Search This Blog

Monday, October 24, 2022

NYUMBA ILIYOJAA DHAMBI - 4

 







    Chombezo : Nyumba Iliyojaa Dhambi

    Sehemu Ya Nne (4)



     Kuna wakati kipindi hicho nilikuwa najiambia kwamba kwenye ujana wako ndipo ambapo unatakiwa kufanya ujinga wote unaotaka kuufanya ili ukiwa mzee utulie.

    Leo unakutana na wazee, vitambi vina vinyweleo mpaka vimeota mvi lakini bado wanataka watoto wadogo, yaani hii inamaanisha kwamba ujana wao hawakuufaidi kwa kufanya ushenzi kama huu na ndiyo maana zama hizo zilianza kujirudi kwao.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mimi nilitaka nifanye yote ili hata siku moja mtu akinifuata na kuniuliza kama niliwahi kufanya ushenzi huu na huu basi nimwambie nilifanya na sikuona faida yoyote ile. Wanawake wawili ndani ya kitanda kimoja, mambo hayo niliwahi kuyaona kwa Wazungu tu lakini si huku Tanzania.

    Basi nikakubaliana nao, wakaniambia niwapoze tu elfu hamsini kila mmoja, chakula na pesa ya nauli, nikawaambia poa, pesa si tatizo, tatizo ni wao tu kunipa huduma ya kitu moyo inataka.

    Tukaondoka na kuelekea hotelini. Nilijiona Mfalme Mswati. Niliona hotelini mbali, wakati mwingine nilitamani hata kupiga picha na kuwaonyeshea Watanzania wote kwamba si mnaona sasa nilivyo? Si mnaona jinsi ninavyoondoka na watoto wawili?

    Tulipofika hotelini tukaingia, sikutaka kuchelewa, mambo yakaanza mara moja huku nikionekana kuwa na kasi kama Hussein Bolt. Nilitaka kuwaonyeshea kwamba hela ya mwanaume haiendi bure, ilikuwa ni lazima wailipie na ndicho kilichotokea. Ilichukua masaa matatu, wote wakawa hoi.

    “Wewe mtu balaa!” aliniambia Doreen huku akiniangalia kwa mshangao, pamoja na mambo yake machafu lakini alikiri kwamba hakuwahi kukutana na mimi.

    “Balaa langu lipi sasa?”

    “Utadhani siyo mwanaume wa Dar!” alidakia Amanda.

    “Kwa hiyo mnaniambiaje? Mmeshakula laki moja yangu na huduma mliyonipa ni ya shilingi elfu sitini tu, kuna ya arobaini imebaki huko kwenu,” nilimwambia.

    “We kaka utatuua!”

    “Basi nawaongezeni, mimi mpaka niridhike!”

    “Kwani hujaridhika tu?”

    “Bado hata kidogo!” niliwaambia.

    Niliongea kama masihara lakini nilimaanisha, ni masaa matatu lakini ilionekana kama nusu saa kwangu. Filimbi ikapigwa tena na wachezaji kuingia uwanjani.

    Watu walikuwa wakihema kama mbwa, mpira wa siku hiyo ilikuwa balaa, viungo walikuwa wakimiliki mpira kwa kasi kubwa, kila ulipokuwa ukitoka, mpira mwingine ulirushwa ndani kuonyesha kwamba siku hiyo ilikuwa ni ya kazi tu, wachezaji wasiokuwa na uwezo wa kumaliza dakika tisini hawakutakiwa kucheza mechi hiyo.

    Nakumbuka tuliingia majira ya saa kumi jioni na waliondoka pale saa tano usiku, niliwang’ang’aniza walale, wakakataa kabisa.

    “Nitawapeni milioni moja kila mtu!”

    “Hapana! Hata ukinipa milioni hamsini silali! Mwanaume gani hutosheki!” aliniambia Doreen.

    “Jamaniiiiiiii....”

    “Aku! Tena usiniguse,” aliniambia Doreen manake alishaona mkono wangu ulianza kumletea shobo.

    Nikaachana nao, wakaondoka na mimi kulala hotelini. Asubuhi ilipofika, baba yake na Zamaradi akaniambia kwamba siku hiyo ndiyo walitaka kuhama hivyo nilitakiwa kuonana naye.

    Halikuwa tatizo, tukaonana, tukaongea na siku hiyo kuhama na hivyo kuanza kuirekebisha nyumba ile kwa kuvunja baadhi ya sehemu na kuboresha sehemu nyingine kuwa na mvuto zaidi.

    Nilikuwa na pesa, niliitengeneza kwa wiki moja tu, ikawa nzuri mno kiasi kwamba kila mtu aliyekuwa akiiangalia aliipenda kupita kawaida kutokana na mapambo yake yaliyokuwa kwa nje.

    Kwa ndani niliamua kufanya kufuru, nilitaka nipafanye kuvutie, yaani msichana yeyote ambaye angeingia basi awe anatamani tu kuolewa na mimi ili aishi humo.

    Ilitumia siku kadhaa kila kitu kikakamilika. Nilichokuwa nikihitaji nilikipata, nilichokifanya kingine ni kununua coaster tatu ambazo zilianza kufanya biashara, nikanunua bajaj tano, bodaboda ishirini lakini pia nikaamua kuwekeza zaidi kwenye kilimo ambapo nilisafiri mpaka Mbeya na kununua shamba la hekari ishirini na hivyo kuanza kupanda mpunga.

    Haikuishia hapo bali kingine nilichokifanya ni kuwekeza kwenye ardhi, nikajenga nyumba nyingine mbili na kuzipangisha kwa pesa ndefu, ndani niliwawekea kila kitu na malipo yake nilihitaji yafanyike kwa dola kwani niliweka mazingira fulani kama nyumba za Wazungu ambao ndiyo walikuwa lengo langu kuwapata ndani ya nyumba hizo mbili kubwa.

    Kwa kila mwezi, kodi yake ilikuwa ni dola elfu moja, zaidi ya milioni mbili na nilianza kupata wateja wengi hasa Wazungu waliokuwa wakija huku kwa mambo yao ya utalii kwa kuwa kiasi hicho kwao kilikuwa kidogo mno. Ndiyo hivyo nikawa naingiza pesa.

    “Hii nyumba itajaa dhambi sana! Yaani humu, hata mke wa mbunge akijipindua, tutalaumiana,” nilisema huku nikiwa kitandani. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Watu wa kwanza walionijia kichwani ni Halima na Shamila, sasa zake na Issa, nianze nao halafu niende kwa huyo demu wake, hata kama alikuwa amemuoa, kwanza ilikuwa ni lazima nifanye yangu.



    Mafundi walianza kujenga nyumba yangu ambayo nilihitaji kwenda kuishi Tegeta. Nilikuwa na furaha tele, kwa jinsi nilivyokuwa nikiwaangalia mafundi walivyokuwa wakiijenga nyumba hiyo, sikuamini kama kweli ilikuwa ni mimi ndiye niliyewaambia wafanye hivyo.

    Nilikaa pembeni huku nikifuatilia kila kitu. Nilihitaji nyumba kubwa na ya maana ambayo ndani yake kungekuwa na bwawa la kuogelea. Kwa kipindi chote hicho sikuwa nimeonana na Nurat, ilikuwa kama wiki moja hivi, tulikuwa tukiwasiliana kwenye simu tu.

    Kipindi hicho nilitaka niende Kariakoo kuonana na dada zake, Issa na kuzungumza nao. Nilikuwa na ratiba yao, nilijua kabisa kwamba siku hiyo kama ningekwenda huko ningemkuta Halima na hivyo kumfanyia kile nilichotaka kufanya. Nikaondoka kwa gari langu, IST ambayo niliinunua milioni kumi na mbili showroom.

    Nilipofika Kariakoo, nikaenda katika eneo ambalo lilitumika kuegeshea magari karibu kabisa na Big Bon, nikaliacha na kuelekea katika Mtaa wa Kongo kwenda kuonana na Halima.

    Nilipofika, kweli nilimkuta, alishtuka sana kuniona, nilibadilika, niliondoka kwa wiki kadhaa na aliniona kama mpya. Akanisogelea, hakuamini alichokiona, yule Edward aliyekuwa amepotea kwa kipindi kirefu hakuwa huyu, nilikuwa mwingine kabisa.

    Pale hakuwa peke yake, kulikuwa na msichana mwingine mzuri ambaye sikumjua, alionekana kutabasamu na kuwa na shauku ya kutaka kufahamu nilikuwa nani na kwa nini Halima alikuwa akinichangamkia kiasi hicho.

    Wakati nikiwa sijajiandaa hata kumwambia lolote lile, washikaji zangu ambao nilikuwa nikilinda nao na wale walionijua wakanisogelea na kuanza kunisalimia, walinishangaa mno, nilibadilika na kuwa kama mtu fulani ambaye nilikuwa na pesa.

    “Edward! Hivi ni wewe ama naota?” aliuliza jamaa mmoja aliyeitwa Fred.

    “Ni mimi. Inakuwaje Fred!”

    “Poa! Umebadilika, mzee baba mpaka unaanza kuota kitambi,” aliniambia na kuanza kucheka.

    Kila mmoja alihitaji kufahamu ni kitu gani kilikuwa kimetokea mpaka kuwa hivyo nilivyokuwa. Niliwaambia kwamba ni bahati tu, ilitokea nikajikuta kuwa na pesa basi nikabadilisha maisha yangu.

    Kila aliyeniona hakuacha kunishangaa, Halima na yule msichana mwingine walikuwa wakiniangalia kwa macho ya kunitamani tu, yaani kama walionekana kuhitaji kitu fulani hivi.

    Nilikuwa bize na washikaji, tulipiga sana stori, tulipomaliza, wakaondoka na kuniacha na wanawake hao.

    “Umebadilika,” aliniambia Halima, pamoja na mapozi yake aliyokuwa akiniletea siku za nyuma, siku hiyo yalikwisha kabisa.

    “Nimekuwaje? Nina mkia?” nilimuuliza kiutani.

    “Hahah! Umekuwa m’baba! Aisee umependeza,” aliniambia.

    Japokuwa nilikwenda hapo kwa lengo la kumpata Halima lakini yule msichana ambaye naye alikuwa mahali hapo aliniacha hoi sana. Alikuwa mrembo na nilichokifanya ni kutoleta tamaa zangu kwake kwani niliamini ningemkosa Halima na wakati alikuwa kwenye mipango yangu.

    “Na huyu ni nani?” nilimuuliza Halima kuhusu msichana huyo.

    “Huyu anaitwa Haijati. Ni wifi yangu kwa Issa, mtoto wa Zenji,” alinijibu Halima.

    Yaani moyo ukapiga paaa! Sikuamini kile nilichokisikia. Halima aliniambia kwamba huyo alikuwa mke wa Issa, aliamua kumuoa siku chache baada ya mimi kuondoka.

    Aisee nilichanganyikiwa, yaani kwa uzuri wa yule demu, namuachaje sasa? Kwa sababu alisikia juu juu tu, nikaamua kuanza kujifagilia kwanza kwani nilijua ingeweza kuwa njia nyepesi mno kumpata.

    “Halima! Mtaa wa Kongo haujabadilika imenifanya mpaka gari langu nilipaki kule Big Bon,” nilimwambia, Halima akashtuka mno.

    “Una gari?”

    “Sasa unanichukuliaje Halima? Namshukuru Mungu kanijalia vijisenti kidogo! Nimenunua nyumba Sinza na ninajenga Tegeta,” nilimwambia Halima.

    Hakuamini, kile alichokisikia kilikuwa kama ndoto. Kilikuwa ni kipindi kifupi sana kwa mimi kuwa na pesa hizo, nilizipata wapi? Uchawi ama?

    “Imekuwaje?”

    “Ni stori ndefu sana. Si pesa za kishetani, ni za halali kabisa. Yaani Mungu amenibariki mno. Umekula?” nilimuuliza.

    “Sijala!”

    “Utakula nini?”

    “Chochote tu bosi!”

    “Na shemeji hapo?” nilimuuliza Haijati huku nikimwangalia.

    “Chochote tu!”

    “Basi sawa.”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu kumi na kumwambia aende akanunue chakula chao. Akaichukua, akaondoka na kutuacha wawili sisi pale dukani.

    Hilo ndilo nililolitaka, nilihitaji kuzungumza naye kwa dakika kadhaa, ikiwezekana hata nichukue namba yake ya simu kwa ajili ya kuitumia baadaye.

    Mume wake aliutumia udhaifu wangu wa kutokuwa na pesa kumchukua msichana niliyempenda na kufanya naye mapenzi, hii ilikuwa zamu yake, hata kama alikuwa ameoa, moyo wangu ulikuwa na kisasi na nilitamani sana na yeye nimfanyie kama alivyonifanyia, mwenye pesa, muumize masikini tu.

    “Ila umependeza shemeji!” nilimwambia huku nikimwangalia kwa macho ya kuita.

    “Mh! Ahsante shemeji!”

    “Hivi Issa yupo?” nilimuuliza.

    “Yupo! Kwani huwasiliano naye?”

    “Hapana! Katika maisha yangu niliwahi kuongea naye mara mbili tu. Huwa ninamjua sana huyu Halima, yeye hatukuwahi kuongea sana,” nilimwambia Haijati, ilikuwa ni lazima nimkatae Issa kwani nilikuwa na mipango mizito sana kwa huyu mke wake.

    Sikutaka kuchelewa, kazi yangu muda huo ilikuwa ni kumsifia tu, niliujua udhaifu wa wanawake, unapoamua kuwasifia, mara kumuaminisha kwamba alikuwa na mzigo mkubwa kwa nyuma, alifungashia, alikuwa na kifua kizuri, macho ya goroli, uzuri wa Beyonce, niliamini kwamba ingekuwa rahisi kumpata msichana wa hivyo.

    Basi ikawa hivyo. Nilimsifia sana na kumwaminisha kwamba alikuwa mzuri kuliko wanawake wote. Mwenyewe akawa anafurahi tu, akatabasamu kana kwamba nilichokiongea kilikuwa kweli.

    “Umeumbika sana Haijati, u mwanamke mrembo sana,” nilimwambia kwa sauti ya taratibu.

    “Mh! Asante.”

    “Yaani kama ningekuwa na mwanamke kama wewe, hata kazini siendi,” nilimwambia.

    “Hahah! Kwa nini sasa?”

    “Unataka baba mwenye nyumba aniibie! Ningekuwa nawe muda wote ule, yaani ningehakikisha hata nikienda chooni natangulizana na wewe. Haijati u mzuri mno, unajua kupendeza, ngozi yako inang’aa sana, huo uzuri, kweli wewe ni mwanamke wa Kizanzibari,” nilimwambia.

    “Asante sana!” aliniambia huku akisikia aibu.

    “Hivi kuna kitu gani mwanaume atakihitaji zaidi akiwa na wewe?” nilimuuliza.

    “Kwani mimi ndiyo kila kitu?”

    “Ndiyo! Ukiwa na njaa, mtu akikuangalia anashiba, mtu akichoka, anapata pumziko, Haijati, kama ningekuwa na nafasi ya kuwa nawe, nahisi ningekuwa na bahati zaidi ya mwanaume aliyefanikiwa kulala na wanawake wote warembo duniani,” nilimwamia.

    “Jamaniiiiiiii!”

    “Hebu angalia lipsi zako, zinaonekana laini sana, yaani ningekuwa mimi ndiyo Issa, nadhani muda mwingi ningekuwa nazilamba tu. Una kifua kizuri sana, yaani ningekuwa Issa, ningehakikisha saa ishirini na nne nakiangalia tu,” nilimwambia.

    “Mh! Jamaniiiiiii!”

    “Una sauti tamu sana Haijati, tamu mno, hebu ongea kidogo niisikie....kidogo tu jamaniiiiiiii....” nilimwambia huku nikitoa tabasamu.

    “Jamaniiiiiiiiiiiii...”

    “Mashallaaaaaah.......umebarikiwa kuliko wanawake wote,” nilimwambia, akaanza kucheka.

    “Inshallah!”

    “Ila ningependa niwe naisikia sauti yako hata nikiwa mbali nawe Haijati, naruhusiwa?” nilimuuliza.

    “Unamaanisha nini?” aliniuliza na hapohapo nikampa simu yangu aandike namba yake.

    “No! Namba hapana!”

    “Nakuomba Haijati! Naomba unionee huruma katika hili, najua kwamba ni vigumu lakini naomba unionee huruma katika hili, ninaumwa, ninahitaji tiba, nitibu kwa sauti yako, pleaseeeee...” nilimwambia kwa sauti tamu kishenzi, yaani mpaka leo sijui kasauti kale nilikatoa wapi.

    “Nimeolewa ujue.”

    “Najua! Sitokupigia ukiwa na mume wako! Niamini katika hilo!”

    “Huwa ninakuwa na mume wangu kila wakati!”

    “Lakini sasa hivi haupo naye, nitakuwa nakupigia muda kama huu, nakuomba Haijati!” nilimwambia.

    “Daah! Mtihani mgumu huu!”

    “Lakini bado unaweza kupata A.”

    “Hahah! Una maneno wewe!”

    Nilimbana, kila alichokuwa akisema, nilikipangua kiakili sana. Kwa jinsi alivyoonekana tu hakuwa na ugumu wowote ule, alikuwa mteremko ila alitaka kunipima kuona kama nilikuwa mkazaji ama la.

    Wakati nikiendelea kubembeleza, mara Halima huyo akarudi na chakula na kukaa na kuanza kula. Nilichokuwa nikikifanya ni kumwangalia Haijati kisiri kwa jicho lililomaanisha alikuwa na kitu ambacho nilikihitaji sana.

    Akawa anachekacheka tu. Walikula na walipomaliza, nikawaaga ila palepale ili kuonyesha umwamba, nikaingiza mkono mfukoni na kutoa pochi yangu, nikatoa laki mbili, laki moja nikampa Halima na nyingine Haijati.

    “Ahsante sana jamani,” alisema Halima.

    “Nashukuru!” alisema Haijati.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haina shida. Tutaonana! Ngoja kwanza niende kukta tiketi ya ndege keshokutwa niendelea Malawi mara moja,” niliwaambia, sikutaka kubaki, hapohapo nikasimama na kuondoka zangu.

    Kile nilichokifanya niliamini kwamba kilikuwa sumu kali kuliko hata Cynaide, niliamini kwamba kwa namna moja ilikuwa ni lazima nikamilishe mambo yangu.

    Kichwani mwangu niliamini kabisa kwamba Haijati alikuwa akienda kulala kitandani kwangu tu kwani kwa mikwara niliyoipga, ilikuwa balaa ile kishenzi.

    Hawa wawili nilitaka nimalizane nao, nianze na nani? Nikajifikiriaaaa, nikajua kwamba kama ningeanza na Halima, ningepata kazi kumpata Haijati, hii ni kwa sababu Halima angeweza kumwambia, ila kama ningeana na Haijati, ingekuwa rahisi kumpata hata Halima kwa sababu Haijati angefanya siri kwa kuwa alikuwa ameolewa.

    Nikalifuata gari langu na kuondoka zangu. Nilipofika njiani, mara nikasikia simu yangu ikilia mlio uliomaanisha kwamba kulikuwa na ujumbe wa simu, nikaichukua na kuuangalia.

    “Ahsante sana,” ulisomeka ujumbe, kuangalia namba ilikuwa ngeni.

    “Samahani! Nani?” niliuliza.

    “Haijati!”

    “Waooo! Namba yangu umeitoa wapi?”

    “Nimeiiba kwa wifi. Aliniachia simu akapeleka vyombo!” aliniandikia.

    “Nashukuru sana kuipata namba yako mrembo. Hakika hii ni bahati kubwa sana kwangu, naomba nikupigie,” nilimwandikia meseji ndefu.

    “Sawa.”

    Sikutaka kuchelewa, nikalipaki gari pembeni na kumuendea hewani. Nilianza kuzungumza naye, nilihisi kabisa kwamba mwili wangu ulibadilika kabisa, kulikuwa na hali tofauti nilianza kuihisi mwilini mwangu.

    Niliongea naye kidogo, nikamuuliza alipokuwa akiishi, akaniambia alihamia Mabibo yeye na mume wake, Issa. Kutoka mabibo mpaka nyumbani kwangu pale Sinza, hakukuwa mbali, nilimwambia kwamba ninataka kumuona akiondoka kwa Halima.

    “Leo hii?” aliniuliza.

    “Yeah! Nimekumiss sana mpenzi,” nilimwambia, nikaingiza jina la mpenzi nione lingeitikiwa vipi.

    “Nitaangalia. Nitakushtua nikitoka,” aliniambia na kukata simu.

    Jamani! Vijana tafuteni pesa, hiyo ndiyo suluhisho la kutembea na mwanamke yeyote yule unayemtaka. Unapokuwa na pesa unajiamini, unajiona wewe ndiyo wewe na hakuna wa kukubabaisha.

    Yaani hebu fikiria, huyu Haijati nimekutana naye leo, nikamwambia maneno matamu leo na kumsifia kidogo na nilipomgusia kuhusu kuonana naye, akakubali.

    Yaani nimeonana naye leo, ni mke wa mtu, hakuwa akinifahamu kabla lakini mtoto alielekea kibra, halafu nimuache? Sina Ukristo huo.

    Nikasema kwamba siku hiyo ilikuwa ni vita, nilichokifanya ni kwenda kwenye duka moja hivi lililokuwa Mlimani City na kununua pingu fulani za faragha.

    Kwa wale wanaofuatilia sana mambo ya faragha watakuwa wanazifahamu hizi pingu. Huwa zinatumika sana, yaani mwanamke au mwanaume anafungwa kitandani mikono na miguu yake na kumwachia mtu aanze kufanya yake.

    Hilo ndilo nililotaka kulifanya. Haraka sana nikaenda katika duka hilo lililokuwa Mwenge kwenda kununua vifaa hivyo.

    “Nataka seti nzima, huwa kuna nini na nini?” nilimuuliza muuzaji.

    “Kuna pingu, mkia wa farasi (Brainded leather whip), kifaa cha mshine cha mtetemo (Vibrator Rechargable) na pampu (Vibratting Butt),” alinijibu.

    “Kiasi gani?”

    “Laki nne!”

    “Naomba!”

    Hivi vilikuwa vitu muhimu sana, kuna wale wanaume ambao wanadharaulika, wanaonekana kuwa si kitu faragha huwa wanatakiwa sana kuvitumia hivi vifaa.

    Kwa wanawake wanajua, utakuta anakutana na mwanaume anamwambia jamaa amenipaka shombo mno, basi hii ndiyo huwa suluhisho, ni vifaa vya siri sana ambavyo vinapotumika, kama ni mke wa mtu, atakung’ang’ania na kuhitaji umuoe kabisa.

    Basi nikapewa zangu na kuondoka. Nilipofika nyumbani, nikatoa tabasamu, nikasema kwamba siku hiyo ndiyo ilikuwa ni ufunguzi wa nyumba hiyo.

    Ilipofika majira ya saa nane, Haijati ananitumia meseji kwamba alikuwa akitoka hivyo alihitaji kuonana nami.

    “Njoo Sinza!” nilimwambia.

    “Halafu?”

    “Twende sehemu!”

    “Ila sitaki hotelini wala nyumba ya wageni,” aliniambia. Nikacheka sanaaaaaaa.

    “Usijali! Kwangu je?”

    “Chumbani siingiii....”

    “Jamaniiiii!”

    “Labda mpaka tuzoeane!”

    “Haina shida!”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mtu mzima nikaandaa mazingira, ilikuwa ni lazima nihakikishe kila kitu kinakuwa sawa kabisa. Baada ya nusu saa akasema kwamba alikuwa akiteremka Shekilango hivyo nimfuate. Haraka sana nikamfuata, nikamuingiza ndani ya gari na kuondoka zetu.

    Tulikuwa tunaongea mambo mengi mno njiani, baada ya dakika kadhaa, tukafika, nikaliingiza gari ndani, tukateremka na kuelekea ndani.

    Haijati alikuwa akishangaa, hakuamini alichokuwa akikiona. Nyumba ilikuwa kali mno, ilipendeza na kila kitu alichokiona alihisi kama alikuwa kwenye ulimwengu fulani hivi. Tulipofika sebuleni, akakaa kwenye kochi na kumsogelea.

    “Nikuletee nini?” nilimuuliza huku nikiwa karibu naye.

    “Chochote kile.”

    “Kuna maziwa, juisi, soda, chokleti, unahitaji nini bebi,” nilimwambia, jina la bebi nalo nikalitaja kama kurahisisha mambo yangu!”

    “Naomba juisi!”

    “Ya pasheni au maembe!”

    “Yoyote upendayo!”

    “Sawa.”

    Nikainuka na kuelekea kwenye friji na kumletea juisi. Hakuacha kushangaa, nilijua tu alikuwa akiyafikiria maisha yangu kwamba yalikuwaje, kwa nini nilionekana kuwa na pesa kiasi kile.

    “Wifi yangu yupo wapi?” aliniuliza swali la kijingaaaaa...yaani kwenye maswali yote duniani, hili ndilo la kijinga, na mwanaume ukiulizwa swali hili usishtuke, hili humaanisha kwamba nimekubali kuwa na wewe kwa gharama zozote zile.

    “Hakuna wifi!”

    “Kaenda wapi?”

    “Nipo singo tu! Mapenzi yalinipelekesha kishenzi,” nilimwambia kwa sauti ndogo.

    “Kivipi?”

    “Pesa si kila kitu, wakati mwingine mwanamke anahitaji muda, nilikuwa bize na kazi hivyo akaamua kuondoka,” nilimwambia.

    “Mh! Kwa hiyo bado upo bize?”

    “Hapana! Nilijifunza, sasa hivi biashara zangu zote nimeweka wasimamizi, hivyo nina muda mwingi mno,” nilimwambia.

    “Sasa si ndiyo umrudishe!”

    “Ameolewa! Yeye ni Muislamu, hivyo alipoondoka, watu wakanyanyua jiko fasta. Au nimsubiri mpaka aachike,” nilimwambia.

    “Sio vizuri hivyo,” aliniambia.

    Tukawa tunapiga stori. Yaani kama kunakuwa na jambo linataka kutokea, utajua tu. Tulianza kwa kukaa makochi tofauti, tuliongea weeee, nikahama na kuhamia kwenye kochi lake alilokalia la watu wanne. Yeye alikaa kule mwisho na mimi huku.

    Tuliendelea na stori, tukajikuta tunasogeleana tu na mwisho wa siku kuwa karibu-karibu kabisa kiasi cha kusikia pumzi za mwenzako.

    “Una sauti nzuri sana,” nilimwambia kwa kumnong’oneza.

    “Ahsante!”

    “Nataka niisikie sauti yako ikitoa sauti nyingine ya faragha! Naruhusiwa?” nilimuuliza, alikuwa mtu mzima, si mtoto hivyo alijua nilimaanisha sauti gani.

    “Jamaniiiiiiii....” aliniambia, hata kabla hiyo jamani yake haijamalizika vizuri, akashtukia mkono wangu ukianza kazi maalumu ya kuanza kutoa nguo moja na nyingine, hakunikataa, alibaki akiniangalia, yaani kwa kifupi ni kwamba alikuwa tayari kwa kila kitu.



    Nilikuwa mtundu wa kufanya kitu chochote kile faragha, nilimwangalia Haijati huku nikiona kabisa mchana wa siku ile alikuwa akienda kupata tabu sana. Sikutaka kuchelewa, haraka sana nikambeba juujuu na kumpeleka chumbani.

    Nilipomfikisha, nikamuweka kwenye kitanda na kuanza kumwangalia kwa macho yaliyoonyesha ni kitu gani nilikuwa nakihitaji kutoka kwake muda huo. Nilipomkumbuka Issa tu, hasira zikanishika zaidi na kujihakikishia kwamba siku hiyo ilikuwa ni siku ya vita.

    Nikamtoa nguo zote mwilini na kwenda kwenye kabati, nikachukua pingu ya faragha na vifaa vingine na kurudi. Alibaki akinishangaa, hakujua kazi yake kwa sababu si Watanzania wengi wanatumia vitu kama hivi. Kwanza, nikamfunga pingu na kumwambia kwamba siku hiyo ilikuwa ni ya kipekee sana.

    Yaliyotokea hapo, si vizuri kuyaandika hapa ila kwa kifupi ni kwamba Haijati alimsaliti mumewe, nilimchukua mke wa Issa pasipo mwenyewe kugundua kitu chochote kile. Nakumbuka tulichukua saa mbili kitandani ndipo tukaenda kuoga, na huko napo, tukarudia kidogo na kuelekea chumbani kuvaa.

    Aliniangalia, hakuamini kilichotokea, hakutarajia kukutana na harakati za kigaidi kama zile alizokutana nazo. Nilimwangalia kwa macho ya kutaka kusikia kitu chochote kile kutoka kwake kwani niliamini kwa jinsi moto ule nilivyouwasha, asingeweza kukaa kimya hata kidogo.

    “Kamwili kadogoooooo...” aliniambia huku akiniangalia, nikaanza kukenua.

    “Lakini.........”CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kanajua mambo! Yaani pamoja na ujanja wangu...sijawahi kukutana na mtu kama wewe. Umejifunza wapi?” aliniuliza huku akianza kuvaa taiti yake ya ndani kabla ya kupiga dela lake.

    “Hahah! Kwani hivi tunajifunzia sehemu?” nilimuuliza.

    “Si kawaida kabisa. Yaani pale uliponifunga zile pingu zako mikononi na miguuni, haki ya Mungu ungeniua...yaani nilihisi kabisa mtoa roho alikuwa akinifuata,” aliniambia.

    Nikacheka mno, hilo nililijua, nilikuwa mzoefu wa kupata stori kuhusu zile pingu. Kwa mara ya kwanza nilipoambiwa, jamaa alisema kuwa unaweza hata kutaka kumuua mtu kwani inakuwa ni mara tano ya ile hali anayoisikia kikawaida.

    Siku hiyo niliamini, na nilipokumbuka jinsi alivyokuwa akikileta kifua chake juu na kushuka chini, niliamini kabisa ningeweza kumuua. Haijati akachanganyikiwa, aliniambia kabisa kwamba angemsaliti mume wake kwangu katika maisha yake yote, na hata kama ingetokea siku nimeoa, bado angehitaji kupata nafasi ya kuwa nami.

    “Sawa. Wewe tu,” nilimwambia.

    Baada ya dakika kadhaa tukatoka na kumsindikiza mpaka Tabata Bima na mimi kurudi zangu. Nilifurahi sana, unajua unapokuwa na adui yako halafu unafanya kitu ambacho unaamini kabisa kwamba kama ingetokea siku akajua, ataumia sana, basi ungefurahi mno.

    Niliporudi nyumbani, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwasiliana na Halima, nilihitaji kumseti kwanza kwa sababu ni zamu yake ndiyo iliyokuwa ikifuata. Nikaanza kuchati naye mpaka majira ya saa tano usiku, alilegea kwa sababu alijua kwamba nina pesa, basi kila kitu nilichokuwa nikiongea, alikuwa akichekacheka tu.

    “Ila nilikumisi,” aliniambia bila aibu, eti alinimisi, nilikuwa kapuku, alinimisi kwa lipi? Ila kwa sababu na mimi nilikuwa nahitaji kitu kutoka kwake, nikaunganisha.

    “Hata mimi! Nimekuwa nikiota ila siku kuhisi wewe. U msichana wa ajabu sana,” nilimwambia.

    “Kweli?”

    “Yaah! Nikuulize swali?”

    “Niulize!”

    “Hivi umevaa ya rangi gani hapo?” nilimuuliza.

    “Nini?”

    “Acha utoto bwana!” nilisema na kuanza kucheka kile kicheko cha chini.

    Alikuwa mtu mzima, alijua kabisa kile nilichomaanisha ila mwenyewe akaanza kujifanya kama mtu anayesikia aibu kubwa. Akaanza kujiumauma ila mwisho wa siku akaniambia mwenyewe.

    “Rangi ya pinki!”

    “Oh! Daah! Natamani sana siku nione jinsi inavyokupendeza. Unavaa kiuno namba ngapi?” nilimuuliza.

    “Mh! Wala sijui! Mi nanunuaga tu! Kwa nini umeuliza?” aliniuliza.

    “Nataka nikununulie kadhaa, tena nikuvalishe mimi mwenyewe,” nilimwambia kwa sauti fulani hivi ya kimitego.

    “Mh! Utanichungulia!” aliniambia.

    “Nitafumba macho! Kweli sitoona,” nilimwambia.

    Kwenye maongezi kama haya ndipo unapogundua kuwa mwanaume raha sana. Yaani unaanza kuona mwili wako ukianza kupata hali fulani na sehemu moja kuanza kukakamaa.

    Sauti yake ilibadilika kabisa, yaani nilijua alianza kuingia kwenye ulimwengu fulani hivi, na mimi ninavyopenda sifa, tena ninavyojua kuitumia sauti yangu vizuri, basi ndiyo nikaongeza na kuongea.

    “Edward...” aliniita, tena kwa sauti kuonyesha kwamba alichanganyikiwa.

    “Nipo hapa mpenzi!”

    “Hivi ushawahi kufanya kwa kutumia simu?” aliniuliza.

    Kwanza kabla ya kujibu nikanyamaza, nikaanza kujifikiria mambo mengi, swali lake lilikuwa na mitego mingi, kama ningemwambia nimeshawahi kufanya basi angegundua kama mimi nilikuwa malaya tu, na kama ningemwambia kwamba sijawahi kufanya basi angeniona boya.

    Kiukweli niliwahi kufanya zamani sana wakati nasoma, kipindi hicho unajiunga na tigo saa sita usiku na kupewa dakika ishirini na tano. Kipindi hicho ndicho nilichofanya sana kwa kutumia sauti, tena nilikuwa mtu hatari.

    Nilizungumza kwa hisia, nilimtega, niliongea maneno ambayo yalimfanya msichana yeyote yule achanganyikiwe na mwisho wa siku kuniambia alitaka kwenda kuoga kwani alichafuka kana kwamba alitoka kucheza mpira.

    Hako kaswali kake kamoja tu kakanifanya nikumbuke mademu wengi wa kipindi kile shule, hasa Fatuma ambaye kwangu ndiye alikuwa mtu dhaifu sana.

    “Edward ongezaaaa....” niliyakumbuka maneno yake hayo, yaani tulikuwa tukiongea kwenye simu lakini alichanganyikiwa.

    Hakuwa huyo tu, walikuwa wengi, tatizo la Fatuma ni kwamba aliwaambia marafiki zake ambao nao walijilengesha na mimi sikutaka kuonekana mshamba, walihitaji pipi ya kijiti, mimi nikawapa ice cream wanyonye kabisa.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sijawahi kufanya kwa simu, huwa sipendi,” nilimjibu kabisa.

    “Sawa.”

    Nilijua, alichanganyikiwa mno lakini hakuwa na la kufanya. Sikutaka kuendekeza mchezo wa kufanya kwa simu kwa sababu nilikuwa nimekua, sikuwa mtoto kama kipindi kile shuleni.

    Nilimwambia Halima kwamba nilitaka kuonana naye hivyo ingekuwa vizuri sana kama kesho ndiyo ningeonana naye. Akakubali na hivyo kuniambia nijipange kwani yeye alikuwa mtu hatari sana.

    Nikacheka sana, mimi huwa siamini kama kuna mwanamke anakuwa hatari kama mwanaume, na kama yeye alitamba sana kwamba alikuwa hatari, nilitakiwa kumuachia nione ukali wake ulikuwa wapi.

    Nawajua watoto wa kike, huwa hawana pumzi za kutosha. Wapo hivyo, tena wote duniani. Katika kipindi cha dakika kumi za mwanzo, wanaanza kucheza kwa kasi sana ila baada ya hapo pumzi inakata na kukwambia nimechoka. Hapo ndipo zamu yako inapokuja na kumwambia kwamba hutakiwi kuchoka, humu hujaja kulala, umekuja kufanya kazi tu.

    “Hivi una pumzi kweli?” niliamua kumuuliza kwa meseji.

    “Kwa nini umeniuliza hivyo?”

    “Ninataka kujua. Una pumzi?” nilimuuliza.

    “Utaona kesho. Nataka kukuonyesha kwamba kungwi wangu hakufanya kazi ya bure,” aliniandikia.

    Huwa sinaga presha kabisa, baada ya kuniambia hivyo, nikachukua cd yangu ya Kamasutra na kuanza kuangalia, unajua alinitisha sana, nilihisi kwamba alikuwa mtu hatari.

    Nilichukua mafunzo kabisa, sikutaka kupitwa na chochote kile, baada ya kumaliza kutazama, nikanywa maziwa na karanga nyingi nikijiandaa kwa ajili ya siku inayofuata.

    Kweli bwana, siku hiyo ilipofika, Halima mwenyewe akanipigia simu na kuniambia nipange tuonanie wapi. Sijui alikuwa akinitega! Nina kwangu, nimenunua nyumba, inakuwaje twende kwenye nyumba ya wageni? Aje humuhumu, kwanza ndipo kwenye vifaa vyangu.

    “Njoo kwangu!” nilimwambia.”

    “Kwako?”

    “Yaap! Wewe njoo, usiogope, timu nzuri inacheza uwanja wowote ule,” nilimwambia.

    “Sawa! Ngoja nijiandae.”

    Hii ni kwa wanaume wote. Kitu cha msingi ni kutafuta pesa. Achana na kunyanyua vyuma, haisaidii hata kidogo, utaonekana kama mlinzi tu lakini pesa ndiyo kila kitu.

    Wanawake wanapenda pesa, wanapenda kutunzwa, wanapenda kununuliwa zawadi za kila aina na ndiyo maana kwa mtu kama Halima hakuwa akinisumbua hata kidogo kwa kuwa alijua kabisa nilikuwa na pesa.

    Nikafungua friji na kuangalia vinywaji, vilikuwa vimepungua sana na hivyo nilitakiwa kuongeza kidogo. Nikatoka na kwenda kwenye duka moja la vinywaji lililokuwa Sinza Kijiweni.

    Nilipofika hapo, macho yangu yakatua kwa msichana mmoja hivi, alikuwa mdogomdogo tu, alibana nywele zake kwa nyumba na kuvaa kisketi fulani kilichokwenda mpaka juu ya magoti yake kidogo.

    Alikuwa mzuri, pembeni ya pua yake kulikuwa na kidoti. Wanaume walikuwa wakimwangalia, si kwamba alifungashia, bali ule uzuri wake ilikuwa ni balaa. Nililiacha gari nyumbani, hapo nilikwenda kwa bodaboda kwa kuwa hakukuwa mbali kabisa.

    Nilimwangalia, nikasema haiwezekani, nikaanza kumfuata kwa nyuma, sikuona aibu yoyote ile, watu walikuwa wakimwangalia lakini nilijiamini mno.

    “Hey Miss...” nilimuita lakini hakugeuka, aliendelea kwenda mbele huku akiwa na mfuko uliokuwa na boksi la soda.

    Nikamfuata kwa kasi kidogo, nilipomkaribia, nikamshika mkono. Najua hakupenda lakini hakuwa na jinsi, akautoa mkono wake, akageuka na kuniangalia huku akionekana kuwa na hasira na mimi.

    “Niache huko,” aliniambia huku akiniangalia.

    “Samahani dada!" nilimwambia. Akageuka na kuendelea na safari.

    “Unakuwa mkali sana, kwa nini? Au kwa sababu hunifahamu?” nilimwambia huku tukipiga hatua.

    Hakunijibu, alikuwa kimya kama bubu na alivimba mno. Sikutaka kukata tamaa, niliwajua mademu, huonekana wagumu wakati mwingine kwa kuwa wanahitaji lugha fulani tamu, si ile ya kuonekana mhuni.

    “Najua hunijui! Najua unaniona mtu wa ajabu kabisa, ila naomba nikwambie kitu kimoja,” nilimwambia kwa sauti ya chini. Hakujibu.

    “Umependeza sana, yaani kama Tiwa Savage,” nilimwambia. Akabaki kimya tu.

    “Jamani! Yaani pamoja na kukusifia hata asante! Niambie ahsante tu niridhike nirudi,” nilimwambia. Akabaki kimya.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Miss! Naomba niambie niridhike nirudi, sihitaji kukupotezea muda wako,” nilimwambia kwa sauti ya chini lakini bado hakutaka kuzunguma lolote lile.

    Baada ya muda fulani akafika kwenye nyumba moja na kufungua geti na kuingia ndani. Mtu mzima nikabaki nje, sikujua ni kitu gani nilitakiwa kufanya.

    Nikaanza kujiuliza kama ilikuwa ni sahihi kuondoka ama kubaki hapohapo. Kiukweli yule msichana nilimpenda kwa kuwa alikuwa na sura nzuri, nilijisemea kwamba endapo ningeondoka basi ningemkosa, ili kuonyesha kwamba nilihitaji sana kuzungumza naye, nilisubiri kama dakika tano hivi, nikapanga kupiga hodi kumuulizia.

    “Mh! Subiri kwanza,” nilisema.

    Kwa wanawake kupo hivi, endapo tu ungeanza kuzungumza naye kwa kumtaja jina lake basi ungefanikiwa kumpata, kitu cha kwanza angekuwa anajiuliza umemjuaje, hiyo ingekuwa nafasi kwako kuanza kumchambua kama karanga.



    ITAENDELEA





0 comments:

Post a Comment

Blog