Search This Blog

Monday, October 24, 2022

RIGWARIDE LA AFANDE - 2

 





    Chombezo : Rigwaride La Afande

    Sehemu Ya Pili (2)



    ILIPOISHIA

    Kwa mbali nilijikuta nasisimka kama binadamu. Kama mwanamke, tena mwanamke mwenyewe msichana, kijana kama mimi, damu bado changa! Lakini moyoni nilijiambia…



    “Ila mimi ni kiboko…nyumba moja, wanaume watatu tena afadhali ingekuwa siku mbalimbali, leoleo?! Mh!”



    Wakati nawaza hivyo, yule mwanaume alinitegesha, nikakaa mkao wa kutengwa…

    “Ngo… ngo…afande Mwira,” sauti iliita nje baada ya kugonga mlango…

    ENDELEA MWENYEWE SASA…



    “Unaona sasa?” nilimsema yule. Kumbe ni afande Mwira…

    “Shii,” alinipa ishara kwa mkono kuashiria kwamba nisiseme. Nikakaa kimya. Hapo tayari niko kitandani ujue, tena nimeshategwa!



    “Afande Mwira,” ile sauti iliita tena. Safari hii kwa juu kidogo. Niliweza kuitambua kwani nilikuwa makini nayo, nikabaini ni ya yule mbaba wa kwanza kabisa…

    “Ee afande,” aliitika afande Mwira sasa…

    “Umelala?”



    “Hapana, vipi?”

    “Tuongee kidogo basi.”

    Mimi mapigo ya moyo yalishika kasi, kusikia tuongee kidogo maana si afande Mwira alishasema kuwa, kuna mwenzake ana tabia ya kuingia bila kupiga hodi.

    Ingawa mlango ulifungwa lakini nilikuwa nina wasiwasi, hasa nilipojaribu kukumbuka kwamba, huenda nilikuwa natembea kwenye mtego wa wanaume.



    Afande Mwira alitoka kitandani, akavaa bukta na kwenda kufungua mlango kisha akasimama mlangoni ili yule mwenzake asiingie…



    “Vipi…yaani kuna kabinti bwana nilikuja nako leo…weee! Moto! Kabinti katundu kitandani kama kamechezwa ngoma za kwetu. Kuna siku nitakaleta tena utakaona…kabinti kamjini…pale niko tayari kuteketeza hata mshahara wangu ili nikaoe,” hayo maneno yalikuwa yakitoka kwenye kinywa cha yule mbaba.



    Hapo hakuna shaka moja kwa moja kwamba alikuwa ananizungumzia mimi. Nilishangaa sana na misifa hiyo kwangu…kumbe mpango wake ni kunioa, nilichekea moyoni…



    “Lo! Kanakaa wapi?” aliuliza afande Mwira ambaye mimi nilikuwa kitandani kwake…

    “Kwao.”

    Afande Mwira alicheka, mimi mwenyewe pia nilijikuta nikicheka maana sikutegemea jibu hilo. Mtu anaulizwa ‘anakaa wapi?’ anajibu ‘kwao’. Lazima itakuwa kwao, sasa huko kwao ni wapi?



    “Mbona unacheka afande Mwira?”

    “Nacheka maana umenipa jibu ambalo lipo….”

    “Anasema anakaa mitaa ya Wailes kule, kwa baba yake na mama yake.”

    Hakuna kubwa waliloendelea kuzungumza, afande Mwira akamuaga mwenzake, akarudi ndani akifunga mlango kwa kitasa taratibu sana…

    “Hivi wewe binti, kumbe upo hivyo?” afande Mwira aliniuliza…

    “Nikoje?”



    “Yaani humu ndani leo ulikuwa kwa wanaume wangapi?”

    “Kwani vipi?”

    “Huyu afande anasema ulikuwa kwake lakini mimi si nilikusikia ukihema kwa afande mwingine?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Labda mwingine. Nyie wenyewe mnaonekana humu ndani mnapenda sana wanawake…”

    “Kwani we unakaa wapi?”

    “Si Sinza…”



    “Sinza! Hukai mitaa ya Wailes wewe?”

    “Aka! Wailes napajulia wapi mimi.”

    Nilimwona akilainika, akaachana na maswali yake, akazidi kunitega, filimbi ikapulizwa, mchezo ukaanza.



    Safari hii niliamua moja, kwamba hata kama nitajiachia vipi sitahemuka tena kwani niligundua nikihemuka ndiyo nasikika na wengine, halafu wananifanyia taiming.

    Huyu naye alikuwa wa aina yake, badala ya mimi kuwa na sauti ya muhemko nilimshangaa yeye akaanza kupiga kelele…



    “Weee! Weee! Ndiyo nini sasa?” nilimuuliza mwenzangu kwa sauti ya chini…

    “Ni kawaida yangu…hii ni kawaida yangu binti,” alinijibu kwa sauti ya juu huku akiendelea na kelele zake.



    Ilibidi nisitishe kutoa ushirikiano kwani sasa nilianza kuhisi tunaumbuka wote. Nilijua kelele zake za mahaba zingefika hadi kwenye vyumba vya maafande wengine halafu wangefuatilia kujua kwa afande Mwira kuna nini kinaendelea…

    “Sasa inakuaje tena binti…eee! inakuaje?”

    Kusema kweli kwa sauti ya juu aliyokuwa anaisema, ilibidi niache kabisa kuendelea na soka…



    “Kama uko hivyo siwezi kuendelea na wewe. Unapiga kelele kama ndiyo siku yako ya kwanza bwana,” nilimsema.



    Lakini nikahisi dalili kwamba kuna mtu au watu wameshika kitasa cha mlango…

    “Wee unasikia…kuna watu mlangoni…kitasa chako kimeshikwa na mtu,” nilimwambia hivyo, ndiyo kidogo kwa mbaaali nikamwona anaacha manjonjo na kukazia macho kwenye mlango.



    “Afande Mwira…afande Mwira,” sauti za mtu zaidi ya mmoja zilisikika.

    Nilimwona afande Mwira akinyong’onyea kila sehemu ya mwili mpaka kule!

    “Eee,” aliitika…

    “Mbona unapiga kelele?” hii sasa ilikuwa sauti ya yule mbaba wangu wa mwanzo kabisa…



    “Niko sawa jamani…mbona kama tunaanza kufuatanafuatana?”

    “Kama upo sawa hebu fungua mlango basi,” ilisema sauti nyingine lakini nayo niliikumbuka ni ya yule afande wa pili aliyenikatia nusu laki.

    Nilijua kimenuka, msichana naumbuka. Tena mbaya zaidi naumbukia kwa mtu niliyeamua kwenda naye bureee! Kwa kumwonea huruma…

    “Fungua bwana…inasemekana uko na kale kabinti…”



    Nilimwona afande Mwira anatetemeka, lakini hakunishinda mimi. Nilitetemeka zaidi kwani nilianza kuhisi hali ya kupoteza fahamu kutokana na kuzomewa kwa kitendo changu cha kuwanyang’anya wanaume watatu kwenye nyumba moja na kwa siku moja, tena muda huohuo.



    Nilimtaka afande Mwira asingue kwani kufanya hivyo kungenileta balaa zaidi kuliko kutofungua…

    “Na leo atakula jeuri yake,” yule mbaba wa mwanzo alisema ndiyo nikazidi kuchanganyikiwa zaidi, nikaogopa sana.



    Ilifika mahali nikahisi nataka kulia, niliulaumu sana moyo wangu kwa kitendo kile.

    Sasa wale maafande wakawa wanagonga mlango kwa nguvu huku wakitishia kuvunja kama yule afande niliyenaye hatafungua mlango mwenyewe.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwani siwezi kupita kwenye hili dirisha?” nilimuuliza baada ya kuangalia dirisha na kugundua halina zile nondo zinazokatisha katikati ili mwizi asipite. Ni zile nyumba zilizojengwa zamani kidogo.



    Cha ajabu yule afande chumbani badala ya kunijibu, akawa eti anataka tuendelee na zoezi letu la mechi ya kitandani. Nikamkatalia katakata na kutoka kitandani…



    “Hivi wewe una ukali kweli? Yaani unaona kabisa unagongewa na wenzako tena wanaonekana wanajua kila kitu halafu bado unataka tuendelee!” nilimsema nikiwa napanda dirisha, akanisaidia kutoka kwa kunisukuma, nikaangua upande wa pili…tii!

    Kusema ukweli niliumia, hata niliposimama ili nitembee nilijikuta nachechemea.



    Nikachechemea mpaka nyumbani ambapo mama aliponiona nachechemea akataka kujua kisa…

    “Nimeumia mama…”

    “Umeumia na nini?”

    “Nilianguka kwenye mtaro mama.”



    “Kwanza unatoka wapi?”

    “Nilikwenda sokoni mama…”

    “Kununua nini na nani amekutuma?”

    “Vitu vyangu…”



    “Viko wapi?”

    Niliangalia chini kwa aibu maana maswali ya mama yalikuwa ya msingi…

    “Si nakuuliza wewe!”



    “Nisamehe mama,” nilisema nikiwa naangalia chini kwa aibu…

    “Kwanza hutoki kwa mwanaume wewe?” mama alinipiga swali jingine gumu sana. Nilitetemeka, moyoni nikasema…

    “Si mwanaume mama, natoka kwa wanaume watatu, hapa nimechoka ile mbaya.”

    “Si nakuuliza wewe.”



    “Ndiyo mama…”

    “Sasa..?”

    “Sitoki huko mama…”

    “Twende chumbani kwako.”



    Jamani, mama yangu namfahamu vizuri sana, aliposema twende chumbani kwangu nilijua anataka akanipekue. Sasa unadhani ingekuaje?! Ningekubali kwenda? Wee!

    “Mama nisamehe, tusiende chumbani.”



    “Basi niambie ukweli.”

    Nilishindwa kumwambia ukweli mama. Hata ungekuwa wewe ungemwambiaje!

    “Leo humu ndani huingii mpaka useme unatokea wapi?”

    “Mama natoka kwa rafiki yangu.”

    “Wapi?”

    “Temeke Mwisho.”



    “Twende sasa hivi tukamuulize kama kweli wewe ulikwenda kwake. Usimpigie simu wala usimtumie meseji,” alisema mama. Alinipa mawazo mengine tena, nikaona hakuna haja, ni kulisanua tu.



    “Mama nilikwenda kwa mwanaume kweli,” nilimwambia mama huku nikimwangalia kwa macho ya umakini sana ili asije akanivaa na kunipiga.

    “Mwanaume gani?”

    “Simjui mama…”



    “Ha! We mtoto…mwanaume humjui na unakwenda kwake? Twende sasa hivi ukanioneshe hiyo nyumba uliyoingia,” alisema mama akinishika mkono.

    Kweli, mama hakuwa na mchezo wala utani, tulianza safari. Mama yangu mimi ni mkali sana hivyo sikuweza kumkatalia hata kidogo.



    Tulikata mtaa, tukatokezea kwa mbele, tukaingia barabara kuu, tukavuka, tukatokea kwenye mtaro, tukauruka.



    Sasa watu wakawa wanatuangalia. Wapo waliosema napelekwa kuozeshwa kwa nguvu, wapo waliosema nakwenda kukeketwa, wengine walisema napelekwa hospitali kutolewa mimba maana ni mitaa ya hospitali.



    Nilifikiria namna ya kumpotosha mama, kwamba badala ya kumpeleka pale kwa jina afande Mwira nitafute nyumba yoyote yenye kufuli niseme ni hapo, lakini mwenyewe katoka…



    “Bado hatujafika?” mama aliniuliza kwa ukali. Aibu hana wala kuniwazia mimi kwamba naaibika, wala!

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ni pale mama, tumefika,” nilimwambia nikimwonesha nyumba nyingine nikijua mlango umefungwa lakini kumbe wenyewe walikuwepo maana ile tunakaribia tu, wakatoka wanawake watatu.



    “Ndiyo pale wanapotoka wale wanawake?” aliniuliza mama.

    “Hapana, kwa nyuma.”

    Na kweli, kwa nyuma ndiyo nyumba ya akina afande Mwira ilipo, tukafika sasa…



    “Ni wapi?” mama aliniuliza kwa ukali…

    “Hapa mama,” nilimwonesha mama ile nyumba. Cha ajabu sasa, mlango ulifungwa kwa kufuli jambo ambalo lilinishangaza sana mi mwenyewe…



    “Mbona pamefungwa na kufuli?” mama aliniuliza swali ambalo si langu. Sasa mimi ningejibu nini kwa huyu mama, kwani mimi ndiye nilifunga kufuli?

    “Mama hata mimi sijui kwa nini kuna kufuli,” nilimjibu tukiwa tumesimama.

    Mara tukasikia mtu akitembea kwa ndani na kutokea mlango wa uani ambao ulisikika sawasawa.



    Kutembea kule kukawa kunakuja mbele tuliposimama sisi, yaani mimi na mama.

    “Karibuni,” mwanaume mmoja, mrefu sana, mweusi tii, alitukaribisha huku uso wake ukionesha dalili zote za kutoka kulala…

    “Huyu alikuja hapa?” mama aliuliza bila salamu.



    “Kuja kufanya nini?”

    “Nimeuliza alikuja hakuja?” mama alikuja juu.

    “We mama…una akili kweli? Huna salamu…huna maneno mazuri unauliza huyu alikuja hapa…alikuja kwa nani na kufanya nini?”

    Mama alinigeukia mimi…



    “Kumbe unanidanganya siyo?”

    “Mama ni hapa, siwezi kukudanganya mama,” nilimjibu mama nikijua hashindwi kuniachia kichapo mbele ya yule mtu mweusi tii!

    “Kwani binti unamtafuta nani au ulikuja kwa nani?” yule mtu mweusi tii aliniuliza…

    “Namtafuta afande Mwira na wenzake.”



    “Unawajua?”

    “Nawajua.”

    “Muda huu wameshakwenda kwenye lindo. Kurudi hapa ni saa kumi usiku. Mimi ndiyo nimerudi muda si mrefu,” alisema yule mtu.



    Mama alikunja sura, akamwangalia yule mtu, akamuuliza…

    “Huyu hujawahi kumwona hapa baba?”

    “Hapana…”

    “Hapana mama…”

    Mimi na yule afande, wote tulikataa kwa pamoja ila sema mimi niliongezea na neno ‘mama.’



    Mama alisimama akijifikiria kwa muda kisha akafyatuka…

    “Sasa huyo afande Mwira sijui, nataka umjulishe kwamba namwachia mzigo huu. Akija hiyo saa ngapi sijui, atamkuta. Hawezi kumchezea mwanangu hivihivi naona. Kama alimwona anafaa angejitokeza nyumbani.”



    “Mama…mama punguza jazba, nimekwambia afande Mwira na wenzake wanarudi saa kumi usiku, utamwachaje mwanao hapa? Kwanza mbona anaonekana ni binti mkubwa, ina maana hawezi kujichunga mwenyewe?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “We unaangalia mwili, ana ukubwa gani huyu? Amejaa tu manyamanyama…mtu ana miaka 22 ndiyo mkubwa?” alisema mama huku mate yakimtoka kinywani kama mvua za kushtukiza…



    “Huyu ana miaka 22?” aliuliza yule mtu kwa sauti yenye mshangao…

    “Mimi ndiyo mama yake, namwacha hapa. Akija huyo afande Mwira mkabidhi, nitamfuatilia kesho,” alisema mama akiondoka.



    Nilitamani kumfuata mama kwa nyuma lakini nikajua nikifanya vile kwa wakati ule, moto utawaka. Nikaamua kusubiri baadaye sana.



    Lakini moyoni nilisema, ‘mama ungejua…si afande Mwira tu, na wenzake. Sasa kama kubaki au kukabidhiwa nije kukabidhiwa kwa nani?’

    Sasa tukabaki mimi na yule mtu tunaangaliana…

    “Unaitwa nani wewe?” aliniuliza kwa sauti ya chini huku akiniangalia kwa macho ya mlegezo…



    “Rhoda…”

    “Unaishi wapi?”

    “Kule Wailes…”

    “Unaishi na baba yako?”

    “Ndiyo, lakini kasafiri…”



    “Sasa huyo afande Mwira mlikutana wapi?”

    “Kule barabarani.”

    “Akaja na wewe hapa?”

    “Ndiyo.”



    “Kwa ajili ya nini?”

    Eti hilo nalo lilikuwa swali jamani? Mtu anajua afande Mwira ni mwanaume, mimi ni mwanamke. Sasa anadhani pale nitakuwa nilifuata nini?!

    “Kwani we unamzungumza afande Mwira gani?” nilimuuliza swali badala ya kumjibu…

    “Si huyu wa chumba cha kati…”



    “Mwanaume?” nilimuuliza kwa kebehi…

    “Ndiyo,” alijibu…

    “Huyohuyo,” nilimjibu.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akaniambia basi karibu ndani ukae umsubiri afande Mwira tuone inakuaje?

    Wakati anasema hivyo alikuwa akitembea kuelekea ndani nikamfuata kwa nyuma mpaka ndani kwake, yaani chumbani kwake. Nilichobaini ni kwamba, ile nyumba kila mtu alikuwa ana chumba tu. Na chumba hicho ndiyo kilikuwa sebule na chumba cha kulala…



    “Kaa hapo,” aliniambia akinionesha kochi kubwa. Nikakaa pwaa! Maana mimi naye, wowowo peke yake ni shughuli nzito…



    Nilijitupa kwenye kochi na kumwangalia yule mwanaume ambaye naye alionekana kunishangaa sana mimi lakini sikujua ni kwa nini anishangae vile…



    “Kwani wewe una matatizo gani na mama yako mzazi?” aliniuliza yule mwanaume huku macho yake yakipepesa kwingine na si kwangu…



    “Unajua mama ‘angu ana matatizo makubwa. Eti kisa nilikuwa humu ndiyo akamaindi na kuamua kunirudisha.”



    “Ulikuwa humu kweli au ulimdanganya?”



    “Nilikuwa humu kweli?”



    “Humu kwangu?”



    “Hapana, kwa afande Mwira.”



    Niliamua kukomaa na afande mmoja tu kwa vile nikisema watatu, ningekuwa kituko cha mwaka huu unaoisha kwa tumbuatumbua.



    “Ni nani yako?”



    “Mpenzi wangu wa ghafla.”



    “Khaa! Mpenzi wako wa ghafla? Oke! Sasa unadhani mpaka afande arudi usiku wa saa kumi utalala wapi?”



    “Nitarudi nyumbani.”



    “Mama ‘ako atakuelewa?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Najua hatanielewa,  lakini sasa wewe unadhani mimi nitalala wapi kama siyo nyumbani?”



    “Oke..umekula?”



    “Sijala na njaa imenikaba ile mbaya.”



    “Nikupe nini ule?”



    “Umepika nini kwani?”



    “Sijapika chochote. Wewe sema utakula nini?” aliuliza huku akiniangalia kwa macho yenye maswali mengi kuhusu mimi.



    “Utakachoamua wewe mimi nitakula tu,” nilimjibu kwa sauti iliyojaa ushawishi kwa mwanaume yeyote rijali wa kweli.



    Alikwenda kwenye friji, akatoa mayai matano, akaenda pembeni ya mlango ambapo pana meza yenye jiko dogo la gesi, akasetiseti mambo yake pale, akaanza kukaanga mayai bwana.



    Alipomaliza akayaleta meza ndogo ya katikati kisha akaenda kuchukua chupa ya chai, akaileta, akarudi tena kwenye friji akatoa mkate, akauleta mezani, akaniambia karibu chai…



    “Nakunywa peke yangu?” nilimuuliza kwa sababu nilimwona yeye akikaa kwenye kochi jingine pembeni…



    “Sasa ulitaka unywe na nani? Afande Mwira si nimekwambia atarudi usiku sana?” alisema.



    Nilihisi anaweza kuwa mwanaume mwenye utofauti na wenzake. Hakuonekana kunishobokea kama maafande wenzake wa mwanzo, akina afande Mwira.



    Nilijiungia chai, nikanywa wewee na mayai yote matano nikayamaliza, nikashiba vizuri sana. Nilitoa vyombo mwenyewe nikaviweka kwenye ndoo chini ya meza ya jiko. Nikarudi kukaa na kumshukuru huku simwangalii usoni…



    “Nakushukuru sana kwa chai, nimeshiba,” nilisema, lakini hakujibu, nikamshukuru tena, pia hakujibu, nikamwangalia. Kumbe alikuwa amelala zamani gani!



    Nilimfuata na kumtingisha…

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Oyaa! Anko…anko.”



    Alishtuka na kunikodolea macho mekundu ya kutoka kulala…



    “Vipi?” aliniuliza…



    “Nasema asante sana kwa chakula. Nimeshiba.”



    “Sawa, pumzika sasa, ukijisikia kwenda kwenu nenda,” alisema, akaendelea kujiliza.



    Nilianza kuamini kuwa, duniani kuna wanaume wakamilifu na wengine siyo. Na huwezi kumjua kwa kumwangalia kwa macho ya kawaida mpaka vitendo.



    Yaani jamaa alivyo na mvuto, mwili wenye siha njema, yuko na binti kama mimi, mbichi, nina mvuto wa kisichana halafu anachengachenga…mh!



    Nilichofanya, badala ya kukaa pale kwenye kochi, nikaenda kujilaza kitandani. Miguu ilining’inia, kuanzia kiunoni kwenda juu kulikuwa kitandani.



    Kila dakika kadhaa, niliinua shingo kumwangalia mwenyeji wangu pale alipolala, nikabaini anakoroma…



    “Loo! Maskini…ananikosa hivihivi kwa kuendekeza usingizi,” nilisema moyoni huku na mimi nikiwa nanyemelewa na usingizi kwa mbali maana nilikuwa nalishia kama samaki kwenye bwawa.



    Nilishindwa kujivumilia, maana mwanaume ni mwanaume, mwanamke ni mwanamke, kitendo cha kuwepo wawili chumbani kwangu hakikuvumilika. Afadhali basi angekuwa anko wangu au mtoto wa shangazi, lakini simjui, hanijui, loo!



    Niliinuka, nikatembea kwa kunyata mpaka alipokuwa amelala, nikakaa jirani yake lakini nikijitahidi nisimguse kwanza.



    Baada ya kukaa, nilimgeukia kumwangalia. Kumbe alikuwa ametoka kunyoa, nilikuwa nahisi manukato ya kunyolea yale.



    Nilipeleka mkono kumshika kidevu, nikakipapasa, akatingishika, nikaacha. Akaendelea kukoroma, nikapeleka mkono kifuani, nikaanza kumpapasapapasa kwa mbali sana, akatingishika, akapeleka mkono pale kifuani kama aliyehisi pana mdudu kwa hiyo alitaka kumtoa. Nikaacha, akaendelea kukoroma.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikapeleka mkono kinywani sasa maana kinywa kilikuwa wazi, akakivuta na ulimi, nikakitoa. Nikajua kumbe anapenda vitu vikiwa kinywani, nikamsogelea huku natoa ulimi, akapanua kinywa tena!





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog