Search This Blog

Monday, October 24, 2022

SEX MACHINE - 1

 







    IMEANDIKWA NA : AHMED JIRIWA



    *********************************************************************************



    Chombezo : Sex Machine

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    MWANZO.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Saa 05:45 alfajiri, bado pumba za kigiza cha usiku zilikuwa bado hazijapukutika na kuufanya mwangaza wa asubuhi hiyo kushindwa kuyapata mamlaka ya siku yake hiyo kwa ufasaha. hakukusikika sauti za milio ya ndege wala mapokezano ya majogoo kama ilivyozoeleka sehemu nyingi, utulivu ulikuwa mkubwa sana ndani yaa mtaa huo ambao ulikuwa ukiishi watu wazito. ambao ulikuwa ukifahamika kwa jina la Forest. mtaa ambao unapatikana pembezoni kidogo mwa mji kasoro bahari, mji wa Morogoro. Na kwa majira hayo, ni mageti tu ya baadhi ya nyumba kadhaa ndiyo yaliyokuwa yakifunguliwa. Magari ya kifahari yakitoka na kupotea barabarani ikiwa ni katika harakati za kila siku za kiutafutaji huku yakisindikizwa na kigiza hicho chembamba cha asubuhi hiyo. Lakini ndani ya jumba moja kubwa la kifahari kwa majira hayohayo, ndani ya chumba kimoja, alipata kuonekana kijana mmoja ambaye alikuwa akigaagaa kitandani mithili ya Funyo juani. si kama ni kutokana na kukatika kwa usingizi na kuukosa tena kwa nyakati hizo, laa hasha! Usingizi kwake haukuwa kitu cha thamani sana na kuukosa pia lilikuwa ni jambo la mazoea kabisa kwani si mara moja wala mara mbili, amekuwa akilala kiutaratibu tu kwamba inapofika usiku hana budi kaulala lakini si kwa usingizi kama ilivyo kwa wengine. hata kwa siku hiyo usingizi haukupata kumtembelea kijana huyo hadi anakutwa na alfajiri hiyo, aliishia kubingilia tu kushoto na kulia, nyuma mbele kama mcheza sarakasi. hayo ndiyo yalikuwa maisha yake. Usingizi kwake kwa usiku mzima ulikuwa kama lulu au pande la dhahabu, haukumtembelea kabisa kijana huyo. "sijalala kabisa leo Mungu wangu?" alijiwazia kijana huyo huku akiwa kalala chali akilishangaa dari la chumba hicho chenye thamani kubwa, lililopambwa kwa michoro mbalimbali ya kupendeza. ni kama alikuwa akilitafuta kosa la fundi aliyetengeneza lakini si hivyo, alikuwa analundo kubwa la mawazo ubongoni mwake. "ninaishi katika wakati mgumu sana, nimekuwa kama pambo la Paka ndani ya nyumba hii ni wa kusogezewa kila kitu na kila wakati, lini maisha haya kwangu yatakuwa historia? Lini na mimi nitakuwa na maisha yangu kama ambavyo vijana wengine wanaishi? Lini basi Mungu wangu, lini?" ndivyo alivyokuwa akijiuliza maswali mengi kijana huyo. alitulia kidogo na kuvuta pumzi ndani na kuzitoa pasi na utaratibu maalumu kasha akaendelea kuutiririsha mkanda huo wa mawazo. "ni kweli sijawahi kusumbuliwa wala kunyanyasika kwa mjomba hata siku moja na mkewe pia amekuwa akinijali sana, anaupendo wa hali ya juu huyu mama, sijawahi kukosa mahitaji ya muhimu iwe kwake ama kwa mjomba, wananijali kwakweli Mungu awajaalie na awape maisha marefu kwa upendo wanaonionesha sina cha kuwalipa kwa hili. Ni kiasi gani cha pesa nikihitaji na wasinipe, lakini maisha haya mpaka lini sasa"? alijinyanyua kitandani na kukaa kitako mara baada ya kuwaza hayo, akapiga kite kikubwa cha kujikatia tamaa na kuvamiwa na mfadhaiko mkubwa wa moyo. mawazo yalijenga ukuta mzito sana kwenye moyo wa kijana huyo. Alishachoka kujigeuza kama mgonjwa wa tumbo la kuhara pale kitandani. " naonekana ni shababi niliyekamilika sana, ni nani kwa muonekano huu ataamini kuwa nina shida. najua utashangaa mimi kusema kuwa ninashida, ninashida ndiyo. miaka ishirini na miwili sasa bado napangiwa. kila anitazamae anadhani labda ni kijana ninayejimudu sana kimaisha. Naonekana hivyo. Ndiyo, ninaonekana wa kisasa sana. navaa vizuri, nafanya mazoezi kiasi cha kuwa na mwili mzuri wa kuvutia, mwili ambao ni kivutio kikubwa kwa nabinti wengi wanaonitazama. Ninakula vizuri pia kiasi cha kuufanya mwili wangu kuwa na afya nzuri na yenye muonekano wa mtu asiye na dhiki lakini si kwa jasho langu, si kwa nguvu zangu mwenyewe. Hii inaniuma sana" alizidi kuwaza na kuwazuwa kijana huyo. Na hivyo ndivyo alivyoikaribisha asubuhi yake hiyo na sidhani hata kama ingekuwa ni siku njema kwake kwani ule usemi wa siku njema huonekana asubuhi, kwake ilionesha dhahiri kuwa itakuwa ni siku yenye mashaka makubwa sana.



    Kijana huyo kwa jina alikuwa anaitwa Chriss. kijana mpole na mstaarabu, mweupe kidogo, nywele zake fupi alizozikata kiafrika, mrefu kwenda juu na anasura ndefu kidogo. alikuwa ni kijana asiyependa majivuni japo yu' katika familia yenye utajiri mkubwa sana mjini hapo. aliitazama saa ya ukutani ikamwambia kuwa tayari kwa muda huo ilikuwa imeshatimu saa tatu kasoro robo za asubuhi. akapiga kite kilichoashiria uchovu kasha akajitoabkivivu pale kitandani na kukiweka kitanda chake katika hali ya usafi pamoja na chumba chake kwa ujumla. kilikuwa ni chumba kikubwa na cha kisasa chenye kila kifaacho kwa kijana wa kileo. kitanda kikubwa, kulikuwa na sofa moja linalotosheleza watu wawili sambamba na vikolokolo vingine vingi. alipohakikisha kuwa kila kitu kipo katika hali ya usafi, alichukuwa taulo na kujiingiza maliwatoni kwa ajili ya kujiweka safi. alipomaliza kujifanyia usafi huo, alivaa bukta yake ndefu na pana ambayo maranyingi hupenda kuivaa akiwa mazingira ya nyumbani, juu alitupia na fulana iliyomkaa vizuri na kutoka chumbani humo. Alifika sebuleni na kuwakuta wenzake wakiwa katika meza ya chakula wakipata staftahi safi kabisa. Mezani hapo alikuwepo mke wa mjomba wake, dada wawili wa kazi Salome na Maida pamoja na binti mdogo apatae miaka sita anayefahamika kwa jina la mery. alimsalimia shangazi yake huyo kasha akawasalimia na wale mabinti na yeye kuvuta kiti na kujumuika nao pamoja mezani hapo. "umechelewa sana kuamka leo na nimeshangaa kumkuta mjomba wako akiwa anafanya mazoezi mwenyewe, nini kimekusibu Chriss au ni uchovu wa kawaida?" aliuliza anti yake huyo huku akimsogezea sahani iliyo na mayai ndani yake. "leo sikuwa sawa nimeamka na mawazo mengi sana anti" akajibu Chriss. "najua Chriss, najua sana kwa umri ulionao unahitaji kuwa na kazi pia uwe na kwako lakini hupaswi kuwaza namna hiyo kwani mjomba wako analihangaikia sana suala hilo, unachotakiwa kufanya ni kuwa na subira mwanangu sawa?"

    "sawa anti nimekusikia na nitajitahidi kuwa mvumilivu kwani nimejitahidi sana kutafuta ajira bila mafanikio yoyote pamoja na elimu kubwa iliyoambatana na utaalamu wa tehama lakini pia ni bure. Wacha nimsubiri mjomba, ninaimani nae sana kama aliweza kuisimamia elimu yangu kwa kiasi kikubwa hadi hapa nilipo, hashindwi kunitafutia ajira. Acha tu nimsubiri ninaimani hata yeye hili liamuumiza sana kichwa" alisema Chriss na alikuwa akimaanisha sana hicho akisemacho. "ni kweli kabisa mwanangu" alijibu shangazi huyo mwenye mapenzi makubwa sana kwa Chriss waweza sema ni mtoto wake wa kumzaa. Alimpenda sana Chriss anti Martha labda ni kwasababu alimlea kijana huyo tangia alipotupwa mikononi mwake baada ya wazazi wake kupata ajali mbaya sana ya gari angali akiwa na miezi sita tu tangu kutoka tumboni mwa mama yake. yeye akiwa na mumewe wakajitolea kumchukuwa na kuamua kuishi nae na hata alipokuja kukua aliamini kabisa kuwa hao anaoishi nao ndiyo wazazi wake halisi. Kumbe haikuwa hivyo. Wakamsomesha kwa gharama kubwa kuanzia darasa la awali hadi kufikia elimu ya juu kabisa. huko ndipo kijana huyo alipopata kujua ukweli huo. Mara baada ya kumuuliza mlezi wake huyo ambaye kwa kipindi hicho aliamini kabisa kuwa ni mzazi wake. Hapo akapewa ukweli wote kuhusu yeye na jinsi wazazi wake kupata ajali ya gari na kupoteza maisha. Chriss alifarijika sana na kuona kumbe anajaliwa na kupewa thamani kubwa na watu ambao si wazazi wake halisi bali ni ndugu wa mama yake tu. "ninaimani baba yangu anafarijika sana huko aliko kwa kuona kijana wake bado niko hai, mlale mahala pema peponi wazazi wangu na nawapenda sana" ndivyo alivyosema Chriss kipindi anapewa historia hiyo yenye kuhuzunisha sana. Hakuwa na budi aliamua kuisifu kazi ya Mungu na kumshukuru tu kwani yeye ndiye mwenye mamlaka na milki ya kilakitu duniai kote. Bahati mbaya au nzuri, mjomba wake na mkewe hawakuwa na uwezo wa kupata mtoto kwa mujibu wa matokeo ya vipimo vya wataalamu mbalimbali duniani kama alivyoelezwa hivyo wakaamua kuweka nguvu zao zote katika kuhakikisha Christiano anapata malezi bora na salama kabisa kwani huyo ndiye mrithi pekee wa kuendeleza mali hizo. Wakampeleka katika vyuo mbalimbali vilivyobobea kwa Sayansi duniani kote. Chriss akapata elimu ya juu kabisa ya masuala ya Sayansi ya mawasiliano kitaalamu ilifahamika kama Scientific comunication (SC). Cha ajabu na cha kushangaza ni pale kijana huyo alipotaka kutafuta ajira, alikutana na vikwazo vingi sana. Alihangaika kutuma maombi kwenye ofisi za serikali na makampuni binafsi bila mfanikio. kuna kipindi akaamua kuomba afanye hata bure bila malipo yoyote kwa muda fulani ili tu kuonesha uwezo wake pia hakukuwa na majibu mazuri. alijisikia vibaya sana lakini ndiyo hivyo tena. "nini faida sasa? Kusoma kote huku ni show tu ooh! no." jambo hilo lilimkosesha kabisa amani kijana huyo, alikonda kwa muda mfupi. hadi pale mjomba wake alipomwambia kuwa asiwe na wasiwasi atalisimamia suala lake hilo anachotakiwa kufanya ni kuwa mvumilivu na kufanya sala kila wakati. Baada ya kusubiri kwa muda kidogo ndipo mjomba wake alimjia na kumwambia kuwa muda si mrefu angepata kazi na ilikuwa ni kazi nzuri sana. Chriss alifurahi sana na kuona sasa Mungu amekisikia kilio chake na maombi aliyokuwa akimuomba kila siku. Hicho ndicho pekee kilichomfanya Chriss kuwa mpole na kusubiri hicho alichoahidiwa. Maongezi hayo yaliendelea taratibu huku wakiendelea kupata staftahi hiyo hadi pale matumbo yao yalipotosheka, wakaiacha meza hiyo na kila mmoja kukamata jukumu lake linalomkabili kwa asubuhi hiyo.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    ****************



    Chriss yeye baada ya kutoka mezani hapo, aliekea kwenye bustani yake ya maua aliyoitengeneza mwenyewe kwa mikono yake. Akawa anaifanyia fanyia usafi wa hapa na pale wa kuzidi kuipendezesha bustani hiyo iliyokuwa imelizunguuka bwawa la kuogelea nyumbani hapo. Wakati akiwa anaendelea kufanya usafi, kuna mtu alifika kwa kunyata na kuligusa bega lake la upande wa kulia na kumfanya ageuke. "bustani inapendeza sana Chriss kwa ajili yako, ulipokuwa nje ya nchi jaikuwa ikipendeza kama hivi. unaijali sana bustani hii" mtu huyo alisema. "ndiyo, Salome na nimekuwa nikiiwaza tangu nikiwa huko. Unajua bustani hii nimeianzisha tangu nikiwa darasa la tatu na nimekuwa nikiiboresha kwa kila hatua" alijibu. "naona. Kweli inapendeza hadi mtu unavutika kuja kukaa tu angalau" Chriss akatabasamu baada ya kauli hiyo kutoka kwa Salome, akasema. "vipi Salome unataka kunisaidia nini? Lakini umechelewa kodogo tu maana nimekwisha kumaliza usafi leo hakukuwa na kazi kubwa sana nilikuwa nikiondoa baadhi ya magugu haribifu. Hapa nipo naangalia ufundi wa Mungu kwa kupitia wale watoto wa Bata kwa jinsi wanavyoyakata maji kwa ustadi wa hali ya juu kabisa"



    "najua" akasema Salome. "najua nimechelewa Chriss na ndiyo maana nipo hapa. Sipo hapa kwa ajili ya Bata wale ambao mapenzi yao makubwa ni maji, ni kweli wanakifurahia wakipendacho na Muumba amewaumba hivyo. Mimi nipo hapa kwa ajili yako na nipo hapa kwa ajili ya penzi langu Chriss. nisifurahi kwa nikipendacho? Au kwanini nisiwe kama wale mabata Chriss? Angalia wanavyofuatana, angalia wanavyoifurahia siku yao hii mpya, angalia tu. Nimekuwa na moyo gani sijui mimi Salome? Nimekuwje najishangaa. Hivi Chriss unafikiri ni kwanini nang'ang'ania kuwa na mwanaume malaya?"

    "unamaanisha nini Salome?" aliuliza Chriss akiwa katika mshangao mkubwa sana baada ya Salome kuongea maneno yale tena akiwa katika hisia kali sana. "namaanisha haya niyasemayo. Unafikiri ni kwanini labda? Ninaumbo zuri, shepu namba nane, ninasura ambayo bila vikorombwezo wala vitakatishi bado inauzika. Sasa kwanini nimekung'ang'ania wewe mwanaume usiyejua kumthamini mwanamke akupendaye kwa dhati?" alizidi kutema cheche za moto mwanadada huyo. Alionekana dhahiri hakuwepo pale kimasihara hata kwa thumni moja. aliikuwa anamaanisha kweli. Chriss aligwaya. Hakuwa na utetezi thabiti juu ya shutuma hizo, huwenda yote ayasemayo binti huyo yanaukweli ndani yake. "Ni kweli Salome ni mpenzi wake wa siku nyingi sana lakini hili la kuwa kunausaliti unaoendelea humo ndani pia linawezekana kwani Chriss alikaa kimya tu kila alipokuwa akishutumiwa. "Mungu wangu hili nini tena, au ameshajua tayari kuwa nimetembea na Maida?" alijiuliza mawazoni Chriss.

    Maida ni miongoni mwa mabiti ambao ni watumishi wa ndani wa jumba hilo kubwa. pia Maida alikuwa akijua fika kuwa Chriss anatoka na Salome. Hapo Chriss alijifanya kujizunguusha na kujifanya kutokujua jambo lolote lile. Ni kweli tupu kuwa Chriss alishiriki kitanda kimoja na Maida lakini kitu kilichomchanganya kwa wakati huo ni je, Salome amejuaje? hili lilimpa wakati mgumu kidogo na hakulielewa. "sijakuelewa Salome mpenzi hebu niweke wazi juu ya jambo hilo unalolizungumza" akasema Chriss. "hujaelewa? Hujaelewa si ndiyo? Hivi kilikuwasha nini ukatembea na Maida?"

    "what!!?" Chriss akajizugisha na kujifanya ndiyo kwanza anayasikia yale maneno na alishangaa kwelo si utani. Na si kwamba hakujua kweli laa! Alijua sana ala kilichokuwa kikimuumiza kichwa, ni vipi atajitetea hapo. Salome akazidi kufurika kwa ghadhabu, akaja juu kama moto wa kifuu uwakavyo. "nini kinachokushangaza sasa? Hujui? Hujatembea nae? Nakuzushia au ni lipi linalo kushangaza weww mwanaume?" akachachiwa kwa maswali mfululizo. Chrisa hakujua lipi alijibu na lipi liwe la mwisho kujibu, akabaki kabung'aza macho kama Pono baharini, akashusha pumzi nzito. "mbona siyo siku nyingi sana tangu nifanye mapenzi na Maida, inamaana ndiyo mchezo wao sasa si ndiyo? Ok, nimeelewa" akawaza Chriss na kukumbuka mambo mengi sana yaliyopita. Alikumbuka jinsi Maida alivyomvamia chumbani kwake majira ya usiku wakati akiwa anajiandaa kulala huku msichana huyo akiwa ma khanga moja tu nyepesi kifuani tena akiwa jajavaa kitu kingine chochote kabla na baada ya hiyo khanga na Chriss yeye ikiwa ndani ya bukta mtepweleko. mshituko mkubwa ukamvaa kijana huyo asielewe nia na dhamira kuu ya ujio huo chumbani kwake tena mvamizi mwenyewe akiwa katika vazi tatanishi. Alishtuka. "Maida!" ndilo neno la kwanza lililomtoka kinywani mwake mara baada ya mtoto huyo wa kike kuufunga mlango kwa ndani vizuri. "naomba unisamehe kaka Chriss kwa kuwa mgeni nisiye rasmi ila tambua kuwa imenibidi kutokana na kukosa budi kaka" alisema Maida. Chriss alizidi kupata bumbuwazi la mshangao na maswali lukuki yakipita kichwani mwake. "amekosa budi? Nimsamehe? Aaama! Inamaana amekusudia kuja humu ebbo! Sasa kwa nini?" maswali hayo ya kijinga jinga yalizidi kumuandama kijana huyo bila ya mupatikana kwa jibu hata moja. "kaka Chriss nimechoka, nasema nimechoka kabisa na siwezi" alisema na kutulia akiyaacha yale maneno yageuke kuwa ni swali tata kwa Chriss kishapo alikiruhusu tena kinywa chake kiendelee kuzungumza. "Salome amekuwa akininyanyasa sana kaka Chriss, kila siku nimekuwa mtu wa kuhadithiwa kila ambcho amekifanya na wewe na imekuwa ni desturi yake sasa. Halali chimbani kwake hadi aje kuniumiza kwa kunikashifu eti, nakosa sana raha" maneno hayo kutoka kinywani mwa Maida, yalikifanya kinywa cha kijana huyo kubaki wazi mithili ya mtu aliyeona kambo la kuogofya sana. "Salome!" aliita moyoni Chriss. "kwanini sasa umeamua kulifanya hili jambo lisiwe siri, kwanini unataka mjomba anielewe vibaya, kwanini sasa? Unafikiri ugomvi wenu utakuwa siri pale mtakapoanza kutupiana maneno?" alijiuliza mwenyewe kijana huyo pasina kutoa sauti yoyote huku kinywa chake kikiwa wazi vivo hivyo. "Salome huyu huyu wa humu ndani?" Chriss akauliza swali la kipumbavu kabisa ambalo hata hakulitarajia. Maida alitamani kucheka kwa jinsi kijana huyo alivyopagawa kwa uchache tu wa maneno hayo aliyompa, akajua kama ataugongelea zaidi msumari huo wa moto, ni dhahiri kabisa angefanikiwa kulifaidi penzi la kijana huyo msifiwa. "huyu huyu ndiyo, kuna yupi mwingine" alijibu Maida huku akiikunja ile khanga zaidi na kuifanya miguu yake mizuri iliyojaa vema kupata kuonekana. Waswahili husema, macho siku zote huwa hayana pazia na kitazamwacho ndicho kitamaniwacho. Haya maneno ni dhahiri kabisa na yamejidhihirisha kwa huyo kijana kwani Chriss alijikuta akimeza funda kubwa la mate mara baada ya kujionea mguu huo mzuri usio na hata kovu la bandia. Hali hiyo ilionekana vema kabisa na binti huyo kiasi kuona ushindi uko jirani kabisa, alijiaminishia ushindi haswa kwa kijana hiyo. Mwanaume ni kama Mbwa kwa Chatu, mitego kidogo tu akinasa hafurukuti. Maida akaona hapo ndipo hasa alipopataka hakulaza damu, akaanguka mzimamzia. "kaka Chriss na mimi nataka"

    "niniii!!?" akashtuka Chriss. "unataka kuniambia hujanisikia kaka Chriss?" aliuliza Maida huku sauti akiwaameibadilisha kabisa na kuifanya itokee puani. Maidaalidhamiria kuhahakikisha jambo hilo ni lazima lifanikiwe. "no, haiwezekani kabisa Maida, siwezi kufanya hivyo. Wewe unajua kuwa tayari nimeshatembea na Salome sasa na wewe tena unataka. Hapana tena naomba utoke humu ndani haraka, ni ngumu mimi kufanya hivyo siwezi Maida please" akasema Chriss tena akiwa anamaanisha. Maida hakutegemea kama Chriss angetoa jibu hilo tena akiwa mkavu kabisa lakini nini dhamira yake. ni kuingia humo chumbani na kuangalia mandhari ya chumba hicho? Ah, ah, kumuonesha Chriss kuwa hata akiwa mbele ya mwanaume anaujasiri wa kuvaa khanga moja. Pia ah, ah. Sasa nini dhamira yake kwa kwenda chumbani kwawanaume huyo tena usiku kama huo. Leo atoke pasi na kuitomiza. Inamaana atakuwa yupo tayari kuyapokea manyanyaso ya mwanamke mwenzie tena naye akiwa ni mrmbo pengine kuliko hata yeye. Maida alichoshwa na masakamo. "kaka Chriss utanisamehe, leo lazima nitimize azma yangu niliyo iazimia toka nipo chumbani kwangu" pengine labda binti huyo alisema hivyo moyoni mwake. "kak Chriss nadhani unayajua maisha tunayoishi humu ndani si ya kumruhusu mtoto wa kike kutoka, mimi nitaipunguzia wapi mihemko yangu? Mwanaume ni wewe tu humu ndani Chriss jakuna mwingine na ndiyo maana nimekuja kwako. Au simfikii Salome kwa uzuri na urembo au labda ni nini haswa, hebu niangalie. nina kila sifa please Chriss i'm tired" aliamua kulalamika kabisa Maida huku akijigeuza na kujiringisha mbele ya mwnaume huyo ili tu kumunesha Chriss kuwa hata yeye ni mwanamke na anakila sifa ya urembo aliosusiwa na mola wake na wala si wakichanganyia na madawa ya kichina. Chriss alishusha pumzi nzito sana na kubaki hoi. alishindwa kujua afanye nini kati ya kuendelea na msimamo wake wa kutomkubalia binti huyo au amkubalie. Je, akimkubalia si ndiyo mwanzo wa kutambiana maana kila mmoja atakuwa nacho cha kumtmbia mwenzake. Na akimkatalia, Maida anaweza akachoshwa zaidi na kejeli za Salome mwishowe akaamua kumwambia shangazi na akimwambia shangazi, inamaana na mjomba naye atajua. "ooph! My god please help me, naelekea kichanganyikiwa sasa kwa hili" aliwaza Chriss. "lakini hata Maida ni mzuri sana na anaumbo huyu mtoto. naweza kufanya anachotaka kwani si mara moja tu" alijishauri zaidi kuhusu hilo jambo. Macho yake yaliusawiri mwili wa msichana huyo uliostiriwa na upande wa khanga tu tena iliyo nyepesi kabisa. Pumzi zikamshuka zaidi. "anakifua kizuri mno, macho yake yananifanya nikose kabisa ujasiri wa kumkatalia. Hapana Mungu wangu niepushie hili jambo siko radhi kufanya mapenzi na huyu msichana. sitaki kabisa kushiriki kitanda na huyu binti nisaidie Mungu wangu" hakuwa na msimamo thabiti Chriss, moyo wake ulishaingiwa na tamaa lakini pia akitaka kushindana nayo. Ni kama alichelewa kwani alisahau kuwa aiyachaye kweli huirejea. Moyo wake ulishajenga vyumba viwili tofauti vilivyokuwa vikishindana nguvu. Lakini sikuzote kweli itabaki kweli na uwongo daima hautpata nafasi ya milele katikati ya ukweli. Hadi kufikia hapo tayari ari ya Chriss kumtamani Maida ilishajidhihirisha waziwazi kilichobaki ni kujikaza kisabuni tu. Na ndiyo maana alikuwa akimuomba Mungu wake amuepushe na jambo hilo. Ukweli ni kwamba dhambi yashinda imani tepetevu na ili uishinde dhambi basi huna budi kuwa na imani thabiti. Na shetani siku zote huibomoa ngome yenye imani mbovu kwa wepesi zaidi kama kulivunja kwa ugoko bua la Uwele kama alivyofanya kwa Chriss. Shetani hakucheza mbali hapo hata mara moja na Shetani ni rahisi kumvaa mwanamke kuliko mwanaume. Maida alishapandwa na pepo la ngono bila yeye mwenyewe kujijua. Ibilisi ndiye aliyekuwa akiiongoza akili ya Maida kwa majira hayo na alishajua cha kufanya ili kuimaliza kabisa ngome mbovu ya uvumilivu kwa kijana huyo. Maida alililegeza jicho lake huku akijitafuna kucha zake za vidoleni lakini kubwa zaidi na lililomstajaabisha Chrisss, ni pale nguo ya msichana huyo ilipotoka mwilini na kudondoka sakafuni na kumuacha binti huyo akiwa mtupu wa ngozi. Macho yalimtoka Chriss na midomo kumcheza vibaya mno. Hakuamini hicho alcohol I ob mbele ya macho yake ni kweli kinamtokea au ni ndoto za asubuhi. "Ma....ma....Maida!!" aliita kwa kitetemeshi kikubwa sana. Macho yake yakakodoka ilipo sehemu adimu ya msichana huyo, funda la mate likapita kooni bila matarajio. Alipoyarudisha kifuani hapo ndipo alipokosa nguvu kabisa, sehemu zake za siri zikanyanyuka na kumpa habari kuwa zimehisi hali ya hatari na ziko tayari kwa mashambulizi hata ya kushtukiza. Moyo wa Maida ukatabasamu kwa furaha kubwa kwani alama ya ushindi ilishajichora dhahiri. "acha kushangaa wewe, ni wakati wako sasa kumuonesha kuwa hata wewe umezaliwa" sauti hiyo kutoka moyoni mwa Maida na aliisikia yeye mwenyewe tu na kujikuta akiivuta miguu yake ili kuukabidhi mwili huo kwa mwanaume wa kwanza tangu analiona jua la dunia hii. "ayasemayo Maida ni kweli tupu, kwa maisha ya jumba hili na kwa jinsi wanavyoishi ki-geti kali, ukizingatia na sifa anazopewa kuhusu mimi, ni lazima ashindwe kujizuia" aliwaza hivyo Chriss huku akimpokea m

    binti huyo mbichi kwa kumbatio mwanana.

    ..............

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    "Nilifanya nae kweli mapenzi lakini chanzo cha yote ni wewe" alisema Chriss mara baada ya kukumbuka kila kitu kilichopita na yote ambayo alifanya na Maida. Roho ilimuuma sana Salome, alihisi kama kuna kitu kinautafuna moyo wake na kuutema kwa jinsi ambavyo alikuwa akiumia. "ni kweli Chriss ninamakosa lakini siyo kwa hukumu hiyo, inamaana umeshindwa hata kujizuia my love? No, i don't belive that Chriss umenikosea sana" alilalamika sana Salome hakutegemea kutokea kwa jambo hilo kiwepesi namna hiyo. Chriss alimuangalia msichana huyo kwa kina na kisha akakifungua kinywa chake tena. "naomba unisikilize kwa umakini mkubwa we binti, ulishindwa kulifanya hili liwe siri baina yangu mimi na wewe ukaamua kumwambia kila kitu Maida. Ukitegemea kwa mtoto wa kike kama yeye angekwenda wapi kumalizia haja zake na ilhali mnajua mazingira mnayoishi ee..................!!"

    "hata kama siyo kwa namna hiyo Chriss, mimi siyo wa kuchangia penzi na Maida" Salome alimkatisha Chriss na kusema maneno hayo kwa sauti ya juu sana tena alikuwa akiongea huku machozi yakianza kujichora machoni mwake. "hujui ulisemalo na laiti ungejua, ungekwisha kuufunga mdomo wako" alisema namna hiyo Chriss na kumfanya Salome kuganda kwa muda mithili ya mtu aliyepigwa na shock ya umeme. "kivipi?" akauliza. "msinifanye mimi ni mashine yenu ya ngono. na kuanzia sasa ninavyoongea naomba usinikaribie na usahau kabisa kama ulikuwa na mimi kimapenzi"

    "eeeeenh!!?" Salome alishtuka, macho yalimtoka kama kapatwa na taarifa mbaya, ulikuwa ni mshtuko mkubwa sana na wala hakuutarajia kabisa. Chriss please he.....he.....hebu acha utani" akasema sasa akiwa makini kabisa kumsikiliza. "nimesema hivi, nisikilize kwa makini tafadhali, sihitaji mahusiano na wewe tena na si wewe tu hata huyo Maida. naona mnanichezea share, nimefunga mahusiano na nyinyi na naomba uondoke hapa mbele yangu"

    "Chriss are you........!"

    "I said i do not want, tokaa! you are so stupid, you can not make me your sex machine" alifoka Chriss akionesha dhahiri hakuhitaji tena majadiliano juu ya suala hilo. Salome aliangua kilio kizito sana, machozi yalimtiririka mashavuni mwake kama mifererji ya maji. yalikuwa ni maamuzi magumu sana alitamani kumuomba msamaha mwanaume huyo lakini tayari alishachelewa, Chriss alikwisha kuondoka eneo hilo na kumuacha mwenyewe. "i swear Maida utalipa hili, sikuachi hata kidogo lazima uniambie ulichompa huyu mwanaume. Chriss hawezi kuwa hivi lazima atakuwa amefanya hivi ili aendelee na wewe" aliwaza Salome na kujikuta akifika mbali zaidi. Hakujua nini sababu hasa ya mwanaume huyo kuwa hivyo bali fikra zake zote alizipeleka kwa Maida.



    Chriss alipotoka pale bustanini, moja kwa mja alielekea ndani. alipofika sebuleni alimkuta shangazi yake akiwa anacheza na Mery. Chriss alimtazama sana shangazi huyo jinsi alivyo na upendo mkubwa kwa watoto japo yeye hakubahatika kuwa na mtoto lakini hakuwa akiwachukia watoto. Hata Mery hakuwa mwanae wa kumzaa alikuwa ni mtoto wa mdogo wake wa kike ambaye pia alipoteza maisha yeye na mumewe kwa ajali kama walivyokufa wazazi wa Chriss na shangazi huyo kuamua kumlea mtoto huyo. "itakuwaje kama nitamuuzi shangazi, kwanini nionekane mkosaji kisa mapenzi" aliwaza Chriss akiwa hapo hapo kwenye kona iliyotenganisha chumba chake na sebule. "Salome nakuchukia, umenikosea sana kwa hili" alizidi kujisononesha kijana huyo. Donge zito likamkaa kooni na kufuatiwa na kilio cha kwikwi. Ni kweli alikuwa akimpenda sana binti huyo lakini kwa jambo hilo alikosa kabisa jinsi. alikimbilia chumbani kwake huku akiuzuia mdomo wake kwa kiganja cha mkono ili asiweze kutoa sauti. aliubamiza mlango kwa nguvu hadi anti huyo akasikia hali iliyopelekea kusitisha kidogo kwa muda mchezo aliokuwa akiucheza na Mery sebuleni hapo. alijitupa kitandani Chriss na kukiruhusu kilio hicho kilichoamsha hisia kubwa za maumivu.



    SEHEMU MOJA KATIKATI YA MJI WA MOROGORO.

    "Boss nafikiri ni muda muafaka wa kikao kama alivyoagiza Mkuu" binti mmoja mrembo, mrefu kwenda juu, asiyemwembamba wala mnene, mwenye miguu minene na pua ya kisomali na nywele nyeusi tii! Akaongezewa na weupe wa asili akiwa katika vazi ghali kabisa. alikuwa amesimama mbele ya meza kubwa ya mninga iliyokaliwa na kompyuta mpakato akimfikishia ujumbe huo mtu huyo aliyemuita boss huku akilitua faili fulani mezani hapo. Ilikuwa ni ofisi kubwa na nzuri iliyo ndani ya kampuni kubwa sana inayojihusisha na masuala ya utalii. ambayo ilikuwa imebeba jina la SAFARIES COMPANY (S.C). Ni kampuni kubwa ambayo shughuli zake tambulishi ni upokeaji na usafirishaji watalii wa ndani na wa nje kutokea hapo Morogoro mjini hadi zilipo mbuga za wanyama na vivutio mbalimbali vinavyopatikana ndani ya mkoa huo uliozunguukwa na safu ya milima ya URUGURU. "Suzane!" aliita mtu huyo anayefahamika kwa jina la Boss kasha akasema "najua unajua cha kujibu sitegemei uniangushe"

    "najua Boss toa shaka kabisa kuhusu hilo lakini hata wewe si unaweza kujibu baadhi ya mambo au ni mimi tu?" alijibu Suzane katibu muktasi wa Boss huyo na kuuliza swali. "tunategemeana" akaongea Boss, Suzane akajibu sawa na kutoka ofisini humo akimuacha Boss akijiandaa. Ulikuwa ni ukimbi mkubwa sana uliopo flow ya juu ya jingo hilo kubwa. kulikuwa na meza kubwa ya thamani sana yenye umbo la mstatili iliyokuwa imezunguukwa na watu saba waliotakata. Fedha ilijitangaza yenyewe mbele ya watu hao hakukuonekana hata mmoja aliyechoka mahala hapo. kila mmoja alikuwa na hadhi ya kuitwa Boss. kati ya viti hivyo saba vilivyopangwa kufuatana na meza hiyo ya mstatili yaani vitatu kushoto na vitatu kulia huku kimoja kikiwa kimekaa kichwani mwa meza hiyo, sita vilikuwa vimebeba watu walionyuka suti za rangi nyeusi safi lakini huyu wa saba pekee ndiye aliyekuwa tofauti. yeye alikuwa ndani ya suti ya kijivu iliyomkaa vizuri mwilini mwake. "mhg, mhg!" yule bwana aliyevaa suti ya rangi ya kijivu alijikohoza kidogo kuliweka koo lake sawa kabla ya kukifungua kikao hicho rasmi. "habariza muda huu ndugu zangu? Natumai wote mko hapa kujua nini kinachokwenda kuzungumzwa. mimi sina mengi sana ya kuzungumza ila kila kitu atatueleza Mkuu" alipokwisha kusema hayo mtu huyo ambaye alifahamika kwa jina la Boss kama mimi na wewe tunavyomfahamu, sauti ya mkoromo ikasikika kutoka kwenye spika maalumu zilizofungwa kitaalamu sana ndani ya ukumbi huo. mara zikaanza kusikika sauti za mhemo kisha sauti ya mtu anayezungumza ikarindima mahali hapo. "tuko katika hali mbaya sana kiuchumi na ninyi mnajua, kampuni inaangamia. Gharam zinazotumika ni kubwa kuliko faida inayoingia. Joesan!" sauti hiyo nzito iliunguruma kwa maelezo machache yasiyo na salamu mwisho ikalitaja jina la Joesan. "naam Mkuu!" yule mtu anayefahamika kwa jina la Boss akaitika kwa sauti ya chini kidogo lakini iliyoweza kupenya vema kwenye masikio ya Mkuu. "kampuni ikifa jua umemruhusu Iziraili andoke na uhai wako, utakufa kweli Joesan uzembe ni wako. Tunashindwa kupokea oder kubwa na za pesa nyingi za kunawirisha utajiri wetu sababu yako. SEX MACHINE alikufa kwa uzembe wako." ilisema kwa nguvu sana sauti hiyo, mtu huyo alionekana kuwa na ghadhabu kubwa huko aliko. Joesan alikuwa kimya akiisikiliza sauti hiyo kwa umakini mkubwa. Hofu ikauvaa moyo wake, afanye nini hapo. alihema kwa nguvu nyingi baada ya sauti hiyo kuweka tuo. "najua Mkuu!" akaificha hofu mbele ya watu wanaomtazama na walio chini yake kiutendaji na kujikaka mua kusema. "nini utetezi wako sasa, unaliambia nini jopo la watu wanaokutegemea hapo ulipo?" iliuliuliza sauti hiyo. Joesan alitulia kwa muda bila kutoa utetezi wowote. Ukumbi ule ulikuwa kimya sana. Wote walikuwa wakimtazama yeye. Joesan aliona kama jumba bovu linamuangukia na hakuna kizuizi chochote cha kuweza kulizuia. afanye nini sasa? Hilo likabaki kuwa swali gumu ubongoni mwake. Alichokifanya kwa wakati huo ni kuyainua macho yake na kumtazama Suzane yeye alishachanganyikiwa tayari. Hakujua nini cha kulieleza jopo hilo, alitaitika haswa. Suzane aliiona hali hiyo akajua kuwa bosi wake yupo katika hali mbaya mno, akawatazama wote waliopo mbele yake kasha kushotoni kwake, akashusha pumzi ndefu iliyowafanya watu wote pale kugeuka na kumtazama. Mtoto wa kike huyo akabeba ujasiri na kusema. "tupe siku tatu mkuu naa.............!" akakwama na kumgeukia bosi wake aliyepatwa na mshtuko wa waziwazi kabisa kasha akamalizia "nadhani tutalishughulikia hilo na kabla ya siku ya nne Sex machine atakuwa mbele yako" akaweka tuo. Miguno ikasikika mule ndani kasha ukimya tena. Sauti ya Mkuu ikarindima. "mmejifunga wenyewe that is bracket mkienda kinyume mnajua nini kitawakuta. Nimefunga mjadala na nyinyi sasa nageukia kwako Mahmood. Vipi Mahmood, hujaniambia chochote kuhusu mamilioni ya pesa yaliyopotea mikononi mwako kwa uzembe tu?" watu wote sita pale mezani wakageuka na kumtazama mtu huyo mwenye asili ya kiarabu. Mahmood hakujibu kitu alibaki kimya tu "unachochote cha kuniambia sasa?" Mahmood alishtuka baada ya sauti hiyo kumgutusha. "Mkuu nimejitahidi sana lakini sijafanikiwa kuwapata wale wavamizi walioondoka na ile pesa"

    "kwa hiyo?" akapokea swali jingine. "nisamehe mkuu ni makosa yangu" akajitetea. "ha ha ha haaa!" cheko zito la fedha likatikisa ukumbi huo, Mahmood akashtuka na wote mule ndani wakajua nini kitakachokwenda kumkuta Mahmood muda mchache ujao. Kicheko cha mtu huyo wanaemuita mkuu, siku zote walikitafsiri ni kama hasira zake na ndivyo hivyo. Mara nyingi linapoibuka jambo la kumchukiza yeye hucheka tu lakini madhara yake huwa ni makubwa. Hivyo walijua dhahiri nini kinachokwenda kujiri mahali hapo. "Mahmood, kirahisi rahisi tu kama unamuomba mkeo unyumba. Bloodl foolish" ikasema sauti hiyo na mara hiyohiyo ghafla, sauti ndogo ya maumivu ikasikika. watu hao walipogeuka na kumuangalia Mahmood, walimuona akiwa ameegamia kiti chake akiwa na alama ya nyota kwenye paji la uso. Halikuwa jambo la kushangaza na hali hiyo walisha izoea. "milioni mia moja na hamsini halafu unasema nikusamehe. Nani kasema kuwa ninasamehe kipumbavu kwenye pesa. Amenitia hasara sana huyo shoga, mzigo amekosa .............................



    na pesa zimekwenda mbaya zaidi amesababisha vifo vya vijana wangu wawili. Hivi mnajua hii kazi ni ya kuchambua mchicha eenh! Inabidi muwe ngangari kwenye kampuni hii na sitawavumilia watu wazembe tena. Mtakufa." ikamaliza sauti hiyo kisha mkoromo wa spika ukafuatia na kufuatiwa na ukimya kuashiria kuwa mkuu huyo alishakata mawasiliano. minong'ono midogo midogo ikaibuka mahali hapo huku vijana maalumu wakihangaika na kuutoa mwili wa Mahmood eneo hilo. Joesan na Suzane wakaondoka na kuwaacha wazee hao wakizidi king'atana masikio. "kwanini huyu binti anajipendekeza sana kwa Joesan?" aliuliza mzee mmoja wakiwa wawili baada ya kutoka kwenye ule ukumbi wa mikutano. "Mgobo, Suzane ni lazima ampigie kifua Joesan, kwani yule ni bosi wake na anafanya kazi chini yake tukiachilia mbali ukaribu walionao" akazungumza mzee wa pili. "naona kama anajipalia makaa mwenyewe, Mkuu si mtu mzuri kabisa ujue?"

    "haijalishi mgobo na hiyo ni juu yao tunachotakiwa sisi ni kuomba hiyo mashine ya ngono ipatikane bila hivyo ajira zetu zipo mashakani maana kampuni yetu ipo katika hatua mbaya sana, sasa hii ni hatari mno"

    "haya ndiyo matatizo ya kuongozwa na kijana mdogo lazima aende kinyume tu" walizidi kunong'ona wazee hao kasha kila mmoja akapita njia yake na kuelekea kunako mhusu. Joesan baada ya kuingia ofisini kwake akiwa na Suzane, alijitupa kitini mwake na mwanadada huyo naye akajitwalia nafasi yake. Joesan akafikiri kwa muda kisha akavuta pumzi nyingi ndani ya mapafu yake na kuziachia kwa mkupuo, akasema. "umefanya nini sasa Suzane, kile ulichokisema pale kumbe ndicho ulichokuwa umekipanga?"

    "ulitaka nisemeje Boss, tulikuwa hatuna utetezi mwingine pale na niliona kuwa hukuwa na njia nyingine Boss. unafikiri ningetoa wazo gani ambalo Mkuu angeliafiki. wewe mwenyewe nadhani umeona kilichomtokea yule mwarabu. Hakukuwa na cha kujibu Boss." alisema Suzane. Joesan alpingana na maneno ya mwana dada huyo hakumuelewa hata kidogo. Suzane kutoa odder kuwa Sex Machine atapatikana ndani ya siku tatu, hilo lilikuwa ni jambo gumu kabisa na alishindwa kuelewa mategemeo mazima ya mwanadada huyo. "pamoja na hayo lakini si kwa jibu lile, pale tumeshajitia kitanzi wenyewe Suzane. Ok, haya tunafanyaje sasa maana hata sielewi." akalalamika Joesan. Alichanganyikiwa haswa. "sikiliza Joesan" alizungumza binti huyo na kumtazama bosi wake usoni, akaendelea. "kwa sasa hauko sawa Boss hata kama tutaongea, hatutafikia muafaka mzuri, chakufanya mimi nitakuja nyumbani kwako jioni na ni lazima hili tulipatie ufumbuzi kabla ya siku ya kesho. Tutaongea kwa utulivu mkubwa"

    "kabla ya kesho!?" Joesan akahoji kwa mshangao. "ndiyo, ukumbuke ni kama tumesaliwa na siku mbili pekee?"

    "najua lakini nashangaa wewe kusema kabla ya kesho tuwe tumepata ufumbuzi wa hili. Unajua unanichanganya sana Suzane, kwani unampango gani wewe mwanamke?" akahoji tena Joesan bado alikuwa katika mkanganyiko mkubwa wa mambo na hakumuelewa huyo binti kabisa. "acha papara Boss najua nini tutafanya" akajibu. Joesan aliurudisha mgongo wake nyuma ya kiti na kuegamia. akapiga kite cha hasira na uchovu kasha akavuta faili fulani pale mezani akachukua na kalamu na kukaa katika mkao wa kutaka kuandika jambo lakini hakuandika chochote, akaishia kuizunguusha ile kalamu vidoleni mwake na kuirudisha kwenye kopo maalumu lililojaa kalamu za rangi mbalimbali akalifunga lile faili. akatafakari hili na lile kwa haraka haraka mara mlio wa simu ukamshtua. akaipokea na kuiweka sikioni. "nimemaliza mihangaiko sasa nafikiri leo ni nafasi nzuri ya mimi na wewe kukutana, nipo Morogoro Hoteli." ilisema sauti hiyo kutoka upande wa pili wa simu hiyo. "ok, kaka nakuwa hapo sasa hivi" akaikata na kuitia kwenye mfuko wa koti lake na kusimama. alilinyakuwa faili fulani akalifukia kwenye mtoto wa meza kisha akamgeukia Suzane. "naomba umalize kila kitu kinachonihusu mimi kikazi, ikiwa kuna mtu atanihitaji utamwambia anitafute kwenye namba yangu binafsi. Natoka kidogo na sitarudi tena, tutaonana jioni mimi na wewe" Suzane akajibu sawa. bwana huyo akatoka hadi ilipo Toyota prado nyeusi, akapakia garini humo na kuondoka. Alifika Morogoro hoteli akapitiliza ndani kabisa ya hoteli hiyo kubwa mjini hapo. Alifika hadi mahali alipoelekezwa na kumkuta mwenyeji wake akiwa katulia kitini akipata kinywaji ghali kabisa. Mbele yake kukiwa na kiti kimoja ambacho ndicho alichokitwaa Joesan

    "habari za masiku tele bwana Babu Ally?" ndivyo walivyoanza maongezi yao namna hiyo. "nzuri tu ndugu yangu, ni siku nyingi kweli maana ni muda mrefu hatujaonana. vipi yule kijana wako ni mkubwa sana sasa hivi?"

    "aah! Unamzungumzia Chriss?"

    "haswaa huyohuyo"

    "ni mkubwa sasa hata masomo amemaliza, yupo nyumbani kwa sasa" alisema Joesan. "ndiyo, vipi wife naye anaendeleaje" aliuliza Babu Ally na Joesan akajibu "my wife keeps well na ni wa afya tele kabisa shida hakuna." wakati wakiwa wanaendelea na salamu za kawaida, muhudumu akafika mahali hapo na kuchukua oda na kuondoka akiwaacha mabwana hao wakiendelea kupepeta domo. "nimetoka ughaibuni juzi na huu ni mguu wako bwana Joesan maana huu ndiyo ule muda tulioupanga wa mimi na wewe kukutana. Unajua ni muda sasa tangu biashara yetu isimame, naona tuna kila sababu sasa ya kuirudisha tena au unasemaje Joesan?" akaacha swali Babu Ally. Wakati Joesan akiwa anafikiria kulijibu akaongeza "hatukuwa na mawasiliano mazuri hapa katikati kiasi kwamba hatukuweza kuzungumzia mustakabali mzima wa biashara zetu. Tutazifanya kwa namna gani Joesan nadhani unajua kuwa utajiri wetu unategemea hizi biashara kwa asilimia kubwa?"

    "Babu Ally kakaa, najua sana hilo na hivi unavyoniona siko sawa ndugu yangu. huko ofisini ni moto" akanyamaza kidogo, akameza mate na kuendelea "Mkuu amenijia juu vibaya sana. Si unajua yule Sex Machine alikufa katika harakati za kuupigania mzigo wetu huko Australia?" aliuliza Joesan. "ndiyo" Babu Ally" akajibu. "sasa nimepewa siku tatu tu za kumrejesha Sex Machine ndani ya kampuni."CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "come on Joesan! Wewe!!?" alishtuka Babu Ally na kusema "sasa wewe utampatia wapi huyo Sex Machine ndugu yangu lakini kwanini ameamua kukufanyia hivyo sasa?"

    "hapa ninapozungumza haya hata sielewi ndugu yangu lakini Mkuu hana kosa kwa hili, kwasababu hata yeye anachong'ang'ania ni kwamba Sex Machine alikufa nje ya kazi za kampuni naa.........!"

    "hebu ngoja kidogo muhudumu analeta chakula" Babu Ally akamkatisha na kuifanya sentensi yake kuelea hewani. Chakula kikawekwa mezani kila mmoja akijiweka mkao wa kula huku wakiendelea na maongezi yao. "na isingekuwa urafiki wetu kati yangu na Mkuu..........!"

    "wee! Angekwisha kukuuwa zamani aisee." alidakia Babu Ally. "sasa tunafanyaje maana tunataka kuifanya hii biashara kitaalamu zaidi. nimetafuta watu wa kuwatumia lakini sioni kama watafiti kwemye hili" aliongeza Babu Ally. "achana na hao watu kwanza na naomba huu mjadala tuufunge, acha mimi nikatafakari kwa kina nyumbani kesho nitakuwa na jibu zuri la kukupa. kwasasa ni uwongo nimechanganyikiwa sana acha niende nyumbani nikapumzike." alizungumza Joesan. "vpi chakula naona umegusa tu kaka"

    "utanisamehe kaka sioni kama hicho chakula kina ladha wacha niende nyumbani nikajipe muda mwingi wa kufikiria na nijue nini cha kufanya" akasema akaondoka. Babu Ally alitikisa kichwa kwa masikitiko makubwa. Alimhurumia sana jamaa yake huyo lakini hakuwa na jinsi ya kufanya na aliogopa sana kujihusisha na hilo jambo japo kwa namna moja au nyingine, upotevu wa Sex Machine unamhusu na wote walishiriki. Shughuli ya huyo mtu anayejiita mkuu alijua vilivyo. "utanisamehe Joesan kwa hili, bado napenda kuishi" ndivyo alivyokuwa akiwaza Babu Ally. Joesan alitoka hadi nje ya ile hoteli na kujiingiza garini mwake, alifunga mlango wa gari vizuri pamoja na kuufunga mkanda kasha akajilaza kwenye kiti hicho cha dereva akiweka hili na kupangua lile kabla ya kulirudisha hili. Baada ya muda kidogo alinyanyuka na kuwasha gari yake hiyo, ila kabla ya kuliondoa, aliwasha redio na kuutafuta wimbo wa mwanamama Celine Dion. wimbo unaokwenda kwa jina la 'That the way It is'. ambao aliamini kidogo unaweza kuyapeperusha mawazo yake kwa muda huo.

    "When you want it the most,

    there's no easy way out,

    when your heart's left in doubt" ndivyo alivyokuwa akiufuatisha wimbo huo huku akitngisha kichwa kidogo kidogo. Wimbo huo ulimfanya ayasahau mawazo lukuki yaliyokuwa kichwani mwake.

    "When you question me for a simple answer,

    i don't know what to say,

    no but it's plain to see,

    if we stick together. Your gonna find the way yeah"

    Kwakweli wimbo huo ulimpeleka mbali kihisia, ulimfariji kwa kiasi fulani hadi nyumbani kwake akapaona karibu sana. alifika nyumbani kwake bila matarajio. Aliibonyeza kitufe fulani kwenye rimot na lango kubwa la jingo hilo likafunguka. lilikuwa ni jingo kubwa na la thamani kweli ambalo limejengwa kisasa kabisa.



    Joesan ndiye aliyekuwa mjomba wa Chriss na alikuwa ni mtu mwenye utajiri mkubwa sana mjini hapo. Alikuwa akimiliki majumba kadhaa mjini na biashara kubwa mno. Hakuna asiyemjua Joesan, alifahamika kila kona na alikuwa ni mtu mwenye kumsadia kila anayehitaji msaada. Hilo likapelekea jina lake kukuwa siku hadi siku. Alimiliki mwili mkubwa uliobeba kitambi cha wastani na kifua kipana. Huyu ndiye hasa aliyeyafikisha maisha ya Chriss hadi kufikia hapo alipo na alikuwa akimpenda kijana huyo kupita kiasi. Yeye ndiye aliyebeba historia nzima ya maisha ya kijana huyo. Aliufunga mlango wa gari vizuri na kupiga hatua ndogo ndogo kuelekea ndani ya jumba hilo na lenye thamani ya juu mno waswahili wenyewe huita Villa. Aliingia ndani na kumkuta mkewe akiwa sebuleni na Mery wakiwa wako bussy na Tv wakifuatilia filamu ya kibongo. Mery aliruka kutoka mahali alipokaa na kumrukia Joesan. "Ankoo huyoo! Shikamoo Anko?" alisalimia Mery akiwa yupo mikononi mwa anko wake akining'inia baada ya anko wake huyo kumnyakuwa na kumbeba. "marahaba anko hujambo?".............



    "sijambo anko"

    "ok, vizuri, haya endelea kuangalia muvi sawa anko?" Joesan alimwambia mtoto huyo huku akimshusha binti huyo mdogo. Akamgeukia mkewe. "vipi mmeshinda salama?"

    "ndiyo ni salama tu sijui wewe huko kazini?" akarudisha salamu anti martha. kazini si kubaya sana ila bado hakujatulia, vipi mbona mko wenyewe wengine wako wapi namaanisha Chriss maana hao mabinti si sana kukaa hapa muda huu?" akauliza Joesan baada ya kujuzana hali na mkewe. "tokea alivyotoka bustanini kufanya usafi, ameishia kujifungia tu huko chumbani kwake sasa sijajua ni kipi kilichomsibu au labda atakuwa amelala"

    "siyo Chriss!" alidakia Joesan. "sasa anafanyaje maana ni muda sana eti" alisema tena anti Martha. "hebu ngoja nikamuangalie chumbani kwake" akaongea Joesan na kuelekea kilipo chumba cha Chriss lakini kabla hajakigusa kitasa cha mlango, akasikia kelele za majibizano kutokea upande wa jikoni. zilikuwa ni kelele haswa. "mh! Kuna nini tena mbona kelele hivi" alijiuliza Joesan. "hebu ngoja" akajishauri na kuacha zoezi la kufungua mlango wa chumba cha Chriss na kuelekea zinapotokea sauti hizo. "nimekwambiaje, kuanzia sasa basi kama hujui ndiyo ujue upo hapo bibi wewe. Chriss yuko hapa tenaa! Nilikuwa sijajua raha unazozipata kutoka kwa mwanaume yule. Sasa kwa taarifa yako ameshaukubali mziki wangu. Halafu sijakuambia eenh! Anasema hivi, hawezi kuendelea na wewe aliyekukuta umesha haribiwa njia, mtoto kanikuta sild upo hapo?" yalikuwa ni maneno ya maida akimtambia Salome. yalikuwa ni maneno yenye kuudhi sana, kama ni vijembe basi hivyo vilikuwa ni vijembe haswa. Salome alikuwa kafura kwa hasira vibaya sana hapo sasa aliamini kweli hana chake kwa Chriss. "sijui hata nikufanye nini wewe malaya nakuchukia sana Maida, sikutegemea kama ungekuja kunigeuka namna hii Hivi...........!"

    "tee!" Maida alimkatisha Salome "mimi na wewe malaya nani? Nakuuliza hivi, mimi na wewe malaya ni nani? Malaya ni wewe uliyeliwa mtaani. mimi Chriss amenikuta mzima na bikira yangu, wewe je? Na kwa taarifa yako bibi wewe, Chriss akiwa na hamu tu hapa" Maida akakipigapiga kifua chake kuashiria kuwa Chriss ndipo anapolala. Akaendelea kutema shombo mtoto huyo. "na simuachi mwanaume yule hata ukaroge. Mwanaume dakika arobaini na zaidi hatoki kifuani utadhani katokea milimani au kala miti shamba!" alikuwa akitamba kweli kwa maneno mtoto huyo. Salome hakutia neno hata moja na si kama hakupenda kusema bali hakujua ni neno gani linafaa kumwambia Maida hadi limuingie. kwa hapo ni wazi Salome alikiri kuwa amepatikana. Ni kweli Maida ana haki ya kujitapa maana tayari Chriss alishauonja utamu wake. Tangu siku hiyo ya kwanza tangu alipomruhusu mwanaume huyo auchungulie mwili wake na kula vile vilivyofichwa, ambapo ilikuwa ni kama wiki mbili zilizopita. Salome hakuonekana tena kumfuata Maida nyakati za usiku na kwenda kumtambia hali hiyo ikajenga maswali mengi sana kichwani mwa msichana huyo. "Salome amekuwa kimya sana siku hizi, simuoni tena akija kunipa sifa za Chriss sijui ni kwa sababu gani?" ndivyo alivyokuwa akijiuliza siku moja Maida. "au hakuna mitindo mipya siku hizi au amekuwa nini?" alijiuliza tena namna hiyo na kuachia tabasamu pana. Si kwamba alisema hivyo kwa kujua laa hasha! Ila kuna jambo alihisi. Huwenda labda mwenzake hapati nafasi kwa sababu muda wote yeye ndiyo yuko na mwanaume huyo. Salome aliuvunja kabisa utaratibu wake wa kwenda chumbani kwa Maida kila anapotoka kushuhulika na mwanaume huyo. Hali hii ndiyo iliyompa Maida nafasi kubwa ya kujiona yeye ni bora kuliko mwenzake. Kile kitendo cha kuja chumbani kwa Maida na kujitupa kitandani kujifanya amechoka kwa kusulubishwa na mwanaume huyo, ziliyeyuka kama Ubuge kwenye upepo wa kisulisuli. Maida hakutaka kujiaminisha moja kwa moja kisa tu kutomuona Salome chumbani kwake bali aliamua kwenda kumuuliza Chriss kabisa juu ya jambo hilo. Ndipo Chriss alipomwambia kwamba havutiwi na Salome hata kidogo kwanza alimkuta mweupe hana bikira hivyo mara nyingi amekuwa akimtolea mbavuni kila anapohitaji kukutana nae kimwili. Maida kwa kiburi akamfuata Salome usiku huo huo na kwenda kumuuliza sababu za kutomtambia usiku kila akitoka kufanya mapenzi na ni nini. Salome naye bila kufikiria akamueleza kila kitu akidhani anatengeneza au Maida angekwenda kumpigia kifua kumbe ndiyo alikuwa akizidi kumpa kichwa mwanadada huyo. Hapo kibao kikamgeukia. Maida akamwambia Salome waziwazi kuwa asijisumbue kwani kwa muda huo hakuwa na jipya tena mbele ya Chriss. Ameshamkamata na asitegemee kupata penzi la mwanaume huyo mwenye utamu wa aina yake, kisha akatoka chumbani humo na kumuacha mwenzake akiwa na maswali mengi ya kujiuliza. Na jambo hilo ndilo lililompa Salome msukumo mkubwa wa kumfuata Chriss kule bustanini alikokuwa akifanya usafi na kumuuliza. Malumbano yote hayo yaliyokuwa yakiendelea, yalikuwa yakisikiwa na kuonwa moja kwa moja na Joesan. Hakutia neno lolote alikaa mahali hapo akifuatilia majibizano hayo mwanzo mwisho hadi pale alipoona mabinti hao wanataka kupigana ndipo akajikohoza na kuwafafanya washtuke na kila mmoja kujifanya kama siyo yeye aliyekuwa akijibizana na mwenzake mahali hapo. Joesan alikunja sura na kuwatazama mabinti wale kwa muda na kuwasontea kidole. " hili siyo danguro sitaki hizo kelele zenu na nikizisikia tena mtanieleza vizuri. Sitaki kusikia huo ujinga wenu tena sawa" Joesan aliwagombeza sana mabinti wale hadi wakaogopa na kuwa wadogo. Haikuwahi kutokea hata siku moja kwa bosi wao kuwa mkali kiasi hicho. Joesan aliondoka hapo akiwa ameghadhibika sana alielekea chumbani kwake akiwa na lengo la kwenda kujipumzisha. Alijitupa kitandani na kujilaza chali, alitulia kitandani hapo kwa muda kidogo akitafakari hili na lile, lile na hili. "hawa mabinti siwaelewi kabisa, kwanini hawaiheshimu nyumba hii, kwanini wanaifanya nyumba hii ni sehemu ya majibizano ya kijnga jinga, wangejua nilivyo vurugwa wala wasingeleta uwenda wazimu wao. Hii hali ni mpya sana na haijawahi kutokea" aliwaza joesan akiwa kitandani hapo amejilaza kiwiliwili lakini upande wa miguu wote ukiwa nje ya kitanda. "Chriss amefikia hatua hii ya kugombaniwa (akacheka kidogo) ameitoa wapi hii tabia ya kutembea na wanawake wawili kwa wakati mmoja tena wakiwa ndani ya nyumba moja. Hayajui mapenzi huyu kijana, hajui mapenzi yanauwa, yameuwa, yalishauwa na yanaendelea kuuwa. Hajui kuwa mapenzi ni hatari sana. Hapana lazima nimuweke chini niseme nae hii ni hatari sana na inaweza kuleta balaa" Joesan alizidi kumfikiria kijana wake na kwa muda huo alisahau kabisa kwenda kumgongea kijana huyo chumbani kwake ili kuweza kujua nini sababu za kujifungia hadi majira hayo ya jioni ilhali si kawaida yake. "amekuwa hodari sana huyu kijana, dakika arobaini na tano mtu bado yuko maungoni mwa mtu" aliongea Joesan baada ya kukumbuka maneno ya Maida kuwa hawezi kumuacha Chriss kwasababu anajua kumfikisha safari zake ipasavyo na huwa anatumia muda mrefu sana awapo kifuani kwake. "Chriss!" aliita Joesan kwa sauti ya chini na kukumbuka kauli ya mkuu wake. "mmejifungia wenyewe, that is bracket"

    "huwenda Chriss............ooh! no, siwezi kufanya hivi. Kwanini sasa nawaza ujinga namna hii, hapana, hapana, hapanaaaa!" alipiga kelele kubwa sana. hakutaka wazo la kumfanya Chriss kuwa Sex Machine limkae kichwani mwake. lilikuwa ni wazo baya sana. kwnini wazo hilo lilimjia Joesan, huwenda labda ni sababu ya kuchanganyikiwa na hakujua ni wapi atampata huyo Sex Machine. Lakini pamoja na hayo, wazo hilo alipingana nalo kwa kiasi kikubwa sana. alipinga na hakutaka limzoee kabisa. Chumba hicho akakiona kama kinamshangaa kwa wazo la kipumbavu lililotaka kumjia. Hakupenda kuwepo hapo tena. Kila alichokitazama chumbani mule alikionea haya. Alinyanyuka Joesan na kutoka mule ndani ikiwa sasa imetimu saa 05:30 za jioni. Alikwenda hadi bustanini na kujituliza pembezoni kabisa mwa bwawa la kuogelea. "ninamuda mrefu sana sijafika mahala hapa, kazi hizi zinanifanya kuwa bussy kila wakati" akawaza. "leo imenilazimu kufika hapa bila kutarajia mawazo yamenizidi sana sielewi nifanye nini mimi" aliwaza tena bwana huyo. Baada ya muda akahisi mikono laini ikimkumbatia kutokea nyuma na kukipapasa kifua chake kilichochanika kutokana na mazoezi mazito. "mume wangu leo ni maajabu sana kufika mahali hapa, si kawaida yako maana hata chakula umegoma kula leo, nini kimekupata my dear?" sauti mwororo ya Martha ikasikika kutokea nyuma ikimuuliza kwa utaratibu mkubwa. "hapana mke wangu ni u bussy tu wakazi hakuna kitu kingine" akazungumza Joesan. Martha alizunguuka kwa mbele na kumtazama vizuri mumewe huyo na kumuuliza "mbona kama kuna kitu unanificha honey, hata kukataa kula chakula changu leo ni ubize wa kazi?"

    "mmh! Hapana mke wangu, unajua nilipata ofa leo. Rafiki yangu kutoka Marekani alinipigia simu leo wakati nipo kazini, akaniomba tukutane maeneo fukani hivi so nimekula vizuri tu na nimeshiba sana, usijali mke wangu pika chakula kizuri cha usiku na tutakula wote leo" akasema kwa utulivu Joesan huku akizichezea nywele za mke wake na kuyashikashika mashavu yake laini. Martha aliripuka kwa furaha baada ya mume wake kumwambia jambo hilo. alimisi sana kula pamoja na mumewe. " waaooh! Nitafurahi sana kula pamoja leo mume wangu, nimemiss sana chakula cha pamoja"

    "punguza ubize sweetie jamani unakuwaje hivyo hadi naumiss uwepo wako" alizidi kulalama Martha. "ni kazi mke wangu ndiyo inaniweka hivyo lakini hata mimi ninamiss sana uwepo wako karibu yangu, kiukweli nakosa tu jinsi lakini sina amani kabisa" akasema Joesan. "nakupenda sana honey wangu"

    "nakupenda zaidi ya unavyonipenda marth.......!"

    "wapenda nao hao naona mpo kwenye ubora wenu?" sauti hiyo ikawashtua na kuwatoa kwenye maongezi yao. "ooh! karibu sana Suzane" akakaribisha Joesan. "haa! Jamani Suzane, vibaya hivyo ukipotea ndiyo jiii! Unapotea kabisa jamani!" alisema Martha huku akimgeukia Suzane, alimlaumu sana, akaendelea "inamaana bosi wako asipokuwepo nyumbani na wewe huonekani, leo yupo basi na wewe unaonekana vibaya hivyo ujue"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "unanilaumu bure tu shosti ni kweli nastahili lawama hizo lakini kiukweli kazi zinabana sana muda wa kuwa free ni mdogo sana kiasi kwamba tunashindwa kuonana" alisema Suzane "muulize mumeo, unafikiri ataniruhusu niondoke kazini ndani ya muda wa kazi?"

    "mmh! Muda mwingine uwe unamtoroka tu huyu kwani atakufanya nini" alisema Martha. "humjui Joesan akiwa kazini wewe, muone hukuhuku akicheka tu. Akiwa ofisini ni Simba huyu hataki utani hata kidogo" alisema Suzane. wakazidi kiongea mengi sana na utani wa hapa na pale. Mwishowe Joesan akamuomba mkewe awapishe kidogo kwani kulikuwa na mambo muhimu walitaka kuyajadili. Anti Martha hakuwa na ajizi ikibidi awapishe ili waweze kujadili mambo yao ya kiofisi kwa uhuru zaidi. Joesan ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuanzisha maongezi. "twende kwenye poit Suzane muda umekwnda sana. Unajua kuwa nakusikiliza wewe mimi hata sielewi nifanye nini nimechanganyikiwa kabisa" aliongea Joesan. Lakini muda wote huo wakati Joesan anaongea maneno hayo, Suzane alikuwa ameyaelekeza macho yake lilipo bwawa la kuogelea hali iliyomfanya Joesan naye kuyageuzia macho yake huko ambako mwanadada huyo alionekana kuduwaa. Joesan alichanua tabasamu baada ya kumuona kijana wake akiwa amesimama upande wa kaskazini mwa bustani ile. Palikuwa si mbali sana aliposimama Chriss na wao walipo ika kijana huyo hakujua kama mjoba wake yupo mahali hapo. "ile ndiyo iliyokuwa target yangu" alijisemea moyoni Suzane huku akitabasamu usoni. "Joesan!" aliita Suzane baada ya kujiridhisha na kile alichokiona mahalo hapo. Joesan akaitikia kwa kichwa na kumuonesha ishara kuwa anamsikiliza. Suzane akafungua kinywa chake tena na kusema. "nadhani hakuna ugumu katika hili, lisikufanye ukose raha na kushindwa kufanya maamuzi yaliyo sahihi." Joesan akashtuka. Hakumuelewa huyo binti hata kidogo. Jambo hilo siyo zito? Kivipi? Anawaza kufanya nini Suzane mbona kama anashindwa kuelewa. Alijiuliza sana Joesan lakini hakupata majibu ya uhakika ikabidi amtazame kwa kumshangaa maana hata sauti hakuamini kama ingetoka kwa ufasaha kwa jinsi sintofahamu ilivyompata ghafla. Suzane alitabasamu na kuyageza macho yake kule alikosimama Chriss kabla ya kuyarejesha kwa bosi wake na kunena. "amekuwa kijana mzuri sana Chriss, hongera sana Joesan kwa kumpa malezi bora kijana wako" Joesan akajitahidi kulilazimisha tabasamu, akafanikiwa lakini bado hakumuelewa kabisa binti huyo. "ooh! Yaa, ni jambo la kumshukuru Mungu sana, sasa ni kijana mkubwa" Joesan alizungumza huku akimuangalia tena Chriss na kuyarejesha macho yake kwa Suzane ambaye bado alikuwa ameliachia tabasamu. alizidishatabasamu kabisa na kuifanya sura yake ya urembo kuzidi kuwaka. "Chriss should be on our program Joesan, amenivutia sana" alisema Suzane huku akiwa ameyakaza macho yake kutazama kule alipo kijana huyo. mshtuko mkubwa ukamkumba Joesan, hakutegemea kupokea kauli hiyo kutoka katika kinywa cha katibu muktasi wake. Alimtazama Suzane kwa mshtuko mkubwa sana. "sijakuelewa Suzane, Chriss anafaa vipi kuwa kwnye mpango wetu?" alizungumza Joesan. Suzane alimtazma bosi wake usoni kwa muda kodogo na kumuambia. "ondoa waswasi Boss, akatulia kidogo na kuendelea " maana yangu ni kwamba ni lazima Chriss awe SEX MACHINE"

    "eti, nini!!?" alishtuka tena kwa kiasi kikubwa sana Joesan, hilo jambo si kama hakukitegemea tu pekee bali pia lilikuwa haliwezekani kabisa. "Joesan nadhani umenisikia kwa dhati kabisa niliyoyasem........!"

    "hapana Suzane, hilo haliwezekani. Kama hiyo ndiyo ilikuwa plani yako, haiwezekani hata mara moja Chriss is my boy tutafute mtu mwingine" alilalamika Joesan tena alikuwa akiongea kwa sauti kubwa sana. Alidata kabisa bwana huyo. "kwanini nimuingize Chriss kwenye huu mchezo mchafu, mchezo wa kifo, mchezo ambao sikupanga hata siku moja kuja kumhusisha huyu kijana. Ni kweli nili.........!" alitaka kuongea jambo fulani Joesan akasita. Kwanini alisita baada ya kutaka tu kulitamka jambo hilo? Na ni jambo gani basi? Yote hayo yalikuwa ni maswali ya kujiuliza. Majibizano yale yaliendelea kila mmojaakitaka lake. huyu alisema hivi na huyu alisema hapana na haiwezekani nani ni nani, hakukuwepo na alitaka kushidwa. Joesan alilipinga kabisa jambo hilo. Suzane akaona kuwa hakuna .................





    hakuna sababu ya kuendelea kulumbana kwa jambo ambalo amelibeba kama msaada tu hivyo akaamu kujishusha. "ok, sina njia Boss na najitoa katika jambo hilo mimi sitahusika tena. Niliubeba mzigo wako na kutoa siku tatu tu kwa Mkuu kwa kujua unae Chriss ambaye ni msomi mkubwa na anauwezo wa kufiti vizuri kabisa kwenye hiyo nafasi ya Sex Machine, aliyekufa kwa kazi zenu binafsi. Naomba unisamehe Boss kwa kukushauri vitu vya kijinga" aliongea Suzane na kuangalia pembeni kabisa. Joesan akapigwa na butwaa jingine la ghafla. Ni kweli alikuwa hapendi Chriss aingie kwenye huo mchezo lakini kwa hilo alilolizungumza Suzane hapo ni kwa namna gani atalikabili. "Suzane ni mtu ninayemtegemea sana, sasa vipi kama akiacha kunisaidia" aliwaza Joesan kisha akasema. "hapana Suzane, huu mchezo hauhitaji hasira, kwanini unafanya maamuzi magumu hivyo nadhani unajua ni kwa jinsi gani ninavyo kutegemea" Suzane akageuka na kumtazama bosi wake huyo usoni na kumwambia "hakuna njia ya kupita Joesan zaidi ya hiyo, unadhani tutafanya chaguo gani zaidi ya hilo?" Joesan alishusha pumzi nzito sana. "hapo najua hawezi kupindua, hana chaguo jingine Joesan zaidi ya kijana wake labda kama atafeli jaribio lakini kama atashinda, Chriss anafaa sana, rangi yake, kifua chake kipana na mwili wake kwa ujumla vimenivutia sana hata mimi namtamani." aliwaza Suzane. Joesan hakuwa na la kufanya alijikuta mpole ghafla. Jibu alilo bakiza ni moja tu na hilo ndilo ambalo lilikuwa likisubiriwa na huyo msichana. "unadhani tutaweza kumshawishi vipi hadi kuingia kwenye hii kazi?" aliuliza Joesan. "Joesan! Usitake kuniambia hujui. Yule ni kijana wako na anakusikiliza sana acha huko kukuheshimu, sidhani kama ukimwambia kuwa unajambo la msingi unataka kumueleza, anaweza kukukatalia. Hakikisha unaongea naye mambo mazuri na kila ulichomuahidi sasa kinakwenda kutimia na wewe mwenyewe unajua Joesan kuwa anaiingizia kampumini mamilioni ya mapesa lakini hata yeye ataingiza pesa nyingi zitakazo badilisha maisha yake kwa kazi hiyo."

    "ndiyo najua" akadakia Joesan na kisha mwanadada huyo akaendelea. "sasa, anakwenda kuwa milionea. Hakuna mtu anayekataa pesa lazima ukimueleza hili atakubali hawezi kukataa hata kidogo"

    "lakini sina hakika kama Chriss anaweza kukubali kirahisi, huyu ni kijana mbishi sana kuelewa" akasema Joesan. "Joesaan!" aliita binti huyo na kuendelea "si wewe wala mimi atakayembadilisha Criss. Chriss atbadilishwa na Sex Machine Controller (SMC). Hii ndiyo itakayobadilisha maisha yake na akiwa mbishi tutajua njia nyingine ya kufanya hatujawahi kushindwa na binadamu wa kawaida hata siku moja we mwenyewe unajua" aliongea kwa kiburi sana. "ooh! Yeah, nilitaka kusahau jambo hilo. Hapo sawa sina kipingamizi tena" akasema Joesan. "nashukuru sana Boss kama tumeweza kufikia muafaka. Suala lilikuwa dogo sana ulitaka kulifanya kubwa bure tu" aliongea binti huyo na kumalizia kabla ya kuondoka. "jaribio la kwanza ni leo, naomba umtume nyumbani kwangu kwa njia yoyote ile ifikapo saa mbili usiku. Kifua chake kimenivutia sana sasa nataka kuiona shughuli yake awapo kitandani na mzigo alionao si unajua tunatafuta watu walio kamilika kila idara" kasha akaondoka mahali hapo mara baada ya kusema maneno hayo na kumuacha Joesan mdomo wazi. huyu mtoto si dhani kama atakuwa yuko sawa" aliesema bwana huyo huku akicheka cheko la ndani kwa ndani. Aliondoka kwa mwendo wa Twiga binti huyo, umbo lake jembamba lililojigawa chini kuanzia kiunoni kwenda chini na kumfanya kuonekana mrembo zaidi. Alikuwa akilitingisha umbo hilo kutokana na mwendo wake wa kimiss lakini macho yake hayakuacha kumtazama Chriss. Hata alivyokuwa amemkaribia bado alikuwa akimtazama kwa matamanio makubwa sana. Na kutokana na kijana huyo kuwa amemezama ndani ya jinamizi la mawazo, basi ndiyo kabisa mrembo huyo aliiyona kuwa hiyo ndiyo nafasi ya pekee kabisa kwa majira hayo ya kuweza kumtazama awezavyo. Alikuja kuacha kumtazama mara baada ya kumpita kwa hatua tano ndipo akaacha kabisa zoezi hilo la kumtazama na kuondoka zake. "amenivutia sana huyu kijana, natamani ndiyo ungekuwa muda huu niko nae kitandani nakichezea kifua chake huku na yeye akiyatomasa maungo yangu aaaaaaah! I was a mad. Lazima nilale nae ili nijue uwezo wake" alijisemea moyoni dada huyo alipokuwa garini akirudi zake nyumbani kwake. Chriss alijawa na mawazo sana siku hiyo hakuwa na furaha hata kidogo. Moyo wake ulikuwa umebeba mzigo mzito wa majuto. alijuta kushiriki mapenzi na wasichana hao kwani kitendo hicho cha kufanya nao mapenzi wote wawili ndicho kinachomfanya kukosa raha, furaha ilimkimbia kabisa kijana huyo. Macho yake yalikuwa yakitazama mbele lakini lenzi ya jicho lake ilikuwa haioni picha yoyote ile na hata kama angetokea mtu mahali hapo na kumuuliza ni nini atazamacho, ni wazi asingekuwa na jibu la kuridhisha. "Salome sitokaa nikupende tena wewe mwanamke, umekuwa sababu kubwa ya haya mawazo" moyo wa Chriss ndivyo ulivyokuwa ukizungumza pasi na kuushirikisha mdomo wake. "bila ya wewe ninaimani isingefikia mimi kutembea na Maida. Ona sasa nimetembea naye na si yeye tu bali pia nimetembea na ninyi nyote. Lakini sikulaumu. Ndiyo, sikulaumu kwasababu umenifanya nisiione thamani yako tena mbele ya Maida. Sikuwahi kufikiria kama ipo siku ningekuja kukutana na mwanamke mtamu kama Maida, nakiri kuwa I love this girl. Utanisamehe Salome na naomba ukae mbali kabisa na mimi" moyo wa kijana huyo ulizidi kutiririsha maneno kisha akatabasamu, tabasamu ambalo ni ishara tosha kuwa kile ambacho kimetoka kuzungumzwa na moyo wake amekiridhia na kukipitisha.



    *************************



    Wakati Chriss akiwa anazidi kuwaza na kuwazua hili na kulitoa lile, huku nyuma kulikuwa na mtu ambaye alikuwa akijivuta taratibu na kusogea mahali alipo. Si kama hakuhisi kitu laa! Alihisi sana na hisia zake zilimwambia kabisa kuwa kipo kiumbe kinakuja mahali hapo lakini kwakuwa ni mazingira ya nyumbani, hakushtuka wala kujisumbua kutaka kujua kiumbe huyo ni nani. Alijiaminisha kuwa kitakuwa ni kiumbe salama na hakitakuwa na madhara yoyote ile. Kiumbe huyo alisogea hadi ubavuni mwa Chriss upande wa kushoto, akasimama sawa kabisa na Chriss. Akasema "uncle, unawaza nini uncle?" ndivyo alivyosema mtu huyo ambaye hakuwa mwingine bali Joesan. Chriss alichelewa kidogo kulijibu swali hilo hivyo Joesan akaendelea "nilikuwa nimesimama pale kwenye Swimming pool nikitazama mazingira kidogo, ndipo nikakuona hapa muda mrefu sana ukiwa umetulia tuli, nikajua si kawaida yako ni nini mjomba?"

    "mmh!......ha......hapana uncle, nimeamua tu kutulia hapa kwasababu sijiskii kufanya kitu chochote kwa wakati huu" akasema Chriss kwa kitete kidogo. Joesan aliacha kumuangalia Chriss na kugeukia upande ambao kijana huyo alikuwa akiuwangalia kwa muda mrefu sana, akashusha pumzi ya wastani kidogo na kusema. "unajua Tikiti maji ni tunda hata likiwa changa lakini thamani yake ni kubwa zaidi linapokomaa" Chriss akashtuka. Nini maana ya msemo huo. Akamgeukia mjomba wake na kumtazama kwa makini zaidi. Ni nini anachokimaanisha sasa? Ndilo swali lililokuwa limekitawala kichwa chake kwa majira hayo. Joesan akajifanya kutouona mshtuko wa kijana wake huyo na kuendelea na kile alicholenga kukisema huku akiwa bado anatazama mbele hivyo hivyo. "huwezi kuyazuia matamanio ya watu juu ya kile wanachokitamani. Akaweka tuo na kendelea tena " Chriss, umeshakuwa kijana mkubwa sasa. Kuna maamuzi ya lazima yaani haya huna budi kiyafanya lakini kuna mambo mengine huja tu yenyewe, haya nayo pia huna budi kukabiliana nayo" akaweka tuo tena kasha akamgeukia na kumtazama usoni, akatabasamu kidogo na kumalizia "huna budi kuyaacha yafanyike yaliyojitokeza kwenye maisha yako. Huna njia ya kuyakimbia na uzuri wa changamoto ni kuitafutia ufumbuzi na siyo kuikimbia"

    "sijakuelewa mjomba ungeniambia unamaanisha nini labda!?" akauliza kwa mshangao mkubwa sana Chriss. "najua kuwa hujanielewa" akasema. "lakini maana yangu si kwamba unielewe sasa Chriss. Ninachotaka kukwambia kwa sasa ni kwamba, usiibebeshe mzigo mzito akili yako kwa kumuwaza Salome na Maida"

    "Mungu wangu!" moyo wa Chriss ulipiga sarakasi za nguvu na kubadili kabisa mfumo mzima wa mapigo yake. Amejuaje? swali hilo jingine likakivaa kichwa chake. Aliogopa sana. "inamaana na mjomba amejua? Mungu wangu, atanielewa vipi sasa tena amejua kuwa wote nimetembea nao. Ndiyo maana yake, kwanini sasa amewataja wote kwa pamoja? Si inamaana........mama weeee! Hii ni mbaya kabisa hii" alichanganyikiwa kijana huyo, hofu ya kuonekana mshenzi wa washenzi ndiyo iliyokuwa ikimtafuna. Hakutaka kuamini mara moja kuwa eti, mjomba wake amejua. "Chriss!" aligutushwa kijana huyo kutoka mawazoni. Chriss aliogopa hata kumtazama mjomba wake usoni na kuyaelekeza macho yake chini lakini hali hiyo haikumfanya Joesan kutokufikia amuzi lake au kuacha kusema alichopanga kukisema. "giza limeingia sasa my boy acha mimi nielekee ndani ila ukitoka hapa unione kuna mahali nahitaji kukutuma usiku huu hivyo ni vema zaidi kama ungejiandaa mapema ili uwahi kurudi" kasha akaondoka mahali hapo akimuachia kijana wake sinto fahamu ya hali ya juu kabisa. Joesan alifika sebuleni na kujibwaga sofani, macho yake akiyaekekeza luningani. "naamini hakuna kitakacho haribika, acha nimtumie huyu kijana na ninaimani naye sana" aliwaza. "Chriss si lele mama hata kidogo, amepitia mafunzo makali ya kimapigano yale ya self face difence na ya silaha pia hivyo ninampeleka kijana ambaye hata mkuu mwenyewe hataamini. Sikuwa na lengo la kukufanyia hayo my boy lakini sipendi kuupoteza utajiri wangu. Nitaulinda utajiri wangu hata kama ni kwa kuyatoa maisha ya mtu" alizidi kuwaza bwana huyo na mawazo yake hayo yalikuja kukoma mara baada ya Chriss kufika ma kukaa kwenye kochi la pembeni yake. Akamgeukia na kumwambia "kula kwanza basi ili uwahi kwenda"

    "hapana anko ni vizuri ningekwenda kwanza kula nitakula hata nikirudi" akajibu Chriss. "ok, sawa kamata hii" akamkabidhi bahasha ndogo ya khaki, Chriss akaipokea kisha Joesan akasema. "utakwenda nyumbani kwa Suzane na kwenda kumkabidhi hiyo bahasha. ukifika wewe muachie tu mimi nitaongea nae"

    "sawa mjomba basi acha niwahi"

    "kuwa makini na barabara maana wewe na gari kama mlizaliwa pamoja"

    "ondoa shaka anko" aliongea Chriss na kutoka mule ndani. alichagua gari ambayo anaipeda kuliko gari zote zillizopo hapo na kuingia garini humo. "Suzane amekuwa ni mtu anayenisaidia sana ninamuamini na ninaamini hawezi kushindwa kumshawishi huyu ................

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Suzane amekuwa ni mtu anayenisaidia sana ninamuamini na ninaamini hawezi kushindwa kumshawishi huyu kijana. Nimekuwa karibu nae kwa miaka mingi sana na ninamjua kinagaubaga" aliwaza Joesan na kujinyanyua pale kochini na kwenda kuchukua mkanda mzuri wa muvi apendayo kuangalia na kuiweka. akajitupa tena sofani akiwa na rimoti mkononi.



    Safari haikuwa ndefu sana hivyo Chriss alifika nyumbani kwa Suzane kwa muda mfupi sana. Akapaki gari maegeshoni na kutembea mwendo wa haraka hadi ulipo mlango wa mwanadada huyo. Sauti ya kugongwa kwa mlango ndiyo iliyomshtua Suzane ambaye alikuwa mezani akijipati chakula cha usiku. akaamka na kuelekea mlangoni kabla ya kufungua mlango kwanza alichungulia kwenye kijitundu kidogo kinachoruhusu kumuona mtu aliyeko nje kisha akaufungua mlango huo. Tabasamu pana likiwa usoni mwake "karibu sana Chriss, karibu ndani" alikaribisha. "asante madam habari za hapa?" alijibu Chriss na kusalimia. "za hapa nzuri sijui za huko utokako?"

    "za huko ni nzuri pia" alijibu na na kuingia ndani, Suzane aliufunga mlango kwa komeo kabisa na kumpita kijana huyo akiwa amesimama. Akasema "karibu ukae tupate kwanza Dinner than ndiyo urudi nyumbani"

    "ooh! No, madam Suzane. Nyumbani nimecha kula nikaona nije kwanza nikufikishie huu uju.......!" alisema Chriss lakini hakufika mwisho wa sentensi yake, Suzane akamuwahi "najua Chriss lakini sitapenda uondoke hivi hivi bila kupata chochote kitu, hiyo si kawaida ya nyumba hii hebuu kaa hapa ule japo kidogo" alizidi kuongea Suzane lakini Chriss akabaki kwenye msimamo wake hakutata kula kabisa. Alichosema ni kwamba ipo siku atakula lakini si kwa siku hiyo. "ok, sawa kama umegoma kula kwangu ila ningependa ule japo kidogo tu any way, nisubiri mara moja nakuja sasa hivi" alisema Suzane na kuingia chumbani kwake. "oouh shiit! Kwanini moyo unanienda mbio hivi, huyu kijana anafanya nisijiamini kabisa niwapo mbele yake sijui ni kwanini hasa" aliwaza Suzane mara baada ya kuingia chumbani kwake kisha akavua nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa na kulitoa gauni lililokuwa maungoni mwake na kuchukua nguo laini na nyepesi sana tena ikiwa fupi mno kiasi cha kuifanya iishie juu kidogo ya magoti yake. ilikuwa ni nguo nyepesi sana ambayo iliruhusu kuonekana kwa kila kitu cha ndani. "lazima adhma yangu itimie hawezi kuondoka bila kuonja utamu wangu. Chriss ni handsom sana. Kifua chake sijui kikiwa hakijazibwa na nguo kinakuaje. Chriss please huwezi kutoka hivi hivi leo, mimi ndiyo Suzane bwana" alikuwa akizidi kuwaza Suzane. alipoona ameridhika kwa jinsi alivyo, alitoka chumbani mule. "kitu gani umetumwa ukilete kwangu Chriss?" aliuliza Suzane. Chriss alipatwa na mshtuko wa wazi kabisa. nguo aliyovaa dada huyo ilikuwa ni sawa na mtu ambaye hajavaa nguo kabisa, kila kitu cha dada huyo kilichopaswa kufichwa kilionekana. "ni....ni.....metumwa nikufikishie hii bahasha madam!" alisema Chriss kwa kitetemeshi. Lilikuwa ni jambo asilolitarajia kabisa kuliona kwa mwanadada huyo aliyekuwa akimheshimu sana. Chriss licha ya kujizuia kumtazama tena lakini kuna msukumo fulani ulimsukuma angaalie tena huku akijisemea moyoni labda huenda aliangalia vibaya. alipoangalia kwa mara ya pili alikuta ni kile kile tena alikutana na tabasamu lililozidi kumuacha hoi. sehemu zake za siri zikapokea taarifa juu ya kile kilichotazamwa kwa mara ya pili. Suzane akapeleka mkono na kuipokea hiyo bahasha cha ajabu ni kwamba hakuwa hata na muda wa kuangalia hiyo bahasha imeandikwa nini. Aliitupia mezani na kumuangalia kijana huyo usoni na kumuambia. "Chriss umekuwa kijana mzuri sana kiasi kwamba siwezi kuzizuia hisia zangu juu yako. naomba tushiriki penzi usiku wa leo Chriss" alisema Suzane huku akiwa tayari ameshaitupa ile nguo chini na kumfuata kijana huyo na kumkumbatia. Chriss alimsukuma Suzane na kumtupa kwenye kochi lililopo sebuleni hapo. muanguko huo wa Suzane ukaleta jambo jingine la kushangaza kwa kijana huyo. Suzane alianguka na kuitanua miguu yake na kuzifanya sehemu zake za siri kuonekana bila kificho. Mwili wa Chriss ukaanza kutetemeka, matamanio yakamkaa mwilini mwake. kitu kilichopaswa kufichwa kimeonekana hadharani, mapigo ya moyo wake yakaongeza kasi. macho yake yalikuwa yameganda kifuani mwa binti huyo, alikwa katika hali nyingine kabisa ya liwalo na liwe. Suzane naye tayari akili yake ilishamwambia kuwa ni kazi ndogo tu iliyobakia ili aweze kufanikisha hicho alichokipanga kwa muda huo. Alikuwa akimsogelea Chriss taratbu huku akiwa amelirembua jicho lake vilivyo, alipomfikia cha kwanza kukifanya ni kumkumbatia kwa nguvu sana. Kiukweli kabisa wanaume ni wadhaifu sana hasa linapokuja suala la kushindana na hisia mbele ya kiumbe mwanamke, wengi hufeli sana hapo na kujikuta wakishiriki kufanya vitu hata vilivyo nje ya maamuzi yao. Chriss alikuwa ni mmoja katika ya hao, hata ungemwambia asichokitarajia angefanya kwa muda huo kwani tayari akili ilikuwa si yake tena. Kitendo kile cha kijana huyo kukumbatiawa kilipeleka hisia kali sana kwenye ubongo wake na kumfanya apate msisimko wa ajabu. Suzane akaona hapo ndipo pa kujizolea ushindi hivyo hakutaka neno kulaza damu limtawale, alishuka taratibu hadi chini kabisa na kupiga magoti akafungua mkanda wa suruali na kuishusha akamalizia na nguo ya ndani. Kitu adimu alichokuwa akikihitaji kikatoka , kilikuwa ni kifaa cha haja sana kilikuwa ni kifaa cha kazi kweli, kirefu na kinene. "waao! Chriss ni kidume cha haja na kimekamilika si utani, anamzigo wa haja. Oooh! my god leo nita enjoy sana" alisema Suzane na kuutia mdomoni huo mzigo. Chriss alinung'unika akafumba macho kwa hisia kubwa alikuwa akipokea raha za aina yake. Ilikuwa ni miguno ya mautamu na raha iliyokuwa ikiendelea sebuleni hapo. Suzane alitaka kuhakikisha anataka kuona ni kiasi gani kijana huyo anauwezo. Chriss alipatwa na nguvu za ajabu, alimkamata Suzane na kutaka kumtupia kochini lakini mwanadada huyo akamzuia na kumwambia kuwa aelekee chumbani Chriss hakupinga, alimtitika hivyohivyo hadi chumbani na kumtupia kitandani. Akaanza kumshambulia kwa mashambulizi ya awali, alihakikisha kila part ya Suzane anaitendea haki hakutaka kuacha hata sehemu moja. Suzane alipagawa sana kelele za maraha zikarindima chumbani humo. Hadi unafikia muda ambao Chriss anataka kupanda na kummeng'enyua dada huyo, Suzane alishavunja madafu si chini ya mawili. Chriss akapanda na kumpelekea moto wa hatari, Suzane alilalama hadi akalalamika vya kutosha lakini hakuachiwa hata muda wa kupumua kitanda alikiona kikubwa kila alivyojitahidi kuogelea ili kumzidi kijana huyo aliambulia patupu. awamu ya kwanza ya Chriss kufika tamati ilikuwa ndiyo ahuweni ya Suzane kuomba maji. "asante sana Chriss sikutegemea kukutana na mwanaume mwenye uwezo mkubwa wa kujamiiana kama wewe. Hakika leo umenifundisha jambo, leo umenikumbusha methali ya 'kama hujaizunguuka dunia kwa pande zake, usiseme wajua kila kitu' nimejiona si lolote si chochote leo ndani ya chumba changu mwenyewe" aliongea Suzane huku akiwa amejilaza chali akiwa hoi bin taabani. "na mimi pia nikiri kwamba nimekutana na fundi Suzane pamoja na uhodari wangu wote leo nimefikishwa kileleni mapema sana sijui awamu yapili ya mchezo itakuaje" alisema Chriss. Suzane akashtuka. Alicho kisikia ndicho anachomaanisha kijana huyo au masikio yake yamesikia tofauti. "eti leo nimemuwahisha kufika kileleni, nusu saa ya kunifulugusa hapa kitandani tena ikwa ni awamu ya kwanza, hata asinitanie kabisa huyu mwanaume. Ni kweli nilikuwa na hamu sana ya kufanya mapenzi lakini tayari hamu yangu yote imekwisha na nimeridhika tayari. Eti anataka awamu ya pili aaa wapi atanifanya kesho nichelewe kazin huyu. Na kama la kwanza ni nusu saa, hilo ka pili si tupu yangu itawaka moto?" alijiuliza mawazoni Suzane halafu akamuuliza "kwahiyo unataka turudie mchezo baby?" Chriss akamtazama dada huyo na kutabasamu kisha akamjibu" ndiyo Suzane, nimenogewa sana na penzi lako hapa hadi nirudie ndiyo nitajiona sawa kabisa. Alisema hivyo kijana huyo huku akianza kuyachezea maungo ya mwanadada huyo mwenye umbo zuri la kuvutia. "hapana Chriss nina muda mrefu sana sijafanya mapenzi hivyo nimejikuta leo nikitumia nguvu nyingi sana pasipo maarifa hivyo nimechoka sana wangu we will try another timu is not now i'm very tired" alisema Suzane kwa kujitetea akijaribu kuitoa mikono ya Chriss iliyoanza kumpa mshawasha.



    Wakati hayo yote yakiwa yanaendelea usiku huo nyumbani kwa Suzane, kwa upande wa Salome mambo yalikuwa tofauti kodogo. Baada ya kumaliza kuandaa chakula aliingia chumbani kwake na kujifungia kimya kabisa akitafakari jambo. "nimekosa nini mimi Muumba wangu" Chriss ni wa kunifanyia hivi, Chriss ni wa kunidhalilisha mimi kwa huyu malaya? Hapana siamini" alijisemea Salome alipokuwa ndani humo machozi yalishaanza kuyaloanisha mashavu yake kwa majira hayo, kilio cha kwikwi kikashika hatamu, macho yalimuiva kama pilipiki kichaa. "ama kweli yamenikuta Salome mwana wa Nindi lakini si mimi tu yamenikuta hata Maida lazima limkute kama lililonikuta mimi haiwezekani mimi nilie yeye afurahie. Chriss amekuwa wa kunipiga chenga mimi kila ninapolihitaji penzi lake kwa sababu yako wewe malaya hapana" alizidi kuwaza Salome. Lakina Ghafla alikatisha kilio alichokuwa akilia na kutoka mule chumbani kwake na kuchukua uelekeo wa jikoni, alipofika jikona alichukua kisu na kukichomeka kwenye lastiki ya nguo yake ya ndani kisha akarudi chumbani kwake tena. akakitoa kile kisu na kukitazama kwa muda kidogo kabla ya kusema. "sitakuwa na kosa kwa hili nitakalokwenda kulifanya kwayo. Maida naomba uipokee adhabu hii kwa mikono miwili kama ulithubutu kuniumiza kwa makusudi nami sina budi kukuuwa kwa makusudi. umenifanya mtu wa kulia kila wakati Maida kwanini lakini. Lazima nikuuwe Maida kwanini ubaki hai sasa wakati wewe ndiyo kikwazo cha furaha yangu, kwanini usife hata sasa hivi basi ili niyafurahie maisha yangu" alisema Salome wakati huo akikirudisha kile kisu kwenye lastiki ya nguo yake ya ndani kama alivyokuwa amekihifadhi awali. Ewe mwanadam Nafsi hufumbata kiza inapogubikwa na mawazo ya kinyama na ukatili. Nafsi hukosa maamuzi sahihi pale inapogubikwa na kiza hicho. Maamuzi yoyote yatokayo moyoni basi husharabiwa na nafsi hiyo japo mara nyingi mtenda baya nafsi humshauri juu ya baya alitendalo ikiwezekana aliepuke lakini ni ushauri gani basi utakaotolewa na nafsi hiyo ingali imefunikwa na kiza cha kufanya maasi tayari. Nafsi ya Salome ilishabeba kiza tayari kiasi kwamba hata zile sauti za kumzuia asifanye hicho anachotaka kukifanya hakuzisikia. "lazima ufe" huo ndiwo uliokuwa wimbo uliokitawala kichwa chake na alipenda kuuimba kila wakati. alitoka mule ndani na kwenda kuuvamia mlango wa chumba cha Maida. Alidhmiria kweli kufanya unyama huo kwa mtu aliyeishi nae nyumba moja tena wakiwa ni kama ndugu kabisa, lakini alipoufungua ..................



    mlango wa chumba hicho .ambao ulikuwa bado haujafungwa. alipoingia mule ndani hakukuwa na kiumbe chochote alikuta nguo tu zimevuliwa na kutupwa juu ya kitanda na kwakuwa ndizo nguo ambazo Maida alizivaa mchana, akajua kwa vyovyote vile Maida atakuwa bafuni hivyo akaamua kukaa hapohapo na kumsubiri. Kweli hakuwa amekosea kwani baada ya muda mfupi, Maida aliingia mule ndani akiwa amejifunga khanga moja tu huku akichuruzika maji kuashiria kuwa kweli alikuwa bafuni. Maida alikumbwa na mshtuko mdogo baada ya kumkuta Salome ndani ya chumba chake. "hee! Vipi tena mwenzetu ndani ya chumba changu kwema lakini" aliuliza Maida huku akichukua nguo nzito na kuaza kujifuta maji. jibu halikuja kutoka kwa muulizwaji. Maida ikabidi kuuliza tena huku akiitupia ile nguo kwenye kochi na kumtazama Salome usoni. "haitakusaidia chochote hata kama ukijua ni kwema au siyo kwema" akasema na kunyamaza Salome. Maida akastaajabu kidogo na kumshangaa mwenzake huyo akasema "hivi uko sawa Salome?"

    "nimechanganyikiwa Maida na ndiyo maana nipo hapa kwa ajili moja tu ya kukuuwa." alisema Salome na kumfanya Maida ashangae na kuangua kicheko kabisa. "hee! Hivi umechanganyikiwa wewe yaani huoni hata haya eti, niko hapa kwa ajili ya kukuuwa yaani wewe uniuwe mimi?"

    "kwaiyo unashangaa kuwa mimi siwezi kukuuwa au kinachokushangaza ni nini, ngoja uone vile nitakufanyia sasa" alisema Salome wakati huo akiwa tayari ameshamsogelea Maida karibu. Siwezi kukuacha Maida, mimi moyo wangu kwa sasa hauna amani sababu yako. umeninyang'anya furaha yangu, siwezi kuishi kwa namna hiyo. Chriss hataki hata kuniona mimi sababu yako" aliongea kwa uchungu mkubwa sana Salome. Maida alimtazama binti huyo kwa dharau kubwa kasha akatazama pembeni akasema "nilidhani labda leo umewekwa style ya mbuzi kagoma kwenda ndiyo umekuja kunihadithia kama kawaida yako kumbe limekushuka pol.......!" hakufika mwisho wa kauli yake Maida, kofi zito la haja likatua kwenye shavu lake la kushoto. Maida alihisi kama shavu linataka kudondoka, nyama za shavu zilimchonyota. Binti aliyerusha kofi hilo akawa anatamba kwa maneno. "unadhani nimekuja hapa kucheza siyo, Maida hujui kuwa maneno yako ni kama kisu butu kwenye shingo yangu? Inamaana hujui kama naumia Maida, hujui"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Salome unathubutu kunipiga?" badala ya kujibu maswali aliyoulizwa Maida akainuka na swali huku akiwa kalishika shavu lake lililokuwa likimuwanga. "na siyo kukupiga tu mwanahizaya wewe, leo lazima ucheze ngoma ya asili ya kabila letu" alibwata Salome. Hasira kali zikampanda Maida aliinuka kama Nyati na kumvaa Salome na kumtupa kweye meza iliyopo chumbani hapo. Salome akajipigiza kwe ye mbao ngumu ya meza hiyo hadi paji lake la uso likapasuka. Damu nyingi zilimtoka. Maida hakujua alilolifanya ni kosa linalokwenda kuyagharimu maisha yake. hakujua kuwa

    mwaenzake hakuwa na imani tena roho yake ilibadilika kabisa na kuwa ya mnyama hatari. aliinuka kutokea mezani hapo mithili ya mzimu akafunua gauni alilolivaa na kujipekuwa kwenye kufuli lake akatoka na kisu. Maida akabaki mdomo wazi kwa kile alichokiona hapo kikifanywa na mwanamke mwenzie tena pasipo matarajio yake. kisu kile kikajaa kifuani. Maida akatokwa na ukelele mdogo, Salome akachomoa na kukirudisha tena tumboni mwa mtu ambaye walikuwa wakichangia jiko pamoja wakiwa katika harakati za kuwaandalia mabosi wao chakula. kisu kile kikafanya kama kilivyoagizwa. Maumivu makali yakazidi kumtambaa binti huyo masikini. Salome hakuwa yeye tena akakitoa na kuchoma tena na tena ni kama alikuwa akiamrishwa hivi. hadi pale Maida alipodondoka chini akiwa anapambana na hatua za mwisho za uhai wake ndipo jini baya la ukatili likavuka mwilini mwa binti huyo na kumuacha mwenyewe. Kitu cha kwanza kukiona kilikuwa ni kisu kilichojaa damu nyingi mkononi mwake, macho ya hofu yakamtoka pima. Alipokuja kutazama sakafuni kulikuwa na dimbwi dogo la damu, hapa aliogopa zaidi na mbaya zaidi ni pale alipomuona Maida akiwa chini akikunja na kunyoosha miguu ikiwa ni moja ya hatua za mwisho za kupambana na sakaratul mauti. "mama weee! Nimeuwaaa!" alikema vibaya sana sauti kubwa ikapaa. akajirusha mlangoni ili aweza kutoka mule ndani, akajipigiza mlangoni na kudondoka chini akakukuruka na kunyanyuka kwa spiidi kali, sasa badala ya kuwa mlangoni akajikuta kwenye mwili wa Maida ambaye kwa wakati huo jina lake lilikwisha badilika tayari. alikuwa ni marehemu. Mayooo!" aliita mama kikwao. "nimeuwa kweli mimi Salome! Haa! Maida nilikuwa nakutania tu amka bwana usife kweli" ama kweli upumbavu huja mara moja tu pasipo matarajio. Unawezaje kumtania mtu kwa kumkita mara zaidi ya nyingi. Wimbo wake wa kuwa nimeuwa kweli ukachanganya, akachoropoka huku akipiga kelele akimuita bosi wake kwa hamaniko kubwa kabisa.



    "hapana Chriss leo nimechoka sana tufanye siku nyingine bwana" alikuwa ni Suzane ambaye alitoa malalamiko mbele ya kidume cha mbegu kilichokuwa kinataka mchezo urudiwe. alimuweka kwenye himaya yake hadi mwanadada huyo akakosa kufurukuta, akabaki akitumia utetezi wa maneno. Chriss ikambidi kuwa mpole na kuamua kuchukua nguo zake na kuzirudisha mwilini kisha alimuaga mrembo huyo na kuondoka. Chriss alipotoka tu mazingira hayo, Suzane alichukua simu na kumpigia Joesan. simu iliita kwa muda mrefu sana pasipo kupokelewa, akarudia tena na tena lakini bado iliita tu. "mh! Atakuwa amelala huyu hebu niache asijekupokea mkewe ikawa shida maana namjua vema Martha kwa wivu" alisema lakini wakati akiwa anawaza hayo, simu yake ikaita na mpigaji akiwa ni Joesan. "vipi Chriss ametoka kwako tayari?" lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Joe. "ndiyo mbona unawasiwasi sana Joe?"

    "hapana ooh! Ngoja kuhusu yaliyojiri huko utanieleza kesho kazini hapa nyumani kuna tatizo kidogo limejitokeza hivyo hatutaweza kuelewana" alizungumza Joe. "ok, boss" akajibu Suzane. Chriss alifika nyumbani akajua amechelewa sana hivyo hawezi kueleweka kwa mjomba wake lazima ataonekana kuna sehemu amepitia. lakini hakujua kuwa ni yeye ndiye anayechezewa share. Hali ya tafarani ndani mule ikamtisha, akawa anaingia kwa kunyata kuhofia isije ikawa ni majibizano kuhusu yeye lakini alivyozidi kuvuta hatua ndipo aliposikia kuwa Maida amekufa kabla hata ya kufika hospitali. Mwili ukaanza kuingiwa na baridi ni Maida yupi, aliyemuacha nyumbani au ni yupi? yakawa ni maswali ya kujiuliza kichwani mwake. Akafika sebuleni pale ambapo ndipo mjadala ulipokuwa ukiendelea. "Maida yupi Uncle?" akajikuta akipata msukumo mkubwa wa kuuliza swali. wote pale ndani wakawa kimya hakuna aliyejua alijibu vipi swali hilo japo ilijulikana kuwa ni Maida wa humo ndani. Mjomba alishajua moyo wa Chriss ulipo lalia, ni vipi sasa akisema eti Maida ameuwawa na Salome? Joesan alimjua vizuri kijana wake, Salome asingeachwa. Sasa ili kutomchanganya kijana huyo na mambo yaliyokusudiwa yasiharibike ni kumdanganya. "ni Maida wa humu ndani Chriss na amedondoka ghafla tu chumbani kwake. Salome ndiye aliyetuletea taarifa hiyo. nimejaribu kumkimbiza hospitali lakini hali si hali tulichelewa" alisema Joe huku akionesha masikitiko makubwa sana. Chriss alijisikia vibaya sana kwa taarifa hiyo. Alisha muhusudu binti huyo na alishaweka nadhiri kuwa Maida ndilo chaguo lake, leo eti, anapokea taarifa ya kifo chake. "Maida alikuwa anasumbuliwa na nini? Mbona ghafla namna hii? Kwanini Salome awe wa kwanza kupokea taarifa hiyo na kuja kumjuza Uncle? Si bure" aliwaza Chriss na mwisho akajishauri na kuelekea mbio chumbani kwa Maida. Chumba kilikuwa kimefungwa. akanyong'onyea, alipogeuka nyuma akakutana uso kwa uso na mjomba wake. "Chriss hata sisi pia tumeumizwa sana na hili jambo, hutakiwi kuwa katika hali hiyo uliyokuwa nayo sasa" alizungumza Joesan kwa sauti ya upole sana. "lakini Unle kwanini hiki chumba kimefungwa sasa?" aliuliza Chriss. Joesan akajibu "ndiyo, tumekifunga ili kisitumike tena kwani huwezi jua baada ya mwili wa marehemu kufanyiwa uchunguzi, wakahitaji kujua mazingira ambayo marehemu alifia. Sasa kuingia kwako kunaweza kuwa siyo sahihi kiusalama"

    "ok, nimekuelewa mjomba sasa Salome yuko wapi kwa sasa?" akauliza. Joesan baada ya kuulizwa swali hilo ilibidi awe mpole kwanza hakutaka kukurupuka kulijibu kwani baada ya binti huyo kufanya hilo tukio Salome alikimbilia chumbani kwake na kujifungia hivyo haikujulikana huko aliko anafanya nini au amechukua amuzi gani. Alichokifanya kwa wakati huo Joesan ni kukimbilia chumbani kwa Salome ili kujua usalama wake. Chriss naye akakimbilia huko huko huku akiwa na alama ya kujiuliza kichwani mwake, nini hasa sababu ya mjomba wake kukimbia kwa haraka namna hiyo mara tu alipomuuliza hilo swali. Waligonga mlango lakini haukufunguka hata kidogo, Joesan akaenda chumbani kwake na kwenda kuchukua ufunguo wa hakiba ili kuweza kuufungua mlango huo. "mjomba kunausalama kweli lakini" akauliza Chriss. "hata sielewi mjomba, hawa watoto wanamichanganya kabisa" alijibu Joesan. Walipofanikiwa kuufungua mlango huo, break ya kwanza ni sakafu ya chumba kile ambacho alikuwa akikitumia binti huyo ilikuwa haitamaniki kwa damu. Joesan macho yakamtoka kama mjusi aliyebanwa na mlango. Hofu ikawatanda. Joesan akapagawa kabisa. Kitendo cha kumficha Salome kwa dakika chache ili tu kumsitiri na hasira za Chriss endapo angemkuta katika hali ile ya kuchanganyikiwa ilhali akiwa na damu mwili mzima, vipi sasa akute damu na asimkute muhusika. Chriss alishindwa kuelewa ni kwanini yale yote yanatokea. nini sababu ya mambo yote yale, hakuelewa hata kidogo. wakaingia mule ndani kwa mwendo wa taratibu huku wakiangaza macho yao kwenye kila kona ya chumba hicho. "Salome.......! Salomee......!" aliita Joesan bila mafanikio. wakaendelea kutafuta mule ndani. "unauhakika mjomba kuwa Salome yuko humu ndani?" akauliza Chriss. "asilimia zote na aliingia humu ndani akiwa amechanganyikiwa sasa sielewi ata.......!" akakatisha maneno yake Joesan baada ya kusikia sauti za manung'uniko kuashiria kuwa kulikuwa na mtu aliyekuwa akipambana na maumivu makali sana.





    wakaelekea kwenye upande mmoja wa kitanda, huko wakamkuta Salome akiwa anapambana na maumivu si ya kawaida huku kisu kikiwa kifuani mwake. "Salome nini tatizo mbona umechukuwa maamuzi magumu hivi, kwanini unataka kujiuwa?" aliuliza Chriss akiwa na sura ya huruma sana.Zile hasira zote juu ya msichana huyo ziliyeyuka huruma kwake kilikiwa ni kitu cha kwanza kumkaa moyoni mwake kijana huyo. "niambie Salome nini tatizo" alizidi kuuliza. Salome akalilazimisha tabasamu lakini ilionekana dhahiri maumivu aliyokuwa akiyapata yalikuwa si lelemama hata kidogo. Sura yake haikukunjuliwa kabisa na tabasamu hilo. akanyanyua mkono wake mmoja na kulishika paji la uso la Chriss na kulipapasa kisha akasema. "ni...ni....sa...mmehe...sana......!" akanyamaza kidogo na kuikunja sura yake hadi pale maumivu yalipopungua kiasi akaendelea "Chriss nimeamua kijiuwa ili kuukwepa mkono wa sheria, najua mjomba anao uwezo wa kunipeleka hospitali na nikahudumiwa hadi kupona lakini sihitaji kupona Chriss, napenda nife tu"

    "hapana huwezi kufa hata kidogo Salome lakini kwanini umeamua kujikatishia maisha?" akauliza Chriss akiwa kamshika mabegani. "Chriss nakupenda na nimeamua kufa kwasababu tu nakupenda. Sikuiona sababu ya kuendelea kubaki hai wakati sipo moyoni mwako, sikuona sababu hiyo hata kidogo" akaweka koma na kulazimisha cheko. Damu zikamtoka kinywani kwa wingi sana lakini hakuacha kucheka hadi pale alipogoa akatulia zaidi halafu akaendelea kusema "unajua kwanini ninacheka? Unajua au hujui?" alivyosema hivyo akaygeuza macho yake na kumtazama Joesan ambaye alikuwa kimya muda wote. Joesan akatikisa kichwa kukataa kuwa asiseme hicho alichotaka kukisema lakini Chriss aligeuza haraka shingo yake na kumtazama mjomba wake na kumkuta katika hatua za mwisho za kutingisha kichwa. akashangaa na kunyanyuka kwa hasira sana na kumkabili mjomba wake kwa maneno. "mbona sielewi, kuna siri gani inayoendelea hapa. Kuna kitu mnanificha, mjomba hata mimi unani....!"

    "unafichwa nini Chriss, hakuna kitu unachofichwa hapa" alidakia Joesan na kupunguza makali ya sauti ya kijana huyo ambayo ilikuwa ikipaa kwa kiwango kikubwa mno. " siyo kweli, siyo kweli mjomba mnanificha, niambieni na mimi nijue kwanini mnanificha sasa unajua mimi sielewai Maida nimemkuta hayupo na mkasema kuwa amefariki dunia kwa maz.......!"

    "Chriss!" aliita Joesan kwa sauti ya juu sana. Chriss akawa mpole. Sauti hiyo iliashiria hasira kwa mjomba wake. Macho makali yakamtazama yeye. "naona umekuwa sasa kiasi cha kunijia juu kwa kibesi siyo" akawaka. "hapana Uncle siyo hivyo n

    tatizo ni kwamba nashindwa kuwaelewa" alijibu Chriss akiwa ameishusha kabisa sauti. mjomba huyo alizidi kumtazama Chriss kwa ghadhabu sana mithili ya mtu mwenye kisasi kizito juu yake lakini kabla ya kusema chochote, Salome akaita. "Chriss!" wote wakamgeukia binti huyo ambaye kwa muda huo alikuwa katika hatua ngumu kabisa. "msiwe na sababu ya kuminyana na mjomba mimi ndiye niliye muuwa Maida. Ni bora tumekosa wote sasa na nikwambie tu kuwa nakufa nikiwa naku....ku...!" akaishia hapo bila kumalizia. Kichwa kikaanguka upande mmoja na pumzi kumkimbia, mwili ukabaki bila roho ungali ukitoka damu mdomoni na puani kabla ya damu hizo kuganda. Salome alipoteza uhai wake mazima. Chriss mwili ilimnyong'onyea, nguvu zote zilinywea mwilini. "Salome umemuuwa Maida? Why? Why Salome? Sababu ni mimi. Salome hata kama ni mapenzi lakini hatua ulioichukuwa ni mbaya sana. umenikosea sana, umeutafuna moyo wangu na kuutema bila huruma" aliwaza kijana huyo. "sikutegemea kama itatokea siku na kukutana na mwanamke mwenye roho ya ajabu kama yako. Nani kakudanganya kuwa ukimuuwa nimpendae utaiteka nafasi yake. nakuchukia Salome, nakuchukia kuliko hata ninavyo lichukia tumbo la kuhara. Wewe si mwanamke hata kidogo ila umevishwa tu uhaiba wa kike. Mungu akulaani uwendako Maida, ulaaniweee!" akasema kwa sauti kubwa mwishoni. Kilio kikachukuwa nafasi Alilia sana Chriss machozi yalimwagika kama maji, alilia kama mtoto mdogo hadi pale Joesan alipoamua kumshika mabegani na kumwambia "hupaswi kulia kwa kupitiliza namna hiyo Chriss, ukumbuke kuwa haya yote yamekuja sababu ni wewe. Kama si wewe haya yote yasingetokea. Mapenzi ni kitu kibaya sana kijana wangu, mapenzi yanaweza kubomoa nyumba imara iliyojengwa kwa theruji bora kabisa. kumbuka kuwa nilikuambia nini jana, unakumbuka?" akauliza Joesan baada ya kuongea maneno hayo. Chriss akabaki kimya bila kuongea jambo lolote. aliwaza mengi sana, aliwaza na kuona ni jinsi gani alivyo haribu uaminifu wake mbele ya watu waliomheshimu, aliona jinsi atakavyoeleweka vibaya. "kumbuka" akaendelea Joesan. "nilikuambia kuwa huna budi kuyaacha yaliyotokea yaendelee na wewe ugange ya mbele, huna uwezo wa kuubadilisha uhalisia. Usihofu kwani haya mambo hata sisi walezi wako tumeyapitia hivyo si jambo la kukufanya ukose raha"

    "najua uncle lakini sikutegemea kama Salome anaweza kufanya haya aliyoyafanya, Salome ni katili sana mjomba hana ubinadamu anawezaje kumuua mwenzake kikatili namna ile." akasema Chriss. "imembidi kufanya hivyo na ndivyo tulivyo wanadamu hata wewe huna budi kufanya lolote lile linalowezekana kufanyika pale tu linapokukuta"

    "sijaelewa Uncle unamaanisha kuwa alichokifanya Salome ni sahihi kisa tu ni mapenzi juu yangu au?" aliuliza Chriss huku akiwa na mshangao mkubwa sana machoni mwake. "Chriss, nafikiri muda umekwenda sana na umechafuka kwa damu mwilini mwako, hebu nenda kaoge na ubadili hizo nguo. Unapaswa kupumzisha kichwa sasa wacha mimi nihangaike na kuupeleka huu mwili hospitali maana hatuwezi kukaa nao hapa ndani ni hatari sana kiusalama" akasema Joesan. Chriss alinyanyuka kishingo upande na kuuangalia ule mwili wa Salome kwa ghadhabu sana kisha akaondoka chumbani humo. "nilitaka asijue chochote kuhusu kifo cha Maida maana najua ni jinsi gani Chriss anavyompenda Maida lakini imeshindikana. Salome ameamua kusema ukweli kabla hata ya kukata roho, lakini hakuja haribika kitu lazima nilichokianzisha nikimalizie" akawaza Joesan baada ya Chriss kutoka humo ndani. Akatoka mule ndani na kumpita mkewe ambaye alikuwa amechanganyikiwa kutokana na jambo hilo. akageuka na kumwambia kuwa lile suala atalimaliza bila shida yoyote hivyo hakuna haja ya yeye kuendelea kuchanganyikiwa na kutoa machozi. "nenda ndani ukapumzike mke wangu acha mimi nielekee hospitali kwa ajili ya kwenda kuuhifadhi huu mwili kesho tutajua nini cha kufanya" akasema. Anti Matha hakupinga aliondoka hapo na kuingia ndani japo alijisikia vibaya sana lakini ndiyo hivyo tena ilibidi awe mpole. Joesan alitoka hadi nje kabisa ya geti na kutoa simu yake mfukoni akapiga mahali. "nisikilize Sembugi, lete hiyo gari hapa kuna mwili mwingine wa huyu malaya amejiuwa mwenyewe kabla ya mpango wetu" alisema Joe na kukata simu. Haukupita muda gari ndogo Toyota Mark II ilipiga break karibu kabisa na bwana huyo. Wakatoka vijana wawili na kumkaribia Joesan. "tuelekee ndani tukautoe huo mwili halafu niwaelekeze cha kufanya" akasema. wakaingia ndani na kuutoa ule mwili na kuja kuupakia garini. Baaada ya kuupakia mwili huo, Joesan akawageukia na kuwaambia kuwa ile miili haikutakiwa ionekane tena kwenye macho ya watu hivyo watajua wao ni jinsi gani waitokomeza. Wale vijana wakatikisa vichwa kukubali na kuagana na boss wao kisha gari hiyo ikaondolewa. "bila kufanya hivi ni lazima Chriss atahoji na atataka kushiriki kumzika Maida na ukicheki ni muda mchache sana uliobakia" akawaza na kungia ndani. Chriss hakupata usingizi kabisa usiku huo, mawazo yalikuwa mengi sana kichwani mwake. Nini sababu ya yote hayo, ni kweli sababu ni yeye au kuna jambo jingine nyuma ya pazia. Alihangaika usiku kucha huku kichwa chake kikiwa kimebeba mzigo mzito wa mawazo. Usingizi ulikuja kumpitia muda ambao hata mwenyewe hakuujua. Alilala kwa muda mfupi sana na kuja kushtuka asubuhi sana.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Simu ya Joesan iliunguruma na kumfanya bwana huyo kuamka kutoka usngizini. Akanyoosha mkono na kuivuta simu hiyo iliyopo mezani akaipokea na kuiweka sikioni. "ndiyo" akasema na kutulia kidogo kuusikilizia upande wa pili wa simu hiyo kasha akasema tena. "naamini mtakuwa mmefanya kazi vizuri" akanyamaza na kumgeukia mkewe ambaye alikuwa akijigeuza upande wa pili na kumkumbatia. Joesan akautoa mkono huo na kunyanyuka kitandani hapo na kuelekea upande wa chooni akasema. "sitaki kusikia chochote kuhusiana na hao marehemu, njooni nyumbani mida niliyowaambia na mfanye kama nilivyo walekeza mkimaliza mtanipigia simu na kuwaelekeza wapi mtakapo kwenda kuchukua pesa yenu sawa" akamaliza na kukata simu hiyo na kurudi kitandani. "ulikuwa unaongea na nani honey?" aliuliza anti Martha. "acha wivu mke wangu ni simu ya ofisi hiyo"

    "mmh! Simu ya ofisi ndo ukaongelee mbali hivyo ni kitu gani ambacho mimi sipaswi kujua?" akauliza. "si kila kazi ya ofisi unapaswa kuisikia, pamoja na hayo yote pia nimetoa taarifa kuwa nitachelewa kwenda kazini kutokana na haya matatizo yaliyotokea na.....!"

    "hupaswi kwenda kabisa kazini mume wangu hili jambo ni kubwa sana, unatakiwa ulimalize kwanza hili, ulipaswa kuomba kabisa ruhusa hata ya siku tatu" akatoa ushauri Martha lakini Joesan akamuangalia kwa macho makali sana na kusema kwa sauti iliyomshtua kidogo mkewe. "ungejua kilichotokea kazini wala usingepata nguvu ya kuongea jambo hilo hata kidogo, kazini ninajukumu zito sana na sijui nitalimaliza vipi leo unasema niache kwenda kwa wapumbavu tu walioamua kujikatishia maisha wenyewe. Kama hujui sasa mimi nilishajua kabla yako kuwa Chriss anamahusiano na mabinti wote wawili. Nina kazi kubwa ya kufanya na Chriss na atanisaidia sana hivyo hata kama wasingekufa, walikuwa wapo katika mpango wa kufa na ni lazima wangekufa tu ili wasiwe kikwazo na maisha ya Chriss kwani namjua Chriss ni mbovu sana katika kupenda asingekubali kuifanya kazi yangu na nategemea kuingiza pesa nyingi kwayo" akakomea hapo Martha akabaki mdomo wazi. Alishasahau tabia ya mumewe ya ukatili na unyama alionao ni miaka mingi sana Joesan alikuwa hivyo na alidhani labda baada ya kupata utajiri huo angeacha kabisa mambo hayo. "unataka kumtumiaje Chriss mume wangu?" akashindwa kuvumilia Martha na kuamua kuuliza. Joesan alimvuta Martha hadi karibu kabisa na yeye kisha akampiga busu la shavu na kumwambia "usiku wa jana sijapata kabisa mambo maana nilijua umechanganyikiwa sana hivyo ni bora nijilie hii asubuhi kabla mambo mengine hayajafuatia" akamvuta zaidi na kuanza kumpapasa. "no, Joesan haileti picha nzuri kweli tunafurahi wakati watu tulioshi nao vizuri hatupo nao, please mume wangu hebu kuwa na moyo wa imani hata kidogo" akasema Martha. "kwahiyo hao ni bora kuliko mimi mumeo ninayehitaji haki yangu ya ndoa?" akauliza Joesan. "hapana .............................





    "hapana sina maana hiyo"

    "ila?" akauliza kisha akapanda kwa juu na kuanza kumnyonya kwa fujo. Martha ilibidi awe mpole na kutoa ushirikiano kwani hakumuelewa kabisa na alikuwa na hofu kubwa juu ya maisha ya Chriss. Hakujua ni kazi gani atakayokwenda kufanyishwa na mume wake. Mchezo ukanoga zaidi na kuamua kujificha kabisa ndani ya shuka. Joesan akaitoa shuka hiyo na kuitupia pembeni "napenda kufanya mapenzi na wewe huku nikiliona umbo lako zuri kwani linanipa raha ya aina yake na kuniongezea munkari ya kushughulika zaidi. Aaaaaghr shiit! alilalama Joesan akiwa anajifaidia tunda tamu kutoka kwa mkewe huyo. miguno ya mahaba ikachukua nafasi chumbani hapo na kuwasahaulisha kabisa juu ya kile kilichotokea.



    %%%%%%%%%%%%%%%



    " ngriiiiiin, ngriiiiin,ngriiiiiiinn!" sauti ya kengele ya langoni iliita kwa fujo asubuhi hiyo ya saa nne kama na nusu hivi kuashiria kuwa kulikuwa na mtu langoni hapo. "Chriss hebu kaangalie ni nani huyo anayegonga asubuhi hii" alikuwa ni Joesan akimpa maagizo kijana wake. Chriss alitoka sebuleni hapo na kuelekea getini hadi kilipo kidirisha kidogo cha kuruhusu kumuona mgongaji. Akachungulia kisha akalifungua lango hilo. wazee wawili na vijana watatu walio katika mavazi ambayo yaliashiria kabisa kuwa watu hao walikuwa ni wa maisha ya kawaida sana. "karibuni sijui niwasaidie nini?" akauliza Chriss na kuwatazama watu hao. Mzee mmoja akanyanyua macho yake yaliionekana kubeba majonzi makubwa kabisa na kuruhusu maneno kutoka kinywani mwake kwa shida kidogo. "tumemkuta bwana Joesan?"

    "ndiyo mmemkuta" akajibu Chriss huku akipata picha kwa mbali juu ya ujio huo wa watu hao hapo nyumbani. "sisi ni wageni wake na tupo hapa kwa ajili yake hivyo ni vema kama tungeonana naye" akasema mzee huyo ambaye ndiye aliyejivika usemaji mkuu. Chriss akaurudisha mlango na kuwaongoza watu hao hadi sebuleni. akawakaribisha wakakaa sambamba na yeye mwenyewe kujitwalia nafasi ya kuketi. "karibuni sana jamani mimi ndiye Joesan mwenyewe" akawakaribisha Joesan mara baada ya kuelezwa kuwa watu hao wapo hapo kwa ajili yake. Mzee yule yule aliyejivisha uongeaji akakohoa kidogo na kifua kikamsaliti kwa kubanja kabisa kudhihirisha kuwa mzee huyo kama si mtumiaji wa pombe aina ya gongo basi ni mtumiaji wa pombe nyingine za kienyeji na tumbaku lisilopitia kiwandani. Alikuwa na sura mtindio, mashau yaliyolegea kama mgonjwa wa safura, kitambi kisichoeleweka kama ni cha minyoo au kiriba tumbo tu kutokana na kula pasipo utaratibu. Akakohoa tena sasa ikiwa si kwa kurekebisha koo bali kumalizia mabaki ya kile alichokianzisha kwa bahati mbaya kisha akasema. "mimi naitwa Nindi Mchujuko kwa majina yangu na mwenzangu hapa ni Athumani Kidaru tukiongozana na vijana wetu kama unavyowaona. Sasa kama msemaji mkuu" akabanja tena na kumeza huku akijitafuna, akaendelea "nasimama kwa niaba ya mwenzangu hapa. Tumetokea kijiji cha Mkwajuni kilichopo wilaya ya Muheza Mkoani Tanga. Kwa kweli kabla ya yote tuwape pole kwa hili lililowakuta la kuvamiwa na majambazi na kuweza kusababisha vifo vya mabinti zetu na kama mngekuwa wote humu ndani sijui hata ingekuwaje, ila yote ya yote niseme ni mipango ya Mungu tu." akaweka tuo na kuwatazama wenzake hususan yule mzee mwenye umri sawa na yeye. "mimi" akaendelea. "ndiye mzazi wa Salome Nindi na huyu mwenzangu ni mzazi wa Maida Athumani. Tumeipata simu yako. Kwakweli nimeipokea katika majonzi makubwa sana ndipo nikampa mzee mwenzangu taarifa hiyo. Tulihuzunika sana na niseme tu ukweli habari hizo zimemfanya hadi mke wangu amepoteza kabisa fahamu kwani huyu ndiye aliyekuwa tegemezi kwetu" mzee huyo akafuta chozi lililokuwa likitoka jicho moja la kushoto kuonesha kuwa alikuwa yu katika majonzi mazito. "poleni sana wazee wangu kwanza kwa kutoka mbali, pili kwa kuwapoteza wapendwa wenu ila hakuna mwanadamu anayeweza kusimamisha kazi ya Mungu. Hilo ndilo lililotokea na kwa bahati mbaya mimi nilikuwa kazini na huyu kijana alikuwa kwenye shughuli zake na mke wangu nae alitoka nahisi hivyo wakavamiwa wakiwa wenyewe na kwa kuwa walichokikusudia hawakukipata ndipo wakaamua kutenda unyama huo kwa hasira zao." ulikuwa ni uwongo mkubwa sana uliokwa ukitolewa hapo na Joesan. Chriss hakuelewa kabisa kitu ambacho kilikuwa kinaendelea mahali hapo. Joesan alikuwa akiongea uwongo tena bila wasi wasi wowote, alikuwa mkavu kabisa. "Salome na Maida walivamiwa? Saa ngapi? Mbona mjomba simuelewi jamani, ananichanganya kabisa. Maida ameuwawa na Salome na Salome amejiuwa mwemyewe leo mjomba anasema ni majambazi wamevamia, hii inaingia akilini kweli." aliwaza Chriss akiwa amejiinamia chini. hakuelewa kwanini mjomba wake anakuwa muongo kiasi hicho. "lakini huwenda akawa ametumia triki hiyo ili kuficha sababu za vifo vya mabinti hao, kama anafanya hivyo sawa" alizidi kujiwazia kisha akanyanyua macho yake na kuwatazama watu ho ambao nyuso zao zilikuwa zimebeba majonzi makubwa. "masikini wazee hawa wametoka mbali sana hadi napata uchungu moyoni. Aah! Salome kwanini umesbabisha madhara makubwa namna hii, hivi ulimuona baba yako alipokuja kukutazama Monchuary, si alilia sana au hukumuona ulijifanya kufumba macho. Niseme tu ukweli nakuchukia sana Salome na nitakuchukia hadi siku unafufuliwa" alisema Chriss moyoni. Shutuma nyingi alimtupia Salome akimuona ndiye msababishi wa hayo yote akijitoa yeye kwenye sekeseke hilo. Hakujua kuwa bila yeye hayo yote yasingetokea. "kwa mila na desturi zetu" akaendelea kusema mzee huyo muongeaji. "huwa hatuitupi miili ya ndugu zetu hata wakifa umarekani tunabeba na kwenda kuzika kwetu hivyo ujio wetu hapa ni kuja kukuambia kuwa tumekuja kubeba mizigo yetu na kwenda kuzika nyumbani" Joesan alijiinamia chini akawa kama anayetafakari jambo fulani akasema. "nimewasikia na kuwaelewa vizuri wazee wangu na mimi sina pingamizi juu ya jambo hilo. Sasa mimi nitawapa gari ambalo litawapeleka hadi mnakokwemda nadhani hapo nitakuwa nimerahisisha kwa kiasi fulani" akasema. Yule babu muongeaji akapiga magoti akifuatiwa na mzee mwenzake, wakimshukuru Joesan kwa msaada huo. Baada ya hapo aliwakabidhi wale wazee kila mmoja kitita cha fedha kisha akawatakia safari njema huku akitoa sababu nyingi za kutofika kwenye msiba huo. wale watu wakamshukuru sana Joesan na kumtakia heri na fanaka tele. Joesan alizipokea na kumpigia simu mtu fulani ambaye baada ya muda mfupi alifika hapo na gari ambayo iliwachukuwa watu hao. Aliporudi ndani kabla hata hajakaa, alikutana na maswali mengi sana kutoka kwa Chrisi. Akamwambia kuwa ilikuwa ni lazima atumie uwongo ule ikiwa ni pamoja na usalama, pia kumlinda yeye kwani sababu kubwa ya vifo vya binti hao ni yeye. Chriss hakuwa na neno la kuongeza tena akaamua

    kukaa kimya kabisa. Joesan akamwambia Chriss watoke kidogo kwani alikuwa na maongezi naye. wakatoka na kuelekea ilipo bustani. Muda wote huo Chriss alikuwa na maswali mengi ya kumuuliza mjomba wake huyo, kitendo hicho cha kutoka hapo ndiyo ikawa nafasi kubwa sana kwa kijana huyo ya kuweza kuuliza kile ambacho kilikuwa kikimsumbua. "Unle unajua sijakuelewa pale ulipokuwa unawaeleza wale wazee pale, mbona hukuwaambia ukweli sasa?" ndilo swali la kwanza la Chriss kwenda kwa Joesan. Joesan aliachia tabasamu kidogo na kusema, "nilijua tu kuwa hilo litakuwa ni swalia lako la kwanza" maneno hayo yakamfanya kijana huyo kuongeza umakini wa kumsikiliza, Joesan akaendelea. "ilikuwa ni lazima nifanye vile na nilifanya vile kwa sababu mbili tofauti. Ya kwanza ni usalama. Unafikiri kama wangejua kuwa mabinti zao wamechomana visu ndani kwangu, ni nani kati ya wale wazee au wale vijana uliowaona pale angenielewa, ni lazima wangefika mbali na ingebidi wewe ndiyo uwajibike. Lakini pili nimefanya vile ili kuondoa kabisa mizizi ya fitina baina yangu na wao, sitaki tena wanisumbue wala mimi niwasumbue nafikiri utakuwa umenielewa vizuri kijana wangu?" alisema Joesan kwa urefu zaidi. Chriss akashusha pumzi ndefu sana na kutulia kwa muda kidogo akitafakari hili na lile bila kupata pa kuanza kusema. "mjomba amefanya jambo la busara sana sidhani kama ningeeleweka kwa jambo lililotoke ni dhahiri mimi ningekuwa pabaya" aliwaza Chriss. "Chriss!" Joesan aliita. Chriss akageuza macho na kumtazama. "najua kuwa upo kwenye wakati mgumu sana na mawazo mengi yamekujaa kuhusu hili lakini tambua kuwa wewe ni mwanaume huna budi kupambana na kila matatizo, usiuruhusu moyo wako kupokea maumivu kirahisi namna hiyo umenielewa?"

    "nimekielewa Uncle na nipo sawa kabisa japo siamini kama binti kama Salome angeweza kufanya mambo ya kikatili namna ile, sijui ana roho gani yule mwanamke" aliongea Chriss na kumfanya Joesan aangue cheko kubwa sana hadi Chriss akashtuka, alicheka sana Joesan. "usinichekeshe Chriss, hivi unataka kuniambia haya mambo kwako ni mageni kabisa?" akauliza. Chriss akajibu ndiyo. Joesan akamshika bega na kumwambia. "unataka kuniambia ulipokuwa China kwenye mafunzo yako ya mapigano, hukuwaona wanawake?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "niliwaona tena ni wengi sana" akajibu Chrss. "vipi uhodari wao katika nyanja ya mapigano?" akauliza tena Joesan. Chriss akajibu kuwa uhodari wao ni mkubwa tena usipokuwa makini hata mwanaume unaangushwa kirahisi kabisa. "sasa hao wote usifikiri kuwa wanaitafuta self diffence, wengine wamewekwa katika mafunzo hayo na vikundi hatari kabisa na wanatengenezwa ili waje kuwa wauwaji wa kutisha" alisema Joesan. Chriss akabaki akishangaa asiamini maneno anayoyasikia kutoka kwa mjomba wake. wakatembea kidogo na hatimae wakafika chini ya mti fulani uliokuwa umestawi sana, hapo wakasimama na kuzidi kupiga domo. "kwa sasa acha mimi nielekee kazini ila kaa ukijua kesho kutwa tunaondoka wote hapa kuna kitu kimoja nimekiandaa kwa ajili yako." akasema Joesan. Chriss akaitikia kwa furaha sana na kisha wakaondoka wote hapo na kuelekea ndani. Joesan alifika ofisini kwake na kujiweka kwenye kiti chake cha kiofisi na kutulia. Haukupita muda mrefu Suzane aliingia ofisini humo na kumsalimia boss wake huyo na kuchukua nafasi akaketi. "nilitegemea simu yako tena maana mimi sikuwa sawa kabisa jana, mambo yalikuwa shaghala baghala mno vipi mambo yanasemaje?" Joesan alianza mazungumzo. "ni kweli boss nilipanga kukupigia tena lakini usingizi ukanichota na kuja kushtuka ni asubuhi, nikaona siyo mbaya tutakuja kuyaongea ofisini" akatulia kidogo akavuta pumzi na kuendelea. "kwanza nikupe hongera kwa kujua kulea Joesan, Chriss ni bonge la mwanaume, jana Chriss amenifanya kitu kibaya sana sijawahi kufanywa namna ile nikiri hivyo. amenizidi kila idara na anao mzigo utakaotufaa kwenye kazi yetu na.......



    "unataka kuniambia Chriss anafaa kuwa Sex Machine" alidakia Joesan. "kabisa, tena yuko vizuri mno. Anao uwezo binafsi wa kukimiliki kitanda nafikiri tutatumia nguvu kidogo tu ya kumuongezea ili afikie kwenye kiwango tunachokihitaji ili aweze kuwa Sex Machine kamili" akazungumza Suzane. Joesan alipatwa na furaha kubwa sana. Hakutegemea kama angempata Sex MChine kwa haraka kiasi hicho. hakujali kama Chriss ni kijana wake tena alimsomesha kwa gharama kubwa kabisa. Alicho jali kwa wakati huo ni kuzidi kupata pesa na sio utu ambao ndiyo uliomfanya apate jina na sifa kubwa mjini hapo kwa jinsi alivyojitolea sehemu mbalimbali, kwenye vituo vya watoto yatima na katika jamii zisizojiweza. Leo anaharibu nyumbani kwake kwa kumfanya kijana wake mwenyewe kuwa mashine ya ngono. Jambo baya sana. "nakwenda kuirudisha heshima yangu ndani ya kampuni, kila mtu alinidharau baada ya kufa kwa Sex Machine wa kwanza. Sasa huu ni muda wangu wa kuwaonesha kuwa mimi ndiyo Joesan." alijitapa mawazoni Joesan. "Chriss mimi siyo baba yako mzazi hivyo sioni kama utanipunguzia kitu kwenye familia yangu, ninachojali ni pesa na si kitu kingine hivyo kufaa kwako kwenye kazi hii ni ushindi mkubwa sana kwangu" alizidi kuwaza bwana huyo. Mawazo yake yalipotezwa na swali kutoka kwa Suzane. "vipi kwenye masuala ya mapigano?"

    "oooh! Huo ni moto wa kuotea mbali usimuone mtaratibu ukadhani ni bwege? Chriss amefuzu mafunzo mbalimbali ya mapigano huko Uchina, Urusi na Marekani. Yuko fiti sana huyo kijana hadi mimi mwenyewe namhofia" akajibu Joesan. "basi kama ni hivyo sawa kabisa nafikiri Mkuu hata kuwa na la kuongea tena"

    "ni kweli Suzane maana nilikuwa sina amani moyoni mwangu kabisa hasa nikiliwaza hili jambo. Nafikiri sasa tuachane na hili hebu chukua hiyo sample ya barua ukaipitie na uwaandikie wale jamaa waliotaka kuleta mizigo nchini kupitia jina la kampuni yetu kisha utaipitisha kwangu" akasema Joesan na kuinamia kompyuta yake mpakato na kuanza kubofya bofya. Simu yake ya mkononi ikaingia ujumbe mfupi wa maneno. Akaupitia na kutabasamu kama kawaida yake. Akarudisha jibu na kutulia kidogo kabla ya kuparaza kioo cha simu yake na kuiweka sikioni. "Babuu!" alisema Joe. "niambie kaka, naona umeamka na nguvu kidogo vipi?" akasema Babu Ally. "yaa, niko poa sana leo nafikiri Mungu anapenda niendelee kuwa tajiri tu kaka"

    "unataka kuniambia nini tena Joe?" akawahi Babu Ally na kuuliza swali. "niko ofisini kwa sasa lakini baada ya masaa mawili nitakuwa free so tunaweza kupata chakula cha mchana pamoja?" akasema Joe. "yes, of cause"

    "basi tutaongea mengi kwa sasa wacha niwajibike ndugu yangu"

    "poa poa kaka baadae" akajibu Babuu. Alipokata simu hiyo simu nyingine ikaingia lakini hii hata alipoipokea, haikuwa na maongezi mengi sana. Yalikuwa ni maongezi mafupi na ilionekana ni simu ambayo ilileta taarifa fulani yenye kufurahisha kwa Joesan alijawa na furaha muda wote aliokuwa akiongea na simu hiyo. "nimefurahishwa na technique Muliyokuja nayo nadhani hakuna mtu yeyote atakayefahamu jambo lile. Pesa yenu imeshaingia kwenye akaunti zenu mimi na nyinyi hatudaiani" ndivyo alivyosikika akisema Joesan. akakata simu na kuiweka mezani kasha akaigamia kitini mwake na kujizunguusha juu ya kile kiti cha kiofisi. "najua sasa Chriss hawezi kuwa na maswali tena nimefanikiwa kwa namna moja ama nyingine kwa hili. Kitendo cha kumdanganya msomi kama yeye si jambo dogo hata kidogo. Mandi na Sembugi wamenikosha sana, wale wazee sijui wametolea wapi" akawaza Joe na kuangusha cheko la nguvu akisema. "Joesan, nazirudisha upya biashara zangu na hakutakuwa na mawazo tena maana hili ninaloliingiza huku ni jembe" alizidi kupaza sauti kabisa, ni kama alipagawa Joesan. Utajiri kwake ndilo jambo lililokuwa muhimu kuliko maisha ya mtu, alikuwa yuko radhi kuuwa lakini si kuona anafilisika. Alinyanyua macho na kuitazama saa ya ukutani. Muda ulikuwa umesonga sana, akanyanyuka kitini na kuchukua koti lake akatoka ofisini mule. Alichukua gari hadi maeneo ya Tango Cafe akapaki gari na kuelekea ndani ya Cafe hiyo. akaagiza sharubati ya Karoti na kujimiminia tumboni taratibu huku mara kwa mara akionekana akitazama saa yake ya mkononi. Haukupita muda mrefu sana, akafika Babu Ally mahali hapo na kuomba radhi kwa kufika nje ya muda akatwaa nafasi na kuketi. Nae akaagiza Sharubati ya Embe wakawa wanakunywa taratibu wakiwa wanasubiri oda yao ya chakula. "ndiyo ndugu yangu?" alianzisha maongezi Babuu. "safi tu kijana mambo yanakwenda vizuri sasa muda si mrefu tunarudi katika mtandao wetu wa biashara" alizungumza Joe. "wacha weee! unataka kuniambia Sex Machine amepatikana?"

    "ndiyo na ndiyo maana nikasema hivyo, unafikiri nimesema hivyo kwa sababu gani." akaweka kituo na kumtazama rafiki yake huyo usoni kisha akamalizia kwa kusema "na ni kijana hodari sana ni mzuri katika mapambano nadhani hatutakuwa tukisumbuliwa tena na vile vikosi vilivyokuwa vikitupa presha"

    "oooh! Ni jambo zuri Joesan" akaongea Babuu na kuvuta pumzi akasema. "umempatia wapi huyo mtu wa haraka namna hiyo maana jana na leo ni muda mfupi sana?" akauliza Babuu. Joesan akavuta birauli ya sharubati na kupiga kupuo la mwisho lote kinywani mwake. Akahema kwa nguvu sana na kujiweka sawa. "najua utashangaa" akasema. "lakini yote ya yote pesa ndiyo kila kitu kwangu"

    "unamaanisha nini?" akauliza Babuu kwa kuto kumuelewa bwana huyo. "ni kijana wangu!" akashusha pumzi zile alizozivuta awali na kuuwegamiza mgongo wake kitini. Macho yalimtoka Babuu, masikio yake aliona kama yana mdanganya. Akaweka mikono yake mezani na kumuinamia Joesan na kuuliza kwa karibu kabisa. "Chri........Chri ss ndiyo amekuwa Sex machine? no, Joesan hatuendi hivyo"

    "Babu Ally, utajiri kwangu unathamani kubwa kuliko maisha ya kiumbe chochote hapa duniani, kwahiyo kumfanya Chriss Sex Machine si jambo baya na wala sioni kama ubaya wake utakuja kutokea hapo baadae, pia hakuna madhara kwangu wala hakutanipunguzia kitu wewe unaogopa nini" aliongea Joesan. lakini Joe ukumbuke kuwa uliahidi nini, ukumbuke Joesan. Chriss siyo wa kustahili adhabu hiyo maana hiyo ni kama adhabu. Ulimuahidi nini Isihaq?" aliuliza Babuu na Joesan akajibu na kumwambia "nakumbuka lakini hilo siyo la kunizuia mimi kamwe. Unajua wakati mwingine Babuu, siyo kila ahadi unayoahidi uitimize. Nyingine zinakuwa ni geresha tu za maisha hivi wewe unajua sababu ya mimi kumsomesaha huyu kijana kwa gharama kubwa namna hii?"

    "najua ndyo" alijibu Babuu. "ni ipi?" aliuliza tena Joe. Babuu akajibu. "ni kwasababu ni ndani ya ahadi zako kwa Chriss pindi tu ulipo muulia baba yake"

    "ha ha ha haaa! Kweli Babuu wewe unajifanya mjahidina sana tena unajifanya ni wale wasomi wa juu kabisa katika dini. Hivi inawezekana vipi," akaweka koma na kutulia kama anayesiliza kitu kisha akaendelea na alipokomea. "inawezekana vipi nimuangamize mtu kwa ajili ya kupora mali zake, halafu eti aje arithi kijana wake. Wrong Babuu, mawazo yako hayaendani na kile ninachokifiria mimi, mimi nilichukua jukumu la kumsomesha Chriss ili tu nije kumtumia katika mambo yangu. Ilikuwa ni lazima gharama zangu za kumsomesha zirudi na ndiyo maana nikampa mafunzo ya mapigano pia" alisema Joesan na kucheka kwa madaha sana. Babuu alitulia kimya akisikiliza maneno hayo. alinyanyua birauli akapiga funda jingine kubwa la sharubati na kuirudisha birauli hiyo mezani ikiwa tupu. Akagoa kidogo na kusema. "Kaa ukijua Chriss akijua hili hatakuacha hai hata kidogo ni lazima atalipiza kisasi cha wazazi wake"

    "siwezi kumpa hiyo nafasi hata kidogo na......!" akakwama kidogo kisha akanyanyuka na kumuinamia Babuu akaendelea. "na nitauwa kila atakaye karibiana na mtu huyu am Joesan" akapiga kifua chake kwa nguvu na kuondoka kwa kasi. "Joesan amekuwa katili sana siku hizi mimi nilijua anaachana na tabia hii kumbe bado kabisa" aliwaza Babuu huku akimtazama rafiki yake akiwa anatoka nje ya jingo hilo. Joesan aliingia garini mwake na kutulia, akalegeza tai na kujilaza kitini. "Babuu anamaana gani kusema kuwa Chriss anaweza kujua kuwa mimi ndiye niliye wauwa wazazi wake. Hii siri ni ya siku nyngi sana na mimi na yeye tu ndiyo tunaifahamu, anaweza kuwa nyoka hatari sana kama nitamuacha" aliwaza Joesan. Akawasha gari na kuliondoa kwa mwendo wa taratibu. "Babuu wewe ni rafiki yangu wa siku nyingi sana lakini sikuamini tena na taratibu zangu zinasema yeyote nisiyemuamini hana haki ya kuishi. Utanisamehe lakini ni lazima kabla ya kesho uwe maiti, wewe si mwema tena kwangu" akawaza tena Joesan, akabadili gear na kukanyaga mafuta injini ya gari ikalalamika.



    **********************************************



    Usiku wa siku hiyo Babuu akiwa ametulia kwenye hoteli aliyofikia akiwa ameyaelekeza macho yake luningani akifuatilia taarifa ya habari, mlango wa chumba alichopo ukagongwa kwa utaratibu mara tatu. Babuu akanyanyuka na kwenda kufungua mlango. Akaingia mtu mmoja aliyevaa kofia pana ya chepeo iliyoyafunika macho yake kisha mtu huyo akaivua hiyo kofia na kumtazama Babuu usoni. "Joesan, mbona usiku bila taarifa nini tena ndugu yangu!?" aliuliza kwa mshangao Babuu baada ya kuiyona sura ya mtu huyo. "umefanya vizuri kunifahamu maana mimi na wewe hatuto fahamiana tena baada ya hapa" akasema Joesan kwa upole sana. "sijakuelewa Joesan"

    "utanielewa tu Babuu" akaongea Joe na kumtole rafiki yake wa siku nyingi bomba la bastola na kumuelekezea usoni. "nini tena Joesan" alipatwa na mshangao wa hali ya juu sana na macho kumtoka. Joesan akarudi nyuma hatua tatu na kusema. "nimeamua kukuuwa ili Chriss asije kujua chochote kuhusu kifo cha wazazi wake napenda maisha yake yote anitumikie mimi hadi pale nitakapoamua kumuua kwa mikono yangu mwenyewe na napenda ubongo wake ubaki na picha moja tu kwamba wazazi wake wamefariki kwa ajali. Nakuuwa huku naumia moyoni, nakupenda sana Babuu na nitakukumbuka siku zote" akamaliza na kuiruhusu bastola ile ifanye yake. Risasi mbili zikalichapa paji la uso la Babuu, alama ya nyota ikajitokeza na Babuu kushindwa kuubeba tena mwili wake. akadondoka chini kama mzigo. Joesan aliivaa ile kofia tena na kutoka mule ndani na kutoweka pasipo kujulikana.



    Siku ya kwanza ikaisha, ya pili ikawadia ambayo ndiyo siku ya ahadi ya kumpeleka Sex Machine. Chriss jiandae haraka nikukute kwenye gari saa mbili natakiwa niwepo kazini nipo nje ya muda" alisema Joesan. "niko tayari Uncle nakusubiri wewe tu" akajibu Chriss...........



    akajibu Chriss. wakaelekea maegeshoni na kuingia garini. Chriss ndiye aliyekuwa dereva, akalito langoni na kuikamata barabara ya mjini. hawakuchukua muda mrefu sana kufika mjini. Chriss akapaki gari nje ya jingo kubwa sana, wakashuka na Joesan kumuongoza kijana wake kuingia ndani ya jingo hilo. Alifika sehemu ambapo kulikuwa na chumba kikubwa chenye samani mbalimbali za kileo, Joesan akamwambia Chriss asubiri hapo kisha yeye akachukua lifti na kupanda flow ya pili. Alipofika flow hiyo, alitoka na kuingia kwenye chumba fulani ambako aliwakuta wadada watatu wakipiga soga, akawasalimia na kuwauliza mahali Suzane alipo kwani sehemu yake ya kazi hakumkuta. Akaambiwa kuwa yupo kwenye Computer room lakini kabla hajachukua uelekeo wa huko, Suzane akatokea akiwa na tabasamu usoni kama ilivyo ada yake. "nimekuona tangu ulipokuwa nje, ila kukawa na kijikazi kidogo ambacho nilikuwa nakimalizia" aliongea Suzane akatulia kidogo na kumalizia "wewe elekea kwenye chumba cha mawasiliano kwa ajili ya kumpa taarifa mkuu, mimi acha nimfuate Chriss na wote tutakutana katika chumba maalumu kabla mambo mengine hayajafuata."

    "ok" Joesan akajibu na kuingia katika chumba fulani huku Suzane akichukua lifti kurudi flow ya kwanza. "ooh! Chriss, karibu sana my love" aliongea Suzane huku akimpa mkono Chriss ambaye naye alisimama na kuupokea mkono huo akisema "nimekaribia Suzane, leo nimevamia kazini kwenu ni jingo zuri sana aisee hongereni sana"

    "hongera ya nini sasa?" akauliza Suzane. Chriss akasema " si ya kufanya kazi kwenye jingo zuri na lenye hadhi" aliongea Chriss huku akicheka. "vipi kama utapata nafasi ya kufanya kazi hapa?" likawa ni swali la mtego kutoka kwa Suzy. "unadhani Uncle atapenda nifanye kazi anapofanyia yeye?"

    "si jibu la swali nililokuuliza Chriss wewe ni msomi bwana sasa mbona unajibu kama huna Master kwenye ubongo wako" akasema Suzane huku akitabasamu zaidi. "ooh! samahani Suzy, lakini sidhani kama kuna mtu anaweza kukataa kufanya kazi kwenye kampuni nzuri na yenye sifa kubwa Afrika mashariki kama yenu, ni bahati ya mtende kuota jangwani hiyo" akasema Chriss na kumfanya Suzy acheke kwa nguvu sana. Alipoacha kucheka, alimuomba Chriss amfuate. Chriss hakupinga alimfuata, wakavipita vyumba kadhaa na kuingia kwenye lifti na kuiruhusu iwapeleke flow namba tatu. walipofika mlango wa lifti hiyo ukafunguka wakatoka na kungia ndani ya chumba kimoja kizuri sana kilichosheheni vifaa vya kiofisi.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa upande wa Joesan baada ya kuingia chumba cha mawasiliano, alikaa kitina na kutulia kimya na mara hiyo hiyo sauti ikasikika ikisema. "kuna habari gani nzuri Joesan?" Joesan aliiweka suti yake vizuri na kujibu kwa madaha makubwa "ahadi yangu nimekwenda kuitimiza leo mkuu"

    "Joesan utanifanya niwe katili sana kwako endapo kama unajaribu kunidanganya, ukumbuke kuwa nimekuvumilia kwa muda mrefu"

    "najua mkuu na ndiyo maana niko hapa kwa kujiamini zaidi" alijitapa Joe. "any way fanya linalowezekana kesho asubuhi angie kwenye jaribio la kwanza" ikahitimisha sauti hiyo ya mkuu na mawasiliano yakakata. Joe hakuwa na muda wa kupoteza tena alijua ni wapi kwa kuelekea. Alitoka mule chumbani na kuelekea kwenye chumba ambacho alikuwamo Suzane na Chriss. "mtanisamehe kwa kuwachelewesha jamani, nilikuwa namalizia jambo fulani hapo chini enhe! Vipi lakini" aliongea Joesan. "hujachelewa sana Boss" akasema Suzy na kumgeukia Chriss na kumwambia. "Chriss, kama nilivyokuambia kuwa ujio wako wa leo hapa si wa bure hivyo kuna jambo la msingi sana ambalo wewe limekuleta." aliweka tuo kidogo na kumtazama Joesan kisha akaendelea. "kuna kazi....!"

    "kuna kazi!?" ni kama hakuamini Chriss alichokisikia. "ndiyo ni kazi itakayokuingizia pesa nyingi sana ambazo hukutarajia kuzipata"

    "ni kazi gani hiyo?" Chriss akawahi kwa swali ambalo lilimfanya Suzane ameze mate kwanza kabla ya kuzungumza. "kabla hujaijua hiyo kazi yenyewa ni vema kama utafahamu haya machache nitakayo kueleza." akaweka tuo na kuendelea "Chriss, utajiri una siri nyingi sana, utajiri unaficha mengi usidhani kuna tajiri duniani anayepata pesa kwa njia halali. Matajiri wengi duniani wanaingiza pesa kwa njia haramu na njia hizo ndizo zinazomfanya mtu kuwa tajiri pia kumpa heshima kubwa. Hivyo basi, kazi iliyopo hapa kama utapenda kuifanya ni kazi itakayokwenda kuyabadilisha maisha yako kabisa" akatulia Suzane ili kuyaruhusu maneno yale yapenye panapo stahiki. Chriss alikuwa ametulia kimya akiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kuhusu kazi hiyo. Joesan ameomba nafasi hii ambayo ni aghalabu sana kuipata mara nyingi nafasi hii hutolewa kwa watu maalumu na kampuni inafanya hivyo ili kila kitu kiende kwa usiri mkubwa na kwa kuwa kampuni inamuamini sana mjomba wako, ikaamua kumpa nafasi hiyo kwa masharti makubwa sana. Chriss unatakiwa kuwa SEX MACHINE."

    "whaaat!!!!?" akang'aka Chriss baada ya kusikia kauli hiyo ni wazi hakuielewa. Ni vipi awe Sex Machine, inamaana hiyo ndiyo kazi hasa iliyomfanya kufikishwa mahali hapo? Yalikuwa ni maswali mengi sana aliyojiuliza. "Suzane!" akaita Chriss. Suzane akamuangalia Chriss. "sijakuelewa bado?" akaongea Chriss. "najua kuwa ni vigumu kuelewa lakini ukiamua kuifanya kazi niliyokuambia nakuhakikishia kuwa hutakuwa Chriss huyu wa leo" akaongea Suzane. "mjomba ni kweli analosema madam hapa?" akauliza Chriss. "ndiyo Chriss, najua kuwa utaiona ni kazi ya kishenzi sana lakini ni kazi yenye utajiri mkubwa. Vijana wengi Afrika na dunia wanatajirishwa na kazi hii, nimejipendekeza kwenye kampuni ilimradi na wewe kijana wangu upate hiyo nafasi inakufaa sana. Wewe ni msomi mkubwa na unaujuzi ambao utashinda kwenye comperition mbalimbali" aliongea Joesan. Chriss alipinga vikali sana. Hakutaka kabisa kufanya kazi hiyo aliyoiita ya kishenzi na kidhalilishaji. Wakatumia ushawishi wa kila namna na aina mbalimbali ili kuweza kumteka kijana huyo ki fikra lakini hawakufanikiwa. "niko radhi kwenda kuishi popote pale kama utakuwa umechoka kuishi na mimi mjomba lakini si kufanya kazi hiyo" alifikia uwamuzi wa kuongea maneno hayo Chriss. Alidhamiria kabisa kuwa hawezi kufanya hiyo kazi na yuko radhi hata kama ni kufukuzwa nyumbani. Joesan alichoka. Mategemeo yake ya kudhani kuwa kazi itakuwa rahisi ya kumshawishi kijana huyo iligonga mwamba. "nimejiingiza pabaya sana Suzane, sijui adhabu yangu ni ipi. Nilidhani nafanya hivi kumsaidia kijana wangu kumbe najiharibia mwenyewe, Chriss mwanangu naomba unisamehe kwa kukulazimisha kitu usicho kipenda ila....!" hakumalizia Joesan. Alikuwa mnyonge kupita kawaida na baada ya kuongea kauli ile ambayo iliishia katikati, alinyanyuka kinyonge sana na kuwapa mgongo. Alipiga hatua tatu mbele na kugeuka kuwaangalia. Macho ya Joesan yalijaa machozi mengi sana ishara ya mtu aliyekuwa katika majonzi mazito kasha akageuka na kutoka mule ofisini. Chriss hali ile kwake ilikuwa ni ngeni kabisa, hakuwahi kumuona mjomba wake akiwa katika hali ile hata siku moja ikambidi kumuuliza Suzane, kulikoni na ni nini kinachoendelea mahali hapo. "hata mimi naishangaa hali hii huwenda kuna jambo kubwa sana litamtokea si kawaida hii" aliongea Suzane. Kimya kikatanda mahali hapo kila mmoja alitafakari lake. Suzane akavunja ukimya na kumwambia Chriss ni nini anafikiria kwa wakati huo. Chriss akamjibu kuwa hana analolifikiria na hawezi kubadili msimamo wake hata iweje. Suzane akagonga mwamba kabisa na hakuwa na jinsi tena. Ushawishi wake kwa kijana huyo mwenye msimamo mkali ulifika mwisho. Wakahamia kwenye maongezi mengine na kuliacha jambo hilo lakini hali ya mabadiliko ya Joesan bado ilikuwa ikimtesa sana Chriss alikuwa akijiuliza mara kwa mara mawazoni nini kimembadilisha ghafla namna ile, ni yeye kukataa kuwa Mashine ya ngono? Na kama si hivyo ni nini sasa? jibu ndilo lilikuwa mtihani. Akamgeukia Suzane na kumuuliza "unaweza kujua ni wapi mjomba atakuwa ameelekea kwa sasa maana hali aliyoondoka nayo kwa kweli na maneno aliyoyaongea yananitia hofu kidogo" Suzane alimuangalia Chriss kisha akayakwepesha macho yake na kuangalia pembebi akasema. "unaloliongea ni la msingi sana Chriss hebu nisubiri hapa nikamtafute nijue wapi ameelekea" kasha akanyanyuka na kuondoka akimuacha Chriss katika mawazo. "kinachopangwa na sisi ni lazima kitimie, hatuwezi kufeli hata kidogo" alisema mawazoni Suzane alipokuwa akitoka ndani ya chumba hicho. Chriss alisubiri kwa muda wa kama dakika tano, Suzane akarudi na moja kwa moja alisimama kijana huyo ili kujua ni haki gani au ni kipi kilichosababisha Mjomba wake kuwa katika hali ile ya majonzi. Suzane hakusema kitu bali alitulia tuli na kila alipotaka kusema ni kama kulikuwa kuna donge fulani linamzuia kooni mwake, alichokifanya ni kumshika mkono Chriss na kutoka nae mule ndani. Waliingia katika chunba kimoja ambacho kilikuwa na giza sana na walipoingia tu taa za rangi ya kibuluu zikawaka. Kilikuwa ni chumba kidogo sana ambacho hakikuwa na kitu chochote na pia hakikuwa na hata sehemu ya kukalia. "hukupaswa kuja huku Chriss lakini kwasababu ya mapenzi yangu kwako imenibidi ni kulete ili uweze kuona mjomba wako anavyoteseka sababu yako" aliongea Suzane na kupiga hatua tatu mbele akabonfya kitufe fulani na pazia kubwa jeupe likajivuta kwa kila upande. Mbele macho ya Chriss yaliona kioo kikubwa na upande wa pili kukiwa na mtu aliyekuwa amefunikwa kwa mfuko mweusi huku kukiwa na watu wawili walioziba sura zao wakionekana wakimpa mateso makali mtu huyo. mfuko ule aliokuwa amefunikwa ukafunuliwa. Sura ya Joesan iliyokuwa inavuja damu nyingi ilionekana. Kipigo kikali kilikuwa kikiendelea, hakupewa hata nafasi ya kupumua Joesan. Alipiga kelele sana japo zilikuwa hazisikiki kutokana na uzito wa kile kioo lakini ilonesha dhahiri mtu huyo kuwepo katika maumivu makali. mtu mmoja miongoni mwa wale watesaji alishika waya fulani na kuziunganisha kwenye umeme. Joesan alionekana akifulukuta kutokana na shoti kali aliyokuwa anipata mahali hapo. "nooooo!!" alipiga kelele Chriss na kukivamia kile kioo na kuanza kukitandika makonde mazito huku akizidi kupiga kelele kuhakikisha watu wale wanaacha lile zoezi la kumtesa mjomba wake. Ni kama alikuwa anacheza mchezo wa kuigiza mbele ya kioo kile kwani hata angekuja na bastola asingeweza kukipa hata ufa kioo hicho acha huko kukipasua. Watesaji wale walikuwa wakizidi kumtesa kwa sifa kubwa sana tena walikuwa wakitoa nateso huku wakimcheka kijana huyo kwa jinsi anavyokiparamia hicho kioo. Chriss naye hakuchoka kukipelekea makonde kioo kile hadi mikono yake ikawa inavuja damu kabisa. "Chriss" Suzane aliita na kumshika bega Chriss akasema huku akiwa anatokwa na machozi si utani. "huwezi kuvunja hicho kioo my love, ni kioo kigumu sana, hicho kioo kimetengenezwa na material ya kuzui risasi sasa unadhani wewe utaweza kukivunja?"............



    "wanataka nini sasa waniachie mjomba wangu Suzane na ni kwa nini wanafanya haya yote?" aliuliza Chriss akiwa analia kabisa. "nilikuambia kuwa kampuni ilimuamini na kujua kuwa hawawezi kumuangusha kwani mtu huyo ambaye ni Sex Machine ni muhimu sana na waliamini watafanikisha kuingia kwenye ushindani mkubwa wa kibiashara. Kitendo cha wewe kukataa, kilimfanya Joesan ashindwe kukulazimisha nadhani unajua ni kiasi gani Joesan anavyo kupenda na hapendi ukumbwe na matatizo. Akaamua kuiambia kampuni kuwa ameshindwa kumleta huyo Sex Machine. Sikutegemea kama wangefikia uamuzi huu na nilipouliza sababu za kumfanya hivi, pale nilipokuwa nimekuacha pale ofisini, nikaambiwa kuwa mkuu amekasirika sana na amekichukulia kitendo hicho ni cha kitoto na dharau kubwa hivyo akatoa amri Joesan ateswe hadi kifo n....!" alishindwa kuendelea kuongea Suzane. Kilio kikashika hatamu ni kama alisemalo mahali hapo lilikuwa na ukweli asilimia mia. "unataka kuniambia mjomba anateswa hadi kifo?" aliuliza Joesan. Suzane alishindwa kujibu kwa kujifanya kilio kimemzidi. Chriss alipandwa na hasira kali na kukigeukia kile kioo, alikiparamia huku anapiga kelele mtindo mmoja kisha amkamgeukia tena Suzane. "huyo mkuu ni nani na yuko wapi?" lilikuwa ni swali lililobebwa na sauti nzito hadi Suzane akaogopa. "hajawahi kuonekana hata nywele zake zaidi ya sauti pekee" alijibu Suzane na kutoa macho ya mshangao kule kwenye kioo na Chriss alipogeuka, alimshuhudi mjomba wake akiwa ameangusha shingo upande mmoja kuonesha kuwa yupo katika hali mbaya kupitiliza. "nini wanataka Suzane, wanataka nini waniachie mjomba wangu watamuua kweli?" alisema Chriss huku akiwa anamtikisa Suzane. Dada huyo alitabasamum moyoni furaha ikiwa kubwa kabisa. "kwisha jeuri yako" alisema moyoni namna hiyo huku akiwa amebeba huzuni ya bandia usoni. "ni wewe kukubali kuwa Sex Machine" alisema Suzane. Chriss akataka kugoma lakini alipotazama kwenye kile kioo, aliona mjomba wake akiwa kashikiwa bastola tayari kumalizwa kabisa. Upendo alionao Chriss kwa mjomba wake ni mkubwa kupita kiasi. alifikiria mambo mengi, aliifikiria elimu aliyopewa, aliyafikiria malezi mazuri jinsi alivyokuwa analelewa na bwana huyo kama ni mtoto wa kumzaa mwenyewe. Ni vipi basi angeamua kumuacha pindi tu wazazi wake walipokufa, ni nani basi angejitolea na kumlea, kumsomesha hadi kufikia elemu ya juu kabisa. Mbaya zaidi leo pia anaamua kufa kwa sababu yake, Joesan alikuwa ni kama mzazi wake wa maisha yake, hakuna ambaye ataruhusu mzazi wake auwawe mbele ya macho yake hata kama itakuaje. "waambie waache kumuuwa mjomba Suzane nime.......!" alikwama Chriss, machozi ya uchungu yalimtoka anaamua kuwa Sex Machine kwa sababu ya maisha ya mtu anayempenda. Chriss alifumba macho kwa uchungu mkubwa na kuikunja ngumi yake ya mkono wa kushoto akimalizia kusema "nimekubali kuwa Sex Machine" Suzane alitamani aruke kwa furaha lakini isinge leta picha nzuri. Furaha aliyokuwa nayo ni kubwa sana. Aliwapa ishara wale watu wasimamishe zoezi walilokuwa wanalifanya. Watesaji wale wakaacha na kuzirudisha silaha zao kibindoni kisha wakamfungua pale kwenye kiti na kumtoa. Kitu cha kwanza alichokihitaji Chriss ni kumuona mjomba wake kwanza na si kitu kingine. Suzane akamchukua na kutoka nae hadi kwenye chumba kingine hapa akamwambia amsubiri, hakupinga Chriss. Suzane akachepuka kona kadhaa na kunyanyua kifaa cha mawasiliano. "Boss Chriss anahitaji kukuona" akasema. Upande wa pili ukamjibu kuwa aelekee chumba cha tiba. Akakata mawasiliano hayo Suzane na kurudi alipomuacha Chriss. "nifuate tafadhali" aliongea Suzane na wakaongozana hadi ilipo lifti wakaingia na kushuka chini zaidi hadi flow namba mbili ambayo ipo chini ya ardhi. lift ikafunguka wakatoka na kukifuata kikorido kidogo kisha wakaingia kwenye chumba kimoja. Walimkuta Joesan akiwa taabani kabisa sura yake ilikuwa inamajeraha ya kutosha huku akiwa amevimba mdomo. Chriss alikimbilia hadi hapo kwenye kitanda na kupiga magoti. "mjomba uko salama kweli mjomba?" aliuliza Chriss. "usijali mjomba niko salama" aliongea Joesan akionekana kupambana na maumivu makali sana. "nisamehe sana mjomba sikujua kama yangekukuta haya yote ningejua kama watafikia hatua ya kukufanya hivi nisingebishana na wewe, nisamehe sana mjomba wangu" aliomba radhi Chriss huku machozi yakimbubujika ni wazi kabisa jambo lile lilikuwa likiuumiza sana moyo wake. Joesan alimwambia asiwe na shaka ilhali amekubali kuwa Sex Machine basi hawawezi tena kumgusa kwani hiyo ndiyo ikiyokuwa sababu kubwa ya mateso yale yote.



    ILIVYOKUWA.



    Joesan baada ya kutoka kwenye ile ofisi akiwa katika hali ya majonzi, alikwenda kwenye chumba kinacho tumika kwa uendeshaji wa mitambo na suala hilo, Suzane alikuwa akilifahanu kabisa na walipanga hivyo kwamba Chriss akiwa mbishi kuelewa, basi wangetumia njia hiyo. Alipofika kwenye kile chumba alimkuta mtaalamu wa kuindesha mitambo hiyo iliyokuwa ikitumia Computer. Joesan akamueleza kitu anacho kihitaji. Na alieleza kila kitu kwa mtaalamu huyo na kumfanya mtaalamu huyo afurahi sana kwani haikuwa kazi ngunu kwake. wakaitwa vijana wawili wakavalishwa maski maalumu na wote wakakalishwa kwenye viti maalumu ambavyo vilikuwa maalumu kwa kazi hiyo. Wakafungwa na mikanda kisha wakafunikwa na mfuniko wa kioo. Mtaalamu huyo akaanza kazi yake ya kuchezea kompyuta. Akavuta picha tatu ambazo zilikuwa ni za wale waliofungiwa kwenye ule mtambo na kuanza kuzichezesha picha hizo mithili ya mtu achezaye gemu. kila kilichokuwa kinaendea hapo ndicho kilichokuwa kinatazamwa na Chriss pamoja na Suzane kule ambako Chriss alipelekwa. Joesan hakuwa akipata mateso yoyote kilichokuwa kikifanyika ni usanii tu na si kitu kingine. Chriss alivyokubali kuwa sasa yuko tayari kuwa Sex Machine, yule mtaalamu aliona kupitia kwenye mashine yake hivyo kuamua kuusitisha mchezo huo kisha wakamuingiza Joesan kwenye chumba ambacho alifanyiwa opareshen ndogo na kumfanya aonekane ni mtu aliyepata mateso makali. Lilikuwa ni zoezi la muda mfupi sana wala halikuchukua hata dakika mbili kisha akaelekea katika chumba cha matibabu ambako ndiko Chriss alipomkuta akidhani ni mgonjwa kumbe alichezewa picha la kuigiza ili kuweza kumuingiza mkenge na kweli aliuingia bila ya kupenda. "muda umekwenda sana Chriss nadhani sasa ungekwenda nyumbani" aliongea Joesan. "wewe unabaki hapa Uncle?"

    "ndiyo daktari amesema ni vema kama leo ningepumzika hapa kwa ajili ya matibabu zaidi nafikiri hadi kesho ndiyo nitaweza kuruhusiwa"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "tuta baki wote mjomba ziwezi kwenda nyumbani unafikiri nitamjibu vipi shangazi akiniuliza kuhusu wewe" aliongea Chriss. "sawa kama ni hivyo lakini kama unavyojua kuwa hii ni kampuni kubwa hivyo kila kitu wanasimamia wenyewe hutoruhusiwa kubaki hapa na mimi watakachofanya watakupa chumba kingine ulale na si hapa"

    "haina shida mjomba ni sawa tu nitalala lakini si kurudi nyumbani bila wewe" alizungumza Chriss na kukubaliana hivyo. Muda huohuo daktari akaingia na kumuoba Chriss atoke kwani haruhusiwi tena kuwepo mahali hapo. Joesan akamueleza daktari huyo na kumuambia Chriss apewe mahali pa kupumzika. Daktari akatoka na Chriss hadi sehemu ya juu ya lile jingo na kuoneshwa chumba atakacho lala kisha daktari huyo akatoka na kumuacha kijana huyo akiwa ni mwingi wa mawazo sana. "umenisaidia sana mjomba, siwezi kukuacha ufe kizembe nilipa kukulinda pindi tu uliponipeleka China kuchukua mafunzo makali ya kijeshi ambayo yalikuwa ni ya siri sana hukuishia hapo, pia ukanipeleka Urusi na kumalizia na Cuba kote huko ulitaka nipate ujuzi ili nije kuwa hodari zaidi." aliwaza Chriss mara tu baada ya kutoka bafuni na kujitupa kitandani. Akaendelea kuutiririsha mkanda huo wa mawazo "nimekuwa hodari kweli uncle Joesan, hakuna kinachonitisha mbele yangu. Sasa kwanini mtu muhimu kama wewe ufe ningali hai. Nakumbuka kuna kauli yako unapenda kuniambia uncle, 'the second name may be first' ukimaanisha kuwa jina la pili linaweza kuwa la kwanza sasa nahisi ulikuwa unamaana kubwa sana, labda leo kidogo naweza kuihisi maana hiyo kuwa mimi nimekuwa wewe sasa" ndivyo alivyokuwa akiwaza Chriss lakini kwa upande wa Joesan naye mambo yalikuwa mazuri kabisa na yalikuwa yakienda kama alivyo panga. "Suzane wewe ni mtu muhimu sana kwangu kila kitu sasa kina kwenda vizuri" alisema Joesan. "usiwaze Boss, kama unakumbuka nilichowahi kukuambia, nilisema sisi hatujawahi kushindwa na binadamu wa kawaida. Chriss anaamini uko hoi kwa mateso yale aliyoyaona kumbe hata uchovu huna ha ha haaa!" aliongea Suzane na kuachia cheko la nguvu. Joesan alimshika mwanadada huyo mkono na kutoka naye nje ya jingo hilo, walifika hadi kwenye gari ya Joesan na kuzidi kuongea. "kesho asubuhi nitawahi lakini nataka anikute fiti kidogo ili tuweze kuwatangazia wafanya kazi wote kuwa Sex Machine amepatikana na baada ya hapo Chriss atapelekwa kwenye test ya kwanza" akasema Joesan. Suzy akatingisha kichwa na kusema "vipi lakini maana test hiyo mimi naiogopa sana, unaimani naye katika hilo?"

    "hiyo kesho ikifika ndio utajua kuwa Chriss ni nani" akasema Joesan na kuingia garini na safari ikaanza. Hakuchukua uelekeo wa nyumbani kwake, aliiongoza gari yake hadi maeneo ya Mazimbu road. Alikanyaga mafuta na kuifanya gari yake kuongeza kasi ya maana kisha akaiacha barabara inayoelekea Kihonda akaingia kulia huku akiwa anapunguza mwendo taratibu, alikuja kusimama kwenye nyumba moja iliyokuwa imejitenga sana. Akateremka garini na kuuelekea mlango wa nyumba hiyo ambayo haikuwa na uzio wowote. Akafungua na kuingia ndani, ilikuwa ni nyumba nzuri sana kwa ndani, giza lilikuwa limetanda mule ndani hivyo aliwasha taa na kuingia kwenye Chumba kimoja ambacho kilikuwa kama ofisi. Akavuta kiti na kukaa kisha akaifunua computer iliyopo mezani hapo na kuiwasha kisha akaingiza securit code na kuandika ujumbe. "kiongozi nimekamilisha nilichokipanga kwa muda mrefu tutakutana Nairobi siku ya jumamosi" akautuma ujumbe huo na kuufoward kwa kila aliyepanga kumfikishia ujumbe huo. Alipomaliza akanyanyua simu yake ya siri na kupiga namba fulani akaiweka sikioni. "ndiyo kiongozi?" upande wa pili wa simu uliongea. "yaa, saa mbili usiku leo tukutane Tango restaurant" akasema Joesan kisha akakata simu bila kusikiliza jibu la upande wa pili. Alitoka ndani ya nyumba hiyo na kurudi zake mjini. Moja kwa moja alielekea Tango kwa ajili ya kuisubiri miadi ya mtu aliyempigia simu. Aliagiza kinywaji akawa anakimimina taratibu tumboni mwake, dakika kama kumi na tano mbele, mtu aliyekuwa akisubiriwa alifika na kumkuta mwenyeji wake akizungumza na kinywaji laini. "unakwenda kwa wakati Mandi".................................





    alisema Joesan. "ni kawaida yangu kufika kwa wakati kwenye miadi ya aina yoyote ile, enhe, niambie bwana mkubwa" aliongea Mandi. "kwanza nikupe pongezi kwa kuweza kucheza tric ya maana, wewe ni mtu mbaya sana Mandi sijategemea kama utakuja na technique ile, hivi ulifikiria nini aisee? Na wale wazee mliwatoa wapi wewe na Sembugi, unajua sikutegemea kama mambo yangekuwa rahisi kiasi kile. wazee wale, waliubeba uhalisia kabisa hadi Chriss akajua ni kweli kumbe watu tumecheza dili na ile miili ikaenda kutupwa milimani huko watu tufanye yetu"

    "unajua brother kazi hizi tumezianza kitambo sana hivyo tumekuwa ni ma-professional. Kwa kazi ndogo kama ile ya kudanganya au kuigiza kama mzazi si kazi ya kitoto sana" alijitapa Mandi. "ni kweli ni kweli, aah vipi, mimina kinywaji au?" aliuliza Joesan baada ya kuona anakimeng'enyua kinywaji hicho peke yake. Mandi akasema kuwa hajisikii kunywa chochote kwani tumbo lake halikuwa sawa kabisa. "ok, nilichokuitia hapa Mandi kuna kazi iko mbele inakuja nadhani hii itakuwa ngumu kidogo lakini kwa kuwa wewe nakufahamu, huwezi kuniangusha"

    "ni kazi gani hiyo boss?" akadakia Mandi. "usiwe na haraka nitakupa taarifa ya siku husika na aina ya kazi" alihitimisha Joesan na kutoa kijitabu cha benki na kuandika cheque kisha akamkabidhi Mandi cheque hio na kusema. "hayo ni malipo ya kazi ile ya kufanikisha kumzuga Chriss juu ya vifo vya wale malaya zake maana bila kufanya vile angenicheleweshea kazi yangu, hiyo ni yako tu achana na ile ambayo nililipa kwa wote. Hii ni pongezi kwako na hata Sembugi nitamuita nimpe pongezi yake. Ninyi ni vijana wangu wa kazi bwana na mmefanya vema sana nitakutafuta wewe na vijana wako siku moja kwa ajili ya kukata maji tu mmenifurahisha sana" alipokwisha kusema hayo, alinyanyuka na kumuacha Mandi mezani hapo yeye akaelekea kwenye gari na kuelekea zake nyumbani huku akiwaza mengi na kubwa ikiwa ni safari ya Nairobi ambayo ilikuwa inampa wakati mgumu wa kuamua ni lini aende.

    "naweza hata kuwapigia simu wale jamaa kuwa sitakwenda huko Nairobi, nimezingirwa na kazi nyingi sana. Naweza hata kutuma mzigo kwa njia nyingine" aliwaza Joesan mara baada ya kukumbuka wale jaama aliongea nao kwenye simu.



    Asubuhi kulipokucha watu walikutana tena ndani ya kampuni. ilikuwa ni kwenye ukumbi wa mikutano kama kawaida, wafanya kazi wote wa kampuni hiyo walikuwepo hapo wakisubiri utambulisho wa Sex Machine mpya. "mabibi na mabwana, leo ni siku tofauti kidogo kwani tumekutana kwa namna tofauti pia. Najua mlikuwa mkiisubiria sana siku hii ili muweze kumjua Sex Machine mpya kabisa ndani ya kampuni hii" alisema Joesan akiwa katika suti safi ya rangi ya kijivu kama ilivyo ada yake. Alijikohoza kuweka koo sawa na kuendelea kuongea. "ninayofuraha kuwaambia kuwa Sex Machine amepatikana na amekamilika kila idara na kwa muda huu niwape fursa ya kuweza kumuona mtu huyo" makofi yakapigwa kwa mikupuo mitatu kisha ukimya ukafuatia. Wote wakageukia ulipo mlango wa kuingilia ukumbini hapo na kumuona Suzane akiingia na kijana mtanashati, mrefu kiasi na mwenye umbo la kuvutia hakika kwa mtazamo wa haraka kijana huyo alifiti kabisa katika kazi iliyokusudiwa. Aliletwa hadi mbele kabisa na kusimama kisha kuwageukia wafanya kazi hao na kuonesha sura ya tabasamu. Makofi yakarindima tena, wanawake ndiyo walionekana kuvutiwa zaidi na kijana huyo. "anaitwa Christiano Robin Isaya lakini jina la pili linaweza kuwa la kwanza inategemea wewe utakavyopenda kumuita" aliongea kwa mbwembwe sana Joesan. Baada ya utambulisho huo kila mmoja pale alijua nini kinafuata. "Rafael hivi ukimuangalia huyu kijana anaweza kufaa kwenye hii kazi?" mzee mgobo kama kawaida yake alimtupia mzee mwenzie swali. Mzee huyu alionekana kumpinga sana Joesan, pale Joesan anapokosea kwake ilikuwa ni furaha kubwa sana kwani aliamini katika akili yake kuwa hawezi kuongozwa na kijana mdogo asilani. Kila alichokuwa akikifanya Joesan yeye alikiona kibaya kazi yake kubwa ikawa ni kujaribu kutafuta watu wa kuwashawishi ili waweze kuwa wengi wa kumpinga kijana huyo. Ubaya ni kwamba kila anapogusa anakuta hakuna msaada na wengi walikuwa na imani sana na kijana huyo. "Joesan namuamini sana kwanza kazi zake huwa hakurupuki, huyu kijana aliyemleta anaonekana ni kidume cha shoka kweli" alijibu Rafael jibu ambalo lilikuwa ni baya sana kwa Mgobo. "nakuambia huyo kijana hawezi kupafom kwenye mapambano kijana anaonekana mchovu kabisa huyu" alizidi kuongea Mgobo. Rafael akageuka na kumtazama Mgobo kwa macho ya udadisi kidogo na kumuuliza. "unauhakika gani kama Chriss hataweza ku-perfom kwenye compertition?"

    "ni kwasababu mimi ndiye ninayepanga majemadari wa kupambana naye sasa unafikiri nitachagua mdebwedo lazima nichague vijana watakaoweza kumshinda huyo Chriss na lazima niwaambie wamuue kabisa. Nataka Joesan asiwe juu kuliko sisi wakongwe" akaongea Mgobo. "mmmm!" aligumia kidogo mzee Rafael na kuongea huku akiwa anamtazama Chriss akiwa anateta jambo na Suzane. "kumbe unania ya kumuangusaha Joesan?"

    "ndiyo, mzee mwenzangu Joesan hawezi kuwa juu yetu hata mara moja na ningependa tushirkiane tuweze kumuangusha kabisa" alisema. Yalikuwa ni maongezi ya kimya kimya sana hakuna mtu aliyeweza kusikia zaidi yao wao wawili pekee. "unajidanganya Mgobo Joesan siyo mtu wa kuchezea hata kidogo usifikirie mkuu hana akili kumpa kijana huyu uongozi wa juu" Rafael alizidi kumuweka sawa mzee mwenziye lakini bado Mgobo alizidi kuwa mgumu kuelewa. "subiri uone hapo ndipo utakapojua mimi ni nani nadhani sasa ni muda wa kuelekea kwenye uwanja wa kifo hatoki mtu akiwa hai leo" alisema hivyo mgobo baada ya kumuona Joesan akinyanyuliwa kwenye kiti na kukokotwa kuelekea kwenye uwanja wa mapambano ambao ulifahamika kama uwanja wa kifo kwani kila anaepambana hapo kama hana uwezo basi anazawadiwa kifo kabisa ili kulifanya jambo hilo kuwa ni la siri kubwa hivyo wengi akiwemo Mgobo na yeye akiwa kama mpangaji wa fighters watakao pambana na Chriss, waliamini kabisa kuwa huo ndiyo mwisho wa shababi huyo. Jopo lote la wafanyakazi wa kampuni hiyo, walielekea chini kabisa ya jingo hilo. Flow ya kwanza ambayo ipo chini kabisa ya ardhi. "sheria za pambano hilo ni kali Chriss na kila anayengia kwenye mpambano, edha auwe ama auwawe. Pambano lako ni kufa na kupona hivyo huna budi kuhakikisha unapigana kweli ili kumuweka mjomba wako katika furaha zaidi" alikuwa ni Suzane akimsihi Chriss afanye kweli na asithubutu kuleta mzaha. "nina muda mrefu sana sijapambana hivyo nitapambana kwa weledi wa hali ya juu toa shaka Suzy kwa hilo" alijibu Chriss. Wote walifika flow ya chini na Chriss akaingizwa kwenye mlango fulani na kutokea kwenye ukumbi mkubwa ambao ulikuwa umezunguushiwa vioo, nje ya vile vioo aliwaona wafanyakazi wote wa ile kampuni wakiwa wamekaa wakimtazama yeye. Macho yake yakazunguuka kila upande ili kujua kama mjomba wake yupo. Alipoangalia pembeni kwenye kona ya ule ukumbi ndipo akamuona Joesan akiwa amekaa kwenye kiti akimtazama kwa makini. Akayakumbuka mateso aliyokuwa akiyapata kwa ajili yake akajikuta akipata ari kubwa ya kutaka kupambana. "mbele yako kuna mistari ya rangi nyekundu, mistari hiyo imepishana kwa umbali wa futi tano, ipo mistari kumi kila mstari utakaouvuka inamaanisha umewaruhusu maadui kuja kupambana na wewe, sijui watakuja kwa njia gani lakini watakuja. Mstari wa kwanza ukiuvuka utakuwa umeruhusu maadui wawili na kila mstari utakuwa ukiongeza maadui wawili yaani mstari wa pili utakapouvuka, utegemee kupambana na maadui wanne kama wawili wa mwanzo utafanikiwa kuwauwa ila kama huja wauwa wa mwanzo na ukavuka mstari wa pili inamaana utapambana na maadui sita." sauti kutoka kwenye spika ilikuwa ikimpa maelekezo. Macho yalimtoka Chriss asiamini anachokisikia kama ndicho anachotakiwa kukifanya. "sasa basi" sauti hiyo kwenye spika ikaendelea. "kupona kwako ni mpaka pale itakapoondoka roho na mwili wakoko kuuacha mahali hapo, nakutakia mapambano mema unaweza kuanza." Chrss alikuwa kama kapatwa na bumbuwazi fulani hivi. "inamaana nikifika mstari wa kumi nitapambana na maadui ishirini? Washenzi sana hawa watu" aliwaza Chriss na kufanya sala ya moyoni na kupiga hatua kuuelekea mstari wa kwanza akiwa ni mtu mwenye kujiamini sana. Kitendo cha kuuvuka tu ule mstari, walichomoka watu wawili ambao haikujulikana wametokea pande gani. Walikuja kama mshale na kumvamia Chriss, wakampelekea makonde ya kushtukiza. Japo alikuwa akijiamini lakini hakuwa amejiandaa na ujio huo, alijikuta akichezea kipigo cha Mbwa mwitu katika hizo hatua za awali. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Chriss alipigwa kama mtoto tena yalikuwa ni mapigo ya kuchanganya kabisa. Alijtahidi kurusha ngumi lakini ngumi zake zilikuwa zikikosa lengo, alipewa pigo moja la nguvu lililompeleka mpaka chini na kubaki akitweta kama Mbwa aliyekosa windo alilolikimbiza kwa masafa marefu. Huku kwa watazamaji, mzee Mgobo alifurahi sana kuona Chriss amepigwa kwa hatua hiyo ya awali tu hivyo aliona ni jinsi gani Joesan anavyokwenda kudharauliwa na wafanyakazi wenzake huku akiziona hasira za Mkuu zikishuka kwa kijana huyo. "nilikuambia Rafael huyu kijana anaonekana si mpambanaji hata kidogo, anapigwaje kipumbavu katika hatua za awali namna hiyo" alijisifu Mgobo huku akiiweka tai yake vizuri kwa kuibana kidogo. Mzee Rafael alimtazama Mgobo kwa muda mrefu lakini hakusema kitu, aliigeuza shingo yake na kuendelea kumtazama Chriss pale chini alipoanguka. "ha ha haaa!" siwezi kuongozwa na kijana mdogo hata mara moja lazima nihakikishe Joesan anapigwa chini" alisema Mgobo. "Joesan siyo mtu kama unayemfikira wewe hebu tuuone huu mchezo hadi uanavyoisha" alisema Rafael mzee aliyeonekana ni mtu mwenye busara sana. Chriss aliwatazama wale watu kisha akatazama kule ambako watu walikuwa wamekaa wakimtazama yeye. Alinyanyuka tena kwa kasi kwa ajili ya kupeleka mashambulizi lakini aliambulia kichapo hevi, alipigwa Chriss tena alipigwa vibaya sana hadi akalegea kabisa na kudondoka chini akiwa anavuja damu. Akatulia kimya hapo chini akiwa anapumua kwa nguvu sana, kila mtu hapo alikuwa hana imani tena na kijana huyo na ukumbi mzima ukazizima. Mgobo peke yake ndiye alikuwa akitamba hapo hadi wafanya kazi wenzie wakawa wanamshangaa, Joesan aliumia sana kumuona mzee huyo anafurahia jambo ambalo yeye binafsi lilikuwa likimuumiza lakini hakutaka kumfanya chochote alimuacha tu azidi kutamba mahali hapo. Chriss akapata nguvu na kunyanyuka tena kwa mara nyingine, hii ndiyo alipigwa vibaya mno. Wale jamaa wawili waliruka hewani na kuja kutua kwa pamoja kwenye kifua cha kijana huyo na kumrusha mbali kabisa hadi akajipigiza ukutani kwa nguvu sana. Maumivu makali yakamtambaa kijana huyo, damu zikimtoka kwa wingi sana. ...........





    . Alinyanyua uso wake na kulitazama lile jopo la watu wanao mtazama mahali hapo. Alimuona mzee mmoja ambaye alikuwa akicheka sana mwisho akamuwekea ishara ya kukata koo kwa kupitisha mkono shingoni. Ishara hiyo Chriss aliichukulia ni kama tusi kwake hivyo akaapa kumuonesha kuwa pale hakukuwa na type yake hata kidogo. Alinyanyuka kama kimbunga na kupeleka shambulio ambalo kila mtu lilimuacha hoi maana hakuna aliyetarajia shambulio la namna ile. Chriss alihakikisha kila pigo anauwa. Aliwapa wale jamaa kichapo cha sekunde tatu kisha akairuka mistari mingine miwili akiwaacha hawa wa nyuma wakiyapigania maisha yao ya mwisho. Chriss alikuwa ni kama mzuka uliorudi duniani kwa lengo la kulipiza kisasi, hakuna adui hata mmoja aliyethubutu tena kuugusa mwili wake. Kila aliyejaribu kumkaribia aliambulia maumivu ambayo alikuwa akiyasoma kwenye simulizi mbalimbali kama ile ya I was born to die iliyoandikwa na mwandishi Frank Mansai. aliimaliza awamu ya pili kama kumsukuma mlevi. Mbele yake alibakiwa na mistari sita ambayo ilikuwa ni migumu sana kuvuka hadi kufika mwisho kwani kila hatua aliyokuwa akipiga alikutana na maadui wenye uwezo tofauti lakini maajabu aliyowaonesha hakuna aliyewahi kuona wala kufikiria kama kuna binadamu anaweza kutokea akawa na uwezo kama huo aliyouonesha huyo kijana. Chriss aliivuka mistari minne kwa wakati mmoja kisha akarudi nyuma kuwavuta. Kilikuwa ni kijiji cha watu na kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi, walikuja kwa pamoja hakuna aliyemsubiri mwenzie. Hofu ikajaa kwa Joesan alijua sasa huo ndiyo mwisho wa maisha ya Chriss na alikuwa akifa kifo kibaya sana. Haikuwa hivyo, mambo yalikuwa tofauti, Chriss alipita kama kimondo katikati ya wale watu na alikuwa akizunguuka kama pia. Alipokuja kutulia alibakiwa na watu wawili tu na mkononi kwake kukiwa na cheni iliyofungwa visu vitatu mbele. Kila aliyekuwepo pale alibaki mdomo wazi, yalikuwa ni maajabu ya mwaka. Wale watu wakichinjwa kama kuku wa kisasa. Waliobaki wakawa wanatetemeka badala ya kushambulia, kijana huyo aliruka sarakasi za nyuma na kuja kutua karibua kabisa na mmoja wa wale maadui huku yule mwingine wa pili akiwa kashika shingo iliyokuwa ianavuja damu, yule aliyebakia alipoona amekaribiwa alijichoma kisu mwenyewe na kudondoka chini yaani aliona ni bora kujiuwa mwenyewe kuliko kukutana na huyo mtu wa ajabu. Hakungojea Chriss alimalizia na mistari iliyobakia na sasa mbele yake kukawa na watu wapatao 38. Wote wakiwa ni mapande ya watu. Chriss akatabasamu na kuanza kutembeza kichapo akiwa kabadilisha kabisa mtindo, hapa alikuwa hachinji bali alikuwa akicheza na shingo zao na alizivunja kweli, ndani ya sekunde thelathini, alikuwa amebakiwa na mtu mmoja tu na huyu alibaki kwasababu alikuja mwishoni kabisa mwa mchezo. Jamaa hilo lilikuwa bonge la mtu lenye tumbo kubwa na lilikuwa likitembea taratibu kumfuata Chriss. Chriss hakuwa na presha na jitu hilo, alikaa kimya akiwa anamuangalia jinsi anavyokuja. Mtu huyo alipomkaribia Chriss, alirusha konde zito Chriss akaliona, akarusha jingine nalo hola, akarusha la tatu na la nne, kijana huyo machachari akayumba na kunesa kisha akapiga msamba na kupiga ngumi kama ishirini na mbili hivi kwenye korodani za jitu hilo. Jamaa lilipiga kelele kama beberu aliyekatwa koo. Chriss alirudi juu haraka sana na kumzunguuka kwa kasi ya hatari mkononi akiwa na kisu alichokiokota hapo chini na kukiweka kooni. Akamkazia macho yule yule aliyekuwa anamcheka hapo mwanzo kisha akakipitisha kile kisu shingoni mwa lile jitu na kulisukumia mbele likaanguka kama nguzo ya umeme. Hapo chini palikuwa hapatamaniki kwa umati wa miili ya watu iliyopokonywa uhai kwa dakika chache tu. Kwa wale watazamaji hakukuwa na ailiyekuwa akiongea wote walikuwa kimya kabisa. Mgobo ndiye aliyekuwa haamini kile alichokiona pale, aliona kama ndoto ya mchana, mtu anapigana kwa sekunde chache na kudondosha umati wa watu? Hilo kwake lilikuwa ni swali gumu kabisa. "unapotaka kufanya kitu uwe unafikiria kwanza, bila shaka sasa utakuwa umeelewa kuwa Joesan ni kijana hatari sana" Rafael alimkashifu Mgobo huku tabasamu likiwa usoni pake. Mgobo alikasirika sana kwa kashfa zile, sura ilimbadilika rangi na nyama zake za uso kukunjamana kwa hasira. "kufeli plan A siyo kushindwa kwa plan B. Lazima nilichokipanga kitimie Rafael kama unamkubali huyo mjinga siyo mimi na nakuapia, akifa huyo lazima mimi ndiyo niwe bosi wenu" aliongea Mgobo huku akiwa karibu kabisa na Rafael kisha akaondoka hapo akiwa na hasira kemkem. Mzee mwenzie alitabasamu kwa mbaali huku akitingisha kichwa chake kumsikitikia. "plan A umefeli, plan B pia utafeli na utakosa maisha, nivema ungeachana na mambo ya tamaa Mgobo. Joesan ni dangerous man na atakuuwa ukileta mchezo" aliwaza mzee Rafael, mzee mwenye maono ya mbali. Chriss alikuwa hatamaniki kwa damu alikuwa amesimama palepale akimshuhudia mjomba wake akipewa pongezi za ushindi. Moyo wake ulifarijika sana, aliinama chini na kuzitazama maiti zilivyozagaa, roho ilimuuma kwa kufanya mauwaji yale ambayo hakuwahi kuyafikiria lakini akikumbuka ahadi aliyowahi kumuahidi mjomba wake kuwa atamlinda, alifarijika kwa kuona amemtoa mjomba huyo kwenye mikono ya kifo alichoamini kama asingelikuwa yeye kukubali kuwa Sex Machine, angelikwisha kufa tayari. Joesan alikuwa akizipokea zile pongezi lakini macho yake yote yalikuwa kwa Chriss. Alijua ameandaa silaha hatari sana ambayo kama hatakuwa makini basi inaweza kumrudia mwenyewe. "sitaruhusu mtu akukaribie Chriss, sitamuanini mtu yoyote juu yako. Nitauwa" aliwaza Joesan huku akizidi kupokea pongezi hizo.

    Ni rahisi sana kutengeneza ubaya na ubaya huo kuufanya uishi mbali na himaya yako ukiamini kuwa hakuna kitakacho kutisha wala kukusogeza karibu ya ubaya ulioutengeneza. Unasahau semi za wahenga kuwa mchuma janga hula na wa kwao. Joesan amemtengeneza Chriss ili aje kumtumia katika shughuli zake za kiharamia lakini hajui kuwa Chriss ni binadamu na anaishi kwenye jamii, ni vipi kama atajua kuwa Joesan ni chanzo cha vifo vya wazazi wake, vipi akigundua kuwa yule anayemtumikia kwa kila hali ndiye mbaya wake. Je, itakuwaje na Chriss atajuaje mambo yote hayo? Twende sawa.



    Mlango ulifunguka wa ule ukumbi Chriss akatoka na kuingia katika chumba kingine alichotakiwa aingie. "hakikisheni leo hii hii anaingia kwenye mtambo utakaobadilisha akili yake pamoja na kumfanya kuwa sex Machine kamili, fanyeni hivyo kabla hajabadilisha maamuzi nadhani mmeona wenyewe uwezo wake sasa akibadili maamuzi mnafikiri itakuwaje" alisema Joesan lakini kabla hajajua afanyeje, binti mrembo alifika hapo na kumwambia kuwa anahitajika na mkuu kwenye chumba cha mawasiliano. Akatoa maelekezo ya mwisho kwa Suzane kisha akaelekea kwenye wito. Chriss, hongera sana my love kwa kazi nzuri kweli wewe ni mwanaume wa shoka" alikuwa ni Suzane mara baada ya kuingia kwenye chumba alichokuwa Chrss. Kijana huyo alitabasamu tu bila kuongea chochote. Suzy akamwambia kuwa avue nguo kwa ajili ya kwenda kuoga. Hakusita, alifanya hivyo mbele ya binti huyo. "jamani huyu kijana ni mzuri sana kila ninapomuona hivi ninajikuta nikimtamani" aliwaza Suzy. Chriss alipangusa nguo zote mwilini mwake na kuelekea bafuni. Alilifungulia bomba la mvua na kujiweka katikati akiyaruhusu yale maji yauloanishe mwili wake, aliyafurahia sana maji yale ubaridi wake na jinsi ambavyo yalikuwa yakimwagika kwa wingi ndiyo kabisa yalizidi kumpa raha. Alipokuwa akijisugua taratibu baada ya kupaka sabuni mwilini mwake, alihisi ulaini wa mikono iliyokuwa ikiupapasa mwili wake. Alifunguwa bomba na kujimwagia maji kwa lengo la kutoa sabuni kisha akaitazama ile mikono iliyokuwa imemkumbatia kutokea nyuma akajua siyo mwingine mtu huyo zaidi ya Suzane. Chuchu mkito zilizokuwa zikiukita mgongo wake, zikaanza kumletea shida. mikono ile laini haikuacha kulipapasa tumbo lake sambamba na kifua chake kipana. "Chriss natamani unifanye kila saa kwa jinsi ninavyovutiwa na wewe, cheki kifua chako kilivyo kizuri, cheki tumbo lako lilivyotengeneza matuta kama raster za barabara ya kwa minchi au yale matuta ya hospitali ya Bombo. Ooouu yaaa, angalia ulivyo na mashine ya kazi. Please Chriss nijaze nao tunduni nifaidike" aliongea kwa sauti tamu iliyofanya misuli ya gongoo la muhogo la kijana huyo kutuna na kulifanya lisimame wima. Mikono laini ya Suzy ikiusugua taratibu mtalimbo huo. Chriss alimgeuza na kumvutia mbele akaudaka mdomo na kuanza kupata ladha ya juisi ya miwa huku mikono yao ikisema kwa lugha wazijuazo wao wenyewe. Miguno ya mahaba ikashika hatamu. Chriss akashuka kwenye chuchu mkito za mtoto huyo na kuzitia mdomoni. Suzi akapagawa zaidi na kuzidi kukibinua kufua chake mbele ili kidume hicho kifaidi utamu wa embe dodo zake kifuani. "ooouuu yaaa, tafuna kila kitu baby kula kwa uwezo wako leo nipo hapa kwa ajili yako Chriss cause umenifurahisha sana. Nitakupa chochote unachotaka leo" alizidi kulalama Suzane. Chriss ni kama alipagawa, alimbeba na kumuweka juu ya sinki la kunawia mikono kisha akazama kunako ladha ya chumvi.. Kelele zikazidi maradufu lakina bado kijana huyo hakutaka kuacha. Utundu aliokuwa akiutumia hapo ulimchanganya Zaidi Suzy. Alipoona amempagawisha vya kutosha, alimshughulikia vya kutosha. Alimpa mambo hadi akajuta kujifahamu yeye ni nani. Roundi mbili za mchezo Suzane alikuwa taabani. Walioga na kutoka mule bafuni huku suzy asiamini kama shughuli aliyopewa na kijana huyo ni baada ya kijana huyo kutoka kwenye pambano la watu si chini ya sitini tena wote wakiwa ngangari kimapigano. aliogopa sana, hakujua kuwa huyo ni mtu wa kawaida ama laa. lakini ukweli wa yote ni kwamba kila alipokuwa akikutana na mwanaume huyo,moyo wake huwa unafarijika sana hakika alikiri kuwa Chriss ni mwanaume wa aina yake. Mipango yote ya kuhakikisha Chriss anapelekwa kwenye chumba cha kumtengeneza kuwa sex machine, ilikuwa imeshaandaliwa. Hivyo alichokifanya Suzane ni kutoka na Chriss mule ndani kwa lengo la kwenda kupata chakula cha jioni. Walipita sehemu mbalimbali mule ndani ya lile jingo na kupishana na watu wa kila aina hadi katika lifti ambayo iliwachukua na kuwapeleka kwenye flow ya kwanza kutoka usawa wa ardhi ambayo ni flow ya tatu kutoka chini. Mlango wa lifti ukafunguka wakatoka lakini wakapishana na watu wawili waliokuwa wamevaa suti nyeusi. Hapa Chriss alikwaruzwa na kitu chenye ncha kali walipokuwa wakipishana na hao watu hadi damu zikawa zinatoka kabisa. Chriss akataka asimame na awaulize lakini bi dada huyo akamsihi awaache kwani anaweza akaeleweka vibaya na ukizingatia watu wote humo ndani walimuona wakati anapambana. "acha waende tu haina haja ya kuwafuatilia" ndivyo alivyosema Suzane. Akaachana nao watu wale na wao kuamua kuendelea na hamsini zao. Hatua tatu mbele zilikuwa ni nyingi sana Chriss alianza kuhisi kizunguzungu, kichwa kilianza kumuuma na nguvu za miguu kupungua .........................



    hatimae akawa anashindwa kabisa kutembea ndipo Suzane alipo muwahi na kumkamata. Aliuzunguusha mkono wake kupitia mgongoni na kutokea kwapani mwa kijana huyo, akamkokota taratibu hadi walipokuja kuchepukia kwenye korido moja ndefu sana. Hapa Chrss ndiyo alikuwa hawezi kabisa kutembea nguvu yote ya mwili wake ilikuwa imemuelemea Suzane. Alizidi kumkokota hadi alipoukaribia mlango wa rangi ya buluu, mlango huo ukafunguliwa na kuingia ndani ya chumba hicho. Hicho kilikuwa ni chumba kilichobeba mitambo ya kutisha sana, mikubwa na iliyokaa kiajabu ajabu. "mlazeni hapo juu ya hicho kitanda" dokta alisema huku akioneshwa sehemu aliyotakiwa kulazwa Chriss. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Kilikuwa ni kitanda cha chuma kilichounganishwa na mtambo mkubwa. Chriss akalazwa mahali hapo na kufungwa na mikanda migumu kama tahadhari. Dokta Emmy, mwanadada bonge mfupi mweupe mwenye asili ya watu wa bara Hindi. alielekea kwenye kioo kikubwa na kubofya kitufe fulani na kuanza kusoma taarifa za mtu huyo kasha akasubiri amri ya utendaji kazi ili aanze kufanya yake. Watu wote wakamtazama yeye na kumpa ishara ya kuendelea na kazi yake. Alibonyeza batani nyingine na kile kitanda kusimama wima kisha kikajongea na kujiingiza ndani ya mtambo mkubwa, dokta yule akawa na kazi ya kubofya batani hii na ile mara taa nyekundu ikawaka. Watu hofu zikawatanda. "nini kimetokea hapo?" msaidizi wa dokta Emmy akauliza huku akiwa ni mwenye wasiwas sana. "mtambo unakataa kuleta ripot zake" alijibu Emmy huku akiwa macho ameyaelekeza kwenye kioo hicho cha kompyuta kilichochukua nafasi kubwa ukutani. "itakuwaje sasa kama mapema namna hii inaleta shida" aliongea msaidizi huyo lakini hakujibiwa na badala yake mtu aliyemuuliza akaongeza kasi ya kile alichokuwa akikifanya pale kweye ile kompyuta. baada ya pilika pilika za hapa na pale, ikaanza kuwaka taa ya manjano na hatimaye ya kijani ikafuatia. Nyuso za furaha zikawagubika mule ndani kila aliyekuwepo hapo alifurahi na kugongeana tano kabisa. Ripoti iliyokuwa ikisubiriwa ikatokea, dokta Emy akawa anazisoma huku msaidizi wake akiwa anazinakili mahali. walipo maliza, Emmy akapiga simu muda si mrefu Suzane akafika. "nipe ripoti daktari?" akauliza. "ripoti kamili ni kama unavyoiona"

    "inasemaje?" akuliza tena Suzane ikabidi dokta Emmy aisome. "mwili wake unaonekana kuwa na nguvu sana na hii ni kutokana na kuwa na uzito mzuri ana kg 75, hivyo haipaswi kumuongeza uwezo wa aina yoyote ile huu alio nao unatosha sana" Suzy akatikisa kichwa kuafiki kasha dokta akaendelea. "anauwezo mkubwa wa kufikiri na ubongo wake ni mwepesi sana kukumbuka hivyo humfanya awe mwepesi wa kufikiri jambo na kulitolea maamuzi ya papo kwa hapo"

    "nashindwa kuelewa Chriss ni kiumbe wa aina gani na kama ni binadamu wa kawaida basi Mungu amempendelea sana" aliwaza Suzane lakini akiwa makini kumsikiliza daktari. "tukija kwenye upande wa homon zake, huku hakuna shaka kabisa ni kidume kilicho kamilika hana chembechembe zozote za kuharibu uwanaume wake, seli zake zinazalisha nguvu ya kutosha. Na uume wake unaurefu wa nchi sita ukiwa haujasimama, unasemaje kuhusu hapa" aliongea daktari huyo na kumtupia swali Suzane. Suzane akasema kuwa inabidi iongezwe kidogo hadi kufikia nchi nane na pia akauliza kuhusu unene, daktari akajibu. "unene ni 4omm. Ikiwa imesimama"

    "unene huo unatosha najua hapo ikirefuka hadi kufikia nchi nane, anaweza kubakiwa na mm38 au 36 kamili" akasema Suzy kisha akauliza tena. "je, itachukua muda gani hadi kuwa tayari kwa kila kitu ikiwa ni pamoja na kuuharibu mfumo wa ubongo wake asiweze kukumbuka kila kilichopita na awe ni mtu wa kutekeleza anacho tumwa tu bila kupinga chochote maana hapo ndipo tunapokwenda kuliuwa jina la Chriss na kumbatiza jina la sex machine rasmi."

    "ni muda wa wiki moja na siku tatu nikiwa na maana ya kwamba ataishi ndani ya mtambo huu bila kutolewa kwa siku 10" alijibu daktari huyo. Suzane akaichukua ripoti hiyo ambayo ilikuwa imekwisha chapwa tayari na kutoka nayo.



    "habari yako mr. Joesan?" ilisalimia sauti ya mkuu baada ya Joesan kufika ndani ya chumba cha mawasiliano. "nzuri tu mr. Li Kim" alirudisha majibu bwana Joesan. "ok, kaa kwenye kiti hapo rafiki yangu ili tuweze kuzungumza" ilisema sauti hiyo na Joesan akakaa kwenye kiti kilichopo karibu kama alivyo elekezwa. "leo usiku zero, six (06) leo saa 20:00 usiku" ilisema hivyo sauti hiyo kasha mawasiliano yakakatika. Joesan alicheka kidogo bila kutoa sauti yoyote. "si alikuwa na uwezo wa kuniambia bila ya mimi kukaa? Sasa ananiambia nikae wakati kumbe sentesi yenyewe ni moja tena fupi kama kimo cha watu aina ya mbilikimo" alijisemea moyoni Joesan lakini akiwa kaelewa kile alichoambiwa mahala hapo. Akatoka ndani humo na kukutana na Suzane akiwa anatoka chumba kinachoongoza mitambo, Suzy akamkabidhi Joesan ile riport kisha akataka kuondoka, akakutwa na swali "time?"

    "ten days" Suzy naye akajibu kwa kimombo kisha akaondoka na kuelekea sehemu yake ya kazi.



    Mgobo alipiga ngumi mezani kwa kishindo kikubwa. Ngumi iliyotuwa mezani hapo kama ingelikuwa ni meza ya kioo, haki ya manani isingelivumilia uzito wa utuaji wa ngumi hiyo. Ilikuwa ni ngumi inzito na huwezi kuilinganisha na umri alionao mzee huyo. Aliilegeza tai kabisa na kuurudisha mgongo nyuma ya kiti chake. "haiwezekani kila anachokifanya Joesan kiwe kizuri asilimia mia moja. Kwanini yeye ndiyo awe taa inayong'aa kila kukicha na kukichwa? Kwanini yeye ndiyo awe kila kitu kwa mkuu? No, siwezi, siwezi kuwa chini ya mtoto mdogo kama Joesan. mimi ni mkongwe kwenye kazi hizi iweje yeye apewe kipaumbele sasa na alinikuta kazini tena eti, ndiyo ananipangia kazi" aliwaza Mgobo akiwa amekiegamia kiti chake kama vile kiti hicho kilikuwa kimepata moto, maana alikuwa amejiegamia upande mmoja huku mkono wake wa kuume akiwa kaukunjia mezani. "nini nifanye kumuangusha?" akajiuliza tena na kuskuti kwa muda kidogo kabla ya kuachia tabasamu, tabasamu ambalo ndilo lililoleta jibu la swali alilojiuliza moyoni muda huo, akacheka kabisa cheko zito, cheko la furaha moyoni mwake baada ya kupata njia ya kumuangusha Joesan ili aonekane hana maana kwa mkuu na kwa kuwa baada ya Joesan ni yeye kwa utendaji, aliamini cheo cha kijana huyo katili anakwenda kukaa yeye sasa. "nakwenda kuharibu program ya utendaji kazi wa mtambo najua nikifanya hivyo huyo Sex Machine wake anakufa na hili litamfanya aonekane bado hajafanya kitu. Mkuu atamuangamiza huyu bwege na mimi nitakuwa ndio general wa kila kitu hapa kwenye kampuni baada ya Mkuu" alisema kisha akacheka tena kwa nguvu kubwa na kujiapiza ifikapo usiku ni lazima akamilishe hilo jambo. Akaweka tai yake vizuri na kuitengeneza vizuri suti yake kisha akaivuta kompyuta yake na kuendelea na taratibu za kiofisi.



    ***********************%%%%%%%%%%%%



    SEHEMU MOJA HUKO BRAZIL.

    Ndani ya casino moja kubwa lililopo ndani ya mji wa Fortaleza. Mziki laini ulikuwa ukiwapa burudani mabwana wakubwa wenye pesa zao huku warembo wa ki brazil na wa mataifa mengine wakijipitisha pitisha karibu na meza za matajiri waliokuwa wakicheza kamari ili kuona kama wanaweza kupata bahati ya mtende ya kununuliwa na vibosile hao ambao dau lake kwa usiku mmoja linakutoa uchovu wa siku kadhaa ulizokosa soko. Si wote walikuwa hapo kwa niaba ya kutafuta wachumba, wengine walikuwa kibiashara zaidi na wengine walikuwepo hapo kwa lengo la kuzifurahisha nafsi zao kwa kulewa na kucheza michezo mbalimbali ya kamari. Kwenye pembe moja kulikuwa na meza moja upande wa VIP, iliyokuwa imezunguukwa na watu watatu wa mataifa tofauti. Mmoja alikuwa mrusi huyu alikwenda kwa jina la Chalkovich. mwengine alikuwa ni mfaransa mr. Santiano na huyu wa tatu ni mmarekani mweusi aliyefahanika kwa jina la BC au Black Clocodile. Vinywaji vikali ndivyo vilivyokuwa vikiwakata makoo yao kwa wakati huo mahali hapo. "natumai kila mmoja wetu hapa amepata ujumbe kutoka Tanzania?" aliuliza yule mrusi bwana Chalcovich. Wote pale wakatikisa vichwa kukubali. Nadhani mnamjua yule jamaa huwa hasemi uwongo hata mara moja na huu ni ujumbe kwetu kwamba tuwe tayari kwa biashara iliyokuwa imesimama." akaweka tuo na kuwatazama wenzake. "bila shaka atakuwa kapata Chombo kipya cha kazi?" aliuliza BC. "yeah, bila shaka we si unajua kuwa kazi zetu ni ki proffesional zaidi" akajibu Chalcovich na wote wakaitika na kugonga cheas kisha wakagida pombe kali na kuvishusha mezani vijichupa hivyo vidogo vilivyobeba pombe kali ya kirusi. "ninaamini milele na milele hatuwezi kufilisika" aliongea yule mfaransa na wote wakacheka kwa furaha kubwa. Walifurahi kweli tena walifurahi kupita kiasi kwani waliamini utajiri wao uliokuwa ukiendeshwa kwa kufanya biashara kubwa ya kusambaza madawa ya kulevya duniani kote, inarejea. Walikunywa wakanywa na kulewa kabisa. Kitu ambacho hawakukijua ni kwamba wakati wakiwa wanaongea hayo, pembeni yao meza ya tatu kutoka ilipo meza yao, kulikuwa na msichana mrembo ambaye alikuwa akisikia kila kitu lakini hakuelewa kifaa hicho cha kazi kilichopatikana ni kifaa gani lakini kitu kilichomfanya afurahie maongezi hayo na kupenda kuyafuatilia zaidi ni baada ya kutajwa jina Tanzania. Akawasubiri watu wale waleweshwe na kile kilevi ili afanye anachojua yeye. Masaa machache baadae kile alichokuwa akikisubiria yule binti ambaye hakujulikana ni nani, kilitimia. Jamaa wote wale walikuwa wako miwani japo si sana lakini pombe ilisha vigonga vichwa vyao. yule binti hakutaka kupoteza muda, alikizunguusha kitu fulani kwenye mkono wake, kilikuwa ni kijidude kidogo sana ambacho si rahisi kukigundua kwa macho kisha akanyanyuka pale alipokuwa amekaa na kwenda kwenye ile meza ya wale jamaa. Alikuwa amevaa bikini nyekundu, na alikuwa na asili ya mtu mweusi. Sura yake haikuonekana kwa ufasaha. Akafika hadi kwenye ile meza na kukaa kimitego, aliinama na kuyafanya matiti yake aliyoyatega kiustadi kumtamanisha kila kidume mkora. "habari za usiku huu?" alisalimia kwa lugha ya kiingereza. "ooh! ni kama bahati kuja mrembo kama wewe kwenye meza hii maana nilitaka kuita malaya wa kuondoka naye vipi nikulipe kiasi gani kwa usiku huu?" aliongea BC yule mmarekani. "sina shaka nawe kwenye malipo tunaweza kuongelea suala la bei tukiwa hotelini" alijibu yule binti huku akiwa anakibinua zaidi kifua chake hali iliyomfanya BC awaage wenzake na kuahidi kuwa atawatafuta kesho kwenye simu. "hey we malaya twende ukanipe burudani nikulipe ujira ....................................................



    .na sita angalia sehemu ya kula naweza kukulipa kiasi chochote utakachohitaji." alibwata BC huku akimshika makalio binti huyo na kuyaminyanya na kuyapigapiga kwa furaha na matamanio ya kwenda kumla mtoto mzuri mweye asili ya kiafrika ka yeye. Yule binti aliumia sana kitendo cha yeye kuitwa kahaba na kuchezewa mwili wake namna ile, lilimkera sana hilo jina la malaya sema hakuwa na jinsi ilibidi atii kila kitu ili atimize azma yake. Wakatoka nje ya ile kasino na kuelekea ilipoegeshwa gari ya kifahari. BC akamfungulia binti yule mlango na yeye akajifungulia na kuwasha gari, safari ya katikati ya mji ikaanza. waliegesha gari nje ya hoteli moja kubwa na kuingia ndani moja kwa moja bila shaka kibopa huyo alishalipa kila kitu hapo. wakazama chumbani, kilikuwa ni chumba namba 37. Kitu cha kwanza alichokifanya yule binti ni kuelekea bafuni kwanza, alipofika alitoa kijipacti fulani kidogo sana kutoka kwenye mkanda mwembamba wa ile bikini. Akakipasua na kukiminya yakatoka mafuta ambayo aliyapaka kwenye chuchu zake kwa haraka sana na kuchezea maji kwa dakika chache ili kumdanganya jamaa kuwa amekwenda kujisaidia ama kujisafisha kama sio kuoga kabisa kisha akarudi chumbani na kumkuta yule jamaa akiwa anamsubiri kwa hamu kubwa. Binti aliivua nguo yake ya juu na kuonesha jinsi matiti yake yalivyo nona na kupanda kitandani ambako jamaa alikuwa mdomo wazi baada ya kumuona binti huyo alivyo umbika. Akazifakamia chuchu za binti huyo bila kufikiria huku akiwa yuko katika hisia kali za uhitaji wa mchezo huo wa ajabu. hakudumu sana katika kifua hicho cha huyo binti ni kama sekunde 30 hivi za kudumu katika mchezo, akalegea na kuporomoka taratibu hadi kwenye godoro akiwa hajielewi kabisa. Akamlaza vizuri na kutia mkono kwenye suruali yake ya jins aliyokuwa amevaa. Akatoa simu. akaizima na kuifungua taratibu kisha akakichukua kile kifaa alichokuwa akikichezea mkononi mwake ndani ya Casino, akakipachika kitaalamu zaidi kwenye ile simu kiasi kwamba hata angeifungua asingegundua chochote. kasha akairudisha kama alivyoikuta na kuitia mule mule mfukoni. Akamuinamia BC na kumpiga busu la kwenye paji la uso na kurudi tena maliwatoni kwa ajilia ya kuoga kabisa.

    Wakati hayo yakiwa yanaendelea mahali hapo, huku Morogoro, Joesan alikuwa ndiyo anapaki gari maeneo ya Mazimbu ndani. Alishuka kutoka ndani ya gari hiyo na kupiga hatua ndogo ndogo hadi ulipo mlango wa kuingilia ndani kabisa ya mjengo huo. Walinzi wawili wenye silaha za kivita wakampisha bwana huyo, akaingia ndani kwa madaha yote. Alipofika kwenye sebule ya nyumba hiyo, alitokea binti na kumchukua hadi eneo jingine kubwa huko ndiko alikowakuta wenyeji wake. Hili jengo ndilo lenye namba 06 kama utambulisho wake, ni miongoni mwa majengo ya siri ya bwana huyo wa Kikorea. "karibu sana Joe?" alikaribisha mzee mmoja mfupi aliyekuwa amevaa fulana ya mawingu, alikuwa amempa mgongo anaye mkaribisha. Joesan aliupokea ukaribisho huo kwa shanapa kubwa na kusogea karibu kabisa ya mtu huyo. "ni siku niliyopata kufurahi kuliko siku zote za maisha yangu Joe, hata mama yangu mzazi hakuwahi kunipa furaha kama uliyonipa leo wewe" alisema mr. Kim akiwa ametoa mgongo hivyo hivyo. "sijajua kwanini mkuu" akauliza Joesan. "sikutegemea kama ndani ya kampuni yangu kutatokea mtu mwenye akili nyingi kama zako. Yule kijana ni mwiba na riport zake nilizozipata ni kama vile nusu mtu nusu Jini, umemtoa wapi yule kijana?" akauliza mr. Kim. " unamfahamu mkuu labda kama umemsahau lakini nikikukumbusha ninaimani utamkubuka ni.....!"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ooh! Basi, nimekumbuka, ni yule kijana aliyekuwa akiishi kwako?"

    "ewaa! Ndiye huyo"

    "ni siku nyingi sana Joe tangu kipindi kile nikiwa naazisha ile kampuni, siwezi kuikunbuka sura yake vizuri. hongera sana kwa kutengeneza kitu hatari kiasi kile unapaswa kuwa makini nae sana kwasbabu historia yake yote yule kijana mimi nina ifahamu usikubali akanasa hata harufu ya sababu ya vifo vya wazazi wake. Ukifanya hivyo,atakuwa mbwa wako hadi siku unakufa" alisema Kim. "sitaruhusu hilo litokee hata kwa bahati mbaya"

    "ok, vizuri hebu nifuate huku" akasema Kim na wote wakaongozana hadi Sebuleni, mzee huyo akasogea mbele ya scrin kubwa ya kompyuta na kusimama hapo mbele akasema. "muogope sana mtu anayependa urudi nyuma, ogopa sana mtu mwenyekupenda kukwamisha mipango yako, mtu huyo ni hatari kuliko hata hatari yenyewe. Anaweza kukufanya ukaharibikiwa kimaisha na kuchanganyikiwa kabisa endapo atafanikiwa kuku haribia. Siku zote za maisha yako Joesan huwa nakukumbusha jambo hili, ni bora kuishi na Mbwa mwenye ugonjwa wa kichaa, kuliko kuishi na binadamu mwenye wivu na tamaa. Joesan, wewe ni rafiki yangu, unanijua muda mrefu sana na nilidiriki unifahamu mimi na sura yangu kwa ujumla kwasababu ninakujua na wewe unanijua pia. Unaijua tabia yangu na vile nilivyo, ninaijua tabia yako na vile ulivyo. Hawajui kwanini nilikupa mamlaka ya kuwa kila kitu kwenye kampuni ile, hawajui." alitulia hapo Kim na kuvuta pumzi upya na kuendelea. "sasa kuna wajinga wachache tu badala ya kufikiria ni kwanini wanaisikia tu sauti ya mkuu na hawajawahi kuiona sura yake, wanatengeneza fitina za kijinga. Kabla sijaendelea mbele hebu nijibu hili swali kwanza" alisema na kuuliza swali baada ya Joesan kuonesha utayari kujibu. "ni dhahiri ulitengeza shamba na ukapanda mazao ambayo unaamini yatakuletea faida, sasa ni vipi utamfanya kiumbe mharibifu anayetaka kuharibu mazao yako na ungali umetumia gharama nyingi kwayo?" swali likakomea hapo. Joesan akajibu kuwa ni kukiangamiza kiumbe hicho kabisa. Alipotoa jibu hilo, mr. Kim alibofya ile luninga na kuiwasha. Ilipowaka, alibofya tena kitufe kingine na kumwambia atazame kwa umakini. Joesan akakaza macho pale kwenye luninga, kitu alicho kiona kilimfanya atetemeke kwa hasira kali sana. Alishuhudia mpango mzima na kila kitu kilichokuwa kikizungumzwa na Mgobo. Hata walipokuwa wakijadili na mzee Rafael huku akimshawishi mzee huyo awe pamoja nae. Mbinu ya kutaka kumuangusha kwa kumtafutia wapiganaji wa hali ya juu wakati wa majaribio ya kumpima Chriss na hata walipokuwa wakijibizana wakati Chriss ameibuka kidedea kwa kuwachapa na kuwauwa watu wake aliokuwa amewandaa. Vyote hivyo na vingine vingi alivishuhudia, mwisho kabisa alimuona ofisini kwake akiwa anapanga jambo. Mgobo alijua labda kila anachokifanya kilikuwa siri hakujua kuwa ndani ya kampuni ile kulikuwa na ulinzi wa kila aina tena ukiwa ni ulinzi wa siri sana uliotapakaa kila mahali ya jingo lile. Alijulikana nje ndani au kwa waswahili safi wanasema alijulikana kinagaubaga. Kim akazima ile kompyuta na kumtazama Joesan kisha akasema neno moja tu "msafirishe" kisha akapiga hatua tatu hadi kwenye mlango wa kile chumba walicho kuwamo awali, akageuka na kumwambia "kuna hafla fupi usiku wa leo maeneo ya zero one (01). Hiyo ni kwa ajili yako my friend" alipomaliza kusema hayo akatokomea ndani ya chumba hicho na asionekane tena. Joesan alieleke ndani ya gari yake na kuchukua uelekeo anaoujua yeye. Baada ya kama dakika kumi na tano, alikuwa nje ya ghorofa ndefu kiasi maeneo ya nane nane. Mziki ulikuwa akipiga kwa mbali sana kutokea ndani ya jengo hilo. akafungua mlango na kushuka, akapiga hatua ndogondogo kuingia ndani ya ghorofa hiyo. "karibu boss, karibu sana" binti mmoja alimpokea Joesan na kumkaribisha, akaongozana naye hadi mahali ambapo palikuwa na meza kubwa iliyosheheni vinywaji, akakaa. "tupo hapa kwa ajili ya kukupongeza boss, hongera sana" alikuwa ni mzee Rafael aliyekuwa akisema maneno hayo ya pongezi. Joesan akamkata jicho mzee huyo halafu akatazama pembeni, ni kama alikuwa na kimuhemuhe cha kutaka kuuliza jambo lakini akasita, akawataza watu wote walioko pale na kujibu. "nimefarijika sana sikutegemea kama mko pamoja nami na muna imani na mimi kiasi hiki, niseme ahsante kwa nguvu mliyonipa" wote wakapiga makofi ya furaha na shampain ikafinguliwa kwa shangwe kubwa, watu walikunywa wakafurahi sana. "asante sana Mr. Kim kwa kuniamini kwa kiasi hiki. Ni wazi bado unaendelea kuufurahia uwepo wangu nami nakuhakikishia sitaleta uzembe hata kidogo" aliwaza Joesan. Baada ya kula na kunywa sana, mziki laini ukapigwa. Watu wakanyanyuka kwenye viti vyao na kwenda kusakata lumba. Kwenye meza ile alibaki Joesan mwenyewe lakini muda si muda alikaa binti mmoja mwenye mavazi ya utupu kabisa na kumtazama Joesan kwa macho ya ushawishi. "tumeagizwa tukupe furaha ya kila aina leo, Mkuu amesema leo ni siku yako boss hivyo ni wajibu wetu kukupa raha" alisema binti huyo mdogo na kumpa mkono Joesan ambaye kinywaji chenye alcohol ya kutosha kilishaanza kuilegeza mishipa yake. "op, no mrembo, asante sana binti, come on, she is beuty fuul." alisifia Joesan huku akipelekwa kwenye chumba safi na chenye thamani ya juu mno. akawekwa juu ya kitanda na kusauliwa nguo moja baada ya nyingine hadi akawa kama alivyoletwa duniani kwa mara ya kwanza. Mtoto huyo wa kike alikuwa yupo hapo kweli kwa kazi hiyo maana Joesan alikuwa akigumia kwa raha si za kawaida hadi hajielewi kabisa kwa utamu aliokuwa anaupata mahali hapo. Alimsahau kabisa mkewe kwa muda huo, alichojali ni burudani kutoka kwa mburudishaji mwenye kujua kuburudisha awapo katika kuitoa burudani hiyo. Binti alikuwa akimsulubu kweli bwana huyo hadi Joesan akawa anajikunja kabisa kila anapojikuta akipokea raha ya aina yake. Mtoto huyo wa kike alijua kuutumi mwili wake vilivyo tukiachilia mbali kuwa ni ajira yake lakini pia alikuwa si haba katika mambo hayo ya chumbani. Mwili wake laini usiojuwa shuruba za kujikata kwa kisu kwa kisingozio cha kukata vitunguu na nyanya, mwili ulio maalum kwa kupapasa miili ya vibosile kama Joesan. Chuchu ndizo zilizomuuwa kabisa bwana mkubwa huyo kwani hazikutoka mdomoni hata mara moja hadi anakuwa hoi kwa mtanange huo.



    "Pole kwa shuguli nzito ya usiku" binti yule mrembo alimwambia BC. Tayari binti huyo alikuwa ndani ya bikini yake nyekundu na kijinguo kifupi kwa juu, tabasamu likiwa mahala pake. Bwana BC alikenua tabasamu kanakwamba kamuona mwanae wa mwisho, kusema asante alishindwa na kuacha kumpa asante pia alishindwa na kubaki akitabasamu huku midomo ya juu ikimcheza. "morning?" ndilo neno rahisi kwake. Binti huyo hakujibu na badala yake aliinama na kumpiga busu la mdomoni na kumwambia "asante kwa kujua kuniendesha usiku, mkeo anafaidi sana" maneno hayo ya huyo binti yakamfanya azidi kubaki njia panda, neno kuwa amemla likaja na kuondoka kwa kasi ubongoni mwake na kubaki na neno ah, ah! Sijamla. "mbona kama namtamani kwa kasi hivi hapana sijamla bwana" aliwaza na kutaka kumkamata ili amrudishe kitandani aendelee na mzigo lakini alisita baada ya kukutana na mkono uliokuwa unaonesha ishara kama unavuta uradi, pesa. BC akachukua kitabu cha hundi na kumuandikia binti huyo pesa nyingi sana, sasa haikujulikana ni kwa kuchanganyikiwa ama laa. Binti huyo mwenye bikini nyekundu akafungua mlango baada ya kupokea ile karatasi ya malipo na kusepa akimuacha BC na utamu wake. BC alijipiga kichwani na kujilaumu kwanini anachukua watoto wazuri akiwa amelewa. Akazishutumu pombe bila kujua kuna mchezo kachezewa na mtu akaweka kifaa maalumu cha kunasa kila maongezi atakayoongea huku akiwa amebahatika kunyonya chuchu tu za mtoto huyo wa kike na ndizo zilizomlaza hoi na kumpa ndoto za kufanya mapenzi hadi asubuhi. Binti mwenye bikini nyekundu alipofika nje ya hoteli ile, alizama ndani ya teksi na kuomba apelekwe kule Casino. Gari ilipoingia barabarani, aliichana ile hundi vipande vidogo vidogo na kuvitupa nje hii ilimaanisha kuwa hakuwa na shida na pesa bali kilichompeleka pale ni kazi. Alifika kwenye kasino ile na......................



    kumlipa dereva tax ujira wake na kuelekea kwenye gari ambayo alikuja nayo usiku kwenye Casino hilo. Aston Martin ikaingurumishwa injini yake na bidada huyo kisha akaiingiza barabarani na kupotea. Ni nani binti huyo? Swali hili mimi na wewe tujiulize na tuliache kama lilivyo.



    Lakini asubuhi hiyohiyo kwa upande mwingine, Joesan alikuwa akijinyoosha baada ya kutoka usingizini. Alipofumbua macho, alimuona binti mrembo akiwa pembeni yake. Kumbukumbu za raha na mautamu aliyopewa na mtoto huyo wa kike zikakivaa kichwa chake akichanganya na tabasamu lililopo usoni kwa mtoto huyo asubuhi hiyo, alijikuta akijiona ni bonge la mfalme mwenye himaya si chini ya mia mbili. "hongera kwa kujua kunipa shida usiku" alisema Joesan kwa sauti nzito ya asubuhi. "ni wajibu wangu boss kuhakikisha unapata furaha muda wote unapoihitaji"

    "jina lako?"

    "naitwa Merina."

    "ooh! Uko hapa kwa muda gani Merina" alizidi kuuliza Joesan huku akikipapasa kifua laini cha mtoto huyo naye akiwa anachezea nywele za boss wake. "niko hapa kwa muda mrefu sana"

    "kweli?" akadakia Joesan. "ndiyo" akajibu Merina na kuendelea. "sina muda wa kutoka nje ya jumba hili na ndiyo maana ni ngumu kujua"

    "kwa kipindi hiki utatoka Merina na nakuhakikishia" alisema Joesan huku akipanda kifuani kwa mtoto huyo mwenye urembo wa aina yake na kupokelewa vizuri kwa mashamsham makubwa. Mchezo ukarudiwa tena hadi walipo tosheka kabisa. Joesan akaongea. "kuna kitu kingine unacho tofauti na hiki?"

    "ndiyo, ninacho zaidi ya hiki na ndiyo maana unaona nipo ndani ya jumba hili la siri lenye namba ya siri 01. Si jambo dogo mkuu kukuweka hapa bila kuwa na cha zaidi mwilini mwako."

    "basi kuanzia leo unatoka ndani ya 01 house na kwenda kufanya kazi chini ya Suzane, kila kitu utajifunza huko. Huduma yako imekuacha huru leo na utafanya vitu vyako kwa uhuru zaidi, utapewa nyumba nzuri na gari ya kutembelea kuna kipi kingine utahitaji"

    "hakuna kingine boss, asante sana na nakuahidi kufanya kazi kwa weledi mkubwa bila kukuangusha" aliongea Merina akiwa ni mwenye furaha ya kupitiliza. Joesan alikwenda kuogeshwa siku hiyo na kusuguliwa kila mahali. Akavalishwa suti yake safi akafungwa tai na kabla hajatoka mule ndani, akamtazama Merina na kumwambia. "hukukutana na mimi popote hivyo tutafanya kazi kama wafanya kazi wengine, nikikuhitaji nitakutafuta nje ya ofisi, namaanisha kuwa sitavumilia ujinga wako wowote ule katika kazi. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Uwapo katika kampuni ile wewe ni mfanyakazi na siyo mpenzi wa bosi." Merina akakubali kwa kutikisa kichwa kisha Joesan akatoka mule ndani ya jumba kubwa lenye jina la zero one. hili ni miongoni mwa majumba sita ya siri kubwa ya Mr. Kim na inasemekana miongoni mwa majumba haya lipo jumba moja ambalo linatumika kama Club lakini linahusika na biashara za kishenzi na ni jumba linalomuingizia pesa nyingi sana mzee huyo wa kikorea ambaye tangu miaka hiyo ya nyuma aliyokuja kwenye ardhi ya Tanzania hajawahi kurudi kwao na wala wazo la kufanya hivyo hana. anamiliki biashara kubwa za halali na zinazo lipa kodi na biashara hizo kapandikiza wazawa huku yeye akiwa mafichoni asiwahi kuonekana hata mara moja. miongoni mwa biashara hizo ni hiyo kampuni kubwa ya Safaries Company (S.C) ambayo imeshikiliwa na Joesan. Wapo wafanyakazi wengi sana wanaofanya katika kampuni hiyo lakini pia hawajui kuwa kampuni hiyo ina biashara nyingine kubwa na haramu inayoendeshwa ndani ya jengo la kampuni hiyo. Wasomi wengi wanaajiriwa hapo na nyuma ya pazia wanaajiriwa maharamia na watoaji roho za watu wa kuogopwa. Na ikitokea kuna mfanya kazi wa kawaida amegundua uchafu unaofanyika ndani ya jingo hilo basi huyo hana bahati, atauwawa na watu siku ya pili wanaarifiwa msiba. Hakuna aliyewahi kumuona Mr. Kim zaidi ya Joesan pekee. Mzee katili, mzee aliyeigeuza tanzania kama choo chake cha kujisaidia haja kubwa na ndogo na pia ni mzee huyo huyo anayewaona watanzania kama makapi ya maembe aliyotoa kinywani mwake baada ya kuyatafuna. Mr. Kim anauhusiano mkubwa sana na wafanya biashara mbalimbali duniani kote. "nitaishi na wewe kama utaamua kuishi na mimi Joesan na utakuwa si rafiki tu bali mwanangu utakayekwenda kuzishikilia biashara zangu pande zote za dunia" siku moja Mr. Kim alikuwa akimwambia Joesan baada ya kumkuta ni hohe hahe asiyeweza hata kujikunjua kununua baiskeli. "nitawezaje kuwa mtu wa dizaini hiyo rafiki yangu?" aliuliza Joesan akiwa haelewi maneno ya mtu huyo aliyeonekana mpole na mcheshi wa sura kumbe moyoni amemeza nyongo ya Mamba mjane. "usiseme huwezi hata kama huwezi kweli, kwani kitendo tu cha kulitamka neno siwezi tayari moyo wako umesha pokea hofu si chini ya kumi zitakazo kufanya uogope kujaribu. Penda kulitumia neno naweza hasa pale usipoweza na utaona jinsi utakavyoweza usipopaweza sawa." ni muda mrefu sana maneno hayo yalitamkwa na ni katika harakati za Kim kutafuta watu ngangari wa kufanya kazi ili aweze kuwekeza kwao na akafanikiwa kweli na kufikia hatua ya kumshawishi Joesan kuwa muuwaji wa kuogopwa kabla na baada ya kumpa mafunzo makali a ya Judo ambayo mwenyewe aliyaita ni mafunzo ya kujihami.

    "habari yako Mandi?" alisalimia Joesan baada ya kuiweka simu sikioni. "safi boss" ulijibu upande wa pili wa simu hiyo. "kuja nyumbani muda huu kuna kazi nataka nikupe, usichelewe sana kuna mahali nataka kwenda"

    "ok, boss nakuja sasa hivi" alijibu Mandi na simu hiyo ikakatwa. Baada ya nusu saa Mandi alifika nyumabani hapo kwa Joesan na kumkuta mtu huyo nje ya nyumba yake akiwa ameegamia gari. Hakukuwa na maongezi mengi alikabidhiwa picha mkononi na kuitazama, akauliza kuhusu picha ile. Joesan akampa maelekezo kuwa huyo mtu pichani anafanya kazi katika kampuni yake ila kuna tabia ambazo ni hatarishi amezianzisha mtu huyo hivyo anahitaji kumpoteza kabisa. Mandi akatabasamu maana neno kuuwa kwake lilikuwa ni neno muhimu kuliko maneno yote ayapendayo. "kila siku ifikapo saa 18:00 ikizidi sana ni dakika tatu au nne, mtu huyu ndiyo anatoka ofisini. Nataka siku ya leo umsindikize kuzimu kwa amani, nakuamini sana Mandi sitegemei jambo tofauti na hilo. Hakikisha ukimkosa awe amekufa tayari, silaha utatumia niliyokupa" akamaliza kuongea Joesan na kuingia ndani kwake Mandi naye akichukua hamsini zake. "vipi dokta, maendeleo yanaridhisha?" Suzane aliuliza baada ya kuingia kwenye chumba cha mitambo. "mambo yanaenda vizuri na kila kitu kinaenda kwa haraka tofauti na nilivyotegemea"

    "kwaiyo inaweza isifike siku iliyopangwa?"

    "hapana kufika itafika lakini atakuwa strong zaidi ya alivyo sasa" alijibu daktari huyo na kuendelea na kazi ya kusoma kila kinacho andikwa katika kompyuta yake. " huu ndiwo mtambo unaomuandaa Sex Mchine, kwasasa zimesalia siku tano za kutolewa kwenye mtambo huo" alisema Suzane akiwa amemgeukia Merina ikiwa ni katika harakati za kumpa maelekezo ya kila anapopita. "hee kumbe kazi ni kubwa sana sasa akifa je inakuwaje?" akauliza Merina akiwa na mshangao machoni mwake. "si rahisi kufa daktari yupo makini sana na tunamuamini kuliko ilivyo kawaida" Suzane alijibu na kuongozana, wakatoka mule ndani wakimuacha daktari akiwa anaendelea na majukumu yake.

    Kwenye chumba cha ofisi cha Mgobo, kulikuwa na utulivu mkubwa sana. Mzee huyo alikuwa ametulia sana akitafakari hili na lile, alishakwenda mara tatu katika chumba cha mitambo lakini hakufanikisha zoezi lake la kuisimamisha mitambo hiyo. Kila alipokuwa akienda huko alikutana na madaktari wakiwa busy na kazazi. Nini afanye? Hilo likawa ndio swali lililokuwa likikisugua kichwa chake mahali hapo. "siwezi kuondoka hapa bila kuhakikisha nimeharibu mambo lakini hata kama nikifeli leo kesho itabidi niwe wa kwanza kufika hapa kazini." aliwaza mzee huyo. Hakujua sababu za kushindwa kizembe hivyo zilikuwa ni nini. siku tano tayari zimekatika tangu apange azma ya kufanya mauwaji ya sex machine kwa kubadili mfumo wa uendeshaji wa mitambo au kuizima kabisa. alichukua chupa ya maji na kupiga funda kadhaa kisha akajinyanyua mahali hapo akatoka ofisini humo. kituo cha kwanza ni katika chumba cha mitambo ambako alimkuta dokta Emmy akiwa peke yake kwenye mtambo. Hakutaka kumsemesha, alipitiliza moja kwa moja hadi sehemu ambayo ilikuwa ikionesha sura tu ya Chriss. Mgobo alimtazama kijana huyo kwa ghadhabu kubwa kama vile anaugomvi nae. Alitamani hata mtambo huo uzime wenyewe na kumfanya kijana huyo akose pumzi na kufa kabisa. "umebakisha muda mchache wa kuishi kijana lazima nihakikishe unakufa kama sio leo kesho, nimekuwa nikikufuatilia kwa kitambo kirefu tangu umewekwa hapo ila nachelea kusema buriani kijana" aliwaza Mgobo na kutandika tabasamu la ubaya usoni mwake kisha akatoka mule ndani kwa haraka akiwa amekubali kushindwa kwa siku hiyo maana dalili ya daktari huyo kutoka ndani humo hakuiona. Laiti angeilijua ni bora hata angetumia nguvu kuharibu kila kitu kwani kitende cha yeye kusema kuwa kesho ndiyo atakamilisha ni kama anajisumbua tu. Kuwhindwa kwake kwa muda huo na hicho ambacho kimemfanya ashindwe, ndicho hicho hicho kitakachomfanya ashindwe hiyo kesho pia. Mbaya zaidi kila mfanyakazi wa kile chumba cha mitambo iliyombeba Chriss, walishapewa taarifa kuhusu mzee huyo na kuambiwa kuwa humani juu yake unahitajika. Aliangalia saa na kukunja sura, tayari muda ulisha kwenda sana hadi kupita ule muda wa kawaida wa yeye kurudi nyumbani kwake. Alifunga ofisi yake na kutoka nje kabisa ya jengo hilo hadi maegeshoni ambako aliingia ndani ya gari yake na kuliwasha. Mwendo wa taratibu aliokuwa akiutumia haukuchelewa kumfikisha maeneo ya kituo cha daladala cha mjini. Foleni ndogo ya hapo ikamfanya asimamishe kabisa gari na kusubiri amri ya trafiki. Mara kioo cha gari yake kikagongwa, alipoangalia alikutana na sura ya kijana mtanashati. Akashusha kioo bwana mkubwa huyo kusikiliza shida ya huyo kijana. "nini shida kijana?" akahoji. "kuna bidhaa hapa mzee wangu natembeza saa nzuri kama hiyo uliyovaa pia tuna waleti safi" akasema kijana huyo huku akionesha bidhaa hizo alizokuwa akizinadi mahali hapo. Mgobo alichukia vibaya sana, aliona kijana huyo anamkosea adabu kabisa. Tusi zito la nguoni kwenda kwa kijana huyo likamtoka na kutaka kupandisha kioo cha gari yake. "pia tuna hii mzee wangu nadhani itakufaa zaidi" alisema huyo kijana "nimesema to......!" hakuimaliza kauli yake mzee Mgobo, macho yakamtoka baada ya kuangalia kile kiliochopo kwenye paji lake la uso. Midomo ikaanza kumcheza kwa hofu iliyomkumba ghafla, akiwa bado anashangaa ...............................



    asijue la kufanya, akashtukia kijana huyo akiwa pembeni yake yaani alijifungulia mlango mwenyewe kupitia pale kwenye kile kioo na kujikaribisha mwenyewe ndani. kilikuwa ni kitendo cha haraka sana ambacho hata Mgobo hakukitegea. "askari amesharuhusu magari kuendelea na safari, twende mzee wangu" aliongea kijana huyo akiwa amemuelekezea mzee huyo bastola maeneo ya tumboni kwa kificho sana ili asiweze kugundulika kwa urahisi na akari huyo wa barabarani tena aliongea kwa utulivu mkubwa kanakwamba anamuomba hele ya chai mzee huyo. "kwan....ni..we..we...nina....nani na unataka nini kwangu?" aliuliza Mgobo kwa kitetemeshi kikubwa. "mimi ni hasimu wako pale kazini au hunijui? Kama umenisahau kwa jina naitwa Joesan na niko hapa kukuambia kuwa si kila unayemuona anafaa kumuingilia" Mandi aliongea kwa majivuno makubwa sana. Mgobo akabaki ameduwaa. Inamaana yeye Joesan hamjui? Si anamjua vizuri sasa mbona huyo kijana anajitambulisha kuwa ni Joesan, Joesan yupi sasa? Au hao wakina Joesan wako mapacha. Huwenda ndivyo alivyokuwa akijiuliza mzee huyo.

    "haiwezekani Joesan awe hapa muda huu au amegundua kuwa ninampango siyo mzuri kwake ndiyo ameamua kunitumia mtu wa kunimaliza?" alizidi kujiuliza hadi akajikuta hajui hata uelekeo wake ni upi."ooo hapana usipite njia hiyo kunja kulia hapo twende kituo kikubwa cha polisi" Mandi alielekeza baada ya kumuona mzee huyo anataka kunyoosha moja kwa moja. Akaingiza gari kulia kwa kufuata maagizo ya mtu huyo asiyemfahamu. Walikwenda wakapita kidogo kituo cha polisi Morogoro na akaamrishwa aipaki gari karibu kidogo lango la uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri. "nimetumwa kuja kung'oka na roho yako na nasikitika kwasababu kile ulichokipanga kinashindwa kutimia. Kuna watu ni mafia toka wanazaliwa wewe unaweza kuwagusa watu hao wakati hata ukiona damu ya Kunguni unakimbia." aliongea Mandi kasha akaitoa usalama silaha yake iliyofungwa kiwambo safi cha kuzuia sauti. Mgobo alitamani gari ligeuke tenga na kijana huyo aonekane na raia wema kila anachotaka kukifanya kwake. Alitamani hata apate nafasi ya mwisho ya kujisalimisha kwa Joesan mwenyewe angalau angeweza kusamehewa. "plan A umefeli Plan B utashindwa pia na roho yako utaikosa, Joesan siyo mtu wa mchezo kama uanavyodhani" maneno ya Rafael yalijirudia kichwani mwake na kutamani ndiyo angekuwa anaambiwa muda huo ili awe msikivu lakini wapi, alishakikanyaga kinyesi chake mwenyewe kwa makusudi nani ampe maji ya kujisafisha kwa kitu alichokifanya kwa kudhamiria. Alihisi mikojo ikimtoka mahali hapo. "nikupe kiasi gani cha pesa uniache niende nikafie mbele kwa kudra za muumba wangu" aliomba Mgobo kwa sauti ya kujikatia tamaa. "muumba wako alichokiandika hakiepukiki, alishaandika kifo chako kitaponzwa na tamaa za kindezi sasa unataka kibadilike nini, ngoja nimsaidie Malaikatul mauti kutoa roho yako Mbweha mweusi wewe" aliposema hivyo Mandi, risasi tatu zikakita kwenye chembe ya moyo ya Mgobo. Akatulia kimya bila kelele kisha muuwaji huyo akatoka kwa furaha kama ametoka kuongea jambo la maana na mtu aliyemuacha garini kumbe tayari aliyemucha garini humo ni maiti. "kazi imekwisha na niko hapa kituo kikubwa cha polisi naelekea Kilakala" ndivyo alivyotoa taarifa Mandi mara baada ya kuweka simu sikioni. Upande wa pili ukamjibu kuwa wakutane usiku kwa ajili ya kupongezana. Akasema poa akakata simu na kuirudisha mfukoni mwake alisimamisha bodaboda na kutaja mahali anapokwenda akadandia na kupotea.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku hazigandi na kila lijapo giza ni ishara ya kuimaliza siku na ijapo asubuhi, tunasema ni siku mpya. siku zilikatika kama upepo ukatikavyo ghafla na hatimaye ikasalia siku moja tu ya kukamilika kwa sex machine. watu walikuwa busy sana ndani ya jingo hilo kila mmoja alikuwa akiandaa kazi yake maana kile kipindi cha utendaji kazi kilikuwa kimewadia. Kompyuta ziliandaliwa vizuri kabisa ili kuwa imara katika kazi inayotaka kuanza pindi tu Sex Machine atakapoingia mzigoni. "niambie mtaalamu, nini umeweza kuandaa hadi sasa?" swali la Joesan kwenda kwa mtaalamu wa ugunduzi wa mambo makubwa kabisa ya ki technology. huyu ndiye anayehusika na uundaji wa nitambo na mashine mbali mbali za kampuni hiyo. anafahamika kwa jina moja tu baya Tai, ni raia wa uingereza. ukimuona kwa mara ya kwanza unaweza ukasema ni mpungufu wa akili kwa jinsi alivyo jiweka lakini ni kichwa cha hatari sana. Muda wote ukimkuta ni lazima atakuwa na kijiti mdomoni hiyo ndiyo ilikuwa hobi yake na mara nyingi humkuti kavaa suti au nguo yoyote ya heshima, utamkuta kapita pensi ya jeans na fulana ya kukata mikono. Hilo ndilo vazi lake kuu hata kama aambiwe kunaugeni kutoka ikulu, yeye hahofii. "hakuna jipya zaidi ya lile vazi atakalovaa Sex Machine" alijibu Tai huku akiacha kuchezea kicharazio cha kompyuta yake. "umewezaje kutengeneza vazi bila kumpima?"

    "nilisha muona na vipimo vyake vingine nilichukua kwa dokta Emmy"

    "ni la namna gani hilo vazi?" swali jingine kutoka kwa Joesan kwenda kwa mzungu huyo. Tai hakujibu kitu na badala yake aliamka na kuingia katika kijichumba kitogo sana, aliporudi mahali hapo, alikuwa na kitu cha ajabu sana mwilini mwake akamkabizi Joesan. Joesan alikigeuza kitu hicho na kukigeuza tena na tena lakini hakuelewa kitu hadi alipoamua kuuliza. "hiyo ni rangi halisi ya Sex Mchine hivyo atakapo livaa hilo vazi hakuna ambaye atajua kama kunakitu amevaa mwilini mwake. Ni vazi la ajabu sana hilo nililo litengeneza na nimelitengeneza kwa material ya kipekee mno. Litaendana kabisa na umbo lake lakini hata yeye mwenyewe hatahisi kama amevaa chochote mwilini mwake tena akivaa hilo pekee atajihisi yupo uchi kabisa. Ni vazi la tofauti sana." alitoa maelezo hayo mtaalamu huyo na kumfanya Joesan abaki mdomo wazi. Kilikuwa ni kitu cha ajabu sana kwake na ni mara ya kwanza alikuwa analisikia jambo hilo.

    "nini kazi yake sasa?" akauliza. "hili litakuwa linarahisisha kazi yetu kwa urahisi zaidi litakuwa linanasa kila anachokifanya Sex Machine.....!"

    "what?" akashtuka Joesan. "ndiyo, kila atakapokuwa ana sex ndipo litakapoanza kufanya kazi vazi hili, ni automatic ni maalumu kwa kazi hiyo tu si nyingine na ndiyo maana nimelipa jina la Sex Machine Cloth (SMC). lina sens maalumu ambayo huhisi tu pale kijana huyo atakapotaka kuanza kazi na ni vazi ambalo litapiga picha za mnato na mjongeo" alimaliza kujibu swali aliloulizwa na alilijibu kwa mapana kabisa. Hapo Joesan moyo wake ukafarijika baada ya kuambiwa kuwa litakuwa lina nasa mambo ya ngono tu na si vitu vingine maana alishaanza kuchanganyikiwa, aliona ni kama ataumbuka kwa jambo hilo kama lingekuwa lina nasa kila kitu. Alilirudisha lile vazi mikononi mwa Tai kasha akatoka mule kwenye kile chumba cha mtaalamu na kuelekea kwenye ofisi ya Suzane. Alimkuta Suzy akiwa anapiga domo na Merina, akavuta kiti akakaa. "mnaongea umbea tu hapo hakuna lolote la maana" akasema Joesan baada ya kukaa. "umbea kwa mwanamke ni kama jadi nakushangaa unaliona ni jambo jipya kwako" akajibu Suzane. "namshangaa hata mimi labda kama na yeye anataka kujiunga" alichangi Merina.

    "wewe yaani mimi nijumuike katika kuongea umbea?"

    "ndiyo, sasa cha ajabu nini" akakazia kabisa Suzane.

    "Merina naona Suzy amekufundisha ujinga kiasi cha kunikosea heshima" akasema Joesan. "aah! Nitakuogopa hadi lini boss" aliongea Merina na wote wakacheka kwa furaha kubwa kabisa. Waliendelea na maongezi ya hapa na pale hadi pale Joesan alipouliza swali lililobadisha mada waliyokuwa wakiiongea mahali hapo. "inabidi tuandae test ya awali lakini itakayo tuingizia pesa pia maana kesho Sex Machine ndo anatoka mtamboni?"

    "shaka ondoa, nimesha kwenda kwenye kitengo cha utalii nimeangalia wageni wanaokuja ili kujua ni nani anapenda huduma hizi"

    "enhe!" akachochea Joesan huku akivutika zaidi na habari hiyo iliyoukonga moyo wake. Suzy akaendelea "nimempata mmama mmoja hivi raiya wa uingereza na tayari tumeshaongea biashara, amesema atalipa dola laki mbili na nusu lakini huduma ikimpendezea atakuwa anaongeza dau kila atakapo hitaji"

    "funtastic, ndiyo mana nakupenda sana Suzane unaukonga sana mtima wangu. kila siku utabaki kuwa karibu yangu Suzy na utazidi kutengeneza pesa nyingi tu. Merina umemuona mwenzako alivyo makini, kuwa kama yeye ili niwe na timu imara na nzuri." alizungumza Joesan kwa furaha kubwa na kumgeukia Merina na kumtaka awe hodari pia. Merina alitabasamu na kukubali kwa kichwa. Joesan alitamani hata iwe ni siku hiyo ili mambo yawe mazuri, alithamini pesa kuliko utu bwana huyo. wakati wakiwa wanaendelea kufurahi mahali hapo, alifika mzee mwenye busara nyingi na kuketi bila ya kukaribishwa. akawatazama watu wote pale na kusema. "nisamehe sana boss kwa kutokukuambia mapema juu ya mipango mibaya ya Mgobo, pamoja na kumuonya kwangu lakini alikuwa mkaidi sana."

    "kwanini sasa hukuniambia hadi nimegundua mwenyewe?" aliuliza Joesan akiwa amebadilika kabisa kama sie yeye aliyekuwa akicheka muda huo. "ndiyo maana nikatanguliza msamaha kwanza kwa kujua ni kosa nilifanya lakini pamoja na hayo yote niliamini kabisa kuwa anajisumbua sana yule na naamini ulikuwa unamuona kwa kila nyendo" aliongea Rafael kwa unyenyekevu wa hali ya juu kwani ni kweli alifanya kosa la kuto kutoa taarifa za uhatari wa mtu mmoja. Joesan akamshika mkono mzee huyo na kumuambia kuwa anamuamini na anamtegemea pia hivyo asingependa kuona anafumbia mambo yanayoweza kuhatarisha usalama wake na usalama wa kampuni kwa ujumla. Mwisho akahitimisha kwa kumuonya mzee huyo kwa kumwambia, hawezi kufumbia macho ujinga na hatomvumilia mtu atakayesabisha ujinga, atauwa kama alivyo muuwa Mgobo. Rafael akashusha gunia zito la pumzi na kujiweka sawa kitini, akashukuru na kuaga akiwaacha watu hao wakiendelea na soga zao. Neno la Joesan la kumwambia kuwa atauwa kama alivyomuua Mgobo lilimshtua kidogo. Hakutegemea kusikia kuwa Mzee mwenzake aliyekuwa akimshauri mambo ya busara na muhimu kuwa amekufa mapema.kiasi hicho.

    "nilimwambia lakini kuwa plan A. Aliyoipanga, imeshindwa na plan B pia itadhindw na hata uhai ataukosa. Amejitakia mwenyewe bwana mimi sina lawama tena kwake" aliwaza mzee huyo na kuelekea inje ya jingo hilo.

    Asubuhi ya siku iliyofuata, wafanyakazi wote walikuwepo katika chumba maalum cha siri na kumpokea Chriss akiwa tayari ni Sex Machine kamili. Aliletwa kijana huyo aliyekuwa amepoteza kumbukumbu zote kichwani mwake, kila kitu alichokuwa akikiona kilikuwa kipya machoni mwake. Ni kama alikuwa amezaliwa upya kila kitu alihitaji kuelekezwa. Hakuwa amepoteza uwezo wake na utaalamu aliokuwa nao bali alikuwa hamkumbuki mtu yeyote yule akilini mwake ni kama mtu aliyekuwa hana ndugu. Joesan alisogea .......................................



    Joesan alisogea karibu ya kijana huyo na kumuuliza kama labda anamkumbuka au kama alishawahi kumuona mahali. Kijana huyo akajibu kwa kichwa kukataa kuwa hamfahamu na hakumbuki kama walisha wahi kukutana. Joesan akatingisha kichwa juu chini na kutabasamu. Akamgeukia daktari na kumkonyeza kama ishara ya kumpa heko kwa kazi nzuri aliyoifanya, daktari akatabasamu kwa kupokea pongezi hizo kutoka kwa bosi wake ambaye ni mtu muhimu sana kwake. "anatakiwa kufundishwa kila kitu kwa sasa. uwezo wake wa utambuzi wa kitaaluma haujapotea, tulichopoteza ni ufahamu wa kumtambua mtu yeyote hata kama aliishi nae miaka mingi na sasa atakuwa anaamini zaidi alichoambiwa na kukihifadhi. Hakuna mtu atakayeweza kumbadilisha kile alichokihifadhi awali baada ya kupewa bali atakuwa tayari kupokea kitu kipya na kukifanyia kazi, pia hakuna mtu atakayeweza kumbadili kutoka hivi alivyo na kurudi kama awali tunaoweza ni sisi wenyewe." alijitapa kwa tambo kubwa huku akitoa maelezo daktari Emmy. Wote pale wakatikisa vichwa kuafiki kisha daktari akaendelea.

    "ni muhimu ajifahamu yeye ni nani kwa sasa yaani jina lake. pili, aelezwe kuwa yeye ni mtu wa namna gani. Hapo sasa atakuwa tayari kitumiwa na kwa uwezo mkubwa aliokuwa nao itamchukua siku moja tu ya mafundisho hayo" alihitimisha daktari na kukikabidhi kiumbe hicho kipya kilichokuwa kimefungwa nguo za ajabu na kikapokelewa na Joesan. Joesan akageuza shingo kila upande na kumtazama Merina. Akamuita asogee karibu na kumkabidhi Chriss ama Sex Machine kama ilivyofahamika. "hakikisha anakuwa fiti kwa kila kitu mfundishe na umueleweshe kazi anayotakiwa kuifanya kisha utamvisha nguo zake ambazo tulizihifadhi kabla ya kumuingiza mtamboni na unirudishie mimi." alitoa maelekezo Joesan na kumgeukia tena mzee Rafael akamwambia "wewe utashika nafasi aliyokuwa ameshika Mgobo. Utaendesha mazoezi makali kwa vijana naujua weledi wako wa mafunzo na naamini utawaimarisha vijana. Suzane baada ya hapa tuonane na wengine wote naomba muelekee kwenye vitengo vyenu na mkumbuke kuwa kazi inaanza rasmi siku baada ya kesho." alimaliza kutoa maelekezo hayo na kutoka mule ndani akifuatiwa na Suzane. Walifika ofisini kwa Joesan na kukaa kisha Joesan bila kukawia akaongea. "Suzane ujue lingekuwa si jambo la busara sana kama ningelizungumza hili pale, liko chini yetu sisi kama sisi sawa?"

    "ndiyo boss" akajibu Suzane. bwana huyo akaendelea. "ewaa! Sasa cha kufanya kwa sasa wewe ni kufuatilia kwa siri sana ujue ni wapi huyo mteja wetu anafikia kabla hata hajaondoka kwenda kutalii si ndivyo mlivyo kubaliana?" akauliza. "yaa ndiyo," alijibu binti huyo. "basi ukishajua hoteli ambayo atafikia, hakikisha umejua na ulinzi uliopo hotelini hapo ili iwe rahisi kumueleza Sex Machine nini cha kufanya. Na itatubidi sisi tuwe tuna muelekeza kwasababu hatutampa ramani yoyote kama itakavyofanya kampuni"

    "ok, nimekuelewa boss tegemea majibu mazuri kabla ya saa 12 jioni." alijibu Suzane na kutoka mule ofisini kwa bosi wake na kuianza kazi hiyo rasmi. Joesan alitulia pale kitini akitafakari hiki na kile, akishika hiki na kutazama kile. Mara ashike simu, mara file, hakuwa na la kufanya ofisini hapo. aliwasha kiyoyozi kwa spidi aitakayo na kujilaza pale kitini na kuyaruhusu mawazo yajiendeshe kichwani mwake. Pesa ilimgeuza kabisa bwana huyu, upole wake wa zamani alipokuwa anafanya biashara za kawaida, uliyeyuka wote na kufikia hali ya kuwa mtu muogopwa. alikumbuka jinsi alivyokuwa akimfuata rafiki yake wa zamani bwana Isihaq na kumtaka msaada wa kuweza kuikuza biashara yake. kipindi hicho akiwa bado hajakutana na mr. Lee Kim na kumbadilisha kabisa kwa kumtangazia utajiri. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Bwana Isihaq akamuahidi kuwa wiki inayofuata kuna kiasi kikubwa cha pesa kinatarajia kuingia hivyo kabla pesa hiyo haijaingia bank, ni lazima amkatie rafiki yake huyo kiasi kikubwa cha pesa ili ajikuze kibiashara na kuwa kama yeye kwenye nyanja hizo za kibiashara. Joesan alifurahi sana na kuona sasa ile hali ya kubangaiza inakwenda kufa na kutoweka kabisa. Alimuamini sana Isihaq, hakuwa mtu wa kupindisha ahadi, anachokiahidi ujue ni lazima kitimie. Ahadi aliyoahidi Isihaq haikufika, japo ilikuwa ikikaribia kwa kasi sana. Bwana Joesan akatembelewa na ugeni dukani kwake. Ugeni huu haukuchukua muda ukajenga urafiki na kumjengea tamaa bwana Joe na kwakuwa mgeni alikuwa ni mtu mweupe Joe akaona hapo ndipo palipokuwa na njia nyepesi ya kufikia malengo yake ya kuwa mtu tajiri mwenye pesa lukuki na kuwa mtu maarufu pia. Mgeni akazidi kujizatiti kwa kumpa mwenyeji wake sifa za kuwa anaweza kufika mbali kama ataachana na dhana za mimi bado zamu yangu, mimi bado Mungu hajanipangia au mimi bado ni mdogo kibiashara hivyo siwezi kushindana na wafanya biashara wakubwa. Pia akamwambia uwoga wa kufanya jambo la haraka ili yajayo taratibu yapate nafasi ni mbaya sana na asiogope kuondoa mmoja ili kuwakaribisha wengi anaolingana nao. Hapo Joesan akashindwa kuelewa ikabidi kuuliza. Hapo ndipo alipoanza kusukwa na kujazwa sumu moyoni mwake na hatimaye akawa na tamaa ya kufanya chochote na kwa wakati wowote kwa mtu yoyote yule. "ninaye rafiki ni tajiri kiasi na anajimudu" alisema Joesan alipoulizwa kama yupo mtu atakayemfanya yeye kuanza kumiliki pesa nyingi kwa wakati mmoja. "uwa na nikufundishe mbinu za kuwa mtu tofauti" ndivyo alivyoambiwa Joesan. bwana huyo tamaa ya kumiliki pesa kwa haraka ikamjaa, akasahau ahadi aliyoahidiwa na rafiki ya kupewa kiasi kikubwa cha pesa kama mtaji na kutaka kumfanyia ubaya. Aliyaamini maneno ya huyo mkorea kwa asilimia mia moja kuwa ukitaka kuwa tajiri usiwe muoga wa kuamua unacho fikiri. "nitawezaje kuuwa sasa?" akauliza Joesan. "kwanza uwe tayari kufanya hivyo my friend, uko tayari kumuuwa rafiki yako kwa dhati kabisa?" ndivyo alivyokuwa akiulizwa Joesan naye akajibu kwa ajili ya pesa yuko radhi hata kumuuwa ndugu yake wa tumbo moja. Jibu hilo likamfanya Mkorea huyo afurahi hadi moyoni kabisa na kuona amepata mtu sahihi kabisa. mbinu zikasukwa kwa siku chache hata kabla ya pesa aliyokuwa akiisubiria Isihaq haijaingia. mipango ilipokamilika, mbinu za kumuuwa Isihaq zikakamilika pia,Joesan akatekeleza mauwaji hayo. Na hapo ndipo alipobadilika kabisa kimaisha na kiroho. Hakuwa yule Joesan mpole na mpenda haki bali alikuwa mnyama, katili na muuwaji huku akiwa tajiri mkubwa akilindwa na wema wa bandia aliouwanzisha wa kutoa misaada katika majumba ya ibada na kuwasaidia wajane, wazee na watoto yatima. Ule umaarufu aliokuwa akiuhitaji akaupata. Akawa ni msamalia mwaema alijivika ngozi ya Kondoo huku akiwa ni Chui mbaya ndani yake. akakenua tabasamu la kejeli na kujinyoosha pale kwenye kiti chake cha kiofisa na kausingizi kakaja na kumtoa kwenye yale mawazo ambayo ni dhahiri akiyakumbuka, nafsi inamsuta. Alikuja kushtuka baada ya kama dakika kumi na tano mbele, alijipangusa uso lake baya na kukumbuka kitu. Simu. Ndiyo, alikumbuka kuwapa taarifa jamaa zake wa kukaa mkao wa kula kwano mambo tayari yalikuwa mazuri. akatazama saa ya ukutani tayari ilikuwa ni saa kumi za jioni na ushenzi. Akachoropoka pale ofisini na kueleke nje yalipo maegesho ya magari.



    "habari yako kaka?" alianza kwa kusalimia Merina akiwa karibu kabisa na Sex Machine. "safi tu dada mrembo, samahani, unaweza kuniambia mimi ni nani?" aliuliza Sex machine. Kiukweli ni kwamba alikuwa hafahamu chochote kuhusu yeye, alikuwa ni kama flash disc empt. "jina lako ni sex Machine hilo ndilo unalotakiwa kulifahamu hakuna jina jingine zaidi ya hilo na uko hapa kwa aijili ya boss. Unatakiwa kumsikiliza yeye kwa kila kitu, yeye ndiye kiongozi wako kwa sasa hata baadae." elimu ilianza hivyo akafundishwa vingi. Mwisho baada ya mafunzo ya utambuzi akatakiwa avue nguo alizo nazo ili akabidhiwe nguo zake ambazo pia hakuzikumbuka kama ndizo alizokuwa akizitua awali. Hakuwa akiogopa kitu Sex Machine, Akili yake ilisshabadilika mazima, alikuwa ni mtu wa fanya hiki na kukitekeleza na siyo kupinga. Alivua nguo mbele ya binti huyo. "my God! Mbona ni kijana mzuri sana huyu kaka? Oooouu yaaa, cheki alivyo na mpini wa haja jamani hata siamini" alijisemea moyoni Merina. Aliganda kabisa na kujikuta akisahau hata kufanya kile alichokikusudia. Macho yalimganda mahali kilipo kiungo cha uzazi cha kijana huyo. Sex machine alikuwa hajui chochote kitakachofuata hapo alibaki amesimama tu akimtazama binti huyo ili amuelekeze hatua inayofuata hata kama angemwambia abakie hivyo hivyo mtupu angeona ni sawa tu, akili ya kijana huyo iligeuzwa na kuwekwa katika utayari wa jambo lolote lile hata kama baya. Merina alijikuta akilegeza nguo zake na kumsogelea Sex Machine, alikuwa katika hali mbaya tayari ya kutaka kufanya nae ngono kiumbe huyo. "ni mara moja tu hakuna madhara yoyote, anamwili mzuri sana amenisisimua kwakweli." aliongea Merina huku akimalizia nguo yake ya mwisho ili aweze kuivunja amri ya sita miongoni mwa zile amri kumi za Mungu na ni amri ngumu inayowafelisha wengi sana katika harakati za kujizuia kuitekeleza. Sex Machine akaona mahali panapo leta mtafaruku katika nyumba za wanandoa, sehemu ambayo ndiyo chanzo cha usaliti katika mapenzi. Kama mwanaume aliyekamili, vyombo vikanyanyuka. Kidume mwenye hisia kali akataka mzigo na alitengezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Akamvaa Merina na kumpandisha kwenye meza iliyopo ndani hapo kasi ya kumcheze binti huyo ikawa ya aina yake, Merina akajikuta kwenye raha ambayo hakuwahi kupewa na mtu yoyote yule. Akashindwa kujizuia kupiga kelele, sauti za mahaba zikakimeza kile chumba. Mtoto akanyanyaswa na mwili wake mwenyewe, akaomba sex machine ale mzigo sasa maana hicho ndicho hasa kilichomvutia. Ni wajibu wake kutekeleza alichoambiwa. Akazamisha mpingo ndani ya kimia na kuanza purukushani. kasi iliyokuwa ikitumiwa hapo ni ya aina yake. mchezo huo ulimvutia sana Merina alitamani kijana huyo asishuke. kutoka Mwilini mwake kumbe hakujua kuwa amekosea sana. siku hiyo

    ilikuwa si ya kumpa penzi kijana huyo ambaye ametoka kwenye mtambo. Nguvu alizokuwa nazo ni kubwa na ndiyo maana daktari akatahadharisha mapema kuwa asitumike kwa siku hiyo hadi siku inayofuata, kiherehere chake cha tamaa kimemungiza kusiko Merina. Moto wa msuguano ukaongezeka, ule utamu aliokuwa akiusikia ulianza kupotea taratibu na alianza kuhisi maumivu. Sasa akawa anaomba amalize ili tu apate kupumua. Sex Mchine hakumaliza na wala dalili ya kufanya hivyo haikuwepo. akawa anageuzwa tu kwa kila mkao mara huu mara ule, Merina akanza kuhisi mauvivu yasiyo pimika, kelele za kumtoa kijana huyo mwilini mwake, hazikufua dafu. Akaona ni bora atumie nguvu kumnasua maungoni mwake napo ikashindikana kiumbe huyo alishakuwa katika moto mwingine. raha ya mchezo huo ilishamkolea. Merina akaona sasa anachubuka, sehemu zake za siri alihisi zikitoka damu, maumivu ndiyo yalikuwa hayasemeki. Kikaanza kilio cha kimyakimya hatimaye sauti ikaongezeka. Merina alilia na .................................................



    kusaga meno. Sex machine hakutoka ndiyo kwanza alikuwa akifumba macho kwa utamu aliokuwa akiupata kwa binti huyo, wazo la kuhisi kuwa mwenzie anaumia wala hakuwa nalo kabisa. Sauti kali za kilio zikamkuta dokta Emmy ambaye alikuwa akijiandaa kutoka kurejea zake nyumbani mapema maana hakuwa na kazi siku hiyo. Sauti hiyo akaijengea mashaka na bahati nzuri hakuipuuzia. Akatoka mbio kuitafuta sauti inapotokea ndipo alipokuja kugundua kuwa sauti hiyo inatoka katika chumba ambacho Merina alipewa kazi ya kumfundisha Sex Machine jinsi ya kujitambua. Akazama ndani ya chumba hicho kwa ghafla ndipo alipomkuta Merina katika hali mbaya sana. Sex Machine akiwa anazidi kushindilia huku dalili za kushuka zikiwa hazipo. Dotka Emmy akampiga kofi kijana huyo, alinyanyua macho akamkemea kwa sauti ya juu ya kumtaka aache kufanya hicho anacho kifanya. Sex machine alinywea na kujitoa mwilini mwa Merina akiwa mpole kabisa. Bado mashine yake ya kazi ilikuwa hewani. Hayo ndiyo yalikuwa maisha mapya ya Chriss, maisha ya kutumiwa kama chombo cha kumtajirisha mwingine kwa kutumia mwili wake. Merina alikuwa akijiangalia kila wakati kama yupo sawa, kilanga chote kilimuisha, alimshukuru sana daktari laa kama si yeye, angeimba kila wimbo anaoujua. Dokta Emmy alimtaka Merina avae nguo zake na watoke mule ndani.



    **********************************************

    Joesan alikuwa ndani ya nyumba yake ya siri ambayo aliitumia kufanya mambo yake ya siri. Alichukua simu yake ya siri ambayo ni aghalabu sana kuitumia na amekuwa akiitumia kwa kuwapigia watu wake maalum tu. Aliandika namba ya mtu aliyemhitaji na kuiweka sikioni.



    SAN ANTONIO.

    Simu ndogo ya kiganjani iliyokuwako mezani ilitetema, mmiliki wa simu hiyo aliitazama kwa muda simu yake na kugeuza macho pembeni ambako alikuwako binti yake kasha akaikwapua ile simu na kutoka nayo nje ikiwa bado inaita hivyo hivyo. Akaipokea na kiweka sikioni huku akiangalia usalama wa hapo alipo kama yuko mwenyewe ama laa. BC. Ndilo jina la mmiliki wa simu hiyo. "habari ya muda huu mr.?" alisalimia kwa lugha ya kiingereza bwana huyo. Upande wa pili wa simu ukajibu ni nzuri tu kisha mtu huyo wa upande wa pili akaelekea kwenye kiini cha kupiga simu hiyo kwa mtu huyo. Alieleza kuwa ni muda wa kuwa tayari hivyo ahakikishe kila kitu kinaandaliwa katika utaratibu mzuri. "mizigo iko safi J, ni huyo mvukishaji tu ndiye aliyekuwa akisubiriwa." alisema Black Clocodile. upande wa pili ukaridhika na maneno yale kisha akaahidi siku ambayo kiumbe huyo atafika nchini humo kuchukua mzigo huo na kuupeleka nchini Brazil kwa biashara ili wao waendelee kuneemeka. "ok, sawa" maongezi hayo yakahitimishwa namna hiyo. Lakini ndani ya nchi hiyo hiyo ya Marekani. ndani ya jiji la Los Angeles huko California, ndani ya mjengo wa kisasa kabisa. Kulikuwa na binti aliyekuwa amejianika sebuleni kwa mavazi yake ya kihasara hasara ayapendayo. Huyu ndiye yule yule binti tusiyemjua ni nani, alikuwa amepiga bikini nyekundu kama ilivyo ada yake na juu alikuwa na kitopu cha rangi ya pinki. Alikuwa akiyafuatilia maongezi ya watu wale bila mawimbi yoyote na alikuwa akiyarekodi. alipomaliza aliweka tabasamu safi usoni mwake na kuchomoa flash fulani aliyokuwa ameipachika kwenye kifaa chake hicho na kupandisha mguu mmoja juu ya mwingine na kuegamia kwenye kiti alichopo na kujimiminia kinywaji tumboni mwake. "J? Ni nani huyu?" alijiuliza binti huyo ambaye tunaweza kumuita bikini nyekundu kilingana mtindo wa uvaaji wake. Jibu hakulipata kwa urahisi akaishia kumalizia na neno from Tanzania. Kisha akamalizia kile kinywaji na kutoka lile eneo na kuelekea chumbani kwake ambako alivua nguo zote na kubaki mtupu kisha akaelekea maliwatoni.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya Joesan kuongea na BC, aliishusha ile simu na kuvuta pumzi nyingi kwenye mapafu yake na kabla hajazitoa pumzi hizo, simu yake ya kawaida ikaita. Alikuwa ni daktari. "ndiyo daktari?" akauliza. "kazi imekwisha tayari tunakusubiri wewe tu boss"

    "ok, niko njiani nakuja" alijibu Joesan na kutoka mule ndani baada ya kuhakikisha kila kitu amekiacha katika usalama umzuri na kuingia kwenye gari yake akaondoka mwendo wa mashindano. Alipofika kwenye kampuni alimchukua Sex Machine na kuondoka naye huku akimuacha dokta Emmy na Merina maeneo hayo. "kama si wewe shost mbona ningekoma leo, hee! Kwanini yule mkaka ana nguvu kiasi kile kama roboti?" alisema Merina akimwambia dokta Emmy na kumfanya dokta huyo aangue kicheko cha haja. "wala usinicheke shost, mwanzo niliona utamu alivyokuwa ananisugua vizuri, nikatamani hata asimalize lakini doo! Mambo yakanigeukia na mchezo mzima ukanitumbukia nyongo. Niliona kama anataka kung'oka na tupu yangu" maneno hayo ya Merina yalizidi kumuacha hoi dokta Emmy kwa kicheko, alicheka hadi anayumba kabisa. "na wewe umezidi bi dada, huoni ukuni, kila ukuni unataka upikie, miti mingine ina moshi bibi wewe utapikia lakini chamoto utakiona. Macho yatakuiva hayo hadi uhisiwe umwanga. Shost, yule ametengezwa na ni mashine ya ngono ile si kama sisi hatuwezi kumtumia kwa kutufurahisha laa! Tunaweza lakini si kwa pupa kama ulivyo fanya wewe. ametoka leo kwenye mtambo uliokuwa unampika hivyo bado haja poa, ana nguvu za kutembea na wanawake hata sita na wala asichoke pale alipo. Sasa wewe umepeleka kidude chako kimoja hicho na unabahati angekuchana leo." alitoa maelezo dokta na kumfanya Merina aheme kwa nguvu nyingi sana. "yote hayo nimeyajuaje mwenzako, nilipokiona kifua kizuri cha mtoto wa kiume yule mihemko ikanipanda, mtoto wa kike kifuniko cha soda kikaniwasha. Lakini sasa kwa mtindo ule si watakoma hao watakao muhitaji maana mimi hapa nilipo sina hamu nahisi pia kanichana, kidude kinaniumaje hapa nilipo maana nilitoka damu kabisa." alisema Merina na kuhoji. "no, kuazia kesho na siku zijazo atakuwa kawaida na jinsi alivyo mtundu yule kaka, atatuingizia pesa nyingi sana maana ninaimani watu watakuwa wanalipa double kwa jinsi atakavyo wafurahisha"

    "ni kwa muda gani atakuwa anafika kileleni?" akauliza tena Merina. "kuanzia dakika 30 hadi 45 kwa mzunguuko wa kwanza na atakayetaka kurudia hapo namaanisha, atakayelipia tena kwa mzunguuko mwingine ni lazima ajue kuwa kuanzia dakika 45 hadi 55 mtu huyo atakuwa mwilini mwake. Lakini kwa jinsi atakavyokuwa anakuingilia, utatamani hata asimalize ni kitaalamu zaidi" alijibu daktari na kumuweka Merina katika hali ya usawa maana alishaanza kumuogopa Sex Machine. "siwezi kukubali huyu mtu anipite ninakuhakikishia ni lazima awe tulizo langu ni wa ukweli sana. Sijawahi kutengeneza Sex Machine mzuri na mwenye mwili wa kuvutia kama huyu

    "hata mimi wee, lazima nirudie mchezo ananivutia huyu kaka hadi napagawa" alidakia Merina na kuonesha kuwa hatanii. "punguza umalaya mwanamke unafikiri Suzane akijua atakuacha"

    "bibi wee, acha woga hii mali ni yetu wote hakuna aliyesaini mkataba naye hivyo atagonga huku na kule"

    "utakufa malaya wewe shauri yako, hebu niende zangu nyumbani miye giza lisije kunikuta hapa"

    "nikifa mimi sasa wewe ndo utabaki, kama mimi malaya wewe ndiyo changu doa kabisa lione kwanza kilivyo na ndiyo maana hukondi wewe hata kama ukifanya dayati kwa kukalia madude makubwa yasiyo saizi yako" akarusha dongo Merina lililomuendea moja kwa moja dokta Emmy ambaye alikuwa tayari ndani ya gari. Emmy alimuangalia Merina na kumpindishia mdomo kama kakumbwa na degedege, akasema "dawa yako ilikuwa ni kukuacha ufuluguswe hadi kidude chako kingeota sugu hiko" dongo hilo lilimfanya Merina kupandisha kioo chake cha gari maana akikumbuka kitu alichofanyiwa damu zote za mwili zilimkimbia.

    "

    mimi ndiyo Joesan, najua ulisikia nikitajwa lakini hukuwa ukinifahamu" alijitambulisha Joesan kwa Sex Machine walipokuwa wanaingia kwenye nyumba moja ya kisasa kabisa. Ni nyumba ambayo ilikuwa haikaliwi na mtu kifupi ni kwamba ilikuwa ni mpya kabisa. Sex machine akatikisa kichwa kuafiki aliyoyazungumza bwana huyo. Ni kweli alikuwa hamfahamu kwani kila kitu kiliharibiwa na kusahaulishwa kabisa na hapo alikuwa akiingiza vitu upya ndani ya ubongo wake. Kitu kimoja tu ambacho hakijaharibiwa ni taaluma aliyo nayo lakini kila kitu kilifutwa. Huyo ndiye Joesan, mnyama wa unyamani. "mimi ndiye mwenye amri kuu juu yako, si kama huto sikiliza amri za wengine laa! Ila kauli nitakayoitoa mimi ndiyo itakuwa ya mwisho kwako." alisema huku akimzunguusha ndani ya lile jengo kuanzia ndani nje na hata vyumbani. Walipofika chumbani, wakatulia na kuendelea kuongea. "nadhani umeiyona hii nyumba vizuri?" Joesan aliuliza. "ndiyo nimeiyona"

    "basi hapa ndipo yatakapokuwa maisha yako yaani hii ndiyo nyumba utakayoishi hadi pale utakapoamua kutafuta makazi mapya ila kwa sasa ni hapa."

    Sex machine alifurahi sana hakuamini macho yake kukabidhiwa nyumba nzuri kama ile. Si nyumba tu bali na vyote vilivyomo ndani ya nyumba hiyo. Alifungua kabati la chumbani humo na kukuta mavazi ya gharama yakiwa yamepangiliwa kwa umaridadi mkubwa kabisa, vyote hivyo mmiliki ni yeye. "kila kitu ni chako humu ndani" sauti ya Joesan ikamfanya kijana huyo kutoka katika hali aliyokuwa nayo na kumuangalia mtu huyo aliyejitambukisha kama bosi kwake. "hii ni kadi yako ya benki tayari nimekuwekea kiasi cha shilingi milioni 15 na itakuwa inaongezeka kwa kiasi kikubwa kila utakapokuwa umetoka kufanya kazi huo ndiyo mkataba wangu mimi na wewe na hautovunjika" maneno hayo ya Joesan yalizidi kumshangaza kijana huyo na kuzidi kumuona mtu huyo ni wa pekee sana. Alizidi kumpenda kwa kila hatua na kuanza kumuona wa thamani. Kazi ya kufanya ngono ndiyo ilikuwa kazi yake na alishaikubali tayari hata kama angetokea mtu na kumwambia aiache ni sawa na kuununua ugomvi kwa bei chee kabisa. Joesa alifika kwenye kabati la vioo lililokuwa limeunganishwa na ukuta, akaufungua mlango wake hadi mwisho kisha akamtaka Sex machine asogee karibu. "hili ndilo vazi lako la kazi, hakikisha kila utakapokuwa unataka kufanya ngono, vazi hili linakuwa mwilini mwako yaani ni bora ivuke ngozi yako kuliko hili vazi wakati wa sex na utalivua pindi tu utakapofika hapa" alizidi kutoa lecture Joesan kwa kijana huyo na kumwambia kuwa kazi atakayoifanya siku inayofuata kama itakuwepo, hatotakiwa kulivaa vazi hilo kwani kazi hiyo ni test tu kwake ili.......



    ili kuona kama ameiva. alipomaliza kusema hayo, akabonyeza batani fulani ya rangi nyekundu iliyopo kwenye kola ya lile vazi lililokuwa limetundikwa vizuri kwenye enga ya mule ndani ya lile kabati. Akamtaka Sex machine atoe nguo zake zote asibakiwe hata na nguo moja kisha akamuamuru asogee karibu kabisa na lile vazi. Akamwambia ageuke na alipe mgongo, Chriss hakupinga alifanya kila kitu alichokuwa akiellekezwa na bosi wake huyo. Akaamriwa atanue mikono mithili ya mtu anayetaka kupaa. Alipofanya hivyo tu, lile vazi likaruka mwilini mwake na kujivalisha lenyewe. Pamoja na kwamba lile vazi lilikuwa mwilini lakini bado alijihisi kama yuko uchi kabisa kwani vazi hilo liliendana na kila kitu kilichopo mwilini mwake kuanzia ngozi, hadi maumbile isipokuwa sehemu zake za siri tu ndiyo zilikuwa wazi lakini ni ngumu kujua kama ziko wazi sehemu hizo. Yalikuwa ni maajabu sana kwa kijana huyo. "vipi lina kubana?" alitupa swali Joesan. Sex machine akajibu kuwa anajiona sawa kabisa na hakuna tofauti yoyote na alivyo kuwa uchi. Joesan akachanua tabasamu la ushindi akijua sasa umilionea ulikuwa ukimuibukia hapo mithili ya mvuvi apigae mbizi na kuibuka palipo na samaki wengi. Alipohakikisha kila kitu kiko sawa, alimwambia abonyeze kitufe kile kile alichokibonyeza yeye awali. CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/Sex machine akafanya hivyo na lile vazi likatoa mlio mdogo kama uminyavyo vitufe vya simu aina ya Nokia uanpoandika namba au utakapo kumpia mtu na kutoka kama lilivyokuja na kurudi mahala pake. Akamwambia sasa avae nguo na watoke nje. walipofika nje alimuonesha gari iliyopo maegeshoni, ilikuwa ni Toyota Prado ya rangi nyeusi mpya kabisa. "hiyo ni gari yako na ufunguo na uchafu mwingine wote, uko ndani ya hiyo gari. Ni wajibu wako kuitumia utakavyo hakuna mipaka katika hilo" alipomaliza kusema hivyo Joesan alimpa kijana huyo simu mpya ya kisasa pia akasema. "ipo kadi humo iliyosajiliwa lakini nakujua kuwa wewe ni mtumiaji mzuri wa kompyuta hivyo unaweza kubadili usajili huo utakavyo wewe na hata ile kadi ya benki pia unahaki ya kubadili namba ya siri maana ni yako na utakuwa na uhakika wa ulinzi wa pesa zako." akaweka tuo na kusubiri kama kuna neno kutoka kwa kijana huyo. Halikuwapo neno jingine zaidi ya asante na shukurani za kuzidi zilizomfanya Joesan kujiona ni zaidi ya mfalme. Kitendo cha kumteka mtu fikra na akafuata kila takwa lako si jambo dogo hata kidogo. Ni jambo kubwa na la kujivunia sana Alijiona ni kama Mungu bwana huyo kwa jinsi atakavyonyenyekewa na kiumbe huyo aliyemtengeza na yeye kumtumia vile atakavyo. "nitakupigia jioni nikupe taarifa kamili na jinsi ya kuanza kazi" alisema Joesan kisha akapanda kwenye gari yake na kutokomea.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog