Search This Blog

Monday, October 24, 2022

AAH...SHEMEJI...AACHAAA...! - 1

 





     IMEANDIKWA NA : HAWA D. OMARY





    *********************************************************************************



    Chombezo : Aah Shemeji ... Achaaa !

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    AISHA alijiona kama mtu mwenye bahati kwa kutongozwa na shemejiye. Aliwaza endapo akimkubalia au asimkubalie kwa kuona kuwa ni shemeji yake. Alifikiria sana juu ya utajiri wa shemeji yake na hali aliyonayo yeye .



    “Endapo nikikubali dada akigundua itakuwaje?” aah!! Lakini si amenitongoza mwenyewe,siwezi kupiga teke fuko la pesa… Potelea mbali.”



    Siku iliyofuata Aisha alikutana na rafiki yake aliyeitwa Anita. Aisha alimsimulia Anita kuhusu shemejiye.



    “Shoga basi ngoja nikupe mkanda”.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapo ndipo ninapokupendea tukikutana baraza huchangamka kwa stori, haya shoga hebu nipe huo mkanda”.



    “Jana usiku wakati tunakula,dada aliwahi kushiba akaenda zake kulala, sebuleni tukabaki mimi na shemeji tukipata dinna. Basi shoga’angu shemeji si nd’o akaanza… Ooh Aisha unajua wewe mzuri sana kuliko hata dada’ko mi nikabaki kucheka tu. Dakika chache zikapita mara akaanza tena… Aisha najua wewe ni mtu mzima unayeweza kutunza siri,mi nataka we uwe mpenzi wangu lakini dada’ko asijue. Shoga nlishtuka kwani sikutegemea hata sikumoja kama shemeji atakuja kunitamkia maneno kama yale, ukizingatia jinsi ninavyomheshimu.”



    “Heehee shuntu babuu ….. Aaa babu wee heshima hiyo kwani baba’ko mzazi yule.” Anita alidakia, wote kwa pamoja waliangua vicheko vya umbea.



    “Sasa sikiliza shoga yangu nikwambie maisha ndo hayo yanaanza kukunyookea ukizingatia shemejiyo alivyo na utajiri,kuuacha ni sawa na kukataa kuolewa na mfalme ili uje kuwa malkia”.



    “Kwa hiyo ndo unaniambiaje?”



    “ Hee bibi ee tulia mbona una haraka kama mkojo wa asubuhi,utakukurupua kitandani utake usitake,usiombe ukakuta chooni kuna mtu utaisoma, utarukaruka kama umepewa adhabu na mwalimu. Kama kakuanza mwenyewe basi kamaindi figa huyo.



    Vibaya kama umemuanza wewe au umemtega? Maana na sisi wanawake hatujambo.Ukimpenda mwanamume utamfanyia kila visa hadi ataingia laini mara urembue macho,mara umvalie khanga moja na hiyo mikalio yako shoga kama umemfanya hivyo mwanamume wa watu utamuua.”



    “ Acha utani Anita”



    “Basi ndo hivyo shoga’angu.”



    “Mimi jana nilimwambia angoje nifikirie maana niliishiwa pozi, nkashindwa hata kuongea. Taratibu nlielekea chumbani kwangu na kuanza kufikiria. Mpaka leo asubuhi sikupata jibu, nlijumlisha na kutoa lakini jibu halikupatikana. Lakini sasa nimepata jibu zuri nd’o ma’na nakupenda hapo hapakosi jibu la uhakika,ama kweli we ndo jembe langu”.



    ********

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Aisha”



    “Abee” Aisha aliitika na mazungumzo yao yalikatishwa na wito ule, hivyo kila mmoja alielekea kwao.



    ”Kachukue pesa juu ya meza wende sokoni.Unataka kumpikia nini leo shemejio?”



    “Mi si ninajua shemeji yangu anapenda wali na samaki, basi nami ntapika hivyo.”



    “Haya nenda basi.”Nasra alimsihi Aisha ambaye alikuwa akitoka kuelekea sokoni.



    Akiwa njiani Aisha alijawa na mawazo juu ya shemeji yake, alifikiri kama shemeji yake alimpenda kweli au alimtega tuu ili

    kupima imani yake.



    “Atajijua mwenyewe, mimi leo akiniuliza nitamwambia nimekubali. Kama lengo lake ni kunipima imani yangu basi atapata robo kilo.”



    Aliwaza Aisha ambaye tayari alikuwa ameshafika sokoni na kuchukua mahitaji aliyoagizwa.



    *****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kama kawaida yao usiku ulipowadia chakula cha usiku kilikuwa tayari mezani na wote watatu walikutana mezani kwa ajili ya kupata msosi.



    “Mume wangu, leo Aisha amesema shemejiye wapenda sana wali kwa samaki ndiyo maana ameamua kukupikia.” Nasra alisema kwa utani bila ya kujua kinachoendelea. Wote walicheka.



    “Kumbe ndiyo maana chakula cha leo kitamu. Kumbe hii ni spesho dinna for me?” Bwana Abduli alitabasamu huku akimwangalia

    Aisha ambaye yeye alionekana akimwangalia kwa aibu.



    Nasra kama ilivyo kawaida yake. Msichana asiyependa kujaza tumbo kisha kushindwa kuvaa bodisuti. Taratibu alivuta birika lililokuwa na maji ya kunawa. Akajimiminia maji,baada ya kuhakikisha kuwa mkono wake umetakata taratibu alinyanyuka na kuelekea chumbani kwake huku akimtakia mdogo wake usiku mwema. Bw. Abduli alionyesha tabasamu huku akimkonyeza Aisha. Dakika kadhaa zilipita kukiwa kimya Bw. Abduli alianza ule utani wake.



    “Sa’ Aisha ndo vipi mbona hujanipa jibu langu au nd’o hunipendi?”



    “ Hapana shemeji mi mbona nshakubali.”Aisha alijibu kwa kusitasita huku macho yake yakiangalia chini na kidole kimoja kikiwa mdomoni.



    “Siamini kama uyasemayo ni ya kweli,mbona bado unaniita shemeji badala ya kusema namekubali mpenzi.” Bw. Abduli alisema kwa utani. “Basi nashukuru mpenzi kama umekubali ombi langu naminajiona kama mwenye bahati kumpata msichana mrembo kama wewe.” Bw Abduli alinyanyuka na kumbusu Aisha ili kuonesha kuwa wameshafungua ukurasa mpya wa mapenzi



    Kule chumbani Nasra alitandika kitanda kisha akabadili nguo alizokuwa amevaa, alichukua taulo akalivaa kisha akajitupa kitandani, akimsubiri mumewe ili wakaoge. Dakika zalipotea bila Bw. Abduli kutokea. Nasra alijigaragaza kitandani hadi akapitiwa na usingizi. Baada ya dakika kama ishirini hivi Nasra alishtuka toka usingizini nakutupia machosaa iliyokuwa ukutani ambayo ilimtaarifu kuwa ni saa tano usiku lakini hakumwona mumewe.”



    Hee! Kula huko kula gani wanakula mawe?” Nasra alijisemea huku akiwa amejawa na hasira. Mara mlango wa chumbani ulifunguliwa taratibu Bw. Abduli aliingia ndani na kuelekea mahali lilipokuwa taulo. Alibadili nguo alizokuwa amevaa na kujifunga taulo kiunoni. Kisha alielekea mahali alipokuwa mkewe na kumshika mikono kisha kumnyanyua taratibu kuelekea bafuni.



    *****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni siku ya Jumapili ya mwisho wa mwezi, vitu vyote vilikuwa vimeisha ndani.Hakukuwa na unga, mchele, nyanya, vitunguu wala mafuta ya kupikia.



    Bw. Abdul alimshauri mkewe kuwa anahitaji kuongozana na Aisha ili wakanunue bidhaa. Nasra hakuwa na kipingamizi kwani hakuelewa lolote juu ya uhusiano wa kimapenzi kati ya Bw. Abdul na shemejiye. (Aisha).



    “Aisha!” Sauti ilisikika masikioni mwa Aisha .



    “Abee!” Aisha aliitika toka chumbani kwake alijua fika kuwa sauti ile ni ya dada’ke.



    Alichukua kanga mbili moja aliipachika kifuani na nyingine kiunoni taratibu akielekea chumbani kwa dada’ke.



    “Nenda kajiandae wende sokoni na shemejiyo.”



    Baada ya dakika chache Aisha alikuwa tayari ameshajiandaa.Alitoka nje.Mbele yake alikuwa amesimama Bw. Abdul mkononi ameshika funguo za gari.



    “Chukua funguo kanisubiri ndani ya gari.”



    Wakati Aisha akipokea funguo zile Bw. Abdul alimbinya vidole huku akimkonyeza.



    Dakika chache zilipita wakati Bw. Abdul akimuaga mkewe. Kisha alitoka nje na kuelekea mahali alipoegesha gari lake. Taratibu Bw. Abdul aliwasha gari na kuliondoa.



    Njiani stori za utani na mapenzi zilitawala.



    “Umependeza sana leo.” Bw. Abdul alisema huku akimgusa Aisha sehemu za mapaja.



    “Acha utani shemeji.”



    “Aaaa!Aisha mambo gani hayo ni lini utaanza kuniita mpenzi au mi sifai kuitwa mpenzi.” Bw. Abdul alitamka huku midomo yake ikichezacheza kwa uchu wa mapenzi .



    “Mambo mazuri hayataki haraka nitazoea taratibu.” Aisha alitamka huku macho yake yakiwa yamebadilika rangi na kuwa mekundu.



    Wote walishajawa na uchu wa mapenzi. Bw. Abdul aliendelea kumpapasa Aisha sehemu mbalimbali za mwili. Lakini sehemu aliyomvutia zaidi ni matiti,yaliyoumbika vizuri na kujaa kifuani mithili ya kifuu cha nazi. Mapaja yake pia yalikuwa ya namna ya pekee ambayo yangeweza kumvutia mwanamume yeyote ambayeni rijali, yalikuwa manene, meupe na mwororo yasiyokuwa hata na chembe ya doa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Naye Aisha hakuwa mbumbumbu, akaupenyeza mkono wake hadi sehemu fulani mwilini mwa Abdul na kushika kile alichotaka kukishika. Akamtomasa kwa mapozi, kiganja chake laini kikizidi kumchanganya Abdul na kumwongezea mhemuko. Hakika Bw. Abdul alipagawa sana hadi kufikia hatua ya kutaka kuvunja amri ya sita ndani ya gari.



    “Aisha uvumilivu umenishinda mpenzi, tufanye basi hata kidogo,” Abdul alisema kwa tabu, akizidi kumvuta Aisha na kumkumbatia.

    Aisha hakuona kuwa ni ustaarabu kufanya mapenzi ndani ya gari hivyo alimshauri shemejiye kuwa wapange siku nyingine ya kufanya maangamizi kunako sita kwa sita.



    Kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana hivyo wote walikubaliana kupanga siku nyingine ya kutimiza azma yao.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog