Search This Blog

Monday, October 24, 2022

UTAMU WA ZEGE - 2

 





    Chombezo : Utamu Wa Zege

    Sehemu Ya Pili (2)




    JANETH alipatwa na aibu. Alimwangalia Amosi kwa macho ya kuibia. Ile hali ya kujibu kwa ukali haikuja na wala hakuifikiria. Upole ulemvaa na kusahau kuhusu maji.
    “Saa nne na robo usiku, simu ya Amos ilianza kuita. Hakuwa na haraka nayo kwani alijua ni Janeth anabipu. Alimalizia kumimina chai yake tayari kwa kuinywa. Alipiga funda mbili na kuichukua simu yake. Alikuta ni Janeth aliyebipu. Alitabasamu kidigo na kujiweka sawa.
    “Halow, “ Amos alianza kumwita Janeth.
    “Ehh, mambo,” Janeth aliitikia na kumsalimia Amos.
    “Poa, nimefurahi ulivyonibipu.”
    “Ndio, ulikuwa unasemaje kwani.” Sauti ya Janeth ilikuwa ya woga. Ilitetema kama mtu aliyehojiwa kwa mara ya kwanza na polisi kwa kosa la kusingiziwa.
    “Janeth, ni kama bahati leo nimekutana na wewe. Haikuwa mara ya kwanza kukuona.Ila kwa uzuri wako na jinsi ulivyo umenivutia sana. kwa kifupi tu. Napenda tuwe wote.”
    “Haloow,” Amos aliita.Janeth alikuwa amenyamaza kimya akimsikiliza Amos. Aliona kama bahati ikija mbele.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    ******
    Akiwa ni mtoto wa kwanza na wa mwisho katika familia ya mzee Joshua. Janeth alilelewa katika maisha ya tabu. Wazazi wake walifariki na kumwacha akiwa hana hili wala lile. Alihangaika na maisha peke yake maada ya wazazi wake kumwacha akiwa na miaka kumi na tatu. Hakubahatika kusoma hata darasa moja.
    Baada ya wazazi wake kufariki aliishia kuzurura mitaani. Aliokota chupa za maji na kuziuza. Alikumbana na mambo mengi ya hatari ikiwemo kubakwa. Hata hivyo mbakaji hakufika mbali kwani alifanikiwa kumchoma na kitu chenye ncha kali kilichosababisha kifo chake. 
    Janeth alilia sana baada ya kufanyiwa unyama huo. Alijikongoja hadi katika nyumba ya bibi mmoja na kujilaz nje karibu n mlango wake hadi asubuhi alivyokutwa na bibi huyo.
    Yule bibi alimchukua na kumwingiza ndani. Hakuwa na redio na hivyo hakusikia lolote juu ya taarifa kuhusu yule mtu aliyembaka. Hakujali. Alikubali kuishi na yule bibi ilia pate pa kulala na kumsaidia.
    Yule bibi alifurahi kwani ni miaka mingi alikuwa akiishi peke yake. Alimhudumia uji baada ya kumfanyia usafi mwili wake ambao ulikuwa umechoka sana. 
    “Asante sana bibi,” Janeth alimshukuru yule bibi.”
    “Karibu mjukuu wangu.”
    Janeth alipata pa kuishi. Alianza maisha mapya na bibi. Bibi alikuwa na shilingi elfu tano. Alimkabidhi Janeth. Alifanya hivyo kwa kuwa hakuweza kufanya lolote katika biashara. Aliishi kwa kuokoteza na kuomba chakula.Janeth alifikiria cha kufanya. Alikuwa na shilingi elfu tano alizopewa na yule bibi. 
    Alianza kazi ya kuuza maji mjini. Aliondoka nyumbani kwa yule bibi Kikuyu asubuhi sana na kuzunguka mjini hadi jioni. Alinunua chakula na kurudi nyumbani baada ya kumaliza kuuza maji.
    Aliendelea na biashara hiyo kwa muda mrefu mpaka alipokutana na Amosi. Alikuwa tayari ameshafikisha miaka kumi na tisa. 
    Alikuwa na umbo lililovutia. Mweupe kiasi na mfupi kiasi. Hali duni ilifanya wanaume wengi wamwone havutii. Nguo zake zilikuwa ni chakavu na kana zilizoraruka hadi pale alipoweka hela na kununua kanga moja na kugawana na yule bibi. 




    *****
    Amos alikutana na Janeth siku iliyofuata. Alidhamiria kuwa na Janeth. Uzoefu wake wa kuangalia wanawake katika nchi alzosafiri ilikuwa ni moja ya sababu za kuona Janeth angemfaa. Alikumbuka jana yake alivyokitazama kifua cha Janeth wakati akishusha ndoo yenye maji. Alihisi msisimuko usiomithilika.Akili yake yote ilihama.
    Sasa alimtafta Janeth. Alimpigia simu na kukutana naye. Waliongea mengi pasipo kufichana jambo lolote. Janeth alikubali kuolewa na Amos.
    Taarifa hizo zilifika kwa yule bibi. Janeth alienda na Amosi hadi kwa yule bibi na kuongea naye. Janeth alishamfanya kama mzazi wake na hivyo asingeweza kufanya jambo lolote kubwa pasipo kumweleza yule bibi. Yule bibi hakukataa pendekezo lao. Baada ya ujua Amosi ni mtu mzuri. Alikubali kuishi mwenyewe na kumwacha Janeth aede kwa Amosi.
    Japokuwa Amos alikuwa na wazazi na ndugu zake. Alichelewa kuwaambia kuhusu mipango yake juu ya kukmuoa Janeth. Aliamua kwanza kuishi na Janeth ili kujua vizuri alivyo.
    Ni mara ya kwanza ambapo Amos alikuwa na Janeth kitandani kwake. Amos alijua Janeth hakufahamu chocote kutokana na ugeni wake katika mapenzi. Alimwona ni mwanamke mwenye aibu sana. Alitaka kujaribu ili amjue.
    “Usizime taa, hatutafaidi hivyo,” Janeth alimsihi Amos asizime taa. Hakuwahi kumsikia Janeth akiongelea mapenzi wala kuhusu ngono. Janeth hakuwa na mpenzi wala hakuwahi kufanya mapenzi. Aliyembaka alimuumiza kiasi cha kumfanya asitamani kufanya mapenzi tena. Huo ukawa msimamo wake. Aliyasikia tu na wakati mwingine alijionea katika video nyumbani kwa rafiki yake Agness ambaye yeye alikuwa akifanya hivyo ili kumshawishi Janeth ajiingize katika mapenzi baada ya kumwona kama asiyejua lolote. Hilo halikumshawishi Janeth zaidi ya kupuuzia.
    Amos alizidi kumshangaa Janeth. Janeth alimvaa Amos katika kochi lake na kukaa juu yake. Alikuwa amevalia kanga moja tu baada ya kutoka kuoga. Alimkumbatia kwa nguvu Amos na kupitisha ulimi wake sikioni. Amos alijiondoa haraka. Hakuamini kinachotokea.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Amos!” Janeth alimshangaa Amos.“Unaenda wapi, tafadhali rudi hapa. Nimeishia tu kuona wenzangu, naomba leo na mimi niwajibike,” Janeth alilalamika huku akimfuata Amos. Amos alirudi, hakuamini macho yake. Aliiondoa kanga aliyokuwa amejifunga ili Amos aone umbo lake. Amos alichanganyikiwa.
    Amos alimshika Janeth na kumbeba. Alimwaga kitandani huku wakiendelea na mfululizo wa mabusu yaliyomchanganya Amos. Amos alifanya kazi yake sawa sawa. Kilio cha Janeth kilimfanya Amos azidishe kasi huku Janeth akizidisha utundu.
    “Huyu atakuwa ananidanganya, kashafanya sana huu mchezo.” Aliwaza Amos huku akiendelea na zoezi lake.
    Asubuhi Amos hakuona sababu ya kuongelea juu ya lililotokea jana usiku. Furaha aliyokuwa nayo hakutaka kuchelewesha mpango wake. Amosi alifanya mipango ya ndoa na kumpeleka Janeth kwa wazazi wake. Haikuwa na pingamizi kwao. Walifunga ndoa na kuanza maisha ya ndoa. Amos alimfungulia Janeth kibanda cha kuuzia chakula na matunda. Alijua kitamsaidia kwa matumizi ya nyumbani wakati yeye akiwa safarini.




    *****
    Baada ya mienzi miwili ya ndoa yao. Janeth alipata mimba. Hali hiyo ilimfanya Amos afute baadhi ya safari zake ili kumsaidia mke wake hadi atakapojifungua. Alishinda naye nyumbani wakati mwingine ili kumfariji na hali aliyokuwa nayo. Amos alimpenda sana Janeth.
    Miezi mbele walibahatika kumpata mtoto Jane. Ilikuwa ni kama ndoto kwa Janeth. Amos alisimamisha safari kwa mwezi mmoja akikaa nyumbani na kucheza na kichanga chake. 
    Ndugu wa Amos na rafiki wa Janeth walifika kwa Amos na kumsalimia Janeth pamoja na kumbeba mtoto. Ilikuwa ni faraja kwa baba na mama yake Amos kupata mjukuu. Kwa uzur aliokuwa nao Jane, kila mtu alipenda kumbeba na hata kupiga naye picha.
    Janeth alikuwa akibaki tu kitandani akiendelea kuuguza maumivu ya kichwa chake. Alisaidiwa na baadhi ya ndugu wa Amos. Maumivu yalikuwa makali hali iliyopelekea kukimbizwa hospitali kupatiwa matibabu. Huko aligundulika kwamba alikuwa ana malaria kali sana. Kwa hali aliyokuwa nayo Janeth, Amos alikata tamaa juu ya mke wake kupona. Haikuwa rahisi kuzuia kwani jitihada alizozifanya daktari pamoja na Amos hazikuzuia uwezo wa Mungu kumchukua kiumbe chake. Hatimaye Janeth alifariki dunia akimwacha Jane akiwa na miezi miwili. Hilo lilikuwa pigo kali sana kwa Amos. Hakuamini kilichotokea. Alikuwa kama amechanganyikiwa na kukosa raha. Alimlilia sana mke wake Janeth.




    ****
    Amos alikuwa amesimama mlangoni kwake. Alikuwa amemkumbatia Jane huku amembeba. Jane alikuwa akilia sana kuliko ilivyokuwa akiwa na mama yake aliyekuwa akimbeba huku Jane akiwa anasikilizia joto la mikono ya mama yake akiwa katulia. Amos alibembeleza sana Jane. Alizunguka naye kila kona. Chupa ya maziwa haikuwa mbali. Alimpa kila wakati. Hakujua ameshiba au la. Yeye alimpa kila tu aliposikia Jane akilia.Wazo la kuoa mke mwingine lilimjia. Haraka Amos alifunga safari hadi kwa wazazi wake. 
    Alitaka kumwoa Debora Mwilego. Mwanamke aliyekutana naye baa na baada ya kuongea naye kwa kirefu na kuelewana hatimaye Debora aliamua kuolewa na Amos.
    Debora, mwanamke aliyeonekana nadhifu wakati wote. Uso wa mviringo wenye mashavu manene. Umbo la mwanamke wa Kichaga mfupi kiasi na mweusi kiasi aliyejilazimisha kuwa mweupe huku akijipa matumaini ili kumvutia zaidi Amos.
    Vipodozi vyote viliijaribu ngozi yake iliyokuwa ikipambana na ngozi ya walimbwende waliokutana nayo barabarani. Muda mwingi aliishia kwenye kioo akitafakari mwonekano mpya wa ngozi yake. Weusi aliokuwa nao ulikuwa ukibadilishwa taratibu kwa mchanganyiko wa vipodozi. 
    Kitandani ndio hasa alipopajali hasa alipokuwa na Amos. Alijua kikubwa kilichomshawishi Amos hadi kumtamkia maneno ambayo aliona ni ndoto kwake ni kwa sababu alimpagawisha mara ya kwanz walipokutana katika nyumba ya wageni ya Royal Inn. 
    Hakukata pumzi hadi alipohakikisha anamshinda Amos ambaye nay eye alionyesha kwamba ni mwanaume aliyekamilika. Takriban saa zima Amos na Debora walilitumia kugaragara na kubinuka kitandani. Hakuna aliyekuwa mchoyo katika kuonyesha ufundi wake. Mihemko ilitawala chumba chao. 
    Baada ya kilichowapeleka, Amos alimtamkia tena na tena Debora kama amekubali kumlea Jane.
    “Siwezi nikakataa kwa hilo. Naona pia ni bahati kwangu kupendwa na wewe. Nakuahidi nitamlea vizuri kama alivyotarajia kumlea marehemu mama yake. Nitampa mapenzi ya mama kwa mtoto.”
    Amos alifurahi kusikia aliyoyasema na hapo hapo alimrukia tena Debora na kurudia tendo lile lile lililowaleta pale. Ilikuwa ndo kama wameingia. Amos hakuonyesha kuchoka wala Debora. Alimmpokea vizuri Amos na kumpa kile alichokitaka. Alimzungusha hivi na kumgeuza vile. Sasa kila mmoja aliridhika na kumshukuru mwenzake.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    *****
    Ndoa ilifungwa na Jane alipata mama wa kumlea. Alimlea kwa mapenzi yote. Kila Jane alilotaka Debora alimpa. Alitaka kumridhisha Amos. Hadi pale Jane alipoanza kucheza mwenyewe na akaambiwa kitu akaelewa Debora alimshawishi Amos wamtaftie Jane mwenzake wa kucheza naye. Haikuwa pingamizi kwa Amos. 
    Baada ya miezi tisa ya ujauzito. Debora alijifungua mapacha wa kike, Marry na Neema. Jane aliwapenda wadogo zake. Hadi walipoanza kujitambua Jane alikuwa amekua. Walimpenda sana Jane. Walimheshimu sana Jane kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa mkubwa kwao kiumri. Walimsikiliza sana japo kuwa Jane hakupata malezi mazuri kutoka kwa Debora. Neema na Marry waliona utofauti kati yao na Jane lakini hawakuwa na la kufanya.
    Jane alipigwa sana na mama kwa kosa dogo huku Neema na Marry walipendwa sana. Mashtaka ya Jane kwa baba ilikuwa ni kawaida. Jane alivumilia sana. Kipigo kutoka kwa mama wa kambo kilimfanya abadilike na kuwa mjeuri kupita kiasi. Alijua anaonewa sana, akili yake ilimfanya ajiulize kama kweli huyu ni mama yake au la. Aliwaza sana. Akakosa raha na hata kupungua mwili wake uliokuwa na nyama mwanzo.
    Alionekana mnyonge muda wote hali iliyomfanya aanze hata kumchukia mama ambaye hakujua kama si mzazi wake. Kwa nini aliwapenda sana Marry na Neema, kwa nini hapewi malezi kama ya Marry na Neema? Jane aliwaza sana. 
    Alisoma hadi kidato cha nne. Hakuweza kuendelea kwa sababu ya mama yake wa kambo kumsema vibaya. Mazungumzo kati ya baba yake na mama yake wa kambo aliyasikia. Katika mabishano hayo baba ake alikubali Jane asisome. Alifanya hivyo ili mke wake asiondoke. Alichosema Debora baba yake Jane hakudiriki kukataa.
    “Mke wako baada ya kufariki ulinifuata mimi. Nilikuwa na ndoa yangu nikaitoroka kwa ajili yako kwa taarifa yako. Najua hadi leo yule mwanamume ananitafuta lakini siwezi kurudi kwake. Mi nasema sasa ni zanu ya Neema na Marry kusoma. Jane asubiri kwanza. Mtu mwenyewe unasema huna hela,” Debora alifoka chumbani huku Jane akisikiliza mabishano yao kupitia katika upenyo wa mlango. 
    Baba yake alisafiri tena.Hakumwambia lolote kuhusu shule. Hapo sasa Jane alipata jibu kwa nini mama yake hakumpenda. Baba yake Jane alikuwa ni dereva wa lori ambalo lilikuwa linapeleka mizigo nje ya nchi. Leo lingekuwa Zambia, kesho Kenya, Malawi, Msumbiji na Congo. 
    Ni wakati baba yake akiwa safarini ndiyo Jane alionja joto ya jiwe kutoka kwa mama yake huyo. Pindi baba akirudi hakudiriki hata siku moja kunyanyua mdomo wake na kusema lolote bali mama ndiye aliyekuwa akimsema kwa baba'ake na kuambulia kipigo kikali.
    “Pole dada Jane,” Marry na Neema walikuwa wakimpa pole mara apatapo kipigo kutoka kwa mama au pindi baba'ake arudipo. 
    “Mwacheni huyo amezidi,” mama wa kambo alizidi kumshambulia Jane. Alimpa kazi zote na kuwakataza Neema na Marry kumsaidia.
    “Yeye ndo mkubwa anatakiwa afanye kazi, nyie bado hamjaweza.Subirini mkue.”
    “Lakini mama si tunamsaidia dada Jane?” Marry ambaye ndiye mdogo alisema.
    “Nimesema nyamaza, siyo kazi zenu hizo.” Jane aliona tabu sana. Shule hapelekwi tena na mama anamshambulia. Uhuru hakuna na hakujua hatima yake. Baba alionekana kwa nadra sana. Alijiona kama yuko ndani ya mto wenye mamba wengi. Aliamua asubiri hadi baba'ake atakaporudi ili amweleze, lakini ataanzaje wakati hata baba hakumwamini. Aliamua ni bora atoroke nyumbani.


    *****
    Alikuwa na miaka 20, Jane alikuwa na akili ya kutambua zuri na baya. Alijua wazi kwamba yule hakuwa mama yake aliyemzaa. Aliona utofauti kati yake na wadogo zake Marry na Neema, watoto wa mama'ake wa kambo. Hawakufanana naye. Yeye alifanana na baba'ke na watoto wale hawakufanana na baba yao, walifanana na mama yao. Hata hivyo hakutaka kujua juu ya hilo. Yeye alikuwa ni mzuri zaidi yao. Hata neema na Marry walimsifia sana kwa uzuri wake. Alikuwa ni mweupe mwenye mvuto sana. Ni kovu dogo sana ambalo aliachiwa na mama'ake wa kambo karibu na sikio lake la kushoto lakini uzuri wake haukujificha. Umbo lake lilikuwa nadhifu.
    Ni siri ambayo hakuijua. Mama yake wa kambo alimwonea wivu sana kwa sababu aliwazidi watoto wake kwa kila jambo. Hata darasani alifanya vizuri lakini ni hila tu za mama wa kambo ndizo zilizomkwamisha asiendelee na shule. Jane hakujali kwani hakuelewa, kutokuendelea na shule kulimuumiza sana lakini hakuwa na la kufanya. Mama wa kambo alisisitiza kwa mumewe kwamba ni zamu ya wadogo zake kusoma kwanza na hivyo Jane asubiri kwanza kisha baadaye na ye ataendelea. Ni kauli hiyo ambayo ilimfanya Jane kuamua kutoroka. 
    Aliondoka nyumbani jioni sana ili awahi magari yaliyokuwa yakiondoka asubuhi sana. Jioni hiyo alipoondoka nyumbani alienda na kulala guest moja iliyoko karibu na kituo cha mabasi ya mikoani cha Dodoma. Neema na Marry walimtafuta sana bila mafanikio. Baba yake alikuwa bado yu safarini nchini Zambia. Mama yake wa kambo hakujali.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Inatosha, hakuna kumtafuta tena, kwani ye mtoto? Anajua afanyalo. Mwacheni aende atarudi,” hiyo ni kauli ya mama yake wa kambo akiwarudisha nyumbani Marry na Neema wasiendelee kumtafuta dada yao Jane. Jane alifanikiwa kuondoka. Kiasi cha pesa alichokichukua nyumbani, kilimtosha kumfikisha Dar es Salaam. Hakujua atafikia wapi lakini hakujali. Aliona ni bora akafie huko kuliko kuendelea kuishi na mama yake wa kambo.
    Taarifa za Jane kuondoka nyumbani zilimfikia Amos. Alirudi haraka kuhoji wapi alipokwenda. Debora alionyesha kutokujali wala kuogopa.
    “Hakuna anayejua alikoenda. Na ye ni mkubwa anajua kutafuta acha akatafute. Angekuwa anajali nyumbani asingeondoka.” Kauli hiyo Amos haikuifurahia. Aliingia ndani na kupumzika. Jane alikuwa ameshaondoka. 


    AMOS ANAMTAFUTIA JANE MAMA. DEBORA ANAOLEWA NA AMOS. ANAMLEA JANE KWA MAPENZI YOTE LAKINI BAADAYE ANABADILIKA NA KUWA MBOGO KWA JANE. JANE ANATOROKA AKITAKA KWENDA DAR ES SALAAM KUTAFUTA MAISHA. 
    JE ATAFANIKIWA KUFIKA NA KUPATA MAISHA ANAYOYATAKA……




    ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

Blog