Search This Blog

Monday, October 24, 2022

CHUZI NDO HILO, HAKUNA KUONJA! - 3

 







    Chombezo : Chuzi Ndo Hilo, Hakuna Kuonja!

    Sehemu Ya Tatu (3)



    Giza likiwa limeshaingia, Musa anarudi sasa, akakutana na

    mama Shua njiani… “Musa vipi? We unajua namba yako sina, kwa nini usinitafute wakati we unayo? Kwani ule ujumbe wangu asubuhi kupitia kwa mtoto hukuulewa?”



    “Ujumbe upi?” aliuliza Musa…

    “We si tulipanga tukitoka job unipigie!”

    “Tuliongea wapi mama Shua?”

    “Kwani hukunielewa muda ule asubuhi ulipokuwa unajibizana na mwanangu Shua?”

    “Oh! Kumbe pale ulikuwa unanipa ujumbe wa moja kwa moja siyo?”

    “Sasa je?”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ungesema sasa.”

    “Sasa pale ningesemaje we unavyodhani?”

    “Basi yaishe…sevu upya namba zangu.”

    “Zitaje, lakini sitazisevu, nitaziweka kichwani tu.”

    “Sawa,” alijibu Musa huku akimtajia mama Shua namba zake.

    Kisha, haraka sana mama Shua alirudi ndani akimtaka Musa kuchelewa hata dakika tano ndipo aingie…

    “Usiingie sasa hivi, itajulikana. We kaa kwanza mahali, baada ya dakika tano ingia, sawa mpenzi wangu?”

    “Sawa. Lakini da! Jamaa naye anafuatilia sana bwana,” alisema Musa akirudi alikotoka.

    Alikwenda kwenye duka la jirani na kuomba soda ili apotezee muda. Alikunywa, alipomaliza alikwenda kwake. Ni baada ya dakika kama kumi na mbili hivi.

    Chumba kilikuwa kizito kwa Musa kwani muda mwingi alijikuta akimuwaza mama Shua na mambo yaliyojitokeza kuhusu mume wake…

    “Nahisi hii nyumba si ya kuishi mimi. Kama ndani ya mwezi mmoja tu jamaa ameshtuka kitu. Je, nikikaa mwaka mmoja si nitakatwa masikio mimi!”

    ***

    Kwa upande wake, mama Shua hali ilikuwa ya utulivu wa kimawazo. Yeye alishatekwa na kijana huyo hivyo alikuwa akiwaza namna atakavyodumisha penzi…

    “Musa ni kijana mzuri sana. Lakini sasa itakuaje wakati mista naye kama hataki kumsikia achilia mbali kumwona?” alijiuliza, akakosa jawabu.

    Muda ulivyozidi kwenda, alipanda kitandani akalala. Alitamani sana kumtumia meseji Musa lakini mume wake alishalala hivyo aliamini angeweza kuzua mapya jambo ambalo hakulipenda hata kidogo!

    ***

    Kulikucha, oyaoya za kujiandaa ndani ya nyumba zilipamba moto. Baba Shua, mama Shua, Shua walikuwa uani na msichana wa kazi. Musa yeye alivaa bukta na singilendi huku taulo akilitupia begani kwa ajili ya kwenda kuoga.

    “Hujambo mchumba?” alianza Musa. Safari hii alikuwa tayari kupokea ujumbe kutoka kwa mama Shua kama alivyomwambia jana yake…

    “Mwambie sijambo, nimekumisi sana.”

    “Jambo…misi sana.”

    “Hata mimi. Sasa leo tutapata wapi lanchi mchana mchumba?”

    “Mwambie unipigie, popote ulipo nitakuja.”

    “Nakuja…”

    Walicheka wote kwani Shua alishindwa kunyoosha Kiswahili, Musa akaendelea…

    “Mchumba, kweli utaweza kuja nikikuita mahali kwa ajili ya lanchi?”

    “Mwambie nitaweza bila shida,” hapo alisema baba Shua…

    “Aweza.”

    “Haya, basi nitakupigia.”

    “Mwambie sawa usikose, iwe saa saba kamili,” hapo alidakia mama Shua…

    “Saa saba …amili.”

    Walicheka tena, Musa akaingia kuoga chapuchapu. Alitoka, akaingia mama Shua. Yeye alioga akifurahia kusikia raha anaoga huku akiyaona majimaji yaliyobaki kwa kuoga Musa.

    Alipomaliza naye alitoka kwa kasi akisema amechelewa sana siku hiyo…

    “Mbona siku ile nakwenda Arusha ulichelewa sana na sikukusikia ukilalamika. Imekuaje leo?” aliuliza baba Shua.

    “Hata siku ile nililalamika, sema sikukwambia tu.”

    “Mh!” Aliguna baba Shua.

    Musa alitoka, wakati anapita kwenye dirisha, mama Shua alimwona, naye akajiandaa haraka sana huku moyoni akisema…CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwani akinipa lifti mbele kwa mbele kuna tatizo gani? Yaani mume wangu yeye anawaza mabaya kila wakati.”

    Tangu, Musa atoke, mama Shua alitumia ndani kama dakika tano, naye akatoka lakini alishamtumia meseji Musa kumwambia amsubiri ampe lifti. Na Musa naye alijibu…

    “Mh! Huogopi?”

    “Wala!” alijibu mama Shua.

    Mama Shua alitoka mbio kiasi kwamba mumewe akashtuka sana…

    “Kinachokufanya ukimbie ni nini mama Shua?”

    “Nawahi baba Shua, si nimekwambia wakati natoka kuoga jamani mume wangu!?” alijibu mama Shua huku akikimbia kitendo kilichomfanya baba Shua kushindwa kuendelea kuhoji au kusema lolote jingine.

    Mama Shua alipotea akimuwahi Musa, mumewe akiwa ndani ya bukta na singilendi kwa juu naye alitoka mbio akimwambia msichana wa kazi…

    “Dada nakuja sasa hivi.”

    Mbele kidogo, baba Shua alikutana na Bajaj inashusha abiria…

    “Eee bwana niwaishe mahali,” alimwambia suka wa Bajaj.

    Bajaj iligeuzwa kwa kasi kutokana na hali ya uso wa baba Shua, dereva akajua anawahi sehemu kwa dharura.

    “Nipeleke kule, kanyaga mafuta kama unafukuza mwizi.”

    ***

    Mama Shua alizama ndani ya gari la Musa…

    “Ondoa gari, maana kama sijamuelewa mume wangu, anaweza akafuatilia,” alisema mama Shua.

    Ile anafunga mlango tu, Bajaj aliyopanda mume wake ikatokea kwa mbali kidogo.

    Baba Shua alitumbua macho mbele akiamini kama mke wake atakuwa anaondoka na daladala lazima angemwona anakaribia kituoni na kama hayupo, ina maana atakuwa ndani ya gari analoliona la Musa ambalo yeye baba Shua halijui.





    “Unaweza kuendesha kwa kasi hadi kulifikia lile gari?” baba Shua alimuuliza dereva ambaye badala ya kujibu aliongeza mafuta kwa kasi.Lakini wakati analikaribia, gari hilo likawa limeshaingia barabara kuu. Kwa mbali, ndani aliona watu wawili akiwemo dereva lakini hakuweza kupata mtazamo kamili kama ni wanaume, wanawake au mwanaume na mwanamke kwa vile vioo vya gari vilikuwa ‘tinted’…

    “Unajua kuna Bajaj inatufuata kwa kasi sana,” Musa alimwambia mama Shua. Ilibidi mwanamke huyo ageuke kuiangalia lakini akaiona kwa gizagiza sana. Kwa hiyo hakujua ndani ya gari lile mlikuwa na nani na ni nani!

    Baba Shua alimwambia suka waishie pale lakini akaisoma namba na kuandika kwenye simu yake kisha akarudi nyumbani akiwa amefura sana. Aliamini moyoni kwamba, mkewe alipanda lile gari…

    “Yaani mama Shua sasa amefika pabaya, anafuatwa na magari hadi nyumbani! Hii kwa kweli siwezi kuivumilia hata kidogo,” alisema moyoni huku akituma meseji kwenda kwa mkewe…

    “Kwa hiyo sasa umefikia hatua ya kufuatwa na gari hadi nyumbani ili likupeleke kazini. Tutawezana kweli?”

    Mama Shua aliposoma meseji hiyo alishtuka sana…

    “Mh! Au alikuwa kwenye ile Bajaj nini?”

    Alitaka kumfowadia meseji Musa lakini akahisi atakuwa anamtisha kijana wa watu, akaacha…

    “Gari gani mume wangu?”

    Wakaanza kujibizana sasa…

    “Gari gani? Kwani we umepelekwa kazini na gari gani?”

    “Nilipanda basi baba Shua.”

    “Usinidanganye mimi wewe. Umepanda gari lenye namba za usajili T 349 CAT, unabisha?”

    Mama Shua hakuzijua namba za gari lile, lakini akajitutumua na kujibu kwa ufupi…

    “Ina maana uliniona nikiingia kwenye gari au?”

    “Ndiyo,” baba Shua alifanya kusudi kujibu hivyo ili aone, mkewe atajibu nini.

    Mama Shua alihema kwa kasi, akajua kweli alionekana na mumewe, ilibidi asiijibu meseji hiyo.

    Baba Shua alipoona nusu saa inapita bila majibu, alituma meseji nyingine…

    “Mimi umenichosha na vitabia vyako vya siku hizi, kwa nini usije kuchukua vitu uondoke hapa nyumbani? Maana najua unataka uhuru hapa kwangu umebanwa!”

    Ilikuwa meseji nzito sana kwa mama Shua. Alianza kuingiwa na wasiwasi. Aliamini hali ndani ya ndoa yake si nzuri, akaanza kuona hatari ya siku za mbele.

    Hakuwahi kufikiria hata siku moja kwamba, mumewe angeweza kumtamkia maneno mazito kama hayo, lakini siku hiyo alitamka bila kutumia lugha ya mafumbo. Hata meseji hiyo hakuijibu.

    ***CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Saa saba juu ya alama, Musa alimpigia simu mama Shua…

    “Haloo,” alipokea mama Shua bila maneno ya kuchombezea kama ‘haloo baby’, ‘niambie darling’ na mengineyo…

    “Vipi sweet, mbona umepokea simu kama hunifahamu vile?”

    “Ah! Siko sawasawa bwana…”

    “Kuna nini?”

    Mama Shua alijua akisema amwambie yaliyojiri, hata yeye Musa angeshtuka na kuogopa sana, akamdanganya…

    “Mwili wangu kama unaumauma kwa mbali halafu moyo kama hauna furaha vile.”

    “He! Kuna nini tena? Uko wapi kwani?”

    “Nipo job. Wewe..?”

    “Mimi nipo hapa hotelini napata mchemsho wa samaki. Kama vipi njoo unywe.”

    “Ah! Yaani hata kutoka hapa pia sijisikii kabisa.”

    “Basi twende chumbani baby, nikakupetipeti, nikakufinyefinye wee mpaka useme basi. Halafu mambo yetu yawe kama ya siku ile, unasemaje?” alisema Musa na kumfanya mwanamke huyo kusisimka, akajikuta akichangamka mwili…

    “Jamani baby, usinifanye nicheke darling…lo! Maneno yako matamu kama asali…”

    “Hata mimi mwenyewe nipo kama asali kama ulivyo wewe,” alisema Musa, mama Shua sasa akawa si yule aliyepokea simu, akaachia kicheko cha haja…

    “Wapi sasa?”

    “Si nimekwambia napata mchemsho…”

    “Ina maana huko kunifinyafinya utanifinyia hapohapo hotelini?”

    “Aah! Si kule bhana…”

    “Saa ngapi?”

    “Wewe tu, hata ukisema leo mimi niko tayari.”

    “Kweli?”

    “Kweli kabisa. Mimi nitaondoka kazini maana leo sina kazi nyingi sana,” alisema Musa na kumfanya mama Shua kuliangalia begi lake lilipo.

    Alichofanya, alimtumia meseji mumewe…

    “Naumwa, nakwenda hospitali.”

    Mumewe hakuijibu meseji hiyo zaidi ya kuachia tabasamu la mshangao huku moyoni akisema…

    “Amejua ana msala sasa anatafuta namna ya kuumaliza.”

    Mama Shua aliomba ruhusa kazini, akisema anakwenda hospitali hajisikii sawasawa.

    Alichukua usafiri huku akimtumia meseji Musa ya kumuuliza kule hotelini aende muda huo au bado!

    “We umeshatoka kwani?”

    “Niko njiani.”

    “Tangulia na mimi natoka hapa nakwenda chukua gari kisha hotelini, hapa nilipo mawazo yangu yote nipo na wewe kitandani.”



    Mama Shua alizidi kusisimka mwili, hata maneno ya mumewe akayaweka pembeni kwanza…

    “Basi baby usichelewe bwana,” alisema mama Shua huku akihisi kuchelewa kufika kwenye hiyo hoteli.

    Alifika, akazama ndani huku mikono ikibonyeza vitufe vya simu kumtaarifu Musa kwamba ameshafika eneo la tukio…

    “Baby, nipo eneo la tukio tayari.”

    Musa alitoka kama swala, akafika hotelini ndani ya dakika chake…

    “Umechukua rum?”

    “Kilekile.”

    “Oke.”

    Mlango ulisukumwa, Musa alizama ndani na kumkuta mama Shua ameshavua kila kitu na yupo na suti ya ngozi tu…

    “Du! Baby unanihamasisha siyo?” alisema Musa akimwangalia mama Shua kwa macho yaliyojaa tafsiri ya ‘mahaba niondolee uhai wangu’.

    Musa, kwa kasi ya mashine ya cherehani alivua suruali, akatupa huko, akachua shati akatupa kule, akavua boksa akaivurumishia mbali, akachojoa singilendi na kuirushia mbali, akapanda kitandani huku akichekacheka lakini moyoni alipokumbuka kwamba anaweza kuchemsha licha ya mbwembwe nyingi alijikuta akikosa nguvu ghafla…

    “Daa! Inawezekana lakini…sijui mganga gani atanisaidia mimi?” alisema moyoni Musa.

    Mama Shua kwa kujua kuwa Musa ana ‘ugonjwa’ wa kumaliza haraka, alimdaka, akampa mabusu motomoto huku akimsema kwamba amechelewa…

    “Hivi kwa nini umechelewa baby lakini?”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mh! Mbona nimewahi darling…”

    “Hakuna bwana, yaani mpaka uongee na wanawake wako wee ndiyo uje kwangu.”

    “Sikuwa na mwanamke baby, ndiyo maana nilikuita pale. Sasa kama ningekuwa na mwanamke ningesema uje? Acha mawazo yako hayo.”

    Muda wote wa mazungumzo, wawili hao walikuwa wakishikana sehemu mbalimbali za mwili huku wamelala. Musa alichaji sana lakini kule kupambana na lawama za mama Shua kulianza kumkatisha tamaa kwa mbali…

    “Lakini baby mbona umekuwa mtu wa lawama sana? Huniamini, huniachii nafasi ya kufurahia tukio, vipi kwani?” alilalamika Musa…

    “Sikuamini ndiyo, sasa wewe unanisaliti hivihivi naona halafu nikuache kweli?”

    Ilifika wakati, mama Shua akiwa anaendelea kumlaumu Musa, mechi ikaanza pamoja na lawama zake juu…

    “Nikwambie kitu kimoja baby, mimi sipendi kabisa usaliti. Usaliti utanifanya mimi na wewe tuachane kabisa,” alisema mama Shua huku mechi imeshaanza…

    “Mimi sikusaliti mpenzi wangu, hayo mawazo yatupilie kwa mbali. Nakupenda wewe, nakupenda sana.”

    Mama Shua hakuacha kumtuhumu Musa kwa usaliti mpaka Musa akajikuta anachukua dakika kumi na tatu hivi akiwa bado uwanjani, ndipo mwanamke huyo akaamua kuachana na lawama na kumsifikia kwa mahaba anayompa, Musa akajikuta anamaliza mchezo, wakamaliza sambamba.

    Sasa walikuwa wamelala wakiangalia juu huku wote wakihema kwa sana…

    “Hivi baby mbona kama lile tatizo halipo, we unatumia dawa gani?”

    “Naijua mwenyewe, wala sikwambii ng’o.”

    “Niambie kidogo baby jamani.” “Sikwambii ng’o na hiyo dawa naijua mwenyewe. Ukienda kwa mwanamke mwingine utaipata ile hali, dakika moja tu mpira umeisha, aibu kwako,” alisema mama Shua huku akigeuka kumwangalia Musa kwa macho ya utani.

    ***

    Simu ya baba Shua iliita, mama Shua alipoiangalia, akasonya kisha akaacha bila kuipokea…

    “Huyu naye,” alisema moyoni mama Shua…

    “Mbona hupokei, nani kwani?”

    “Mista.”

    Musa aliposikia ni mista, damu zikamkimbia mwilini, alihisi baba Shua amesimama mlangoni na kupiga simu ya mkewe…

    “Mh! Atakuwa wapi?” aliuliza Musa…

    “Mi sijui.” “Siyo kwamba yupo hapo nje kweli!”

    “Nje ya mlangoni?”

    “Ndiyo.”

    “Hawezi. Namjua yule. Ajue mimi nipo ndani humu halafu asimame na kupiga simu! Angeingia na mlango mpaka ndani.”

    Mara ikaingia meseji…

    “Umekwenda hospitali gani?”

    Mama Shua hakuijibu meseji hiyo kwani ilikuwa ngumu kwake kueleza. Angeitaja si ina maana mumewe angemfuata!

    ***

    Baada ya mapumziko ya kama lisaa limoja, mama Shua akataka mechi tena, akamfanyia vilevile Musa na mechi ikaanza kwa uzuri mpaka dakika ya kumi, Musa akamaliza.

    Walikaa ndani ya hoteli hiyo mpaka saa kumi na nusu. Musa ndiye aliyeanza kutoka hadi kwenye gari, akafungua mlango na kuzama ndani, akamtumia meseji mama Shua…

    “Njoo, kuko shwari.”

    Mama Shua naye akachomoka mpaka kwenye gari ambapo alikuta mlango wa upande wa abiria upo wazi.

    Musa aliwasha gari, wakaondoka.

    “Sasa utashukia wapi?” aliuliza Musa…

    “Mh! Jirani na kile kituo, saa hizi najua yeye atakuwa ameshafika nyumbani,” alisema mama Shua.

    Musa aliegesha gari pembeni, mama Shua akashuka na kuanza kutembea polepole.

    Musa naye alipanda kaukuta na kulipeleka gari anapolilaza. Baba Shua alikuwa akienda dukani, akakutana na mama Shua, lakini pia akaliona gari la Musa na Musa mwenyewe akishuka, akashtuka…



    baba shua aliiangalia ile namba ya gari na kukumbuka kuwa ndo ile ile aliyoiona ikiwa mbele yake asubuhi walipokuwa wakiifukuzia na bajaji, pale ndipo hofu yake ikazidi kuongezeka juu ya Musa, alitaka kumuuliza Mama shua lakini akaghairi na kuendelea na shughuli zake,

    ¤¤¤¤¤¤¤¤

    .CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama shua aliondoka akiwa na wasiwasi kwamba atakuja kujibu nini kwa baba shua kama ameshtukia ile ishu, aliingia chumbani akabadilisha nguo na kujifunga kanga yake tayari kwa kwenda kuoga,

    Upande wa pili Musa yeye alikuwa anasikilizia meseji ya kutoka kwa mama shua kujulishwa kinachoendelea je baba shua atakuwa ameshtukia?, mara meseji ikaingia "baby nakuja sasa hivi tumalizie tena" Musa alistuka "tena?" ndio wangu, "tena sasa hivi?" aliuliza Musa akionesha kuwa na wasiwasi "ndio", alijibu mama shua kiuhakika zaidi,

    Kwani baba shua kaenda wapi? Aliuliza Mussa,

    Ametoka bhana sijui kaenda wapi atajijua mwenyewe, mi nabeba kanga mbili na maji nayapeleka bafuni alaf kanga moja nitaiacha kanga huko moja ndo nitakuja nitaingia kwako, alimshauri mama shua,

    Mmh, "haya njoo" maelezo ya mama shua yalionekana kumuingia Musa,

    "Poa usitume meseji tena mi ndo natoka"

    Poa.



    Mama shua aliiweka simu chaji, akatoka kama alivyopanga akaingia bafuni, akaiweka kanga moja ikiwa inaning'inia akaingia chumbani kwa Musa, haraka haraka wakalianzisha sebene.

    ¤¤¤¤¤

    Baba shua alirudi toka dukani na kuingia ndani, alikuta nguo za mama shua akagundua kuwa ameenda kuoga, alipoangalia mezani akaiona simu ya mama shua ikiwa chaji, aliichukua na kuanza kuipekua upande wa meseji, bahati nzuri meseji zote alizifuta, Baba Shua alipokosa meseji yoyote yenye kutia shaka, aliizima, akairudisha simu kwenye chaja kisha akatoka sebuleni. Alikaa akisikiliza maji yanavyomwagika bafuni mkewe akioga lakini hakusikia…

    “Mh! Huyu amekwenda bafuni kweli au..?”



    Baba Shua wakati ameshtuka hivyo, mama Shua alitoka chumbani kwa Musa haraka. Akanyata mpaka uani, akazama bafuni.

    Baba Shua alitoka sebuleni, aketembea, naye kwa kunyata mpaka uani. Akasimama.

    Mama Shua alipozama bafuni, alianza kuoga maana alitoka uwanjani, hivyo lazima awe msafi.

    Baba Shua aliposikia maji ‘chwaa’ akatingisha kichwa kwa maana ya kukubali…

    “Maana usikute mtu kasema anakwenda kuoga kumbe ameingia kwa mwanaume wake,” alisema moyoni baba Shua huku akirudi sebuleni.

    Musa alianza kuona njia nyepesi ya kumpata mama Shua… “Kumbe hata kwangu hapahapa nyumbani inawezekana? Sasa kuna haja gani ya kupoteza pesa hotelini?” alijihoji Musa.

    “Basi itakuwa nikimhitaji na’mbuku mapema ili ajipange jinsi ya kumpiga chenga mumewe.”

    ***

    Mama Shua aliingia chumbani, akajifuta na kupanda kitandani huku akijifanya hana habari na mumewe.

    ***

    Ilikuwa usiku wa saa saba, baba Shua alishtuka akiwa amelala kuangalia juu au chali. Akamwamsha mke wake …

    “Mama Shua…” “Abee,” mama Shua aliitika haraka sana. Ilionekana hata yeye hakuwa amelala usingizi…

    “Hivi unajijua kwamba umebadilika nyendo zako?”

    “Mimisijabadilika, ila wewe mawazo yako yanasema hivyo.” “Mh! Mawazo yangu yanasema hivyo…ama kweli wanawake mwalimu wenu kipofu! Hivi unadhani wewe uliyekuwa na mimi mwaka jana ndiye nakuona yuleyule wa mwaka huu?”

    “Si ndiyo maana nimesema mawazo yako.”

    “Mawazo yangu ee? Sawa bwana, mawazo yangu, usiku mwema,” mama Shua alilala zake. Mama Shua hakutaka kunyoosha maneno wala kuweka sawa hali hiyo. Kwake akaona ni sawasawa tu. Alishalewa penzi la Musa.

    ***

    Asubuhi kulikucha, mama Shua kama kawaida yake, anakuaga wa kwanza kutoka uani na binti yake, Shua na kumkuta msichana wa kazi akiwa wa kwanza kutoka kuliko yeyote ndani ya nyumba hiyo.

    Baba Shua siku hiyo alichelewa kidogo, wakati mkewe ametoka kuoga, yeye ndiyo akaenda kuoga.

    Musa siku hiyo alipotoka, hakukutana na mama Shua wala Shua mwenyewe, ila msichana wa kazi wa mama Shua alikuwa akifagia… “Mchumba wangu yuko wapi?” alimuuliza msichana wa kazi…

    “Kaingia ndani na mama yake.”

    “A…haa! Kaamka poa lakini?”

    “Eee.” ***CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Musa ndiye aliyekuwa wa kwanza kufika nje, akawa anavaa viatu tayari kwa kuondoka. Mara akafuata mama Shua. Baba Shua alisimama mlangoni akisikiliza…

    “Za asubuhi?” alisalimia Musa…

    “Salama, mzima wewe?” “Mimi mzima, naona kumekucha.”

    “Eee…ndiyo unaondoka?” aliuliza mama Shua…

    “Eee…”

    “Nitapata lifti?” mama Shua aliomba lifti huku akiwa hajui kama mume wake anasikiliza… “Itakuaje sasa? Utaeleweka?”

    “Ah! Achana naye huyu.”

    Baba Shua alimwomba Mungu amsaidie katika kusimamia uvumilivu wake ili asijitokeze akiamini kwamba anaweza kufanya jambo baya kuliko inavyofikiriwa…

    “Eee Mungu, nipe uvumilivu kwa ushahidi huu,” alijisemea moyoni baba Shua huku macho yake yakiwa kwa Shua kitandani.

    “Teh! Teh! Teh!” alicheka Musa kwa kicheko kile cha ‘da! Jamaa namwibia hivihivi anaona’.

    Musa ndiye aliyeanza kutoka, mama Shua akachelewa nje kidogo akijifanya anaweka sawa gauni lake jekundu alilovaa siku hiyo. Baba Shua hakutoka nje, alikwenda kukaa kwenye kitanda na machozi yakaanza kumchuruzika kiasi kwamba alijuta, si kumuoa mwanamke huyo bali hata kukutana naye siku ya kwanza…

    “Hivi kumbe ameumbwa hivi? Hakuna haja ya kuelimishana tena, dawa yake ni kuamua kuachana naye tu,” alisema moyoni baba Shua, akasimama, akapiga ishara ya msalaba kifuani kama kuashiria kwamba, anamuachia Mungu.

    Kwa upande wake mama Shua, alishangaa kutomwona mumewe akitoka ili kumsindikiza kwa macho kama ilivyo kawaida yake…

    “Huyu vipi? Mbona hatoki wakati mimi nataka kuondoka?” alijiuliza mama Shua, akarudi ndani, tena mpaka chumbani… “Mi naondoka,” aliaga Mama Shua huku macho yake yote yakiwa kwenye simu. Aliamini Musa atamtumia meseji.

    Baba Shua hakumjibu mkewe, alikaa kitandani. Alikuwa akimuangalia tu!

    Ilibidi mama Shua atoke mbio kuwahi lifti huku moyoni akijua kwamba mumewe ana kitu moyoni… “Au jana alijua niliingia chumbani kwa Musa? Lakini hapana, asigeweza kuacha kuniambia. Lakini lazima ana jambo ndani ya moyo wake.”

    Mama Shua alipanda gari la Musa huku akiwa hana amani. Pia alipanda kimachale sana akiangalia nyuma. Aliamini mumewe anaweza kutokea ghafla





    “Ondoa gari haraka Musa, tunaweza kufuatwa,” alisema mama Shua akifunga mlango na kutulia kama kibaka aliyepakiwa kwenye ‘difenda’. *** Siku hiyo, mama Shua alifanya kazi lakini si kwa kasi ya kawaida. Ilipofika saa saba mchana, meseji ya mama yake mzazi iliingia kwenye simu yake ikiwa imeandikwa… “Najua tabia yako imebadilika, lakini jua kwamba upo kwenye ndoa. Aibu unayoitengeneza, usije kutuletea hapa nyumbani.” Mama Shua jasho jembamba lilimchuruzika. Alihisi amejivua nguo kwa wazazi wake… “Ina maana mama amejua mimi nachepuka?” alijiuliza mama Shua. Mapigo ya moyo yalibadilika, yakashika kasi. “Musa,” aliita mama Shua… “Naam…” “Mama amenitumia meseji sijapenda…” “Mama mwenye nyumba au?” “Mama yangu mzazi…” “Inasemaje?” Mama Shua aliisoma tena ile meseji ya mama yake mzazi, lakini safari hii kwa sauti ili Musa asikie. Alijiuliza sana mama Shua, nani alimpa mama yake taarifa maana anaishi mkoani. Aliamua kumpigia simu mdogo wake aitwaye Selina ambaye anaishi hukohuko mkoani… “Shikamoo dada…” “Marhaba mdogo wangu….za hapo nyumbani?” “Njema, hajambo Shua?” “Shua hajambo sana…eti nisaidie kitu mdogo wangu… mama kanitumia meseji, anasema nijitambue nipo kwenye ndoa, aibu ninayoitengeneza nisije nikaileta nyumbani…ana maana gani? Baba Shua kaleta habari gani huko?” “Kwani sasa we unavyoona baba Shua anaweza kuleta habari gani kuhusu wewe?” “Sasa mbona unaanza ligi Selina?” “Sianzi ligi bali nimeshangaa sana swali lako. Wewe kuna mtu kakuona mara mbili unaingia sijui gesti sijui hotelini. Unaingia peke yako kutoka na mwanaume ana gari…huyo ndiye kampigia mama simu jana, akamuuliza ‘yule binti yako Sesilia si bado anaishi na mwanaume yuleyule?’ Mama akajibu ndiyo. Akasema ‘sasa mbona mara mbili namwona akiingia na kutoka hotelini na mwanaume mwingine?’ ndiyo mama juzi na jana presha imepanda,” alisema Selina. Mama Shua palepale alikata simu, akakunjua kiti na kukilaza kwa nyuma, yeye naye akalalia kiti huku akitetemeka… “Oya vipi, kuna nini?” aliuliza Musa macho yakiwa mbele barabarani. “Kuna soo nyumbani Musa…” “Nyumbani wapi?” Musa aliuliza huku akionekana kupunguza spidi ya kuendesha. Aliamini hilo soo ni nyumbani kwake mama Shua walikotoka hivyo angehitaji kurudi… “Mkoani…”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/ “Kuna soo gani sasa?” Mama Shua alisimulia kila kitu kuhusu meseji ya mama yake na maneno aliyoambiwa na mdogo wake kuhusu wao kuingia hotelini na kutoka… “Daa! Hatari baby…sasa?” “Hata sijui baby…nahisi sasa mambo yatafumka zaidi…” “Una maanisha nini?” “Yalishaanza kufumka kwa mbali…” “Wapi?” “We jua hivyo.” Mara, meseji nyingine ikaingia kutoka kwa mumewe, baba Shua, ilisomeka… “Bado tuna imani na wewe baba Shua lakini kama ukiona mwenendo wa mkeo si mzuri, hafai kuwa mke ruksa kumwacha na hapa kwangu asije-Mama.” Baada ya meseji hiyo, baba Shua alisindikizia na meseji yake yeye akisema… “Sijamwelewa mama lakini nahisi ujumbe huu wewe umeuelewa ana maana gani na ni kwa nini!” “Musa nishushe hapo please,” alisema mama Shua… “Vipi kwani mambo yamezidi kuwa mabaya?” aliuliza Musa akiwasha indiketa kwenda kushoto ili aegeshe gari… “Ah! Nitakupigia simu baadaye,” alisema mama Shua huku akishuka. Mama Shua alitembea kama mtu aliyelowa maji ya baridi bila ridhaa yake. Hapo alikuwa akikitafuta kituo cha daladala. Kila aliyekutana naye macho, alihisi anajua yeye ni mchepukaji mpaka wazazi wake mkoani wamejua na kumwambia… “Hii ni kali. Mimi mama Sesilia ndiyo nimefikia hatua hii kweli? Hapana…hapana…iko haja ya kujitafakari upya,” alisema moyoni. Alipanda daladala kuelekea mjini lakini akiwa ndani ya basi, kuna mwanamke mmoja alikuwa akimsimulia mwenzake namna jirani yake mmoja alivyoachika kwa sababu ya uchepukaji… “Yaani mimi nataka nilimshangaa sana yule mwanamke. Yaani unachepuka mpaka unaachwa? Si laana hiyo? Kwanza ni kutojitambua gani huko?” “Si ndiyo walivyo wanawake wa siku hizi. Wanasema kichwani wana akili kumbe wana matope. Wanataka mume akirudi saa nne usiku basi yeye awe amerudi saa nne kasoro dakika saba.” *** Siku hiyo mama Shua alifanya kazi kama mfanyakazi mgonjwa aliyegomewa ruhusa na mwajiri wake asiende hospitali. Mchana, alijikuta akivutwa na hisia za kumpigia simu mama yake ili amdanganye kutoka kwenye tuhuma zake. Alidhamiria kumwambia kuwa, pale hotelini walikuwa wanatoka kwenye semina tu na mwanaume aliyeonekana naye ni mfanyakazi mwenzake. Alipoona wazo hilo limesimama, akampigia. Simu iliita wee, alipokata tamaa, mama yake akapokea… “Unasemaje?” alipokea mama yake… “Shikamoo baba.” “Marhaba…nakusikiliza…” “Mama nilipokea meseji yako kwamba…” “Mimi siyo mahakama,” alisema mama mtu na kukata simu huku akisikika akisonya.





    Mama Shua alibaki ameduwaaa asijue la kufanya kwani majibu ya mama yake yalimpa picha kamili ambayo hakuwahi kuiona hata siku moja. “Loo! Yamenikuta…huyo mzee wa nyumbani aliyeniona hotelini mpaka akapeleka umbeya huu kwa mama sijui nani?” alijiuliza moyoni… “Lakini kwani lazima nikiwa naingia hotelini iwe kwa sababu ya kufanya zinaa? Kwa nini mama asiniulize mimi kwanza halafu jibu langu ndiyo likatoa mwanga wa uamuzi wake?” aliendelea kujiuliza mama Shua, alikosa raha. Pia akakosa amani ya moyo. Palepale akampigia simu mdogo wake, Selina… “Ee dada…” “Selina, ni kwa nini mama anatoa maamuzi bila kuniuliza mimi akasikia nitajibuje?” aliuliza palepale mama Shua… “Kivipi?” “Yeye ananihukumu tu kwa vile kasikia eti nimeonekana nikiingia na kutoka baa… anajua nilifuata nini? Pengine niliingia kuzungumza na mtu je? Hotelini si kunakuaga na ukumbi wa mikutano!” “Dada Sesilia….mama akuulize wakati yule mzee amekuwa akikuona ukiingia chumbani na unakaa sana humo! Huo ukumbi upo chumbani dada Sesilia? Unajua mpaka ile presha ya mama ilishuka! Yaani wewe dada Sesilia…mh! Mi mwenyewe sijaamini hata kidogo…yule mzee akasema alikusalimia kwenye korido ukampotezea.” Mama Shua alikata simu. Hakuwa tayari kuendelea kusikia maneno yenye maumivu makali kama hayo… “Mh! Yule mzee akasema alikusalimia kwenye korido ukampotezea’,” mama Shua aliyarejea maelezo ya mdogo wake kiasi kwamba, alitamani ardhi ipasuke. Alipowaza sana, mama Shua akakumbuka kwamba, ni kweli siku moja akiwa anatoka kwenye hoteli anayokutanaga na Musa, alimwona mzee mmoja ambaye aliachia tabasamu na akamsalimia. Alikumbuka kwamba, sura ya mzee huyo haikuwa ngeni machoni pake lakini aliamini ni wazee wa Jiji la Dar es Salaam ambao wanapenda dogodogo! “Aaaa! Mzee Magunia…yule aliyenisalimia siku ile ni mzee Magunia wa kijijini kwetu…da! Ndiyo maana nilijiuliza huyu mzee mbona kama namfahamu vile! Lo!” *** Mchana wa saa saba, Musa alimtumia meseji mama Shua… “Haloo…” Mama Shua baada ya kuisoma meseji hiyo alisonya, akasema moyoni… “Ungejua ulivyoniletea matatizo wala usingetuma helo zako.” Musa alipoona hajibiwi na mama Shua aliamua kupigia simu. Iliita weeee! Mpaka ikakatika! Ikaita tena wee mpaka ikakatika… “Khaa! Huyu ana nini sasa?” alijiuliza Musa. Akapiga tena… simu ikaita weee mpaka ikakatika! Akamtumia meseji… “Kuna tatizo baby?” Meseji hiyo haikujibiwa, Musa akasema moyoni kwamba kama angekuwa anapajua ofisini kwa mwanamke huyo angekwenda ili akajue kuna nini kilichotokea! Baada ya nusu saa, baba Shua alimtumia meseji mkewe… “Kama mama amejua uovu wako, ni zaidi sana mimi. Jua umesimama katikati. Unaweza kuingia au kutoka. Lakini yote hayo yametegemea maono ya moyo wako katika kuamua baya na zuri.” Mama Shua alijikuta akichukia sana, akamjibu… “Unahukumu kama mchungaji au hakimu?” “Kama wote…” “Ungechunguza kwanza kabla ya kusema…” “Namshukuru Mungu nimechunguziwa na mama yako.” “Niache tafadhali…nataka niendelee na maisha yangu…” “Uachwe mara ngapi?” “Basi hakuna haja ya meseji zako,” alisema mama Shua. Lakini naye akawa hajui mumewe amemwacha kwa maana gani? Kwamba hamtumii tena meseji… hamfuatifuati na mambo yake au anamwacha kwa maana ndoa basi tena! Kweli, baba Shua hakutuma tena meseji kwa mama Shua kiasi kwamba, mwanamke huyo alichanganyikiwa. *** Muda wa kutoka kazini ulifika, mama Shua alitamani siku hiyo asirudi nyumbani kwake kwa mambo yaliyotokea. Alijisikia kulalalala mahali mpaka saa mbili usiku au tatu ndipo arudi nyumbani. Lakini kama angekwenda kulala mahali, angekuwa na nani? Maana kuwa peke yake pia ilikuwa tatizo, mawazo yangekuwa palepale. Alihitaji kampani, tena ya mwanaume. Ilibidi amkumbuke Musa. Aliaga wenzake akatoka, nje akampigia simu Musa… “Uko wapi baby?” “Niko baa…we si unasikia kelele hapa!” “Baa wapi?” “Posta.” “Tunaweza kuonana?” “Wapi?” ”Wapi! Si kule mahali kwetu!” “Saa ngapi?” “Mimi ndiyo nimetoka, naelekea.” “Oke, nakuja.” “Please, usichelewe baby.” Mama Shua alichukua usafiri, ukampeleka hadi kwenye hoteli hiyo. Alishuka, akamalizana na mwenye usafiri, akatembea mpaka mapokezi. Alilipia chumba yeye mwenyewe, akapelekwa chumbani. Alikuwa ameshavua nguo, amejifunga taulo tu na alilala kitandani simu ikiwa mkononi akianza kuchati. Kwanza kabisa alimtumia meseji mumewe… “Natoka kazini napitia kwa rafiki yangu Rukia… kuna ishu ya kuzungumza naye…” Hakujibiwa meseji hiyo lakini yeye hakujali, akamgeukia Musa… “Mimi nimeshafika, wewe uko wapi baby?” “Nakaribia baby,” alijibu Musa. Mara, ikaingia meseji nyingine. Hii ilitoka kwa mama yake kijijini… “Kwa hiyo hiyo hoteli ndiyo umeigeuza nyumbani kwako sasa??!!”.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog