Search This Blog

Monday, October 24, 2022

GUBERI LA KIMANYEMA - 1

 





    IMEANDIKWA NA : INNOCENT A. NDAYANSE (ZAGALLO)





    *********************************************************************************



    Chombezo : Guberi La Kimanyema

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    ALIPOCHEKA, alipendeza. Tabasamu lake zuri, tabasamu linaloshawishi na kusisimua, huwafanya watu hususan wanawake, wamsogelee na kumsalimia. Baadhi ya wanawake hao husisimkwa miili pindi tu waisikiapo sauti yake. Alikuwa na sauti ya kipekee, sauti iliyogusa hisia zao na kuamsha gharika la maraha kwenye michipuo ya fahamu zao.

    Alikuwa ni kijana wa kiume, mwenye sura ya ucheshi na macho ya upole. Hakuwa mwoga wa kutazamana na mtu, lakini hakupenda kutazamana na mwanamume mwenzake. Kwake, macho ya mwanamume mwenzake yalikuwa na kitu asichokijua, kitu kisichopendeza.

    Hali hiyo ilikuwa kwa wanaume tu, siyo kwa macho ya wanawake. Aliyapenda macho ya wanawake na ilipotokea akakutanisha macho na kiumbe yeyote wa kike, katu hakuyabandua macho yake. Ndani ya mboni za mwanamke yeyote kulikuwa na kitu fulani kisichoelezeka, lakini kilichomvutia na kumsisimua.

    *****

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ALIPOZALIWA wazazi wake walimpa jina la Maftah, jina ambalo baada ya miaka kadhaa lilipotea na kuzaliwa kwa jina jingine, Kiwembe, ambalo alipachikwa kutokana na yale ayapendayo na ayatendayo, yale aliyokwishayageuza sheria badala ya kawaida.

    Ni katika kitongoji cha Ujiji mjini Kigoma ambako Kiwembe alizaliwa. Wazazi wake walikuwa na nyumba katika Kata ya Kasingirima, na katika ndoa yao walibahatika kupata mtoto mmoja tu, huyo Kiwembe.

    Kiwembe hakubahatika kufaidi vilivyo malezi ya baba na mama. Mwaka 1978 mji wa Kigoma ulitikiswa na maradhi ya kipindupindu, maradhi yaliyowakumba wakazi wengi, na wengi wao wakafariki dunia. Wazazi wa Kiwembe walikuwa miongoni mwa waliofariki kwa maradhi hayo. Walimwacha Kiwembe akiwa na umri wa miaka kumi na miwili.

    Mzigo wa kumlea mtoto Kiwembe ulihamia kwa mama yake mdogo ambaye aliishi mtaa wa tatu kutoka kwao Kiwembe. Hayakuwa maisha yaliyostahili kwa mtoto wa rika la Kiwembe. Huyo mama yake mdogo hakujali kuwa Kiwembe kala nini au kama anahudhuria masomo ipasavyo. Hivyo, mara nyingi Kiwembe akawa anazurura mitaani.

    Akiwa ni mtoto ambaye alijaaliwa kukua harakaharaka, Kiwembe alikadiriwa na wengi kuwa ana umri wa miaka kumi na minane au ishirini.

    Ni umbo lake hilo kubwa ndilo lililomfanya Mama Kadala wa mtaa wa pili amtazame mtoto wa watu kwa macho yenye kila dalili ya njaa dhidi yake. Mama huyo aliyekuwa na umri wa kutosha kuwazaa akina Kiwembe wengine kama watatu, hakuwa mtu wa kujali eti huyu ni kijana aliyekwishabalehe au bado.

    Alichopenda yeye ni ‘kupakata dogodogo.’ Na baada ya kumwona mtoto Kiwembe akiwa hana uangalizi mkubwa, akaamua kumwinda taratibu. Jimama hilo tipwatipwa likawa haliishi kujipitishapitisha jirani alikoishi mtoto Kiwembe.

    Jimama hilo lilimpenda Kiwembe na likawa tayari kufanya jambo lolote na mtoto huyo potelea mbali hayo matokeo yake yatakavyokuwa. Na hata kama matokeo hayo yatakuwa ya kumfedhehesha, hakujali. Aliapa kuwa ni lazima ‘aanguke naye kisahani.’

    Ndipo ikaja siku ambayo Kiwembe alijikuta akiingia kwenye anga za Mama Kadala. Walikutana njiani, saa 12 jioni, Mama Kadala akamwomba Kiwembe msaada wa kumbebea kijifurushi kidogo hadi kwake. Kilikuwa kijifurushi kilichosheheni vitunguu, nyanya na vikorombwezo vingine vya kutayarishia mboga.

    Kiwembe hakuwa na hiyana, kwa heshima zote akamsaidia mama huyo mzigo huo mdogo hadi kwake. Ni hicho alichokihitaji mama huyo asiyejua soni au heshima ni kitu gani.

    “Karibu Kiwembe,” Mama Kadala alisema huku akimtazama Kiwembe kwa macho yaliyoongezwa utaalamu wa kutazama kimapenzi.

    Umri wa Kiwembe haukuwa wa kumfanya aweze kutambua kuwa Mama Kadala ana maana gani kumtazama kwa namna ile. Yeye alitii ile ‘karibu’ kwa kuingia na kijifurushi kile hadi ndani na kukitua sebuleni

    Hapo Mama Kadala akavuta kigoda na kumkabidhi Kiwembe kisha naye akavuta kingine na kujibweteka puu!

    Wakatazamana.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ukaaji wa Mama Kadala ukampeleka mbali kimawazo mtoto Kiwembe. Akazidi kumkodolea macho jinsi alivyokuwa ameketi pale kwenye kigoda; kiti kidogo cha jikoni. Alionyesha kushangaza mama huyo jinsi alivyokaa huku tako moja tu likiwa limekijaza kigoda kile, tako jingine likiwa kando, kama vile likining’inia.

    Jimama la nguvu!

    Jimama tipwatipwa!

    Ndiyo, Mama Kadala alikuwa amejaaliwa umbo kubwa na teketeke, umbo jeupe, lililonawiri na kunang’anika. Kwa ukubwa wa umbo lile, alionyesha dhahiri kuwa anakionea tu kigoda kile. Lakini yeye hakujali wala hakukihurumia. Alianza kutayarisha mlo huku wakiwa hapohapo, uso kwa uso na mtoto Kiwembe.

    Mama Kadala akazidi kuchuchumia na kukifanya kile kitenge alichojifunga mwilini mwake kianze kuuachia wazi mwili kutokana na hekaheka za mwiko na sufuria. Wala hakujali Mama Kadala, kwamba yule mtoto anamkodolea macho.

    Zaidi, alijiachia kwa uwazi, labda akitaka mtoto huyo akishuhudie kile anachosikia au ambacho aliwahi kukisikia. Mama mtu mzima huyo hakujali kuwa macho ya mtoto Kiwembe hayakuwa na pazia. Yeye aliithamini ile methali isemayo “MTOTO USIYEMZAA NI MKUBWA MWENZIO…”

    Ni ile nguo pekee, ndogo, laini ya ndani ndiyo iliyomkinga na macho ya Kiwembe, asione vyote. ‘Sukari ndani, sukari nje!’ Lakini macho ya Kiwembe yalikuwa shahidi wa yote, yakaona kisichostahili kuonwa.

    Punde Mama Kadala aliuachia mwiko ule, akashika sehemu ya pindo la kitenge alichojifunga, akajipangusa jasho usoni. Kitendo hicho kilimfanya awe mtupu, kama aliyedhamiria kumuumbua mtoto wa mwenzie.

    Macho ya Kiwembe yalitazama kwa ukomo wa fahamu zake. Akayatembeza macho hayo taratibu, kutoka kwenye unyayo wa mama yule, unyayo uliokolea hina, akayapeleka hadi kwenye shina la mapaja; alichokiona hapo akakiundia taswira isiyoelezeka wala kueleweka akilini mwake. Akahisi ibilisi akimnyemelea kichwani. Kizunguzungu kikamvaa ghafla.

    Fahamu zikamtoka!

    Alizinduka muda mrefu baadaye, usiku ukiwa umeshaingia. Akajikuta kalala kwenye kitanda cha Mama Kadala, mwenzi wake katika kitanda hicho akiwa ni yuleyule Mama Kadala, na wote wakiwa tupu kama walivyozaliwa, wamejifunika shuka moja!

    “Haa! Mama Kadala! Hapana! Unaniwangia Mama Kadala,” Kiwembe alinong’ona kwa sauti iliyoonyesha woga. Akakurupuka kutoka, hakuweza.

    “Tulia…tulia mtoto…tulia mtoto mzuri,” Mama Kadala alimbembeleza huku akimkumbatia na kumpapasapapasa. “Tulia, usihofu… wasiwasi wa nini?”

    Kiwembe akaishiwa kauli. Na huo ukawa mwanzo wa kijana mdogo, Kiwembe kulijua penzi. Tangu siku hiyo penzi lao likawa penzi la siri. Siri ikawa siri hadi siku alipojikuta akibalehe kifuani pa Mama Kadala, mwanamke mwenye mwili mkubwa, asiye na haya wala staha.

    Wakazidi kupendana. Kiwembe akapikiwa ‘wali wa tako moja na chai ya maandazi ya sukari ndani, sukari nje’ na michuzi ya mapaja wazi. Ujiji ikamfanya mtoto Kiwembe abalehe kabla ya wakati!

    *****

    “UNAUMWA?”

    “Hapana, siumwi.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa ujumla hata yeye mwenyewe alishangaa, kipi kilimchanganya hata ashindwe kula? Kama ni mpunga uko shamba, kuulima hawezi, lakini akiuhitaji anaupata. Mchele uko kwenye ungo, ukipepetwa na kuchaguliwa chuya, kisha ukapikwa, ukaiva, basi ndio huo unaoitwa “wali.” Na sasa wali huo ndiyo ulikuwa umepakuliwa, umo ndani ya sahani pale mezani. Kijiko anacho, vipi ashindwe kula? Badala yake kaduwaa, msichana mrembo wa rika lake akiwa mbele yake akimhimiza kula.

    Tangu abalehe, mawazo yake yote yako kwenye mapenzi tu. Kila akifikiriacho ni mapenzi.

    “Kula basi jamani, mbona huli?” alihimizwa tena. Lakini bado hakufanya kitu. Badala yake aliunyanyua uso na kumtazama msichana huyo mdogo na mwenye mvuto mkali. Akamtazama kwa haya kidogo.

    “Kwani unaumwa?” msichana aliuliza tena. Kisha akaongeza, “Pole basi ka’unaumwa.”

    “Mmmh!Hapana, siumwi,” Kiwembe alijitahidi kuipata sauti yake. “Ni wewe tu ndiye unipaye maradhi. Naamini mtoto mzuri kama wewe ndiye chanzo cha maradhi niuguayo. Sura yako na umbo lako ndivyo vinavyonifanya nipate hamu ya kustarehe na wewe. Tafadhali…”

    Alikipa uzito kila alichokitamka. Kinywa kilitamka, sauti ikaghani, macho yakasihi na mikono ikashawishi alipokuwa akilitomasatomasa bega la Sharifa, mtoto wa Mama Kadala.

    Kiwembe alizidiwa na kiwango cha matamanio hata akashindwa kujizuia. Akatamani penzi kila wakati. Penzi la Mama Kadala likawa halitoshi, penzi la usiku kwa usiku. Mchana kutwa Mama Kadala hushinda kwenye biashara zake za ‘mama lishe.’

    Na hapo nyumbani hushinda Kiwembe na Sharifa, peke yao! Sasa Kiwembe anahofia nini ilhali alishagundua kuwa hata Sharifa mwenyewe anamtamani? Kiwembe hakuisahau ile siku ambayo Sharifa alimwingilia chumbani wakati kajipumzisha kitandani. Sharifa aliingia huku kajifunga kanga moja tu maungoni bila nguo nyingine.

    Umbo lake lililotoa taswira ivutiayo, lilikuwa likitikisika kwa namna ambayo Kiwembe alisisimkwa mwili. Na hata walipokutanisha macho, Kiwembe aliona kitu, zaidi ya utazamaji wa kawaida katika mboni za macho ya Sharifa.

    Hata hivyo Sharifa alijitia kutafuta kitu ambacho Kiwembe hakukijua kisha akatoka huku makalio yake yakitikisika kwa nguvu na kuwa kivutio kingine akilini mwa Kiwembe.

    Akilini mwa Kiwembe vitendo vile vya Sharifa ulikuwa ni uchokozi wa dhahiri. Kumbe Sharifa alifikiria nini ilhali alitambua fika kuwa yeye, Kiwembe, kijana ambaye hawajapishana sana kwa rika, ni mpenzi wa mama yake?

    Siku hiyo ya majaribu ya Sharifa, Kiwembe alitaka amtamkie bayana hitaji lake, na kama angekataa, angembaka. Lakini mtoto wa kiume alijitahidi kumzuia shetani wake huku akijifariji kuwa ipo siku ataumia naye. Na huenda siku yenyewe ndiyo hii. Kiwembe aliamini hivyo.

    Moyo ulikuwa wamdunda Sharifa. Hakujua afanye nini na huyo mpenzi wa mama yake. Maneno ambayo Kiwembe alikuwa amemwambia muda mfupi uliopita yalikuwa yakielea kichwani mwake na kumzulia utata usiotatulika.

    “Lakini…lakini wewe si ni baba wewe?” Sharifa alijikuta akitokwa na maneno hayo. Hakuwa na neno jingine la kujitetea. Alikuwa kama anayepima uzito wa jambo lenyewe. Hata kauli yake, hata sauti yake vyote vilikuwa dhaifu, vikiwa havina nguvu wala punje ya upinzani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sikatai,” Kiwembe alisema. “Lakini pamoja na hayo, haya si nd’o mageuzi yenyewe? Na hizo stori za “baba…baba” achana nazo. Hebu tazama umri nilionao, na alionao mama yako. Mimi ni mtu wa kufaa kuwa bwana’ake? Inakuingia akilini wewe? Achana na umbea wa waswahili, umbea usiojenga bali kubomoa. Sharifa, wewe ndiye saizi yangu. Wewe ndiye halali yangu kabisa! Cheki hata maumbo yetu yanavyoshabihiana.”

    Sharifa alilainika kama mboga ya bamia. Akakamatwa kiuno na kuvutiwa kwenye kitanda cha mama yake. Wakashiriki dhahama. Naam, hawakujua ni ngoma ipi waliyocheza pale kitandani. Kama ni sindimba, basi ilikuwa sindimba kweli. Kama ni Mduara basi ulikuwa ni Mduara halisi. Kama ni Mugongomugongo, ilitisha. Chumbani kwa Mama Kadala, kitandani kwa Mama Kadala, na mtoto wa Mama Kadala!

    Kiwembe! Kabalehe kwenye kifua cha Mama Kadala, na sasa anafanya mazoezi kwenye mwili wa mtoto wa Mama Kadala! Kwenye kitanda kilekile!

    Huo ulikuwa ni mwanzo tu, mwanzo uliofungua ukurasa mpya wa uhusiano baina yao. Penzi likawanogea. Awali ilikuwa ni siri, siri iliyofichika, lakini hatimaye minong’ono ikaanza kuzagaa mitaani. Siri hiyo ilianza kufichuka.





    Penzi likawanogea. Awali ilikuwa ni siri, siri iliyofichika, lakini hatimaye minong’ono ikaanza kuzagaa mitaani. Siri hiyo ilianza kufichuka.

    “Kiwembe anachukua mama na mtoto…!” watu walinong’ona.

    Walinong’ona lakini haikuwa ni minong’ono iliyokuwa na mipaka maalum. Hapana. Iliyafikia masikio ya watu tofauti, na hatimaye Mama Kadala akaipata. Hakukubali kupuuzia taarifa hizo. Alimjua bintiye jinsi alivyo na mvuto mkali katika sura na umbo lake. Ni rijali gani atakayestahimili kutomtamkia neno lihusulo mapenzi endapo watakuwa na wasaa wa kuwa pamoja kwa muda mrefu?

    Ndipo akaamua kufanya uchunguzi wa kina, taratibu na kwa siri kubwa. Hakutaka kumshirikisha mtu yeyote katika uchunguzi huo. Hatimaye, siku ya siku akashuhudia kwa macho, Kiwembe na Sharifa wakiwa kitandani kwake, mchana kweupe!

    Alichokiona hapo, hakivumiliki wala hakisemeki. Kwanza alihisi yu ndotoni, akiota ndoto isiyopendeza. Hatimaye akazinduka na kubaini kuwa anachokishuhudia mbele yake si ndoto wala tamthiliya bali ni tukio halisi, tukio ambalo halikutofautiana na maumivu ya kisu chenye moto kikipenya kifuani mwake.

    Chozi likamtoka Mama Kadala. Chozi lenye tani kadhaa za uchungu nyuma yake. Kwa ujumla hakutegemea kuwa kijana yule aliyebalehe kifuani pake, leo atokee kuwa mpenzi wa mwanae, Sharifa, wakidiriki kuchojoa nguo na kukitumia kitanda chake kwa starehe zao.

    Mama Kadala alisononeka, uvumilivu ukamshinda, akaamua kupasulia ukweli Kiwembe.

    “Nakuapia kijana wewe, kama hukubalehe kwenye maungo yangu haya, utaendelea kuwa kichaa wa mapenzi bila ya kudhurika. Lakini kama umebalehe hapa maungoni mwangu, halafu eti unamrudi binti yangu, wallahi nakuapia, janga litakupata katika huo wendawazimu wako.”

    Wakati Mama Kadala akiongea hayo, alikwishavua nguo zote, yuko mtupu kama alivyozaliwa, machozi yakiendelea kububujika mashavuni, akimwonyesha Kiwembe kile kilichomfanya mtoto huyo akawa kichaa wa mapenzi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku hiyo, saa hiyo na dakika hiyo ukawa mwisho wao wa kujuana. Kiwembe aliondoka kwa Mama Kadala kama alivyoingia. Akawa mtoto wa mitaani, mtoto asiyejali mambo ya kwenda shule wala kujitafutia riziki kwa kusaka vibarua huku na kule. Zaidi alikuwa akivizia tu kupata mlo kwa mama yake mdogo, ambaye kama kawaida yake aliendelea kutomjali.

    Kwa jinsi kitongoji cha Ujiji kilivyokuwa kidogo, Kiwembe angeweza kukimaliza kimapenzi. Hata wake za watu ambao wangeingia kwenye ‘anga’ zake asingewachekea. Aliwaza mapenzi tu, na kila mwanamke mzuri aliyemtia machoni alitamani awe mpenzi wake.

    Pumzi yake, mapenzi!

    Shibe yake, mapenzi!

    Lakini, pamoja na hayo, maneno makali ya Mama Kadala yalielea kichwani mwake bila ya kukoma, yakamfadhaisha na kumtia hofu. Akakiona kitongoji hicho kikiwa hakitofautiani na Jehanamu. Akahamia kitongoji cha Mwanga, mtaa wa Kitambwe kinyemela.

    *****

    Saa 2 usiku

    NDANI ya gari dogo, jekundu aina ya Mercedes Benz 320 SE, lililoegeshwa chini ya mti kando ya Barabara ya Lumumba, jirani na soko la Mwanga, kulikuwa na watu wawili, Kiwembe aliyekuwa ni abiria na Hidaya Sufiani aliyelimiliki gari hilo.

    Hidaya alishika tama akashusha pumzi ndefu huku akimtazama Kiwembe kwa macho ya huba. Akajiwa na huruma kadri alivyomtazama Kiwembe aliyekuwa akitokwa machozi huku akibembeleza na kuomboleza.

    Ndiyo, alibembeleza, aliomboleza, na kama kuna wanaume dhaifu kwa wanawake, basi Kiwembe ni mjumbe wao mwakilishi. Mwanamume Kiwembe ambaye sasa alikuwa ametimiza umri wa miaka kumi na tisa, alipangusa machozi yaliyotiririka mashavuni akitumia kiganja cha mkono wake wa kulia. Alikuwa amekwishasema mengi, na sasa alikuwa akiendelea:

    “Kwa nini lakini…kwa nini unaniweka roho juu wakati unajua fika kuwa sura na umbo lako vinanipa mzubao wa moyo? Kwa nini lakini… kwa nini ulikataa kulitimiza ombi na ahadi tuliyoahidiana kwa…”

    Akasita na kuhema kwa nguvu, akionyesha kuwa yu hoi kwa fikra zilizomsonga moyoni. Kisha akaendelea, “Basi unisamehe kama kwa kupanga miadi ile nilifanya kosa. Naomba unisamehe kwa kuwa halikuwa kusudio langu kuyaeleza yale niliyokueleza, na haya nikuelezayo. Unisamehe tafadhali- siyo kejeli bali ni sababu ya penzi langu, kwako. Penzi la kutoka moyoni. Nimeshindwa kuvumilia, nisije kuwa mnafiki kwa jambo hilo, nikajitia sipendi kumbe napenda; huo ni unafiki wa mapenzi.

    “Lakini Hidaya, nakuomba uyatafakari haya nikwambiayo, uyatafakari vizuri kichwani mwako na kuyachombeza, yakikushinda, yaache kama yalivyo, na mzigo wa penzi uniachie unielemee kwa kunikataa kwako, Hidaya.”

    Alipomaliza kuyaghani maneno yake,Kiwembe alipangusa machozi kwa kiganja cha mkono wa kulia. Ni dhahiri alikuwa akilia, hali iliyoujaza uchungu moyo wa Hidaya hata akajikuta naye akitokwa machozi. Chozi lake mwenyewe!

    Hidaya! Hidaya kaambukizwa kilio asichokitegemea! Kuna ile methali isemayo: “Kichwa cha kuku hakistahili kilemba.” Hidaya ataitafsiri vipi methali ile ilhali yeye ni mke wa mtu? Tena ni mke wa Khalifa Mwinyimkuu, mtu aliyeogopwa hata na kunguni!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Hidaya Sufiani, mke wa Khalifa Mwinyimkuu alishusha pumzi ndefu kisha akapumua taratibu. “Nimekuelewa Kiwembe,” hatimaye alisema kwa upole. Akaongeza, “Umeongea na nimekuelewa, lakini ni vizuri ukinielewa na mimi. Unisikilize na unielewe, maana mimi nimekusikiliza muda wako wote ulipokuwa ukiongea.”

    Akatwaa mkoba, akaufungua na kutoa leso. Akafuta machozi taratibu, tendo lililomtia faraja kidogo Kiwembe.

    *****

    ALIMWELEZA bayana kuwa yeye ni mke wa mtu, na ndiyo maana juzi ile siku ya ahadi hakutokea. Na alihofia kuitimiza ahadi ile kwa kuhofia kuwa siri ingevuja.

    “Mume wangu ni mtu hatari sana, Kiwembe,” Hidaya alisema. “Naomba ulitambue hilo. Akigundua kitu, hasa ambacho kinahusu raslimali zake anabadilika sana. Hana simile. Ni mawili; kifo changu au kifo chako. Au hata vifo kwa wote. Ana hasira na wivu wa kupindukia.”

    “Nimekuelewa, Hidaya,” Kiwembe alisema kwa huruma. “Lakini tambua kuwa nakuheshimu sana. Ninakupenda na ninakuheshimu. Nitailinda heshima yako. N’taitunza siri kama mboni ya jicho langu. Wallahi nakuapia, Hidaya. Tafadhali, naomba uamini nikwambiavyo.”

    “Ya kweli hayo, Kiwembe?”

    “Ni kweli tupu!”

    Hidaya alimtazama Kiwembe kwa makini, macho yake yakionyesha huruma zaidi ya mapenzi. Akashusha pumzi mtoto wa kike, kichwani mwake akizirejesha kumbukumbu za siku alipoonana na Kiwembe kwa mara ya kwanza.

    *****



    MWENYE hulka yake, siyo rahisi kuiacha. Kiwembe alikuwa akimpenda kila msichana mzuri aliyekatisha mbele yake. Udhaifu huo ulidhihirika machoni pake jinsi alivyowatazama kwa matamanio wanawake wote wazuri bila ya kujali marika yao. Alikuwa hakosi kugeuka nyuma kila alipopishana nao njiani, akitazama vikalio na migongo yao. Kichaa wa mapenzi!

    Pamoja na udhaifu huo, Kiwembe alikuwa na sura nzuri, yenye kupendwa na wanawake wa rika zote, wengi wao wakijisikia wafu kila wamwonapo.

    Ndiyo maana, jioni ya siku moja, msichana mmoja mzuri alipokutanisha naye macho, msichana huyo akahisi kupasukwa moyo huku macho ya Kiwembe yakigoma kabisa kuangalia kando, yakawa yakimsindikiza mrembo huyo aliyekuwa akiliacha soko la Mwanga, kapu la vyakula mkononi hadi pale alipoliegesha gari lake.

    Watu walioliona tukio lile pale sokoni, macho yao yalimshuhudia Kiwembe akimfuatilia mrembo huyo kwa tamaa yake isiyo kificho.

    Naam, Kiwembe bila hata ya chembe ya soni alimfuata mrembo huyo kama asiyejiamini. Na wakati huo hakuyabandua macho yake katika mwili wa mwanamke huyo.

    “Kwani vipi wewe kaka? Umepoteza mtu?” Kiwembe alishtukizwa na sauti nyororo ya msichana huyo, aliyeshangazwa na macho ya Kiwembe aliyemtazama bila ya kupepesa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kiwembe hakuipata sauti yake. Alishasahau kuwa anamtazama mtu. Akazidi kumsogelea mwanamke huyo.

    “Samahani shangazi,” hatimaye Kiwembe alijikakamua na kusema. Mara akacheka kidogo, kicheko cha kutojiamini. Akaendelea, “Tafadhali, shangazi, tafadhali nakuomba uniruhusu tu…uniruhusu nikutazame shangazi, maana tangu nimekutia machoni, nimehisi macho yangu yamepata kengeza. Niruhusu, tafadhali niruhusu tu nikutazame, huenda ninavyozidi kukutazama nikapata tiba ya macho yangu, shangazi. Niruhusu…tafadhali uniruhusu, shangazi.”

    Wakati Kiwembe akiomboleza hivyo alikuwa ameikita mikono kifuani, akiwa hatofautiani na mtu aliyefumaniwa ugoni na mwenye mke au mume.

    Mrembo huyo alimtazama kwa mshangao. Akajiuliza kimoyomoyo, Aruhusiwe mara ngapi wakati tayari alishaanza kumtazama na anaendelea kumtazama? Ama kuna kingine anachohitaji kutazama zaidi ya hicho anachotazama?

    Badala ya kukasirika, mrembo huyo alicheka, kikawa kicheko kilichozidi kuuboresha urembo wake. Hakucheka ulimbukeni wa Kiwembe, bali alifurahi kujiona kuwa yeye naye ni ‘manyanga’ (msichana mzuri katika lindimo la mapenzi), mwenye kuwababaisha wanaume hata wakapata kichaa kama huyu amtazamaye.

    “Hujambo, bibie?” Kiwembe alimsalimu huku akimsaidia kuliingiza kapu garini.

    “Mie mzima kama unionavyo. We’ vipi hali yako?”

    “Aah, dhofu bin hali, lakini hayo tuyaache tu bibie. Pamoja na njaa yangu ya kukutazama, sura yako iwe shibe yangu, pia naomba msaada wako, shangazi. Msaada mdogo tu, wa lifti.”

    “Unakwenda wapi?”

    “Pale kwenye kilima cha Lubengera, shangazi’angu.”

    Mrembo yule akatabasamu kidogo. Akakosa hoja ya kulikataa ombi lile la lifti. Hatua iliyofuata ni kumbeba kichaa wa mapenzi katika gari lake la kifahari, na huo ukawa mwanzo wa kupeana ahadi ya kukutana mahala fulani.

    Naam, na ndiyo hivyo wapo wawili ndani ya gari lile, Kiwembe akimlaumu Hidaya kwa kutoitimiza ahadi ile, na ndipo naye akaamua kuueleza ukweli wake. Kwamba, yeye ni mke wa mtu japo mumewe kasafiri, na kwamba mumewe huyo ni hatari kuliko kifo na mkali zaidi ya pilipili.

    Mke wa mtu huyo hakuwa mwingine bali ni Hidaya Sufiani, mke wa Khalifa Mwinyimkuu.

    *****

    JAPO alijieleza kuwa yeye ni mke wa mtu, hata hivyo ibilisi alishatinga na kutia nanga moyoni mwake. Wakati wakiwa garini Kiwembe alimshawishi kuitimiza ahadi yao siku hiyo.

    “Mmh,” Hidaya aliguna. “Itakuwa vigumu kwa leo.”

    “Tatizo liko wapi, mpenzi Hidaya?”

    “Tatizo…” Hidaya alisema na kusita.

    “Ndio, tatizo ni nini?”

    “Mume wangu huwa hana kawaida ya kushinda nyumbani,” Hidaya alisema. “Lakini siwezi kujua atakuwa wapi saa’izi. Yeye ni mtu wa kusafiri mara kwa mara, mikoani na hata nje ya nchi. Ni juzi tu alirejea kutoka Bujumbura, Burundi. Nampenda mume wangu, na n’namheshimu. Kwa kweli sijisikii kumsaliti huku tukiwa hatujakorofishana kwa lolote.”

    “Hidaya,” Kiwembe aliita kwa unyonge. “Yote uliyosema yana uzito mkubwa. Lakini unadhani kutakuwa na tatizo lolote kama utaupooza moyo wangu japo kwa dakika tano tu?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kiwembe, tambua kuwa saa hizi ni usiku,” Hidaya alisema kwa sauti isiyokuwa na uthabiti. “Hapa tulipo ni Mwanga- Majengo, na kwangu ni Lubengera. Jaribu kulinganisha umbali uliopo kati ya hapa na Lubengera, kisha uangalie na muda tulionao. Kwa kweli sidhani kama kuna chochote tunachoweza kukitekeleza kwa wakati huu. Muda hauturuhusu.”

    “Hidaya, naomba unielewe,” Kiwembe alikuwa king’ang’anizi. “ Siyo kwamba nakuhitaji kwa muda mrefu, hapana. Dakika tano tu zitatosha. Na siyo kwamba ni lazima twende mahala fulani penye maficho. Usichukulie pia kuwa kwa leo nina papara ya kufanya ngono. Hapana. Ni kiasi cha kuligusa paja lako tu nitafarijika kwa kiwango usichoweza kukikadiria. Ukiniruhusu nikakubusu shavuni, kwangu nitajisikia niko paradiso.

    “Hidaya, tafadhali unielewe. Tuko peke yetu muda huu, na tuko ndani ya gari. Hakuna anayetuona. Tafadhali Hidaya, niruhusu nikubusu japo kidogo…”

    “Hilo tu?” Hidaya alimuuliza kwa sauti ya chini.

    “Ni hilo tu, Hidaya, mpenzi.”

    Ukimya mfupi ukatawala. Hidaya akashusha pumzi ndefu. Kiwembe akahisi kuwa tayari kibali kimetolewa. Akautupa mkono juu ya paja la Hidaya, paja lililonona. Mkono huo ukateleza taratibu juu ya paja hilo. Hidaya akabadilika, hema yake ikawa ya taabu. Kiwembe hakuishia hapo, mara akaupeleka mkono kwenye titi moja la Hidaya na kuanza kulitomasatomasa huku akiuwinda ulimi wa Hidaya.

    Muda mfupi baadaye wakawa katika hatua ambayo walishindwa kustahimili, nguo zikachojolewa. Gari la kifahari, Mercedes Benz 320 SE likageuzwa kuwa gesti. Hidaya na Kiwembe wakaifurahia dunia mpya. Huo ukawa ni mwanzo wa uhusiano wa penzi la wizi.

    Penzi kati yao likakua na kumea. Wiki tatu baadaye walikuwa wameshaingia gesti bubu kadhaa katika maeneo ya Buzebazeba, Mwanga-Majengo na Gungu, wakizifurahisha nafsi zao kwa namna waliyotaka.

    **HUYO KIWEMBE HUYOOOO……..Tunza mali yako asije akaikwangua bila wewe kujuaaaaa……SIJUI TUMLAUMU MAMA KAJALA??? Au mtoto wake

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog