Search This Blog

Monday, October 24, 2022

TOROJO BAMIA ( WINGA TELEZA ) - 2

 





    Chombezo : Torojo Bamia (Winga teleza)

    Sehemu Ya Pili (2)



    “Nina imani elfu inakutosha, una jingine?” Suzy alinyoosha mkono kumpa Shuku lakini hakupokea kitendo kilichomuuzi Suzy na kumkazia macho kumuuliza.

    “Kuna mtu kakutuma? Haya niambie.”

    “Sivyo hivyo Suzy.”

    “Sasa unashida gani Shuku? Unajua kuna sehemu nawahi kuna ofa.”

    “Nashida na wewe,” Shuku alijikakamua.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mimi?” Suzy alishtuka na kujishika kifuani.

    “Eeh.”

    “Shida gani?”

    “Unajua Suzy nateseka kila nikuonapo.”

    “Mmh! Makubwa, jamani mbona mapya, Shuku mimi nikutese wewe? Nimegeuka mchawi nakuchukua usiku na kukugeuza fisi?”

    “Hapana Suzy kimapenzi.”

    “Unamaanisha unanitaka niwe mpenzi wako?”

    “Ndi..ndi..yo Suzy.”

    “Muone huna hata haya hata kuzungumza huwezi unajua kabisa mimi si saizi yako. Shuku umenidharau kiasi gani kunisimamisha na kunieleza ujinga wako?” Suzy alikuja juu na kupaza sauti iliyosikika umbali mrefu.

    “Si..si..hivyo..Su..su zy...na..na kupenda.”

    “Shuku mbona unataka kunitia nuksi huko niendako mambo yangu yaende ndivyo sivyo.”

    “Lakini Suzy mpenzi hayapo hivyo nami nina haki ya kuyasema mateso yangu kwako.”

    “Hebu niangalie,” Suzy alisema kwa sauti huku akijigeuza mbele ya Shuku kitu kilichomfanya Shuku ajute kumsimamisha mbele za watu na kujiona kama kavuliwa nguo. Alitamani kukimbilia kuepuka aibu ile lakini miguu ilikuwa mizito alibakia kasimama kama sanamu.

    “Jamani mimi ni hadhi ya Shuku?” aliwauliza mashoga zake kwa sauti ya juu waliokuwa mbali kidogo na yeye.

    “Ha! Ndicho alichokusimamishia?” waliuliza.

    “Eti jamani mbona leo kajua kunitia nuksi, najiona kama nimekutana na paka mweusi.”

    Yalikuwa maneno yaliyomdhalilisha Shuku na kujiona kama kajipaka kinyesi, Shuku akiwa ndani ya gari aliyawaza yale yaliyomfanya awaogope wanawake wazuri kama ukoma. Alijiuliza siku ile yule demu na shoga zake waliomtoa nishai wakimuona yupo vile watasemaje.

    Alikwenda kupiga picha na kuzipeleka kwa mkuu wa usalama barabarani, kisha alirudi uswazi kwake kulipa kodi ya nyumba. Alipokaribia nyumba aliyokuwa akiishi alifungulia muziki kwa sauti ya juu na kuwafanya wote kuliangalia lile gari.

    Alilifunua na kuwafanya wote waliokuwa wamekaa akiwemo Suzy kulishangaa lile gari lilionekana la ajabu mtaani,alilipaki pembeni ya nyumba anayoishi.

    Alitulia kidogo kabla hajateremka kuwaacha watu washangae kwa muda kisha alilifunga na kutulia tena kabla ya kuteremka huku kila mmoja akimtumbulia macho. Suzy na kampani yake walijiuliza zungu la unga limetoka wapi. Baada ya kutembea kuelekea ndani wote walishtuka kumuona Shuku.

    “Suzy yule si Shuku?”

    “Hapana Shuku awe vile labda ndugu yake.”

    “Hapana ni Shuku.”

    “Makubwa mbona tutakoma, gari na pamba kali katoa wapi?”

    “Najua?”

    “Mmh! Inawezekana alinitongoza akijua mimi ni hadhi yake, maskini sikujua,” Suzy alijikuta akijilaumu kumkataa Shuku.

    “Dharau zako shoga, lakini bado una nafasi, sasa zamu yako kujipendekeza kwake,” shoga yake alimshauri.

    “Naona aibu.”

    “Aibu ya nini wakati ni jambo la kawaida bila kuwa kauzu mjini hatukai.”

    Wakati wakijadiliana na hali ya Shuku, ndani walimpokea kwa mshtuko.

    “Jamani hodi,” Shuku aliingia kwa mama mwenye nyumba.

    “Ha! Shuku?” alishtuka kumuona alivyolipuka.

    “Ndiyo mimi mama.”

    “Ha! Mwanangu siamini!”

    “Amini mama ni mimi.”

    “Karibu mwanangu.”

    “Asante, sasa mama mi si mkaaji kile chumba alichohama mtu jana kina mtu?”

    “Hakina baba.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa mama, sasa hivi nitalipia miaka miwili na deni ulilokuwa ukinidai.”

    “Hakuna tatizo baba, tena utakuwa amenisaidi maana hali ilikuwa tata.”

    “Ila chumba changu kitakuwa na vitu vyangu nami nitakuja siku moja moja, lakini sasa hivi nina maisha mengine kabisa.”

    “Jamani Shuku sasa hivi unaishi wapi?”

    “Utajua muda si mrefu mama.”

    Shuku alimuhesabia fedha ya miaka miwili na deni kisha alimpa elfu ishirini ya soda.

    “Asante mwanangu, Mungu akuzidishie huku uliko.”

    “Atuzidishie wote, ila baada ya muda nitakuja kubadili vitu vya ndani, na hii fedha atampa salmini amihamishie vitu vyangu.”

    Shuku baada ya kulipia pango miaka miwili aliagana na mama mwenye nyumba na kuelekea kwenye gari lake. Wakati anatoka aliwakuta wale wanawake wakisumbiri kwa hamu wamuone kwa mara nyingine, Shuku aliyelipuka pamba za nguvu na kamba nzito shingoni, chini alikuwa na raba kali. Kwa jinsi alivyokuwa hakukuwa na mwanamke yeyote anayeweza kusimamishwa na Shuku akakataa.

    Kabla ya kutoka nje alivaa miwani ili aweze kuwasanifu waliombele yake, alipofika mbele ya gari lake aliwatazama wale wasichana macho yalivyowatoka kama wameona meli barabarani, Shuku alichekea moyoni. Kabla ya kuondoka walitokea washkaji zake waliokuwa wakirudi toka kwenye mihangaiko, kwanza walimpita bila kumjua alipowaita ndipo waliposhtuka na kushangazwa na maajabu ya dunia.

    “Shuku ni wewe?”

    “Ni mimi ndugu zangu.”

    “Mbona kama njozi ni asubuhi tulikuwa pamoja ajabu sasa hivi umekuwa kama mtu wa hadithini?”

    “Ni historia ndefu ila tutazungumza wiki endi.”

    “Sasa tuachie basi mshiko, yaani baada ya kuachana asubuhi siku ya leo imekuwa na gundu tupu.”

    “Poa wangu,” Shuku aliingiza mkono mfukoni na kutoa fedha alizozihesabu kwa kuzionesha ili wale wasichana waone na kuhesabu elfu therasini na kumpa kila mmoja elfu kumi kisha aliwaaga rafiki zake.

    “Sasa washikaji ngoja nirudi nikapumzike, nilikuja kulipia chumba changu pia nilipitia kwa mkuu wa trafiki kwa ajili ya leseni si mnajua sina gamba sitaki nikitembea na gari nipate usumbufu.”

    “Mmh! Hatukuwezi, sasa ndo upo anga zipi?”

    “Mtajua tu washikaji zangu nikija jumapili mtaelewa.”

    Baada ya kusema vile aliingia kwenye gari, kabla ya kuondoka alilifunua gari na kuwafanya rafiki zake wapige kelele za mshangao.

    “Wawooo, si mchezo mwana una kitu cha nguvu mwaka huu wanga lazima wazime zao.”

    “Poa washkaji baadaye,” Shuku alisema huku akiwasha gari aondoke. Wakati Shuku akiagana na rafiki zake ili aondoke zake Suzy na shoga zake walikuwa kwenye kigagaziko kikubwa wafanye nini ili kumnasa Shuku.

    “Sasa jamani nitafanyaje na Shuku ndio anaondoka?



    “Jamani mimi ni hadhi ya Shuku?” aliwauliza mashoga zake kwa sauti ya juu waliokuwa mbali kidogo na yeye.

    “Ha! Ndicho alichokusimamishia?” waliuliza.

    “Eti jamani mbona leo kajua kunitia nuksi, najiona kama nimekutana na paka mweusi.”

    Yalikuwa maneno yaliyomdhalilisha Shuku na kujiona kama kajipaka kinyesi, Shuku akiwa ndani ya gari aliyawaza yale yaliyomfanya awaogope wanawake wazuri kama ukoma. Alijiuliza siku ile yule demu na shoga zake waliomtoa nishai wakimuona yupo vile watasemaje.

    Alikwenda kupiga picha na kuzipeleka kwa mkuu wa usalama barabarani, kisha alirudi uswazi kwake kulipa kodi ya nyumba. Alipokaribia nyumba aliyokuwa akiishi alifungulia muziki kwa sauti ya juu na kuwafanya wote kuliangalia lile gari.

    Alilifunua na kuwafanya wote waliokuwa wamekaa akiwemo Suzy kulishangaa lile gari lilionekana la ajabu mtaani,alilipaki pembeni ya nyumba anayoishi.

    Alitulia kidogo kabla hajateremka kuwaacha watu washangae kwa muda kisha alilifunga na kutulia tena kabla ya kuteremka huku kila mmoja akimtumbulia macho. Suzy na kampani yake walijiuliza zungu la unga limetoka wapi. Baada ya kutembea kuelekea ndani wote walishtuka kumuona Shuku.

    “Suzy yule si Shuku?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapana Shuku awe vile labda ndugu yake.”

    “Hapana ni Shuku.”

    “Makubwa mbona tutakoma, gari na pamba kali katoa wapi?”

    “Najua?”

    “Mmh! Inawezekana alinitongoza akijua mimi ni hadhi yake, maskini sikujua,” Suzy alijikuta akijilaumu kumkataa Shuku.

    “Dharau zako shoga, lakini bado una nafasi, sasa zamu yako kujipendekeza kwake,” shoga yake alimshauri.

    “Naona aibu.”

    “Aibu ya nini wakati ni jambo la kawaida bila kuwa kauzu mjini hatukai.”

    Wakati wakijadiliana na hali ya Shuku, ndani walimpokea kwa mshtuko.

    “Jamani hodi,” Shuku aliingia kwa mama mwenye nyumba.

    “Ha! Shuku?” alishtuka kumuona alivyolipuka.

    “Ndiyo mimi mama.”

    “Ha! Mwanangu siamini!”

    “Amini mama ni mimi.”

    “Karibu mwanangu.”

    “Asante, sasa mama mi si mkaaji kile chumba alichohama mtu jana kina mtu?”

    “Hakina baba.”

    “Sasa mama, sasa hivi nitalipia miaka miwili na deni ulilokuwa ukinidai.”

    “Hakuna tatizo baba, tena utakuwa amenisaidi maana hali ilikuwa tata.”

    “Ila chumba changu kitakuwa na vitu vyangu nami nitakuja siku moja moja, lakini sasa hivi nina maisha mengine kabisa.”

    “Jamani Shuku sasa hivi unaishi wapi?”

    “Utajua muda si mrefu mama.”

    Shuku alimuhesabia fedha ya miaka miwili na deni kisha alimpa elfu ishirini ya soda.

    “Asante mwanangu, Mungu akuzidishie huku uliko.”

    “Atuzidishie wote, ila baada ya muda nitakuja kubadili vitu vya ndani, na hii fedha atampa salmini amihamishie vitu vyangu.”

    Shuku baada ya kulipia pango miaka miwili aliagana na mama mwenye nyumba na kuelekea kwenye gari lake. Wakati anatoka aliwakuta wale wanawake wakisumbiri kwa hamu wamuone kwa mara nyingine, Shuku aliyelipuka pamba za nguvu na kamba nzito shingoni, chini alikuwa na raba kali. Kwa jinsi alivyokuwa hakukuwa na mwanamke yeyote anayeweza kusimamishwa na Shuku akakataa.

    Kabla ya kutoka nje alivaa miwani ili aweze kuwasanifu waliombele yake, alipofika mbele ya gari lake aliwatazama wale wasichana macho yalivyowatoka kama wameona meli barabarani, Shuku alichekea moyoni. Kabla ya kuondoka walitokea washkaji zake waliokuwa wakirudi toka kwenye mihangaiko, kwanza walimpita bila kumjua alipowaita ndipo waliposhtuka na kushangazwa na maajabu ya dunia.

    “Shuku ni wewe?”

    “Ni mimi ndugu zangu.”

    “Mbona kama njozi ni asubuhi tulikuwa pamoja ajabu sasa hivi umekuwa kama mtu wa hadithini?”

    “Ni historia ndefu ila tutazungumza wiki endi.”

    “Sasa tuachie basi mshiko, yaani baada ya kuachana asubuhi siku ya leo imekuwa na gundu tupu.”

    “Poa wangu,” Shuku aliingiza mkono mfukoni na kutoa fedha alizozihesabu kwa kuzionesha ili wale wasichana waone na kuhesabu elfu therasini na kumpa kila mmoja elfu kumi kisha aliwaaga rafiki zake.

    “Sasa washikaji ngoja nirudi nikapumzike, nilikuja kulipia chumba changu pia nilipitia kwa mkuu wa trafiki kwa ajili ya leseni si mnajua sina gamba sitaki nikitembea na gari nipate usumbufu.”

    “Mmh! Hatukuwezi, sasa ndo upo anga zipi?”

    “Mtajua tu washikaji zangu nikija jumapili mtaelewa.”

    Baada ya kusema vile aliingia kwenye gari, kabla ya kuondoka alilifunua gari na kuwafanya rafiki zake wapige kelele za mshangao.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wawooo, si mchezo mwana una kitu cha nguvu mwaka huu wanga lazima wazime zao.”

    “Poa washkaji baadaye,” Shuku alisema huku akiwasha gari aondoke. Wakati Shuku akiagana na rafiki zake ili aondoke zake Suzy na shoga zake walikuwa kwenye kigagaziko kikubwa wafanye nini ili kumnasa Shuku.

    “Sasa jamani nitafanyaje na Shuku ndio anaondoka?”

    Suzy aliuliza baada ya kuchanganyikiwa hasa akikumbuka kuna siku alimtoa niashai mbele za watu na mashoga zake. Alijiulaumi bora angemkatalia kistaarabu kuliko alichomfanyia na siku ile aliamini kabisa hawezi kumsikiliza.

    “Shoga jitoe akili muwahi kabla hajaondoka na kumwita mpenzi, Suzy unalipa hawezi kuchomoa.”

    “Kweli eeh!”

    “Muwahi kabla hajageuza gari.”

    Suzy alitoka mbio kukimbilia gari la Shuku, alipolikaribia alimwita.

    “Shuku.”

    Shuku kabla ya kuitikia aligeuka kumtazama na kumuona ni Suzy alichekelea moyoni na kuona alichokitaka kimefanikiwa. Suzy alilisogelea gari huku akimwita kwa sauti.

    “Shuku mpenzi.”

    Shuku alisimamisha gari na kumsubiri anataka kumwambia nini.

    “Shuku mpenzi mambo?”

    “Poa, vipi unasemaje?”

    “Jamani Shuku mpenzi maneno gani hayo, siku ile uliponitongoza nilijilaumu kwa maneno niliyokutolea, lakini lazima nikueleze ukweli. Shuku nimegundua wewe ni mwanaume mzuri.”

    “Asante.”

    “Kwa hiyo?”

    “Mimi si taipu yako.”

    “Jamani Shuku yale yalikuwa maneno tu, lakini ukweli kama ulivyosema ulikuwa na haki ya kuyasema yale.”

    “Ni kweli, lakini mimi sasa hivi mademu wangu wa geti kali si ninyi kunguru wa Zanzibar hamfugiki mmezoea kula utumbo wa kuku nikikupeleka Masaki utachafua.”

    “Ha! Shuku?”

    Shuku hakujibu kitu alilifunga gari kwa juu na kuwa ndani kisha alimtimulia vumbi na kumwacha Suzy amesimama kama sanamu huku akiaibika mbele za watu na shoga zake kutokana na kuoneka matawi ya juu mwanaume yeyote apindui kwake. Ilikuwa aibu ya mwaka kwa Suzy kumtokea, alisimama kwa muda akiitumbulia macho gari mpaka lilipopotea. Kurudi miguu ilikuwa mizito, kwa aibu iliyomkuta alitamani ardhi ipasuke immeze lakini haikuwezekana. Shoga yake mmoja alimfuata na kumshika mkono na kumuondoa alipokuwa amesimama kama kagandishwa na gundi.

    “Pole dada.”

    “Mmh! Siamini yaani Shuku ndiyo kaniadhiri namna hii tutaona, nipo radhi hata kumroga hawezi kunidhalilisha kiasi hiki.”

    “Achana naye si unajua tena maskini akipata matako hulia mbwata.”

    “Yaani wee acha tu sijui aibu hii utafutika lini, hivi Mwaju mtaani watu watanitazamaje kwa kitendo cha Shuku?” Suzy alisema huku akitokwa na machozi ya uchungu.

    “Lakini dada usisahau muosha huoshwa, kwa kweli hata mimi sikufurahi siku ile ulivyomdhalilisha Shuku.”

    “Lakini kwa wakati ule ningemuweka wapi na hali yake ile hata angetupwa jalalani asingeliwa na paka?”





    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Lakini dada usisahau muosha huoshwa, kwa kweli hata mimi sikufurahi siku ile ulivyomdhalilisha Shuku.”

    “Lakini kwa wakati ule ningemuweka wapi na hali yake ile hata angetupwa jalalani asingeliwa na paka?”

    “Hizo nyodo zako ndizo zilizokuponda, shoga una maneno ya shombo lakini leo umepatikana. Basi leo umepata pa kumweka na yeye amekukosa pa kukuweka.”

    “Mmh! Kweli usimdharau mtu hujui kesho atakuwaje.”

    Suzy hata kijiweni alishindwa kukaa kwa aibu alikwenda chumbani kwake na kujifungia ndani kwa aibu ya mwaka iliyompata kwa kudhalilishwa na mtu aliyemdhalilisha.

    ****

    Shuku kitendo cha kupapatikiwa Suzy kilimpa kichwa kilichomfurahisha zaidi kitendo cha kumuadhili Suzy aliyejifanya queen wa mtaa. Baada ya kumtimulia vumbi na kuondoka moyo wake ulifurahi sana na kuamini kweli malipo yapo duniani kesho hesabu.

    Aliamua kupitia maeneo ya Temeke Mkoroshini kwa yule msichana aliyempagawisha. Alipofika pale alikuwa ndiyo anaingia kwenye gari la mshefa wake na kuondoka. Alipanga siku ya pili awahi mapema ili aweze na yeye kutangaza ufalme wake. Aliamua kurudi nyumbani kupumzika, alipofika nyumbani alimkuta MJ anataka kutoka akiwa na binti mmoja mdogo aliyeonekana mwanafunzi ya sekondari lakini alikuwa na mgongo wa haja. Alijiuliza kipi kinachomfanya Mj apende wanawake wenye migongo mikubwa au alikuwa na ajenda nayo.

    “Vipi mzee unatoka nini?”

    “Ndiyo maana yake, shemeji yako huyu anaitwa Mamu.”

    “Asante, mambo shemu?” Shuku alimsalimia demu wa rafiki yake aliyekuwa amejilaza kifuani kwa Shuku.

    “Poa,” alijibu huku akimwemwesa midomo na kumfanya Shuku ateseke na kutamani MJ angempa yule.

    “Sasa?”

    “Mi ndo naingia kupumzika nimechoka.”

    “Acha ushamba hapa ni raha kwenda mbele badili nguo tunaondoka pamoja nataka leo nikupeleke viwanja ulijue jiji.”

    “Kwani shemu mgeni?” Mamu aliuliza.

    “Mwenyeji ila anaogopa jiji.”

    Shuku hakujibu kitu aliingia ndani na kujimwagia maji kisha alibadili nguo za kutokea kisha alitoka na MJ katika gari moja kwenda viwanja.

    “Twende Bills,” MJ alimwambia Shuku aliyekuwa dereva MJ na demu wake walikaa siti ya nyuma.

    “Bills ndiyo wapi tena?” Bills lilikuwa jina geni kwa Shuku aliyezoea disco vumbi.

    “Jamani mbona unaniangusha Best.”

    “Sasa kama sehemu siijui niende tu si ndiyo utanicheka.”

    “Bilicanas.”

    “Kumbe ndiyo Bills.”

    “Kwa kifupi, ukirudia mara ya pili watakucheka.”

    “Siogopi kuchekwa ipo siku wanaonicheka nami nitawacheka, kama nilivyomtoa leo mtu shoo.”

    “Wacha wee, uswazi nini?”

    “Nitakupa kituko baadaye.”

    Shuku aliiwasha na kuelekea Bills, muda ulikuwa umekwenda sana ilikuwa saa tatu na nusu usiku. Walifika majira ya saa nne usiku Bills na kuingia ndani ambako kulikuwa kuna shoo ya Twanga.

    Walipanda juu na kutafuta sehemu nzuri na kuagiza vinywaji, muziki ulipokolea Mj na demu wake waliteremka chini kusugua kisigino. Shuku yeye alitulia huku akinywa bia yake taratibu, alitembeza macho yake ndani ya ukumbini na kushangaa kuona kila mwanamke mle ndani alikuwa mzuri sana.

    Moyoni aliamini alichokiamini siku zote mwenye fedha ndiye mwenye haki ya kula na kuishi maisha mazuri hata kufanya anavyotaka. Pamoja na kupewa uhuru wa kufanya lolote lakini kikwazo kilikuwa kutegemea kila kitu, alijiuliza kama atamtongoza mwanamke na kumuomba fedha itabidi amuombe MJ kitu ambacho aliamini atakuwa anajidhalilisha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alinyanyuka na kuelekea msalani, alipokuwa akielekea msalani macho yake yalipatwa na mshtuko. Msichana aliyeutesa moyo wake asubuhi alikuwa akitoka msalani huku akiremkebisha nguo yake iliyopanda sana hadi nguo ya ndani kuonekana.

    Alishangaa kumkuta na yeye yupo mule akila raha , alijikuta mateso ya asubuhi yakianza upya. Yule msichana aliponyanyua macho alikutana na Shuku aliyemtumbulia macho kama fundi saa. Alimkuta Shuku macho yamemtoka pima alicheka na kusema:

    “Kaka yangu acha kuangalia sana nguo zinaweza kudondoka ukawa kipofu,” alimminya jicho na kutabasamu na kuachana naye kurudi ukumbini.

    Shuku alijikuta akienda mbele huku akiangalia nyuma na kujikuta akiuvaa ukuta kitu kilichomfanya yule msichana aseme.

    “Wee kaka jamani, poleee.”

    Yule msichana alirudi hadi alipokuwa amesimama Shuku na kumshika sehemu aliyojigonga na kujishika kwa mkono.

    “Jamani kaka yangu nini tena? Kipi cha ajabu umekiona kwangu?”

    “Wee acha toka asubuhi unanitesa,” Shuku alimtoka bila kujielewa vibia viwili vilimpa ujasili.

    “Makubwa, mimi nimekutesa toka asubuhi, mbona ndo tunaonana?”

    “Ipo siku utajua tu.”

    “Mmh! Haya kwaheri eeeh,” alisema yule msichana huku akiondoka kwa mwendo wa madaha na kuzidi kumuweka Shuku kwenye wakati mbaya kiasi cha kutamani kulia ili aonewe huruma.

    Baada ya kujisaidia alijikuta akitafuta sehemu aliyokaa yule msichana, hakuwa mbali na meza aliyokuwa. Alikaa usawa wa kutazamana yule msichana kila aliponyanyua uso alikutana na yule msichana ambaye kila walipotazamana alimkonyeza na kumbusu busu la hewani ambalo lilimchanganya sana Shuku ambaye ili kupoza mateso alijikuta akinywa pombe nyingi na kuanza kuona giza kiasi cha kushindwa kuona mbele.

    MJ aliporudi alimkuta mshikaji wake kalewa sana, kwa vile muda ulikuwa umekwenda alimnyanyua na kurudi naye nyumbani. Alipomfikisha nyumbani alimwingiza chumbani kwake na kumlaza kitandani na kushangazwa na rafiki yake kunywa pombe kiasi kile.

    Siku ya pili baada ya kurudi kupata supu Mj alimuuliza rafiki yake:

    “Shuku jana umeniaibisha unywaji gani ule?”

    “Wee acha tu rafiki yangu nilichanganyikiwa sana.”

    “Unachanganyikiwa nini wakati fedha ninayo hukutakiwa kunywa pombe vile kama kwenye sherehe, najua umezoea pombe za uswahilini. Kwa kweli sipendi unywe tena kama vile.”

    “Kaka wala si sababu unayofikiria,” Shuku alijitetea.

    “Kipi kilichokufanya unywe kiasi cha kupoteza kumbukumbu, kibaya zaidi ulikuwa unalia eti umaskini mbaya. Shuku rafiki yangu nimekunyanyasa?” MJ alimuuliza kwa maskitiko.

    “Hapana.”

    “Sasa kipi kilichokufanya umwage machozi huku ukilalamikia umaskini, Shuku nimekupa uhuru wa kufanya kila kitu bila kukuingilia, nikufanye nini rafiki yangu?”

    “MJ umefika mbali sana wala mimi siku huko, yaliyonichanganya nikikueleza utacheka mwenyewe.”

    “Yapi hayo tena?”

    “Unajua mkasa wangu unaanzia jana asubuhi kabla ya kuonana na wewe mwokozi wangu.”

    “Mkasa gani?”

    Shuku alimueleza yaliyomkutanayo jana yake asubuhi kutokana na kunyanyaswa na mwanamke mmoja ambaye aliamini asingeweza kumpata labda ndotoni, na hiyo ilitokana na msichana mmoja aliyewahi kumtoa nishai mtaani kutokana na kuonekana pangu pakavu tia mchuzi, ambaye jana yake naye alilipa kiasi cha kumfanyia kitu mbaya.

    “Basi jana Bills si ndiyo wakati nakwenda msalani nikakutana naye uso kwa uso.”

    “Wewe! Ehe ikawaje?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mambo aliyonifanyia yalinichanganya nilipotoka msalani si nikaa karibu na alipokuwa amekaa na jamaa mmoja kila tulipokutanisha macho alinibusu busu la hewani hapo ndugu yangu nilizidi kuchanganyikiwa na kujikuta kupoza mateso yale si ndiyo nikaanza kufakamia mipombe bila kujijua.”

    “Ina maana demu mkali sana?”

    “Kwa upande wangu ni mkali sijui wewe ukimuona.”

    “Anawazidi mademu wangu?”

    “Siwezi kumlinganisha na wa kwako kwa vile bado ni chaguo langu si la kwako.”

    “Unasema alikuwa na jamaa?”

    “Ndiyo.”

    “Jamaa ana mikuki?”

    “Mbuzi hawezi kukufikia wewe unatisha mwanangu.”

    “Basi kama mchovu demu tunachukua.”

    “Atakubali?”

    “Kwa maelekezo yako demu kaelekea kibra anatakiwa kutia kisu tumchinje.”

    “Tutamchinjaje naye ana mtu wake?”

    “Fedha ni kila kitu, kama leo utamuona niite uone tutafanya nini?”

    “Mmh! Sawa MJ.”

    “Shuku usituone tuna majina makubwa mjini, umatemate ndiyo kila kitu.”

    “Nikimpata nitachanganyikiwa.”

    “Mwanamke yeyote tumkimtaka ndugu yangu hapindui, labda leo usiku asije.”

    “Mmh! Nikimpata nitakuwa kama umeninunulia Vogue.”

    “Shuku! Demu mwenyewe yupoje mbona kakuchanganya sana?”

    “Utamuona si mzuri kivile basi tu kanichanganya ile mbaya, hata mgongo laini kama mchicha.”

    “Unakwenda nini?”

    “Walaa, basi tu katokea kunichanganya tu.”

    “Basi usiku tutamuona.”

    Wakiwa katikati ya mazungumzo simu ya MJ iliita aliipokea na kuzungumza kwa sauti:

    “Haloo Baby..eeh nipo utanikuta...wewe njoo siwezi kutoka...Poa.”

    MJ baada ya kukata simu alimgeukia Shuku aliyekuwa amejilaza kwenye kochi akisikiliza muziki huku akimsikiliza MJ na majigambo yake.

    “Shuku ngoja uone chombo cha haja ndipo ujue mwenye umatemate anakula vyote vitamu.”

    “Demu mwingine?”

    “Unauliza shombo kwenye samaki, mi ndo MJ bwana, kila mtoto mzuri mjini ananijua mimi nani?”

    “Basi inawezekana hata ninayemtaka nimempitia?”

    “Sijui tutamuona jioni, kama ni mmoja wa mademu niliowapitia nitakuachia kwa vile ninao wengi.”

    Wakiwa katikati ya mazungumzo kengele ya mlangoni iliita. MJ alifungua kwa rimoti, mlango ulifunguka na kuingia msichana ambaye hakuwa mgeni machoni kwa Shuku, alikumbuka aliwahi kumuona kwenye tivii au kwenye magazeti.

    “Wawooo ma baby,” MJ alinyanyuka kumpokea yule msichana mwenye umbile la kimis.

    “Kwenda huko unipendi wala nini, hujawahi kunipigia simu hata siku moja mpaka nikupigie.”

    “Sasa mama unataka nikupigie hata ukiwa na mheshimiwa.”

    “Basi hata kunibeep?”

    “Kukubeep mtu kama mimi ni aibu, hata huyo mheshimiwa namheshimu kwa vile ni rafiki yangu pia ni mtu mkubwa serikalini. Lakini hafiki hata nusu ya uwezo wangu nilionao.”

    “Haya baba umeshinda.”“Karibu mpenzi mmerudi lini?”

    “Jana usiku, nimekukumbuka sana mpenzi wangu nikasema leo silali mpaka nije niutafune muhogo wangu.”

    “Hakuna tatizo mama nimejaa tele, jamaa yupo wapi?”

    “Amekwenda Ikulu ana kikao na mkuu wa nchi na kesho tunakwenda tena Uingereza kula kuku.”

    “Jilie mama, utakula kaburini?”

    “Ndiyo maana yake, kainmgia kichwakichwa nami namnyoa bila huruma.”

    “Wewe alikuacha wapi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hotelini, hataki hata niende nyumbani bwana yule ana wivu kama dume la mbwa.”

    “Sasa akirudi na kukukosa?”

    “Hawezi kurudi sasa hivi kikao ni kizito, kapigiwa simu na mkuu wa nchi na kutakiwa arudi haraka bila hivyo bado tulikuwa na wiki mbili za kula fedha za walala hoi.”

    “Haya mama.”

    “Siyo haya mama, nataka ukazikamue zote za muda wote ambao hatukuwa pamoja.”

    “Na mzee akitaka?”

    “Hii siyo juu yako, nitajua nifanye nini?”

    “Haya mama elekea mwenyewe juu ya kizimba nikute shingo umeinyonyoa kabisa manyoya nikifika mi nachinja tu.”

    “Wewe nani kakwambia mi mwanamke wa usiku asiojua maandalizi, ukikutana naye anadandia na kupiga pedeli na kumwaga mzigo. Siyo mimi, tena leo kwanza unitandike kama pweza mpaka nilegee mtoto wa kike ukinitia mdomoni nitafunike bila tatizo.”

    “Haya mama tangulia naja.”

    “Ooh! Samahani shemu nitakusalimia nikirudi maana zimenipanda, natangulia mwenyewe gerezani kabla ya hukumu.”

    “Hakuna tatizo shemu,” Shuku alimjibu huku akimeza mate kwa uzuri wa yule msichana.

    Yule msichana ambaye mchanganya Shuku na kushindwa kupata jibu la moja kwa moja ni nani na alimuona wapi, alitembea kwa mwendo wa haraka kuwahi chumbani.

    “Umeona kitu?” MJ alimuuliza Shuku.

    “Nimeona huyu si..siii..”

    “Si nini Shuku?”

    “Namfananisha na Miss Tanzania?”

    “Ndiye yeye hapa ndo kwa MJ kijana nayejua kuutumia ujana wake.”

    “Mmh! Kaka sikuwezi.”

    “Habari ndo hiyo, tutaonana baadaye si umeona mtoto alivyonipiga biti ngoja nikampe kipigo cha pweza.”

    “Sasa akirudi kwa mjanja wake na kuombwa mzigo itakuwaje?”

    “Jibu ameishajibu mbele yako.”

    “Haya kaka mchezo mwema.”

    “Asante.”

    MJ alielekea chumbani na kumwacha Shuku akijiandaa kuzunguka nyumba kwenda kupiga chabo. Kwa mara nyingine Shuku alijiingiza kwenye mateso ya kujitakia baada ya kushuhudia MJ akitoa dozi nyingine nzito huku mtoto wa kike akionyesha umahiri wa kucheza mipira yote ya mwisho kwa umahiri mkubwa.

    Moyoni alijishangaa yeye kuteswa na msichana mmoja wakati MJ kwa siku mbili wameshuhudia mademu wakali wakiingia na kutoka na kila mmoja akiwa mkali kuliko mwingine. Shuku alishuhudia uwezo ya yule msichana kwa kumkataza MJ asifanye lolote amuache afanya mwenyewe kila kitu. Yalikuwa mateso makubwa kwa Shuku kushuhudia nyonga laini ya msichana iliyozunguka kama kifuu cha nazi kwenye meno ya kibao cha kukunia(mbuzi).

    Bila kutegemea mkono uliingia chaka na kuanza kujichua taratibu alijikuta mchicha ukikolea nazi na yai la mbuni kumpasukia mkononi nguvu zilimuishia na kujikuta akijilaza ukutani na taratibu aliseleleka chini huku akikisugua kichwa chake ukutani.

    Akiwa chini amekaa miguu ikiwa haina nguvu mkononi kulikuwa na ute mwingi wa yai ambalo halikuwa la kuku bali la mbuni kwa wingi wa ute.









    Akiwa chini amekaa miguu ikiwa haina nguvu mkononi kulikuwa na ute mwingi wa yai ambalo halikuwa la kuku bali la mbuni kwa wingi wa ute.

    Baada ya kupumzika kwa muda huku akiendeleza kupata mateso kutokana na kilio cha mtoto wa mbwa mwenye njaa kilichokuwa akilia yule msichana kwa utamu wa kuugegeda muhogo. Alinyanyuka pale chini na kurudi ndani japo ndani kilio cha mtoto wa kike kilishawishi kurudi kuangalie MJ anafanya machejo gani yenye kumfanya mtoto wa kike apagawe kiasi kile.

    Japo sauti ile ilimshawishi arudi tena kupiga chabo, lakini yai alilojivunjia lilimfanya akimbilie bafuni ili kujiswafi kwani alikuwa ameloa sana kama gari lilikanyaga dimbwi la maji mengi yaliyomrukia na kumlowesha. Akiwa bafuni alipofungua maji ajimwagie alisikia maumivu makali pembeni ya jicho.

    Alipokwenda kujiangalia kwenye kioo aligundua amechubuka baada ya kujikwangua ukutani bila kujua. Alijikuta akijitazama na kucheka mwenyewe kisha alirudi kuoga huku sehemu aliyojichubua ikiwa na mchubuko ilioonekana wazi.

    Alirudi kukaa sebuleni kumsubiri MJ aliyekuwa akijilia vyake. Baada ya muda alitoka yule msichana akiwa ameongozana na MJ macho yakiwa yamemuwiva kwa utamu wa muhogo.

    “Shemu siku nyingine.” alisema huku akielekea nje.

    “Karibu tena,” Shuku alimkaribisha huku akimpiga jicho la wizi na kujisemea moyoni wenye fedha wanafaidi.

    Baada ya MJ kumsindikiza mpaka nje alirudi ndani na kumuuliza rafiki yake:

    “Vipi kitu umekionaje?”

    “Mungu kakijalia kila idara kaka unafaidi tuache utani.”

    “Mmh! Kawaida sema kuna mheshimiwa mmoja kaingilia penzi letu lakini huyu ndiye niliyetaka kumuoa.”

    “Bonge la demu na kazi linaweza mtoto wa kike anajua kutumika na kuulilia,” Shuku alijisahau na kutaka kumwaga mtama kwenye kuku wengi.

    “Shuku umejuaje? Unanipiga chabo nini?”

    “Walaa, anaonekana tu mtu wa kudeka,” alipindisha ukweli.

    “Na..na hapo jichoni vipi?” MJ alishtuka jeraha la Shuku.

    “Nimejikwangua getini.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Si ungekwenda Dispensary uwekewe dawa kwenye jeraha?”

    “La kawaida haliumi sana.”

    “Sasa mi najipumzisha, mambo mengine utashughulikia mwenyewe.”

    “Poa.”

    Mj alirudi chumbani kwake na Shuku naye aliingia chumbani kwake kupumzika kuvuta muda. ****

    Majira ya saa tatu na nusu usiku waliingia Bills, baada ya kuingia ndani ya ukumbi macho ya Shuku yalitazama kila kona huenda kamuona yule msichana aliyemchanganya jana yake lakini macho yake yalitoka kapa na kujikuta akianza kuichukia siku ile.

    Walikwenda kutafuta sehemu ya kukaa na kuagiza vinjwaji, wakati wote macho ya Shuku alitembea kama setilite kumsaka mrembo wa jana yake. Siku zote MJ hakuwa anatulia sehemu moja kila alipoingia kwenye kumbi za starehe.

    “Shuku mi nazunguka kidogo maana kukaa sehemu moja siwezi.”

    “Poa, wee nenda mi nipo.”

    “Shuku acha ushamba zungukazunguka kidogo ili kusafisha macho unaweza kupata demu wa kula naye raha.”

    “Hata nikimpata si mpaka nikufuate unipe mkwanja?”

    “Ooh! Nilisahau,” MJ alitoa pochi na kumkatia laki mbili.

    “Hizi zinakutosha kama hazitoshi utaishtua.”

    “Poa.”

    MJ aliachana na Shuku na kuteremka chini na kumuacha akipiga ulabu macho yake yakiwa na shauku ya kumuona yule mwanamke. Pamoja ndani ya Bilicanas kulikuwa na wanawake wengi wazuri wenye maumbile ya vishawishi vya ngono kwa wanaume marijali, lakini Shuku macho yake hayakuwaona zaidi ya kumtafuta yuleyule mwanamke kama kipofu aliyeahidiwa kuona.

    Baada ya kunywa kidogo aliamua na yeye kuteremka chini ambako kulikuwa na msanii wa kizazi kipya Dully akiporomosha burudani ya kufa mtu. Kila mmoja alikuwa akirukaruka kutokana na Dully kuwapeleka puta. Shuku akiwa na bia mkononi wakati akijichanganya kwenye kundi la watu waliokuwa wakiondoka sambamba na Dully.

    Aliamua na yeye kufurahia siku ile kwa kuamini siku ya pili atakwenda maeneo anayokaa yule demu na gari kali amng’oe kwa upole. Wakati akicheza kwa bahati mbaya alimkanyaga dada mmoja na kujikuta akigeuka kumuomba radhi wakati huo muziki ulikuwa umenyamaza.

    Macho yake yalipatwa na mshtuko baada ya kukutana na mtu aliyekuwa na hamu ya kumuona.

    “So..so..rry mrembo,” alipatwa na kigugumizi.

    “Mmh, He! ni wewe tena?” yule msichana alimuuliza kwa kumshangaa.

    “Haikuwa dhamira yangu,” Shuku alijitetea.

    “Mmh! Mbona unajitetea sana kama nimekulaumu?” Yule mwanamke alizidi kumshangaa Shuku.

    “Najua nimekuumiza.”

    “Kaka wee aliyeniumiza hakujitetea kwa vile alikuwa ndo ananiingiza dunia ya wakubwa, sasa hivi wanakula wengine wala hana habari.”

    “Basi...na..na.”

    “Wee kaka vipiii? Usinigeuze mwalimu wa chekechea ninayefundisha watu kusoma, hebu nyoosha maneno nitakuelewa tu.”

    “Ni..ni..nili...” Shuku alijikuta akimung’unya maneno.

    “Mmh! Makubwa, sasa fanya hivyo nipe simu yako,” yule msichana alisema huku akinyoosha mkono.

    Shuku kwa haraka alitoa simu ambayo ilikuwa ya bei mbaya aliyonunuliwa na MJ alingane na yeye.

    “Mmh! Unatisha unatembea na kiwanja mkononi,” msichana alichanganyikiwa kuiona simu ya milioni moja na nusu aliyokuwa nayo Shuku.

    “Mbona mambo ya kawaida tu,” Shuku alicheka kicheko cha dharau cha kujiamini.

    “Sasa hii ndiyo namba yangu naomba kesho tuwasiliane,” yule msichana alisema huku akimrudishia simu Shuku.

    “Leo vipi?”

    “Nipo na mtu na jamaa mtata ile mbaya.”

    “Poa basi mrembo, ya vocha,” kwa kuchanganyikiwa Shuku alimpa laki mbili zote alizopewa na MJ.

    “Asante baby,” yule msichana naye alichanganyikiwa na kujikuta akimbusu na kuachana naye kurudi kwa mjanja wake aliyekuwa mezani akinywa.

    Shuku alikuwa kama yupo ndotoni, kabla ya kuondoka yule msichana alifikicha macho ili kupata uhakika kweli kakutana na yule mrembo. Bado hakukubaliana na kilichotokea alijifinya kidogo na kusikia maumivu na kuamini kweli kilichotokea mbele yake ni cha kweli wala si ndoto.

    Akiwa bado amesimama yule mwanamke alipita mbele yake akiwa ameongozana na mwanaume ambaye hakuwa mgeni alikuwa jamaa wa siku zote. Wakati wakitoka yule msichana aliugeuka nyuma na kusema kwa ishara.

    “Kesho basi.”

    “Poa.”

    Walitoka nje na kumwacha Shuku akiwa bado amesimama palepale kama sanamu akimsindikiza kwa macho na kuuapia moyo wake siku atakayomtia kwenye himaya yake atamaliza ufundi wote kuhakikisha akionja achonge mzinga kabisa.

    Akiwa bado yupo katikati ya dimbwi la mawazo simu yake iliita, alipoangalia alikuwa ni MJ. Alipokea:

    “Haloo vipi?”

    ”Upo wapi?”

    “Chini.”

    “Basi nilijua bado upo juu.”

    “We upo wapi?”

    “Nipo juu.”

    “Poa nakuja.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Noo, nakuja hukohuko nataka tuondoke kuna demu wangu mmoja wa chuo kanipigia simu yupo home ananisubiri.”

    “Hakuna tatizo nakusubiri.”

    Shuku alikata simu na kukumbuka alikuwa hajasevu ile namba ya mrembo.

    “Ooh! Shit,” alipiga kelele peke yake baada ya kugundua namba imefutika.

    Alitoka nje mbio labda atamuwahi lakini alipofika nje aliiona gari ndo inaondoka. Alijikuta akichuchumaa na akipiga ngumi chini na kujiona bwege namba moja. Simu yake iliita tena alipoangalia ilikuwa ya Mj na kujikuta akiongezwa hasira.

    Hakuipokea aliendelea kuchuchumaa akitamani kulia kwa kuamini amepoteza alichokitafuta kwa muda mrefu.

    MJ baada ya kumtafuta kwa muda mrefu sehemu aliyomuelekeza kisha kumpigia simu iliyoita bila kupokelewa, aliamua kutoka nje ili aondoke kwa kuamini Shuku alikuwa na fedha ya kutosha ya kuweza kukodi teksi kwa muda ule mpaka nyumbani.

    Alipotoka nje alishangaa kumuona rafiki yake akiwa amechuchumaa chini mkono mmoja kashika chini na mwingine kashikilia simu.

    Alimshangaa rafiki yake na kujiuliza mbona yupo vile, wasiwasi wake labda pombe zimemzidia na pale alipochuchumaa alikuwa akitapika. Alimsogelea na kumshangaa kumkuta rafiki yake akipiga ngumi chini huku akijilaumu.

    “Shuku vipi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wee acha, mimi bonge la fala.”

    “Bonge la fala! Una maana gani?”

    “Yaani nimefanya bonge la mistake.”

    “Mistake gani tena, umeibiwa?”

    “Hapana.”

    “Umefanya kosa gani lililokuchanganya?”

    “Si yule demu.”

    “Eeh! Kafanya nini?”

    ” ITAENDELEA 

0 comments:

Post a Comment

Blog