Search This Blog

Monday, October 24, 2022

NITAKUPENDA USIKU TU - 4

 

      

                                     

                                            



    Chombezo : Nitakupenda Usiku Tu

    Sehemu Ya Nne (4)



    “Kwanini Mash, Kwanini nilimkubalia??” Niliulaumu sana moyo wangu.

    Nilikaaa pale chini kwa muda nikiugulia maumivu. Si maumivu ya kupigwa bali maumivu ya uchungu kwa kumuona mtu niliyemuamini kwa muda mfupi nakumkabidhi kasuku wangu tena kwa uchu wa kutokufanya toka nizaliwe nikamkabidhi kavu kavu. Leo hii amenibadilikia?

    Iliniuma sana hata kama ungelikuwa wewe msomaji ingekuuma sana. Leo hii mtu huyo huyo anatoa tena kavu kwa mwingine?

    Nilijikaza, Nikajikaza nakujikaza japo niweze kuinuka kuelekea kwangu kupanga mikakati juu ya nini kifanyike. Mwili uliweza kuamka kwa shida sana. Nikainuka nakuanza safari ya kwenda kwangu. Kupanga na kupangua!!

    Haikuchukua muda sana nikawa nimeshafika getto. hoi!!. Mimi na maumivu maumivu na mimi. Nikaugulia hivyo hivyo kindani ndani. Nikajitupia kitandani nikikaribisha changamoto za mawazo katika kuwaza na kuwazua!!

    Mawazo mengi nikayakaribisha, yakakaribia!! Kuna ambayo yalinishauri kutokumwambia mtu yoyote iwe ni siri yangu tu. Mengine yakanijia kutokwenda kupima kwa aibu na woga. Pengine ningechekwa ama kutengwa endapo ningejulikana nimeathirika. Nisingepata wa kunisaidia hata kwa kunigeuza kitandani pindi ugonjwa ukinizidia! Moyo wangu ulikuwa mzito sana katika kufanya maamuzi. Nilijiona moja kwa moja ni muathirika wa ugonjwa wa ukimwi tena yule anayesubiri siku ya kufa tu.

    “Baba aliniambia kuhusu ukimwi na hata mama pia, nitawaeleza nini wakati niligoma kabisa kuwasaidia kilimo kijijini? Niliwadanganya uku mjini kunamaisha mepesi nitawasaidia. Nitawasaidia nini sasa kwa kuwapelekea ukimwi nyumbani?, anhhh!! Seif mimi kwishaaa kabisa!!”

    Nikiwa katika kujilaumu nakuumia mwenyewe kwa hisia kali mara hodi ikabishwa. Hasira!!

    “Nani? ingia!” Niliongea kwa sauti ya ukali.

    Alikuwa ni Jof. Alikuja akiwa na mijasho imemzunguka mwili mzima kama vile mtu aliyotoka kukimbizwa kwa wizi au kushikwa ugoni. Alikuwa akihema sana juu juu!

    “Seif? Seif mwana ulikuwa wapi wewe?”

    “Jof usiku sana sasa hivi hujalala tu na umetoka wapi mbona upo hivyo?”

    “Hapana Seif siwezi kulala mwana.Nikilala basi ujue Dar nzima hakuna kigodoro!! Nimekuja hii mara ya sita kukutafuta hapa getto. Kila nikija patupu!. Jiandae fasta fasta. Leo sasa ndio kuna mgodoro siyo kigodoro!!. Liko palee mitaa ya kina Zuena! twende zetu”

    “Jof? Jof?”

    “Nambie!!”

    “Wewe ni zaidi ya mshkaji. Kuanzia sasa sitaki kusikia mavigodoro yako, niache kama nilivyo na ukiendelea na vigodoro vyako, urafiki mimi na wewe basi kuanzia sasa. Nenda kwenye mavigodoro yako mimi niache!”

    “Seif yamekuwa hayo tena?, Hujajua tu wewe!! Kule nilipotoka kuna mijimama balaa,Hatariii!! halafu wanaume wachacheeee!”

    Hasira zilinipanda zaidi. Zilinipanda baada ya Jof kusema neno mijimama. Tayari roho yangu ilishawachukia. Niliunganisha picha kwa mijimama anayosema Jof na Jimama Mash. Jimama liongo kama nini!!. Kwa nguvu na hasira niliushika mkono mmoja wa Jof nakumuongoza mpaka mlangoni kwangu.

    “Nenda sitaki kukuona. Ukija hapa zungumza mambo mengine. Sitaki Sitaki Jof kwanini?”

    Jof aliondoka akiwa hajiamini amini. Akiwa anageuka nyuma asiamini kama ni Seif mimi ndiye niliyemfukuza. Nilirudi mpaka katika kakitanda changu nakuegemeza mwili ambapo usingizi mkali uliochanganyikana na mawazo ukanizoa. Tukazoana!!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ********





    Asubuhi kulipokucha nilichelewa kuamka sana. Uchovu ulikuwa ni mwingi sana mwilini na hata akili yangu ilionesha wazi kuchoka sana kwa misukosuko ya ndani ya muda mfupi. Si ushajua misukosuko gani?. Ya jimama Mash!!

    Kwakuwa sikuwa na akiba ya kutosha ya pesa nilihisi uko mbeleni naweza kufa njaa. Nikajiinua kitandani nakuanza kutengeneza kahawa kwani ratiba ya kuuza chai asubuhi na mchana niliiua kwa siku nzima. Nikaanza kuandaa birika kubwa kwa ajilli ya kuingia mitaani kuuza kahawa kuanzia saa kumi.

    Nilipomaliza kuandaa kahawa niliingia bafuni kuoga na punde nilipotoka kufika nje ya mlango wangu nilikutana na viatu vya kike vikinisubiri. Nikasita kwa sintofahamu kisha nikaingia moja kwa moja mpaka ndani. Mshtuko!!

    “Mash? Mash umefuata nini hapa?” Nilimuuliza kwa ukali.

    Alikuwa ni Mash yule yule aliyenitoa machozi jana yake usiku. Mash lile jimama langu. Jimama ambalo ni liongo kupindukia. Jimama lililotoa mwili wake mbele na nyuma kwa tamaa ya pesa. Sasa lilikuwa mbele ya macho yangu. Lilikuwa limejianika kwa kujilaza kwenye kitanda changu bila ya mantahofu!!

    “Seif mpenzi kumbe ulikuwa unaoga? na hata kama ungekuwa umeenda kazini uko mie ungenikuta tu kwani nilikuwa na ratiba ya kulala mchana kwako mpaka utakaporejea leo nipo off usiku siendi kazini kabisa mpaka kesho labda. Hapa unaponiona nimetoka kuwatumia wazazi wangu pesa pia nimekuletea juisi ya boksi mpenzi hiyo hapo. Leo nitakupikia, nitakufulia na chochote utakachotaka mie ni wako. Haya sogea hapa nikufute maji maji kwanza!!” Aliongea jimama Mash kwa kujiamini.

    Nilijihisi viungo vyangu vya mwili kukosa ushirikiano. Vilikataana kwa muda!! Upande mmoja vikalegea na upande mwingine vikakaza!! Niliyapikicha macho yangu mara mbili mbili kufumba na kufumbua labda huenda si Mash ni mzimu wake. Jibu lilikuwa hapana!! yule alikuwa Mash mwenyewe. Mash jimama. Mishipa ya hasira kichwani na shingoni ikanitutumka. Nikatamani kutoa machozi ya hasira. Nikashusha pumzi kwa haraka! nikamtolea macho!!

    “Mash mie na wewe tulishaachana toka jana usiku unanitaka nini?”

    “Unasemaje Seif?”

    “Mie na wewe basi. Jana umeniumiza vya kutosha Mash?”

    “Embu ongea ueleweke mwanaume wewe kwa kipi nikuumize mimi au nilivyotoka kwako asubuhi na mihasira yangu? anhhh mpenzi!! Yalishaisha yale toka jana asubuhi na ndio maana nimekuja hapa kwako nikupatie kile roho yako inapenda!!”

    “Nini unipatie? embu rudia tena??”

    “Jamani si mashine lako hilo nimelimiss, yaani hapa duniani hakunaga!!”

    “Na jimashine la jana usiku? lile hujalimiss siyo sio enhh?”

    “Seif nadhani ulikuwa ukiota wewe? Jana usiku? nini tena wakati tulionana asubuhi hapa kwako?”

    “Mash? Mash? Mash tena hunijui vizuri? Siku zote unanichukulia mimi zamwamwa siyo enhh?? Au kwakuwa nimetokea kijijijni ukaniona bonge la mshamba! la kudanganywa tu!! enhh? Jana usiku kwa macho yangu nimekushuhudia Buguruni ukijiuza”

    “Ndio kwani vipi si nilishakwambia kazi yangu ndio ile inayoendesha maisha yangu na ya wazazi wangu na watoto?”

    “Hapana Mash kwa kujiuza namna ile. Sawa nilikuvumilia uvaaji na kushikwa shikwa kwa matamanio. Haya na lile njemba? na kwanini uwe muongo kwangu Mash?”

    “Njemba? Embu biashara zangu usiingile Seif. Mbona mie sikuambii chochote kuhusu kuuzia kahawa mabinti wadogo na wengine wake za watu? Kwani mie sina wivu. Ile kwako ni kazi na kwangu pia ni kazi.”

    Mash alikuwa muongeaji sana. Muongeaji yule wa kizaramo ukichanganya na mngoni. Alijitetea sana. Kadri alivyokuwa akijitetea ndivyo alivyokuwa akinipandisha hasira zaidi. Akaniwahi!! siyo kwa kunipiga. Hapana!! akaniwahi kunishika kwa kunikumbatia. Akatoa taulo yangu iliokuwa na rangi tofauti tofauti kutokana na uchafu wa jasho na hata mabao mengine niliokuwa nikipigia pindi nipatapo hamu kitandani kwangu. Akalitupa lile taulo upande wa pili.

    Purukushani zikaanza!!

    “Mash sikuhitaji ondoka!!. Sina haja na limwili lako!!” Nilimtamkia maneno bila kusita.

    “Kama uliutaka nakuupenda toka kwenye vigodoro leo utautaka tena tu” Aliongea Mash.

    Haraka haraka akaupenyeza mkono wake kwenye kasuku wangu. Kasuku naye aliniunga mkono katika kuonesha mgomo. Mgomo wa kumchukia Mash. Hakusimama!! Mash akatoa dela lake aliokuwa amelivalia. Akabakiwa na michachandu yake kibao kiunoni. Akatoa na bikini yake akaitupa kule. Bado kasuku wangu akaendeleza mgomo na hata mie mwenyewe sikuonesha kufanya chochote zaidi ya kuishiwa nguvu nakumuangalia tu Mash.

    “Seif? Seif nataka mashine yako sasa hivi?”

    “Unamatatizo ya akili wewe?? Sio mzima? Usiku kutwa umelalia uko tena mashine zaidi ya kwangu unadhani sikuona? Kwa taarifa tu tulikuwa wote buguruni jana usiku na nilikuwepo dirishani nikiwachungulia na nimeona vyote mpaka ulivyompatia mwili wako lile njemba likufanye na nyuma. Unabisha? au nikutajie mpaka hela alizokuongeza?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mash alibaki kunyong’onyea mwili. Hakuamini kabisa kwa yale niliokuwa nikiyaongea. Ujanja wote kushnei!! Akalegea nakulegea!!. Akajitupa kitandani kwangu na lile limwili kisha akalegeza sauti na machozi yakimlenga lenga.

    “Seif nakupenda na nilishakwambia pale nipo kazini hata kama na wewe ungetaka nyuma ningekupa tu tena bure kwakuwa ni mpenzi wangu. nakupenda Seif moyo wangu upo kwako kwanini nikudanganye jamani.”

    “Sawa nashukuru kwa kunipenda na kunipa magonjwa. Na kwanini ulinidanganya kuwa hujawahi kwenda kavu kavu? na kwanini ulilipa lile njemba mbele na nyuma tena kavu?”

    “Seif? Seif niliona ungenikataa kwa siku moja endapo ningekwambia vile kuwa naendaga kavu wakati mwingine pesa inapokuwa kubw..

    Kabla Mash hajamaliza kuongea chochote pale pale akaanza kutapatapa. Mwili wote ukawa na mtetemo. Akatetemeka kwa muda mrefu. Hofu!!

    Nichukua lile taulo langu haraka haraka nakuanza kumpepelea japo apate hewa. Sikujua nini tatizo. Niliogopa sana. Kadri nilivyokuwa nikimpepea ndivyo na jasho lilivyokuwa likizidi kumtoka mwilini mwake. Likamchuruzika ,nakuchuruzika mithili ya maji ya chem. chem. yakifuata mkondo wake.

    “Mash? Mash?” Niliita kwa sauti.

    kimya. Mash hakuweza hata kutoa neno. Alikuwa kimya. Kimya mithili ya mtu aliyeaga dunia. Hofu ilioje!!

    Haraka haraka nikaanza kumvalisha lile dela lake aliokuwa nalo. Ushamba huu!! Dela nikaligeuza nje ndani ndani nje na hata nyuma mbele mbele nyuma.Nikasahau kumvalisha ile bikini yake. Ilikuwa mbali na macho yangu. Ikawa siri yangu!

    Niliona kama inanichelewesha. Nikapumua kwa muda.

    Wazo la ghafla likanijia kuwa nikumuwaisha hospital tu akapate matibabu. Kila nikitaka kumnyanyua nilishindwa nakudondoka mwenyewe.

    “Hapa ni kutafuta taksi tu” Nilijisemea mwenyewe baada ya kukaa muda nikitafakari jinsi ya kutoka na Mash. Niliwazia sana kupunguza mtaji wangu wa kahawa kwa kumpeleka Mash hospital. Wakati nikiwa na waza hili na lile mara pochi ikadondoka kutoka katika dela la Mash. Ilikuwa imekaa vibaya katika dela.Nikaiwahi kutaka kuirudishia. Wazo likanijia la kuisachi. Ilikuwa si haba!!

    Shilingi elfu 40 zilikuwa zikisimama ndani ya pochi ya Mash.

    Mtaji wa kahawa umepona!

    Sikutaka kupoteza muda. Nilitoka mbio mpaka eneo wanapopaki taksii. Nikachukua taksi nakugeuza mpaka kwangu ambapo tuliingia ndani nakusaidiana na dereva taksi katika kumpakiza Mash garini. Haraka haraka safari ya kuelekea hospitali ikaanza. Nilikaa siti ya nyuma. Kichwa cha Mash kikiwa katika mapaja yangu.

    Mwendo haukuwa mrefu sana mpaka kuifikia hospitali. Tulipokaribia tu kufika na hospitali Mash akaonekana kama kushtuka mwili wake. Akashtuka mithili ya mtu aliyetetemeshwa kwa shoti. Akatoa jicho moja kisha na jingine akaniangalia.

    “Seif mpenz? tunaenda wapi?”





    *********



    Kigugumizi cha muda kilinikamata. Nikakamatika!! Sikuwa na jibu la kumpatia Mash zaidi ya kumtolea macho kwa woga kisha nikaangalia siti ya mbele ambapo na dereva naye alikuwa amelisimamisha gari pembeni ya barabara baada ya kuisikia sauti ya mash. Naye alibaki akimuangalia Mash kwa jinsi alivyokuwa akiongea. Bumbuwazi!!

    “Mash? Mash?” Nilimwita.

    “Seif ujue sielewi tunaenda wapi?”

    “Ni story ndefu Mash ila nakuomba uniweke wazi! tena sasa hivi”

    “Nikuweke wazi kwa kipi tena Seif?”

    “Ulizimia Mash? Ulipoteza fahamu kwa kutetemeka mwili mzima na hapa tulikuwa tukikupeleka hospitali!”

    Mash alishtuka kama mtu aliyerushwa na ndege kutokea angani. Aliinuka katika mapaja yangu nakushikilia kifua chake kwa mikono yake miwili. Taharuki!!

    “Mimi? Mimi Seif nilizimia!! Anhh!! haaa!! haaa!! embu twendeni turudi nyumbani jamani”

    Nilijichekea kimoyo baada ya kuona tabasamu la Mash. Hakuonesha kuumwa kama nilivyodhania mwanzoni. Tulimuamuru dereva aturudishe nyumbani kisha tulipofika dereva nilimpa chake nakubaki na Mash nje ya getto langu.

    “Mash!”

    “Abee!!”

    Nakuomba kwa sasa uende tu nyumbani kwako mie najiandaa kwenda kuuza kahawa zangu. Nenda tu siku nyingine tutaonana sawa!” Nilimwambia Mash.

    Aliangua cheko kubwa.

    “Hujanijua tu Seif enhh?” Aliongea Mash.

    Hakuonesha dalili zozote za kusogeza mguu wake zaidi ya kuendelea kuniangalia. Akanishika mkono kwa nguvu nakuniongoza mpaka getto kwangu.

    “Mimi ndio Mash!! Seif!” Aliongea Mash kwa majigambo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sikutaka hata kumsikiliza safari hii nilimuona kama ananipotezea muda na biashara zangu. Nikamuacha akibung’aa. Nikachukuwa birika langu nakuelekea nje kwa ajili ya kuwekea moto tayari kwa safari. Kabla sijatoka nje na birika tu. Mash akaniwahi. Akanidaka tena mkono wangu. Akausogeza mdomo wake mpaka karibia na sikio langu.

    “Seif!! Nakupenda na..

    Kabla hajamaliza kuongea alichukuwa birika langu nakuliweka chini kisha akaichukuwa mikono yake nakuniwekea mabegani kwangu. Tukatazamana!!

    “Vyote vile nilivyokuwa nikikufanyia mpaka nimezimia ni ujanja wangu wakujua unanipenda kiasi gani Seif! Nimeamini unanipenda tena sana!! Na ile pesa shilingi elfu 40 nilikuletea wewe yote kwa sababu nakupenda Seif” Aliongea Mash.

    “Unasemaje Mash?”

    “Seif unanipenda na mimi nakupenda tena sana mpenzi wangu. Hakika wewe ndio chaguo langu maishani na nikwambie kitu Seif?”

    “Sitaki uniambie chochote ondoka!!”

    Nilimtoa mikono yake mabegani mwangu. Mash alikuwa zaidi ya kiroboto. Alikuwa king’ang’anizi khaswaa! alikuwa ni zaidi ya ruba!! hakutoa mikono yake. Kila nikiutoa mkono mmoja alikuwa akirudishia mwingine. Nilihangaika sana.

    “Seif narudia tena, sitochoka kukuimbia neno hili nakupenda na nataka tuishi wote pamoja kuanzia sasa. Nipo tayari uchukuwe vitu vyako vyote twende kwangu au tukatafute sehemu yoyote tuishi na wewe!” Aliongea Mash.

    Safari hii alikuwa yupo tofauti. Machozi yalianza kwa kumlenga lenga. Nilijikaza kiume kumkazia lakini udhaifu ukaanza kujipenyeza taratibu. Huruma ikanitawala!!

    “Nikwambie kitu kizuri Mash?”

    “Niambie niko tayari!”

    “Kama kweli unataka tuishi wote mie na wewe nakuomba sana, tena sana twende tukapime afya zetu na kama tuko sawa niko tayari kuishi na wewe!”

    “Unasema kweli Seif?”

    “Ndio!”

    “Lini tufanye hivyo?”

    “Hata kesho asubuhi ili niwahi kwenda kuuza kahawa jioni”

    Nilishtuka kumuona Mash akiwa na furaha zaidi. Furaha isiyo kifani. Hakuonesha hata kuogopa. Alinifanya namimi kupata ujasiri wa hali ya juu. Nikajihisi huenda sijaathirika kwa furaha alizokuwa akinionesha Mash. Nikamkumbatia kwa nguvu zote. Mwili ukanisisimka!!

    “Mash ila nataka tukaishi nyumbani na pia biashara zako za kujiuza achana nazo tutafute bishara nyingine ya mimi na wewe ya kutuingizia kipato”

    Maneno hayo yalimuingia sana Mash. Akakaa kimya kwa muda kisha akaniangalia kwa majonzi.

    “Ujue Seif, watu huwa wanatuchukulia tofauti sana sisi tunaojiuza na wengi hawajui nini haswa kinachotupelekea tukajiuza miili yetu.

    Kuna wengine ndugu zao wa kiume walikuwa wamewadhulumu mali za urithi walioachiwa na wazazi wao wakaingia katika kujiuza, wengine ni yatima walioondokewa na wazazi wao na kukosa mtu wa kuwaangalia! Wengine walikuwa wametupwa na wazazi wao baada ya kuzaliwa wengine… wengine!

    Ndio vitu vinavyopelekea sisi kujiuza japokuwa wengi sana huwa wanatudharau na hata wengine kufikia kutudhulumu nakuishia tukilala nao bure bila kutulipa”

    Alionge Mash kwa sauti ya kwikwi.

    “Sasa Mash nakuhusu kujikinga na ukimwi? mbona uliamua kwenda kavu jana?”

    “Seif natamani sana kama ungelikuwa ukinichungulia kila siku kazini. Ni mtu mmoja tu ambaye naendaga naye kavu na ni yule uliyomuona usiku. Nilishawahi kwenda naye kupima tukakutwa wote tukiwa safi na nilimkatalia kuishi naye kwakuwa alikuwa na mkewe japokuwa mkewe alikuwa ni mgumba, hawezi kuzaa ndio mana siku nyingine anakujaga kazini kule nampatia hata kavu kavu akiwa na pesa!!”

    “Na wenzako? kuhusu mimba na ukimwi wanajikingaje?” Nilianza kumdodosa lengo haswa ni kujua kama kweli kale kabinti ka jana usiku nilikapa mimba au la!

    “Huwa wote tunajikinga sana na wakati mwingine tukiwavalisha kondomu kabisa wateja wetu. Kuna wengine hata wanakunywaga dawa za kuzuia mimba”

    Niliishiwa nguvu kabisa. Nikakaa kitandani kwa maneno mazuri ya Mash. Nikajilaumu sana kumchukia Mash kwa muda. Kwa maneno yake hayo yakanifanya nisimtizame kwa jicho baya tena.

    “Seif mpenzi wangu niambie chochote sasa hivi unataka nini kutoka kwangu?”

    Maneno yale ndio kwanza kama yakamfufua kasuku wangu kuzimu. Kasuku akashtuka! akatamani kutoka nikambana kwa mapaja kama kawaida yangu.

    “Sitaki chochote kwa sasa” Nikamjibu Mash

    “Hapana Seif. Kuanzia sasa naacha biashara ya kujiuza na wewe nakuomba uachane na hiyo ya kahawa nataka tuanze maisha mapya na kazi mpya mimi na wewe. Kama pesa tayari nimeshapata za kutosha zipo kwenye akaunti yangu nyingine zipo tu ndani kama akiba. Tutafute biashara ya kufanya mpenzi wangu.”

    “Hapo umenena mpenzi wangu lakini uko tayari tukafanye biashara kijijini kwetu na siyo mjini?”

    “Kwa ajili yako Seif! na kwa kukuonesha nakujali na nakukuthamini mimi niko tayari unipeleke popote pale na nitaishi vizuri tu na wewe!”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Maneno yale yalizidi kuutamanisha moyo wangu. Moyo ukatoa bonge la tabasamu!! Nikahisi Mash ni chaguo langu nililoshushiwa na mwenyezi Mungu. Nikamvuta vizuri mpaka kitandani. Tukabiringita nakubiringita!! Mash akaanza kunivua nguo moja baada ya nyingine. Nami nikamtoa lile dela lake ambalo ndani yake hakukuwa na hata nguo ya ndani zaidi ya nanii yake kutuna tu!

    Kitendo cha kulitupia lile dela kwa pembeni tu karatasi nyeupe ilioonekana kama kufinyangwa ikaonekana ndogo. Nikaipuuzia nakuendelea kumtomasa Mash. Mash jimama langu. Nilianza kwa kumparua ile mishanga yake pembezoni mwa kiuno. Michirizi michirizi kiunoni na kwenye mapaja ilimuhamasisha zaidi kasuku wangu. Kasuku akataka, nikamnyima kwa muda uku nikiendelea kulilegeza jimama langu. Mash Hoi!! Chaliii!! akatanua mipaja yake meupe minene nakunisubiri nifanye yangu.

    Nilikaa kimya kw amuda fupi huku nikivuta picha zile sinema nilizokuwa nikiziangalia kwenye mabanda ya kuoneshea Video. Sinema ambazo zilikuwa zikionesha picha za X nyakati za usiku. Nikavuta taswira picha mojawapo niliokuwa nikiipenda sana haswa kwa jinsi mwanamke alivyokuwa akinyonywa mwili mzima, Nikaibia!!

    Mautundu yote ya kwenye ile sinema nikayaamishia kwa Mash. Nikaanza kwa kumnyonya likifua lake lote kuanzia mdomoni shingoni nakuingia kifuani ambapo niliyanyonya maziwa yote japo toka nizaliwe sikuwahi kunyonya maziwa ya msichana yoyote zaidi ya yale ya mama yangu mzazi tena nikiwa mchanga hata sijitambui. Nikaendelea kuyanyonya mpaka nikajing’ata mwenyewe kwa utamu. Sikujali damu za kujing’ata zilizoanza kutoka mdomoni kwangu kutokana na kuendelea kupata utamu wa kunyonya.

    Nikaanza kushuka kwenye kitovu cha jimama Mash. Mash akaonesha kulegea sana kwani ile mihemo ilibadilika kila nikimnyonya. Kichwa sasa kikawa kimefikia eneo ambalo kasuku wangu huwa analipenda sana. Nikajilamba vizuri damu zangu za ndani ya mdomo. Nikameza fundo la mate!! Nikaliangalia tena vizuri eneo ambalo lilinitesa sana kwa muda mrefu bila kulipata mpaka Mash alivyokuja kunionesha lipoje kwa mara ya kwanza kwenye kigodoro.

    Nikaanza kulichambua kwa kutumia ulimi wangu. Nikaanza kusindikizia na vidole vyangu taratibu. Mash akajitupa tupa. Akagala gala!! Akaweweseka!! Akashutu shutu!! Akakishika kichwa changu kwa nguvu sana. Akatamani kukiingiza chote. Nguvu za mikono yake zikamlegea. Akaniachia!!

    Nikaanza kumtoa kasuku wangu nakumsogeza mpaka eneo husika. Kasuku ambaye sikumvalisha hata kondomu. Kasuku akafurahi joto la Mash na unene wake wa mapaja yake. Kasuku akapenyeza na kutoka,. Nikampa raha zaidi kwa kuingia nakutoka mara kwa mara. Hatimaye nikamaliza cha kwanza. Ninapokwambia cha kwanza ni cha kwanza kweli haswa kwa sisi tuliotoka kijijini. Mash akalegea sana kwa kufumba macho na mapaja akiyaachia wazi. Nikatoka kifuani mwake nakukaa pembeni kujiandaa na cha pilli.

    “Mash nakupenda sana!” Nilijisemea kimoyomoyo uku nikimuangalia Mash kisha kasuku wangu. Jicho likaama sasa. Likaamia kwenye kile kikaratasi kilichokuwa chini. Kilichokuwa kikitokea katika dela la Mash. Nikasita kukichukua nikajigeuza kwa mara ya pili kwa ajili ya kuendelea kumlizisha Mash na kasuku wangu. Kabla sijaanza cha pili nikahisi kukosa amani. Furaha na mzuka vikanipotea ghafla!!

    Nikainama chini nakukichukua kile kikaratasi. Kilikuwa kimefungwa fungwa dawa ambazo sikuwahi kuziona maishani mwangu. Dawa za malaria na magonjwa madogo madogo zote nilizijua lakini kwa hili hata sikulijua, Kile kikaratasi kilikuwa na maneno ambayo sikuyaelewa kwa haraka. yalitaka nikae kwa muda kuweza kuyasoma.Nikaamua kuyasoma!





    Kwako,



    Seif..,



    Natumai ni mzima mpenzi wangu. Ninapokuambia mzima inamaana ni mzima wa afya. Pole kwanza na majukumu na kazi nzito ya kuuza kahawa pamoja na chai kutwa nzima. Najua umechoka sana! pole sana ndio maisha hayo!!



    Baada ya pole hiyo nianze kwa ufafanuzi kidogo. Nimeumia nakulia mwenyewe Seif toka alfajiri. Hivi unajua kati ya watu ambao wametembea na mimi ni wewe tu ndiye uliokaa moyoni mwangu tena kwa haraka sana? Nashindwa kuelewa kwa nini kama utakuwa umeniandea kwa waganga sawa lakini tambua kuwa najuta kwa wewe kukaa moyoni mwangu katika kipindi hiki kibaya sana kwangu.



    Seif, Ni miezi mitano sasa imepita toka niambiwe na madaktari kuwa ni muathirika wa ugonjwa huu mbaya wa ukimwi. Sikuamini mpaka nilipobadili hospitali zaidi ya tatu jibu likawa vile vile. Mimi Mash ni muathirika Seif hapa nilipo kila siku nina ratiba ya kwenda hospitali kwa ajili ya kuchukuwa madawa ya kuongeza uwezo wa kuishi.



    Jana usiku nilikuona sana ukiwa umechanganyikiwa nje ya dirisha la gesti. Nilikugundua tu pale nilipotoka na yule mwanaume ndani ya gesti na ndio mana ikanipelekea kuandika barua hii kwako utambue. Hivi wapi ulishawahi kuona mtu anayejiuza tena akupe mapenzi kwa mara ya kwanza tena kavu kavu na uwe salama?

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ukweli ni kwamba Seif wewe ni mtamu tena sana na ni bado kijana mdogo ila moyo wangu umenifanya nikuunganishe pamoja na wale wote niliokuwa nikijiuza kwao. Nimekuua Seif mimi mwenyewe tena kwa ugonjwa mbaya unaoogopewa na kila mtu duniani. Maumivu ya ndani kwa ndani kuanzia kwenye matiti yangu mpaka vipele vinavyoniwasha mara kwa mara katika sehemu zangu za siri uku vikitoa damu damu ya rangi nyeusi ni wazi nakaribia kufa mimi Mash.

    Najua ipo siku utakuwa kitandani hoi na utaikumbuka barua hii na utanikumbuka mimi kwa umbo langu zuri. Mahaba niliokupa na hata ukimwi niliokupa ipo siku utakumbuka.

    Ila Seif tambua kwamba wazazi wangu wote wawili walishafariki miaka zaidi ya kumi iliyopita kwa ajali ya treni. sina mtoto wala watoto na nasikitika nakaribia kufa nikiwa sina hata damu yangu duniani. Kama ningerudi kuwa mzima leo hii nikaambiwa nichague nipendacho dunia hii ningechagua kuzaa na wewe japo watoto wawili. Ningekuwa na furaha sana Seif. Si hata na wewe ungefurahia?



    Seif! Sasa nimekuwa mtu wa kutembea na madawa ya kuongeza siku za kuishi kila siku na kila mahali. Nateseka sana Seif. Na kuonesha kuwa nimeshaathirika tayari vidonda visivyopona na vinukavyo vimeanza kunitawala katika sehemu zangu za siri na hata ndani ya mdomo. Niandikapo barua hii nawashwa! nawasha sana Seif!! najua na wewe utakuja kuwashwa hivi siku moja. Tazama sasa Mash mimi leo hii nimekuwa marehemu ninayetembea kwa kuwaambukiza wengine.



    Nina mengi sana ya kuongea lakini naendelea kuumia zaidi Seif wangu.

    Niko tayari kuishi na wewe tukiwa wote tumeshaathirika na ningependa tufe wote siku moja ili tuweke historia dunia nzima itutambue.

    Pochi hii nilioificha humu ndani kwako ina shilingi elfu 40 chukuwa zote ni hesabu yangu ya siku ya jana na hata ukitaka hesabu zangu zote niko tayari kukupatia lakini si kuonana na wewe tena macho kwa macho. Pale tuliposex kwa mara ya kwanza unapozani ni kwangu sio kwangu. Ni danguro tu la kufanyia kazi zetu pindi wateja wakiwa wengi.

    Najua hapo ulipo unahasira kali sana Seif. Siwezi kujionesha tena kwako!! Ila nitatumia kila njia kuweza kukufikishia pesa za kukusogeza maisha kama mimi popote pale. Cha msingi katafute dawa na kubaliana na ushauri wa madaktari.





    Wako umpendaye,



    Mashaalah au Mash!





    **********



    Hasira kali zilinishika. Nilihisi huenda ni ndoto pengine nitaamka itakuwa siyo kitu kwangu lakini jibu lilibaki pale pale hapana!! Haikuwa ndoto zaidi ya ukweli mtupu.

    Niliishika ile karatasi kwa hasira na nguvu zote. Kwa machungu yote!! Nikayafumba macho kwa nguvu sana!! Yakafumbata!!

    Laiti ile karatasi ingekuwa hata ni tofali nadhani lingemung’unyika madonge donge kwa jinsi nilivyoishika.

    Nikaifinyanga kama ilivyo nakuitupia chini ya uvungu kisha nikayarudisha macho yangu kwa Mash aliyekuwepo bado yupo kitandani hoi akisubiria cha pili kutoka kwangu.

    “Seif mpenzi vipi tena? Tuendelee jamani!!” Aliongea Mash.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ni kama alizidi kunipandisha mashetani. Ninapokuambia mashetani siyo ya kutisha la hasha mashetani yaani zaidi ya hasira za mtu mwenye kichaa. Nilimuinamia Mash nakujifanya kama namshika shika sehemu zake za siri kwa kutumia mikono. Kisha nikajifanya kama mdomo ukisogelea eneo hilo. Mash hakuwa akijua dhamira yangu ni nini. Alichokijua nikuwa nataka kumlamba lamba kama hapo awali. Lengo langu kuu likiwa ni kulinganisha maneno ya kwenye kile kikaratasi na mwili wa Mash. Maneno kama aliyoandika Mash katika ile barua juu ya kuwa na vidonda vinavyomuwasha.

    Mwanga hafifu kutoka katika upande wa dirisha langu moja niliokuwa nimelirudishia ulinisaidia tosha kumuangalia Mash maupele yake.

    Maskini Seif mimi!! Mash alikuwa ameharibika vibaya vibaya. Vidonda donda sugu vya rangi tofauti vilikuwa vimemtanda na vingine vikionesha wazi kutumbuka.

    Nikapiga moyo konde! Ama kweli majuto ni mjukuu!!

    Nikajiona mpumbavu. Mpumbavu kwa kunyonya mara ya kwanza bila kuangalia vizuri. Nikahisi kutapika!!

    Nikasogeza mkono katika ile sehemu. Kitendo cha kugusa tu vile vidonda vikawa vikitumbuka vyenyewe kwa vyenyewe. Nikageuzia macho yangu katika sehemu zangu za siri kujiangalia kwa mara nyingine. Eneo langu lote lililokuwa likizunguka sehemu za siri nalo lilikuwa limetapakaa damu za rangi rangi kijani si kijani na hata nyeusi si nyeusi. Zilikuwa nzito zenye kuganda katika mwili wangu. Niliumia sana!! Nikajikaza kisabuni!! Mash akainuka nakukaa vizuri.

    “Seif jamani tuendelee au ninyonye basi nipate raha mwenzako!!” Aliongea Mash.

    Hapo ikawa kama amenipa fikra tofauti. Ukali!!

    Nikajihisi meno yangu yamekuwa kama ya wale wanaowaita ma ‘vimpare’ au mazombi. Nikatamani nimararue rarue vipande. Nguvu zikataka kunilegea nikajikaza tena kiume nakuinuka.

    “Mash? Mash?”

    “Nini Seif? vipi mbona huendelei?”

    “Hapana Mash inatosha, nasema inatosha Mash!!”

    “Jamani Seif mwenzako bado nataka Mashine yako nimeimiss jamani tuendelee cha pili wala mwenzako bado sijaridhika”

    “Hivi wewe Mash? Embu kwanza inuka! inuka? Inuka nimesema” Nilimbadilikia ghafla. Mash akainuka na sintofahamu!! Kimuhemuhe!!

    “Seif nini?”

    “Wewe Mash wa kuniua mimi? na bado unataka kuendelea kunididimiza kabisa ennhh?”

    “Seif embu kuwa muwazi nini kimekupata kwani au cha kwanza sikukuridhisha? Niambie cha pili nikupe chenyewe? Au ndio unataka na nyuma kama yule jamaa wa usiku?”

    Maneno yale ni kama yalikuwa yakiuchochoea ubongo wangu ulazimishane na akili pia mwili ufanye kazi yake kutenda. Niliuvuta mkono wangu kwa nguvu nakumpatia bonge la bao Mash. Bao la haja!! Mash akaweweseka nakulala kitandani akiziba uso wake.

    “Seif nimekufanya nini mpenzi? Kwanini unaanza kunitesa? Nimekukosea nini niambie nijirekebishe, niambie seif?”

    “Pumbavu mkubwa wewe? Unajifanya hujui chochote siyo? Haya jichungulie uchi wako ujiione, jichungulie ulivyo?” Niliongea kwa Jazba.

    Mash akawa analia kwa kwikwi. akainuka tena kitandani nakkukaa vizuri. Akajiangalia katika eneo lake la sehemu za siri kisha akanigeukia.

    “Seif? Seif kwani kuna nini? Mbona sioni kitu? Umenifanya nini kwani?”

    “Mash umetumwa enhh? Haya si ndio ulivyotaka kuniachia ukimwi..

    “Ukimwiiiii?” Alishtuka Mash

    “Ndio na hapa leo hutoki? nimesema mguu mmoja mimi na wewe mpaka hospitali?”

    “Seif si nilishakwambia mimi sina wasiwasi na nipo tayari kwenda kupima na wewe na ndio malengo yangu ili niishi na wewe vizuri tuzae watoto” Aliongea Mash kwa kujiamini.

    Nilichukua kopo la kuogea na maji kidogo kisha nikaelekea bafuni nakuhakikisha Mash nimemfungia tena kwa ufunguo chumbani kwangu. Nikajisafisha zile damu damu zake zilizokuwa zimegandia katika mwili wangu kuzunguka eneo la sehemu za siri. Nikatoka nakuelekea chumbani ambapo nilimkuta Mash akiwa ameshamaliza kuvaa dela lake.

    “Hilo libikini lako unamuachia nani hapo chini? Chukua uvae sasa hivi?”

    “Seif? haya nachukua!” Aliongea Mash kwa unyenyekevu.

    Hakuwa Mash yule wa papara. Mash yule wa kujisikia!! Mash wa kuropoka chochote mbele yangu. Alinitii!! Alikuwa mpole sana baada ya kumuonesha hasira kidogo. Nilivaa nguo haraka haraka nakuelekea mpaka hospitali na Mash.





    *******



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mkono wangu mmoja ulikuwa na nguvu ya ziada. Nguvu ya kuweza kuung’ang’ania mkono wa Mash vilivyo usiniache. Baada ya kutoka tu nje ya getto kwangu Mash alionesha kuwa mbishi kidogo japo baadaye sana alikubaliana na mimi tukatoka nakuanza safari ya kuelekea hospitali.

    Wenge!! Nilitamani hata kupaa kuweza tu kufika hospitalini ili kujua afya yangu. Nilikuwa kama mtu aliyekuwa katika njia panda asielewe njia gani sahihi kwake kwenda. Baada ya ka mwendo Mash alionesha kuchoka.

    “Seif, Seif?” Aliniita Mash.

    “Unasemaje?”

    “Zahanati nzuri ni ile ya kule kwa Dokta Nyange twende hiyo ya hapo Tabata shule inakuwaga na foleni sana?”

    “Unasemaje wewe?”

    “Hiyo ya Tabata shule mpenzi inakuwaga na foleni sana na pia sijui hata kama wanapimaga ukimwi!!”

    “Mimi ndio nataka hiyo hiyo foleni kwani lengo letu ni kujua afya zetu na hata foleni ingekuwa kesho si uliniambia leo huendi kazini siyo?”

    “Ndio”

    Mash alianza kama kuonesha woga fulani tulipokaribiana na hospitali ya Tabata. Woga wake ulizidi kunipa hasira sana. Akagoma kuingia hospitali ya Tabata shule. Sikuona aibu ya watu kutuangalia kwa kuvutana. Nilimvuta sasa kiwazi wazi na si kwa kujificha tena.

    “Seif niache, Niache niende mwenyewe nimesema?” Aling’aka Mash

    Alikuwa ameshachukizwa na kitendo cha mimi kumvuta kwa nguvu mbele ya umati wa wapita njia.

    “Kama uko kupima tunaperekeshana hivi nenda mwenyewe!! kwanza kupima ni hiari ya mtu. Kwanini utumie nguvu kunivuta hivyo? Nimekuvumilia kote huko kunishika mkono toka tupo kwako sawa ila kukwambia tubadilishe hospitali wewe ndio uning’ang’anize? enhh? Sasa mimi huwa naendaga zahanati ya kwa Nyange mtaa wa tatu kulee na kule kuna huduma zote tena haraka haraka. Twende kama hutaki niache nirudi zangu nyumbani usinilazimishe”

    “Unasemaje Mash?”

    “Kama nilivyosema kama hukunisikia niache nirudi zangu kwangu!”

    Sikutaka tena kumvumilia Mash. Mash alizidi kunitia hasira zaidi na zaidi. Aliuchoma sana moyo wangu kwa kisu kikali. Moyo ambao ulikuwa umeshajua kila kitu kumuhusu yeye. Umeshajua tabia zake na ugonjwa aliokuwa nao kupitia barua. Aliuchakaza na kuniachia maumivu makali. Nilimuachia mkono nakuushika moyo wangu uliokuwa kama umeingiwa na ubarafu mkali. Machozi ya hasira yakapenya katika mashavu yangu nakudondoka. Makamasi nayo yakaomba njia kutoka. Yakatambaa!!

    “Mash? Mash kwanini unanitenda hivi? Kwanini umeniua kiumbe mimi ninayetegemewa nyumbani na wazazi? Kiumbe mie nisiye na hatia? kwanini?” Nilianza kuropoka maneno ya uchungu kwa Mash. Maneno ambayo kwa namna moja ama nyingine yalianza kumuingia Mash. Mash akanisogelea kwa aibu nakuanza kunifuta machozi kwa kutumia dela lake. Alishajua fika nimeshajua kama ameathirika japokuwa hakuniona nikiisoma ile barua yake. Kila akinifuta machozi ndio kwanza chemchem ya kubwa ya machozi ilikuwa ikiomba njia zaidi. Umati!!

    Wapita njia wakaanza kuweka wingi taratibu.Wakaanza kufurika na kufurika kuangalia kitu gani kinaendelea kati yangu mie na Mash. Kwa aibu tulishikana mikono na Mash nakuondoka. Ule umati nao ukatawanyika japo kuna baadhi walikuwa kwa nyuma wakitufuata, Huenda walituona kama tukiigiza movie kama zile za kina JB ama kutalakiana.





    **********



    Mpaka tunaingia katika Zahanati ya kwa Nyange maeneo ya Tabata shule bado machozi yangu yalikuwa yakinibubujika. Yakinibubujika kwa uchungu. Uchungu wa kulia ulikuwa bado umeng’ang’ana katika mwili wangu. Mwili uliokuwa hauna hatia. Uliojiingiza katika raha na mateso kwa wiki moja. Kila nikivuta ile taswira juu ya ile barua nakumuangalia Mash ndio kwanza nilikuwa nikipata chuki dhidi yake. Nikaapa kumwambia yote juu ya barua baada ya kupewa majibu kwa daktari. Nikaapa hata kumwambia dokta juu ya barua aliyoniandikia Mash nijue atanishauri vipi. Nikaapa kukubali ushauri wowote atakaotoa dokta juu yangu.

    “Tuwasaidie nini?” Aliongea mmoja kati ya manesi wa Zahanati ya Nyange.

    “Tupo hapa kwa ajili ya kuchukuwa vipimo. Tunataka kujua afya zetu!” Nikaropoka.

    “Vipimo gani?” Aliuliza yule Nesi.

    “Ukimwi”

    “Mmeshaandikisha majina yenu hapo?”

    “Bado” Aliropoka Mash.

    “Kabla ya hapo andikisheni majina yenu hapo meza kuu. Kuna chumba cha ushauri kile pale!! Hapo mtaelekezwa jinsi ya kukabiliana na ugonjwa huu wa ukimwi kabla ya vipimo endapo utakutwa nao ni njia gani zifuatwe na endapo utakuwa hauna pia ni njia gani zifuatwe.Halafu baada ya hapo mtaingia mmoja mmoja kwa ajili ya kuchukuliwa damu. Ingieni kwenye chumba hapo msubiri kupewa ushauri kabla ya vipimo”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tulikubaliana kabisa na maneno ya yule nesi. Tukajisogeza na Mash mpaka eneo lililokuwa na kumbi ndogo na televisheni. Tukakaa huku tukisubiri kitakachoendelea. Muda wote huo Mash hakuongea neno lolote zaidi ya kuniangalia tu usoni mara kwa mara nakukaa kimya.

    “Seif?” Aliita Mash baada ya kukaa kimya kwa muda.

    “Unasemaje?”

    “Nakuomba niende chooni mara moja kwani sijisikii raha. Sina amani mkojo umenibana sana pia nahisi kuumia kwani nawashwa sana katika sehemu zangu za…



    **************



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog