Search This Blog

Monday, October 24, 2022

MZEE WA DODO - 2

 





    Chombezo : Mzee Wa Dodo

    Sehemu Ya Pili (2)





    ILIPOISHIA:



    Wazo lake lilikuwa kumfukuza kazi ili kuifanya nyumba yake kuwa katika hali ya utulivu. Wasiwasi wake ilikuwa hali ya dharau na kujiamini kwa msichana wa kazi kwa vile alikuwa ameisha ujua mnazi wake na kibaya siku ile hakutumia kinga risasi zilitua ndani. Lakini alijiuliza ataanzia wapi kumfukuza kazi bila maelezo ya kutosha, kutokana na sifa walizokuwa wakimpa msichana wao wa kazi ya heshima na kumlea vyema mtoto wao kama mwanaye wa kumzaa pamoja na umri wake ndogo mkewe asingemuelewa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pia ingekuwa vigumu kumwondoa haraka kwa vile hakukuwa na mbadala wake hasa wakizingatia wasichana wengi wa kazi hawako makini na malezi ya mtoto mdogo. Moyoni alipanga kesho yake amweleze kuwa hakufurahishwa na kitendo kila pia alichokifanya asimweleze mtu yeyote ibakie siri yao.

    Baada ya kuondoka Tumu, Teddy alibakia na maswali yasiyo na majibu juu ya shemeji yake kuondoka bila kumuuliza chochote kuhusiana na kitendo cha usiku wa kuamikia siku ile.

    Hakutaka kusubiri kufukuzwa kazi bali kuomba mwenyewe kuacha kazi.

    SASA ENDELEA...

    ****

    Jioni tajiri wake wa kike aliporudi, alimsubiri atulie kwanza ndipo amweleze dhamila yake ya kuacha kazi. Baada ya kuoga na kupata kinywaji, alimfuata na kusogea karibu yake kitu kilichomshtua Snura na kujiweka tayari kumsikiliza msichana wake wa kazi.

    “Dada," Teddy aliita huku akichezea kucha zake.

    “Abee mdogo wangu, mama yake Gift,” alimwitikia huku akizichezea nywele za Teddy zilizokuwa fupi za kipilipili.

    “Samahani dada.”

    “Bila samahani mdogo wangu,”alimjibu huku akimtazama usoni.

    “Naomba niache kazi.”

    “Nini?” Snura alishtuka.

    “Na...na..omba kuacha kazi.”

    “Kwa nini mdogo wangu?”

    “Nimewakumbuka nyumbani.”

    “Teddy jamani, hata miezi minne haijakatika toka wazazi wako waondoke?”

    “Basi tu dada, nimewakumbuka nyumbani.”

    “Hapana mdogo wangu, au mshahara mdogo?”

    “Hapana dada.”

    “Nimekuudhi?”

    “Hapana.”

    “Sasa nini?”

    “Hakuna kitu dada basi tu nimewakumbuka nyumbani.”

    “Teddy au shemeji yako kakuudhi?”

    “Hapana dada.”

    “Kakutongoza?”

    “Hapana.”

    “Sasa mdogo wangu unataka kuondoka, mwanao Gift atabakia na nani?”

    “Si mtafute mtu mwingine.”

    “Si rahisi kumpata kwa haraka pia hawezi kumzoea mwanangu kama alivyokuzowea. Siku zote anajua mama yake ni wewe. Naomba kama kuna kitu chochote nieleze hata kama unaona mshahara mdogo nitakuongeza mara mbili ili usiondoke,” Snura alimbembeleza Teddy.

    Muda huo Tumu alikuwa akirudi, alipoingia Teddy alinyamaza kimya. Baada ya kuwasalimia alielekea chumbani kubadili nguo. Snura alimwacha Teddy amekaa kwenye kochi na kumfuata mumewe chumbani.

    Alimkuta akivua nguo, alipofika alimsimamia kama jini la kutumwa.

    “Vipi mbona hivyo?” Tumu alimuuliza mkewe huku akiteremsha suruali na kubakia na nguo ya ndani.

    “Teddy umemfanya nini?” Alimuuliza amemshikia mkono kiunoni.

    Kauli ile ilimshtua na kujua aliyoyahofia ametokea. Lakini hakutaka kukubali kirahisi kwa aliamini hakukuwa na ushahidi wowote wa kumtia hatiani.

    “Teddy!” Tumu alijifanya kushtuka.

    “Eeh!”

    “Nimemfanya nini?”

    “Mbona anaomba kuacha kazi?”

    “Kwa hiyo kakwambia mimi ndiye niliyemfukuza kazi?”

    “Siyo kwanza kaniambia umemfukuza kazi, haiwezekani nirudi leo aombe kuacha kazi bila tatizo lolote.”

    “Kwa kweli sijui lolote muulize wenyewe sababu ya yeye kuacha kazi.”

    “Mmh! Sawa nitajua kama umemtaka kimapenzi na ikiwa hivyo nitajua nifanye nini, maana wanaume ninyi hamtosheki,” Snura alisema huku akielekea sebuleni alipomuacha Teddy aliyekuwa njia panda kwa vile hakuwa na sababu za kuacha kazi.

    Maneno ya Snura kidogo yamchekeshe Tumu kwani mkewe hakujua tatizo lililotokea usiku chanzo ni yeye aliyekuwa hamridhishi kimapenzi. Lakini bado alibakia na wasiwasi wa siri kutoka nje, lakini aliamini hakumbaka bali yeye ndiye aliyebakwa.

    Alitoka sebuleni na kuwakuta wanazungumza, aliingilia mazungumzo na kumuuliza.

    “Teddy mke wangu eti kwa nini unataka kuaacha kazi?”

    “Nimewakumbuka nyumbani,” Teddy alijibu akiwa ameangalia chini.

    “Au mimi nimekuudhi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapana.”

    “Sema tu yoyote aliyekuudhi akuombe radhi mbele yetu.”

    "Hakuna aliyeniudhi.”

    “Sasa shida yako kuacha kazi au kwenda kuwaona nyumbani kwenu?”

    “Kwenda nyumbani.”

    “Utakwenda basi, dada yako siku ya sikukuu atapata mapumziko ya wiki nzima, mtakwenda pamoja, sawa mama Gift?”

    “Sawa,” Teddy ilibidi akubali kwa vile hakuwa na sababu ya msingi ya kumfanya aache kazi. Walikubaliana kumuongeza nusu ya mshahara ili kuhakikisha anaendelea kuwepo pale nyumbani.

    ****

    Tumu ilibidi awe makini na Teddy kutokana na kitendo kilichotokea siku za nyuma. Aliamini kabisa msichana wa kazi naye alikuwa na hamu zake ambazo hakuwa na sehemu za kuzitolea.

    Hali aliyoikuta siku ile ilidhihirisha Teddy alikuwa na muda mrefu hajapanda mnazi kutokana na ugumu aliokutana nao. Aliamini lazima Teddy naye atapata maumivu kwa vile mpambano haukuwa na upashaji wa moto misuli.

    Aibu ya Teddy ilikuwa kubwa sana ilikuwa tofauti na zamani baada ya kumtengea chakula hukaa karibu ya Tumu kusubiri kuagizwa kitu, lakini baada ya tukio lile alikuwa akitenga chakula tu anakimbilia chumbani kwake pia hata ule utani wa zamani ulipotea.







    Hali ile iliifanya nyumba ipooze hata mkewe aliiona hali ile na kuwa na wasiwasi na uwepo wa Teddy pale labda kuna siri ambayo haijui inayomfanya msichana wa kazi apoteze uchangamfu wake wa zamani. Kila alipokaa naye kumuuliza kuna kitu gani kinachomkosesha raha Teddy alikataa na kusema yupo sawa.

    Snura alimbana mumewe huenda anajua sababu ya Teddy kuwa katika hali ile ya kukosa uchangamfu waliouzoea.

    “Mke wangu nikuambie mara ngapi sijui chochote kwa Teddy,” Tumu alimtetea.

    “Hapana mume wangu au umemkalipia?”

    “Walaa, wee si mwanamke mwenzako kwa nini usimbane akueleze ukweli.”

    “Nimembana sana lakini hajaniambia kitu.”

    “Amesemaje?”

    “Anasema yupo sawa lakini nikimwangalia nagundua ana kitu kinamsumbua.”

    “Kuna umuhimu wa kumpa ruksa hata ya wiki moja ili tu furaha yake irudi kama zamani.”

    “Hapana mume wangu tukimruhusu Teddy aondoke tutamkosa, tunatakiwa kumuonesha upendo ili ajisikie kama yupo nyumbani kwao.”

    “Basi siku unazopata muda wa kupumzika unamchukua na Gift unakwenda nao ufukweni ili kumrudisha katika hali ya kawaida.”

    “Nitafanya hivyo mume wangu Teddy ni muhimu sana kwangu, kama akiondoka nitaadhirika.”

    “Nami nakuahidi kurudisha furaha ya Teddy.”

    “Nitashukuru mume wangu jitahidi.”

    Wakati Tumu na mkewe Snura wakitafuta sababu ya msichana wa kazi kupoteza uchangamfu wa zamani, ambao Tumu alikuwa akijua sababu yake ambayo hata yeye ilimshtua na kuwa na wasiwasi huenda akibanwa sana anaweza kusema.

    Pamoja na wasiwasi ule aliamini yeye kama yeye hakuwa na kosa lolote kwa vile alibakwa hakumbaka. Wazo lilikuwa ni kukaa na Teddy na kumtoa wasiwasi na kumweleza jambo lile alione kama la kawaida.

    Alipanga siku ya pili wakibaki wawili amtoe wasiwasi kabisa ili kumfanya aone tukio lilitokea lilikuwa la kawaida wala halina ubaya wowote. Upande wa pili ilikuwa tofauti na mawazo ya Snura na Tumu ambao walikuwa na mawazo tofauti.

    Teddy alikuwa kwenye wakati mgumu toka siku alipoonja kuupanda mnazi wa shemeji yake ulimchanganya na kuamini hata upanda tena. Wasiwasi wa kufukuzwa kazi uliondoka baada kuonesha wote wanamuhitaji. Kilichoendelea kumtesa ndoto za kila siku kuota anaukwea mnazi wa bosi wake tena akisaidiwa kuukwea mpaka kufika kileleni.

    Kila aliposhtuka alijikuta amejivunjia yai la bata mzinga lililomchafua na kuhisi kichefuchefu, asubuhi alipoamka na kumkuta shemeji yake akienda mezani kufungua kinywa akiwa amevaa bukta na singland anajikuta kwenye hali mbaya ambayo aliamini mwenye uwezo wa kutuliza mzuka wake ni tajiri yake ambaye alimuona kukamilika kwa kila kitu.

    Usiku pia alikuwa kwenye wakati mgumu baada ya kumuandalia chakula na kusuburi ale kisha aondoe vyombo. Kwake ilikuwa ikimpa mateso kila alipokuwa akitazama akila kwa pozi na kutamani siku moja angekuwa mke wa mtu na kuwa pembeni ya mumewe wakila pamoja kisha wanaenda kulala pamoja na kupewa haki yake ambayo aliishia kuipata ndotoni.

    Mateso yale yalimfanya aione nyumba chungu na kupanga kuondoka la sivyo ashee na bosi wake kujiti cha rilei cha mbio za utamu wa hamu usioisha hamu. Lakini hakuwa na jeuri ya kumweleza shemeji yake ambaye alikuwa na mke mzuri kuliko yeye tena mfanyakazi wa mshahara mkubwa kuliko yeye muosha mtoto kupika na kuosha vyombo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hali ile ilikuwa ikimzidi kumtesa binti mdogo na kuiona nyumba ile kama sehemu ya mateso. Wazo alililokuwa nalo ni kuacha kazi ili akaolewe kijijini kwao na bwana yake wa zamani aliyemuingiza dunia ya wakubwa.

    Usiku kwake ulikuwa wa mateso kila siku lazima amuote tajiri yake tena akimtandika kisawasawa na yeye kukata mawimbi vilivyo. Lakini alinaposhtuka usiku hujikuta peke yake na kuanza kujisindikiza kama mpapasa kinanda na mwisho wake hubaki na hamu zake na kuona njia nyepesi ilikuwa kuacha kazi na kwenda kuutafuta utamu nje.

    ****

    Siku ya pili kama kawaida Teddy baada ya kuandaa kila kitu mezani alirudi chumbani kwake kusubiri Tumu aondoke. Akiwa amejilaza kitandani kwake macho ametazama juu alishtushwa na mlango kugongwa. Alishtuka na kunyanyuka kitandani bila kuuliza alijua ni shemeji yake.

    Alijitengeneza vizuri na kutoka hadi mlangoni kabla ya kufungua aliitika.

    “Abee shemeji.”

    “Vipi mbona umejificha ndani?”

    “Hapana shem nilikuwa nacheza na Gift.”

    “Njoo basi tuzungumze.”

    “Nakuja shemu,” Teddy alijua anakwenda kupewa maelekezo ya siku ile kabla ya shemeji yake kwenda kazini.

    Alipotoka alishangaa kumkuta shemeji yake amevaa kaptula fupi na singland na kuufanya mwili wake wote uwe nje. Tumu hakujua sehemu za mwili wake ndiyo mateso kwa msichana wake wa kazi.

    Alipotoka alisimama kama jini wa kutumwa asijue afanye nini aibu ilimtawala kama ndo kavunja ungo usiku wa kuamkia siku ile.

    “Teddy.”

    “A..a..bee,” aliitikia vidole mdomoni shingo kangalia pembeni.

    “Teddy una nini?”

    Alimuuliza huku akimshika sehemu za shingoni kitu kilichofanya Teddy asisimke na kuhisi vitu vikitembea mwili mzima mara ghafla yai lilipasuka na kumfanya amng’ang’anie shemeji yake asianguke. Alimshika kwa nguvu mpaka alipomaliza maji yote kwenye dafu kisha alishusha pumzi ndefu na kumwachia tajiri yake.

    Kisha alitimua mbio kukimbilia bafuni kujisafisha kwani aliamini asingeweza kuzungumza na tajiri yake kwenye hali ile. Kila kilichotokea kilimwacha njia panda Tumu na kujiuliza kinachotokea ni kweli au usanii wa msichana wake wa kazi.

    Alishindwa afanye nini alikwenda kukaa kwenye kochi kumsubiri Teddy aliyekuwa amekimbilia bafuni. Teddy baada ya kuingia bafuni alijisafisha na kuoga kabisa na kufanya usafi wa kufuli huku akijiuliza hali ile itaendelea mpaka lini.

    Aliona heri aseme ajue moja kama atapata au atakosa, alijiapiza kama atakosa basi ataacha kazi kwa kuondoka bila kuaga.





    Baada ya kumaliza kufanya usafi alijifunga upande wa khanga na kwenda chumbani kwake na kupita mbele ya Tumu bila kumsemesha.

    Tumu alimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea machoni mwake, mwili wa Teddy ulikuwa mchanga uliokuwa una kivutio kwa mwanaume rijali mpenda ngono. Kifua chake kidogo kilichojaza dodo zilizojaa na kukifanya kifua chake kipendeze kutazamwa kila wakati muda wote.

    Mwili wake mdogo ulikuwa kama kompyuta mpakato (Ipad) unayoweza kutembea nayo popote. Kiuno kilikuwa kidogo kilichobeba makalio ya wastani lakini yenye kumpendezesha kama akivaa suruali. Siku zote Tumu alimfananisha na mdogo wake hivyo hakuwa na wazo la kumtamani hata siku moja.

    Lakini hali iliyokuwa ikiendelea na tukio lilitokea siku ya nyuma aliamini alitakiwa kufanya maombi mazito, kwani shetani alionekana kuwa na nguvu na kuanza kuusambaratisha moyo wake.

    Chumbani Teddy akiwa anabadili nguo alikumbuka mchezo aliomfanya shoga yake kwa tajiri yake mpaka akafanikiwa kufanya naye mpenzi na mwishowe akawa nyumba ndogo. Alipanga kama siku ile shemeji yake hatamuelewa basi naye atajitoa akili kuhakikisha anamnasa kimapenzi.

    Baada ya kubadili nguo alivaa gauni fupi lenye kuuweka mwili wake sehemu kubwa nje ndani hakuvaa kitu chochote kama angetanua miguu angemwaga radhi. Wakati wa kutoka sebuleni macho ya Tumu yalitua kwenye kifua kilichoonesha sehemu kubwa ya dodo, ilikuwa tofauti na alivyoondoka alirudi akiwa amejiamini sana na kwenda kukaa pembeni ya tajiri yake na kukunja mguu na kuyafanya mapaja yote yawe nje.

    Alimuona Tumu akiyaangalia kwa chati, Teddy aliona mtego wake kama unataka kunasa, mtoto wa kike alizidi kuitanua miguu yake bila wasi huku akijifanya hajui anafanya nini. Macho ya Tumu yalishtuka kuona kama duka la Teddy lipo wazi, alikaza macho vizuri ili apate uhakika Teddy alijigeuza kwa ghafla na kumsemesha tajiri yake aliyeshtuka mpaka akadondoka kwenye kochi.

    “Ndiyo mume wangu.”

    “E..e..ee,” Tumu alibabaika.

    “Jamani mume wangu kulikoni,” Teddy alimfuata alipokuwa ameteleza ili amnyanyue.

    “Niache nitaamka mwenyewe.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Pole mume wangu,” Teddy siku ile alichangamka kuliko kawaida tofauti na mwezi mzima uliopita alikuwa mwoga na mwenye aibu.

    “Asante,” Tumu aliitikia huku akikaa kwenye kochi.

    “Vipi tena?” Teddy aliamua kujitoa akili ili siku ile ijulikane mbivu na mbichi. Alimsogelea na kumshika shingoni na kumwinamia.

    “Nipo kawaida tu.”

    “Pole, hukuumia?”

    “Nipo sawa sijaumia.”

    Teddy alirudi alipokuwa amekaa awali na kutulia kumsikiliza shemeji yake kwa kuamini ujumbe utakuwa amefika. Tumu alijikuta akijiuliza ni kweli Teddy hakuvaa kufuli na kama hakuvaa kwa nini amefikia hatua ile. Kwa hali ile aliamini nyumba yake ipo katika majaribu makubwa. Isingekuwa mkewe angemfukuza kazi ili kulinda nyumba yake lakini asingeeleweka kwa mkewe na kuonekana pengine yeye ndiye mwenye tatizo.

    Tumu alijikaza kiume ili aweze kumuuliza Teddy alichomuitia, binti aliyeonekana amekuja kwa nia moja ya kuhakikisha anakipata alichokikusudia.

    Alijitahidi kuchezesha mbali macho yake na mtego wa Teddy, lakini macho yalikataa yaling’ang’ania kutazama paja changa za msichana wa kazi zilizoonesha hazitumii dawa za kuchumbua zilizidi kumweka kwenye hali mbaya.

    Kwenye kambi hali ilikuwa mbaya sana mkuu wa majeshi alitaka kutoka nje ya kambi. Alijikuta akiona aibu kwa kuuweka mkono juu ya kambi ya jeshi ili kuficha hasira za mkuu wa kikosi. Teddy naye alizidi kufanya makusudi kwa kuitanua miguu yake kama amejisahau hajavaa kitu ndani.

    Tumu alijikuta katika wakati mgumu, kwani kila alipokwepesha jicho lake alishindwa na kubakia kutazama mateso bila chuki. Teddy alirudisha jicho lake na kukutanisha na bosi wake ambaye mahanjamu yalimfanya awe kama mtu aliyekula kuberi iliyokuwa ikipanda taratibu na kukimbilia machoni.

    Alimuangalia Teddy kwa jicho la ‘nihurumie unanitesa mwana wa mwenzio’. Teddy aliamini mtego ulikuwa umenasa sawasawa kama samaki alikuwa amemeza doano mpaka tumboni, kuitoa lazima itoke na utumbo.

    Bila hofu alinyanyuka na kusimama huku akimtazama bosi wake aliyekuwa dhoofu lihari na kukitoa kiblauzi kilichomwacha mti wa mwembe uoneshe dodo zilizotulia. Ile ndiyo ulikuwa ugonjwa uliokuwa ukimtesa sana Tumu alipoziona dodo zilizosimama sawa bint sawia kama askari vijana waliotoka depo juzi wakiwa kwenye ukaguzi.

    Teddy akiwa ameuma mdomo wa chini upande mmoja kama anataka kuutafuna, macho yaliyolegea kama kibatari kilichoishiwa mafuta na kuwaka kwa kujilazimisha. Alimtazama Tumu aliyokuwa ametokwa na macho kama kaona sisimizi kambeba tembo.

    Teddy baada ya kuamini Tumu ni kuku wake hakutakiwa kumshikia manati. Aliitupa chini blauzi na kuzishika dodo zake kama mfungaji anayetaka kukamua maziwa na kuziminya kidogo kama anaziogopa na kuzidi kumtesa tajiri yake.

    Aliamua kumpiga tajiri yake pigo la mwisho kwa kumalizia sketi na kuinama kuiweka chini, ilikuwa tofauti na alivyovua blauzi aliitupa chini. Lakini sketi aliiweka chini tena akiwa amemgeuzia mgongo tajiri yake na kumwachia ateseke na kiti cha nyuma kilichokuwa kimechongoka kama cha baiskeli ya Wakulya wa Kitunda ya kubebea mayai.

    Tumu alimshika mkuu wa majeshi kwa nguvu ili atulie, mapigo ya moyo yalimwenda mbio na kujiuliza kama mkewe anatokea pale nini kingetokea. Alitaka kunyanyuka kwenda chumbani lakini mwili haukuwa na nguvu kwa vile tayari sumu ya hamu ilikuwa imemsambaa mwilini.









    Teddy baada ya kuusambaratisha moyo wa Tumu taratibu kama jini wa kutumwa alimfuata bosi wake kwenye kochi kama mteja aliyekuwa akisubiri kufanyiwa masaji. Alipofika alimkalia kwenye majapa na kumpa juisi laini ambayo aliipokea na kujikuta wote wakiimba wimbo mmoja.

    Taratibu chombo kiliingia katikati ya maji ya kuanza safari ambayo ilionekana kumfurahisha dereva na abiria. Baada ya mwendo abiria hakufurahia barabara na kuomba wahamie barabara nyingine.

    “She..she..me..me..meeeji,” Teddy alimwita Tumu kwa sauti ya mtu aliyekuwa akitafuna pilipili.

    “U..u..unase..semaje?” Tumu alipata kigugumizi cha ghafla baada ya mchicha kukolea nazi.

    ”Ha..ha..pa, ha..ha..pa..fa..fai.”

    “Kwa..kwa..hiyo?”

    “Tu..tu..ha..ha....hame ha..ha..pa.”

    “Su..su..bi..bi..bi i..ii..ii.”

    Mwanaume alijikuta akichanganya miguu kama Ronardo na kuanza kuingia nao kama Mesi kwa kuwatambuka mabeki mmoja baada ya mwingine.

    Teddy naye hakukubali alikula naye sahani moja, alimfukuza mpaka ndani wa wavu na kutulia wote wakiwa wameangukia banda la kuku na kuvunja mayai ya mbuni kwa mpigo.

    Kwa vile mechi ilikuwa ya kumshtukiza Tumu hakukumbuka kofia nyepesi kwa ajili ya taadhari ya safari. Baada ya kutulia kwa muda kama wapiganaji wa mieleka waliochoka kupigana, Teddy aliita.

    “Shemu.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Naam.”

    “Twende ndani hapa sifaidi.”

    Tumu ambaye alikosa gemu la live kwa muda mrefu, hasa la mchana alihamia kwenye chumba cha mfanyakazi na kuendelea mpambano ambao baada ya muda Teddy alichoka sana na kuomba mchezo uharishwe.

    “She..shem to..to..sha, nimechoka.”

    “Poa.”

    Tumu alikipaki chombo pembeni na kuteremka na kumwacha Teddy amelala alikuwa amechoka kama alikuwa akifua vyuma. Tumu alimwacha apumzike na siku ile kushinda nyumbani akimlea Gift kumpa na mapumziko Teddy baada ya mtanange uliomfurahisha Tumu mwanzo mpaka mwisho wa mpambano na kutamani kila siku ingekuwa kama vile.

    Wasiwasi wa kuivunja ndoa yake iliondoka moyoni na kuamini kwa mtindo ule wa kutoka na Teddy ndiyo utakuwa muarobaini wa tatizo lake la kulishwa kiporo na mkewe.

    Tumu alijikuta akijimilikisha msichana wake wa kazi, kila siku usiku alikuwa akijishindia shamba kwa raha zake. Kila asubuhi Teddy alikuwa na heshima zote kama msichana wa kazi.

    Lakini baada ya Snura kwenda kazini na kumwacha mumewe ambaye alibadili ratiba ya kuwahi kuondoka na kuchelewa kila siku. Walipobaki wawili waligeuka mtu na mkewe, walioga pamoja na kunywa chai pamoja kisha Tumu alipata cha asubuhi na kuoga tena kisha aliwahi kazini.

    Siku zote Teddy alionesha utiifu mbele ya Snura huku akionesha kuifurahia kazi yake. Bila kujua mama mwenye nyumba alishukuru kwa msichana wake wa kazi kubadili uamuzi wa kuendelea kufanya kazi bila kujua kageuzwa babu jinga inama ufikiri mali zako zinaliwa kwa uvivu wako.

    Teddy alibadili hata utaratibu wa kila usiku alimsubiri Tumu arudi wale pamoja kwa kulishana kama ndege. Wakati huo Snura amelala kama maiti akiamini mumewe shida yake kubwa kumwaga mzigo tu na kusahau raha ya wimbo kupokezana.

    Mtoto wa kike ndani anaanza kunawili na kuvutia. Umbile nalo lilinona kutokana na mbolea ya majimaji ya tajiri yake ambayo ilikuwa hajachangwanywa na madawa ya sumu.

    Pamoja na kupewa penzi la ushirikiano kwa binti mchanga Teddy tena mwenye chungu kilichokuwa kipya kilichoonesha kimetumika kidogo hakikuwa tofauti na kipya.

    Teddy alikuwa mgeni wa mapenzi siku zote alipenda mtindo wa kuhudhulia mazishi ya mende yasiyo na mazishi. Pamoja kuwa mgeni wa mahanjumati lakini binti alikuwa na nyonga laini kama ute wa yai.

    Tatizo lingine alikuwa anakwenda nje biti kwa kunyumbulika kwa papara kwa kuamini mwanamke nyonga na kusahau raha ya ngoma ifuate mdundo.

    Tumu ilibidi aingie kazi ya kumfundisha binti kunata na binti kwa kuzungusha nyonga taratibu kulingana na mzungusho wa mwiko kwenye chungu ili kukifanya chakula kiive vizuri.

    Mwanzo ulikuwa mgumu kwa kujisahau pale ngoma inapokuwa inogile na kujikuta akipandwa na wazimu wa mapenzi. Kila alipoanza kupandisha mashetani alimkumbusha.

    “Teddy taratibu.”

    “Shemu si..si..wezi.”

    “Utaweza taratibu.”

    “Najitahidi lakini najikuta nimepandisha mashetani, najisahau na kutoka nje ya biti.”

    “Lakini lazima nikusifu mambo unayaweza.”

    “Namzidi dada?”

    “Ukimzidi itakuwaje?”

    “Si unioe niwe mke wa pili.”

    “Taratibu basi.”

    “Shemeji hata sijui kwa nini?”

    “Hujui nini tena?”

    “Nini hatima ya penzi letu yaani najikuta naumia ukienda kulala kwa mkeo.”

    “Mmh! Lakini kama usiku sikuja asubuhi si nakupa raha kamili.”

    “Siku nyingine unanizidishia dozi asubuhi na kunifanya nilale muda wote. Kazi inakuwa ngumu, kama vipi uwe unaanza kunipa dozi ya kunilaza kisha unakwenda kwa dada.”

    “Teddy kila kitu kitapangwa usiwe na shaka.”

    “Lakini kumbuka sasa hivi nimekuwa kama mkeo kila kitu nakufanyia zaidi ya mkeo. Nakupikia nakufulia nakulelea mtoto na mwisho nakupa penzi kamili ambalo naamini kwa mkeo hulipati.”

    “Umejuaje?”

    “Siku ile baada ya kukusafirisha wakati wa kukutua uwanjani aliniambia nakupa penzi tamu kuliko mkeo.”









    “Mimi?” Tumu alishtuka.

    “Jamani nani mpenzi wangu humu ndani?”

    “Mimi.”

    “Mmh! Siamini kama nilisema mimi,” Tumu alijikuta akiona aibu kwa vile hakutaka kuitoa siri ya mke wake kwa msichana wa kazi ambaye angezidi kumdharau.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Umenifundisha mwenyewe, sasa hivi full dozi kwenda mbele na nitahakikisha unamwacha mkeo na mimi kuimiliki nyumba hii.”

    “Ukifikia huko utakosa kila kitu, we jilie vyako vingine havikuhusu,” Tumu alizungumza kwa sauti iliyoonesha hakufurahishwa na maneno Teddy.

    “Nimekuelewa shemeji.”

    Teddy baada ya kujua kamuuzi tajiri yake alijituma mtoto wa kike kiasi cha kimrusha akili na kusahau yote yaliyopita huku akimuahidi wakipata msichana mwingine wa kazi ampangie chumba.

    ***

    Wakati penzi la tajiri na mfanyakazi wake yamepamba moto, mama mwenye nyumba alijikuta akijishtukia na hali aliyokuwa akijikuta nayo asubuhi akiamka. Kila aliposhtuka na kushika kwenye sahani alikuta hapajatumika.

    Alijikuta akishtuka na kuona kama mumewe kachoka na penzi self service la kujipakulia mwenyewe. Alijikuta akikosa raha kila alipoamka na kufikiri labda asubuhi ya siku ya pili akiamka atakuta sahani umetumika. Lakini kila alipoamka aliikuta kavu kuonesha haikuguswa kabisa usiku.

    Kitendo kile kilimyima raha hata kazini alikuwa mtu wa mawazo mengi, kuna kipindi alihama kabisa kimawazo kitu kilichomshtua shoga yake Edna.

    “Shoga vipi unajua wiki hii yote sikusomi, lakini leo naona imezidi.”

    “Mmh! Wee acha tu.”

    “Hapana shoga, lako langu langu lako usinifiche naweza kukupa msaada,” Edna alimbembeleza Snura.

    “Unajua siku hizi mume wangu simuelewi kabisa.”

    “Kivipi?”

    “Zamani japokuwa sikumpa ushirikiano lakini ilikuwa haipiti siku mbili ukiamka usubuhi unakuta sahani imetumika mi kazi yangu kuiosha ili jioni iwe safi kwa ajili ya mlo mwingine.”

    “Kwa hiyo ukiiosha asubuhi ndiyo basi?”

    “Hapana shoga, kabla ya kulala unakikisha sahani safi kwa kujua lazima mume wangu atajipakulia na kujilia tani yake.”

    “Mmh! Lete habari.”

    “Basi sasa hivi mwezi unakatika kila asubuhi nikiamka nakuta kavu haijatumika.”

    “Labda akimaliza kutumia anasafisha.”

    “Shoga wee hata shombo linalobaki kwenye sahani halibaki! Shoga najifahamu mwenyewe nikitumika najijua?”

    “Mmh! Basi labda anaumwa.”

    “Walaa haumwi, huenda kachoka kujilia mzoga.”

    “Mzoga?” Edna alishtuka kusikia neno lile.

    “Eeh mzoga, kisichochinjwa si mzoga tu.”

    “Una maana gani kusema hivyo?”

    “Penzi lisilo na maandalizi si sawa na kula mnyama asiyochinjwa?”

    “Mmh! Makubwa, kwani umemuuliza shemeji kwa nini siku hizi hajipakulii.”

    “Mmh! Shoga aibu, kwetu matusi kuuliza kitu kama hivyo kama humpi mumeo haki yake kwa asilimia mia.”

    “Kwa hiyo?”

    “Wasiwasi wangu huenda kapata nyumba ndogo inampa penzi la ushirikiano tofauti na langu.”

    “Mmh! Shoga wasiwasi wako tu.”

    “Siyo wasiwasi wangu, tena kilichonichanganya zaidi leo asubuhi wakati nakuja kazini kwenye redio ya kwenye gari langu, nilisikia sababu ya wanaume kuwa na nyumba ndogo tena yangu ndiyo walisema mbaya sana inaweza kusababisha talaka.”

    “Kwa hiyo unataka kuniambia ndiyo sababu?”

    “Nina imani kabisa ndiyo sababu.”

    “Lakini naamini kama utajipanga kazi utafanya na mzee atapate haki yake sawasawa.”

    “Lazima nifanye hivyo, kazi naipenda lakini mume wangu nampenda zaidi. Kama mwezi mzima hajanigusa ndoa yangu inakwenda sehemu mbaya.”

    “Basi shoga jipange kazi na mumeo ili tusipoteze chochote katika vitu vyote.”

    “Yaani wiki nzima sina raha, lakini mada ya leo niliyoisikia kwenye redio imenichanganya sana na kuninyima raha. Kidogo nigeuze gari nirudi nyumbani nikampe haki yake mume wangu.”

    “Shoga usiumie sana, leo fanya kazi kwa kiasi ili mwili uwe na nguvu ili kumfanya mzee kama ana kidumu basi kuanzia leo usiku arudishe penzi nyumbani.”

    “Yaani nitakachokifanya leo mume wangu mwenyewe lazima atachanganyikiwa.”

    “Na uhakikishe kutenga sahani leo mwisho.”

    “Shoga mwezi huu hata nikifukuzwa kazi potelea mbali lakini nihakikishe nyumba nairudisha mkononi mwangu.”

    Walipeana moyo na kuendelea na kazi.

    ***

    Snura alikuwa kazini kimwili lakini mawazo yake yalikuwa nyumba akiwaza jinsi kuhakikisha siku ile anamfanyia mumewe kitu kipya ambacho kitamshtua na mshtuko ule uwe wa siku zote.

    Alikumbuka kitu kingine kuhusu chakula cha jioni ambacho aliamini alitakiwa kukipika mwenyewe. Alimpigia simu msichana wa kazi na kumkataza asipike chakula cha jioni.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Teddy za saizi?”

    “Nzuri tu dada.”

    “Vipi Gift hajambo?”

    “Hajambo anacheza tu baada ya kushiba.”

    “Asante mdogo wangu kwa kumtunza vizuri mwanangu, sasa Teddy.”

    “Ndiyo dada.”

    “Chakula cha jioni pika cha kwako.”

    “Leo mnakwenda kwenye pati?”

    “Hapana , nitakuja kupika mwenyewe.”

    “Na hiki nilichonunua?”

    “Kiweke utapika kesho, lakini chakula cha mume wangu nitapika mimi.”

    “Jamani dada kwa nini ujitese? Acha nitakusaidia.”

    “Hapana Teddy, leo nitawahi kurudi usiwe na wasi.”

    “Hakuna tatizo dada yangu.”

    Baada ya kumkataza msichana wa kazi asipike chakula cha jioni, alimpigia simu mumewe ili kumuulizia jioni ya siku ile angependa kula nini.

    “Haloo my love leo jioni unataka kula nini?”

    “Maagizo nimemuachia Teddy.”

    “Teddy ni nani katika nyumba yangu?” Snura alikuja juu.

    Kauli ile ilimshtua sana Tumu na kujawa na mawazo huenda mkewe kashtukia mchezo.

    “Mke wangu hilo ni swali gani?” naye alijifanya kukasirika.

    “Nakuuliza Teddy ni nani ndani ya nyumba yangu?”

    “Maswali ya kipumbavu kama hayo yameanza lini?”

    “Mimi na Teddy nani anayetakiwa kupanga chakula cha ndani?”

    “Lakini mke wangu haya unayoyasema leo yameanza lini. Kila siku unasema kila kitu umezungumza na Teddy, kosa langu nini kukueleza chakula cha jioni Teddy anajua?”

    “Hata kama anajua, sina haki ya kukuuliza?”

    “Unayo, lakini nilijua chakula cha jioni kila siku kipo mikononi kwa Teddy.”

    “Kwa hiyo kama kila kipo kwa Teddy sina haki ya kuuliza unachokula mume wangu?”

    “Unayo.”

    “Sasa kwa nini nakuuliza unampa kipaumbele msichana wa kazi au ndiyo amekuwa mkeo?”

    “Hapana mke wangu, sikuwa na maana hiyo, najua unachelewa kurudi na ukirudi umechoka sasa suala la nyumba uliliacha mikononi kwa Teddy.”

    “Hata kama, leo nimeamua kukupikia chakula cha jioni mume wangu.”

    “Mmh! Nitafurahi sana mke wangu hata mimi nina hamu nacho.”

    “Haya mume wangu niambie leo unataka kula nini?”

    “Kama kawaida tambi nyama.”

    “Mume wangu majibu si hayo, unataka turumbane bure.”

    “Basi nisamehe mpenzi wangu.”

    “Nisamehe miye kwa kukufokea mume wangu, naomba unisamehe sana nipo chini ya miguu yako.”

    “Mke wangu wala usiwe mnyonge, una haki ya kuwa makali, siku zote nyuki mkali kwa asali yake.”

    “Jamaniii, asante mume wangu.”

    “Basi mke wangu nikutakie kazi njema.”

    “Na wewe pia ubavu wangu mmmwaaa,” Snura alimchumu mumewe.

    “Asante na wewe mmmmwaaaa,” Tumu naye alijibu.

    Snura baada ya kukata simu alimgeukia shoga yake Edna.

    “Vipi naona unampiga mkwala mzee?”

    “Shoga kweli nyumba yangu ipo katika hali mbaya.”

    “Kivipi?”

    “Anasikilizwa msichana wa kazi kuliko mama mwenye nyumba.”

    “Shoga sasa huo wivu wa kijinga, leo ndiyo umejua. Lini aliingia jikoni jioni zaidi ya kurudi unakula na kulala.”

    “Lakini nilipomuuliza anakula nini angenijibu.”

    “Kwa vile si mpikaji alikuwa na haki ya kukujibu hivyo. Kweli tunafanya makosa kuwaachia wasichana wa kazi wafanye kila kitu.”

    “Sasa kwa kazi zetu unafikiri tutafanyaje?”

    “Kama hatuna la kufanya tusilalamike." "Shoga hali iliyonitokea na majibu ya mume wangu, inaonesha kabisa nyumba imenisahau na mwanangu muda si mrefu ataniita shangazi badala ya mama.”

    “Umeona eeh! Tubadilike.”

    Baada ya kazi hakutaka kufanya za ziada ambazo zingemuingizia fedha za muda wa ziada katika mshahara wake. Alipita sokoni na kununua mahitaji ya jioni kisha alirudi nyumbani.

    Alipofika alijifunga upande wa kanga na ndani alikuwa na kufuri tu, kisha aliingia jikoni kuandaa chakula cha mumewe. Aliandaa chakula kitamu ambacho aliamini mumewe atakipenda.

    Baada ya kumaliza kupika alikiandaa vizuri juu ya meza na kwenda kujimwagia maji kisha alijipulizia utuli uliomfanya anukie sana na kujifunga upande wa kanga nyepesi bila kitu ndani na kukaa mkao wa kumpokea mumewe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tumu naye siku aliwahi kurudi ili asimuudhi mkewe, alipofika mkewe alimpokea kwa kumkumbatia na kumbusu kisha alimshika mkono hadi chumbani.

    Alipofika alimvua nguo zote kisha alimfunga upande wa kanga na kumpeleka bafuni kuoga. Wakiwa bafuni alikumbuka mwanzo wa mapenzi yao, kwani kabla ya kuoana walikuwa marafiki baada ya penzi kukolea ndipo walipotangaza ndoa.

    Snura alianza kumliza mumewe chozi lisilo na msiba bafuni, Kitendo kile kilimshtua sana Tumu na kujiuliza mke wangu alikuwa na ajenda gani siku ile. Toka mchana alikuwa mkali pia hata kutaka baadhi ya mambo ya ndani afanye mwenyewe.

    Wasiwasi wake huenda machale yamemcheza kuwa karibu na Teddy. Hakutaka kuhoji alitaka kuona mwisho wake. Baada ya kutoka kuoga Snura alitenga chakula kitandani. Walikuwa salesale maua hakuna aliyekuwa na nguo mwilini.

    Walikula kwa kulishana kama ndege, kwa vile Snura alikuwa amejiandaa muda mrefu alijikuta akipandwa na mzuka na kusahau kama walikuwa wakilishana baada ya kupeleka chakula kilichokuwa mdomoni kwake mumewe alipoteremsha mdomo aliudaka na kuanza kudendeka.

    Walijikuta wamesahau kama walikuwa wakila na kujikuta wapo katikati ya bahari. Snura kujituma kukumbushia enzi walipoanza mapenzi, japokuwa kulikuwa na tofauti ya mwili. Zamani alikuwa na mwili mdogo na mwepesi kwenye nyonga lakini baada ya kunenepa alijitahidi lakini nyonga ilikuwa nzito.

    Mchakamchaka haukuwa wa kitoto kila mpira ulipotua Snura alifika, faulo ulipiga yeye kona yeye golikiki yeye kutupa yeye. Mpaka wanakwenda mapumziko palikuwa pamechimbika bila jembe.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog