Search This Blog

Monday, October 24, 2022

TINGINYA LA BA'MDOGO - 2

 





    Chombezo : Tinginya La Ba'mdogo

    Sehemu Ya Pili (2)



    ALIENDELEA kumtesa Tonny na kumfanya awe akifumba-fumba macho na kuonekana kuwa yuko mbali zaidi kifikra, akikunja na kuikunjua miguu yake.



    Caroline alikuwa mtundu sana katika fani hii. Humo ndani mwake alikuwa na mkanda wa video wa picha za ngono uliochezwa na wasanii wa filamu wa Amerika Kusini. Ulikuwa ni mkanda wenye kila kitu kinachopaswa kufanywa na mwanamume na mwanamke anayependa kufanya ngono kikamilifu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ni mkanda ambao ulimpa ujuzi maradufu Caroline na akaamini kuwa bila ya kujiachia na kutokuwa na kinyaa kamwe hataweza kufanikiwa katika zoezi analotaka kufanikisha. Na aliamini kuwa ni utundu na ubunifu wake wa hali ya juu ndiyo sababu zilizomfanya hata akafanikiwa kimaisha japo bado anaishi hapo Kariakoo akiwa amepanga chumba.



    Kutahamaki saa 6 usiku!



    “Haa! Tonny,” kwa mara nyingine Caroline alimwita. “Huendi kwa mkeo?Saa sita hii!”



    Tonny alishusha pumzi ndefu akatupa macho darini.Kisha akajibu, “Leo siendi,” hatimaye alijibu, sauti yake ya chini ikionyesha dhahiri kuwa hatanii.



    “Huendi?!Kwa nini?”



    “Basi tu.”



    “Bwana nenda,” Caroline alimwambia kwa sauti ya deko huku kwa 'mapozi' akiutumia ulimi wake wa moto kunyonya hapa na pale.



    “Nasema, leo siendi,” Tonny alisisitiza. “Kulala kwako usiku kucha itakuwa mara ya kwanza kwangu, na pia itakuwa ni mara ya kwanza kulala nje, tena kulala na mwanamke. Hii itakuwa ni mara ya kwanza tangu nifunge ndoa na Lilian. Najua nitakaporudi nyumbani asubuhi, patachimbika.Lakini siendi.”



    Caroline akaguna.Kisha akamuuliza, “Sasa kwa nini usiende?”Hakusubiri jibu, aliongeza, “Mimi sijawahi kuolewa, lakini napenda kuwa na mume wangu.Nawaonea wivu wanawake wenzangu wenye waume zao.Hata mkeo namwonea wivu.Lakini ninamwonea huruma kuwa katika ndoa yenye matatizo.”



    “Ndoa yenye matatizo?” Tonny alimuuliza kwa mshangao.



    “Ndiyo,” sasa Caroline alikuwa ameacha kufanya ule utundu wake. Akawa ameukita mkono wa kushoto kwenye mto. Akaongeza, “Ana ndoa yenya matatizo. Mumewe saa hizi yuko kwa Caroline, na hataki kurudi kwake. Hiyo ni ndoa gani?”



    Tonny alisonya na kusema, “Achana na mambo ya Lilian. Tule raha mpenzi.” Wakati huo alishamvuta tena Caroline na kumkumbatia. Akambusu shavuni na kumpapasa makalio.



    Caroline aliutoa mkono huo kistaarabu, akaendelea kusema, “Nenda bwana.Usimuudhi mkeo. Tukitaka tule raha kwa uhuru usimuudhi mkeo. Mtu mwenyewe yule anaonekana ni mtulivu, s'o mhuni ka' akina Caroline hapa.” Baada ya kusema hivyo akacheka kidogo.



    “Sio mhuni?Unajuaje?”Tonny alimuuliza.



    “Anaonyesha tu,” Caroline alijibu.“Ni mtu anayekuheshimu.Sasa kwa nini uanze kumfanyia vituko vya aina hii?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nataka aondoke.”



    “Aondoke?!” Caroline alimkazia macho Tonny, akionekana kushangazwa na kauli yake. “Unataka aondoke!Yaani mwachane?Ndoa ivunjike?”





    “Nd'o maana'ake,” jibu la Tonny lilikuwa la mkato.



    “Kwa nini?”



    “Ili wewe uchukue nafasi.”



    Yalikuwa ni maneno yaliyomshtua Caroline. Akamkazia macho Tonny. Akauona ukweli wa maneno yake katika uso wake.



    “Huo sasa ni uzushi, Tonny,” hatimaye Caroline alimwambia. “Masihara hayo. Huwezi kuchukua uamuzi wa kunioa kwa siku hizi chache tulizofahamiana. Ni mapema mno.Bado hujaijua vizuri tabia yangu. Bado...”



    “Sihitaji muda zaidi wa kuchukua uamuzi huo,” Tonny alimkata kauli.“Mradi ni'shakupenda, basi.Tutajuana vizuri mbele ya safari.”



    Kicheko cha chini kikamtoka Caroline. Pamoja na kuingiwa na upendo kwa Tonny, hata hivyo hakuwa na wazo la kuolewa naye. Kuolewa! Aolewe halafu awe kama aliyetiwa pingu! Na halafu huenda baada ya siku kadhaa naye akafanyiwa vituko kama hivi anavyofanyiwa Lilian!



    Ni mawazo hayo yaliyomfanya acheke kichini-chini, na kukikata ghafla kicheko hicho. Badala yake, kwa upole akamwambia, “Sikia Tonny, huna haja ya kuachana na mkeo. Ishi naye, mtunze familia.Tayari mna mtoto.Unadhani mkitengana mtakuwa mnamweka mtoto wenu katika mazingira ya aina gani? Kaeni kwa amani na utulivu. Siku ukiwa na nafasi unakuja tunakukuruka halafu unarudi. Leo nenda.”



    Tonny aliguna.Akamkazia macho Caroline.Kisha akamuuliza, “Lakini kwa nini unasisitiza n'ende?Au kuna mtu wako anayekuja kulala hapa?”



    Caroline alicheka, kikiwa ni kile kicheko chake cha kimbea-mbea. Kisha akabibitua midomo. Na kwa kuwa hakutaka shari, alisema, “Aah! Babu we! Mwanamume umekazania ka' ni ugali! Haya lala, ule tani yako…utachoka mwenyewe!” akajigeuza kivivuvivu na kulalia tumbo.



    Taswira iliyojitokeza hapo kikawa kivuto kingine kilichomchanganya Tonny kwa kiasi kikubwa. Kulikuwa na kijimlima kilichojitokeza na kumsisimua Tonny.



    Mwanamume akawa akimtazama Caroline kwa uchu mkubwa.



    Hakuvumilia zaidi, akaupeleka mkono na kuutua juu ya makalio hayo makubwa yaliyobinuka. Mkono huo ukakosa ustaarabu zaidi pale ulipoanza kutomasatomasa kwa namna iliytomfanya Caroline agunegune huku naye akiyatikisatikisa makalio yake hayo yaliyokuwa ndani ya kanga pekee, uteketeke wake ukimfanya Tonny aendelee kufanya kile alichokuwa akikifanya.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hatimaye Caroline akasonya na kugeuka. Akamtazama Tonny kwa macho ambayo ni kama vile alikuwa amekerwa na kile alichokuwa akifanyiwa. kisha akainuka na kuketi. Akaendelea kumtazama Tonny huku kakunja uso kisha akamuuliza, “Nd’o nini ivo Tonny jamaniii?”



    Sauti yake ya deko, iliyojaa mikwaruzo isisimuayo, ilizidi kumchanganya Tonny. Akawa akiyamininyaminya makalio hayo huku tayari mwenye kule chini kukiwa kunatuna.



    “Jamani Tonny,” Caroline aliendelea kulala huku akijitikisa zaidi na kutanua miguu, hali iliyozidi ‘kumuua’ Tonny.



    Mwanamume akashindwa kusubiri zaidi.Akaipandisha kanga hiyo mgongoni mwa Caroline kisha mwanamume akapanda. Caroline akamkaribisha kwa kuichanua miguu zaidi na kujibinua zaidi. "Aaa...Asss...Assaaante..." ikamtoka kwa taabu wakati aliskia kitu chenye joto, kilichokakamaa kikipenya kwa poazi la aina yake.



    *****



    KAMA kuna usiku uliokuwa wa ajabu na wa kuogofya kwa Lilian basi ni huu uliopita. Kama kuna asubuhi ya majonzi na mawazo chungu mbovu akilini mwa Lilian basi ni hii ya leo. Tangu Tonny alipoondoka jana asubuhi, hadi jua lilipotokomea hakuwa amerudi. Na ilipofika saa 6 usiku, Lilian alianza kuingiwa na wasiwasi. Hakukijua kilichomsibu mumewe. Na wasiwasi huo ulitokana pia na pale alipojaribu kumpigia simu na kukuta haipatikani.



    Hakupata usingizi usiku kucha hadi kunakucha! Na hapo ndipo zile fikra za kuchelewa kurudi zilipotokomea na badala yake fikra za mumewe 'kulala nje' zilipotwaa nafasi.



    Mabadiliko yaliyoanza kujitokeza kwa Tonny tangu alipopata mafao yake yalimtia shaka Lilian. Na wasiwasi huo uliegamia zaidi katika nyanja ya ufuska. Alijiwa na hisia hizo tangu Tonny alipoanza kuchelewa kurudi nyumbani, na akirudi anakuwa amelewa, na pia akawa hayuko tayari kutoka naye 'out' kama ilivyokuwa kawaida yao kwa takriban mara mbili kwa wiki. Sasa huyu Tonny amekuwa sio tena wa kuchelewa kurudi bali ni wa kulala hukohuko!



    “Ee Mungu mlinde mume wangu huko aliko, arudi salama, mengine tutayajulia hapahapa,” alinong'ona kwa uchungu. “Kama kweli amekumbwa na matatizo, nd'o tutajua. Mradi tu arudi salama,” alisema hayo akiwa amejilaza kitandani, saa 11:30 alfajiri, hasira zikizidi kumpanda.



    Saa 12.30 akasikia mlango ukigongwa. Akashtuka na kujitoa kitandani. Akajitanda kanga na kuufuata mlango.



    “Tonny! Tonny!” Lilian alinong'ona kwa hasira, macho yake mekundu yakimtazama Tonny kwa shari. “Tonny...Baba...” sauti ikamkwama. Akabaki akimtazama Tonny bila ya kupepesa.



    Macho yao yaligongana. Kwa sekunde chache wakawa wakitazamana kama majogoo, kila mmoja akihema kwa nguvu. Tonny akajipa ujasiri wa aina yake, ujasiri uliomfanya ajikute akiwa na uwezo wa kumjibu Lilian.



    Akaingia ndani huku akifoka, “Acha kushangaa-shangaa ovyo. Zungumza kitu kinachoeleweka s'o unakalia kunitumbulia mimacho ka' vile umeona kitu kigeni.We vipi?”



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    MACHO yao yaligongana. Kwa sekunde chache wakawa wakitazamana kama majogoo, kila mmoja akihema kwa nguvu. Tonny akajipa ujasiri wa aina yake, ujasiri uliomfanya ajikute akiwa na uwezo wa kumjibu Lilian.



    Akaingia ndani huku akifoka, “Acha kushangaa-shangaa ovyo. Zungumza kitu kinachoeleweka s'o unakalia kunitumbulia macho ka' vile umeona kitu kigeni. We vipi?”



    Lilian hakujibu. Alimpisha mlangoni na kubaki akimsikiliza huku akimsindikiza kwa macho. Kilichomshtua na kumshangaza Lilian ni manukato makali ya mumewe yaliyokijaza chumba hicho. Humo ndani walikuwa na chupa mbili za manukato, lakini sio manukato ya aina hii.



    Haya manukato yaliyotoka mwilini mwa Tonny yalikuwa makali, na Lilian alijua ni ya thamani ya kiasi gani. Lakini hakuwa na haraka. Hakutaka kuchukua pupa. Alimwacha aingie ndani akidhamiria kufanya mambo kwa utaratibu na sio kuyamwaga hadharani kwa masikio yasiyohusika.



    Baada ya Tonny kuingia, Lilian naye akamfuata huku akiufunga mlango nyuma yake. Akamtazama Tonny ambaye sasa alikuwa akivua nguo na kuvaa taulo.



    “Tonny,” Lilian alimwita kwa sauti ya chini.



    Tonny hakuitika. Alitwaa sabuni na kuanza kuufuata tena mlango.



    “Tonny, si nakuita?”



    “Subiri kwanza nikaoge,” lilikuwa ni jibu la Tonny.



    Lilian bado hakuwa na makuu. Alimpisha na kumwacha akielekea bafuni. Alipobaki peke yake chumbani, aliketi kitandani na kujiinamia kwa huzuni. Akajiuliza ni kipi alichomkosea Mungu? Hakuiona raha ya ndoa yake. Wala hakuiona faida ya kuolewa. Machozi yakachuruzika mashavuni na kusahau kuyafuta.



    Mara akakurupuka na kuzifuata nguo za Tonny. Akazishika na kuzisogeza puani. Ile harufu kali ya manukato ikajidhihirisha katika shati. Kwa hasira akazitupa kitandani huku akisonya. Akaendelea kujiinamia.



    Tonny aliporejea kutoka bafuni alimkuta bado kajiinamia. Hakumshtua, alifungua kabati na kutoa nguo nyingine. Akawa katika zoezi jingine za kubadili mavazi. Ilionekana kuwa alitarajia kutoka tena asubuhi hiyo.



    “Tonny,” kwa mara nyingine Lilian alimwita, sauti yake ikitoka kwa shida. Hatimaye akaamua kumwita kwa jina mtoto wao. “Baba Sambe unanisikia au ndiyo dharau yenyewe?



    “Unasemaje?” sasa Tonny alisitisha kila alichokuwa akikifanya. Akamtazama mkewe kwa macho makali.



    “Una matatizo gani?” Lilian alimuuliza, safari hii naye akimkazia macho.



    “Kivipi?”



    “Haueleweki-eleweki. Unataka kun'ambia nini kuhusu wewe kulala nje leo?”



    “Hilo siyo tatizo,” Tonny alijibu kwa kujiamini. “Najua umeshawaza kuwa nimelala kwa mwanamke. Sishangai, ni kawaida ya wanawake wengi kuwaza hivyo pale mume anapotokea kurudi nyumbani asubuhi.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Tonny! Usinifanye mie chizi au mtoto mdogo!” Lilian aliwaka. “Nimechoka. Nimechoshwa na tabia yako. Hivi una mawazo gani wewe? Yaani hujijali wala huogopi Ukimwi!”



    Tonny hakuonyesha kujali. Aliendelea kujiandaa, na sasa alikuwa akijitazama kwenye kioo huku akijifuta uso kwa leso. Hali ya kuonekana kutoyajali maneno aliyoambiwa ilimkera sana Lilian.



    Akasonya huku akinyanyuka. Akatwaa mswaki na kwenda nje kusafisha kinywa. Dakika kadhaa baadye akarejea na kutwaa sabuni kisha tena akatoka. Sasa alikwenda bafuni kuoga.



    Akiwa huko bafuni bado hasira zilimtawala kwa kiwango kikubwa, lakini ikafikia wakati akahisi mzigo ukimtoka. Akacheka kwa sauti ya chini, kicheko kisichokuwa na chembechembe zozote za furaha lakini kilichomtia faraja kwa kiasi fulani.



    Alipotoka bafuni alifikia chumbani ambako hakujali Baba Sambe anafanya nini. Jambo jingine ambalo lilimfanya afarijike ni kutokuwapo kwa mwanaye, Sambe aliyekuwa na umri wa miaka mitano. Mtoto huyo alikuwa Arusha kwa mjomba wake. Angerudi baada ya miezi minne au mitano.



    Hivyo, Lilian alijiona kuwa ana uhuru zaidi ya uhuru wa kawaida. Papohapo akatwaa mafuta na kuanza kujipodoa. Hakujali wakati huo mumewe atakuwa anafanya nini, alijali kukamilisha alichokuwa akikifanya. Kisha akatwaa suruali nyeusi, nyepesi ambayo mara nyingi alishindwa kutoka nayo kutokana na ilivyokuwa ikimshika sana makalio. Leo akaivaa na kufuatisha ‘tisheti’ nyeupe juu.



    Hakuweza kutoka hivyo alivyo, bado alijali heshima kwenye macho ya watakaomtazama huko nje. Hivyo, alitwaa kanga na kujifunga kifuani; akiichukulia hatua hiyo kuwa itamsitiri kidogo kutokana na mnyumbuliko na mtimbwiliko wa hayo makalio yake manene.



    Alilijua umbo lake lilivyo tata mbele ya macho ya watu hususan wanaume wanaopenda makalio-tinginya, ambao lazima walikuwa wakiguna kila alipopishana nao huku utanukaji wa mapaja yake makubwa ukijidhihirisha bayana na kuwa kivutio kikubwa kwa wanaume waroho.



    Sasa akajiona yuko kamili. Akaifuata pochi yake ambako alitwaa noti moja ya shilingi 10,000, akaipachika kwenye pochi yake ndogo. Akatupa macho kitandani na kuiona simu yake. Nayo akaitwaa na kuishika mkononi akiwa ameiviringishia kitambaa.



    Sasa akaanza kuvuta hatua akitoka. Alipofika mlangoni aligeuka na kutaka kusema, umeyaanza, wenzio tutayamaliza.’ Hata hivyo alisita kutamka kwa kushtukia kuwa anaweza kuwa amemzindua Tonny.

    Akatoka na kuubamiza mlango kwa nguvu nyuma yake.



    Tonny aliishia kucheka tu huku sasa akitwaa manukato kabatini na kujipulizia. Hakujali wala kuwaza kuwa ni kwa nini mkewe kamwambia hivyo, alijali burudiko la mwili na faraja aliyoipata kwa Caroline usiku uliopita. Caroline, mwanamke ambaye hadi asubuhi hiyo Tonny aliwaza kama kweli huyo ni mwanadamu wa kawaida aliyezaliwa katika sayari hii au kateremshwa tu kutoka katika sayari nyingine.



    Aliwaza hivyo kutokana na pumzi na mbinu mbalimbali alizozimudu kitandani. Caroline aliyajua yote na alikuwa tayari kwa lolote….hakuwa na kinyaa. “Ni kama ananijulia,” alinong’ona akikumbuka jinsi mwanasmke huyo alivyomudu staili za ‘MBUZI KAGOMA’ na ‘JIPIMIE MWENYEWE.’



    Alizidi kumtukuza Caroline kwa kukumbuka kuwa alipenda sana kulishika ‘gunzi’ na kulinyonya kitaalamu huku akigunaguna kwa namna ambayo lazima mwanamume achanganyikiwe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Halafu eti huyu bwege anajitia kuniwakia…dah…aende mahakamani au akaandamane…mbwa koko…au vipi ajinyonge…” alibwata kwa mnong’ono wa kifahari wakati akiendelea kujipulizia manukato.



    Dakika tano baadaye alijiona kuwa yuko kamili, na kwamba anaweza kuingia mitaani. Akafungua pochi yake na kuyaangalia masalia ya pesa zake. Akashusha pumzi ndefu baada ya kubaini kuwa zilikuwemo shilingi 50,000 tu.



    Kwake, hizo hazikuwa pesa za kutambia kwa siku hiyo. Aliamini hivyo. Akachunguza vizuri ndani ya pochi hiyo ambayo pia kulikuwa na vijikaratasi vidogovidogo. Alikuwa akiisaka kadi yake ya benki.



    Akaiona.



    Sasa hakuwa na kingine cha kumkalisha humo ndani. Alitoka huku akitembea kwa madaha, akijisikia mwepesi huku pia akiiona dunia kaishika mkononi na wanadamu kawatia mfukoni.



    Nani kama yeye?



    ******





    LILIAN alitoka ndani ya nyumba hiyo bila ya kuwa na uelekeo maalum. Alishika barabara hiyo ya Rufiji hadi akaja kukutana na Mtaa wa Swahili ambako alitulia kidogo kisha akaanza kufuata uelekeo wa soko la Kariakoo.



    Alitembea kwa kasi na watu wachache aliokutana nao, waliomfahamu na wasiomfahamu, kama kawaida yao walimtazama wakivutiwa na mtikisiko wa matako yake makubwa ambayo licha ya kujitanda hiyo kanga bado ni kama yalimuumbua, yakijitupa huku na kule kwa namna ya kipekee.



    Hakujali kutazamwa, waliopiga miluzi, walioguna na waliomsifia wote aliwasikia na kuwaacha kama walivyo. Yeye akaendelea kutembea bila ya wasiwasi japo bado alihisi kitu kikimkera moyoni.



    Alizinduka wakati alipokuwa amelikaribia soko. Akausogelea mgahawa mmoja uliokuwa jirani na soko hilo. Akaingia na kuangaza macho huku na kule. Sehemu moja ya mgahawa huo ilikuwa chini na nyingine ilikuwa juu kwenye kijighorofa.



    Akaamua kupanda huko ghorofani. Alipofika alikuta watu takriban ishirini ambao baadhi walikuwa wakinywa supu, na baadhi walikuwa wakinywa bia.



    Lilian hakujua kama angepaswa kunywa nini au kula nini. Akabaki kaduwaa hadi alipoguswa bega na mhudumu mmoja wa kiume aliyemwambia, “Karibu shangazi. Karibu kiti.”



    Lilian alishtuka na kukumbuka kuwa alistahili kuketi na kuagiza chochote. Akakifuata kiti na kuketi. Mhudumu yule wa kiume akamsogelea na kumuuliza, “Tukusaidie nini, shangazi?”



    “Kwani kuna nini?”



    “Kuna supu, chapati na mtori.”



    “Supu ya nini?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ipo ya kuku, samaki na ng'ombe.”



    “Leta supu ya kuku na chapati mbili.”





    Mhudumu alipotoka Lilian alitwaa simu yake na kuanza kubofyabofya akilisaka jina fulani. Alipolipata alibonyeza sehemu ya kuita na kutega sikioni na aliposikia ikiita upande wa pili akakata. Alijua kuwa huyo aliyepigiwa atajua ni nani 'aliyem-beep.'



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog