Search This Blog

Sunday, February 26, 2023

SAFARI - 4

    

Chombezo :  Safari 

Sehemu Ya Nne (4)

wasaidia, ishala ya kumuomba samahani kwa kile kilichotokea, lakini YOROBI hakuwa tayri kufanya hivyo kwani alijihisi yupo sahii kumtandika risasi, binti NGUVA, ndipo binti BERALITA yeye pekee ndie aliye inuwa mkono wake nakuupunga kwa binti NGUVA, kumuaga na kumpa ishara nzuri ambayo hata NGUVA yule nae alijibu kwakunyoosha mkono juu ana kuupunga.

binti NGUVA alishindwa kuwatahadhalisha juu ya huko waendako, alibaki akitazama mabaki yalio salia kwani alihisi kazi bado ya kupambana na PAPA wale, lakini alipoona hali iko shwali wala hakutaka kuangaika, na ndipo alipo jitizama kidonda chake, ambaacho kilianza kuhuma kwanguvu akashikilia jelaha, na kuangalia JAHAZI kwa machungu, kwani alipata tabu ya kupambana nao lakini hawakuona kazi aliyokuwa kafanya, na kumzawadia kidonda ambacho hakusitahiri kukipata, basi nae hakutaka kuonesha kinyongo kwao, alibaki akijisemea moyoni, "hawa ndiyo binaadamu, nilikuwa nawasikia tu," alimkumbuka sana binti BERALITA kwani ndie aliye onesha kuwa anafahamu mchango wake alioutoa wakati huo.

kwenye jahadhi nako, BERALITA alibaki akimlaumu sana YOROBI, kwa kitendo alichofanya kwa binti NGUVA, alimkumbusha kuwa ndiye aliye wasaidia yeye pamoja na MWAIPAMBA, na kumuelezea vizuri juu ya alichofanya, mpaka sasa wao ni wazima, YOROBI alichoshwa na kelele za binti huyu, akamtazama kwa mcho makali sana, hakutaka kuongea mengi, zaidi ya kumuomba asirudie tena kuobgea upuuzi wake, akidai yeye anaamini vipi kuwa yule bint alikuwa nimwema kwao, "mtu akikusaidia japo na wewe muoneshe shukrani" maneno hayo aliyatamka binti BERALITA, kwasauti ya upole yenye hisia kali, huku akimtaka sana YOROBI kuacha visa na pindi aonapo msahada, asitie jeuri zake maana alionekana kuwa kama BEPARI, kumzidi mpaka kiongozi wao chifu.

waliendelea na safari yao huku ikionekana kuwa yenye mikosi, sana licha ya kila mmoja wao kujipa matumaini juu ya kufika, lakini kukweli hali ilikuwa mbaya kwao, safari ya kurudi kwenye makazi yao ilipo kuwa ikiendelea,lakini akuna ata mmoja aliekuwa anajuwa, wanapo pelekwa na mfalme huyo, maana siunajuwa kwenye maji ataukigeuka ulipo toa wewe uelewi labda uwe na compas,ndipo kijana MWAIPAMBA nae alipo changia juu ya swala alilokuwa akipewa somo YOROBI na binti BERALITA, huku akimwambia kile kilichotokea ndani ya maji, na msaada mkubwa alikuwa ni huyo NGUVA, nae MWAIPAMBA alimlaumu, pia huku akimsihii asije fanya tena hayo, kamaita watokea tena mbele ya safari, basi nae alipoona hayo nae YOROBI alikubaliana nao, na kuwaomba radhi juu ya kile kilicho tokea, basi nao hawakutaka kujibizana basi yaliisha na kila mmoja wao kuelekea kwneye sehemu yake ya kukaa, safari ilikuwa imepambamoto, hivi huko wanakokwenda kuna nini? ebu somak kisha nijulishe alfu tuone walicho kikuta mbele ya




NO 14: Basi kila mmoja wao alurudi mahali pake na kuangalia chombo kikichana maji huku kikisonga mbele, ili kufika hitimisho

la safari yao, Basi kijana.YOROBI aliendelea kuongoza vijana wenzake, kukipa nguvu chombo ili wawai safari, yao ndipo nae

alipo tulia, na kufikilia kile alicho ambiwa na binti BERALITA juu ya kufanya makosa kwa binti NGUVA, ane alifikiria sana

nakukili kimoyo moyo, huku akiapa mwenyewe, hatofanya tendo kama hilo endapo akiona NGUVA yoyote akiwapa msaada.

binti BERALITA alikuwa akitizama sana maji huku yeye akifikiria juu ya safari yao, ambayo misuko suko na vijimambo,

vilivyokuwa vikiwaandama kwenye safari yao, basi alifikilia sana, juu ya hayo yanayotokea, kwani lengo lake ni kufika kwenye

kijiji chake salama, hakufahamu ya kuwa walikuwa wameuzwa na licha ya kudanganywa sana, nae alikuwa na imani ya kufika kwao

basi jioni iliingia kwa kasi, kwani matazamio yao hayakuwa ya kulala kwenye maji, ila vile vikwazo vilivyokuwa vikitokea

njiani vilifanya mpaka giza kuingia wakiwa ndani ya maji,

Waliamuwa kuwasha taa, kwenye jahazi lao, huku nae alikuwa nataa yake ndani ya begi lake, nae alipoona wakiwasha taa, nae

aliwasha ili apate mwanga maeneo yalio mzunguka, huku akilinda usalama wake kwani toka kijana MWAIPAMBA kufanya tukio, lile

hakupenda tena itokee juu yake, binti BERALITA.

Basi nae alikuwa makini sana, kwani hakutaka tena kuamini mtu, bali kujiamini yeye mwenyewe tu, kwani wote walikuwa ni

watumwa, nahakilizao uwa wanazijuwa wenyewe, ndipo kwa mbali aliona kitu kama mwangaza flani, lakini hakutaka kujifanya

kimbelembele, kuwa kaona kijiji chao, basi alikaa kimya, akiamini kuwa nawenzake watakuwa wameona, maana sasa likuwa

zikionekana taanyingi sana walizidi kukisogelea, huku akitafakali ule ni mji gani, kwani kulionekana kuwa ni mji mkubwa na

siyo kijiji kama alivyo zowea, kwani taa ziling'aa sana, na kuwaka kila kona, nae akaamua kutulia, mpaka atakaposikia tamko

kutoka kwa kijana YOROBI,

kijana MWAIPAMBA nae alikuwa amekaa pembeni, nyuma ya mrembo wetu, alibaki akimtizama sana binti BERALITA, akimtafakari

binti huyu maana siyo wa kumchezea, asa kwa kile kichapo alichopatia ,hato kaa na kumsahau binti huyo, alipokuwa akimtizama

alimpa heshima zake, kimoyo moyo huku akitupa huusika aliokuwa kauvaa juu ya binti, japo kuwa ni mdogo kuliko kwakw, lakini

kwake ilionekana tofauti sana, na kuwa kinyume chake,... vipijamani nikweli wameanza kuuona mji? ebu tuone katika sehemu ya




NO 15:alibaki akimtizama sana binti BERALITA, akimtafakari binti huyu maana siyo wa kumchezea, asa kwa kile kichapo alichopatia ,hato kaa na kumsahau binti huyo, alipokuwa akimtizama alimpa heshima zake, kimoyo moyo huku akitupa huusika aliokuwa kauvaa juu ya binti, japo kuwa ni mdogo kuliko kwakw, lakini kwake ilionekana tofauti sana, na kuwa kinyume chake, safari ilizidi kusonga mbele, binti BERALITA alianza kujiliwaza kwa kuimba wimbo ambao hata kijana MWAIPAMBA alipousikia tu alivutiwa nao, lakini cha kushangaza hakuweza kumsogelea zaidi, sababu alitokea kumuogopa sana binti huyo, kwa kipigo ambacho hato sahau miaka nenda rudi, basi alicho amua ni kusaidia kuimba wimboule sambamba na mrembo BERALITA, MWAIPAMBA alizidi kuimba kwa sauti ya chini huku akimfatisha binti BERALITA. YOROBI alizidi kuwa amuru vijakazi wake wafanye haraka kwani safari ilionekana ya kutumia muda mrefu sana, huku giza nalo lilitanda, nakusaidia zile taa wanazoziona mbele yao wazione vizuri, huku kila mmoja wao akiwa na hofu juu ya kulala ndani ya maji, huku wakijionea visa na mikasa inayotokea, walianza kupata matumaini ya kufika mapema sana kwenye kijiji chao, na ndipo YOROBI alichukua kifa chake cha kutazamiambali, ambacho kina uwezo wa kuona kilomita ata 20, kwenye maji, na kujua wamefikia wapi, wahenga wanakiita jicho la jini, basi nae alifanya hivyo hivyo, alipoweka tu jicho lake kwenye kionw mbali, akaona kitu ambacho kilimshangaza sana, hakuamini alicho kiona kwa wakati huo, akapachika tena ilikujilidhisha, ndipo alipoona vizuri tena kwa mara ya pili, taa zikimulika kwakung'aa sana. Ndipo alipo wageukia wenzake nakuanza kuangua kicheko, huku akiwachanganya vijakazi wake, na vijana hao walimuuliza "vipi kiongozi kulikoni? mbona unacheka mwenyewe?, tujuze nasi tucheke pamoja na wewe" nae alijibu kwa kujiamini na kusema "haaaaah nimeona kitu ambacho hata nikiwaambia, mtafurahi sana, kwakifupi lisaa limoja mbele tuna weza tukawa tumefika" kauli hiyo ilifwatiwa na shangwe na Vicheko, vilitawara mahari pote, huku sasa ule wimbo wa BERALITA, ulikuwa ukiimbwa na karbia nusu ya jahazi, safari ilizidi kuendelea nawakazidi kusogea, dakika chache baadae, walianza kuona vizuri kabisa bila kutumia kifaa cha jicho la jini, walifanya sherehe, huku wakisahau yaliopita kuwa bahari hiyo ilikuwa ya mahajabu sana, basi walizidi kuongeza kasi ya kukifata kijiji au mji huo maana ulionekana ni kama mji wakisasa, matazamio yao ni kufika haraka, kwani safari iliwachosha huku chakula nacho ni chashida, walishindia mkate mdogo kutwa nzima, binti BERALITA waki wote, akiyashuhudia, hayo nae alitoa tabasamu, ambalo lilimchanganya akili kijana YOROBI, huku kijana huyo alijionesha yuko bize na shangwe za vijana hao. muda ulizidi kuhesabiwa na kijana YOROBI, huku mkadilio wake ni kufika yalikuwa ni kutumia saa limoja au moja na nusu, huku akijitamba kuwa ataonekana shujaaa pindi washukapo ndani ya JAHAZI hiyo. wakati bado watu wana shangilia huku wakiona kile kijiji au mji wanasogelea kwakasi, lakini YOROBI gunguwa jambo lakushangaza juu ya mji ule, kwanza kabisa..... haya sasa husicheze mbali rudi tena baadae ujuwe kama kweli wanakaribia au ni mauza uza, wakati huo unajiandaa kumsoma BINTI NGUVA anvyozimika kwa mjukuu wa Mzee KOMBA,hapa




NO 16:wakati bado watu wana shangilia huku wakiona kile kijiji au mji wanasogelea kwakasi, lakini YOROBI gunguwa jambo

lakushangaza juu ya mji ule, kwanza kabisa, jinsi awalivyokuwa wanausogelea ulemji, japo mwendowao ulikuwa wakawaida, lakini

walionekana wakiusogelea kwaharaka sana, kingine mwonekano waule mji, nitofauti ya alivyozowea kuuona, Basi walizidi

kukata maji, huku kelele za shangwe, zikichangia kuwapa nguvu ya kuendelea na safari yao, wakiamini inaenda kufika tamati,

kufika mahari walipokuwa wakienda. ndipo binti BERALITA,alipojipa moyo kuwa mambo yako sawa, ile kutazama vizuri, mbele

zaidi, aliona wamezidi kukaribia, alizidi kuimba kwa hisia, akisidiwa na wenzake, huku moyoni mwake akiwa mwingi na shauku

ya kukanyaga aridhi yao, kwani kilikuwa ni kipindi kirefu sana, tangu atoke kwenye aridhi yao,

YOROBI aliendelea kuwaahimiza vijakazi wake, kufanya haraka kufikisha chombo inchi kavu, kulikuwa na wengine wakisita

kufanya upesi kufikisha chombo hicho, lakini akilini mwake alikuwa ikiwaza sana, na huku kichwa chake kikiwa kimejaa sifa,

mpaka kikataka kuonekana kupasuka, kwa sifa alizokuwa akizitaka pindi atakapo shuka na kuwafikisha watumwa kwenye ngome yao.

pindi watakapo fika tu atapandishwa cheo, na kumpa ngazi kubwa sana lakini huku akiendelea kuwaza hayo, alishangaaa kuona

kitu kidogo kikitoka kwenye maji na kufika mahari alipo na kuzama tena, ndani ya maji hilo tukio lilimshangaza kijana huyo,

huku ajui nini afanye kwani tukio hilo aliliona mwenyewe tu!, na kuwaza sana kiashirio cha hilo tukio, lakini alitupa kule

mawazo hayo chini, na aliposikia shangwe zikiendelea, alijawa na furaha tele, huku na kule alisahau hata tukio lilitokea

mda mfupi tu na kubaki akitazama mbele nakuona viashilio vyote vya kuwa wamefika.

Upande wa binti BERALITA, yeye alikuwa akiendelea na nyimbo zake, huku akiwa akimkosha sana kijana MWAIPAMBA mpaka kijana

huyo aliona kuvunja ukimya na kumfata binti huyo, uku akiendelea kuimba, ili apate kufurahia pamoja, kuwa wemefika safari

yao, basi nae alifanya hivyo kwa tahadhari sana, maana alijuwa kitachotokea, endapo atakosea kidogo, lakini hatimaye

alimfata, kumbe binti BERALITA hakuwa na mawazo hayo, aliyokuwa akiwaza kijana MWAIPAMBA, yeye alikuwa kawaida tu, yale ya

nyuma alikuwa ameyasahau, basi nae alipomuona tu kijana MWAIPAMBA ... kitugani alichokiona YOROBI, unazani wamefika kweli?

nijulishe kama umesha isoma kisha subiri jibu ambalo utalipata, hapa hapa kwa mdau wako




NO 17: kumbe binti BERALITA hakuwa na mawazo hayo, aliyokuwa akiwaza kijana MWAIPAMBA, yeye alikuwa kawaida tu, yale ya

nyuma alikuwa ameyasahau, basi nae alipomuona tu kijana MWAIPAMBA Alipomwona tu wala hakujawa na hasira nae aliona ni jambo

la lakupiata tu, baada ya mda kidogo walimaliza kuimba, na kuanza kupiga story na kusahau yale yaliopita. kijana MWAIPAMBA

alizidi "mmh samahani dada, BERALITA, nyimbo uimbazo, zinagusa hisia zangu, maana nyimbo hiyo nimeimbiwa sana na mpenzi

wangu, kipindi cha nyuma, kabla sijaletwa huku," binti BERALITA aliimba kidogo ile nyimbo, akimwambia kijana MWAIPAMBA kisha

akamwambia "karibu wala uiogope kwani namimi hii nyimbo, huwa naipenda sana kuimba, pindi nikiwa sina kitu cha kufanya".

ndipo kijana akakaribia huku woga ukimwisha, wkati wakiongea hayo walikuwa waki zidi kukaribia ule mji, lakini kunakitu

tofauti alikiona BERALITA, akamwambia kijana MWAIPAMBA, "tumeuzwa mala yapili"MWAIPAMBA alimwangalia BERALITA, akimshangaa

kwamaneno yake, lakini alimwona binti huyo akiwa amekaza macho yake kule wanako elekea, naye akatazama mbele, "kweli

tumeuzwa tena" maana walishuhudia tofauti na kwao ambapo bandari yao haina majengo marefu yanayo waka taa, kama haya, wakati

kijana huyu akipiga mahesabu ya kujirusha kwenye maji ikiweze kana awakimbie wakina YOROBI, wakati anataka kumwambia

BERALITA, mpangowake huo, aone kama ataukubari, maana aliuona uwezo wake wakucheza na maji, ghafla wakashuhudia zile

taambele yao, zikizima ghafla, wote wakapigwa na butwaa, kimya kikatanda kama dakika moja hivi, huku wakiona mawimbi

yakianza kuwa makubwa kidogo, hapo minog'ono yachini chini ikaanza, kila mtu akiongea lakwake, wengi wakisema wale ni

walinzi wa mwambao, wamezima taa kwaajili ya usalama wa mji hule, kwamaana walitaka kuwa tambua kama ni watu wao au maadui,

wakati kiza kime tawala, mawimbi yakaongezeka kila dakika, wakati kiza kime tawala, mala taa zika waka nakuzima tena,

lakini kila mmoja alione kilicho kuwa mbele yao, ambacho muda wote walizania kuwa ni mji, kila mmoja alipigwa na butwaa

wakamtazama YOROBI, kwamacho yakuomba msaada, ...... unajuwa nini kiliwapata hawa jamaa, ebu tuonane kesho ilinikujuze sifa

tabia na uwezo, wa kitu walicho kiona, pia tuone ilikuwaje, chakufanya nijulishe kama umeshaisoma, kisha kesho mapema sana



NO 18 :wamezima taa kwaajili ya usalama wa mji hule, kwamaana walitaka kuwa tambua kama ni watu wao au maadui, wakati kiza kime tawala, mawimbi yakaongezeka kila dakika, wakati kiza kime tawala, mala taa zika waka nakuzima tena, lakini kila mmoja alione kilicho kuwa mbele yao, ambacho muda wote walizania kuwa ni mji, kila mmoja alipigwa na butwaa wakamtazama YOROBI, kwamacho yakuomba msaada, mbele yao waliona kiumbe mkubwa sana, mwenye umbo la hajabu, likipamwa na mikia kama ya pweza huku, ikiwa na vitu kama macho mengi sana yanayo ng'aa kama taa, ukubwa wakiumbe hicho, nisawa na mlima mkubwa huku vitu kama pembe zikiwa zime chomoza kwenye kichwa cha kiumbe hicho, wakiwa wanatafakari wafanye nini, waka shuhudia mkia mmojammoja wakiumbe kile, ukiinuka juu nakushuka kwakasi kwenye maji, nakusababisha wimbi kubwa, ambali lilipelekea chombo chao kupata msukosuko, kikiplekwa huku na huku, hapo zilisikika kelele, kila mmoja akipiga kelele kwa namna yake, mwengine "mayo" "mawe" "mama yoyo" "nakufa" wakati wakiendelea, kupigakelele, wakashuhudia mikia kama minne ya kiumbe kile, ambayo inafanana kabisa na pweza, kisha akaishusha tena kwenye maji, hapo waliona chombo chao kikizidi kuyumba, huku binti BERALITA hakiwa hajui wapi pakuanzia, mara aliona mkia mkubwa wa ajabu, ulipita karibu kabisa na uso wake nakumguza kidogo, ambao ulimfanya akate moto kidogo, kwani le kumgusa tu! ulimkwaluza, nakumletea maumivu, maeneo ya kichwa chake, nae alidondoka chini hapo hapo na kubaki akiwa kama amezima, na ndipo kijana MWAIPAMBA kuona vile alitoka nduki, kumfwata binti BERALITA pale alipo dondokea, kwalengo la kwenda kumsaidia, haikuwa lahisi hivyo kwake, kwani chombo kilikuwa kiki pata kash kash, kutokana na vurugu za kiumbekile, chenye mikia kama ya pweza, na pembe kama zakifaru, YOROBI alichanganyikiwa, aliganda kwa mda, akishanga sana, ni kiumbe gani hicho mfano wa ngome, na kukaa kati kati ya BAHARI hiyo, akupata majibu na kubaki eme jishikilia kwenye nguzo moja, maana tukio hili lilimfanya achoke kimwili na akili, hapo akakumbuka bastola yake, akaitowa kiunoni, akaishika siraha yake vyema, na kuamlishia vijana wake kupambana vilivyo, kiukweli kilikuwa ni kiumbe cha ajabu, huku akiwa hana hili wala lile akiwa anasubiri vijana wake wawe tayari, iliatowe amri ya mapigano, mara aliona mkia ukija usawa wa kichwa chake, nae alikuwa mwepesi, akainama na kukwepa, hapo akaanza kurusha risasi ovyo ovyo. kuelekea kwa yule kiumbe, lakini kiumbe kile hakikuonyesha dalili yakwamba kina guswa na risasi, huku upande wa kijana MWAIPAMBA alifanikiwa kufika mahari alipo dondokea BERALITA, na kuanza kumpa huduma ya kwanza, huku akiweka jitihada za kumfanya aweze kuamka, arudi kwenye hali yake, araka iwezekanavyo, maana angeweza kupaoteza mahisha endapo ile jahadhi ita pigwa na ile mikia, nakupasuka, huku BERARILITA, akiwa bado kakatamoto, MWAIPAMBA alijitoea kwa jitihada za hali yajuu sana, adi alipo mwona akifumbua macho, hapo MWAIPAMBA akatabasamu, lakini basi wakati BERALITA anajiandaa kuuliza ilikuwaje, akashangaa kuona kitu kikimkamata, NAAM NINI TENA KIMEMKAMATA BINTI HUYU?, WATATOKA KWELI HAPA? AU SUBIRI JIBU




NO 19: MWAIPAMBA alijitoea kwa jitihada za hali yajuu sana, adi alipo mwona akifumbua macho, hapo MWAIPAMBA akatabasamu, lakini basi wakati BERALITA anajiandaa kuuliza ilikuwaje, akashangaa kuona kitu kikimkamata usawa wakiuno na tumbo, ile kutahamaki, lilikuwa ni limkia moja wapo la yule kiumbe alie fanana na pweza, huku likitumia mkia wake kumtoa ndani ya chombo hicho Binti BERALITA, alishangaa sana huku akiwa amekosa nguvu, akiwa hajui nini afanye, basi nae alikubaliana na tukio alilokuwa akifanya JITU hilo, lakini akuhacha kuomba mungu, kwani alijua ndio unakuwa mwisho wake siku hiyo, wakati huo tayari YOROBI alikuwa anamimina risasi, akizani utakuwa msaada kwa binti BERALITA, huku kijana MWAIPAMBA akikamata mguu wa BERALITA nakujaribu kumvuta, ilikujaribu kumchomoa toka kwenye mkia walile dude, haikusaidia kitu, licha ya risasi zote na kuvutwa na MWAIPAMBA, akashuhudia MWAIPAMBA akizidiwa nguvu na kumwachilia, hapo binti BERALITA aliona akipelekwa mpaka kwenye mdomo wa JITU hilo na ndipo alipo fumba macho akutaka kuangalia kitu kinachofwatia, maana alijuwa anatumbukizwa mdomoni, wakati huo akasikia kishindo kikuwa sana kikipiga jahazi, Gafra aliashangaa akiona akishushwaa tena chini huku,wakati huo hakuweza ata kupiga kelele, kwani hakuwa hata na nguvu za kupambana ilikujiokoa, kwanamna ule mkia walile dude, moyoni alisema kimya kimya "MUNGU NISAIDIE MWANAO KWENYE JANGA HILI". alisema hivyo hukuakishangaa hasijuwe nini kime tokea, maana lile dude pweza, lili mshusha huku likipiga kelele, mfano wa ng'ombe dume, lakini ilikuwa sauti kubwa sana, lili mshusha mpaka chini, likiwa bado lime mbana na mkia wake, BERALITA alifumbuwa macho nakushuhudia jahazi lao likiwa limevunjwa matanga yote, huku likiyumba huku nakule, kutokana na dhoruba ya mawimbi yaliyo sababishwa na kiumbe kile cha hajabu, lakini alipo tazama vizuri ndipo alipoona kitu ambacho hakukitegemea, kitu kilichompata matumaini ya kuokolewa, haya sasa ilikujuwa ni msaada hupi






NO 20: kutokana na dhoruba ya mawimbi yaliyo sababishwa na kiumbe kile cha hajabu, lakini alipo tazama vizuri ndipo alipoona

kitu ambacho hakukitegemea, kitu kilichompata matumaini ya kuokolewa, maana alisha kata tamaa kutokana na lie jitu kuto

sikia maumivu ya risasi, BERALITA aliduwaa akiushuudia mkia mmoja wa lile dubwana ukishuka chini ukijitoa kwenye kichwa cha

lile dude, baada ya kupitiwa na upanga mmoja mkubwa sana wa dhahabu, ulioshikiliwa nakijana mmoja alievalia kifalme,

akipambwa na vifaa ya kimapigano navyo ni vya dhahabu,BERALITA alishuhudia kijana yule shupavu akipambana na lile dude,

akilirukia na kukata mkia moja baada ya mwingine, ammbapo lile dude lilikuwa na mikia mingi sana iliyo fanana napweza,

likijaribu kumshambulia yule kijana, ambae alikuwa mjanja sana kuliko dudu pweza pweza, Beralita hakusahangaa peke yake,

walishangaa wengi sana maana hawakujuwa ule msaada umetokea, wapi sasa lile dude lilionekana kulemewa na mashambulizi,

likaanza kufanya vulugu kubwa na kusababisha mawimbi mazito ambayo yali sababisha msukosuko zaidi kwenye jahazi lile, huku

bahadhi ya watu wakione kana wakitupwa kwenye maji, na wengine wakishikilia kwanguvu wasimwagike, lile dudu bado lilikuwa

lime mng'ang'ania BERALITA, huku BERALITA akianza kuhisi vitu kama miba, kwenye ule mkia, vikianza kumchoma bahadhi ya

sehemu katika mwili wake, lakini aliona juhudi ya yule kijana mwenye upanga wa dhahabu, akifanya juhudi za kuli maliza lile

dude, huku akiamini yakuwa kijana yule ndie msahada wpekee, maana vijana wenzake walikuwa wame jishikilia kwenye kingo za

jahadhi, wakishangaa mapambano, kitu kingine kilicho mshangaza BERALITA nawenzake nikwamba, chini ya maji zaidi ya mikia ya

lile dude, waliona kama kuna vitu vinapita kwa kasi, na kulishambulia lile dude pweza, walishindwa kuvitambua kutokana na

kuwa usiku, sasa mikia yalile dude ilianza kuonekana ikitapakaa baharini, lakini bado lilionekana kuwa na nguvu za hajabu,

likiendelea kupambana na yule kijana mwenye upanga wa dhahabu, bado BERALITA aliendelea kuhisi vimiba viki mchoma nakuanza

kusikia maumivu, akashuhudia yule kijana akiangalia pale alipo kuwa amebanwa na lilelimkia la dudu pweza, kisha kama spider

man akamwona akiruka na kuushusha upanga kwenye ule mkia, ulio mviliga yeye kwanguvu zote, lakini kabla upanga hauja gusa

ule mkia, alishuhudia yule kijana, ambae sasa alifanikiwa kuiona atasura yake, kwamba alikuwa wakuvutia kuanzia mwili na

sura, pia akagunduwa kuwa, HAYA MDAU WANGU WANGUVU, MSAHADA UMEFIKA, JE KIJANA HUYU NI NANI? NAHUKO KWENYE MAJI NIAKINA

NANI, AU PAPA WANA TAFUNA MIKIA YA DUDU PWEZA, CHAKUFANYA NIJULISHA KAMA




NO 21 bado BERALITA aliendelea kuhisi vimiba viki mchoma nakuanza kusikia maumivu, akashuhudia yule kijana akiangalia pale

alipo kuwa amebanwa na lilelimkia la dudu pweza, kisha kama spider man akamwona akiruka na kuushusha upanga kwenye ule mkia,


ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog