Search This Blog

Monday, October 24, 2022

ASIA DIGITALI - 2

 





    Chombezo : Asia Digitali

    Sehemu Ya Pili (2)



    Juma akiwa katika kitanda hospitalini akiwa hoi kiafya analetewa taarifa ya kusikitisha lakini inayotia matumaini kidogo.

    Gari lilikuwa limepatikana. Taarifa haikuishia hapo.

    Gari lilikuwa ni sawa na kopo.

    Tairi zote tano hadi ya spea, usukani, viti, taa, na redio havikuwepo tena.

    Ilichekesha kuiita gari.

    Jumanne akazimia tena.

    ****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakati Jumanne akiwa katika mashindano ya kuzimia na kuzinduka huku akifikiria maisha mapya bila kuwa na gari.

    Wasichana watatu wenye maumbo ya tofauti lakini wakishabihiana rangi walikuwa katika meza mojawapo ya baa isiyokuwa maarufu sana katikaji ya jiji.

    Walikuwa wameichafua meza kwa vinywaji mbalimbali huku nyama ya mbuzi ikiwafanyia tabasamu la dhihaka.

    Walikuwa wameishughulikia na sasa ilikuwa imewakinai.

    “Kwa hiyo hiyo laki mbili ya viti wanatoa lini.” Asia aliuliza baada ya kumeza funda la bia baria aina ya Kilimanjaro.

    “Kesho jioni.” Mdada mnene kuliko wote aliyeathiriwa na utumiaji wa vipodozi vikali alijibu.

    “Na yule bwege aliyechukua tairi mpya nd’o kasema anatuma kwa Mpesa au.”

    “Kama kawaida yake.” Sasa alijibu Janeth.

    “Kuhusu redio?” swali jingine kutoka kwa Asia.

    “Ipo nyumbani kwao Messi”

    Asia alimgeuzia macho yule dada aliyeathiriwa na vipodozi vikali.

    “Husna Hakikisha huingii tamaa ukaiuza maana hukawii.” Asia alimwambia yule dada ambaye walimzoea kwa jina la Messi kutokana na mambo yake mengi.

    Husna akatabasamu kisha akasema, “Nina dili jingine murua, redio kitu gani?” Husna alisema. Asia akapaliwa na donge la bia.

    “Dili gani?” aliuliza kwa shauku.

    Husna badala ya kutoa jibu, alizama katika mkoba akatoka na ‘business card’. Akamkabidhi Asia.

    “Ya nini hii we Mmanyema.” Aliuliza.

    “Chukua namba hizo.”

    Asia hakuuliza swali, akaichukua namba.

    “Nimekutana naye maeneo ya benki. Sho me me what u can do.”

    Asia ahakujibu kitu. Alielewa Husna anamaanisha nini.

    Janeth alikuwa amejikita katika kuzishambulia nyama huku Salome akiwa anafuatisha mashairi ya wimbo wa taarabu uliokuwa unapigwa katika baa hiyo.

    Mavuno kwa siku hiyo yalikuwa mazuri sana.

    *****

    Dennis Kazinyingi alikuwa amejikita katika kutazama filamu ya kusisimua nyumbani kwake, mara uliingia ujumbe katika simu yake ya mkononi. Simu ilikuwa katika kiti kilichokuwa mbali naye.

    “Neema….nipatie hiyo simu” alitoa amri.

    Mtoto wake wa kike akaifuata na kumpatia.

    Akaitazama namba iliyotuma ujumbe. Ilikuwa mpya.

    Akaufungua ule ujumbe.

    Kabla hajaanza kuusoma mara ikaingia simu.

    Nayo ilikuwa namba mpya.

    Akaipokea kwa utulivu wa hali ya juu.

    “Halow…..Deniss Kazikwesha hapa.” Alijitambulisha kwa ujivuni wa hali ya juu.

    “Samahani…aah shkamoo anko….sorry aaah nimekosea namba pliiz, nilikuwa namtumia mdogo wangu pesa nimetuma kwako.” Sauti ililibembeleza sikio la Dennis, hakika ilikuwa sauti ya kike isiyohitaji aina yoyote ya nakshi kuipendezesha.

    “Pesa? Saa ngapi?”

    “Sasa hivi, yaani muda si mrefu kaka yangu.”

    “Ok ngoja nitazame nitakupigia.”

    Simu ikakatwa, ujumbe uliokuwa unafunguka ulikuwa ujumbe unaoonyesha pesa imeingia.

    Kutoka katika namba ile ile iliyompigia.

    Shilingi laki mbili na nusu. Deniss akastaajabu kidogo, hakuingiwa na roho yoyote ya tamaa. Alikuwa ni mtu ambaye pesa kama ile si chochote kwake.

    Akanyanyua simu yake akaipiga namba iliyompigia awali ikilalamika kukosea kutuma pesa.

    “Wewe nd’o Asia?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ni mimi kaka nisaidie tafadhali.”

    “nipe dakika moja tafadhali.”

    Simu ikakatwa tena. Kama alivyoahidi baada ya dakika moja alikuwa ametuma pesa kurudi kwa mmiliki.

    “Game limeanza…..” ilikuwa sauti ya Asia akijisemea mwenyewe huku akimtazama Husna ambaye alikuwa amelala tayari.

    Asia alijipongeza kwa karata ya pata potea aliyoweza kuicheza japo alikuwa na hofu ya kuibiwa ama kudhulumiwa kiasi hicho cha pesa.

    Asia alikosea kutuma pesa maksudi, mwanzoni alitaka kutuma meseji na kujifanya kuwa amekosea namba, mbinu hiyo akaiona ya kianalojia sana.

    Akataka kupiga na kujifanya amepiga bahati mbaya akaiona mbinu hiyo pia batili. Akaamua kuitumia mbinu ambayo matapeli wachache wanawewza kuitumia.

    Akatuma kiasi hicho cha pesa.

    Sasa pesa ilikuwa imerudi.

    Asia akamshukuru Mungu wake, kisha akachukua simu yake akazipiga namba za Dennis, bila shaka jambo hilo hata Deniss alilingojea.

    Nd’o maana akajitoa nje ya nyumba na kwenda katika bustani yake ndogo kuingoja simu ile.

    “Ubarikiwe kaka yangu, yaani ubarikiwe sana, ni watu wachache sana wenye moyo kama wako, utaongezewa mara mia ya ulichonifanyia. Ujue ni ngumu sana kwa mtu ambaye hamfahamiani, ama kweli umenipa nafasi nyingine ya kuamini kuwa duniani bado kuna watu wana utu…..naomba nisizungumze mengi asante sana kaka yangu.” Alitiririka Asia, maneno kuntu lakini sauti mahaba,

    “Usijali Asia, mambo madogo hayo nadhani huu ni mwanzo wa urafiki wetu, utajuaje maana ya Mungu mengi.’ Deniss alirusha kete yake.

    “Haya Deniss mi nikutakie usiku mwema.”

    “Haya asante japo hata sijajua unaishi wapi.”

    “Mimi nipo Dar, sema ni mzaliwa wa Mwanza na mara kwa mara huwa nasafiri hapa na pale. Lakini kwa kifupi nipo Dar.” Alijibu.

    “Ok mimi nipo Dar pia lakini nyumbani Maswa Shinyanga huko..ona sasa kumbe mimi na wewe wa kanda ya ziwa.”

    Asia akatoa cheko la kisasa, cheko linalotangaza huba.

    Walizungumza mengi. Usiku huu ukapita.

    Asia akiwa hajamuuliza Deniss anafanya kazi gani. Hakutaka kupaparuka alitaka kushambulia taratibu lakini kwa umakini sana.

    Siku iliyofuata, Asia akategemea kuwa Deniss atamuanza. Haikuwa hivyo.

    Asia akajihisi kuchanganyikiwa kwani aliona dalili za kuupoteza ushindi zikimsogelea, na hakuwa tayari kukubali kushindwa ilhali alimuhakikishia Husna kuwa baada ya siku nne mambo yatakuwa sawa.

    Asia akaamua kucheza pata potea nyingine.

    Binti huyu aliyeemrejesha Jumanne kutoka katika kutembelea makalio mpaka kurejea mtaani kwa kutumia miguu, sasa alikuwa akicheza na namba nyingine asiyoifahamu.

    Dennis. Anachokumbuka ni kwamba aliambiwa Deniss hana njaa na anaonekana ana pesa za kutosha.

    Asia akisikia pesa, basi kuchanganyikiwa ni halali yake. Hakuna alichopenda kama pesa.

    Asia akarusha kombora jingine.

    Akaingia katika simu yake kitu cha kwanza akaandika ujumbe kisha akauhifadhi. Kitendo kilichofua akamtumia Deniss pesa kiasi cha elfu sitini za kitanzania. Kisha upesi akatuma ule ujumbe.

    “Habari. Naomba upokee kiasi hicho kama shukrani zzangu za dhati kwa ukarimu ulionifanyia jana. Wewe ni wa ajabu sana. Ubarikiwe. Ninapotea hewani kwa dakika kadhaa naingia katika ndege naruka hapo Kampala mara moja. Nadhani kesho kutwa nitakuwa Dar. Take care.”

    Kisha akazima simu yake.

    Hakuna aliyeshirikishwa wakati mambo haya yanaendelea.

    Deniss aliupokea ujumbe na pesa zile na kweli alivyojaribu kupiga namba haikuwa inapatikana.

    Akaghafirika, hakutaka kushukuriwa kwa namna ile.

    Alituma ujumbe lakini haukupokelewa na baadaye ulirejesha majibu kuwa haukufanikiwa kumfikia muhusika.

    Deniss alikuwa katika mshangao wa hali ya juu, ujasiri wa Asia ulimshangaza. Hatimaye akapatwa na kile kitu ambacho Asia alikuwa anakijenga kwa kutumia gharama hizo.

    Deniss akatamani kumuona huyu mwanadada ambaye kiuhalisia anaonyesha kuwa ni mjasiriamali haswaa.

    Ni hicho Asia alikuwa anakihitaji.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Deniss na pesa zake zote alikuwa hajawahi kuipanda ndege, leo hii anatamkiwa na mtu kuwa ‘eti naruka hapo Kampala mara moja’.

    Ni mtu wa aina gani huyu?

    Akatamani kuiona sura ya Asia.

    Baada ya siku mbili.

    Asia alikuwa anapatikana tena.

    Sauti ya ujivuni na majigambo ya Deniss haukuwepo tena kama awali, daraja alilokuwepo akamuweka na Asia hapo hapo.

    Hata kumwambia kuhusua kuonana alikuwa anatetemeka. Lakini baada ya kumweleza Asia, alipata jibu jepesi lakini linalokera.

    “Ngoja nicheki na ratiba zangu basi.”

    Deniss alingoja kwa masaa mawili hatimaye akapokea ujumbe kutoka kwa Asia.

    “Kesho saa moja hivi. Nitakuwa na kikao maeneo ya Hotel Valentine Kariakoo, na nitaimaliza siku katika hoteli hiyo kwani kuna mgeni wangu amefikia hapo. Karibu kama utaweza” Deniss akavuta pumzi. Akairudiua tena meseji ile. Hakika ilikuwa imetumwa na mwanamke jasiri sana, ambaye kukutana na watu ni jambo la kawaida sana.

    Asia aliutuma ujumbe ule baada ya kufanya tathmini ya kina. Hakuhitaji kumchelewesha Deniss iwapo atajiweka machinjioni mapema.

    Baada ya ujumbe ule alijitoa muhanga tena, akachukua chumba katika hoteli ile ambayo ina hadhi ya kuitwa hoteli. Hakuwa na kikao chochote bali alikua katika mawindo.

    Alikuwa radhi kutumia pesa nyingi lakini mwisho wa siku apate nyingi zaidi, si kwa kuua mtu bali kuutumia mwili wake katika namna ya digitali.

    Na katika dili hili hakutaka kuwashirikisha shoga zake wengine, hata Husna alitakiwa kungojea majibu tu.

    SIKU ya siku ikafika, Asia kwa uvaaji wake hakika usingeweka tofauti yao na mfanyakazi yeyote katika benki ya dunia ama ikulu.

    Siku iliyofuata majira ya saa moja jioni, Deniss alikuwa bize kubadili nguo, mara avae jeans.

    “Ah hapa ataniona muhuni.”

    Mara avae suti.

    “Ah hapa nitaonekana mshamba sana….usiku huu na hili lisuti.”

    Mara avae hiki mara kile.

    Hatimaye akajituliza katika vazi la Jeans lakini juu akitua shati la mikono mirefu lililomkaa haswa.

    Akaiendea gari yake na kuitia moto.

    Safari ya kwenda kuonana na Asia.

    Mtoto wa mjini.

    Laiti kama angejua mtu anayekwenda kuonana naye.



    Gari liliegeshwa katika maegesho ya magari kwa kulipia.

    Deniss kabla ya kushuka katika gari lake, alichukua manukato makali na kujipulizia tena kisha akajitazama katika kioo.

    Alikuwa ametakata.

    Akatabasamu peke yake, ndevu zilizounda mfano wa ‘O’ kidevuni zikachanua. Akazidi kuvutia kumtazama.

    Kwa utulivu na umakini wa hali ya juu akashusha mguu mmoja chini kisha ukafuata na ule wa pili.

    Akabofya kitufe katika rimoti iliyobeba funguo za gari.

    Yakatoka makelele kidogo yasiyokera masikioni.

    Kisha akaanza kunyata akaufikia mlango, walinzi wakamkaribisha kwa macho, kisha wafanyakazi wa kike wakamlaki kwa bashasha.

    Alifanania na mfalme.



    Alipofika mapokezi alifuata maelekezo aliyopewa na Asia.

    Simu ikapigwa katika chumba alichokuwa Asia.

    “Samahani dada kuna mgeni wako hapa.” Sauti ya muhudumu ikatambaa.

    Kimya kikatanda kisha akaitoa simu sikioni na kuuliza, “Unaitwa nani? Na je ulikuwa na miadi naye?” muhudumu alimuuliza deniss.

    “Yah..nilikuwa na miadi naye…..naitwa Deniss..mwambie tuli…” kabla hajamalizia ngonjera zake muhudumu alikuwa amerejesha simu sikioni. Akatoa majibu.

    “Nenda chumba namba 18…” alimweleza Deniss.

    Japokuwa hakusema neno, Deniss alionyesha macho ya kuonyesha kuhitaji kuelekezwa zaidi. Muhudumu akaling’amua hilo.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akamwita muhudumu mwingine akampa zoezi la kumpeleka Deniss kwa Asia.

    Chumba namba kumi na nane.



    Deniss akaugonga mlango.

    Zikapita kama dakika tatu.

    “Ingia…” sauti kutoka ndani ikajibu.

    Deniss akakishusha kitasa akaingia.

    Marashi yake yakasahaulika yalikuwa yananukiaje hapo awali.

    Akakutana na marashi makali ya kisasa zaidi yakinukia kutoka ndani.

    Akapiga hatua mbili, akakutana na mwanadada akiwa amejikita katika kompyuta mpakato (laptop) yake.

    Alitumia dakika nyingine moja, akanyanyua kichwa. Akafanya tabasamu mwanana. Vishimo vikajichora katika mashavu yake.

    “Hi Denny!!” sauti nyembamba kama inayojilazimisha kutoka lakini yenye kuliwaza na kusahaulisha kama kuna shida duniani ilitoka katika kinywa cha Asia.

    Deniss akakodoa macho hakuwahi kuitwa kwa maringo namna hiyo hata mkewe a ndoa hakuwahi kumtolea sauti inayoliwaza namna ile.

    “Hi!!” hatimaye alijibu.

    “Karibu…karibu kitandani maana humu naona kuna kiti kimoja tu. Pole lakini next time nakukaribisha kwangu.” Alijieleza Asia.

    Deniss akaketi.

    Alichokosea ni kujionyesha kuwa mapema sana ameshangazwa na urembo wa Asia. Binti huyu alipata wasaa wa kumsoma.

    Kosa kubwa sana wanalofanya wanaume wengi katika mfumo wa analojia.

    Maongezi yakaendelea kidogo, asia akaitazama saa yake. Ilikuwa inakaribia saa mbili usiku.

    Akaitwaa simu ya mezani. Akabofya namba kadhaa.

    “Nahitaji mtu wa jikoni tafadhali.”

    Simu ikakatwa.

    Baada ya dakika tano. Hodi ikasikika.

    Kwa mara ya kwanza Asia akasimama, kwenda kuufungua mlango ili muhudumu aweze kuingia.

    Zilikuwa ni hatua sita tu lakini kila hatua haikutakiwa kuchezewa.

    Kinguo kifupi alichovaa kiliruhusu michirizi ya utamu kuonekana nyuma ya goti, wepesi wake ukaruhusu mitikisiko ya kawaida na nyongeza ya mitikisiko ya kichina, mgongo nao haukuwa nyuma.

    Asia alikuwa kifaa cha nguvu.

    Akaufungua mlango. Muhudumu akaingia.

    “Msikilize huyu kaka.” Asia alitoa amri kwa muhudumu.

    Deniss akaanza kujiuma uma.

    “Chipsi kuku….” Akaropoka.

    “Mimi niletee mchemsho wa kuku.” Asia akauendea mkoba akaamua kulipa mapema. Akatoa kwa maksudi burungutu kubwa kiasi la pesa alizokuwa amezikomba katika akaunti yake.

    Deniss akaziona.

    “Mtoto hana njaa huyu.” Akabashiri.



    Muhudumu alipoondoka, Deniss na Asia wakaendelea na stori za hapa na pale.

    Mara simu ya Asia ikaita.

    Akaitoa, akausoma ujumbe.

    “Mh msichana mrembo kama wewe unatumia Nokia Obama ya tochi?” Deniss alitania.

    Asia akafanya mfano wa tabasamu.

    “Hebu simu yako…” akamuomba.

    Deniss akamkabidhi, ilikuwa ni iPhone5.

    “Umenunua bei gani hii?”

    “Milioni moja na ushee.” Alijinadi Deniss.

    Asia akatikisa kichwa kwa masikitiko.

    “Deniss…..unajua kuwa kuna viwanja vinauzwa kijijini hiyo pesa uliyonunulia simu. Mimi niliyenunua kiwanja ambacho hakifutiki kabisa, na wewe uliyenunua simu nani amewekeza? Shtuka Deniss sisi ni vijana tunatakiwa kuwa na mawazo ya miaka kadhaa mbele sio kuwaza leo tu, chimbia pesa zako chini Deniss chimbia pesa kizazi chako kizikute, mwanao hataikuta hiyo sijui funifuni faivu sijui nini…simu uliyozungumza na mimi ndo hii je? Ulibaini tofauti?” asia alizungumza kwa hekima zote. Maneno kuntu kama kawaida yake. Yakamchoma Deniss akaanza kujichekesha kisha akajaribu kujibu hoja.

    Asia alikisubiri kipengele hiki.

    “Lakini Asia, huwezi jua mimi nimenunua kiwanja na bado nimenunua na simu, kama pesa ipo na inabaki nd’o ninunue viwanja tuuu.” Alijibu kwa kulalamika.

    Asia akapata alichokuwa amehitaji.

    “Kumbe bwege ana pesa chafu eeh…” alimuwazia huku akimtazama usoni.

    Jicho la Asia likamwathiri kisaiokolojia Deniss lakini hakuweza kuanza.

    Simu mfululizo zikawa zinaingia katika simu ya Asia.

    Kila simu ilikuwa ya kibiashara.

    Hakika Asia alikuwa namba nyingine. Deniss alikiri.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Majira ya saa tano usiku Deniss aliaga kuwa anaondoka.

    Asia akamsindikiza mpaka mapokezi, wakaagana.

    Deniss akatoweka bila kufanya lolote na Asia, alikiri kimoyomoyo kuwa alimuogopa sana binti yule mjasiriamali.



    Siku iliyofuata mawasiliano yaliendelea kama kawaida.

    Baada ya kutumia pesa nyingi kujaribu kumuweka sawa Deniss sasa Asia akaamua kulipua bomu lake.

    Deniss akiwa anamuamini sana Asia kama rafiki wa karibu tena mshauri mzuri.

    Ikafikia siku ambayo kamwe haitasahaulika katika kumbukumbu za Deniss.



    Simu kutoka kwa Asia ilimkurupua kutoka katika kiti cha ofisi yake.

    “Asia ametoka Msumbiji?” alijiuliza.

    “Nambie.”

    “Ukwapi Denny.”

    “Ofisini vipi umerudi bongo?”

    “Yeah nimerejea. Upo bize sana nahitaji kukuona.”

    “Hapana sio bize sana.”

    “Nipo huku Royal Temeke..kule pa siku ile.”

    Dennis akaelewa akaingia garini akaelekea alipokuwa Asia.

    Akamkuta chumbani akiwa mnyonge sana.

    Tofauti kabisa na siku nyingine.

    Vazi lake jepesi la kitambaa laini liliyaruhusu yale mapaja yaliyompagawisha Jumanne na hatimaye kulizwa gari yalikuwa nje.

    Alikuwa amejilaza kihasara hasara haswaa.

    Deniss alipoingia.

    Asia hakushtuka akajiweka vyema kitandani huku akijifanya kujisitiri mapaja yake.

    Deniss alitegemea Asia atasema jambo lolote, hakusema.

    Akamsogelea pale kitandani.

    Akamgusa.

    “Asia…we Asia.”

    Asia hakugeuka, Deniss akaamua kumgeuza.

    Lahaula. Asia likuwa ameuchafua uso wake kwa machozi.

    Mrembo alikuwa analia.

    Kilio cha kimya kimya.

    “Asia….kuna nini…nani Asia kakufanya hivi.” Deniss akataharuki.

    “Niache Denny, niliumbiwa shida hizi. Niache tu.” Alizungumza huku analia.

    Deniss hakukubali kumwacha. Akazidi kuuliza.

    Ndipo Asia alipohamia digitali na kuendelea kucheza na akili ya Denny.

    “Denny, mume wangu…mume wangu ananinyanyasa sana, mie wa kuwa naamua kulala hotelini kisa kitanda cha nyumbani kichungu.”

    “Asia umeolewa?”

    “Ndio. Lakini ni bure…bure kabisa Denny.”

    “Nini kwani?”

    “Ubunge wake ananiletea mimi hadi nyumbani….ubunge wake unanifanya mimi mtumwa. Ameona hiyo haitoshi kisa dini inaruhusu kaniongezea mke wa pili.” Asia alisikitisha na kama angekuwa muigizaji, wengi wangekuwa wanalia akiigiza vipande kama hivi.

    Denny akahamaki, “kumbe Asia mke wa kigogo, ndo maana ana pesa huyu mtoto……dah…..watu wengine hawapendi shobo hata siku moja hajanambia.”

    Denny akajaribu kumsihi sana asilie, Asia akazidi kulia.

    “Denny asante kwa kuja katika maisha yangu, japokuwa ni karibia mwezi mmoja tu tangu tufahamiane nimejifunza mengi kwako. Na ukiwa kama rafiki mwema nimeamua kukuzawadia kitu kama utakuwa tayari.”

    “Asante Asia hata mimi nafurahi kuwa rafiki yako. Nitafurahi kupata zawadi kutoka kwako” Denny alijibu huku mawazo yake yakiwaza ngono tu.

    “Zawadi zipo za aina mbili, zote nitakupa.” Alisema Asia kisha akasita, “Zawadi ya kwanza itakuwa ni swali, na zawadi ya pili itaanza kabla ya zawadi ya kwanza.” Aliongea Asia huku akiwa ameremba sauti yake.

    “Denny….nimeamua kujitolea pesa yangu milioni thelathini kwa ajili yako.”

    “Kivipi?” aliuliza Denny.

    “Nilikwambia huwa kamwe sinunui magari ya bei ghari wala simu. Nilikwambiaje?”

    “Unachimbia chini..” alimalizia Denny.

    “Ok..unapafahamu Bahari Beach..”

    “Napafahamu kwa wazito kule….”

    “Nataka nawe uwe mzito lakini kwa kujibu swali langu.”

    “Niulize tu Asia.”

    “Nitatoa katika akaunti yangu pesa taslimu milioni thelathini….nawe utatakiwa kufanya kitu kidogo tu milioni kumi….ifike milioni arobaini.”

    “Ehee.”

    “Kisha nakununulia kiwanja kikubwa pande zile, na ukionyesha uhai katika kujenga nitachota pesa nyingine nitakusaidia ujenzi….pesa inafukiwa chini mpenzi wangu….sio katika iPhone sijui nini” Asia alisema kwa maringo, walau aliweza kutabasamu.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nakufanyia haya yote kwa ukarimu ulionionesha kabla na baada ya kujuana.”

    “Nilisema sihitaji jibu kwa sasa maana patakuwa na mjadala mrefu, kwa kuwa umezikubali zawadi zote, Denny ipokee zawadi yangu hii ya pili…”

    Asia alimrukia Denny akamkumbatia, akajivika uso usiokuwa na soni hata kidogo. Akamnong’oneza Denny, “Ukiamua kuniona mimi Malaya sawa Denny lakini naomba niwe wazi…..Denny unanitesa…unanitesa Denny….”

    Kijana hakukumbuka kama anayo pete ya ndoa, hakukumbuka kama anao watoto nyumbani.

    Denny akachukua mkondo wa wanaume wengi, kuwa watumwa wa ngoni linapokuja suala la ana kwa ana na msichana.

    Akamkumbatia Asia.

    Ulikuwa mchezo wa dakika zisizopungua hamsini, sakafu ilihangaishwa, kitanda kiliteseka, bafu nalo liliona kilichotokea.

    Deniss hakuwahi kufanyiwa manjonjo hayo na mkewe wa ndoa.

    Walipotoka bafuni. Deniss akakumbuka kujibu swali.

    “Nipo tayari kwa zawadi ya kwanza, nami nitakupa zawadi pia mpenzi.”

    “Ok siku ukiipata hiyo pesa utanambia…” Asia akauliza swali la mitego.

    “Sio kuipata ipo tayari..yaani siku ukiwa na nafasi tu my dear.” Deniss akajileta kwenye kumi na nane. Asia akachekelea maana hakuna mchezo alioupenda kama mchezo ndani ya kumi na nane.

    “Basi tufanye kesho kutwa maana kesho nakimbia Mbeya…..narudi keshokutwa mchana…” alidanganya Asia ili aweze kujipanga kuchuma baada ya kupanda mwezi mzima.




     ***TEGO linakaribia kunasa……..nini kitajiri???



    ITAENDELEA…..

0 comments:

Post a Comment

Blog