Search This Blog

Sunday, February 26, 2023

NIPE BHANA - 4

   


Chombezo : Nipe Bhana 

Sehemu Ya: Nne (4)



Baadaye kidogo nilipata nguvu na kutoka nikimuacha yule nesi ofisini. Wakati natoka niliona msichana fulani mrembo akitoka katika mlango wa kile chumba cha ICU.


Msichana yule aliponiona alinipisha na kunijulia hali huku akionekana kuwa katika hali ya haraka,kutokana na mavazi ya kidaktari aliyokuwa amevaa nilijua ni mmoja wa madaktari waliokuwa wakimtibu Cathy hivyo nilijaribu kumsimamisha nikihitaji kujua hali ya mke wangu, cha ajabu nilipo muita msichana yule aliendelea kutembea na bila kuniangali aliniambia mke wangu yupo salama.


Nilizidi kupata hofu juu ya Cathy nikajua huenda kuna tatizo limetokea "Au amefariki"nilijiambia.


Lakini moyoni nilijipa moyo kusubiri tamko la madakitari. Niliendelea kukaa pale nje huku hofu pamoja na shauku ya kujua kilichoendelea vikiongezeka ndani yangu.


Kadiri muda ulivyo sogea ndivyo ukimya ulivyo tawala, hakukuwa na daktari aliyetoka kunijuza habari za afya ya Cathy.


Hata yule daktari wa kike aliyetoka mwanzo sikuona akirudi, nilipata hofu nikaamua kurudi kwa yule nesi nimuombe afuatilie kwani ilikuwa vigumu kwangu kuingia katika chumba cha ICU bila ruhusa maalumu.


Nilipofungua mlango wa ofisi ya nesi yule nilishtuka baada ya kuona damu iliyo tapakaa ardhini, nesi yule alikuwa amelala sakafuni huku damu zikimtoka puani na masikioni, hakuonesha dalili ya uhai, tayari alisha fariki.


Haraka huku hofu imenijaa nilitoka mbio na kwenda mojakwamoja mpaka kilipokuwa chumba cha ICU na kugonga kwa nguvu, hakukuwa na muitikio wowote hivyo nikaingia kwa pupa.

Haraka yangu yote iliisha kwa niliyo yaona, nilijikuta nikianza kupiga hatua za taratibu.



Ilipoishia...

Nilipofungua mlango wa ofisi ya nesi yule nilishtuka baada ya kuona damu iliyo tapakaa ardhini, nesi yule alikuwa amelala sakafuni huku damu zikimtoka puani na masikioni, hakuonesha dalili ya uhai. Nilitoka mbio na kwenda mojakwamoja mpaka kilipokuwa chumba cha ICU na kugonga kwa nguvu, hakukuwa na muitikio wowote hivyo nikaingia kwa pupa.

Haraka yangu yote iliisha kwa niliyo yaona, nilijikuta nikianza kupiga hatua za taratibu.


Endelea....


"Mungu wangu!"nilijikuta nikitamka maneno hayo.

Mbele ya macho yangu alionekana Cathy akiwa amelala sakafuni huwezi amini msomaji tumbo lake lilikuwa limechanwa vibaya kwa kisu kikali halafu kiumbe kilicho kuwa tumboni mwake kikatolewa na kuwekwa pembeni yake. Madaktari waliokuwa katika operesheni nao pia walikuwa sakafuni wakiwa katiha hali ya umauti kifo chao kikifanana na cha nesi niliye tangualia kumuona.


Machozi ya uchungu yalianza kuulowesha uso wangu, miguu nayo iliiisha nguvu nikajikuta nikipiga magoti na kuanza kujongea taratibu ulipokuwa mwili wa Cathy. Hakika tukio lile lilikuwa zaidi ya unyama, na aliyelifanya nazani alikuwa na roho ya kutisha kabisa, hakuwa na hadhi ya kuitwa mwanadamu, huwezi amini msomaji kichanga ambacho hakikuwa kimefikia muda wa kutolewa nje ya tumbo la mamaye, kilitolewa kwa lazima na zaidi ya yote kikikatwa kichwa na mbaya zaidi ni njia iliyotumika kukitoa ya kupasua tumbo la mamayake bila hata kutumia ganzi.

Kwakweli nilivyoendelea kuitazama miili ile ndiyo jinsi nilivyozidi kuugulia machungu na ndivyo hasira zilivyozidi kunipanda.


Niliapa kwa mbingu na ardhi kwa jinsi yeyote ile lazima nimshughulikie aliye fanya unyama ule ambao sikuijua sababu ya mtu huyo kufanya yote hayo, na kwanini afanye kwa mwanamke dhaifu tena mjamzito kama yule, niliamua kwa gharama zozote lazima nimjue mtu huyo na nimshughulikie ipasavyo.


Katika mkono wa kile kichanga kulifungwa kamba iliyofungiwa karatasi, nilipoitazama vizuri karatasi hiyo niligundua ilikuwa na maandishi fulani hivyo nikaifungua taratibu katika kamkono kadogo ka kiumbe yule asiyekuwa na hatia kisha nikaifungua.


Ghafla kwa mbali nilisikia sauti ya ving'ora vilivyodhihirisha ujio wa polisi.

Niliona bora niondoke eneo lile kuliko kukamatwa na kusekwa ndani na polisi kwani ningekuwa mshukiwa mkuu wa mauaji yale ya kutisha.


Niliyafumba macho ya Cathy nikimuahidi kumlipia kisasi na kuruka dirisha nikatembea hatua kadhaa na kuifikia fensi ambayo niliiruka. Nikitembea kwa uangalifu nikaelekea mpaka ulipokuwa usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda.


Bodaboda hiyo ilinifikisha nyumbani kwangu, nikaoga na kuvaa nguo nyingine kisha zile nilizokuwa nimevaa nikazituka katika shimo la takataka.

Baada ya kutulia nilifungua karatasi ile na kuanza kuisoma,ikisomeka kama ifuatavyo,

"Najua tukio hili litakusaprise sana, maana yake 'litakushangaza sana' ila nazani hutakiwi kushangaa kwani yote umeyataka mwenyewe.

Natumai umeshasahau tukio ulilofanya miaka sita iliyopita, mauaji ya kinyama tena ukifanya hadharani bila huruma ukaangamiza familia isiyokuwa na hatia mbele kamera kabisa ukaondoka kifua mbele bila kujua ni machungu kiasi gani umeyaacha kwa wapendwa wa marehemu hao. Nataka ujue huu ni mwanzo tu, nitasambaratisha kila kilicho na uhusiano na wewe, halafu baada ya kuwamaliza wote, nikamilishe kazi kwa kukupa zawadi ya kifo ambayo katika maisha yako yote hata huko kuzimu unapoelekea hatokaa usahau maumivu yake.

Sidhani kama una haja ya kujua mimi ni nani 'wala hupaswi'.

Wakati huu unapoisoma barua hii ndiyo wakati ambao mama yako na ndugu zako kule kijijini wanamalizia kupumua kwa mara ya mwisho.

Mwaaah!!


Byee mr lover".


Ndivyo ilivyosomeka barua ile iliyoniacha katika hali ya kuchanganyikiwa kuliko pitiliza, barua hiyo ndiyo iliyo nikumbusha tukio la mauaji nililofanya miaka kadhaa iliyopita siku niliyowaua Jane na babayake nikishuhudiwa na umati mkubwa wa watu.


Baada ya kulikumbuka hilo niliweza kutambua kuwa adui yangu alikuwa na uhusiano na Jane na huenda hata akawa ndugu yake.

Nilianza kujiuliza muuaji huyo atakuwa nani lakini jibu sikuweza kulipata.


Kichwa kilizidi kupata moto baada ya kuyakumbuka maneno yaliyotamatisha barua ile yakiniweka wazi juu ya hatari iliyoikabili familia yangu.


Nilichukua simu na kuitafuta namba ya mama nikapiga, simu iliita kwa muda kisha ikapokelewa.

"Hellow mr. Lover mamayupi unampigia, mimi? au yule aliye kuzimu"ilisikika sauti ya kike ikisema maneno hayo yaliyo nikata maini kabisa, nilipiga tena lakini namba ile haikupatikana.


Nilitafuta namba ya kaka na kupiga lakini naye hakupatikana.. hapo nikazidi kuchanganyikiwa nikipata mapigo bila kumjua mpigaji..


Nini kitaendelea usikose chombezo hili la kusisimua..




Nilichukua simu na kuitafuta namba ya mama nikapiga, simu iliita kwa muda kisha ikapokelewa.

"Hellow mr. Lover mamayupi unampigia, mimi? au yule aliye kuzimu"ilisikika sauti ya kike ikisema maneno hayo yaliyo nikata maini kabisa, nilipiga tena lakini namba ile haikupatikana.

Nilitafuta namba ya kaka na kupiga lakini naye hakupatikana.. hapo nikazidi kuchanganyikiwa nikipata mapigo bila kumjua mpigaji..


Endelea...


Mambo yalizidi kuwa magumu. Siku hiyohiyo niliamua kufunga safari kuelekea kijijini. Nia yangu ilikuwa kudhibitisha niliyo yasikia na kama ni ya kweli basi nifanye mipango ya mazishi kisha nijiweke tayari kukabiliana na adui.

Wakati safari ikiendelea nikiwandani ya basi dogo la abiria wakati huo nikisafiri kutokajijini Arusha kuelekea mkoani Kilimanjaro ghafla mbele ya basi nililopanda ilionekana gari aina ya BMW nyeusi ikija kwa kasi. Kwa kawaida magari hayo yalizoea kutumia na vigogo wakubwa serikalini au matajiri waliokuwa na kiasi kikubwa cha fedha.

Baada ya kuifikia gari yetu cha kushangaza gari ile haikutupisha bali ilifunga breki na kukunja kona kisha ikawa kama imetuzibia njia naam, iliziba njia.

Kwa mshtuko dereva wa gari yetu alikanyaga breki na kukunja kona ya ghafla iliyosababisha gari ile ipoteze muelekeo na kuingia mtaroni.

Ilitokea ajali kubwa, watu wengi waliumia sana, na tena hayakuwa makovu madogo ilikuwa michaniko mikubwa ya vioo. Namshukuru mungu siti niliyokuwa nimekaa ilikuwa na mkanda hivyo kitendo cha kuuvaa mkanda ule mwanzoni wa safari kiliifanya pona yangu kwahiyo sikuumia popote.

Kwenye ile BMW walitoka wanaume watatu mikononi wakiwa wameshika bastola ndogo na kulifata basi letu lililokuwa limebinuka upande mmoja.

Baada ya kuwatazama kwa umakini machale yalinicheza nikahisi huenda watu hao walikuja kwa ajili ya kunikamata.

Walifungua mlango wa basi lile wakipata kazi ngumu kutokana na mlango huo kuwa sehemu ya juu ya basi iliyobinuka.

Nilijitoa katika siti niliyokuwa nimekaa nikajilaza pembeni ya mwanamke mmoja aliyekuwa akitoka damu nyingi usoni baada ya kuchanwa na kioo.Niliifuta damu usoni kwa mwanamke huyo na kujipaka sehemu za usoni na shingoni mwangu. Kisu kidogo maalumu kwa ajili ya kujilinda nilikitoa mfukoni na kukipaka sumu ya nyoka ambayo niliiichukua kwa masai baada ya kuhisi nitafuatiliwa na manyamera.

Nilitulia na kusubiri. Wakati huo wanaume wale waliovalia mavazi ya rangi nyeupe yaliyofanana yaani kombati nyeupe kabisa walianza kukagua abiria waliokuwa ndani ya basi lile kwa umakini mkubwa huku bastola zao zikimnyookea kila waliye mkagua.

Walimkagua watatu kutoka nilipokuwa, kisha wapili mwishowe wa kwanza ambapo mmojawao aliponigusa bega akitaka kunigeuza aione sura yangu, nilijivuta kama risasi na kumdunga kisu cha shingoni ambapo aliniachia na kuanguka.

Wakabaki wawili ambao kwa mshituko waligeuka kujua kilicho kuwa kikiendelea, hapo nikaruka mateke mawili ya juu nikijishikiza katika chuma na kuanguka nao mpaka chini, mmoja aliidondosha bastola yake mbali kidogo hivyo akabaki mmoja aliyekuwa na silaha, nikaamua kuanza naye huyo, kwa kuukunja kwanguvu mkono uliokuwa umeshikilia silaha ile na kumdunga kisu cha bega.

Bahati mbaya mwenzake aliyekuwa amedondosha bastola alinyanyuka haraka wakati nikipambana naye na kuiokota bastola ile kisha akanilenga risasi ya begani.

Hapo nilihisi maumivu makali mno nikamuachia yule mwanaume niliyekuwa napambana naye kwakuwa sumu iliyokuwa katika kisu kile ilishaanza kumuangamiza.

Nilijirusha chini ya siti za gari ile kukwepa risasi zilizokuwa zikilengwa kwa pupa na mvamizi yule ambapo zilisababisha tafrani ndani ya ile gari kwani ziliwapata baadhi ya abiri waliokuwa katika majeraha makubwa na hivyo kupelekea umauti wa watu wale.

Baada ya kujificha chini ya kiti nilimpimia mvamizi yule aliyekuwa akisogea taratibu kufuata sehemu nilipokuwa huku akiendelea kurusha risasi, alipofika karibu na siti ile nilimtega mguu ambapo aliinama kidogo baada ya kuteguka hapo nikakishusha kisu katika mgongo wake huo ukawa mwisho wa uhai wake.

Nilipokuja kutazama nje niliona gari ya thamani aina ya BMW ikiondoka huku ikisikika sauti kutoka katika miili ya wavamizi niliokuwa nimewauwa ikinisifu kwa kuweza kukabiliana na watu hao lakini pia ikinihatarisha juu ya bomu lililokuwa likija kuilipua ile gari.

Kweli nilipotazama nje niliona bomu ndogo aina ya 'missle' likija kwa kasi huku likitoa moshi mkubwa.

Ili kuokoa maisha yangu nilijirusha kwenye kioo cha basi lile na kutokea nje nikiangukia sehemu iliyokuwa na korongo kubwa ambapo kulikuwa na umbali mkubwa wa mwinuko kutoka lilipokuwa basi lile.

Nyuma yangu ilifuata sauti ya mlipuko mkubwa na nilipotazama upande wa juu nilishuhudia basi lile likiteketea kumaanisha kila kilichokuwa ndani kilipotea.

"Hii ishu si ya utani asee hapa inabidi niwe mgumu"nilijiambia.

Wakati huo maumivu begani yalikuwa makali sana. Nilivua koti nililokuwa nimevaa pamoja na kaushi kisha nikachukua kile kisu na kukiosha kwenye maji halafu nikakipaka ungaunga fulani kulingana na maelekezo niliyopewa na masai wakati akinipatia dawa ile, nia ya yote ilikuwa kuondoa sumu kali ya nyoka iliyokuwa katika kisu kile.

Baada ya hapo nilijikaza kiume na kukiingiza kile kisu katika sehemu ilipokuwa risasi ile ndogo na kuitoa kwa kuibinua kutoka kwenye nyama, hapo nilijikuta mwenyewe nikitoa ukelele wa maumivu, kisha nikachukuma majani fulani yaliyokuwa kari na kuweka katika kile kidonda kuzuia kuendelea kuvuja kwa damu.

'Lazima niwe mwanajeshi la sivyo hawa manyamera watanimaliza'nilijiambia tena nikiwa na maana ya kuwa na roho kama ya mwanajeshi ili kuikomboa roho yangu na watu wangu wa karibu.

Kwakuwa wakati ule yalishatimia majira ya saa kumi jioni sikutaka kuendelea kubaki katika lile korongo nilipanda taratibu mpaka ilipokuwa sehemu ya barabara ambapo niliamua kupita mbali na eneo mlipuko wa lile basi ulipotokea kukwepa purukushani za polisi.

Nilichukua simu yangu na kumpigia rafiki yangu Joh aliyekuwa akifanya kazi ya bodaboda na kumuomba ajaze mafuta anifuate maneneo ya kia ambapo hazikupita dakika ishirini Joh alifika nikamuagiza anipeleke mpaka Moshi kijijini nyumbani kwa wazazi.

Haikuwa safari ya muda mrefu sana kwani mpaka saa kumi na mbili tulishatia nyayo zetu katika ardhi ya Moshi.

Lakini baada ya kufika nyumbani niliishiwa nguvu kwa niliyo yaona. Ene lote la nyumbani kwetu halikuonekana zaidi ya majivu, siyo hilo tu, hata mashamba yaliteketezwa kwa moto ambao baada ya kuuliza majirani waliniambia ni wa mabomu.

Siyo wazazi na ndugu zangu wala mifugo yao walioweza kutoka wakiwa wazima kila kitu kiliteketea katika moto ule. Machozi ya uchungu yalitiririka usoni mwangu. Hata majirani nao kila waliponitazama walilia kwa uchungu.

Siku hiyo walifanya mpango wa kukusanya majivu yote ambayo tuliyazika katika shimo la pamoja, familia yangu ikawa imeteketea katika hali hiyo.

Sikutaka kuendelea kukaa kule kijijini usiku huohuo nilirudi na Joh mpaka jijini Arusha. Kwa kuwa siku hiyo nilikuwa na stress sana niliingia bar na kuagiza kiasi kikubwa cha pombe kali, sikuwa peke yangu, nilimualika na rafiki yangu wa pekee niliyemuamini kwa wakati huo Joh.

"Joh huwezi amini haya yote niliyokuambia na uliyoya shuhudia yamenikumba, sina mtu yeyote aliye upande wangu ambaye niseme anaweza kushirikiana na mimi katika kupambana na hawa maadui zangu wasioonekana, unaonaje ukiungana na mimi ukaacha hii kazi ya pikipiki nikawa na kulipa kila siku mara mbili ya hela unayopata kwa siku ukashirikiana na mimi kunipa taarifa kuhusu watu wanao nifuatilia maana nakuelewa wewe mtoto wa mjini kila kona unaijua"

"Haina noma hiyo kaka cha msingi hela na sidhani kama kuna haja ya kuacha bodaboda kazi ntaendelea nayohuku nikiendelea kufuatilia chinichini ili siwe rahisi kujulikana"

"Ok sawa kuanzia leo wakati huu , kazi imeanza nitahitaji nidhamu katika kazi"

"Naahidi kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa bosi naapa kutokuangusha"

Hapo nilimalizana na Joh tukaendelea kupiga vinywaji mpaka ilipofika mida ya saa nne na nusu usiku, wakati ambao nilijikuta nikiamka kwenye kiti baada ya kushuhudia mwanaume aliyekuwa meza ya mbali kidogo akimpizaba makofi msichana ambaye alikuwa akilia huku akijitetea bila kusikilizwa.

Nikiwa bado katika hali ya ulevi nilifika pale na kuudaka mkono wa mwanaume yule ambao ulielekezwa moja kwa moja katika shavu la msichana yule mdogo na mrembo.

"Sam" ni sauti niliyosikia ikilitaja jina langu ikitoka katika kinywa cha yule msichana mrembo.


Je nini kitaendelea?, usikose inayofuata..


N:B Ukisoma tafadhali naomba unisaidie kushare kweny magroup ya facebook uliyo nayo akaunti yangu imezuiwa kupost kwenye groups huku fb hivyo inakuwa ngumu kuifikisha simulizi hii kwa wadau mbalimbali.

Share zikiwa nyingi kesho mapema naileta. Pia



Nikiwa bado katika hali ya ulevi nilifika pale na kuudaka mkono wa mwanaume yule ambao ulielekezwa moja kwa moja katika shavu la msichana yule mdogo na mrembo.

"Sam" ni sauti niliyosikia ikilitaja jina langu ikitoka katika kinywa cha yule msichana mrembo.


Endelea...


Sura ya msichana yule haikuwa ngeni machoni mwangu ila muonekano wa msichana yule kwa wakati huo vilifanya nishindwe kumtambua kwa urahisi hivyo nilibaki nikimtazama kwa macho yaliyo dhihirisha maswali yaliyousumbua ubongo wangu.

"Sam inamaana umenisahau Amina jirani yako kule Tanga kwa kina Zena"

Aliniambia msichana yule maneno yaliyoniridisha kipindi cha nyuma wakati nikiwa katika hifadhi kijijini nyumbani kwa mzee Said.

Hapo niliweza kumtambua msichana yule hivyo kwa hasira nikaushusha mkono wa yule mwanaume na kumuonya asirudie kumsumbua tena yule binti.

Yalifuata mazungumzo kati yangu na Amina ambaye aliniambia kuwa ulishapita muda mrefu tangu aachane na yule mwanaume aliyekuwa akimsumbua kule Tanga hivyo kwa sasa alikuwa akiishi jijini Arusha akifanya kazi katika ile Hoteli.

Na kwakuwa alimaliza muda wake wa kazi wakati wa jioni baada ya kubadilishana na mhudumu aliyeingia usiku aliamua kukaa eneo lile apunguze uchovu ndipo mwanaume yule aliyekuwa mlevi alipomfuata akimtaka kimapenzi na alipomkatalia mwanaume huyo aliyekuwa akiongozwa na pombe alianza kumpiga bila huruma. Kumfuata mwanaume yule na kumpa kipigo lakini Amina akaniomba niachane naye.

"Kwahiyo siku hizi unaishi wapi?"

"Nipo hapahapa Arusha, si unajua mimi chali ya R"

"Mhh sawa nakuona, ila siku hizi umetakata we mkaka, unakula nini, au umepata jiko?"

"Amna wala, bado nipo single sijafikiria kuoa ila maisha yangu ya siku hizi bora kipindi kile"

"Kwanini unasema hivyo?"

"Dah stori ndefu da Amina usione nagambeka hivi, kwanza tusiongee sana, bora hata nimekuona unipe kampani, kwani unakaa wapi"

"Florida, alafu unaonekana umelewa sana twende ukalale kwangu maana ni karibu kidogo".

Baada ya mazungumzo hayo niliondoka na Amina mpaka katika mtaa wa Flarida ilipokuwa nyumba yake.

Usiku huo hakika ulikuwa mrefu. Baada tu ya kuingia ndani Amina alinishika mkono tukaenda moja kwa moja mpaka chumbani kwake. Huko msichana yule akavua kigauni chake kifupi na kuelekea lilipokuwa kabati kubwa la nguo nakutoa taulo mbili nyeupe kisha akanirushia moja.

Wakati huo macho yangu yaliganda katika mwili wake uliokuwa umesitiriwa kwa chupi za kisasa zijulikanazo kama bikini huku kifuani kukiwa na brazia iliyokuwa na rangi sawa na ile chupi. Ngozi nyeusi ya wastani na umbo matata la saizi ya kati vilizidi kunitoa udenda. Niliendelea kumtazama.

"Khaa! muone mbona unanitolea mimacho hivyo utazani leo ni mara ya kwanza kuuona uchi wa mwanamke"

Aliniambia Amina ambapo kwa makusudi alijitupa pale kitandani na kualala chali kisha akatanua miguu yake na kuanza kuivua chupi yake kwa madaha huku akinipa tabasamu la utani.

Nilitupa ile taulo pale kitandani na kumfuata lakini nilipomfikia alijifunga taulo na kutupa ile chupi pembeni akaanza kunivua nguo taratibu huku akiupapasa mpini wangu uliokuwa umesimama vilivyo ukidai haki.

Alipomaliza kunivua nguo zote, alinifunga taulo kisha akanishika mkono tukaenda pamoja mpaka katika bafu la kisasa aina ya Jakuzi.

Huko mpambano ulianza, maji ya moto wastani yaliyokuwa yakitolewa na jakuzi lile yaliziamsha hisia zetu na kutufanya kama wageni wa shughuli ile ya usiri.

Niliishika taulo ya Amina pamoja na yangu na kuzitupanje ya jakuzi lile. Amina akaanza kuniparamia kwa kuninyonya masikioni,shingoni na chuchu zangu kifuani. Kwa kweli mahaba ya binti yule wa kitanga hayakuwa ya kuzoeleka, kila alichonifanyia kilionekana kipya na chenye msisimko usiokuwa wa kawaida. Nilijikuta nikigugumia kwa utamu nilioupata.

Sikuwa mbali nami nilijibu mapigo na kumfanyia Amina kama alivyokuwa akinifanyia huku nikimchombeza sikioni kwa maneno matamu, yaliyozidi kumzamisha msichana yule katika bahari ya huba.

"ohhh!!! Jamani...Samm...!!! Unayajua..!!!!! Nani!!!!alikufundisha!!!!"

Aliniambia msichana yule huku akijinyonganyonga wakati huo nimembeba nikizikamata nyonga zake na kuzibinya kimahaba huku shughuli ya kuzilamba embe dodo zake ikiendelea kuchukua nafasi.

Amina naye hakutaka nimshinde wakati nimembeba aliendelea kuusugua mtarimbo wangu kwa msambwanda wake laini akifanya kuukalia kwa juu na kuusugua kwa zigo lake.

Baada ya kuona msichana yule kalainika vilivyo nilikaa katika sehemu maalumu kwa ajili ya kukalia iliyokuwa ndani ya jakuzi lile na kumkalisha Amina katika mtarimbo wangu. Hapo nikaanza kukichezesha kiuno cha msichana yule mwepesi katika mtarimbo wangu kwa mwendo ambao nilihisi unafaa kwa wakati ule.

Amina alizidi kunikumbatia kwa nguvu huku akijihudumia kwa kunyonya ndimi zangu na kunilamba sehemu za shingoni kimahaba.

Wote tulikuwa ndani ya bahari ya huba, bahari ambayo haikuwa na dhoruba wala upepo kwa mbali.

Maji ya uvuguuvugu yaliyoendelea kutimwagikia yalitupa mihemko zaidi hivyo tulibadili mikao mbalimbali. Nilihakikisha namkuna msichana yule, mpaka wote tutakapo kidhi haja zetu. Sikuwa nimefanya mapenzi kwa muda mrefu hivyo siku hiyo Amina alikiona cha moto.Ulifika wakati akawa ameridhika baada ya kuvunja vidafu ambavyo kwa kazi niliyokuwa nikiifanya sikuwa na muda wa kuhesabu, msichana yule alianza kutoa sababu mbalimbali mara unaniumiza Sam, mara nahisi mkojo na sababu nyingine nilizo zitafsiri kama za kitoto.

Niliendelea kumsugua vilivyo msichana yule mpaka nilipohakikisha nimekidhi haja zangu ambazo nilikosa kwa muda mrefu.

Baada ya kumaliza kwa kufunga goli zito ndipo nilipoutoa mpini wangu katika pango la msichana yule, aliyetaka kuamka aondoke lakini karibu aanguke kutokana na kukosa nguvu hivyo nikamdaka na kumbeba kama mtoto.

Tukajikuta wote tukitabasamu tukaelekea chumbani nikiwa nimembeba vilevile huku tukipigana mabusu yafuraha. Kama unavyojua raha ya mwanamke akutanapo na mwanaume ni kufikishwa pale anapohitaji hivyo siku hiyo nilioga maneno mengi ya kupaka mafuta kutoka kwa mrembo yule.

Usiku huo nililala kwake lakini majira ya saa tisa usiku niliamshwa na sauti ya Amina aliyekuwa akinitikisa, nilikurupuka na kumtazama, uso wake ulionyesha hofu, alinyooshea kidole chake katika moja ya dirisha lililokuwa katika chumba kile.


Nini kimetokea?, usikose muendelezo wa chombezo hili la kusisimua..


Like na share na kama bado hujalike hii page ingia na ufanye hivyo.




Usiku huo nililala nyumbani kwake lakini majira ya saa tisa usiku niliamshwa na sauti yake huku akinitikisa, nilikurupuka na kumtazama, uso wake ulioonyesha hofu, alinyooshea kidole chake katika moja ya dirisha lililokuwa katika chumba kile.


Endelea...


Nilichungulia nje kupitiaa dirisha lile. Walionekana watu watatu waliokuwa wamevalia mavazi meusi yaliyofunika sehemu kubwa ya miili yao.

Watu hao walitembea kwa umakini sana mikononi mwao wakishika vyuma vidogo vilivyofanana na kisu.

Nilirudishia pazia vizuri na kumuomba Amina ambaye alikuwa katika hali ya hofu sana aingie katika moja ya kabati la nguo atulie bila kutoa sauti.

Baada ya hapo nilitoa kisu changu kidogo na kukipaka sumu ya nyoka hatari aina ya koboko. Kisha nikafungua mlango wa chumba kile na kupanda juu yake kwa ukimya.

Ikaanza kusikika mishindo ya sauti za unyayo zilizosikika kwa mbali sana, nilijiweka tayari kufanya shambulio, kisha akaingia mmoja wa wale watu katika hali ya tahadhari mkononi akishikilia kisu kidogo kilicho ng'aa sana kwa ukali.

Akavuka mlango na kuingia ndani. Hapo katika hali ya ukimya nikaruka nikilirusha teke langu nikilenga eneo la mgongo la mtu yule. Kabla pigo langu halijamfikia mtu yule aliinama hivyo nikamkosa ambapo kabla sijatua sakafuni alinidaka mguu mmoja na kurusha ngumi nzito iliyotua katika maungo yangu ya uzazi, hapo niligugumia kwa maumivu baada ya kutua sakafuni nikijishika maeneo hayo yathamani kabisa kwa kila mwanaume.

Lilifuata teke zito kutoka kwa mtu yule, aliyekuwa na mwili mdogo na mwembamba lakini uliokakamaa kwa nguvu. Nilijikuta sakafuni nikibwabwaja kwa maumivu huku damu zikivuja katika mdomo wangu.Mtu yule alinifuata na kuinama akitaka kuninyanyua huo ndiyo ukawa wakati wangu muafaka wa kufanya shambulizi kwani nilijigeuza kama mshale na kuipiga miguu yake ambapo mtu yule aliteleza akijaribu kujizuia kuanguka nikaruka kwa haraka na kumdunga kisu cha shingoni. Kwa kuwa bado sikuwaona wale wenzake nilitembea taratibu nikinyata mpaka ilipokuwa sebule ambapo ukimya ulitawala kukionesha hakukuwa na tukio lolote lisilokuwa la kawaida.

Niliangalia jikoni ambapo pia ukimya ulitawala hivyo kwa tahadhari zaidi nilirudi kule chumbani nikidhamiria kumchukua Amina tuondoke eneo lile kwani halikuwa salama.

Nilipofika karibu na mlango wa kuingilia chumbani nilisikia sauti ya Amina akiomba msamaha huku pia zikisikika sauti nyingine za kike.

"We must kill you, you got no other choice than telling us where he is(lazima tukuuwe, huna chaguo jingine zaidi ya kutuambia mahali alipo)"ilisikika sauti ya kike ikizungumza kwa lugha ya kiingereza.

Nilichungulia na kuona watu wawili waliokuwa wamemfunga Amina mikono nyuma na kumuwekea kisu shingoni wakimlazimu kuwaambia sehemu nilipokuwa.

Hapo niliiamua kujitokeza mbele yao ambapo baada ya kuniona mmoja wao alininyooshea bastola huku mwingine akikikandamiza kisu shingoni kwa Amina.

"Tunamuua huyu mwanamke na kuufumua ubongo wako iwapo utajigusa"waliniambia.

Nilinyoosha mikono yangu juu huku nikisogea taratibu nikiwauliza ipi sababu ya wao kunivamia usiku ule. Wanawake wale walioonekana dhahiri kutokuwa watanzania waliniambia sikuwa na haki ya kujua sababu ya uvamizi wao hivyo nilichotakiwa kufanya wakati ule nikutulia na kufuata masharti yao.

Taratibu alinisogelea yule mwanamke aliyekuwa ameshikilia bastola akiwa bado ameninyooshea na kunitaka niiweke mikono yangu nyuma na endapo ningeleta ubishi, angenimaliza muda ule ule.

Niliweka mikono yangu nyuma na kujipanga kufanya shambulizi la kushitukiza, huku nikimkonyeza Amina aliyekuwa akinitazama kwa hofu.

Mwanamke yule baada ya kunifikia alitoa mnyororo mdogo uliokuwa na funguo maalumu na kuanza kunifunga lakini kabla hajakamilisha kufanya hivyo, niliukanyaga mguu wake kwa nguvu na kushitukiza jambo na kumpiga kiwiko cha uso kwa kuwa aliinama chini kidogo ambapo pigo lile lilimfanya apoteze muelekeo na kuanza kufyatua risasi mfululizo. Moja ya risasi zile ilimpata mwenzake ambaye muda huo alikuwa akimyanyua Amina ili amdunge kisu kwa kuwa nilikaidi amri, hivyo likawa anguko la mpango wake.

Nilimwamuru Amina alale chini kwa kuwa mwanamke yule aliendelea kufyatua risasi zilizo haribu samani mbalimbali katika chumba kile ambapo kabla hata sijamaliza kauli yangu risasi moja ilimpata Amina sehemu za kifuani aliyeanguka na kuyafumba macho yake palepale.

Nilihisi kichaa kunipanda kwani nilijikuta nikiruka na kumsukuma yule mwanamke kwa nguvu na kuanguka naye sakafuni ambapo risasi aliyokuwa ameishikilia mkononi ilimponyoka hivyo nikamkunja na kumshindilia ngumi nzito.

Mwanamke yule alijikaza na kuniingizia vidole viwili machoni hali iliyofanya nimuachie kutokana na maumivu makali.

Alinyanyuka na kukunja ngumi kisha tukaanza kurushiana makonde mazito pamoja na mateke. Nilijitahidi kwa kila namna kuhakikisha nammaliza mvamizi yule lakini uwezo niliokuwa nao ulikuwa mdogo ukilinganisha na wa kwake. Kwa jinsi mwanamke yule alivyopigana ilionesha alipitia mafunzo fulani mpaka kufikia hatua ile, alipigana kwa kutumia fomula na akili zaidi pia alikuwa mwepesi sana kukwepa na kuruka mateke ya angani.

Nilipigana kwa kutumia uzoefu na nguvu ili kuyaokoa maisha yangu, nilirusha ngumi nyingi nzito ambazo msichana yule alizikwepa japo baadhi zilimpata na kunirudishia mapigo hatari sehemu mbalimbali za mwili wangu. Wepesi wake ulimwezesha kunishambulia kirahisi sehemu za shingoni kifuani na maeneo ya familia.

Muda wote wa takribani dakika thelathini tulizo pigana hakuonesha kuchoka, alikuwa na nguvu ileile aliyoanza nayo. Pumzi pamoja na maumivu makali viliufanya mwili wangu kusarenda mateke mawili ya hewani aliyorusha msichana huyo mwepesi kama karatasi yalitosha kunilaza sakafuni kama mzigo. Mwili ulichafuka kwa damu, nilivimba sana sehemu za usoni.

Nikiwa pale sakafuni nilimtazama Amina aliyekuwa amelala usingizi wa kifo, hasira zilinikaba koo, nilijilazimisha kujinyanyua pale sakafuni lakini mkanyago wa nguvu wa msichana yule uliniridisha sakafuni na kunifanya nitulie kama mtoto, damu nyingi zilinitoka puani na mdomoni, nilizidi kumuwekea chuki, mtu aliyekuwa akinifanyia yote hayo, niliapa lazima kabla ya kumuua niinywe damu yake kwanza, aliamua kuyaharibu maisha yangu, hakuna kitu kibaya duniani kama kushuhudia ndugu na wapendwa wakifanyiwa mauaji ya kikatili, bora kushuhudia mali na utajiri ukipotea kuliko kupoteza uwapendao.

"Yes, Boss mission completed(ndio bosi mpango umekamilika"yalikuwa maneno ya msichana yule aliyenisurubu bila huruma ambaye mpaka wakati huo sikuwa nimeiona sura yake.

"Ok im coming with him(sawa nakuja naye"alisikika tena akiongea msichana yule akitumia kifaa maalumu kilichokuwa shingoni mwake.

Msichana yule alirudi na kuchukua mnyororo kisha akaanza kuifunga miguu yangu, ambapo kuna wazo lilinijia kichwani mwangu nikakumbuka sindano ndogo niliyopewa na mmoja wa madaktari katika hospitali moja jijini Arusha niliye mlaghai nikihitaji anipatie sumu ambayo nitaweza kuitumia kufanya mauaji bila kustukiwa ambapo alinipatia sindano tatu ndogo akiniambia sindano hizo zilitengenezwa kwa sumu maalumu iitwayo Cinincroxic ambayo endapo itamuingia binadamu, mtu huyo huugulia maumivu makali ndani ya mishipa ya damu ambayo hupelekea mishipa hiyo kupasuka hivyo uwezo wa muathirika wa dawa hiyo kuishi ni masaa ishirini na manne tu, pia alinipatia na kijichupa kidogo kilichokuwa na dawa fulani ya majimaji aliyoniambia dawa hiyo ilikuwa maalumu kwa ajili ya kumaliza nguvu ya sumu hiyo (antidote).

Vyote vilikuwa mfukoni mwangu, hivyo kidogo niliweza kupumua na kuachia tabasamu la mbali nikajua hiyo itakuwa njia rahisi kwangu ya kuweza kumtumia msichana yule.

Baada ya kumaliza kuifunga miguu yangu na kuhakikisha sitoweza kufurukuta msichana yule aliamia katika mikono yangu na kuanza kufunga mnyororo ule, kwa haraka niliugeuza mkono na komchoma na kisindano kile kidogo kiganjani. Hapo alistuka na kuuangalia mkono wake "Cinincroxic"

Alitamka akipokelewa na kicheko cha dharau kutoka kwangu, ambapo kwa kujikongoja niliweza kujiegemeza ukutani.

"Nilijua dawa yako ndogo tu, sasa kama unapenda ukendelea kuishi fuata masharti yangu"nilimwambia nikitumia lugha ya kiingereza.

"Wewe mpumbavu.. Uumewezaje??"alisema mwanamke yule huku akijinyonganyonga kwa maumivu makali.

"Hahaha!! Njoo ifungue miguu yangu"nilimwambia ambapo katika maumivu makali alikuja na kunifungua.

"Haya onyesha sura yako"nilimwambia.

Hakuwa na budi taratibu alivifungua vitambaa vyeusi alivyokuwa amejifunika usoni, ambapo mbele yangu alionekana msichana mrembo sana aliyekuwa na asili ya kutoka bara Asia.Alifanana na wanawake niliozoea kuwaona katika tamthilia za kichina na kikorea. Hakika alikuwa mzuri wa sura.

Aliukunja uso wake huku machozi yakimtiririka kutokana na maumivu makali,nilipoitazama sura yake kidogo nisiamini ni msichana aliyekuwa akinisurubu dakika chache zilizo pita bila huruma.

"Msichana mrembo, una sura ya upole lakini matendo yako hayaendani na sura yako, fuata amri zangu mama utakuwa hai"nilimwambia huku nikitabasamu kwa dharau.

Msichana yule alinitazama kwa hasira huku akijikunja kuugulia maumivu makali, hakuwa na la kusema zaidi ya kufuata maagizo yangu.

Wakati uleule nilimpigia Joh simu na kumtaka afike mahali pale akiwa na taxi ambapo hazikupita dakika kumi na tano Joh aliwasili akiwa na taxi ya kukodi ambapo alionekana kulewa sana.

Kwa kuwa sikutaka msichana yule wa kichina aonekane na kila mtu nilimtaka avae mavazi ya kawaida yaliyokuwa yakimilikiwa na Amina ambaye tayari alikuwa marehemu na kuifunika sura yake.

Hilo lilifanyika haraka ambapo safari ya kurudi nyumbani kwangu ilianza nikiwa garini mimi pamoja na yule binti wa kichina huku tukimuacha Joh ambaye alionesha kuingiwa na hofu kutokana na hali aliyokutana nayo katika lile eneo lakini hasa kifo cha msichana Amina ambaye masaa kadhaa nyuma tulikuwa tukizungumza naye.

"Kama unakifaa chochote kitakachoweza kukuunganisha na hao maadui zangu chonde kitoe tu iwapo unahitaji kuendelea kuvuta pumzi"nilimwambia yule msichana aliye nihakikishia hakuwa na kitu chochote wakati huo akiendelea kusurubiwa na maumivu makali.

Hatimaye tulifika nyumbani kwangu ikiwa ilishatimia majira ya saa kumi ambapo nilimlipa dereva taxi pesa yake nikamnong'oneza masikioni msichana yule amuue kwani dereva huyo alionesha kututilia shaka sana, nikahisi huenda angeturipoti polisi.

Kesho yake asubuhi ndani ya jiji la Arusha na nchi ya Tanzania kwa ujumla ilitawaliwa habari kubwa ya mauaji ya kinyama ya mwanamke mmoja wa kitanzania na wanawake wawili raia wa China walioonekana kuvalia mavazi ya kivamizi na kukutwa na silaha za mauaji. Lakini swali lililotawala miongoni mwa watu wengi likiwemo jeshi la polisi ni kuhusu mtu aliyefanya mauaji hayo ya kinyama ya kutumia silaha.

Msako mkubwa ulianza, ukifuatiwa na upelelezi wa kisirisiri uliofanywa na makachero walio sambazwa kila kona ya jiji.


Je nini kitaendelea? Usikose muendelezo wa chombezo hili la kusisimua.





Siku iliyofuata asubuhi ndani ya jiji la Arusha na nchi ya Tanzania kwa ujumla ilitawala habari kubwa ya mauaji ya kinyama ya mwanamke mmoja wa kitanzania na wanawake wawili raia wa China walioonekana kuvalia mavazi ya kivamizi na kukutwa na silaha za mauaji. Lakini swali lililotawala miongoni mwa watu wengi likiwemo jeshi la polisi ni kuhusu mtu aliyefanya mauaji hayo ya kinyama ya kutumia silaha.

Msako mkubwa ulianza, ukifuatiwa na upelelezi wa kisirisiri uliofanywa na makachero walio sambazwa kila kona ya jiji.


Endelea..


Taarifa hizo zilinifikia baada ya kupitia katika kurasa za mitandao ya kijamii ambapo karibu kila kurasa ilipambwa kwa habari za tukio hilo.

Nilimweleza msichana wa kichina Zhing chen kama alivyojitambulisha kuhusu kilichokuwa kikiendelea wakati ule.

Msichana yule alitoa rejesho la mazungumzo hayo akiniambia uwezo wa kutoroka tulikuwa nao lakini hilo lingewezekana iwapo ningempa ile dawa (antidote) ya kutibu sumu iliyokuwa katika mwili wake.

Nilifikiri kwa muda juu ya swala hilo mwishowe nikaafiki kumpatia dawa hiyo lakini sikuwa mjinga, nilikuwa na mipango yangu kichwani.

Baada ya kutumia ile dawa msichana Zhing chen alirejewa na nguvu kidogo kwani.maumivu yaliyokuwa yakimuandama yalipungua.

Hapo mipango ya kutoroka ilianza ambapo tulipanga kila mmoja aondoke peke yake tukutane maeneo ya Namanga ambapo tungevuka mpaka pamoja na kuingia nchini Kenya.

Kila mmoja alijiandaa nikimkumbusha Zhing chen kuvaa mavazi ya kiislamu ambayo yangeufunika mwili wake wote ilimradi tu kuepuka kuhisiwa na polisi waliokuwa kila kona ya mtaa.

"Twende kwanza Arusha bike tukachukue pikipiki baada ya hapo kila mmoja ataendelea na safari"nilimwambia msichana yule kwa lugha ya kiingereza.

"Ok hakuna tatizo kama hela ipo"

"Hapana hatuendi kununuua, tunaiba"

"Sawa kama hivyo wala usijali hiyo kazi rahisi sana"

Mazungumzo kati yangu na yule msichana wa kichina yalimalizika kama hivyo.

Tulitoka pamoja tukiwa tumeshikana mikono huku msichana yule akivaa shungi ya kiislam iliyoweka ugumu kwa mtu yeyote kumtambua kwani wakati ule alitafutwa kama shilingi.

Dereva Tax alitufikisha mpaka nje ya eneo ilipokuwa kampuni kubwa ya Arusha bike iliyojihusisha na uuzaji wa pikipiki za aina zote kuanzia pikipiki ndogo zilizotumika kama bodaboda mpaka zile kubwa kabisa za kijerumani.

"Karibu kaka, Habari mrembo"

Alitusalimu kwa bashasha kijana mmoja wa kihindi aliyeonekana kuwa muuzaji wa bidhaa zile.

"Asante, ila huyu si mrembo ni mke wangu kwa hiyo kaa mbali kidogo"

Nilimtania kijana yule ambapo vilifuata vicheko vilivyomfanya msichana Zhing chen naye atabasamu japo hakuelewa chochote katika mazungumzo yale.

"Ok nahitaji baja kubwa mbili ni shilingi ngapi"

"Karibu, baja zipo za aina mbalimbali ambazo hutofautiana bei"

Aliongea kijana yule huku akitutembeza mpaka zilipokuwa pikipiki kubwa kabisa zilizojulikana kama baja ambazo kwa kipindi fulani miaka michache iliyopita zilihusishwa na matukio ya uchunaji ngozi, pamoja na ujambazi.

Kijana yule aliendelea kutuonyesha ambapo niliafiki kuchukua pikipiki mbili hivyo tukachukuana na kijana yule mpaka lilipokuwa eneo la malipo na tulivyofika pale nikawataka wahakikishe pikipiki zile zinakiasi cha kutosha cha mafuta, jambo ambalo waliniahakikishia kwa asilimia mia moja.

Mpango tuliopanga na Zhin chen ukawa umekamilika hivyo ulifika wakati wa kuuweka katika vitendo.

Mara moja Zhin chen kwa kutumia miguu yake miwili alikanyaga klachi za zile pikipiki mbili kwa pamoja huku mikono yake ikiwatayari imekamilisha shughuli ya kuziwasha pikipiki zile kisha alivuta mafuta kwa nguvu na kuweka gia katika pikipiki zote mbili ambapo ulishuhudiwa moshi tu katika chumba kile maalumu huku milango ya kioo ya chumba kile ikivunjwavunjwa. Msichana Zhin chen alishatokomea kusiko julikana.

Sikutaka kuchelewa maana tuliweka muda maalumu wa kumaliza kazi ile. Haraka nilichomoa bastola iliyojificha kiunoni mwangu na kufyatua risasi mfululizo zilizo iacha chali miili ya wazaji wale.

Muda huohuo lilikuja kundi la walinzi wa tano mikononi wakiwa na mitutu yao, wakaanza kunifyatulia risasi.

Kwa mwendo wa umeme nilijificha nyuma ya kabati kubwa la chuma na kufyatua risasi ambazo nilihakikisha zinafika katika bongo laini za walinzi wale,ndani ya sekunde kadhaa kazi hiyo iliisha hivyo katika dakika kumi nilizokubaliana na Zhin chen kukutana katika barabara ya taraj iliyokuwa nje kidogo ya mji zilibaki dakika nne hivyo nilitumia sita.

Nilitoka nje ya kampuni lile ikiwa ni baada ya kuziharibu kamera maalumu za CCTV zilizokuwa zikirekodi matukio yaliyokuwa yakifanyika katika eneo lile. Sikuishia hapo kompyuta maalumu iliyotumiwa na kurekodi mauzo ya kila siku ya kampuni hiyo pia niliondoka nayo.

Dakika tano baadae nilishuka katika Tax iliyonikutanisha na Zhin chen aliyenijulisha nilichelewa kwa dakika moja, hapo tukacheka na kuingia vichakani zilipokuwa zile pikipiki mbili.

Safari ya Kenya ilikuwa ndefu mno kwani ilibidi tutumie njia za panya kuingia ndani ya nchi ya Kenya kwani eneo la mipaka ya Namanga lilirindima kwa ulinzi mkali. Shambulizi lile lilipewa hadhi ya kimatifa hivyo wahusika walitafutwa kwa udi na uvumba.

Majira ya saa kumi na mbili jioni tulikuwa nchini Kenya katika kaunti ya Kajiado ambapo huko tulikutana na mwenyeji wetu Matha msichana wa kikenya aliyekuwa akifahamiana na Zhin chen.

Msichana yule alitupokea kwa bashasha na kutukaribisha ndani ambapo ndani ya chumba kile nilijikuta nikishangaa baada ya kuona msichana yule akifunfua kijimlango kilichokuwa sakafuni tukakutana na ngazi zilizotufikisha mpaka chumba kingine kikubwa kilichokuwa chini ya ardhi.

Huko tulikaribishwa tukakaa na kupewa vinywaji laini.

"Ngoja niingie jikoni kidogo niwaandalie"

Alisema Matha kwa lugha ya kiingereza.

Nilibaki na Zhin chen pale sebuleni tukinywa juisi ile baridi taratibu ambapo msichana yule aliuvunja ukimya kwa kunieleza uhusiano wake na msichana huyo wa kikenya.

Aliniambia kuwa Matha alikuwa mmoja ya watu kutoka Afrika waliotumwa kufanya biashara haramu ya madawa ya kulevya akitumiwa kama msafirishaji kwa kumeza madawa hayo au kuyaingiza katika sehemu za siri.

Mihadarati hiyo ilifika nchini China katika kampuni iliyokuwa ikiongozwa na kumilikiwa na baba yake, ambaye pia alikuwa na cheo kikubwa katika serikali kuu ya watu wa China.

Aliendelea Zhin chen kwa kuniambia kuwa kampuni ile pamoja na biashara ile, vilikuja kuugharimu uhai wa babayake baada ya kuzungukwa na wenzake walipokuwa mapatna katika biashara hiyo waliofikia hatua ya kumuua kwa kumpiga risasi huku yeye akishuhudia kwa macho.

Baada ya mauaji hayo yaliyofanyika katika jumba la kifahari waliloishi wauaji wale walitaka kumuua na yeye hivyo aliamua kutoroka ambapo msaada huo aliupata kutoka kwa msichana Matha ambaye alimsaidia kwa kumuonea huruma kwani naye alikuwa mmoja wa wauaji wale lakini alihusika katika tukio hilo bila ridhaa yake, hivyo huo ukawa mwanzo wao kujuana.

Kwa kutumia pesa za babayake wasichana hao waliweza kutoroka nchini China ambapo walikuwa wakiandamwa na watu waliotaka kuzichukua roho zao na kutimkia nchini Kenya katika nyumba ile waliyoinunua na kuamua kuishi pamoja.

Msichana huyo hakuamua kuishia hapo kwani aliapa kulipiza kisasi kwa kuwasambaratisha watu wote waliokuwa wakifanya biashara ile pamoja na baba yake na mwishowe kuamua kumsaliti. Watu hao wakitoka katika mataifa mbalimbali duniani yakiwemo ya barani Afrika.

Msichana huyo alimaliza kwa kuniambia kuwa mpaka wakati huo alishazikatisha pumzi za manyamera sita kati ya ishirini aliotakiwa kuwamaliza.

Nilitaka kumuuliza sababu ya kunifanyia uvamizi lakini sauti ya Matha aliyekuwa akitukaribisha chakula ilinikatisha.

Tulikula chakula kile huku yakiendelea maongezi ya hapa na pale yaliyotiwa nakshi kwa utani vikifuatia vicheko kati yetu hali iliyozidisha amani mioyoni mwetu.

"Zhin, now yo've got your your black man"

Aliongea Matha akimtania rafiki yake huyo akimaanisha kuwa msichana huyo alipata mwanaume mweusi.

Zhin alitabasamu wakati huo alishautoa ushungi wake hivyo nilijikuta nikiugua kwa kuutazama uzuri wa msichana yule.

Usiku uliwadia ambapo kutokana na uhaba wa vitanda nilitakiwa kulala kitandani huku Zhin na Matha waliamua kulala kwenye makochi.

Matha kwa makusudi alimkatalia Zhin kulala kwenye makochi na kumtaka alale na mimi kitandani ambapo msichana yule hakuwa na jinsi zaidi ya kumsikiliza mwenyeji wake huyo, alikuja kitandani huku amevaa kigauni chepesi cha kulalia kilichoniwezesha kushudia mwili wake laini na uliovutia sana.

Kwenye kochi Matha naye alilala akijiweka katika mikao ya kihasarahasara hivyo hisia kali za mapenzi zilizidi kunipanda.

Nilikishika kiuno cha Zhini na kumlaza juu yangu ambapo msichana yule alitulia bila kufanya lolote kumaanisha alikubaliana na tukio lile.

Nilionyesha tabasamu na kusogeza uso wangu nikifuata midomo yake, tukaanza kunyonyana ndimi kimahaba. Hatimaye mechi ikawa mechi, tulikuwa katika hisia kali za mapenzi, miili yetu ilichemka kwa mihemko, pilikapilika zilianza pale kitandani, asee!! msichana yule mwepesi alikuwa mtundu mno, niliamua kumuanzishia mashambulizi ya kiafrika, mbona msichana wa watu alikoma.

Mahaba niliyompa yalimfanya ajisahau na kuzidi kuongeza mihemo yake. Naam, ilikuwa mihemo iliyomtoa Matha katikati ya usingizi mzito. Alifikicha macho yake na kujinyanyua pale kwenye kochi, kisha huku akiufungua upande wake wa Khanga kabla ya kuutupa pembeni alishatufikia..


Je nini kitaendelea? Usikose chombezo hili la kusisimua.





Mahaba niliyompa yalimfanya ajisahau na kuzidi kuongeza mihemo yake. Naam, ilikuwa mihemo iliyomtoa Matha katikati ya usingizi mzito. Alifikicha macho yake na kujinyanyua pale kwenye kochi, kisha huku akiufungua upande wake wa Khanga kabla ya kuutupa pembeni alishatufikia..


Endelea..


Wakati huo Zhin Chen alikuwa katika pepo ya huba. Hakika msichana yule wa kichina alipagawa. Kama ni chachandu basi alipata iliyoendana na aina ya chakula alichokula. Papo hapo Matha alinifikia na kuuleta mdomo wake karibu yangu, kisha akanivuta kidogo na tukaendelea kupata busu maridhawa. Wakati huo msichana Zhin chen bila kinyongo alibadili mkao na kukaa mkao ambao ungemuwezesha yeye kunipa mahaba. Basi ikawa mbili kwa moja.

Niliendelea kutomasana na Matha kimahaba wakati huo nikigugumia kwa utamu aliokuwa akinipa Zhin. Nilihakikisha namgusa Matha sehemu hatari zilizomfanya agumie kimahaba. Mwishowe msichana yule alikuja na kunikalia usoni. Nikawa na kazi ya kuusafisha mgodi wake kwa kutumia ulimi wangu.

"Ashhhh !!!! Nilambe na huku" alinihimiza Matha akitaka nimnyonye kiharage chake. Kazi hiyo haikuwa ngumu. Nilifanya hivyo mpaka alipo vunja dafu.

Sekeseke lilianza wakati Zhin chen alipotakiwa kumpisha Matha naye afaidi utamu. Huwezi amini msichana huyo wa kichina aligoma kabisa. Kukazuka kutokuelewana baina ya wasichana hao ila sikutaka kutia neno maana nilijua ilikuwa ngumu kwa msichana yeyote kushare mwanaume na mwenzake tena katika kitanda kimoja.

Matha alijaribu kumwelewesha Zhin aliyekuwa akiendelea kukichezesha kiuno chake chembamba akihakikisha mpini wangu ulimkosha vilivyo lakini yote hayo, yalishindwa kupenya katika ngoma za masikio ya msichana huyo wa kichina.

"Hivi Zhin uko unanijua kweli"

Aling'aka Matha kwa hasira.

Wakati huo Zhin aliongeza kasi ya kuzungusha mauno yake mpaka alipofika ukomo uliomuacha hoi akijilaza kifuani kwangu bila hata kuuchomoa mpini kutoka kwenye kitumbua chake.

Matha aliendelea kuongea akimtaka msichana huyo kutoka amwachie japo kwa sekunde kadhaa lakini msichana huyo aligoma. Baada ya kuona msichana Zhin ametulia nilimbinua na kupanda juu yake nikaanza kumshushia mashambulizi mazito.

Matha hamu na wivu vilimzidi akatusukuma pale kitandani tukaanguka sakafuni kama gunia.

Nilipiga ukelele mkali wa maumivu baada ya kutua sakafuni. Mpini wangu ulichomoka kwenye kitumbua cha Zhin ambapo kwa kuwa ulikuwa umesimama, nilivyoanguka nikauangukia na kuupindisha. Maumivu niliyo pata hayasimuliki, mpini wangu ulibaki umepinda vivyohivyo. Machozi ya maumivu yalianza kunitoka.

Hapo ilizuka vita nzito baina ya wasichana wale waliokuwa uchi. Kila mmoja alitaka amwonyeshe mwenzake ubabe. Makonde na mateke mazito yalitua katika nyuso za kila mmoja. Nilikuwa sakafuni nikiutazama mtanange huo huku nikiugulia maumivu makali ya kuvunjwa mtarimbo.

Hakika Matha naye hakuwa haba katika mkono Pamoja na unene wa kiafrika aliokuwa nao aliweza kuyakwepa, kukinga na kurudisha mapigo kwa msichana yule wa kichina.

Hatimaye Matha alirusha teke zito lililotua barabara katika tumbo la Zhin. Msichana huyo wa kichina akaanguka chini akiwa hoi. Nazani uchovu wa mechi nao ulichangia. Matha akamnyanyua Zhina na kumkaba shingoni akimwinua kwa mkono mmoja. Zhin akaanza kutupa mikono na miguu huku na kule. Nilijaribu kunyanyuka niamue ugomvi huo lakini maumivu yalinirudisha sakafuni.

Hali ya Zhin ilizidi kuwa mbaya, alijaribu kupumua na kutoa sauti lakini ilishindikana. Kisha nikamwona akiuinua mkono wake taratibu, akaupeleka mpaka shingoni na kukata mkufu wake. Akaushika vizuri na kibonyeza kiurembo cha mkufu huo. Kikaonekana kisu kidogo katika urembo wa mkufu huo. Kwa mwendo wa umeme kisu hicho kikatua shingoni kwa msichana wa kikenya Matha. Msichana huyo alimwachia Zhin na kuanza kutapatapa huku na kule. Damu nyingi ilivuja kumaanisha Zhini aliukata mshipa mkuu wa damu shingoni kwa msichana huyo.

Zhin naye alianguka sakafuni kama mzigo, akawa akikoroma kama chura. Baada ya angaiko la sekunde kadhaa Matha alianguka sakafuni na kutulia. Nilijisogeza mpaka sehemu alipoangukia na kumgusa kifuani kuuhisi moyo wake. Mapigo ya moyo ya msichana huyo yalienda taratibu sana hatimaye yalisimama. Tayari kifo kilimchukua. Nilijikuta nikijilaumu kwa kuwa uwepo wangu mahali pale ulisababisha msiba. Nilijisogeza tena taratibu mpaka ulipokuwa mwili wa Zhin ambaye hakuonesha dalili ya uhai. Nikasikiliza mapigo yake ya moyo na kugundua yalienda taratibu sana. Nilikumbuka kabla ya kuzimia alikuwa akikoroma kwa shida hivyo wazo la kupungukiwa na pumzi lilinijia. Niliupanua mdomo wake na kukutanisha na wa kwangu nikaanza kumpulizia pumzi. Sekunde kumi na tano baadae msichana huyo alikohoa na kufanya nisitishe zoezi hilo.

Niliendelea kukaa pale sakafuni mpaka Zhin aliporejewa na fahamu ikiwa ni baada ya saa moja kupita. Alihamaki baada ya kujiona katika hali ya utupu akakimbilia kitandani akachukua shuka na kujisitiri, akanitazama kisha akamtazama Matha aliyekuwa sakafuni. Alionyesha kushtushwa na hali aliyooina. Akashika paji lake la uso nazani kumbukumbu za matukio ya nyuma zilimrudia. Haraka akanitupia shuka na kuchukua lingine akaenda kuufunika mwili wa Matha. Machozi yalimtoka nikasikia akitamka "kwa heri rafiki yangu, sikuwa na chaguzi nyingine" kisha akanifuata na kuniwezesha kunyanyuka. Tukaongozana mpaka sehemu iliyokuwa na picha kubwa ya mnyama Twiga. Hapo akaweka kiganja chake cha mkono katika uso wa huyo Twiga, mara katikati ya picha hiyo kubwa kukajifungua na kufanya uwazi uliokuwa na usawa wa mlango. Tuliingia pamoja huku nikijikongoja tukafikia sehemu iliyokuwa na makabati makubwa ya vyuma huku kwa mbele kukionekana kitanda kidogo cha hospitali.

"Hii ndiyo hospitali yetu ndogo, mambo yote ya matibabu huwa tunafanyia huku, kwahiyo nimekuleta huku nikutibu tatizo lako ambalo si kubwa sana kama unavyozani"alisema Zhin na kuniongoza mpaka kitandani na kunilaza chali.

Kisha akafunua shuka nililokuwa nimejisitiri. Akachukua kifaa fulani kilichokuwa kimeunganishwa kwenye mashine maalumu iliyokuwa na screen akanimulika na kifaa hicho. Kisha akatazama screen iliyokuwa ikionyesha sehemu ya ndani ya mpini wangu uliokuwa umelala kama mfu na kuniambia, tishu za uume wangu ziliathiriwa kwa mkunjo wa ghafla hivyo kusababisha kupinda kwa sehemu ya tishu hizo huku zikivilia damu. Msichana huyo alijiandaa kitabibu na kunifanyia upasuaji mdogo ili kuondoa damu iliyovilia katika uume wangu.

Nusu saa baadae upasuaji huo ulikamilika lakini akanionya kutosimamisha kwani nitasababisha kazi ya ushonaji kuanza upya.

Nilijitahidi japo ilikuwa ngumu kidogo kwani msichana huyo alipendelea kuvaa vibukta vifupi vilivyoyaacha mapaja yake wazi huku muda mwingi akiwa karibu yangu, akinilisha na kunituliza iwapo nilipata maumivu.

Pambazuko la siku iliyofuata lilikuwa maalumu kwa ajili ya kuuchoma mwili wa Matha jambo lililofanyika ndani ya nyumba ile bila bughudhi kwani kulikuwa na tanuru maalumu lililotumika kwa kazi hiyo. Wiki nzima ilikatika nikiishi katika na Zhin katika nyumba ile, nikiendelea kupona taratibu ijapokuwa nilipata changamoto kwa kuwa tulikuwa jinsia tofauti. Hatimaye nilipona kabisa na kuweza kumsimamisha vilivyo askari bila maumivu.

Hapo niliamua kumaliza haja zote kwa msichana huyo lilifanyika penzi zito lililompagawisha kila mmoja.

Baada ya siku hiyo nilimuweka wazi Zhin kuwa nilitaka kuendelea na mipango yangu hivyo nisinge penda kumuweka matatizoni. Msichana huyo hakuwa tayari kutengana nami, aliniambia yu tayari kwa lolote ilimradi niwe karibu yake. Nilimkumbusha kuhusu visasi alivyohitaji kulipiza kwa manyamera walio isambaratisha familia yake nikimuonya kuwa kufuatana nami kutasababisha ashindwe kuikamilisha mipango yake. Hapo kidogo maneno yangu yalimwingia msichana huyo ambaye aliniachia ujumbe mzito akiniambia alitokea kunipenda sana na hakuwa tayari kuona nikiwa na mwanamke mwingine zaidi yake, akaniomba kwa machozi nisije kumsaliti na siku atakayomaliza kulipiza kisasi chake atarudi kunitafuta ikiwezekana tusaidiane kummaliza adui yangu na kuishi pamoja kama mume na mke. Sikutaka kupinga ombi lake nilionyesha kukubaliana naye, jambo ambalo lilimfurahisha sana akaanza kuchezea kidevu changu kilichojaa ndevu hisia za mapenzi zikanijia nikamshika kwa nguvu kiuno chake dakika chache baadae tukawa ndani ya dimbwi la huba.

Jioni ya siku hiyo nilijiandaa vilivyo kwa kuchukua silaha ndogondogo lakini hatari pamoja na mkufu mdogo alionizawadia Zhin.

Nilianza safari ya kurudi Tanzania ambapo nilikwenda mpaka Mombasa nikachukua boti iliyonifikisha jijini Dar es salaam. Kwa kuwa nilikuwa ni kiasi kikubwa cha fedha nilizopewa na Zhin nilichukua chumba katika hoteli ya kifahari ya Golden Tulip. Kwa kuwa nilijawa na uchovu na mawazo kichwani haswa kitendo cha kusahau kumuuliza Zhin aliyekuwa amemtuma kunishambulia, nilioga nikabadili mavazi yangu na kuvaa mengine nadhifu nikaelekea saluni ambapo nilinyoa nywele zangu katika staili ya kuvutia pamoja na ndevu zangu nikiwaacha wahudumu wa kike katika saluni ile wakinimwagia misifa kibao kwa jinsi nilivyovutia.

Saa mbili na nusu usiku nilikuwa katika hoteli hiyo ya kifahari nikisubiri chakula nilichoagiza. Wakati huo taratibu niliendelea kupata mvinyo kutoka Italia. Haukupita muda mrefu chakula kiliwasili nikaanza kula taratibu. Wakati naendelea kuburudika na chakula kile mara aliingia msichana mrembo ambaye macho yangu hayakutaka kuamini nilichokiona. Hakika kama ni kuumba, mungu hakukosea nisikuelezee sana kwani najua unazijua sifa za msichana mrembo lakini kwa yule ongezea mengi zaidi ya hayo uyawazayo. Wakware wote waliokuwa wakipata huduma zao katika hoteli ile iliwalazimu kugeuka kutazama jinsi msichana huyo alivyokuwa akipiga hatua zake kwa maringo huku kila kiungo katika mwili wake kikizidi kuidhihirishia dunia umaridadi uliofanya na muumba katika mwili wa msichana yule.

Nilimeza funda la mate wakati msichana huyo alivyopita hatua kadhaa karibu yangu na kuniachia harufu nzuri ya marashi iliyozidi kunidatisha, macho yangu hayakutaka kucheza wakati nilipokuwa nikiyaangali a maumbile ya nyuma ya msichana huyo hakika hakukuwa na makosa katika mwili wake.

Alitembea hatua kadhaa na kusimama. Kisha wasichana wawili aliofuatana nao wakavuta kiti na kumkaribisha akae. Taratibu msichana akajiweka kitini.

Nilijipa ushindi baada ya msichana huyo kukaa katika meza iliyokuwa jirani yangu. Nikajiapiza lazima niondoke naye usiku huo.

Kazi ya kula ilinishinda hivyo nikasitisha shughuli hiyo. Nilisogeza kiti ili niweze kutazamana na msichana huyo nikaendelea kupiga mvinyo wangu taratibu.

Nilipokuja kumrushia macho msichana yule niliona akinitazama sana huku haiba usoni mwake ikionyesha tamanio fulani hivi kupitia macho yake aliyoyalegeza, tabasamu laini alilotoa na jinsi alivyoichezesha midomo yake. Mkononi naye alishika glasi ya mvinyo.

Nilirudisha tabasamu nikijitahidi kuonyesha haiba yenye mvuto ambapo kwa kidole kimoja msichana yule aliniita.

Nilinyanyuka pale kitini huku nikitolewa macho ya kutoamini na wakware wale pamoja na wanawake waliokuwa wakimtaza msichana huyo kukiwa na hisia za uchu na chuki dhidi yake.

Nilifika kwenye meza hiyo na kumpa salamu kwa bashasha..

Salamu yangu ikapokelewa na sauti laini iliyokuwa na mvuto wa kila namna pamoja haiba halisi ya kike..


Je nini kitaendelea ? Usikose muendelezo wa chombezo hili lililo tawaliwa na visa vya kila namna.



Nilinyanyuka pale kitini huku macho ya kutoamini ya wakware pamoja na wanawake waliokuwa wakimtaza msichana huyo kukiwa na hisia za uchu na chuki dhidi yake.

Nilifika kwenye meza hiyo na kumpa salamu kwa bashasha..

Salamu yangu ikapokelewa na sauti laini iliyokuwa na mvuto wa kila namna..


Endelea..


Hapo yakafuata maongezi marefu yaliyotiwa nakshi na mvuto wa kihisia uliokuwa kati yetu, kila mmoja akijaribu kuhakikisha unaunasa mtima wa mwenzie. Mwishowe tuliangukia katika penzi zito. Mpaka ilipotimia mishale ya saa sita tulikuwa pale tukiendelea kuburudika na mvinyo huku tukichombezana kwa maneno matamu. Ukaribu wetu ulifanya wasichana wawili waliokuwa wameambatana na msichana huyo wachukue meza ya pembeni ilikutupatia uhuru zaidi.

Sikutaka kuchezea bahati hiyo kwani tayari pombe zilisha itawala akili yangu vivyohivyo kwa msichana yule mrembo Narnia. Ukaribu ukazidi kuwa ukaribu. Hatimaye sumaku ya penzi ilituvuta pamoja. Tukaanza kunyonyana ndimi palepale. Hakika msichana yule kigori, alikuwa na joto kali. Joto hilo liliutetemesha mwili wangu kwa shoti kali ya umeme. Nilizidi kupagawa damu ikanichemka kama niliyetumia dawa kali za kusisimua mwili.

Wakati tukiendelea kupeana mahaba niue, walikuja wale wasichana wawili na kunishika begani.

"wewe tunaomba umuache bosi wetu, hatukuja kwa ajili ya hili unalotaka kumfanyia, hii ni akili ya ulevi tu bosi wetu hawezi kufanya kitu kama hicho, tafadhali tunaomba umuache tuondoke muda umeenda"alizungumza mmoja ya wasichana wale.

Kauli yake ilitulizwa kwa sauti ya laini ya Narnia aliyelalamika kuchoka akataka nitafute chumba kwa ajili ya kupumzika naye huko.

Niliishia kutupiwa macho ya hasira na wasichana wale ambao nao kusema kweli hawakuwa haba. Ila urembo wa bosi wao uliweka uzio katika macho ya wengi wasiweze kuuona urembo waliojaliwa wasichana wale.

Nilimshawishi Narnia akubali tupumzike katika chumba nilichokuwa nimechukua jambo ambalo lilipingwa vikali na wale wasichana wawili lakini kauli ya kukubali ya Narnia iliiziba midomo yao kwa kujazwa pamba. Hatimaye nilikuwa ndani ya chumba kimoja na msichana huyo aliyekuwa kamilifu kila idara.

Kichovu alijibwaga kitandani bila hata kuvua viatu huku akikaa mkao mbya ulioniwezesha kuchungulia kofuli yake nyeupe iliyokuwa ikilisitiri tunda lake.

Nilijikuta katika hisia kali za mapenzi.

"Njoo tulale mpenzi"aliniambia Narnia katika maruweruwe ya pombe.

"Njoo tujimwagie maji kwanza alafu mengine yatafuata"

"Mhh ! sawa bebi wangu ila naomba ugeuke basi nivue nguo"

"Khaa ! Ila wewe kwani unakipi nisichokijua"

"Vyote geuka bana, ujue mi sipendi"

Sikuwa na budi kumsikiliza mrembo huyo kwani nilishachanganywa na muonekano wake ulionivuta kama chuma kwenye sumaku.

Alizidi kunishangaza baada ya kukataa kuoga pamoja na mimi akisema hajazoea. Yote hayo niliyapokea bila kipingamizi lakini nikibaki katika mshangao

Baada ya kumaliza kuoga msichana huyo, nami nilipata nawasaa wa kujimwagia maji huku hamu ikizidi kunipanda kila nilipoikumbuka taswira ya mwili wa msichana yule niliyo uaona baada ya kugeuka kabla hajajifunga taulo.

Nilirudi chumbani na kulitoa taulo nililokuwa nimejifunga, nikalitupa pembeni kabisa.

"Khaa mpenzi ndio nini hicho, mbona unavua nguo mbele yangu ujue sipendi mimi"

Alisema Narnia kauli zilizozidi kunichanganya.

"Kwani mpenzi kipi hujawahi kukiona kwa mwanaume ? "

"Jamani mi sipendi bana jifunike ujue sio vizuri"alisema tena Narnia wakati huo akitazama pembeni kabisa.

"Sasa mbona umerudia zile nguo ulizokuwa umevaa"nilimuuliza kubadilisha mada maana alionyesha kukasirika kidogo.

"Sikuja na nyingine nimefanya kuja kupumzika na wewe tu kwa sababu nakupenda"

"Ok sawa basi haitakuwa vizuri kama utalala na nguo chafu ivue bana ujue na mimi sipendi"nilimwambia kumtega kwani nilishalijua tatizo lake.

"Aku, mi sivui siwezi na wala sijawahi kulala uchi tena katika kitanda kimoja na mwanaume"

Hahah ! Acha kunichekesha bana mbona unanifanyia maigizo, basi kama umeshindwa kutii kauli yangu, nimeamini unipendi lakini kwa kuwa nakupenda ngoja nije kukuvua peke yangu"

Nilimwambia huku nikimsogelea ambapo baada tu ya kumshika paja lake lililoachwa wazi kwa ufupi wa kigauni chake, msichana huyo alitulia kama aliyepigwa na mshangao huku akivuta pumzi kwa nguvu.

Niliuhamisha mkono wangu na kuzidi kuuingiza ndani zaidi huku nikimtomasa taratibu na mkono wa pili nikiuweka kifuani mwake.

Hapo.msichana huyo akaanza kulegeza macho huku akipumua haraka, pia mapigo ya moyo wake yalienda kasi mno. Joto la mwili wake nalo liliongezeka sana.

Nilipenyeza vidole vyangu viwili na kuisogeza kofuli yake kisha nikaanza kukisugua kiharage chake kidogo kilicholoweshwa kwa ute pamoja na joto kali lililokuwa katika mgodi wa msichana yule. Nipojaribu kuingiza kidole mgodini kiligoma kabisa na nilipozidisha msichana yule alirudi nyuma kidogo kumaanisha kuna kitu kiliziba pale.

Naam, maajabu ya karne msichana yule mrembo kuwahi kumuona hakuwahi kukutana na mwanaume kabisa. Alikuwa bikra.

Sikutaka kumuonesha mshangao wangu nilimvua kile kigauni na kichupi chake nikabaki kutazamana na mwili ulioumbika sio mchezo. Chuchu za saizi ya wastani zilizosimama na kujaa vizuri zilinitazama kwa uchu.

Msichana huyo hakuacha kuionyesha aibu aliyokuwa nayo.

Nilimvuta kufuani kwangu na kuanza kuzinyonya chuchu zake kistadi hali ilizidi kumpagawisha msichana yule. Nilifanya kumuandaa kikamilifu lakini mtihani ulikuja wakati nilipotaka kuuzamisha mpini wangu.

Kwakweli msichana huyo alinisumbua sana, kila nilipojaribu kupenyeza, alinisukuma na kubana miguu yake. Hapo niliamua kutumia akili kwa kumtuliza kwa maneno matamu huku nikimlamba sehemu za shingoni na sikioni ambapo alitoa miguno ya utamu. Hiyo ikawa nafasi tosha kufanikisha kazi hiyo ambapo niliizungusha mikono yangu nyuma ya mgongo wake na kuibana kisha kwanguvu nikausukumiza mpini wangu ndani ya tunda lake. Hapo niliambulia kuparuzwa na kucha za msichana yule huku akijaribu kunitoa akilia kwa maumivu.

Ingawa alitoa damu nyingi sikutaka kumsikiliza mpaka hapo nilipoachia wazungu weupe katika tunda lake.

Narnia aliendelea kulia kwa maumivu akinilaumu kumuumiza vibaya. Shuka jeupe lilichafuka kwa damu.

Kwa kuwa haikuwa mara ya kwanza kukata nyuzi. Nilijua jinsi ya kumuhudumia.

Asubuhi hali yake ilikuwa sawa ingawa aliugulia maumivu ya mbali.

"Sam naomba uukumbuke usiku huu, naomba ukumbuke kuwa mimi Narnia nimekubali kulala na wewe na ukautoa usichana wangu. Tambua wewe ndiyo mwanaume wa kwanza na pekee niliyekukabidhi mwili huu na ninaye kupa ridhaa ya kuumiliki mpaka kufa kwangu. Nafanya yote haya kutokana na upendo nilio nao juu yako. Nipo tayari kufanya lolote kwa ajili yako. Nipo tayari kupoteza kila kitu ilimradi uwe karibu yangu. Naomba uniahidi hautousahau usiku huu, hautoniumiza kwa lolote na utakuwa wangu wa pekee maishani."aliniambia Narnia maneno yaliyotawaliwa na hisia kali zilizotoka katika uvungu wa moyo wake.

Sikuwa mtu wa kuvunja moyo hivyo nilikubali na kuweka ahidi kadiri ya matakwa ya mrembo yule. Asubuhi hiyohiyo nilimuomba tunda ambalo alinipatia japo kwa shingo upande huku akiendelea kulalama maumivu.

Saa nne na nusu asubuhi ya siku hiyo tulitoka na Narnia kwa ajili ya kupata chakula ambapo wasichana waliokuwa naye walionyesha kutopendezwa kabisa na kitendo hicho haswa ukaribu uliokuwa kati yangu na bosi wao.

Saa nane mchana nikiwa katika mambo yangu sokoni kariakoo jijini Dar katika umati ule mkubwa wa watu nilihisi nikifuatwa. Wanaume wawili wakizungu walikuwa nyuma yangu wakifuatilia kila hatua niliyopiga. Nilipogeuka walijifanya kuwa bize na mambo yao. Kengele ya hatari iligonga katika kichwa changu. Nilijua mambo yalishaharibika hivyo nikaweka tahadhari. Mbaya zaidi sikuwa na silaha yeyote.

Nilipenya katikati ya umati na kutoka nje ya soko hilo nikachukua hatua za haraka na kutokomea mitaani.

Nikaingia katika jengo bovu na kujibanza. Wazungu wale waliokuwa wakinifuata walipita na kuelekea mbele kunitafuta.

Hapo nilirudi sokoni na kulipia mahitaji yangu kisha nikachukua bajaji na kurejea hotelini. Nilipofika katika chumba namba 125 nilichokuwa nimepanga nilipigwa na butwaa baada ya kukuta vitu vimepanguliwa na kurushwarushwa hovyo huku na kule.

Nilikwenda moja kwa moja mpaka zilipokuwa silaha zangu na kukuta upepo, hakukuwa na chochote.

Hali ya hatari ikazidi kunipa onyo. Nilijinyanyua taratibu mpaka katika kabati ndogo niliyoweka pesa zangu. Vivyohivyo hakukuwa na chochote.

Nilipokuja kunyanyuka nilirudishwa sakafuni kwa teke zito lililotua usoni inchi kadhaa kutoka yalipokuwa macho yangu. Sura nyeupe ya kizungu iliyopambwa kwa pua ndefu na nywele nyeupe ilitazamana nami. Nilijinyanyua haraka na kurusha ngumi nzito iliyotulizwa kwa goti la mzungu huyo mgumu na kuniacha katika maumivu makali. Mzee huyo wa kizungu alitabasamu kabla ya kunishushia konde zito usoni. Kisha akanishika nywele zangu na kukipigiza kichwa changu katika kabati la vioo vilivyopasuka na kuniacha na majeraha usoni ya kuchanwa na vioo.

Nikaona nisipofanya jambo mzungu huyo nisiyemfahamu angeniulia mbali.

Kwa kuwa nilikuwa sakafuni Niliokota kioo kidogo na kukishika pima kisha nikanyanyuka nacho kwa nguvu na kumdunga tumboni mzungu huyo aliyebaki akitoa macho asiamini kilichotokea, akatema damu na kuanguka chini.

Kabla sijajigusa, risasi kadhaa zilitua katika bega na mguu wangu wa kulia. Kisha zikasikika sauti za watu waliokuja wakikimbia kufuata sehemu mlio wa risasi ulipotokea.

Kijana wa kizungu akatoka mbio na kuruka dirishani kisha kwa kutumia kamba yake akashuka mpaka chini ya ghorofa na kuchepuka nje ya mpaka wa hoteli ile.

Waliingia walinzi wa hoteli ile na kunikuta sakafuni ni katika majeraha ya risasi. Simu ikapigwa polisi ambapo dakika chache nilikuwa chini ya ulinzi wa polisi nikipelekwa hospitali. Uchunguzi uliendelea kufanyika katika chumba kile.

Huko hospitali nilikaa wiki mbili nikiendelea kupata matibabu. Nilikuwa chini ya uangalizi wa polisi nikisubiri kusomewa mashitaka ya mauaji yaliyo nikabili. Mwanzoni mwa wiki ya tatu wakati wa usiku nilistuka usingizini na kukuta mwanaume fulani wa kizungu ambaye sura yake haikuwa ngeni machoni kwangu akiwa katika mavazi ya kidaktari akiweka dawa katika dripu yangu. Hapo niliiona hatari iliyokuwa mbele yangu. Taratibu nikaichomoa kwenye mkono wangu sindano iliyounganisha dripu ile hapohapo nikamdunga daktari yule feki aliyeanza kutweta kama chura na kuanguka sakafuni.Niliinama na kumsachi nikachukua bastola iliyokuwa kiunoni mwake.

Nikajinyanyua kwa kujikongoja pale kitandani, nikatoka mpaka nje ya chumba cha wodi ambapo mlangoni ililala miili ya askari wawili waliokuwa wakiniwekea ulinzi mpaka matibabu yangu yatakapokamilika nichukuliwe kizimbani kujibu mashitaka.

Nikavuta hatua na kupita katika korido ambapo huko pia ililala miili ya nesi wawili iliyokuwa na majeraha ya risasi kifuani.

Kidogo nilishukuru kwa kuwa niliweza kuwatoroka polisi wale wa magereza kwani kila siku niliwaza ni jinsi gani nitaweza kuwatoroka.

Kwa kupitia mlango wa nyuma wa jengo lile niliweza kutoka nje ambapo huko nilikutana na mlinzi aliyenifuata akitaka kunisimamisha huyo nikamtuliza kwa risasi iliyotua katika paji lake la uso.

Nikatoka nje ya hospitali kwa kupitia bomba pana la maji ya mvua nikapiga hatua za kichovu mpaka barabarani ambako nilichukua taxi kwa nguvu nikimuamrisha dereva huyo anitoe mpaka nje ya mji. Nilidhamiria kwenda mkoani Tanga kwa mzee Said kwa kuwa nilihisi huko ningeweza kupata msaada na ingekuwa sehemu salama kidogo kwa ajili yangu.

Mpaka inatimia saa Nne asubuhi tuliitafuta muheza ambapo ghafla nyuma yetu ilitokea gari nyingine ikaanza kusikika milio ya risasi. Nilishuhudia dereva taxi akijilaza katika stelingi huku damu zikimtoka shingoni.

Taxi ile ilianza kuyumba na kupoteza mwelekeo. Ikatoka nje ya barabara na kuangukia korongoni..


Nini kitaendelea ? Usikose mwendelezo wa chombezo hili..




Mpaka inatimia saa Nne asubuhi tuliitafuta Muheza ambapo ghafla nyuma yetu ilitokea gari nyingine ikaanza kusikika milio ya risasi nikashuhudia dereva taxi akijilaza katika stelingi huku damu zikimtoka shingoni.

Taxi ile ilianza kuyumba na kupoteza mwelekeo. Ikatoka nje ya barabara na kuangukia korongoni..


Endelea..


Damu nyingi ilitoka katika sehemu mbalimbali za mwili wangu. Taswira katika uso wangu ilipotea kutokana na majeraha makubwa yaliyochukua nafasi katika uso wangu. Damu nayo ilivuja kama bomba.

Nikiwa ndani ya gari ile ndogo iliyokuwa imebinuka ikiharibika vibaya kwa kupondeka na kunibana vibaya sehemu za miguuni. Kwa mbali niliona kundi la watu wakipasua mawe. Watu hao walionyesha kudhohofu sana, miili yao ilipoteza nuru ya afya kabisa. Ilikuwa jinsia moja tu ya kiume. Mavazi waliyovaa watu hao yalikuwa chakavu mno yakiwa na matundu katika sehemu mbalimbali. Rangi halisi ya vazi ilitoweka, rangi ya vumbi ikachukua nafasi.

Mara niliona wanaume wawili waliojazia miili yao wakivuta hatua upande gari lilipokuwa. Wanaume hao walikuwa na haiba tofauti kabisa na wale niliowaona wakifanya kazi, miili ya wanaume hawa ilinawirishwa kwa afya tele. Mikononi mwao walishika fimbo maalumu zilizotengenezwa kwa mkia wa farasi. Nazani zilitumika kulazimisha wale watu dhohofu kufanya kazi.

"Khaa ! Jamaa kapata ajali huyu, halafu anabahati gari haijalipuka."

Alisema mmoja wa wanaume wale huku wakizidi kusogea.

"Hajafa huyu jamaa bado yupo hai"

"Duh, kama yupo hai kweli ujue ni hatari kwetu. Kila kitu kitagundulika. Huyu tunatakiwa tummalizie halafu kama anapesa tuchukue"

"Mimi sioni haja ya kummalizia njoo tusachi kama kuna hela tuchukue, huyu jamaa ni wa kufa tu hawezi pona hata kama tukimuacha".

Alisema mmoja wa wanaume wale jambo ambalo mwenzake hakulipinga. Haraka walianza kukagua sehemu mbalimbali katika gari ile mpaka katika mifuko yangu bila kujali hali mbaya niliyokuwa nao.

Walinyanyua kiti cha nyuma cha gari hiyo na kukuta begi jeusi ambapo baada ya kulifungua, walipagawa na kuanza kupiga kelele.

"Kaka tumeuaga umasikini hizi ni dola kaka begi zima"alisema mmoja kati yao aliyekuwa mweusi wa sura.

"Asee hii bahati kabisa lakini niliyeziona ni mimi kwa hiyo wewe kaa mbali"

"Khaa ! Sasa jombaa unataka uchukue zote !, aki na kuapia siwezi kukubali bora tuonane wabaya"

"Hili chizi ehh ! Yani hela nitafute mimi wewe utajirike wewe kilaini. Dhubutu kugusa hili begi kama sikutoi roho sa hivi"

"Hunijui ehh ! sasa ngoja nikuonyeshe"

Hapo uliibuka mzozo mkubwa wanaume wale wawili waliojazia miili yao kwa mazoezi makali, walianza kuburuzana. Ngumi nzito mateke na kila aina ya silaha zilizokuwa karibu vilitumika katika mpambano huo. Niliwalaani sana watu wale kwani badala ya kuuokoa uhai wa binadamu mwenzao walipigana kisa pesa ambazo hata hawakuzifanyia kazi.

Jasho jingi lililochanganyika na damu lilivuja kutoka kwenye miili ya wanaume wale iliyochemshwa kwa hasira. Begi la pesa liliwekwa juu ya jiwe kubwa lililokuwa pembeni kidogo. Ni vumbi tu ilitimka eneo lile. Ghafla ulisikika mlio mkubwa wa risasi. Ni mpaka vumbi lile zito lilivyotoweka nilipoweza kuishuhudia miili ya wanaume wale ikiwa ardhini. Hawakuwa na hadhi ya kuitwa binadamu, walipewa jina jipya la maiti.

Kwa mbali walionekana wanaume wawili waliokuwa na asili ya kizungu. Walivalia makoti marefu meusi. Walivuta hatua kujongea upande niliokuwa nikiugulia majeraha ndani ya gari la ajali.

Walipofika lilipokuwa gari walisogea karibu zaidi mmoja wao akanigusa shingoni na mtutu wa bunduki. Hapo niligeuza shingo yangu na kumtazama vizuri.

"Ooh ! He's alive" alisema mzungu yule akionyesha kushangaa uhai wangu japo ni muathirika wa ajali ile mbaya kusimulika.

Akaweka mkono katika mfuko wa koti lake refu jeusi na kutoka simu aina ya Nokia sabuni. Akabofya kisha akaongea akiagiza kufika kwa timu ya watu kadhaa.

Kisha ukasikika ukelele wa mshangao kutoka kwa mwenziye akapiga hatua za haraka mkononi akilishika begi lililokuwa na kiasi kikubwa cha fedha. Alipomfikia mwenziye akalifungua. Wooo !! Mshangao ulioje?. Vijana wale wa kizungu waligutuka kwa furaha. Kwa furaha nikaona wakigonga tano na kuweka mipango kibao.

Hapo ndipo nilipotambua utofauti kati ya mzungu na muafrika. Muafrika ni mtu mbinafsi sana na anayejipenda peke yake na yupo tayari kuutoa uhai wa mwenzie kwa ajili ya kitu ambacho hakikuwa haki yake.

Haukupita mda mrefu likaja kundi la vijana watatu wakiafrika. Weusi tii na warefu sana.

Wakapokea maagizo ya kunitoa katika ile gari na kunipeleka katika chumba cha matibabu.

Yote yalifanyika kulingana na matakwa ya vijana wale wa kizungu walionionyesha ubinadamu kidogo.

Siku tatu zilikatika nikiendelea kupata matibabu katika chumba maalumu kilichokuwa ndani ya korongo lile ambapo siku ya nne nilipata nafuu nikiweza kusimama kabisa.

Siku hiyo niliitwa katika ofisi ya mkuu wa eneo lile ambaye mpaka wakati huo sikujua chochote kuhusu yaliyofanyika upande ule.

"A slave is here and he is really strong, look at these muscles" "(Mtumwa yuko hapa na ni mkakamavu kweli, tazama hii misuli) "alisema mzee mmoja wa kizungu aliyenitoa katika kile chumba cha matibabu huku akiushika mkono wangu uliokomaa kwa mazoezi na kazi ngumu.

Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida. Leo hii ndani ya nchi yangu iliyosifika kwa amani katika kila kona ya ulimwengu niliitwa mtumwa. Hapo nikajua nimekamatika. Picha ya watu waliodhohofu niliowaona katika eneo lile ilijirudia katika kichwa changu ikizidi kuniumiza kichwa.

"Boy you are our new slave, you have to work hard, any thing against us we kill you.. Just keep that in mind"

Aliniambia mwanaume mwembamba mrefu kichwani akipambwa na upaa uliong'aa sana kutokana na mwanga mkali wa taa ndani ya chumba kile kilitengenezwa kwa katikati ya miamba.

Ilichukuliwa pingu kubwa ya chuma na kufungwa katika miguu yangu yote ilikuweka ndoto ya kwangu kutoka katika eneo lile.

Vijana wale weusi waliokuwa na asili ya kabila la nubia huko Sudani walinichukua mkokomkoko na kunipeleka katika sehemu kubwa ya wazi iliyojaa watumwa wengine wengi ambao idadi yao kwa kweli sikuweza kuitambua, waliokuwa wakifanya kazi kama siafu miili yao ikidhoofu na kutisha huku wakipokea vipigo vizito kutoka kwa wasimamizi wao ambao wengi walikuwa na asili ya kizungu.

Naam, utumwa ulikuwa ukiendelea ndani ya bara Afrika tena katika nchi iliyonadiwa kwa wingi wa amani na utulivu.

Ni katika mgodi wa siri wa machimbo ya madini ya Uranium uliogunduliwa na serikali ya marekani na kupewa kibali na serikali ya Tanzania kupitia viongozi wake, walioendekeza masilahi yao. Walijua kila kilichoendelea katika eneo lile. Walitambua fika kuwa jeshi la polisi lilitumika kukamata watu bila makosa na kuwapeleka katika eneo lile lililomilikiwa na serikali ya Marekani na kuwafanya watu hao raia wasiokuwa na hatia watumwa katika nchi yao. Hali duni ya chakula, mavazi,malazi na matibabu yaliyochangia asilimia kubwa ya vifo katika eneo hilo, ilieleweka vyema ndani ya bongo za watu hao waliopoteza utu.

Kiasi kikubwa cha fedha pamoja na ahadi timilifu kutoka kwa wazungu hao wauaji ziliwalevya viongozi hao wakasahau utu, pamoja na uzalendo. Wakairudisha nchi katika kipindi cha biashara ya watumwa. Naam, kila mtu mmoja aliyefikishwa pale bei yake ilikuwa zaidi ya dola laki tano.

Lakini jiulize wamarekani hao walipata faida kiasi gani ? . Gramu moja ya madini hayo ya Uranium ambayo yalikuwa na upekee kabisa tofauti na yaliyozoeleka duniani iliuzwa kwa dola za kimarekani milioni mia nane. Jiulize ni gramu ngapi zilivunwa kwa siku na watumwa hao ambao walifanya kazi saa ishirini na nne. Hakika kilikuwa kiasi kikubwa cha fedha, hakika ulikuwa udanganyifu na ulaghai uliopitiliza. Japo sikuwa msomi, kwa fikra za kawaida niliweza kuiona upeo mdogo waliyokuwa nao viongozi wetu. Sikuwa mchumi wa kujua biashara hiyo ingelisaidia taifa kiasi gani lakini, akili yangu fupi na ya kawaida iliniwezesha kutambua madudu hayo yaliyoendelea.

Nikiwa katika kina cha mawazo mara waya mkali ulitua katika mgongo wangu uliokuwa uchi. Nilivaa tu suruali.

Hapo nilikurupuka na kushika nyundo vizuri kisha nikazama katika korongo kuendelea na kazi.

Ingawa sikuwa na elimu ya kitabibu lakini nilipata wazo kuhusu madhara bayo yangeweza kuwapata wachimbaji ambao hawakutumia njia yoyote kujilinda na madhara yatokanayo na mionzi ya madini hayo hatari.

Nilitaja jina la mungu nikiomba aniokoe na matatizo mazito yaliyokuwa yakiniandama kila leo.

Hatimaye siku zilikatika nikiendelea kutumikishwa kama mtumwa katika mgodi ule wa siri usiojulikana sehemu yeyote duniani nikipata mlo mmoja ugali maharagwe wa kuonja kwa siku,nikilala nje na kuwa chakula cha mbu na kukosa matibabu kwa magonjwa madogomadogo, mwezi mmoja ukatimia .

Nilishuhudia vifo visivyohesabika vya watumwa wenzangu wakifa kwa njaa, magonjwa,kiu na vipigo vikali kutoka kwa wasimamizi wa mgodi ule. Hali hiyo ikazidi kuudhohofisha mwili wangu. Nilipukutika mpaka nikafanana na mgonjwa wa ukimwi aliyekaribia mauti.

Kipindi chote hicho sikukaa bure niliendelea kuyasoma mazingira yale na kupanga mipango. Nilitafuta pia watu waliokuwa na mawazo yaliyofanana na ya kwangu. Naam, nilipanga kutoroka katika eneo lile ambalo niseme lilikuwa eneo hatari zaidi katika dunia kwa kipindi hicho.

Mamilioni yaliendelea kuchotwa pale kupitia migongo yetu siye tusiokuwa na kauli. Kila jioni ilitua helikopta na kuondoka na tani kadhaa za madini ya Uranium.

ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog