Search This Blog

Monday, October 24, 2022

MZEE WA DODO - 4

 





    Chombezo : Mzee Wa Dodo

    Sehemu Ya Nne (4)



    ILIPOISHIA:

    "Apate tabu ya nini na sisi tupo na hatujaonyesha kukutenga zaidi ya kukujali na kukuona zaidi ya ndugu zangu. Teddy wema ulioupanda hauta oza milele," Mmh! Makubwa kauli yangu ile ilimfanya Teddy alie kwa sauti na kumfanya Snura achanganyikiwe na kujiuliza kwa nini analia vile.

    "Dada inatosha maneno yako yanauchoma moyo wangu...inatosha dada," Teddy alisema huku akijilaza kifuani kwa Snura.

    SASA ENDELEA....

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Mmh! Teddy mbona sikuelewi kama umeambiwa ukipata ujauzito unakufa, hata hao walioathirika hawako hivi."

    "Unajua dada nimewaongezeeni mzigo."

    "Hapana mdogo wangu, ondoa wazo hilo jisikie ni mmoja wa familia, Teddy huwezi kuamini nakupenda hata kuliko ndugu zangu wa tumbo moja."

    "Ndiyo maana moyo unanisuta dada."

    "Hapana, nipo pamoja na wewe muda wote na siku zote sasa hivi ni zaidi ya ndugu, Teddy umenifanyia mambo makubwa pengine bila kuwepo wewe nyumba yangu ingeyumba, nakupenda sana."

    Maneno yale yalikuwa makali sana moyoni kwa Teddy ambaye aliona amefanya kosa kubwa sana. Pamoja ya kupendwa na Snura na kumpa kila kitu alimchukulia mume kibaya zaidi amebeba ujauzito wake.

    “Sawa dada nimekelewa nashukuru kwa kunijali.”

    “Basi kapumzike kazi zote za usafi nitafanya mimi.”

    “Hapana dada uwezo wa kazi ninao wewe pumzika tu, nitamaliza kazi zote.”

    “Basi wacha nikazungumze na shemeji yako ikiwa pamoja na kukupatia msichana wa kazi wa kukusaidia mapema.”

    “Sawa dada.”

    Snura alielekea chumbani kumfuata mumewe aliyetangulia na kumkuta akiwa mbali kimawazo.

    “Vipi mume wangu naona upo mbali kimawazo?”

    “Kwani Teddy amekueleza nani mwenye ujauzito?” lilikuwa swali lililomtoka mdomoni Tumu alijaa wasiwasi wa kutajwa.

    “Anasema hamjui.”

    “Sasa hiyo mimba kapata ndotoni?”

    “Sasa kama aliyempa hajui yupo wapi tufanyeje?”

    "Mke wangu la muhimu unaonaje kama Teddy akienda kwao akatunzie ujauzito wake lakini matumizi tutamtumia kama kawaida?"

    "Mume wangu yaani tumtoe mjini kwenye huduma nyingi za kiafya tumpeleke kijijini, kisa cha kumuua au kumpotezea mtoto. Pengine ndio yai lake hilo hilo moja unataka akose mtu wa kumwita mama."

    "Mke wangu huyu mtoto wa watu tumrudishe kwa wazazi wake kuepusha lawama.”

    "Au mume wangu ni wewe ndiye unayemuona Teddy ni mzigo basi nasema hivi haondoki nitamuhudumia mimi."

    "Mke wangu walaa, muulize kama kuna siku nilimuuliza kuhusu mambo yake kwanza mimi mambo ya wanawake yananihusu nini?" Tumu alijitetea.

    "Basi kaa kimya niachie mimi, huyu Teddy ni zaidi ya ndugu zangu ametulea sisi na mtoto wetu."

    "Mimi sina neno,” Tumu alikubaliana na mkewe kwa shingo upande.



    Usiku ulikuwa mrefu kwa Tumu kila alipofikiria ujauzito wa Teddy alichanganyikiwa. Aliamini kabisa msala ule ni wake, wazo la haraka lilikuwa kumshawishi aitoe ili kurudia amani ya moyo wake. Aliamini kabisa ipo siku lazima atasema ukweli na kusababisha kuivuruga ndoa yake.

    Pamoja na mkewe mwanzo kutompa ushirikiano kitandani lakini alikuwa na mapenzi ya dhati hakupenda kumuudhi kama mkewe akijua amempa ujauzito msichana wa kazi ambaye mwanzoni alikuwa akimdharau.

    Alisubiri mkewe amelala na kukoroma aliamka taratibu kitandani na kutembea mwendo wa kunyata hadi mlangoni na kuzungusha kitasa cha mlango taratibu bila kutoa kelele na kuufungua mlango kisha kunyata kutoka nje.

    Alitembea peku mpaka kwenye chumba cha Teddy na kuzungusha kitasa nacho kilitii amri na kuusukuma ndani kisha aliingia bila kumshtua Teddy aliyekuwa amepitiwa na usingizi.

    Kwa vile ndani palikuwa giza aliwasha taa na kumkuta msichana wa kazi amejilaza kihasarahasara bila kitu chochote mwilini. Alijikuta akipandwa na mzuka lakini hakutaka kuziruhusu hamu zake kwani sicho alichokuwa amekifuata kwa muda ule.

    Alisogea hadi kitandani na kupiga goti na kumtisikisa Teddy taratibu aliyekuwa amejiachia kwa raha zake kila kitu kilikuwa wazi.

    “Teddy...Teddy,” alimwita kwa sauti ya chini huku akiendelea kumtikisa.

    “Mmh!” Teddy aliitikia bila kufumbua macho.

    “Teddy amka mara moja.”

    Teddy alifumbua macho na kukutana na shemeji yake akiwa amemuinamia, alikurupuka na kumkumbatia kwa kupitisha mikono nyuma ya shingo na kumvutia kwake.

    “Mmh! Afadhali nimekuja mpenzi mtoto anataka kuongezwa viungo.”

    “Teddy sicho kilichonileta.”

    “Sawa lakini nipe huduma ya kwanza hali ni mbaya,” Teddy alisema huku akiutafuta mdomo wa Tumu ili ampe denda.

    “Teddy nisikilize kwanza kilichonileta kabla ya kufanya unayotaka kuyafanya.”

    “Shemeji siwezi kukuelewa zimejaa nilikuwa naota tupo pamoja na kujikuta nikiteseka peke yangu. Lakini kumbe upo karibu yangu.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Teddy taratibu.”

    “Taratibu nini mwenzio navujiwa nasikia baridi.”

    Teddy alisema huku akielekea ikulu kwa kupapasa kama kipofu.

    “Teddy na..na..omba kwa..kwanza unisiki..li..ze ,” Tumu alijikuta akipata kigugumizi cha ukubwani baada ya Teddy kufanikiwa kuingia kwenye shamba la muhogo na kuanza kuumenya kwa mdomo.

    Teddy hakuwa na shida ya kumsikiliza zaidi ya kuendelea na shughuli yake huku chini hali ikizidi kuwa mbaya bwawa lilijaa na kumwaga nje. Baada ya mchicha kukolea nazi mtoto wa kike alimpanda farasi wake na kuanza mwendo kwa kupanda na kushuka juu ya mgongo kwenye mabonde.

    Tumu naye hakutaka kuonekama mshiriki bali mshindani, ilianza kama mzaha mara moto ukashika majani makavu, hukuwepo bali shetani wako alikuwepo. Mtoto wa kike alijituma huku akitoa kilio cha kuonewa ambacho kilikuwa kama chachandu yenye kuongeza ladha ya chakula na kumfanya Tumu asahau kilichompeleka usiku ule.









    Teddy mashetani yalipanda na kuanza kutaja jina:

    “Tu..tu..tummmmu.”

    “U..u..na..nasemaje?”

    “Muongezee viungo mtoto ili afanane na wewe...aah sikio hilo Tumu, mtoto hajakamilika ooh! Jicho hilo jitahidi mpenzi wangu mtengeneze mwanao afanane na wewe..mmmh! pua hiyooo...oo..oo..ongeza viungo mpenzi mtoto akamilike. Tumu mwanao nitamwita jina la baba yako...aah! noo nitamwita jina la mama yakoooo ..ha..ha.ki ya..ya..a nani mtoto kopi laiti na baba yake usimkatae mwanao...tu..tu..tuuuuu....mmmmmu,” mtoto wa kike alipanda juu kama mkizi aliporudi chini alitulia alikuwa amemaliza safari ndefu.

    Teddy alishusha pumzi ndefu na kutulia tuli kitu kilichomtisha Tumu na kufanya amsogelee na kumshika kifuani na kukuta anahema kwa mbali.

    Alijiuliza ameua au vipi, lakini kitu kama kile hakikuwa kigeni kwake. Alimwangalia Teddy alijiyekuwa amejilaza akiwa hoi bin taabani na kujua alichokifuata hatokipata. Alimlaza vizuri na kumfunika kisha aliondoka kurudi ndani akiwa amekosa alichokifuata.

    Japokuwa alitaka kupata ukweli juu ya ujauzito ule lakini maneno ya Teddy ulimuhakikishia ule ni wake hivyo alitakiwa kufanya mpango kuhakikisha anautoa kabla mambo hayajabumbuluka. Alipofika alikwenda bafuni kujiswafi na kurudi kitandani kujilaza pembeni ya mkewe.

    Kabla hajalala mkewe aligeuka na kumwita.

    “Bebii.”

    “Naam.”

    “Upo wapi mpenzi wangu?”

    “Nipo sweet.”

    “Nasikia baridi mpenzi nikumbatie.”

    Tumu alimsogelea mkewe na kumkumbatia huku akiomba Mungu asilianzishe kwa vile alikuwa amechoka sana.

    “Mpenzi.”

    “Naam.”

    “Mbona hunipi ushirikiano.”

    “Upi tena si nimekukumbati?.”

    “Joto lako limenitia hamu nishike huku mpeenzi,” Snura aliongelea puani.

    Tumu ambaye alitegemea kumkuta mkewe amepitiwa usingizi alichanganyikiwa. Lakini alipanga kumpiga mkewe pigo moja pigo la nguvu pigo lililo nyooka ambalo litamfanya apate muda wa kupumzika. Baada ya kushika alipoelekezwa, mkewe mashetani yalipanda na kusubiri kupungwa.

    Lakini ajabu pikipiki ya Tumu alipopigwa kiki alikataa kuwaka.

    Snura aliingia kwenye kazi ya kupasha moto kiporo cha mnofu ambao ulioneka kwa muda ule hauliki.

    “Baba Gift leo una nini?” Snura alishtuka kwa vile hali ile hakuwahi kuiona katika ndoa yake, siku zote alimjua mumewe moto mara moja.

    “Hata sijui,” Tumu alijitetea.

    “Hapana baba Gift lazima leo umetumika,” Snura alilalamika.

    “Kutumika wapi mke wangu?”

    “Hii nini?”

    “Hata mi nashangaa.”

    “Baba Gift lazima utakuwa umetumika tu.”

    “Hapana mke wangu.”

    “Hebu ona kilivyochoka, mume wangu umetumika leo,” Snura alisema huku akiuchezesha mtalimbo uliokuwa umelala dolo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tumu alikuwa hana jinsi kwani muziki wa Teddy haukuwa wa kitoto hasa baada ya kuuzoea mnazi wake mtoto wa kike alikuwa akiupanda kama anateremka na kumfanya mwanaume badala ya kuonja ajikute akikwangua mpaka ukoko.

    Baada ya mtanange na Teddy kisha mkewe kutaka haki yake muziki kugoma kupigwa kilikuwa kitu ambacho hakukitegemea. Aliamini kama mzigo angemwaga safari moja siyo gari kugoma kabisa kupanda mlima.

    Snura hakukubali kuona mchezo unalala alijitahidi kuotesha makucha ya mumewe ili akunwe kwani muwasho ulikuwa mkubwa kama katambaliwa na utitiri. Mtoto wa kike akijitahidi anavyojua huku jasho likimtoka kama maji kuhakikisha anamuamsha aliyelala.

    Kila alichokifanya kilikuwa kazi bure na kujikuta akichoka na muda kwenda bila mafanikio. Machozi ya uchu yalitoka huku akiendelea kumshtumu mumewe kuwa ametumika.

    “Mume wangu leo umetumika.”

    “Hapana mke wangu hata mimi nashangaa.”

    “Sasa mbona babu hataki kuamka.”

    “Subiri kidogo,” Tumu alitaka kuvuta muda kurudisha nguvu.

    “Mume wangu haziwezi kusubiri hali ni mbaya zimejaa sasa zinamwagika.”

    “Sasa tutafanyaje?”

    “Sijui lakini mpaka nijue mwisho wake.”

    Snura aliendelea uipa kashkash bakora angalau isimame dede kama mtoto anayejifunza kutambaa ili aidandie lakini hali ilikuwa tofauti mtalimbo uliendelea kulala ndolo. Kutokana na kutumia nguvu nyingi alijikuta akipitiwa usingizi kutokana na uchovu, aliposhituka alimkuta mumewe kapitiwa usingizi lakini mnofu ulikuwa mkononi ukiwa bado umelala dolo. Hakukubali aliendelea na zoezi lake bila kumuamsha mumewe.

    Sauti ya muadhini ilimshtua Snura na kugundua kumbe kumekucha, lakini, ndo kwake kidooogo ndiyo palikuwa panapambazuka jogoo ndo kwanza alianza kuwika kwa kujilazimisha. Hakukata tamaa aliendelea kuupasha moto unofu ambao ulianza kupata joto.

    Tumu baada ya kupumzika kwa muda alirudiwa na nguvu na kufanya mkonga kuanza kushika netiweki. Baada ya muda chuma kilikolea moto Snura alimzaba kibao mumewe aliyekuwa usingizini ili ampe mshirikiano.

    Tumu kibao kilimpata sawasawa na kuamka usingizini na kuuliza huku macho yamemtoka pima:

    “Vipi?” alimuuliza mkewe aliyekuwa amesimama pembeni bila kitu mwilini.

    “Hujui?” Snura alimuuliza mkono ameshika kiunoni.

    “Sijui nini, umenipigia nini?”

    “Acha ujinga, ulivyonifanyia mazuri?”

    “Yapi mke wangu?”

    “Tumu chuma kikipoa hichoo atatafuta mbeleko ya kunibeba,” Snura alitoa onyo kali kwa mumewe baada ya kuupepea moto kwa shida na kuhofia mbwembwe za mumewe kuuzima.

    Tumu aliposhtuka kuwa anatakiwa kuchangamka kuchemsha maji kabla moto haujazima. Kwa haraka alikimvutia chombo majini na kuanza kupiga kasia. Alishangazwa na mkewe siku ile kutatalika kama ndiyo siku ya kwanza kutafuna soseji.

    Akiwa amerudi upya nguvu mpya na kasi mpya hakutaka kumuudhi mkewe na kufukia makosa aliyofanya. Mwanaume alijituma kama ndiyo siku yake ya kwanza kukutana na mkewe na kutumia mitindo yote uliyomfanya mkewe aangue kilio kilichomshtua Tumu.

    “Nini mke wangu?”

    “Siwezi..si..si..we zi..”

    “Nini mke wangu?”

    “M..m..mh!”

    “Nini mke wangu?”

    “Si..si..o wewe.”

    “Ni nani?”

    “Leo mume wangu umekuwa mpya.”

    “Kivipi?”

    “Nitakwambia...nitakwambia mwisho.”

    Snura alipagawa alikuwa kama kidonda kilichowekewa chumvi jinsi raha zilizokuwa zikimchonyota. Si wajinga waliosema ukiwa na hamu hata utafune makalatasi utayaona matamu. Snura alizitengeneza hamu mwenyewe alipoonja utamu ukakolea.







    Baada ya mshikemshike wa kukata na shoka Snura alichoka kama aliyekuwa akitwaga chuma na usingizi mzito ulimchukua. Tumu naye alijilaza pembeni ya mkewe alikuwa amechoka sana baada ya kupiga mbili kwa moja.

    ****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Teddy baada ya mshikemshike wa usiku alizinduka usingizini baada ya kuamshwa na alam aliyotega kwa ajili ya kumwamsha kufanya kazi ya kufanya usafi na kuwaandalia matajiri zake kifungua kinywa na chakula la Gift. Kila alipotaka kunyanyuka kitandani uchovu ulikuwa mkubwa sawa.

    Alijikuta akichukia kuwa msichana wa kazi, aliamini kama angekuwa mke wa Tumu basi angeamka muda anaotaka. Alisema alale kidogo kabla ya kuamka lakini aliposhtuka alikuta ameamka saa mbili kasoro asubuhi. Alinyanyuka haraka na kujiuliza tajiri zake wameondoka bila kupata kufungua kinywa.

    Alitoka hadi sebuleni na kushtuka kukuta mlango umefungwa kwa ndani hakuna dalili zozote za watu kutoka. Ili kupata uhakika alikwenda hadi kwenye mlango cha chumba cha tajiri wake na kuonekana umefungwa ndani.

    Alikwenda kuoga na kuandaa kifungua kinywa na chakula cha mtoto.

    Mpaka anamaliza kuandaa pia kumlisha mtoto, tajiri zake walikuwa hawajaamka. Alijikuta akijiuliza siku ile ni siku gani kwani aliamini si mwisho wa wiki pia haikuwa siku ya sikukuu.

    Wazo la kwenda kuwaamsha alikuwa nalo kwa kuhofia tajiri zake kuchelewa kazini japokuwa muda ulikuwa umekwenda. Wakati akienda kugonga mlango Tumu alikuwa ameshtuka usingizini na kuangalia saa iliyomuonesha ni saa tatu za asubuhi. Alishtuka usingizini na kumuamsha mkewe.

    “Mke wangu tumechelewa kazini.”

    “Kwani saa ngapi?”

    “Saa tatu.”

    “Duh! Sasa nifanyeje?”

    “Itakuwaje kazini leo?”

    “Watajijua wenyewe.”

    “Mke wangu oga uwahi kazini.”

    “Nikafanye nini?”

    “Leo huendi?”

    “Siendi”

    Snura alijibu huku akigeuka na kujilaza kifudifudi na kumuachia nundu mumewe ambayo kwa muda ule alikuwa amemkinahi. Japokuwa naye alikuwa amechoka alinyanyuka na kutoka kwanza nje ili kuangalia hali iliyo. Alipofungua mlango alikutana na Teddy na kushtuka.

    “Vipi Teddy?”

    “Leo hamuendi kazini?”

    “Ndiyo.”

    “Kwa nini?”

    “Siyo juu yako.”

    “Mmh! Sawa.”

    Tumu aliamini muda ule anaweza kuzungumza mawili matatu na Teddy kabla mkewe hajaamka.

    “Teddy vipi?”

    “Safi, shikamoo shemeji.”

    “Asante. hebu ngoja,” Tumu alisema huku akirudi ndani.

    Tumu alirudi ndani kwenda kumuangalia mkewe na kumkuta ndiyo kwanza anajigeuza katikati ya usingizi na kuendelea kulala mlao wa mchoko.

    Alirudi haraka kumfuata Teddy ambaye wakati huo alikuwa jikoni akifanya usafi wa vyombo, alipofika alimtekenya.

    “Aiiih!” Teddy aliruka na kusababisha chombo alichokuwa ameshika mkononi kidondoke chini na kupasuka.

    “Muongo! Bado hazijaisha?”

    “Ziishe wapi ulikuwa unamkomaza mwanao ukanisahau mama yake.”

    “Mmh! Mpenzi si umesema wewe imetosha.”

    “Ulitaka sifa nilikula vikataka kurudi lakini hamu haaishi.”

    “Jamani si ulitaka mtoto akamilike viungo.”

    “Mmh! Mwenzio sijui hata nilikuwa dunia gani, yaani namuonea wivu mama Gift. Ingekuwa kila siku kama yeye ningenenepaje .”

    “Mpenzi tuachane na hayo kuna kitu nataka kukuuliza.”

    “Kipi mpenzi?”

    “Eti mimba hii ya nani?” Tumu alimuuliza akiwa anamtazama usoni kwa jicho kavu.

    “Sijakuelewa una maana gani?” swali lilimshtua Teddy.

    “Hapana, lazima nijue nani mwenye ujauzito huu.”

    “Simjui,” Teddy alijibu huku akimpa mgongo Tumu.

    “Kwa hiyo baba wa mtoto humjui?”

    “Ndiyo, unamjua wewe.”

    “Sasa mimi nitamjueaje ukiwa mwenye tumbo ni wewe?”

    “Mwenye tumbo ni mimi lakini muwekaji ni wewe, sasa sijui kama humjui muwekaji.”

    “Teddy hebu kuwa mkweli ili tujue nani mwenye mzigo.”

    “Simjui,” Teddy alijibu kwa mkato na kuinama kookota vipande vya sahani vilivyo pasuka.

    “Sasa mbona unasema wangu.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nikuulize wewe unayejitoa akili,” Teddy alikuwa mkali.

    “Akili kivipi?”

    “Hii mimba kanipa nani?” alimuuliza huku akinyanyuka na kumuangalia jicho kavu.

    “Ndiyo maana nakuuliza.”

    “Unaniuliza nini?”

    “Ili nimjue.”

    “Kanipa Gift.”

    “Gift ndiyo nani?”

    “Mwanao.”

    “Mwanangu! Acha utani.”

    “Si ndiye ninaye lala naye kila siku.”

    “Unajua mimi nakuuliza jambo la maana wewe unaleta utani.”

    “Nitamwambia mkeo akiamka, nina imani utamuelewa kwa vile mimi hutanielewa.”

    “Ina maana mimba ni yangu?”

    “Sijui.”

    “Ina maana unataka kumwambia mke wangu ili iweje?”

    “Utajua tu, mi kukaa kimya unanifanya mjinga, ulipokuwa ukiniteremsha kufuri uliona raha leo hii unalishangaa tumbo, sasa subiri nipasue jipu kwa mkeo.”







    “Hapana usifanye hivyo nilitaka kujua tu wala si kuikataa mimba.”

    “Umeishajua?”

    “Ndiyo, sasa basi unaonaje tuitoe.”

    “Weee koma, ishia hapohapo we unaye mimi wangu nimtoe, siyo lazima nikae kwenu na mkeo akiamka namwambia naondoka.”

    “Sasa ukikaa hapa akijua itakuwa mbaya.”

    “Labda umwambie wewe.”

    “Basi nakuomba kitu kimoja ukazalie kwenu matumizi na pesa za kujikumu nitakupatia.”

    “Hilo ndilo nililokuwa nataka.”

    “Basi mpenzi naomba siri hii ibakie moyoni mwako.”

    “Mbona mimi toka zamani niliimeza.”

    Walikubaliana kuifanya iwe siri huku Tumu akimuandalia fedha ya kutosha Teddy ili akajifungulie nyumbani kwao.

    Wazo la Tumu, Teddy aliliafiki kwa kuamini mazingira ya pale hayakuwa mazuri na kama Snura angegundua aliyempa ujauzito ni mumewe pangewaka bila kiberiti.

    Hakutaka kumshtua haraka mama Gift alijipanga taratibu, aliamini kumwambia kwa ghafla atakuwa amemkosea heshima kwa mtu aliyemlea kama mdogo wake wa kumzaa.

    Alitaka atafute sababu ya kumfanya Snura amruhusu kuondoka lakini akiwa ameishapata msichana wa kazi mwingine ili Gift apate mlezi.

    Tumu baada ya wiki alimtafutia Teddy laki tatu za kwenda nazo kwao na kuahidi kumpelekea mahitaji yote muhimu mpaka atakapojifungua na kumlea mtoto wake kama Gift.

    Baada ya makubaliano yao alitegemea Teddy kuondoka kama walivyokubaliana. Lakini, alishangaa wiki ilikatika bila kuwepo dalili zote za kuondoka. Alijiuliza anasubiri nini, usiku kama kawaida baada ya kumpa mkewe dozi nzito na kuwacha akiuchapa usingizi alimfuata Teddy chumbani kwake na kumkuta amelala milalo yake ya hasara mguu mmoja mashariki na mwingine magharibi kwa bibi pakiwa chekwa.

    Hamu zilimpanda upya baada ya kuliona lindo tupu, lakini sicho kilichompeleka usiku ule. Alichukua kanga na kumfunika kisha alimsogelea na kumtikisa.

    “Teddy..Teddy,”alimwita kwa sauti ya chini.

    “Mmh!” aliitikia bila kugeuka.

    “Teddy ...Teddy.”

    “Abee.”

    ‘Amka.”

    “Tutaongea kesho bhana.”

    “Hapana amka unisikilize.”

    Teddy alifumbua macho na kutabasamu baada ya kumuona shemaji yake.

    “Vipi mpenzi, afadhali umekuja yaani nina wasiwasi mtoto hajakamilika vizuri.”

    “Kivipi?”

    “Mbona hachezi.”

    “Atachezaje ujauzito bado mdogo.”

    “Basi hujamkomaza.”

    “Silo nililolifuata.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hata kama silo ulilolifuata lakini ukiingia chumba cha upasuaji lazima upasuliwe.”

    “Sawa lakini naomba uniambie nini kinachokukwamisha mpaka leo ikiwa mshahara wako upo tayari na fedha za matumizi nimekupa.”

    “Nilifikiri jambo kubwa kumbe ni hilo?” Teddy alijibu kwa dharau huku akibinua midomo.

    “Wewe unaliona dogo?” Tumu alimshangaa.

    “Kwani tatizo nini?”

    “Mpaka mtoto akomae, ili niondoke hakikisha kuanzia usiku huu unanipa dozi kamili ili nikiondoka mwanangu asiwe na mapungufu. Kama ungekuwa mume wangu tungeacha kumkomaza mtoto siku ambayo nakwenda kujifungua, kwanza nasikia ukipata asubuhi mtoto anateleza kama samaki.”

    “Teddy acha utani.”

    “Utani wa nini?”

    “Mimi nakuambia vitu vya maana, nataka ujauzito wako akautunzie sehemu salama ili kuondoa wasiwasi wa kushukiwa, wewe unaleta utani.”

    “Labda wewe ndiyo unaona utani, ujauzito wa Gitf nasikia mmeacha wiki moja kabla ya Gift kuzaliwa. Mimi mwangu unataka miezi miwili?”

    “Achana na mama Gift muongo.”

    “Tena nasema hivi nikiondoka nataka kwa mwenzi hata hata mara moja, nitakuwa nafunga safari kuifuata.”

    “Nimekuelewa, sasa utaondoka lini?”

    “Baada ya miezi miwili ijayo tena unipe huduma ya kuridhisha na siyo kupakana shombo bora liende lazima nipate kipigo cha pweza.”

    “Sasa Teddy unanikomoa?”

    “Wenye kukomoka mimi au wewe? Nani aliyebeba mimba. Wewe kwa raha zako hupati kichefuchefu wala kutapika. Chakula unakula unachotaka lakini mwenzio nimekuwa kama mchuzi bila ndimu sijisikii vizuri. Hapo nani anakomoka?” Teddy alimtoka.

    “Lakini Teddy siyo makubaliano yetu.”

    “Ni kweli, lakini kuna niliyozungumza na dada.”

    “Yapi hayo?”

    “Kwanza nipe haki yangu mtoto tumboni anataka kusimama lakini hana mguu mmoja hebu muongezee mwanao mguu wa pili aweze kusimama dede tumboni.”

    “Teddy maneno hayo imeyatoa wapi?”

    “Nitakwambia baada ya kumkomaza mwanao.”

    “Tufanye kesho, mama Gift amesinzia.”

    “Waswahili bhana tunaweza kubishana mpaka asubuhi, lakini kunipa unaona mkeo utashtuka. Nilifikiri ni wanawake tu huwa wanazungusha kumbe hata wanaume.

    “Lakini kumbuka ulipokuwa na hamu zako uliniamsha hata usiku wa manane nikidhi haja zako hata kama nimechoka na kazi za kutwa nzima. Leo hii unaniona kero.”









    “Leo nitakupa, ila naomba katikati ya wiki hii uondoke hata fedha za matumizi nitakuongeza.”

    “Sawa utaniongeza shilingi ngapi?”

    “Elfu hamsini.”

    “Hata laki siondoki.”

    “Unataka ngapi?”

    “Laki tatu.”

    “Nyingi sana nitakupa mbili.”

    “Sawa.”

    Tumu ilibidi atoe dozi nyingine huku akichanganyikiwa na utundu wa Teddy na kujikuta akipata wazo la kumpangia chumba palepale mjini na kumuwekea kila kitu ili aendelee kupata huduma adimu toka kwa Teddy.

    Lakini amiamini mkewe akijua ingesababisha kuvunjika kwa ndoa yake. Baada ya dozi nzito Tumu aliondoka kama kawaida alimuacha Teddy hoi bin taaban baada ya kipigo cha pweza.

    Tumu alijitahidi katika siku mbili kumpatia Teddy laki mbili ili aondoke. Lakini zilikatika wiki mbili bila kuonesha dalili za kuondoka. Kumwambia mkewe kuhusu kumpeleka Teddy kijijini wasingeelewana. Siku zote alimuona mkewe akimng’ang’ania Teddy bila kujua ndiye panya anayekula mahidi kwenye ghala lake.

    Ilikuwa tofauti na siku za nyuma alipomnyatia usiku Teddy alikuta mlango upo wazi lakini ajabu kila alipokwenda alikuwa umefungwa kwa ndani na alipogonga mlango haukufunguliwa.

    Kitendo kile kilimfanya awe katika wakati mgumu, kila siku asubuhi ilikuwa lazima aondoke na mkewe tofauti na zamani. Alijiuliza Teddy ana ajenda gani na mkewe. Wasiwasi wake labda mambo yapo wazi kama vazi la kahaba.

    Tumu baada ya kuona hamuelewi Teddy siku moja alirudi ghafla ili kujua hatima yake kwa vile aliishaona mchezo. Siku zilikuwa zikikatika bila kuonesha dalili mtu kuondoka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wasiwasi wake Teddy atajifungua palepale na mtoto sura ikifanana na Gift itakuwa aibu kubwa kwake hata kama angejitetea vipi ushahidi ungekuwa umekamilika.

    Aporudi nyumbani alimkuta Teddy akifanya usafi jikoni. Ajabu Teddy alipomuona hakushtua alimuangalia kama mtu wa kawaida huku akipinua mdomo.

    “Karibu,” Teddy alikuwa na nyodo kitu kilichozidi kumweka Tumu kwenye wakati mgumu.

    “Teddy,” alimwita kwa sauti ya ukali.

    “Babu wee hebu sema kwa sauti ya chini, mwanangu amelala utamwamsha,” Teddy alijibu huku akimwangalia Tumu juu mpaka chini kwa dharau.

    Majibu ya Teddy kidogo yamchekeshe Tumu lakini hakutaka utani muda ule, japokuwa Teddy alionekana kujiamini kupita kiasi.

    “Teddy hivi kitu gani kinachokupa kiburi?”

    “Kiburi gani, halafu hii tabia ya kufokeana imeanza lini? Nimekuwa nakutazama tu, unaona raha kunifokea, mbona ulipokuwa ukipata raha zangu hukunifokea zaidi ya kubembeleza nikuongezee tena.”

    “Lakini tumeongea nini?”

    “Tatizo nini?”

    “Tumekubaliana uondoke hata fedha ya matumizi nimekuongezea sasa tatizo nini?”

    “Mmeisha mpata mlezi wa Gift?”

    “Tutafuta ukiondoka.”

    “Naomba hayo akija mke mwenzangu jioni umeeleze, kesho alfajiri naondoka.”

    “Sasa unataka kunigombanisha na mke wangu nitaanzia wapi?”

    “Kivipi?”

    “Wewe tafuta mbinu yoyote ili uondoke.”

    “Unataka nitoroke na kumwacha Gift?”

    “Hapana.”

    “Sasa unataka nini?”

    “Ungesingizia kwenu kuna tatizo ili ukiondoka usirudi.”

    “Sema una wewe pupa kila kitu nimekipanga vizuri kuna mtu ameagizwa toka nyumbani anafika mwisho wa wiki, kisha nitaondoka kama nimeitwa na mama ndiyo sirudi tena.”

    “Sasa kumbe mambo si hayo,” Tumu alitabasamu kupata taarifa ile.

    “Nyooo, mambo si hayo unapeeenda,” Teddy alisema huku ameshikilia pua.

    “Na ninaondoka anakuja mdogo wangu ukitembea naye humu ndani patakuwa hapatoshi.”

    “Teddy sirudii tena.”

    ”Kwa hiyo umeridhika? Maana kila ukiniona presha juu kama umemuona mtoa roho.”

    “Yaani katika siku umenifurahisha leo umenifurahisha nakuahidi kabla ya kuondoka nitakununulia vitu vya kutumia na laki moja juu.”

    “Haya wewe umefurahi naomba na mimi unifurahishe.”

    “Kivipi?”

    “Mwanao anataka joto la baba.”

    “Teddy nimetoroka kazini ili tuje tupange, usiku nitakuja.”

    “Usiku yako, yangu mchana, ukiacha kunifurahisha nitakuudhi na kutamani ardhi ikumeze.”

    “Basi njoo nikupe la jikoni.”

    “Wewe tu lakini uwe makini kwa sababu mwanao anapenda kukaa sebuleni usimbemende tu.”

    “Teddy maneno yote hayo umeyatoa wapi, hukuwa mzungumzaji umejifunza wapi?”

    “Nimekuwa mkubwa sasa, nina haki ya kuzungumza chochote kwako, tofauti na mwanzo nilikuogopa kwa kuwa ulikuwa bosi wangu.”

    “Sasa hivi siyo basi wako?”

    “Ubosi uliisha toka nilipokufungulia kufuri lango na kupenyeza funguo yako.”

    “Haya mama punguza maneno niwahi kazini.”

    “Wewe tu mi kama mgonjwa wa sindano, nikinyanyua pa kuchoma unapaona.”

    Teddy alisema huku akipembua na kukaa mkao kama gari limepigwa jeki upande mmoja.

    Tumu aliteremka kioo kidogo mchezo ukaanza, walijikuta wakihama toka jikoni mpaka chumbani mambo yakawa mambo. Teddy alikuwa na kilio kipya ambacho kilikuwa kama mtoto wa mbwa na kuwa kama ndimu kwenye mchuzi na kumfanya mlaji ale sahani tatu badala ya moja aliyotaka ndivyo ilivyokuwa kati ya Tumu na Teddy.

    Walijikuta wametumia saa mbili na kumfanya Teddy achoke na kuendelea kulala na kumwacha Tumu aondoke ambaye alipata wakati mgumu wa kuona Teddy anaondoka na raha zake.

    Wazo lake lilikuwa kumshauri atoe mimba ili aendelee kuwa mchungwa wa uani ambao si lazima kupata hata mti wa ufagio unatumia kuangushia na kujilia kwa raha zako.

    Siku ile Teddy alichoka sana hata kazi za ndani zilimshinda alishinda amelala. Alichokifanya kikubwa kilikuwa kumlisha Gift na kumuogesha baada ya hapo alipanda kitandani na kujilaza mpaka usiku.

    Snura aliporudi alishtuka kukuta nyumba ipo sagalabagala. Nilipokwenda chumbani kwa Teddy alimkuta amejilaza.

    “Vipi mdogo wangu?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/“Mwili leo siuelewi kabisa.”

    “Pole mdogo wangu, mimba changa zina matatizo yake.”





    “Mmh! Kama mambo yenyewe ni hivi sizai tena,” Teddy alikoleza uongo wake.

    “Walaa mdogo wangu hali hii ya mpito tayaisha tu.”

    “Sasa hivi si kumuhangaikia Gift nipo hoi unafiriki hali hii mpaka lini?”

    “Vumilia mdogo wako mwisho wa wiki si anakuja.”

    “Nitajitahidi.”

    “Unajua familia yenu nimeipenda sana, isingekuwa hivyo ningemtafuta yeyote lakini wasichana wa kazi wa siku hizi hawaaminiki.”

    “Hakuna tatizo nina imani familia yetu tumelelewa malezi mazuri.”

    “Umeisha kula?”

    “Hata hamu ya kula ninayo!”

    “Hapana mdogo wangu ngoja nipike ule.”

    Snura aliingia jikoni kupika bila kupumzika kwa kumuonea huruma Teddy aliyekula amelala kwa uroho wake na kusingizia ugonjwa.

    ***

    Baada ya siku nne alikuja mdogo wa Teddy kuja kumsaidia dada yake kazi za ndani huku Snura akijua kabisa Teddy atakuwepo pale mpaka atakapo jifungua.

    Lakini Teddy alikuwa na siri yake kwa kujua ule ulikuwa muda wake muafaka wa kuondoka.

    Wiki moja baada ya Tina mdogo wake Teddy kumzoeana na Gift, Teddy alipanga jinsi ya kuondoka. Siku aliyopanga kuzungumza na familia ilipofika, baada ya chakula cha usiku aliwaita matajiri zake sebuleni na kueleza nia ya kuondoka.

    Wakiwa kimya sebuleni wote kumsikiliza Teddy, baada ya kupita kimya kifupi huku Tumu akiwa haelewi kikao kile ni cha nini. Alijikuta mtu mwenye wasiwasi mwingi kwa hofu labda Teddy ameamua kupasua jipu.

    Kabla Teddy hajasema Tumu mapigo ya moyo yalikuwa ya kasi, lakini alificha hofu yake.

    Baada ya kusimama alikohoa kidogo na kusema:

    “Samahanini kwa kuwachelewesha kulala.”

    “Bila samahani,” Snura alisema huku akiwa na hamu ya kumsiliza Teddy anataka kusema nini usiku ule.

    “Dada Snura na shemeji, napenda kutanguliza shukurani kwa yote mliyonitendea kwa kipindi chote nilichokuwa hapa kama msichana wa kazi ambaye nilikuwa si msichana wa kazi bali sehemu ya familia.

    “Baada ya kupata ujauzito najua hata wewe dada ulichanganyikiwa kuhusu matunzo ya kipenzi changu Gift kukosa mlezi makini. Lakini nashukuru alikuwepo mdogo wangu ambaye kaja kushika nafasi yangu.

    “Nimefurahi Gift amemzoea haraka, hivyo nina imani hata leo nikiondoka nimeacha mtu makini. Najua uamuzi wangu dada na shemeji utawashtua hata kipenzi changu Gift kitanikosa.

    “Pamoja na dada kunieleza niendelee kukaa, nimeona nitaongeza mzigo naomba niondoke niende nikajifungulie nyumbani. Mwisho wa wiki nimepanga kuondoka. Nina imani nimeeleweka,” Teddy alimaliza.

    Kauli ile ilikuwa suprises kwa Tumu ambaye furaha yake kidogo apige kelele ya kufurahia baada ya ombi lake la kuondoka kuiva.

    “Sawa Teddy ni wazo zuri, japokuwa tulikuwa tumekuzoea, mi sipingani na wazo lako, nikutakie safari njema,” Tumu alikuwa wa kwanza kusema.

    “Mume wangu yaani umefurahi Teddy kuondoka?” Snura alimuuliza mumewe.

    “Hapana mke wangu kama umembembeleza akae lakini kaamua kwenda kwao naomba tukubaliane na uamuzi wake. Teddy sasa mkubwa kwa hiyo aliyoamua ana sababu zake. Kwa vile tupo naye karibu nina imani tutamtazama kwa jicho la karibu.”

    “Yote hayo kujitetea, lakini umefurahi kuondoka kwa Teddy kwa vile ujauzito wake ulikuwa mzigo kwako.”

    “Mke wangu usinifikirie hivyo, basi nimuombe Teddy usiondoke,” Tumu alijifanya kutetea hoja yake yenye siri ndani yake.

    “Jamani naomba usitoane macho, dada naomba niende nyumbani kwa sababu mama kaita kwa kipindi hiki cha ujauzito mdogo kama nitatulia basi nitarudi kujifungua huku.”

    “Sawa basi, kwa hiyo utaondoka lini?” Snura aliuliza.

    “Mwisho wa wiki.”

    “Nashukuru mdogo wangu kwa kunijulisha mapema ili nikuandalie vitu vya kwenda navyo kwenu.”

    “Nitashukuru dada.”

    Tumu alipokutanisha jicho na Teddy walitabasamu na kumpa dole kuonesha amemfurahisha kwa kukubaliana naye kuondoka. Moyoni Teddy aliapa siku zilizobakia lazima apate dozi ya kila siku bila hivyo atabadili uamuzi wa kwenda kwao.

    Kwa vile muda ulikuwa umekwenda, waliagana na kwenda kulala. Baada ya kuingia chumbani Teddy alimpa somo mdogo wake kabla ya kuondoka.

    “Tina kama nilivyo kueleza, muangalie sana shemeji yako. Itakuwa aibu kupewa ujauzito ndugu wa familia moja na mwanaume mmoja kibaya mke wa mtu.

    “Dada yako nilijilegeza kidogo matokeo yake nimeruka na mimba.”

    “Nitajitahidi dada.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mdogo wangu nimekulea hapa kwa sababu maalumu ili niweze kuwasiliana na shemeji yako kwa karibu mimi nikiwa mbali. Sasa siyo urudi na tumbo nyumbani, itakuwa aibu kwa familia yetu.”

    “Sawa dada nitakuwa makini.”

    “Najua nawe mwanadamu kama itashindikana hakikisha unatumia kinga sana mdogo wangu?”

    “Sawa dada sitakuangusha, lakini nitajilinda.”

    “Basi mdogo wangu mi ndo naondoka sifa kubwa acha uvivu jiepushe mavazi ya ushawishi pia isijichekeleze kwa shemeji yako muone kama baba yako.”

    “Sawa dada.”

    “Haya tulale mdogo wangu.”

    Teddy na mdogo wake walijilaza kitandani kuitafuta siku ya pili. Wakati mdogo wake akilala yeye alitoka kumvizia Tumu kama atatoka basi amkamate ili kukidhi haja zake.

    Siku ile Teddy alikesha kumsubiri Tumu atoke lakini hakuwa kama alivyowaza. Muda ulikatika akiwa amekaa sebuleni bila dalili zozote za kumuona baba kijacho wake.

    Muda ulizidi kuyoyoma huku sumu ya chini ikipanda taratibu mpaka kisima kikaanza kumwaga maji nje taratibu. Mtoto wa kike hali ilizidi kuwa mbaya alipokuwa amekaa pakawa pachungu.

    Alipitisha mikono katikati ya miguu na kuibana na kupuliza kama anapiga mruzi, labda utitiri uliokuwa ukimtambaa ungepungua lakini wapi. Alijiuliza atateseka mpaka saa ngapi ikiwa mwenye kupunguza utitiri au kuutoa kabisa yumo ndani na siku za kumkomaza mtoto zilikuwa zimebakia chache.

    Kutokana na sifa za Snura anapolala huwa kama amekufa, aliamini kama angekwenda kugonga mlango lazima angetoka baba kijacho. Alijizoa mtoto wa kike, aliponyanyuka kanga aliyokuwa amejifunga ilidondoka. Aliiokota na kuiweka begani kujifunga aliona kazi. Alikuwa kama mchawi anayekwenda kuwanga.

    Kutokana na kukamatika hata kutembea kwake kulikuwa kwa shida kama mwanamke aliyeshikwa na uchungu. Mkono mmoja kiunoni na kutembea kwa kujilazimisha kwani utitiri ulikuwa umemshika hasa.

    Alipofika mlangoni dua zake akigonga atoke Tumu alipanga kama akitoka Snura aangushe kilio kama kafiwa na angeulizwa jibu lingekuja hapohapo.

    Alipofika mlangoni kwanza mkono mmoja akishika ukutani na mwingine kiunoni kama alikuwa anapanda mlima na kutoa pumzi ndefu. Chezea wadudu wadogowadogo wanapoamua kukunyemvua utalala hoi, kama nazi iliyopasuliwa na kukosa mkunaji.

    Kanga aliyokuwa begani ilimdondoka bila kujua wala hakuijali. Baada ya kupumua aligonga mlango huku akijiuliza Snura akimuona yupo vile kama mtu aliyeshikwa na uchungu wakati ujauzito ulikuwa na miezi nne sijui angemwambiaje.

    Aligonga mlango taratibu, bila kupata majibu. Aliongeza kugonga kwa nguvu na kusababisha Snura aliyekuwa katikati ya usingizi kuamka.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog