Search This Blog

Monday, October 24, 2022

RIGWARIDE LA AFANDE - 4

 





    Chombezo : Rigwaride La Afande

    Sehemu Ya Nne (4)



    Nilishtuka sana mwenyewe kubaini kuwa, nimesema kwa sauti. Nikamwona afande Mwita akiniambia shiii!

    “Ah! Haya sasa, mambo yote tayari sasa…tunasubiri nini?” alisema mama akiashiria kwamba, amenisikia…

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Rhoda hakuna jinsi, itabidi nifungue mlango tu utoke, mama yako ameshasikia kila kitu,” aliniambia afande Mwita kwa sauti ya chini. Uso wake ulijaa wasiwasi na mshangao mkubwa.



    Niligeuka kuangalia dirisha, nikabaini ni kama la kwa yule afande wa muda ule. Lilikuwa dirisha kubwa, lakini halikuwa na nondo…

    “Kwani siwezi kutokea dirishani?” nilimuuliza.



    “Afande mwita ungekuja na huyo binti, mama yake ameshamsikia,” alisema afande Mwira huku sauti yake ikimalizikia kuonesha anaingia chumbani kwake. Bila kupoteza muda, nilipanda kwenye lile dirisha ili nirukie nje, afande Mwita akanishika mguu kunizuia…



    “Ukiumia je?” aliniambia kwa sauti huku amenitumbulia macho.

    Sasa akiwa bado amenishika mkono, alifungua mlango ili tutoke na tuonekane na mama.



    Mama ile kuniona tu akanivaa, tukaenda wote mpaka chini…

    “Mama unaniua…”



    “Na mimi lengo langu ufe, malaya mkubwa wewe. Sasa huyu ndiye nani? Kwa nini ulin’tajia mtu mwingine wakati anayehusika ni huyu,” alisema mama kwa sauti ya juu, nikajua nje ‘nzi’ watajazana sasa hivi…



    “Mama hata mimi siye ninayehusika, shetani tu ametupitia mimi na yeye. Mtu wake ni huyu afande uliyeingia naye ndani…”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wewe baba wewe…acha uongo wako. Hauna maana. Mimi ni mtu mzima, najua kila kitu. Wewe ndiye nimekunasa na mwanangu, lazima utamuoa,” mama alisema akiendelea kunishushia kipondo cha nguvu.



    Ikabidi afande Mwita aingilie kwa nguvu, kiaskari sasa ili kuniokoa. Ikawa ndiyo salama yangu…



    “Mama ukiendelea kumpiga huyu binti hatua kali za kisheria zitafuata juu yako,” alisema afande Mwita.

    “Mimi ninachojua baba, huyu binti kuanzia sasa anaishi kwako na ni mkeo. Kula, kunywa, kulala mpaka matibabu ni juu yako, kwa heri Rhoda,” alisema mama na palepale kuondoka zake huku akitembea kwa hasira.



    Nilibaki chini huku nikiendelea kulia kidogokidogo, kilio changu kikisindikizwa na kwikwi kwa mbali huku mkono mmoja nikiufunika uso…



    “Ingia ndani sasa,” afande Mwita aliniamuru, nikasimama na kuingia ndani kwake.

    Nilifikia kwenye kitanda na ndiyo nikaacha kulia na kuangaliana na afande Mwita.

    Nasema kuangaliana kwa sababu wakati namwangalia, nilibaini na yeye ananiangalia. Kwa hiyo ni sahihi kabisa nikesema tulikuwa tunaangaliana. Nilimlegezea macho, yeye akanikazia na kusema…



    “Ndiyo umeshakuwa mke wangu sasa.”

    Kwa mara ya kwanza nilijikuta nikitabasamu…

    “Unatabasamu mazuri hayo?” alinijia juu…



    “Jamani sasa nilie…mama kanikuta kwako, nimekwambia nitokee dirishani ukanikatalia. Nikisema ulitaka mwenyewe kuozwa kwa nguvu nitakuwa nakosea?”

    “Utakuwa unakosea sana. Wewe ndiyo ulitaka ujulikane uko kwangu. Ni nini kilikufanya useme kwa sauti muda ule?”



    Wote tukawa kimya, mimi mwili ulishalegea kwa kipigo cha mama. Japo kwa muda mfupi lakini nilichoka sana.



    Tukiwa chumbani, tulimsikia afande Mwira akija mlangoni kwa afande Mwita…

    “Afande,” aliita kwa sauti ambayo hakupenda kurudia tena kuita kwamba, afande Mwita hakusikia…

    “Ee afande.”



    Kulipita ukimya wa sekunde kama tano, afande Mwira hakusema njoo wala lolote lingine, afande Mwita akajua shida yake aende. Alifungua mlango, akasimama katikati…

    “Ee bwana pole sana. Lakini ndivyo maisha yalivyo. Sasa utafanyaje?”



    “Ndiyo niko naye hapa binti,” alisema afande Mwita huku akigeuka na kuniangalia nilipokuwa kwenye kitanda kisha akaufungua mlango kidogo ili afande Mwira anione, nikaachia tabasamu baada ya kukutana macho na afande Mwira, ‘nikakumbuka mbali’.

    “Hujambo binti?”



    “Sijambo, shikamoo.”

    “Marhaba…pole sana…”

    “Asante,” niliitikia nikiwa najificha uso.

    “Au afande Mwita ungemwambia aende kwa ndugu yake yeyote kama anaye hapa Temeke,” alisema afande Mwira…



    “Akha! Mi sina ndugu hapa Dar,” nilidakia mwenyewe tena si kwa kusema Temeke tu, Dar nzima.



    “Lo! Imekula kwako afande Mwita…sasa lakini wewe binti naye, ikawaje mpaka ukakubali kumleta mama yako hapa nyumbani?” alisema afande Mwira. Kabla hajajibu, afande Mwita akasema anakwenda chooni mara moja. Afande Mwira akabaki amesimama mlangoni…

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kwanza utakuwa mke wa nani humu ndani sasa?” aliniuliza kwa sauti ya chini, nikatabasamu…

    “Wewe hapo,” nilisema kwa sauti ya chini. Akanifuata kitandani haraka sana, akanipa denda, nikalipokea bwana…



    Tuligandana ndani ya denda kwa muda wa sekunde kadhaa mpaka tuliposikia mlio wa mlango wa chooni, tukaachana, afande Mwira akarudi kusimama palepale mlangoni…

    “Kwa hiyo ndugu yangu afande Mwira utanisaidiaje na huu ugeni?” alisema afande Mwita akimpita mwenzake mlangoni, akaingia ndani na kukaa kitandani…



    “Da! Mzigo huu bwana itabidi uwepo tu hapa nyumbani. Mimi naamini baada ya siku kadhaa, mama ataurejesha moyo wake nyuma, atamwita au atamfuata binti yake.”

    “Kweli?”



    “Kabisa. Kwa sasa si unajua ana hasira.”

    “Lakini kweli kabisa. Hapo na mimi nadhani iwe hivyo,” alisema afande Mwita akimuunga mkono mwenzake.



    Tulikutana macho na afande Mwira, nikaachia tabasamu nikijua kwamba, yeye hatafanya hivyo kwani alikuwa anatuangalia wote, mimi na afande Mwita. Nikamkonyeza kama mara tatu hivi…

    “Sasa mimi narudi kazini, sijui itakuaje?”



    “Oke, basi mimi utanikuta naye. Leo sitoki kwenda popote pale,” alisema afande Mwira huku akianza kutembea.

    Alipofika usawa wa dirisha kwa nje, afande Mwita alimuita afande Mwira…

    “Haloo, afande Mwira hebu nisuburi kidogo,” alisema afande Mwita huku akitoka chumbani.



    Alizunguka, akaenda kusimama na afande Mwira usawa wa dirishani. Walizungumza kwa sauti ya chini lakini nilichobaini ni kwamba, afande Mwita alikuwa anaazima pesa kwa afande Mwira. Nilisikia kwa mbali akisema ‘nitazirejesha mwisho wa mwezi.’

    “Twende nikakupe ndani,” alisema afande Mwira kwa sauti…



    “Nenda kalete, utanikuta hapahapa,” alisema jamaa yangu afande Mwita.

    Afande Mwira alitoka, afande Mwita akasimama usawa wa dirishani akimsubiri. Lakini mtu aliyesimama dirishani nje ilikuwa si rahisi aone ndani kukoje.

    Afande Mwira alifungua mlango, akazama ndani kwake. Mara akatoka, akasikika akitembea kuja kwenye chumba nilichokuwepo. Akashika kitasa, akasukuma mlango, akazama ndani kabisa ya chumba.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wote tukawa tunamwangalia afande Mwita alivyosimama kule nje ya dirisha akisubiri. Afande Mwira akanisogelea na kusema…

    “Jamaa yako kaniazima pesa…ndiyo nimemfuatia sasa.”

    Niliachia tabasamu laini huku nikimlegezea macho afande huyo kwani alikuwa amesimama akiniangalia kwa chini. Mimi mfupi yeye mrefu.



    Akanikumbatia, nikamkumbatia, akanibusu ndani kwa ndani, nikambusu ndani kwa ndani ili jamaa nje asisikie. Nikamwangalia tena, akaniangalia tena.

    “Mh! Kwa hali ninayohisi sitakubalia aondoke mpaka tufanye kweli hata kama huyo afande Mwita yupo hapo nje,” nikawaza.



    Muda wote huo tulikuwa tukiachana kuangaliana, tunakimbiza macho nje kupitia dirishani kumwangalia afande Mwita. Alikuwa akitembeatembea hapa na pale akisubiri pesa.



    Nilimwona afande Mwira akinipa denda, nikalikubali, tukadumu hapo tukihema kwa mhemko wa mahaba mazito huku afande akinishikashika sehemu mbalimbali za kifuani. Nikajikuta naishiwa nguvu zote.

    “Ila wewe mtoto unanipa raha sana tena sana,” afande huyo aliniambia huku akiwa kaishika vizuri nido yangu ya kulia.



    “Kwa nini unasema hivyo dia?” nilimwuliza.

    “Kwa mengi, kwanza siyo muoga na pili unayajua mapenzi sana,” afande Mwira alinifagilia.



    Tukiwa tumesimama kila mmoja wetu akiwa hajiwezi, afande Mwira akanitegesha sawasawa, nikategeka vilivyo.

    Akaniangalia kuashiria kwamba alihitaji nimpe, kwa kuwa akili ilikwishahama nami nikamwangalia huku macho yangu yakimweleza ‘sasa unangoja nini bwana!’



    Kwa kuwa macho nayo huwa yanazungumza, afande Mwira alinielewa akanivutia kwake na shughuli ikaanza palepale. Ilikuwa nusu tabu nusu furaha kwetu kwani macho yalikuwa yakicheza ndani na nje aliko afande Mwita.



    Lakini tulijitahidi kwa tabutabu hivyohivyo mpaka tukajikuta tunazoea. Sasa tukawa kama tupo huru kama nje hakuwepo afande Mwita. Maana mimi nilianza kuweweseka sasa, nikawa napagawa kwa maneno.



    Kadiri afande Mwira alivyokuwa akiwajibika ndivyo nilivyoshindwa kujizuia kupiga mayowe ya raha, ilibidi afande Mwira anishike kinywa ili nisipige kelele au sauti yangu isitoke nje ambako ingesikika vilivyo na kuzua balaa.



    Ili kwenda na muda, nikakazana sana, nikaona mwenzangu akitetemeka na mimi nikatetemeka. Loo! Afande Mwira akawasili kituo kikuu kama mimi nami nilivyowasili muda huohuo.



    Nikiwa nimeishiwa nguvu baada ya kumaliza mwisho wa safari isiyo na bughudha zaidi ya raha, afande Mwira alinikumbatia kisha kunichumu mara kadhaa midomoni na shavuni.



    Aliponifanyia hivyo kama tuliambiana tuangalie nje alikokuwa afande Mwita, tulipofanya hivyo tulimuona akitembea kuelekea upande wa choo, akazama ndani.

    “Jamaa yako kasubiri hadi kabanwa na haja ndogo,” afande Mwira akiwa bado kanikumbatia akaniambia.



    Kutokana na kauli yake hiyo, nikacheka kwa sauti kwa sababu nilijua hakuna mtu ambaye angenisikia na kumuuliza alijuaje kama ni haja ndogo na siyo mzigo mkubwa!

    Afande Mwira alicheka na kuniambia anaangalia saa kama afande Mwita atakaa kule msalani kwa zaidi ya dakika tano basi itakuwa amekwenda kukata gogo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Afande Mwira una maneno, sasa kukata gogo ndiyo nini?” nilimwuliza.

    “Na wewe kukaa kote katika hili jiji tena Temeke, hujui maana ya kukata gogo?” afande Mwira akaniuliza kisha kufunguka moja kwa moja maana yake.

    Nilicheka sana mpaka akaniziba mdomo kwa kiganja maana alihofia rafiki yake angesikia jambo ambalo hakupenda litokee.



    Tukiwa tunaangalia nje kupitia dirishani, tulimuona afande Mwita akitoka msalani ndipo afande Mwira akaniachia haraka na kutoka huku akijiweka sawasawa. Alikwenda nje, akampa pesa afande Mwita na kumwomba msamaha kwa kumchelewesha…



    “Usijali afande Mwira bwana. Kawaida sana, mimi nakushukuru kwa kila kitu, umenifaa maana nilikuwa sina kitu,” alijibu jamaa yangu. Akaja ndani. Lakini ghafla alisimama na kuniangalia sana…



    “Mbona macho yako mekundu na kama ulikuwa unalia?” aliniuliza…

    “Ni kweli nilikuwa nalia…”

    “Unalia nini?”



    “Nawaza mama kunisusa hapa…”

    “Hilo umelijua muda huu? Mbona muda wote ulichangamka?”

    “Imetokea tu, hata mwenyewe nashindwa kuelewa.”

    “Halafu mbona nasikia harufu ya jasho la mwanaume?”

    “Mh!” Niliguna, nikaogopa mwenyewe…



    “Mbona mimi silisikii,” nilisema nikijishauashaua na kuangalia pembeni.

    “Niambie ukweli Rhoda, kuna mwanaume gani aliingia humu ndani?”

    “Hakuna jamani! Kwani we umemuona nani?”



    “Kuna harufu ya jasho la mwanaume humu, huwezi kunificha mimi,” afande alinijia juu. Na mimi niliendelea kukataa. Moyoni nilisema haitatokea nikakubali.

    “Afande Mwira hajaingia?”



    “Sijamwona. Na angeingiaje wakati nilikusikia ukisema unamshukuru kwa kukukopesha fedha. Si ina maana aliingia ndani kwake kukuchukulia!”

    Niliposema hivyo tu, nilimwona afande Mwita akiishiwa nguvu na kukaa kwenye kochi…

    “Wewe umejuaje kama alinikopesha fadha?” eti alitaka kubisha.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Si nilikusikia hapa dirishani ukisema usijali afande Mwira bwana. Kawaida sana, mimi nakushukuru kwa kila kitu, umenifaa maana nilikuwa sina kitu.”

    Afande Mwita aliishiwa nguvu. Akawa anaangalia pembeni huku akiimba nyimbo za kwao. Mimi moyoni nikasema ‘kwisha kazi wewe.’

    ***

    Giza liliingia, sikumwona mama wala kupata simu yake. Nilikuwa nimelala wakati afande Mwira aliposema anakwenda baa kupata bia mbili tatu.

    Nilipitiwa na usingizi na nilikuwa sijala, kuja kushtuka ni pale afande Mwira alipoingia chumbani akiwa amebeba mfuko wa rambo…



    “Amka ule, nimekuletea chipsi kuku,” aliniambia.

    Niliamka haraka sana. ilikuwa chipsi kuku mzima! Du! Mate yalijaa yenyewe mdomoni, akatoa na kopo mbili za bia. Nilijua pale tunazitumbua pesa za mkopo kutoka kwa afande Mwira…



    “Kunywa na bia hizi,” alisema afande akiniwekea kwenye stuli…

    “Asante baby…”

    Kwa mara ya kwanza nilimuita baby lakini akanikataza nisimuite jina hilo yeye si mtoto…



    “Nani baby wako wewe! Koma kabisa! Niite mpenzi. Mimi si mtoto mpaka unaniita baby.”

    Nilijua jamaa zangu wa kule hawajuagi mambo hayo. Nikamwomba radhi na kumuita mpenzi.

    Baada ya kula, tulikwenda kuoga wote. Taulo lilikuwa moja. Kwa hiyo nililivaa mimi, yeye akavaa bukta.



    Tulipotoka kuoga tulipanda kitandani kulala. Kazi ikaanza hapo…

    “Wewe mbona kama unasinzia. Hakuna kulala hapa,” aliniambia…

    “Ha! We, yaani nisilale kisa nini wakati nasikia usingizi?”

    “Hapa kwangu hakuna kulala.”



    “Kwa nini? Ina maana na wewe hutalala?”

    “Tutalala wote baadaye,” alisema na kuanza kunishikashika. Nikamwelewa sasa kumbe alikuwa na maana gani kusema kwake hakuna kulala…



    “Sasa si ungesema tu,” nilisema moyoni huku nikianza kumuunga mkono kwa alichokuwa akikifanya yeye. Tulishikanashikana, tukashikanashikana.

    Ni yeye ndiye aliyeanzisha mchezo na mimi nikaingia uwanjani kupambana naye.

    Ilikuwa ni bandika bandua…bandika bandua!



    “Sasa tungepumzika kwanza jamani,” nilisema…

    “Tutapumzika,” alijibu kwa mkato huku akiendelea kupeleka mashambulizi upande wangu. Mwili uliisha nguvu lakini kama vile tena, sikuruhusiwa kutoka uwanjani kabla kipyenga cha mwisho wa mchezo hakijapulizwa.

    Ilifika mahali mimi nikawa nalia tu kwa sauti ndogo maana sikuwa naweza hata kusogeza mpira hatua tatu mbele lakini nilimshangaa mwenzangu yeye, nguvu kama ndiyo kwanza anaanza mechi.



    Shetani akamjalia akanitangazia kwamba anafika juu ya kichuguu, ikawa salama yangu. alipofika kichuguuni alijitupa huko, akajilaza akiangalia juu na kuhema kwa nguvu.

    Tulipitiwa na usingizi bila kujijua, tukauchapa usingizi. Mimi nilikuja kushtuka saa tisa usiku baada ya kuangalia saa ya kwenye simu. Nilijisikia kwenda haja ndogo, nikamtingisha afande Mwita ili aamke, anisindikize…



    “Nini wewe?” aliniuliza.

    “Nisindikize chooni bwana.”

    “Hapa kwetu hakuna wachawi, wezi wala vibaka, wewe nenda tu,” alisema afande Mwita huku akigeukia ukutani…

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Bwana mimi naogopa peke yangu.”

    “Hivi husikii wewe. Unadhani nani atakuja kujibanza hapa kwa maafande, hajipendi?”

    Nikatoka hadi chooni. Ile nageuza kurudi ndani, yule afande mbaba naye anatoka kwake, akanishika mkono…





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog