Search This Blog

Monday, October 24, 2022

NILAMBE TENA - 5

 





    Chombezo : Nilambe Tena

    Sehemu Ya Tano (5)



    Mbele yangu alisimama Lina tumbo lake kubwa kuashiria alikuwa mjamzito. Nikabaki kuduwaa kwasababu ile miaka aliyoisema kukaa huko Florida, ilikwa bado haijakamilika. Lakini sikutaka kumtoa katika furaha kwa wakati huo. Nikamchangamkia kwa kumkumbatia lakini hakunionyesha upendo kama wa awali. Kiasi nilistaajabu kwakuwa hakuwa Lina niliyemsindikiza uwanja wa ndege.

    “Kuna tatizo?” nilimhoji lakini badala ya kunijibu akaanza kulia kilio cha kwikwi. Kama dakika tano alizitumia kulia huku nikijitahidi kumbembeleza japo haikuwezekana.

    “Ni kwanini hukunielewa maana yangu kukuuliza uhusiano wako na mama yangu? Kwanini ulishindwa kuwa muaminifu? Ulidhani nisingerudi nchini na wewe kuendelea kuufaidi mwili wangu ambao haujawahi kuguswa na mwanaume mwingine? Kwanini huna fikra kabla ya kuamua?” aliniporomoshea mvua ya maswali ambayo yalianza kunitia hofu moyoni mwangu na kunisababishia baridi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Endelea kuyafurahia maisha huku mimi nikiutesekea ujauzito wako.” Baada ya kusema hivyo, aliondoka na kuniacha nikiyatafakari maneno yake. Nilichokifanya ni kuelekea kituo cha afya. Nikapima afya yangu ambapo ilikuwa salama. Sikuridhika na vipimo vyao. Nikaelekea kwingine nako vipimo vikadhibitisha afya yangu ni salama. Moyo wangu ukalipuka kwa furaha baada ya kuona kile alichokuwa akikiwaza Lina sicho. Nikarejea nyumba kwa furaha na kuinyanyua miguu yangu juu ya kitanda huku nikicheka. Nikajaribu kumpigia simu Lina ilia je kujionea vipimo vyangu lakini hakuwa akipatikana. Nilirudia mara kadhaa lakini jibu lilikuwa ni lilelile. Majira ya jioni mama yake alikuja nyumbani kwangu. Hakuzungumzia habari za Lina wala hakuonekana kujishughulisha nazo.

    “N’na kiu?” ndivyo alivyoniambia.

    Nikachukua glasi na kumuwekea maji kisha nikampatia. Yale maji yalikuwa ya baridi sana. Akanywa funda moja na kurudisha mezani. Si kwamba sikuelewa maana yake bali ni katika hali tu ya utani. Alivyoirudisha mezani nami nikaichukua na kuweka funda moja kinywani. Sikulimeza. Nikalihifadhi wakati huo akianza kunipapasa. Nikamvua nguo na kumlanza chini haraka maana yale maji yalichokuwa yakinifanya kinywani ni siri yangu. Nilichokifanya baada ya kumlaza, niliyamwaga maji yale mgongoni mwake kwa staili ya kushuka na kumfanya ahisi hali tofauti kimsisimko. Ni kitu ambacho hakukitegemea pengine huenda hakuwahi kufanyiwa hapo kabla. Akageuka na kunikumbatia. Nami nikamkumbatia na kuzishika chuchu zake zote kwa pamoja. Moja nikaitia kinywani mwangu na nyingine nikawa nikiipikicha kwa vidole vyangu. Akaanza kulalamika kwa sauti ya juu kuashiria utamu umemzidi uwezo. Nikazidisha kwa kuhamia masikioni mwake. Nikaanza na sikio la kushoto kwa kutumbukiza huko ulimi wangu. Nikaanza kulilamba huku mkono wa kulia ukicheza na chuchu zake.

    “Inatosha nipe ba-aa-si-ii-I” aliongea katika hali ya kutia huruma. Nikaanza kumpa raha. Yale maneno ya Lina nikayasahau. Sikutaka kuyapatia nafasi kwa kuona alikuwa akinitisha tu. Kuona pale chini hapanifurahishi, nikamuahamishia juu ya sofa. Akaweka mguu mmoja juu ya mkono wa sofa na kunipatia nafasi ya kuifaidi tamu yake bila tabu. Ikawa ni raha ndani ya raha. Akaanza kugugumia kwa nguvu huku akionesha kunikadamiza. Dalili za kufika kilele lakini kabla hajamaliza safari yake, mlango ukasukumwa akaingia Lina. Aisee ndugu mfuatiliaji wa hadithi hii, nilishindwa kuuchomoa uume wangu kwa jinsi mama Lina alivyokuwa amenibania kifuani mwake huku akiachia mapaja yake ili niweze kumpatia kile kilichokuwa kikimsababisha agugumie. Lina akabaki kuduwaa asijue la kufanya. Akajitwisha mikono yake asiamini kile kilichokuwa mbele yake akikitizama kwa macho yake yote mawili.hadi hapo mama yake bado hakuwa amemuona mtoto wake kutokana na kuzidiwa na raha. Wakati hali ile ikiwa bado namna hiyo mara akaingia mtu mwingine ambaye huyu hakuwahi kufika pale japo haikuwa mara moja wala mbili kufanya naye mapenzi. Huyu ndiye aliyeonyesha kuyabadili maisha yangu lakini hali aliyokutana nayo hakuamini. Alikuwa mke wa Mzee Abas au Clara. Nilichokishuhudia ni kuwaona watu wawili wakishuka chini kwenye sakafu kama mizigo. Hapo ndipo mama Lina akashtuka lakini wakati huo tayari alishamaliza haja yake bila ushirikiano wangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nd’o nini hiki?” aliniuliza kana kwamba hakuwa akiona ni nini kipo mbele yetu. Haukupita muda Lina akaanza tokwa na mapovu mdomoni hali iliyozidi kunitisha. Nikavaa nguo zangu na mama Lina akavaa za kwake. Nikambeba Lina hadi kwenye gari lake ili kumuwahisha hospitali. Nikarudi nadani kumchukua Clara ili kwa pamoja naye apelekwe hospitali. Nikapishana na mama Lina mlangoni akitoka nje. Nikaingia ndani na kumbeba Clara lakini nilipotoka nje mama Lina alikuwa akiondoa gari kwa kasi na kuliacha la kwake. Bahati mbaya sikuwa nikifahamu kuendesha gari. Nikabaki kumlaani na kumlaumu kwa kitendo chake hicho cha kinyama. Ikanibidi kukimbia hadi barabarani na kukodi bajaji. Haraka tukampakia huku wapangaji wakinisikitikia kwa jambo lile. Sina uhakika kama walielewa nini kilitokea. Na laity wangelitambua ni kipi kilitokea wala wasingelithubutu kunihurumia. Nilikuwa zaidi ya mchavu nyuma ya mgongo wangu.

    Mwanadamu huyatenda mengi kwa kiburi na madaha lakini mwisho wake huwa ni siri. Hakuna anayetambua lililo mbele yake. Uringe katika nafasi yoyote haijalishi. Ni ndani ya bajaji kuelekea hospitali huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio. Kadri sekunde zilivyokuwa zikisogea, ndivyo mapigo ya moyo wake yalivyokuwa yakizidi kushuka hali hiyo ilinitisha na kunifanya nianze kufikiria kumwambia dreva bajaji asimame ili nitoe fedha katika m pesa lakini lengo langu likiwa si hilo bali kukimbia na kwenda mbali kwasababu hali ilivyoonekana, nilikuwa nikikaribia kuogelea katika kisiwa cha matatizo. Nilikuwa nikiishi Majengo hivyo ulikuwepo mwendo mrefu kiasi hadi kufika hospitali ya Seliani. Huwa najiuliza hadi leo hii. Nafikiria na kujaribu kurudisha kumbukumbu lakini huwa sipati picha kamili ilikuwaje niko hai hadi leo hii. Ni katika hali ambayo wote hatukuitarajia. Ghafla daladala moja iliyokuwa katika mwendo kasi kutaka kuipita daladala nyingine ikatupamia. Ile hofu kusababisha mshtuko nilijikuta nikizimia. Sikujua kilichoendelea hadi pale niliposhtuka na kujikuta nipo hospitali na mirija zaidi ya miwili ikiwa mkononi mwangu. Niliangaza huku na kule ndani ya chumba kile cha hospitali na kuona wagonjwa kama mimi wengi wao wakiwa wamekatwa miguu yao. Nilistaajabu na ndipo nikakumbuka ajali niliyoipata. Hamu yangu kubwa ikawa ni kujua hali ya Clara pamoja na Lina. Lakini ningeanzia wapi. Sikujua ni wapi alipelekwa na mama yake ivyo ingekuwa ni vigumu kwa wakati ule labda mpaka nikitoka hospitali. Nikainuka ili kujua kama angalau ninaweza kutembea. Hakika msomaji nilijikuta yakinibubujika tu pasipo kutegemea. Niliyaacha yatoke kwakuwa hayakuwa mategemeo yangu. Sikuhangaika kuyafuta.



     Sikuhangaika kuyafuta. Nililia kwasababu sikuwa na miguu tena. Nisingeweza kutembea tena pasi na nyenzo. Ama kwa hakika nililia kilio kisichokuwa na mbembelezaji. Kila tone la chozi lilipodondoka, fahamu zangu zilikuwa zikinirejesha nyuma na kuyakumbuka mengi. Jinsi nilivyokuwa nikipita katika mitaa mbalimbali kutafuta riziki na kila aliyejipendekeza sikumchelewesha.

    “Maskini mimi!” Nilijisemea lakini nikasikia sauti ikinijibu.

    “Usihuzunike kwa kupoteza viungo vyako bali shukuru kwa maisha yako kunusurika. Wenzako tayari wanaliwa na mchanga. Bora wewe uliyepoteza fahamu kwa wiki moja.” Nilishtuka sana kwa maneno ya daktari alivyoyanena huku akitabasamu. Kumbe dreva wa bajaji pamoja na Clara mke wa Mzee Abasi walipoteza maisha. Nikaikumbuka safari yetu ya Mwanza na jinsi alivyokuwa akinirushia maji ndani ya Malaika beach.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ‘Eee! Mungu wangu! Kwanini hivi?” nilijikuta nikitamka kwa sauti bila machozi kukauka machoni mwangu.

    “Machozi ni mateso ya macho wala si kufariji maumivu ya moyo” Aliongea dokta na kutoka. Sikupata nafasi ya kuongea naye siku hiyo japo nilitamani kujua mengi na vipi nitalipa gharama za pale hospitali kwasababu hakuna yeyote ambaye angeweza kunilipia. Nilihisi unyonge usioelezeka.

    “Pole.” Hiyo ilinifanya kuzinduka katika lindi zito la mawazo. Nikageuka na kuangalia ni nani aliyenipatia pole ile. Alinikuwa ni nesi lakini wala hakujishughulisha na mimi pamoja na kunipatia pole ile. Sikuona sababu ya mimi kuwa kimya.

    “asante.” Lakini hakuongea lolote. Akampatia huduma ya dawa mgojwa aliyekuwa kitanda cha tatu kutoka cha kwangu kisha akatoweka. Nilikaa pale hospitali kwa muda wa mwezi mmoja pasipo kuonana na mtu ninayefahamiana naye.

    ‘Kuna mgeni wako.” Nilishtuliwa na mmoja wa nesi. Nikaongozana naye hadi nilipotakiwa kuonana na mgeni aliyekuja kunitembelea. Ajabu mtu niliyeambiwa ni mgeni wangu sikumfahamu. Nilipofika nikamsalimia naye akaniitikia kisha akanisaidia kusukuma ile wheelchair niliyokuwa nikiitumia akanitoa hadi nje tayari kwa mazungumzo lakini wakati huo moyo wangu ukinienda mbio.

    “wewe ni nani?” nilimuuliza.

    “Mimi ni mwema kwako na nimeagizwa nije kukuchukua ila siwezi kuharibu kazi yangu kwasababu makubaliano yetu na muajiri wangu ni kutokukwambia ni nani aliyeniagiza. Ila tu unachotakiwa kuamini ni kwamba upo katika mikono salama.” Aliniondoa hofu wakati huo akinifikisha pale alipokuwa ameegesha gari lake. Kiasi hofu ikanipungua na mapigo yangu ya moyo yakapungua. Kama alivyonisukuma, akanipandisha na kukirudisha kile kiti hospitalini. Sikushangaa hilo kwasababu ndani ya gari kilikuwemo kingine tena kizuri. Hakuchukua muda, akarejea na kuingia ndani ya gari. Akaliwasha na safari ikaanza. Aliendesha gari kwa kasi na kusababisha ule uoga uliokwishatoweka unirudi tena. Pamoja na mwendo wake kuwa wa kasi, sikuthubutu kuongea chochote. Baada ya mwendo usiokuwa wa kuchosha, alisimama mbele ya geti rangi nyeusi na kupiga honi. Geti likafunguliwa akaingiza gari ndani na kupaki. Akateremka na kunifungulia mlango kisha akanikunjulia wheelchair nikapanda juu yake akanisukuma kuelekea ndani. Kitendo cha kufungua mlango vikasikika vigelegele na mbele ya macho yangu nikamshuhudia Linda akivishwa pete na mwanaume wa mzungu. Hakuwa na mimba niliyomuona nayo. Nilistaajabu. Hali niliyojisikia pamoja na moyo kunienda mbio, ilinifanya kupata mshtuko ulionipelekea kupoteza fahamu. Kilikuwa ni kitendo kilichoniumiza roho mno. Sikukitegemea kutoka kwa Lina.

    “pole sana rafiki yangu. Maisha ni mapito lakini ikiwa utapata upenyo wa kupita ili kujikinga na mapito yasiyokuwa ya lazima, usikubali kuuachia upenyo huo. Rafiki yangu ulijisahau sana ilihali ulitambua fika Lina alikuwa akikupenda.” Alikuwa ni rafiki yangu Sam. Nilikuwa ndani ya chumba changu juu ya kitanda.

    “Nani amenileta hapa?” Umeletwa na marafiki zake Lina hadi nje nikakuingiza ndani. Kumbe sikuzimia muda mrefu lakini angalau kwa huruma wangenipeleka hata hospitali.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ni kweli rafiki yangu lakini alichonifanyia Lina sitakisahau.” Nilimwambia huku nikilia lakini naye hakusita kunikumbusha kile nilichomfanyia Lina hadi nikashangaa aliyajua vipi ilihali hakuwepo. Tuliongea mengi na jinsi alivyosimuliwa mambo yote na Lina na mwisho akaniambia kuwa Lina alikuwa bado akinipenda. Sikulitia moyoni kutokana na kile alichokuwa amenionyesha. Ilikuwa ni zaidi ya dharau. Sikuhitaji tena mateso ndani ya Arusha. Nikasafiri kimyakimya hadi Mwanza katika nyumba niliyopewa zawadi na Clara kabla ya kifo chake. Nikayaanza maisha yangu mapya huku nikiepukana na wanawake.

    **

    Miaka miwili tangu nianze maisha mapya jijini Mwanza.

    Ilikuwa ni jumamosi tulivu majira ya jioni nikiwa ziwani nikiyatizama mawimbi yalivyokuwa yakiyumbayumba. Fikra zangu zilikuwa mbali mno hasa nikiyakumbuka maisha yangu ya hao awali nay a wakati huo.

    “Nahitaji kuoa.” Nilijisemea huku nikiyachezea maji. Ni kweli nilihitaji kuoa ili kujenga familia. Tayari nilikuwa nikijiweza kutokana na mazingira aliyonitengenezea Clara pamoja na kujituma kwangu. Nikamkumbuka dada mmoja ambaye alikuwa akija mara kwa mara dukani kwangu huku akipendelea sana utani na mimi na hata wakati mwingine kunisukuma.

    “Ananifaa.” Nilijisemea na kusogea karibu na gari langu. Nikaingia na kutoweka mahali pale. Zilipita takribani wiki tatu pasipo kumuona dada yule ambapo tayari nilishajenga nia juu yake. hivyo hisia zikaanza kunituma vibaya. Nikazidi kuvumilia lakini nikashindwa ikanibidi kumuweka wazi rafiki yangu mmoja juu ya jambo lile.

    ‘Cha msingi ni kutafuta ni wapi anaishi au ni wapi anafanya kazi. mbona itakuwa rahisi tu.”

    “Kaka tatizo sifahamu pa kuanzia kwasababu sina mawasiiano naye.”

    “Kazini kwako unao wafanyakazi wa kike na sidhani kama waweza kukosa hata mmoja mwenye mawasiliano yake.” Kidogo alinitia matumaini. Nikaanza kuhangaikia ushauri wa rafiki yangu. Bahati nzuri nikafanikiwa kupata mawasiliano yake. lakini nilipopiga namba haikuwa hewani. Nikadhani labda ni kwa siku hiyo peke yake lakini haikuwa hivyo. Nikaanza kukata tamaa kidogokidogo na hatimaye nikakata kabisa na kukosa matumaini.

    Ni majira ya usiku nilipofungua luninga na kuweka chanel ya Star Tv kutizama taarifa ya habari. Haikuwa kawaida yangu ila nadhani Mungu alitaka kunionyesha yeye ni ndiye mleta furaha na huzuni. Sikuamini aliyeonekana akisoma taarifa ya habari. Alikuwa yuleyule aliyenifanya nikose usingizi na kupoteza matumaini. Sikuangalia tena. Nikazima tv na kulala kwasababu furaha ilirejea ghafla. Kumbe alikuwa mtangazaji katika kituo kile kikubwa cha tv.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilipanga kwenda hadi nje ya jengo lao la utangazaji ili wakati akitoka nipate nafasi ya kuzungumza naye. Lakini kabla sijafanya hivyo, kesho yake majira ya mchana alikuja kazini kwangu. Sikumchelewesha. Nikamuelezea nia yangu lakini hakunikubalia zaidi ya kuniambia tutembeleane kwanza ndipo yatafuata mengine. Nikakubali. Akaanza kuja kwangu na ilipofika siku ya kwenda kwake, akaniweka chini na kuniambia, “Ukikubali kusamehe utakuwa huru kila wakati. Usikubali kukosa amani kwa makosa ya mwanadamu aliyokutendea nyuma. Usishindwe kutengeneza maisha kwasababu ya kuwaza kilichotokea nyuma. Kile kinachomtokea mwanadamu kina chanzo na sababu zake. Mimi nakupenda ila yupo anayekupenda sana na kila siku huwa haipiti bila kukuona pasipo wewekutambua. Kumbuka waweza kukosewa na chanzo cha kosa ikawa ni wewe.” niseme ukweli sikumuelewa kwa wakati ule. Wala sikutaka kumhoji hata swali la uzushi. Tukaongozana hadi nyumbani kwake. Ujue nini msomaji wangu, baada ya kucheka ni huzuni au baada ya huzuni ni kucheka. Ndiyo maana hata mimi mwanzo wa chombezo hili nilianza na AAHHH ooooohhh ashhhh. Lakini mwisho tunamaliza na huzuni pamoja na kicheko. Aliyetufungulia mlango hakuwa mwingine bali ni Lina. Akiwa nan a mtoto wa kiume pembeni tena amesimama. Akaniita baba. Ujue niliduwaa si kidogo. Nilishindwa niseme nini. Lina akanisogelea na kupiga magoti kisha akanikumbatia na kuanza kulia. Mtoto akatusogelea na kutuinamia. Sikuongea neno lolote zaidi ya kulia. Kadri nilivyokuwa nikilia ndivyo na hasira zilikuwa zikiniondokea. Lina hakuwa na mahusiano na yule mzungu bali alifanya vile kunihuzunisha kama mimi nilivyomhuzunisha.

    “Mama yangu ameshatangulia. Naomba unipe furaha tu na siyo kingine.” Aliniambia Linda wakati huo mtangazaji wetu Belinda akitabasamu tu. Nikamfurahia Lina naye akanifurahia. Tukapeane furaha. Belinda akaondoka na mtoto wetu na kutuacha. Haoo tukaingia chumbani. Na vibingu vyangu vya miguu lakini wee nikamvua nguo Lina. Nikapeleka ulimi wangu juu ya uke wake. Nikaanza kuulamba kwa fujo huku nikizipa tabu chuchu zake kwa kuziminya. Mkono wangu wa kushoto nao haukuwa mbali na mapaja yake. nikawa nikiyapapasa na kumfanya aanze kutokwa na machozi ya raha. Hutaki au?? Sikuwa nimempa utamu siku nyingi. Nikahakikisha namnyonya uke wake hadi akamaliza kwa kukunja vidole vyake.

    “Asante baba James. Nitakupenda mpaka siku ntakayokufa.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nitakulinda pia mpaka siku ya kufa kwangu.” Nami nilimjibu wakati huo akinipanda na kuushika uume wangu kisha kuanza kuupitsha juu ya kine… chake. Basi niseme ikawa raha juu ya raha. Hasira zikawekwa kando.

    Labda kama ni katika safari nyingine tena. Hii imefika tamati. Nikuombe radhi pale ambapo hukupafurahia msomaji wangu. Katika safari nyingine sitajikwaa ili kukukwaza. Sawa msomaji wangu mpendwa????

    ‘Furaha ni watu kamwe hakuna furaha pasipo watu. Kujitenga na watu kisa dharau ni kujiandalia mwisho mbaya wa maisha yako.”



    MWISHO.!!!!!

0 comments:

Post a Comment

Blog