Search This Blog

Monday, October 24, 2022

TINGINYA LA BA'MDOGO - 1

 





     IMEANDIKWA NA :  BABU LAO---WA UKWELI





    *********************************************************************************





    Chombezo : Tinginya La Ba'mdogo

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    CAROLINE aligugumia kwa nguvu huku akizidisha juhudi na akizidi kusisimkwa pale mikono sugu ya kiume ilipokuwa ikiyatomasatomasa makalio yake na hivyo kumwongezea hamasa ya kuendelea kujishughulisha mwilini mwa Toony. Alikuwa akijikunja na kujikunjua katiaka namna ya kipekee, miguu kaitanua na kumweka Tonny katikati ya mapaja yake makubwa na kuzidi kujituma kama aliyedhamiria kuua!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Matiti yake makubwa, yenye uhai, yalikuwa yalikuwa kivutio kingine kwa Tonny kiasi cha kujikuta mara akiyapapasa makalio haya makubwa na laini na mara akiyashika matiti hayo na kuyanyonya.



    “Tulia…tulia…” sauti ilimtoka Caroline kwa shida. “Leo ni zamu yangu…acha nile ninavyopenda….acha nijilie vyangu… ” alibwata huku akimlalia Tonny na kuzidi kunengua huku sasa akipenyeza ulimi sikioni.



    Mara akajiinua na kuikita mikono kulia na kushoto, akimweka katikati Tonny. Macho yake yalikuwa yamelegea na aliuma meno kwa nguvu na kuzidi kumwadhibu Tonny kwa namna iliyomtia wazimu zaidi Tonny.



    Tonny naye alionekana kukunja uso na kuwa katika mwonekano tofauti kama anayeumizwa na kitu fulani ilhali kwa jumla starehe aliyokuwa akiipata iliihamisha akili yake yote hadi katika sayari nyingine.



    Mara Caroline akajing’atua na kujitupa pembeni huku akihema kwa nguvu. “Asante baby…” hatimaye alisema huku akichukua kanga na kuanza kumpangusa Tonny hapa na pale, upangusaji ambao uliibua upya moto uliokuwa umepungua maungoni mwa Tonny.



    Ulikuwa ni kama uchokozi vile, kwani baada ya Caroline kutumia kanga kwa muda mfupi akimpangusa Tonny jasho usoni na kifuani, hatimaye aliitupa kando na kuutumia ulimi kwa fujo, akianzia kifuani ambako alizinyonya chuchu za Tonny kwa mapozi yanayosisimua kisha akashuka chini taratibu hadi kitovuni ambako aliliendeleza zoezi lake ilhali mkono mmoja ukiwa umeshika kile kitu alichokipenda, kitu kikubwa kilichokakamaaa, akawa akikiminyaminya kwa utaalamu aliojaaliwa, kiganja chake laini cha mkono wa kushoto kikaifanya kazi hiyo kwa namna ambayo ni vigumu kuielezea.



    Huku ulimi wake wa moto ukiendelea kuteleza kitovuni kwa Tonny na kulamba kwa staili ambayo ilimchanganya Tonny kwa kiasi kikubwa, ilifikia hatua sasa Tonny akaanza kugunaguna, akifumba macho na kuyafumbua huku akizipapasa nywele nyingi na nyeusi tii za Caroline.



    Caroline alikiacha kitovu, sasa akashuka chini zaidi na kuutua ulimi palepale alipopakusudia. Kwanza akasita na kubaki amekishika kitu hiki cheusi, kikubwa na kilichokakamaa, akakitazama kwa macho yenye uchu maradufu. Mtoto wa kike akahema kwa nguvu huku akikiminyaminya kitu hicho na wakati huohuo, mara akikitazama na mara akimtazama Tonny.



    Ghafla akakielekeza kinywa chake kwenye ‘kijigunzi’ hicho kikubwa. Akautoa ulimi na kuanza kulamba juu-juu. Akawa akifanya hivyo huku akigugumia tena, safari hii kwa sauti ndogo zaidi na pia akihema kwa nguvu. Ulimi huo ukawa ukipanda na kushuka ukilizungukia ‘gunzi’ hilo jeusi. Mara akaupeleka ulimi hadi kwenye zile gololi zilizojihifadhi katikati ya miguu. Akawa akinyonya na kulamba kwa utaalamu uleule aliojaaliwa, akidhihirisha kuwa alifundwa, akafundika.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hakuridhika, akalishika gunzi hilo na kulibwia kinywani. Akawa akifanya mchezo wa ndani, nje, ndani, nje huku akiendelea kuchombeza kwa miguno ya raha na wakati huo mikono yake laini ikitalii sehemu nyingine za mwili wa Tonny kwa namna ileile ya kuwehusha. Mara akaking’atua kinywa chake kilichojaa ute mzito. Akauacha ute huo ulimwagikie lile ‘gunzi’ jeusi.



    Akautoa ulimi na kuupitisha kwenye papi za mdomo akiyalamba-lamba mabaki ya ute huo kisha akalirudia ‘gunzi’ lile na kuugandisha mdomo wake. Sasa Tonny akawa akikunja na kuikunjua miguu kwa raha.



    “Mmmmmh…” alilalama mwanamume huku akiking’ang’ania kichwa cha Caroline. Caroline naye akatii, akakituliza kchwa pale kwenye gunzi, mdomo ukiwa unamung’unya na kufyonza naye akiendelea kulalama kwa namna ileile ya kuchanganywa na mahanjam.



    Dakika kadhaa baadaye ndipo Caroline alipojing’atua tena na kubaki akikitazama hicho alichokishika, akionekana kuvutwa na mwonekano wake, ukubwa na ukakamavu wake.



    “Mmmh…baby…sikuachi…hak’yanani…umejaaliwa,” yalimtoka huku akiendelea kukitazama kitu hicho kwa uchu.



    *****



    TONNY alikuwa akiishi Mtaa wa Rufiji, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

    Mkewe, Lilian naye aliheshimiwa na kusifiwa na wengi kwa tabia yake ya ucheshi kwa yeyote sanjari na kumsaidia yeyote mwenye shida kulingana na uwezo wake.



    Tonny na Lilian walihamia hapo Kariakoo wakitokea Tandika na walikuwa wakihitaji vyumba viwili na sebule, vyumba ambavyo baada ya kuhangaika huku na kule ndipo walipodokezwa kuwa hapo Mtaa wa Rufiji kuna vyumba hivyo.



    Katika kipindi hicho Tonny alikuwa akifanya kazi katika kampuni moja ya kigeni iliyomilikiwa ma mwekezaji mmoja kutoka Afrika Kusini. Alikuwa ameshafanya kazi katika kampuni hiyo kwa miaka mitano, na mwaka mmoja baada ya kuhamia hapo Kariakoo kampuni ikaamua kubana matumizi. Wafanyakazi wengi wakapunguzwa katika ajira.



    Tonny alikuwa mmoja wa waliopunguzwa. Na alipata mafao ya shilingi milioni 10. Ndiyo, alipoteza ajira, lakini akilini mwake aliamini kuwa maisha ni popote na kwa njia yoyote, siyo lazima mtu uwe umeajiriwa, hapana, unaweza kujiajiri.



    Mafao aliyopata yalimvimbisha kichwa. Alikuwa na kumbukumbu sahihi kuwa tangu alione jua hakuwa amewahi kumiliki shilingi milioni tano kwa mkupuo na kuzitumia kwa jinsi apendavyo. Mshahara wake haukuzidi shilingi laki tatu. Hizi milioni kumi za mkupuo kwa nini zisimtie kichaa?



    Sasa alijiona yu mtu kati ya watu. Akaanza kuonesha makeke yake mapemaa! Kwanza alisheheneza samani za kisasa ndani ya vyumba alivyopanga, kisha akanunua nguo nyingi zake, za mkewe na za mtoto wao, Sambe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa jumla aliiona kama dunia iko mikononi mwake. Na ndipo pia ratiba zake zilipobadilika ghafla. Awali alikuwa na tabia ya kurudi nyumbani mapema mara tu atokapo kazini, akautumia muda mwingi kwa kukaa na mkewe, akitazama televisheni. Na baada ya kula walioga na kulala. Na hata ilipotokea akahitaji kupata bia mbili, tatu, alitoka na mkewe na mtoto wao wakaenda katika baa iliyo jirani ambako walikata kiu kwa kinywaji hicho.



    Huo ndio ulikuwa utaratibu wake wakati akiwa na ajira, siyo baada ya kupoteza hiyo ajira na kupata mafao yake. Sasa ratiba ilibadilika, mabadiliko yaliyoanza taratibu. Mara kwa mara alikuwa akitoka peke yake na kuchelewa sana kurudi, na aliporudi tayari alikuwa kalewa. Na hata ilipotokea akatoka na Lilian, hakuonekana kuwa na furaha kama siku zote na mara kwa mara alikuwa akipoteza muda mwingi akichati kwa simu.



    Lilian alipojaribu kumhoji, mwanamume akaja juu: “Nahangaika kufanya mipango ya kazi.”



    Tabia hiyo ilimshangaza sana Lilian. Na alizidi kushangaa baada ya Tonny kuanza tabia ya kuwahi sana kuamka asubuhi na kuoga harakaharaka kisha huyoo anatokomea zake. Ni utafutaji gani huo wa ajira unaomwondoa kitandani saa 11 alfajiri? Hakukubali, na hakuamini.



    Alfajiri moja akadiriki kumuuliza, “Lakini ni kipi hasa kinachokutoa usiku-usiku hivi?”



    Kabla ya Tonny hajamjibu alimtazama kwa jicho kali. Ndiyo kwanza alikuwa ametoka bafuni kuoga, na ilikuwa ndiyo imetimu saa 11.30.

    Akasonya na kuigeukia kabati ambako aliifungua na kutoa shati na suruali.



    “Huna swali jingine zaidi ya hilo?” naye alimuuliza.



    “Una maana kuwa hilo siyo swali?”



    Tonny ‘akauchuna.’



    “Haya mwenzangu, yangu macho, lakini najua ipo siku mambo yatakuwa hadharani.”



    Tonny hakujibu kitu, aliendelea kuvaa nguo kisha akajitazama kwenye kioo kikubwa kilichobandikwa kwenye mlango wa kabati. Akairekebisha tai yake vizuri kisha akamgeukia tena Lilian.



    Wakatazamana.





    KABLA ya Tonny hajamjibu alimtazama kwa jicho kali. Ndiyo kwanza alikuwa ametoka bafuni kuoga, na ilikuwa ndiyo imetimu saa 11.30.

    Akasonya na kuigeukia kabati ambako aliifungua na kutoa shati na suruali.



    “Huna swali jingine zaidi ya hilo?” naye alimuuliza.



    “Una maana kuwa hilo siyo swali?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tonny ‘akauchuna.’



    “Haya mwenzangu, yangu macho, lakini najua ipo siku mambo yatakuwa hadharani.”



    Tonny hakujibu kitu, aliendelea kuvaa nguo kisha akajitazama kwenye kioo kikubwa kilichobandikwa kwenye mlango wa kabati. Akairekebisha tai yake vizuri kisha akamgeukia tena Lilian.



    Wakatazamana.



    “Vipi, bado una shauku ya jibu la swali lako,” Tonny alimuuliza. Na hakusubiri jibu, papohapo akamalizia, “Kinachonitoa mapema hivi ni kutafuta ajira. Na hilo nilikwishakwambia mara nyingi sana.”



    “Lakini sidhani kama ni lazima kutoka mapema hivi.”



    “Usijali, nitakaporudi jioni tutaongea kwa kirefu kuhusu jambo hilo.”



    Lilian alikosa nguvu. Akageukia ukutani na kuendelea kujilaza hapo kitandani ilhali hana amani wala utulivu moyoni. Alikosa amani na utulivu kwa kuwa hii ilikuwa ni wiki ya pili, akilala kitanda kimoja na chumba kimoja na mumewe, Tonny. Lakini akiwa na mke wa ndoa mwenye kustahili huduma zote na haki zote, yeye alikosa kitu muhimu alichokiheshimu na alichoamini kuwa ndicho kingefanya ajisikie kweli kaolewa.



    Kwani Tonny ni kaka yangu au ndugu yangu kwa namna yoyote katika ukoo? Ni kwa nini kila siku akirudi anaishia kuoga, kula na kulala hata asithubutu kunibusu, kunipapasa na hata kuniomba penzi? Ni kipi nilichomkosea hadi afikie hatua hii? Alijiuliza maswali mengi na akakosa majibu.



    Akasonya kwa uchungu.



    *****



    KITUO cha kwanza baada ya Tonny kuondoka nyumbani kwake alfajiri kilikuwa ni katika nyumba moja ambayo haikuwa mbali sana kutoka hapo kwake. Ni katika mtaa huohuo wa Rufiji ambako aliishi Caroline, mmoja wa wanawake waishio mijini wakitegemea pesa kutoka kwa wanaume mbalimbali kwa mikataba maalumu.



    Tonny aliamua kwenda kwa Caroline mapema kiasi hicho ili tu kuyaepuka macho ya wambeya. Na kwa kuwa chumba cha Caroline kilikuwa cha uani, hakupata shida kukifikia. Huko alikaribishwa kwa namna zote zilizomsisimua Tonny.



    Caroline alikuwa ni mwanamke ambaye mwanamume aliyekamilka kila idara na akiwa timamu kisaikolojia lazima akiri kuwa Mungu alifanya upendeleo wa aina fulani wakati akimuumba.



    Urefu wake wa futi tano, akiwa na ule weusi wa kutakata ulimfanya avutie zaidi na hasa ile ngozi yake laini iliyoteleza kama ngozi ya kambare.



    Siyo hiyo rangi tu bali pia mruhusu akutazame; utakiona kitu cha ziada katika tazama yake na itakuwa kama vule anakwambia… ‘nina nyege na wewe…’ Akitabasamu, meno yake meupe yaliyopangika vizuri kinywani huwa ni kivutio kingine ambacho wanaume wengi hujikuta wakishawishika kumfuatilia na wenye bahati, hukipata kile walichokihitaji.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Lakini siyo kwamba Caroline alihitaji kubanwa. Hapana, aliuhitaji uhuru, zaidi ya uhuru wa kawaida. Kwake, kuolewa kilikuwa ni kifungo. Kwa hilo hakuwa tayari, na ndiyo sababu alijikuta akifanikiwa kupata samani mbalimbali za thamani kubwa na hivyo kujikuta akiishi kama binadamu wengine wajisikiao kuishi katika ‘dunia ya kwanza.’



    Alipata kiwanja huko Kibamba na tayari alishajenga msingi wa nyumba ya vyumba vinne. Eneo la Bunju nako alikuwa na kiwanja cha ekari mbili ambazo tayari zilishazingirwa na majumba mawili makubwa ya kifahari na hivyo kukiongezea thamani kiwanja chake kwani kilimezewa mate na wengi wenye pesa za kutakata.



    Mara kadhaa alipokuwa akizungumza na watu aliozoeana nao, akidiriki hata kutaniana nao, aliwaambia, “Kile kiwanja cha Bunju thamani yake si chni ya milioni mia tano, kama mtu huna kafie mbele.” Kauli hiyo ikawa inachukuliwa kama ukweli halisi kwa wale waliokuwa wakikijua kiwanja hicho.



    Na wakati mwingine alidiriki kuropoka, “Usidhani nimevipata viwanja hivyo kwa kumbwelambwela…kha…kiuno kimelipa mwenzangu…na uchafu wote nimefanya ili nipate pesa.



    “Mwanaume wa leo mfanyie vimbwanga vyote halali na haramu uone….shoga, atakupa cheki ya mamilioni usiku huohuo…na ukizidisha manjonjo na mauchafu yote ndo kama hivi…unawezeshwa tu…. hahahahaha…shauri zenu, jitie eti unauthamini mdomo wako…kunyonya, hunyonyi…supu ya bamia hunywi…na eti unaogopa kutukanwa na manesi siku ukienda kujifungua…nyooo utaishia ivoivo…umaskini mpaka kufa…hehehehee haloooo…wewee….mi nina motto wangu mmoja ananitosha na yuko huko kwa mama’aangu” aliwatambia shoga zake.



    Japo maisha yake yalitegemea pesa kutoka kwa wanaume, hata hivyo haikuwa rahisi kwa mtu wa kawaida, mwenye akili ya kawaida kuweza kulibaini hilo. Hakuwa ni mwanamke wa kuchukuliwa na kila mwanamume kirahisi-rahisi; alichagua. Ndiyo, alikuwa akichagua mtu wa kustarehe naye. Na katika uchaguzi huo alijali sifa kuu mbili kutoka kwa mawanamume; sura nzuri, pesa mifukoni na mahiri kitandani.





    Tonny ni kati ya walioipata nafasi ya kustarehe naye kutokana na kuwa na sifa hizo, na zaidi yeye alikuwa na sifa ya nyongeza. Alikuwa ni mwanamume mtundu, mwanamume ambaye alijua kumwandaa mwanamke faraghani. Hakuwa na papara, na ilipotokea ukafika ule wakati muhimu, kwa utekelezaji wa jambo muhimu, Tonny aliudhihirisha umahiri wa uwanamume wake wa sirini.



    Ni sifa hizo tatu, hususan hii ya tatu ndizo zilizomfanya Caroline ajikute akiingiwa na kitu 'kupenda' katikati ya mtima wake. Alianza kumpenda Tonny. Na ni hali hiyo ndiyo iliyomfanya amfungulie tena mlango leo, siku ya tatu, na kumkaribisha kwa namna waliyozoea, wakitumia nguvu na maarifa waliyojaaliwa.



    Hawakuwa watu wa kufanya chochote zaidi ya kuisulubisha miili yao kwa namna iliyowasisimua na kuwafariji. Uchovu ulipowajia waliingia bafuni kujimwagia maji. Njaa alipowasakama, Caroline alipewa fedha akaenda kwenye kwenye baa moja ambako kulisifiwa kwa kuoka kuku wa kienyeji, chips na ugali. Caroline alibeba mlo wa kutosha na uliposhushwa matumboni mwao nguvu ziliwarudia upya. Ikawa ni chumbani, bafuni, chumbani.



    Usiku mchezo ulikuwa huohuo. Lakini leo Caroline alishangaa; Tonny hakuonyesha dalili ya kuondoka.



    “Tonny,” Caroline alimwita huku akimtazama.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walikuwa bado kitandani, mikono ya kila mmoja ikipita hapa na pale mwilini mwa mwenzake.



    Tonny alikuwa mbali kimawazo. Alikuwa akifumba macho na kuyafumbua kwa taabu kufuatia mikono hii laini ya Caroline ilivyopita kitaalamu kila penye chimbo la mhemko na kufanya kile ambacho mwanamume yeyote angependa kufanyiwa na mwanamke mjanja.



    “Tonny,” Caroline aliita tena, safari hii akiwa ameacha kufanya kile alichokuwa akikifanya.



    Tonny alishusha pumzi ndefu na kumtazama kidogo Caroline huku akiachia tabasamu la mbali.



    “Mbona nakuita, huitiki?”



    “Umenikumbusha mbali, mpenzi.”



    “Nimekukumbusha mbali wapi, kwa mkeo?” Sasa Caroline naye aliachia lile tabasamu lake ambalo huwachanganya wanaume.



    “Aaa wapi!” Tonny aliruka. “Umenikumbusha jina ambalo ni'shaanza kulisahau. Ni jina la utotoni.”



    Caroline aliachia kicheko kikali, kicheko cha kimbea-mbea. “Mara ya mwisho uliitwa hivyo lini?” hatimaye alimuuliza.



    “Kabla sijapata mtoto.”



    Kwa mara nyingine Caroline alicheka, safari akiurudisha mkono wake pale kwenye maskani ya maraha ya Tonny na kuanza tena kulishikashika gunzi lile kwa namna ile ile ya kumwehusha mtu.



    “Mbona mimi umekuwa ukiniita tu Caro...Caro kwani sina mtoto? Kwa nini usiniite Mama Betty?”



    Yalikuwa ni maswali yaliyopenya masikioni mwa Tonny kwa usahihi. Alisikia, akaelewa lakini hakuwa na uwezo wa kuyajibu. Caroline alikuwa akiuendeleza uchokozi wake. Alikuwa amekiegemeza kichwa kifuani pa Tonny, lakini sasa alikuwa akizinyonya chuchu kwa utaalamu uliomchanganya zaidi Tonny. Wakati huohuo viganja vyake laini vikizidi kumtia ‘kichaa’ mwanamume wa watu.



    Aliendelea kumtesa Tonny na kumfanya awe akifumba-fumba macho na kuonekana kuwa yuko mbali zaidi kifikra, akikunja na kuikunjua miguu yake.



    Caroline alikuwa mtundu sana katika fani hii. Humo ndani mwake alikuwa na mkanda wa video wa picha za ngono uliochezwa na wasanii wa filamu wa Amerika Kusini. Ulikuwa ni mkanda wenye kila kitu kinachopaswa kufanywa na mwanamume na mwanamke anayependa kufanya ngono kikamilifu.



    Ni mkanda ambao ulimpa ujuzi maradufu Caroline na akaamini kuwa bila ya kujiachia na kutokuwa na kinyaa kamwe hataweza kufanikiwa katika zoezi analotaka kufanikisha. Na aliamini kuwa ni utundu na ubunifu wake wa hali ya juu ndiyo sababu zilizomfanya hata akafanikiwa kimaisha japo bado anaishi hapo Kariakoo akiwa amepanga chumba.



    Kutahamaki saa 6 usiku!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog