Search This Blog

Monday, October 24, 2022

NYUMBA ILIYOJAA DHAMBI - 2

 







    Chombezo : Nyumba Iliyojaa Dhambi

    Sehemu Ya Pili (2)



     Nilishtuka sana, nilijiona kama mtu ambaye alikuwa kwenye mlango wa kuelekea kwenye mafanikio makubwa. Ile ilikuwa ni dhahabu, kipande kikubwa kabisa ambacho kama ningekiuza basi ningepata pesa nyingi mno na kuwa tajiri mkubwa.

    Hii ilimaanisha kwamba ningechukua msichana yeyote ninayemtaka na kulala naye, ningenunua simu kubwa zaidi, kujenga nyumba ya kifahari na kukunua gari moja matata kabisa.

    Nilifurahi lakini sikutakiwa kuwa na pupa, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kutaka kumfahamu zaidi yule mzee, nilimfanyia utu, hii haikumaanisha kwamba nilitakiwa niachache naye kisa tu nimepata almasi.

    Siku hiyo mchana nikaondoka na kuelekea hospitalini kumuona mzee huyo. Nilipofika hapo, nikakutana na manesi ambao walinipeleka mpaka kwenye chumba alichokuwa ambapo huko nikakutana na familia yake iliyokuwa na majonzi mno.

    Kulikuwa na mwanamke mmoja mtu mzima ambaye nahisi ndiye alikuwa mke wake, mabinti wawili wazuri wa umri wangu lakini pia kulikuwa na kijana mwingine.

    Nesi akanitambulisha kwao kwamba mimi ndiye niliyemuokoa kutoka kwa wauaji na kumchukua kumpeleka hospitalini hapo. Walifurahi na kunishukuru kwani mimi ndiye niliokoa maisha yake.

    Niliwahadithia kilichokuwa kimetokea, walinisikiliza na kunishangaa, haikuwa rahisi kwa binadamu wa kawaida kwenda kumuokoa mtu kwa watu waliokuwa na bastola na wakati hakukuwa na kitu mkononi.

    Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa urafiki wangu na familia hii, tuliendelea kuwa karibu na kukutana hospitalini hapo kuzungumza huku upande mwingine wa moyo wangu nikiwa na hamu ya kufahamu kuhusu yule mzee.

    “Mimi naitwa Nurat,” aliniambia msichana mmoja miongoni mwa wale watoto wa mzee yule.

    “Ulijitambulisha mule ndani!” nilimwambia huku nikicheka.

    “Najua! Ila ninahitaji kukufahamu zaidi!”

    “Naitwa Edward Francis! Nipo singo, sijaoa, sina demu, mpenzi wala mke,” nilimwambia huku nikitabasamu, akaanza kucheka.

    Huyu Nurat ambaye nilikuwa nazungumza naye alikuwa msichana mrembo mno, alikuwa na nywele ndefu, sura nyembamba na macho ya goroli. Kwa kumwangalia tu ilikuwa ni rahisi kusema kwamba alikuwa Mwarabu halisi na hata Kiswahili chake alichokuwa akiongea kilikuwa ni kile Kiswarabu kabisa.

    Nilimpenda kutoka moyoni, tangu nizaliwe sikuwahi kufanya mapenzi na Mwarabu, siyo hivyo tu, hata kushika kiuno chake sikuwahi kufanya hivyo.

    Nilikuwa na hamu kubwa, nilitamani kumwambia kwamba nilimpenda na hivyo nilihitaji penzi kutoka kwake. Kwa jinsi alivyokuwa akiongea, lipsi zilivyokuwa zikicheza, kifua saa sita nilipagawa kupita kawaida.

    Kila nilipomwangalia, moyo wangu uliniambia ‘Edward! Unasubiri nini?’. Sikutakiwa kuwa na presha kwa sababu watoto wazuri kama hawa unatakiwa kuwafuata kwa mahesabu makali sana.

    Naweza kusema kwamba huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuzoeana na Nurat. Kila siku tulikuwa tukionana na yeye ndiye aliyejaribu kuyabadilisha maisha yangu baada ya kufika katika chumba kidogo nilichokuwa nikiishi.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alininunulia kitanda cha chuma, chumba kikapigwa rangi na kunipa kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya matumizi yangu mengine.

    Kumbuka mpaka kipindi hicho sikuwa nimeiuza ile almasi kwa sababu sikujua soko lipo wapi na sikuwa na mtu wa kumwamini hata kidogo.

    Wakati hayo yakiendelea, upande wa pili niliendelea kutafuta soko taratibu. Siku ziliendelea kukatika na baada ya siku mbili nikapata taarifa kwamba rafiki yetu, Mrisho aliuawa na mwili wake kutupwa baharini.

    Nilishtuka sana, huyu Mrisho alikuwa mlinzi mwenzangu pale Kariakoo na alikuwa miongoni mwa watu ambao tulimsaidia yule mzee kumpeleka hospitalini.

    Msiba wake uliwagusa watu wengi, alikuwa kijana mpole, sasa ilikuwaje awe na maadui na wakati kila wakati alikuwa mcheshi na hakubagua ni nani wa kuongea naye?

    Tulihuzunika sana hivyo tulichokifanya ni kwenda kwenye mazishi na baada ya kumzika tukaendelea kufanya mambo mengine kama kawaida.

    Katika hayo yote, sikuacha kuwasiliana na msichana Aisha. Nilimkumbuka na wakati mwingine alikuwa akija na kwenda naye chumbani. Aisha alikuwa malaya tu lakini kitu cha ajabu kabisa alionekana kunikubali kupita kawaida.

    Nilikuwa masikini, aliujua ukweli lakini wala hakujali kiasi kwamba nikawa nashangaa kwamba ilikuwaje anikubali kiasi kile?

    “Hivi unanipenda kweli ama?” nilimuuliza.

    “Nakupenda sana Edward! Huamini?”

    “Naamini ila si unajua tena jinsi nilivyo! Mtoto mzuri kama wewe kuwa na mimi, huwa naona kama naota,” nilimwambia huku nikitoa tabasamu pana.

    Maisha yaliendelea, sikumwambia mtu kuhusu ile almasi, niliificha chumbani sehemu salama kabisa. Siku zikakatika, baada ya wiki mbili tukapata msiba mwingine wa jamaa yetu wa karibu (Selemani) ambaye alikuwa mlinzi kama mimi.

    Taarifa za awali zilisema kwamba jamaa alichomwa kisu na mtu asiyejulikana usiku wa manane nyumbani kwake kwa sababu siku hiyo hakuja kazini.

    Kama ulivyotuuma msiba wa kwanza, hata huo ulituuma sana kwa kuwa alikuwa Selemani alikuwa kama Mrisho, kijana mchangamfu ambaye alizungumza na kila mtu. Ilituuma sana lakini hatukuwa na jinsi, Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihidiwe.

    Siku hiyo usiku wa saa tisa nilipokuwa nimekaa sehemu nikiyafikiria maisha yangu huku nikiendelea kufanya kazi ya ulinzi hapo sokoni nikaanza kujiuliza swali moja muhimu sana.

    Lilikuja tu kichwani, nadhani kama Mungu alihitaji kunifumbua kitu fulani. Nikaanza kujiuliza kuhusu vifo vya watu waliokuwa wameuawa. Nilichanganyikiwa kidogo kwa sababu niligundua kwamba walikuwa walinzi, kwa nini wauawe ndani ya siku chache?

    Wakati nikiendelea kujiuliza hilo, moyo wangu ulikuwa na shaka mno, nilihisi kabisa kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea. Sikutaka kubaki kimya, nikawaita wenzangu na kuwaambia kuhusu maswali niliyokuwa nikijiuliza, kwamba kwa nini waliokuwa wakiuawa walikuwa walinzi?

    “Unaogopa sana! Acha kuogopa mtoto wa mama,” alisema Fred huku akiniangalia, sura yake ilikuwa na tabasamu pana.

    “Fred! Unajua siriazi wazee inabidi tujiulize kuhusu haya mauaji!” niliwaambia.

    “Kwa hiyo unahisi watu wanaanza kutuua sisi walinzi? Kama wanatuua, kwa nini hawaibi?” aliuliza mwingine, huyu aliitwa Msekwa.

    Kiukweli hili lilinichanganya kichwa sana lakini wenzangu hawakuwa na hofu hata kidogo. Nilichanganyikiwa mno ila kwa kuwa wenzangu hawakuonekana kuwa na hofu, basi na mimi nikajifariji kwamba hakukuwa na tatizo hivyo sikutakiwa kuhofia hata kidogo.

    Japokuwa nilikubaliana nao lakini sikutaka kupotezea kabisa, kichwa changu kiliniambia kwamba kulikuwa na jambo lililokuwa likiendelea nyuma ya pazia.

    Asubuhi ilipofika, huku nikiwa katika chumba changu, Nurat akapiga simu kwamba alikuwa akija kuniona kwa kuwa hakwenda chuo siku hiyo.

    Nikamkaribisha! Ndani ya dakika chache, akafika, akatulia na kumwambia niende kumnunulia kinywaji dukani. Alikataa lakini si unajua lazima mwanaume uonyeshe umwamba, nikaenda hivyohivyo huku yeye akinisubiri ndani.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Duka halikuwa mbali sana na mahali hapo, kulikuwa na vichochoro vichache kabla ya kuingia kwenye barabara kubwa iliyokuwa na maduka mengi.

    Nilipofika kwenye barabara hiyo, macho yangu yakatua kwenye gari moja lililosimama pembeni, ilikuwa Noah Nyeusi. Sikulitilia maanani, nilielekea dukani, nikanunua soda na kuanza kurudi.

    Ghafla mlango wa gari lile ukafunguliwa na mwanaume mmoja kuteremka huku akiwa na sigara mkononi. Akaniita kwa kuniomba sana, nikamsogea.

    “Samahani ndugu yangu, wewe ni mwenyeji maeneo haya?” aliniuliza huku akiniangalia.

    “Ndiyo! Kuna nini bosi?”

    “Unamfahamu huyu?” aliniuliza huku akinionyeshea picha ya mwanamke mmoja.

    Niliiangalia kwa makini, sikuwa nikimfahamu na sikuwahi kumuona hata siku moja. Nilimrudishia na kumwambia kwamba sikuwa nikimfahamu.

    “Haina shida! Unaweza kuingia ndani ya gari twende tukazungumze?” aliniuliza huku akiwa na tabasamu pana.

    “Ndani ya gari? Hapana! Nina haraka,” nilimwambia.

    “Kweli?” aliniuliza huku akinionyeshea bastola yake iliyokuwa kiunoni.

    Nilishtuka mno, nilitamani kukimbia lakini nilipokumbuka kwamba bastola ilikuwa na uwezo wa kukuua hata ukiwa mbali, niliogopa kupita kiasi.

    Sikumjua mtu huyo alikuwa nani, alihitaji nini ila alichotaka ni mimi kutii kile alichokuwa akiniamba. Sikubisha, mlango ukafunguliwa, ndani ya gari hilo kulikuwa na watu wengine kama watatu hivi, wote kwa kuwaangalia tu sura zao zilikuwa ngumu, yaani zilionyesha kuwa ni watu wasiokuwa na masihara hata kidogo.

    “Ingia fasta dogo tusije kukumwaga utumbo,” alisema mwanaume mmoja aliyekuwa ndani ya gari, kusikia hivyo, haraka sana nikaingia ndani. Gari likawashwa na kuondoka mahali hapo.

    Nilikuwa na hofu, nilijua kabisa kwamba siku hiyo ndiyo ilikuwa mwisho wangu. Niliogopa na kutetemeka mno, nilitekwa na majamaa hao waliokuwa kwenye Noah Nyeusi, nililia lakini sikutakiwa kuongea kitu chochote kile kwani vinginevyo wangeweza kuniua.

    “Tukifika tutakuuliza swali moja tu kuhusu almasi, na ukijifanya kuwa mjanja kama wale walinzi wenzako, tutakuua kama tulivyowaua,” alisema mwanaume mmoja huku akinipigapiga kibao shavuni.

    Moyo wangu ukapiga paaa! Kumbe hawa ndiyo majamaa wale waliowamaliza marafiki zangu, sasa zamu yangu ilifuata.





    Ndani ya gari nilikuwa nikitetemeka, niliona kabisa kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wangu, sikuwafahamu watu wale, kwa jinsi nilivyokuwa nikiwaangalia tu walionyesha kwamba ni watu wenye roho mbaya kuliko wote katika dunia hii.

    Waliniambia kuhusu almasi, hicho ndicho kitu nilichokuwa nikikitegemea kuniondoa kutoka katika maisha niliyokuwanayo. Umasikini wangu ule ungeondolewa na almasi hiyo ambayo niliichukua na kuificha chumbani.

    Leo, waliniteka na kuniambia kuhusu almasi, hii inamaana kwamba kama ningewaambia mahali ilipo au hata kuwapa basi ningekuwa masikini kama nilivyokuwa milele yote.

    Sikutaka kuona hilo likitokea, kwenye ishu ya almasi, nilikuwa radhi kupigwa, kuteshwa, kulawitiwa lakini si kuikabidhi ile almasi mikononi mwao, yaani nilijitolea kufanywa kila kitu lakini si kuwapa kwa mkono wangu.

    Gari liliondoka hapo Kariakoo na kuchukua njia ya kwenda Jangwani, niliambiwa nitulie, nilifanya hivyo huku moyoni nikianza kusali sala yangu ya mwisho.

    Kumbuka kwamba kule nyumbani nilimuacha Nurat, alikuwa akinisubiri, nilitekwa na nilikuwa na uhakika hakujua mahali nilipokuwa muda huo.

    Gari liliendeshwa mpaka lilipofika Kinondoni, nikachukuliwa na kuingizwa kwenye jumba moja kubwa, kwa ndani lilikuwa zuri lakini nilipopelekwa katika chumba nilichotakiwa kuhifadhiwa, nilishangaa kuona chumba hicho kuwa cha kutisha sana.

    Ni kama mule ndani walikuwa wakifanya upasuaji wa watu, pembeni kulikuwa na mguu wa mtu, haukuwa na vidole, kulikuwa na minyororo imefungwa ukutani, yaani mtu unasimamishwa, unafungwa minyororo na kupewa mateso mahali.

    Ukiachana na hivyo, kulikuwa na pasi ya umeme, nilijua kazi yake, pia kulikuwa na michirizi ya damu, kila nilipokuwa nikiangalia hali ya chumba kile, nilijua tu kwamba watu hao walikuwa siriazi kutaka almasi yao.

    “Bora waniue lakini si kusema mahali almasi ilipo,” nilijisemea huku nikiwekwa kwenye kiti kimoja.

    Muda wote huo mpaka naingizwa ndani sikuwa nimeongea kitu chochote kile, nilionyesha ujasiri fulani mkubwa kwani wanaume hao hawakuwahi kuona mtu aliyekuwa mbishi kama mimi.

    Mmoja aliniambia kwamba inawezekana mimi niliwahi kufa, nilifufuka na hivyo kutakiwa kufa tena na ndiyo maana sikuonekana kuogopa kwa sababu wenzangu waliokuwa wamechukuliwa hapo kabla, walikuwa wakilialia mpaka kujikojolea.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wewe mwamba sana. Unajiamini mno, wenzako walikuwa wanajikojolea, wewe upo hivyohivyo. Ila bro! Humu ndani ukitoka salama, shukuru Mungu. Unauona huo mguu, ni wa mshikaji wako, macho yake yapo humo kwenye ndoo,” aliniambia, nilijua tu kwamba yote hiyo ilikuwa ni kunitisha ili niwaambie mahali almasi ilipokuwa.

    Nilibaki ndani ya chumba hicho, nilijifikiria ni kwa namna gani ningeweza kutoroka. Niliogopa, kama nisingefanya harakati za kutoroka inamaanisha kwamba ningeteswa na hata kuuawa kwa kuwa mimi mwenye nilikuwa mbishi.

    Baada ya nusu saa, kijana mmoja akaingia, japokuwa ilikuwa ni asubuhi lakini humo kulikuwa na giza zito na ni taa tu ndiyo iliyokuwa imewashwa. Kwanza taa ikazimwa, wakati nikijiuliza nini kilitakiwa kuendelea pale kwenye kiti nilichokuwa, nikashtukia nikipigwa ngumi nzito iliyonifanya nianguke chini.

    “Tunaanza. Hii muvi ina season tano, hii ndiyo episode ya kwanza, Na kila season ina episode arobaini. Ukimaliza season zote tano, wewe mwamba,” aliniambia huku akiiwasha taa, akachukua mjeredi, akanifunga ile minyororo huku nikiwa kifua wazi, mgongo ukageukia kwake na kuanza kunichapa.

    Nilisikia maumivu makali mno, mwanaume yule alinichapa mjeredi ule kwa nguvu kubwa pasipo kuanza kuniuliza swali lolote lile kuhusu ile almasi.

    Nilisikia maumivu makali kupita kawaida. Alinichapa kwa dakika tano nzima, mgongo mzima ulijaa damu, nilikuwa nikilia kama mtoto mdogo huku nikimuomba aniachie kwani sikuwa nikijua kitu chochote kile.

    Baada ya kumaliza, akanifungua na kuniweka kwenye kiti, mgongo wote ni kama ulikuwa na ganzi na kwa jinsi damu zilivyokuwa zikichirizika ni kama mtu alichukua ndoo ya maji na kunimwagia mgongoni.

    Kwenye kiti kile wakaniweka na kuanza kuniuliza maswali kuhusu yule mzee niliyekuwa nimemuokoa na almasi. Nilichokigundua ni kwamba hawakujua ni mlinzi gani aliyekuwa amemuokoa yule mzee na mbaya zaidi hawakujua ni nani alikuwa na almasi waliyokuwa wakiitaka.

    Kila walichoniuliza, niliwaambia kwamba sifahamu chochote kuhusu almasi lakini nilisikia kuhusu mzee huyo kwamba alitakiwa kuuawa.

    “Wewe ulikuwa wapi?” aliniuliza.

    “Nilikuwa Kimanzichana kwa mama! Nilipewa likizo ya siku saba,” niliwajibu kwa sauti ya chini.

    “Kwa hiyo hujui chochote kuhusu almasi?”

    “Hapana mkuu! Sijui chochote kile, hata huyo mzee niliambiwa tu,” nilimjibu mwanaume aliyekuwa akiniuliza.

    Niliwadanganya, walionekana kuniamini lakini hiyo haikuwa sababu ya kuniacha, waliendelea kunitesa mno, soku hiyo ilikuwa ni ya hatari sana kwangu, muda wote nilikuwa nikilia lakini watu hao hawakutaka kuniacha, waliendelea kunitesa zaidi na zaidi kiasi kwamba mpaka ukafika muda nikahisi kabisa mwili mzima ulikufa ganzi na sikuwa nikiskia maumivu yoyote yale.

    Siku hiyo nilitakiwa kuwa humo huku nikisikia maumivu makali mwilini mwangu. Walipanga itakapofika majira ya saa saba usiku waniue na kwenda kuutupa mwili wangu katika soko la Kariakoo kwa ajili ya kuwatisha walinzi wenzangu kama walivyokuwa wamefanya kwa wengine.

    Nilitakiwa kupambana, ni kweli nilikuwa mateka lakini nilijua kabisa kwamba endapo ningepambana ningeweza kuchomoka ndani ya chumba hicho.

    Humo niliachwa na jamaa mmoja ambaye alionekana kuwa kama mlinzi, yeye ndiye ambaye alitakiwa kuhakikisha nakaa humo, sifanyi kitu chochote mpaka muda wa kuchukuliwa na kuuawa utakapofika.

    Nilimwangalia jamaa mwenyewe, kiukweli nilitakiwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha natoka ndani ya chumba hicho. Sikuwa na nguvu lakini mdomo wangu nilihisi kabisa ulikuwa na nguvu za kuongea, nikamuita kwa kuwa nilihitaji nimshawishi ili twende sawa.

    “Bro! Njoo tuongee,” nilimwambia, akanisogelea, alijua sina nguvu kwa kuwa niliteswa sana lakini kupitia mwanaume huyohuyo ilitakiwa nifanye kila liwezekanalo kuhakikisha natoka.

    “Unasemaje?” aliniuliza kwa sauti ya kibabe.

    “Ninamjua mtu mwenye almasi. Kuna jamaa nilimsikia akituambia kwamba aliokota kitu kilichokuwa kama chupa, ila sikujua kama ni almasi,” nilimwambia, akaniangalia vizuri, akalisogeza sikio lake karibu mwangu.

    “Unasema kweli?”

    “Ndiyo! Ninamjua! Kama mtakuwa tayari niwapeleke,” nilimwambia.

    Mwanaume huyo akawaita wenzake na kuwaambia nilichomwambia. Wote hawakuamini kama mwisho wa siku ningekubaliana nao na kuwaambia kuhusu mtu aliyekuwa na almasi hiyo.

    Wakaanza kuniuliza maswali mengi, nilikuwa makini kwenye kutoa majibu yangu, niliwaambia kila kitu kwamba kama tungemtafuta huyo mtu kwa kwenda kwao basi ilikuwa ni lazima tuipate hiyo almasi.

    “Anaitwa nani huyo?” aliniuliza mwingine.

    “Alfred!”

    “Anaishi wapi?”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Jirani yangu kulekule Kariakoo! Kama mtataka kumpata, twendeni,” niliwaambia.

    Hakukuwa na mtu aliyeitwa kwa jina la Alfred lakini waliniamini kwa sababu ya hali niliyokuwanayo. Walijua kwamba kwa jinsi nilivyokuwa nimeteswa basi kila kitu ambacho ningekisema mahali hapo kingekuwa ni ukweli kabisa.

    Niliwaambia kwamba nilisikia mwanaume huyo alitaka kuiuza almasi hiyo huko maeneo ya Posta keshokutwa ila kama kweli waliitaka bai ningekuwa radhi kuwapeleka mpaka huko.

    Waliniangalia, kwa jinsi nilivyoonekana, mateso niliyopewa kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba kile nilichokuwa nikikizungumza kilikuwa kweli kabisa.

    Hawakumjua Alfred, ili kufika huko ilikuwa ni lazima niende nao. Waliitana na kujadiliana, sikujua walichokiongea, wakanichukua, tukapanda gari na kuelekea huko.

    Njiani nilikuwa kimya kabisa, akili yangu ilikuwa ikifikiria mambo mengi mno kwamba mara baada ya kufika huko, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwatoroka.

    Mtu ambaye nilimfikiria mara ya kwanza alikuwa ni polisi, yaani niende kwenye nyumba moja yenye wapangaji wengi halafu niwaambie kwamba huyo Alfred alikuwa akikaa humo na kama walitaka niende kuwaitia napo kusingekuwa na tatizo lolote lile.

    Safari hiyo ilichukua kama dakika arobaini na tano hivi, tukafika karibu na nyumba hiyo. Nakumbuka muda huo ulikuwa ni saa moja usiku, niliwaoyeshea nyumba aliyokuwa akiishi huyo Alfred na hivyo walitakiwa kwenda kumuulizia.

    Jamaa mmoja akateremka na kuelekea huko, akapiga hodi kwenye nyumba hiyo ya wapangaji wengi, mlango ukafunguliwa, akaulizia na kuambiwa kwamba hakuna mtu mwenye jina hilo, hivyo akaja kutuambia.

    “Kwa nini umetudanganya?” aliniuliza mwanaume mmoja.

    “Jamani! Nimewaambia huyu Alfred ana almasi, hivi mnadhani naye ni mjinga kiasi cha kukubali kwamba yupo? Inawezekana amewaambia wapangaji wenzake kwamba akiuliziwa na mtu yeyote waseme hayupo au hakuna mtu kama huyo. Hivi kama ni wewe mkuu, una almasi ndani halafu kaja mtu usiyemjua kukuulizia, ataambiwa kama upo ndani?” niliwauliza swali ambalo lilikuwa na maana kubwa sana.

    Wakajifikiria na kukubaliana kwamba inawezekana kabisa niliwaambia ukweli kwani kwa akili ya kawaida tu kama ndani kulikuwa na mtu ana almasi halafu akauliziwa na mtu asiyemjua, ukweli ni kwamba asingeweza kutoka na kusema kwamba yupo.

    “Ila kweli! Kwa hiyo tufanyeje?” aliuliza mwanaume mmoja, nikaona hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yangu.

    “Nenda naye! Mkifika aulizie yeye!” alisema mwanaume mwingine.

    Nikateremshwa na mwanaume mmoja na kuelekea kule, tulipoufikia mlango, nikaugonga na ulipofunguliwa tu nikaulizia Alfred, nilikuwa namuhitaji.

    “Jamani! Si nimeshasema kwamba hakuna Alfred humu ndani,” alisema mwanamke aliyeufungua mlango.

    “Dada! Najua hunifahamu! Mimi ni mlinzi mwenzake!” nilimwambia.

    Kwa jinsi nilivyokuwa nikizungumza nilionyesha dalili zote za kuwa hoi, nilihitaji mwanamke yule anisome kwanza ili ajue ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.

    Nahisi alilijua hilo kwani kila aliponiangalia aligundua kabisa huyu mtu hayupo sawa. Alichokisema ni kwamba hakukuwa na mtu huyo ila angetuitia mwanaume ambaye inawezekana alijua kila kitu kuhusu huyo Alfred.

    Tukamwambia sawa, akatuitie. Akarudi ndani. Kwa yote niliyomuonyeshea tu nilijua angekwenda kumuita yule polisi. Ni ndani ya sekunde chache, mwanaume huyo akatokea huku akiwa na kaoshi tu, akasimama mlangoni na kutuangalia.

    “Mnataka nini?” aliuliza kibabe.

    “Tunamuulizia Alfred!” alijibu mwanaume yule huku akijiandaa kuupeleka mkono wake kiunoni kwa nyuma.

    Hilo lilionekana kuwa kosa kubwa kwani mwanaume aliyekuwa ameufungua mlango na kuja, alikuwa na bastola yake na aliambiwa kwa kifupi kilichokuwa mlangoni, yaani mpaka leo hii namshukuru yule dada.

    Jamaa alipoanza kuupeleka mkono kwa nyuma, yule polisi ambaye alifundishwa sana huko mafunzoni alijua tu alikuwa akifuata nini, kwa kasi ya ajabu akatoa bastola yake na kumpiga mbili za mguu na mkono, akaanguka chini, wale jamaa waliokuwa kwenye Noah, wakawasha gari na kuondoka mahali hapo kwa kasi.

    Nilishukuru Mungu, mwanaume yule akatuweka chini ya ulinzi, akampekua jamaa yule na kuichukua bastola yake na kutuchukua kutupeleka kituoni.

    Huko ndipo nilipoelezea kila kitu kilichokuwa kimetokea, kwamba nilitekwa na watu hao kwa lengo la kuuawa kama wenzangu kisa tu kumuokoa mzee fulani.

    “Ulitekwa?”

    “Ndiyo! Tangu jana! Niliwekwa kwenye chumba cha mateso na kuanza kuchapwa, hebu angalia,” nilisema huku nikiwaonyeshea mgongo.

    “Mungu wangu! Ulipelekwa wapi? Unapajua?” aliniuliza polisi mmoja.

    “Napajua! Naweza kuwapeleka ila naogopa sana,” niliwaambia.

    “Wewe tupeleke tu sisi tutakulinda,” aliniambia polisi mmoja na hivyo kukubaliana nao.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Japokuwa nilikuwa naogopa lakini sikuwa na jinsi, nikawachukua polisi na kuondoka nao kuelekea katika nyumba ile iliyokuwa huko Kinondoni.

    Kila mmoja ndani ya gari alikuwa kimya, wale polisi wanawake walishindwa kuvumilia, kila walipouangalia mgongo wangu, kwa jinsi ulivyochakazwa walishindwa kuamini kama nilipona.

    Nilichokihitaji sana ni kwenda hospitali tu kupata matibabu lakini kutokana na polisi wale kutaka kuifahamu nyumba hiyo, nikawachukua na kwenda huko.

    Hatukuchukua muda mrefu tukafika, tukateremka na kuingia ndani. Hakukuwa na mtu yeyote yule, nahisi walijua kwamba polisi wangefika mahali hapo, walikimbia, polisi wakapitiliza mpaka kwenye kile chumba, picha waliyoiona wao wenyewe iliwatisha.

    Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa kufuatilia kuhusu watu hao, sikutaka kuendelea kuwauliza ni kitu gani kiliendelea baada ya hapo kwani nilipoondoka, sikutaka kurudi kituoni, nilipotea na kwenda hospitalini.

    Hospitalini madaktari walikuwa wakishangaa, hawakuamini walichokuwa wakikiangalia, mgongo wangu ulichakazwa sana kiasi cha nyama ya ndani kuonekana. Kila walipokuwa wakinigusa nilisikia maumivu makali hivyo hatua ya kwanza walichokifanya kilikuwa ni kunisafisha na kunipaka dawa ya kuua vijidudu.

    Sikujua kwa Nurat ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, hakujua kama nilikuwa hospitalini, mara ya mwisho kuondoka nyumbani siku iliyopita ni pale nilipokwenda dukani, na sikurudi tena.

    Nilijua kwamba alikuwa akijiuliza sana, ilibidi niwasiliane naye na kwa sababu nilimpenda na kumtamani sana, hata namba yake iliniganda kichwani, hivyo nikamuomba daktari simu yake na kumpigia.

    “Naongea na nani?” niliisikia sauti yake nyororo.

    “Edward!”

    “Edward! Ooh my gosh! Upo wapi?” aliniuliza kwa mshtuko.

    “Nilitekwa!”

    “Ulitekwa? Na nani? Kisa nini? Ilikuwaje?” aliniuliza maswali kadhaa ambayo sikujua nimjibu lipi.

    “Nurat! Nipo hospitali hapa Palestina! Naomba uje kuniona,” nilimwambia.

    Nikakata simu na kuanza kumsikilizia, ilipita kama dakika thelathini hivi Nurat akafika hospitalini hapo, akaulizia, na kwa sababu ulikuwa muda wa kuona wagonjwa, akaruhusiwa na kuja kuniona.

    Alishangaa na kile alichokikuta, nililala kifudifudi huku mgongo mzima ukiwa na pamba. Alishindwa kuvumilia, akaanza kububujikwa na machozi, alionekana kuumia sana na kile alichokuwa amekikuta.

    Akaniuliza kilichotokea kwani tangu nilipoondoka kwenda dukani kufuata soda sikurudi tena. Nikamuhadithia kila kitu kilichotokea kitu kilichomshtua kupita kawaida.

    “Unasema walikuteka?”

    “Ndiyo!”

    “Kwa sababu gani?”

    “Kwa sababu ya baba yako!”

    “Baba yangu? Kivipi?” aliniuliza huku akishangaa.

    Nilimwambia kuhusu kile kilichotokea usiku wa siku ile, watu wale walitumwa kwa sababu walikosa walichokuwa wakikifuata kwa baba yake ila sikumwambia ni kitu gani, nikaongezea kuwa kulikuwa na walinzi wenzangu ambao waliuawa na bila shaka watu wale ndiyo waliokuwa wamewaua kwa sababu niliwasikia wakiongea kuhusu hilo.

    Ilikuwa ni stori fupi lakini iliyomsisimua mno. Akanisogelea na kunibusu shavuni, yaani hilo busu likanipa nguvu ya ajabu kupita kawaida. Kuanzia siku hiyo akaanza kuja hospitalini hapo kuniona akiwa na ndugu zake wengine ambao walinionyeshea thamani kwa kuwa niliyaokoa maisha ya baba yao.

    Kichwa changu kilikuwa kikifikiria kuhusu ile almasi iliyokuwa chumbani kwangu, nilitamani sana niiuze, nipate mamilioni na kuendelea na maisha yangu. Nilikaa hospitalini hapo kwa wiki moja huku Nurat na mama yake wakigharamia matibabu, na nilipopata nafuu, nikaruhusiwa kuondoka.

    Nilipofika nyumbani kwangu, sikutaka kukaa humo, nilipekua nilipoificha almasi ile, nikaichukua na kuondoka zangu. Kumbuka sikuwa na pesa lakini ilikuwa ni bora kukaa mitaani, niteseke nikitafuta duka la almasi kuliko kubaki mule chumbani kwani niliamini kwamba vijana wale wangefika na kuniua kama walivyokuwa wakipanga.

    Maisha yakawa mtaani. Sikumwambia Nurat kuhusu maisha hayo, nilijua kwamba angenitafutia chumba kitu ambacho sikutaka kabisa kuona kikitokea.

    Niliamua kufanya hivyo makusudi kabisa, unajua watu wa mitaani hawafuatiliwi kwa kuwa wanaaminika kwamba hawana pesa wala kitu chochote kile cha thamani na ndiyo maana na mimi nikajifanya kuwa mtu wa huko.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nusrat alipotaka kuonana nami, nilitafuta sehemu ya kawaida na kuonana naye huku nikimwambia kwamba kulikuwa na kazi nafanya ambayo iliyaendesha maisha yangu.

    “Pole sana! Ila nitakusaidia,” aliniambia kwa sauti ya chini.

    “Nitashukuru mno. Naweza kuuliza swali?” nilimuuliza.

    “Uliza tu!”

    “Nina lengo la kwenda Shinyanga kuchimba dhahabu ila tatizo ni moja tu, kama nikipata dhahabu huko nitakwenda kuiuza wapi?” nilimuuliza makusudi, nilihitaji kujua kuhusu hilo.

    “Kule huwa kuna makampuni, hutakiwi kutoka nayo!”

    “Najua! Tufanye nimefanya magumashi, nikafanikiwa kutoka nayo, niende wapi?’ nilimuuliza.

    “Kwenye maduka ya kuuza dhahabu na almasi!”

    “Sonara?”

    “Hahaha! Hebu acha hizo. Nenda hata Posta, kuna duka moja pale linanunua vitu hivyo, ukipata niambie nikupeleke,” aliniambia Nurat.

    Nilikuwa makini kumsikiliza, aliniambia mambo mengi pasipo kugundua kwamba nilikuwa na almasi ndani. Tuliongea mambo mengi siku hiyo na akaamua kuondoka zake huku akiniachia kiasi cha shilingi elfu hamsini kwa ajili ya matumizi yangu.

    Mpaka siku hiyo sikuwa nimemwambia lolote lile, nilihofu moyoni mwangu, nilimwangalia jinsi alivyokuwa, mtoto wa Kiarabu, mzuri, mwenye shepu bomba, halafu nikajiangalia na kapuku mimi, nilivyokuwa kituko, yaani niligundua kabisa nisingeweza kufanikiwa kuwa na mtoto mzuri kama yeye.

    Siku iliyofuata tu nikaondoka na kuelekea huko Posta kulitafuta duka hilo. Almasi hiyo nilikuwa nayo, nilivalia suruali yangu ya jinsi, kwa ndani nilifunga kamba fulani ambayo niliiunganisha kwenye kitambaa cha peke yake na kuiweka ile almasi.

    Sikutakiwa kumwamini mtu yeyote yule, na hata nilivyokuwa nikitembea, sikuwa nikijiamini hata kidogo. Nilifanikiwa kufika kwenye hilo duka, nikaingia ndani, nikamkuta mzee wa Kihindi na vijana wawili, nikawasalimia na kuomba kuuliza.

    “Kuna nini?” aliniuliza yule mzee.

    “Nataka niuze mali yangu!” nilimwambia.

    “Mali gani?” aliniuliza.

    Sikumjibu, nilibaki nikimwangalia. Wote watatu walinikodolea macho, mzee huyo alijua kwamba najishtukia, akanichukua na kunipeleka ndani ya chumba kimoja, tukakaa na kuanza kuzungumza.

    Nilimwambia ukweli kuhusu ile almasi, akahitaji nimuonyeshee, nikafanya hivyo, alishtuka, hakuamini kama ningekuwa na almasi kubwa kiasi hicho.

    “Umeipata wapi?”

    “Nimeitoa mgodini. Mimi ni mchimbaji, zali tu limeniangukia,” nilimwambia.

    “Hii ni kubwa sana. Nikupe kiasi gani?” aliniuliza, najua alihitaji kujua uwezo wangu wa kugundua kuhusu madini.

    “Wewe una kiasi gani?”

    “Milioni mia tano?” aliniambia, nikashtuka lakini nilijua yeye ni mfanyabiashara, kiasi hicho kilikuwa kikubwa kwangu lakini kwake, kulingana na mzigo, kilikuwa kiasi kidogo mno.

    “Duuh!” nilitoa mguno.

    “Niambie hata sasa hivi nakupa!”

    “Yaani nikuuzie kwa milioni mia tano! Mzigo huu? Mzee unazingua,” nilimwambia, sikutaka kubaki hapo, nikairudisha na kusimama kutaka kuondoka.

    “Sasa mbona unaondoka? Usifanye hivyo, rudi tuongee,” aliniambia huku akinishika mkono, alijua tu kwamba nilitaka kwenda kwenye duka jingine.

    “Mzee unazingua, halafu unaniona mimi wa kuja, bora niende kwenye duka la mzee Sunil atanipa kiasi kinachostahili,” nilimwambia, hilo jina lenyewe nililitunga hapohapo.

    “Hakuna! Hii biashara! Basi niambie nikupe kiasi gani.”

    “Hapana nahitaji 1.2 B,” nilimwambia.

    “Bilioni 1.2?” aliniuliza kwa kushtuka.

    “Mzee! Nakuuzia almasi kubwa, sikuuzii dhahabu. Ndiyo maana nilisema kama hutaki acha niondoke nikale bilioni mbili,” nilimwambia kwa kujiamini.

    Mpaka hapo niliweza kumdanganya kwa muonekano wangu, sikwenda kimama, nilikwenda kama mtu ambaye nilijua sana madini. Mzee akaniambia ukweli tu kwamba kwa ile almasi niliyokuwanayo, gharama yake ilikuwa ni shilingi bilioni 1.5 ila kama ningependa nimuuzie hiyo bilioni moja ili akiiuza apate faida ya milioni mia tano.

    “Yaani upate nusu yangu? Hapana! Weka bilioni moja pointi mbili, kama hutaki naondoka,” nilisema huku nikiinuka na kuufungua mlango.

    “Subiri kwanza!” aliniambia.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ilikuwa ni kama utani lakinid ndiyo tukawa tunazungumzia pesa nyingi. Akaingia kwenye chumba fulani na aliporudi alikuja na chombo fulani cha kuangalia kama ile ilikuwa almasi kweli ama la. Akaipima, mzigo ulikuwa wenyewe. Akatoa tabasamu pana, nikajua tu kuwa aligundua ina thamani sana, ila kwa kuwa na mimi sikujua kitu, nikaona poa tu, hata nikipigwa, kwani nilinunua?

    Akakubaliana nami na kunichukua kuelekea benki kufungua akaunti na kuniingizia kiasi hicho cha pesa. Zilikuwa pesa nyingi mno, nilichanganyikiwa, sikuamini kama mimi, Edward nilikuwa na pesa hizo kwenye akaunti yangu.

    Nilichokumbuka ni watoto wazuri, si walinikataa, wakajiona wao ndiyo wao, si waliniambia mimi kapuku, sina pesa, halafu yule Issa si alitembea na demu wangu, halafu hakukumbuka kama ana wadogo zake, na huyohuyo Issa naye ana demu wake aliyetaka kumuoa, sasa nitaanza nao hao kwanza, halafu ndiyo nitadili na wengine, kuhusu huyo demu wake, hata kama amemuoa, nitatembea na mkewe kulipa kisasi, pesa ndiyo itaongea lugha tamu ya kumshawishi.



    ITAENDELEA





0 comments:

Post a Comment

Blog