Search This Blog

Monday, October 24, 2022

PIPI YA KIJITI - 4

 





    Chombezo : Pipi Ya Kijiti

    Sehemu Ya Nne (4)



    ILIPOISHIA....



    "Suziiiii, hiki nini?"

    Nilijikuta nikishindwa kuelewa alikuwa na maana gani? hata

    kuliokota gazeti nilishindwa, nilishindwa kuelewa kwenye gazeti kuna nini?. Mume wangu aliliokota na kulifunua

    mbele yangu.



    ENDELEA...



    Mbele ya gazeti kulikuwa na picha yangu na ya baba

    yangu, ajabu picha ya baba alifunikwa usoni ila yangu ilikuwa wazi usoni ila sehemu za siri na kwenye matiti waliziba.

    Kila aliyenifahamu alipoiona ile picha alinifahamu, juu ya picha yangu kuliandikwa DOEZI LA WANAUME ZA WATU LAUMBUKA.

    Lakini kwenye maelezo jina langu ndilo lililo andikwa, lakini baba yeye hakugusiwa chochote. Japo iliniuma na kuonyesha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    jinsi nilivyo dhalilishwa. Lakini nilishukuru

    Mungu kwa kumficha baba

    yangu.

    Hata kama mama mdogo aliamua kuniumbua, lakini nilimshukuru kwa kuificha aibu ya familia. Kama angetoa picha ya baba kama yangu ilikuwa aibu ya karne. Mume wangu alikuwa amebadilika kutoka weupe na kuwa mwekundu. Mishipa ya kichwa ilimsimama na macho kumtoka pima.

    "Suzy mke wangu nini umekifanya kufikia kunidhalilisha hivi mume wako?"

    "Nisamehe mume wangu si kweli ni njama za watu" nilijikuta

    nimechanganyikwa mara mbili, nguvu ziliniishia na kujikuta nakaa chini bila kupenda. Mbona ule mwaka ulikuwa wangu,

    nilijiuliza nitamueleza nini mume wangu anielewe.

    "Hapana..hapana..Suzy sasa too much, siwezi kuwa na wewe mimi na wewe tosha"

    "Hapana mume wangu sirudii tena" nilijitetea kwa kumshika miguu

    "La mimba ningekusamehe lakini hili ambalo nchi nzima wanajua hata wazazi wangu. Siwezi kukupiga ila nakuomba chukua kila kilichokuwa chako uondoke uende kwa huyo

    aliyekupa ujauzito"

    Kwa kweli niliamini sikuwa na uwezo wa kumbembeleza mume wangu anisamehe. Alikuwa na kila sababu ya kunifukuza, nani imani hata marafiki zake walichangia ili nifukuzwe.

    Siwezi kuwashangaa kutokana na kila mchuma janga hula na

    wa kwao.

    Nilijinyanyua chini mtoto wa kike na kuona dunia yote kama ikinizomea baada ya kutembea uchi. Nilikwenda chumbani na kukusanya kila kilichokuwa changu, nilijifikilia mabegi zaidi ya sita nitayapeleka wapi na kwa baba nisingeweza kurudi. Nitamuangaliaje mama mdogo hata baba yangu, nilichagua nguo zangu muhimu na kuziweka kwenye begi moja kubwa

    na pesa zangu zilizokuwa kama laki nane. Nilitoka hadi sebuleni na kumkuta mume wangu akilia huku amejiinamia kwenye kochi. Ilionyesha wazi jinsi mume wangu alivyoumizwa na fedheha ya mwaka mbele ya macho ya ndugu na rafiki zake.

    Nilimpita bila kumsemesha lakini kabla ya kutoka nje mume wangu aliniita

    "Suzy mke wangu umeniachia jereha ambalo halita pona mpaka naingia kaburini" mume wangu alizungumza machozi yakimtoka

    "Sina jinsi mume wangu maji yamekwisha mwagika"

    "Ingekuwa mimba ningekusamehe...lakini hili hata rafiki

    zangu waliona na kunipigia simu, hii aibu nitauweka wapi uso wangu...kwa nini Suzy"

    "Hata nikikueleza hutanielewa kwa vile sehemu ilipofika ni mbaya"

    "Suzy mke wangu tunatengana lakini elewa bado nakupenda kama mtoto aliyekatishwa ziwa la mama yake akiwa bado analipenda"

    "Hilo nalielewa lakini kama nilivyosema haina jinsi, vumilia atapata mzuri zaidi yangu na mwaminifu kuliko mimi"

    "Hapana ..hapana..Suzy umenidhurumu penzi langu"

    Niliona nahau zinazidi niliburuza begi langu lililokuwa kubwa na kuelekea nje. Mume wangu alikuja karibu yangu na kuniangalia kwa jicho lililokuwa jekundu kwa kulia kwa kweli

    nilimuonea huruma bila kujua nini

    hatma ya maisha yangu.

    "Suzy unakwenda wapi?" aliniuliza

    "Nyumbani"

    "Nakutakia maisha mema, ondoka na hili gari nitalifuata kwenu"

    "Hapana nitakodi gari hadi nyumbani"

    Alinisindikiza hadi mlango wa geti na kunisindikiza kwa macho, nililiburuza begi langu hadi barabarani. Wazo la kwenda mjini sikuwa nalo, niliamua kwenda Morogoro kutuliza akili kabla ya kuamua niende wapi.

    Nilivuka barabara upande wa pili na kupanda basi la Morogoro, Nilibahatika kupata siti baada ya mtu mmoja kunionea huruma kwa kuwa yeye alikuwa anaishia Kibaha maili moja. Mbona kwenye gari niliona aibu kwa kukuta maongezi ya siku ile ni kuhusu habari zangu.

    Nilijifunika ushungi ili nisifahamike, nilimsikia mtu mmoja akizungumza na mwenzake ambao walikuwa kiti cha mbele

    yangu.

    "Yaani hivi huyu msichana alivyo mzuri hivi kwa nini asitulie na kuolewa kuliko kukimbilia waume za watu"

    "Yaani jinsi alivyo mzuri ndio maana wanaume wanamkimbilia"

    "Lakini si ameolewa?" mmoja alirukia wa kiti cha upande wa pili

    "Labda mume wake hamridhishi, hivi kitu kama hiki bao moja si kukipaka shombo"

    "Nina wasiwasi bwana yake huenda ni mzee" Konda alichomekea

    " Inawezekana kuna wazee kwa tamaa zao wanachukua shamba zuri lakini uwezo wa kulilima hawana"

    "Lakini siamini huenda wameamua kumdhalilisha mbona

    mwanaume hakuonekana"

    "Inawekana kuna mchezo umechezeka huenda ni mume wa

    rafiki yake"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mjadala ule kwa kweli uliniumiza moyo, nilitamani niwaambie wanyamaze, lakini niliwaacha wamalize kiu

    yao ya kuongea. Tuliingia Morogoro majira ya saa saba mchana, nilitafuta hoteli iliyokuwa pembeni ya mji ya

    Mikumi Lodge.

    Nilichukua chumba kutokana na kuwa na njaa, niliagiza chakula na kula. Kisha niliagiza pombe kali ambayo nilikunywa mpaka nikawa sijitambui na kulala kwenye zuria, wakati huo nilikuwa nimezima simu. Nilizinduka majira ya saa sita usiku njaa ikiwa inaniuma kama kidonda.

    Nilikwenda hadi jikoni na kukuta kuna ndizi nyama tu, nilichukua na kurudi chumbani kwangu. Nilishambulia

    kile chakula kama sina akili nzuri. Baada ya chakula niliingia

    kwenye kinywaji tena, sikutaka kupata muda wa kufikili kila nilipokumbuka moyo uliniuma na kujikuta nalia peke

    yangu.

    Nilikunywa tena pombe mpaka nikafloti na kulala nilipokuwa nimekaa mpaka asubuhi baada ya kushtushwa na mlango uliokuwa ukigongwa. Nilipofumbua macho nilikuta jua

    limeisha toka, nilikwenda hadi mlangoni kufungua mlango.

    Nilikuta ni mfanya usafi wa vyumba alikuwa mvulana

    "Samahani sister kwa kukukatisha usingizi"

    "Bila samahani kaka yangu, kwani muda huu ni saa ngapi?"

    "Inakimbilia saa nne na nusu sasa"

    "Mungu wangu usingizi gani huu"

    Nilimpisha afanye usafi, kisha nilikwenda kuoga na kupata kifungua kinywa. Nikiwa chumbani kwangu nimejilaza, nilipata wazo la kumtafuta rafiki yangu kipenzi Monika niliyesoma naye A-level. Namba yake ilikuwa kwenye simu yangu.

    Kwa vile sikutaka kuendelea kutumia laini ya zamani nilihamishia majina muhimu kwenye phone kutoka kwenye simcard.

    Nilinunua laini nyingine na kumpigia rafiki yangu Monika.

    Nilishukuru Mungu simu yake ilikuwa ikiita, iliita kwa muda na

    kupokelewa

    "Haloo nani mwenzangu?" upande wa pili uliuliza

    "Ni mimi Suzy mama mirindimo"

    "Oooh mpenzi kwanza pole kwa yaliyokusibu nilijua umeisha jitia kitanzi"

    kweli habari zangu zilifika mbali

    "Tuachane na hayo, upo wapi mpenzi?"

    "Nipo Arusha, hebu nipe kwa mktasari"

    "Ni hivi nakuja huku naomba unipokee, mwenzio nimepoteza dira"

    "Kwa hilo tu usikonde shoga yangu unakaribishwa muda wowote, kwa sasa upo wapi?"

    "Nipo Morogoro"

    "Sasa AR utakuja lini?'

    "Hivi leo naondoka nina imani tutaonana leo hii"

    "Oooh karibu sana tena jisikie kama umefika kwa nduguyo"

    Nilikata simu na kukusanya kila kilichokuwa changu na kuondoka muda ule ule kwa kupanda gari hadi Charinze. Nilikuwa na bahati nilipata basi la Arusha. Yaani wee acha tu

    kwenye kila basi mazungumzo yote yalinilenga mimi juu ya habari zilizokuwa kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti la udaku.

    Kila mmoja alizumgumza yake wapo walionitetea na wapo walionikandamiza, ili mladi kila mmoja alizungumza kadri ya uwezo wake kwa jinsi alivyo zipokea habari zile. Nilijiuliza hivi kama zile habari zingetoka kama zilivyokuwa wale watu wote nilio wasikia wangelizungumza vipi?.

    Nashukuru Mungu mpaka tunaingia Arusha hakuna hata mmoja aliyenitambua. Tuliingia Arusha majira ya saa moja usiku, nilimpigia simu rafiki yangu ambaye alinifuata baada

    ya dakika ishirini.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Aliponiona alinivamia na kunikumbatia kwa furaha

    "Wawoooo best, karibu Arusha"

    "Asante nimekaribia" tulikumbatiana kwa furaha, kisha tulikodi teksi hadi kwake Karoleni.

    Nilifika kwa shoga yangu na kuvutiwa na chumba chake. Nilijua tu lazima atakuwa ameolewa, nilijiuliza kama chumba kimoja na yupo na mumewe itakuwaje.

    Kwa kweli chumba kilikuwa na kila kitu muhimu chumbani kwa mtu. Japo chumba kilikuwa kimoja, baada ya kufika shoga yangu alinikaribisha

    "Karibu shoga yangu hapa ni kwangu nina imani hata wewe ni

    kwako" alisema huku akionyesha uchangamfu wa hali ya juu

    "Asante shoga kuonyesha moyo wa upendo, vipi shemeji una kaa naye au anakuja na kuondoka"

    "Suzy yaani maisha gani ya kuolewa" alisema huku akijishebedua mtoto wa kike kwa kuchezesha makalio yake makubwa kidogo.

    Nasema hivyo kutokana na mzigo wangu kumzidi sana.

    "Kwa hiyo huna mume"

    "Wa nini?"

    "Rafiki?"

    "Wa nini?"

    "Ina maana upo peke yako?"

    "Ndio maana yake hapa una uhuru wa kukaa muda wowote, jisikie upo kwako"

    "Na shukuru Mungu akujalie"

    Nilimkumbatia shoga yangu kwa furaha ya ajabu kwa kunipa uhuru. Ilionyesha alikuwa akifanya kazi yenye kumpa kipato kizuri.

    "Shoga kwanza kaoge ili upate chakula na kupumzika"

    Alinitayalishia maji ya kuoga na kunionyesha bafu, nilijifunga upande wa kanga na taulo juu na kuelekea bafuni

    kuoga. Nilipotoka kuoga nilimkuta Monika akizungumza na kina dada ambao walikuwa na mavazi ya utatanishi.

    Ilionyesha ni machangudoa, waliponiona walishtuka kwa kusema

    "Moni una ugeni?"

    "Ndio ndugu yangu"

    "Ooh karibu sana dada"

    "Asanteni"

    "Vipi wa kupita au?" mmoja akiuliza huku akinitazama kwa jicho la matamanio japo alikuwa mwanamke

    "Huyu mtamchoka"

    "Mmmh vipi mambo yetu vipi?"

    Nilishindwa kuelewa walikuwa wana maana gani

    "Nyinyi wote cha mtoto, hapa mwisho wa reli"

    "Usituambie"

    "Habari ndiyo hiyo, ukiiona paki gari yako pembeni. Akitangulia mpaka aondoke ndio zenu ziingie barabarani"

    "Kwa mtaji huu hatutii neno"

    Nilijikuta njia panda nisijue wana maana gani, baada ya muda wale wanawake walimuaga Monika, huku Monika akiwaambia

    "Jamani leo mtanisamehe siwezi kumuacha mgeni peke yake"

    "Una haki dada kesho au tutakuwa naye pamoja"

    "Mmmh mwacheni apumzike kidogo, kwanza ayajue mazingira ya Arusha kisha aweze kuingia kilingeni

    kikamilifu"

    Kwa kweli naweza kusema unaweza kumsikiliza mtu akizungumza lakini usijue ana maana gani. Sikuwa na haraka ya kuuliza, nilijua lazima nitashilikishwa haraka ya nini.

    Baada ya kupata chakula ambacho kwa kweli kilikuwa kizuri sana na kupata mapumziko mazuri. Kabla ya kulala Moni siku ile kwa kweli tulikesha tukizungumza. Alitaka kujua sababu ya sikendo yangu.

    Nilimdanganya kwa kumueleza uongo ambao aliuamini. Nilificha siri ya kufanya mapenzi na baba kwa kujua hapo lazima atasema nimevuka mipaka. Siku ya pili Monika alinitembeza baadhi ya maeneo ya Arusha na kurudi nyumbani

    Siku ile hatukupika tulikula chipsi na kuku, nilijikuta nikiyainjoi maisha na kujikuta napata uhuru na kusahau yaliyonifanya nilikimbie jiji la Dar. Jioni ilipofika nilimuona shoga yangu akienda bafuni kuoga na baadae alijipodoa. Nilishangaa

    mbona aonyeshi kama tutakuwa pamoja kwenye safari yake. Baada ya kujipodoa nilishangaa kumuona akivaa mavazi ya nusu uchi. Mmmh nilijikuta nikipatwa maswali juu ya mavazi yake na mashoga zake waliompitia jana yake.

    Nikiwa bado sijapata jibu, rafiki zake walimpitia kwenye mavazi sawa na Monika. Nilishindwa kumuuliza kuwa anakwenda wapi, kabla ya kutoka aliniaga

    "Suzy tutaonana kesho, ila kama utakuwa na shida ndogo ndogo. Chini ya kitambaa kuna pesa kidogo usiku mwema"

    Aliondoka akiongozana na mashoga zake, ambao wote

    walionekana wapo kwenye biashara ya kujiuza. Kwa kweli sikujisikia vizuri lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    matokeo bila kuuliza swali.

    Siku ya pili alirudi saa kumi na moja alfajiri kwa kunigongea dirisha. Nilimfungulia mlango na kuingia nywele zake zikiwa timutimu, vile vile alionyesha amekunywa kidogo.

    Baada ya kuingia alinipiga busu na kwenda moja kwa moja na kujitupa kwenye kochi. Kwa sauti ya kilevi aliniuliza

    "Vipi mpenzi umelalaje?"

    "Aah salama sijui mwenzangu"

    "Huwezi kuamini Suzy umekuja na ngekewa"

    "Kivipi best?"

    "Yaani leo biashara ilikuwa nzuri ajabu" Mmmh nilishindwa kuhoji ni biashara gani. Ni wazi kutokana na

    mavazi aliyoondoka nayo itakuwa na mwili.

    "Aaah usiniambie!"

    "Hebu hesabu hela hizi" alisema huku akinipa noti mchanganyiko za kitanzania na dola. Kwa hesabu siku ile

    alikuwa na laki mbili kasoro

    "Basi ndugu yangu kwa wewe unaweza kutengeneza milioni"

    Bado sikutakiwa kuuliza biashara gani, si unajua kama bado mgeni na yeye ndiye mfadhiri wangu mkubwa.

    Vile vile nilikaa kimya kusubili alikuwa na maana gani. Lakini kama ndio biashara ya ukahaba mbona nitakuwa naruka mkojo na kukanyaga kinyesi.

    ***************

    Nilikaa kwa shoga yangu kwa muda wa wiki mbili bila kubughudhiwa kwa lolote. Wakati huo nilikuwa nimeisha ijua kazi yake inayompatia riziki. Ilikuwa kazi yake kubwa ni

    kuuza mwili, hakusita kunisifia kwa kuniambia

    " Shoga nakuaminia kazi unaiweza, kwa hili umbile lako utakula vichwa kama huna akili nzuri. Tena nakuhakikishia ndani ya miezi sita utakuwa na nyumba na gari"

    Kwa mara nyingine nilishindwa kumkatalia au kumbishia, yote ilitokana na kuulilia wembe sina budi kuvumilia maumivu. Kila siku niliyokuwa nikitoka kuoga na kusimama

    mbele ya kioo nikiwa mtupu.

    Niliuangalia mwili wangu kwa kuuchunguza kona zote, sikuamini hata siku moja kama mwili wangu nitautoa

    sandakalawe kwa wanaume. Nilijua kama nikigoma basi ndio hivyo, lazima mwenyeji wangu atanifukuza.

    Mmmh mtoto wa kike siku ilifika, majira ya jioni baada ya kuoga niliupara na kupewa nguo za nusu uchi.

    Mgongo wote ulikuwa nje na chini nguo iliishia juu ya magoti. Kwa kweli nilikuwa nipo uchi mtoto wa kike, muda ulipofika tuliingia mitaani. Tuliongozana hadi pembeni

    ya hotel kubwa, ukistaajabu ya Musa utayaona ya Filauni.

    Tulipofika nje ya moja ya hoteli kubwa pale Arusha. Baada ya kufika shoga zake rafiki yangu walitawanyika na kuniacha mimi na Monika. Monika alinipa maelezo ya kazi.

    "Suzy kazi ndiyo hii, sasa ni hivi akitokea mteja mkimbilie huku ukionyesha maungo yako. Lakini ulivyo sidhani kuna mteja wa kutaka kukuchunguza zaidi ya kufika bei kwa bei mbaya"

    Baada ya kusema yale aliniacha kwenye kona yangu na yeye kwenda kusimama mbali kidogo niliposimama mimi. Usifikili tulikuwa sisi peke yetu, eneo lile tulikuwa zaidi ya wanawake

    kumi na tano. Nikiwa nimesimama sijui hili na lile na kibaridi cha Arusha kilinichonyota.

    Nilishangaa kuwaona wenzangu kila gari likisimama hulikimbilia na kulizunguka. Kila mmoja alionyesha

    mwili wake kwa kujivua nguo kwa kupandisha gauni juu hata kuonyesha nyeti zake bila aibu.

    Kwa kweli kwa upande wangu kazi ilikuwa ngumu sana. Shoga yangu alinifuata na kunifokea kwa kusema

    "Suzy utaniudhi hebu changamka bwana"

    Nilishindwa kumjibu, kidogo nimwambie kazi ile siiwezi. Lakini nilishindwa nianzie wapi, nilibaki nikipepesa macho huku nikizidi kujikunyata kwa baridi.

    Mara lilikuja gari aina ya Toyota Vx new model nyeupe na kusimama mbali kidogo tulipokuwa tumesimama.

    Kama kawaida wanawake wote waliokuwepo pale walilikimbilia. Shoga yangu Monika alinishika

    mkono na kunivuta kukimbilia kwenye gari. Tulipofika kwenye gari kila mwanamke aliyekuwepo pale

    alikuwa yupo uchi kwa kujivua nguo kujionyesha maumbile yake.

    Hata shoga za Monika nao walikuwa kwenye kunadi mali zao. Kulikuwa na maneno ambayo kwa kweli yataka moyo kuyatamka, kila mmoja alisema lake

    "Mimi yangu kavu" mwingine

    "Matiti yangu yaone yanavutia kwa kunyonya"

    "Mimi natoa vyote bei maelewano"

    Mwingine alinimaliza kwa kusema

    "Nini nakupa bao moja ofa mengine unalipia"

    Nilibakia kama sanamu nilishindwa nifanye nini au nisema

    nini,mmh kweli kiranga haliliwi wala hawekewi matanga. Hali iliyokuwepo pale, nilimkumbuka mume wangu na kutamani nirudi Dar nimlambe miguu.

    Nikiwa bado sijui nifanye nini Monika alinisukuma kwenye umati wa watu hadi mbele ya gani na kujikuta nikijigonga kwenye mlango wa gari. Kabla sijajua nifanye nini Monika aliinyanyua gauni na kuniacha chini mtupu. Kibaya zaidi nilikuwa siku hiyo nimelazimishwa kuvaa bikini.

    Mmh Monika kweli kazi anaiweza pale aliposema kwa sauti ya juu

    "Achana na kongoro hizo angalia mali mpya"

    Alininadi kwa sauti ya juu, nilimuona aliyekuwemo kwenye gari macho yakimtoka pima alifungua mlango na kunivutia ndani. Baada ya kuingia ndani alifunga mlango.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kabla gari halijaondoka Monika alikuja hadi dilishani na kuning'oneza

    "Suzy changamka malipo yasipungue elfu 20"

    Wakati huo jamaa ambaye alionekana mtu mwenye wadhifa

    wake. Aliondoa gari na kwenda mwendo wa kama dakika mbili. Alifunga vioo vyote na kuwasha kiyoyozi.

    Lakini nilimuomba azime kutokana na baridi kali lililonipiga.

    Aligeuka na kuniuliza

    "Mrembo unaitwa nani?"

    "Suzy"

    "Oooh jina zuri" yule jamaa alisema huku akipeleka mkono wake mapajani kwangu, nilitaka kuutoa lakini nilista baada ya kuushika mkono wake kisha kuuacha uelekee unapotaka.





    Mkono uliendelea kusafili na kuivuka bikini na kutelemka kwenye kisima cha burudani. Mwanaume taratibu aliipaki gari pembeni na kuendelea kuupeleka mkono kwa kufanya

    upekuzi kama amepoteza kitu.

    Japo kwa mbali nilihisi raha fulani na mwili kutamani kupewa kitu fulani. Sikuwa na jinsi kukubali kugeuzwa mpira wa kona. Kila alivyonichezea moyo uliniuma na kujikuta nikilia peke yangu, machozi yalinitoka kama maji.

    Mara jamaa alinigeukia na kuanza kunipa denda, nililipokea kwa vile sikuwa na jinsi. Baada ya kupashana miili huku nikiwa na hamu ya kitu lakini moyo haukuwepo eneo la tukio.

    Nilijilazimisha na kufanya naye mapenzi.

    Mtoto wa kike niliuanza mchezo kwa kuuogopa uwanja kama vile una vidimbwi kwa kuchagua nikanyage wapi. Nilijikuta nitokwa na woga baada ya kunigusa kunako. mmh

    mtoto wa kike nilijisahau na kuanza kuutawala mchezo kwa pasi fupifupi na chenga za maudhi.

    Nilimsikia mtoto wa kiume akitangaza ndoa huku akilia kilio cha mbwa. Nami nilivyokuwa napenda sifa niliongeza vibweka na kusahau hata mapatano ya bei ya kazi ile nilimsikia akisema

    "Mmh hapana siwezi kula nisishibe, wacha nikagombane na mke wangu leo lazima tulale pamoja mpaka asubuhi"

    "Wewe tu baba" wakati huo nilikuwa ninausafisha muhogo uliotoka ardhini muda si mrefu kwa ulimi.

    Baada ya kuusafisha na kuumenya kwa meno, nilimsikia akisema

    "I.i.inatosha tutamalizia hotelini"

    Nilimsafisha kwa ulimi na kuurudisha muhogo gharani kisha niliufungia na kumpiga busu huku nikimpa pole

    "Asante, lazima nikuoe" nilichekea moyoni na kumuona pamoja na utozi wake alikuwa hajapata machejo. Niliuapia

    moyo wangu kutumia uwezo wangu wote kuhakikisha sirudi

    kwenye ile biashara hata tutakapokutana kwenye uwanja mfupi kuliko yoyote duniani.

    Nilimshukuru Mungu kwa kunipa uwezo wa kukabiliana na mwanaume na kuweza kumkata kiu bila kumuudhi. Lakini nilisahau kuuliza kwa Monika penzi ka short time na kulala

    mpaka asubuhi malipo yake yakoje.

    Tulikwenda hadi kwenye hotel ya new Arusha na kuchukua vyumba. Baada ya kupata vyumba tulikwenda kuoga, kutokana na kujua uwezo mdogo wa mpinzani wangu. Tukiwa bafuni nilimliza machozi mawili ya hewani.Usiku hukuwemo ila Malaika wako alikuwepo, mtoto wa kiume alimaliza maneno yote mdomoni kutokana

    na machejo niliyomchezea.

    Huwezi kuamini hata mapenzi hatukufanya zaidi ya kuliza kwa mkono na mdomo. Mtoto wa kike nilikuwa imeipruvu

    kutokana na kozi aliyonipa baba. Tulijikuta tukilala saa tisa usiku, usiku kucha simu yake iliita. Niliamua kuizima

    kutokana na kunyimwa raha, asubuhi tuliamka saa tatu.

    Asubuhi kabla ya kuondoka akaomba mchezo wa mwisho. Siku zote huwa sichagui mchezo wa ligi au wa kirafiki nilipanga kikosi cha kwanza, mshike mshike ulitufanya

    tupitiwe usingizi na kuamka saa saba tukiwa na njaa kama kidonda.

    Wakati huo kina Monika walinitafuta kama nini, wao walijua nimepotea. Kibaya simu zao zilipozidi niliamua kuzima kabisa ili nifaidi raha zangu. Baada ya kuoga na kupata chakula cha nguvu, niliagana na yule bwana ambaye alinipa laki tatu

    taslimu.

    Tuliagana huku akinipa bussines card yake na kuniomba nisiende kijiweni ila ikifika saa kumi na mbili tukutane

    Arusha hotel. Alilipia chumba kabisa na hela ya chakula na vinywaji.

    Nje ya laki tatu alinipa elfu hamsini ya teksi nilimtuma muhudumu wa guest ile kwenda kuninunulia kitege ili niweze

    kuingia nyumbani bila kuonekana kihoja kutokana na nguo nilizokuwa nimevaa jana yake.

    Niliagana na mteja wangu na kukodi gari hadi kwa shoga yangu. Gari lilipo simama nilimuona shoga yangu, alishangaa kuniona nimejifunga vitenge.

    "Vipi Suzy umekubwa na nini?" aliniuliza macho ameyatoa pima

    "Ondoa wasiwasi, dada sio mchezo biashara inalipa" nilimjibu

    huku nikielekea mlangoni

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Usiniambie!" Alinikimbilia na kunikumbatia. Baada ya kuingia ndani nilikwenda hadi bafuni kuoga, nilipotoka kuoga Monika alikuwa na hamu kujua mgeni nilipotelea wapi? Baada ya kupumzika huku nikipata bia ya kilimanjaro baridi, nilimsimulia yote yaliyotendeka usiku, na mtu jinsi alivyopangawa na machejo adimu niliyompa

    "Usiniambie! kwa hiyo bei ileile buku ishirini"

    "Aaah unaniaonaje yaani mimi wa elfu ishirini"

    "Vipi kakupa ngapi?"

    Sikumjibu nilikwenda hadi kwenye mkoba wangu na kumpatia laki tatu taslimu, nilimuona amepagawa mtoto wa kike

    "Usiniambie yaani siku ya kwanza umeruka na kilo tatu, wacha wanaume za watu wachanganyikiwe"

    "Huo ni mwanzo, mtu kapagawa hataki kuugawa utamu huu kwa watu wengine"

    "Ina maana anataka kukuoa kabisa?"

    "Hilo hajaniambia ila ameniambia hataki kuniona tena sehemu zile"

    "Mmmh basi mwenzangu una kizizi yaani jamaa kagusa tu amenasa kwa hiyo mtaonana naye vipi?"

    "Amenipa Bussines Card yake na kesho amesema niende ofisini kwake"

    "Mmmh hongera huenda nikagomboka na mimi na tabu za baridi za usiku"

    Kumuonyesha namjari nilimpa laki moja katika pato langu la siku ya kwanza. Monika alifurahi na kuniona zaidi ya ndugu yake, jioni ilipofika sikutoka na wenzangu nilibakia nyumbani

    kwa raha zangu na kuwaacha Monika na shoga zake waliompitia wakienda kwenye lindo lao la kawaida.

    ************

    Siku ya pili nilitafuta nguo moja ambayo nilijua mtoto wa kiume akiniona lazima achanganyikiwe. Nilipendeza vilivyo kwa vile nilikuwa nimeisha kuwa mwenyeji jiji la Arusha, nilikodi teksi hadi maeneo ya posta. Ofisi niliyoelekezwa haikuwa imejificha sikuchelewa kuiona, nilijitengeneza

    vizuri kisha niliingia ndani ya ofisi.

    Niliingia hadi ofisini na kumkuta msaidizi wake akiwa bize mbele ya kompyuta, aliponiona aliacha kazi yake na kunikaribisha.

    "Karibu dada yangu"

    "Asante" nilimjibu huku nikiachia tabasamu kama kawaida yangu

    "Sijui nikusaidie nini?"

    "Sijui nimemkuta?"

    "Nani?" mmh hata jila lake nilikuwa silijui

    "Sijui meneja ooh no mkurugenzi"

    "Wewe ndiye mgeni wa Mr Paroko?" yule msichana aliniuliza

    huku akiniachia tabasamu pana kuonyesha jinsi gani amefurahishwa na kubabaika kwangu

    "Ndi.i.yo" nilijibu kwa kubabaika nikiwa na wasiwasi huenda

    nimekosea sio pale.

    "Mbona dada unaonekana hujiamini, kwani kuna kitu una wasiwasi nacho?"

    "Ha.pana"

    "Nina imani unaitwa Suzy?"

    "Ndiyo"

    "Ok, pita moja kwa moja"

    Nilishusha pumzi kabla ya kuondoka na kumfanya binti ambaye ni msaidizi wa Mr Paroko kama jina lake

    nilivyolisikia kuzidi kunishangaa. Nilijitengeneza tena upya bila kumjari yule msichana na kushangaa kwake.

    Mbona hashangai mlima Meru kutoa barafu bila kuwa na friza. Baada ya kuwa na uhakika nipo sawa niliingia

    moja kwa moja ofisini kwa mkurugenzi.

    Mbele yangu nililakiwa na kijana mmoja nadhifu mtanashati tena maridadi aliyeyejaa tele kama pishi ya mchele. Alinikaribisha kwa tabasamu pana

    "Karibu mrembo"

    "Asante" nilijibu huku nikiwa badonimemsimamia kama askari kwenye ukaguzi

    "Karibu kiti"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Asante" nilijibu huku nikiketi

    Baada ya kimya kifupi nikiwa nimejiinamia nikichezea kucha zangu nilishtushwa na sauti nzito ya kiume lakini tamu masikioni mwangu

    "Mhu mrembo karibu"

    "Asante"

    "Nikusaidie nini?" ilionyesha alikuwa amenisahau kutokana na

    nguo nilizokwenda nazo, niliamini alitegemea kwenda na nguo za ajabu

    "Mmh Paroko ni jana tu mchana tumeachana na tulikuwa pamoja usiku na nusu siku, au nimebadilika?"

    Kauli yangu ilimfanya Paroko kushtuka na kuniangalia vizuri na kumfanya aachie tabasamu pana na kusema

    "Oooh Suzy yaani nimeamini wewe ni mwanamke mzuri usiye

    sitahili kuishi maisha yake uliyochagua.. samahani kwa kukupotea inaonyesha jinsi gani unapotulia unahamia

    ulimwengu nyingine"

    "Usijari, sipendi ni ugumu wa maisha" nilimjibu huku nikibinua

    midomo kwa pozi

    "Siamini Suzy, wewe si msichana wa kupigwa na baridi na kuliwa na mbu usiku wa manane, ila unatakiwa kuwa liwazo la moyo wa mwanaume mwenye pesa kama mimi"

    "Mlikuwa hamuonekani ndio maana tumeamua kuingia kwenye kazi ile"

    "Suzy unataka kuniambia kazi ile umeianza lini?"

    "Ndio kwanza jana bismillah"

    "Usiniambie, na kabla ya kazi hii ulikuwa wapi?"

    "Nilikuwa naishi na baba yangu na mama wa kambo, baba alinifukuza kwa maneno ya mama wa kambo" nilitengeneza uongo

    "Usiniambie Suzy, ulikuwa hapa hapa Arusha au nje ya mkoa?"

    "Nje ya mkoa"

    "Samahani dada karibu kinywaji" msaidizi wake alinikaribisha kinywaji kilichokuwa kwenye sinia

    "Asante" nilijibu huku nikikipokea kinywaji

    Baada ya msaidizi kuondoka Mr Paroko alinigeukia na kuniuliza

    "Ni mkoa gani?"

    "Dar"

    "Ooh na hapa Arusha upo kwa nani?"

    "Kwa shoga yangu niliyesoma naye shule moja"

    "Ooh vizuri, hebu nieleze ukweli una muda gani hapa Arusha?"

    "Wiki ya tatu sasa"

    "Oooh my God, Suzy ina maana hujawahi kufanya kazi ya ukahaba hapo nyuma"

    "Wala siijui ndiyo jana nilikuwa najifunza"

    "Mmmh kabla yangu iliwahi kukutana na mwanaume yoyote hara Arusha?"

    "Wewe ndiye wa kwanza, ndiyo maana ulipata shida sana mwanzo"

    "Suzy jiite mtu mwenye bahati sina uwezo mkubwa nitakupangia nyumba nzima kisha baadae nitakutafutia na

    usafiri sijui unasemaje?"

    "Usiniambie Paroko!"

    "Habari ndiyo hiyo"

    Baada ya ,mazungumzo na kukubaliana kukutana tulipolala juzi yake kwa mara ya mwisho na baadae nipangiwe nyumba nzima. Mmh kweli Mungu hamtupi mja wake, nilimshukuru

    Monika kwani bila yeye kunipeleka mnadani bahati ile

    nisingeipata.

    Niliagana na Paroko ambaye alinipa pesa taslimu laki mbili, nilirudi nyumbani nikiwa nafuraha ya ajabu ya kupata bwana mwenye pesa tena mwenye mapenzi na mimi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog