Search This Blog

Monday, October 24, 2022

KITANDA CHA MPANGAJI MWENZANGU - 2

 





    Chombezo : Kitanda Cha Mpangaji Mwenzangu

    Sehemu Ya Pili (2)



    Ha! Mama Sindilia, unavyoona naweza kufanya upuuzi kama huo kweli, mimi mama Tina? Na ndoa yangu tamu?"

    "Ndiyo nikashangaa. We hujasikia?"

    "Sijasikia kokote."



    "Basi kaa ujue hivyo."

    "Wewe nani kakwambia?"

    "Mh! Mwenzangu hayo mengine sana, tutaonana siku nyingine," alisema mama Sindilia huku akiondoka zake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama Tina nusura presha impande kwani watu wa mtaa ule anawajua vizuri, si ajabu kumwambia mume wake kuhusu tetesi hizo jambo ambalo litamuweka pabaya.

    "Hivi atakuwa nani? Au Halima? Huyu atakuwa Halima tu," alisema moyoni mama Tina wakati akiingia nyumbani kwake.



    Licha ya kuwepo kwa madai hayo, mama Tina alitafuta muda wa kuonana na Os Anjelus ili amsimulie habari za mtaani.

    Ilikuwa wakati kijana huyo amerudi, kabla hajaingia kwake, mama Tina alimdaka kwenye korido

    "Anko kuna kitu kikubwa sana na cha hatari kinataka kutokea."



    "Kinahusu nini anti?"

    "Mimi na wewe."

    "Nini tena anti?"

    "We nenda, usifunge mlango nitakuja kukwambia."

    "Poa."



    Os Anjelus alizama chumbani mwake, akapumzika kidogo kisha akatoka kwenda kuoga, aliporudi alivaa bukta tu na kujitupa kitandani huku akiwa amefungulia feni kwa spidi ya kawaida.

    Mama Tina alimalizana mambo yake, akatembea kuelekea kwa kijana huyo huku akiwa katika hali ya tahadhari. Kabla ya kuingia alimpigia simu Halima akiwa amesimama usawa wa mlango wa chumba chake

    "Halina leo unarudi saa ngapi nataka kukuagiza kitu."

    "Mh! Kusema ukweli nitachelewa sana, kuna sehemu nitakwenda kujirusha, labda kwenye saa sita, saba usiku. Ulitaka kuniagiza nini?"

    "Sabuni."



    "Labda nikununulie nikupe asubuhi."

    "Hapana, nitakwenda kununua pale kwenye duka la urembo la kisimani."

    "Poa."

    Mama Tina akaondoa wasiwasi, maana alidhani Halima angeweza kuingia muda wowote ule. Alizama ndani kwa Os Anjelus.



    "Vipi, naona umelala?"

    "Nimepumzika tu anti, si unajua tena."

    "Ni kweli," alisema mama Tina akikaa pembeni ya kitandani, akashika godoro kulia na kushoto kama anayetaka kuaga kuondoka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mwenzangu, leo nimekutana na mama mmoja jirani, akasema amesikia eti mimi natembea na wewe, he! Nilishangaa sana, mimi sijawahi kupata kashfa kama hiyo hata siku moja katika maisha yangu ya ndoa."

    "Mh! Kweli? Yeye huyo mwanamke alisikia wapi?"

    "Kagoma kuniambia, lakini mimi nahisi Halima."

    "Halima yupi, huyu dada wa chumba cha pili?"

    "Huyohuyo."



    "He! Mbona anataka kuleta balaa."

    "Balaa balaa, tena ni uuaji, maneno kama hayo yakifika kwa mume wangu si ndoa sina!"

    "Kabisa anti. Dah! Ni wa kumwonya lakini."



    "Mh! Mimi sitamwambia kitu, ila Mungu atanilipia, iko siku yake. Mi najua anakutaka ndiyo maana anafanya hivi, yeye anadhani mimi na wewe ni wapenzi," sasa mama Tina alianza kupunguza sauti. Akaendelea

    "Tena naomba anko, isije ikatokea hata siku moja umekaa naye ukasema ninavyokusaidia kusafisha nyumba au kukupa chakula



    "Anti, mi si mtoto, siwezi hata siku moja

    "Unanihakikishia anko?"

    "Kweli kabisa."

    "Mh! Tushikane mikono tule kiapo."



    Os Anjelus akatoa mkono, mama Tina akaupokea, akaubana;

    "Ukikiuka itakula kwako."

    "Siwezi kukiuka."

    "Kweli?"

    "Kabisa."



    "Siamini," sasa mama Tina alimsogelea usoni kijana huyo;

    "We amini."

    "Nifanyie kitu chochote niamini," alisema mama Tina.

    "Unataka nikufanyie kitu gani?"

    "Chochote ambacho mimi nitaamini kweli hutaweza kuanika siri yetu."



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Os Anjelus akashtuka, akamvutia kwake, mama Tina akatua kwenye kifua cha kijana huyo.

    "Jamani, unajua mwenzio nikifanyiwa mautundu kama haya napata tabu," alisema mama Tina kwa sauti yenye aibu.

    "Pole sana anti, lakini ikiwa polepole sidhani kama utananihi," alisema kijana huyo ambaye tangu mwanzo alishahisi kwamba mwanamke huyo ana lake jambo



    Sasa mama Tina alikuwa amelala kifuani kwa Os Anjelus, amelegea kama vile ametoka kutundikiwa dripu kwenye zahanati ya mbali na nyumbani kwake.

    Alikuwa akihema kwa kasi, mapigo ya moyo yalikuwa si yake. Alipojaribu kufumbua macho yalikataa kwa kujisikia vibaya.



    Os Anjelus akajua ni yeye ndiye anayetakiwa kuendesha jahazi la mahaba kwa wakati huo, akamshika na kumtoa kwenye kifua chake, mama Tina akakaa.

    "Anti

    "Be"

    "Uko sawa?"



    Mama Tina alitingisha kichwa kuonesha kwamba hayuko sawa;

    "Unatakaje?"

    Mama Tina kuulizwa unatakaje ikawa kama amechochewa, alimvaa kijana huyo wakaanguka kitandani wote, akaanza kumpapasa sehemu ya kifuani huku akionekana anafanya vile kwa sababu tu ya hali iliyomkumba, la sivyo asingethubutu!



    Os Anjelus alishuka chini, mama Tina akabaki kitandani. Alimvuta miguu na kuichanua kila mmoja na upande wake, wa kaskazini ulikwenda huko wa kusini pia ulishika nafasi yake.



    Ili kumwonesha mwanamke huyo kwamba yeye ni mahiri kwenye soka la chumbani, Os alipeleka kichwa eneo la wachezaji kukutania ili mpira uanze. Hapo palimchanganya sana mama Tina akaanza kuimba nyimbo za maombolezo ya mahaba huku akijitahidi sauti ya wimbo huo isifike nje wakacheza hata wasioalikwa itakuwa aibu kwake.



    Os Anjelus alipoona sauti ya mwimbaji huyo imeanza kukatika, akajua hata mashairi yameanza kumalizika alichotakiwa ni yeye kuingia kucheza ili onesho likamilike.

    Alianza kwa staili ya kushambulia upande wa kulia, akaja wa kushoto ili kumchosha mwanamke huyo ambaye hakuonyesha kushambuliwa wala kujikinga ili magoli yasiingie kwenye lango lake.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dalili za watu kupita nje ya mlango waliokuwemo ndani yake zilikuwa za wazi na mama Tina alimtahadharisha kijana huyo kuwa makini na namna yoyote ya kutoa sauti itakayofika nje kwani itajulikana.

    "Poapoa mama," alikubali kijana huyo huku akiendelea na mashambulizi.



    Ilifika mahali Os ndiye aliyekuwa akimzuia mama Tina kutoa sauti ya juu kwani alikuwa na dalili zote kwamba hakujali tena lile onyo lake.

    "We Tina mama yuko wapi?" sauti ya mpangaji mmoja ilisikika kwa nje, akimuuliza mtoto huyo

    "Sijui," alijibu Tina."

    "Basi nenda ndani Tina."



    "Mi namngoja mama," alisema Tina na kuanza kulia.

    "Ohoooo!" Os Anjelus alihamaki kwa mbali huku akipunguza nguvu za mashambulizi, lakini mama Tina alimhamasisha kwa kumshika mwili na kumwashiria kwamba alichotakiwa kufanya ni kuzidisha kasi ili dakika tisini za mchezo zifike haraka na mambo yaishe.



    Lakini dakika hizo kila kijana huyo alipotaka kuzimaliza kwa kuzidisha kasi, mama Tina aligugumia kwa sauti hali iliyomlazimu mwenyeji wake kumziba kinywa ili waliopita nje ya ukumbi wasisikie anavyoimba wakafika getini ili na wao waingie kucheza kama siyo kushuhudia.

    Mama Tina alipunguza biti ambapo sasa alikuwa akiimbia ndani ya chumba sauti ambayo alikuwa akiisikia mwenyeji wake tu.



    Ilikuwa wakati mama Tina anataka kufika kwenye kilele cha mlima waliokuwa wakiupanda ambapo alitoa uyowe mmoja wa juu kuashiria furaha yake ya kufika akiwa haamini kwa jinsi mlima huo ulivyokuwa na changamoto kibao wakati wa kupanda.



    Nje, au kwenye korido yule mpangaji aliyemuuliza mtoto Tina mama yuko wapi alisikia ukelele wa mama Tina, akashtuka na kusimama.



    Kujua, alikuwa anajua kwamba chumba kile kimeingiliwa na mpangaji mgeni ambaye hamjui jina zaidi ya kumwona, lakini ukelele wa mama Tina kama ulimwingia kichwani japo si kwa ushahidi mkubwa.

    "Mh! Huyo si mama Tina kweli?" alijiuliza yule mpangaji huku mapigo ya moyo yakiwa yanampiga kwa mwendo wa mabasi yaendayo mikoani akiwa haamini hata maneno yake ya kumtuhumu mama Tina.



    "Eti Tina, umesema mama amekwenda wapi vile?"

    "Sijui mimi."

    Yule mpangaji akaingia ndani kwake. Akatulia humo huku anatafakari kama alichokisikia ni cha kweli au masikio yake yalikaa vibaya

    "Hivi mama Tina huyu ninayemjua mimi anaweza kufanya hivi?" alijihoji mwenyewe yule mpangaji.

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Suka nisubiri dakika tano tu, nachukua kitu nakuja unipeleke nilikokwambia," Halima alimwambia dereva wa bodaboda aliyempeleka nyumbani hapo.

    Alikuwa na safari ya kwenda kwingine lakini alilazimika kurudi nyumbani mara moja kwa ajili ya kuchukua kadi ya benki au ATM.

    "Poa anti," alikubali dereva wa bodaboda.



    ***

    "We Tina mbona unalia?" Halima alimuuliza mtoto huyo

    "Mama yuko wapi?"

    Tina aliendelea kulia. Yule mpangaji mwingine akatoka kuungana na Halima pale kwenye korido ili kumuuliza Tina aliko mama yake.



    "Hata mimi nimemuuliza lakini kasema hajui," mpangaji mwingine alisema.

    "Sasa na yeye atakuwa amekwenda wapi mpaka anamwacha mtoto kama maskini hapa nyumbani?" alisema Halima huku akiweka simu sikioni na kumpigia mama Tina.



    Kule chumbani mama Tina alijisahau, aliingia na simu yake lakini hakuipunguza mlio, akashtukia inaita tena namba ya Halima ambaye alimsikia akiongea nje kwenye korido.

    Mlio wa simu ya mama Tina ni wimbo wa Bahati Bukuku wa Dunia Haina Huruma kwa hiyo ulipolia, si Halima wala yule mpangaji aliyeujua, bali hata Tina mwenyewe japokuwa ni mtoto lakini alisema

    "Mama huyo."



    Ilikuwa tabu chumbani kwa Os Anjelus, mama Tina ameshajulikana aliko, Halima amejua mwanamke huyo yumo chumbani kwa kijana mpangaji mgeni;

    "Ha! We mama Tina, mtoto wako analia huku husikii kwani?" Halima aliulizia akiwa amesimama mlangoni sasa



    "Nakuja Halima," ilibidi mama Tina ajifanye ni jambo la kawaida tu yeye kuingia kwenye chumba cha kijana huyo.

    "Sasa mbona hujamuaga mwanao, anaulizwa anasema hajui ulipo."

    Mama Tina alijikusanyakusanya kwa kuvaa haraka na kutoka, uso umechoka, macho mekundu ile mbaya. Alikutana uso kwa uso na Halima pembeni yake akiwa yule mpangaji mwingine



    "Nilikuwa naongea na huyu kaka mgeni," alisema mama Tina huku akiwa anajibalaguza kiaina. Aibu ilimkaa. Alitamani siku hiyo iwe haijafika.

    "Mama," Tina alisimama akilia na kumfuata mama yake hadi miguuni na kumshika.

    "Twende ndani mwanangu."

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Halima aliingia ndani kwake, akachukua kama dakika tatu tu kisha akatoka nje. Mama Tina aliamini anaondoka zake baada ya kuiona bodaboda kwa kutumia dirisha lake la sebuleni.

    Lakini mpaka dakika kumi zinakatika hakusikia mlio wa bodaboda ikilia kuondoka, akatoka. Akamkuta dereva wa bodaboda amesimama upenuni mwa nyumba, Halima hayupo.



    "Yuko wapi huyu msichana?" alimuuliza dereva.

    "Ameingia nyumba ile pale."

    Mama Tina alishtuka sana kwani nyumba aliyoambiwa ameingia Halima ni ya yule mwanamke aliyemuuliza yeye mama Tina kwamba amesikia anatembea na kijana mpangaji mgeni, akakataa.



    "Mh!" aliguna mama Tina.

    Akiwa ameduwaa nje, mara Halima alitoka akiwa anasindikizwa na mwanamke huyo. Walipokutana macho, mama Tina alishtuka sana



    "Mama Tina hujambo?" yule mwanamke alimsalimia.

    "Sijambo za leo?"

    "Salama, hawajambo wengine humo ndani kwako?"



    Salamu hiyo ilimshtua sana mama Tina, kabla hajamjibu ikawa inajirudia kichwani mwake

    "Salama, hawajambo wengine humo ndani kwako?"

    "Hatujambo, Tina hajambo yupo ndani," mama Tina aliiua salamu ya mwanamke huyo kwa staili hiyo.



    "Na mpangaji wenu mgeni naye hajambo jamani?" yule mwanamke alisema akiachia tabasamu la msuto kwa mama Tina. Halima naye alicheka akimwangalia mama Tina kwa macho ya kumsuta au kugundua kile alichokifanya chumbani kwa kijana mpangaji mgeni.



    "Mh! Na wewe mama nanihii bwana, una maneno mengi," alijibalaguza mama Tina lakini uso wake ulionesha kukasirika kiaina.

    Halima alipanda bodaboda na kuondoka huku akimwacha mama Tina bado amesimama nje kwa aibu. Yule mama jirani alishaingia ndani kwake.



    Mama Tina baadaye sana aliingia ndani, akapitiliza hadi chumbani kwa Os Anjelus

    "Kimenuka. Huyu malaya amekwenda kumwambia mwanamke mmoja jirani," alisema mama Tina akiwa amesimama.



    "Da! Kwa hiyo?" Os Anjelus aliuliza.

    "Hata sijui. Ila nitajua cha kufanya. Lakini siwezi kuondoka bila kukupiga busu japo moja tu;mwaaa. Lakini umenifurahisha hata kama tuliingiliwa," alisema mama Tina na kutoka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ***

    Usiku wa saa tano, Halima alirejea nyumbani hapo na kukuta nyumba yote kimya! Wapangaji wengine walishalala.

    Aliingia ndani kwake, akaweka mkoba na kubadili nguo kwa kuvua alizovaa na kujitupia kanga moja tu iliyokatisha kifuani kwa kuziba nido tu.



    apo kwa ndani hata kufuli' hakuwa nayo.

    Alifungua mlango akatoka, akaenda kusimama mlangoni kwa Os Anjelus. Alikuwa akiwaza amgongee au la! Aliamini akigonga, wengine watasikia.



    Katika kufikiria huko alijikuta akishika kitasa cha mlango, akakizungusha, mlango ukafunguka. Kumbe haukufungwa kwa funguo.

    Bila woga, Halima alizama ndani kama mwizi huku akimtupia macho kijana huyo aliyekuwa akiuchapa usingizi.



    "Huenda walikubaliana na mama Tina mlango uwe wazi ili aingie muda huu," aliwaza moyoni Halima huku akiwa amesimama mbele ya kijana huyo bila woga wala kujifikiria itakuwaje endapo ataamka.

    "We kaka wa Kingoni;we kaka wa Kingoni," alisema Halima akimwamsha mpangaji huyo kwa kumtingisha.



    Os alishtuka na kujikuta ana mgeni bila kumtegemea;

    "Vipi, mbona ulilala mlango wazi?"

    "Khaa! Nilifunga anti, ila sikufunga kwa funguo nilijisahau."

    "Mimi nimeukuta upo wazi kabisa, nikahisi wezi wameingia."



    "Mh! Kweli?"

    Os alifikiri na kuhisi kwamba mama Tina aliingia akamkuta amelala, wakati wa kuondoka akasahau kuurudishia.



    "Uwe makini anko, utakuja kuibiwa siku moja," alisema Halima huku akikaa kitandani.

    "Vipi, siwezi kulala na wewe kwa usiku wa leo kaka;angu?"

    "Sasa sista umeshasema kaka;ako kuna sababu gani ya kulala na mimi?"

    "Haya, tufanye si kaka ni watu tu."



    "Mh! Ungekwenda kulala kwako tu."

    "Hamna bwana, mwenzio najisikia," alisema Halima akimshika kijana huyo na kumvutia kwake.

    "Halima unatangaza kwa watu mimi nalala na huyo kijana mbona na wewe upo kwake tena usiku huu?" sauti ya mama Tina ilisema mlango ukiwa wazi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wote walishtuka mle chumbani, mama Tina akaganga. Halafu alivyo jasiri akapenyeza mkono na kuwasha taa ya ukutani, tap! Kukawa na mwanga.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog