Search This Blog

Sunday, February 26, 2023

ISABELAH - 5

    


Chombezo : Isabelah

Sehemu Ya: Tano (5)




du! bibi Mbuya aliona sasa pamenuka, akaona bola afanye kitu kuwa saidia vijana wake, ambao sasa nikama walibaki wawili,

baada ya mmoja kupoteza fahamu, na ata kwabahati mbaya wasinge weza kupambana na liyule kiumbe ane mshuhudia mbele yake,

hapo akachukuw kile kimfuko chake alichoifadhi bomu lake, akafunua gauni lake nakuiweka uvunguni mwagauni hilo, ambalo huwa

habadirishi (utamwona kwenye story ya MBUYA NA VITUKUU) alikiwa amekiweka uvunguni kwake kile kifuko akaanza kukata viuno

kama nacheza ngoma flani ya huko visiwani inaitwa 'kidumbatu' huku akiongea maneno mfululizo kwa lugha ambayo mimi binafsi

sijaielewa mpaka leo hii tunapo waletea simulizi hii, wakati huo Yenda alikuwa akiwatazama wale binadamu huku akiwa anaamini

kuwa tayari wmesha slimu amri, lakini ghafla akili ikamtuma mtazame yule bibi nje ya mto, alipo mtazama limwona akifanya

mtendo flani ya kichawi, kwauwezo lionao aliweza kugunduwa nacho kifanya yule bibi, ndipo alipo amua chukuwe jukumu la

kwenda kumzuwia, bibi Mbuya kuona hivyo, akaongeza kasi ya kufanya alicho kuwa nafanya huku akirudi nyuma, lkini Yenda

likuwa amesha karibia hpo kitendo bila kuchelewa bibi Mbuya katowa kile kifuko uvunguni kwake, kisha haraka sana akafungua,

huku Yenda kijaribu kupora, lakini alisha chelewa maana bibi alikwepa kidogo nkuingiza mkono kwenye kile kijifuko alicho

jaza ushuzi, Yenda nae kuona amemkosa akaamua kujaribu tena, nahii kutokana naumbo alilokuwa nalo, maana ili mlazimu kubaki

kwenye maji, huku sehemu ya juu ya mwli wake ikijaribu kusogea nchi kavu, nakupambana na bibi Yenda au bibi mkwe, Yenda

akarushamkono ili kukwapua kifuko kile toka kwa bibi Yenda wakati huo wle vijana wawili wakiwa wametoka kwenye maji, huku

menzao wame mlaza chini kakata moto, walitazama pambano labibi na shemeji yao, bibi aliuona mkono wa Yenda, akakwepa tena

kisha akatowa mkono kwenye kijifuko chake, ukiwa umefumbatwa kisha akaukunjuwa na kupuliza kiganja chake, kuelekea kwa

Yenda, hapo Yenda aliona kitu kama moshi wa rangi ya kijani, ukiambatana na arufu kali sana, akabla haja chukuwa uamuzi

wowote, akaanza kuona arufu ile ikimtibua nakuanza kujisikia vibaya, mala akaanza kuona kizunguzungu, hapo akajuwa

amepatikana, akaona bora ajiokoe kwa kukimbilia kwenye kina cha maji kisha apotee, wadau leo nimechelewa sana kuandaa, husi

ondoke subiri safari na mama mwenye nyumba nikuletee japo kwa ufupi, hapa hapa kwa rafiki




NO 23: ukiambatana na arufu kali sana, akabla haja chukuwa uamuzi wowote, akaanza kuona arufu ile ikimtibua nakuanza kujisikia vibaya, mala akaanza kuona kizunguzungu, hapo akajuwa amepatikana, akaona bora ajiokoe kwa kukimbilia kwenye kina cha maji kisha apotee, lakini alisha chelewa, maana mwili wake ulikosa nguvu nakuanza kulegea, kisha akajibwaga kwenye maji pwaaa! "mshambulieni" bibi Mbuya aliongea kwasauti kubwa sana akiwaambia vijana wake, hapo Kadoda na Kinje wakaingia kwenye maji, nakuanza kupapasa kwenye maji, wakitafuta mapanga yao ambayo waliyadondosha kipindi wakipamba na Yenda, walitafut kwapupa uku huoga umewatawala, maana hawakuamini kama kweli Yenda amekata moto, wakwanza kuliona panga lake alikuwa ni Kadoda, alilinyanyuwa juu pangal ake na kumshushia Yenda kifuani, akaona Yenda anajitikisa akijaribu kujitetea lakini akuwa na nguvu, kilicho fwatia hapo ni mapanga mfululizo yalimshukia Yenda, kuona hivyo Kinje aliekuwa bado ajaliona panga lake, alimua kuinua jiwe kubwa na kumshushia Yenda, sasa ikiwa ni panga kwa mawe, lakini ktk okota okota ya mawe, Kinje akaliona panga moja, akalichukuwa nakuanza kumcharanga Yenda, wakawa kama wana kata kuni kwa kupokezana, mfano ni wale watu wanao twanga kinu kimoja, dakika chache baadae majitoye yaligeuka rangi nakuwa mekundu, kwa jinsi yalivyo tapakaa damu, muda wote bibi Mbuya alikuwa amesimama akitazama kipigo kile, kikiendelea kumshukia mjukuu mkwe wake, alitamani aondoke nakichwa chake kabisa, ili akamwonyeshe Isabelah, maana amewasumbua sana kwakukataa wanaume wapale kijijini, wakati bibi huyu akiwa anaendelea kutazama pambano lile huku akiamini kuwa Yenda amesha poteza maisha, ghafla akajishika sehemu ya makalio kwamikono yote miwili akijiziba, kama mtu aliebanwa na haja kubwa ya kuvurugwa na tumbo, ghafla akastuka tena nakurudisha kiuno nyuma, huku akiamishia mkono mmoja mbele, nakuziba kwenye kitumbua chake, kama amebanwa namkojo, akatazama kushoto nakulia akionyesha kuwa mwenye wasi wasi mwingi sana, akaanza kuongea yale maneno yake yasiyo eleweka, lakini hile ali iliendelea nakumfanya bibi Mbuya aonekane akicheza cheza kama kiduku, mkono mmoja mbele mmoja nyuma "twendeni ameshakufa huyoooo," aliongea bibi huyo, lakini vijan wale hawakusimamisha mapigo, bibi Mbuya aliendelea kukatviuno vya kiduku, nasasa alionekana akiongeza speed, "nyie hacheniiiii, kuna hatari inakuja, mchukueni Njenje tuondoke" hapo wakina Kadoda wakatoka mtoni nakumkabidhi mapanga bibi yao, ambae aliyapokea kwa shida huku akicheza kiduku, "machale yamenicheza, kuna hatari inakuja, tena hipo karibu sana fanyeni haraka tuondoke" dakika moja baade walikuwa wamepotea pale mtoni, wakati huo walipishana na Fadhira akiingia speed pale mtoni, kisu mkunjo mkononi, akaduwaa baada yakumwona Yenda akiwa amelala kwenye maji yaliyo tapakaa damu, akamkagua baadhi ya sehemu ambazo zinge mjulisha kama nimzima au amekufa, alimgusa kifuani na kwenye mkono, haya wadau ilikujuwa kama Yenda ni mzima au mfu, na kujuwa kuwa taharifa ile Isabelah aliipokeaje, ebu endelea kufwatilia kisa hiki, hapa hapa kwa mtu wako




NO 24 wakati huo walipishana na Fadhira akiingia speed pale mtoni, kisu mkunjo mkononi, akaduwaa baada yakumwona Yenda akiwa amelala kwenye maji yaliyo tapakaa damu, akamkagua baadhi ya sehemu ambazo zinge mjulisha kama nimzima au amekufa, alimgusa kifuani na kwenye mkono, kisha akamchukuwa nkuelekea kwenye kina cha kilefu cha maji, nakuzama nae, safari yakurudi kwao ikaanza, huku nyumbani Isabelah allipo yaona yale mapanga yaliyolowa damu, moyo wake ulilipuka, pia kilicho mzidishia hofu kubwa ni tabasamu baya lakutisha la bibi yake, ambae alikuja moja kwamoja alipo kaa yeye Isabelah, Isabelah akawatazama wakina Kadoda na Kinje, walio mbeba Njenje, aliwaonawakimwingiza ndani kisha wakatoka na kunza kupongezana, wakti anajiuliza wanapongezana nini, mala akastuliwa na bibi yake "wewe ebu safisha hayamapanga, kisha nenda mtoni kautazme mzoga wa hawala yko" hapo binti huyu alijuwa kilicho tokea, kwanza aliisi kizunguzungu cha ghafla, akajaribu kusimama lakini miguu ilikosa nguvu, akajikuta akiyumba nakukaa chini pasipo kujari kidimbwi cha maji kilicho tokana na maji machfu yaliyooshewa vyombo, hapo akaanza kuangua kilio changuvu, akimlilia mpenzi wake, kilio ambacho kilikuwa kama burudani kwa bibi mbuya na vijana wake, kiukweli ilitia huruma, Isabelah aliamini mpenzi wake ameshapoteza maisha, tena kwakushambuliwa na mapanga, aliumia sana Isabelah maana aliyahisi mteso aliyo yapata mpenzi wake, kabla yakifo hicho cha kinyama, tena mbaya zaidi ame kufa wakati akimsubiri yeye, Isabelah akajiona kuwa amesababisha kifo cha mtu ampendae, aliwachukia wote waliopo mbele yake, kuanzia bibi yake na wakina Kadoda, alilia sana binti huyu kiasi chakufiki kiasi cha kuomba mungu amchukuwe, wakati huo bibi yake na wakina Kadoda, walikuwa pembeni kabisa wakimcheka Isabelah, wakati Isabelah kiwa anaendelea kulia huku amekaa kwenye dimbwi la maji, mala akastuka kuona kile kidimbwi cha maji kikianza kumeza, kwa maana ya kuongezeka urefu, huku yeye akizama ndani yake, mh! hapo akasimamisha kilio, nakuanza kujiokoa... itaendelea.. ilikujuwa kama alijiokoa au lizama,



walikuwa pembeni kabisa wakimcheka Isabelah, wakati Isabelah kiwa anaendelea kulia huku amekaa kwenye dimbwi la maji, mala akastuka kuona kile kidimbwi cha maji kikianza kumeza, kwa maana ya kuongezeka urefu, huku yeye akizama ndani yake, mh! hapo akasimamisha kilio, nakuanza kujiokoa, lakini hakuweza ndoyo kwanza aliona kizidi kizama, kwenye tule tumaji ambato ata kwenye ndoo tusinge jaa, nasasa alisha zama mpaka tumboni, mwanzo wakina bibi walizani kuwa Isabelah bado anamililia mwanamume wake, lakini walistuka baada ya kuona zile kelel ni za kuomba msaada,ndipo walipo mtazama, nakuona kinacho mtokea binti yao, kuona vile wakina kadoda walisogea kwa haraka, kisha kado akamda mikono nakuanza kumvuta, lakini haikuwezekana maana alikuw mgumu sana, Kadoda akaongeza nguvu na kuanza kumvuta zaidi, lakini haikuwezekana, Isabelah alizidi kuisi kunakitu kinamvuta kwenda chini, tena nikitu chenye nguvu sana, akaingiwa na hofu kubwa sana, akihisi ni adhabu toka kwa ndugu zake yenda, labda wanahisi yeye ndie amesababisha kifo cha Yenda, bibi Mbuya baada yakuona mambo ni magumu aka kimbilia ndani, ile kuingia tu, akasula nguo zote nakubaki mtupu, akachukuwa kile kibuyu chake nakutoa kitu kinacho fanana na kichwa cha mwewe kilicho kauka, aka chukuwa tena vijiti toka kwenye kile kibuyu, akatumbukiza mdomoni, akatafuna nakutemea kwenye kile kichwa cha mwewe huku akiongea maneno yake kwa lugha hisiyo eleweka, huku akizunguka chumba kizima, lkini ghala machale yake yakacheza kama yalivyo cheza kule mtoni, akashikilia makalio kisha akashikilia tena kwambele, akaonekana kuangaika dakika kazaa huku sura yake ikikunjamana kwa hofu.. duu ! kwanini hiwe hivyo.. ebu tusuburi kuona kama watayanusuru maisha ya Isabelah, ni hapa hapa



akatafuna nakutemea kwenye kile kichwa cha mwewe huku akiongea maneno yake kwa lugha hisiyo eleweka, huku akizunguka chumba kizima, lkini ghala machale yake yakacheza kama yalivyo cheza kule mtoni, akashikilia makalio kisha akashikilia tena kwambele, akaonekana kuangaika dakika kazaa huku sura yake ikikunjamana kwa hofu, aliendelea kuangaika huku akijishika sehemu zake nyeti kama kunavitu vinamchoma kwadakika mbili mbele, alipoona imezidi, akachukuwa gauni lake akalikobeka mwilini nakutoka nje, huko alikuta mambo yamezidi kuwa mabaya, maana hakumwona Isabelah zaidi ya Kinje na Kadoda alie kuwa anavuta nywele bila mafanikio yoyote, mpaka ikafikia kiasi cha kuchofoa nywele zenyewe, huku wenzake yani bibi na Kinje wakibaki na mshangao, kumbe Basi Isabelah baada ya kuangaika kujinasua toka kwenye vile vimaji, akisaidiwa na kaka yake bila mafanikio yoyote, alijikuta akivutwa kwenda chini adi alipofikia shingoni nakubaki kichwa tu, kikiwa nje, ndipo alipoanza kuona mabadiliko, licha yakuwa pale chini hapakuwa ndalili ya mto, lakini chakushangaza sehemu yote ya mwiliwake iliyo ingia ndani ya kile kidimbwi cha maji, alihisi kuwa hipo ndani ya bawa kubwa la maji, na kabla haja shangaa vizuri alihisi mwili wake ukikosa nguvu, nakizungu zungu kikali kika mshika, ikafwatiwa nagiza zito usoni mwake, akakata moto, nandicho kipindi ambacho wakina kadoda waliona akivutwa kwa speed kwenda chini nakuzama kabisa, kile chini Isabelah alizinduka naujikuta yupo ndani ya maji, akabana pumzi zake kama wafanyavyo wazamiaji wakwenye maji, alifanya hivyo kwadakika kadhaa, lakini akaona kuna utofauti kidogo, maana aiweza kuona vizuri pasipo kubuguziwa na maji akajaribu kutowa mikono yake mdomoni na puani akaona anapumuwa vizuri kama yupo nchi kavu, wakatazama kushoto kisha kulia, hakuona kitu zaidi ya eneo lote kuzungukwa na maji kuonyesha yupo ndani ya mto mkubwa uliofunikwa na ardhi, alipo tazama nyuma yake akastuka sana.... haya wadau tusimalize uondo wote, like kisha comment kisha subiri mama



lakini akaona kuna utofauti kidogo, maana aiweza kuona

vizuri pasipo kubuguziwa na maji akajaribu kutowa mikono

yake mdomoni na puani akaona anapumuwa vizuri kama yupo

nchi kavu, wakatazama kushoto kisha kulia, hakuona kitu

zaidi ya eneo lote kuzungukwa na maji kuonyesha yupo

ndani ya mto mkubwa uliofunikwa na ardhi, alipo tazama

nyuma yake akastuka sana, ni baada kumwona binti mmoja

ambae ameshawai kumwona malanyingi pale kijijini,

alimwona akimtaza huku akitabasam, kiukweli alishawai

kumwona akiwa na kijana mmoja aitwae James wanapenda

kumwita mjukuu wa mzee Komba, licha ya kukutana nao

malanyingi lakini hakuwa na ukaribu nae, iweje leo

amkute huku chini ya maji, "au ni mzimu", aliwaza

Isabelah juu ya binti huyu, aliemfahamu kwa jina la

Fadhira, kilicho mshangaza zaidi nikwamba, na yeye

anawezaje kukaa kwenye maji na kupumua kama hivi,

akajihisi yupo kwenye ndoto, "husi ogope Isabelah, ni

mimi Fadhira" kama vile Fadhira alikuwa anayasoma mawazo

ya Isabelah, "sasa umenileta huku kufanya nini?"

alijaribu kuongea Isabelah akaweza, "husiwe na pupa

utajuwa muda siyo mrefu, nifwate tafadhari" alisema yule

binti Fadhira ambae ni binti Nguva, kisha akabadirika

miguu nakuwa samaki mtu, akaanza kuogelea akuelekea

mbele akimwonyesha ishala ya kumfwata, inshu ilikuwa

hivi, binti Nguva au Fadhira baada ya kuondoka na Yenda

toka pale mtoni, alimfikisha kwao huku akipiga kelele za

msahada, ndipo walipofika wenzake nakuanza kutoa msaada

kwa kijana Yenda, ambae kipindi hicho alikuwa anasubiri

kutimiza umri wa kukabidhiwa madaraka yake nakuwa mfalme

kamili, matibabu yalianza nakwamuda mfupi tu! alianza

kupata nafuu, huku muda wote akitaja jina la Isabelah

misiri ya mtu anaye weweseka kwenye ndoto, ndipo chifu

wao alie shikilia madaraka kw kipindi hicho, akamwuliza

Fadhira "huyo Isabelah ni nani?"aliuliza hivyo akizani

kuwa Isabelah ni Nguva mwenzao, Fadhira akajibu

"Isabelah ni rafiki yake binadamu" hapo akita waganga

wake nakuwataka wafanye jambo....... ok husindoke ebu



huku muda wote akitaja jina la Isabelah misiri ya mtu anaye weweseka kwenye ndoto, ndipo chifu wao alie shikilia madaraka kw kipindi hicho, akamwuliza Fadhira "huyo Isabelah ni nani?"aliuliza hivyo akizani kuwa Isabelah ni Nguva mwenzao, Fadhira akajibu " Isabelah ni rafiki yake binadamu" hapo akaita waganga wake na kuwataka wafanye jambo, ili kumleta huyo binadamu maali pale, hapo kila mganga bila kuchelewa akaanza maufundi yake, huku wakiwelekeza binti Fadhira aende chini ya usawa wa nyumba yakina yule binti, ata Fadhira alipo uliza kuwa atawezaje na kule kwakina Isabelah hakuna mto, akaambiwa yeye akamate uelekeo, atajionea mwenyewe, ndipo binti Nguva alipo shika njia na kuelekea uelekeo wa kina Isabelah, akitegemea kukutana na ukingo wa mto matimila, lakini chakushangaza kila alipo karibia ukingo mto uliongezeka, adi alipo gota baada ya kufika usawa wanyumba ya bibi mbuya, akiwa me tulia hapo hajuwi chakufanya ndipo alipoona miguu ya bina damu ikichungulia toka kwenye paa la ardhi lililo funika eneo hilo, nayeye hakuzubaa akaiuta ile miguu, akishindana na binadamu waliokuwa wanamvuta Isabelah, wakidai wanamwokoa, binti Nguva alimvuta mpaka alipo fanikiwa kumzamisha, alimwona akiwa amepoteza fahamu, ilikuwa ni uoga,

Huku nako Yenda alipata nafuu huku madoctor wajadi wakiendelea kumpatia huduma ya matibabu, baada ya muda mfupi wa matibabu ya hali ya juu na kwakutumia ufundi wao wote, wale waganga, kijana Yenda alipona kabisa, hapo akasimulia kilicho mtokea huku akionyesha shauku ya kutaka kujuwa mpenzi wake yupoje, ikiwa pamoja na kumfanyia jambo ambalo aliamini kuwa litakuwa zawadi kubwa sana kwa mpenzi wake, lakini kabla haja elezwa chochote akamwona Fadhira akija huku akiwa ameongozana na mpenzi wake Isabelah, kwanza hakuamini macho yake, inawezekanaje Isabelah kuingia kule chini ya maji wakati yeye ni binadamu wa kawaida, akahisi kuwa wenzake wame mchezea kiini macho, ili kumliwaza, maana siyo siri Yenda alionekana wazi kukosa amani, akijuwa ndio ulikuwa mwisho wa yeye kumwona Isabelah, siyo yeye peke yake ata Isabelah pia, baada ya kuogelea kwa mwendo mrefu kidogo, akishangaa kuona anamudu jambo hilo pasipo kuchoka, walipita sehemu ambazo zili mzashangaza sana binti huyu maana aliona mfano wa mji mkubwa sana kie chini ya maji, aliendelea kumfwata binti Nguva, nyuma hukua akishanga mandhri ya sehemu ile, safari iliendelea huku Isablah akijiuliza huku anapelekwa wapi, wakati anawa hili na lile mala......nizawadi gani hiyo? ebu tusubiri kuona kilicho tokea kwenye mkasa huu, chakufanya




walipita sehemu ambazo zili mzashangaza sana binti huyu, maana aliona mfano wa mji mkubwa sana kule chini ya maji, aliendelea kumfwata binti Nguva, nyuma huku akishangaa mandhari ya sehemu ile, safari iliendelea huku Isablah akijiuliza huku anapelekwa wapi, wakati hanawaza hili na lile mala awakatokea sehemu moja nzuri sana yenye Nguva mmoja wa kike mrembo sana, akiwa ameshikilia vito vya mathani vyenye kung'ala kama dhahabu, hapo yule nguva walio mkuta ambae alionekana ndie mpambaji, kwanza aliinamisha kichwa chake kama ishala ya salamu ambayo ana pewa mtu kwa heshima, akimsalimia Isabelah, kisha akaanza kumpamba Isabelah, akishirikiana na binti nguva Fadhira, wakimvishe vile vito vya thamani na mavazi flani yaliyo shikiziwa na vito vya thamani, katika vitu vyote walivyo mvalisha Isabelah, kitu kilicho mshangaza ni kile kidani cha kichwani kama wanavyo vaa malkia, kiukweli kilimwacha na maswali mengi sana, moja kubwa ni kwamba, anaota au ni maluweluwe bada ya kujikuta amelegea na kuona kizungu zungu, mda ule anaanza kuzama kwenye kidimbwi cha maji ya kuoshea vyombo?, maana hakuelewa elewa jinsi mambo yalivyo kuwa yana mtokea, ndani ya dakika kama sela thini tayali Isabela alikuwa ame pambwa akapambika, huku wakificha baadhi ya sehemu zake nyeti, binti ngua alipo lizika na upambaji, ndipo wakaanza safari nyingine, ndani ya dakika chache baadae, walitokea sehemu moja hiliyokaa kama jumba la kifalme, likiwa nangazi nyingi kiasi huku Nguva kadhaa wakike wakiwa wame tanda pembeni ya ngazi hizo, wakishanilia kwa kupiga makofi, ni baada ya kuanza kwa kuinama kama ishar ya heshima kwa Isabelah, kitendo ambacho Isabelah kilimpa laha sana, Isabelah alipo tazama juu kabisa ya ngazi hizo alishanga kumwona mpenzi wake Yenda, ambae alizani atakuwa amesha uawa, bibaada ya kuona mapnga yaliyo tapakaa damu, nasasa alimwona akiwa mzima kabisa, pembeni ya mfalme, huku nywele zake zikizidi kung'aa, kiukweli Isabelah alijwa na fulaha sana, wote wawili wakaonekana kuchekeleana, kama walikuwa hawajaonana miaka mingi iliyo pita,**** tusi wa sahau wakina Mbuya mundu ambao walikuwa hapo nyumbani sehemu aliyo potetela Isabelah nasasa walishuhudia sehemu ile ikianza kujiziba na kuwa kama ilivyokuwa mwazo, ndani ya dakika chache baadae walishuhudia sehemu ikiwa ime rudi kama mwanzo, na hapakuonekana dalili yoyote ya kama kuna mtu alizama sehemu hiyo, hapo ibi Mbuya akaona amezidiwa kete, lakini mwanga ni mwanga tu kama wanga wengine, hakukubali kushindwa, akakimbilia ndani nakusaula nguo zake kama alivyofanya mwanzo, kisha akaanza shughuri, kwanza kabisa akapekua kwenye kona moja ya chumba kile chenye giza nene, na kutoa mfuko mmoja wangozi ijuwi ningozi ya nini ile maana ilitaka kufanana na ya kiboko, akatoa kitambaa cheusi akakitandika chini, kisha akatowa kitu kama fuvu kidogo lenye kufanana na la mtoto mchanga, likiwa lime fungwa kwenye kamba, akafunga kichwani na lile fuvu lika ni'inia kwenye paji lake la uso, akatoa kikamba kingine kilicho fungiwa vimifupa vingi kama vijiti vya kuhesabia watoto wa darasa la kwanza au chekechea, akafunga kiunoni, sasa akafwata kibuyu chake, na kutoa kitu kama unga flani hivi nakuanza kujipaka usoni, alipo maliza akarudi kwenye mfuko, na kutoa kitu kama mkia wenye mabaka mabaka kama mkia wa fisi, kisha aka chukuwa bakuri kubwa sana jeusi sana lenye maji ndani yake, akaweka juu ya kile kitambaa alicho kitandika pale chini akachota ule unga alio jipaka usoni toka kwenye kibuyu, na kumwagia kwenye lile bakuri, kisha akaanza kuzungukz chumba kizima akirudi kinyuma nyuma, na kila alipo fika kwenye kona ya chumba kile, alisugua makalio yake kwenye ukuta, alifanya hivo kwa dakika kama tano hivi, mala akasitisha na kuelekea kwenye bakuri lake, akaonekana kustuka kidogo, maana alimwona mjukuu wake akiwa amevaa kama malkia, akachota tena ule unga na kuumwagia kwenye lile bakuri, kisha akaanza kuzunguka kama alivyo fanya mwanzo, lakini sasa alikuwa anaimba kwa lugha ile ile ambayo kiukweli sijawai kuambulia ata neno moja, lakini alifanya hivo kwa nucta chache tu! akarudi tena kwenye bakuri, hapo bibi Mbuya alipiga ukelele uliombatana n mshangao "toobaaa, nimekwisha mimi yoyooo," hapo ata mimi sijuwi kaona nini kinacho mfanya aseme hivyo? ebu tuwepo




unga na kuumwagia kwenye lile bakuri, kisha akaanza kuzunguka kama alivyo fanya mwanzo, lakini sasa alikuwa anaimba kwa lugha ile ile ambayo kiukweli sijawai kuambulia ata neno moja, lakini alifanya hivo kwa nucta chache tu! akarudi tena kwenye bakuri, hapo bibi Mbuya alipiga ukelele uliombatana na mshangao "toobaaa, nimekwisha mimi yoyooo," hapo alikurupuka na kuchukuwa lile gauni lake na kulikobeka mwilini kisha aka kimbilia nje akisahau kama alisha jilmba kwa yale maunga unga meupe usoni na kifuvu kichwani, alitoka moja kwa moja mpaka mlangoni, nakutazama upande wa njia ya kuelekea mtoni macho yake yaka gota chini ya mti mmoja mkubwa uliopo kwenye pori lililo zunguka mto matimila, ni kama macho yake yaliona kitu ambacho kilizidi kumtia wazimu, wakati Kinje na Kadoda wakimshangaa bibi Mbuya wakamwona akirudi ndani kwaharaka sana huku akipiga kelele, "mayooo! jamani mwengaaaaa" wakabaki wame shangaa akatazama kule aliko tazama mwanzo, yaani chini ya mti ndipo walipo anza kuona kama kuna watu ambao mwanzo hawakuwafahamu idadi yao wamekaa pale chini ya mti, wakaanza kusogelea sehemu ile huku taratibu na kwa tahadhari kubwa, wakiwa wamejawa na uoga, **** huku nako chini ya maji shangwe na fulaha zilitawala, hapo Isabelah alipanda ngazi taratibu akielekea juu huku Yenda naye akitelemka kumfwata mpenzi wake, kila mmoja wao aliona kama ndoto ile tukio hilo, asa Yenda ambae alikuwa anazani amefanyiwa kiini macho, "kama ni yeye akirudi kwao ataona zawadi iliyo mwandalia" walisogeleana kwa mwendo taratibu huku wakitumbuizwa na nguva wakike walioimba kwa ustadi... nizwadi gani hiyo ambayo yenda anaisisitiza sana vipi kuhusu bibi Mbuya? anachanganikiwa nanini, pia tuonane sehemu ya mwisho ya story hii kujuwa walicho kiona wakina Kadoda, mkali wako Mbogo Edgar anakuambia tuwemo Saidatiy Muhammad Muhammad




Isabelah alipanda ngazi taratibu akielekea juu huku

Yenda naye akitelemka kumfwata mpenzi wake, kila mmoja

wao aliona kama ndoto ile tukio hilo, asa Yenda ambae

alikuwa anazani amefanyiwa kiini macho, "kama ni yeye

akirudi kwao ataona zawadi iliyo mwandalia"

walisogeleana kwa mwendo taratibu huku wakitumbuizwa na

nguva wakike walioimba kwa ustadi, wakipuliza

matalumbeta , walipo kutana walikumbatiana na kitu cha

kwanza kabisa wakaunganisha midomo yao nakuanza kulana

denda, kitu hicho watu hawa walikipa kipaumbele sana,

walipenda sana haina hiyo ya romance, walidumu kwa

sekund kadhaa kisha wakaachiana "siamini kama nimekuona

mpenzi wangu" alisema Isabela huku akirudisha tena

midomo yake kwenye midomo ya Yenda nakuendelea kulambana

denda, baada ya dakaika moja wakaachana ni baada ya

kuona vitu vina amka, hapo ika fwata tukio la kumtawaza

lasmi yenda kuwa mfalme na kuwa fungisha ndoa na

Isabelah, kishabaada ya hapo akapewa ulinzi mzito wa

Binti nguva na wengine watatu, "mkewangu Isabelah kuna

watu nataka ukutane nao, tutaongozana wote ukawaone"

alisema Yenda na Isabelah hakuwa na kipingamizi ,

akaongozana na mpezi mume wake, huku walinzi wakiwa

wamewazunguka, mwisho wa safari hii ulimsahangaza sana

Isaelah, maana ilikomea kwenye kingo za mto matimila,

hapo akapewa nguo nzuri, za kimalkia na yenda pia akavaa

nguo za kifalme, huku walinzi wakiongozwa na binti Nguva

walivaa nguo za kiaskari, safari ya kwenda kwakina

Isabelah ikaanza wakiwa wameshikana mikono, dakik chache

baadae walianza kukaribia nyumbani wakina Isabela nyumba

ambayo ni ya kwanza kabisa toka mtoni, lakini Isabela

alishangaa kuona kundi kubwa la watu likishangaa kitu

flani, mwanzo alizani kuwa wanashangaa pale alipo zama

yeye, lakini walipo fika pale watu wote wakageuka

nakuwatazama wao, wakiacha kutazama walicho kuwa

wanakitazama, mala ghafla akaja Kadoda mbio mbio akapiga

magoti mbele ya dada yake, "hooo dada siamini kama bado

ni mzima" aliongea kadoda akitaka kumshika miguu dada

yake lakini walinzi wakiongozwa na binti nguva

walimzuwia, lakini Yenda akawaambia "mwacheni aongee na

dada yake huyo ni shemeji yangu, wakamwacha Kadoda ambae

alikuwa anatililikwa na machozi alianza kuongea "dada

bibi ni mtu mabaya sana , kumbe baba na mama hawakufa,

yeye aliwaficha kiuchawi, leo tume waona mala tu baada

ya wewe kupotelea pale chini," kusikia hivyo Isabelah

alikurupuka na kuelekea kwenye kundi la watu, huku nao

wakimpisha akaingia katikati ya kundi hilo, ndipo alipo

aona baba na mama yak wakiwa katika hali ya kutisha

nywele na kucha zikiwa ndefu sana, pasipo kujari

aliwakumbatia huku machozi yakimtililika, mfalme wa maji

Yenda aliamulu walizi wa wasafishe wale wazee yaani

wakwe zake, kisha wakapewa nguo nzuri sana, baadae

wakapewa chakula kizuri, ndipo Yenda alipo mwambia

Isabelah kuwa hiyo ndiyo ilikuwa zawadi yake kwake,

maana alitambua toka zamani kuwa wazazi wakewali fichwa

na bibi huyu baada ya malumbano ya kukataa kupewa uchawi

na kutaka kurudi mjini, baada ya kusikia hivyo kijana

Kadoda aliomba msamaa kwa shemeji yake huku wazazi wao

ambao walisharudi katika hali zao kama zamani

wakimshukuru kijana Yenda na kubariki ndoa yao kiloho

safi, huku wenye nyumba ya bibi mbuya ambae alikuwa

amejifungia ndani kwa kuogopa kuuwawa na wananchi wenye

hasira kali, wananchi hao walichoma nyumba moto bibi

huyo akiwa ndani, hakuna alie mwonea huruma maana

aliwatesa kwa muda mrefu sana, katin ya watu walio

furahia tukio hilo , alikuwepo kijana Edgar alikuwepo,

unajuwa kwanini nilifulahisana rudi baadae, nikusimulie

alicho nifanyia huyu bibi sina ata hamu naye, mpaka hapo

tumefikia MWISHO WA MKASA HUU, shukulani za dhati kwa

Cheve Peter kwa kutuwezesha kupata burudani hii,asanteni

sana wadau kwa like na comment zenu pia maoni na ushauri

wenu uliowezesha kufanikiwa kwary hii, jiandae kusoma

mkasa wa FADHIRA binti Nguva, hapa hapa kwa mkali wako


MWISHO


0 comments:

Post a Comment

Blog