Search This Blog

Monday, October 24, 2022

FACEBOOK CHATTING - 2

 





    Chombezo : Facebook Chatting

    Sehemu Ya Pili (2)




    Leo hii, vita vya chini chini vimeanza, vita ambavyo sitotaka kuwaambia marafiki zangu mpaka pale ambapo ningekamilisha ‘mission’ yangu na kuwa naye. Hebu jifikirie kwanza, Dorcas angetoka vipi? Angeweza kuanzia wapi kunikataa na wakati nilikuwa na maneno mengi ya kuandika? Sikuona angetokea wapi, ila kama atanikubali, siku ya kuonana sijui ingekuwaje kama atagundua kwamba ni mimi atafanyaje? Ila hiyo siyo ishu, ishu kubwa ni kumfanya aangukie kimapenzi kwenye mikono yangu iliyo salama juu ya maisha yake......thats all. 
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: (Nikalog out na kulala huku nikisubiri kesho nianze pale nilipoishia)


    Siku iliyofuata, nakumbuka kabisa sikuwa na fedha kwenye line yangu ambayo nilikuwa naitumia sana kuunganisha na huduma ya internet. Siku hiyo nilikaa katika hali ya unyonge kupita kawaida, akili yangu ilikuwa ikimfikiria Dorcas tu. Sikujua ningepata vipi fedha ya kujiunga na internet kwani muda wa kifurushi nilichokuwa nimenunua muda wa kujiunga, ulikuwa umemalizika jana usiku. 
    Kwa sababu nilikuwa mjanja nikaanza kuwasiliana na baba, mzee Chilongani na kisha kumwambia kwamba nilikuwa na shida ya kiasi cha shilingi elfu thelathini. Japokuwa alinihoji maswali mengi, nilimjibu kisomi mpaka akanitumia kiasi hicho ambacho nikaamua kuchukua kifurushi cha mwezi mzima cha Vodacom, sikutaka tena kupata usumbufu wa kutokuwa na huduma ya internet katika harakati zangu za kumtia mikononi Dorcas.


    Nilijiunga na huduma ya mwezi mzima ya Internet ya Vodacom na kisha kuanza kufungua akaunti facebook. Kwa wakati huo, akili yangu ilikuwa ikifikiria maneno mengi matamu ambayo nilipaswa kumwambia Dorcas katika kipindi ambacho ningemkuta online. Baada ya kufungua mtandao wa facebook, nikaanza kuangalia listi ya marafiki zangu ambao walikuwa online, walikuwa nane tu kwani kipindi hicho nilikuwa na marafiki 102 tu. 


    Kati ya watu ambao walikuwa online, Dorcas hakuwepo kabisa, nilinyong’onyeaje. Ikabidi nizuge zuge na marafiki ambao walikuwa online kwa wakati huo kwa kupiga stori mbili tatu. Nakumbuka ilipofika saa 9:17 alasiri, Dorcas akaingia online. Kwanza nikashtuka sana, mapigo yangu ya moyo yakaanza kudunda kwa kasi ya ajabu, sikutakiwa kuhofia chochote kile, nikaamua kumpa hi.


    MIMI: Mambo Dory! (Nilimsalimia huku nikitoa tabasamu kana kwamba alikuwa akiniona).
    DORCAS: Poa. Mzima Brother?
    MIMI: Nipo poa. Nimekusubiri sana online.
    DORCAS: Acha kunidanganya Brother.
    MIMI: Nikudanganye ili iweje? Kwani kunatolewa tuzo kwa atakayemdanganya mwenzake?
    DORCAS: Hahaha! Hujaacha tu maneno yako?
    MIMI: Maneno gani?
    DORCAS: Si hayo hapo unayoongea.
    MIMI: Mbona yapo kawaida tu. Hebu acha nikuulize kitu kimoja. Uliniota jana usiku?
    DORCAS: Hapana.
    MIMI: Dah! Kwa hiyo uliniacha nikuote wewe tu bila kuniota?
    DORCAS: kwani uliniota?
    MIMI: Yeah! Nilikuota sana. Nilikaa nawe sana tukipiga stori. Nilifurahi sana.
    DORCAS: Uliota tukipiga stori wapi? Humu facebook?
    MIMI: Hapana. Ulikuja nyumbani.
    DORCAS: Kwenu?
    MIMI: Yeah!
    DORCAS: Mmmh!
    MIMI: Mbona unaguna tena?
    DORCAS: Siamini.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Huamini nini?
    DORCAS: Kama nilikuja kwenu.
    MIMI: Je nikikwambia kwamba ulikuja nyumbani na kuingia chumbani kwangu na kuanza kupiga stori chumbani humo, utaamini?
    DORCAS: Acha utani bwana.
    MIMI: Kweli tena. Halafu nikwambie kitu?
    DORCAS: Niambie.
    MIMI: Asilimia mia moja za ndoto zangu huwa kweli.
    DORCAS: Hahaha! Kwa hiyo unamaanisha hata hiyo itakuwa kweli?
    MIMI: Wewe unaonaje?
    DORCAS: Haitoweza kuwa kweli.
    MIMI: Okey! Tufanye haitoweza kuwa kweli. Ila ukiulizwa kama ungependa iwe kweli, utakubali?
    DORCAS: Inategemea.
    MIMI: Inategemea na nini?
    DORCAS: (Kimyaa)


    Dizaini nikaliona swali langu ambalo nilimuuliza lilikuwa gumu kujibika, nilikuwa nikimuona akilini akiwa anafikiria jibu la kunipa. Wala sikuwa na wasiwasi kabisa, nilikuwa najiamini sana, hivyo nikakaa kimya na kuanza kumsikilizia angejibu nini. Ghafla katika hali ambayo sikuitegemea, akatoka online. 
    Nilionekana kuchukia sana, kwa nini Dorcas atoke online na wakati alijua fika kwamba nilikuwa online kwa ajili yake, nilinyong’onyea sana. Mara ghafla huku nikiwa simuoni online, nikashtukia napokea meseji kutoka kwake.


    DORCAS: Samahani Brother.
    MIMI: Samahani ya nini tena Dory?
    DORCAS: Nilikuwa Intenet Cafe, nilichukua nusu saa kwani kuna kitu nilikuwa namtumia kaka kwenye email yake, muda uliniishia. Kwa sasa natumia simu yangu.
    MIMI: Usijali. Upo wapi now?
    DORCAS: Nipo kwenye daladala naelekea nyumbani.
    MIMI: Take care njiani.
    DORCAS: Usijali wangu. Nikifika home nitakushtua.
    Mimi: Poa.


    Hiyo ndio hatua ambayo ilikuwa ikiendelea. Kutoka kuitwa Brother mpaka kuanza kuitwa ‘wangu’. Hapa ngoja nikwambie kitu. Kwangu mimi, hasa katika kipindi kile cha nyuma kabla sijazoea, nilikuwa nikiona kuitwa ‘wangu’ lilikuwa jina moja ambalo lilikuwa likinichanganya sana. Mtoto wa kike aniite ‘wangu’? Anamaanisha nini aisee? Kwa nini niwe wake? Kila nilipojiuliza, nikabaki na mshangao wenye furaha moyoni mwangu.


    Siku hiyo sikutaka kutoka online. Japokuwa nilitakiwa nionane na Rich Carter Jr saa kumi jioni lakini siku hiyo nikaamua kumchunia. Nilichokifanya ni kuizima simu yangu. Katika kipindi hicho, Dorcas alionekana kuwa muhimu sana kuliko Rich Carter Jr. Rafiki alikuwepo tu, hata kama ningekataa kuonana naye siku hiyo wala asingekasirika sana kwa sababu yeye yupo maishani mwangu. 
    Ila hali ilikuwa tofauti na Dorcas. Kama angekuta kwamba sipo online au amenitumia meseji halafu imekaa muda mrefu bila majibu ingekuwaje? Ningemkasirisha kitu ambacho sikutaka kitokee. Kwangu, hasa kwa wakati huo, Dorcas alionekana kuwa kama yai au sahani ya udongo ambayo ilitakiwa kushikwa kwa uangalifu mkubwa sana. Kama kawaida, mara baada ya kufika nyumbani kwao, nikakuta meseji ikiingia kutoka kwake, kwa haraka haraka nikaifungua.


    DORCAS: Nimefika salama wangu.
    MIMI: Mungu amejibu maombi yangu.
    DORCAS: Maombi gani tena?
    MIMI: Nilikuwa namuomba akulinde njia nzima.
    DORCAS: Kwa hiyo wewe mwanamaombi siku hizi?
    MIMI: Yeah! Halafu dizaini kama Mungu anajibu kila ombi ninaloomba.
    DORCAS: Ahahaha! Kwani ulikwishawahi kumuomba maombi gani ambayo aliwahi kukujibu?
    MIMI: Kuna siku nilipiga goti na kumuomba kwamba anipe bahati ya kuchati na msichana mzuri. Jana amenipa.
    DORCAS: Hahahaha! Msichana gani huyo nimjue?
    MIMI: Wewe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    DORCAS: Hahahaha!
    MIMI: Unanicheka?
    DORCAS: Hapana wangu. Nimefurahi tu. Endelea kuomba tu.
    MIMI: Yeah! Jana nilipiga tena goti.
    DORCAS: Uliomba nini?
    MIMI: Niweze kukutana na huyu msichana niliyeanza kuchati naye jana. Ila kwanza kabla ya kukutana tuwe wapenzi.
    DORCAS: Una utani sana Brother.
    MIMI: Kweli tena. Namsubiria ajibu maombi yangu. Natumaini atajibu hivi soon.
    DORCAS: Ombi lako hilo bila kufunga na kuomba sijui kama litajibiwa.
    MIMI: Kwa nini?
    DORCAS: Ni ombi moja ambalo linahitajika kuwa na nguvu sana.
    MIMI: Litafanikiwa tu. Au wewe hauamini hilo?
    DORCAS: (Kimyaa)
    MIMI: Swali gumu?
    DORCAS: Hapana. Omba sana.
    MIMI: Nikuulize swali?
    DORCAS: Uliza.
    MIMI: Unanipenda?
    DORCAS: Kama rafiki wa facebook tu.
    MIMI: Hebu chukua sekunde kumi za kuzungumza na moyo wako juu yangu. 
    DORCAS: Hata nikichukua dakika kumi, bado wewe ni rafiki yangu tu.
    MIMI: Nikwambie kitu Dorcas.
    DORCAS: Niambie.
    MIMI: Ukweli ni kwamba unanipenda. Nadanganya?
    DORCAS: Hahaha!
    MIMI: Nimekwishazungumza na moyo wako. Unaonekana kuwa mnyonge sana, moyo wako ulihitaji furaha ya kipindi kirefu sana, unayapenda sana mapenzi japokuwa wakati mwingine unaona kwamba mapenzi hayakupenda, labda umekata tamaa na kujiona kwamba una bahati mbaya sana katika masuala yote ya mahusiano. Labda umelia sana, au umehuzunika sana moyoni mwako kwa sababu ya mapenzi. Moyo wako nauona una kidonda kikubwa sana, kidonda ambacho hauamini kama kuna siku kitakuja kupona. Ngoja nikwambie kitu leo, mimi ndiye ambaye nitakuwa dawa kubwa sana ya kukiponyesha kidonda chako moyoni, kidonda ambacho kinaweza kuoza na kuuharibu moyo wako wote. Nitakuwa na uwezo wa kuja na kufanya kazi kubwa ya kukurudishia furaha yako iliyopotea......ila yote yatawezekana kama utafanya kitu kimoja tu.
    DORCAS: Kitu gani?
    MIMI: Kunipa ruhusa ya kuingia moyoni mwako na kuufungua ukurasa mpya wa kimapenzi. Tunaweza kuufungua sasa?
    DORCAS: Naogopa.
    MIMI: Unaogopa nini?
    DORCAS: Utaendelea kuumiza.
    MIMI: Unaniamini?
    DORCAS: Nakuamini.
    MIMI: Basi fanya kama nilivyokwambia. Niruhusu sasa.
    DORCAS (Kimyaa)
    MIMI: Dorcas.
    DORCAS: Abee.
    MIMI: Nakupenda sana.
    DORCAS: Nafahamu sana. Najua kwamba unanipenda sana. Kila siku umekuwa ukiniambia neno hilo. Nakumbuka ulikuwa ukikaa sana uchochoroni kwa ajili yangu, wakati mwingine ukinisindikiza shuleni na hata dukani na kuniambia kwamba unanipenda. Nilikuwa nikikufikiria sana, sikuamini kama kweli ulikuwa ukinipenda ila mpaka nilipohama Tandale ndipo nilipoamini kwamba unanipenda. Yaani ilikuwa ni sawa na kitu ambacho unacho, huwezi kukiona thamani yake mpaka unapokipoteza. Najua unanipenda Nyemo, najua unanihitaji sana.
    MIMI: (Kimyaa)


    Kwanza nikashtuka, kumbe nilikuwa nikizuga muda wote huo na wakati Dorcas alikuwa akijua kwamba mtu ambaye nilikuwa nikijiita Brother Prince nilikuwa mimi. Moyo wangu ukaanza kujisikia aibu, nilitamani niache kuchati naye muda huo huo. Nilijihukumu moyoni kwa kuona kwamba inawezekana Dorcas alianza kuniona mimi malaya kwa kuwadandia wasichana wa Facebook.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    DORCAS: Nyemo.
    MIMI: (Huku nikijisikia noma moyoni) Naam.
    DORCAS: nakupenda sana.
    MIMI: Dah!
    DORCAS: Nini tena?
    MIMI: Nikuulize kitu?
    DORCAS: Uliza.




    Kwanza nikakaa kimya kwa muda, kichwa changu hakikuwa kikionekana kuwa sawa kabisa katika muda huo. Ni kweli kwamba nilikuwa nikitamani sana kuwa na Dorcas kwa sababu tu nilikuwa nampenda sana tena toka kitambo, sasa swali ambalo lilikuja akilini mwangu kwa wakati huo, ni kwa jinsi gani alikuwa amefahamu kwamba mimi nilikuwa Nyemo na wakati nilitumia jina langu la A.K.A? Kila nilipojiuliza, nikakosa jibu.


    MIMI: Umejua vipi kama ni mimi?
    DORCAS: Nilikuwa na machale.
    MIMI: Acha kunitania Dorcas...machale gani hayo yaliyokufanya unitambue?
    DORCAS: Si kwa sababu ulikuwa unanipenda.
    MIMI: Si kwamba nilikuwa. Nakupenda mpaka sasa.
    DORCAS: Nashukuru kusikia hivyo.
    MIMI: Ila bado haujanijibu Dorcas.
    DORCAS: Hiyo ni kwa sababu natumia akaunti mbili. Kuna kipindi nilikutumia meseji kwa kutumia akaunti yangu nyingine na kisha kukutumia ombi la urafiki, ukanikubalia. Sasa uliponitumia urafiki kwa kutumia akaunti hii, nikaona ‘matual friend’ akiwa mmoja. Nilipocheki, nikakuta ni akaunti yangu nyingine. Kwanza nikashtuka, sikujua kama nilikwishawahi kuwa na rafiki mwenye jina hilo. Nilipoangalia meseji za kule, nikagundua kwamba ni wewe.
    MIMI: Mmmh!
    DORCAS: Nini tena?
    MIMI: Wewe mjanja sana.
    DORCAS: Kawaida tu Nyemo.
    MIMI: Sawa. Ila mbona haujanijibu? Upo tayari?
    DORCAS: Tayari nini?
    MIMI: Kuwa na mimi.
    DORCAS: Mmmh! Unataka nipigwe tu.
    MIMI: Na nani tena?
    DORCAS: Msichana wako.
    MIMI: Yupi?
    DORCAS: Una marafiki wengi sana Nyemo, kuna wasichana wengine wanapenda sana kufuatilia hadithi zako, sasa unafikiri watajisikiaje kama wakiona nipo na wewe?
    MIMI: Watajisikia kawaida kwani hawajawahi kuniambia kwamba wananipenda.
    DORCAS: Hahaha! Hapana bwana Nyemo. Kwa hiyo wangekwambia?
    MIMI: Ningekataa.
    DORCAS: Kwa nini sasa?
    MIMI: Kwa sababu moyo wangu upo kwako.
    DORCAS: Nyemo unataka kunitafutia ugomvi bwana. Sipendi maneno maneno bwana. Nianze kuzungumziwa sana kisa natoka na wewe. Wasichana sisi tuna mambo sana Nyemo. Acha niwe peke yangu kwa sasa.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Hicho ni kitu ambacho sitaki kitokee. Najua kwamba inawezekana kuna msichana au wasichana wanapenda kuwa na mimi, okey, hiyo ni hali ya kawaida kutokea facebook japokuwa sitaki itokee kwa sababu napenda kufanya mambo yangu kwa uhuru facebook, lakini watakwambia maneno gani na wakati uhusiano wangu ni kati yangu na wewe tu. Usiwaogope bwana, wataongea sana mchana, usiku watalala tu.
    DORCAS: Ila kila siku nitakuwa nikiumia sana Nyemo.
    MIMI: Kivipi?
    DORCAS; Mtu akitokea na kuanza kukuita ‘wangu, kipenzi, sweetie’ na majina mengine kwenye comment, unafikiri nitafurahia?
    MIMI: Ni majina ya kawaida tu, labda uwe na wivu kupitiliza.
    DORCAS; Wivu ndio mapenzi Nyemo. Kama nisipojisikia wivu kwako, hiyo inamaanisha sina mapenzi kwako. Ili nijulikane kama nina mapenzi, wivu muhimu.
    MIMI: Kumbe ndivyo ilivyo?
    DORCAS: Yeah!
    MIMI: Sawa, nimekuelewa. Nipe jibu la uhakika sasa....upo tayari?
    DORCAS: Dah!
    MIMI: Nini tena?
    DORCAS: Mambo magumu sana Nyemo. Nauonea huruma moyo wangu tu.
    MIMI: Usijali. Nitaujali na kuulinda.
    DORCAS: Kabla sijakujibu naomba nikuulize swali moja.
    MIMI: Uliza tu.
    DORCAS: Umekwishawatongoza wasichana wangapi humu facebook?
    MIMI: Mmoja tu. Wewe.
    DORCAS: Hahaha! Na umekwishawahi kutongozwa na wasichana wangapi humu facebook?
    MIMI: Hakuna hata mmoja.
    DORCAS: Una rekodi ya kutongozwa na msichana yeyote maishani mwako?
    MIMI: Hapana.
    DORCAS: kwa hiyo huwa unatongoza wewe tu?
    MIMI: Maswali yamekuwa mengi kweli Dory.
    DORCAS: Hahaha! Mbona unaonekana kulikimbia swali. Nijibu kwanza.
    MIMI: Kwa hiyo kisa nataka cha uvunguni, kwanza sharti niiname?
    DORCAS: Ndio.
    MIMI: Sijazoea kutongoza. Huwa najisikia aibu sana.
    DORCAS: Sasa mbona mimi umenitongoza.
    MIMI: Sijakutongoza.
    DORCAS: kumbe umefanya nini hapo?
    MIMI: Nimekukumbusha tu juu ya upendo ambao nilikuwa nao juu yako toka zamani.
    DORCAS: Hahaha! Wewe mwanaume mjanja sana. Yaani unakwepa kwepa.
    MIMI: Huo ndio ukweli. Upo tayari?
    DORCAS: Naomba unipe muda.
    MIMI: Muda! Wa nini tena?
    DORCAS: Kujifikiria.
    MIMI: Yaani hata ukumbusho wangu pia unahitaji kufikiriwa?
    DORCAS: Ndio.
    MIMI: Ukinijibu hapa hapa kuna nini?
    DORCAS: Kuna mengine si ya kujibu haraka haraka Nyemo.
    MIMI: Kwa hiyo unakwenda kuomba ushauri kwa mama?
    DORCAS: Umejuaje! Si unajua kila kitu lazima nimshirikishe.
    MIMI: Hebu acha zako. Niambie basi kwanza nijue ni nini hatma yangu, kama kujiua au kuendelea kuvuta pumzi.
    DORCAS: Hahaha! Ujiue kisa mapenzi?
    MIMI: Yeah! Sasa kama mtu unampenda halafu yeye hakupendi, unategemea nini? Kujiua tu.
    DORCAS: Sasa mbona hukujiua toka zamani?
    MIMI: Nilikuwa sina akili ya kujiua. Ila sasa hivi ninayo. Ukinikataa tu, najiua, nishachoka maisha ya kukataliwa na mtu mmoja.
    DORCAS: Owkey..Usijali. Tutaongea zaidi baadae. Nataka kwenda kusuka.
    MIMI: Daah! Naomba kwanza unipe jibu langu.
    DORCAS: Itakuwa ngumu kwa sasa. Unaonaje tukionana baadaye.
    MIMI: Tuonane wapi?
    DORCAS: Unapajua nyumbani?
    MIMI: Hapana.
    DORCAS: Njoo hapa magomeni Mapipa then nitakufuata kituoni.
    MIMI: Sasa hivi?
    DORCAS: Usiwe na haraka. Nikimaliza kusuka nitakushtua.
    MIMI: Poa. 
    DORCAS: Kwa heri.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Ila namba yangu si unayo?
    DORCAS: Sina. Hebu nipatie.
    MIMI: 0716 008866
    DORCAS: Mtoto wa Tigo.
    MIMI: Kama kawa mchumba.
    DORCAS: Basi baadae.
    MIMI: Pwaxxxxx


    Kilichofuata baada ya hapo ni Dorcas kutoka online. Moyoni nilijisikia amani kupita kawaida, furaha ambayo ilikuwa imetoweka ikaanza kurudi. Dorcas yule ambaye nilikuwa nikimfuatilia kwa kipindi kirefu, leo hii alikuwa ameamua kukutana nami na kisha kukaa pamoja na kuzungumza. Kiukweli nilikuwa katika mudi nzuri sana, yaani kwa hali ya furaha ambayo nilikuwa nayo katika kipindi hicho, hata kama ungekuja kwangu na kuniambia nikukopeshe 10,000/=, nisingekukopesha, ningekupa kama rafiki yangu kutokana na furaha ambayo nilikuwa nayo.


    Hii facebook hii...yaani hawa wasichana hawawezi hata kujishika kabisa. Kipindi cha nyuma kabla ya kuanza kumfuatilia Dorcas, wala hawakuwa wakinifuata fuata ila baada ya hapo ndipo nao wakaonekana kubadilika kiasi ambacho mpaka nikaanza kuiona facebook kuwa chungu. Mapenzi haya + facebook = bado nusu yanitoe roho hasa mara baada ya kuingia katika mahusiano na huyu Dorcas ambaye kwa wakati huo nilikuwa namuita moyoni ‘QUEEN OF MY HEART’.


    Nilionekana kuwa mwingi wa presha, muda wote nilikuwa naiangalia simu yangu tu, sikujua ni muda gani ambao mtoto Dorcas angepiga simu ile. Macho yangu yalikuwa kodokodo kila wakati. Nilikuwa na hamu kubwa ya kuonana na Dorcas kuliko mtu yeyote katika dunia hii.


    Kuna kitu kimoja ambacho kilikuwa kikiniudhi sana na ninaamini kwamba hata wewe kimekwishawahi kukutokea mara nyingi sana. Utakuta mtu unasubiri simu ya mtu muhimu sana, halafu katika kipindi hicho hicho mtu mwingine anaanza kukupigia simu, unakuwa kwenye hali gani? Sasa hicho ndicho kilichokuwa kikinitokea katika wakati huo.


    Sijakaa vizuri, Vonso, rafiki yangu kapiga, sijakaa vizuri, Shedrack Joshua kapiga, sijakaa vizuri, utakuta nae Muksin Muhinga nae kapiga, siku hiyo nilikuwa nikikasirika sana kiasi ambacho nilitamani kuwatukana. Katika kipindi hicho, sikutaka kupokea simu ya mtu yeyote yule, simu ambayo nilikuwa nikitaka kuipokea ni ya msichana Dorcas tu.
    Saa 11:20 jioni, simu yangu ikaanza kuita tena, nilipoiangali, ilikuwa ngeni, unafikiri nilifikiri nani hapo? Nilipoipokea, sikio langu likakutana na sauti nzuri, sauti nyororo ambayo sidhani kama nilikwishawahi kuisikia sehemu yoyote zaidi ya waimba kwaya hasa wale wanaoimba sauti ya kwanza. Alikuwa Dorcas.


    DORCAS: Mambo!
    MIMI (Huku nikitoa tabasamu kana kwamba Dorcas alikuwa akiniona): Poa. U mzima?
    DORCAS: Mzima. Otea unaongea na nani.
    MIMI: Naongea na Malaika wangu, Dorcas.
    DORCAS: Hahaha! Upo wapi?
    MIMI: Nipo home.
    DORCAS: Unaweza kuja sasa hivi au upo bize?
    MIMI: Naweza. Sipo bize wala nini, yaani hapa nilikuwa nasubiria simu yako tu.
    DORCAS: basi poa. Nakusubiria hapa Mapipa.
    MIMI: Poa. (Nikakata simu)


    Vitu vingine si lazima nikuambie ni kwa jinsi gani katika kipindi hicho nilikuwa na uharaka. Nilivaa nguo fasta fasta halafu mbaya zaidi, kila nguo niliyokuwa nikiivaa niliiona kuwa haijanikaa vizuri na wakati siku nyingine zilionekana kunikaa vizuri. Kiu yangu katika kipindi hicho ilikuwa ni kumuona Dorcas kwa mara nyingine tena, katika kipindi ambacho ningekaa nae chini na kuanza kuzungumza nae.


    Nilipotoka nyumbani, sikuaga, nikachoma mazima na kukimbilia tigo pesa. Sikutaka kwenda mifuko mitupu au labda ningekuwa nakutana na rafiki yangu Babi De Councious. Nikatoa shilingi elfu kumi na tano na kisha kuchukua bajaji. 


    Nadhani hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza kukodi bajaji kutoka Tandale mpaka Magomeni. Japokuwa Dorcas alikuwa akiijua hali yangu ni ya kawaida lakini siku hiyo nilitaka kuonekana tofauti kidogo. Bajaji ilichukua dakika tano, ikafika Magomeni Mapipa na kisha kuteremka.


    Macho yangu yalipotua kwa Dorcas, alionekana kuwa mrembo sana asikwambie mtu. Alikuwa amevaa kipedo cha jinzi fulani zile laini laini, kishati kidogo cha rangi ya pinki pamoja na raba fulani simpo sana huku kichwani akiwa amevaa kofia fulani za kisista duu. 
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Duh!
    DEREVA BAJAJI: Vipi?
    MIMI: Demu mwenyewe yule pale. Kulalaleki, kawa mkali ile mbaya.
    DEREVA BAJAJI: Yupo wapi? Yule mwenye hijabu?
    MIMI: Hapana. Yule aliyevaa kipedo.
    DEREVA: Duuuh!
    MIMI: Vipi?
    DEREVA BAJAJI: Mmmh! Yule demu mkali aisee.
    MIMI: Ndio huyo bwana. Chukua kwanza hii hela yako then tutaonana nyumbani (Nilimwambia huku nikimgawia fedha zake)
    DEREVA BAJAJI: Poa (Akaipokea fedha ile na kisha mimi kushuka chini)


    Nikaanza kupiga hatua kumfuata Dorcas, kwa mbali nilikuwa nikitetemeka huku kijasho chembamba kikinitoka. Kwa mbwembwe zake, Dorcas aliponiona, akapiga uyowe mkubwa na kisha kuja kunikumbatia kwa furaha. Nilijisikiaje aibu.
    Dorcas alikuwa akinukia kupita kawaida, pafyumu yake ambayo alikuwa amejipulizia siku hiyo nadhani sijawahi kuisikia sehemu yoyote ile.


    MIMI: Mmmh! Unanukia vizuri (Nilimwambia karibu na sikio lake huku akiwa kanikumbatia)
    DORCAS: Asante
    MIMI: Natamani nikubebe juu, na hivi ulivyokuwa mwembamba.
    DORCAS: Hahaha (Alitoa kicheko fulani cha kizushi na kisha kujitoa kifuani mwangu)


    Kilichofuata mahali hapo ni kwenda kwenye ule mghahawa uliokuwa katika jengo lililokuwa na internet ya Virus na KISHA Dorcas kumuita mhudumu.


    DORCAS: naomba Mirinda nyeusi pamoja na kababu. Msikilize na huyo mume wangu (Dorcas alimwambia mhudumu yule)
    MIMI: Naomba bia. Pombe kali yenye kilevi kuanzia 5%.
    DORCAS: Wewe Nyemo.
    MIMI: Naam.
    DORCAS: Wewe si umeokoka.
    MIMI: Najua.
    DORCAS: Pombe ya nini sasa?
    MIMI: Hahaha! Nilikuwa namzingua. Naomba uniletee juisi ya maembe pamoja na chipsi.
    MHUDUMU: Aweke kila kitu kwenye chipsi?
    MIMI: Yeah! Mwambie aweke kila kitu. Mpaka sumu.
    MHUDUMU na DORCAS: Hahahaha (Mhudumu akaondoka mahali hapo)


    Hiyo ndio tabia yangu, huo ndio muonekano wangu wa kila siku. Mara kwa mara ninaonekana kuwa mcheshi huku nikijaa utani bila kutambua kama hiyo ni siku ya kwanza kukutana nawe au la. Kila nilichokuwa nikikifanya mahali hapo ni kumruhusu Dorcas aendelee kujua kwamba sikuwa nimebadilika, nilikuwa Nyemo yule yule ambaye nilikuwa nikimfuatilia toka kitambo. Vinywaji na vyakula vikaletwa mahali pale na kisha kuanza kula.


    DORCAS: Naomba uniambie kuhusu mapenzi (Dorcas aliniambia huku akiniangalia)
    MIMI: Mapenzi ni kama kiti cha basi.
    DORCAS: Sipendi kusikia msemo huo.
    MIMI: Okey! Mapenzi ni kama maua.
    DORCAS: Bado sijaridhika.
    MIMI: Sasa unataka nikwambie mapenzi ni kama nini?
    DORCAS: Jaribu kutunga. Wewe si mtungaji.
    MIMI: Okey! Mapenzi ni kama darasa.
    DORCAS: Ndio kwanza nasikia kwako.
    MIMI: Si umeniambia nitunge?
    DORCAS: Yeah! Endelea.
    MIMI: Tufanye mapenzi ni darasa, wewe ni mwanafunzi. Mara kwa mara unapokwenda shule, unapenda kuliweka darasa katika hali ya usafi. Unapofunga shule au kumaliza, huwa unatamani sana kama ungerudi shuleni, si ndio hivyo?
    DORCAS: Ndio.
    MIMI: Sawa na mapenzi. Unapokuwa haupo kwenye mapenzi, huwa unatamani sana urudi tena katika mapenzi kama unavyotamani kurudi darasani unapomaliza shule.
    DORCAS: Kidogo naanza kukupata.
    MIMI: Unapopata nafasi ya kurudi darasani, unajisikia mwingi wa furaha kwa sababu unakutana na watu tofauti tofauti ambao ulikuwa umezoeana nao. Si ndio hivyo?
    DORCAS: Yeah!
    MIMI: Unapokuwa darasani unaongea na wenzako kwa furaha, mwalimu wa somo usilolipenda anapoingia, huwa unajisikiaje?
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    DORCAS: Vibaya.
    MIMI: Hao ndio vidudumtu kwenye mapenzi. Huwa mara kwa mara hawapendi wakuone kwenye furaha, unapojaribu kufanya hivi, wao watataka kufanya kile, utakapojaribu kufanya kile, wao watataka kufanya hiki. Waepuke sana watu hawa, huwa si wema sana, huwa ni wabaya ambao wanaweza kuharibu kila kitu. 
    DORCAS: Mmmh! Una maneno mengi sana Nyemo. Ila ulichosema kuhusu watu hao, ni cha ukweli kabisa.
    MIMI: nawajua sana. Ninaposema kwamba leo nataka kukaa na mpenzi wangu niyafurahie mapenzi, wao watakasirika tu huku wakihoji kwa nini nikae na mpenzi wangu. 
    DORCAS: Nimekuelewa. Hebu kwanza tuachane na hilo. Nikuulize swali?
    MIMI: Uliza.
    DORCAS: Unanipenda?
    MIMI: Sawa na kuulizia makofi polisi.
    DORCAS: hahaha!
    MIMI: Sawa na kuulizia ushungi Pemba.
    DORCAS: hahahah!
    MIMI: Ni sawa na kuulizia bunduki jeshini.
    DORCAS: hahaha! Acha kunichekesha Nyemo. Hebu nijibu kwanza.
    MIMI: kwani si tayari nishakujibu.
    DORCAS: bado.
    MIMI: Swali lako ni sawa na kuulizia mapenzi juu ya Dorcas moyoni mwa Nyemo. Nakupenda, nakupenda sana, nakupenda zaidi ya unavyofikiria, nakupenda zaidi ya unavyojipenda, ninakupenda zaidi ya marafiki zako wanavyokupenda.
    DORCAS: Huo umekuwa kama wimbo Nyemo. Sound nyingi.
    MIMI: Huu ni kama wimbo, naamini hilo. Kila siku umekuwa ukiambiwa kwamba unapendwa na watu wengi kiasi ambacho umeona kwamba neno ‘nakupenda’ kuwa kama wimbo masikioni mwako. Ila nataka kukwambia kitu kimoja. Neno hili limekuwa wimbo kwako, lakini leo huu wimbo umekuwa remix masikioni mwako.
    DORCAS: Unamaanisha nini?
    MIMI: Msanii anapotoa wimbo na kisha kutoa remix yake ina maana kwamba kuna vitu alikuwa amevisahau hakuviweka sasa anataka kuviweka katika remix yake. Hiyo ni sawa na mimi. Wengi wamekwambia kwamba wanakupenda ila kuna vitu hawajavisema kwako.
    DORCAS: kama vipi?
    MIMI: Kupendwa zaidi ya unavyojipenda. (Nilijibu, akatoa tabasamu ambalo likanifanya nimpende zaidi)


    Ukinisikiliza, nilikuwa naongea kiutani sana ila kumbuka kwamba ndio nilikuwa nazidi kupiga hatua zaidi na zaidi. Nilikwishamsoma Dorcas kwa kipindi kirefu sana, hakuwa msichana wa kumwendea sana siriasi, unamuwekea utani, unamchombeza kwa maneno haya, unamfurahisha hapa, unamchekesha kule. Hiyo ndio hatua ambayo nilikuwa nikiifanya kwani nilijua kwamba kama ningekuwa naongea huku nikiwa siriasi, kumpata kwangu ingekuwa ndoto ya mchana.
    DORCAS: maneno yako matamu sana, yanafanana na post zako unazoziandikaga kwa facebook.
    MIMI: Tabasamu lako zuri Dorcas, linafanana na maneo uliyoniandikia jana kwamba unanitakia ‘FURAHA YA SIKU YANGU YA KUZALIWA’.


    Siku hiyo ikaonekana kuwa siku ya furaha katika maisha yetu wote wawili, tulikula na kunywa huku tukipiga stori za kizushi mahali pale. Dorcas alionekana kuwa mwenye furaha kubwa sana kiasi ambacho hakutana nitoweke mbele yake. Tulitumia muda wa saa moja na nusu kukaa pale na ndipo tukahitaji kuondoka mahali hapo. Kwa mara ya kwanza, nikambusu Dorcas shavuni mwake jambo ambalo lilionekana kunifurahisha kupita kawaida. Ukurasa mpya wa mahusiano ya kimapenzi ulikuwa umefunguliwa mahali hapo.


    DORCAS: Usiniumize.
    MIMI: Nami natakiwa kukwambia maneno hayo hayo.
    DORCAS: Naijua facebook. Japo una marafiki mia moja na kadhaa lakini unaweza kupata marafiki wengi zaidi kutokana na uandishi wako. Kuwa makini na watoto wa kike.
    MIMI: Usijali Dorcas. Siwezi kufanya jambo lolote baya, hasa kukusaliti wewe (Nilimwambia huku nikitoa tabasamu pana ambalo lilimfanya kuniamini zaidi).


    Kiukweli tofauti na watu wengine, Dorcas sikutaka kumchezea na kumuacha, hapana, nilikuwa nikimaanisha mapenzi yale ambayo nilikuwa nimemwambia, hata kama ingewezekana, basi haikuwa budi kumuoa. Siku hiyo tukaongea mengi na hatimae kuagana. Sikutaka kuondoka nyumbani, nilichokifanya ni kumng’ang’ania kwenda naye huko alipokuwa akiishi, tukaenda na kupaona na ndipo nilipoondoka kuelekea nyumbani.


    MIMI: Nitakupenda mpaka nakufa (Nilijisemea ndani ya daladala katika kipindi naelekea nyumbani kana kwamba Dorcas alikuwa pembeni yangu)


    Mahusiano yale yaliendelea zaidi na zaidi, sikuachana na uandishi wa hadithi humu facebook, bado nilikuwa nikiendelea nao kama kawaida. Watu walinipenda, watu walipenda kusoma simulizi zangu ambazo nilikuwa nikiziandika katika staili ambayo ilikuwa ikinishangaza hata mimi mwenyewe. Nikazidi kupata marafiki zaidi mpaka ndani ya wiki moja kupata marafiki zaidi ya 500. Kazi ya uandishi ilikuwa ngumu sana lakini sikutaka kuiacha, bado nilikuwa nikiendelea nayo kama kawaida jambo ambalo lilikuwa likinipa marafiki wengi.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    JULIET: Unajua sana Nyemo. Nafurahi sana kila ninaposoma simulizi zako, yaani kama naangalia muvi Mlimani City.
    MIMI: Asante. Ila kawaida tu, namshukuru Mungu kwa hiki kipaji.
    JULIET: Yaani kama na mimi ningekuwa najua kuandika kama wewe, ningefurahi sana.
    MIMI: Tofauti na kipaji, wakati mwingine ukijifunza unaweza.
    JULIET: Sasa mimi nitajifunza wapi?
    MIMI: Kupitia hadithi nyingi. Jitahidi kusoma hadithi mbalimbali. Ukiona kwamba unataka kuandika hadithi kama za Nyemo, basi penda kusoma hadithi za Nyemo, ukiona kwamba unapenda kuandika hadithi kama za Sultan Tamba, pendelea sana kusoma hadithi zake.
    JULIET: Na kama nikisoma hadithi za wote?
    MIMI: Utachanganyikiwa. Katika maisha ya mwandishi, wengi hushindwa kuandika hadithi za aina tofauti. Mungu amegawa vipaji ila kavitofautisha tu.
    JULIET: Kivipi?
    MIMI: Kuna mwingine anaweza kuandika hadithi kuhusiana na mambo ambayo huwezi kuyafikiria kabisa, mfano ninavyoandika, huwezi kujua ni staili gani ninayotumia, naweza kukuandikia vitu ambavyo havipo katika jamii ya Kitanzania, huwa ninafurahi kuandika kuhusiana na mambo ya nje, huo ndio uandishi, nazunguka duniani kote. Ila katika hili, kuna mwingine anaweza kuandika hadithi ambayo inahusu jamii inayomzunguka tu, kutoka nje ya jamii inayomzunguka inakuwa ngumu sana kwani kuandika kuhusu jamii tofauti na hizi za Kiafrika, basi inabidi Mungu awe amkupa kitu kingine cha ziada sana.
    JULIET: Mmmh! Umetoa maelezo marefu sana.
    MIMI: Hiyo ni kwa sababu unataka kujifunza.
    JULIET: Na mbona hauandiki hadithi kuhusiana na jamii inayotuzunguka, hadithi zako nyingi zinakwenda nje ya Afrika?
    MIMI: Nilikwishawahi kuandika hadithi kama Maria, mwanzo mwisho ilizungumzia maisha halisi ya Mtanzania, ila baadae nikajuta.
    JULIET: Kwa nini?
    MIMI: Huwa sipendi kuziandika hadithi hizo humu Facebook japokuwa ninazo nyingi. Humu facebook, ngoja niwe naziandika hizi hizi za kwenda nje, zile zinazohusu jamii husika ya Mtanzania, ningependa kuzifanyia muvi na si kuzirusha hewani, ndio maana nafanya hivyo. Watu wabaya wanaweza kukopi na kupaste, ili kuwachanganya, acha niwaandikie mpaka za nje, kama wana uwezo, waigize huku wakisafiri kwenda nchi mbalimbali.
    JULIET: Hahaha! Mtoto mjanja wewe.
    MIMI: Kawaida tu.
    JULIET: Asante kwa muda wako.
    MIMI: usijali.


    Huyu msichana ndiye alikuwa wa kwanza kabisa ambaye alikileta kitu fulani moyoni mwangu, kitu ambacho kilionekana kuwa doa katika mahusiano yangu na Dorcas. Kwangu mimi, nilikuwa nachukulia kila kitu kuwa kawaida sana lakini kumbe mwenzangu alikuwa tofauti na mawazo yangu. Mawasiliano yangu na Juliet yalikuwa yakiendelea kama kawaida kwa njia ya inbox. Kitu ambacho kila siku alikuwa akikifanya ni kuniomba namba ya simu, sikuwa mwepesi, nilikuwa nikimyima sana ila kutokana na wadau wengi kunisumbua kwamba walikuwa wakitaka kunipongeza kupitia simuni, nikaiweka namba yangu hadharani jambo ambalo likaonekana kuwa kosa kubwa. Usumbufu ukaanza rasmi kutoka kwa Juliet,


    MIMI: Unasemaje?
    JULIET: Sauti yako nzuri. Naweweseka kila ninapoisikia.
    MIMI: Ok! Usijali. Kawaida tu.
    JULIET: Kwani yangu sio nzuri Nyemo?
    MIMI: Nzuri.
    JULIET: Hauweweseki?
    MIMI: Ndio...siweweseki
    JULIET: Naomba kitu kimoja kutoka kwako.
    MIMI: Kitu gani?
    JULIET: Naomba tuonane.
    MIMI: Haiwezekani. Nipo bize sana kwa sasa.
    JULIET: Hata kwa dakika kumi tu.
    MIMI: Hapana Juliet, nafikiri kuwasiliana simuni na facebook kunatosha.
    JULIET: Hapana bwana, nataka kumuona mtu ambaye kila siku anaufanya moyo wangu kufurahia. Naomba tuonane...nakuomba.
    MIMI: Haiwezekani. Sipo Dar, au uje huku mkoani Kagera ninapoishi (Nilidanganya)
    JULIET: Upo Kagera?
    MIMI: Ndio.
    JULIET: Mbona umeandika unaishi Dar?
    MIMI: Niliamua kuandika hivyo ili watu wengi waone nilikuwa nikiishi katika jiji hilo.
    JULIET: Nahisi unanidanganya.
    MIMI: Kweli tena. Sioni haja ya kukudanganya.
    JULIET: Sawa. Naweza kuja huko Kagera kesho kuonana nawe?
    MIMI: Kuja Kagera? Kesho? Mvua zinasumbua sana huku, barabara mbovu.
    JULIET: Usijali. Nitakuja na ndege.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Mmmh!
    JULIET: Nini tena?
    MIMI: Hakuna kitu. Usijali. Unaweza kuja.
    JULIET: Sawa. Nitakuja na ndege ya saa nne asubuhi. Ngoja nimwambie baba anikatie tiketi kabisa.
    MIMI: Poa. (Simu ikakatwa).


    Dizaini sikuwa sawa katika hali hiyo, nikaanza kujiuliza kuhusiana na Juliet, mpaka kufika hapo, kuna kitu ambacho nilikuwa nimekifikiria kwa kuona kwamba juliet alikuwa ametoka katika familia ambayo ilikuwa ikijiweza sana kuhusiana na mambo ya fedha. 


    Ila, sikutaka kuamini, nilikuwa naona kwamba msichana yule alikuwa muongo, nilitaka kuona kama kweli ingewezekana kusafiri mpaka Kagera kwa ajili ya kuniona. Usiku wa siku hiyo, niliiona post yake akiwa ameandika ‘Nakwenda Kagera kesho, nahitaji maombi yenu’. Nilishtuka sana, nikaona kwamba Juliet alikuwa akimaanisha kile ambacho alikuwa ameniambia, nilichokifanya, nikaLIKE na kisha kuendelea na mambo yangu.


    Kutokana na usiku uliopita kuchelewa kulala, asubuhi ya siku hiyo niliamshwa na mlio wa simu yangu ambayo ilikuwa ikiita, nikaamka na kisha kuangalia kioo cha simu ile, namba haikuwa imehifadhiwa simuni lakini kwa kuiangalia tu, nilikuwa nikiijua, ilikuwa ni namba ya Juliet. Huku nikionekana kuwa katika uchofu, nikabonyeza kitufe cha kijani na kisha kuipeleka sikioni.


    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    ****************************************
    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog