Search This Blog

Monday, October 24, 2022

TINGINYA LA BA'MDOGO - 5

 





    Chombezo : Tinginya La Ba'mdogo

    Sehemu Ya Tano (5)



    MANENO haya ya mwisho yalimfanya Lilian agune na kuachia kicheko cha chinichini kisha tena akaupeleka mkono wake mahala Fulani mwilini mwa Sammy ambako ulitomasa kidogo huku kwa dharau akisema, “Hata akijua nd'o atanifanya nini?”



    “Huenda asikufanye kitu lakini huenda akaniua.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nyooo!”Lilian aliwaka. “Hawezi kukuua! Na akikuua na mimi nitajiua!”



    “Kwa nini ujiue?”



    “Kwa sababu nakupenda sana, Sammy wangu,” Lilian alijibu huku akiendelea kutomasa pale mkono wake ulipong'ang'ania. Sauti yake nyororo na aliyoitoa kwa uchovu wa kuigiza, ilikuwa burudani nyingine masikioni mwa Sammy sanjari na kichocheo cha kuyapandisha mashetani yake.



    Akaendelea, “Kwa kweli umeuteka sana moyo wangu, Sammy, na kinachonifanya nikupende hivi nakijua mwenyewe. Kwa ujumla ni kwamba wewe ni mwanamume uliyekamilika.”



    Wakakumbatiana tena. Vinywa vyao vikakutana.Wakadumu kwa takriban dakika mbili katika busu hilo.



    “Mpenzi,” Sammy alimnong'oneza Lilian baada ya kutenganisha vinywa vyao. “Nakuahidi kuwa sitaweza kukusaliti japo wewe ni mke wa mtu. Nakuomba sana usiwe na mtu mwingine zaidi yangu. Tayari umeshatoka nje ya ndoa, lakini usitoke zaidi ya kwangu.”



    “Sina hulka ya ufuska, Sammy,” Lilian alisema huku kakunja uso, akimtazama Sammy sawia. “Kukubali kulala na wewe sio kigezo cha kunihalalisha kuwa mimi ni malaya. Hapo utakuwa umenikosea.”



    “Mpenzi,” Sammy alikuwa mpole.“Sijadhamiria kukukwaza. Kama nimekuudhi naomba radhi. Nilichotaka ujue ni kwamba wewe ni mzuri sana. Una umbo zuri sana na una sura nzuri sana. Kwa hilo hakuna ubishi. Sio mimi peke yangu ninayekuona kuwa una mvuto, hapana. Ni wanaume wengi wanaokutamani. Jitahidi uwaepuke kila watakapokufuatilia.Umenielewa, mpenzi?”



    “Nimekuelewa,” Lilian alijibu huku akiupeleka mkono wake katikati ya miguu ya Sammy na kuuanzisha tena ule uchokozi wake. Kisha, huku akiendelea kukifanya hicho alichokuwa akikifanya, akasema, “Dear, ili utambue kuwa nakupenda, nataka leo twende ukalale kwangu.”



    Sammy alishtuka, mshtuko ulimshangaza hata Lilian kiasi cha kusitisha ule mchezo aliokuwa akiucheza maungoni mwa Sammy. Wakatazamana.



    “Unasema?” Sammy aliuliza kwa sauti ya chini yenye chembechembe za taharuki ndani yake.



    “Nataka leo tukalale kwangu,” Lilian alisisitiza.



    “Hapo sasa unanitafutia kifo cha haraka.”



    “Kwa nini?”



    “Ni hatari. Ni hatari sana mpenzi.”



    “Najua hivyo,” Lilian alisema.“Lakini hebu n'ambie, unanipenda au hunipendi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nakupenda sana,” Sammy alijibu haraka.



    “Basi kama unanipenda uje nyumbani, tukitumie chumba kilekile ninachotumia na Tonny na kitanda kilekile ninachotumia na Tonny. Usiku wote uwe wetu.”



    Sammy alimtazama Lilian kwa makini zaidi na kushangazwa na maneno yake. Akamwuliza, “Kwa nini umeamua hivyo? Na Tonny atakuwa wapi?”



    “Sitaki unikumbushe juu ya laana yule,” Lilian alisema na kusonya. Kishaakaendelea, “Yule sio mwanamume wa maana. Hanifai! Laiti ungelijua...” akaiacha sentensi hiyo ikielea.



    “Mbona unaniweka roho juu? Zungumza kitu kinachoeleweka,” Sammy alisema.



    Lilian alishusha pumzi ndefu na kumtazama Sammy usoni sawia. Uso wake haukuonyesha furaha hata chembe. Ni kama vile kulizungumzia hilo suala ilikuwa ni kulitonesha jeraha la moyo wake.



    “Sikia mpenzi,” hatimaye alianza kusema.“Siku hizi Tonny kahamia kwa mwanamke mwingine ambaye simfahamu. Hurudi asubuhitu, na siku nyingine hata asubuhi haonekani. Vipesa vyake vinamzuzua



    “Kwa hiyo tabia ya kulala huko kwa mwanamke wa nje ni ya kila siku?” Sammy aliuliza kama asiyemwamini Lilian.



    “Sasa nina wiki sijui ya pili simwoni nyumbani usiku. Kila siku niko peke yangu...”



    “Lakini una hakika gani kwamba hatakuja usiku wa leo?”



    “Hawezi kuja!”Lilian alijibu kwa msisitizo. “Mbona hujiamini? Acha woga wewe!”



    Kulinganishwa na mwoga ilikuwa ni udhalilishaji kwa Sammy. Hakuwa tayari kuonekana mwoga. Papohapo akasema, “Siogopi, mpenzi. Kwa hiyo gesti nd'o hatuendi?”



    “Achana na mambo ya gesti. Mambo ya gesti s'o freshi. Gesti hakuna ustaarabu na mijitu inaweza kuwapiga chabo bure!”



    Sammy alicheka.



    “Kweli tena,” Lilian alikazia usemi wake. “Gesti huwa kuna tabia hizo kwa sana tu, na wakati mwingine wahusika ni wahudumu wenyewe wa gesti. We, fanya hivi, kesho uje kwangu. Sawa?”



    “Poa.”



    *******



    TONNY NA CAROLINE

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    MCHANA huu Tonny alikuwa chumbani mwa Caroline akitazama televisheni. Hii ilikuwa ni siku ya tano hajalala kwake. Ilikuwa ni kulala kwa Caroline, asubuhi anakunywa supu na mchana ndipo anakwenda kwake. Jioni ikitinga anaondoka tena na kuja kuponda raha na Caroline.



    Hata ile simu yenye namba ya siku nyingi, ambayo kulikuwa na namba za watu wengi, hakuwa anaitumia hapo kwa Caroline. Alikwishanunua simu nyingine na ikawa na namba chache sana za wale watu aliopenda kuwasiliana nao.



    Muda aliokuwa akitazama chaneli fulani katika televisheni, Caroline alikuwa njiani akirejea kutoka Sinza kwa shoga yake alikokwenda kumjulia hali baada ya kusikia kuwa alikuwa akiumwa.



    Tonny aliendelea kuangalia muziki kwenye televisheni lakini mara usingizi ukaanza kumnyemelea na hatimaye akasinzia. Alishtuka pale aliposikia mkono ukimpapasa usoni. Akakurupuka na kufikicha macho. Kicheko kikali kikasikika. Ndipo alipobaini kuwa Caroline kaingia.



    Akajiweka vizuri sofani na kumwangalia Caroline aliyekuwa kamsimamia mbele yake, gauni la kitambaa laini lenye mistari mieusi na mieupe kama pundamilia likimfanya awe mzuri maradufu.



    Vipi mbona usingizi mida hii?Au njaa?”



    “Siyo njaa baby…ni mambo yako tu…”



    “Mambo yangu gani?”



    “Si jana.”



    “Jana imekuwaje?”



    Tonny alicheka kichinichini. Akakumbuka jinsi Caroline alivyomwambia wakati walipokuwa kwenye baa fulani eneo la Gerezani jana yake. “Leo nataka tukate kiu ya vyote,” ndivyo alivyomwambia wakati Caroline akiwa na bia nne na akionekana kuanza kuchangamka.



    Waliporudi nyumbani, walioga na kujitupa kitandani. Hapo ndipo Tonny alipobaini kuwa Caroline alidhamiria kuikata kiu yake. Alitupa kanga pembeni na kubaki mtupu na kumsogelea Tonny aliyekuwa kajifunga taulo pekee kiunoni. Akamkumbatia na kuigusanisha miili yao. Tonny akahisi msisimko fulani unaofariji. Kitu kikaamka taratibu. Naye akamkumbatia Caroline akiipitisha mikono mgongoni na kuishusha hadi kwenye makalio ambako aliituliza akiyaminyaminya kwa namna iliyomfanya Caroline ajinyongenyonge kama nyoka.

    Mara Caroline akaivuta taulo na kuitupa kitandani.

    Wakabaki tupu wote!



    “Tonny…Tonny…” Caroline aliiita kwa sauti yenye njaa, mkono wa kushoto ukiwa umeshuka hadi kwenye kile kitu alichokihitaji. Akashika kidogo, akaminya kwa pozi, Tonny akahema kwa nguvu. Caroline akaendelea kuminyaminya palepale, kwa mapozi yaleyale huku akihema kwa nguvu, huku kamwegemea Tonny kifuani na kuongeza joto lisisimualo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tonny akamvuta Caroline hadi kitandani. Kitanda kikawalaki. Tonny akawa mwepesi wa kutaka kuuonyesha uanaume wake. Akaushusha mkono hadi katikati ya miguu ya Caroline na kugota palepale alipopakusudia. Vidole vyake vikaanza kutekenya kwa namna fulani. Akachezea na kupachezea. Caroline akazidi kutapatapa.



    Mara Tonny akapanda juu ya Caroline. Mzungu wa nne! Akaenda chumvini mwanaume…. Akawa anafanya kile kilichompagawisha Caroline….mwanamume akautumia ulimi wake kitaalamu kunyonya huku mikono ikiyapapasa mapaja makubwa ya Caroline aliyekuwa kachanua migu kwa raha zake.



    Caroline akagugumia kwa nguvu huku naye wakati huo akiwa ameizamisha kinywa ile ‘kitu’, akifyonza na kumung’unya kama kichaa. Mwanamume akawa anapanda na kushuka kinywani mwa Caroline ilhali Caroline yeye akinengua kwa namna ya kipekee na kumfanya Tonny apenyeze ulimi hadi ndani zaidi na kuzidi kuufanya ‘ukarabati’ kama ‘mwendawazimu mwenye akili’.



    MARA Tonny akapanda juu ya Caroline. Mzungu wa nne. Akaenda chumvini mwanaume. Akawa anafanya kile kilichompagawisha Caroline….mwanamume akautumia ulimi wake kitaalamu kunyonya huku mikono ikiyapapasa mapaja makubwa ya Caroline aliyekuwa kachanua miguu kwa raha zake.



    Caroline akagugumia kwa nguvu huku naye wakati huo akiwa ameizamisha kinywani ile ‘kitu’, akifyonza na kumung’unya kama kichaa. Mwanamume akawa anapanda na kushuka kinywani mwa Caroline ilhali Caroline yeye akinengua kwa namna ya kipekee na kumfanya Tonny apenyeze ulimi hadi ndani zaidi na kuzidi kuufanya ukarabati kama ‘mwendwazimu mwenye akili’.



    Hatimaye walisitisha zoezi hilo. Caroline akamwambia, “Baby, lala chali nami nijilie vyangu…baby…”



    Tonny alitii. Caroline akapanda kifuani huku akimweka katikati Tonny. Akapeleka mkono wake wa kushoto hadi kwenye lile gunzi gumu la Tonny na kulishika, akaliminyaminya huku akimtazama Tonny kwa yale macho yaliyodhihirisha kiu na njaa kali. Kisha taratibu akalilenga palepale alipopakusudia.



    Akashusha pumzi ndefu alipokisikia kitu hicho chenye joto kikipenya katikati ya miguu yake taratibu na kuzua joto fulani lenye burudiko isiyoelezeka kwa urahisi.



    Akaikita mikono kushoto na kulia kwa Tonny na akawa amejiweka katika mkao halisi wa ‘kula.’



    Akashuka taratibu huku akimwangalia zaidi Tonny kwa yale macho yake yaliyochoka na ulimi kautoa nje kidogo akiwa ameung’ata na meno. “Tonny….Tonny…” aliita kwa taabu huku akijizamisha zaidi na kuanza kunengua polepole lakini kwa namna ya kipekee, akionyesha kuwa habahatishi wala hajifunzi. Akamlalia Tonny huku akikibinua kidogo kiuno, akiendelea kunengua na kulitawala lile gunzi lenye joto maungoni mwake, akikandamiza na kuzamisha kitaalamu zaidi.



    Tonny akajihisi hayuko katyika dunia hii. Burudani aliyoipata ikampeleka hadi katika dunia nyingine, katika sayari ya kipekee, akawa akigunaguna kwa sauti nzito na kutamka maneno mazito, akimwagia sifa Caroline na kukisifia kila kiungo chake nyeti huku Caaroline naye akikiita kwa jina kile kiungo nyeti alichokimiliki wakati huo maungoni mwake…akakitaja kila sekunde…

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Caroline aligugumia kwa nguvu huku akizidisha juhudi na akizidi kusisimkwa pale mikono sugu ya kiume ilipokuwa ikiyatomasatomasa makalio yake na hivyo kumwongezea hamasa ya kuendelea kujishughulisha mwilini mwa Tonny. Alikuwa akijikunja na kujikunjua katika namna ya kipekee, miguu kaitanua na kumweka Tonny katikati ya mapaja yake makubwa na kuzidi kujituma kama aliyedhamiria kuua!



    Matiti yake makubwa, yenye uhai, yalikuwa kivutio kingine kwa Tonny kiasi cha kujikuta mara akiyapapasa makalio haya makubwa na laini na mara akiyashika matiti hayo na kuyanyonya.



    “Tulia…tulia…” sauti ilimtoka Caroline kwa shida. “Leo ni zamu yangu…acha nile ninavyopenda….acha nijilie vyangu… ” alibwata huku akimlalia Tonny na kuzidi kunengua huku sasa akipenyeza ulimi sikioni.



    Waliendelea, wakaendelea na kuendelea…kila mmoja akijitahidi kuiridhisha nafsi yake na kumridhisha mwenzake.



    Kama kawaida yao, baada ya zoezi hilo, waliagiza vinywaji na kuanza kufakania na baadaye Caroline alikwenda kununua kuku wa kuoka na viazi mbatata, wakayajaza matumbo yao.



    Lakini ilipofika jioni, Caroline alimwambia Tonny, “Leo inabidi uende baby. Unajua ni siku ya ngapi? Hapana tunafanya dhambi. Usimnyanyase mkeo.”



    Vituko vya Caroline kitandani au hata sofani vilikuwa vimemchanganya sana Tonny. Siku tano hajalala kwake! Kwa kiasi fulani akajisikia kuwa na hatia lakini hakujali, alijali kuufaidi uhondo wa Caroline. Akasema, “Poa, lakini kwa leo tulale. Nitakwenda kesho.”



    “No! Wewe ni mume wa mtu bwana…mimi naiba tu…akha! s’o vizuri, Mungu atanilaani,” Caroline alisema huku akiachia kicheko cha dhihaka. Kisha akaongeza, “Hapana. Itakuwa ni kudanganyana. Utanisumbua-sumbua bure usiku, wakati mwenzio n'na usingizi kibao. Nenda bwana. Leo kampooze mkeo.”



    Saa tano usiku huo Tonny alilazimika kuondoka japo kwa shingo upande.



    *******





    PANGABOI lililoning'inia darini ndani ya chumba hiki cha Tonny na Lilian lilizunguka kwa kasi na kuweza kutengeneza kijiubaridi maridhawa. Ndiyo, kulikuwa na ubaridi wa wastani lakini kwa wapenzi hawa wawili waliokuwa chumbani humo, kitandani, pangaboi hilo halikuwa lolote wala chochote. Miili yao ilitota jasho wakati walipokuwa wakijistarehesha kwa juhudi na maarifa, kila mmoja akitaka kudhihirisha umahiri wake kwa mwenzake.



    Miili yao iling'ang'aniana huku ikipinduana-pinduana, pumzi zikiwa ni nyenzo madhubuti katika kulifanikisha zoezi lao. Walifanya hivi, wakafanya vile kisha na vile tena. Hawakuhisi uchovu, wala hawakuhisi chochote kibaya kinachoweza kuwatokea. Huyu alimnyonya huyu na huyu akamnyonya huyu. Wakanyonyana.



    Kikafikia kipindi ambacho Lilian alibaini kuwa pumzi zilimpungukia Sammy. Huku akiwa amelala kwa staili ya ‘mbuzi kagoma,’ Lilian aliona kuwa kasi ya Sammy haikuwa ya kuridhisha. Kwa mnong’ono ambao uliyafikia masikio ya Sammy kwa usahihi, akasema, “Mpenzi subiri…subiri…toka kwanza…nataka nikukalie… nataka nikukalie baby...”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Pendekezo hili ni kama Sammy alikuwa akilisubiri. Akashusha pumzi ndefu na kujing’atua, kisha akajilaza chali kwenye kitanda hiki kikubwa, cha Lilian na mumewe, Tonny.



    Lilian, mwanamke aliyeumbika vilivyo, akapanda kitandani na kujikita maungoni mwa Sammy, mfano wa mkuna nazi. Ikawa kazi nyingine nzito.



    Ni nani kakwambia kuwa mwanamke mwenye makalio makubwa au mwili mkubwa huwa ni mzito kwenye shughuli hizi? Ni imani potofu. Ukubwa wa makalio au mwili wote hauna uwiano wowote na uwezo wa mtu au utaalamu kitandani, na hilo lilijidhihirisha kwa huyu mwanamke mwenye mwili mng’aavu, mwili mkubwa kiasi, Lilian.



    Naam, Lilian alijua anachopaswa kukifanya na akakifanya! Akajisugua mwanamke…akatoa mlio mdogo kwa mbali kama anayepandwa na mashetani. Alikuwa akikisikilizia kwa umakini kitu hiki kikubwa cha Sammy kilichokuwa lindini, ‘kimtaiti’ kama chuma cha pua. Mara akamlalia kijana huyu wa kiume na kuanza kuzungusha kiuno kwa ustadi zaidi, makalio yake makubwa yakiwa kivutio pale Sammy alipotupa macho kwenye kioo kikubwa kabatini, kioo kilichowachukua kama wako kwenye ‘screen’ kubwa ya televisheni. Akayafinya na kuyaachia makalio hayo kiasi cha kuibua mtikisiko unaosisimua.



    Lilian, ndiyo Lilian alikuwa akimwadhibu Sammy, akimwonyesha kuwa anajua hicho anachokifanya. Sammy akawa akiyapiga makofi ya kimahaba makalio hayo makubwa yaliyokuwa yakipiga mawimbi.



    Lilian aliamua!



    Sammy aliamua!





    *******



    TONNY hakuchelewa kufika kwake. Na alipofika hakutaka kuingia kwa kugonga mlango wa mbele. Aibu ilimfanya asite kufanya hivyo. Akaamua kunyata kwa kupitia uchochoro ili alifikie dirisha la chumba chake na mkewe na huko atamgongea Lilian.



    Alipolifikia dirisha hilo akainua mkono ili agonge, lakini akasita. Hakujua kama mkewe atakubali kufungua au hatafungua. Alijiona mwenye hatia, aliyestahili adhabu. Mwishowe akapiga moyo konde na kuamua kugonga. Ndiyo, agonge na aone kitakachotokea. Yeye ndiye mume! Lilian ni mke!



    Lakini alipounyanyua mkono kwa mara nyingine, bado aliuhisi mkono huo ukiwa mzito. Na hapo ndipo masikio yake yaliponasa miguno na minong'ono ya ajabu huko chumbani. Hakuamini!



    Akahangaika kutafuta upenyo utakaomwezesha kushuhudia hicho alichokisikia kutoka huko ndani. Mapigo ya moyo yakamwenda kasi. Hatimaye akapata upenyo mdogo uliomwezesha kushuhudia hicho alichokuwa akikitafuta!



    Hakuvumilia!



    Alitoka kwa hatua ndefu hadi kwa mjumbe wa shina na kumtaarifu juu ya hali halisi aliyoikuta kwake. Muda mfupi baadaye mjumbe na Tonny walikuwa tena pale dirishani, na mjumbe akashuhudia alichoambiwa na Tonny.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wakachukua uamuzi wa kupitia mlango wa mbele ambao haukuwa umefungwa. Wakaingia taratibu na kukifuata chumba kilicholengwa. Na mlango ule wa chumbani pia ulikuwa umerudishwa tu, hali iliyowarahisishia mjumbe na Tonny waingie bila pingamizi lolote.



    Wakawakuta Sammy na Lilian wakiwa katikati ya starehe yao. Roho ikamuuma sana Tonny. Akamtazama Lilian kwa hasira. Macho yao yalipokutana, Lilian alitabasamu, kisha akamuuliza, “Vipi, mkuki kwa nguruwe, je, kwa binadamu?”



    Maneno hayo yalipenya masikioni mwa Tonny na kutua moyoni mithili ya kaa la moto. Aligeuka na kutoka asijue wapi anakokwenda. Hakwenda kwa Caroline, lakini hakurudi kwa mkewe.

    Hakuna aliyekumbuka kumfuatilia wakati akitoka. Kila mtu aliwastaajabia hawa wafumaniwa!



    Kama siyo uamuzi wa mjumbe kuwataka watu waondoke, huenda ingekuwa ni nhabari nyingine. Wengi walitaka wafumaniwa wachukuliwe hatua kali, lakini mjumbe akatoa kauli, “Mwenye mali kaondoka. Nimekuja naye na kaniacha, yeye kaondoka. Ni ya Ngoswe, tumwachie Ngoswe.

    Siku ya pili zilipatikana taarifa za mwili wa mwanamume uliokutwa ndani ya chumba cha hoteli moja hapohapo Kariakoo, ukiwa umeanza kuharibika. Kando ya mwili huo kulikuwa na vidonge kumi vya Quinine na Vallium. Chupa ya maji ilikuwa juu ya meza. Kinywani kulikuwa na baadhi ya vidonge hivyo ambayo vilikuwa havijashuka kooni.



    Tonny alijiua!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    MWISHO

0 comments:

Post a Comment

Blog