Search This Blog

Monday, October 24, 2022

CHUZI NDO HILO, HAKUNA KUONJA! - 5

 







    Chombezo : Chuzi Ndo Hilo, Hakuna Kuonja!

    Sehemu Ya Tano (5)



    Baba Shua alirudi akamkuta mama Shua sebuleni akiwa katika hali ya kutojua nini kinaendelea. Aliingia chumbani bila kusalimia, akapanda kitandani kulala maana alishaoga nyumbani kwa Maua na kupakwa mafuta ya losheni na pafyumu juu.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kitendo cha baba Shua kumpita kama hamuoni kilimuumiza akili mama Shua, akahisi kama kuna la ziada ya pale…



    “Afadhali hata angenisalimia lakini kunipita kasi bila salamu maana yake nini sasa?” alijiuliza mama Shua.

    Alijishauri kuhusu kumfuata au kutomfuata mumewe, chumbani lakini mwisho wa yote aliona itakuwa ujinga kumfuata…



    “Yaani kumtenda kote kule halafu nimfuate? Je, akinipiga nitasema amenionea? Pengine karudi bado na hasira, kaepusha mabaya kwa kwenda chumbani halafu eti nimfuate, si itakuwa naendekeza ushetani!”

    ***

    Kule chumbani akiwa tayari kitandani, baba Shua naye aliwaza yake kwamba, endapo mama Shua atamuibukia chumbani salama yake afikie kulala. Lakini akisema amuulize kwa nini hajamsalimia, atavaa na kuondoka zake kurudi kwa Maua…



    “Tena kwanza ngoja nimpigie simu Maua, aliniambia nikifika nimjulishe,” alisema moyoni baba Shua, akashika simu yake na kumwendea hewani Maua lakini wakati huohuo, mama Shua naye akaingia kwa lengo la kupanda kitandani kulala…



    “Ee mambo vipi? Umelala nini..? Bado..? Oke…mimi ndiyo nipo kitandani muda huu…nilisema nitakupigia nikiwa nimejilegeza kitandani…usijali…aaa! Wewee…wewee! Mmmh! Acha bwana…teh…the! Haya poa…na wewe pia…aaaa bwana acha mambo yako wewe…oke oke.”

    Mama Shua alifuatilia sana mazungumzo hayo ili kujua mumewe anaongea na nani kwenye simu. Kwa mbali alihisi anaongea na mwanamke, lakini pia akahisi ni mwanaume, hasa kwenye vile vipengele vya ‘acha bwana…oke oke poa.’



    Baba Shua naye akawa anamuwaza Maua na maneno yake ya kwenye simu…

    “Mh! Maua bwana…ei nibusu…hivi anavyoamini ningembusu kweli? Ingewezekana wapi kwanza? Ye anajua mke wangu atakuwepo sasa ningembusu vipi? hata kama kweli tumerudisha majeshi nyuma lakini si kwa kiasi cha kuleta ubaya. Mbaya aachwe na ubaya wake.”



    Usiku wa siku hiyo ulikuwa mrefu kwa wote wawili lakini kila mmoja alikuwa akiwaza yake.

    Mama Shua yeye aliwaza maisha yatakavyokuwa baada ya kutoka kwa baba Shua kutokana na hali ilivyokuwa wakati baba Shua yeye alikuwa akiwaza maisha yake na Maua…

    “Siamini kama atanitenda kama mama Shua…kwanza Maua hata tulipokuwa klozdi enzi zile sikuwahi kumuwazia kwamba ananisaliti. Naamini si msaliti,” aliwaza baba Shua.

    ***

    Kwake Maua mambo yalikuwa vilevile kama baba Shua. Muda mwingi alimuwaza mama Shua na uovu wake kwa mumewe hasa akizingatia kwamba, ndiye aliyevunja uhusiano wake na baba Shua…

    “Mshenzi sana yule mwanamke. Yaani aliingilia penzi langu kumbe hawezi chochote. Haya sasa…ndoa imemshinda sijui atasemaje!”

    ***CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baba Shua alilala usingizi mzito siku hiyo, tena akikoroma jambo lililomshangaza sana mkewe mama Shua kwani alitarajia kuwa, kutokana na mambo yaliyotokea, angelala kimang’amumang’amu.

    “Mh! Yaani baba Shua pamoja na mambo yote yaliyotokea, bado analala usingizi kweli? Ina maana kitendo changu hakijamkera? Mbona mi mwenyewe nimekereka?” alijiuliza mama Shua bila kupata majibu. Mpaka kunakucha, mama Shua hakuwa amelala usingizi unaoeleweka.

    ***

    Kulikucha, mama Shua alitoka kitandani, akaenda uani kufanya kazi za usafi huku akiwa ametenga maji ya kuoga kwa ajili ya mumewe baba Shua.



    Lakini baba Shua akiwa kitandani hajatoka bado lakini alishaamka, akaanza kuchati na Maua…

    “Mambo baby, ndiyo naamka mimi,” alituma ujumbe huo baba Shua…

    “Ooh! Thanx God kwa ajili ya wewe! Mimi nimeshaamka. Ila natamani sana kama ungekuja kuoga kwangu kabla ya kwenda kazini…”



    “Da! Nguo sasa ndiyo tatizo mama…”

    “Nguo! Si utabeba za kuvaa baada ya kuoga.”

    Baba Shua aliamini ni ushauri mzuri hasa akizingatia kwamba, hana mawasiliano pale kwake zaidi ya msichana wa kazi na binti yake Shua.



    Alitoka kitandani, akachukua begi dogo la mgongoni, akaingiza suruali moja, singilendi moja na shati moja, viatu na soksi alivaa kabisa, akaondoka zake bila kuaga mtu.

    Wakati anaondoka, mama Shua alikuwa uani. Alijua mumewe angeenda kuoga lakini alipoona kimya, akaingiwa na wasiwasi, akaenda chumbani na kukuta kiasi cha pesa juu ya meza, lakini baba Shua hakuwepo…

    “Khaa! Huyu kaenda wapi tena?” alijiuliza. Alimwamsha Shua na kumuuliza lakini alionekana hajui lolote maana alikuwa usingizini.



    Aliingiwa na wasiwasi kwamba, huenda ameamua yeye ndiyo ahame kwenye nyumba hiyo na kumwacha yeye na Musa wake, lakini alipofungua kabati la nguo hakuona mabadiliko. Wingi wa nguo ulikuwa uleule na haikuwa rahisi kubaini kwamba, mumewe ametoka na begi lenye nguo chache.

    Hata alipokwenda kwenye sehemu ya viatu alibaini kuwa, ni pea moja tu haipo kwa tafsiri rahisi ni kwamba ndivyo alivyovaa…



    “Mh! Mimi sijui sasa,” alijisemea moyoni kama vile aliisikia sauti kichwani ikimuuliza.

    Alitoka nje na kukuta na Musa naye akiwa ametoka ili akaoge…

    “Mambo?” Musa alisalimia.

    “Poa tu,” mama Shua alijibu kwa mkato sana huku akichukua tahadhari kwa lolote endapo mumewe angetokea na kuhisi vibaya.



    Akili haikumpa mama Shua, akaamua kumpigia simu baba Shua lengo ni kutaka kujua aliko lakini simu yake iliita kwa muda mrefu sana bila kupokelewa.

    Je, nini kitaendelea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Ijumaa, siku ya Ijumaa.



    Baba Shua aliiona simu hiyo ya mkewe lakini hakuona sababu ya kuipokea…

    “Kwanza niipokee ili iweje? Najua anataka kujua kuhusu nilipo, halafu akishajua ili iwe nini? Mbona mimi sitaki kujua mambo yake?” alisema moyoni baba Shua na ili kupangua simu ya mkewe, alimpiga mabusu Maua mpaka wakajikuta wakiangukia kwenye kochi kubwa……puu..!



    Ukimya ulitawala, kilichosikika ni miguno ya mmmmm…mmmm, Maua alikuwa akihema kwa nguvu kama aliyetoka kufukuzwa…

    “Mmmm…mmmm…”



    “Ngoja nikafunge mlango,” alisema Maua, baba Shua akamwachia kwa muda.

    Maua alifunga mlango haraka na kumrejea baba Shua pale kwenye kochi kubwa. Ukimya ukaendelea kutawala lakini mihemko ya hapa na pale ilisikika kiasi kwamba, kama chumbani kungekuwa na mtu mzima anafuatilia, lazima angetoka kuungana na wawili hao…



    “Benny,” aliita Maua kwa sauti iliyotoka kwa chini sana…

    “Yes Maua,” Benny naye aliitika kwa kufuata biti ya kuita ya Maua…

    “Si utachelewa kazini wewe?”

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hata kama…usijali Maua.”

    Maua kusikia hivyo, akamshika mkono wa kulia baba Shua na kusimama naye, wakaenda chumbani, wakajifungia na kupanda kitandani..!



    Figisufigisu ilitawala kitandani, Maua alikuwa akionesha umahiri kwenye uwanja kwa mkakati wa kumrejesha baba Shua kwenye himaya yake. Muda mwingi wa mchezo alimtaka asahau machungu ya kwa mkewe, kwani yeye yupo kwa ajili yake.

    ***

    Baada ya nusu saa, Maua alikuwa amemshika mkono baba Shua, wakawa wanatoka nje. Mkononi Maua alishika funguo za gari…



    “Sasa baby si uende na gari…au utakuwa umesahau kuendesha?” alisema Maua…

    “Nisahau kuendesha gari sweet..! Haitawezekana hata siku moja.”

    Baba Shua alipokea funguo, akazama kwenye gari na kuondoka…



    “Kishakwisha huyu…safari hii hachomoki! Ndiyo atajua mapenzi ya kweli yalikuwa wapi kati yangu na yule malaya wake wa nyumbani,” aliwaza Maua akiwa anarudi ndani.

    Yeye ni mfanyabiashara wa kuuza nguo za kike na vipodozi toka nchini Thailand na shughuli zake ni popote. Wakati mwingine wateja wake hufika hadi nyumbani. Tena wengi ni wale wanaonunua kwake kwa jumla na kwenda kuuza rejareja madukani mwao.



    Kuna siku Maua anaweza kushinda nyumbani na kujikuta akiingiza milioni mpaka kumi.

    ***

    Mama Shua akili ilimlala kabisa. Hakuamini kama baba Shua anaweza kumchunia kiasi kile…

    “Ana maana gani sasa kukaa kimya kiasi hiki? Mimi nifikirieje? Kama ameona mimi na yeye basi, si aseme tu kuliko kuwekana roho juu namna hii,” alisema moyoni mama Shua lakini sauti nyingine ilimjibu…



    “Kwanza shukuru Mungu wewe…angekuwa mwanaume mwingine angekuua hata kwa kukuchinja! Wewe umeona wapi mume au mke anamwona mwenzake akiingia chumbani kwa mtu mwingine ili kusaliti halafu anavumilia tu?”

    Mama Shua aliamua kuvaa, akaondoka. Lakini si kwenda kazini kwake, bali kwa baba Shua akajue nini kilimsibu.



    Akiwa ameshatoka, mbele alimwona Musa akiingia kwenye gari lake, mama Shua akasimama mahali ili kumpa nafasi Musa ya kupotea kwanza mbele ya macho yake ndipo na yeye aendelee na safari yake.

    Mama Shua anafika nje ya ofisi ya mume wake, baba Shua naye anawasili kwa gari la Maua.



    Aliegesha gari mahali, akashuka na kutembea kwa mwendo wa pole kuelekea ndani. Mama Shua hakuweza kuvumilia na alijuwa kwa tabia ya mume wake ya siku mbili zile, angeweza kumpita bila kumsemesha, akasimama njiani kwenda ndani…



    “Baba Shua nataka tuongee kidogo,” alisema mama Shua kwa sauti ya chini sana…

    “Mimi na wewe tutaongea nini sasa? Na tangu lini mahali pa kuongelea pamekuwa hapa ofisini?” alijibu baba Shua akiwa anaendelea kutembea kiasi kwamba, baadhi ya wafanyakazi walipoiona picha hiyo walishangaa kwani wanawajua wawili hao kwamba ni mke na mume.



    Mama Shua hakutaka makuu, akaamua kugeuza kuondoka huku moyoni akiwa na faraja kwani alishajua mumewe amefika kazini lakini alikuwa na maswali kibao…

    “Hili gari ni la nani? Halafu kama jipya! Kalitoa wapi? Au huko alikokwenda? Maana kwa muda aliotokea nyumbani isingekuwa rahisi ndiyo awe anafika kazini muda huu, lazima alipitia mahali…



    “Atakuwa amelinunua au kalikopa? Lakini lilishaanza kutembea,” aliwaza moyoni mama Shua akitokomea kabisa eneo hilo.

    Alifika nyumbani akiwa amechoka sana kiakili na mwili. Aliwaza namna ya kuwasiliana na mama yake na kumweleza matatizo yake lakini moyo ulisita. Alijua ataamsha hasira za mama huyo.

    Alimwangalia mtoto wake, Shua. Akamhurumia sana huku akitingisha kichwa.

    ***CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Saa sita mchana, Musa alimtumia meseji mama Shua…

    “Upo?”



    Mama Shua alipoisoma meseji hiyo alisonya kwa nguvu kiasi kwamba, kama nyumba ya tatu kulikuwa na mtu muda huo angesikia…

    “Huyu kijana mjinga sana. Yaani anadhani mimi niko poa? Kwani ye hajaona yaliyotokea?” alijiuliza moyoni mama Shua.

    Musa alipoona meseji haijajibiwa, aliamua kupiga. Simu yake iliita mpaka ikakatika…

    “Khaa! Huyu mbona hapokei simu?” alijiuliza Musa, akapiga tena. Safari hii, mama Shua aliamua kupokea huku uso ameukunja vibaya sana…

    “Haloo…”

    “Baby, mbona hupokei simu yangu jamani? Unajua nimekuandalia zawadi gani lakini?”

    Uso wa mama Shua ulianza kukunjuka kwa mbali sana…

    “Ah! Samahani sana jamani baby, nilikuwa mbali na simu…enhe! Zawadi gani hiyo my darling?”

    “Ni ‘sapraizi’…”

    “Jamani baby wa mimi si uniambie tu…”

    “Tukikutana nitakuonesha achilia mbali kukwambia…”

    “Da! Lini sasa tutakutana..?”

    “Wewe tu…”

    “Basi iwe leo jioni…”

    “Wapi?”

    “Panga wewe ila isiwe kule kwa siku zote maana kuna mzee mmoja wa kijijini ni mnoko vibaya sana…”

    “Nyumbani kwako lakini kukoje?”

    “Wapi?” “Kwa wewe na mume wako…hajamaindi ile ishu?”

    “Wee hayo yaache Musa bwana…nitakwambia kitu siku nyingine lakini… ila hali si nzuri kivile.”

    Walizungumza, wakapanga kukutana maeneo mengine jioni ya siku hiyo ambapo mama Shua angetokea nyumbani na si kazini kwani hakwenda kazini.

    ***

    Maua, muda mwingi aliutumia kuchati na baba Shua kwa kumtumia meseji mbalimbali za mahaba na kumpa pole kwa kazi. Pia kumsifia kwamba yeye ni mchapakazi hodari.

    Ilipofika mchana wa saa saba, Maua alimtumia meseji baba Shua ya kumuulizia kuhusu chakula…

    “Baby lanchi.”

    Kwa baba Shua lilikuwa jambo geni na jipya pia. Hakuwahi kuwaza kwamba, Maua anaweza kurejesha mapenzi ya dhati kiasi hicho. Alijisikia furaha moyoni, ilimsaidia pia kumsahau mama Shua na tabia zake.

    ***

    Saa kumi na moja, baba Shua alikuwa ndani ya gari akielekea Kinondoni kwa rafiki yake anayeitwa Jome.

    Alipofika kwa Jome, akashtuka sana Jome…

    “Ee bwana vipi?” aliuliza Jome.

    “Poa, vipi kwani?” “Mbona nimemwona shem mahali…”

    “Wapi?”

    “Pale Hoteli ya Bwawani One…”

    “Na nani?”

    “Ah! Sina hakika lakini wewe ni mwanaume utakuwa unajua namaanisha nini!”

    “We niambie tu, umemwona na nani?”

    “Na dogo mmoja hivi…”

    “Namjua…” “Ah! Kwa hiyo unajua kila kitu kuhusu shemeji?”

    “Najua.”

    “He! Ee bwana…kwani kuna nini?”

    “Kaka…mama Shua si yule tena…mama Shua kadanganyika na huyo dogo uliyemwona naye…nilitaka kuchukua hatua kali, lakini nimeona nimwache yeye na maisha hayo na mimi niwe na maisha mengine, naamini itanisaidia…”

    “Da! Kwani yule dogo unamjua?”

    “Nini kumjua Jome, naishi naye nyumba moja. Nikienda chooni napita mlangoni kwake.”

    “We Benny…kweli?”

    “Kweli Jome…”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ah! Ina maana nafuu na Maua?”

    “Ndiyo niko naye sasa…”

    “Ha! Kweli kaka?” “Kweli Jome.”

    Basi, baada ya hapo walizungumza mambo mengi mpaka ikafika hatua wakaagana. Jome alimsindikiza baba Shua nje mpaka kwenye gari…

    “Ha! Benny, una usafiri mara hii?”

    “Wa Maua…”

    “Heee! Maua huyuhuyu Maua shemeji yangu wa kitambo?”

    “Huyohuyo bwana…amekuja kwa kasi sana.”

    “Safi sana…safi sana…sasa Maua ndiye mke,” alisema Jome…

    “Kaka ni kweli. Nimekwenda hadi kwake. Kaniingiza ndani kasema hakuna mwanaume aliyewahi kuingia. kanitambulisha mpaka kwa majirani zake kwamba mimi ndiye mchumba wake nilikuwa nje ya nchi kimasomo.”

    Hapo, baba Shua na Jome walisimama nje kwenye gari wakizungumza…

    “Inaelekea wapi sasa?” aliuliza Jome…

    “Home kwanza, halafu Kimara kurudisha gari la Maua…”

    “Nipe lifti, niache hapo mbele tu,” alisema Jome, wakaingia garini wote.

    Baba Shua alipita barabara ileile yenye Hoteli ya Bwawani One, akaliona gari la Musa…

    ***

    “Yaani baby nimeshukuru sana kwa zawadi. Bonge la gauni, kama ulinipima vile,” alisema mama Shua akimwambia Musa huku wakiwa wamekaa kwenye baa ya Hoteli ya Bwawani One wakinywa juisi kwanza kabla ya kuzama chumbani kwa ajili ya majomboz…

    ***

    “Jome ndiyo hoteli hii ulipomwona mama Shua?” aliuliza baba Shua…

    “Hapahapa…tena wale pale wamekaa. Hebu ingia na sisi tukakae tuone,” alishauri Jome, baba Shua akaingiza gari kwenye maegesho ya hoteli hiyo na kupaki sanjari na gari la Musa, wakashuka wote.





    Walikwenda kukaa nyuma ya meza waliyokaa mama Shua na Musa na walipokaa, Musa aliwaona kwa sababu aliwafesi, mama Shua aliwapa mgongo…



    “Mama Shua tumekwisha…mume wako na jamaa mwingine wamekaa nyuma yako,” alisema Musa kwa sauti ya chini huku akiangalia sakafuni kwa aibu kubwa…



    “Wewe Musa…unasema kweli?” aliuliza mama Shua…



    “Mungu vile! Halafu inaonekana wamejua wewe upo hapa. Na mbaya zaidi walipokaa, huwezi kukimbia wala kufanya lolote zaidi ya kuonekana.



    Baba Shua, kwa hasira kubwa aliamua kumpigia simu Maua na kumwelekeza alipo kisha akamuuliza kama anaweza kumfuata…



    “Jamani kwa nini nisije? Nakuja sasa hivi…” alisema Maua…



    “Chukua teksi nitalipa,” alisema baba Shua…



    “Teksi ya nini? Nachukua bodaboda tu…”



    “Ha! Jamani mke wangu, yaani uchukue bodaboda kweli wakati gari lipo ndiyo maana kwa hadhi yako nikasema uchukue teksi…”



    Benny bwana, mimi kuwa na hicho kigari si kwamba nina hadhi ya juu, niko sawa tu mbona. Nakuja sasa hivi.”



    Baba Shua alimsimulia Jome kwamba, Maua atafikia pale muda si mrefu…



    “Safi sana…safi sana…nadhani sasa itakuwa ngoma droo. Mwenye chuki atajulikana,” alisema Jome.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ***



    Pale kwenye meza yao, mama Shua alikuwa akitokwa na jasho, lakini hakuwa na la kufanya. Mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi. Alifikiria nini kitatokea endapo mumewe ataamua kufanya fumanizi hotelini na wateja kibao wakishuhudia…



    “Musa nifanyeje?” aliuliza Maua…



    “Kwa kweli huna la kufanya, maana unajua hata ukisema uondoke atakuona, ukisema uende uani, atakuona. Yaani wapo hapo nyuma yako,” alisema Musa kwa sauti ya chini sana ili asisikike.



    Dakika kumi mbele, Maua aliwasili. Kweli alishuka akiwa kwenye usafiri wa bodaboda, akalipa, akaingia ndani kumfuata baba Shua…



    “Sikia mama Shua…sasa kuna dada mmoja ameingia, naona anakuja kukaa nao,” Musa alimwambia mama Shua…



    “Kweli? Atakuwa nani? Unaweza kumpiga picha kwa simu nikamwona?”



    “Yeah! Ngoja nifanye hivyo…da! Halafu anambusu mume wako…na yeye anambusu pia…sasa anavuta kiti na kukaa jirani na mume wako…” Musa alimpa picha kamili mama Shua huku akimpiga picha…



    “Huyu hapa,” alimwonesha mama Shua picha hiyo…



    “Haa! Namjua huyu dada, anaitwa Maua. Ndiyo alikuwa amuoe kabla yangu…ina maana baba Shua amerudiana na huyu mwanamke kweli..? Haiwezekani,” alisema akilia mama Shua.



    ***



    “My sweetheart Maua,” aliita baba Shua…



    “Yes baby…”



    “Unajua kwa nini nimekuita hapa?”



    “No! Sijui kama kuna kitu zaidi ya kuamini umependa uwe na mimi muda huu.”



    “Hilo ni moja na dogo sana. Ila kubwa ni kwamba, mke mwenzio yule pale. Na yupo na yule kijana niliyekwambia ndiye anayemzuzua.”



    “Haa! Benny…”



    “Nini Maua?”



    “Yaani unashuhudia hayo na unafumbia macho? Au umeshakwenda kuzungumza nao?”



    “Hapana shemeji Maua…unajua huyu bwana kwa hali ilipofikia, akisema aanze kufuatilia mpaka kuzungumza au kufumania atavuruga fiucha yake bure, hii ndiyo inatakiwa. Uamuzi ni wake sasa, aamue kuendelea kuwa na mwanamke huyu au aachane naye…wewe si upo bwana,” alidakia Jome, Maua akaachia tabasamu jepesi, hasa baada ya kusikia yeye yupo.



    Baba Shua akabakia kumkazia macho Maua kama anayesema moyoni ‘maneno ya Jome ni kweli kabisa.’



    “Sawa, lakini sasa mwisho wake ni nini?” aliuliza Maua…

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Dawa ya wale ni kuwaita hapa kisha kukabidhiana. Benny mkabidhi mama Shua kwa yule kijana halafu wewe jikabidhi kwa Maua hapa,” alisema Jome.



    “Hapana, mimi ninachotaka ufanya si hicho. Nataka wakati wa kuondoka nikawaage lakini safari yangu breki ya kwanza ni nyumbani, nikachukue nguo zangu niondoke. Sikuwa na lengo la kutengana na yeye, ila kwa tabia yake imebidi. Hata kujitokeza kwa Maua naamini ni Mungu tu kwani kaja wakati mwafaka…



    “Kwa mwanaume yeyote yule hawezi kuvumilia ujinga wa huyu mwanamke. Kweli kabisa mke ndani ya nyumba anakwenda kuingia kwenye chumba cha mpangaji mwingine na kufanya usaliti wa wazi? Ningekuwa mtu mwingine ningevunja ule mlango na kuua…”



    “Kweli kabisa,” alidakia Jome.



    Walikunywa ndani ya nusu saa tu, ukafika muda wa kuondoka. Wakasimama wote, wote wakaenda kwenye meza ya akina mama Shua…



    “Jamani tumechelewa kuwasalimia lakini kwa sababu tunaondoka acha tuwape hai,” alisema baba Shua huku akiwapa mkono akianzia na Musa.



    “Poapoa,” alijibu Musa kwa kujikaza sana. Mama Shua aliinama kwa aibu…



    “Za leo?” Maua alimsalimia Musa tu, akaondoka.



    Jome yeye hakusalimia yeyote yule, naye akafuata nyuma ya Maua. Baba Shua akafuatia, wakaingia kwenye gari na kuondoka.



    ***



    “Musa,” aliita mama Shua…



    “Vipi?”



    “Ee! Chuzi ndiyo hilo sasa…hakuna kuonja.”

    “Una maana gani mama Shua?”

    “Nimeshaachika, hakuna tena ndoa.



    Sasa wewe uliyeniharibia usije ukaniacha. Ulikuwa unanitaka kwa machale ukimwogopa mwenye mali, sasa kaniacha ndiyo maana nasema chuzi ndiyo hilo hakuna kuonja,” alisema mama Shua kwa sauti ya uchungu huku machozi yakimchuruzika…

    “Mama Shua, kwanza nataka kukwambia siko tayari kuonekana mimi ndiye chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yako.”



    “Heee! Musa una akili kweli wewe? Yaani wewe ndiye chanzo halafu mara hii unataka kujitoa? Kwa taarifa yako sasa, mimi sijawahi kuchepuka tangu nimefunga ndoa. Ndiyo kwanza kwako…”



    “Kwani mimi na wewe mama Shua nani alianza kumtongoza mwenzake?” aliuliza Musa kwa sauti ya juu sana…

    “Wewe…”



    “Una kumbukumbu vizuri? Wewe hukumtuma msichana wako wa kazi aombe namba yangu ya simu? Wewe si ndiye ulikuwa unanitumia meseji zako za kuniuliza kama nimeshakula? Kwani kuna siku nilikwambia huwa nashinda njaa? We vipi bwana!” Sasa Musa alikuja juu kiasi kwamba, baadhi ya wateja walianza kuhisi kitu kutoka kwenye meza yao.

    ***

    Baba Shua alifika nyumbani, akachukua nguo, viatu, sendozi, mikanda, soksi na makufuli, akatumbukiza kwenye begi moja kubwa na kuondoka. Maua alimsubiri kwenye gari kwa mbali kidogo. Hapo walikuwa wameshatengana na Jome ambaye alishuka mahali na kuendelea na mambo yake.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Waliondoka, baba Shua ndiye aliyekuwa akiendesha mpaka Kimara nyumbani kwa Maua. Maua alifurahi kupita kiasi. Aliamini sasa Benny amekuwa wake tena kwani kati ya mambo yaliyokuwa yakimnyima raha ni kitendo cha umri kukatika na hakuna mchumba anayejitokeza…



    “Benny,” Maua aliita wakiwa wanakula…

    “Yes!”

    “Mpango wako ni nini juu na mkeo na mimi?”



    “Maua, acha kumtaja yule mwanamke kwenye akili yangu. Sitaki presha, sitaki aina yoyote ya mawazo juu yake. Mimi niko kwako Maua…Kama na wewe utakuja kunifanyia tukio kama lile, basi mtakuwa mmeamua kuniua,” alisema kwa hasira baba Shua huku akiwa amemtumbulia macho demu wake huyo.

    ***

    Kule hotelini, Musa alifika mahali akaondoka kwa hasira na kumwacha mama Shua ambaye alibaki akimwaga machozi tu. Ndoa chali, mpenzi naye chali! Alilia sana akijutia uovu wake.



    Alijikongoja, akaenda kupanda bodaboda mpaka nyumbani kwake ambapo alimkuta msichana wake wa kazi na mtoto wake, Shua wakiwa nje…

    “Vipi, mbona nje?” aliuliza mama Shua akiwa na hali ya mshangao…

    “Baba,” alisema Shua huku akinyoosha mkono.



    “Baba kafanyaje? Eti dada Shua anamaanisha nini?”

    “Baba kaja, akachukua begi kubwa, sijui ni nini, akaondoka akisema kwa heri ya kuonana. Sasa Shua alikuwa anamlilia.”



    Mama Shua alianguka chini na kupoteza fahamu. Alipokuja kuzinduka, alishangaa kujikuta katikati ya majirani akiwa amelala kwenye kochi kubwa sebuleni…

    “Pole mama Shua…”



    “Pole jirani yangu…”

    “Jamani mama Shua pole…kwani ni nini?” majirani walimpa pole nyingi.

    Alipepesa macho, akamwona mwanaye, Shua, akaanza kulia…

    “Jamani kwani nini mama Shua?” majirani walimuuliza…

    “Baba yake huyu ameondoka.”



    “Kwenda wapi?”

    “Eti amenihisi nina mwanaume mwingine kwa hiyo amekasirika na kuondoka zake,” mama Shua alijibu huku dhamira ikimuuma kwani alikuwa anaujua ukweli wote…

    “Isijekuwa yule kijana mmoja anayekupakupa lifti mama Shua?” aliuliza jirani mmoja…

    “Huohuyo…eti ndiyo bwanaangu…”



    “Lakini mama Shua kuna yule mama anayefanya kazi mahakamani, aliwahi kutuambia ameshakuona na huyo kijana kama mara tatu mkiwa mnatokea hotelini. Siku moja akasema amemuona huyohuyo kijana akiwa anatoka ndani kwako.”

    “Jamani humu ndani si ndiyo kapanga! Anakaa chumba kile pale. Lakini mimi si bwanaangu,” alijitetea mama Shua.



    Mara, Musa akaingia ghafla…

    “Wewe mama Shua wewe…usije ukarogwa kunitangazia eti mimi nimesababisha ndoa yako ivunjike,” alibwabwaja Musa na kuwafanya wale majirani kushtuka sana kusikia hivyo.

    Mama Shua akapoteza fahamu tena. Kuja kuzinduka, yuko mwenyewe, hata Shua hakuwepo. Alikuwa uani na dada wa kazi.

    ***

    Mama Shua alianza maisha mapya akiwa hana mume. Hakutaka kumwambia mama yake mzazi kijijini na wala baba Shua naye hakuwa na habari ya kuwaambia wakwe zake kwamba, amemmwaga binti yao.



    Mama Shua alipungua sana, akapoteza nuru yake ya kawaida. Waliomfahamu walishangaa kumwona alivyo. Kwanza, alikuwa mweusi bila ung’avu. Pili, alionesha dhahiri kwamba amekongoroka vibaya sana.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila kukicha, mama Shua alikuwa akimtumia meseji, akimpigia simu baba Shua lakini hakupokelewa wala kujibiwa sms zake.

    Ndoa ya mama Shua ikawa imevunjikia hap



    , kwani baada ya miezi sita kupita, wazazi wake wakajua kila kitu, naye akakiri lakini aliwaumiza sana wazazi hao.



    Mama Shua akawa mwanamke wa leo na huyu, kesho na yule, kama mpira. Heshima yake ilishuka kabisa kwani kuna siku wanaume wawili walipigana baa kwa sababu yake, akapasuliwa kichwani.



    Lakini mwisho wa yote, alikwenda kijijini kwao na kuangukia kwa wazazi wake kuhusu matendo yake, wakamsamehe kwa maana ya mzazi ni mzazi, wangefanyaje sasa! Lakini baba Shua alimkosa.



    MWISHO.

0 comments:

Post a Comment

Blog