Search This Blog

Monday, October 24, 2022

TOROJO BAMIA ( WINGA TELEZA ) - 3

 





    Chombezo : Torojo Bamia (Winga teleza)

    Sehemu Ya Tatu (3)



    “Wee acha, mimi bonge la fala.”

    “Bonge la fala! Una maana gani?”

    “Yaani nimefanya bonge la mistake.”

    “Mistake gani tena, umeibiwa?”

    “Hapana.”

    “Umefanya kosa gani lililokuchanganya?”

    “Si yule demu.”

    “Eeh! Kafanya nini?”

    “Si nimekutana naye na kunipa namba ya simu, bahati mbaya nilisahau kuisevu, uliponipigia ikafutika kutoka nje nimemkuta ndo anaishia.”

    “Sasa tatizo nini?”

    “Si kaniambia nimpigie simu kesho, sasa akikosa simu yangu si ataniona miyeyusho hata kunipiga chini mtu anayeutesa moyo wangu.”

    “Kwani somo si kalielewa?”

    “Ndiyo.”

    ”Sasa tatizo nini?”

    “Wasiwasi wangu atasubiri simu akiikosa atanidharau.”

    “Kwao si unapojua?”

    ”Ndiyo.”

    “Basi kesho mtilie timu kwa vile umesema mtu wake mchovu chukua gari lolote mwibukie tumia kiasi chote cha fedha. Kesho nitakuongezea nyingine ili kukuhakikishia rafiki yangu na wewe unafurahia maisha.”

    “Zile ulizonipa nimempa zote sijui itakuwaje?”

    “Achana nazo tayari samaki kala chambo wewe kazi yako kumvuta tu tena hutumii nguvu.”

    “Yaani bila wewe nilikuwa nimeisha changanyikiwa.”

    Shuku alinyanyuka na kuelekea kwenye gari ili warudi nyumbani.

    Wakiwa njiani Shuku alionekana kujifyonza mwenyewe kitu kilichomfanya MJ amuulize rafiki yake.

    “Vipi Shuku mbona sikuelewi?”

    “Wee acha tu.”

    “Si tumezungumza, ni hilohilo au kuna lingine?”

    “Leo nimefanya ujinga wa mwaka.”

    “Shuku acha ushamba huyo demu wako yupo vipi kiasi cha kukuchanganya kiasi hicho?” MJ alimshangaa rafiki yake kudatishwa na demu.

    “Siyo demu bali ujinga niliofanya wa kutosevu namba, mfano kama nisingekuwa najua anapoishi si ingekuwa imekula kwangu.”

    “Ile kwako kivipi kwani watoto wazuri wamekwisha, hii ndiyo tabu ya kutotembea matokeo yake umekuwa kama kipofu aliyeona kwa bahati mbaya kila kitu akiambiwa huamini akifanani na kile alichokiona.”

    “Huwezi kuamini MJ mi si mtu wa mademu lakini yule demu nimejikuta kanichanganya hata sijielewi.”

    “Mmh! Haya siwezi kuingilia utashi wa moyo wako.”

    Walipofika nyumbani MJ alimkuta mtu wake aliyempigia simu. Kwa mara nyingine Shuku alishuhudia msichana mwingine wa nguvu akiwa anamsubiri Mj. Alipomuona walikumbatiana na mabusu mengi.

    “Baby kidogo nikufuate nilijua nitaibiwa,” alilalamika mtoto wa kike ambaye alikuwa na umbile dogo lakini mzigo msalie mtume.

    “Hakuna baby unaniona kicheche siyo?” MJ alijitetea na kumfanya Shuku ajiulize anawezaje kutembea na wanawake wengi kiasi kile bila kufumaniana na wote huja nyumbani kwake bila taarifa.

    Walipoingia chumbani kwao Shuku naye alikwenda kulala, siku ile hakutaka kuangalia filamu kama ilivyo kawaida yake. Kufutika kwa namba katika siku yake kulimnyima raha sana.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku ya pili Shuku aliwahi kuamka na kujiandaa kumfuata yule demu aliyemchanganya. Baada ya maandalizi yote alimfuata MJ chumbani kwake, baada ya kugonga kwa muda MJ alitoka kajifunga taulo. Baada ya kufungua mlango na kumkuta rafiki yake alimuuliza akifikicha macho.

    “Vipi mzee?”

    “Poa.”

    “Mbona asubuhi asubuhi? Halafu umeulamba safari ya wapi, kanisani?”

    “Si kwa yule demu.”

    MJ alijikuta akicheka mpaka machozi yakamtoka na kumfanya Shuku ashtuke na kumuuliza rafiki yake.

    “Unacheka nini sasa?”

    “Kweli rafiki yangu umepania.”

    “Si unajua leo jumapili anaweza kwenda sehemu ikawa tatizo na yeye anajua nitampigia simu.”

    “Mmh! Haya kaka ulikuwa unasemaje?”

    “Nataka gari?”

    “Unataka gari gani?”

    “Utakalonipa.”

    “Shuku hebu acha kujishusha, nimekueleza humu ndani wewe si mgeni chukua chochote unachotoka sitaki mtu ajue hii mali ni yangu kuanzia leo mali yangu ni yako.”

    “Nimekuelewa best.”

    “Funguo zipo kwenye kabati.”

    “Poa wacha niwahi huenda akaenda kanisani.”

    “Kumbe demu wako ni mkristo?”

    “Hata najua.”

    “Kwani anaitwa nani?”

    “Ndugu yangu wee, hata nilikumbuka kumuuliza jina lake.”

    “Kweli umechanganyikiwa mpwa wangu.”

    “Wee acha tu,”

    “Sijui ukimpata itakuwaje?”

    “Lazima nitangaze ndoa.”

    “Acha ushamba, kula raha wewe, huwezi kukimbilia kuoa watoto wazuri kama hawa utamuachia nani.”

    “Ngoja nimpate nitajua yote.”

    “Unaweza kumpapatikia kumbe si mali kitu utafanya nini?”

    “Tutayajua yote nikimtia mkononi.”

    Baada ya mazungumzo ambayo Shuku aliona kama yanamchelewesha kwa kurefusha maneno, aligeuka ili aondoke MJ alikumbuka kitu.

    “Una fedha ya kutosha?”

    “Sina hata senti tano.”

    “Zote nilizokupa umezifanya nini?”

    “Si unakumbuka nilikuambia nimempa zote yule demu.”

    “Ooh! Sorry, nilisahau, subiri,” MJ alisema na kurudi ndani, baada ya muda alitoka na fedha mkononi na kumpa Shuku.

    Shuku alipokea na kushukuru kidogo amlambe miguu.

    “Asante sana rafiki yangu.”

    “Kawaida usijali huu ni mwanzo nataka usahau shida zako.”

    “Nashukuru wacha niwahi.”

    “Kama zikipungua nijulishe nikutumia kwenye akaunti ya simu yako.”

    “Hakuna tatizo.”

    “Kwa fedha niliyokupa mnaweza kwenye hoteli yoyote kubwa jijini na kula chochote na msiimalize.”

    “Asante, wacha niwahi.”

    “Wahi mzee nakuona una ugwadu naye usije ukachemsha si unajua mkamia maji.”

    “Haya lazima niyanywe hata kwa dilip.”

    “Teh teh teh.. haya baba kila la heri,” kauli ya Shuku ilimchekesha MJ.

    Shuku alitoka nje na kwenda kuchukua gari la kufunuka juu ambalo alilipenda sana. Akiwa amepiga pamba za kweli na kamba nzito kifuani aliondoka na gari kuelekea Temeke Mikoroshini kwa yule demu aliyemdatisha kichizi.

    Shuku aliendesha gari hadi Temeke Mikoroshini eneo analoishi yule msichana. Alipokaribia pale aliendesha gari taratibu huku akipepesa macho kuangali nyumba aliyomuona akiingia yule msichana siku ya kwanza akichota maji .

    Akiwa bado aking’aa macho kwenye nyumba ile macho yake yalitua kwa msichana mmoja aliyekuwa anatoka kuchota maji akiwa amevaa dela lililokuwa limechomekwa kwenye nguo ya ndani na kufanya umbile ya nyuma kuonekana huku likipishana kama wasafiri wa mbagala wakigombea kuingia kwenye daladala muda wa jioni.

    Shuku alitabasamu moyoni baada ya kumtambua kumbe ni yule msichana aliyemfuata na kujisemea moyoni. “Nitafaidi” alimuona akikaribia kuingia kwenye geti la kwao. Alipiga honi lakini yule msichana hakugeuka aliingia ndani, alisogeza gari na kwenda kulisimamisha sehemu ambayo alimuona Sharobaro anayemchukua yule demu akilisimamisha siku alipomfuata.

    Alilifungua gari na kuwa wazi kumsubiri akitoka, kama asingetoka ingebidi amtume mtu amfuate. Alitoka nje ya gari na kulikalia kwa mbele mguu mmoja ukiwa chini na mwingine umekanyaga mbele ya gari.

    Akiwa ananyanyua macho alipokuwa akiangalia simu yake, alimuona yule msichana akiwa na ndoo mkononi akielekea bombani. Shuku alimshtua:

    “Psiiii,” yule msichana aligeuka na kumtazama lakini hakumtambua, aligeuka kuendelea na safari yake,Shuku alirudia tena kuita.

    “Psiiiiii.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Yule msichana alisimama tena na kugeuka kisha alijishika kifuani na kuuliza.

    “Mimi?”

    “Ndiyo.”

    Yule msichana alirudi taratibu akiwa amemkazia macho mtu ambaye alionekana anazo kutokana kulipuka kwa pamba pia mkoko wa nguvu. Alipomkaribia alimgundua Shuku, alishtuka na kuitupa ndoo kisha alikimbia hadi aliposimama huku akipiga kelele na kwenda kumvamia.

    “Wawooo baby,” alimkumbatia kwa nguvu na wote kulalia gari.

    “Jamani baby ndiyo nini kunitesa mwenzio yaani nimesubiri simu yako kama wokovu?”

    “Wee acha tu.”

    “Niache nini baby, nilijua labda umenitosa.”

    “Nikutose mtoto mzuri kama wewe?”

    “Sasa mbona hujanipigia simu.”

    “Nilitaka nikufanyie Surprise.”

    “Mmh! Asante, umejuaje ninapokaa?”

    “Huwezi kuamini nakupenda muda mrefu, nimekufuatilia muda mrefu.”

    “Jamani baby, mi sitaki, mbona hukuniambia zamani au sikukuvutia siku za nyuma?”

    “Walaa, nilijua nimewahiwa, wasiwasi wangu yule mchovu amekuoa sikupenda kuingilia ndoa yako.”

    “Kipi kilichokufanya unitokee?”

    “Aah! Nilimuona jamaa mwenyewe mchovu hata kiganjani hajai.”

    “ Kweli baby yaani hata usafiri wako si wa kawaida.”

    “Tuachane na hayo, nimekufuata.”

    “Kweli baby?”

    “Sikutanii kama upo tayari tuondoke nikakupe maisha ya ndotoni.”

    “Mbona asubuhi sana baby?”

    “Au baby una safari nyingine?”

    “Walaaa,” mtoto wa kike aliruka kimanga.

    “Basi baby nipendapo huwa sina subra.”

    “Mmh! Haya, basi nakuja,” yule msichana alirudi ndani, safari ya kwenda bombani ilikufa.

    Shuku aliingilia kwenye gari na kufungulia muziki kwa sauti ya juu kidogo. Kila mtu alivunja shingo kumuona tajiri mtoto. Ilikuwa ni vigumu kumwambia mtu huyo siku mbili zilizopita alikuwa hajui kula yake na kuishi maisha ya kubahatisha alitembea kwa miguu miguu imempauka asingekubali hata kwa mtutu.

    Shuku akiwa na simu yake ya bei mbaya muda wote alijifanya yupo bize na simu yake ili tu kuwakonga watu mtaani ambao walimtazama kwa jicho la matanio. Shuku alijiuliza mtoto mzuri kama yule ampe machejo gani ili akigusa anase asitoke tena.

    Moyoni alijiapiza kumaliza utundu wote anaoujua na asioujua ili kuhakikisha anagawa dozi maridhawa itakayomfanya mtoto wa kike kila akimkumbuka basi ampigie simu. Wazo la kumpeleka nyumba hakukubaliana nalo.

    Aliamini kwa vile alikuwa na mshiko wa nguvu alitakiwa ampagawishe ili hata jamaa akija ampe kibuti cha nguvu. Akiwa ameinama alishtushwa na sauti tamu.

    “Sweeeti.”

    Shuku alinyanyua macho na kukutana na mtoto mrembo, siku ile alipendeza mara dufu. Binti alikuwa amevaa gauni fupi la rangi ya papo lililoishia chini kidogo ya makalio lenye mkono mmoja na upande mwingine bega lilikuwa wazi juu alivalia wigi liliongeza uzuri wake na chini alivaa viatu virefu vyenye rangi sawa na gauni lake.

    Begani alikuwa amebeba mkoba mdogo mwenye rangi sawa na gauni. Aliachia tabasamu pana na kuonesha meno yake madogo kama mahindi ya bisi yaliyonakshiwa na mwanya mwembamba. Midomo yake ilipambwa na rangi ya midomo inayofanana na gauni na kumfanya apendeze zaidi.

    “Wawooo, kweli najua kuchagua, wewe ni mwanamke mzuri kuliko wote walio chini ya jua.”

    “Asante baby wangu.”

    Shuku bila kujielewa baada ya kuchanganywa na uzuri wa mrembo yule alijikuta ameteremka kwenye gani na kwenda kumlaki mrembo ambaye mpaka muda ule hakulijua jina lake na kumpokea kama malkia. Alimshika mkono na kuingia naye ndani ya gari.

    “Karibu malkia wangu.”

    “Asante mfalme wangu,” binti alijibu kwa sauti ya kudeka huku akiketi kwenye kiti kwa mbwembwe.

    Shuku alikaa upande wake kabla ya kuondoka alilifunika gari kwa juu na kumfanya yule mrembo kushtuka.

    “Wawooo, baby sikuwezi upo juu.”

    “Kawaida tu haya ni mambo madogo.”

    Baada ya kufungua kiyoyozi na kuwasha muziki kwa sauti ya chini tofauti na mwanzo alifungua muziki wa matangazo. Alimgeukia mrembo na kumsifia:

    “Hongera mpenzi umependeza sana.”

    “Asante, na wewe pia baby wangu hongera umependeza.”

    “Asante,” Shuku alisema huku akimbusu na kuondoa gari

    “Asante baby, yaani busu lako limenisisimua sijui mambo yatakuwaje?”

    “Kawaida tu, mmh, niambie unataka twende hoteli gani ambayo unaamini tukipumzika leo utafurahi.”

    “Yoyote?”

    “Yoyote ile ambayo unaamini tukipumzika leo moyo wako utakuwa kwatu.”

    “Mmh! Unajua mimi na ujanja wangu sijalala hoteli ya Serena zamani Royal. Lakini naona kama ya gharama sana, ungechagua yoyote baby kwangu sawa.”

    “Babiii utaniangusha, nimekueleza fedha si tatizo bali matumizi.”

    “Basi Serena baby.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Shuku aligeuza gari na kuelekea katikati ya jiji kula raha na mrembo. Walipofika Serena hoteli walipaki gari kwenye maegesho na kuingia ndani kwa mwendo wa madaha kama wapenzi wa muda mrefu. Shuku akijifanya kujichelewesha nyumba ili aweze kuzisanifu sehemu za nyuma za binti mrembo. Kila alivyotembea mtikisiko wa nyuma ulizidi kumuacha hoi huku akijiuliza ndani itakuwaje wakati wa hukumu ya kisu na nyama.

    Msichana naye baada ya kujua sababu ya kutangulizwa aliongeza manjonjo ya kulegeza makalio ambayo yalizidi kutetemeka kama yamemwagiwa maji baridi usiku wa manane.

    Shuku alijisahau na kusimama akishika mikono kiunoni kumtazama binti mrembo na kutikisa kichwa na kunyanyua mikono juu kumshukuru Mungu kwa utundu wake. Binti mrembo baada ya mwendo mfupi aligeuka nyuma na kumkuta Shuku akimshukuru Mungu.

    “Babiii vipiiii mbona huji?”

    “Nakuja mpenzi.”

    Shuku alichepua mwendo hadi alipokuwa amesimama mrembo na kumshika kiunoni hadi mapokezi.

    “Karibuni wapendanao,” msichana wa mapokezi aliwakaribisha.

    “Asante, habari yako?” Shuku alimsalimia mfanyakazi wa mapokezi.

    “Nzuri tu kaka yangu, karibuni sana.”

    “Asante, tunahitaji chumba.”

    “Vipo, unataka cha daraja lipi?”

    “Cha daraja la juu.”

    “Daraja la juu ni VIP.”

    “Ndicho hichohicho ninachokitaka.”

    “Mmh! Lakini unajua bei yake?”

    “Tatizo bei au kulipata chumbani?”

    “Si kulipia chumba bali kutumia fedha nyingi wakati kuna vyumba vizuri ambavyo vya daraja la kati unavyoweza kuinjoi na wifi yangu. Vyumba kama hivi hulala wageni kutoka nje kama marais na watu wazito.”

    “Samahani dada yangu, hivi hapa Dar kuna hoteli nyota tano ngapi?”

    “Zipo nyingi.”

    “Kwa nini nimekuja hapa?”

    “Kwa sababu umeipenda hoteli yetu.”

    “Na kwa nini nimechagua chumba cha VIP?”

    ”Sijui, lakini wasiwasi wangu labda ulidhania bei yake ni ndogo, hivyo sikupenda Mtanzania mwenzangu kutumia fedha nyingi bila sababu.”

    “Hebu nipe menu niangalie.”

    Dada wa mapokezi alimpa Shuku menu ambayo aliingalia bei ya vyumba na kusema:

    “Mbona fedha kidogo hata ingekuwa mara tatu yake ningelipa,” Shuku alijitapa mbele ya mrembo.

    “Hebu baby.”

    Mrembo alichukua na kuitazama na kushtuka lakini hakuonesha mshtuko wake na kuona tofauti ya nyumba za wageni wa uswazi na za anga za wakubwa.

    Shuku alitoa kiasi cha kulipia chumba, baada ya kuandikisha walielekezwa chumba kwa kupelekwa na mhudumu. Baada ya kuingia ndani mrembo alifurahi sana kuona bonge la chumba ambalo hakuwahi kuingia katika maisha yake yote.

    “Wawooo baby hii ya leo umenifanyia bonge la surprise.”

    Mrembo alisema huku akimkumbatia Shuku.

    “Kawaida tu baby hivi vitu vidogo sana kwangu.”

    Shuku alijikweza wakati na yeye ndiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kuingia kwenye chumba kama kile. Shuku alimbeba juujuu hadi kwenye kitanda cha nguvu na kutua.

    “Yaani baby siamini kuingia na kulala kwenye hoteli na chumba cha gharama kama hiki.”

    “Mbona mambo madogo tu jiandae kula raha zaidi ya hizi.”

    “Kwa nini usinioe kabisa?”

    “Ni haraka sana kula kwanza raha mambo mengine baadaye.”

    “Nakuahidi mimi Lily sitampenda mwanaume yeyote zaidi yako,” Shuku alijikuta akifahamu jina la yule mrembo kwa mara ya kwanza.

    “Lily wewe tu, tulia ule raha.”

    “Yaani yule mchovu anikome tena anikome.”

    “Wewe mwenyewe kuamua kuishi Masaki au Tandale kwa Mtogole.”

    “Baby sihami Masaki hapa nimefika sihami tena.”



    “Lily wewe tu, tulia ule raha.”

    “Yaani yule mchovu anikome tena anikome.”

    “Wewe mwenyewe kuamua kuishi Masaki au Tandale kwa Mtogole.”

    “Baby sihami Masaki hapa nimefika sihami tena.”

    Lily alinyanyuka na kwenda kutoa nguo mwililini ili aweze kujitawala zaidi. Alipofika kwenye kabati alitoa nguo zote na kubakia na bikini iliyoupendezesha mwili wake na kuelekea alipokuwa amekaa Shuku ambaye macho yalikuwa yamemtoka kama mjusi kabanwa na mlango asiamini na yeye kwa mara ya kwanza anakula mtoto wa viwango.

    Shuku alijikuta akijisemea kwa sauti ya chini:

    “Kweli fedha mwana haramu, leo Shuku nakula mtoto wa kiwango.”

    “Baby vipi mbona unanishangaa?”

    “Sikushangai bali penati nilitopiga lilikuwa bonge la penati kama la Pirlo.”

    “Baby kumbe na wewe unacheza mpira?”

    “Siyo penati ya uwanjani.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sasa penati gani tena hiyo?”

    “Si kukuchagua wewe.”

    “Jamani baby kumbe hivyo?”

    “Lily wewe bonge la demu.”

    “Asante mpenzi.”

    Wakati huo Lily alikuwa amefika kwa Shuku na kuanza kumpembua kimoja baada ya kingine kisha alimshika mkono hadi bafuni. Lily alikuwa mzoefu kuingia sehemu kama zile japo hakuwahi kuingia hoteli yenye hadhi ya juu kama ile.

    Kama ingekuwa amemuachia kila kitu afanye Shuku angeumbuka, alizoea vigesti vya vichochoroni vya buku mbili au kumbambia changudoa kichochoroni na kumalizana juu kwa juu, lakini anga kama zile hakuota kuingia na kama ingekuwa fedha yake basi angempeleka demu kwenye hoteli isiyo kuwa na gharama kama ile.

    Baada ya kuingia bafuni waliingia kwenye jakuzi na kujimwagia maji huku Lily akionesha utundu wake asionekane hayupo nyuma kila kitu alikifanya yeye ili Shuku ajue na yeye mambo kama yale si mageni kwake. Kufanya ile kulimpa nafasi Shuku ambaye pia alikuwa mgeni wa vitu vile kujifunza kupitia kwa Lily kwa haraka ili siku ya pili asiwe mgeni tena. Baada ya utundu wa Lily aliomfanya Shuku apasue yai mdomoni huku akigugumia kama dume la njiwa.

    Kwa mara ya kwanza alijikuta akipata raha mwanzo mwisho alizokuwa akiziona kwenye kioo. Naye aliapa kuonesha yeye nani ndani pichi. Baada ya kumaliza kuoga walirudi kitandani huku Lily akionekana kupandwa na mahanjamu kila jicho lake lilipotua kwenye muhogo wa Shuku mwili ulimsisimka.

    “Baby muhogo unanisisimua nipe niugegede mwenzio mate yananidondoka.”

    Shuku alikuna nazi na kuchemsha maji baada ya tui kuchemka alitia mchele na kumfanya mtoto wa kike kutatalika kama makalio yanaumwa na siafu kwa kukipandisha juu kiuno na kuiacha nyonga ukate mawimbi huku Shuku akitandaza soka maridadi iliyowafanya wapenzi walipuke mayowe muda wote kwa pasi za uhakika za Shuku ambazo zilimfikia mlengwa na kumfanya Lily aonesha umahiri wa wepesi wa nyonga yake kuiwahi mipira yote iliyopigwa na Shuku na kuufanya mchezo uwe wa ufundi zaidi kuliko nguvu.

    Lily alikuwa wa kwanza kugeuka golini kuokota mpira baada ya gonga safi za hapa na pale zilizompelekea kusogea mbele ya goli na Shuku kuuchopu mpira uliomfanya anyooshe mbavu bila mafanikio ya kuugusa mpira, goli lile lilimfanya amsifie mfungaji kwa goli tamu alilofungwa na shuku kwa kumng’ang’ania kwa nguvu kuliacha dafu limwage maji baada ya kupasuka.

    “Be..be..be....beeeee,” Lily alipagawa baada ya siku za nyuma kuchezewa na teja kwa muda mrefu lakini siku ile alikutana na mwanaume wa shoka mwenye kuijua kazi yake uwanjani. Aliitafuna midomo kama kamwagiwa kopo la asali.

    “Niite Shuku baby,” Shuku alimwambia huku akimpa uhuru Lily alifuahie utamu wa maji ya dafu yaliyokuwa yakimwagika kwa kumng’ang’ania shingoni.

    “Shuku...Umeniweza...siamini ...siamini.. Shuku kumbe nilikosa raha hizi jamani, ulikuwa wapi Shuku? Mungu kakupendelea kila kitu mbona nitafaidi Lily mimi.”

    Baada ya kutulia Shuku naye alianza kulitafuta bao la kusawazisha kwa kutumia mashuti ya mbali ambayo kwa mara nyingine yalimpeleka Lily marketi kwa kuvunja yai la pili baada ya kuangukia banda la kuku.

    “Shu..shu ..ku we..we..we..kiboko haki ya na..nani lingine hi.. hi..hiloooo.”

    Lily alisema kwa sauti ya kudeka safari hii Shuku akufanya fair play alianzisha mpira mara moja kwani naye alianza kuiona pwani hivyo hakutaka kushusha stimu iliyokuwa inapanda kama sumu ya nyoka.

    Baada ya kuwatoroka mabeki na kuukuta mpira ambao Lily aliamini ni off side, mwanaume aliingia nao kwa kasi huku akimfungasha tela Lily aliyekwenda kumkatia ndani ya wavu kiliwa bao moja la Shuku huku Lily naye akipasua yai la tatu.

    Wote walitulia kama mkwezi mwizi aliyedondoka kwenye mnazi na kufikia kiuno na kumfanya atulie hata kama mwenye mnazi angetokea asingeweza kumkimbia. Walitulia kwa muda kama wamepakwa nta kwa muda.

    Baada ya kila mtu dafu lake kukata maji, alimuachia mwenzake na kujilaza pembeni ya mwenzake. Moyoni bado Shuku aliona kama yupo ndotoni kulala hoteli ya gharama na mtoto mzuri tena mwenye kuijua kazi yake. Lily naye aliamini baada ya kuhangaika sana pale alikuwa amefika mwisho wa reli aliuapia moyo wake atampa mwili wake mwanaume mwingine zaidi ya shuku.

    Siku ile waliimalizia pale mpaka siku ya pili Shuku alimrudisha Lilly nyumbani kwao, walipofika Shuku alifungua gari kwa juu na kutoka nje na kwenda kukaa mbele ya gari ili aagane na mpenzi wake.

    “Kwa hiyo bebi?” Lilly aliuliza.

    “Tutaonana jioni.”

    “Si utanifuata?”

    “Wewe ulitakaje?”

    “Nataka unifuate bebi.”

    “Hakuna tatizo.”

    “Bebi katika maisha yangu sijawahi kuinjoi kama jana.”

    “Huo ni mwanzo tu bebi.”

    “Kwa nini usinioe kabisa.”

    “Ni haraka sana.”

    “Basi bebi utakuwa na mwanamke mwingine zaidi yangu.”

    “Sina mwanamke mwingine bebi bahati hiyo umekuangukia wewe tu.”

    “Mmh! Bebi basi nioe nijue unayosema ni kweli.”

    “Bebi bado hujaniakikishia nipo peke yangu kwa vile nimekukuta na mtu.”

    “Nakuapia yule mshenzi hapa atapaona kama kituo cha polisi na muuza bangi.”

    “Ni mapema sana, bebi si ndiyo tumeanza haraka ya nini?”

    “Bebi nina hamu ya kuolewa na wewe.”

    “Nimekusikia, basi jioni kodi gari uje home.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Si umekubali nitanifuata imekuwaje tena, bebi hunipendi.”

    “Nakupenda mpaka nasikia maumivu.”

    “Sasa kwa nini usinifuate, bebi unajua mtaa huu wanajifanya wanajua sana ukinifuata wataniheshimu.”

    “Mbona mtaa wenyewe haupo kivilee?”

    “Kuna vicheche fulani wana waume zao wenye nazo, hivyo basi huja na vigari vyao kutukonga.”

    “Wanazo kunishinda mimi?”

    “Hawakufikii lakini lazima wajue mimi ni matawi ya juu.”

    “Wana gari kama hili?”

    “Noo, wana Prado za milioni 75.”

    “Basi bebi jioni nitawafunika wote.”

    “Kweli bebi?”

    “Sasa chagua nije na gari la milioni mia moja au mia mbili.”

    “Bebi la mia mbili ili wakome kabisa.”

    “Basi poa, nataka wajue wewe si mtu wa kuchezea pia nataka niivunje nyumba yenu na kujenda bonge la bangaruu simulizi la kitaa.”

    “Bebi nijengee yangu ile nyumba ya familia watanidhurumu.”

    “Basi nitakujengea Masaki unasemaje?”

    “Yaani nitafurahi ile mbaya.”

    “Na gari la milioni mia moja.”

    “Jamani bebi yaani nakuahidi hata yule Mpemba aliyeniahidi kuninunulia Lav4 nampiga chini.”

    “La4 nini bwana zile gari za wanafunzi.”

    “Umeona eeeh!”

    “Basi bebi jiite mwanamke mwenye bahati.”

    “Hata mimi naona, ndiyo maana siku ile nilikupa namba yangu bila kukuhoji kwa vile nilijua nimelamba dume.”

    “Baadaye basi.”

    “Pouwa bebi.”

    Shuku naye alijifanya kauzu japo hakuzoea alidendeka na Lilly mbele za watu. Baada ya kuachiana Lilly alikimbilia kwao akiwa amevimba kichwa na kujiona ana bahati kuliko kiumbe chochote cha kike.

    Shuku alirudi kwenye gari lake na kupiga honi kabla hajaondoka kitu kilichomfanya Lilly ageuke nyuma, alibusu kwa kulipeperusha busu, naye Lilly alilipokea. Kisha aliwasha gari na kuondoka kwa kasi huku akitimua vumbi.

    Shuku alikuwa bado haamini kilichotokea kumpata mtoto mzuri kulala hoteli ya bei mbaya. Moyoni aliomba aikute Vogue lipo nyumbani ili akazidi kumkonga Lilly na kuwatesa wavimba macho wote.

    Alipofika nyumbani alimkuta MJ akitoka kuoga akiwa ameongozana na msichana mwingine mkali.

    “Vipi mzee?” MJ alimuuliza Shuku.

    “Poa tu mkubwa.”

    “Ndo unarudi nini?”

    “Wee acha.”

    “Kwa nini?”

    “Wakubwa unafaidi, mambo niliyokutanana nayo sikuyategemea, bila umatemate huwezi kula raha kama zile.”

    “Vipi mtoto?”

    “Yuko bomba kila idara.”

    “Mbona hukuja naye?”

    “Jioni, nimempitisha kwao abadili nguo, nitamfuata baadaye.”

    “Kwa nini hukumpitisha kwenye maduka ya nguo mkabadili, au mkwanja umekwisha?”

    “Bado upo mwingi tu.”

    “Mlikwenda wapi?”

    “Sijui.. hoteli ya Serena.”

    “Usiniambie!”

    “Wee acha wakubwa wacha mfaidi.”

    “Umelala chumba cha shilingi ngapi?”

    “VIP.”

    “Weweee.”

    “Si umeniambia nitumie niwezavyo.”

    “Mtoto kasemaje?”

    “Mambo niliyomfanyia kachanganyikiwa, mara ooh nioe si mtaki mwanaume mwingine.”

    “Ndoa noma, ukioa dunia itakucheka.”

    “Kwa nini?”

    “Watoto wazuri kama hawa utamuachia nani?”

    “Lakini mimi bado siwazi mwingine zaidi ya Lilly.”

    “Demu wako anaitwa Lilly?”

    “Ndo maana yake.”

    “Basi mzee kazi kwako mi nabadili nguo natoka mara moja kuna mzigo umeingia.”

    “Poa,” Shuku alipotaka kuondoka alikumbuka kitu.

    “MJ nimekumbuka kitu.”

    “Kitu gani?”

    “Vipi Vogue utatumia leo?”

    ”Hapana, nitatumia hummer”

    “Mmh! Hummer na Vogue lipi la bei mbaya?”

    “Chezea Hummer wewe?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Basi mimi nilijua Vogue ndiyo matawi.”

    “Imechelewa kujua.”

    “Basi leo nitamfuata mtoto na Vogue siku nyingine nitafunga kazi kwa hummer.”

    “Wewe tu.”

    Shuku kwa vile alikuwa amechoka baada ya kushindana na kilichowashinda wahenga na wahenguzi kinyama cha hamu kisichoisha hamu, alikwenda kulala na kumuacha MJ akijiandaa kutoka na mtoto mzuri.

    ****

    Majira ya saa kumi na moja jioni Shuku aliamka kitandani na kwenda kuoga tayari kumfuata Lily Temeke. Baada ya kutimba pamba kali, alitoka nje na kwenda kuchukua Vogue kwa ajili ya kwenda kumkonga mpenzi wake na wavimba macho wa mtaa ule.

    Wakati akitoka alikutana na MJ akiingia, ilibidi asubiri kwanza aingie swahibu wake ndipo naye atoke. Baada ya MJ kuingiza gari ndani aliteremka na demu mwingine mkali kuliko aliyelala naye.

    “Vipi mzee hujatoka?” MJ alimuuliza Shuku.

    “Ndo natoka nimelala sana.”

    “Poa utanikuta, huyu ni shemeji yako Angel,” MJ alimtambulisha demu wake.

    “Ooh! Nimefurahi, mambo shemu?” Shuku alimsalimia kwa kumpa mkono.

    “Poa, mbona wageni tunakuja wenyeji mnaondoka?” Angel alionekana mcheshi.

    “Narudi sasa hivi.”

    “Mmh! Sijui kama atanikuta.”

    “Acha hizo, mbona hata nusu saa haichukui nitakuwa nimerudi.”

    “Haya baba umeshinda, niletee zawadi tu.”

    “Umepata, zawadi gani?”

    “Yoyote itakayo ona inalingana na hadhi ya shemeji yako,” Angel alisema huku akijishebedua.

    Shuku aliingia kwenye gari lake na kuondoka kumuwahi Lily ambaye aliamini ana kimuhemuhe cha kumsubiri kwa hamu. Akiwa njiani alijikuta akijiuliza ubadilishaji wa MJ watoto wazuri, alijiuliza watoto wakali kama wale anawatoa wapi. Kilichomshangaza toka afike hakukuwa na msichana aliyejirudia.

    Alijiuliza hizo nguvu ya kugawa dozi kila kukicha anazitoa wapi. Lakini kwake pamoja na kuwaona wanawake wazuri pengine kumzidi hata Lily, lakini kwake Lily penzi lake lilikuwa limefika mwisho kama reli iliyogota Kigoma.

    Alipofika maeneo Temeke Mikoroshini alikutana na lile gari lililotumiwa na mjanja wa Lily. Alishtuka na kutupa macho ndani ya gari labda Lily kaondoka, lakini ndani alikuwepo msela peke yake.

    Alijiuliza imekuwaje huko baada ya msela kurudi peke yake, alipofika alisimamisha gari kwa makeke na kumpigia honi Lily. Alimuona Lily akichungulia na kurudi ndani alishindwa kumuelewa. Alipiga tena honi lakini safari ile hakutoka kabisa.

    Aliamua kutoka nje ili Lily amuone, baada ya kusimama mbele ya gari Lily alitoka mbio na kwenda kijitupa kifuani kwa Shuku na kuanza kulia.

    “Vipi bebi?”



    Aliamua kutoka nje ili Lily amuone, baada ya kusimama mbele ya gari Lily alitoka mbio na kwenda kijitupa kifuani kwa Shuku na kuanza kulia.

    “Vipi bebi?”

    Shuku alimuuliza.

    “Si huyu mshamba kaja hapa namwambia simtaki ananilazimisha na kuanza kunitukana eti mi malaya tena muathirika kwa vile tu nimemkataa.”

    “Basi bebi, ingia kwenye gari nikakuliwaze.”

    Lily aliingia kwenye gari na kutulia huku akiendelea kufuta machozi.

    “Pole sana bebi.”

    “Asante, lakini bebi naomba unihamishe huku.”

    “Kila kitu kitakwenda vizuri usiwe na wasi.”

    Shuku aliondoa gari kwa mbwembwe huku watu wakipiga miruzi. Wakiwa barabara ya Mandela baada ya kutoka vetenari Lily alikuwa kama anazinduka usingizini.

    “Ooh! Bebi yaani yule mpumbavu kasababisha nishindwe kujimwaga mtoto wa kike. Bebi unatisha bonge la gari, umewafunika wote wavimba macho, mbona mwaka huu watakoma.”

    “Huu ni mwanzo kuna gari la milioni mia tano ambalo siwezi kulileta kwenye vumbi.”

    “Bebi si umesema atanijengea Masaki?”

    “Ndiyo maana yake.”

    “Yaani nitafurahi ile mbaya.”

    “Wewe tu.”

    “Mimi si umeona nimempiga chini jamaa kama naua nyani sijamuangalia usoni na mwisho akaanza kashifa zisizo na msingi mpaka watu wakamshangaa.”

    Walipofika Tabata gari lilingia kwenye geti na kujikuta akiingia kwenye Jumba la kifahari. Baada ya kuteremka alimkaribisha ndani ya nyumba.

    “Karibu mpenzi.”

    “Wawoooo bebi unatisha, lazima nijisifu nina bahati kumpata mwanaume anayenipenda tena mwenye uwezo kufuru.”

    “Wewe tu kutulia kula raha.”

    Walipoingia sebuleni walikumkuta MJ amejilaza kwenye sofa akitazama filamu.

    “Ooh! Mkubwa karibu,” MJ alijinyanyua na kukaa kitako.

    “Asante, mpenzi karibu sana hapa ndipo petu. Huyu ni ndugu yangu ambaye tupo hapa pamoja.”

    “Asante kukufahamu,” Lily alisema huku akitabasamu.

    “Mkuu, huyu ndiye mamaa Lily anayenirusha akili kila kukicha.”,

    “Wawoo lazima uchanganyikiwe Lily ana kila sababu ya kukuchanganya umejua kulenga. Karibu sana shemeji yangu wa ukwee.., karibu ujisikie upo home,” MJ alimkaribisha Lily huku alimthaminisha, kweli alikuwa mwanamke mzuri mwenye kila sababu ya kuitwa mrembo lakini kwake alikuwa wa kawaida kutokana na kukutana na watoto wengi wakali kumshinda Lily.

    “Asante shemeji.”

    “Tupo chumbani,” Shuku hakutaka kupoteza muda walielekea chumbani.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Poa mkuu.”

    “Shemu baadaye,” Lily aliaga na yeye.

    “Hakuna tatizo,” MJ alijibu huku akimpiga jicho la wizi.

    Walielekea chumbani huku MJ akiwasindikiza kwa macho na kuzidi kumtathimini Lily kwa nyuma. Aligundua makalio ya Lily hayakuchosha kuyatazama hayakuwa makubwa sana yenye kukinaisha wala madogo yenye kuchusha.

    Aliamini ulimbukeni wa Shuku ndiyo uliomfanya achanganyikiwe. Lakini kwake angegonga na kutimua zake labda siku moja moja kwa vile maumbile mengine kama ya Lily yalikuwa hayachoshi kuyarudia.

    Shuku baada ya kuingia chumbani kwake Lily alikuwa bado haamini.

    “Bebi hii nyumba yako?”

    “Bebi sipendi maswali hayo, mambo yangu unayatakia nini?” Shuku alikuwa mkali kidogo.

    “Samahani bebi kama nimekukosea,” Lily aliomba msamaha.

    “Jana tulilala wapi?”

    “Hotelini.”

    “Kwa nini hukuhoji kama Hoteli nimeinunua.”

    “Basi bebi nisamehe sana.”

    “Siyo nikusamehe, wee kula raha mengine hayakuhusu.”

    “Nimekuelewa bebi wangu.”

    Siku ile walishinda pale jioni walikwenda Maisha club, walirudi saa saba usiku na kulala mpaka siku ya pili. Siku ile Lily alishinda tena huku siku ile Shuku akimpeleka kumnunulia nguo kwa ajili ya kubadili ili jioni wajitupe kiwanja kingine.

    MJ alibidi amwite Swahibu wake na kumueleza:

    “Kaka vipi umeoa kabisa?”

    “Kwani vipi?”

    “Tumekubaliana nini?”

    “Lakini mbona ni jana na leo kesho anarudi kwao.”

    “Shuku, si unajua mi mzee wa kubadilio mademu, demu wako akiona anafikiri atanifikiriaje?”

    “Kweli.”

    “Sikukatazi kula starehe zako, ruksa kuja naye mara moja au mnalala kisha anakwenda kwao, kama unataka kutumia muda mwingi wa kuwa na mpenzi wako nitakupa fedha ya kukaa naye hata mwenzi mzima hoteli yoyote uitakayo lakini hapa tunagonga na kuondoa.”

    “Nimekuelewa mkubwa.”

    “Ila ukitaka gari lolote chukua na chochote fanya la muhimu fuata ninavyotaka ili twende sawa.”

    “Poa hakuna noma jioni atasepa.”

    “Siyo asepe kama bado una ugwadu naye, unaweza kwenda kulala naye hoteli yoyote.”

    “Hakuna tatizo.”

    Jioni ya siku ile baada ya kutoka Billis Shuku na mpenzi wake walikwenda kulala hotelini kitu kilichomfanya Lily ahoji.

    “Vipi bebi leo mbona tumelala huku?”

    “Kwani pabaya.”

    “Siyo pabaya, kwa nini uharibu fedha bila sababu?”

    “Nyumbani mzee wamekuja.”

    “Si ingekuwa vizuri niwatambue wakwe zangu.”

    “Si vizuri kwa mila ya Kiafrika mzazi akutambue bila kutambulishwa kwanza kabla ya kukuona.”

    “Mmh! Sawa, wanaondoka lini?”

    “Nitakujulisha kwa vile tupo pamoja.”

    Shuku alianza kuona kama mambo yake yanaweza kwenda ndivyo sivyo na demu wake kugundua siri ile na kumpiga chini. Lakini ilikuwa tofauti na MJ yeye hakupenda mwanamke mmoja akae pale kwa muda mrefu angeweza kugundua mambo yake mengi ya hatari ambayo hakutaka mtu mwingine ajue zaidi ya Shuku.

    Ilibidi akubaliane na masharti ya rafiki yake ya kumleta mpenzi wake na kuondoka ili kumpa nafasi MJ kuingiza mademu wake kwa kuwabadili atakavyo. Kwa vile Lily alipewa uhuru wa kwenda pale wakati wowote, kila alipojisikia alifika kwa Shuku kukidhi haja zake muda wa mchana kabla ya kutoka usiku kwenda viwanja.

    Akiwa amekaa sebuleni peke yake MJ wakitazama DVD ya filamu, Lily aliingia akiwa katika vazi la utata lililokuwa ‘transpalent’ lilimrusha roho MJ na kumuona Lily kila siku alikuwa mpya kwake.

    Alipofika alikwenda moja kwa moja alipokaa na kumlalia huku akimpiga mabusu mfurulizo.

    “Mmmmmmwa, shemeji langu hilo.”

    “Asante,” busu la Lily lilimsisimua MJ na kujikuta akitamani kitu kwa muda ule, kama Shuku asingekuwa mtu wake wa karibu kwa jinsi Lily alivyokuwa siku ile alikuwa yupo radhi kuvunja benki kwa kiasi chochote ili alionje joto lake. Lakini bahati mbaya kisu kilikuwa kimegusa mfupa hivyo alikubali kula kwa macho hasa akizingatia yule mwanamke alikuwa amemrusha akili swahibu wake Shuku.

    Siku zote MJ hakukubali kuteswa na mwanamke alikuwa yupo radhi kuhonga hata gari ili ampate hasa mademu na wake za marafiki zake. Lakini kwa Shuku aliona pale si sawa hasa baada ya kumkaribisha mwenyewe hakukuwa na haja ya kupimana ubavu na nguvu zake mwenyewe. Alikubali kula kwa macho japo siku ile naye alipagawishwa sana na Lily.

    “Mambo shemu?” Lily alimuuliza akiwa amemshika mabegani huku akimtazama kwa jicho lililohitaji msaada wa mwanaume shababi.

    “Poa tu shemu, karibu,” MJ alijitutumua.

    “Asante,” Lily alijibu akiwa bado amemkalia MJ.

    “Hongera sana umependeza.”

    “Asante, vipi babaa yupo?”

    “Kaingia ndani muda si mrefu amesema anasikia usingizini, kwani hajui kama unakuja?” MJ alimuuliza huku macho yake yakitua katika kifua kilichojaa sawa bin sawia na kuzidisha uzuri wa mrembo aliyekuwa mbele yake.

    “Hajui, nimeamua kumfanyia surprise.”

    “Haya mama kazi ni kwako.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Siyo kwangu kwetu wote, badae,” Lily alisema huku akinyanyuka na kuondoka kuelekea chumbani kwa Shuku akitembelea vidole kwa kuchanganya miguu kwa madaha kuwahi chumbani.

    MJ alijikuta akimtazama Lily kwa nyuma jinsi maumbile ya nyuma yalivyokuwa yakitetemeka kama yanasikia baridi kali la Njombe. Alitikisa kichwa na kusema kwa sauti ya chini:

    “Kweli Shuku anafaidi.”

    Kwa mara ya kwanza alifahamu kilichomdatisha rafiki yake Shuku kwa Lily, mrembo alikuwa na vigezo vyote vya kumchanganya mwanaume. Baada ya kumfikiria sana Lily, aliyahamisha mawazo yake na kutazama kwenye kioo kitazama picha iliyokuwa imefika mbali kutokana na kumtazama sana Lily.

    Baada ya muda alijikuta akiwaza wazo la kijinga kwenda kupiga chabo dirishani kwa Shuku ili aone unyambulikaji wa mwili wa Lily kwenye uwanja mfupi anautendea haki au ndiyo analala kama nyoka mkubwa aliyeshiba baada ya kumeza mbuzi hata kujitikisa hawezi.

    Alitoka hadi nje na kuzunguka nyuma ya nyumba hadi kwenye dirisha na kufanikiwa kuona ndani. Alipofika alikuta ngoma inogile mtoto wa kike akitumia wepesi wa nyonga yake kutawala dimba la kati kitu kilichozidi kuongeza mateso kwa MJ.

    Aligundua uwezo mkubwa wa Lily katika mapenzi tofauti na wanawake wengi. Alijituma muda wote wa mchezo huku akifurahia mchezo kitu kilichomfanya MJ naye nje kwenda na muvu ya goli baada ya Lily kuwatambuka mabeki na kumpiga chenga golikipa na goli kubakia wazi.

    Mzee nzima nje bila kujijua anasugua kichwa ukutani wakati akikwea mnazi makavu bila kupenda wakati huo alikuwa anateremka juu ya mnazi naye taratibu alikaa chini huku akizidi kuusugua uso wake ukutani na kumpa jeraha upande wa kushoto wa uso kwake.

    Baada ya bomba la maji kukata alinyanyuka alikuwa amekaa na kukimbilia ndani ili wasimkute akitoka nje kwani alikuwa kama kaangukia banda la kuku kwa jinsi alivyojichafua na ute wa yai.

    Alikwenda moja kwa moja bafuni kujiswafi alipojimwagia maji alisikia maumivu makali sehemu ya kushoto ya uso, alisogea kwenye kioo na kujitazama na kugundua amechubuka usoni, kama ilivyokuwa kwa Shuku siku alipompiga chabo MJ naye alitabasamu na kumalizia kuoga na kujipaka dawa ya kupuliza kwenye kidonda na kurudi sebuleni.

    Moyoni alijiapiza lazima naye aanguke na Lily hakuwa tayari kuteswa vile wakati aliyeshika mpini. Siku zote aliamini anaye kula vizuri ni mwenye mali na mpambe hula makombo.

    Akiwa katikati ya mawazo juu ya uzuri na uwezo wa shemeji yake katika mapenzi, mara alitoka Lily peke yake na kusogea alipokaa na kumkalia kwenye mapaja.

    “Shemu mi nakimbia,” alimwambia kwa sauti ya kudeka.

    “Haya bibie, mbona peke yako?”

    “Kuna sehemu nakwenda nitarudi kesho hivyo nilikuja kujaza mafuta ili gari lisizimike huko niendako.”

    “Haya mama, kwa hiyo Shuku anafanya nini?”

    “Nimemuacha amelala, nimemchezesha tokomile bila filimbi yupo hoi kalala.”

    “Naona, sasa hebu subiri,” MJ alisema huku akinyanyuka kwenye sofa.

    “Sawa shemu,” Lily alikubali na kusubiri alichoelezwa akimtazama Mj aliyeelekea chumbani kwake.

    MJ alikwenda hadi chumbani kwake na kuchukua mkufu wa bei mbaya na kumletea Lily.

    “Shemu zawadi yako.”

    Lily alifungua na kukutana na mkufu wa bei mbaya ambao aliwahi kuuona kwa shoga yake alionunuliwa na basha wake wa Kiarabu wa milioni mbili na nusu.

    “Wawooo shemu,” alisema huku akimrukia na kumkumbatia kwa furaha.

    “Asante sana shemu, umeniazima au umenipa?”

    “Shemu kipi cha ajabu?”

    “Hapana.. hii zawadi kubwa sana kupewa na shemeji yangu.”

    “Ya kawaida hapo nje umeona magari ya thamani gani?”

    “Kubwa sana, kwani mali hii ya nani maana Shuku nilimuuliza akawa mkali.”

    “La muhimu ni kupokea tu si kujua mali ya nani hii ni mali yetu.”

    “Asante shemu, yaani unaonekana una upendo mkubwa sana kwangu kwa kunipa zawadi kubwa kama hii,” Lily alisema akiwa anautazama mkufu kwa kuuning’iniza.

    “Kwangu hiyo ni ndogo sana, una gari?” MJ alitupa turufu nyingine.

    “Si..si..na ila bebi alisema ataninunulia.”

    “Achana na bebi wako, unazungumza na mimi, una gari?’”

    “Sina shemu.”

    “Unapendelea gari la aina gani?”

    “Lolote la kike.”

    “Basi kesho nitakupigia nikueleze uje wapi ili nawe umiliki gari lako.”

    “Shuku akiniuliza nimjibu nini?”

    “We mkubwa sasa, ukila na kipofu ushimshike mkono.”

    “Nimekuelewa, nije na Shuku?”

    “Hapana shemu njoo peke yako sitaki Shuku ajue ili siku moja umfanyie surprise.”

    “Na hii cheni?”

    “Hata hiyo usimwambie, hebu nisubiri nje nakuja.”

    Lily alitoka nje akiwa hamuelewi shemeji yake, moyoni alijisemea:

    “Kama amezimikia flagi shauri yake, Shuku si mume wangu wa ndoa kama akiingia kichwa kichwa namnyoa bila maji.”

    Alitangulia hadi nje kusubiri alichoambiwa asubiri, baada ya muda MJ alirudi na bahasha la kaki lililokuwa na fedha za kutosha.

    “Kaisabie nyumbani kuna namba yangu ya simu utanipigia kwa wakati wako.”

    “Asante, shemu naomba basi unirudishe nyumbani,” Lily baada ya kuona MJ amechanganyikiwa alideka.

    “Hakuna tatizo, unapendelea gari gani?”

    “Lolote yote mazuri.”

    MJ alichukua Jeep na kumrudisha Lily nyumbani, njiani Lily alizidi kumfanyia visa MJ na kumchanya muda wote koo limcheze kama mtu aliyekuwa na kiu kikali aliyehitaji msaada wa maji.

    Alipomfishisha Lily kabla ya kuteremka alimbusu Mj na kumvutia kwake na kukutanisha midomo na kumpa uhuru wa kubadilishana mate. Walitulia huku MJ akipandwa na mzuka na kuanza kutembeza mikono yake katika mwili wa Lily, lakini Lily alimuwahi na kujitoa na kusema:

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Tosha kwa leo shemu.”

    “Kwa hiyo siku nyingine?”

    “Wewe tu.”

    “Au leo?”

    “Hapana ni haraka sana.”

    “Lily sema unataka kiasi gani ili usiku wa leo niwe na wewe?”

    “Chochote utakacho taka kunipa.”

    “Kwa hiyo jioni ya leo tutakuwa wote?”

    “Mmh! Lakini sio kwenu.”

    “Tunakwenda hotel yoyote unayotaka.”

    “Sawa, na kuhusu Gari?”

    “Tukitoka hotelini tunapitia kwenye show room.”

    “Wawooo, yaani nakuahidi kukupa penzi ambalo hujawahi kupewa, sasa itakuwa kwa Shuku?”

    “Endelea naye penzi, letu litakuwa la siri tukiwa pamoja unakuwa upande wa Shuku, ila tukiwa wawili kama kawaida.”

    “Nimekusoma, kwa hiyo jioni inakuwaje?”

    “Nitakujulisha nitakupitia.”

    “Hakuna tatizo, bai bebiii.”

    “Bai.”

    Lily alifungua mlango wa gari na kutoka nje na kumuwacha MJ akimsindikiza kwa macho. Lily alichepua mwendo kukimbilia ndani akiwa amekumbatia mfuko wa fedha.

    ****

    Lily alipofika ndani aliingia chumbani kwake na kuzimwaga zile fedha kitandani na kuanza kujimwagia mifedha ambayo hakujua hesabu yake. Baada ya kuoga fedha alinyanyuka na kuzikusanya kisha alianza kuzihesabu. Kila alivyohesabu alipofika katikati alisahau alirudia zaidi ya mara tatu na kuamua kuzirudisha kwenye mfuko na kuziweka ndani ya kabati na kujilaza kitandani akiwaza bahati ya mtende iliyomwangukia.

    Akiwa amejilaza alijishika kifuani na kujiuliza kwa sauti kama anazungumza na mtu.

    “Mimi Lilian siamini, yaani kesho na mimi nitatembelea gari langu, mbona wavimba macho wa mtaa watanikoma. Yaani nitakavyompa mapenzi motomoto leo lazima achanganyikiwe mtoto wa kike nitajituma mwanzo mwisho.”

    Alikwenda kwenye kabati na kuchangua nguo ya kuvaa jioni akitoka na MJ mtu aliyempagawisha na mijizawadi ya kumwaga. Moyoni alikuwa na maswali magumu yasiyo na majibu kuhusu kuutoa mwili wake kwa ndugu wa Shuku.

    “Watajijua mwenyewe, kwani yeye hakujua nipo na ndugu yake shauri yao na tamaa zao. Mi nifanye nini, la muhimu hiyo kesho nipate hilo gari,” Lily alizungumza kama anazungumza na mtu kwa sauti ya chini.

    “Shauri yao mwenye kisu kikali ndiye atakaye kula nyama, Shuku kwa uwezo wake alimnyang’anya Tony na sasa MJ akitoa dau kubwa kumshinda ndugu yake naachia ngazi si mume wangu hata kama angekuwa mume wangu mapenzi masilahi...mmh! Lakini Shuku akijua ndugu yake natoka naye sijui itakuwaje..Sasa mimi nifanye nini eti msomaji?”

    Lily alijilaza kusubiri muda ili akutane na MJ na kumpa machejo ya mtu mzima kwenda dukani si mtoto, si unaukumbuka ule usemi mtoto hatumwi dukani.

    ***

    Majira ya saa mbili usiku MJ alisimamisha gari mbele ya nyumba ya kina Lily. Alipiga honi na kumfanya Lily aliyekuwa amejiandaa toka saa kumi na moja na kumsubiri kwa hamu kutoka mbio na kwenda kumkumbatia MJ aliyekuwa nje ya Hummer.

    “Waawoo bebiii.”

    “Waawoo my love.”

    Walikumbatiana kwa mapenzi mazito.

    “Mmh! Umependeza,” MJ alimsifia Lily.

    “Asante, lakini kawaida yangu.”

    “Unaona eeh, halafu mtoto mzuri kama wewe unatembea kwa miguu.”

    “Nitafanyaje bebii?” Lily alisema kwa sauti ya kudeka akiwa amemlalia MJ kifuani na kuchezea ndevu chache chini ya kidevu.

    “Tatizo kuwapenda wachovu.”

    “Jamani bebi Shuku mchovu?”

    “Sijasema hivyo.”

    “Sasa mchovu gani, wa zamani nimeishampiga chini, sasa hivi ananiona muislamu na banda la nguruwe.”

    “Watu sahihi kwa wanawake wazuri ni watu kama sisi.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Si ndiyo maana nipo na Shuku?”

    ”Toka uanze kuwa na Shuku amekupa nini?”

    “Mmh! Kwa kweli vitu vya kawaida tofauti na wewe hatujaanza umeonesha matusi yako. Sijui baada ya mwezi nitakuwa wapi?”

    “Nataka niyabadilishe maisha yako kabisa,” MJ alisema huku akimshika kiunoni na kuingia ndani ya gari baada ya kuwasha gari na kuliondoa alimgeukia Lily baada ya kuulizwa swali ambalo hakupenda kuulizwa na mtu yeyote juu ya mali yake na Shuku.

    “Kwani hii mali ya jumba na magari ya kifahari ni ya nani?”

    “Yetu sote,” alimficha.

    “Sasa mbona wewe si bahiri kama mwenzako?”

    “Ndo maana nilikuambia ulitakiwa kuangukia katika mikono salama kama hii.”

    “Nimekuelewa mpenzi.”

    “Tena ukijituma kama unavyompa penzi Shuku si muda mrefu nitakujengea na jumba la kifahari.”

    “Shuku! Nilimpaje?” Lily alishtuka kusikia vile.

    “Mpaka kupagawa una mpa penzi la kitoto?”

    “Mmh! Nimejua kumbe kila tukiachana anakuja kukueleza, basi shauri yake kauza mpango wa wizi kwa polisi.”

    “Una maana gani?”

    “Si umeelezwa uwezo wangu wa mapenzi, sasa hata akijua atamlaumu nani?”

    “Hawezi kujua, penzi letu lazima liwe la siri wewe endelea na jamaa, nikikuhitaji nitakuwa nakujulisha tunafanya mambo yetu bila jamaa kujua.”

    “MJ yaani niwatumikie wanaume wa nyumba moja kwa nini nisimpige chini Shuku niendelee na wewe?”

    “Hapana, sitaki kugombana na ndugu yangu kwa ajili ya mwanamke.”

    “Kwa hiyo mi nitakuwa chombo cha starehe kwenu?”

    "Siyo chombo cha starehe, wee endelea na mpenzi wako lakini kila nilichokuahidi nitakupatia.”

    “Mmh! Haya.”

    MJ alipunguza mwendo wa gari ili kuingia Sea Cliff hotel, baada ya kulisimamisha gari eneo la maegesho, MJ alimweleza Lily amsubiri.

    “Nisubiri ndani ya gari.”

    “Hakuna tatizo.”

    MJ aliteremka na kwenye gari yake na kuelekea kwenye vyumba kwa ajili ya kwenda kuchukua chumba kwa ajili ya kupumzika na mtoto mzuri, ambaye moto wake ulimshtua baada ya kumuona ajituma kwa Shuku na kutaka kuuota. Baada ya kuchukua chumba alitoka na kufunga gari kisha alitangulia na Lily alimfuata nyuma.

    Walikwenda hadi chumbani, walipofika MJ alimkaribisha kuonesha ni mzoefu wa starehe tofauti na Shuku.

    “Karibu mrembo.”

    “Asante mpenzi.”

    MJ alimbeba juujuu hadi kitandani na kumtupia, baada ya kumtupia kitandani hakumpa nafasi alianza kashikashi za kuutembeza ulimi na mikono ambao uligusa sehemu muhimu na kumchanganya mtoto wa kike na kuona tofauti ya Shuku na MJ ambaye alionekana mtaalamu katika medani ile.

    Baada ya mshuke mshike uliomfanya Lily apasue dafu likiwa juu ya mti bila kudondoka chini. Lily aliomba wakaoge.

    “Mpenzi mwezio tayari, naomba nikaoge kwanza,” Lily alisema kwa sauti ya mafua.

    “Hakuna tatizo.”

    Walikwenda kuoga pamoja huku Lily akitumia muda mwingi kujipanga jinsi ya kukabiliana na MJ kwa moto aliouonesha kabla ya mchezo. Uwezo alioonesha MJ baada ya kumshika kitandani kulimtisha na kujiandaa asiadhirike.

    Kuna jamaa aliishawahi kunieleza kuna timu iligoma kuingia uwanjani baada ya kuwakuta wapinzani wao wametangulia na kuanza kupasha misuli. Kupasha misuri tu wakakausha majani, wapinzani wakajiuliza kupasha wamekausha majani mechi si watachimbua mpaka udongo kwa hiyo wakagoma kucheza.

    Pamoja na hofu ya uwezo wa MJ bado gari aliitaka aliapa kufia kitandani lakini ahakikishe wakiamka asubuhi breki ya kwanza show room kuchagua gari. Aliogopa kulianzishia bafuni kwa kuogopa mshikemshike wa MJ aliamini angeliswa chozi la pili hivyo angepunguzwa uwezo kukabiriana naye.

    Baada ya kufika kitandani walendeleana kupashana joto huku Lily akirudi mchezoni kwa kurudisha mashambulizi na kuweza kusawazisha bao kwa kumliza MJ kilio kisicho na msiba.

    Baada tui kuchemka uliwekwa mchele na shughuli pevu ilianza. Hukuwepo ila shetani wako alikuwepo, mtoto wa kike alijituma muda wote kila mpira alicheza yeye, kutupa kupiga goli kiki kona penalti vyote yeye. MJ hakuwa na kazi kubwa zaidi ya kumalizia mipira yote ya mwisho.

    Mpaka wanapumzika kila mmoja alikuwa hoi huku MJ akiwa ametiwa wazimu na uwezo wa Lily katika medani ya uroda.

    “Wacha jamaa achanganyikiwa mambo unayaweza,” MJ alimwambia Lily.

    “Kwani nduguyo anachanganyikiwa madogo,” Lily alijibu huku akijigeuza na kulalia tumbo na kuiacha nundu iliyonona juu na kumfanya MJ ameze mate ya hamu, lakini hakuwa na uwezo wa kuendelea alikuwa amechemka na kuendelea kula kwa macho, ‘mdomo wataka kula maungo yaona woga.’

    Pamoja na kujituma sana Lily aligundua tofauti ya MJ na Shuku katika medani ya uroda. Shuku alikuwa na nguvu alipomshika mwanamke alimkamua tui mpaka machicha ya nazi yakabakia meupe.

    MJ alikuwa akichemka hata kasi yake ya kupiga kasia ilikuwa ndogo tofauti na Shuku, Lily ilibidi atumie mtindo wa kujihudumia mwenyewe bila hivyo angeumbuka baada ya kumuona MJ rigwaride limemshinda.

    Kwa vile walikuwa wamechoka walijilaza ili kupumzika kabla ya kupata chakula cha usiku.



    Mambo aliyofanyiwa MJ na Lily yalipagawisha na kufikiria mara mbili kumuachia rafiki yake aendelee na yule msichana. Katika kutembea kote na wanawake hakuwahi kukutana na mwanamke anayejua kukitendea haki kitanda kama yule.

    Hata alipochemsha aliendelea kula raha huku akiwa ametulia kwa mtoto kujituma muda wote. Alijua kudeka wakati pipi imo mdomoni utafikiri mtoto wa paka mwenye njaa aliyelilia maziwa.

    Alijifikiria ili kumteka lazima amnunulie gari kali ili hata mwenyewe achanganyikiwe. Siku ya pili MJ na Lily walikwenda mpaka show room kuchagua gari. Baada ya kufika alimweleza Lily:

    “Mtoto mrembo chagua gari utakalo”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nataka hilo,” Lily alichagua BMW X6 ambayo ndiyo ilikuwa bado ipo katika chati. MJ hakumung’unya maneno wala kupepesa macho, aliandika hundi na kumnunulia Lily gari la kuwatesa wanuka vikwapa na wavimba macho.

    Baada ya kumnunulia waliagana na MJ na kuahidiana kuonana baada ya siku mbili.

    “Jamani sweet kwa nini nisiwe na wewe tu kuliko kuendelea na Shuku?” Lily alinogewa na kumsahau Shuku.

    “Hapana, jamaa kawahi sitaki kuvunja penzi lenu hasa ukizingatia sisi ni ndugu.”

    “Basi naomba kila siku tuwe tunakutana basi, jamaa nitakuwa namyeyusha.”

    “Hapana siyo kila siku na siku tukikutana tunachuniana ila ukishindwa unaweza kushangaa tunasitisha zoezi.”

    “Zoezi gani?”

    “Si kila mtu anaanza kivyake.”

    “Nimekuelewa baby, usiniache nakupenda baby.”

    Waliagana kila mmoja alikwenda kwake huku Lily akikanyaga mchuma wake mpya hadi kwao. Alilipaki kwao na kuteremka kila mtu alijua ameazima. Aliingia ndani kwa mbwembwe nakwenda kuutupa ufunguo wa gari kwa dada yake aliyekuwa amejilaza kwenye kochi.

    “Vipi mwenzetu?” dada yake alishtuka.

    “Dada, mwanamke ukijua kutumika utapata kila kitu.”

    “Una maana gani?

    “Dada usiku wa jana ulikuwa wa kukumbukwa.”

    “Usiniambie mdogo wangu!”

    “Twende nje ukaone?”

    Walitoka nje na kukuta gari la kifahari, dada yake aliuliza:

    “La nani?”

    “Langu.”

    “Muongo!”

    “Kweli langu, kazi ya usiku wa leo imezaa gari hili.”

    “Kumbe yule shemu ana umatemate sana?”

    “Siyo yule ni ndugu yake.”

    “Lilian! Mbona sikuelewi aliyekununulia ni yule mpenzi wako mpya au ndugu yake?”

    “Ndugu yake.”

    “Sasa ndugu yake akununulie kwa misingi ipi?”

    “Dada ndiye niliye lala naye usiku wa kuamkia leo.”

    “Kwa hiyo umewachanganya ndugu?”

    “Ndiyo.”

    “Wewee! Mbona unataka kuleta balaa?”

    “Walaa, wao wenyewe, yeye anajua natembea na ndugu yake kaanza kunipa zawadi mara cheni, mara mifedha, si unakumbuka nilikueleza siji kwenye shughuli alitaka niwe naye usiku wa jana. Basi mambo niliyompa Shuku si kamweleza ndungu yake kuwa nina uwezo wa kuupanda mnazi bila kutumia mikono.”

    “Mwari wee temea chini, mhu?” stori zilimpagawisha dada Lily.

    “Basi mwanaume kaingia kichwa kichwa na kuniahidi gari kama nitamfurahisha kama nduguye.”

    “Kama nakuona, mhu mdogo wangu lete utamu,” dada alitia chachandu ya maneno ya mdogo wake.

    “Si ndiyo tukakubaliana tulale pamoja?”

    “Ehe, koleza utamu.”

    “Mtoto wa kike niliapa kufia kitandani ilimradi nilipate hiyo gari. Wasiwasi wangu nilijua patachimbika bila jumbe kumbe...”

    “Eeh!”

    “Aah! Wapi,kumbe mwepesiii, hata kiganjani hajai, mbona gari nimelipata buuuure.”

    “Kivipi mdogo wangu?”

    “Yaani nilivyojiandaa kumbe si lolote si chochote, nilikuwa sawa na kuburuza maiti ndani ya maji.”

    “Wewee!”

    “Dada alivyoonza nikaogopa nikajua mtoto wa kike naweza kukimbia na kufuri mkononi. Kila dakika zilivyokuwa zikizidi kukatika ndivyo alivyokuwa akipoteza uwezo wake. Yaani hatua za mwisho ilibidi niwe mpiga debe, konda na dereva mwenyewe.”

    “Mmh! Sasa kipi kilichomfanya akununulie gari?”

    “Dada wakati ana nguvu nilichokifanya hawezi kusahau hata alipochoka kama dume la bata niliendelea kumpa machejo ya kinyozi wa kipara.”

    “Mdogo wangu kwa maneno, kinyozi wa kipara ndiyo machejo gani tena?”

    “Dada si unajua mtu anayenyolewa kipara hatakiwi kijitikisa, akijitikisa amekatwa?”

    “Ndiyo, ehe?”

    “Basi, baada ya kuchoka nilimuweka mkao wa mtu anayenyolewa kipara, mtoto wa kike nikageuka kinyozi kwa kukwangua kila kilichopo kichwani na kuwa mwepesiiii.”

    “Hongera mdogo wangu, sasa itakuwaje? Mmoja unampiga chini?”

    “Mmh! Jamaa amekataa nisiachane na ndugu yake, eti niendelee naye penzi letu liwe la siri.”

    “Mmh! Haya, kwa hiyo kadi ya gari amekupa?”

    “Kila kitu dada, gari mali yangu.”

    ****

    Kama kawaida Shuku jioni alimfuata mpenzi wake na Jeep, alipofika aliisimamisha sehemu yao ya kawaida na kupiga honi. Lily aliyekuwa amejilaza chumbani alinyanyuka na kuchukulia nje.

    Alipoliona Jeep alifurahi na kujua MJ amekuja, kutokana na tamaa alijikuta mapenzi yote kayaamishia kwa MJ.

    “Dada jamaa amekuja.”

    “Nani?

    “MJ.”

    “Mbona hajakujulisha?”

    “Labda kanifanyia surprise, machejo ya yana lazima angenitafuta.”

    “Naona ukimpa mara tatu atakununulia ndege.”

    “Wacha nimuwahi baba asije kasirika.”

    Lily alisema huku akitoka nje na kwenda mbio kumlaki mpenzi wake. Alipokaribia Shuku alitoka kwenye gari na kumfanya Lily ashtuke.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ha! Ni wewe?”

    “Ndiyo mpenzi nimeamua kubadili gani?”

    “Mmh! Karibu.”

    “Asante, vipi mbona kama hujajiandaa.”

    “Naumwa.”

    “Nini tena mpenzi ingia kwenye gari twende hospitali.”

    “Nimeisha kwenda.”

    “Pole sana mpenzi,” Shuku alisema huku akivuta pochi na kuhesabu wekundu ishirini na kumpa.

    “Zitakusaidia kununua matunda.”

    “Asante.”

    Lily aliona kama Shuku anacheza lakini alizipokea na kuagana naye. Alirudi ndani ya Shuku alirudi zake nyumbani na hamu zake. Lily alipofika ndani dada yake alimuuliza.

    “Vipi mbona shemu kaondoka leo hamtoki?”

    “Si kaja yule mchovu nikamdanganya naumwa si kajiiiikakamuuua na kutoa vilaki viwili eti ninunue matunda.”

    “Mmh! Mbona makubwa laki mbili tu ununue matunda?”

    “Umeona nyingi?”

    “Tena sana, kwa hiyo umeanza kumchoka?”

    “Dada siwezi kutumikia mabwana wawili tena wa nyumba moja, lazima niachane na Shuku.”

    “Lily..Lily mdogo wangu usiache mbachao kwa msala upitao. Kwanza hiyo mali ya nani?”

    “Sijajua kila mtu ukimuuliza anasema ya wote.”

    “Sasa nataka kukuambia huenda mali ni ya Shuku, siku zote mwenye fedha huwa mgumu kuliko mtumiaje asiyejua uchungu wa fedha. Kuwa makini unaweza kumuacha Shuku kumbe ndiye tajiri na huyo MJ mpambe mshika pembe tu.”

    “Mmh! Kweli eeh!”

    “Tumia akili, heri uende nao wote kwa siri ili Shuku asijue, hujiulizi kwa nini MJ amesema usipokwenda anavyotaka atakupiga chini unafikiri ni kwa nini?”

    “Hata sijui.”

    “Basi anaongopa kuharibu kwa ndugu yake ambaye ndiye mwenye mali.”

    “Mmh! Dada sasa nimepata picha mali ni za Shuku.”

    Lily alikubali kuendeleza penzi la siri huku akiendelea na Shuku kama kawaida.

    ****

    Penzi la siri la MJ na Lily liliendelea bila Shuku kugundua kilichokuwa kikiendelea huku Lily akizidi kuchanganyikiwa na ofa za MJ zilikuwa tofauti na Shuku ambaye kila siku alitoa ahadi zisizo timia.

    Mabadiliko ya Lily alimshtua Shuku kutokana na kuwa na dharula kila wakati tofauti na siku za nyuma kitu kilichompa wasiwasi. Aliamini aliyemnunulia lile gari ndiye aliyekuwa akimchanganya na kumfanya amuone si lolote si chochote.

    Alitamani naye kuonesha makeke yake lakini alikwama kutokana na MJ kumueleza matumizi makubwa kwake yasizidi milioni mbili.

    Hali ili ilimnyima uhuru na kujiona kama anacheza makida kwenye penzi lake na msichana mrembo kama Lily. Aliamua kwenda naye hivyohivyo lakini akiamini penzi lao lilikuwa limekalia kuti kavu kudondoka asingeshangaa.

    Alipanga kumpiga chini baada ya kumpa penzi zito ili popote atakapokwenda ajue jamaa hana fedha lakini mapenzi anayajua. Siku aliyompigia simu Lily wakutane ndiyo ilikuwa siku ya kuonana na MJ. Aliendelea na danadana zake.

    “Haloo bebi vipi leo?”

    “Mmh! Leo mama kaja.”

    “Sasa akija tatizo nini?”

    “Sasa nitaondoka vipi na mama kaja jioni hii.”

    “Bebi mbona sikuelewi.”

    “Unielewi kivipi?”

    “Yaani si Lily niliyemzoea, najua siku hizi unipendi.”

    “Nakupenda sana wasiwasi wako tu.”

    “Hapana Lily hunipendi mapenzi yetu yamekuwa kama umeme wa mgao kama hunipendi si uniambie nijue moja,” Shuku alilalamika.

    “Nakupenda Shuku.”

    “Si kweli najua sasa hivi una mwanaume mwingine.”

    “Shuku unalalamika sana au ndo unataka kuniacha kwa kusingizia nina mwanaume mwingine?” Lily alilia wivu wa uongo.

    “Si kukuacha bali sasa hivi penzi limekuwa shubiri.”

    “Niamini mpenzi wangu nakupenda sana, Shuku si muda mrefu nitarudi katika hali yangu ya kawaida. Naomba univumilie mpenzi wangu.”

    “Yaani hali hii ikizidi nitashindwa mimi.”

    “Basi kesho nitakuja ili kukufuta machozi, hakuna mwanaume chini ya jua ninaye mpenda kama wewe hujui tu,” Lily alimpaka Shuku mafuta kwa mgongo wa chupa.

    “Mmh! Sawa nimekuelewa mpenzi wangu punguza kunitesa.”

    “Nikuahidi sitakuumiza tena nakupenda Shuku wangu kesho nitakuja kweli.”

    Shuku aliamini kabisa Lily hakuwa na mapenzi na yeye bali alijali kitu na baada ya kununuliwa gari la kifahari mapenzi yote aliyahamishia kwa mtu aliyemnunulia gari. Moyoni bado alijiapia kufanya mapenzi ya mwisho na kumpiga chini na yeye kuishi maisha ya rafiki yake MJ ya kubadili wanawake kwa vile hakuna wa kumuumiza zaidi heat and run.

    ***

    Usiku wa siku ile Lily alikutana na mpenzi wake MJ Sea Cliff hotel. Walichukua chumba kama ilivyo kawaida na kusaluana nguo huku Lily akipanga kujituma zaidi baada ya kupewa ahadi ya nyumba moyoni aliapa siku ile ndiyo siku ya kununuliwa nyumba.

    Wakati tui linakaribia kukolea nazi na Lily kulegea kama ute wa yai kusubiri hukumu kutoka kwa Mj, simu ya MJ iliita alipoangalia ilikuwa ya demu wake mtoto wa waziri aliyekuwa nje ya nchi. Alinyanyuka na kwenda kuongelea pembeni kwa sauti ya chini:

    “Bebii.”

    “Bebii upo wapi?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Nimetoka kidogo, vipi upo wapi?”

    “Ndo nakaribia kwako.”

    “Umekuja lini?”

    “Ndo nimetua na ndege na breki ya kwanza kwako, kesho ndo natinga home. Nimewadanganya nitatua kesho kutwa nitakaa kwako siku mbili, nina hamu ile mbaya mpenzi wangu.”

    “Mmh!” MJ aliguna na kujiuliza lazima aonane na yule binti ambaye alidanganya familia yake kwa ajili yake alijua akimkimbia ataharibu kila kitu.

    “Bebii mbona unaguna au hutaki nije kwako, basi nalala hotel kwa siku bili kesho ndo nakwenda home ila ilewa nisipokuona leo nitaumia vibaya. Si unajua nilitaka nikufanyie surprise.”

    “Hapana bebi lazima tutaonana japo nipo mbali kidogo.”

    “Basi utanikuta kwako.”

    “Hakuna tatizo bebi wangu ngoja nimpigie mtu akufungulie nyumba.”

    “Hakuna tatizo ndo maana nakupenda MJ wa ukwe..ehe.”

    “Umeona eeeh, poa nakuja,” MJ alikata simu na kurudi kitandani Lily alipokuwa akimsubiri ili apate nyumba usiku ule kama alivyopata gari. Japo alikuwa ameahidiwa nyumba aliamini kupitia utamu wa nyonga yake mpaka kunakucha wangetoka na kwenda moja kwa moja kwenye nyumba.

    Akiwa anajiandaa kumpokea MJ kwa mahaba motomoto alishangaa mwenzake kukaa kitako na kuinama mikono kichwani.

    “Bebii vipi, kuna nini?”

    “Kuna tatizo lazima niondoke.”

    “Tatizo gani tena bebeiii?”

    “Nitakueleza kesho lakini lazima niondoke.”

    “Utarudi?”

    “Sina uhakika sana.”

    “Basi nipe kidogo mpenzi nipo kwenye hali mbaya,” Lily alilalamika kwani alikuwa amejiandaa vilivyo.

    “Hapana bebii lazima niondoke.”

    “Sawa nimekubali uondoke, lakini si unajua ushazipandisha nani wa kuzishusha mpenzi, nipo katika hali mbaya basi nipe hata moja la mguu wa jini.”

    “Sorry mpenzi, unavyonichelewesha ndivyo unavyozidi kunifanya nisirudi kabisa.”

    “Kwani unakwenda wapi?”

    “Bebii si lazima kila kitu changu ukijue,” MJ alisema huku akichukua nguo zake na kuvaa. Baada ya kuvaa alimfuata Lily na kumbusu.

    “Mmmwa bebi baadaye.”

    MJ baada ya kumbusu alichomoa nyekundu kumi na tano na kumtupia.

    “Bebi kama nisiporudi utaweka mafuta kwenye gari lako, baii.”

    Lily alishindwa kumuaga kwani moyo ulikufa ganzi baada kushindwa kutimiza malengo yake. MJ hakugeuka nyuma alitoka kumuwahi demu wake mtoto wa waziri. Alimpigia simu Shuku ampokee.

    ****

    Muda ulizidi kukatika bila MJ kutokea saa ya ukutani ilimuonesha Lily ni saa tisa za usiku akiwa macho kumsubiri. Wazo la kwenda kwa Shuku alikuwa nalo lakini alikuwa na wasiwasi wa MJ kurudi na kumkosa.

    Aliamua kukomaa mpaka asubuhi huku sumu ya mahanjamu ikiwa juu bila mshushaji kutokea. Kwa tamaa ya nyumba alijikuta akisubiri mpaka saa mbili asubuhi ndipo alipoamini MJ harudi hata simu yake haikuwa hewani.

    Kwa hasira aliamua kwenda kwa Shuku ili kumkata kiu hasa alivyoufahamu uwezo wa Shuku wanapopotezana muda mrefu siku wakikutana huchimbika bila jembe. Aliwasha gari lake mpaka nyumbani kwa Shuku.

    Muda alipofika alikuta bado amelala baada ya kumpigia simu alimfungulia na kuingia ndani. Alipofika alijifanya amemmisi sana Shuku na kumpiga mabusu mfurulizo.

    “Vipi mbona asubuhi?”

    “Kwani kuna ubaya mtu kuja asubuhi kwa mpenzi wake?”

    “Hiyo iliishapita.”

    “Kivipi tena bebii?”

    “Ndio maana nakushangaa toka upate gari umekuwa matawi ya juu.”

    Kauli ile ilimtisha sana Lily na kuona kama dhamira yake haiwezi kutimia na kuondoka na hamu zake.

    “Mpenzi si nilikueleza nina matatizo jamani.”

    “Matatizo kwa vile umenunuliwa gari unasahau nina uwezo wa kununua magari kama hayo kama elfu moja kwa siku moja,” Shuku alijitapa.

    “Si ungeninunulia mpenzi?”

    “Kwa hiyo kazi yako kuhongwa siyo?”

    “Basi mpenzi, lakini nilikueleza gari hili nililikataa, lakini aliyeniletea alisema nichukue. Lakini anajua kabisa nipo na wewe na sipo tayari kurudiana naye nakupenda sana Shuku,” Lily alisema huku akimchezea chuchu na kumfanya Shuku askari ashtuke kambini na kusimama imara kutoa kipigo kitakatifu kwa adui. Lily alimvutia ndani na kumtupa kitandani na kusaula nguo chache za Shuku na yeye kuzitupa za kwake pembeni. Kutokana na kushika alikuwa kama mbwa kwa chatu.

    Shuku moyoni alijiapia atakachokifanya lazima Lily amkumbuke miaka mia moja itakayo kuja kwa kuamini amezidiwa uwezo hivyo alitakiwa kutumia nguvu alizipewa na Mungu ili kumfanya Lily akitoka pale awe amechanganyikiwa. Alimuweka mkao wa kuku kwa mchinjaji na kujiandaa kupitisha kisu huku Lily akimpigia kelele baada ya kuona anachelewa.

    “Shuku jamani shingo umeiona mbona unachelewesha kukipitisha kisu, Shuku nichinje...nichinje Shuku mpenzi wangu shingo yangu ni halali yako. Mpenzi ukichelewa naweza kufa...chinja...chinja shuku.” Lily alilalama baada ya kuona Shuku akileta mbwembwe.

    Shuku akiwa na usongo siku ile alimuona Lily kama mpya baada ya danadana ya muda mrefu, alijiapiza kumpa penzi la mwisho kisha anampiga chini kwa kujua hakuwa na uwezo wa kumnunulia gari wala nyumba aliyomuahidi.

    Lily akiwa amepagawa baada sumu ya mahanjamu kumpanda kama nyoka mwenye hasira alitamani bakora tu kwa muda ule.

    “Jamani Shukuu mbona unanitesa kosa langu nini mpenzi wangu?” Alilalama huku akimtazama Shuku kwa jicho la ‘nihukumu mpenzi.’

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Shuku hakujibu kitu alimweka mkao wa samaki feri na mpaaji na kuanza kumpaa kwa kucha kitu kilichozidi kumuweka Lily kwenye wakati mgumu ilikuwa kama mwenye kidonda kuweka chumvi, aliweweseka kama mtu anayetaka kupandisha shetani.

    “Shu..Shu..uu..Jamani kucha hazipai samaki tumia kisu unanitesa mwezio.”

    Shuku baada ya kuona magamba ya samaki yamelainika na maji ndipo alipoaanza kumpaa kwa kisu taratibu na kuzidi kumchanganya Lily aliyetoka na hamu zake hotelini alipoachwa na MJ baada ya kupakwa upupu na kufungwa kamba mikono ili asijikune.

    Kutokana na kuujua uwezo wa Shuku aliamini muwasho wote utaisha. Shuku alifanya penzi la kisasi kwa kutumia kikosi cha kwanza kuhakikisha anapata ushindi wa kishindo. Kutokana na koo la Lily kukauka sana matone manne ya maji yalimtosha kulegeza koo na kwenda marikiti.

    “Shukuuuuuu,” Lily alipiga ukelele mmoja na kumkumbatia Shuku kwa nguvu kama nyani aliyeukumbatia mnazi baada ya kuteleza kwenye kuti la mnazi. Alitulia kwa muda kisha kuliacha yai lipasuke kwa nafasi. Baada ya kutulia kidogo sumu ikapanda tena na kutaka itolewe.

    Kwa vile Shuku alikuwa na lake moyoni baada ya Lily kurudi uwanjani aliendeleza mateso bila chuki kwa kushambulia mfululizo bila kumpa nafasi na kumfanya Lily amalize maneno yote mdomoni.

    “Shuku nakupenda.”

    “Muongo.”

    “Kweli nakupenda Shuku wangu.”

    “Siamini.”

    “Kweli Shuku, mbona leo tufauti na siku nyingine, umetia nini mpenzi.”

    “Kawaida tu.”

    “Muongo, kuna mtu ulikuwa ukimpa raha hizi.”

    “Hakuna wewe tu.”

    “Shuku nakupenda, lakini mpenzi umezidi ubahili ninunulia gari ili nirudishe hili.”

    “Nitakununulia.”

    “Lini mpenzi?”

    “Nitakwambia.”

    “Ja..ja..jamani Shuu..Shuu..Shuu...te..te..tee..ee na..naaa.”

    Lily alitulia na kushusha pumzi ndefu, alifumbua macho kwa shida kutaka kumuona vizuri Shuku aliyekuwa amejilaza pembeni chuma kikiwa kikoli moto.

    “Shuku,” alimwita kwa sauti ya kilevi huku macho yakiwa kama mtu mwenye usingizi mzito.

    “Bebi naomba basi uninunulie gari nitulie na wewe.”

    “Lily ni wazi penzi lako la fedha si mapenzi ya dhati.”

    “Hapana bebi unafikiri nianze kutumia gari kisha leo tena kutembea kwa miguu nitauweka wapi uso wangu kwa wavimba macho wa mtaani?”

    “Kwa hiyo nisivyo kununulia huwezi kuwa na mimi?”

    “Nitakuwa na wewe lakini itakuwa ngumu kuwa nawe muda wote.”

    “Sikiliza Lily kuna kitu nataka kukueleza ili usisumbuke.”

    “Kitu gani dia?”

    “Mi naona penzi letu limepoteza mwelekeo unaonaje penzi la leo ndilo liwe la mwisho?”

    “Sijakuelewa unasemaa?”

    “Nasema hivi kwa vile penzi lako la maslahi zaidi, mimi na wewe naona inatosha.”

    “Kwa nini bebi?”

    “Siwezi kuwa na mpenzi anayefanya biashara ya mwili, kama nataka dada poa wapo tena kwa bei rahisi.”

    “Shukuu umefika huko?” Lily alishtushwa na kauli ya Shuku.

    “Sijafika huko bali ukweli ni huo.”

    “Shuku nakuahidi basi kukusikiliza kwa chochote nakupenda sana mpenzi wangu. Naomba uniache nakupenda kama nimekukosea naomba unisamehe.”

    “Utanipendaje wakati sijakukununulia nyumba wala gari?”

    “Shuku nakuahidi kukupenda ulivyo.”

    “Lily unayoyasema ukienda kinyume wala usisumbuke kunitafuta kila mtu ashike hamsini zake.”

    “Shuku mbona hivyo au umempata mpenzi mwingine?”

    “Sina shida ya mwanamke mwingine, nikishikika nakwenda kwa dada poa nakata hamu zangu narudi kulala.”

    “Basi mpenzi nitakufurahisha.”

    “Wewe tu.”

    “Basi mpenzi nipe raha zangu yaani leo uniishi hamu kila nikitulia mashetani yanapanda tena.”

    Shuku kama kawaida aliendeleza makamuzi yaliyomtia wazimu Lily na kumwacha njia panda afuate kipi gari na fedha za MJ au penzi tamu la Shuku. Katika maisha yake yote toka avunje ungo hakuwa kukutana na mpaa samaki kama Shuku anayejua kumpaa na kumfanya samaki afurahie kuondolewa magamba.

    Shuku aliamua kumtesa Lily kiungo cha kati alikikamata yeye na kumfanya Lily muda wote autafute mpira. Shuku hakutaka kumfunga kila alipobaki na kipa alirudisha mpira nyuma na kumfanya Lily alalamike.

    “Shuku mpenzi nifunge jamani mateso gani haya yenye raha, nifunge npenzi nipumzike hapa nilipo nipo hoi. Shuku aliamua kufunga bao la Shuti la mbali lililomfanya Lily kujipita kama mkizi bila mafanikio. Bila Shuku kumdaka angeanguka vibaya.

    Baada ya kuvunja yai la nne kwa moja la Shuku Lily alikuwa hajitambui kwa kuangusha usingizi mzito. Shuku Naye alijilaza pembeni yake kwani naye kutaka sifa kulimfanya achoke haraka aliopojilaza usingizi ulimchukua.

    ***

    Walishtuka wote jioni wakiwa wamechoka na njaa kali.

    “Mpenzi nasikia njaa.”

    “Twende tukaoge kisha tukapate chakula.”

    Walikwenda kuoga walipomaliza kuoga na kubadili nguo, Lily alitangulia kutoka na kumuacha Shuku akichukua fedha. Alitoka akiwa hana hili wala lile mbele ya macho yake alishtuka kumuona MJ akiwa amekumbatiana na msichana wakilishana denda.

    Alishindwa kwenda mbele na kurudi nyuma, wakati huo Shuku alikuwa akitoka.

    “Vipi hujafika mbali, nilijua umeishafika nje?”

    “Mm..eeh..aah,” Lily alipata kigagaziko.

    “Nini mpenzi?”

    “Aah..basi.”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Shuku alipotazama mbele alimuona MJ aliwa na mpenzi wake katika penzi zito.

    “Sasa dia kipi cha ajabu umekiona? Hebu twende.”

    Walitoka wameshikana mikono na kuwapita huku Lily akitazama pembeni moyoni akiwa na bonge la wivu. Walipotoka nje kabla hawajaingia kwenye gari Lily alimuuliza Shuku swali la kizushi.

    “Yule ndiye mke wa MJ?”

    “Mke! Malaya tu.”

    “Ina maana si mpenzi wake wa siku zote?”

    “MJ ana mpenzi mmoja? Kila kukicha anabadili wanawake kama nguo. Huyu sijui mtoto wa kigogo alikuwa nje ya nchi nasikia kaidanganya familia yake anakuja kesho ili ale raha na MJ jana na leo kisha kesho anakwenda kwao.”

    “Amefika lini?”

    “Jana usiku.”

    “Saa ngapi?”



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog