Search This Blog

Monday, October 24, 2022

MWAJUMA UTAMU - 3

 







    Chombezo : Mwajuma Utamu

    Sehemu Ya Tatu (3)



    Mazungumzo yaliyokuwa yakizungumzwa mahali hapo yalikuwa ni ya kibiashara, Ibra muda wote alikuwa akanitazama.

    Nilitakiwa kufanya biashara ya uchangudoa na nilikubali kuifanya hivyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea nilikubaliana nacho bila wasiwasi wowote, niliamini ilikuwa ni biashara ambayo ingeweza kunipa utajiri wa haraka.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kwahiyo mnakula nini?" aliuliza Ibra wakati huo alimuita muhudumu akawa anasubiria oda yetu.

    "Mimi niletee mchemsho wa ndizi nyama," alisema Savela.

    "Mimi niletee chochote tu," nilijibu jibu lililowafanya wote wakacheka.

    "Hakuna chakula hicho, wewe sema unataka chakula gani?" aliniuliza Ibra.

    "Basi niletee Chips," nilisema.

    "Chips nini, kuna mayai, kuku, mishikaki au kavu unataka?" aliniuliza yule muhudumu, alikuwa ni wa kiume.

    "Chips mayai," nilimjibu kisha akamgeukia Ibra na kumuuliza huduma ya chakula ambacho alihitaji.

    "Hapana nipo sawa aisee, wewe wahudumie hawa warembo tu usijali," alijibu kisha yule muhudumu akaondoka, baada ya dakika kadhaa alirudi na vyakula tulivyomuagiza.

    Tulianza kula huku stori za hapa na pale zikiendelea, Savela aliniambia siku hiyo nilitakiwa kwenda kulala na Ibra.

    Kiukweli kila nilipokuwa nikimuangalia Ibra jinsi alivyokuwa akionekana halafu nilipokumbuka kuwa usiku huo nilitakiwa kwenda kulala naye nilihisi kuingiwa na uwoga.

    "Hutakiwi kuogopa kitu Mwajuma halafu tafadhali naomba usiniangushe," aliniambia Savela.

    "Sawa dada siwezi kukuangusha," nilimwambia kisha tukaendelea kula mpaka pale ambapo tulimaliza, Ibra akalipa bili ya chakula.

    "Kwahiyo nini kinachofuata?" aliuliza Ibra huku akimtazama Savela, hapohapo nikamuona Savela akinipa ishara ya kuniambia niondoke na Ibra.

    "Nitamrudisha asubuhi," alisema Ibra kisha akanishika mkono tukaanza kuondoka.

    "Sawa hakuna shida," alisema Savela.

    Tulifika mpaka alipokuwa amelipaki gari lake, tukapanda kisha tukaondoka.

    ****

    Safari yetu iliishia nje ya hoteli moja ya kifahari iliyokuwepo maeneo ya Sinza Makaburini. Hatukutembea umbali mrefu sana kutokea Sinza Afrika sana, ulikuwa ni mwendo kama wa dakika kumi na tano hivi tukawa tayari tumeshafika katika hoteli hiyo.

    Ibra hakutaka kupoteza muda, alichukua chumba na baada ya muda mfupi tukaingia ndani ya chumba hicho. Kila nilipokuwa nikimtazama Ibra nilikuwa nikiogopa, niliingiwa na wasiwasi, nilitamani masaa yakimbie ili niondoke mahali hapo.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tulipokuwa ndani ya chumba cha hoteli hiyo hakukuwa na stori nyingine alizoziongea Ibra zaidi ya mapenzi, umbo langu lilionekana kumchanganya kupita kawaida, muda wote alikuwa akinisifia.

    "Umewahi kulala na wanaume wangapi katika maisha yako?" aliniuliza.

    "Watatu tu," nilimjibu.

    "Kumbe mtoto bado mbichi kabisa?" aliniuliza.

    "Ndiyo," nilimjibu.

    "Leo nataka uniliwaze, nataka unipe mapenzi mpaka nimsahau mke wangu huko alipo," aliniambia huku akitabasamu.

    "Kumbe una mke?" nilimuuliza kwa mshangao.

    "Ndiyo nina mke lakini naishi kama sina mke."

    "Kivipi?"

    "Amepooza hivyo naishi naye kama sanamu tu, siwezi kufanya lolote lile," aliniambia huku akiniomba tusiyazungumzie hayo.

    Ibra hakutaka kupoteza muda, alianza kunipapasa huku akijaribu kunionyesha utundu aliyokuwa nao wa kunifundisha hesabu za 2x+3y.

    Nilisisimka mwili, hata hivyo sikutaka kubaki kuwa kama mwanafunzi wakati somo lenyewe nilikuwa nalifahamu tena zaidi yake.

    Nilikuwa nikifahamu mbinu na mahesabu yote ya kitandani. Hakukuwa na kitu kigeni kwangu, siku hiyo haikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kufanya mapenzi.

    Kila kitu nilichokuwa nikikifanya kilimshangaza sana Ibra, hakutaka kuamini kama nilifahamu mambo yote yale.

    Nisingependa kusimulia kila kitu nilichokifanya usiku huo kwasababu ya kuheshimu sheria za kimitandao ila nataka mfahamu kuwa siku hiyo nilifanikiwa kufanya mapenzi na Ibra tena kwa asilimia mia moja.

    Asubuhi ya siku iliyofuata tuliamka kisha tukaenda kuoga kwa pamoja, tulipomaliza tulijiandaa tayari kwa kuondoka.

    "Umenifurahisha sana mrembo, umenipa mapenzi ambayo sijawahi kupewa hapo kabla, hivi nani aliyekufundisha?" aliniuliza.

    "Hakuna mtu aliyenifundisha kufanya mapenzi," nilimjibu kwa kujiamini.

    Nilishangaa akitoa kiasi cha pesa kama laki mbili na nusu hivi kisha akanipa, nilipokea na kumshukuru.

    "Hutakiwi kusema asante, hiyo ni haki yako," aliniambia huku akikenua.

    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kulala na wanaume tofauti tofauti, kila siku nilikuwa nikifanya nao mapenzi na walikuwa wakinilipa vizuri.

    Katika kipindi hicho biashara ya uchangudoa ilionekana kuwa nzuri kwa kiasi fulani, ilikuwa ikinipa faida kubwa na lilikuwa ni jambo gumu kuiacha biashara hiyo kwani tayari ilikuwa ni sehemu moja ya maisha yangu. Kila kitu nilichokuwa nikikifanya, kuanzia kula yangu, kuvaa kwangu ilitokana na biashara hiyo.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kipindi hicho bado nilikuwa nikiishi nyumba moja na Savela, tangu alipoweza kunisaidia na kunishawishi mpaka nikajiingiza katika biashara ya uchangudoa.

    Jambo ambalo wengi wenu hamlifahamu kuhusu hii biashara ya uchangudoa ni biashara kama zilivyobiashara nyingine. Kuna wakati unaweza ukapata hasara au faida.

    Hakuna kipindi kigumu ambacho biashara inakuwa ngumu kufanyika kama kipindi cha hedhi, pale tunapokuwa katika siku zetu. Tunapata maumivu makali sana.

    Kila msichana anayejihusisha na biashara hii ya uchangudoa sikufichi kitu ambacho tunakichukia ni kwenda hedhi kila mwezi.

    Kipindi hicho biashara inakuwa ngumu kufanyika, maisha yanabadilika na ndiyo kipindi ambacho huwa tunasaidiana mpaka pale tunapokuwa sawa na biashara kuendelea kama kawaida.





    Nilikuwa nikifanya mapenzi na wanaume wanne na wakati mwingine nilikuwa nikifanya na wanaume sita kwa siku. Walikuwa wakinilipa vizuri.

    Kwa siku nilikuwa sikosi si chini ya laki moja na nusu, biashara ya siku hiyo ikiwa nzuri zaidi nilikuwa naingiza laki mbili.

    Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu kwa wakati huo, sikujali nililala na mwanaume wa aina gani, mwenye umri upi, mwembamba, mnene, mfupi au mrefu.

    Yoyote aliyejitokeza mwenye pesa nilienda kulala naye bila kujali lolote, nilihakikisha nafanya naye mapenzi kama sikutakiwa kufanya tena katika maisha yangu.

    Nilitengeneza kiasi kikubwa cha pesa tena ndani ya muda mfupi.Savela alionekana kukubuhu katika biashara ya uchangudoa, kipindi ambacho nilikuwa nikienda Sinza kujiuza yeye alibaki nyumbani, wanaume walikuwa wakimfuata.

    Sikutaka kuendelea kuishi nyumba moja na Savela, kwa kuwa nilifanikiwa kutengeneza kiasi kizuri cha pesa nilipanga kupanga nyumba yangu.

    Nilipomwambia Savela kuhusu mipango hiyo alionekana kufurahi, alinipongeza kwa hatua nzuri ambayo nilikuwa nimefikia.

    "Kwahiyo umepanga kuishi wapi?" aliniuliza.

    "Sinza," nilimjibu.

    "Sawa," aliniambia.

    Baada ya siku kadhaa kupita, nilitafuta dalali ya nyumba ambaye nilimuelezea nyumba niliyokuwa nikiihitaji.

    Dalali alionekana kuifahamu Sinza kiundani, baada ya kunisikiliza kwa muda mfupi akaniambia nyumba ilikuwepo tena kama ningezembea kuna mtu mwingine alikuwa akiihiitaji.

    "Iko wapi?" nilimuuliza.

    "Sinza kwa Remi," alinijibu.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Ni nzuri na itaendana na mimi?" nilimuuliza.

    "Ndiyo tena itaendana na hadhi yako," alinijibu.

    Sikutaka kupoteza muda, nilienda naye mpaka kwenye nyumba hiyo ili nione kama kweli yale aliyokuwa akinieleza kuhusu nyumba hiyo yalifanana.

    Kweli bana nilipofika nilikuta kila kitu nilichokuwa nikikihitaji katika nyumba, ilikuwa ni nyumba ya vyumba vitatu, sebule, chumba, jiko pamoja na choo.

    "Umeipenda?”

    "Ndiyo nimeipenda, ni nyumba nzuri."

    Baada ya makubaliano na dalali alinikutanisha na Mama mwenye nyumba hiyo, aliyejulikana kwa jina la Bi Latifa. Nilipokutana naye alinieleza kila kitu kuhusu nyumba yake, haikuwa na tatizo lolote na aliniambia angenipangishia kwa shilingi laki mbili na nusu kila mwezi.

    "Laki mbili na nusu?" nilimuuliza.

    "Ndiyo tena nimekupunguzia baada ya kukuona, nilikuwa naipangisha kwa laki tatu au Jafari hujamwambia?" aliniambia huku akimuuliza yule dalali.

    Kwa kuwa nilikuwa nina shida na uhitaji mkubwa wa nyumba kwa wakati huo sikutaka kuweka longolongo nyingi, nilichoamua kukifanya ni kuingia mkataba na Bi Latifa.

    Nilimlipa kiasi cha shilingi milioni moja na laki tano, kodi ya miezi sita kama mkataba alivyokuwa ukisema. Bi Latifa alifurahi sana baada ya kumpatia kiasi hicho cha pesa.

    Hatimaye niliyaanza maisha mpya katika nyumba hiyo, nilinunua kila kitu kilichokuwa kikihitajika ndani ya nyumba.

    Kwa maisha niliyokuwa nikiishi ilikuwa ni vigumu mtu kuamini kama nilikuwa ni changudoa ambaye nilivizia usiku ndipo niende kufanya biashara hiyo.

    ****

    Lengo la kuyaandika haya yote sina maana kwamba wasichana wenzangu wanaopitia maisha magumu, waamue kujiingiza kwenye biashara ya uchangudoa kwasababu tu inalipa la, isipokuwa nataka kuwaonyesha jinsi biashara hii ilivyokuwa na madhara makubwa na mwisho wake unavyokuwa mbaya.

    Nilikuwa tayari nimefanikiwa kupanga nyumba maeneo ya Sinza kwa Remi, maisha yalikuwa mazuri tu, kipindi hicho nilikuwa nimeshafungua akaunti benki na pesa nilizokuwa nikizipata nilikwenda kuzihifadhi huko.

    Nilikuwa katika mipango ya kununua kiwanja ambapo ningeanza ujenzi haraka iwezekanavyo hivyo nilihitaji kutengeneza kiasi kikubwa cha pesa.

    Hitaji langu kubwa lilikuwa ni kufanya biashara nyingi ambazo zingezidi kuniingizia pesa nyingi tofauti na biashara ya uchangudoa hivyo muda mwingi nilikuwa nikifikiria ni biashara gani ambayo nilitakiwa kuifanya katika kipindi hicho.

    Pesa ilizidi kuchukua nafasi kubwa sana kwani hata nilipokuwa nikiwaza biashara ambayo nilitakiwa kuifanya bado pesa ilihitajika.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Unajua unaweza ukamkuta mtu ana wazo zuri la kufanya biashara lakini unakuta hana pesa, anashindwa kutimiza lengo lake, anaona ugumu, anakata tamaa na mwisho wa siku anaamua kujiingiza kwenye mambo yasiyompendeza Mungu.

    Kila kitu kinachotokea katika maisha kina sababu yake, wakati mwingine Mungu anaamua kukupitisha katika wakati mgumu wa maisha ili kusudi akupime, aone utawezaje kuyastahimili.

    Ni Binadamu wachache sana ambao wanapopata matatizo kitu cha kwanza wanachokikumbuka ni Mungu pekee, wanasali na kumuomba huku wakiamini hicho ni kipindi cha mpito na muda wowote maisha yanaweza kubadilika.

    Sikuwa ni miongoni kati ya binadanu hao wenye imani thabiti, imani yangu ilikuwa ndogo mno. Kitu nilichokiamini katika maisha yangu ni pesa na ndiyo niliyoamini ingeweza kuyabadilisha maisha yangu, kama iliweza kusababisha nikapanga nyumba, nikaishi maisha mazuri basi niliamini pia ingeweza kunitimizia mahitaji yangu yote.

    Siku zilizidi kukatika huku nikiendelea kufanya biashara ya uchangudoa bila mtu yoyote kufahamu hilo, ilikuwa ni siri yangu na sikutaka mtu yoyote afahamu.

    Katika kipindi hicho nilipokuwa Sinza wanaume wengi walianza kunifukuzia, nilipata usumbufu mara kwa mara, kila mwanaume alihitaji kuwa na mimi.

    "Nakupenda Mwajuma," aliniambia mwanaume mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Samir.

    "Asante nashukuru kwa upendo," nilimjibu, akaonekana kuchukizwa na jibu langu lenye madharau.

    Samiri hakuwa ndiye mwanaume wa kwanza kumkataa, hapo kabla nilikuwa tayari nimeshawakataa wanaume kama watano hivi, sikutaka kuwa nao kimapenzi, niliwaambia wanipe pesa kisha nikaweza kulala nao kila mmoja kwa nafasi yake.

    "Kwahiyo?" aliniuliza.

    "Kuhusu nini?"

    "Nakupenda, nahitaji kuwa na wewe."

    "Una pesa?"

    "Ndiyo ila nikubalie kwanza niwe wako."

    "Sasa sikia hatutakiwi kuwa wapenzi, wewe nipe pesa nikupe mapenzi uondoke zako sitaki stress," nilimwambia kisha akaonekana kunishangaa.

    "Nini?" nilimuuliza.

    "Unajiuza?"

    "Ndiyo kama umeupenda mzigo ulipie ukalale nao usiku mzima," nilimjibu kisha nikageuka na kumtishia sehemu za nyuma ya maumbile yangu, nilifahamu nilijaaliwa chura hivyo nilifanya makusudi.

    Samir akazidi kuchanganyikiwa, kwa jinsi alivyokuwa akinitazama kwa macho, alionekana kuwa na hamu ya kuuona uhodari wangu kitandani.

    "Kwani ni bei gani?" Aliniuliza, jinsi alivyokuwa akionekana, alionekana kuwa ni mtu mwenye pesa zake.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Nipe laki mbili tukalale baby wangu," nilimjibu.

    "Hakuna shida," aliniambia kisha tukaenda kulala kwenye lodge moja, huko hakukuwa na maongezi mengi zaidi ya kufanya mapenzi tu.

    Nilikuwa nikijua kufanya mapenzi kuliko kitu chochote hapa duniani, nilijua kucheza mpira dakika zote tisini, mwanaume niliyelala naye nilihakikisha nafanya naye kila aina ya staili, nilijitoa ufahamu wakati wa kufanya mapenzi.

    Kama ni kukata viuno basi nilikata sana siku hiyo, yaani kila nilichokuwa nikikifanya kilikuwa ni cha tofauti.

    Hapa ndipo wanawake wengi wanapofeli, unakuta umeolewa na mwanaume na umeishi naye kwenye ndoa zaidi ya miaka kadhaa na tayari mmefanikiwa kupata watoto.

    Maisha yanazoeleka, unafika wakati hata tendo la ndoa unafanya kwa mazoea kwasababu umeshamzalia watoto mumeo basi unaamini hawezi kuchepuka, ataendelea kuwa wako.

    Maisha hayo mwanaume hawezi kuyavumilia, mwisho wa siku kisirikisiri atatafuta mchepuko wake au kwa wale wasiopenda kuwa na michepuko wanaangukia mikononi mwa Malaya, wanayofanyiwa wakati wa tendo la ndoa yanawashangaza na taratibu anajikuta akimsahau mke wake.







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog