Search This Blog

Monday, October 24, 2022

FACEBOOK CHATTING - 1

 





    IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI


    *********************************************************************************


    Chombezo : Facebook Chatting

    Sehemu Ya Kwanza (1)


    MSICHANA: Mambo Nyemo.
    MIMI: Poa. Mzima?
    MSICHANA: Mzima wa afya. Unafanya nini?
    MIMI: Nachati na friends pamoja na kuangalia muvi kwa kuibia.
    MSICHANA: Hata mimi nachati pia. Muvi gani hiyo unayoangalia kwa kuibia?
    MIMI: Message in the Bottle.
    MSICHANA: Mmmh!
    MIMI: Mbona mguno tena?
    MSICHANA: Hiyo muvi mpya?
    MIMI: hapana. Toka mwaka 1999.
    MSICHANA: Na mimi nataka nije kuangalia. Nakaribishwa?
    MIMI: Duh! Poa. Karibu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MSICHANA: Hahahaha! Inaelekea u kijana mcheshi sana.
    MIMI: Kitu gani kimekufanya kuhisi hivyo?
    MSICHANA: Basi tu. Nimejirubuni kusema hivyo.
    MIMI: Yeah! Hivyo ndivyo nilivyo.
    MSICHANA: Unaishi wapi?
    MIMI: Tanzania.
    MSICHANA: Yeah! Najua. Ila sehemu gani?
    MIMI: Dar es Salaam.
    MSICHANA: Nafahamu. Ila Dar es Salaam kubwa sana.
    MIMI: Naishi Tandale. Unapajua?
    MSICHANA: Huwa ninapita tu na gari mara chache chache.
    MIMI: Okey. Thats gud then.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Ukimya unatawala kati yangu na yake kwa dakika kama tano hivi, mara nasikia kamlio ka meseji kanalia, ninapoangalia, naona ni yeye. Naifungua na kuisoma.


    MSICHANA: Samahani kwa kukaa kimya, nilikuwa nimekwenda kununua Chill souce dukani. Nimefurahi kuchati nawe kwa sasa. Nakwenda kupika mara moja. Tunaweza kuendelea kuchati baadae?
    MIMI: Usijali.
    MSICHANA: Utakuwa online?
    MIMI: Nafikiri kwa sababu sina pa kwenda.
    MSICHANA: Poa basi, baadae kidogo.
    MIMI: Poa.


    Baada ya hapo anakwenda offline. Sikuonekana kujali, sikujua kwa nini msichana huyu alikuwa ameonekana kuwa karibu sana na mimi kwa kipindi hiki kichache, nilikuwa na maswali mengi ya kumuuliza, nikawa navuta subira mpaka katika kipindi ambacho atarudi tena online. Nikawa na hamu kumuona akirudi online na kumuuliza baadhi ya maswali ambayo yalianza kuja kwa haraka sana kichwani.


    Nilikuwa na presha sana juu ya msichana huyu ambaye nilitoka kuchati muda uliopita. Niliporudi online, nikamkuta. Hata kabla sijamtumia meseji, akaniwahi.


    MSICHANA: Naona umerudi.
    MIMI: Yeah.
    MSICHANA: Nimekumiss.
    MIMI: (Kimya)
    MSICHANA: Mbona haujibu chochote jamani?
    MIMI: Sasa ulitaka nijibu vipi hapo?
    MSICHANA: Kwamba na wewe pia umenimiss.
    MIMI: Sasa kama sijakumiss jamani?
    MSICHANA: Dah! Aya yaishe. Nilikuwa online muda mrefu kidogo, nilikuwa nakusubiria tu. Nilikuwa nimekwishaboreka, bora umerudi.
    MIMI: Usijali. Nipo hapa kwa sasa.
    MSICHANA: Kuna swali lolote ungependa kuniuliza?
    MIMI: Yeah! Tena mengi tu.
    MSICHANA: Kama yapi?
    MIMI: Unaishi wapi?
    MSICHANA: Mbezi.
    MIMI: Unajua kama zimegawanyika sehemu mbili?
    MSICHANA: Yeah! Nipo ya huku Beach.
    MIMI: Ok! Unasoma au unafanya kazi?
    MSICHANA: Nasoma sekondari.
    MIMI: Wapi?
    MSICHANA: St' Mary.
    MIMI: Ok! Unaishi na nani?
    MSICHANA: Na wazazi wangu. Baba yangu mfanyabiashara na mama yangu ni mhasibu pale BoT.
    MIMI: Unasemaje?

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MSICHANA: Kwani haujanielewa jamani au unanifanyia makusudi tu.
    MIMI: Sawa. Nimekuelewa. Hivi ni kitu gani ambacho kimekupelekea kupenda kuchati nami na wakati ni jana tu ndio tulianza urafiki?
    MSICHANA: Kwa mara ya kwanza niliweza kukuona pale nilipoingizwa kwenye kundi lako la hadithi la SUSPENSE na rafiki yangu. Japokuwa sicomment wala kulike lakini nimependa sana hadithi zako. Huwa ninapenda sana kuzisoma huku nikiwa kitandani.
    MIMI: Sawa. Usijali.
    MSICHANA: Hivi itawezekana kuendelea kuchati hata kipindi ambacho hatupo online?
    MIMI: Kivipi? (Niliuliza japokuwa nilifahamu alimaanisha nini?)
    MSICHANA: Simuni.
    MIMI: Kwa hiyo unamaanisha unataka namba ya simu?
    MSICHANA: Ndio. Ila kama hautojali wangu.
    MIMI: Hapana. Hapa facebook kunatosha sana.
    MSICHANA: Ila ningependa kuisikia sauti yako wangu.
    MIMI: Usijali, tutaweza kutumia skype pale utakapohitaji kuisikia sauti yangu, tena hadi kuniona utaniona huko.
    MSICHANA: Jamaniiiii
    MIMI: Kweli tena.
    MSICHANA: Sawa.


    Ghafla akakaa kimya, sikutaka kuchelewa, nilichokifanya ni kuanza kupitia picha zake. Mungu wangu! Kwanza nikajuta kwa nini nilimnyima namba ya simu, alikuwa msichana mzuri sana ambaye kwa mwanaume lijali kama mimi basi asingekubali kumuacha.


    Mara nikaanza kupokea notification kwamba alikuwa akiLIKE picha zangu, yaani ilikuwa kama kero, kila wakati anaLIKE...analike.


    MSICHANA: Nimevutiwa na picha zako. Na nimevutiwa na wewe pia.


    Aliniambia maneno ambayo yalinichanganya.


    Kwa kiasi fulani nikauhisi moyo wangu kuingia katika hali fulani hivi, najua wale ambao waliwahi kuwasiliana na wasichana kwa zaidi ya dakika themanini watakuwa wamekwishawahi kukutana na hali hii. Alikuwa msichana ambaye alikuwa wazi na wala hakutaka kujificha chochote kile. Aliniona kumvutia sana.


    MIMI: Asante sana japokuwa najiona kuwa mtu wa kawaida sana.
    MSICHANA: Wa kawaida? Labda kwako mwenyewe. Hivi nikuulize swali la kizushi?
    MIMI: Uliza tu.
    MSICHANA: Una msichana?
    MIMI: Yeah! Ninao.
    MSICHANA: Unao?
    MIMI: Ndio.
    MSICHANA: Wangapi?
    MIMI: Wengi tu. 
    MSICHANA: Kama wangapi?
    MIMI: Ngoja kwanza. 1, 2, 3, 4. Kwa sasa ninao hao tu japokuwa wa 5 na wa 6 nipo kwenye process za mwisho.
    MSICHANA: Sawa. Hongera.
    MIMI: Asante.
    MSICHANA: (Kimyaaaaa)


    Kila wakati nilikuwa mtu wa kupenda sana utani pasipo kugundua kwamba wakati mwingine utani wangu unaweza kuniletea mambo mabaya. Nilikuwa nimeongea nae hayo yote kama sehemu ya utani, nikahisi tu kwamba alikuwa amekasirika japokuwa hakutaka kuongelea hilo. Hakunitumia meseji, alibaki kimya kwa muda wa dakika ishirini, nikashindwa kuvumilia, nikamtumia meseji.


    MIMI: Mbona kimya tena?
    MSICHANA: Nipo bize.
    MIMI: Bize? Ubize wa nini tena?
    MSICHANA: Hautakiwi kujua.
    MIMI: Ok.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Tayari nilikwishaona kwamba nimeharibu, nilichokifanya, nami nikajidai kukaa kimya, si unajua mwanaume hautakiwi kuonyesha udhaifu kirahisi namna hiyo. Nilikuwa nikiumia sana kukaa kimya japokuwa nilikuwa nikijikaza kisabuni sana. Nikamtumia meseji.


    MIMI: Nimechoka.
    MSICHANA: Eehh! Umechoka kufanya nini tena?
    MIMI: Kuwa...ok!
    MSICHANA: Kuwa muwazi bhana.
    MIMI: Nimechoka kuwa online. Nadhani natakiwa kusaign out mpaka wiki ipite ndio nirudi tena.
    MSICHANA: Kwa nini tena?
    MIMI: Sioni umuhimu wa kuwa online.
    MSICHANA: Kivipi?
    MIMI: Kwa sababu hautaki kuchati nami. Umekaa kimya sana
    MSICHANA:Napenda amani Nyemo. 
    MIMI: Nafahamu hilo. Ila unamaanisha nini?
    MSICHANA: Huwa sipendi kuchati na mtu mwenye wasichana wengi.
    MIMI: Hahaha! Nilikuwa nakuzingua bwana. Unadhani naweza kuwa na wanawake wote hao. Utani tu, naomba unizoee wangu.
    MSICHANA: Poa
    MIMI: Unafanya nini?
    MSICHANA: Nipo chumbani. Peke yangu huku kwa mbali wimbo wa Westlife ukisikika.
    MIMI: Wimbo gani?
    MSICHANA: As love as my witness. Unaujua.
    MIMI: Yeah.


    Akakaa kimya tena. Kwa wakati huo kidogo nikaanza kujisikia amani. Muda wote nikawa bize kusikilizia meseji yake, ghafla meseji ikaingia, meseji hii ilikuwa imeambatana na picha moja nzuri, alikuwa amepiga akiwa kitandani huku juu akiwa wazi na nguo yake ya ndani ndio ambayo ilikuwa mwilini mwake.


    MSICHANA: Umeionaje picha hiyo?
    MIMI: Mmmh
    MSICHANA; Kuna tatizo.
    MIMI: Hapana. Ila......una nyingine tena unitumie?
    MSICHANA: Subiri


    Akaanza kunitumia picha nyingi nyingi, picha zote zilikuwa zinanichanganya tu, nilikuwa nikiweweseka tu.


    MSICHANA: Na wewe nitumie zako.
    MIMI: Poa.


    Hapo ndipo nilipoanza kujipiga picha na simu yangu. Nilijipiga picha zaidi ya kumi huku na mimi nikiwa nimevaa boksa tu. Nilipomaliza, nikawasha bluetooth na kisha kuziweka kwenye kompyuta na kisha kumtumia.


    MSICHANA: Unavutia sana. Naomba tufanye kitu kimoja.
    MIMI: Kitu gani?
    MSICHANA: Nitumie namba ya simu, nataka tufanye kitu fulani usiku.
    MIMI: Kitu gani?
    MSICHANA: Mapenzi kupitia maongezi simuni.
    MIMI: Mmmh!
    MSICHANA: Mbona unaguna? Haujawahi kufanya hivyo?
    MIMI: Nimewahi. Tena zaidi ya mara ishirini tena ikiwa zaidi ya masaa sita simuni.
    MIMI: basi naomba tufanye hivyo.


    Hapo nikabaki kimya, nikaanza kujifikiria kama ilikuwa vizuri kumtumia namba ya simu au la. Alikuwa akitamani sana tufanye ngono simuni jambo ambalo nilijua lilikuwa na matatizo sana kisaikolojia. Hata kabla sijajua nifanye nini, meseji yake ikaingia, nikawa na shauku ya kuifungua. Nikaifungua haraka haraka.


    Nikaifungua ile meseji, kwa wakati huu meseji ile ilikuwa imekusanya maneno mazuri ya mapenzi. Nilikuwa nikiziangalia kwa kuzisoma moja baada ya nyingine. Hazikuwa meseji ngeni kwangu, nilikwishawahi kuziona mara kibao.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Unaonekana unapenda sana mahusiano ya kimapenzi pamoja nami?
    MSICHANA: Ndio. Nimetokea kuvutiwa nawe.
    MIMI: Hahaha! Unataka nianze kuwindwa na bunduki mitaani.
    MSICHANA: Kwa nini?
    MIMI: Mvulana wako.
    MSICHANA: Hahahahaha
    MIMI: Unacheka unaona mazuri?
    MSICHANA: Mbona unakuwa muoga hivyo? Yaani unamuogopa hadi mwanaume mwenzako
    MIMI: Si kwamba namuogopa, hapana, naogopa bunduki.
    MSICHANA: Hahahaha! Hapana bwana. Siko kwenye mahusiano, nilikuwa na mpenzi ila tumeachana.
    MIMI: Chanzo nini?
    MSICHANA: Alikuwa anadate na rafiki yangu mmoja hivi. 
    MIMI: Pole sana.
    MSICHANA: Asante sana. Vipi kuhusu wewe?


    Hapo nikabaki kimya kwa muda. Kichwa changu kilikuwa kikifikiri kwa haraka sana. Hii ilimaanisha kwamba kama ningemwambia nina msichana, kwanza angeumia halafu ndio ingekuwa mwisho wangu na
    yeye kuchati. Huku nikiwa najifikiria nini cha kujibu, meseji yake ikaingia.


    MSICHANA: Mbona kimya?
    MIMI: Unajua internet connection inazingua sana. Yaani mara ikate, mara irudi. Yaani tabu tupu.
    MSICHANA: Poleee. Naomba unijibu basi.
    MIMI: Ninae kwa sasa.
    MSICHANA: Unae?
    MIMI: Ndio. Ila hanionyeshei mapenzi ya dhati. Mara nyingi najitahidi kumtumia meseji, hanijibu, nikimpigia simu usiku, ipo bize tu. Tena si hivyo tu, hadi usiku wa manane ipo bize. Unahisi nini hapo?
    MSICHANA: Unaibiwa.
    MIMI: Kama naibiwa, nawe upo tayari kumuibia?
    MSICHANA: Una maana gani?
    MIMI: Hahahaha! Acha utani. Usitake nianze kutoa maana moja kwa moja hadi watu wa facebook washtukie.
    MSICHANA: Kama yeye mwizi, sina budi nami kuwa mwizi.
    MIMI: hauoni dhambi kuiba?
    MSICHANA: Kwenye mapenzi sidhani kama kuna dhambi kuiba. Anayeua kwa upanga nae atauawa kwa upanga.
    MIMI: Mmmhh! Sawa. Ila samahani kidogo. Kuna swali nataka kukuliza.
    MSICHANA: Kuwa huru 
    MIMI: Unaonekana kuwa msichana wa tofauti sana. Yaani sio aina ya msichana ambaye amekulia hapa.
    MSICHANA: Yeah! Nimeishi sana nchini Marekani ambako huko nilikaa kwa muda mrefu sana na ndipo nikalilia kuja Tanzania.
    MIMI: Mmmh!
    MSICHANA: Mbona unaguna tena?
    MIMI: Hakuna bhana. 
    MSICHANA: Vipi kuhusu namba ya simu.
    MIMI: Kwani unaitaka leo?
    MSICHANA: Ndio. Nataka tuongee leo kama nilivyokwambia.
    MIMI: Hivi unajua leo lini?
    MSICHANA: Jumatatu.
    MIMI: Hatutoweza kuongea kwa leo. Kesho inatakiwa niwe chuoni saa tatu.
    MSICHANA: Chuo gain?
    MIMI: Ninaposoma.
    MSICHANA: Kwa hiyo tutaongea lini?. Nina hamu sana ya kusikia sauti yako.
    MIMI: Labda Ijumaa.
    MSICHANA: Kuanzia saa ngapi?
    MIMI: Saa tano.
    MSICHANA: Ok! Kadri tunavyoendelea kuongea na ndivyo ambavyo ninazidi kufall inlove zaidi.
    MIMI: Hahahahaha
    MSICHANA: Unazicheka hisia zangu?
    MIMI: Hapana. Umekuwa mwepesi sana kufall inlove.
    MSICHANA: Yeah! Sijui kwa sababu gani.
    MIMI: Labda kwa sababu una hamu ya kuniumiza hapo baadae.
    MSICHANA: Haiwezekani kabisa. Labda wewe ndio uniumize.
    MIMI: Kwangu haitowezekana kabisa. Niamini.
    MSICHANA: Sawa. Ila naomba unipe namba ya simu ili niwe na amani.
    MIMI: Usijali. Nipe yako ili nikupigie.
    MSICHANA: Yangu ni 0719 878 ……
    MIMI: Poa.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Sikutaka kuchelewa, nilichokifanya ni kumpigia na kuanza kuongea kwa dakika chache na kisha kurudi tena kwenye meseji ndani ya mtandao wa Facebook. Sauti yake ilikuwa nzuri sana, yaani ilifanana na jinsi alivyokuwa. Mara nikashtukia meseji kutoka kwake ikiingia kwenye akaunti yangu ya facebook.


    MSICHANA: Mmmh! Una sauti nzuri mpenzi.
    MIMI: Hahaha! Acha kunizingua bhana. Mbona sauti yangu mbaya sana.
    MSICHANA: Nzuri, nimeipeda sana.
    MIMI: Asante. Hata yako nzuri pia. Ulikuwa muimba kwaya nini?
    MSICHANA: Yeah! Ila nilipokuwa nchini Marekani.
    MIMI: Basi ndio maana.
    MSICHANA: Naomba tuendelee kuchati baadae mpenzi. Mama amenipigia simu na kuniambia anataka twende Mlimani City kufanya shopping ya vyakula na mavazi.
    MIMI: Poa. Ila kama ukichelewa sana, unaweza kunikuta nimelala.
    MSICHANA: Usijali, nitawahi.
    MIMI: Ok.
    MSICHANA: Nakupenda mpenzi.
    MIMI: Nakupenda pia.


    Hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza kuanza mahusiano na msichana ambaye sikuwahi kukutana nae. Nikajiona kikizama kwenye mapenzi kwa asilimia mia moja, moyo wangu ukaonekana kumhitaji kupita kawaida. 


    MIMI: (Mawazoni: Dah! Nimeshachanganyikiwa sasa. Ngoja nilale then nichati nae hiyo usiku).


    Akili yangu ilikuwa imechoka sana na hivyo nilihitaji muda wa kulala. Nililala kuanzia saa kumi na moja jioni mpaka saa mbili usiku. Nilipoamka, nikaelekea kuoga, nikala na kisha kuwasha laptop. Nilipojiunga na mtandao wa facebook, msichana yule alikuwa miongoni mwa marafiki zangu waliokuwa online.


    MSICHANA: Waaaoooo! Karibu mpenzi.
    MIMI: Asante.
    MSICHANA: Nimekumiss mpenzi.
    MIMI: Nami pia baby. Kuna jipya?
    MSICHANA: Mengi tu.
    MIMI: Kama yapi?
    MSICHANA: Nilitaka kumwambia mama kuhusu wewe. Ameniona kuwa wa tofauti sana leo, muda wote alikuwa akiniona kuwa na furaha.
    MIMI: Naomba usifanye hivyo.
    MSICHANA: Kwa nini?
    MIMI: Muda bado wa kufanya hivyo.
    MSICHANA: Lakini ni kitu cha kawaida baby. Unafikiri atanigombeza? Wala hatoweza kufanya hivyo.
    MIMI: Najua ila naomba usifanye hivyo kwa sasa.
    MSICHANA: Sasa unataka nimwambie lini?
    MIMI: Siku yoyote ile lakini sio wiki hii.
    MSICHANA: Sawa. Ninauheshimu uamuzi wako.
    MIMI: Nashukuru kwa kunisikiliza mpenzi.
    MSICHANA: Kuna kitu nataka kufanya.
    MIMI: Kitu gani?
    MSICHANA: Nimemwambia rafiki yangu kuhusu wewe.
    MIMI: Rafiki yupi?
    MSICHANA: Rafiki yangu, Lydia.
    MIMI: Ndiye nani huyo?
    MSICHANA: Ninasoma nae shule. Amefurahia sana. Naweza kumuonganisha tuchati pamoja nae?
    MIMI: Kwani yupo online kwa sasa?
    MSICHANA: Ndio. Tena amenitumia meseji na kuniambia kuwa tuchati wote watatu.
    MIMI: Poa. Tengeneza kundi la watu watatu.
    MSICHANA: Sawa


    Nikabaki kimya, msichana huyu alionekana kuchanganyikiwa zaidi yangu, mapenzi yalikuwa yakionekana kumchanganya akili yake kupita kiasi. Kwa jinsi alivyokuwa na furaha, nilimuona kuwa na kiu ya kutaka kumfahamisha kila mtu kuhusu uhusiano wetu.


    MSICHANA: Tayari.
    MIMI: Mambo Lydia.
    LYDIA: Poa. Mzima shemeji
    MIMI: Mzima tu. Maisha yanasemaje?
    LYDIA: Safi tu. Mbona umemchanganya sana rafiki yangu?
    MIMI: Nimemchanganya au kajichanganya?
    MSICHANA: Umenichanganya.
    MIMI: Hapana bwana. Umejichanganya wewe mwenyewe.
    LYDIA: Kwa hiyo amejichanganya yeye mwenyewe?
    MIMI: Ndio. Au kama nimekosea sana, acha niseme kwamba mapenzi ndio yaliyomchanganya.
    LYDIA: Hahahaha
    MSICHANA: Sasa unacheka nini na wewe.
    LYDIA: Case closed. Wewe umeniambia amekuchanganya kumbe umejichanganya wewe mwenyewe. Hahahaha
    MSICHANA: Unacheka unaona mazuri Lydia? Nimejaribu kusoma lakini nashindwa kabisa, yaani kila nikijaribu, nakuwa sina hamu kabisa. Si unaona hata kukupigia simu nimeshindwa siku ya leo.
    LYDIA: Acha utoto wewe. Unajifunza kupenda nini?.
    MIMI: Ajifunze wapi huyo. Anaonekana mzoefu tu wa mapenzi.
    MSICHANA: Nani kakwambia kama mimi mzoefu? Au kwa sababu ya picha?
    LYDIA: Picha gani tena?
    MSICHANA: Hayakuhusu na wewe.
    LYDIA: Sasa kama hayanihusu kwa nini umeniambia niongee nae?
    MSICHANA: Nimekwambia uongee nae lakini si kumuuliza kuhusu picha. Hilo niachie mimi na Nyemo wangu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Mbona mnakuwa kama hamueleweki? Tatizo nini tena?.
    MSICHANA: Hakuna tatizo mpenzi. Naomba turudi kwenye chartin yetu kama kawaida. Achana na huyu Lydia.
    MIMI: Mbona umebadilika ghafla mpenzi?
    MSICHANA: Kawaida tu.
    LYDIA: Ok! Usikasirike rafiki yangu. Nyemo naomba unitumie friend request.
    MSICHANA: Hapana. Sitaki. Usimtumie mpenzi.
    MIMI: Kwa nini?
    MSICHANA: Basi tu.
    LYDIA: Acha wivu shosti. Haujiamini?
    MSICHANA: Najiamini ila naogopa udhaifu wa mwanaume.
    MIMI: Hahahaha
    MSICHANA: Unacheka kwani uongo? Nyie wadhaifu sana. Huyu Lydia anaweza akaleta matatizo katika mahusiano yetu. Mahusiano yenyewe bado machanga sana.
    MIMI: Aya. Umeshinda wewe mpenzi. Kama vipi usiku mwema Lydia, naona dogo ameshakasirika bhana.
    MSICHANA: Nani dogo?
    MIMI: Wewe. Kwani unajiona mkubwa? Bado mdogo.
    MSICHANA: Sawa. Wewe si mkubwa! Usiku mwema Lydia.
    LYIDA: Nanyi pia.


    Mawasiliano ya watu watatu yakakatika muda huo, kundi la kuchati la watu watatu likafutwa na kurudi katika mawasiliano ya kawaida. Kuna hali nikaanza kuigundua, msichana huyu alikuwa akionekana kuwa na wivu sana, alitaka mimi niwe wake kama wake tena peke yake, hakutaka mtu yeyote amuingilie kwenye mapenzi yake. Tukaanza kuchati kama kawaida yetu.


    MSICHANA: Unataka niibiwe mali yangu.
    MIMI: Hahahaha! Wasiwasi wako tu. Mwizi hawezi kukuibia kama sijampa nafasi ya kukuibia.
    MSICHANA: Sawa bwana.
    MSICHANA: Naomba kitu kimoja mpenzi.
    MIMI: Kitu gani?
    MSICHANA: Nimeshindwa kuvumilia kabisa.
    MIMI: Kuvumilia nini?
    MSICHANA: Nimeshndwa tu. Naomba tufanye mapenzi kwa njia ya simu.
    MIMI: Mbona unakuwa na haraka hivyo?
    MSICHANA: Ndio maana nimesema naomba. Naomba unisaidie katika hilo mpenzi. Pleaaseee
    MIMI: Sawa. 
    MSICHANA: Nashukuru kwa kunisikiliza.
    MIMI: Usijali. Ila mchezo huu una sheria zake ili uchangamke.
    MSICHANA: Sheria gani?
    MIMI: Moja, Utatakiwa kufanya kila kitu nitakachokwambia. Usipofanya tu, umeharibu mchezo.
    MSICHANA: Nitafanya.
    MIMI: Mbili, Unatakiwa kunipa nafasi mwilini mwako. Wewe kuwa kila sehemu ya mwili wako, ila mikono yako acha niwe mimi.
    MSICHANA: Sawa. Hakuna tatizo.
    MIMI: Simu yako inatumia hearphone?
    MSICHANA: Ndio.
    MIMI: Basi kwa leo tumia hizo.
    MSICHANA: Sawa. Kuna kingine mpenzi?
    MIMI: Ndio. Nitumie namba yako ya vodacom. Nataka tutumie mtandao huo leo. Tigo network yao inazingua sana, wanaweza kutukatisha mara kwa mara.
    MSICHANA: Sawa.


    Wala hakutaka kuchelewa, hapo hapo akanitumia namba yake ya Vodacom japokuwa alikuwa akitaka yeye kunipigia. Muda ulizidi kwenda, msichana yule alionekana kuwa na kiu kubwa ya kufanya mapenzi kwa kutumia njia ya simu. Kila wakati alikuwa akiniambia wazi kwamba muda ulikuwa hauendi kabisa. Ilipofika saa tano, nikampigia kwa kutumia laini ya Vodacom, akakata simu na kisha kunipigia. Hakujua kama mimi ndiye nilikuwa mkali wa kufanya mapenzi kwa njia ya simu. Nilikuwa nikiufahamu sana mchezo ule ambao ulikuwa unachezwa sana na vijana kama sisi ambao tulikuwa tumekulia uswahilini, hasa huku Tandale.


    MIMI: Upo tayari?
    MSICHANA: Ndio.
    MIMI: Uko peke yako chumbani?
    MSICHANA: Ndio.
    MIMI: Unaikumbuka sheria yetu ya kwanza?
    MSICHANA: Ndio.
    MIMI: Ilikuwa inasemaje?
    MSICHANA: Nifanye kila utakachoniambia.
    MIMI: Safi sana. Naomba uzime taa.
    v
    Nikaanza kumsikia akiinuka kitandani, baada ya muda, nikaisikia switch ikilia kuona kwamba tayari alikuwa amezima taa ya chumbani kwake na kisha kurudi kitandani.


    MIMI: Umevaa nini hapo?
    MSICHANA: Nguo ya kulalia pamoja na nguo ya ndani.
    MIMI: Naomba ubaki na nguo moja tu. Hautakiwi kuwa na nguo ya ndani.
    MSICHANA: Mmmh!
    MIMI: Unaguna nini sasa? Wewe si ndio umeomba tucheze huu mchezo.
    MSICHANA: Sawa.
    MIMI: Umeshawahi kucheza mchezo huu?
    MSICHANA: Ndio. Ila haukuwa na masharti hayo.
    MIMI: Hahahaha! Huyo uliyecheza nae alikuwa mgeni na mshamba tu. Leo umefika kwangu, mtoto wa uswahilini ambaye nina ujuzi wote wa kuucheza mchezo huo. Unakumbuka sheria yetu ya kwanza?
    MSICHANA: ndio.
    MIMI: Fanya hivyo basi.


    Akabaki kimya kwa muda. Nikasikia kama akiwa anainuka kitandani na baada ya muda, tukaendelea.


    MSICHANA: Tayari.
    MIMI: Safi sana. Itegeshe mike ya Hearphone yako karibu na mdomo. Ipe mikono yako uhuru. Wakati mwingine, unaweza kufumba macho. Itulize akili yako kabisa, achana na kufikiri mambo mengine. Isikilize sauti yangu kwa makini, nitakwenda kuongea maneno mengi, yanayotakiwa kufanya na wewe, fanya kama nitakavyokwambia. Hakikisha umelala chali. Umesikia mpenzi.
    MSICHANA: (Huku sauti yake ikianza kubadilika na kuwa ya chini) Sawa.
    MIMI: Tunakwenda kuanza mchezo huu. Mchezo huu utaanzia mwilini mwako, nitakwenda kuitembelea kila sehemu yako ya mwili. Kumbuka kwamba mikono yako ndio mimi kwa sasa. Hakuna maswali, tulia na niache nifanye kazi yangu.
    MSICHANA: Sawa mpenzi.
    MIMI: Tunakwenda kuanza mchezo wetu. Tunaanzia kifuani kushuka chini.
    MSICHANA; Sawa.


    Kuanzia hapo, mchezo ulivyochezwa hautoweza kuelezwa sana kwa sababu ya matumizi ya facebook kutumiwa hadi na watoto walio chini ya miaka 18. Usiulize maswali wala usibishe. Kuna watoto wengi huku mtaani kwetu ambao ni marafiki zangu na wote wanaisoma post hii. Sitoelezea sana mchezo huu kwani sitotaka kuiharibu saikolojia yao, ufahamu nilio nao kwenye mchezo huu acha ubaki kuwa wangu tu, sitaki kuibiwa maujuzi kabisa. Kila mtu anatakiwa kuucheza mchezo huu kwa kutumia ujuzi wake na si kuiba ujuzi kutoka kwangu kwani unaweza kumuua hata binti wa watu na kuniletea matatizo.


    NB: Watoto wengi, sehemu hiyo inakatishwa kidogo na wala haitoelezewa kwa kina.


    Mchezo uliendelea zaidi na zaidi, kila wakati nilikuwa namsikia akipumua kwa nguvu huku akilalamikalalamika. Bado nilikuwa nikiendelea kama kawaida. Dakika kumi zikapita, niliendelea kuongea nae, dakika ishirini zikapita, nusu saa na hadi saa moja, bado alikuwa akilalamikalalamika tu.


    MSICHANA: Stooooooooooopppppp (Aliitoa sauti yake kimahaba)
    MIMI: Nini tena?
    MSICHANA: Stooooooopppp mpenzi. Aaaaggggghhhhh! Naomba nipumzike.
    MIMI: Mbona unaomba kupumzika tena na wakati bado masaa kama matatu hivi?
    MSICHANA: Utaniua. Nimeshindwa kujizuia mpenzi.
    MIMI: Poleeeee
    MSICHANA: Asante. Ngoja nikaoge kwanza.
    MIMI: Vipi tena?
    MSICHANA: Umenichafua.
    MIMI: Hahahaha! Nimekuchafua au umejichafua?
    MSICHANA: Umenichafua. Haukumbuki ulisema uwe mikono yangu?
    MIMI: Ok! Nimekuelewa. Ukitoka huko naomba ulale. Mimi mwenyewe nimejichafua pia. Nakwenda kuoga, sitokuwa na nguvu ya kuendelea. Acha nilale kwanza mpaka kesho. Usiku mwema.
    MSICHANA: Nawe mpia mpenzi (Bado sauti yake ilikuwa ikisikika kimahaba)


    Nikabaki nikicheka sana, sikuamini kama msichana yule hakutaka kuendelea kuucheza mchezo ule na wakati ndio kwanza tulikuwa tumetumia dakika sitini tu. Nikaenda kuoga na kisha kurudi kitandani. Sikutaka kuwasha simu yangu kwani nilijua kwa namna moja au nyingine angenitafuta tu.
    Kesho, nikaanza kuelekea chuoni. Akili yangu nikaituliza huku ikionekana kama kutokukumbuka kitu chote kilichotokea. Saa tano na nusu nikawasha simu yangu na kukutana na meseji zake tano.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MSICHANA: *Usiku wa jana umekuwa usiku wa kukumbuka sana kwangu.
    *Nilikuwa nikilalamika mpaka mama akasikia na kuamua kuja chumbani kwangu. Sijui amejua nilichokuwa nimekifanya kwani asubuhi alikuwa akiniangalia kwa jicho la wasiwasi sana.
    * Kama mchezo wenyewe upo vile, sijui itakuwaje. Unaonekana kuwa mchezo mzuri lakini uliojaa hatari.
    * Ingawa niliwahi kuucheza mchezo ule lakini jana ilikuwa balaa. Yaani kama ni mpira basi nimekutana na timu inayokimbiza muda wote.
    * Mbona upo kimya mpenzi? Naomba ukizipokea meseji hizi nijibu chochote ili niwe na furaha. Leo sijaenda shule kabisa kwa kuogopa kutokuelewa darasani. Nimesingizia naumwa. Yote kwa ajili yako. Nakupenda mpenzi. Nakupenda My Only Nyemo.


    Nilibaki nikicheka sana. Msichana ambaye ilikuwa imepita siku moja tu tangu tuanze uhusiano wa kimapenzi alikuwa amechanganyikiwa sana. Mahusiano yetu yakawa yamechangamka sana kana kwamba yalikuwa yameanza miezi sita iliyopita. 


    MIMI: Usijali mpenzi. Mchezo ule unahitaji sana maandalizi. Wengi wanashindwa kuucheza kwa sababu tu huwa wanakurupuka. Mimi kama mimi huwa ninakwenda hatua kwa hatua mpaka mwisho. Najiamini, ninafanya kazi zangu kwa uhakika mpenzi.
    MSICHANA: Una tabia mbaya sana. Mbona haukunijibu toka asubuhi nilipokutumia meseji zile?
    MIMI: Nilikuwa darasani baby. Hadi hapa bado nipo darasani.
    MSICHANA: Umejifunza wapi mchezo ule?
    MIMI: Nyumbani.
    MSICHANA: Mmmh! Una hatari wewe!
    MIMI: Hatari ya nini tena?
    MSICHANA: Ungeweza kuniua last night. Yaani kuna kipindi nilikuwa naona viungo vyote vikiishiwa nguvu.
    MIMI: Poleeeee
    MSICHANA: Asante mpenzi.
    MIMI: Naomba leo tucheze tena.
    MSICHANA: Sitaki. Sitaki tena kucheza, utaniua jamani. Jana nilikuwa nahema juu juu kama nakata roho vile.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    MIMI: Polee sana. Ila ndio ukubwa huo.
    MSICHANA: Au ulitaka kunitoa usichana wangu?
    MIMI: Kwani unao?
    MSICHANA: Ndio
    MIMI: Mmmh! Kweli hatari. Unanishangaza sana.
    MSICHANA: Kwa nini?
    MIMI: Ulidumu na mpenzi wako kwa muda gani?
    MSICHANA: Kwa miaka miwili.
    MIMI: Hamkufanya kitu chochote kile?
    MSICHANA: Ndio.
    MIMI: Alikuwa na chembechembe za ushoga nini?
    MSICHANA: Hahahaha! Kwa nini unasema hivyo?
    MIMI: Inawezekana. Miaka miwili halafu kimya. Haiwezekani, kuna jambo hapo nyuma ya pazia.
    MSICHANA: Inawezekana. 
    MIMI: Hivi una miaka mingapi?
    MSICHANA: Kumi na nane.
    MIMI: Hahahaha! Unafaa kuliwa wewe. Umeshaiva mpenzi. Inabidi nikutungue kutoka mtini. Umeiva vizuri kabisa.
    MSICHANA: Hahahaha! Una maneno wewe
    MIMI: Hayo ndio maneno tunayopenda kuyatumia huku kwetu. Miaka kumi na nane mkubwa sana, tena sana. Kama ungekuwa huku kwetu ungekuwa unatafutiwa mume.
    MSICHANA: Ningekuwa natafutiwa mume?
    MIMI: Ndio. Tungekuwa tunakula pilau sasa hivi.
    MSICHANA: Hahahaha! Sawa bwana. Ila inakubidi uwe na shabaha ya kulitungua tunda lililoiva.
    MIMI: Shabaha ninayo tena kubwa sana. Nikiona kama nakukosa, nitakupandia uko uko mtini. Hahahaha!
    MSICHANA: Una visa sana Mpenzi.
    MIMI: Usijali. Lecturer anaingia. Kama vipi tutaendelea kuchati baadae.
    MSICHANA: Poa. Nakupenda mpenzi.
    MIMI: Nakupenda pia.


    Msichana yule alionekana kuwa msumbufu sana, muda wote alikuwa akinitumia meseji za mapenzi lakini sikumjibu hata moja, muda wote nilikuwa nikimfuatilia lecturer alivyokuwa akifundisha. Muda wa kutoka ulipofika, sikutaka kumshtua, nikarudi nyumbani na kujilaza kitandani.


    MIMI: Nipo nyumbani.
    MSICHANA: Namshukuru Mungu umerudi nyumbani salama. Kuna kitu nilikuwa nakifikiria mpenzi.
    MIMI: Kitu gani?
    MSICHANA: Unaonaje tukionana somewhere?
    MIMI: Lini?
    MSICHANA: kesho.
    MIMI: Haitowezekana kabisa.
    MSICHANA: Kwa nini mpenzi?
    MIMI: Labda tufanye weekend.
    MSICHANA: Okey! Ila naomba tuonane mpenzi.
    MIMI: Usijali.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Baada ya hapo, mawasiliano yalikuwa yakiendelea kila siku, alitamani sana kuonana nami lakini nilikuwa bize sana mpaka pale ilipofika weekeend ambapo tulipanga sehemu ya kukutania.


    MIMI: Umesema wapi?
    MSICHANA: Slipway.
    MIMI: Du! Sipajui bwana.
    MSICHANA: Acha kunitania mpenzi. Ila usijali, nitakuelekeza.
    MIMI: Poa.


    Baada ya hapo akaanza kunielekeza. Si kwamba nilikuwa sipajui kweli Slipway ila kwa wakati huu nilikuwa nikitaka kucheza na akili yake tu. Nilitaka afahamu kwamba mimi nilikuwa mtoto wa uswahilini na hata sehemu nyingi za kuenjoy hasa za watu waliokuwa na uwezo fulani nilikuwa sina uhitaji wa kupafahamu.
    Nikafikiria kwa haraka haraka, sehemu ile ilikuwa haiendeki kwa daladala hivyo kama ningependa daladala ya Msasani na kwenda huko, ungekuwa mwendo mrefu kidogo. Sikuonekana kujali, kukutana na msichana wangu ndicho kitu pekee ambacho nilikuwa nikikihitaji.
    Asubuhi ya Jumamosi tukaanza kuchati kwa sms hata kabla hatujaonana.


    MSICHANA: Ndio najiandaa mpenzi. Unataka nivae mavazi gani?
    MIMI: Vyovyote tu. Ila sipendelei kukuona ukivaa suruali.
    MSICHANA: Kwa nini?
    MIMI: Sina sababu.
    MSICHANA: Basi usijali. Nitavaa gauni moja zuri sana ambazlo nilinunuliwa na baba katika moja ya maduka makubwa jijini New York. Nitakuja nalo huko.
    MIMI: Poa. Wewe njoo tu mpenzi.
    MSICHANA: Ili uwahi, naomba ufanye kitu kimoja.
    MIMI: Kipi?
    MSICHANA: Kodi bajaji na hela nitalipia mimi huku.
    MIMI: Poa. Ila usiniingize choo cha kike.
    MSICHANA: Usijali mpenzi.


    Nikaanza kujiandaa kwa haraka sana, japokuwa toka nizaliwe sikuwahi kufika mapema sehemu ya appointment ila siku hiyo nilitaka kufika mapema sana. Nilipomaliza kujiandaa, nikaanza kwenda kwenye maegesho ya madereva wa mabajaji ambako nikamuita rafiki yangu ambaye alikuwa akiendesha bajaji moja.


    MIMI: Sikiliza Moody, nataka unipeleke Slipway. Kiasi gani?
    MOODY: Du! Unakwenda kufanya nini tena?
    MIMI: Achana na hayo. Kiasi gani?
    MOODY: Elfu kumi.
    MIMI: Poa. Ila naomba tufanye kitu kimoja.
    MOODY: Kitu gani?
    MIMI: Tukifika kule, sema gharama ni shilingi elfu ishirini na tano. Umesikia?
    MOODY: Poa. Kwani kuna mtu anakulipia?
    MIMI: Yeah! Mtoto fulani wa kishua.
    MOODY: Poa jembe. Ingia twende.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Nikaingia ndani ya bajaji na safari ya kuelekea Slipway kuanza. Ndani ya bajaji bado nilikuwa nikiendelea kuchati nae huku akiniambia kwamba amekwishafika na ni mimi tu ndiye nilikuwa nikisubiriwa. 


    MIMI: Sasa hiyo elfu ishirini na tano, yako elfu kumi na yangu elfu kumi na tano. Nitaifuata baadae nikitoka kuonana nae. Umenielewa?
    MOODY: Du! Yaani hata hauniongezi kwa mchongo ninaoucheza?
    MIMI: Nikuongeze nini hapo? Kwanza bei yenyewe tu umenibamiza. Halafu kama ningetaka si ningechukua daladala kwa nauli ya shilingi mia tatu na ningefika Msasani ningepiga kwa mguu mpaka Slipway.
    MOODY: Dah! Poa bwana. Mara ya kwanza nilitaka kushangaa eti unakodi bajaji. Mtoto wa uswahilini akodi bajaji!
    MIMI: Ndio hivyo bwana. Yaani hapa najiona kupata zali sana.


    Safari ilikuwa ikiendelea zaidi na zaidi mpaka tulipofika Slipway. Gari nzuri na ya kifahari ilikuwa imepaki nje. Mara msichana yule akateremka. Nikajikuta nikianza kutetemeka kupita kawaida, sikuamini, sikuamini kama duniani kulikuwa na msichana mzuri namna ile. Nilibaki kimya nikimwangalia kwa mshangao. SI mimi tu, hata Moody alikuwa akionekana kushangaa. Uzuri wa msichana yule ulinishtua kupita kawaida.


    MSICHANA: Vipi mpenzi?
    MIMI: Poa
    MSICHANA: Ngoja nimlipe dereva.


    Akaanza kuisogeea bajaji na kisha kumlipa Moody gharama zake. Sikutaka kuzubaa, nami nikaelekea pale pale kuona anamlipa kiasi gani ili baadae Moody asije akanigeuka. Nikaona wekundu wawili na elfu tano wakitoka kwenye pochi yake, nikaona kwa ushahidi ule Moody asingeweza kunizika.
    Tukatoka hapo na kuelekea ndani. Ingawa mule ndani kulikuwa na warembo wengi lakini mbele ya msichana yule wote walionekana kuwa si kitu. Tukatafuta sehemu na kukaa. Vinywaji na chakula vikaagizwa na kuanza kula.


    MSICHANA: Tukitoka hapa nataka twende tukapumzike kwenye chumba chochote kile.
    MIMI: Sawa. Ila jina lako hasa ni nani manake naona kwenye facebook unatumia jina la Precious Angel.
    MSICHANA: Naitwa Angeline.
    MIMI: Ok! 


    Tukala na kuanza kwenda katika sehemu iliyokuwa na vyumba na kuchukua chumba kimoja. Tulipoingia ndani, akaanza kuvua nguo zake na mimi kuvua zangu. Akajilaza kitandani huku akiniangalia kwa macho ya kurembua. Nami sikutaka kuchelewa, ninaanza kumsogelea. Nikaanza kumwangalia usoni.


    GIDEON: Nyemo....Nyemo...Nyemo...amka.


    Ilikuwa ni sauti ya kaka yangu ambayo ilikuwa ikisikika kwa mbali huku akiugonga mlango wa chumbani kwangu. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo nilivyozidi kuisikia sauti ile. Ghafla nikaamka kutoka usingizini. Mungu wangu! Kumbe matukio yote yale ambayo yalikuwa yakiendelea ilikuwa ni ndoto. Nikaamka, nikabaki kimya kitandani, sikuamini.


    MIMI: Ndoto! Mungu wangu! Kumbe ilikuwa ndoto! Damn!


    Nikasimama na kwenda kuufungua mlango wa chumbani kwangu, kaka yangu, Gideon alikuwa amesimama mlangoni. Nilikuwa nimechukia kupita kawaida.


    GIDEON: Rafiki yako amekuja kukuulizia.
    MIMI: Nani?
    GIDEON: Andrew Carlos
    MIMI: Aaaggghhh! Kwa nini usingengoja hata kwa dakika moja.
    GIDEON: Kuna nini?
    MIMI: Dah! Nilikuwa chumbani. Tena kila kitu kikiwa kwenye hatua ya mwisho kaka.
    GIDEON: Mbona sikuelewi.
    MIMI: Naomba modem yangu kwanza.


    Gideon akanipa modem yangu na kisha kuanza kurudi chumbani. Nikachukua laptop ambayo ilikuwa juu ya dressing table, nikaiwasha na kisha kuchomeka modem ile, nikaoganisha na internet na kufungua mtandao wa Facebook.


    MIMI: Anaitwa Angeline.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Nikaanza kuwaangalia marafiki zangu wote huku nikimtafuta huyo msichana mwenye jina la Angeline. Sikuwa na rafiki huyo kabisa kitu kilichonipelekea kuanza kulitafuta. Majina yote yalikuja lakini hakukuwa na msichana yule, sura zao zilionekana kuwa tofauti kabisa na msichana yule mrembo. Sikutaka kuishia hapo, nikaanza kwenda kwenye akaunti zangu zote, twitter, myspace, beareshare, yahoo messenger lakini kote huko hakukuwa na msichana huyo.


    MIMI: Mungu wangu! Kumbe alikuwa msichana wa ndoto! Kumbe nilikuwa nikiota. Ndoto....Ndoto! Kumbe ilikuwa ni ndoto! Nazichukia ndoto.


    Nilijisemea huku nikionekana kukata tamaa. Sura ya msichana huyo bado itaendelea kubaki katika akili yangu, alikuwa ni msichana mzuri ambaye kila ninapowaangalia wasichana wote, hakukuwa na msichana ambaye alikuwa mzuri kama yeye. Miaka miwili imepita tangu niote ndoto hiyo lakini kamwe sura ya msichana huyo haikuweza kuondoka kichwani mwangu, nilikuwa namkumbuka kwa kila kitu. Nimejaribu kwa muda mrefu sana kumtafuta kwenye mtandao wa facebook lakini wala sijafanikiwa kumuona. Angeline....Angeline ataendelea kubaki kwenye akili yangu, nitaendelea kumkumbuka kila siku.


    MWISHO WA SEASON 1


    Unaikumbuka ile Season One niliyoandika kuhusiana mimi na msichana yule wa kishua? Leo hii nakuja na Season two ambayo itakuwa kali zaidi ya ile season one iliyopita. TWENDE PAMOJA.




    Najisikia nimechoka sana huku laptop ikiwa mapajani mwangu na nimeunganisha na internet nikicheki updates za facebook, macho yangu yanakuwa mazito, natamani kulala lakini ghafla naliona jina, jina zuri la msichana mmoja hivi, jina la msichana ambaye nilikuwa namtaka kila siku toka kipindi kile alichokuwa akikaa mtaani kwetu. Ghafla uchovu wote ukanitoka, naanza kumwangalia, ndiye yeye, ndiye yeye kabisa kwani nilikuwa nimemtumia friend request jana tu, leo kanikubali kuwa rafiki yake, halafu yupo online.


    Kwanza nasita kumpa hi, hii ni kwa sababu katika kipindi ambacho alikuwa akiishi mtaani kwetu, alikuwa akiringa sana kutokana na urembo wake, nilikuwa nimemtaka mahusiano ya kimapenzi zaidi ya mara saba, zote alinipiga mbavuni. Leo hii, huyu msichana Dorcas kanikubalia urafiki, lazima nianze upya mpaka anikubalie bila kujua mimi ndiye yule yule ambaye alikuwa akinikataa sana. Kwa kuwa katika kipindi hicho nilikuwa ninatumia a.k.a ya jina langu kama BROTHER PRINCE, hakuweza kunitambua. Ninamfuata na kumpa hi


    MIMI: Mambo mrembo! (Nilimsalimia kwa kujiamini)
    DORCAS: Poa. Mzima Brother?
    MIMI: Nipo poa sana. Asante sana.
    DORCAS: Asante ya nini tena? (Aliuliza huku nikiona kabisa swali lake dizaini kama lilikuja na tabasamu pana)
    MIMI: Kwa kunikubalia urafiki. Nimefurahi sana.
    DORCAS: Usijali Brother.


    Kwanza hapo nikakaa kimya, sikujua ilitakiwa niendelee vipi na mawasiliano naye, kwa dakika kadhaa, vidole vyangu vikabaki kwenye keyboard ya laptop bila kuandika chochote kile. Kuna kitu nikatokea kukikumbuka, nikaona ngoja kwanza niende kuangalia picha zake. 
    Asikwambie mtu, alikuwa Dorcas yule yule, msichana ambaye alinifanya niwe kama chizi mtaani kwetu, msichana ambaye alinifanya niumwe na mbu sana vichochoroni, msichana ambaye alinifanya niwe namsubiria sana kumsindikiza shuleni kwao huku nikiwa radhi nichelewe shuleni kwetu.


    MIMI: Dorcas......! (Niliita kwa mwandiko wa kioga)
    DORCAS (Baada ya dakika mbili): Abeeee.
    MIMI: Upo bize sana?
    DORCAS: Sio sana. Ila kwa nini umeuliza hivyo?
    MIMI: Nimeona nimekuandikia meseji halafu unanijibu baada ya dakika mbili kupita. Kweli haki hii jamani?
    DORCAS:Samahani. Unajua ninachati na watu wengi ndio maana.
    MIMI: Au kwa sababu mimi ni mgeni kwako?
    DORCAS: Hapana jamaniiiii. Nisamehe basi.
    MIMI: Usijali. Naweza kukuuliza swali moja la kizushi?
    DORCAS: Swali gani?
    MIMI: Lakini haujanijibu.
    DORCAS: Sawa. Uliza.
    MIMI: Unaishi wapi?

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    DORCAS: Jamani ndio swali gani tena hilo. Si kila kitu nimeandika kwenye profile langu uangalie.
    MIMI: Ninatamani sana kufanya hivyo. Mtu anapouliza swali hili si kwamba siwezi kuangalia, hapana. Internet zetu kwa sisi tunaotumia simu huwa hazina kasi kabisa na ndio maana nimeona bora nikuulize tu.
    DORCAS: Kwa hiyo hapo unatumia simu?
    MIMI: Yeah! (Nilidanganya)
    DORCAS: Mmmh!
    MIMI: Mbona unaguna?
    DORCAS:Nakuona online.
    MIMI: Hilo si tatizo. Natumia Opera Min mpya. Naomba unijibu.
    DORCAS: Naishi Magomeni.
    MIMI: Ila si unafahamu kama ni kubwa sana.
    DORCAS: Nipo Mapipa.
    MIMI: Sawa. Nashukuru kwa kukufahamu. Naomba tuwe tunachati kila tunapokutana online.
    DORCAS: Usijali. Karibu sana.
    MIMI: Poa.
    DORCAS: Na wewe unaishi wapi?
    MIMI: Naishi Manzese Midizini (Nilidanganya kwani ningesema kweli, angehisi kitu).
    DORCAS: Owkey. Unasoma?
    MIMI: Nimekwishamaliza kidato cha sita (Nilidanganya tena)
    DORCAS: Shule gani?”
    MIMI: Makongo.
    DORCAS: Hongera.
    MIMI: Asante. Wewe unasoma?
    DORCAS: Nasoma kidato cha tano ila mwezi wa pili mwishoni naingia kidato cha sita.
    MIMI: Nawe hongera sana.
    DORCAS: Asante. Naomba nikuulize swali jingine.
    MIMI: Uliza tu.
    DORCAS: Mbona haujaweka picha yoyote ile?


    Swali hilo likanifanya kukaa kimya kwa muda fulani, halikuwa swali gumu kabisa na pia nilikuwa na picha nyingi sana kwenye mashine yangu ila yeye ndiye alikuwa miongoni mwa watu ambao sikutaka waone picha yangu yoyote ile. Kumbuka kwamba Dorcas nilikuwa nikimtaka toka alipokuwa akiishi mtaani kwetu Tandale, tena katika mara zote ambazo nilikuwa nikimtaka, alinikataa sana kiasi ambacho mpaka nikachoka. Leo hii Dorcas alikuwa hapa, ninachati naye moja kwa moja kupitia inbox. Sikuwa tayari kwa kipindi hicho kuweka picha zangu, nilitaka zibaki zile zile za wasanii wa Wamarekani.


    DORCAS: Mbona kimya Brother?
    MIMI: Sina picha. Ninatamani sana niweke picha ila tatizo simu yangu haina kamera. Ila usijali, ndani ya siku mbili, utaziona picha zangu.
    DORCAS: Sawa. Nakwenda kulala. Tutachati kesho Brother Mungu akipenda.
    MIMI: Mungu anapenda labda wewe usipende tu.
    DORCAS: Hahaha!
    MIMI: Huo ndio ukweli.
    DORCAS: Basi sawa mimi nakwenda kulala.
    MIMI: Usijali. Wape hi wote.
    DORCAS: Wa kina nani?
    MIMI: Utakaowaota.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    DORCAS: Na kama nikikuota wewe?
    MIMI: Nipe Hi tu. Ila kumbuka kwamba ukiniota, nami nitakuota, na kama tukiotana basi hiyo inamaanisha tumemisiana.
    DORCAS: Hahaha! Una maneno Brother.
    MIMI: Napenda kuongea tu. Ila usijali. Usiku mwema Dory.
    DORCAS: Nawe pia (Akaenda offline)


    Kuanzia hapo nikawa na amani. Muda wote nilikuwa nikishukuru sana kwa Mungu kwa sababu alikuwa amenipa uwezo mkubwa sana wa kuandika kiasi ambacho uwezo ule nilikuwa nautumia kwenye chatting kiasi ambacho ulionekana kuwa mzuri sana. 
    Huyu Dorcas nilikuwa namtaka sana, tena nilikuwa namtaka kuliko wasichana wote. Japokuwa zamani alikuwa akinikataa lakini nilikuwa nimekwishaapa kwa marafiki zangu kwamba ilikuwa ni lazima nimpate. Wengi walinicheka kidharau kwa kuniona najisumbua, hata alipohama nilichekwa sana kwa kuonwa kwamba sikuwa nimekamilisha lengo langu. 




    *** Unavyodhani atafanikiwa kumpata Dorcas..??


    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog