Search This Blog

Monday, October 24, 2022

LADHA YA TUNDA BIVU - 2

 





    Chombezo : Ladha Ya Tunda Bivu

    Sehemu Ya Pili (2)





    MWANAMUME yule alitikisa kichwa akiashiria kukataa. “Hata kondomu haziaminiki sana. Unaweza kuvaa kondomu na ikakupasukia. Tutakuwa tumefanya nini?”



    Linda hakujisumbua zaidi kumhoji, lakini aliamini kuwa mwanamume huyo siyo mzima katika maungo yake. Na katika kutaka kuthibitisha kuwa huyu mwanamume ni mzima au mbovu, aliamua kufanya upekupeku kwa mashangingi wawili, watatu. Shangingi mmoja aliyeitwa Maimuna akamwambia, “Kha! Yule!…Nikikusimulia hutaamini! Namjua nje-ndani!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “N’ambie mwenzangu…” Linda alisihi, macho kayatoa pima.



    Maimuna akapasua!

    *****



    SIKU fulani, ndani ya daladala lililokuwa likitoka Ubungo kwenda Tabata kulikuwa na abiria wengi. Mvua pia ilikuwa ikinyesha kwa wingi. Kwa Jiji la Dar es Salaam kulikuwa na kijiubaridi cha wastani na hivyo kuwa ni burudani tosha kwa wale waliokuwa wakikerwa na joto kali la kila siku.



    Katika kiti fulani kulikuwa na abiria wawili, mwanamume na mwanamke. Wote hawa hawakupishana sana rika. Mwanamke alikuwa akiuingia mwaka wa thelathini ilhali mwanamume akiukimbilia mwaka wa thelathini na tano.



    Wakati daladala hilo lilipokuwa likipita katika kituo cha Hosteli, mara foleni ikazuka. Magari yakasimama. Ikabainika kuwa kuna ajali imetokea huko mbele.



    Mwanamume huyu alikuwa katuliza macho kwenye simu yake, akiangalia video ya watu wakifanya mapenzi. Japo alikuwa ameishika simu kwa namna ambayo ni kama vile hakutaka huyu jirani yake aone, hata hivyo haikuwa siri. Mwanamke huyu alitupa jicho kwa bahati mbaya au tuseme bila ya kudhamiria na kujikuta akishuhudia yale ambayo hakutarajia kuyaona.



    Mwanamke akashindwa kuyabandua macho yake kwenye simu hiyo, ilhali mwanamume naye akiwa ametopea katika kushuhudia picha ile bila ya kutambua kuwa kuna jicho jingine linaloshuhudia. Kadri picha ile ilivyokuwa ikiendelea, ndivyo mhemko ulivyokuwa ukiwajia abiria hawa kila mmoja kivyake-vyake.



    Mwanamume alishindwa kustahimili; akajikuta akiupeleka mkono katikati ya miguu yake na kujifariji kwa namna aliyojua.



    Huyu abiria mwenzake naye alinogewa katika namna iliyomletea mateso yanayohitaji faraja. Akashusha pumzi ndefu huku akiendelea kuishuhudia filamu ile isisimuayo. Hatimaye akagundua kitu kingine; kwamba huyu mwanamume alikuwa akijisuguasugua mbeleni kwa chati sana huku macho yakiwa yameganda bila ya kupepesa kwenye kioo cha simu.



    Mwanamama akapiga moyo konde na kuamua kuchokoza. Akamuuliza, “We mkaka ni nini hicho unachotazama?”



    Lilikuwa ni swali lililomtoka kwa mnong’ono wenye mvuto fulani masikioni mwa mwanamume huyu. Swali lililotoka huku mwanamke huyu akiwa ameutupa mkono pajani mwa mwanamume na kumfinya kidogo.



    Kama kuna kitu kilichomsisimua zaidi mwanamume huyu basi ni huu ufinyaji wa huyu mwanamke. Ilikuwa ni burudani ya aina yake kwa mwanamume kiasi cha kuuacha mkono huu wa mwanadada uendelee kufanya hiki ulichokuwa ukikifanya na zaidi, mwanamume huyu aliukamata mkono huo na kuukandamiza pale alipopakusudia, akitaka ashikwe zaidi na zaidi, na kutomaswa zaidi na zaidi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kama vile alikuwa akiisubiri fursa hiyo, mwanamke huyu alimsaidia mwanamume huyu kufanya kile kilichowaliwaza wote, mkono wake wenye kiganja laini ukitumika kitaalamu zaidi, ukifungua lisani ya suruali na kuzama ndani zaidi. Huko ukagota palepale palipokusudiwa, ukishika kwa usahihi kile kilichodhamiriwa kushikwa.



    Hata msafara wa daladala ulipoanza tena safari, bado watu hawa walikuwa wamezamisha akili zao katika kile walichonogewa nacho. Isingekuwa rahisi kwa abiria mwingine kati ya wale waliosimama kando yao kugundua kile kilichokuwa kikiendelea. Umakini ulizingatiwa.





    Hatimaye mwanamume akanong’ona kwa sauti nzito, “Unaitwa nani?”



    “Maimuna,” alijibiwa kwa mnong’ono kama wake. Kisha: “Na wewe?”



    “Kiboga.”



    “Unateremkia wapi?” Sasa ni Maimuna aliyetangulia kuuliza, akiwa amesitisha kufanya kile ambacho aliupa mkono kazi ya kukifanya.



    “Naelekea Bungoni.”



    “Mimi pia naelekea hukohuko.”



    “Unaonaje tukipita dansini Amana?” mwanamume aliuliza.



    “Poa tu.”



    Huo ukawa mwanzo wa kuzoeana. Wakashukia Amana ambako kundi moja la taarabu lilikuwa likitumbuiza. Wakaburudika kwa muziki na vinywaji. Saa tatu baadaye waliondoka. Wakaenda mtaa wa pili ambako walijichukulia chumba katika gesti moja. Ni huko gesti ndiko kulikotokea kile kilichomshangaza Maimuna.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Huyu hakuwa yule mwanamume aliyekuwa mkamilifu ndani ya daladala. Pamoja na jitihada zote ambazo Maimuna alizitumia, ukongwe wa kucheza na wanaume faraghani ukipewa kipaumbele na kuwa kama kungwi, bado Kiboga alibaki ni boya.



    Hatimaye Maimuna akamuuliza “Kwani vipi? Mbona sikuelewi-elewi?”



    Kiboga akashusha pumzi ndefu na kumwambia, “Nimechoka tu leo.”



    “Umechoka? Mbona kwenye daladala hukuwa hivi?”



    “Hata mimi nashangaa,” sauti ya Kiboga ilikuwa ya kutojiamini.



    Maimuna akaguna na kujitupa kando. Dakika mbili, tatu zikakatika wakiwa kimya. Kisha Kiboga akampa Maimuna shilingi 15,000 na kuchukua namba ya simu huku akimwambia, “Usikasirike baby. Kesho tafadhali tuonane. Nitakuwa na zawadi yako.”



    Maimuna akaukunja mdomo na kuuliza, “Zawadi gani?”



    “Utaiona tu, na n’naamini utaipenda.”



    “Kweli?”



    “Sikutanii. Leo sijisikii vizuri. Kesho utafurahi.”



    Kesho yake walikutana tena, yakatokea yaleyale! Baada ya siku saba wakakutana tena, yakawa hayohayo! Hapo ndipo Maimuna akajua kuwa hapo hakuna kitu. Pamoja na kwamba kila walipokutana Kiboga alimkatia kati ya shilingi 20,000 hadi 30,000 na kuchukua saa nzima akichezewa, bado Maimuna hakuitunza siri.



    Akampasulia yote hayo Linda!



    ***********



    BAADA ya kupata ukweli huo, Linda hakumjali tena. Kitu alichompendea mwanamume huyo ni pesa. Alikuwa 'kimwaga.' Na kama alikuwa tayari kumpa pesa nyingi kila walipokutana, kuna tatizo gani? Kwa nini asimgidie bwege huyo?



    Huyo ni wa kwanza.



    Wa pili, yeye pia alikuwa na maajabu yake. Huyu alimtokea siku moja kando ya kituo cha daladala, akamsalimia kwa heshima na baada ya hapo hawakuonana tena kwani kila mtu alipanda daladala tofauti. Lakini Linda hakubaini kuwa mtu huyo alikuwa akimfuatilia na kumbe hawakuwa wakiishi mbalimbali.



    Siku ya pili, wakati Linda akirejea nyumbani mtu huyo alimfuata na kumsalimia kistaarabu. Wakaungana katika njia ambayo ilimpeleka nyumbani Linda. Ni siku hiyo na jioni hiyo ndipo mtu huyo alipofunguka. Akasema yale aliyokuwa nayo moyoni.



    Linda alimsikiliza na kuyachambua kwa makini yote aliyozungumza mtu huyo huku moyoni akiwa hahitaji kuzisikia nyimbo za ‘nakupenda’. Suala la kupendwa, kwake ulikuwa ni wimbo uliokwishakinai masikioni na kuwa kero moyoni mwake. Alihitaji kuwezeshwa.



    Hata hivyo, walielewana na kukubaliana kukutana tena siku inayofuata, jioni.



    Miadi yao ikatimizwa. Wakakutana Travertine Hotel ambako walikula nyama-choma na kushushia vinywaji huku wakiburudishwa na muziki wa kundi moja la muziki wa taarabu.



    Siku hiyo ikaishia hivyo-hivyo. Saa 6 usiku kila mmoja akarudi kwake huku mwanamume akiwa ameonja busu la moja la ulimi na papaso dogo la kuvutia.



    Baada ya siku mbili ndipo walipokutana katika gesti moja maeneo ya Magomeni Mikumi. Ni huko chumbani ndiko kulikotoa taswira mpya. Mwanamume alionekana yu tayari kuwajibika, viungo vyake vyote vikiwa timilifu. Linda naye akavutiwa na ujenzi wa maungo ya mwanamume huyu mgeni, maungo yaliyoonekana kukakamaa kiume katika kila idara.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mikono laini ya Linda ikawa ikipita hapa na pale, ikitomasa na kuminya-minya kitaalamu zaidi huku ulimi nao ukifanya ziara ya kistaarabu hapa na pale kwa dakika kadhaa. Hatimaye wakaingia katika hatua nyingine muhimu iliyowapeleka hapo.



    Ni hapo ndipo Linda aliposhangaa. Mwanamume ‘alinywea’. Kile ambacho Linda alikitarajia kwa mwanamume huyu hakukipata.

    Mwanamke akaamua kutumia mbinu za ziada katika kumshtua mtu huyu.



    Bado haikusaidia!



    Wakalazimika kuahirisha huku mwanamume naye akionekana kushangazwa na hali hiyo.



    Siku ya tatu baada ya kubembelezwa sana ndipo Linda akakubali tena na safari hii alimkubalia baada yak kupewa kitita kizito cha pesa, shilingi 70,000.



    Chumba kilipowalaki, kitanda kikawakaribisha, kazi ikawa pevu kwa Linda. Akashika na kushika, akitomasa na kupapasa kwa namna alizojua, hatimaye akaamua kuutumia ulimi kwa jitihada zaidi! Mara mwanamume akajiwa na nguvu kama kimiujiza vile! Akaonekana kuwa yuko kamili, tayari kuwajibika! Linda akajipanga kumkaribisha rasmi. Ni hapo ndipo lilipotokea lile lililomshangaza tena Linda!



    Mashetani yalilala!



    *** *** *** *** ***





    “Huyu mwanamume karogwa?” Linda alijiuliza kimoyomoyo huku akimsikilizia mwanamume huyo aliyekuwa sasa kamlalia kifuani ilhali hakuna chochote alichoweza kukitekeleza kama mwanamume mkamilifu, mwanamume rijali.



    ‘Hili ni jogoo la kisasa,’ Linda aliwaza kwa dharau na akawa akimtazama mwanamume huyu aliyekuwa akihema kwa shida huku maungoni akiwa kama pambo tu.



    Dakika chache baadaye mwanamume huyo alijing’atua kifuani kwa Linda na kujitupa pembeni. Linda akashusha pumzi ndefu na kuendelea kushangaa. Akajiwa na kumbukumbu ya siku mtaalamu mmoja wa afya alipokuwa akitoa mada katika redio fulani kuhusu idadi ya wanaume wanaoshindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu inavyoongezeka siku hadi siku.



    Akayakumbuka maneno machache ya mtoa mada yule:



    *MSONGO WA MAWAZO: NI DHAHIRI KUWA AKILI NA TENDO LA NGONO VINATEGEMEANA SANA. INAJITOKEZA MARA NYINGI SANA KWA WATU WENYE MATATIZO KATIKA BIASHARA, KAZINI NA SEHEMU NYINGINE HUJIKUTA HAWAKO KATIKA HALI YA KUWA NA HAMU YA TENDO LA NDOA MPAKA PALE WATAKAPOTULIA. HII INAWEZA KUWAPATA WATU WA RIKA ZOTE NA TATIZO HILI LINAWEZA KUMALIZIKA HARAKA KUTEGEMEANA NA SHUGHULI ZAO ZINAVYORUDI KATIKA HALI YA KAWAIDA.



    *MAGONJWA YA MOYO NA MISHIPA YA DAMU: MZUNGUKO WA DAMU MWILINI UNA MAANA SANA KWANI KAMA DAMU HAIZUNGUKI VIZURI ITACHANGIA UUME KUTOSIMAMA VIZURI KWA SABABU USIMAMAJI HUTEGEMEA KIASI NA KASI YA DAMU INAYOINGIA KWENYE MISHIPA YA SEHEMU HIYO. DAWA ZINAZOTUMIKA KUTIBU SHINIKIZO LA DAMU HUCHANGIA PIA KUPUNGUA KWA NGUVU ZA KIUME.



    *UNYWAJI POMBE: POMBE INAWEZA KUATHIRI MISHIPA YA DAMU NA MISHIPA YA FAHAMU KWA WAKATI MMOJA. WAKATI MWINGINE MTU AKILEWA SANA HUATHIRI UBONGO NA KUKATA MAWASILIANO KISAIKOLOJIA NA HIVYO KUSHINDWA KUWA KATIKA HALI YA KUWA NA HAMU YA NGONO NA HIVYO KUTOSIMAMISHA UUME.



    *UNENE: UNENE HUWA UNAAMBATANA NA MAFUTA MENGI MWILINI. MAFUTA HAYO WAKATI MWINGINE HUZIDI KWENYE KUTA ZA NDANI ZA MISHIPA YA DAMU NA HIVYO KUPUNGUZA UKUBWA WA MRIJA KIASI KWAMBA DAMU INAPITA KIDOGO NA KWA SHIDA. HII HUCHANGIA KUPUNGUA KWA NGUVU ZA KIUME KWA SABABU KIASI CHA DAMU KINACHOTAKIWA KUUSIMAMISHA UUME KITAKUWA KIDOGO SANA. WAKATI MWINGI UUME UNAWEZA KUSIMAMA KIDOGO NA KULALA KABLA SHUGHULI HAIJAKAMILIKA.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    *KUTOKUFANYA MAZOEZI: KUTOKUFANYA MAZOEZI PIA HUSABABISHA MZUNGUKO WA DAMU KUTOKUWA MZURI NA HIVYO KUTORUHUSU DAMU YA KUTOSHA KUSIMAMISHA UUME. KWA WATU WANAOTEMBELEA MAGARI NA SHUGHULI ZA KUKAA OFISINI MUDA MREFU NA HASA KAMA HAWAFANYI MAZOEZI ASUBUHI AU JIONI WAKO KWENYE HATARI ZAIDI KULIKO WATU WANAOTEMBEA KWA MIGUU MWENDO MREFU NA KUFANYA KAZI NGUMU ZA KUUCHOSHA MWILI.



    *MATATIZO YA KISUKARI: KISUKARI NI UGONJWA UNAOATHIRI MISHIPA YA FAHAMU NA KUFANYA MISHIPA YA DAMU KUTOFANYA KAZI YAKE VIZURI ILI KURUHUSU DAMU KUJAA KWENYE UUME. HII HUMFANYA MGONJWA WA KISUKARI KUSHINDWA KUSIMAMISHA HATA KAMA ANA HAMU YA KUFANYA TENDO HILO.



    Linda alikikumbuka kipindi kile na mada hiyo na akajenga hisia kuwa huenda huyu mwanamume naye yuko kwenye kundi hilo. Kwa kiasi fulani akamhurumia, lakini hakuwa na mbinu ya kumsaidia. Hivyo alichofanya siku hii ni kumchezea hadi alipomfikisha kileleni kisha akajivalia nguo zake na kuondoka.



    Kwa jumla Linda alishafanya mengi, kama siyo yote na wanaume wa rika tofauti na mahitaji tofauti, pale alipodiriki kuwachojolea nguo. Na alishaizoea michezo yote ya ngono, iwe haramu au halali.



    Kwa uzoefu wake katika nyanja hiyo, hakupata shida katika muda huu alioketi na Frank hapo sofani kubaini kuwa tayari Frank alikuwa hoi. Alibaini hivyo pale alipoupeleka mkono chini ya kitovu cha Frank na kuushusha zaidi kabla ya kuupenyeza ndani ya suruali ambako uligota mahala fulani.



    Huko haukutulia, uliminya kidogo, ukatomasa kidogo na kupapasa kidogo, kitaalamu kiasi cha kumfanya mwanamume wa watu akaribie kuwehuka. Kwa jumla aligundua kuwa sasa Frank alihitaji jambo jingine, zaidi ya hatua waliyofikia.



    “Frank, vipi tena? Mbona ivi?” alimuuliza kimasikhara.



    Frank aliikosa sauti yake. Akashusha pumzi ndefu. Akamtazama Linda kwa namna ya kumwambia, 'unanitesa, Linda!'



    Linda akampigapiga mgongoni na kumwambia kimzahamzaha, “Nakutesa vipi baby wangu? Katangulie chumbani basi.”



    Ilikuwa ni kauli ambayo huenda ndiyo Frank alikuwa akiisubiri, zaidi ya kauli nyingine yoyote. Akanyanyuka na kufuata maelekezo. Linda akaelekea bafuni ambako alichukua dakika chache na kutoka. Akaingia chumbani moja kwa moja. Huko akamkuta Frank naye kajilaza kitandani, akiwa na bukta pekee. Akamtazama kwa muda huku pumzi zikimpanda na kushuka. Kisha akaichojoa kanga aliyovaa na kumfuata.



    ********



    CATHERINE aliendelea kufanya maandalizi ya mlo wa mchana huo kwa makini. Lakini mara akakumbuka jambo; chumvi haikuwapo. Ilikwisha tangu jana. Na hakukuwa na utatuzi mwingine, zaidi ya kumtaarifu mwajiri wake, Linda.



    Akatoka jikoni na kuelekea sebuleni ambako alitarajia kuwakuta Frank na Linda. Hakuwakuta. Hata hivyo hakushangaa, alijua wako chumbani. Akaelekea huko. Alipoufikia mlango, aligonga kidogo na kusubiri. Alipoona kimya akagonga mara ya pili, kwa nguvu ileile ndogo. Bado hakuitikiwa. Akaamua kuongeza nguvu katika ugongaji.



    Muda mfupi baadaye mlango ukafunguliwa.



    “Vipi?” Linda alisimama mlangoni akimtazama kwa macho makali huku kanga iliyousitiri mwili wake akiwa ameishika kifuani kama vile kuidhibiti isianguke. Nywele zake zilikuwa timtim na macho hayo makali yalikuwa mekundu.



    “Chumvi hakuna,” Catherine alijibu kwa sauti ya woga, akifinyafinya vidole vya mikono huku akiinamisha uso chini kuyaepuka macho ya bosi wake.



    Linda alirudi ndani na baada ya muda mfupi akatoka tena. Akampatia Catherine noti ya shilingi 500 na kurudi ndani huku akitoa msonyo mrefu.



    Catherine alikwenda dukani huku akijiuliza, hivi kwa nini Linda na Frank wanapenda kujichimbia chumbani kila Frank anapokuja? Kama wana maongezi ya siri kwa nini wasikae hapo sebuleni na kuzungumza? Na kama kweli wana maongezi ya siri si wanamwambia tu kwamba awapishe?

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Lakini pia kwa wakati huo fikra zilikuwa kwa Frank. Alikumbuka jinsi alivyomkumbatia na kumpapasa-papasa. Akaikumbuka starehe aliyoipata wakati mikono sugu ya Frank ilipokuwa ikitalii hapa na pale mwilini mwake.



    Hakusahau jinsi Frank alivyoziminyaminya chuchu za matiti yake machanga kwa namna iliyomtia msisimko uliofariji. Wala hakupoteza kumbukumbu ya jinsi mikono ile ilivyotambaa kutoka shingoni, ikapita taratibu katika uti wa mgongo kabla haijatua katika ile milima iliyojikusanya chini ya nyonga yake na kisha mikono hiyo ikaanza kupapasa na kuminyaminya kwa utaratibu mwingine uliokaribia kumtia wazimu.



    Alihitaji mchezo huo ufanyike tena. Lini,wapi na muda gani hilo hakulijua. Lakini aliuhitaji, tena haraka iwezekanavyo. Alitamani, kama ingewezekana, siku hiyohiyo, saa kadhaa baadaye akutane tena na Frank faragha, wayaendeleze waliyoanza kuyatenda dakika kadhaa zilizopita.



    Hata hivyo haikuwezekana. Frank na Linda walijichimbia chumbani humo hadi saa 1.30, giza likiwa limekwishaingia. Na baada ya mlo Frank aliondoka.



    Siku hiyo ilipita. Siku ya pili nayo ikafika na kupita. Ya tatu, hali kadhalika. Frank hakuonekana tena hapo, Frank ambaye tayari sura yake ilishaganda akilini mwa Catherine, na utaalamu wake wa michezo ya mahaba ukiwa umekwishajipenyeza hadi katika mishipa ya fahamu za Catherine kiasi cha kujikuta akitunza kumbukumbu kila wakati. Sasa kitu kingine kilimjia akilini dhidi ya Frank.



    Alimpenda!



    Alimtamani!



    Alimhitaji!



    Lakini atamwona wapi? Na atamwona lini ilhali hata hajui anaishi wapi?



    *****HAYA, SASA CATHERINE ANAMKUMBUKA FRANK NA ANAYAKUMBUKA YALE ALIYOKUWA AKIMTENDEA. ANA HAMU AFANYIWE TENA NA TENA. KAZI IPO.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog