na utakuwa unajua hutaki kuniambia tu!?

    ?Najua chochote nitakachokwambia bado utaniona muongo tu, subiri labda akija!?



    Juliana alizidi kuogopa. Alitamani arudi zake Bagamoyo akajichimbie na Bitungu waliendeleze gwaride kuliko kuingia ndani ambapo aliona kumeshachafuka. Akili yake ilizidi kuchemka huku mkono wake mmoja ukiwa umekishikilia kitasa cha mlango tayari kwa kukifungua.



    ?Juliana?? aliita baba Juliana kwa hasira baada ya kuhisi kitasa cha mlango kimetikisika.

    Je baba Juliana atamfanyaje Juliana?

    Juliana atasema ukweli alipokuwa?





    Juliana alisita kufungua kile kitasa, akabaki ameduwaa huku mkono akiurudisha.

    "Nani unayefungua mlango kama siyo Juliana?" alisikika baba Juliana.

    "Mh! Baba Juliana?, hata mlango haujafunguliwa unafikiria Juliana tu!"

    "Ndiyo! Sa we' unafikiri atakuwa nani?"



    "Sidhani kama atakuwa Juliana, embu ngoja nikafungue."

    Mama Juliana aliinuka na kusogea hadi mlangoni kisha akafungua ule mlango na kukutana uso kwa uso na Juliana. Juliana aliyeonyesha kutetemeka asijue la kufanya.

    "Haya ulikuwa wapi?"

    "Mama nil..."



    Kabla Juliana hajaanza kujitetea, baba Juliana naye aliinuka kwenye kochi na kuwafuata pale mlangoni.

    "Pumbavu wee ingia ndani mwenyewe!"

    "Baba ndiyo naingia lakini...."

    "Lakini nini? Nimesema ingia..."



    Juliana aliingia huku wazazi wake wakiwa nyuma yake. Aliongoza moja kwa moja hadi kwenye kochi kisha akaketi huku akishikashika vidole vyake vya mikononi.

    "Niambie ulikuwa wapi na kwa nini uliondoka na funguo?" alianza kuhoji mama Juliana kwa ukali.

    "Mama niliondoka na marafiki zangu walikuja kun..."

    "Kimya! Ishia hapo hapo! Na ufunguo ukauacha wapi?"

    "Nilijua nitawahi kurudi."



    Juliana akiwa katika kujitetea. Yale majibu yalimkera sana baba yake. Alichokifanya aliongoza chumbani kwake moja kwa moja na kurudi akiwa na mkanda wa suruali kisha akataka kumvaa Juliana.

    "Nipishe mama Juliana! Nipishe nimuadhibu mpumbavu huyu."



    Roho ya huruma ilianza kumuingia mama Juliana. Akajikuta amemkumbatia Juliana ili aepukane na kipigo cha mkanda kutoka kwa baba yake. Akiwa bado katika kumkumbatia mama Juliana akahisi kitu puani mwake. Harufu kali ya ‘pafyumu' kutoka kwa Juliana ikamuingia puani, akamwachia Juliana kwa hasira.



    "Muadhibu, mpige tu pumbavu huyu!"

    Baba Juliana alimvaa Juliana na kuanza kumpiga mfululizo. Juliana alijitahidi kujifunika kwa mkoba wake lakini kichapo kilikuwa kikimuingia vilivyo.

    "Baba nisamehe, sitorudia tena! Nisamehe!"



    Baada ya kumpiga kwa muda, baba Juliana aliutupa ule mkanda pembeni.

    "Haya nenda chumbani huko."



    Muda wote mama Juliana alikuwa amepigwa na butwaa. Kuanzia Juliana anapigwa hadi anamaliza kupigwa bado alikuwa hajielewielewi, ile harufu ya pafyumu aliyoisikia kwa Juliana ilimpagawisha.

    "Ina maana alikuwa kwa Bitu wangu?" aliwaza na kuwazua lakini bado hakupata jibu.

    "Bitu kumbe msaliti kwangu? Kujitoa kote kule mpaka Bagamoyo ananisaliti bado?" Akili ya mama Juliana bado ilikuwa haipo sawa.



    "Na wewe vipi?" alihoji baba Juliana baada ya kumuona mama Juliana amezubaa mwenyewe.

    "Hapana mume wangu, namfikiria huyu mtoto kwa jinsi alivyobadilika, yaani Juliana wa kutujia usiku namna hii?"

    "Wee si ndo uliyemdekeza, na huu ni mchezo wenu wa kurudi muda huu wala hakuna cha kujitetea hapo."

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Hapana mume wangu."

    "Na huyo mtoto ana bahati naumwa la sivyo ningemuua leo."

    Baba Juliana bado alikuwa katika hasira. Aliondoka pale sebuleni na kuelekea chumbani kwake huku akimuacha mama Juliana peke yake pale sebuleni.

    Alichokifanya mama Juliana ni kukaa kwa muda kwenye kochi kisha akaichukua simu yake na kuanza kutuma meseji kwa Bitungu.



    "Mambo baby wangu! Nilifika salama, nakuwaza sana hadi nakosa raha!"

    Akaituma na baada ya muda, Bitungu akaijibu.



    "Hata mimi Sweet wangu, siwezi kuisahau mechi ya leo. Si unakumbuka hata uwanja tuliochezea, yaani hapa nimejilaza hoi sijiwezi natamani ungekuwepo ungenikandakanda kwa maji ya vuguvugu."

    Mama Juliana aliisoma meseji hiyo na kuiangalia mara mbilimbili kwa hasira za juu. Akajiongeza kuwa huenda Bitungu amechoka zaidi kwa kukutana na Juliana japokuwa hakuwa na hakika zaidi ya kuifananisha harufu ya pafyumu. Akamwandikia tena Bitungu meseji.



    "Baby wangu hivi ile pafyumu yako inaitwaje tena? Maana nimeipenda harufu yake nataka kesho nikainunue ili nikiwa naitumia niwe nakukumbuka."

    Mama Juliana alikuwa mjanja wa maneno, aliweza kuyaungaunga na kumdanganya Bitungu. Akaingia kwenye mstari na kumjibu.



    "Waaaaooh! Sweet wangu, ina maana leo hii umeisahau? ile inaitwa UDV."

    Meseji ikamfikia mama Juliana. Ikamuuma sana baada ya kujua ni UDV ambayo harufu yake ni ile aliyoisikia kwa Juliana. Alichotaka kujua ni kupata uhakika wa jina la pafyumu. Aliondoka pale sebuleni na kuongoza moja kwa moja hadi chumbani kwa Juliana. Akamkuta amejitupa kitandani huku akiendelea kulia kwa uchungu.



    "Wee Juliana? Embu acha uchuro wako hapa!"

    Aliongea mama Juliana huku akifuata mkoba ule wa Juliana na kuanza kupekua ndani yake. Jicho lake likagongana na kichupa cha pafyumu. Pafyumu iliyokuwa ikimuumiza kichwa. Pafyumu ya UDV.

    "Wee Juliana! Juliana?"





    Aliita mama Juliana kwa ukali.

    Ndiyo kwanza Juliana aligeukia upande wa pili huku akiendelea kulia kwa maumivu, maumivu yale ya kipigo kutoka kwa baba yake. Ilibidi Mama Juliana atumie nguvu za mikono na kumvuta kwa nguvu.

    ?Mama niacheee!!?



    ?Si nakuita we mwanaizaya! Kumbe ulikuwa ukinisikia hutaki kuitikia, si ndiyo??

    ?Hapana mama, sijiskii vizuri mwili wote unaniuma!?

    ?Hata kama unakuuma, ujue Juliana!?



    Mama Juliana akapunguza sauti na kuifanya isikike kwa chini ili mumewe asije akasikia kinachoendelea. Lengo lake ni kumuweka Juliana kwenye kumi na nane ajibu kila kitu kuhusiana na ile pafyumu aliyoitoa kwenye mkoba wake. Pafyumu ya UDV.

    ?Nakusikia mama!?



    Juliana alijiweka vizuri. Hakuwa amebadili nguo tangu ametoka Bagamoyo alipokuwa na Bitungu. Alishusha miguu yake kwenye kitanda kisha akakaa.

    ?Nakusikia mama.?



    ?Mwanangu hivi kwa nini unapenda kufanya kitu kwa makusudi? Si nilikwambia usitoke??

    ?Ndiyo mama ila walikuja marafiki za...?

    ?Hivi mara ngapi haohao marafiki zako wanakupotosha we bado unafuatana nao. Kwa nini wewe usiwapotoshe mpaka wao ndiyo wakufanyie hivyo. Halafu mwanangu mpendwa unajua kabisa baba yako ana hasira.

    ?Najua mama.?



    ?Kama unajua kwa nini sasa mwanangu unakosea!?

    ?Nisamehe mama!?

    ?Mimi nilishakusamehe hata kabla baba yako hajakuchapa na mkanda. Ila mwanangu naomba uniambie mimi kama mama yako.?

    ?Nakusikia mama.?

    ?Una mpenzi??



    Juliana alionyesha kushtuka. Alisogea kwenye kile kitanda. Woga ulimshika kwa muda huku macho akiyatoa.

    ?Hapana mama, bado najitunza!?

    ?Kweli unajitunza mwanangu Juliana??



    ?Ndiyo mama wala usiwe na wasiwasi na mimi!?

    ?Sasa mwanangu usiku wote huu tangu mchana ulikuwa wapi??

    ?Marafiki mama...?



    ?Haya hilo tuliache, mwanangu hii pafyumu nani aliyekununulia??

    Juliana alishtuka kwa mara ya pili. Aliona sasa huenda mama yake alimuona kipindi kile Bagamoyo akiwa katika kupanda bajaji katika ile gesti alipokuwa na Bitungu. Mama Juliana alimuonyeshea Juliana ile pafyumu.



    ?Mama hiyo niliinunua mwenyewe!?

    ?Wapi? Na nani alikupa pesa??

    ?Nilijibanabana mama.?



    ?Hii ni pafyumu ya kiume mwanangu na wewe haikufai.?

    ?Nimekuelewa mama ila miye niliipenda harufu yake...?



    Wakiwa katika majibizano, bila hata ya hodi mara baba Juliana akawavamia. Baba Juliana aliyekuwa ameshikilia simu mbili, moja yake moja ya mke wake. Kitendo cha kuingia akamkuta mama Juliana akiwa bado ameishikilia ile pafyumu huku akiwa amemnyooshea Juliana.



    ?Ina maana huyo mpuuzi bado hajalala siyo??

    ?Jamani! Nina maongezi naye kidogo ila atalala tu.?

    ?Na hiyo pafyumu uliyoshika ndiyo maongezi yanaingia vizuri siyo??

    ?Hapana mume wangu.?



    ?Embu leta, leta!?

    Baba Juliana akaiwahi ile pafyumu na kumpokonya mkewe. Akawa ameshagundua kuwa ni ya kiume.

    ?Haya mnaweza kunieleza hii ya nani??

    Wote kimya...

    ?Si naongea na wewe mama Juliana??

    ?Mume wangu embu basi punguza hizo hasira.?



    ?Msinichanganye? Ni nani anayetumia pafyumu ya kiume kati yako na Juliana??

    Juliana aliendelea kutetemeka. Alijihisi kojo kumtoka kwani tayari kitumbua kilikuwa kimedondoka katikati ya mchanga, aliona ni bora alivyogundua mama yake kuwa ni ya kiume kuliko alivyogundua baba yake.



    Alikuwa katika kusitasita huku akitaka kusema ukweli wote kuhusu uhusiano wake na mama yake pamoja na Bitungu ili litakalotokea litokee.

    ?Hiyo pafyumu alin...?



    Kwa haraka mama Juliana alichezwa na machale. Akamuwahi Juliana kabla hajamalizia kuongea.

    ?Mume wangu hii hapa nimeipata huko kwenye vikoba nasikia ni nzuri kwa mabinti hasa mtoto wetu huyu, ndiyo nikawa nimemletea kama atapendezwa na harufu yake nimuachie.



    ?Unasemaje mama Juliana? Ina maana ushaniona mtoto siyo? Haya sawa umemletea mwanetu safi! Embu nielekeze ni wapi wanapouza pafyumu ikiwa robo??



    Kabla mama Juliana hajajibu, simu ikaita. Baba Juliana akaangalia mkononi na kugundua ni simu ya mama Juliana ndiyo ilikuwa ikiita huku jina likiandikwa Bitu. Akaichukua na kuipokea kisha akakaa kimya bila kuongea.

    ***

    Muda wote Bitungu alikuwa hana raha. Aliwaza sana maneno aliyoambiwa mara ya mwisho na mama Juliana. Maneno juu ya pafyumu. Akili zote zilimuhama na kuona huenda anajuana na Juliana.

    ?Haiwezekani? Lakini kwa nini aniulize habari za pafyumu??



    Alijiuliza Bitungu na kujijibu mwenyewe kisha akainuka pale kitandani na kuelekea kwenye meza ambapo aliiweka ile pafyumu yake ya UDV. Alipofika hakuona chochote.

    ?Ina maana kuna mchezo nafanyiwa au? Sasa itakuwa wapi??



    Bitungu aliendelea kujiuliza mwenyewe. Alichokifanya aliichukua simu yake na kuanza kupiga namba ya mama Juliana. Iliita bila kupokelewa hadi ikakata, akajaribu kupiga kwa mara nyingine tena ikapokelewa.

    ?Mpenzi wangu mbona hupokei simu yangu? Embu niambie pafyumu yangu ya UDV uliichukua?







    Bitungu aliendelea kufloo lakini bado upande wa pili hakujibiwa kitu chochote zaidi ya kimya kutanda. Alichokifanya aliikata simu na kuipiga kwa mara ya pili. Napo ikapokelewa tena na kumfanya atabasamu.





    "Sweet wangu nitakuchukia? Embu niambie kama nimekuudhi nisamehe jamani bado nakupenda na sitaki kukupoteza hata kidogo!"



    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Bitungu aliendelea kuchanika maneno ya kimahaba bila hata kujua kinachoendelea upande wa pili. Safari hii aliipoza zaidi sauti yake huku akiwa amejilaza juu ya kitanda cha gesti na kuendelea kutoa sauti ya kubembeleza.





    Akiwa katika kubembeleza bila kujibiwa mara akasikia makelele ya majibizano kati ya mume na mke yakiendelea. Akainuka harakaharaka pale kitandani akiwa hajiamini kwa kinachoendelea. Akaisogeza tena simu yake sikioni na kuendelea kusikia majibizano yale.





    ***Ugomvi uliendelea kuwa mkali kati ya baba Juliana na mkewe. Simu iliyopigwa na maneno yaliyokuwa yakiongelewa yalizidisha hasira za baba Juliana. Alijiangalia mara mbilimbili mwili wake ulivyotota kwa jasho na meno yakiumana kisha akamgeukia mkewe huku akimkazia macho na vidole akimnyooshea.





    "Nikisema nianze kukutandika kama mtoto wako huyo nitakuwa nimekosea?"

    "Kwani nimekosa nini mume wangu?""Si simu! Unajifanya hujui kinachoendelea?"

    "Imefanyaje? Kwani we huwa hupigiwi simu na watu waliokosea namba?"





    "Mama Juliana? Hivi ni mtoto gani utamdanganya kwa hiki kinachoendelea kwenye simu?"

    "Mume wangu, leo unaonekana kuwa na hasira sana. Hiyo namba kubaliana na mimi kuwa imekosewa na imekuja kwa bahati mbaya.""Nakujisevu imejisevu kwa bahati mbaya siyo!"





    "Kwani imejisevuje mume wangu si namba tu imetokea!"

    "Batu sijui Bitu! Si umeandika wewe hapa unajifanya hujui siyo?"

    Baba Juliana alimsogezea kwa ukaribu mama Juliana na kuanza kumwonyesha jina la Bitu kwenye ile simu yake. Simu haikuwa imekatwa hali iliyomfanya mama Juliana ashtuke na kutaka kuikata lakini baba Juliana akamuwahi na kuusogeza mkono wake pembeni.





    "Unataka kufanyaje? Si umesema amekosea! Sasa kuanzia sasa hii namba nakula nayo sahani moja ama zangu ama zake pumbavu!""Msimamo wangu uko palepale mume wangu, siwezi kukusaliti hata siku moja na hiyo namba imekosewa.





    Kama ukichukua maamuzi mabaya shauri yako wala usinishirikishe!"

    "Nitaelewa tu msaliti ama siyo msaliti ngoja nilifanyie kazi. Kukuachia uhuru na mtoto wako mnautumia vibaya!""Amua utakavyofanya na ukweli utaujua maana nakwambia sijui lolote unaendelea kukazania, amua tu!"





    Iliimbidi mama Juliana azuge kuwa amekasirika ili baba Juliana aamini lakini wapi! Ndiyo kwanza baba Juliana aliondoka chumbani mule na kumuacha Juliana na mama yake wakiwa kwenye butwaa. Vita ikaanza upya kwa Juliana na mama yake.





    "Halafu wewe mshenzi wewe? Kwanza una bahati sana baba yako kasahau kuhusu pafyumu hii. Haya niambie ukweli umeitoa wapi hii pafyumu ya kiume?""Mama si nilishakwambia kuwa nilijibanabana nikanunua!""Unasemaje? Ukanunua siyo?"





    Hasira za mama Juliana zilimwishia Juliana. Tayari alishajiona amempoteza Bitungu kwa jinsi mumewe alivyoondoka kwa hasira akiwa na simu yake mbaya zaidi aliposema atakula nayo sahani moja kuhakikisha anamjua na kumpata. Alimshika Juliana kwa nguvu kisha akamwachia."Nakupa nusu saa, naenda chumbani huko alipo baba yako, nikirudi nataka uiniambie ukweli wote hii pafyumu umeitoa wapi?"





    Kitendo cha mama Juliana kuondoka huku nyuma kamwacha Juliana na maswali ya sintofahamu. Cha kwanza mama yake alivyojichanganya kwenye jina la Bitu lililokuwa kwenye simu ya mama yake na pili ni kumjibu mama yake juu ya ile pafyumu alipoitoa.





    "Nitamweleza pafyumu ya Bitungu akinipiga namwambia baba ukweli wote hadi nilivyomshuhudia gesti kule Bagamoyo kama kukosa tukose wote tu."Juliana alijiongelea na kujijibu mwenyewe. Aliiweka ile pafyumu pembeni kisha akajipindua pale kitandani na kuanza kuutafuta usingizi akiwa na maswali kibao kichwani.

    ***

    Muda wote Bitungu alibaki na bumbuwazi asijue lipi la kufanya. Maneno ya mwisho aliyoyasikia kwenye simu yalimpagawisha zaidi. "Ina maana atakula sahani moja na mimi? Hapana mimi kidume kwanza atakuwa ni hawara wake tu."





    "Lakini bado picha haijanijia! Kweli sweet wangu ndiyo aniingize kwenye matatizo? Na kwa nini simu alimpa mume aipokee kama kweli ananipenda?"Alichokifanya Bitungu ni kutoka moja kwa moja hadi bafuni na kuoga kwa mara nyingine kisha akavaa nguo na kulipia mule gesti na kuondoka.





    "Kama anajijua ni mke wa mtu basi na mimi ni mume wa mtu, naenda kuusema ukweli wote kwa huyo mumewe anayetaka kula sahani moja na mimi."







    Hakujali giza lililokuwa limefunika. Muda wa saa nne za usiku wala haukumtisha ndiyo kwanza alielekea moja kwa moja hadi kituo cha daladala ambapo napo alikuta patupu. Daladala nyingi zilikuwa zimeshakwenda kupaki lakini hilo halikumuuza kichwa Bitungu.





    ?Haiwezekani nikaingia matatizoni eti kisa mwanamke!?

    Alijiongelea mwenyewe Bitungu huku akisubiri usafiri wa daladala. Hadi nusu saa inakatika bado hakukuwa na dalili zozote za kutokea kwa daladala zaidi ya Bitungu kuendelea kujiegesha kwenye eneo maalum la kukaa abiria.





    ?Lakini? Hivi kwa nini nisirudi kulala halafu asubuhi nikadamkia huko? Hapana ila nisubiri kwanza tu.?

    Bado akili ya Bitungu haikuwa imekaa sawa. Baada ya kukaa kwa muda moyo wake ukaingiwa na furaha. Furaha baada ya kuiona daladala ikiingia kituoni hapo ikitokea katikati ya jiji la Dar.

    ?Haipakizi tena hii, inaenda kulala.?





    Aliongea kondakta wa ile daladala baada ya Bitungu kupitisha mguu wake akitaka kuingia ndani.

    ?Kama haipakizi sawa nitaenda kulala hukohuko inapolala.?





    ?Mwana mbona husikii! Hii inalala hapo pembeni mpaka asubuhi saa kumi na mbili ndiyo inahamsha tena.?

    ?Lakini nyie makonda mnajifanyaga wajanja sana, mnasema haipakizi halafu baada ya muda inapakiza tuwaeleweje??



    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliongea Bitungu kwa jazba. Lengo lake akilini lilikuwa ni kutoka tu maeneo yale ya Bagamoyo hata kama atafika mjini usiku mnene ingekuwa sawa tu ili mradi atoe dukuduku lake kwa baba Juliana.





    Ile daladala ilipomaliza kushusha ilijisogeza hadi pembeni na kupaki. Bitungu alinyong?onyea ikambidi akubaliane na ukweli kuwa muda ule alikuwa amechelewa. Alichokifanya ni kurudi mpaka kwenye ile gesti kwa mara ya pili na kuchukua chumba kingine kwa lengo la kudamkia asubuhi na mapema kwa mama Juliana akauseme ukweli kwa mumewe.

    ***

    Hadi asubuhi kunakucha, si mama Juliana wala baba Juliana ama Juliana aliyekuwa ameamka. Wote walikuwa wamepitiwa na usingizi. Haikuwa kawaida ya baba Juliana kupitiwa na usingizi kiasi kile ila ilimtokea kwa kuwa alikuwa bado hajisikii vizuri kiafya.





    Juliana alikuwa mtu wa kwanza kushtuka chumbani kwake. Alitoka hadi sebuleni ambapo saa yao ya ukutani ilimuonyesha kuwa tayari ilikuwa imetimia saa mbili za asubuhi. Kumbukumbu za kichapo cha jana yake usiku bado zilimtawala akilini. Kikubwa kilichomuuma zaidi ni kuendelea kuchanganywa kimapenzi na Bitungu. Aliiwasha simu yake na kumpigia Bitungu.





    ?Bitungu mpenzi!?

    ?Niambie sweet, vipi mzima jamani!?

    ?Bitu miye naumwa na nataka uje unione nyumbani??

    ?Unaumwa? Nini tatizo??





    ?Bitu naumwa kwa kukuwaza wewe, unaniweka kwenye wakati mgumu wakati unajua fika kuwa nakupenda!??Sijakuelewa? Nakuweka katika wakati mgumu kivipi wakati wajua fika bado nipo huku Bagamoyo na wafanyakazi wenzangu na huku semina iliyonileta itaisha baada ya wiki.?

    ?Nikuulize kitu bebi??





    ?Nakusikiliza uliza tu??

    ?Unanipenda kabisa kutoka moyoni au unanitamani embu niambie ukweli bebi wangu, samahani lakini!?

    ?Hapana sweet kama ningekuwa nakutamani mbona ningeshaachana na wewe siku nyingi tangu nilipomaliza shida zangu kwa mara ya mwisho.?





    ?Nafurahi kusikia hivyo lakini kuna jambo moja linanitatiza kweli.?

    ?Lipi hilo na mbona leo umeamka na maswali hivyo mpenzi wangu??

    ?Yote hiyo kwa sababu nakupenda, nakuwaza kila muda na sipendi kukupoteza hata siku moja.?

    ?Hata miye sipendi nikuache, haya niambie kinachokutatiza kipi hasa??





    ?Bebi niambie ukweli wako kabisa maana siku nikigundua nitaumia sana! Niambie ukweli umeoa ama hujaoa???Ningeoa mke si ungemuona? Uko peke yako mpenzi wangu na ndiyo maana hata tunavyokutana huwa sina wasiwasi wowote.?

    ?Kweli bebi wangu??





    Juliana alimtega Bitungu kwa makusudi, lengo lake ni kummbana atambue kuwa anashiriki mapenzi na familia moja yaani yeye na mama yake. Kila alipokuwa akitaka kumwambia ukweli alikuwa akisita na kumfanya aongee mengine. Mateso aliyoyapata jana yake usiku yalikuwa yamesababishwa na Bitungu huyohuyo kwa kiasi kikubwa.





    Moyo wake Juliana ulishamwambia kuwa aachie ngazi. Amwachie mama yake aendeleze mapenzi yao. Juliana alijikaza kwa muda akakaa kimya kisha akaikata ile simu aliyokuwa akiongea na Bitungu. Baada ya kuikata akaamua kutuma meseji ya hasira na ya mwisho kwa Bitungu.





    ?Naomba unielewe kwa makini! Kuanzia sasa sitakuita tena mpenzi, bebi wala honey. Mapenzi ya mimi na wewe Bitungu naomba yaishie hapa leo hii. Nilikupenda Bitungu lakini ukweli nilioujua ndiyo umenifanya kuchukua maamuzi haya magumu, ukweli wa wewe kuto....?



    ...Likishaondoka zake tu nitakwambia Bitu wangu wala usiwe na shaka!"

    "Haya bebi wangu, nakupenda! Wewe ndo kila kitu moyoni mwangu.."





    ILIPOISHIA

    ...Likishaondoka zake tu nitakwambia Bitu wangu wala usiwe na shaka!"

    "Haya bebi wangu, nakupenda! Wewe ndo kila kitu moyoni mwangu.."

    SEREBUKA NAYO SASA...



    Baba Juliana aliisoma meseji ile aliyoituma Bitungu kwa hasira kali. Akaizima kabisa simu ile na kuiweka pembeni kisha akainamisha kichwa chake chini na kujikaza kiume. Moyoni alikosa raha, hakuwa na amani tena.



    "Hivi mama Juliana wa kunifanyia hivi? Kitu gani ambacho simridhishi mwanamke huyu?"

    Alijiongelea na kujijibu mwenyewe. Aliamua kutoka nje ya ofisi lengo likiwa kwenda kupata hewa zaidi. Kile kiyoyozi kilichokuwa kimefungwa ofisini kwake alikiona hakitoi hewa yoyote.

    ***

    Siku nzima mama Juliana alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, kila muda alikuwa akimuita Juliana bila kumwambia chochote. Wakiwa wametulia jikoni mara simu ya Juliana ikaita.

    "Haloo!"



    "Mama yako yupo wapi?"

    "Niko naye hapa!"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nipe niongee naye."

    Bado hasira za maneno kutoka kwa Bitungu aliyokuwa ametumiana naye kwa njia ya meseji hazikuwa zimemuisha.



    "Mama! Simu yako, baba anataka kuongea na wewe!"

    "Haloo!""Nisikilize kwa makini mama Juliana! Nina jambo zuri nataka kukwambia mke wangu!"

    "Nakusikia mume wangu!""Nitachelewa kurudi leo lakini ikifika saa moja nitakuhitaji uje sehemu sawa?"

    "Haya niambie ni wapi?"



    "Kuna sehemu nitakuelekeza baadaye tukishaambiwa rasmi hapa ofisini kwani bosi wetu ametushtukiza kuwa leo mke wake amewasili mchana na jioni tutajumuika naye katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.""Haya utaniambia mume wangu ngoja niandae nguo ya kuvaa kabisa!"



    Baba Juliana akawa ameshacheza na akili ya mkewe. Akaikata simu kwa makogo huku akiamini mtego wake utanasa kwa asilimia zote. Akamtumia na meseji ya msisitizo.

    "Usisahau kunibebea na koti langu la suti nililisahau!"

    "Haya, umesema saa moja!"

    "Ndiyo?"



    "Sasa simu yangu unayo nitakujaje mume wangu?"

    "Tumia simu hiihii ya Juliana!"

    "Haya baadaye basi!"

    "Sawa usisahau mke wangu uwepo wako ni muhimu sana kwa siku ya leo.

    ***

    Ilipofika saa kumi na mbili baba Juliana alikuwa bado kazini. Malengo yake ni kuwakutanisha Bitungu pamoja na mama Juliana ili aujue ukweli. Hakuwa ameiwasha ile simu ya mama Juliana tangu mara ya mwisho wamalize kutumiana meseji.



    Kitendo cha kuwasha tu simu ya mama Juliana aliyokuwa nayo, meseji mfululizo zikaanza kuingia, zote zikiwa ni lawama kutoka kwa Bitungu."Sweet, kwa nini unanifanyia hivi? Mbona unanizimia simu lakini muda wote nakutafuta?"



    Baba Juliana akamjibu meseji karibia zote.

    "Sorry bebi wangu jamani, huku kwetu umeme ulikatika na hapa nilipo ndiyo kwanza simu nachati na wewe huku ikiwa kwenye chaji.



    "Haya muda si umeshafika jamani fanya basi tukutane mwenzio nina hamu na wewe kweli!"

    "Tena una bahati nimeshatoka Bagamoyo tangu saa saba za mchana, nipo maeneo ya Tegeta."
"Huko unafuata nini bwana njoo tukutane baa ya Sweet Mama hapa karibia na Sinza Mori kuna gesti moja nzuri sana."



    "Basi nipe nusu saa sweet wangu."

    Bitungu alikuwa na pupa. Hakutaka kuambiwa chochote, meseji kutoka kwa baba Juliana kwa kutumia simu ya mama Juliana zilimchanganya. Asilimia zote alijua anachati na mama Juliana.

    Shangwe zilimtawala baba Juliana na kujiona zoezi lake linaenda kukamilika ndani ya muda mchache. Tayari alikuwa ameshamteka akili Bitungu na kumsubiria ajilete tu.



    "Nimeshafika sweet wangu uko wapi?"

    "Nitachelewa bebi ila chukua chumba kabisa kisha niambie namba ngapi nitakuja moja kwa moja."

    Muda wote baba Juliana alikuwa eneo la nje ya Baa ya Sweet Mama akimsubiri Bitungu. Bitungu alifika na kuchukua chumba namba 32 kisha akatuma meseji.

    "Nimeshafika! Nipo chumba namba 32."



    "Haya bebi wangu nipo maeneo hayahaya nikute mlango wazi huko!"

    Mama Juliana naye alikuwa amewasili. Alikuwa ameongozana na Juliana lakini alipofika alishikwa na mshangao baada ya kumkuta mumewe akiwa amekaa mwenyewe huku kukiwa hakuna dalili yoyote ya sherehe.



    "Juliana amefuata nini hapa?"

    "Mume wangu si umeniambia sherehe nikaona bora tuwe wote!"

    "Ok, sasa tunaelekea kwenye chumba namba 32 kwenye sherehe yenyewe."



    Hofu kubwa ilianza kumjaa mama Juliana. Mapokezi hakukuwa na mhudumu hivyo wakaongoza moja kwa moja wote watatu huku akisitasita lakini baba Juliana alikuwa nyuma yake akimsukuma.

    "Sherehe ipo humu ndani ingia!"

    Baba Juliana akamsukuma mkewe, akafungua kitasa na kuingia huku akibaki nje ya mlango na Juliana.

    "Sweet wangu!"

    http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Haraka Bitungu akamuwahi mama Juliana.

    "Nani?"Kabla Bitungu hajamalizia, baba Juliana akiwa na Juliana wakaingia chumbani. Bitungu akashangaa zaidi."Bitungu?"



    Juliana uzalendo ukamshinda akasimulia yote kuhusu Bitungu alivyowachanganya na mama yake huku mama Juliana akibaki hajielewielewi.



    "Nimejua yote kuanzia mwanzo kisha wewe mama kuanzia leo mimi na wewe ndiyo basi baki na huyo mpumbavu wako. Meseji zote hizi hapa kama ushahidi kwa ndugu zako."



    ************************MWISHOOOOOO*******************?


    .

NI SHIIDA! - 4

 






Chombezo : Ni Shiida!

Sehemu Ya Nne (4)





"Ina maana Mama Zai ndiyo alikuwa amepiga?"

"Sijui mama, wala sikuangalia jina!"



Alichokifanya mama Juliana ni kuangalia sehemu ambazo simu ile imepokelewa na kugundua kuwa alifanyiwa mchezo na Juliana. Mchezo wa kukatiwa simu ya Bitungu.

"Kwa nini umekata simu yangu!"



"Hapana mama iliita yenyewe na kukatika!"

"Ina maana miye mjinga sijui simu? si nakuuuliza?"

"Kweli mama!"



Mama Juliana aliiweka pembeni ya bafu simu ile na kumfukuza Juliana arudi chumbani aendelee na kazi ya usafi.

Juliana alijirudia zake ndani akiwa amejiongeza vya kutosha, alishaelewa picha kamili juu ya kitakachotokea mbeleni. Alichoamua ni kwenda kuchukua simu yake na kumpigia Bitungu.

"Haloo!"



"Yes baby! Nimekumisi upo wapi sasa hivi?"

"Nipo maeneo ya mbali kidogo!"

"Si uniambie tu hata kama mbali, mbali mbinguni bwana"

"Sweet niko Bagamoyo lakini kesho nategemea kurudi!"

"Bagamoyo? Umeenda lini?"



"Embu subiri kwanza kuna simu ya bosi wangu inaingia, ntakupigia."

Aliongea Bitungu kisha akamkatia simu Juliana. Juliana aliishiwa pozi, penzi la Bitungu lilishamkolea, alijifariji na kuona kuwa huenda ni kweli Bitungu atakuwa amepigiwa simu na bosi wake. Akiwa bado anatafakari kuhusu Bitungu kwa mbali akasikia sauti ya mama yake ikiongea na simu. Hatua kwa hatua akasogelea hadi eneo la sebuleni ambapo mama yake alikuwa na kanga moja tu ametoka kuoga huku akiongea na simu.



"Niambie moja nijue nikukute wapi?"

"Utakuja moja kwa moja hadi gesti ya Tupendane ipo mtaa wa Mchopanga huku Bagamoyo,"

"Kwa nini mpenzi wangu umeamua kwenda mbali huko! Embu njoo mjini bwana!"



"Hukuhuku ndiyo safi na kuna amani kuliko huko kuwa na hofu kibao, kwanza dakika 40 tu umeshafika!"

"Haya ngoja nivae haraka nakuja, nilivyo na hamu asikwambie mtu na leo nataka mechi ya kikubwa, sitaki mechi za mchangani za kuishia nusu saa."

"Kwa hilo usijali, miye ndiye Bitungu!"



"Haya mpenzi nipe saa moja nitakuwa nimeshafika hapo."

Maneno ya Mama Juliana aliyokuwa akiongea kwenye simu yalimuumiza sana Juliana, alijinyong'onyea huku akiwa bado amejificha kwa kujibanza kwenye ukuta wa sebuleni kwao, mama Juliana hakutambua kama Juliana ameyasikia yote aliyoongea kwenye simu.



Alichokifanya Juliana ni kukimbia chumbani kwake na kujiandaa tayari kwa kumfuatilia mama yake hadi atakapoelekea, lengo lake kubwa lilikuwa ni kuhakikisha anamtenganisha Bitungu na mama yake.

"Juliana!"

"Abee mama!"



"Natoka ila nitawahi kurudi mwanangu, nimeitwa sehemu kuna mwenzetu anatakiwa kufanyiwa kicheni pati hivyo nimeitwa kushirikiana nao katika kuandaa."

"Sawa mama!"



"Nakuona unameremeta tu, sitaki utoke na wala sichelewi narudi mchana huuhuu nikukute!"

"Sawa mama!"

Aliitikia Juliana huku akiwa ameshapendeza bila mama yake kujua kuwa wapo safari moja huko aendapo.



http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Kitendo cha mama Juliana kutoka kuelekea kupanda bodaboda hadi kituo cha Mwenge ndipo akapande daladala za kwenda Bagamoyo, huku nyuma Juliana alizuga kwa dakika chache na kuufunga mlango kisha akampigia simu Bitungu.

"Haloo"

"Ndiyo sweet!"



"Mbona hukunipigia tena ulipomaliza kuongea na bosi wako!"

Juliana alimtega Bitungu makusudi.

"Ohh! Sorry Sweet, nilijisahau hata hivyo simu yangu inaelekea kuisha chaji muda si mrefu itakatika na huku nilipo hakuna umeme!"

"Jamani! Hata Jenereta hamna baby!

"Ndiyo..."



Kabla Bitungu hajamalizia kuongea akaikata simu na kuizima kwa makusudi, alijua ameshamdanganya Juliana na wala hawezi kujua lolote. Alijiweka sawa akimsubiri mama Juliana. Aliamini baada ya muda ataiwasha simu na kumuelekeza alipo.



Kwa upande wa mama Juliana presha ilikuwa juu, alionyesha kuchanganyikiwa. Alishafika kituoni Mwenge na kumpigia simu Bitungu ikawa haipatikani, akashindwa afanye nini.

"Ndiyo nini ananifanyia! Kama alikuwa hataki kuonana na mimi leo si angeniambia?"

Alijisemea mama Juliana huku hasira zikimzidi, hakuonyesha kukata tamaa kwa sababu maji alishaamua kuyavulia nguo, alichokifanya aliendelea kupiga simu ya Bitungu mara mbilimbili huku ikiwa haipatikani, mara ikaita.



"Haloo!"

"Tushaonana watoto sasa!" Aliuliza mama Juliana kwa jazba.

"Hapana chaji mpenzi, vipi umefika wapi?"

"Nipo kituoni Mwenge, tena una bahati nilikuwa nataka kurudi nyumbani nikalale!"

"Ahhaa!! Usinifanyie hivyo mpenzi utaniua panda daladala uje!"

"Nishuke wapi!"



"Shuka Bagamoyo mwisho, nitakuja kukuchukua stendi, halafu tuelekee hadi eneo ilipo gesti."

Maneno yale yalimpa faraja moyoni mama Juliana, aliona anapendwa kuliko hata mume wake anavyompenda, mwili wake ulikuwa umepatwa na mshtuko kama wa radi na Bitungu tu ndiyo alikuwa fundi wa kurekebisha mshtuko huo. Haikuchukua muda mama Juliana akawa ameshaingia kwenye daladala ya kuelekea Bagamoyo.



Wakati mama Juliana akiwa ndani ya daladala, Juliana naye alikuwa tayari ameshauona mchezo mzima pale kituoni, alikodi bodaboda ya kumpeleka hadi Bagamoyo.

"Hakikisha daladala ile pale mbele yetu haituachi hata chembe!"

Juliana alimwamuru dereva bodaboda.



Kila kituo daladala ilipokuwa ikisimama, dereva bodaboda alikuwa akisimama kwa nyuma yao kidogo. Baada ya mwendo wa zaidi ya nusu saa hatimaye wakaingia Bagamoyo.

"Tusimame hapahapa!" Juliana alimuamuru dereva.



Mahesabu ya Juliana yalikuwa sahihi, alishuhudia mama yake akishuka kwenye daladala moja kwa moja na kufuatwa na Bitungu ambapo walikumbatiana kisha wakaingia kwenye bajaji na kuchomoka.

"Tuwafuate, mpaka nitajua mwisho wake, haiwezekani nifanyiwe mchezo mchafu huku nashuhudia!"

Aliongea Juliana huku dereva bodaboda akiendelea kuwafuatilia bila kujua kama anayemfuatilia Juliana ni mama yake mzazi.



Baada ya mwendo mfupi, ile bajaji ikawa imeshasimama, mama Juliana alitoka sambamba na Bitungu na kuelekea katika gesti ya Tupendane.

"Nimerudi tena!!"



Aliongea Bitungu, akimwambia mhudumu wa mapokezi katika ile gesti huku akielekea kwenye chumba alichopangiwa na kufikia moja kwa moja kwenye kitanda.

"Mpenzi nilikwambia huku kumetulia!"

"Kweli, lakiniii..."



"Lakini nini tena!! Umeshaanza kulalamika!"

"Hapana Bitungu, itabidi tufanye haraka nirudi si unajua huku ni mbali!"

"Najua!"



Mama Juliana alivua nguo zake na kufungua kimkoba alichokuwa nacho na kutoa khanga na kuivaa, kisha akatingisha mwili wake kwa makusudi mbele ya Bitungu aliyekuwa akimtolea macho.

"Twende basi tukaoge mpenzi!"

"Mhh, unajua wewe ni mzuri asikwambie mtu! Utamu ulionao ni zaidi ya kitu chochote!"

Aliongea Bitungu huku akivua suruali yake na kuchukua taulo la gesti na kumshika Mama Juliana hadi bafuni kwenda kuogeshana.



Muda wote Juliana alikuwa yupo nje ya gesti ya Tupendane, presha kwake ilikuwa kubwa, hakujielewa ni njia gani atatumia kujua chumba walichokuwa Bitungu na mama yake mule ndani.

"Kuna vyumba!"



Aliongea Juliana akimwambia mhudumu yule wa mapokezi.

"Ndiyo, unataka single au double?"



"Kwanza shilingi ngapi? Na ingekuwa vizuri kwanza niweze kuviona na ukubwa wake!"

Aliongea Juliana huku akijijua kabisa hakuwa na uwezo wa kulipia chumba kutokana na pesa kidogo aliyokuwa amebeba. Yule mhudumu wa mapokezi alimwelekeza chumba kimoja baada ya kingine huku akikiruka kile chumba ambacho yupo Bitungu na mama yake.

"Mbona vingine hunionyeshi?"

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Ukiona hivyo ujue vina watu ndani yake."

"Kwani?? Yule mama aliyeingia humu ndani na kijana mmoja hivi kama dakika kumi zilizopita kaingia chumba gani?"



Juliana alimuuliza yule mhudumu kimitego.

"Chumba hiki hapa tulichokiacha!"



Alijibiwa Juliana huku akili yote ikimuhama, akaachana na yule mhudumu na kuelekea chumba alichokuwa ameelekezwa, moja kwa moja akaufungua mlango wa kile chumba, haukuwa umefungwa hivyo akaingia moja kwa moja na kuzama ndani.

"Lakini huko si nimekwambia kuna watu!"

"Hata kama!! Nawafahamu ngoja niwasalimie kwanza!"





Aliongea Juliana huku akiwa ameshaingia ndani na kumuacha mhudumu nje akiwa mdomo wazi. Kitendo cha kuingia kwenye kile chumba alikikuta kitupu, macho ya Juliana yaligongana na nguo za mama yake sambamba na mkoba uliokuwa kitandani pale, hakujiamini mara mbilimbili kama alikuwa ni mama yake.



"Lazima watakuwa wameingia kuoga tu!"

Alijiongelea Juliana huku akipiga hatua kuelekea kwenye bafu ambalo lilikuwa ndani mulemule. Alipokaribia katika mlango wa lile bafu aligundua kuwa haukuwa umefungwa, hivyo akausukuma kidogo na kuchungulia kwa jicho moja. Alimshuhudia mama yake akiwa anamsugua mgongo Bitungu, Bitungu naye akimsugua mama Juliana huku wakifurahia kwa kupigana mabusu.



Baada ya kusuguana kwa muda wakajimwagia maji kuondoa mapovu kisha Bitungu akataka kufanya mambo mulemule bafuni...

"Mhh sasa naona mechi yetu kama tukaihamishie kule kwenye uwanja mkubwa maana nahisi huu si uwanja mzuri..."



"Kwani una nini sweet!"

"Wee huoni, vichuguu kila kona, hata mashuti unayopiga nashindwa kuyadaka vizuri!"

"Ni kweli sweet lakini ngoja kwanza nikijikwaa tu ndiyo tuh..."

"Ukijikwaa nini, sitaki kusubiri mpaka ujikwae, miye nainuka bwana!"

"Hapana Sweet subiri kwanza!"



Muda wote Juliana alikuwa akiwapiga jicho kupitia kaupenyo kadogo kwenye mlango, mzuka ulionekana kumpanda hata lile wazo la kutaka kuwafumania likakaukia kwenye ubongo wake kwa muda mfupi.

"Inamaana Bitungu ndiyo mchezo wake enhh!, kwangu miye anajifanya kunibania kwa mama anampa vyote!"



Aliendelea kujisemea Juliana huku akiwa bado kauinamia mlango.

Ndani ya muda mchache Bitungu na mama Juliana walikuwa katika mapumziko ya mechi yao, mama Juliana alikuwa hoi hajiwezi huku Bitungu akishughulika kwa kumvalisha khanga yake.

"Vaa basi jezi yako, tukapumzikie kule!"

"Baby!"



"Nambie!"

"Usinivalishe hiyo khanga kwanza!"

"Kwa nini?"

"Hivi umeniroga ama nini?"

"Kwani vipi sweet?"



"Yaani haiwezekani hata mechi ya kwenye uwanja mbovu uwe unaijulia kiasi hiki!"

"Nilishakwambia miye fundi wa mipira iliyokufa, kiwanja chochote unachokitaka tunaweza kucheza na nikatoka na ushindi tena ule wa kishindo." Aliongea Bitungu kwa kujisifu.



Maneno yale yalipata kusafiri hadi kwenye ubongo wa Juliana, akayanasa kwa hasira ya hali ya juu sambamba na macho yakimkakamaa.

"Bitungu... Bitunguuuu?"



Juliana alijikuta akitoa sauti ya ukali akilitaja jina la Bitungu kwa sauti ya juu, moyoni mwake alishakubaliana na lolote litokee. Alichokifanya kabla Bitungu na mama Juliana hawajatoka mle bafuni, alifungua kitasa cha mlango ule na kutaka kuingia ndani.

"Unafanyaje chumba hiki?"



Sauti nene na kali ya kiume ilimhoji Juliana. Juliana akageuka na kuisikia sauti ile inapotokea, kisura hakuweza kumfahamu zaidi ya kuambulia kumjua yule mhudumu wa mapokezi aliyekuwa amefuatana naye.



"Nilimwambia chumba hicho kina watu akasema anafahamiana nao," alijitetea yule mhudumu wa mapokezi akimuelezea yule kaka mbele ya Juliana.

"Dada hivi unajua utaratibu katika gesti hii?"

"Jamani si nilishawaambia kuwa nawafahamu?"



"Hata kama unawafahamu ndiyo uwachungulie tena wakiwa bafuni?"

"Haya tusubiri watoke muone kama hawanijui!" Aliongea Juliana kwa kujiamini lakini yule mkaka hakutaka kabisa kuaminiana naye, alichokifanya alimshika Juliana mkono na kumtoa katika kile chumba.

"Nimesema sitoki, hata mfanyaje mpaka wa huku bafuni wanione?"

Aliongea Juliana kwa kujiamini.



"Utatoka tu! Wee nani mpaka usitoke na kwanza hivi umelipia hata chumba humu ndani?"

"Sijalipia lakini sitoki!"

Juliana alitolewa kwa nguvu huku akiburutwa mpaka kwenye korido ya mule ndani ya gesti.



***

Wakati yote hayo yakiendelea si Bitungu wala mama Juliana aliyekuwa anajua kinachoendelea. Ndiyo kwanza mama Juliana alikubali kuendelea na kipindi cha pili baada ya kuchanganywa na mechi iliyopigwa kipindi cha kwanza japokuwa uwanja ulikuwa mbovu.

"Bitu mpenzi!"



"Niambie sweet!"

"Nasikia kuna makelele kweli nje na sauti ya dada kama analia kwa mbali?"

"Achana nao wanaweza wakawa watu wamefumaniana hao lakini kwa hapa, hapana! Sidhani kama kuna mambo hayo!"

"Nina wasiwasi Bitu!"

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Achana nao kwanza hayatuhusu tumekuja kula raha zetu hapa na siyo kufuatilia mambo ya watu."

Aliongea Bitungu huku akimvalisha mama Juliana ile khanga yake. Walikuwa tayari wameshatosheka kwa mechi kali mbili. Kitendo cha kutoka bafuni na kuelekea kitandani ile sauti iliyokuwa ikilia ndiyo kwanza ikazidi.



"Bitu, wacha nikaone anayelia mbona sauti kama ya mwanangu!"

"Mwanako? Afuate nini huku? Embu jifute tuagize chakula tupumzike kidogo urudi hayo mambo mengine waachie hukohuko hayatuhusu."

"Bitu kwangu miye nahisi kama yananihusu."







"Hayakuhusu sweet wangu embu nisikilize basi!"

"Bitu?"

"Nakusikia!"

"Kwa kuwa nakupenda! Nimeamua siendi tena!"

"Sawasawa, ndiyo maana nakupenda sweet wangu!"

Mama Juliana aliamua kutii amri mbele ya Bitungu japokuwa kelele alizokuwa akizisikia kwa mbali zilimaanisha. Alitoa mafuta yaliyokuwepo kwenye mkoba wake na kuanza kujipaka kisha akampaka na Bitungu.



"Haya mpenzi kwa sasa tupumzike."

"Lakini..."

"Lakini nini tena!"

"Hapana itabidi nirudi tu sasa hivi kwani kulala nitachelewa jamani na si unajua kuna mwanangu nimemuacha."



"Najua, wee tulale, nitatega mlio wa kutuamsha hapa kwenye simu baada ya nusu saa ndo utaondoka."

"Sawa mpenzi!"

Aliitikia mama Juliana huku akiachana na dera alilokuwa anataka kuvaa, aliendelea kuishikiza khanga yake kifuani kisha wakavutana na Bitungu hadi wakajikuta wamelala kitandani huku Bitungu akiwa juu yake na baada ya muda kidogo usingizi ukawapitia.

***

Bado Juliana alikuwa katika machungu makubwa, machungu ya kushuhudia mama yake akicheza mechi ya nguvu na Bitungu, tena mechi ya mchangani bila viatu. Bitungu aliyekuwa amemuamini lakini kumbe alikuwa akimficha siku zote.



Kwa muda huu Juliana alikuwa ameshindwa kabisa nguvu na wale wahudumu wa ile Gesti ya Tupendane. Alikuwa amejikalia zake nje ya ile gesti akitafakari huku pembeni yake akiwa na dereva bodaboda.



"Turudi tu nyumbani!" aliongea dereva bodaboda akimwambia Juliana.

"Hapana, siwezi ni bora uniache!"

"Nikuache?"

"Ndiyo niache hujaelewa nini?"

"Hasira zako hukohuko, haya nipe changu nirudi zangu?"

"Sh. Ngapi?"



"Unajifanya hujui bei tuliyokuwa tumeongea? Nipe elfu 10 zangu."

Juliana alikuwa ameshajipanga kwa kiasi hicho cha pesa. Pesa ambazo alikuwa akiwekeza nyumbani kwao kidogokidogo. Alifungua kipochi chake kidogo kilichokuwa na zaidi ya shilingi elfu 50 kisha akachomoa noti ya elfu 10 na kumpatia na kuondoka zake.



Macho, mwili viliashiria Juliana kukata tamaa ya kitu flani, hakuwa Juliana wa kawaida kutokana na kitu kilichomtokea. Alijiapiza na moyo wake asiondoke mpaka amshuhudie mama yake akitoka pale nje na Bitungu."Lazima Bitungu achague moja leo, kati yangu na mama nani anastahili kuwa naye!"

Alijikuta akijisemea mwenyewe Juliana huku akikazia macho eneo la mbele ya ile gesti kwa kila aliyekuwa akitoka ama kuingia.



Baada ya kukaa nje kwa zaidi ya nusu saa, giza lilianza kuomba njia. Juliana wala hakutetemeka kurudi kwani mtu aliyemhofia kama akichelewa kurudi alikuwa ni mama yake na siyo baba yake anayechelewaga kurudi nyumbani.



Hatimaye mama Juliana akatoka akiwa ameongozana na Bitungu. Bitungu aliyekuwa amevalia bukta na tisheti ya bluu huku mkono mmoja ukiwa kiunoni mwa mama Juliana.



Hasira kwa Juliana zilikuwa zaidi ya simba jike mwenye njaa kali. Alitamani kwenda kuwasambaratisha lakini moyo wake uligeuka na kuwa mzito kwa kuona kama mapenzi yake na Bitungu yanaweza kuelekea ukingoni. Macho yake yalibaki njia panda yakiwaangalia tu. Baada ya muda alishuhudia bajaj ikifika eneo hilo kisha mama Juliana akampiga busu Bitungu la kumuaga.

"Bitungu! Bitungu! Bitungu!"



Juliana uzalendo ulimshinda na kujikuta akilitaja jina la Bitungu kwa sauti ya juu. Ndo kwanza Bitungu akawa kama hajasikia zaidi ya kuiachia ile Bajaj ikiondoka na mama Juliana. Juliana alichokifanya ni kumsogelea Bitungu karibu.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Umefuata nini huku? Na nani kakwambia nipo eneo hili?"

"Unanigombeza au unaniambia?"

"Nakuuliza nani kakwambia nipo huku?"

"Uliniambia mwenyewe kwenye simu!"

"Kuwa?"



"Kuwa upo Bagamoyo kikazi!"

"Ndiyo nipo kikazi na hapa wafanyakazi wenzangu wengine wapo ndani!"

"Hata miye naona maana kuna mfanyakazi mwingine wa kike nimemuona umetoka naye na kumuangushia mabusu kisha akaondoka na bajaj!"

"Unasemaje Juliana?"



"Mfanyakazi mwenzenu wa kike nimemuona tena mnashikana hadi viuno?"

"Acha kunikosea mpenzi hebu kwanza twende tukakae kwanza pale tupate japo kinywaji!"

"Hapana nataka twende ndani!"

"Ndani kuna wafanyakazi wenzangu."



"Ndiyo vizuri ukawatambulishe kwangu au vibaya?" Juliana alikuwa akicheza na akili ya Bitungu kwa makusudi. Alikuwa ameshaujua mchezo mzima hadi chumba walichokuwa wakicheza mechi ya mchangani.

"Haya twende lakini..."



"Hakuna lakini Bitungu miye ndiye mpenzi wako wa pekee hao wengine si wafanyakazi wenzako?"

"Ndiyo!"

Kitendo cha Bitungu kuongozana na Juliana hadi chumbani, Juliana alimuwahi na kumsukuma hadi kitandani na kuanza kumshambulia kwa mabusu kadhaa. Wakiwa katika mahaba mazito mara simu ya Bitungu ikaita...







Kabla Bitungu hajaipokea ile simu, Juliana akawa ameiwahi na kuishika huku akitaka kubonyeza kitufe cha kupokelea.?Nooo! Nipe simu yangu mpenzi!?

?Hapana sikupi mpaka nijue anayekupigia.?



?Sasa sweet tumefikia huko! Najua tu watakuwa ni wafanyakazi wenzangu tu, nipe pliiz!?

?Hata kama!?

?Nipe basi!?



?Nimekwambia sitaki, embu kwanza.?

Juliana alikuwa wa kwanza kujua aliyekuwa akipiga simu ile ya Bitungu. Jina ambalo lilikuwa limeseviwa katika ile simu lilikuwa limemshtua vilivyo. Alichokifanya ni kuangalia tena ile namba mara mbilimbili na kugundua kuwa ni mama yake ndiye aliyekuwa akipiga, akaikata kisha akampa Bitungu.

?Shika lisimu lako!?



Harakaharaka Bitungu aliichukua na kuangalia aliyekuwa akipiga lakini kabla hajapokea ikawa tayari imeshakatika. Hasira zikamshika baada ya kugundua aliyepiga ni mama Juliana, akabaki akimtolea macho Juliana kwa hasira.

?Umeridhika sasa!?

?Kwa kipi hasa??



?Si umekata simu ya mfanyakazi mwenzangu!?

?Mfanyakazi mwenzako??

?Ndiyo! Unajua alichokuwa akitaka kuniambia??

?Ujue mpenzi sipendi kabisa nikuudhi na hata wewe uniudhi.?

?Kumbe unajua hilo! Kwa nini uniudhi??

?Nisamehe basi!?



?Haya nimekusamehe, tupumzike basi!?

?Bitu...?

?Niambie!?

?Mi sitaki kupumzika bwana! Natamani nikukumbatie muda wote tu!?

?Najua mpenzi lakini leo tulikuwa na kikao cha muda mrefu, hapa nilipo nimechoka sana mgongo kwa kuinama kuandika. Acha tupumzike kwanza na hata akili yangu haijakaa sawa...

?Hivi kweli Bitu unanipenda??

?Ndiyo kwani vipi??



?Hapana mtu unayempenda huwezi kumwambia hivi!?

?Lakini...

?Lakini nini??

Wakiwa katika maongezi huku Bitungu akiwa hana dalili ya kucheza mechi ya aina yoyote kutokana na uchovu aliokuwa ameupata baada ya kumaliza kucheza mechi ngumu ya mchangani na mama Juliana. Kila akijaribu kujiweka vizuri ndiyo kwanza alikuwa akichokozwa na Juliana.



?Ujue Bitu... nahitajika kurudi nyumbani na hii yote nimekuja kwa ajili yako kwa nini unifanyie hivi... kwa nini uutese moyo wangu jamani, nielewe mpenzi...?

?Sweet, nakuomba kesho uje nitakuwa free kabisa!?

?Basi hata mara moja nirudi nyumbani inatosha!?

?Mara moja nini??

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

?Mara moja umuagize mwanajeshi wako afanye mashambulizi.?

Bitungu aliendelea kuwa mgumu hali iliyomfanya Juliana aendelee kuumia zaidi kila akikumbuka alivyokuwa akishuhudia mechi kati ya Bitungu na mama yake.



Mechi waliyokuwa wakiichezea mchangani tena wakiwa na jezi. Baada ya kusumbuana kwa muda, Bitu aliamua kumkubalia Juliana ambapo alimuweka sawa na kuanza kufanya mashambulizi ya kupima uwezo wake wa kulicheza gwaride kabla hajavua rasmi magwanda na kuingia vitani.

***

Usiku ulizidi kuingia. Hadi inafika saa mbili za usiku si mama Juliana wala Juliana waliokuwa wamefika. Siku hiyo baba Juliana alijuta kurudi mapema kwani tangu saa kumi na mbili za jioni alikuwa nyumbani akiwasubiri. Homa aliyokuwa akiisikia ilimfanya kuachana na pombe siku hiyo na kuwahi kurudi ambapo alikuta milango yote ya nyumbani kwake ikiwa imefungwa. Hatimaye mama Juliana akatokea na kumkuta mumewe akiwa amekaa kibarazani kwa hasira.



?Umetoka wapi sasa hivi??

?Baba Juliana ndiyo salam kweli hiyo??

?Sitaki salam, kunigandisha muda wote na simu umezima ndiyo nini??

?Simu imezima??

?Ndiyo! Umeamua kunizimia simu siyo??

?Hapana sijazima simu, siyo hii hapa iko on??

?Sipendi upumbavu mama Juliana, haya nifungulie mlango.?



?Kwani umefungwa? Nilimuacha Juliana, au atakuwa ndani amepitiwa na usingizi??

?Angekuwa amelala tangu saa kumi na mbili si angenifungulia, nimegonga mpaka nimechoka. Ujue msiniletee ujinga!?



?Hapana mume wangu, miye funguo zangu za akiba zote niliziacha nikijua nimemuacha Juliana na nilimwambia kuwa asitoke narudi naelekea kwenye vikoba.?



?Leo mtaniambia vizuri mlikuwa wapi, haiwezakani mnifanyie ujinga wa namna hii kwa kunigandisha, kumbe siku zote ninazochelewaga kurudi nyumbani mnajiachia namna hii siyo??

?Hapana mume wangu!?

?Hapana nini??



Mama Juliana alijitahidi kudanganya lakini ndiyo kwanza baba Juliana alizidisha ukali. Hakutaka kusikia lolote zaidi ya kufunguliwa kwanza mlango halafu aelezwe ukweli juu ya Juliana alipo. Woga ulishaanza kumshika huku akitetemeka mwili asijue afanye nini ili mlango ufunguke, akili ya haraka aliichukua simu yake na kutaka kutoka eneo lile.



?Embu ngoja niiulizie hapa jirani kwa mama Latifa,?

?Uulizie nini wakati kote nimeshaulizia wamesema hakuna ufunguo na mtu wa mwisho kuonwa akitoka alikuwa Juliana.?



Mama Juliana aliishiwa pozi, ujanja wote wa maneno ulikuwa umeshamwishia, alishindwa kujiongeza zaidi ya kuamua liwalo na liwe. Aliichukua simu yake na kuanza kumpigia Juliana kwa papara huku akiiweka loud spika ili wote wajue eneo alipo.





Mikono yake ilionyesha wazi kutetemeka hasa maeneo ya vidoleni, muda wote baba Juliana alikuwa pembeni yake akimuangalia tu. Simu iliita mpaka ikakata yenyewe, akajaribu zaidi ya mara mbili lakini bado haikupokelewa.



?Sasa atakuwa ameenda wapi Juliana huyu??

?Hayo maswali usiniulize mimi, ninachotaka kwanza mlango ufunguliwe kisha ndo mnijibu vizuri kwa nini mnaondoka tena na funguo zote!?

?Jamani baba Juliana! Si nilishakwambia funguo zangu zipo ndani!?

?Fungua sasa!?

?Nitafunguaje??



Baba Juliana bado alikuwa na hasira kali. Alichokifanya ni kujisogeza kwenye ukuta na kutaka kukaa kwa mara nyingine, kabla hajakaa wazo likamjia. Akajiongeza!

?Naenda kumuita baba Latifa!?

?Wa nini??



?Aje aubomoe tu huu mlango!?

?Halafu ukishabomolewa??

?Tunaingia, anaurudishia!?



?Jamani baba Juliana embu kuwa mvumilivu basi hata kidogo, Juliana kama ametoka si atakuja kuliko kuanza kumuita baba Latifa aje avunje.?

?Ndo nishasema sasa!?

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Baba Juliana hakutaka kusikia lolote zaidi ya kunyanyuka na kuongoza moja kwa moja mpaka kwa baba Latifa ambapo alimkuta na baada ya dakika chache alirudi naye kwake akiwa na vifaa vyote vya kubomolea mlango.



?Fanya uwezavyo, uvunje tu tuweze kuingia halafu utaurudishia!?

?Haina shida bosi!?

?Hapana baba Latifa, Hapana usiuvunje!?

?Wee mwanamke! Embu muache baba Latifa auvunje huo mlango.?

?Baba Juliana kwa nini hutaki kunisikiliza mkeo!?



?Mimi si ndo baba Juliana, baba mwenye nyumba? Haya fundi vunja nimesema na kama pesa nakulipa mimi wala si huyu mwanamke??







ITAENDELEA

NI SHIIDA! - 3

 






Chombezo : Ni Shiida!

Sehemu Ya Tatu (3)





"Una uhusiano na nani?"

"Mimi?"



"Wewe ndiyo, mwingine nani?"

"Sina."

"Si kweli. Ile hereni ilikuwa pale iko wapi?"

"Hereni gani?"

"Pale chini palikuwa na hereni sasa hivi haipo, we umeiokota. Na ndiyo nathibitisha kwamba kweli wewe ulikuwemo ndani."

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Hapana, siijui mbona."

"Nikupapase?"Bitungu hakutaka kupapaswa kwani ni kweli aliiweka hereni hiyo kwenye mfuko wa bukta.

"Ina maana huniamini baby?"

"Ndiyo sikuamini. Tena kuna kitu nafuatilia kama ni kweli mimi na wewe basi."

"Kitu gani tena baby jamani?"

"Nakijua mwenyewe."

***

Mama Juliana alihisi dakika zinakatika binti yake hajarudi, akampigia simu.

Juliana alishtuka sana kuona simu ya mama yake ikiingia kwenye simu yake…

"Huyo ni mama, please naomba subiri kwanza kufanya lolote lile kwa sasa," alisema Juliana ili apokee simu hiyo…



"Mama…"

"Uko wapi wewe?"

Ili ajulikane yupo njiani anatembea, Juliana aliwahi kwenye dirisha na kuongelea hapo ili kelele za nje ya gesti hiyo ziingie kwenye simu na kumfikia mama yake…

"Mama natembea nakuja."

"Na huyo Bitte?"



"Hapana mama, nimemkuta ana kazi nyingi sana lakini atakuja kesho asubuhi sana."

Mama alikata simu, Juliana akamgeukia Bitungu…

"Naomba hiyo hereni Bitungu please."

"Yaani dear hayajaisha tu?"



"Hayawezi kwisha labda uamue kuwa wazi kwangu kuhusu mwanamke aliyekuwemo ndani na uhusiano wake na hiyo hereni uliyoiokota."

"Sikia nikwambie ukweli baby wangu…"

"Nakusikiliza."



"Ni kweli nilikuwa na mwanamke kabla yako. Lakini ni yule mke wa mtu niliyewahi kukwambia kwamba ananing'ang'ania mimi simtaki."

"Ulikuwa naye humu ndani ya chumba hiki?"

"Ndiyo."



"Mnafanya nini?"

"Yeye alichukua hiki chumba, akaniita akisema anataka kunipa kazi nimfanyie ili anipe pesa lakini si suala la mapenzi."



"Amekupa hiyo kazi?"

"Ndiyo.""Kwanza huyo mwanamke anaitwa nani?"







?Mh! Jina lake linanitokaga sana.?

?Kwa nini ushindwe kumjua mtu anayekufuatafuata kila wakati mpaka mnaitana gesti??

?Imetokea tu.?

?Anaishi wapi??

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

?Mwenyewe anasemaga Ilala.?

Moyo ulimlipuka Juliana, alianza kuuona ukaribu wa mama yake kutembea na Bitungu. Alitamani sana kumuuliza lakini alishindwa, akaendelea kutumia maswali ili kumchimba kwa undani.

?Umewahi kufika nyumbani kwake??

?Sijawahi.?

?Ni Ilala gani??

?Sijui Ilala gani!?

?Yukoje??



?Mwanamke f?lani hivi hajatulia ndiyo maana mimi namkataa maana najua nitaangukia pabaya.?

?Ameolewa??

?Hapana, shangingi tu,? alijibu Bitungu kwa kukwepesha ukweli kwani alijua akikubali kwamba ameolewa, ataonekana anacheza na hatari kwa wake za watu lakini hakujua kama jibu hilo lilipunguza kiwango cha mawazo cha Juliana kutaka kumhusisha mama yake.

?Kwa hiyo humu chumbani ulikuwa na huyo mwanamke wako??

?Ndiyo.?



?Umesema ndiye aliyekodi chumba??

?Yes baby.?

?Kwa hiyo mimi umeniingiza kwenye chumba alichochukua mwanamke mwenzangu siyo??

?Juliana, punguza hasira mama, punguza maswali pia, usimuwazie sana huyo malaya, wewe shughulika na mimi tu, mimi ni mumeo mtarajiwa Juliana, mtoto mzuri kama wewe unataka kujilinganisha na mwanamke mtu mzima, mzee yule.?



Maneno hayo yalimpa faraja kubwa Juliana, akajijua tena kwamba kumbe yeye ni mzuri sana na anapendwa pia kumbe anaweza kuwa mke wa mtu ndoto ambazo zimekuwa zikimkaa kichwani muda mrefu kwamba atafurahi sana siku moja atakapobahatika kuolewa na kuwa nyumbani kwake.

Kwa mbali, Juliana alianza kuchangamka huku akipeleka mkono wake kumshikashika mwilini kijana huyo na kuachia tabasamu, akasema?



?Lakini ujue baby mimi ni msichana mwenye wivu mkubwa. Kwa hiyo uwe unaangalia unapotaka kunitenda kwani utakuwa unaniumiza sana.?



?Miye wala sikutendi mpenzi wangu, unajua kama ningekuwa na nia mbaya nisingekuita uje hapa.?

Bitungu naye baada ya kumwona Juliana amelegeza uzi aliitumia nafasi hiyohiyo kuhakikisha wanaangukia kitandani na kuanza mechi ya haraka maana dakika zilikuwa zimekatika sana.

?Jamani, nitalala mwenyewe,? alisema Juliana wakati akipelekwa kitandani?

?Si nakusaidia tu baby wangu jamani na wewe!?



?Nitajisaidia mwenyewe jamani sweet,? alilalamika Juliana kwa sauti isiyokuwa na msisitizo, akaenda kitandani na kuangukia puu!



Macho yalishamlegea, sehemu kubwa ya mwili wake ikawa kitandani huku akianza kuongeza mhemo na mhemko wake. Hali ilikuwa mbaya kwa Juliana?

?Baby njoo basi, si umenitanguliza mwenyewe,? alisema Juliana kwa sauti tamu, sauti nzuri, sauti ya kumtoa mwanajeshi kwenye handaki.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Juliana huyohuyo alimvuta Bitungu kitandani na kuanza kumvua bila kujali tabu zake. Bitungu naye alikuwa akijipindapinda, akijinyonganyonga ili kuruhusu nguo zake kutoka mwilini wakati wa kuvuliwa.

Wote wakawa kama walivyozaliwa, Juliana alimwangalia Bitungu kwa macho malegevu sana, kusinzia si kusinzia, kulala si kulala?

?Baby,? akaita?

?Yes dear.?



?Nakupenda,? alisema Juliana kwa sauti iliyotoka nje kwa kupitia tundu za pua?

?Hata mimi baby nakupenda pia.?

?Kweli baby?? aliuliza Juliana akipeleka mkono na kushika maiki ambapo alianza kuimba nyimbo nzuri za mapenzi huku macho yake yakimwangalia Bitungu usoni hali iliyomchanganya kijana huyo na kujikuta akitetemeka kwa kiu ya kulisataka kabumbu.

?Baby,? aliita tena Juliana?

?Yes??



?Mimi tayari.?

?Tayari nini sweet wangu??

?Aaah! Bwana, unajua namaanisha nini!?

Bitungu alimtega vizuri Juliana na kuanza naye soka huku akitembeza mikiki ya mbali na kumfanya Juliana kuhema sana na kutoa mlio wa kubembeleza kwa mbali.



Kitu kimoja ambacho alikisahau Juliana ni kuacha simu yake palepale kitandani hivyo akailalia. Sasa wakati makasheshe yakiendelea, aliiminya na mgongo, akajikuta anabonyeza vitufe mpaka akafika eneo la namba ya mama yake ambayo alimpigia yeye kwenye ?received call?.

Mama Juliana aliipokea haraka simu ya binti yake akijua huenda kuna tatizo kwani walishatoka kuongea muda mfupi tu uliopita?



?Huyu anasemaje tena?? alijiuliza mwenyewe akiwa anaipokea bila kujua kwamba upande wa Juliana, simu hiyo ilijipiga yenyewe.

?Haloo?? alipokea na kuita?

?Haloo??

?Halooo?wee Juliana!?

Mama Juliana alishtuka wakati akiita kwenye simu, upande wa pili alisikia maneno haya?

?Baby?baby jamani?oooo?.baby??

Alisimama?



?Wewe Juliana??









"Juliana si naongea na wewe?"

"Halooo..."

Alihisi presha ya ajabu kumtembelea, hakutaka kuamini kile alichokuwa akiendelea kukisikia kwenye simu.

Muda wote Bitungu na Juliana bado walikuwa katika mechi ngumu, mechi ilikuwa imeshawazidia kwani tayari walikuwa wamefungana mabao ya kutosha na wapo katika mapumziko ya kipindi cha pili.



Juliana hakushtuka kama ile simu ilikuwa imempigia mama yake, ndiyo kwanza aliendeleza mahaba kwa Bitungu.

"Baby..."



"Sema mpenzi wangu..."

"Tupumzike tuendelee basii, ila leo umeniweza kweli!"

"Tena una bahati leo!"

"Bahati? Bahati wapi wakati kawaida yangu kumaliza mechi na ushindi."



Wakiwa katikati ya maongezi, Bitungu akaiona simu kwa Juliana, simu ambayo Juliana alikuwa ameikalia bila kujitambua kuwa imejipiga na mbaya zaidi imempigia mama yake.

"Mpenzi mbona umeikalia simu..."

"Simu? Simu ipi?"



"Ina maana huijui simu yako, au si ya kwako hiyo?"

Harakaharaka Juliana alijisogeza na kuichukuwa ile simu yake, ilikuwa bado iko hewani kwani maneno yote mama yake alikuwa bado anaendelea kuyasikia. Juliana akaanza kutetemeka sambamba na kuumana meno. Akaikata simu ile na kuanza kuangua kilio kana kwamba yupo msibani.

"Nini tena sweet?"

"Hapana..."



"Hapana nini?

"Niache kwanza, niache tu..."

"Siwezi kukuacha sweet wangu wakati umeiangalia simu yako na kuanza kulia kama ni msiba nijuze kuliko kupeana presha..."

"Bora ingekuwa msiba Bitungu..."http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



"Ila! Nini sasa kinachokufanya uendelee kulia tena kwa sauti ya juu hapa na unajua hapa ni gesti?"

"Bitungu, yale yote tuliyokuwa tunafanya na kuongea mama ameyasikia!"

"Unasemaje?"

"Mama ameyasikia yote!"



"Sweet ina maana hukuweka loki kwenye simu yako?"

"Hapana! Wakati tupo kwenye mechi simu yangu ilijipiga yenyewe bila kujua, mama akapokea na kusikiliza yote..."

"Kwa hiyo ndo ameshajua kila kitu.."

"Ndiyo amesikia Bitungu!"



"Ahhh! Haiwezekani sweet, mama yako amesikia kila kitu?"

Bitungu alihisi kuwa mdogo kama piritoni, bado alikuwa mtupu kama alivyozaliwa, mzuka wote wa kuendelea na mechi ukawa umekwisha rasmi, alichokifanya alitupa shuka upande wa pili huku ghadhabu ya hali ya juu ikiendelea kumtoka...

"Lakini..."



"Lakini nini niache kwanza Bitungu..."

"Unatakiwa kwanza tuyazungumze na kupanga jinsi ya kumwambia mama yako..."

"Bitungu unajua kabisa kitumbua kimeshaingia mchanga hapa na hakuna cha kukipangusa, ni bora kiliwe hivyohivyo tu!"



"Una maana gani Sweet?"

"Mambo yameshaharibika hapa, si salama tena!"

"Ngoja, ngoja! Tuliza kwanza jazba."

"Hapana Bitungu... hapana!"



Juliana alikuwa hataki kusikia lolote, ile raha ya mechi iliyokuwa imemtembelea aliona kama moto, moto tena ule wa kuni. Alitamani ardhi ipasuke atumbukie pengine angefarijika.



Alichokifanya, alichukua nguo zake zote na kuanza kuvaa moja baada ya nyingine huku akiendelea kulia kwa sauti ya juu iliyochanganyika na kwikwi. Muda wote Bitungu alikuwa akimtazama tu pasipo kumsogelea karibu, alishajiona ni mkosaji wa hali ya juu kwa kuwachanganya.



Ndani ya muda mfupi, Juliana alikuwa ameshamaliza kuvaa nguo, kitendo cha kuweka nywele zake sawa, mara simu yake ikaita tena."Ona sasa! Mama anapiga simu tena!"

"Sasa?"



"Sasa nini? Ndiyo hivyo anapiga tena..."

"Cha kufanya simu yake usipokee iache kama ilivyo..."

"Hapana Bitungu ni bora nipokee pengine hasira zake zitakwisha maana namjua mama yangu kwa hasira!"



"Juliana! Juliana nisikilize kwanza ninavyokwambia!"

Juliana alitii yale aliyokuwa ameambiwa na Bitungu, hakuipokea ile simu ya mama yake, aliiacha ikaita hadi ikakata yenyewe. Alitoka nje ya ile gesti na kuongoza moja kwa moja nyumbani kwao huku akimwacha Bitungu akimalizia kuvaa nguo mule ndani. Hakuwa Juliana wa kawaida kwa jinsi alivyokuwa amechanganyikiwa akili mpaka mwili.



Muda wote Mama Juliana alikuwa ametulia nje ya kibaraza amefura kwa hasira akimsubiri Juliana, alishaujua mchezo wote aliokuwa anachezewa. Kitendo cha kuonana uso kwa uso na Juliana hasira zikamzidia.

"Juliana?"



"Abee mama! Shikamooo!"

"Sitaki shikamooo yako!"

"Niambie ulikuwa wapi?"http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



"Mama nisamehe nilikuwa..."

Kabla Juliana hajamalizia kujibu alishangaa kupigwa vibao mfululizo kutoka kwa mama yake.

"Usifikiri sijui chochote, najua kila kitu, niambie ukweli ni nani ulikuwa naye gesti...







Kifupi ni kwamba, mama Juliana alimsikia mwanaume akizungumza lakini hakujua kama ni Bitungu, ila kilichomshangaza sana ni kubaini kumbe binti yake ameanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume.



"Mama nisamehe."

"Niko tayari kukusamehe, niambie ulikuwa na nani?"

"Nilikuwa na kijana mmoja hivi."

"Anaitwa nani? Hana jina?"

"Mama mi simjui jina lake."



"Wee, koma kama ulivyokoma kunyonya kwenye ziwa langu, uingie na mwanaume gesti halafu uwe humjui jina?"

Juliana aliamua kumdanganya mama yake akiamini si vizuri kumtaja jina Bitungu...

"Anaitwa Sylvester."

"Anaishi wapi?"

"Kigamboni."



"Mmeanza uhusiani tangu lini?"

"Siku ya tatu leo."

"Umeshalala naye mara ngapi?"

"Mara ya kwanza leo."

"Ina maana amekutoa usichana wako?"

"Hakuweza mama."



"Kwa sababu gani asiweze?"

"Hakuweza tu."

"Unataka nikukague?"

"Hapana mama."



"Sasa kwa nini unanidanganya?"

"Sikudanganyi mama."

"Kwanza hebu niambie, hiyo gesti iko wapi?"

"Ipo Sinza."

"Ipo Sinza? Ina maana wewe hapo muda huu unatokea Sinza?"

"Ndiyo mama."



"Sinza sehemu gani?"

"Mimi siyo mwenyeji sana wa Sinza mama," alijibu Juliana bila kujua kuwa, mama yake alitaka kujua Sinza sehemu gani kwa sababu na yeye alitoka huko muda si mrefu....

"Shekilango unapajua?"

"Ndiyo mama."



"Ukitoka Shekilango ni kituo cha ngapi?"

"Sikumbuki, nilikwenda na bodaboda."

"Hebu nenda ndani haraka sana. Usije ukarudia tena," alisema mama Juliana huku akiiseti simu yake vizuri ili kumtwangia Bitungu. Lakini huku akiwaza...



"Isije ikawa alikuwa na Bitungu! Halafu isijekuwa Bitungu ndiyo yule Bitu wa kwenye simu yake akasema ni Bitte alikosea kusevu? Huyu mtoto isije ikawa anatuchanganya mimi na mwanangu?

"Lakini haiwezekani. Kwa mechi tuliyoicheza leo pale kitandani sidhani kama angeweza kumudu mchezo mwingine tena."

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Simu ya Bitungu ilipokelewa, mama Juliana akaanza kumuuliza maswali...

"Baby, wewe ni msaliti kwangu siyo?"

"Wala, kwa nini baby?"

"Huna mpenzi mwingine kweli wewe?"

"Wala! Nani amekwambia?"



"Sijaambiwa na mtu, nawaza mwenyewe tu."

"Ondoa hayo mawazo mpenzi, mimi ni wako peke yako."

"Kweli mpenzi wangu?"

"Kabisa mpenzi."



"Basi nimefurahi sana kusikia hivyo," alisema mama Bitungu na kukata simu. Roho yake ikawa imefarijika kwa siku hiyo.



***

Asubuhi ya siku iliyofuata, Juliana aliamka akiwa na wogawoga wa kuonana na mama yake ana kwa ana. Lakini alipokumbuka kuhusu ile hereni aliyoiona gesti akiwa na Bitungu ambayo ni moja kati ya hereni alizomnunulia mama yake, aliamua kuanza upelelezi wake hapo.



Kwanza alimvizia mama yake amekwenda kuoga, yeye akazama chumbani maana baba yake naye alishakwenda kazini mapema.



Alifungua kwenye kikopo ambacho mama yake anakitumia kuwekea hereni zake, hakuona hereni hata moja. Akaangalia juu ya dressing table, akaiona hereni moja tu, akatingisha kichwa huku akisema moyoni...



"Ile niliyoiona gesti hii mwenzake, kwa vyovyote vile. Ina maana mama ndiye mwanamke aliyekuwa na Bitungu gesti...itakuwa yeye na ndiyo maana alinibana kuhusu Sinza sehemu gani niliyokuwepo mimi," alisema moyoni Juliana huku akichomoka kutoka chumbani humo.



Aliendelea na mambo yake mengine lakini kuanzia muda huo akawa hamwogopi tena mama yake kufuatia kubaini uozo wake na Bitungu.



Jiliana alianza kufanya utafiti wake kwa kutumia akili ya kujiongeza. Aliamua kwamba siku mama yake akitoka na yeye atoke, amfuate kwa nyuma kwa siri mpaka atakapoingia na yeye aingie.

Lakini pia aliamua kuendelea na uhusiano na Bitungu akiamini kwamba, atatumia akili yake ya ziada ili kijana huyo ammwage mama yake.







Akili ya kujiongeza aliyokuwa nayo Juliana ilikuwa ni kuhakikisha kila mama yake anapopigiwa simu yupo pembeni akisikiliza japo kwa kujificha. Alishajitoa mhanga kwa lolote...

"Haiwezekani hata siku moja, kama kula tutaendelea kula wote tu, lakini kwa nini mama anizidi akili? Hata kama ni mama yangu haiwezekani!"



Maisha ya Juliana na mama yake bado yalikuwa ya kuwindana, Juliana hakutaka kumuachia mama yake hata sekunde, kila simu ilipokuwa ikipigwa Juliana hakosi, kama siyo pembeni yake basi atakuwa eneo hilohilo akisikiliza ni nani amepiga.

Siku moja Juliana akiwa katika kufanya usafi katika chumba cha mama yake alisikia simu ya mama yake ikiita, kipindi hiki mama yake alikuwa bafuni akioga.

"Juliana!"



"Abee mama"

"Niletee simu yangu!" Mama Juliana alikuwa tayari ameshaisikia simu yake ikiita, akili yake ilishajiweka ni lazima atakuwa Bitungu, hakutaka hata kidogo Juliana aishike lakini kutokana na kujua kuwa yupo chumbani kwake karibia na hiyo simu akifanya usafi ikambidi amuagizie tu.

"Mbona huji?"

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Nakuja mama, halafu simu yenyewe imeshakata!"

alisema Juliana huku akihema na kusogelea eneo la bafuni alipokuwepo mama yake, jina la kwenye simu iliyokuwa ikiita kwa mama yake lilimkera sana kiasi cha kuamua kuikata kwa makusudi, alikuwa ni Bitungu.

"Shika mama, lakini imeshakatika"

"Alikuwa nani?"



"Hata sikuangalia mama, nadhani atapiga tena!"

"Unadhani? Embu nipe huko!"

Alisema mama Juliana kwa jazba huku akishika simu ile na mapovu ya sabuni mkononi sambamba na majimaji. Harakaharaka akaangalia ‘missed call' lakini hakukuwa na jina alilodhani zaidi ya kukutana na jina la Mama Zai.







ITAENDELEA

NI SHIIDA! - 2

 






Chombezo : Ni Shiida!

Sehemu Ya Pili (2)





Bwakila aliamua kusamehe na kumpa onyo kwamba akirudia tabia ile sehemu nyingine atajikuta

akibakwa…"Ni kweli mwanangu maneno yako," alisema mama Juliana akitoka na jasho jembamba.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Alikwenda kubisha hodi kwenye mlango mwingine, akafungua mtu mzima f'lani, alipokutana macho na mama Juliana, mtu mzima huyo akaanza kuachia tabasamu…

"Ni wewe?" aliuliza yule mtu mzima fulani…



"Aliye?" alihoji mama Juliana akidhani labda mtu huyo yupo ni Bitungu…

"Tuliyekuwa tukiwasiliana kwenye Facebook, si tumekubaliana kukutana hapa?"

"Akha!" mama Juliana akaondoka hapo, akaenda kugonga mlango chumba kingine ndiyo akatokea Bitungu sasa.



Mama Juliana aliingia ndani na kuangukia kitandani huku akichuruzika machozi…

"Vipi tena?" alihoji Bitungu…"Kidogo nibakwe."

"Kidogo ubakwe! Na nani?"



Mama Juliana alisimulia kisa chote kuanzia kuzimikiwa na simu na yaliyompata ndani ya gesti ile.

"Duu! Pole sana.""Kiranga chote kimeniishia," alisema mama Juliana huku akijifuta machozi na kumkumbatia kijana huyo kama anayasema ‘afadhali nijipoze na wewe sasa'.



Bitungu alichoshwa sana na majambozi ya Juliana mwenyewe, sasa mama mtu kufika pale naye akawa anataka kwa sehemu yake.Alimchombezachombeza kijana huyo kwa kumshikashika sehemu mbalimbali za mwili ili kumchajisha na huku akimbembeleza kwa maneno matamumatamu ya mahaba…

"Bitungu…"



"Naam…"

"Unajua wewe ulitakiwa uwe mume wangu?"

"Kweli mpenzi?""Kweli kabisa. Wewe unadhani nani alistahili kuwa mume wangu miye?"

"Ni mimi mpenzi."



"Kumbe unajijua, yaani nakupenda wewe mpaka basi jamani," alisema mwanamke huyo mtu mzima huku akiwa anashughulika na kipaza sauti.Ilifika mahali Bitungu akachaji, kila kona ya mwili wake ikakaa sawasawa kwa mechi ya kirafiki isiyokuwa na refa.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Leo nataka njia ile nyingine," alisema Bitungu lakini mama Juliana akakataa…

"Mimi nataka njia ya siku zote mimi na wewe," alisema mwanamke huyo huku akimfosi kijana huyo kuanza mpambano kwa kumwingiza mwenyewe uwanjani.



Ulikuwa mpambano wenye kumwelemea Bitungu kwa namna yoyote ile. Alionesha uchovu wa waziwazi mpaka mwanamke huyo akamuuliza…"Mpenzi leo vipi, umevurugwa na nani kabla yangu?" aliuliza mama Juliana lakini kabla hajajibiwa, simu ya Bitungu iliita.



Kwa kuwa pozi lao la muda huo, mama Juliana ndiye aliyekuwa upande wa stuli yenye simu, aliichukua na kuiangalia skrini kidogo aliyepiga huku akiipeleka kwa Bitungu. Kwenye skrini ilionekana jina Julie…



"Ah! Nitampigia baadaye," alisema Bitungu akikata simu hiyo kisha kuizima kabisa…

"Julie ndiyo nani?" mama Juliana aliuliza akiwa amebadilika sura ghafla.

"Mtoto wa shangazi yangu bwana, anataka nimtafutie kazi."

"Mh!"



"Mbona umeguna?"

"Nimeguna maana na mimi nina mtoto anaitwa Julie," alisema mwanamke huyo akimaanisha kifupi cha Juliana ni Julie lakini Bitungu akampuuza na wala hakutaka kujiongeza kwamba pengine Julie wa mwanamke huyo ndiye Juliana anayemjua yeye.



Aliamini Julie si Juliana akafurahi moyoni kwamba, amemchenga mwanamke huyo kwa kumsevu Juliana kama Julie…"Mbalimbali, huyu ni Julie mtoto wa shangazi yangu. Labda wewe ndiyo uwe huyo shangazi yangu," alisema Bitungu…



"Naweza kuwa, maana hata mimi Julie wangu anatafuta kazi," mama Juliana alitia neno kidogo likamwingia Bitungu kwani ni kweli Juliana alimwambia anatafuta kazi wakati wamekaa baa walipokutana kabla ya kwenda gesti.



Ikumbukwe kwamba wakati wanayazungumza hayo walikuwa wakiendelea na mechi kama kawaida kwa kutumia njia ile ya mama Juliana na si ya Juliana mwenyewe.



Mama Juliana ndiye aliyeanza kutangaza kupata ushindi kwani Bitungu alikuwa mchovu kwa wakati huo.

Ilishindikana kabisa kwa Bitungu kukamilisha ngwe ya safari yake na hivyo kutoka uwanjani akiwa ameshindwa kukomboa.

***

Ilikuwa siku ya pili, simu ya Juliana iko mezani sebuleni, mama yake akiwa anapita hapo, mara simu hiyo iliita, akaangalia kwenye skrini huku akimwita Juliana mwenyewe…

"Simu yako inaita huku wewe…Bituu," alisema mama Juliana.



Juliana alifika akiwa mbio na kuhema juu…

"Bituu anapiga."Juliana aliichukua simu na kwenda mbali…

"Haloo…sijambo…niko nyumbani mbona…haya sawa…haya."

Baada ya kukata simu, mama Juliana aliita…

"Juli…"



"Abee mama."

"Bituu ni nani?"

"Siyo Bituu mama, nilikosea kusevu tangu mwanzo, ni Bitte."

"Ndiyo nani?"



"Nilisoma naye kule chuo mama."

"Hebu namba yake," alisema mama Juliana huku akinyoosha mkono kutaka simu ya mwanaye huyo.



http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



Wakati Juliana anampa mama yake simu, mkono ukalegea, ikaanguka chini na kuvunjika kioo…

"Mama simu yangu jamani."

"Mbona umelegea mikono wewe, ala!" alifoka mama mtu. Akaendelea…

"Hakijaaribika kitu, toa laini niweke kwenye simu yangu, nataka kumjua huyo Bitte unayemsema wewe ni nani?"



"Kwani mama wewe umefikiria ni nani?"

"Ndiyo nataka kumjua."

Moyoni Juliana akasema…

"Ungejua si Bitte ni Bitungu…"

Naye mama mtu moyoni akasema…



"Ungejua nafananisha jina hilo na la dogodogo wangu Bitungu."

Juliana alitoa laini, akampa mama yake huku simu yake ikiwa imezima baada ya kuanguka. Naye mama mtu aliichukua laini na kuipachika kwenye simu yake, akawasha. Yalikuja majina mengi sana lakini jina la Bitte halikuwepo. Maana yake ni kwamba, jina liliseviwa kwenye simu yenyewe ‘hand set', au wanasema ‘phone book'.

"Hebu lete simu yako."



Juliana alimpa mama yake simu, akatoa laini na kuipachika humo tena, akawaisha, simu haikuwaka kutokana na kule kuanguka.

Akamtupia simu mtoto wake huku akisema…

"Nitataka kumjua huyo Bitte."

"Sawa mama."



***

Bitungu alishangaa kumkosa Juliana kwa siku hiyo, kila alipompigia ilionekana simu yake imezimwa…

"Huyu leo vipi tena?" alijiuliza kijana huyo.



Juliana alifika kwa fundi na kueleza shida ya simu yake, akaambiwa ni lazima ibadilishwe kioo lakini gharama aliyotajiwa ilimshinda, akaamua kwenda kununua simu ya tochi kwanza.

Hata hivyo, alijua hataweza kumpata Bitungu kwa sababu namba zake ziko kwenye simu iliyokufa kioo.

Alinunua simu, akarudi nayo nyumbani ili kuiweka kwenye chaja kwa muda. Lakini nyumbani hakumkuta mama yake na akashindwa kujua aliko.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Baada ya nusu saa, Juliana alichomeka laini kwenye simu yake ya tochi, akaiwasha. Ndani ya dakika moja meseji kibao zikaanza kuingia mfululizo, ikiwemo ya mama yake akimwambia anatoka kidogo.

Ikaingia nyingine iliyomwonesha kwamba ni ya Bitungu kwani ilisema…



"Baby mbona sikupati hewani? Ujue unanipa wakati mgumu sana mwenzio?"

Juliana aliipiga simu hiyo. Wakati simu inaita, Bitungu alikuwa amekaa na mama Juliana…

"Hebu pokea simu kwanza mpenzi wangu ndiyo tuendelee na mambo mengine," alisema mama Juliana, lakini naye Bitungu alipoona ni Juliana aliogopa. Hata hivyo, ili kuua soo aliipokea huku akipunguza sauti…



"We vipi mbona hupatikani kwenye simu?"

"Simu mbovu my dear, kweli tena!"

"Pole sana, mi nilikuwa sijui."

"Ndiyo hivyo. Uko wapi?"

"Nipo mitaa ya Sinza Palestina, nitakutafuta baadaye."

"Poa."



Baada ya kukata simu, mama Juliana alishangaa kuona simu yake iikimpa mrejesho kwamba meseji aliyotuma kwa Juliana muda fulani ndiyo inamfikia sasa, akampigia…

"Umetengeneza simu?"

"Bado mama, pesa ni nyingi nimeamua kununua simu ya tochi kwanza."

"Sawa, ilimradi simu."

"Uko wapi mama?"



"Nipo maeneo ya Sinza Palestina japokuwa sipendi kuulizwa nilipo na wewe," alisema mwanamke huyo huku akimshikashika mwilini Bitungu. Walikuwa ndani ya gesti.

Baada ya kukata simu, Juliana alijiuliza maswali mawili ya msingi sana…

"Mama anasema yupo maeneo ya Sinza Palestina, Bitungu naye anasema yupo mitaa ya Sinza Palestina. Inawezekana wapo wote?



"Mmh!" aliguna baada ya kukosa jibu na kuamua kuachana na hayo.

Muda ulivyozidi kwenda alihisi kwamba mama yake akirudi lazima atataka kumjua Bitte kwa maana ya kumuuliza maswali mengi. Lakini pia aliisevu namba ya Bitungu upya, akaandika Stella Goms, yaani Stella wa Gongo la Mboto.



***http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Siku hiyo, Bitungu kwa hasira za kumkosa kwa muda mrefu Juliana, msichana aliyempenda sana na furaha ya kumpata baadaye, aliamua kumchakaza mama Juliana kwa mechi kali isiyokuwa na mfano huku akitumia njia ambayo mama Juliana ndiyo anaitaka.



***

Mama Juliana alikuwa sebuleni kwake amechoka sana na mechi ya Bitungu, akamwita mwanaye…

"Abee mama."

"Kaa hapa."

Juliana alikaa sawasawa na maelekezo ya mama yake…

"Bitte ni nani?"



"Mama si nilikwambia nimesoma naye kule chuo."

"Unaweza kumfuata ukamleta hapa?"

"Ndiyo."



"Mfuate haraka sana."

Kwa Juliana zilikuwa habari njema kwani ilikuwa saa kumi na mbili jioni, kupewa kibali cha yeye kutoka Ilala kwenda hadi Gongo la Mboto ni furaha kwake. Alipanga akitoka tu akaonane na Bitungu popote alipo.



Alijiandaa harakaharaka na kuchomoka zake…

"Haya mama nakwenda kumleta," alisema Juliana akiwa na amani jambo lililomshangaza sana mama yake.







"We hebu rudi hapa kwanza," alisema mama mtu. Juliana alirudi huku akionesha sura ya mshangao.

"Mbona umefurahia sana safari ya kumfuata huyo shoga yako asiyekuwa na akili kama wewe?"

"Hapana mama, nipo kawaida tu ila nimefurahi sana kwa sababu najua sina tatizo baya kama unavyonifikiria zaidi ya kwenda kumleta Bitte."

"Haya nenda."



Juliana alisimama kwa mikogo, akaondoka, eti anakwenda kumleta Bitte kwa mama yake kama alivyomuagiza.Juliana alipotoka nje tu, akaweka simu yake sawa na kumtwangia Bitungu…

"Baby mambo jamani?""Poa. Vipi wewe mpenzi wangu? Nimekumisi sana mwenzako."

"Mimi je?"



"Kumbe na wewe umenimisi mpenzi wangu?"

"Sana."

"Uko wapi kwani?"

"Nipo mitaa ya Sinza."



Bitungu aliposema yupo mitaa ya Sinza, Juliana akakumbuka ile hali ya mwanzo ya mama yake kusema yupo Sinza Palestina na Bitungu pia…"Huko Sinza kuna nini leo, halafu hata mama yangu alisema yupo Sinza Palestina leo lakini yeye alisharudi."



"Mimi kuna mtu namsubiri dear," alisema Bitungu akiogopa kusema alikuwa ana mtu angeulizwa ni mtu gani? Si mnajua tena mambo ya wivu."Oke, naweza kukuona leo mpenzi wangu?"

"Wewe tu, si uje.""Oke, nipe kama nusu saa."



Juliana alipanda daladala kwenda Sinza kuonana na Bitungu. Moyoni aliamua kwamba, atakapokuwa kule ampange Bitte kuhusu mama yake. Alitaka amwambie kwamba kesho yake aende nyumbani kwao ana shida naye.

***

Bitungu alimpokea Juliana akiwa baa ambayo pia ina gesti. Na gesti hiyo ndiyo aliyokuwa amechukua chumba akiwa na mama Juliana. Sasa alitaka akae na Juliana pale baa halafu baadaye ajifanye anakwenda kuchukua chumba ndani ili ampeleke Juliana huko kwenye kitanda alicholala na mama yake.



"Baby sasa umekuja kunisalimia tu au na mambo mengine?" aliuliza Bitungu kwa sauti isiyojiamini.

"Na mambo mengine kama yapi?""Kama yapi, mimi si mpenzi wako jamani?"

"Ee, hata kama, mambo mengine kama yapi sasa?"

"Mambo f'lani yale. Ili nikachukue chumba."



Juliana alicheka huu akinywa soda lakini mwishowe akakubali…

"Haya, nimekuelewa, p..."Bitungu hakutaka Juliana amalizie neno oa kwenye poa, akawa ameshasimama kwenda ndani.



Alichokifanya, baada ya kufika chumbani alitandika kitanda vizuri sana kisha akatoka…

"Twende dear, tayari."Juliana alisimama, wakashikana mkono kwenda ndani huku baadhi ya wateja wakiwaangalia kwa macho pima!Waliingia ndani ya chumba hicho lakini Bitungu alipitiliza chooni na kumwacha Juliana amejitupa kitandani.

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Ilikuwa katika hali ambayo hakuitarajia kabisa, Juliana aliona hereni chini kando ya kitanda. Hereni hiyo alivyokumbuka ni moja ya hereni alizomnunulia mama yake miezi miwili nyuma.

"Mh!" aliguna Juliana huku akiiokota. Akajiuliza…"Au mama alipokuwa huku Sinza aliingia hapa nini?"

Lakini alipata wazo kwamba asiichukue, aiache palepale chini ili aone kitakachotokea kama Bitungu ataiona.



Bitungu alitoka chooni kwa kujiamini sana, akakaa kitandani. Lakini na yeye jicho lake likatua moja kwa moja kwenye ile hereni ambapo alionekana kushtuka sana.Kama vile haitoshi, kwa sababu Juliana alilala, yeye alikaa, aliinuka na kuifuata kiaina huku akikumbuka…



"Hii hereni si ndiyo alisema yule mama kwamba ameipoteza, kumbe iliangukia hapa?"

Wakati anaifuata hereni hiyo, Juliana alimwona, akashtuka zaidi kwani sasa alijiridhisha kwamba alichokifikiria ndicho."Lakini huyu si alikuja kuchukua chumba sasa hivi, sasa hereni inamhusu nini? Au na yeye anashangaa kuona hereni ndani ya chumba?" aliwaza Juliana akakaa mkao wa kusubiria atakachosema Bitungu lakini hakikuwepo.



Ghafla Juliana alikosa amani ndani ya moyo wake. Alianza kuingiwa na wasiwasi na hofu ya mambo mengi akivuta matukio kadhaa ya nyuma."Inawezekana mama anatembea na Bitungu? Hilo haliwezekani hata kidogo, yaani Bitungu alale na mimi na mama yangu?"



"Baby vipi?" Bitungu alimuuliza Juliana huku na yeye akipanda kitandani. Juliana alipoitika poa, aliinuka kitandani kiaina na kuangalia ile sehemu aliyoiona hereni, haikuwepo!"Mh!" aligunia moyoni Juliana, alikosa nguvu na raha.



"Baby, mbona kama umekosa raha ghafla?" aliuliza Bitungu akijipendekeza kwa kumshikashika Juliana sehemu mbalimbali za mwili wake."Usinishike bwana, nini?" alikuja juu Juliana. Ni kweli alikosa raha kwani asingeweza kusema maneno hayo kama angekuwa na amani…

"Ha! Ina maana yamekuwa hayo leo mpenzi wangu?" aliuliza Bitungu…

"Ndiyo ee..."



"Kosa langu ni nini..?"

"Unalijua mwenyewe."

Bitungu alijaribu kujiongeza akiamini anaweza kupata mwanga au jibu lakini wapi! Hakuona kosa lake.

Mara, mlango uligongwa na mhudumu, Bitungu akaenda kufungua…

"Samahani kaka, kumbe ni wewe, nilifikiri kaingia mtu mwingine."





http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



"Ni mimi?"

"Lakini ulitoka umerudi tena?" aliuliza mhudumu swali ambalo lilimshtua Juliana pale kitandani.

"Mh! Ina maana kumbe Bitungu alikuwemo humu ndani? Mbona mimi aliniambia anakuja kutafuta chumba alipokipata ndiyo akaniita tuje?" alijiuliza Juliana.



Bitungu hakujibu swali la mhudumu huyo badala yake alifunga mlango tu na kurudi kitandani…

"Baby," aliita Juliana…

"Yes baby…"



"Kumbe ulikuwemo humu ndani?"

"Hapana, amejichanganya yule."

"Mm! atajichanganyaje bwana, we ulikuwemo humu na uniambie ukweli ulikuwa na nani?"

"Baby, mimi sikuwemo humu ndani ya chumba, yule amejichanganya tu, naomba unielewe."

"Hamna bwana, mimi tayari kuna mambo yameniambia ulikuwemo."



"Mambo kama yapi?"

"Wewe unajua mwenyewe."

"Khaa! Mimi sijui mbona."

"Basi yaishe," alisema Juliana na kumfanya Bitungu ajisikie vibaya zaidi kwani na yeye alianza kuhisi kwamba ile hereni aliyoiokota ya mama Juliana ilishaonwa na mrembo huyo ndiyo maana amepoteza furaha kwa ghafla kuliko alivyoingia…



"Yaishije baby wakati najua kwako bado?"

"Yaishe tu! Halafu leo mimi tumbo linaniuma kwelikweli, wala sijisikii kufanya kitu chochote kile," alisema Juliana kauli iliyompotezea dira Bitungu kwani alishajitiuni kwamba anakwenda kushinda mechi ya siku hiyo.



Bitungu ili ajue kama madai ya Juliana ni ya kweli au alitaka kutingisha kiberiti tu, alijifanya kuanza kumshikashika Juliana sehemu mbalimbali za mwili wake huku akimchombezea kwa maneno matamu sana yenye kuchochea mahaba niue!

http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

"Nimesema leo sijisikii kufanya chochote kile si nilishasema mapema lakini baby?"

"Aaa! Juliana, usinifanyie hivyo mimi."

"Mimi sijakufanyia baya lolote lile…"

"Ila..?"

"Basi tu."



"Sasa ikiwa ni hivyo tutafika mbali kweli baby wangu?"

"Hatuwezi," alisema Juliana kwa sauti iliyoendelea kuonesha kuwa, hakuwa sawa kichwani mwake.

Jitihada zote za kutaka kushinda mechi na Juliana ziligonga mwamba kwani mrembo huyo hakuwa tayari kwa njia yoyote ile."Bitungu," aliita Juliana kwa sauti iliyojaa utulivu wa hali ya juu…

"Yes."







ITAENDELEA

Blog