Search This Blog

Monday, October 24, 2022

PENZI LA MKE WA BABA - 5

 





    Chombezo : Penzi La Mke Wa Baba

    Sehemu Ya Tano (5)



    Siku moja nipo (bar) nakunywa, pombe zikanikolea sana, kwa bahati mbaya

    nikamshika mke wa mtu makalio yake bila kujielewa maana mimi nilihisi huenda ni

    dada tu anaejiuza kutokana na mavazi yake aliyo kuwa amevaa. Mume wake alichukia

    kile kitendo cha kushika makalio ya mke wake. Ndipo akaongea na vijana wake

    wanikate mkono wangu kisha wampelekee. Mimi sikujua na wala sikuwa na taarifa

    yoyote kuwa kunamtu anahitaji mkono wangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku moja usiku nikiwa nimetoka kupeleka gari la bosi wangu kwake, nilishangaa

    kukutana na vijana wawili barabarani huku wakiwa wameshika panga, “tunataka

    mkono wako wa kushoto, tumetumwa na bosi, hatuna shida ya kukuua", walisema

    hivyo, “ndugu zangu mkono wangu wa nini tena naombeni mnisamehe bwana,

    chukueni hela hii hapa misinikate mkono" wakachukuwa hela kisha wakasema,

    “tusipo peleka mkono wako tutakatwa sisi, turuhusu tu tukate mkono wako" niliinama

    chini kisha nikawakwepa na kukimbia, nilipo fika mbele kidogo nikakuta ukuta hivyo

    nisinge weza kukimbia tena,jamaa mmoja alinyanyua panga kisha akawa kama

    anataka kukata shingo langu ndipo nikakinga mkono wangu wa kushoto kweli

    ukakatwa na kisha wakauchukuwa ule mkono mpaka wa bosi wao.



    Niliangaika sana kuuguza kile kidonda, na nilijua tu kuwa haya matatizo yote ninayo

    yapata ni sababu ya laana ya baba yangu mzazi. Bosi wangu aliamua kuniachisha kazi

    maana hakutaka tena niwaendeshe watoto wake kwa kutumia mkono mmoja.



    Siku moja nikiwa ndani nalia tu, huku nina mawazo chungu nzima, nikaanza

    kukumbukajinsi baba alivyo kuwa ananipenda leo hii nateseka na dunia peke yangu

    yaani mda mwingine nakosa hata elfu moja mfukoni, wakati najifuta machozi nikasikia

    simu yangu inaita nilipo itazama kumbe baba yangu ndiyo alikuwa na shida ya

    kuongea na mimi.







    Nilipokea simu ya baba kwa furaha nikihisi huenda ana lengo la kunisamee, “hallo

    habari Juma, vipi pesa yangu unanipa lini" alisema baba, “hapana baba mimi sio

    Juma, ni mwanao Meshack", alinisonya kwanza, “hivi kumbe nimekupigia wewe

    mpuuzi, na sitaki kusikia unasema wewe ni mwanangu, nilisha hesabu tangu zamani

    kuwa sijawai kuwa na mtoto, na ninaomba kama nikijisahau nikakupigia wewe tena

    usipokee simu yangu, tafadhali sana" alisema baba kisha akakata simu, nilichoka

    nikajua moja kwa moja kuwa sina msaada tena wa maisha, ndipo nikaamua kutoa

    (line) ya simu kisha nikaitupa ili nisipatikane tena kwenye simu baada ya hapo

    nikanunua line mpya hivyo mimi na baba tukapoteza mawasiliano ya kwenye simu

    tangu siku hiyo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sehemu nilipo kuwa nimepanga, kodi ilikuwa imekaribia kuisha na kibaya zaidi sikuwa

    na pesa kabisa, ndipo nikaanza kutafuta kazi kila nyumba, niliangaika sana maana

    kila mtu alikuwa ananiambia kuwa, “wewe huna mkono mmoja, utafanyaje kazi?" mda

    wote nilikuwa nalia mpaka napiga magoti chini kusudi nipate angalau kazi yoyote

    niweze kutunza pesa kwa hajiri ya kulipa kodi, nilizunguka sana lakini sikufanikiwa

    ndipo nikaamua kurudi nyumbani, kipindi nafika mlangoni kwangu nikakuta mlango

    wangu umebomolewa, nilipo ingia ndani sikukuta begi langu la nguo, kumbe wezi

    walikuwa wameniibia, kibaya zaidi vyeti vyangu vyote vya shule na kuzaliwa vilikuwa

    kwenye ilo begi, hivyo nisingeweza kuomba kazi bila vyeti tena kupitia helimu yangu,

    na kila nilipo pata wazo la kuvifatilia, gharama zake zilikuwajuu ya uwezo wangu,

    ndipo nikakata tamaa kabisa na maisha, lakini nilikuwa najua haya yote yanayo

    nitokea ni laana ya baba yangu mzazi.







    Hali iliendelea kuwa ngumu mpaka kula kwangu kukawa kwa tabu sana, kilicho kuwa

    kina niumiza sana ni pale kazi zilizo kuwa zinapatikana zili-kuwa za kulima kwenye

    mashamba lakini mimi nilikuwa siwezi kulima kutokana ule mkono mmoja kukatwa.

    Siku moja nilizidiwa sana maana nilihisi njaa mpaka nikaanza kuhisi mwili unaishiwa

    nguvu kabisa, ndipo nikamsimamisha dada mmoja hivi barabarani Mungu saidia

    alisimama, “habari dada, ndugu yangu naomba msaada wako, leo siku ya nne

    sijaweka chochote tumboni, naomba hela nikale dada", “ehh kaka siku nne hujala,

    unaishi vipi sasa?" alijibu hivyo, “nishida tu za dunia dada yangu", “sasa cha kufanya

    ni kitu kimoja kaka yangu, twende kwetu nikapike chakula ule maana hapa sijabaki na

    hela yoyote kabisa" niliongozana naye mpaka kwao, alipika chakula tukala pamoja na

    wazazi wake, familia yao ilikuwa imeshika dini sana, hivyo nikalialia sana shida zangu

    mpaka baba wa Vule binti Nancy, akanionea huruma, hata mama Nancy akasema,

    “wewe kijana usijali kabisa, utakaa hapa utaishi tu vizuri maana sio vizuri sisi

    kubakiza chakula kisha tunatupa wakati wewe unasema unakaa siku nne hujala

    chochote".

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilianza kuishi kwenye ile nyumba, ila nilijitahidi sana kufanya kazi nilizo ziweza,

    mpaka wazazi wa nancy na Nancy wote wakafarijika mimi kuendelea kukaa kwao.

    Niliishi kwa mda sana kwenye nyumba yao, baada ya miaka saba, baba yake Nancy

    alifariki dunia hivyo nyumba nzima tukabaki mimi, mama Nancy pamoja na Nancy.

    Tuliishi vizuri sana pale nyumbani na walikuwa wananiheshimu sana maana ndiyo

    nilikuwa mwanaume nilie kuwa nimebaki kwenye ile nyumba. Siku moja tumekaa

    sebreni mama Nancy akaanza kututania kwamba, “hivi nyie wanangu si muoane tu

    mniletee wajukuu maana mnapendana sana, mda wote mnafurahi tu, nyie hamjui tu

    yaani mnapendeza sana kuwa mke na mume, na mimi natamani sana kuona wajukuu

    zangu kabla sijafa".



    Kwa mara ya kwanza nilihisi huenda mama anatania, hivyo basi nikaamua kumuita

    Nancy pembeni kusudi tuweze kuongea kuhusu ilo swala, sikuwamini nancy alivyo

    sema kwamba yupo tayari kuwa mke wangu, “Nancy asante sana kwa kunipenda na

    kunikubalia kutoka moyoni mimi kuwa mume wako, nashindwa kuwamini yaani na huu

    ulemavu wangu umekubali kuwa mke wangu wa maisha", “mapenzi huwa yanatoka

    moyoni Meshack, napenda sana tabia zako tangu nikufahamu, maana kipindi chote

    upo hapa sijawai kukuona na tabia mbaya za kubadilisha wanawake".







    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama Nancy alitukubalia hivyo nikaanza kulala chumba kimoja na nancy, nilifurahi

    sana maana alikuwa ananifariji sana, mda mwingine nikajisahau kabisa kama kuna

    kosa nililitenda kwa baba yangu. Baada ya miezi miwili Nancy alipata ujauzito, Mungu

    alisaidia mpaka akajifungua, lakini tulishangaa sana maana mtoto alitoka akiwa

    kilema yaani mguu mmoja mfupii mwingine mrefu, Nancy aliumia sana kupata mtoto

    wa namna ile ila nilimpa moyo kuwa yote ni mipango ya Mungu, baada miaka miwili

    mke wangu alipata ujauzito, nilikwazika sana maana mtoto alie toka tena alikuwa

    kilema kama wa kwanza, yaani mguu mmoja mrefu na mwingine mfupi, mke wangu

    akauliza, “Meshack mume wangu, hivi kwenye ukoo wenu kuna ndugu wa namna hii,

    mbona watoto wetu wote wanatoka vilema" nilimjibu kuwa, “mke wangu kwa upande

    wetu sijawai kuona kabisa ndugu zetu wapo hivi labda nikuulize kwenye ukoo wenu

    kama wapo wa hivi, maana watoto wetu wote wanatoka vilema tu"tulikosajibu kabisa,

    ndipo tukapanga kuwa tutafute mtoto wa tatu kama na yeye atakuwa kilema basi

    tuache kuzaa tu, ili tuwalee watoto watatu tu, tuliumia sana maana hata mtoto wa tatu

    sawa alikuwa wa kike mrembo sana lakini nayeye alikuwa kilema pia.



    Nilikaa nikawaza sana kwanini iwe vile, ndipo nikamuita mke wangu ili nimpe siri kwa

    nini tunapata watoto wa namna ile, alipo kuja nikamwambia kwamba, “mke wangu

    kuna kipindi nilikuwa dereva wa gari, ila kwa bahati mbaya nilimgonga mtu barabarani

    na kumpasua mguu wake, baada ya hapo nilimkimbia, hata sikuwa na punje ya

    huruma kuweza kumjulia hari hospitali kipindi anakatwa ule mguu, na kuna siku moja

    nilikutana naye barabarani anatumia gongo kutembea nikatamani sana kumuomba

    msamaha ila nikaogopa, mimi naomba twende kumuomba msamaha popote alipo

    kusudi tusiendelee kupata vizazi vya namna hii, huenda Mungu na yeye pia

    atanisamehe, endapo Vule baba akitusamehe kutoka moyoni, mke wangu akasema,

    “sawa mume wangu tumtafute, maana hii ni laana"



    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Tuliangaika sana kumtafuta Vule baba ambae nilimsababishia ulemavu, ilituchukuwa

    mda sana kumpata takribani kama miaka mitatu. hila nilijuta sana, kwanini

    nimemuomba yule bwana msamaha, maana kipindi nimefika kwake, walikuja ndugu

    zake wengi pamoja na majirani zake wa karibu. Kaka yake Vule bwana akasema,

    “ulimfanya ndugu yetu awe kilema, ukamkimbia bila huruma, alafu leo unakuja kisha

    unajifanya unalia eti unaomba msamaha, hivi ulizani sisi ni wajinga tulipo kaa kimya,

    sasa basi msamaha wetu tutakupa lakini kwa sharti moja tu", asante kaka ni sharti

    gani hilo" nilimjibu hivyo nikihisi huenda wanahitaji pesa, “unatakiwa kuwacha mguu

    wako hapa, yaani tukukate pia mguu ndiyo uwe umesamehewa, maana ndugu yetu

    umemfanya kuwa mlemavu kila saa kila dakika anaumia kuupoteza mguu wake na

    chazo cha yeye kuwa hivyo ni wewe maana ulimgonga na gari lako, hivyo hatuwezi

    kukusamehe kwa maneno lazima damu ikutoke pia", mke wangu akasema, “heee!

    Wewe baba ni roho gani hiyo sasa, msameheni mume wangu, kwani hamuoni kwamba

    hana mkono mmoja, sasa mkimkata na mguu mnategemea atakuwa ni mtu wa aina

    gani, huo sini unyanyasaji, maana hata kama sawa alimgonga na gari, lakini ilikuwa ni

    bahati mbaya tu sasa mkimkata mguu mtakuwa mmesaidia nini?".



    Nilianza kulia huku nikijua fika kuwa wale watu hawawezi kunisamehe kabisa, “mume

    wangu usilie, tuondoke tu na tumkabidhi Mungu hili swala," kipindi tunaamka

    kuondoka, nilishangaa kuona napigwa teke, mke wangu akafungwa kamba miguuni na

    mikononi kisha akapelekwa chumba ambacho nilikuwa hata sikujui, nilijaribu

    kupambana nao lakini kutokana na ukosefu wa mkono mmoja wale vijana walishinda

    nguvu kabisa.



    Mke wangu alipelekwa kwenye chumba na kubaki na kijana mmoja ndani wa

    kumshikilia kusudi asitoke nje kuona ninavyo katwa mguu wangu, maana walijua kuwa

    nikakatwa na panga mbele ya mke wangu inaweza kumfanya mwanamke apate

    mshituko na kujikuta hata anajifanyajambo baya. Kibaya zaidi wale watu walikuwa

    wanakaa nje kidogo na mji hivyo kule kijijini hakukuwa hata na kituo cha polisi cha

    kuweza kutusaidia mimi pamoja na mke wangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Walinishika kwa nguvu kisha wakataka kunifunga kamba mkononi, nilikataa na

    kuwanza kupambana nao, walinipiga sana, mwili wote ulijaa damu, nikawa

    mnyongeeee! Wakanifunga kamba mkononi, kisha wakanisimamisha kwenye mti,

    kiuno changu kikafungwa kamba na niliumia sana maana ile kamba ilinifinya ngozi

    mpaka nikaanza kutamani kufa tu, ili niondokane na tabu za dunia.









    Kuna kijana aliitwa kuja kunikata mguu wangu na alijulikana kwajina la Osama, alipo

    fika akashika shoka kisha akanyanyuajuu, nililia kipindi naona kabisa naupoteza

    mguu wangu, “kaka osama, usinikate mguu ndugu yangu nisamee kaka tafadhali",

    Vule kaka alikuwa na sura mbaya sana, sura yake ilikuwa imekaa kikatili, alinyanyua

    shokajuu kisha akasema, “nakataaaa mguu, navunja mimi," kipindi ananyanyua

    shoka lakejuu zaidi kwa bahati nzuri kumbe ule mpini ulikuwa umelegea hivyo kile

    chuma cha kukatia kikachomoka na kumuumiza Osama vidole, aliweka shoka chini

    kisha akasema, “nani ameleta shoka bovu, mpaka limenigonga vidole" alinuna kisha

    akaondoka.



    Nilihisi huenda labda wale watu watanionea huruma na kuniacha niondoke zangu

    lakini wakasema, “kamuiteni chui aje kumkata huyu kijana haraka" nilipo sikia mtu

    amepewajina la chui nikajua lazima nife maanajina lenyewe liliniogopesha. Chui

    aliwasili kisha akaweka shoka sawa, “fumba macho" alisema hivyo, “chui sikia

    usinikate nitakupa pesa chui, naomba usikate mguu chui, nihurumie kaka", “fumba

    macho nimesema" alijibu hivyo.



    Nilifumba macho kweli kisha nikaanza kupiga kelele maana nilijua kuwa siwezi

    kusamehewa, kipindi nalia nikasikia mke wangu analia pia kutoka kule chumbani,

    nilihisi huenda analia kisa kanisikia nalia, lakini kumbe mke wangu alikuwa anabakwa

    na Vule kijana alie ambiwa amshike kule ndani kusudi asione ninavyo katwa mguu,

    mke wangu aliumia sana kufanyiwa ule uchafu bila idhini yake, lakini hakuwa najinsi

    maana Vule kijana alikuwa amemshikia kisu hivyo akakubali tu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Chui alisema, “navunja mfupaa, fumba macho" nilifumba macho na kukaza hisia za

    maumivu, chui alinikata mguu mpaka damu zangu zikamrukia usoni mwake, nililia

    sana maana alipo kata kwa mara ya kwanza mguu haukutoka hapo hapo hivyo

    akakata kama mara tano ndipo mguu ukaachana na mwili, wale watu walikuwa na roho

    mbaya sana, maana hawakupata huruma hata kidogo, mimi nilipata maumivu mpaka

    nikapoteza fahamu, kumbe wale vijana wakajua nimefariki hivyo wakanibeba na

    kwenda kunitupa mbali kidogo na kwao wakanipeleka sehemu zenye vichaka.







    Baada ya hapo wakaenda kumwambia kijana alie kuwa na mke wangu amtoe ndani,

    walipo ingia wakakuta yupo anambaka mke wangu kipenzi, walimlaumu sana na

    kumwambia, “unakosea kufanya hivyo, sisi shida yetu sio huyu mwanamke, shida

    yetu ilikuwa mume wake" mke wangu alipo toka tu akakuta damu nyingi nje, alipo

    ulizia mimi nilipo wakasema, “tumemtupa vichakani nenda kamtafute" wakati huo

    mimi damu zinanitoka mguuni na nimezimia sina nguvu hata kidogo wala sijitambui,

    mke wangu alianza kulia sana kisha akaanza kunitafuta nilipo ndani ya hicho hicho

    kichaka.



    Mke wangu aliangaika sana kutembea umo vichakani akisema,"mume wangu uko

    wapi" alirudia sana hayo maneno bila mafanikio, sasa Mungu saidia mke wangu alifika

    sehemu akahisi uchovu akakaa chini, kumbe nyuma ya kichuguu alicho kuwa amekaa

    nilikuwepo mimi, nilijukuta Napata fahamu huku nikisikia maumivu makari sana, nililia

    sana, mke wangu akaogopa akakimbia mbele, alipo rudi kuwangalia ni nani, alisikitika

    sana kuniona mume wake nipo chini bila mguu wangu. Alinifata kwa uchungu kisha

    akasema, “mume wangu pole sana, tumuachie Mungu yeye ndiyo muweza wa yote,

    atakama wangekukata nini kwenye mwili wako siwezi kukuwacha nakupenda sana

    mume wangu" nilikuwa na maumivu sana ndipo nikamuegemea mke wangu kisha

    tukaanza kujivuta polepole ili niende hospitali, damu zilikuwa zinatoka sana mpaka

    nikaishiwa nguvu njiani nikatamani kufa tu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mke wangu alimuona babu mmoja na familia yake wanatoka shambani kulima, aliwaita

    kisha akawaomba msaada, ndipo nikasaidiwa na kutibiwa kienyeji kwa waganga wa

    kienyeji mpaka nikapona kabisa, lakini nilibaki kilema. Kipindi tupo kijijini watoto

    wetu kumbe walikuwa wanateseka sana nyumbani, maana pesa tuliyo waachia iliisha

    kwasababu tuliacha hela kidogo tukijua tutawai kurudi nyumbani, hivyo waliishiwa na

    wakabaki bila chochote ndani, lakini kilicho wasaidia ni kwamba walitumia ulemavu

    wao kuomba msaada barabarani na kweli watu walikuwa na huruma walipo waona wote

    watatu ni vilema hivyo basi wakawasaidia.







    Hata hivyo mimi na mke wangu tuliondoka na kurudi kwetu, lakini kumbe mke wangu

    kipindi amebakwa na VuIe kijana kumbe alipata ujauzito wa VuIe bwana kwa bahati

    mbaya.







    Kwa mara ya kwanza, sikuweza kugundua kabisa kama mke wangu ni mjamzito, na

    sikuwaza kabisaaa!, Kama angeweza kuwa na mimba, maana tulikuwa tuna mda mrefu

    sana hatujakutana kimwili kwasababu tulikuwa na uoga kwamba tunaweza kuzaa

    mtoto wa nne ambaye ni mlemavu pia. Watoto wangu walishangaa sana kuona baba

    yao sina mguu, na kilicho wakwaza zaidi ni pale walipojiona wao ni vilema, na baba

    yao pia nimekuwa kilema kama wao, “baba tazama hauna mkono mmoja,juzi tu wewe

    na mama mlituaga mnasafiri kwa mda mfupi, tunashangaa umerudi bila mguu mmoja,

    kwanini familia yetu ina mikosi" alisema mtoto wa kwanza, “usijali mtoto wangu kila

    jambo litokealo huwa ni mipango ya mwenyezi Mungu" alijibu mke wangu. Sasa mimi

    kipindi mke wangu pamoja na watoto wanaongea nilikuwa nalia sana machozi

    yakinitoka mbele ya watoto, mtoto wangu wa mwisho alikuwa ananipenda sana,

    alichukuwa kitambaa na kunifuta machozi, “usilie baba, ukilia, utatuliza na sisi"

    alisema “Lidia" mtoto wangu wa mwisho alie kuwa mrembo sana lakini mlemavu pia.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mguu wangu ulikuwa bado haujapona, hivyo hata kujiusisha na swala zima la mapenzi

    na mke wangu ilikuwa ni ngumu sana, kwasababu kidonda kilikuwa hakija kauka

    vizuri. Kumbe mke wangu alikuwa amegundua kuwa ana mimba ambayo sio yangu,

    lakini akaogopa kuniambia akihisi kwamba nikijua nitamuacha na kumtelekeza, hivyo

    akaamua kukaa kimya kusudi mimi nisiweze kudungua. Siku moja nilimkuta anakula

    maembe mabichi yenye uchachu, “mke wangu kipenzi, naona unakula maembe

    mabichi leo, wewe siunasema hupendelei vitu vichachu labda uwe mjamzito"

    nilimuuliza mke wangu, “hapana mume wangu yaani huwezi amini leo kunajirani

    kapita na maembe hapa, nikammezea mate, uvumilivu ukanishida ikabidi nimuombe

    tu embe nile, lakini nililiosha kwanza" alijibu mke wangu. “haya sawa mama watoto,

    mimi naenda ndani", akajibu kwa furaha sana, “sawa mume wangu nakuja pia" ndipo

    nikageuza gongo langu na kuwanza kurudi ndani polepole.



    Siku ziliendelea kwenda, mke wangu akaanza kuwa mvivu sana wa kufanya kazi za

    ndani, vyombo vinashinda vichafu, uwanja pia mchafu, kazini hataki kwenda, mda

    wote yeye anatapika na kutema mate ovyo. Sikuweza kuhisi hata kidogo kama mke

    wangu ana mimba, maana alikuwa sio mtembezi mda wote nakuwa nae nyumbani na

    kazini, hivyo swala la mimba nilikuwa sina wasiwasi nalo kabisaaa. Siku moja

    alizidiwa sana ndipo nikamwambia kwamba, “mke wangu, hali yako kiafya sio nzuri

    itabidi nikupeleke hospitali" mke wangu alichachamaa, “hapana mume wangu, mimi

    siumwi, huo ni uharibifu wa pesa, magonjwa mengine mtu unaweza kulala na kunywa

    maji mengi ukapona tu", “ sawa mke wangu, ila kama ukizidiwa naomba usikae kimya

    niambie kusudi ukatibiwe".





    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kumbe mke wangu alikuwa akiamka asubuhi anafunga tumbo lake kwa nguvu sana

    kusudi nisiweze kugundua kama mimba inaanza kukuwa, nilianza kumuhisi kuwa ni

    mjamzito maana kuna kipindi aliaanza kumchukia sana mtoto wangu wa kwanza nilie

    zaa nae, kila akifanya kosa dogo anampiga, anamtukana mpaka matusi mtoto.

    Nilimuita mke wangu na kumkalisha chini, “mke wangu, naanza kuhisi vitu vibaya

    kwako, hivi ni kweli una mimba kama hisia zangu zinavyo niambia", “heee! Mimba,

    mme wangu kwani hiyo mimba umenipa lini, mimi sio mjamzito mume wangu, ni hisia

    zako tu" alisema mke wangu, “haya sawa kama huna mimba", nilimjibu mke wangu.

    Sura ya mke wangu ilianza kubadilika, akaanza kupata chunusi, kinywa chake kinajaa

    mate kwa mda mfupi sana. Sasa kwa sababu haikuwa mimba yake ya kwanza, hivyo

    nikajiongeza na kutambua kuwa mke wangu amebebeshwa mimba na mtu tofauti na

    mimi. Niliamua kuwa muwazi huku nikitokwa na machozi, “mke wangu, hivi kweli

    umeshindwa kuvumilia kidonda changu cha mguu kipone, ili tukutane kimwili,

    umeamua kuleta tamaa za mapenzi na kuzini nje ya ndoa, hivi ni pepo gani lililo

    kuwasha mpaka ukatoka nje, au kwasababu sina mguu" mke wangu akiwa analia pia

    akasema, “nisamehe sana mume wangu, sikutaka kukwambia maana nilijua

    nitakuumiza sana roho, kipindi wewe umefungwa kamba ili ukatwe mguu, wale vijana

    walinibeba mimi kisha wakanipeleka kwenye chumba na mmoja wao aliniingilia kimwili

    bila idhini yangu, ndiyo maana nimepata mimba ambayo sio yako" nilishtuka,

    nikajisikia vibaya sana, lakini nikaamua kukaa kimya maana nilikumbukajinsi nilivyo

    mpa mke wa baba yangu mimba, leo hii na mimi mke wangu mtu mwingine amemjaza

    mimba, ndipo nikaamini msemo usemao kwamba, “malipo ni hapahapa duniani".

    Sikuwa najinsi niliamua kuvumilia mpaka mke wangu akajifungua, lakini mke wangu

    aliumia sana, maana mtoto alitoka kabla ya miezi yake, na kutokana na kushindwa

    kutimiza njia za kumlea mtoto ambaye hajafikisha miezi tisa tumboni, ikampelekea

    Vule mtoto kufariki dunia.





    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa kipindi nilicho kuwa naumwa huku mke wangu pia ni mzazi, biashara zetu zilikuwa

    zinaendeshwa na binamu yake mke wangu, maana mama nancy alikuwa ni marehemu,

    sasa siku moja usiku kipindi Vule binamu ameleta pesa za mauzo nyumbani, mimi

    nilikuwa sipo pamoja na mke wangu hivyo Vule binamu akamkabidhi ndugu yake mke

    wangu mwingine alie kuja kumsaidia mke wangu baada ya kuwa amejifungua, sasa

    alie pewa pesa akaamua kukimbia nazo bila kutuaga maana alishikwa na tamaa ya

    pesa, Na kibaya zaidi kumbe Vule binamu alie kuwa ameleta pesa za mauzo alipanga

    mbinu na majambazi waje kutuvamia kisha wabebe zile pesa zote. Kipindi tumerudi

    nyumbani usiku mimi na mke wangu tuliwakuta watoto peke yao nyumbani, na Vule

    dada alikuwa ameisha toroka mda mrefu na kibaya zaidi alikimbia na pesa, sasa

    kipindi tupo sebreni nilishangaa kusikia, “kaeni chini" mimi na familia yangu yote

    tukalala chini, wakasema, “tunaomba pesa zote za mauzo yenu ya leo" nikasema,

    “tusamehe ndugu zetu bado binamu hajaleta"jambazi mmoja akasema, “ohh, hamtaki

    kutoa pesa ehh! Sasa hawa ngoja niwaonyeshe kazi" alimshika mtoto wangu wa

    mwisho ambaye ni lidia, alie penda kunifuta machozi mda wowote yalipo nitoka, Vule

    jambazi alimningiiniza mtoto na kumchoma kisu bila huruma, mtoto akafariki mda

    huo huo, “kama hamtaki kutoa pesa tutawaua wote, toa pesa" nikasema, “pesa

    zingekuwepo ningewapajamani leo binamu hajaleta hela" sasa kumbe wale walikuwa

    wanajua kabisa kuwa binamu kaleta hela, lakini kumbe alipo leta alimpa ndugu yake

    mke wangu, na Vule naye akakimbia na pesa bila sisi kujua.



    Jambazi akasema, “naona mnaleta mchezo na sisi" alimchukuwa mtoto wangu wa

    kwanza, alie penda kunishauri na kuniuliza maswali sana kisha akamuua bila huruma

    mbele ya macho yangu. Mke wangu alilia sana akasema, “sisi tumetoka hospitali mda

    sio mrefu hatujui pesa zilipo" nilitamani kupambana nao lakini nilikuwa sina mkono

    wala sina mguu pia, hivyo nisinge waweza maana walikuwa wawili.





    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kilicho niuma ni kwamba alibaki mtoto mmoja tu, kumbe na 9



    yeye alikuwa mjanja alipo ona watoto wenzake wanauliwa



    akaamua kusimama na kukimbia, kibaya zaidi alikuwa mlemayu hiyyo kukimbia

    kwake kulikuwa kwa shida, ndipojambazi mmoja akamfyatua na risasi, akafa hapo

    hapo, Kisha wakasema, “Sasa hivi mmebaki nyie wawili tu, mke na mume, tunaomba

    hela, msipo tupa tunawamaliza" nililia, mke wangu akalia, "'tuhurumie, tutawapa pesa

    za kesho, pesa ni makaratasi msitutoe roho zetu"jambazi akasema, “wanawake huwa

    ni wepesi sana wa kutoa pesa, inaonyesha wazi kabisa, mwanaume ndiyo anafahamu

    pesa zilipo, sasa kama anajifanya kuwa yeye ni mbishi tunamuua mke wake mbele ya

    macho yake" nilipo sikia hiyyo nilianza kutetemeka, maana nilijua kabisa sina akiba

    yoyote ndani ya kuwapa, na pesa za mauzo ni kweli hakuna, nikajutia sana kwanini

    nilikuwa sikai na pesa ndani, wakauliza, "“we mwanaume unawaza nini, unazani

    unaweza kutukwepa, sisi tunaroho ngumu, tumeisha ua sana, tuna hesabu mpaka tatu

    usipo tupa pesa tuna muua mke wako sasa hivi," nilihisi wanatania, “moja...

    mbili....tatu" nilifumba macho na kusikia sauti ya mke wangu ikisikika na kupotea

    ghafla, nilipo fumbua macho nikakuta kisu kimepitiswa katikati ya shingo la mke

    wangu, huku akitoa sauti kama kuku anayyo chinjwa, akaanza kuchezesha sana

    miguu mpaka akafariki.



    Nililia mpaka nikaishiwa nguvu na sauti ikaanza kukoroma, Jambazi mmoja akasema,

    “wewe baki hapa muangalie huyu mjinga, ngoja nikatazame chumbani kama naweza

    kupata pesa" kipindi nimebaki na Vulejambazi mmoja nilikuwa naangaliajinsi ya

    kumkwepa pale kusudi nisife, kuna kipindi aligeuka nyuma kidogo ndipo nikambonda

    na gongo langu kichwani kwake, alianguka na kuzirai hapo hapo, ndipo nikatoka

    haraka haraka, maanajambazi mwingine alikuwa bado anakagua yyumba pole pole

    kutafuta pesa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kesho yake nilirudi nyumbani kwangu, kuwangaliajinsi ya kuendesha mazishi ya

    familia yangu nikakuta ndugu wa mke wangu wapo wote pale, nilichukia sana walipo

    niita pembeni na kuniambia, “shemeji Meshack, tunashukuru sana kwa kuteketeza

    ukoo wetu, umeua watoto, umeua mke wako, tunashukuru, tulitaka kukufunga lakini

    tumemuachia Mungu tu, ila ukoo umekaaa chini na kuongelea hili swala, hivyo basi

    kwanzia leo hauruhusiwi kuishi kwenye hii nyumba, na miladi yote ipo chini yetu

    tungeomba tu urudi kwenu, maana hata wazazi wako hatuwajui wala kuwatambua,

    asante kwa mauaji yako ondoka kabla na wewe hujauliwa,".









    Niliogopa sana yale maneno nikaumia zaidi kwanini mimi nafukuzwa bila hata

    kumwaga mchanga kwenye makaburi ya familia yangu. Sikuwa najinsi nikaona bora

    niondoke kusudi nisije kuuliwa, kama niliyyo katwa mguu na wale watu wengine.

    Niliamua tu kurudi nyumbani ili nimuombe baba msamaha, maana laana za dunia

    zilinikomesha sana, wakati nipo safarini narudi nyumbani, nilikuwa nazungumza

    mwenyewe kwenye basi kama kichaa, kila mtu ananishangaa, kumbe ni damu iliyo

    yuja ya watoto wangu na mke wangu kwa ajili ya laana zangu za kutembea na mke wa

    baba, ndiyo ilikuwa inanisumbua, nilipo fika Dar es salaam, (ubungo) nikashuka

    kwenye basi, nilikutajiji limebadilika, barabara mpya za mwendokasi zimejengwajiji

    linayutia sana.



    Kipindi nimezubaa naangalia mgari ya mwendo kasi, nilishangaa kuona kijana mmoja

    anakuja na kuvuta begi langu kwanguyu kisha akakimbia nalo nilimuona sura yake

    yizuri tu, hiyyo nikabaki bila nguo yoyote, na kukimbia nilikuwa siwezi, hata mawazo

    ya kupiga kelele kuwa nimeibiwa sikuwa nayo, sababu ya mawazo ya mauaji ya

    kikatili kwenye familia yangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Niliamua kwenda mpaka kwa baba, nilipo fika kwenye geti lake, nilianza kujifikilia

    mara mbilimbili, "je nigonge mlango, hivi kweli baba akiniona atanisamehe, acha

    nigonge tu mlango, akija nitamwambia, baba nimerudi kwako naomba unisamehe

    sitarudia kosa " baada ya hapo nikagonga mlango, kweli mlango ukafunguliwa na

    mwanamke mrembo sana, “nikusaidie nini", “dada mimi naitwa Meshack, hapa ni

    nyumbani kwetu sijui baba nimemkuta" akasema, “mhhh! Subiri kidogo nakuja" alipo

    ingia ndani akaja na mme wake, “yipi kijana umesema wewe unaitwa nani" nikawajibu,

    “ohhh! Baba yako alituuzia hii nyumba, na hatujui mpaka leo yupo wapi" nilichoka

    sana, ndipo wakanipa msaada wa kulala kwaojapo siku moja kisha kesho yake

    nizunguke kumtafuta baba yangu mzazi kusudi anisamehe niondokewe na pepo la

    laana.



    Nilijaribu sana kumtafuta baba yangu ikashindikana, siku moja kuna shirika moja

    liliitisha walemayu wote ili tule na kufurahi kwa pamoja huku huku Dar es salaam,

    niliamua kwenda pia maana nilikuwa sina mkono pamoja na mguu, kipindi nipo pale

    nimekaaa huku nikisikiliza ushauri wa wageni mbalimbali walio kuwa wamealikwa

    kuongea na sisi, nilishangaa kumuona “Fey" akiwa hana miguu yote miwili, akiwa

    ameletwa na mtoto wake nilie zaa naye kwenye baiskeli ya vilema, alafu kumbe huyo

    mtoto nilipo mtazama yizuri ndiye ambae aliniibia begi langu kipindi nimefika ubungo.







    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Uvumilivu ulinishinda ikabidi nimfate karibu, “habari dada unanikumbuka,"

    aliniangalia akasema, “Meshack ni wewe!"“ndiyo ni mimi mama" alifurahi sana

    kuniona, akauliza, “mbona hauna mkono na mguu" nikacheka huku moyo ukiwa

    unaniuma sana kisha nikamuuliza, “mbona wewe huna miguu yote pia" akasema, “ni

    hadithi ndefu sana Meshack, lakini hii yote ni kutokana na tabia mbaya tuliyo kuwa

    tunafanya bila kujua malipo ni hapa hapa duniani, nilikuwa nataka kumuua baba yako,

    nikamfanya mpaka akaota peazi tumboni, leo hii baba yako anaishi maisha mazuri tu

    alafu mimi nateseka na ulemavu wangu, kama ningekuwa namuheshimu nisinge kuwa

    hivi" nikamsimulia pia matatizo yote niliyo pitia na laana zilizo nikuta mpaka akalia,

    kisha tukaombana msamaha palepale, kipindi nataka kuondoka akasema, “Meshack

    huyu mtoto anae nisukuma na hichi kibaiskeri, ndiyo mtoto wetu tulie msingizia baba

    yako, mpaka leo hajawai kwenda shule na ukubwa wote huu" mtoto wangu akasema,

    “baba nisamehe najua nilikuibia begi lako lakini nitarudisha tu" tulibadilishana

    mawasiliano kisha nikaondoka.



    Siku moja nikampigia Fey (mke wa baba) kisha akanielekeza sehemu baba anayo ishi,

    nilipo fika nikakuta nyumba yake kubwa sana, walinzi wa kila aina, sehemu za

    kuogelea, maua, nyumba nzuri sana yenye mvuto wa kisasa, baba alipo niona

    akaanza kusikitika mwenyewe kisha akasema, "'tazama sasa, unatembea na gongo

    wakati ulikuwa kijana mzima kabisa, hizo zote ni laana mwanangu, ulimfanya mke

    wangu kama mke wako, bila kukumbuka uchungu na nguvu nilizo zitumia kukulea

    wewe, ukazaa na mke wangu kipenzi, mkaniona mimi mjinga siwezi kugundua, ukazani

    unanizidi akili baba yako, kibaya zaidi mlikuwa mnazini ndani ya nyumba yangu,

    mwanangu haya maisha tunapita tu, alafujiulize swali kwamba baada ya kufa utaenda

    wapi,je ukiisha enda huko ukiulizwa kwanini ulizini na mama yako utamjibu nini

    Mungu" nikamjibu kuwa, “nisamehe baba nimerudi mwanao, ulimwengu umenifunza,

    siwezi kurudi kosa, tazama sina mguu, sina mkono, nihurumie baba ulimwengu

    umenifunza" baba akasema, mwanangu, “waheshimu baba na mama upate heri na

    miaka mingi duniani, nimekusamehe mtoto wangu, sogeza kichwa chako nikushike,

    uondokewe na mikosi, na kwanzia sasa unapaswa kumjua Mungu, na umuombe sana

    ili akusamehe dhambi zako" nilikumbatiana na baba yangu.







    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alinitafutia mguu na mkono wabandia, nikaanza kufanya kazi nilizo ziweza kutokana

    na helimu yangu maana niliyipata yyeti yyangu selikarini, nilianza kupata pesa na

    maisha mazuri, ndipo nikaanza kumsomesha mtoto wangu na kumsaidia maisha mke

    wa baba bila kuzini naye kama zamani, nilifunga safari ya kwenda kuwangalia

    makaburi ya familia yangu. Mpaka sasa naishi mimi na baba nyumbani na

    sijabahatika kupata mtoto tena zaidi ya huyu niliye zaa na mke wa baba, na Mungu

    saidia baba yangu anampenda sana mjukuu wake, Siwezi kurudi tena kutembea na

    mke wa mtu, rafiki, mzazi,jirani au mtu yoyote Yule maana malipo ni hapa hapa

    duniani.



    ******************MwISHo**********************



0 comments:

Post a Comment

Blog