Search This Blog

Monday, October 24, 2022

JAMANI DADA MARTHA... LOOO! - 4

 









    Chombezo : Jamani Dada Martha... Looo!

    Sehemu Ya Nne (4)



    ILIPOISHIA

    “Ngoja nimtumie ujumbe halafu ajibu, ndiyo mtaamini,” alisema mama Anna huku akiandika ujumbe wa simu…

    “Baby, nimefurahi sana kwa mechi ya leo. Halafu mechi ya kuichezea nyumbani kwako kama vile ni nzuri kuliko gesti au hotelini. Nimeipenda sana.”

    SONGA NAYO MBELE…

    Baada ya kuandika ujumbe huo, mama Anna aliwaonesha wenzake kisha akautuma kwenda kwenye namba ya Roi ambayo aliisevu kwenye simu yake kwa jina la ‘Wa Martha.’

    Ni ndani ya dakika tatu tu, meseji ikajibiwa…

    “Mimi pia nimeinjoi sana baby. Da! Yaani wewe ni kiboko, umeniteka kabisa Martha. Kesho twende tena nyumbani kwangu kama leo.”

    Mama Anna alipoisoma meseji hiyo akawaonesha wenzake, wakacheka mpaka kupiga mikono ‘pa…pa’…

    “Mimi nawaambieni, lazima wajina wangu aachike hivihivi anaona. Nimempa biti yule kaka ambazo mwenyewe hajawahi kupewa tangu azaliwe.”

    Baada ya mazungumzo yao, Martha aliingia ndani kwake na kuwaacha wenzake wakiendelea na mazungumzo.

    ***

    Roi alikaribishwa chumbani kwa Martha kwa mabusu mfululizo huku akipewa pole kwa kazi za mchana kutwa halafu akaambiwa…

    “Baby, nilikumbuka kwamba kule nyumbani kwako baada ya kufunga, funguo uliiweka kulekule au ulikuja nayo?” aliuliza Martha…

    “Iko kwenye gari.”

    “Nilipenda kwenda kufanya usafi baby, labda kesho sasa.”

    “Kesho sawa, utakwenda. Saa ngapi?”

    “Jioni, kwenye saa kumi hivi.”

    ***

    Usiku wa siku hiyo, Martha alihisi kitu tofauti kwa Roi. Licha ya kumshikashika ili achaji lakini alionekana hana habari na kwanza alikuwa mbali…

    “Sweet, mbona kama upo mbali kimawazo?” aliuliza Martha…

    “Hapana, kuchoka tu na shughuli.”

    “Mmh! Baby jamani! Sasa ukichoka hivyo mimi nitapataje haki yangu?”

    “Kesho bwana,” alisema Roi akilala baada ya kutoka kuoga.

    ***

    Saa kumi na mbili, Martha alimka na kuamza kumshikashika Roi sehemu mbalimbali za mwili, hasa zile zenye kuamsha joto la mahaba. Roi alimgeukia, wakapashana joto zaidi na kuingia uwanjani kusakata mechi.

    Kulikucha kabisa, Martha alitoka kwa lengo la kumtengea maji ya kuoga jamaa yake ambapo alikutana na mama Anna…

    “Mambo mama Anna?” alisalimia Martha…

    “Poa, umeamkaje?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ah! Mi mzima bwana. vipi shemeji yangu?”

    “Ameamka salama, anataka kuondoka kwenda kazini kwake muda si mrefu, namwekea maji ya kuoga.”

    “Sawasawa, lazima upalilie bwana. Waoaji siku hizi hakuna,” alisema mama Anna akiingia ndani kwake. Lengo lake lilikuwa ni kumtumia meseji Roi kwani alijua Martha hatarudi muda ule chumbani…

    “Baby umeamkaje?” alituma meseji Mama Anna.

    “Poa, vipi wewe sweet, umeamkaje?”

    “Mimi mzima tu. Ni kukumisi tu.”

    “Mh! Je, mimi? Yaani natamani tungelala wote.”

    “Usijali baby, kuna siku. Unakwenda kazini?”

    “Yeah! Ndiyo nataka kujiandaa.”

    “Leo vipi, tutaonana baby wangu?”

    “Muhimu, si nilikwambia muda ule mpenzi wangu!”

    “Saa ngapi na wapi?”

    “Nitakujibu maana…” Roi aliikata meseji hiyo na kumpa wakati mgumu mama Anna kutafuta kwa nini meseji iliishia kwenye maana…

    “Maana nini tena baby?”

    “Nitakwambia Martha.”

    Roi alisema maana kwa sababu, jana yake, Martha wake alitaka funguo ili akafanye usafi nyumbani kwake siku hiyo jioni.

    ***

    Roi alitoka kitandani kwenda kuoga ambapo uani alikutana na wale wapangaji wenzake na Martha akiwemo mama Anna…

    “Jamani mmeamkaje?” alisalimia Roi akiwa ndani ya taulo tu, kifua wazi. Alishangaa kuwaona wanawake wote wakimtumbulia macho yeye tena waziwazi na si kwa kuibia…

    “Tumeamka salama, sijui wewe?” walimjibu, lakini mama Anna akaenda mbele zaidi kwa kusema…

    “Sijui wewe baby wangu.”

    Wakati anamalizia kusema baby wangu, Martha alitokea, akasikia.

    Ili kuonesha kwamba alisikia kitu kisicho cha kawaida, Martha alimtumbulia macho mama Anna kama anayemuuliza unasemaje wewe?

    “Vipi wajina?” mama Anna alijibalaguza kiaina kwani hata yeye alihisi maneno yake yalisikika na Martha…

    “Poa tu,” Martha alijibu kwa mkato sana tena akiwa ameuelekeza uso wake chini.

    Wakati huo, Roi alishazama bafuni kuoga lakini naye akijua maneno ya mwanamke huyo yamesikika na Martha…

    “Hawa wanawake wa uswahilini hawa. Yaani kuvumilia hawawezi kabisa,” alisema moyoni Roi akiwa ameshaanza kuoga.

    ***

    “Baby,” Martha alimwita Roi chumbani akiwa amekaa kwenye kitanda…

    “Yes baby…”

    “Yule mwanamke pale uani alikuitaje?”

    “Yupi?”

    “Yule mama Anna.”

    “Mama ni yupi kati ya wale?” Roi alijizungusha huku akijua anazungumziwa nani.



    “Yule mwenye umbo namba nane!”

    “Mi sikumsikia, kwani alisemaje baby?”

    “Ha! Una uhakika sweet? Mi nimemsikia akikusalimia kwa kukwambia sijui wewe baby?”

    “Mh! Kweli anaweza kunisalimia hivyo mimi? Mbona sifahamiani naye zaidi ya hapa kwako. Sasa mimi niwe baby wake kivipi jamani?”

    “Ndiyo nimeshangaa pale baby.”

    ***

    Roi aliondoka kwenda kwenye shughuli zake, nyuma Martha aliamua kuumiza kichwa kuhusu mama Anna.

    Kuna wakati alivizia mama Anna yuko bize, akamwingia mmoja wa wapangaji wenzake...

    “Mambo shosti?”

    “Poa, vipi Martha?”

    “Poa. Hivi, asubuhi pale wewe si ulikuwepo uani wakati mgeni wangu anakwenda kuoga?”

    “Nilikuwepo ndiyo, vipi kwani?”

    “Hivi, mama Anna alimsalimia vipi mgeni wangu?” aliuliza Martha huku akimkazia macho mpangaji huyo.

    “Alimsalimia kawaida tu. Alimwambia salama sijui wewe hapo?”

    “Kweli?”

    “Kweli. Kwani wewe ulisikiaje?”

    “Mimi nilisikia akisema salama sijui wewe honey.”

    “Hapana, alisema sijui wewe hapo.”

    “Oke basi, lakini usimwambie chochote mama Anna.”

    “Sawa, wala simwambii.”

    ***

    Jioni, saa kumi na moja, Roi ndiye aliyeanza kumtumia meseji mama Anna ambapo mchana kutwa wa siku hiyo hawakuwasiliana...

    “Mzima baby?”

    “Mzima sweet, wewe?”

    “Mzima. Wapi hiyo?”

    “Niko home, wewe?”

    “Mimi nipo njiani. Unapakumbuka vizuri nyumbani kwangu?”

    “Ndiyo. Kumetokea nini kwani baby wangu?”

    “Unaweza kuja?”

    “Sasa hivi?”

    “Yes, mimi naelekea huko muda si mrefu nitakuwa nimefika.”

    “Poapoa.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mama Anna aliwafuata wenzake, akawatonya kuhusu kuitwa na bwana wa Martha nyumbani kwake...

    “Safi sana. Nenda katese mwanamke mwenzetu.”

    “Sawa, baadaye basi.”

    Mama Anna alibeba nguo pea moja. Alipanga atakazovaa akienda siyo atakazovaa akirudi.

    Wakati anatoka, Martha alikuwa amekaa nje na wapangaji wenzake...

    “Mwenzetu mtoko wa wapi huo?” aliuliza Martha.

    “Kwa shemeji yako.”

    “Msalimie basi, siku nyingine mlete tumwone.”

    “Wewe hujatuonesha wako lakini. Sanasana huyu wa sasa unasema ni kaka yako.”

    “Ee! Kaka yangu jamani. Mjue ni kaka yangu, lakini mbona huwa mnamuita shemeji wakati niliwaambia ni kaka yangu!” alisisitiza Martha.

    Walicheka wote, mama Anna akatokomea zake kwa kuchukua Bajaj hadi nyumbani kwa Roi. Anashuka tu, Roi naye anaegesha gari hapo.

    Waliingia sambamba ndani huku Roi akimuuliza habari za alikotoka...

    “Martha hajakuuliza kitu?”

    “Hapana, kwani kuna kitu?”

    “Aliniuliza asubuhi vile ulivyonisalimia kwa kuniita baby.”

    “Kweli?” alishtuka mama Anna...

    “Kweli, lakini usijali, yaliisha palepale. Alijua alisikia vibaya.”

    Wawili hao hawakutaka kupoteza muda, waliingia chumbani, wakachojoana na wakapanda kitandani kuanza mechi.

    Safari hii, mama Anna aliongeza gia namba kubwa zaidi kuliko jana yake. Mfano, wakiwa uwanjani, alimtoa kitandani Roi wakatembea mpaka bafuni na kurudi huku wakiendelea kucheka, Roi akapata ushindi wa kwanza ile anafika tu kitandani. Alianguka chini kwa jinsi alivyochokeshwa.

    ***

    Martha kule nyumbani, akakumbuka kwamba alipanga kwenda kufanya usafi nyumbani kwa Roi, hivyo alijiandaa, akatoka akipanga kwamba atakapokaribia kufika ampigie simu Roi kumwambia ampitishie funguo za nyumba



    Aliwaaga wapangaji wenzake akisema anatoka mara moja...

    “Jamani natoka, nitarudi lakini,” alisema Martha akiwa tayari kwenye ngazi.

    “Poapoa.”

    Martha alichukua usafiri wa Bajaj, akapanda hadi alipokuwa akikaribia nyumbani kwa Roi, akampigia simu...

    “Uko wapi baby?”

    “Niko Magomeni.”

    “Mi nakaribia kwako, nipitishie funguo nifanye usafi.”

    Roi moyo ulimlipuka puu! Maana alijua Martha atakumbana na mama Anna, kama si nje basi mitaa hiyo.

    “Mh!” aligunia moyoni, akatafuta uongo wake...

    “Funguo niliziacha nyumbani kwako mbona.”

    “He! Kweli?”

    “Yes! Kwenye nini?”

    “Kwenye begi langu, kama siyo basi kwenye suruali niliyovaa jana. Kacheki.”

    Martha alimwamuru dereva wa Bajaj ageuze amrudishe nyumbani kwake. Wakati anageuza, mama Anna alimwona mita chache, yeye alikaa kwenye kiduka jirani na kwa Roi, akauchuna, akazungusha sura.

    Alipoiona Bajaj imepotea, akampigia simu mpangaji mmoja...

    “Martha yuko hapo?”

    “Ametoka.”

    “Alisema anakwenda wapi?”

    “Hajasema, kasema natoka kidogo tu. Vipi kwani?”

    “Mh! Kaja mpaka nje kwa huyu jamaa yake, kageuza. Yuko na Bajaj.”

    Wakati mama Anna akiendelea kuongea na mpangaji mwenzake huyo, mara simu yake ikawa inaita, kuangalia ni Roi, akakata simu hiyo na kupokea ya Roi...

    “Niambie baba.”

    “Uko wapi mama?”

    “Niko nje kwako hapa.”

    “Ha! Martha hajakuona kweli? Maana kaja hapo.”

    “Nimemuona, lakini yeye hajaniona. Kwani kaja kufanya nini tena?”

    “Eti alikuja kufanya usafi. Nimemdanganya kwamba funguo ipo nyumbani kwake.”

    “Kwa hiyo kaifuata?”

    “Kaifuata. Sasa mimi nakuja hapo dakika tano tu.”

    “Poa.”

    Baada ya dakika tano kweli, Roi akawa amefika nyumbani kwake, akashuka, akafungua geti na kuingiza gari ndani. Akamwingiza na mama Anna ndani, tena mpaka chumbani.

    “Uzuri wake hata akija, hawezi kuliona gari ndani. Nitamwambia niko njiani bado,” alisema Roi kwa sauti ya kuibiaibia.

    Martha alifika na kuangalia funguo sehemu zote alizoambiwa, hakuziona, akampigia simu...

    “Baby, sijaona funguo bwana, utakuwa nazo kwenye gari, hebu angalia vizuri.”

    “Ngoja niangalie.”

    “Kwani uko wapi?”

    “Nipo barabarani bado.”

    “Poa.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Roi alifunga milango yote, akazama chumbani ambako alimkuta mama Anna akiwa amejilaza na ameshajichojoa nguo zote. Alikuwa kama alivyozaliwa. Na kwa kujua hilo, alipomwona Roi ameingia, akajitingisha makusudi pale kitandani, Roi hoi. Alianza kuhema kimahaba.

    “Si unaoga kwanza baba?” aliuliza mama Anna akiitoa sauti kwa kupitia kwenye tundu za pua.

    “Yes,” Roi alisema kwa sauti nzito huku macho yako kwenye mwili wa mama Anna pale kitandani.

    Roi alizivua nguo zake na kuzitupa chini kama vile hatazivaa tena katika maisha yake...

    “Teh! Teh! Teh!” alichekacheka kwa kicheko cha uchu huku akimfuata mwanamke huyo pale kitandani...

    “Jamani baba, si umesema unakwenda kuoga kwanza.”

    “Yeah! Lakini kuna nini kama nita...nita naniihii kabla sijakwenda kuoga..? Teh! Teh!” Roi alibabaika. Hapo tayari alikuwa mwilini mwa mama Anna. Alilala na kumpapasapapasa sehemu mbalimbali za mwili.

    Mama Anna naye akachangamka maana aliguswa, akapatwa na hisia za mapenzi, hasa kwa joto la Roi...

    “Kwa hiyo utaoga baadaye?” aliuliza mama Anna...

    “Au ngoja nikaoge sasa hivi,” alisema Roi, mama Anna akamzuia maana sasa na yeye mzuka si ulishapanda!

    “Hakuna hapa, kama ungetaka ungekwenda tangu muda ule. Mimi mwenzio tayari sasa,” alisema mama Anna.

    “Tayari nini?” aliuliza Roi akijifanya hajui lakini ukweli ni kwamba alikuwa anajua tayari nini.

    “Kwani hujui?”

    “Sijui,” alijibu Roi.

    Mama Anna akapeleka mkono wake mmoja na kushika maiki akiashiria utayari wake uko wapi.

    Roi naye akaunganisha hisia, wakabilingishana mpaka wote wakawa hoi, wanahema tu. Mama Anna akavuta mpira uwanjani, mchezo ukaanza kupigwa huku ushangiliaji ukiwa mkubwa kwa pande zote mbili.

    Maneno yote, mama Anna aliyatumia, Roi akawa kama amepungukiwa akili, alisema yasiyosemwa.

    ***

    Martha alipoona muda unakwenda aliamua kutoka tena akiamini, Roi alishaziona funguo na sasa atapitia nyumbani kwake ili wakutane.

    Alipanda Bajaj tena mbele ya wale wapangaji wenzake.

    Ile anapotea tu, yule mpangaji aliyepigiwa simu na mama Anna akamtumia meseji mama Anna...

    “Martha katoka hapa tena, nahisi anakuja hukohuko.”

    Mama Anna hakupata nafasi ya kuisoma meseji hiyo kwani wakati inaingia ndiyo kwanza yeye alikuwa katikati ya mashambulizi uwanjani akitafuta ushindi na alishatangaza kwamba anakaribia kuupata.

    Hata alipoupata, Roi hakumwachia ili na yeye apate pointi yake moja ili kusiwe na wa kumzidi nguvu mwenzake. Mama Anna alitumia ufundi kidogo tu, Roi akawa akihangaika mpaka jasho jembamba likamchuruzika, ambapo mama Anna alilimudu kuliondosha kwa taulo.

    ***

    Martha alifika nje ya nyumba na kumpigia simu Roi. Simu iliita kule chumbani, Roi kwa vile alishashinda, akatoka kwa mama Anna na kuiwahi...

    “Du! Wajina wako anapiga,” alisema.

    “Sasa. Anaweza kuwa nje?” aliuliza mama Anna...

    “Inawezekana,” alisema Roi lakini hakuipokea simu hiyo.

    Mama Anna naye akakumbuka, simu yake akaifuata, akakutana na ile meseji. Alipoisoma, akamwonesha Roi...

    “Martha katoka hapa tena, nahisi anakuja hukohuko.”

    Roi alitumbua macho pima, akasimama akiwaza, akasema...

    “Kwa hiyo yupo nje hapo?”

    “Ndiyo maana yake,” alijibu mama Anna.

    Martha alishangaa simu ya Roi kuita bila kupokelewa kwani si kawaida yake.

    Akaenda kwenye kile kiduka cha jirani...

    “Dogo hujambo?” alimsalimia muuzaji.

    “Sijambo.”

    “Eti, huyu kaka anayekaa hapa huwa anafika muda gani?”





    “Mh! We ni nani kwani?”

    “Mgeni wake.”

    “Kutoka wapi?”

    “Tanga.”

    Muuza duka huyo alimkodolea macho Martha akiwa anaonekana haamini kama alitokea Tanga. Tanga bila hata kibegi cha nguo!!

    “Kwani namba yake ya simu huna?” aliuliza muuza duka huyo.

    “Nampigia hapokei. Nikasema nije hadi hapa ili kama anakuja muda huu nimsubiri kama si muda wake nikatafute gesti ya kulala.

    Muuza duka huyo alijua kuna kitu kilimfanya Roi asipokee simu. Na kitu hicho si kingine ni jamaa huyo kuzama ndani na mwanamke mwingine aliyekuwa amekaa kwenye benchi nje ya duka lake.

    Kwa hiyo uamuzi ulikuwa kwake. Aseme ukweli au adanganye.

    Moyoni mwake aliona Roi mwenyewe alitakiwa kuwa muwazi katika mipango yake kuhusu wanawake. Si vizuri kugonganisha...

    ‘’Mimi nimemwona kaingia ndani muda si mrefu,’ alisema muuzaji huyo.

    Martha akashangaa...

    “Kwa miguu?” aliuliza.

    “Na gari.”

    Martha alitupia macho kwenye geti na kubaini kwamba, ni kweli gari linaweza kuwemo ndani halafu mtu aliye nje asilione...

    “Aliingia na nani?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mwanamke mmoja hivi. Alimsubiri kwa muda mrefu hapohapo nje.”

    “Mwanamke mmoja hivi! Kavaaje?”

    “Huyo mwanamke kavaa haya magauni yenu ya siku hizi, marefu mpaka miguuni, amelaza nywele kwa nyuma, mweupe kiasi, ana figa namba nane.”

    Kwa haraka sana, Martha alimuweka kichwani mama Anna kwani anakumbuka ndiye aliyevaa hivyo inavyosemwa.

    “Huyo ni mama Anna tu. Yaani kumbe...mh! Yaani mama Anna na Roi ni wapenzi? Mbona siamini. Wameanzaje kwanza?”

    Martha aliinua simu yake akampigia mpangaji mmoja na kuzungumza naye...

    “Hivi unaweza kuamini mama Anna alipotoka hapo kumbe amekuja nyumbani kwa yule mtu wangu?”

    “Kweli?”

    “Kabisa. Nimepewa ushahidi wote.”

    “Kwa hiyo?”

    “Wamo ndani na geti limefungwa.”

    “Mh! Mama Anna naye bwana. Ana maana gani sasa kufanya hivyo kwa mtu wa karibu kama wewe?”

    “Ndiyo hapo sasa. Mimi leo sitoki hapa getini. Nipo tayari hata kulala hapahapa,” alisema kwa uchungu Martha na kukata simu.

    ***

    Roi na mama Anna walikuwa chumbani sasa, kitandani, wakigalagazana kwa mahaba mazito huku mwanamke huyo akilia kilio cha uongo ili kumkoleza zaidi mwanaume huyo pale kitandani.

    Wote walikuwa wamelegea macho kwani kwa mama Anna yeye alishajua jinsi ya kumnasa Roi huku yeye Roi akiwa hoi bin taaban.

    Simu ya mama Anna iliita mpaka ikakata, ikaita tena mpaka ikakata, ikaita tena...

    “Mh! Hiyo simu itakuwa ya umuhimu kwangu,” alisema Roi na kumtaka mama Anna aipokee...

    “Hakuna lolote, haina umuhimu wowote, ngoja niizime tu,” alisema mama Anna akiifuata.

    Kabla hajaizima aliangalia missed calls akakuta mbili na zote ni za wapangaji wenzake, akahisi kitu. Akampigia wa kwanza...

    “Vipi mama nanihii...”

    “Mwenzangu, Martha yupo getini. Kasema ana ushahidi umo ndani kwa jamaa yake na hatoki mpaka kesho asubuhi.”

    Palepale mama Anna alikata simu, akamwangalia Roi. Naye Roi akamuuliza...

    “Vipi kwani?”

    “Martha yupo getini. Lakini ishu si hiyo bali amejua mimi nimo ndani, eti ana ushahidi.”

    Roi alikumbuka kwamba, atakuwa ameambiwa na muuza duka ambaye alishuhudia kila kitu...

    “Mmh! Atakuwa ameambiwa na muuza duka. Loo! Sasa?”

    “Hata sijui. Kwani wewe hofu yako ipo kwa kiasi gani?” mama Anna alimuuliza Roi.

    “Mimi sina wasiwasi wowote ule. Nimeamua kuwa na wewe japo kibinadamu nitakuwa nimefanya makosa makubwa, kumuumiza mtu jambo ambalo silipendi katika maisha yangu,” alisema Roi kwa sauti ya upole.

    Alitoka kitandani, akavaa. Mama Anna naye akatoka kitandani, akamfuata kwa nyuma yeye akiwa amejizungusha upande wa kanga. Walifika sebuleni, wakaangalia kwa nje kupitia nafasi ya matundu ya ukuta wa fensi. Walimwona Martha amesimama dukani akizungumza na muuza duka.

    Sura ya Martha ilitafsiri uchungu wa maumivu ya kutendwa. Ikawa kama imejikunja, Roi akahisi huruma...

    “Martha... Wajina wako anaumia sana. Sasa itabidi nikutoe kiaina. Pita mlango wa nyuma, nenda mahali hapo nyuma kuna baa, kakae.”

    “Mh!” Aliguna mama Anna, akatoa wazo...

    “Sawa lakini turudi chumbani, nipe haki yangu kwanza ndiyo nitoke, siwezi kutoka hivihivi wakati uliishaanza kunipandisha mzuka wangu na mzuka wangu ukinipanda mimi akili zinachanganyikiwa kabisa.”

    “Kuhusu hilo tu, twende sasa hivi.”

    Walikwenda chumbani ambako Roi aliikuta simu yake ikiendelea kuita kwa namba ya Martha.

    Mama Anna alikimbilia moja kwa moja kwenye kitanda huku akitupa kanga chini.

    Alipokuwa juu ya kitanda akakaa mkao wa mechi tayari akijua anatakiwa kutoka ndani ya nyumba hiyo lakini moyoni alihakikisha anatoa mapigo ambayo, Roi anaweza kuamua asitoke tena na Martha kama kulala nje ya geti alale tu.

    Roi, kuona mkao wa mama Anna alichanganyikiwa. Kama paka aliyeona panya. Akaenda kitandani kwa staili ya kuruka kama golikipa wa timu maarufu ya Ulaya...puu!!





    Palepale alianza kuserebuka na mchezo huku mama Anna akimwangalia kwa hisia kali kama vile alikuwa akitumbuliwa jipu.

    Mama Anna aliamua kujilegeza kabisa hivyo alitoa ushirikiano wa hali ya juu bila kuonesha dalili hata ya chembe kwamba kuna jambo hakubaliani na Roi...

    “E...eti baby,” aliita Roi...

    “Niambie baba...”

    “Unaweza kuhama pale?”

    “Kuhamia wapi baba angu?”

    “Nitakaposema mimi?”

    “Naweza ndiyo mume wangu.”

    Roi kuitwa mume ndiyo kabisa, akajikuta anawewesekea uwanjani na kelele za mahaba kama vile yeye ndiye mama Anna.

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kule nje, Martha alitawala benchi la nje ya duka, mawazo yake yalikuwa usahihi wa mama Anna kuwepo au kutokuwepo ndani ya nyumba ya Roi...

    “Ina maana kumbe niliposema nilimsikia mama Anna akimwita Roi baby nilikuwa sahihi? Lakini hawa walikutana wapi mpaka wakafahamiana?

    “Kwa pale nyumbani hapana, haiwezekani. Lini kwanza? Na ilikuaje? Siku zote, Roi anakuwepo wakati ambao na mimi nipo, akitoka kurudi usiku...

    “Halafu pia mbona si muda mrefu, Roi kaja kwangu! Hawa huenda wanajuana kabla ya hapa. Itakuwa hivyo, wanajuana kabla ya hapa,” aliwaza moyoni Martha akijihisi unyonge f’lani hivi.

    “Lakini wewe Mangi utakuwa unamjua vizuri sana huyu kama anayeishi hapa. Hivi, ni mwadilifu kiasi gani?” Martha alimuuliza muuza duka...

    “Nani, Evender?” muuza duka aliuliza naye...

    “Kwani huyu kaka mwenye nyumba hii anaitwa Evender?”

    “Ndiyo.”

    “Mh! Siyo Roi?”

    “Mh! Mi silijui jina la Roi, namjua kama Evender.”

    Martha alianza kuingiwa na wasiwasi zaidi. Akahisi huenda Roi kujiita Roi alimwingiza mkenge. Na kama ni kweli halafu mpaka wameingia kwenye uhusiano hakusema ukweli wa jina lake, Martha alianza kuona kumbe alikutana na mwanaume tapeli...

    “Labda ni jina la mtaani,” alisema Martha na kuomba Mungu iwe hivyo.

    Mara mzee mmoja mteja aliwasili dukani hapo na kumwangalia sana usoni Martha...

    “We binti kama nakufahamu,” alisema mzee huyo...

    “Mimi sikufahamu.”

    “We siye mdogo wake Benard?”

    Ni kweli, Martha ana kaka yake anaitwa Benard. Ni machepele ile mbaya...

    “Kweli Benard ni kaka yangu,” alisema Martha...

    “Sasa je? Sasa Benard ni rafiki wa mtoto wangu, Mawazo. Akili zao kama sawasawa. Mimi nilikuona siku moja tu pale Kituo cha Polisi Urafiki wakati kaka yako na Mawazo walipowekwa ndani...”

    “Kweli, nimekumbuka,” alisema Martha akiwa amemkumbuka mzee huyo ambaye umri ulikwenda sana...

    “Haya! Mimi naishi nyumba ile ya tatu kutoka hapa. Hapa umefuata nini sasa?” aliuliza mzee huyo huku mkono wake mmoja ulioshika noti ya shilingi mia tano ukiwa umeshaingia kwenye dirisha la kuhudumiwa dukani hapo...

    “Nina shida na kaka mmoja anaishi nyumba hiyo yenye geti jekundu,” alisema Martha huku macho yake yakielekea kwenye nyumba ya Roi...

    “Nani, Ismaili?” aliuliza mzee huyo.

    “Kwani anaitwa Ismaili?”

    “Ee... ndiyo jina lake,” alisisitiza mzee huyo huku na yeye macho yake yakitua kwenye geti la nyumba hiyo.

    Martha na muuza duka wote wakabaki wametumbua macho...

    “Au wewe unamsema mwingine?” aliuliza Martha...

    “Jamani! Kwani kwenye nyumba hiyo kunaishi watu wangapi? Si mmoja tu, kijana kijana hivi...mweupe, ana gari lina rangi ya kijiko cha chai ‘silva’.”

    “Ee...” alikubali Martha...

    “Ndiyo, anaitwa Ismaili. We alikwambia anaitwaje?”

    “Mimi namjua kwa jina la Roi...”

    “Mh! Roi tangu lini? Yule anaitwa Ismail Twalib Mussa.”

    “Mimi namjua kwa jina la Evander,” alidakia kijana muuza duka.

    “Hakuna bwana. Anaitwa Ismail.”

    Mara, gari jeusi lilifika na kupaki getini kwa Roi, wakashuka wanaume wawili, wakiwa wamevaa suti nyeusi. Wakatembea kuelekea pale dukani. Wakasalimia wote kisha mmoja wao akauliza...

    “Jamani tuna shida na Edo...anaishi kwenye nyumba hii,” alisema akionesha kidole nyumba ya Roi...

    “Sisi hatujamwona...kwenye simu vipi?” alidakia mzee huyo...

    “Simu yake inaita tu hapokei,” alisema mmoja wa wanaume hao huku wakirudi ndani ya gari na kuondoka zao...

    “Sasa hawa jamaa wanasema anaitwa Edo...mimi najua anaitwa Ismaili...wewe unasema unamjua kwa jina la Roi...huyu muuza duka anasema anaitwa Evender. Huyu kijana si kawaida,” alisema mzee huyo akionekana kushangaa, akamwangalia Martha...

    “Kwani wewe binti, unamfahamu kivipi?” mzee huyo alimuuliza Martha huku akimshika mkono na kwenda naye kando...

    “Mimi ni jamaa yangu babu...”

    “Jamaa yako?”

    “Ndiyo babu, kwani vipi?”

    “Ha! Sasa mbona watu mtaani pote hapa wanajua ni kijana mwathirika.”

    “Mwathirika?” aliuliza kwa sauti Martha, macho yakapoteza uwezo wa kuona, akaanguka chini.

    ***

    Kule chumbani, sasa Roi alikuwa akikaribia ushindi wa pili na alishatangaza nia. Mama Anna alikuwa amemkaribisha kwa shangwe huku akimuuliza anataka kumhamishia sehemu gani katika Jiji la Dar es Salaam...CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Si...sinza ku...na kufaa...”

    “Sawa, tena Kwaremi...Kwaremi ndiyo kwenyewe,” alisema mama Anna huku mikono yake yote ikiwa mgongoni mwa Roi akimpa joto ambapo mlio wa geti kubwa la nje kugogwa ulisikika kwa nguvu...

    “Mungu wangu, atakuwa nani amejitoa ufahamu mpaka kuamua kugonga geti langu?” alijihoji Roi akiwa anatafuta namna ya kutoka kwa mama Anna.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog