Search This Blog

Monday, October 24, 2022

USIKU WA KIGODORO - 4

 





    Chombezo : Usiku Wa Kigodoro

    Sehemu Ya Nne (4)



    ILIPOISHIA: Lina akiwa na mumewe, Semi alipata mshtuko mkubwa sana kuona simu ya James, akakumbuka kwamba alimwambia atafika Dar saa nane.

    Kwa upande wake James, alishangaa kupiga simu ya Lina mara tatu bila kupokelewa. Mara, akaliona basi la Burudani likiingia, akalifuata.

    SASA ENDELEA…CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Jamani wazima?” aliwasalimia wafanyakazi wa basi hilo.

    “Hili gari linatokea Korogwe?” aliuliza mara baada ya salamu yake kujibiwa.

    “Ndiyo mkubwa.”

    Alipopata jibu hilo, alisimama kando na kusubiri abiria washuke akiamini Lina yuko ndani. Lakini aliendelea kupiga simu yake ambayo haikupokelewa.

    Mpaka abiria wa mwisho anashuka na begi, hakuwepo Lina!

    “Mh! Hii kali! Anamaanisha nini sasa kutokupokea simu yangu? Angepokea aniambie kuna nini! Basi la Burudani ndiyo hili na hayumo!” alisema mwenyewe akiwa anaelekea kwenye gari lake.

    Alipata wazo la kwenda Mlimani City kupumzika akipata kinywaji baridi na moyoni aliamua kwamba Lina akimpigia na yeye hatapokea ili kulipa kisasi.

    Aliingia Mlimani City kwa kutumia geti la kaskazini, akaegesha gari sambamba na gari la Semi. Alishuka akaingia kwenye maduka ya ndani kwanza kwa ajili ya kuosha macho.

    ***

    Lina alisimama kwenda chooni, Kindaundau naye alikuwa anaingia Mlimani City kwa teksi huku akimpigia simu Semi kumuuliza alikokaa.

    “Nimekaa jirani na meza ya Samakisamaki, we uko wapi?” aliuliza Semi…

    “Ndiyo napita getini…hebu ngoja nipokee simu ya shemeji yako kwanza,” alisema Kindaundau.

    Simu hiyo iliyopigwa na mke wa Kindaundau ilikuwa ikimjulisha kwamba, mtoto ameumia mguu alikuwa akicheza na wenzake. Kindaundau alimwamuru dereva wa teksi kugeuza gari kuwahi nyumbani kwake, Makumbusho huku akimpigia simu Semi…

    “Ee bwana, mtoto wangu kaumia, wife amenipigia sasa hivi, ngoja niwahi nimkimbize hospitali,” alisema Kindaundau…

    “Da! Pole sana bwana. Basi utaniambia maendeleo huko.”

    “Sawa.”

    ***

    Inaweza kuwa ni ajabu lakini kweli, James alikatiza meza na kwenda kukaa meza moja na Semi maana watu walikuwa wengi siku hiyo hivyo nafasi ya kukaa ilikuwa ya kutafuta sana…

    “Habari yako ndugu?” James alimsalimia Semi huku akimuuliza kama kwenye kiti alishokishika kina mtu…

    “Njema tu kaka, karibu, hakina mtu. Ila hiki hapa kina mtu,” alisema Semi huku akikishika kiti cha Lina.

    Lina alitoka chooni huku akijiwekaweka sawa nywele zake. Macho yake yalikuwa kwa wateja mbalimbali waliokuwepo eneo hilo. Hakuwa na habari ya kuangalia alipokaa mume wake na sasa waume zake.

    Alikuwa amebakiza hatua chache kufika kwenye meza, alipotupa macho alipata mshtuko kumwona James amekaa na mume wake, akarudi chooni mbio. Baadhi ya watu waliomuona akirudi walimshangaa.

    “Mungu wangu! Kwani wanafahamiana? Loo! Nimekwisha mimi Lina, kiranga chote leo ndiyo mwisho,” alisema peke yake kule chooni huku akijishika kifuani. Mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi ya ajabu.

    Alikumbuka kitu, alichukua simu yake, akatuma meseji kwa James…

    “Nililala baby, uko wapi? Si ndiyo tunaingia stendi Ubungo sasa. Please usiondoke nina mizigo.”

    James alisoma meseji hiyo, akasimama haraka sana…

    “Ee bwana, ngoja niwahi stendi kuna mgeni ameingia hapo,” alimwambia Semi huku akitoa noti ya shilingi elfu tano na kumpa Semi…

    “Hii utanilipia hii juisi na mayai.”

    “Poapoa mkubwa,” alijibu Semi bila kujua mchezo wote unachezwa na mke wake.

    James alikimbilia kwenye gari huku akipiga simu kwa Lina…

    “Haloo, sasa umekuja na basi gani?”

    “Burudani, si nilikwambia.”

    “Mbona basi la Burudani limefika, wewe sijakuona?”

    “Burudani la pili..”

    “Poapoa, nakuja.”

    Lina alihema kwa kuhisi unafuu. Lakini alijua ana kibarua kimoja bado, James atakapomkosa Ubungo itakuwaje? Si atahisi amechukua usafiri kwenda nyumbani? Je, akifika nyumbani na kukuta hajafika?

    James alipoingia Ubungo tu, meseji ya Lina ikaingia…

    “Baby simu inazima chaji, sijui itakuwaje?”

    Lina alipotuma meseji hiyo, akazima simu na kurudi kukaa kwa mume wake, Semi…

    “Sweet, tuondoke, tumbo haliko vizuri ghafla,” alimwambia mume wake…

    “Mimi mwenyewe nilitaka kukwambia hivyo.”

    Waliondoka eneo hilo, wakiwa njiani, Semi alipokea simu…

    “Ee Masua, niambie bosi wangu…eee….wapi? Lini? Aaa, sasa….da! Oke, ngoja nifike nyumbani, nakuja tuondoke.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alipokata simu alimgeukia mkewe…

    “Baby kuna safari ya Zanzibar saa kumi, inabidi nikuache nyumbani mimi niondoke kwenda uwanja wa ndege.”

    “Jamani baby, hizo safari zako bwana,” Lina alijidai hajapenda lakini moyoni alishangilia ile mbaya.

    “Si ndiyo kutafuta hela mke wangu.”

    “Poa, kurudi lini?”

    “Nadhani baada ya siku mbili.”

    ***

    Baada ya mumewe kuondoka, Lina alichukua begi lake aliloondoka nalo kwa James, akaenda kukodi Bajaj hadi sokoni. Alinunua viazi, mkungu wa ndizi, nazi na machungwa. Vitu vyote hivyo akavitia kwenye mfuko wa salfeti na kufungwa kamba.

    Safari ikaanza ya kwenda nyumbani kwa James. Ile anafika tu, James naye akaingia na gari...

    Je, unajua nini kilitokea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Risasi Jumamosi, Jumamosi ijayo.

    Naomba ushauri wako

    “Oo! Baby, pole na safari, nilijua utakuwa umeshakuja kivyako maana si uliniambia simu ipo karibu na kuzima chaja!”

    “Ndiyo hivyo baby, pole na hapa baba angu?”

    “Nimepoa sana mpenzi.”

    Walikumbatiana, wakabusiana, wakashikana mkono kuingia ndani maana tayari mlinzi alishafika kumpokea Lina kwenye Bajaj na ule mfuko wake mkubwa.

    James alibadili zile hisia kwamba Lina ana mume mwingine zaidi ya yeye, aliamini ni maneno ya Kindaundau tu…

    “Mtu awe na mwanaume mwingine wa ndoa kabla yangu halafu afikie kwangu toka safari ya mbali kama Korogwe, haiwezekani, kutakuwa na kitu, tena amekuja na mzigo mkubwa tu,” alisema moyoni James huku picha ya Kindaundau kumdanganya ikimjia kwa mbele walivyokuwa wamekaa siku ile kwenye ule mgahawa kule mjini.

    ***

    Lina, ili ajifanye alikuwa safarini kweli na alimmisi sana mume wake huyo, aliamua usiku huo kumtendea vitu adimu na kumwonesha mapenzi motomoto.

    Walipomaliza kula tu aliomba wakaoge, walikwenda chumbani kuoga, Lina ndiye aliyemtaka James waende wakalale kwa kisingizio kuwahi kuamka kesho yake lakini ukweli ni kwamba alitaka wacheze kandanda kitandani.

    Walipopanda kitandani tu, Lina alitia hisani, maana alipokumbuka jinsi alivyomwona James pale Mlimani City amekaa na mume wake alisikia huruma sana. Aliamini walikaa jirani kwa sababu viti havikuwa vingi na hakuna aliyekuwa tayari kumjua mwenzake kwa undani.

    “Baby, nakupenda sana,” ndivyo alivyoanza kusema Lina akimuweka James kifuani pake…

    “Hata mimi nakupenda sweet, nilikumisi sana mke wangu.”

    “Kweli, kuliko nilivyokumisi mimi?”

    “Hunishindi bwana.”

    Mara kulipita ukimya kwani walijikuta wamezama kwenye penzi la upande wa pili, walikuwa ndani ya denda. Miguno tu ndiyo iliashiria kwamba wapo pembeni ya uwanja wakisubiri kuingia kati ili kuanza kusakata soka.

    Lina kwa mara ya kwanza alimshika James na kumshusha chini, akamuwekea kiti akae. Halafu akashusha godoro, akalitandika vizuri sana, wakalala hapo…

    “Baby leo utanipata kwa staili ya usiku wa kigodoro,” alisema Lina.

    Alimvuta James na kumkaribisha kwake huku akimsisitizia kwamba anahitaji mtoto kutoka kwake.

    Akili za Lina hapo zilikuwa siyo zenyewe, kwani zilibadilika ghafla na kujikuta eti yuko tayari aachane na Semi kuliko kuachana na James.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alitumia staili mbalimbali ambazo James hakuwahi kujua kama anazitambua na kila pozi alisisitiza kupewa mimba ndiyo ilikuwa kilio chake kikubwa katika mahaba ya usiku huo.

    Kwa sababu walitandika godoro chini, kwa hiyo hata pale mmoja wao alipocheza rafu, hakuna mlio uliotoka. Ilikuwa kimyakimya, sanasana kuhema sana kwa Lina na maneno yenye kubembeleza ndiyo yalisikika kwa mbali lakini.

    Lina alimaliza pozi zake zote, sasa akataka kupewa mapozi na James. Naye alikuwa mtaalam, alimuonyesha mapozi ya nguvu, mara wakae wote, mara mmoja asimame mwingine achunge mbuzi, mara mwingine kulia mwingine kushoto lakini bila kuachana.

    Lina alianza kupiga kelele na kutangaza ushindi wake alipokalishwa kwenye baskeli kiti cha nyuma halafu dereva akamwangalia lakini wakiwa wanaenda mbele.

    Kilio chake kilitoa picha kwamba kweli walikuwa kwenye usiku wa kigodoro…

    “Na…na…na mimba nakuhakikishia utapata sweet,” alisema kwa kigugumizi James.

    “Mtoto tutamuita Jali dear, yaani mimi na wewe.”

    Lina alipomaliza kusema hivyo tu akanyoosha miguu na kusalimu amri akifuatiwa kwa karibu sana na James naye, wakawa wanahema wote!

    ***

    Siku iliyofuata, Lina aliondoka kwenda kazini akimwongopea James anapitia saluni kuosha nywele kwanza maana alipokwenda Korogwe zilichafuka hivyo hakutaka lifti lakini walikubaliana kwamba, jioni waende wakapate dina Mlimani City.

    ***

    Ilikuwa saa kumi na mbili na nusu jioni, Semi alirejea kutoka Zanzibar, akafika nyumbani kwake hakumkuta Lina…

    “Uko wapi wewe?” Semi alimtumia meseji mkewe.

    “Nipo saluni baby wangu. Vipi hali yako sweet?”

    “Sawa, hali yangu mi mzima sana,” alijibu Semi bila kusema amerudi.

    Alioga, akavaa akatoka. Safari yake ilikuwa kwenda Mlimani City kwenye ahadi moja ambapo ilimlazimu arejee Dar halafu kesho yake aende tena Zanzibar.

    Alikanyaga mafuta hadi Mlimani City. Kwa folenifoleni alijikuta amefika Mlimani City saa moja na dakika kumi giza likiwa limeingia tayari.

    Aliegesha gari na kwenda kukaa. Ile anaweka kikao kwenye kiti tu, anasikia sauti ikimsalimia…

    “Bro za tangu jana, kama nakukumbuka,” alisema James ambaye kiti alichokaa aliweza kuonana na Semi moja kwa moja wakati kiti alichokaa Lina alimpa mgongo kwa hiyo Semi alimwona kwa nyuma.

    Kabla hajaitika salamu ya James, Semi alikaza macho kwa Lina, akashangaa, akasimama na kumfuata…

    “Lina,” aliita huku akimwangalia usoni na kumshika begani…



    Lina alishtuka sana, aligeuka kumwangalia Semi, akaanguka chini na kupoteza fahamu…

    “Kwani ni nini mkuu?” aliuliza James…

    “Huyu ni mke wangu, kaniambia yupo saluni nashangaa namemkuta hapa. Kwani ndugu yangu huyu ni nani kwako?” aliuliza Semi huku akimkazia macho James…

    “Huyu mimi ni mke wangu,” alisema James kwa kujiamini.

    “Mke wako?”

    “Ndiyo kaka. Kwani vipi?”

    “Lina mke wangu mimi unasema mkeo?” alishtuka Semi.

    “Ama, Lina ni mke wangu, nimefunga naye ndoa kanisani kabisa.”

    “Kaka acha utani. Kwanza wewe jana si ulikuja ukakaa hapa?”

    “Ndiyo.”

    “Mbona nilikuwa naye mimi kama ni mkeo. Acha mambo ya utani bwana. We unaniibia mke wangu, nimekufumania.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sijakuibia na jana hakuwepo.”

    “Alikuwepo, ulipokuja wewe alikwenda chooni,” alisema Semi.

    Kwa mbali James alipata picha kwamba, huenda Lina hakusafiri kama ni hivyo. Pia alianza kuyaamini maneno ya Kindaundau kwamba Lina ana mume wake.

    Wateja walianza kujaa kwenye meza a kujua nini kimetokea. Wengine waliuliza, wengine walitumbua macho tu. Mzee mmoja mwenye busara zake aliingilia kati baada ya kusikia mazungumzo ya James na Semi. Aliwataka watulize munkali kwanza, wahakikishe Lina anazinduka halafu mambo mengine yaendelee…

    “Hivi we mzee unajua inavyouma ukimfumania mke wako? Nina miaka naye minne sasa” alisema kwa hasira Semi.“Umemfumania nani wewe? Mimi Lina nimeshasema ni mke wangu.”

    “Una cheti cha ndoa wewe?” yule mzee alimuuliza James baada ya kumsikia Semi akisema ana miaka naye minne.

    “Ninacho ndiyo,” alijibu kwa kujiamini sana James.

    “Basi kama nilivyowaambia, mwacheni kwanza azinduke mambo mengine yatafuata,” mzee alisema tena.

    Semi aliinama kumtingisha Lina na James naye akafanya hivyohivyo…

    “Lina…Lina,” aliita Semi…

    “Baby…mke wangu,” aliita James naye akimtingisha. Semi alitaka kumrushia ngumi James lakini akajizuia.

    Kwa mbali Lina alionekana kushtuka, akafumbua macho na watu wakaombwa kutawanyika ili aweze kupata hewa safi.Walipoona Lina amezinduka walimsimamisha wote na kumkalisha kwenye kiti…

    “Pole sana, unajisikiaje sasa?” aliuliza James huku akimshika.

    Lina hakujibu akaanza kuporomosha machozi sasa huku akiangalia chini. Alichojua ni kwamba amepoteza ndoa zote mbili.

    Semi alimsimamisha ili waende hospitali, James akasema anampeleka yeye. Ukatokea mzozo mwingine tena na walitaka kuzichapa. Yule mzee akaingilia tena kati, akamuuliza Lina aliyeonesha kukosa nguvu bado…

    “Eti, kati ya hawa wawili nani ni mume wako?”

    Lina alijiinamia, machozi yakamtoka tena…

    “Unajua binti, wewe ndiye mwenye uwezo wa kumaliza hili tatizo hapa, sasa kama utashindwa kuwa muwazi sijui itakuwaje leo.”

    Lina aliendelea kulia, wasiwasi ulimtawala. Kwa muda huo alitamani ardhi ipasuke ili aingie ndani yake na kufia huko.

    “Lina, nini umenifanyia?” aliuliza Semi. Swali hilo likazidi kuchochea kilio cha Lina, sasa alilia kama mtoto ikabidi uongozi wa eneo hilo kumuita mlinzi na kuwataka akina Semi kuondoka na Lina wao…

    “Mkamalizane majumbani mwenu bwana, hapa ni eneo la biashara, mke wangu mimi mke wangu mimi, basi huyo mwanamke atakuwa kiboko, ndoa mbili,” alisema mfanyakazi mmoja wa eneo hilo.

    Mwngine akadakia…

    “Hata huyo mume wa kwanza naye kiboko. Mkeo mpaka anafunga ndoa wewe uko wapi? Kwani kama mlipofunga ndoa mlikwenda fungate?” aliuliza mfanyakazi huyo aliyedakia…

    “Yeah! Tulikuwa honeymoon ya siku kama tatu hivi, tukaenda kuishi nyumbani kwangu Mbezi,” alipasua James…

    “Hamna, mimi mke wangu hajawahi kukosekana nyumbani siku tatu,” alidakia Semi. Kauli zao ziliwakoroga sana watu waliokuwa wakisikiliza.Lina alisimama na kuanza kutembea kuondoka eneo hilo huku akizomewa. Semi na James walimfuata kwa nyuma lakini hawakumkuta kwa vile alishatoka kwenye geti na kuchukua Bajaj.

    Kazi ilikuwa moja kwa Lina, anakwenda wapi? Na huko anakokwenda ataishi mpaka lini? Je, atasema nini kwa wazazi wake? Semi atamuelewaje? Lakini hata James atamuelewaje?

    “Wapi dada?” aliuliza dereva wa Bajaj…

    “We twende tu.”

    ***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    James aliingia kwenye gari lake, Semi naye alifanya hivyohivyo. Lakini kabla James hajaondoa gari, alishuka akamkimbilia Semi na kugonga kioo cha gari…

    Semi akafungua kioo nusu…

    “Unasemaje?”

    “Nipe namba yako bro. unajua kuna uwezekano ishu si sisi ila ni huyu mwanamke. Muhimu sisi kama wanaume tukutane,” alisema James.

    Semi akiwa hana amani, alizitaja namba zake za simu kisha naye James akamtajia za kwake. Wakaagana na kuondoka.

    Semi alisema moyoni kwamba hatampigia simu Lina mpaka atakaposema mwenyewe lolote na pia kama ni kweli alifunga ndoa na James, yeye basi!

    Lina alikwenda kupiga kambi nyumbani kwa shoga yake, Eg ambapo alipofika tu na jinsi alivyokuwa akihema, Eg alijua kuna ishu nzito sana imetokea. Walipokutana macho, Lina akaanza kuporomosha machozi palepale…

    “Lina, nini kimetokea?” aliulia kwa mshtuko Eg…

    “Nimenaswa leo Eg, sijui itakuaje?” alisema Lina huku akilia.

    “Umenaswaje? Hebu nisimulie.”

    “Nilikwena Mlimani City na James, Semi alisafiri kwenda Zanzibar jana na alisema angerudi leo. Sasa nashangaa kumbe kaamua kurudi leo, akaja Mlimani City akanikuta nimekaa na James.”

    “Mmmh!” alishtuka sana Eg. Aliliona tatizo kweli ni zito.

    “Ikawaje sasa?” aliuliza Eg.

    “Yaani Eg, amenikamata hivi nimekaa na James,” kabla hajamaliza kusema, Lina alilia tena. Ilibidi Eg atumie nguvu kubwa sana kumtuliza.

    “Naomba utulie kisha uendelee kunisimulia,” alisema Eg akimkumbatia Lina.

    Lina alitulia kwa muda kisha akasema…

    “Yaani Eg iko hivi. Nilikaa na James Mlimani City, tena kwa kujiachia nikijua Semi si yupo Zanzibar anarudi kesho, kumbe karudi leo. Akaja Mlimani City, alinipigia simu nikamwambia nipo saluni, alipokuja pale kanikuta. Akanishika geba na kusema Lina.

    “Yaani huwezi amini shoga nilianguka nikazimia palepale. Nilipokuja kupata fahamu nikakimbia. Aibu iliyoje?”

    “Da! Pole sana shoga…sasa?”

    “Sijui lolote. We unadhani naweza kwenda kwa nani kati yao?” aliuliza Lina.

    “Mh! Uchaguzi ni wako.”

    “Hamna Eg. Nikienda kwa Semi atanishangaa sana, kwa James pia. Hapa sijui wao wameachanaje! Kama walizungumza kila mmoja akajieleza kwa mwenzake mwisho wa siku si mimi nitaonekana wa ajabu sana?”

    “Sana. Mi nadhani tumtafute mtu mzima mmoja ili asaidie busara zake,” alisema Eg…

    “Eg, nilishaongea na watu wazima wote walishtuka na kuonesha dalili kwamba, mzigo ni wangu mwenyewe.”

    “Mh!”

    ***

    James baada ya kufika nyumbani kwake aliingia chumbani, akampigia simu Semi. Semi naye alikuwa chumbani kwake amelala ubavuubavu akishangaa kilichotokea…

    “Haloo,” Semi alipokea simu…

    “James hapa bwana.”

    “Ndiyo kaka, tunaweza kukutana muda huu?” aliuliza James…

    “Mi nadhani itakuwa muhimu. Wapi sasa?”

    “Tukutane popote pale.”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Wewe njoo nyumbani kwangu, nitakuelekeza ukifika.”

    James alitoka, aliendesha gari akiwa amempigia simu Semi akampa maelekezo mpaka nyumbani kwake. Aliposhuka, alichukua bastola na kuisunda sehemu fulani ya nyuma, akampigia simu Semi kwamba ameshafika.

    Alitoka, akampokea na kumkaribisha ndani. Ile anakaa tu James, macho ya kwanza yakatua kwenye ukuta na kukutana na picha kubwa ya siku ya ndoa ya Lina na Semi…

    “Kumbe kweli,” alisema moyoni.

    Baada ya salamu ya muda huo, James alianza kwa kuelezea alivyokutana na Lina na alivyomuuliza kama ameolewa, akamjibu hana mume na alivyojitosa yeye kufunga naye ndoa…

    “Ina maana umefunga ndoa kweli na Lina?”

    “Kabisa.”

    “Kanisani?”

    “Ndani ya kanisa kabisa na honeymoon tulikwenda.”

    Semi alianza kuunganisha matukio, akaanza kukubali moyoni mwake kwamba, Lina alifunga ndoa na kijana huyo.

    “Inawezekana kweli, maana naanza kukumbuka kwamba kuna wakati amekuwa na safari nyingi za hospitali na wakati mwingine kulala hukohuko,” alisema Semi kwa sauti iliyojaa majonzi…

    “Hata kwangu, kuna wakati alikuwa na safari nyingi na kusema anakwenda kulala kwa mgonjwa wa rafiki yake mmoja anaitwa…”

    Kabla James hajamaliza kumtaja jina, Semi akamtaja…

    “Eg?”

    “Ee Eg. Huyohuyo.”

    Semi alizidi kuvuta picha na kukumbuka siku moja Lina alipomwambia anakwenda kwenye sherehe ya Eg. Akakumbuka siku hiyo alikuwa na safari ya gafla ikabidi amfuate Lina kwa Eg ambapo alimkuta amependeza sana.

    Kifupi aliunganisha matukio na kukumbuka mambo mengi sana yaliyoonesha uhalisia.

    “Hivi mimi leo ninavyojua ametoka safarini kwao, Korogwe, Tanga ambapo alisena anakwenda mama yake ni mgonjwa,” alisema James.

    “Wewe jana si ulikuja pale Mlimani City?” aliuliza Semi.

    “Nilikwenda kumpokea Ubungo maana alisema anarudi. Kufika napiga simu haipokelewi, ndiyo nikaamua kuja hapa.

    “Kufika hapa, nakaa kidogo tu, akanitumia meseji kwamba ameingia Ubungo alikuwa amelala, lakini simu yake inaisha chaji, ndiyo maana nilitoka mbio.

    “Kufika kule sikumpata tena hewani, nikaenda nyumbani naingia na yeye anaingia na bodaboda na ana mizigo.”

    “Ana mizigo kabisa?” aliuliza kwa kuhamaki Semi…

    “Kabisa.”

    “Da! Huenda alinunua vitu sokoni ili ujue alisafiri kweli. Mimi nilikaa naye Mlimani City, wakati umekuja alikuwa chooni. Nahisi alikuona ndiyo maana akakutumia meseji ya kukwambia umefika ili uondoke. Maana ulipoondoka tu, akaja tukaondoka,” alisema kwa kirefu Semi.



    Semi alionesha dalili za kujisikia vibaya kwa kitendo alichokifanya mkewe, Lina…

    “Mimi bwana mzee sidhani kama nina la kuongeza tena, kwani kama nilivyokwisha kwambia, nilifunga naye ndoa na picha unaziona hizo hapo ukutani, hakuna cha kuficha,” alisema Semi huku akihisi kuporomosha machozi.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    James pia alijisikia vibaya sana, naye alijilaumu ni kwa nini hakufanya utafiti wa kina kabla ya kufunga ndoa na Lina. Aliamini kama angechukua jukumu la kwena hadi kwa wazazi wake, yasingetokea hayo.

    “Mimi mwenyewe mkubwa kama ningejua ana mume, sidhani kama ningekubali kugharamia harusi kubwa kama ile,” alisema James.

    “Najua…najua.”

    James aliaga na kuondoka kwa ahadi kwamba, hawezi kumpigia simu Lina. Semi naye akamwambia vivyo hivyo…

    “Mimi nadhani tufanye hivi. Usipokee simu yake akikupigia kwani hata mimi sitapokea akinipigia,” alisema Semi.

    ***

    Lina alilala kwa Eg usiku huo, lakini alishindwa kupata usingizi. Muda mwingi alikuwa akimwambia Eg kwamba anataka kujiua kwa sumu…

    “Hapana, usifanye hivyo. Maisha yako hivyo siku zote. Kuna kupanda na kushuka, kuna raha na tabu. Kwa sasa upo katika kipindi cha tabu, lakini naamini kuna kipindi cha raha uliwahi kukipitia na kitakuja tena,” alisema Eg kwa sauti iliyojaa busara kuliko siku zote.

    “Lakini Eg, wewe kama shoga yangu ulitakiwa uwe mkweli, ungenikatalia tangu mwanzo kwamba dili ninalolifanya lina matatizo mbele ya safari nisingelifanya,” Lina alitupa lawama…

    “Lina! Wewe ndiyo ulikuwa unajua mazingira ya watu wako. Semi unamjua wewe, James unamjua wewe, nilijua unaelewa jinsi gani ungeishi nao maisha wasijuane. Lakini niliwahi kukwambia kwamba huoni ni hatari, ukasema nikuachie wewe.”

    “Basi yaishe bwana, nitamwomba Mungu mwenyewe hadi yataisha tu,” alisema Lina akimwaga machozi.

    Usiku huo ulikuwa wa mang’amng’amu kwake, alishangaa kuona mpaka inagota saa saba, si Semi si James aliyempigia simu…

    “Eg…Eg,” aliita Lina. Eg wakati huo alikuwa akikoroma usingizini…

    “Mmmh! Vipi Lina?”

    “Unajua mpaka muda huu sijapigiwa simu na yeyote yule?”

    “Lina, hii ishu ni nzito sana. Ili upigiwe simu ni lazima mtu awe amekaa na kufikiria kwanza. Kama James angekuwa jamaa tu ndiyo umefumaniwa naye, angekupigia yeye lakini naye anajihesabia kama mume. Ni kazi sana,” alisema Eg huku akichombezea na kufikicha macho kwa usingizi.

    ***

    Mpaka kunakucha, Lina alipata usingizi kwenye saa kumi na moja alfajiri lakini alipoamka na kuangalia simu hakukuwa na hata meseji ya Semi au James…

    “Da! Yamenikuta Lina mimi! Hiki chote ni kiherehere changu,” alisema moyoni, akamuita Eg…

    “Vipi Lina, umeamkaje?”

    “Ah! Nimelala basi. Mimi Eg nafikiria jambo moja…”

    “Lipi hilo? Lilelile la kujiua?”

    “Hapana, naacha kazi pale.”

    “Mh! Unadhani ni busara?”

    “Kuendelea ndiyo siyo busara.”

    “Kwa nini?”

    “James anakuja sana pale, we unajua. Unadhani nitafanyaje kazi?”

    “Ni kweli, lakini nadhani ni bora kupeleka akili kwenye ndoa kwanza kabla ya huko kazini. Unadhani mwisho ni nini kama hakuna aliyepiga simu?”

    “Nataka kwenda nyumbani.”

    “Wapi?”

    “Kwa Semi.”

    “Ukifika?”

    “Nitaangalia mazingira kwanza. Kama yamekaa sawa nitamwomba msamaha kama siyo nitaondoka kurudi.”

    “Lakini Lina jana usiku ulikosea sana, ulitakiwa urudi kwa Semi. Ukienda asubuhi hii anaweza akajua ulipowakimbia ulikwenda kulala kwa James…

    “Ilikuwa mistake, sina jinsi, ngoja niende tu.”

    Lina alijiandaa, akachukua Bajaj hadi nyumbani. Alimkuta Semi ameshaamka, yuko sebuleni anakunywa maji ya moto kwenye glasi…

    Alikaa kwenye sofa, akamsalimia…

    “Umeamkaje?”

    Semi alimwangalia kwa macho makali sana bila kuitikia salamu yake. Alitamani kumrukia.

    Baada ya kuona hajaitikiwa na sura ya Semi haijakaa vizuri, Lina alisimama, akatoka bila kuingia chumbani wala kwenda popote.

    Alipanda tena Bajaj hadi kwa Eg…

    “Vipi? Umemkutaje shemeji?”

    “Mh! Mwenzangu, we acha tu. Nimeamua kuondoka mwenyewe maana nilipomsalimia tu, akaniangalia kwa macho hayo, sijawahi kumwona hata siku moja.”

    “Aliitika?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapana, aliniangalia tu.”

    “Mh! Sasa itakuaje Lina? Hebu mpigie simu James,” alishauri Eg.

    Lina alikuwa kama amechanganyikiwa sasa, kila hoja aliikubali, akampigia simu James ambapo iliita mpaka ikakatika. Akapiga tena, pia iliita mpaka ikakatika. Mwishowe, simu ilipoita ikakatwa upande wa pili!

    “Mh! Mwenzangu, naona anakata,” alisema Lina akianza kulia.

    Mara meseji ikaingia…

    “Kuna nini umesahau kwangu we binti?”

    Ilitoka kwa James…



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog