Search This Blog

Monday, October 24, 2022

ASIA DIGITALI - 1

 



    IMEANDIKWA NA : GEORGE IRON MOSENYA





    *********************************************************************************



    Chombezo : Asia Digitali

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Joto lililokuwa katika chumba kikubwa cha ‘internet café’ liliwafanya wateja wajipepee kwa kutumia makablasha kadhaa waliyoingia nayo ama kuyakuta katika chumba kile.Joto lile lilikuwa kero kwa kila mteja mle ndani, lakini kwa mtu mmoja tu n’do lilikuwa sherehe.Alikuwa ameyaona mawindo sahihi kabisa.Mawindo ambayo yangepewa ushirikiano mkubwa na lile joto.



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mkabala na mahali alipokuwa amekaa alitazamana na kijana wa makamo ambaye afya na mavazi yake pekee yaliidhinisha uwezo wa yeye kuwa ameegesha gari nzuri nje ya jingo lile na mfukoni hakukosa noti kadhaa zenye uzito wa kuitwa pesa. Jasho lilikuwa likimtiririka na alikuwa amejikita katika kujipangusa kwa kutumia leso yake.

     
    Kabla umeme haujakatika kijana huyu alifanya siri na kuchungulia mapaja meupe ya binti huyu ambaye hakuteswa na joto lile bali ilikuwa sherehe. Wakati kijana huyu akidhani kuwa alichofanya kilikuwa siri sana…jicho kali na la kitapeli la binti yule liliweza kushuhudia matamanio ya kijana yule.





    Sasa umeme ulikuwa umekatika, joto limetawala binti akaamua kuitumia nafasi.

    “Atanijua mimi nd’o Asia.” Alijisemea wakati akifungua baadhi ya vishikizo vya blauzi yake. Alifanya hivi huku akkizuga kuwa anateswa sana na lile joto.Maziwa yake ambayo pia yalikuwa meupe pee yalionyesha mchirizi ambao asilimia kubwa ya wanaume wakiutazama hutamani kuona na kinachoendelea chini.





    Asia hakuachia uhondo wote, alimuacha yule kijana katika mtihani wa matamanio.Kwa jicho lililofuzu kulaghai wanaume aliweza kuiona suruali ya kitambaa ya yule kijana ikitoka katika kutepeta na kukakamaa.Akafanya tabasamu la kusanifu, akijifanya anaitazama simu yake.Kijana wa watu hakujua kama anachezewa akili.“Kashajileta pumbavu zake.” Aliendelea kufanya tathmini.





    Mara akaitupa karata ya mauaji ambayo aliamini kwa namna yoyote lazima yule mwanaume atajiingiza katika himaya yake.Asia kwa kutumia vidole vyake vyenye kucha bandia alibofya simu yake iliyokuwa katika mkoba.Ikaanza kuita akaichomoa. “Hellow……..mwenzangu….yaani najaribu kucheki Bro Smith, Skype umeme nao huko umekatika, nimemcheki kwenye simu, dah network ya Germany sijui vipi. Mbona yamenishuka mwenzako.” Asia aliongea kwa sauti nyororo inayobembeleza na bila shaka ilikuwa inatangaza maisha bora anayoishi kwani alikuwa katika kudeka.

     
    Kimya kikatanda kama anayesikilizia kitu fulani kutoka upande wa pili. Kisha akafanya cheko, cheko lililoyaruhusu maziwa yake kifuani kucheza kidogo, akafanya kuiegemea simu akayarekebisha. Jicho lake kama kawaida likamchungulia muhusika wake.
    Muhusika alikuwa amesahau kujipepea, alikuwa anatokwa jasho na alikuwa katika kushangaa.“Mi nataka kuondoka hapa, maana hakuna jipya, ..” akaweka kimya tena. Kisha akaendelea.“Naenda Msasani sahivi, lakini shoga mwenzio si unicheke kabisa mapema….sina gari hapa najishaua tu….maza kaenda nalo Mwanza, na mimi kuendesha ka Lexus kake sitaki.”Akaweka nukta tena.





    “Mh…atoke wapi wa kunichukua wewe……naenda zangu kupanda daladala mie. Nitafanyaje sasa………baadaye basi Shosti.” Alimaliza maongezi akaufunga mkoba wake baada ya kuwa ameweka simu ndani yake.





    Akasimama, akapiga hatua kadhaa, taratibu huku akiruhusu nyamanyama zilizovimbiana kwa nyuma na kumfanya apendeze zikitikisika kwa fujo. Yote haya yalitokea ili fulani aweze kuona.Macho hayana pazia, mikono ikamwenda kinywani, akakunja kunja sharubu zake, kisha mkono mmoja ukamponyoka na kuifikia suruali yake, akauingiza ndani na kusawazisha mambo.Macho ya Asia hayakukosea kumsoma, alikuwa ametamanika.



    Kijana akasimama, akajifanya kunung’unika kutokana na huduma mbovu walizopata, hakukumbuka kudai pesa zake.Akapiga hatua kubwa akamfikia Asia.“Vipi dada na wewe wamekuchosha nini? Watu gani hawa yaani umeme umekatika hawawashi jenereta. Aaaargh.” Alilalamika.Asia akajichekesha kisha akasonya.“It’s boring…..yaani dah basi tu….but it sucks….” Akatema maneno, Kiswahili kwa mbali ung’eng’e mwingi.





    Wakaendelea na mada ya kuwalalamikia watoa huduma hizo. Hadi wakaufikia ukumbi ule wa kuoneshana nani ni nani.Ilikuwa sehemu ya kuegeshea magari.“Kwani dada unaelekea wapi.” Kijana ambaye alikuwa hajajitambulisha jina akauliza.“Msasani, ngoja nikapate kero nyingine ya kugombania magari. We unaenda pande zipi au safari yetu moja?” aliuliza Asia huku akijua nini kinafuata.





    “Mimi nafika Namanga hapo. Kuna watu naenda kuonana nao hivi mara moja. Dah hizi kazi hizi.” Alilalamika katika namna ya kujifagilia njia.“Poa kumbe gari moja twende ukanisaidie kuwania siti.”

     
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Jamaa kusikia vile akajikoholesha kisha akamwonyesha Asia kwa kutumia kidole cha shahada, gari aina ya Noah nyeupe ikiwa imetulia ikimsubiri mmiliki. “Mwenzangu heri yako…poa kaka siku nyingine lakini hapa sirudi tena aisee.” Alisema Asia huku akiondoka.“Twende nikusindikize kidogo bwana..” alisihi yule kijana.

     
    Asia akajifanya kufikiri kidogo kisha akauliza swali la kijinga.“Hamna mahali unapita maana mimi nina haraka kweli.”“Naenda moja kwa moja.”Asia akakubali, wakaongozana garini.Safari ya kuelekea Msasani.

     
    Ndani ya gari maongezi ya hapa na pale yaliendelea….Asia kwa kutumia simu yake akafanya jambo jingine lililompelekea kujikuta anahamishiwa rasmi katika timu nzima ya digitali.Akaandika ujumbe baada ya dakika moja simu yake ikaita.





    “Mh…sorry..simu yangu inatatizo la speaker I hope sitakuboa nikitumia loud.” Asia alisema huku akiyafinya macho yake katika namba ya kumhangaisha mwanaume dhaifu. “Aaah…hata usijali ongea tu….” Alijibu.Asia akapokea simu akaiweka katika spika kubwa.“Ehe nambie….” Akaanzisha maongezi. “Peter kanipigia mwenzangu…..”“Anataka nini?”

    “Asia jamani…msamehe mwenzako …..kabembeleza sana ujue….” Sauti kutoka upande wa pili ikasihi.”





    “Jackline, nakuheshimu sana…nakuomba kwa heshima ya urafiki wetu…usinambie lolote kuhusu huyo tapeli wa mapenzi, Jack umekuwa shahidi wa ujinga alionifanyia Peter….umeshuhudia uchafu wake wote…leo hii unamwombea msamaha…Jack kweli umenichoka kiasi hicho, amekulipa huyo Peter umwombee msamaha……ok Jack labda niseme neno moja tu….ulifurahia alichonifanyia sivyo…..Mbarikiwe sana “ Akamaliza huku analia, akaikata simu, uso ukiwa mwekundu, ngozi yake ya rangi ya chungwa ikikosa ustahimilivu na kuchafuliwa na machozi…kilikuwa kilio haswa. Asia alikuwa analia.





    Kijana aliyekuwa anaendesha gari ambaye mwanzoni alikuwa amemtamani Asia alijikuta akipagawa, mara akaiegesha gari pembeni.Vioo vyeusi tii…nani atajua kinachoendelea ndani. Nd’o uzuri wa tinted Akaanza kumbembeleza Asia. Akamsihi sana asilie, Asia akawa analia huku anawalaani wanaume wote. Alimlaani Peter hadi yule kijana naye akamsaidia katika kumlaani.





    “Mpendwe vipi nyie wanaume …mnataka roho zetu…mnataka tufe nd’o mjue kuwa mlipendwa au? Yaani mtalaaniwa nasema atalaaniwa huyo Peter, kwa chozi hili linalonitoka mimi Asia…Peter alitaka nini mimi nikamnyima, pesa zangu za kutumia chuo, pesa za kujaza gari mafuta zote nimempa mimi. Alitaka nini sasa, nimepigwa na dadiii mimi mamii akanichukia, kaka zangu wamenipiga makofi mimi. Kisa Peter, Peter….aah…” Asia aliendelea kulaani maneno yaliyomsulubu yule kijana.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Akiwa hajui cha kufanya Asia akiwa analia alimlalia, alimlalia kifuani, zile chuchu alizoziona kwa kuibia kule ‘internet café’ sasa zilikuwa zimemlalia zikimchoma katika namna ya kuleta hamasa, kucha za bandia za Asia zikalifinyafinya shingo lenye afya la yule kijana.





    Pumzi za kupishana ndani na nje zikawa zinatesa katika sikio la yule kijana. Sasa alianza kupagawa. Huyu Asia alikuwa anajibembeleza ama.Akawa katika sintofahamu. Nani atampa jibu?Asia akalisikia paja lake likiguswa na kitu ambacho hakikuwepo hapo awali. Hakushtuka Akafanya tabasamu jepesi kisha akamzomea yule jamaa.Hicho kitu kilivimba kutoka katika suruali nyepesi.





    “Bwege linawahi kweli kupata hamu hili.” Asia alikebehi kimya kimya.Hamu zikamzidi yule kijana, mara naye akakumbatia, mara akakumbatia kwa nguvu zaidi. Mara akaanza kunena katika lugha za maajabu zisizojulikana kitaifa wala kimataifa.





    Mikono yake ilikuwa ikitalii katika mzigo wa titi mbili ndogo za Asia.Afadhali yeye alikuwa ananena kilugha.Asia alikuwa hoi kama aliyezirai.Jamaa akajua kuwa Asia kakolea.Laiti kama angejua kuwa Asia anatumia mbinu ya kidigitali, basi ni heri angebaki katika dunia ya analojia aliyokuwa anaishi awali.





    “Baby…..Baby…..unaniua mweenzio….unaniaaa…..pliiz stop…..” “Am sore bebi…am sore vere sore….me you know…” Jamaa akajaribu kiingereza asichokijua, Asia akataka kupitiwa na kicheko.Akajikaza. Alikuwa kazini.





    Mkono wa jamaa ukapenya katika mapaja…..Asia akajua jamaa anataka kumpima kina cha kisima na kutazama kama kina maji ama ni kikavu.“Bwege asije akanichafua bure..akavuka mipaka…..”Asia digitali akacheza kidigitali, alishagundua kuwa jamaa ni mwepesi sana.





    Ulimi mkali kama ule wa kinyonga, ulimi ambao ulishausema uongo hadi uongo ukauzoea ukazama katika sikio la yule jamaa.“Uwiiiiiii….ooooohhh yeees..” jamaa akaganda kama roboti, mkono haukwenda mbele wala kurudi nyuma.Akazidi kunena kwa lugha zake zisizokuwa za kiroho.Asia akagundua kuwa amefanikiwa kwa kiasi kikubwa.Akafanya tekniki ya mwisho.Akajibandua katika mwili wa jamaa….akaanza kujifuta midomo, na kujifanya anaona aibu……jamaa kaduwaa tu hajui digitali inakwenda vipi. Analojia ilikuwa imemwathiri.

     
    Jamaa akawa na aibu za kweli, suruali ilikuwa wima sana. Akajitazama, shughuli ikaja je airekebishe ama aicha ilivyo………

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Yaani sijui tu what to say…but siwezi kujicontrol mwenzio” Asia alivunja kimya, huku akionekana dhahiri kuwa tayari amekolea. Alijifanya haioni ile suruali.

    “Sasa tunafanyaje jamani?” aliuliza kibwege yule mwanaume.

    “Mi siwezi yaani sijui tu unanisaidiaje……” alizidi kulalamika.

    Mwanaume akawasha gari, akaiondoa kwa mwendo wa kawaida.

    Akafika Kinondoni, Chichi Hotel.

    Hapo hakuna aliyekuwa anakumbuka kuwa alisema anaenda Msasani wala namanga.

    Asia alikuwa anaifahamu fika ile hoteli lakini akazuga kuuliza.

    “Vipi hapa nd’o kwenu?”

    “Hapana hii ni hoteli baby wangu. Vipi tunaweza kuingia.”

    “Yaani dah..sawa tu kwa kuwa siwezi kujicontrol. Lakini hapa hapana my dear…pako wazi sana siwezi” Alilalamika kinafiki.

    “Sasa twende wapi jamani.”

    “Popote hata Magomeni lakini hapa hapana, hizi hoteli kubwa kubwa Dady anawewza kunifumania.” Alidanganya. Uongo ukakubaliwa.

    Gari ikageuza kurudi magomeni.

    Baada ya dakika kadhaa walikuwa katika chumba katika nyumba ya kulala wageni ya bei ya kawaida. Asia alikuwa ana maana kubwa ya kuchagua sehemu kama ile.

    “Baby kwani unaitwa nani?”

    “Mimi naitwa Jumanne, niite J fo na Juma tu inatosha.”

    “Ooh J fo nd’o zuri zaidi.”

    Walipotulia kidogo Asia alichukua simu yake, kama kawaida alituma ujumbe kwa umakini mkubwa.

    Kisha vikafuata vitendo.

    Jumanne akiwa anaona aibu bado, mara Asia akamrukia akamfungua kishikizo kimoja, mkono mwingine ukalifikia sikio, kidole cha kati kikapenya katia sikio la kuume, mapigo ya moyo ya Jumanne yakaongezeka mwendo, shati likatoka, mara mkono laini wa Asia ukapenya katika suruali ya Juma, akaanza kujichekesha.

    Asia akaongeza utundu, mara anapapasa huku mara kule.

    Jumanne hoi.

    Hatimaye Juma akawa laini kabisa, akapaparika akamminya Asia chuchu yake ngumu, Asia akatokwa na mlio wa ajabu wa kimahaba, Juma akapagawa zaidi.

    Asia akajiviringisha mithili ya samaki nguva, kinguo chake kifupi kikapanda juu kidogo.

    Shanga kadhaa katika kiuno chake.

    Kama shambulizi basi hili lilikuwa la kimataifa.

    Juma likuwa mlevi katika jambo hili.

    Juma na shanga?? Hakuambiwa kitu na mtu.

    Akamrukia Asia, akakirushia mbali kigauni chake.

    Juma ana kwa ana na bikini nyeupe, jicho la Asia likiwa katika mlegeo wa ajabu kama linalotaka kufumba.

    “Juma mi natakaaa.” Akalia Asia.

    Juma akatoa kibukta kilichobaki mwilini.

    Kama Juma alidhani ni ujanja kwa mwanaume kutangulia kuvua nguo, basi huo ni ujinga katika mfumo wa digitali aliokuwa anautumia Asia, labda kwa wana analojia wenzake huo nd’o ulikuwa ujanja.

    Asia akamtazama Juma anavyokuja kwa kasi, akamuwahi palepale kabla hajakifikia kitanda, akamwangusha chini, mkono mmoja ukaifikia himaya ulimi ukazama sikioni……

    Juma akalegea kama mlenda Asia akaligundua hilo.

    Mdigitali akafumbua macho akakutana na kitu alichokuwa anakisaka kuanzia ‘internet café’.

    Funguo. Zilikuwa funguo mchanganyiko.

    Asia akamgalagaza Juma, hatimaye wakaifikia ile meza mbovu iliyokuwa chumbani.

    Meza ikapinduliwa na Asia huku akilia kimahaba.

    Funguo zikamwagika chini.

    Juma hakujua lolote, mkono wa Asia ulikuwa unamsulubisha.

    Sasa kikafuata kitendo cha maajabu kikiwa katika mfumo wa Digitali.

    Asia akamruhusu yule jamaa kumwingia sasa.

    Lengo likiwa safari ya maajabu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Jumanne akafika kwa kasi zote, akatulizwa kidogo kisha akaruhusiwa.

    Kwa papara akaleta staili ya kibaba na mama.

    Asia digitali sio mjinga, yaani umweke kibaba na mama ili umwangalie usoni anavyofanya maigizo? Hata haiwezekani.

    Lakini cha ajabu alikibali bila kinyongo.

    Akalala chali, bwana mapapara akamvamia.

    Vigaye vikampa raha Asia, kila mara jamaa alivyomsogelea kwa fujo naye alizidi kusogea nyuma. Si kwamba mikito ilikuw a inamzidia Asia alikuwa anafanya jambo ambalo kwa kuhadithiwa tu huwezi kuelewa we muanalojia unatakiwa ufanyiwe uumbuke nd’o utajua.

    Wakati Asia akifanya yake pale chumbani, nje ya chumba mwanadada Janeth ama kwa jina la kazi ‘profesa maji ya shingo’ alikuwa bize akijipitisha hapa na pale akijifanya kuna jambo anatafuta.

    Uzuri wa gesti za hadhi ya kawaida hakuna wa kukuuliza.

    Kilio feki cha Asia kilimpa amani moyoni kwani ule muda ulikuwa umewadia.

    Akajiweka mbali akawa anahesabu dakika.

    “Kwa ninavyomjua Asia hapo ni viuno sita tu mambo tayari.” Janeth alijisemea huku akisoma ramani.

    Mara akausikia mlango wa chumba cha Asia ukiguswaguswa.

    “Tayari mambo...” Jameth alijisemea, akaiweka simu yake mfukoni.

    Akatembea upesi upesi akaufikia mlango wa Asia akainama, akatoka na kitu.

    Laity kama ungebahatika kumuona wala usingeweza kudhani kuwa alikuwa amechukua funguo tayari. Funguo ambayo ilikuwa inasukumwa na mgongo wa Asia kila ambapo Juma alikuwa anakipampu.

    Juma alikuwa katika dunia ya analojia, wenzake walikuwa kazini kidigitali.

    Baada ya dakika kadhaa mwanadada Janeth akiwa katika mataa ya magomeni alikuwa anatafuta mahali pa kuwashia redio ndani ya gari la Juma, ajiliwaze huku akiyangoja mataa yaweze kumruhusu ajiondokee zake na kwenda anapojua mwenyewe. Leseni ilimruhusu kujitapa kwa raha zake.

    Wakati Janeth akiwa anakula kiyoyozi. Asia alikuwa analia, alikuwa analia sana.

    Juma alikuwa anambembeleza.

    “Nipo katika siku za hatari…halafu tumefanya bila kinga….then sijui kuhusu afya yako..” alilalamika.

    Juma alikiri kosa lakini baadaye akasema jambo la kushangaza.

    “Asia usijali mimi ukipata mimba nitalea mtoto..nakupenda kutoka moyoni. Nakupenda sana.” Asia aliyapokea maneno yale kama igizo endelevu.

    Akajifanya yamemfariji.

    Juma akajiona yeye ni mshindi.

    Wakaoga pamoja.

    Wakati wa kuagana pale chumbani, mwanaume akafuta aibu. Akampatia nauli shilingi elfu hamsini.

    Asia akaipokea kwa heshima zote. Moyoni akimcheka Juma kwani hakujua kama anahamishiwa digitali kilazima.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hatimaye ukafika wakati wa kujipekua kama gari huwa inahifadhiwa mfukoni ama kwenye pochi.

    Juma alipagawa, hapakuwa na gari lolote linalofanana na la kwake pale nje.

    Alihaha na kutaka kuwauliza watu. Lakini akakumbana na maneno.

    “Park at owners risk.” Akaishiwa nguvu. Asia naye akajifanya amepagawa lakini kupagawa kwa Asia kulikuwa katika namna ya kidigitali.

    Asia alipiga mayowe, sio mayowe ya kuita watu hapana. Hayo ni ya kianalojia.

    Asia alipiga mayowe ya kumita dereva taksi.

    Alipofika akamweleza huku amepaniki. Hakumweleza juu ya gari kuibiwa, hapana akamuuliza swali jingine.

    “Kutoka hapa hadi Tandika bei gani.”

    “Elfu ishirini nakupeleka.”

    Asia hakujibu kitu, akaingia garini na kufunga milango.

    Juma akabaki kuhaha peke yake.

    Asia digitali, akatambaa na kutoweka upesi kidigitali.

    “Chezea Asia wewe.” Alipokuwa katika taksi alikutana na ujumbe huo. Ujumbe kutoka kwa Janeth Profesa maji ya shingo.

    Asia akafanya tabasamu hafifu.

    Uhakika wa kula na kutesa viwanja kwa mwezi mzima ulikuwepo.

    *****

    Juma akiwa katika kitanda hospitalini akiwa hoi kiafya analetewa taarifa ya kusikitisha lakini inayotia matumaini kidogo.

    Gari lilikuwa limepatikana. Taarifa haikuishia hapo.

    Gari lilikuwa ni sawa na kopo.

    Tairi zote tano hadi ya spea, usukani, viti, taa, na redio havikuwepo tena.

    Ilichekesha kuiita gari.

    Jumanne akazimia tena.

    **ASIA DIGITALI….ameanza mambo…huu ni mwanzo tu……ni aina ya chombezo ambalo lina matukio ya kustaajabisha ndani yake……

    Ni wewe sasa kustaajabika ama kuingia katika hisia….

    JIFUNZE: Msichana upo naye chumbani anachati chati na simu madudu gani....KUWA MAKINI



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog