Search This Blog

Sunday, February 26, 2023

BEPARI TIMOTH - 3

   


Chombezo : Bepari Timoth

Sehemu Ya: Tatu (3)


No 18: aliongeza mwendo Tausi ili awafikie, nawaendelee kuzunguka na wake wa boss zake, ambao walikuwa wana tembea tembea maeneo ya kijiji, wakiangalia manzali ya maeneo ya kijiji kile, maana bepari Timoth alijiwa na ugeni mkubwa wa mfalme kutoka UK. Mfalme huyo alikuja kumtembelea kiongozi mwenzake akiwa na mkewake mrembo sana. nandiye aliekuwa anamkodolea macho sana Beko, wakati anaongea na Tausi anaitwa Shadya, ndiye mke wa mfalme kutoka UK, ambae alikuwa akizungushwa na mwenyeji wake mke wa bepari Timoth, Tausi alikuwa pembeni kuakikisha usalama na huduma zinapatikana kwa wakinamama hawa, waliendelea kutembea huku nahuko huku wakizungumza na kucheka kwa vicheko vikali, basi Tausi alikuwa nyuma yao akiwasindikiza, huku naye mawazo yake kwa mpenzi wake Beko, maana leo alivyo mwona walitumia muda mfupi sana kuongea, na ajawai kutumia muda mfupi kamavile, kuongea na mpenzi wake beko. Tausi na maboss wake Walizunguka sana, takiribani msaa 6, huku shadya akifurahia mazingira ya kijiji hicho, na Afrika kwa ujumla, punde walifika kwenye maeneo ya katikati ya kijiji, na kukuta pamechangamka (center) sana, bi Shadya aliendelea kujionea mazingira na madhari ya kijiji hicho, huku akikifurahia sana kijiji hicho, kumbe basi, wakati wanapita . kumekucha sasa ilikujuwa kilichotokea hapo, tembelea hapa kwa mkali




No 19: wakiwa wanaendele kupiga story, basi mke wa bepari timoth akamtuma Tausi maji ya

kunywa, pia kwa mbali wakaona kijana mmoja mdogo wakiume, akiwa anashindana na ng'ombe

dume kubwa(fahari), basi tukio hilo liliimfurahisha sana mke wake mfalme, ambaye ni bi

Shadya, na kupenda kuangalia nini kitatokea, kwa kuwa yeye aliona na nikivutio flani,

kwani hakuwai kuona kitu kamakile kwamacho yake, Shadya na mke wa mzee Timoth, walishuudia

kijana yule akivutwa huku nahuku, akiwa bado ameing'ng'ania kamba, iliyo fungiwa yule

ng'ombe, baada yakushuhudia kwamuda tukio lile ndipo walipo gunduwa kuwa kijana yule

alikuwa amesha choka, akagundua kuwa kijana huyo yupo kwenye matatizo, na aliitaji msahada

wa alaka. vinginevyo yule ng'ombe mkolofi anaweza kuleta madhala makubwa pale mtaani,

nikweli wali shuhudia yule ng'ombe (fahari) akimshinda nguvu yule Kijana, na kutoka kwa

kasi ya ajabu, ambayo ilimfanya yule Kijana kuogopa, kuwa anaweza Fanya ukorofi hapo

kijijini, pia kile kishindo nauelekeo wa ng'ombe, kiliwaogopesha sana shadya na mke wa

bepari Timoth, maana alikuwa anakuja usawa wao, huku wakitahamaki kipi kitaendelea,

wakamwona yule ng'ombe akiongeza mwendo, akiwafata kwa hasira ... kifupi kitamu, tuonane



No 20: Spidi ya yule ng'ombe, ilisababisha vishindo, vilivyosikika kila kona, pale mtaani, huku bado akiwaelekea wale wamama, ambao walichanganyikiwa nakutawanyika, na sasa yulr ng'mbe alikuwa amemlenga bi,shadya licha ya kujitaidi kukimbia janga lisimpate, kumbe alikuwa kaisha chelewa, maana yule ng'ombe alikuwa amesha mkalibia, na punde sipunde, yule ng'ombe alimvamia shadya, na kumdondosha chini, huku mke wa bepari Timoth akipigwa na butwaa, kwakile kilichotokea muda hule. yule n'gombe, hakwenda mbali, aligeuka, tena na kuanza kurudi kwa speed, mala mbili ya ile ya kwanza, akimfwata bi Shadya, watu wotu waliona tukio hilo ,kelele za hofu zilitawala mahala pale,kumbe vile vishindo na kelele, toka mwanzo kabla haja vamiwa, zilimfikia beko, ambae hakuwa mbali sana na eneo lile, mbali sana. aakatimua mbio na kuelekea kwenye eneo la tukio, akakuta bi Shadya akiwa amesha sukumwa na ng'ombe, nasasa yule ng'ombe alikuwa akimfwata tena yule Shadya, ambae alikuwa ameumia sana, hapo beko akaamua jambo la araka sana, dah! nifupi lakini tamu tuonane kesho, mapema sana.... kujuwa kilichotokea



No 21: kama upepo Kijana Beko shupavu, alimfikia nakumdaka yule ng'ombe, na kuanza

kupambana na yule ngo'mbe (fahari) haikuchukuamuda mrefu tayari Kijana Beko, alikuwa

amesha mshinda yule fahari, maana kijiji kizima kilimjua beko, kwa kuwa na nguvu nyingi

(alijulikana kwa jina la Tarzan). alifanikiwa kumnusulu shadya, kitndo cha Beko kuonesha

ushupavua wana kijiji walimpongeza sana na kila mmoja wao alikuwa wakimwagia sifa Kijana

Beko basi Beko alimbeba shady na kumtoa pale alipo kuwa ameburuzwa na yule ng'ombe

(fahari), na kumweka pembeni shadya,tena kuendelea na safari yao ya kuangalia madhari ya

kijijini. Tausi pia alisikitika sana kwa lile tukio lililomkuta shadya, basi mke wa bepari

Timoth na Tausi walichukua jukumu la kumpatia huduma ya kwanza, pale palipo na majeraha,

haya sasa wadau, tukio hilo lilizaa nini? ebu endelea ku fwatilia mkasa huu hapa hapa kwa

mkari wako Mbogo Edgarr, muda mfupi ujao,



No 22: kikweli Beko alijitaidi sana kumwokoa shadya kwenye lile fahari, maana yule ng'ombe (fahari) angemwangamiza shadya, basi beko aliita vijana wenzake ili kumkamata yule ng'ombe na kunusuru maisha ya shadya, huku wakisaidiana na mke wa bepari Timoth ndipo walipomwagiza binti Tausi, kwenda kumuandalia mahari pa kupumzika bi Shadya, maana alipoteza fahamu. Tausi alikimbia upesi upesi na kuanda mahari pa kumpumzisha shadya. Haraka haraka Beko alitumia mbinu zake za kiasili, kumganga ganga shadya, kwa kutumia mitishamba aliyokua akiitumia pindi tukio kama hilo lilipo tokea, na mtukujeruhiwa kwa kitu chochote, kwani ilimchukua mda sana, kwaajiri ya kuzirudisha fahamu zake mke wa mfalme huyo. Beko alifanikiwa na walichukua jukumu la kumpeleka akapumzike (shadya) kiukweli Beko muda wote Beko alikuwa katika wakati mgumu sana kutokana na mikao ya kihasara hasara ya bi Shadya, iliyo tokana nakuto kujitambua wakati akifanyiwa matibabu, haya sasa tuonane mchana ilitujuwe kilicho endelea baada ya tukio hili




No 23: Basi shadya alipumzika takiribani masaa marefu kidogo, huku binti Tausi akimwangalia kwaukaribu zaidi, endapo tatizo jingine litakapo tokea ajuwe na kuwataharifu viongozi wake. Beko aliludi kwenye kiwanda na kuendelea na kazi yake, huku akifikilia uwezo alio nao wa kupambana na ng'ombe yule (fahari), hapo akwaza kuwa, kwangauvu alizo nazo akipata msaada mdogo, anaweza kupambana na bepari Timoth, nakumng'oa ili kuludisha Uhuru wa kijiji kile. huku nako bi shadya alishituka kwa hofu mkubwa pale kitandani, akizani bado yupo eneo la tukio, na kuuliza nini kilimpata mpaka yuko kwenye hari ile basi binti Tausi alimsimulia ilivyokuwa kwenye lile tukio, na kumwambia alitokea Kijana mmoja na kumsaidia. Shadya akamuuliza Tausi "ni Kijana gani yule?, aliyaokoa maisha yangu, maana nili mwona kidogo alivyo jitahidi" basi Tausi bila kuficha akamwambia, ni Kijana mmoja anafanya kazi kwenye kiwanda cha miwa cha bepari Timoth, "jina lake ni beko" lakini Tausi hakumwambia kama Beko nimpenzi wake. Papo hapo shadya akataka kumjua Kijana huyo, ndipo akamwambia, "Tausi unaweza nisaidia nikamjua huyo Kijana, nataka nikamshukuru kwa kuokoa maisha yangu".pasipo kijuwa nia ya Bi Shadya, Tausi alikubali kuwa atampeleka shadya, ili amkutanishe uso kwa macho na Beko. Ndipo Tausi alichukua jukumu la kumpatia chochote kitu ili aweke mdomoni shadya, maana alichukua muda mrefu kulala, kumwambia apumzike kwanza, jioni ikifika atampeleka mahari ambako Beko anapatikana, basi Tausi alitaka kutoka kidogo kwenda kumuandalia chakula cha jioni, wakati anataka kutoka aliona kitu kilichomstua...kitu gani?.. haya sasa kwamzigo huo leo nazani mambo yanaenda vyema.



No24 Alipokuwa akitoka pale alipomwacha shadya, na alipofika mlangoni, alimwona bepari Timoth akimvuruta kijana. kumbe baada

ya ripoti kufikia makao makuu, kuwa mke wa kiongozi mkubwa, kuwa kaparamiwa na ng'ombe, kumba Tausi alikuwa anajihisi dalili

za kuwa ni mjamzito, nahiyo ni baada ya kuingiliwa na timoth, basi bepari timoth alichomoka na vijana wachache, wapatao 30

na kwenda kumchukua kijana huyo, aliyesababisha mahafa hayo, walipofika tu! eneo hilo la watumwa wakazumguka na kufanikiwa

kumpata kijana huyo wakati wanaondo mara bepari timothy akachezwa na machale na alipogeuka nyuma akaisi kuna kitu kimeingia

mlangoni humo kumbe alikuwa Tausi anataka kutoka kwenda kumuandalia chakula cha jioni ili ale pia akamkutanishe na Kijana

Beko. Ile kumwona bepari Timothy kwa upande wa tausi alishikwa na bumbuwazi baada ya kujigundua kuwa ana ujauzito wa bepari

timoth, alilia sana, na kuwaza atamwambia nini mpenzi wake Beko, na huku akilijua hilo aliogopa hata kumwambia, maana anajua

endapo atameambia kuwa anamimba, anaweza kumuondosha duniani, basi alingoja mpaka alipo mwona timoth, akitokomea ndipo

akatoka na kuelekea alikokuwa akienda, ikiwa nakwend kumjulisha beko, ujio wa bi Shadya usiku huo. Jioni ilipofika Tausi

alikuwa kaisha weka ahadi ya kumkutanisha shadya na Beko, basi Tausi na bi Shadya, walikutana na kupanga mikakati ya

kutoroka na kwenda kumwona beko, huku wakipanga hizo njama, hawakutaka mtu hata mmoja ajue, zaidi yao nini kina endelea

maana bepari Timothy akijua, Beko atapata matatizo, kumbuka bi Shadya hakuwa anajuwa kuwa, kijana beko, ni mpenzi wa Tausi,

ndipo walipo ... kiukweli mimi sijuwi kilicho tokea, unazani kwanini inakuwa siri kwenda huyko kwa



No25: Tausi na bi Shadya, hawakutaka ata mke wa bepari timoth ajuwe, walipo panga mda wa

kwenda kumwona Beko, muda ulipita kidogo kagiza kalitanda, na kufika mda waliopanga, ndipo

walifanya upesi, na kwaumakini mkubwa, na kupita mlango wa nyuma, huku wakiwa makini sana

ili wasijulikane, nawalinzi au mtu yoyote, huku wakinyata nyata kama mwendo wa kinyonga,

au jini, ili vishindo visisikike kwa wale walinzi wa bepari Timoth. Basi walitokomea

kwenye shamba kubwa la miwa, huku wakipiga story mbili tatu, kuusu kijana Beko, njia zote

alikuwa anazijua Tausi, alimwongoza vizuri shadya kuelekea kwa beko, walichukua mda mrefu

kidogo kulimaliza hilo shamba la miwa, kwani lilikuwa kubwa sana, basi shadya huku akiwa

na hamu ya kumwona Beko, pasipo kujuwa ni mpenzi wa Tausi, lakini tausi alimpa matumaini

huku akisema "tumekaribia sasa, bado hatua chache tufike" huku shadya akipiga moyo konde,

nakujipa moyo kuwa mambo yatakuwa kama anavyo yapanga, na atamwona tu! kijana Beko.

Kwambali Tausi aliona vijakazi wa bepari Timoth, na kumwambia shadya wajifiche pembeni na

wasubili wale vijakazi wapite, maana wakiwaona tu! mda huo huo, bepari Timoth atajua,

walipo pita wakaemndelea nasafari yao, huku kichwani bi Shadya, akiwaza yakwake ambayo

endapo Tausi ange juwa angegahili kumpeleka, basi walofika karibu na kibanda cha beko,

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog