Search This Blog

Monday, October 24, 2022

UTAMU WA ZEGE - 3

 





    Chombezo : Utamu Wa Zege

    Sehemu Ya Tatu (3)




    KIASI cha pesa alichokichukua nyumbani, kilimtosha kumfikisha Dar es Salaam. Hakujua atafikia wapi lakini hakujali. Aliona ni bora akafie huko kuliko kuendelea kuishi na mama yake wa kambo.
    Taarifa za Jane kuondoka nyumbani zilimfikia Amos. Alirudi haraka kuhoji wapi alipokwenda. Debora alionyesha kutokujali wala kuogopa.


    “Hakuna anayejua alikoenda. Na ye ni mkubwa anajua kutafuta acha akatafute. Angekuwa anajali nyumbani asingeondoka.” Kauli hiyo Amos haikuifurahia. Aliingia ndani na kupumzika. Jane alikuwa ameshaondoka.




    *****
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    Alifika Dar es Salaam mchana wa saa saba. Ni saa sita tu au saba kutoka Dodoma mjini hadi Dar es Salaam. Jane alishuka kituo cha mabasi cha Ubungo. Watu walikuwa ni wengi sana kituoni muda huo. Alisimama akiangaza huku na huko pasipo kuelewa mahali alipo kutokana n wingi wa watu. Alianza kuwa fuata watu walikokwenda pasipo kujua anakwenda wapi. Kila mmoja alikuwa anajali la kwake. Hakujua aanze kumuuliza nani. 


    “Samahani, naomba ni ya kwangu nimeangusha,” mmoja wa wateja aliyekuwa amesimama dukani Ubungo, aliangusha kadi ya benki wakati akitoa pesa kwa ajili ya kulipia vitu alivyochukua. Jane alimpa ile kadi. Hapo hapo Jane aliamua kuuliza kwa yule dada aliyekuwa dukani.


    “Asante kwa kuniokotea.”


    “Usijali dada.”


    “Unaonekana kama unamtafuta mtu humu ndani.” Yule dada alimuuliza Jane baada ya kumwona akiangaza huko na huko akiangalia pa kuelekea. 


    “Hapana simwangalii mtu dada, mi ni mgeni hapa. Nimepata matatizo ndo maana nimeamua kuja huku kuhangaika na maisha. Sina pa kuishi nimeondoka leo nyumbani, nimekuja huku ili niweze tu kutafuta maisha nipate japo chakula, naomba nisaidie dada sina pa kwenda,” yule dada alimwangalia sana Jane na kumwonea huruma kisha akamuuliza.


    “Unaitwa nani?”


    “Naitwa Jane Amos.”
    “Kwani we unatokea wapi Jane?”


    “Natokea Dodoma Mjini.”


    "Ahaa, unaonekana umechoka sana. yule dada alifikiria kidogo. Aliona Jane atamfaa kwa kazi za nyumbani. ilikuwa ni vigumu sana kupata mfanyakazi wa ndani. Alitokea kumpenda jane na kuamua kumchukua.


    “Twende nyumbani kwangu nitakusaidia. Si unajua kufanya kazi za ndani?"


    “Ndiyo dada,” Jane alijibu kwa upole hadi kumfanya yule dada apate huruma zaidi. Alizidi kuvutiwa alivyomwangalia Jane alivyo mzuri.alimwangalia juu hadi chini. Hakuamini kama Jane alikuwa mgeni pale Dar es Salaam. 


    “Haya subiri nimalize kuchukua vitu alafu twende.”


    “Sawa dada,” Jane aliitikia na kusimama pembeni akisubiri. Alikuwa akishangaa sana huku ameukumbatia mfuko wake ulokuwa na nguo zake chache. Gauni lake alilovaa na malapa, nywele zilizochoka kwa kukosa matunzo na ushamba aliokuwa nao. Vilitosha kumdhihirishia yule dada kwamba Jane alikuwa ni mgeni. 


    Baada ya kuchukua vitu alivyoagiza dukani yule dada aliongozana na Jane hadi kwenye gari lake. Alimfungulia mlango Jane na kuingia ndani kisha akazunguka na kuingia upande wa dereva na kupiga gari moto. Walitoka nje ya geti la kuingilia kituo cha basi Ubungo na kuelekea maeneo ya Kimara Baruti. Wakiwa njiani yule dada alijitambulisha kwa Jane.


    “Mi naitwa dada Sara.”


    “Nashukuru kukufahamu dada....umependeza dada Sara,” Jane alimsifia Sara juu ya mwonekano wake uliomvutia. Alikuwa mweupe kama alivyo Jane na mwenye umbo kubwa lakini lililokaa maridadi.


    “Nashukuru Jane mdogo wangu, mwanamke ni kujithamini na kujiremba, n'na uhakika hata wewe ukijiremba utapendeza kama mimi. We ni mzuri sana Jane.” Sara alitokea kumpenda Jane japo ilikuwa ni mara ya kwanza kuonana naye.


    “Asante dada Sara,” Jane alishukuru.
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Kwangu siyo mbali tumeshafika.” Nyumbani kwa Sara hapakuwa mbali na barabarani. Walitumia dakika 15 kufika nyumbani kwake. Sara alikuwa akiishi peke yake, aliolewa na mzungu ambaye baadaye waliachana na kurudi kwao Canada. 
    Sara maisha yalibadilika baada ya kuoana na mzungu wake 'Graham'. Alimwachia Sara utajiri na pesa nyingi zilizomsaidia kufungua biashara mbalimbali za maduka makubwa ya nguo ambazo aliagiza kutoka nje ya nchi. Hawakubahatika kupata mtoto na hivyo mzungu hakuona sababu ya kuendelea kuishi na Sara ambaye aliona ni mgumba. 
    Hivyo aliamua kurudi kwao. Sara aliumia sana lakini hakuwa na la kufanya zaidi ya kuendeleza maisha yake mwenyewe. Alijiuliza kwa nini Graham hakutaka kupima ili wajue tatizo na kuamua kukimbia. Sara hakujali.


    “Karibu Jane, hapa ndiyo nyumbani kwangu. N’takuonyesha kila kitu kilipo, jisikie poa sana,” Sara alimkaribisha Jane nyumbani kwake, Jane alionekana kushangaa kila alionalo ndani kwa Sara. 


    “Ukaoge kwanza kisha ule afu upumzike mengine tutaongea kesho asubuhi.”


    “Sawa dada Sara.” Sara alimwonyesha Jane mahala pa kuogea na Jane aliingia na kuoga. Alimtayarishia chakula na wote wakala na kisha akamwonyesha chumba ambacho angepumzika hadi asubuhi.




    *****


    Asubuhi Jane aliamka akionekana mchangamfu sana. Sara alifurahi sana kumwona katika hali ile. Jane ndiye alikuwa wa kwanza kuamka na kwenda kuketi katika sofa akimsubiri Sara aamke. Sara alimwonyesha sehemu ya kunawia uso. Sara alitayarisha chai na wote wakaanza kunywa.


    “Jane, ulisema kwenu Dodoma?”


    “Ndiyo dada Sara.”


    “Ulikuwa unaishi na nani huko?”


    “Baba na mama wa kambo, mama angu alishafariki dunia nkiwa mdogo.”


    “Ooh, pole sana Jane. Ikawaje ukaondoka huko nyumbani?”


    “Ni kwa sababu ya mama angu ninayeishi naye sasa hivi. Mambo yake yamenishinda n'kaamua niondoke.”


    “Baba naye akasemaje au alikuwa haoni maana najua hayo ni mateso tu ya huyo mama.”


    “Nimetoroka bila kumwambia yeyote, baba anasafiri na kutuacha nyumbani hata mwezi,” Jane aliendelea kumwelezea Sara matatizo yaliyomfanya apachukie nyumbani na kukimbilia Dar es Salaam.


    “Sasa ulijua huku unakuja kukaa kwa nani?”


    “Hapana sikujua dada Sara, hivyohivyo tu, bora nife huku kuliko kubaki nyumbani na mateso ya yule mama.”


    “Pole sana Jane, matatizo yako hayapo tufauti na yangu kwani hata mimi nimelelewa na mama wa kambo ambaye alisababisha hadi nkatoroka na kuanza maisha yangu binafsi hadi maisha yangu yalivyokuwa mazuri. Sara alimwelezea Jane maisha aliyoyapitia hadi akafikia hapo alipo.


    “Wanaume ni watu washenzi sana Jane, hawana mapenzi ya kweli kama jinsi wanawake wengi wanavyojali. Mwanamume akikupenda utamjua na ambaye anakuchezea tu utamjua kama utakuwa mwangalifu. Usitegemee mwanamume akuambie tu nakupenda alafu awe ni wa kuhitaji tu kila wakati uwe naye kitandani au kwenye starehe. Mwanamume anayekupenda siku zote atakujali na kukuthamini kwa kuona kwamba huyu naye ni mwenzangu na anastahili heshima kama mimi ninavyojiheshimu.”


    “Dada Sara, sasa utamjuaje mwanamume wakati ndiyo anakufuata?”


    “Ukiwa huna tamaa na mali wala fedha na starehe, utampata tu mwanamume anayekupenda kwa dhati na atakayekuheshimu na kukulinda. Pia atakuwa na faida kwako katika malezi ya familia mtakayoianzisha.”
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    “Ina maana wanaume wengi ni waongo sana?”


    “Jane mdogo wangu, mimi niliolewa na mzungu, lakini sikuonja penzi lake zaidi ya kuniona mimi ni mgumba bila ya yeye kwenda kujichunguza pia. Alinioa tukakaa miaka miwili lakini hatupati mtoto. Ni mwaka jana ndiyo aliondoka na kuniachia hizi mali na ye kurudi kwao Canada. Sitamani tena wanaume kwa jinsi alivyonifanyia yule mtu. Hakuthamini mawazo yangu. Nilitaka na yeye akachunguzwe tujue tatizo lakini hakukubali na kuniona mimi ni mgumba. Sikujali kabisa, kwa sababu aliniachia mali, niliamua tu nijiendeleze mwenyewe nikajimilikisha kila kitu na ndiyo mpaka sasa naishi peke yangu hapa.”


    “Nimekuelewa sana dada Sara. Sitaweza kuharibu mwili wangu kwa kutembea na wanaume. Nitajitahidi kujitunza hadi nitakapompata mwanamume atakayekuwa tayari kunijali na atakayenipenda kwa dhati,” Jane alikuwa akisema hayo huku akiondoa vyombo mezani na kuvipeleka jikoni.




    *****
    Baada ya kujitayarisha kwa muda, Sara na Jane walitoka na kuelekea mjini. Jane alipendeza sana. nguo alizopewa na Sara zilimpendeza na kuonekana mrembo zaidi. Walikuwa kwenye gari aina ya Toyota Rav4. Njiani Jane aliangalia huku na huko akiliangaza jiji kwa mara ya kwanza. Wakiwa maeneo ya Magomeni, Sara alikuwa akimwonyesha Jane na kumwelekeza taa za barabarani zilivyokuwa zikifanya kazi. Ghafla alishindwa kuumudu usukani na almanusura amgonge kijana aliyekuwa akivuka barabara.
    “Dada Saraa! Jane aliita kwa nguvu baada ya kumwona Sara akielekea kumgonga yule kaka. Haraka alifunga breki na kumgusa kidogo. Yule kijana hakuumia. Sara alipaki gari lake pembeni na kushuka na kumfuata. Jane naye alishuka na kumfuata Sara ili ajue kitakachoendelea.
    “Samahani kaka yangu. Sijakuona. Umeumia?” Sara alitoa noti ya shilingi elfu kumi na kuishika mkononi na kumuuliza yule kijana kama ameumia.
    “Hapana dada angu, sijaumia. Ila uwe makini sana.” yule kijana alisema huku akivuka barabara kuelekea kibandani kwake.
    “Pole sana kaka,” Jane alimpa pole yule kijana.
    “Nashukuru bibie,” Sara alimkabidhi yule kijana ile noti ya elfu kumi. 
    “Hapana dada, usijali. Kikubwa ni uzima nashukuru Mungu sijaumia kwani ningeshindwa hata kuipata hiyo noti kwenye biashara zangu, nashukuru, asante sana,” yule kijana aliikataa ile noti na kushukuru kwa kuwa hakupata majeraha.
    “Hapana, naomba tu uichukue. Mi nakupa tu.”
    “Haya, asante sana dada angu. Nawatakia safari njema.”
    “Tunashukuru.” Jane alisema huku akimwangalia sana yule kijana. Alidhani kutokana na kugongwa angeleta fujo kana baadhi ya vijana wanavyofanya ikiwemo na kuiba kwenye magari na kumshambulia dereva aliyesababisha ajali. Haikuwa hivyo kwa yule kijana. Alichukua ile noti aliyopewa na Sara na kuiweka mfukoni kisha kuwaaga na kuondoka. Watu nao walitawanyika.
    Sara na Jane waliingia ndani ya gari na kuondoka. Walikuwa wakiogopa sana baada ya watu kujaa pale. Walikuwa wakielekea Kariakoo ambako maduka ya Sara yalipatikana. Sara alimpitisha katika duka moja baada ya lingine na kumtambulisha kwa wafanyakazi wake kwamba ni mdogo wake. Wengi walimsifia kwa uzuri wake. Walimpenda sana Jane.
    Sara alimzungusha maduka ya nguo na kumnunulia nguo nzuri za kutumia. Jane alifurahi sana. Alijihisi mpya katika dunia. Alitamani angewahi zaidi kuja Dar es Salaam ili ajue mengi.
    Jane alikuwa akiwaangalia wapitanjia na watu waliokuwa wakiingia dukani kuulizia bidhaa na kuchagua. Yeye alibaki kimya kusikiliza wateja wakizungumza na wauzaji wa duka hilo. Alikuwa akitazama nguo zilivyojaa ndani ya duka. Alitamani sana kuwa na duka kama hilo.
    Sara alimaliza mazungumzo yake na wafanyakazi na kuondoka na Jane. Waliendelea kuzunguka mjini na kumwonyesha Jane sehemu mbalimbali za jiji kama Posta, baharini na maeneo mengi ya kuvutia. Jane alifurahia sana safari yao. 




    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    *****
    Ilikuwa imepita mwaka mmoja tangu Jane alipoondoka kwao. Maisha ya yake yalianza kubadilika. Alipendeza. Alizidi kuvutia na kuonekana mrembo zaidi ya alivyotua Dar es Salaam kwa mara ya kwanza. Sara alimchukulia kama mdogo wake na siku zote Jane alimpenda Sara kama dada yake wa kuzaliwa pamoja. Kila mmoja alijivunia kwa mwenzake. Hakika walishibana. Alilosema Sara Jane hakukaidi kufanya. Alimheshimu sana Sara kwa kila kitu. Alijua bila yeye asingefika hapo alipo. Alimshukuru kila siku pasipo kujaribu kufanya kile ambacho kingemfanya Sara achukie.
    Sara alichoka kukaa bila ya kuwa na mume. Alishawahi kuongea na Jane kuhusu mipango yake ya mbele lakini hakuwahi kumtajia mpango wa kuolewa. Sasa alihitaji mtu wa kuishi naye ili amfariji na apate ladha ya mapenzi.
    Sebastian Ndauli alikuwa ni mwanamume pekee aliyemvutia Sara. Alikuwa ni mfanyabiashara pia ambapo mara nyingi walisafiri pamoja. Sara aliweza kumjua na kufahamu mengi kuhusu Sebastian. Hakika aliona huyo ndiye angekuwa mwanamume pekee ambaye angeweza kuishi naye.
    Aliamua kumwelezea Jane juu ya uhusiano wake na Sebastian toka wafahamiane miaka miwili iliyopita. Alimwita Jane akiwa jikoni na kumwambia.
    “Mdogo wangu Jane, ni mwaka sasa umeisha tangu tuwe wote.”
    “Ndiyo dada,” Jane aliitikia.
    “Hivi karibuni nitamleta mtu wa tatu.”
    “Nani huyo dada Sara,” Jane aliuliza huku akinawa mikono baada ya kumaliza kuosha vyombo. Alifunga maji na kuketi katika sofa ili kumsikiliza Sara.
    “Ni mchumba wangu nataka umjue, atakuja hapa siku moja.”
    “Dada Sara unataka kuolewa?” alihoji Jane kwa huzuni.
    “Ndiyo Jane, kukaa peke yangu inatosha sasa nataka niolewe na mwanamume ambaye nimempenda na ni mwaminifu. Ni mfanyabiashara mwenzangu ambaye kwa kweli ninaweza nikasema ndiyo chagua langu.”
    “Dada Sara mi nakuaminia sana. Natamani sana niwe kama wewe dada Sara.”
    “Usijali mdogo wangu, tupo pamoja. Nitahakikisha unakuwa kama mimi, umeshamaliza kuosha vyombo?”
    “Ndiyo dada,” Jane alimjibu kwa tabasamu. Umlete nnyumbani dada nimwone.”
    “Usijali mdogo wangu. Atakuja siku yeyote na utamjua.”
    “Sawa dada.”
    “Ahaa, sawa, leo tunatoka, sema nikupeleke wapi tukatembee?”
    “Aaah, dada Sara, kila wikiendi tunatoka, leo tukae nyumbani tu.”
    “Hapana Jane, mi sitaweza kukaa hapa hadi jioni, n’takuacha wewe mi n’tatoka.”
    “Mmmh! Sitabaki mwenyewe, na mi n’tatoka na wewe, n’takuwa mpweke sana.”
    “Haya sema unataka twende wapi leo?”
    “Napenda twende ufukweni kama siku ile tukale urojo,” Jane alifurahia sana siku ambayo ilikuwa ni mara ya kwanza kutembea katika fukwe za Bahari ya Hindi. Alitamani kurudi tena na tena. Sara alimpeleka sehemu alipojisikia kwenda kila wikiendi. Jane aliuzoea sana mji na kuwa karibu sana na Sara wakati wote. 
    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
    *****
    Siku hiyo Jane alikuwa mwenyewe nyumbani. Sara alikuwa akijivinjari na Sebastiani. Aliitamani hiyo raha kwa muda mrefu pasipo kuipata baada ya mzungu kurudi kwao. Ni Sebastiani pekee aliyeweza kumfanya ajisikie mpya katika dunia ya mapenzi. Sara alionekana kuzidiwa na hali aliyokuwa nayo. 
    Hakuupa muda nafasi upite usiku huo kutokana na mihemko yao. Ni usiku uliojikoleza na penzi zito la wawili hao. Hakuwahi kuskia hali hiyo tofauti kwa muda mrefu. Sasa haki yake anaipata. Tena kwa mwanamume aliyediriki kumvulia nguo na kumkabidhi kila kilicho chake akifanye anachokitaka. Mwanamume aliyempenda na kumjali.
    Sebastian alifanya kile alichokijua. Alimshika kila mahali Sara ambaye na yeye alirudisha mapigo kwa ufundi wake. Aliutumia vizuri ulimi wake na kinywa katika kuiburudisha nafsi ya Sebastian na kumlegeza kwa maneno matamu. Wote walifurahia siku hiyo. Ya kwanza kukutana miili yao kama wapenzi. 
    Sara alifurahia zaidi. Upole wa Sebastian alihisi haupo tena. Hakuwa Sebastian yule aliyemzoea. Si mwongeaji sana bali wa vitendo. Kweli alitenda. Akatenda vile alivyokaribishwa atende. Sara alifurahi sana. 


    JANE ANAONYESHWA JIJI. ANAFURAHIA KUANZA MAISHA MAPYA AKIWA PEKE YAKE KUWAPISHA SARA NA SEBASTIAN. 
    JE NINI KITAMTOKEA AKIWA MWENY


    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog