Search This Blog

Monday, October 24, 2022

SHAROBARO WA TANDALE - 2

 







    Chombezo : Sharobaro Wa Tandale

    Sehemu Ya Pili (2)



    Kufuatia sharobaro Dullah kuitwa, aliivaa chupi yake chapchap’ Doreen naye alisimama pale sofani na kuchukua nguo zake na kukimbilia chumbani.

    Zakayo aliendelea kuita ndipo Dullah alitoka haraka pale sebuleni na kwenda jikoni kwa akina Doreen, Zakayo alipoona kijana huyo haitiki alijua alitoka nje ya geti akarudi kumfahamisha fundi Yassin kwamba hakuwepo.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dullah alipoona Zakayo kaondoka alivuta pumzi na kuzishusha akafurahi kwani alijua atakapokuwa akitoka mle ndani asingeonekana, wakati akiwaza hivyo Doreen ambaye tayari alivaa nguo alikwenda na kumshika Dullah begani.

    “Vipi, amejua kama upo humu ndani?” Doree ambaye macho bado yalikuwa yamemlegea alimwuliza.

    “Hajaniona na kaingia ndani,” Dullah ambaye alimlaani sana Zakayo kumkatishia starehe yake alimwambia Doreen.

    “Kama hajakuona vizuri, ili kuwapoteza maboya itabidi nikutoe nje kabisa kwa kutumia mlango huu wa uani, baadaye ugonge geti ujifanye ulikwenda kununua soda,” Doreen alimwambia Dullah .

    “Sasa hiyo soda nitanunua na hela gani wakati kwenye suruali yangu iliyopo ndani kuna shilingi mia tano tu!” Dullah alimwambia mrembo huyo.

    Baada ya kutoa kauli hiyo, Doreen alicheka akamwambia asubiri akaingia ndani kisha kutoka akiwa na soda ya kopo akamwambia atoke nayo nje ili atakapofunguliwa geti ionekane alitoka kuinunua.

    “Du! Kweli wewe mjanja sana,” Dullah alimwambia Doreen kisha aliichukua ile soda ya kopo lakini kabla ya kutoka nje akaona hatakuwa amemtendea haki msichana huyo bila kumbusu.

    “Jamani asante yaani busu lako limenisisimua sana,” Doreen alimwambia Dullah akiwa kamkumbatia bila kujali nguo zake zilizochafuka kwa michanga.

    “Ila basi tu, huyu aliyeniita katuvurugia sana nilitaka kukuonjesha penzi langu,” Dullah alimwambia Doreen.

    Wawili hao wakiwa wanazungumza, si Zakayo akiwa nyuma ya nyumba waliyokuwa wakiweka malumalu akaanza kumwita tena Dullah , kitendo cha bila kuchelewa Doreen alifungua mlango mdogo wa uani na kumtoa Dullah .

    Baada ya Dullah kutoka, Zakayo akaendelea kumwita ndipo kijana huyo aliitika akiwa nje ya nyumba, Zakayo alipomsikia akiitika alikwenda kufungua geti akamkuta Dullah ameshika soda ya kopo.

    “Kaka muda sasa tunakutafuta kumbe mwenzetu umeacha kazi na kwenda kununua soda, hivi utaiweza kazi hii tunayofanya?” Zakayo alimwuliza Dullah .

    “Unajua muda ule sista sijui Doreen kanipa maji nikaendelea na kazi nikaona kiu bado imenishika nikaamua kwenda kununua hii soda kwani huwa nikinywa kidogo inakata kiu,” Dullah alimwambia Zakayo.

    Zakayo alimtazama Dullah alivyokuwa akizungumza na ile soda yake ya kopo aliyokuwa ameishika akaishia kucheka na kujisemea moyoni;

    “Kweli site imevamiwa na sharobaro wa Tandale kwa tumbo, sisi tunawaza kazi yeye tayari kisha kuwa mwenyeji mpaka kaenda kununua soda ya kopo, kweli huyu dogo ni mtoto wa mama.”

    Kwa kuwa walikuwa wakizungumza wakiwa wamesimama pale getini, Zakayo alilifunga kisha wakaongozana kuingia ndani na kwenda moja kwa moja katika chumba ambacho fundi Yassin na wasaidizi wake hao walikuwa wakifanya kazi.

    Fundi Yassin alipomuona Dullah kashika soda ya kopo, awali alifikiria alipewa na Doreen lakini Zakayo akamweleza jinsi Dullah alivyokuwa mwenyeji mpaka kutoka nje na kwenda kununua soda.

    “Yaani alikuwa nje kabisa ya geti?” fundi Yassin alimwuliza Zakayo huku Haruni akiwa amepozi kufanya kazi akimsikiliza.

    “Ndiyo maana yake, si nilikuja kuwaambia nimemwita lakini hakuitika, niliporudia kumwita kwa mara ya pili, nikamsikia akiitika nje ya geti,” Zakayo aliwaambia.

    Fundi Yassin alimkanya Dullah kwamba kilichompeleka pale ni kazi na kumfahamisha jinsi tajiri yao asivyopenda watoke getini ndiyo maana aliwaambia chochote watakachohitaji wamwambie Anne ambaye ni dada wa kazi.

    “Basi bro potezea sikujua, kwa hiyo nikisikia njaa nimwambie huyo dada,” Dullah aliwaambia na kusababisha wote kuangua kicheko.

    Wakati mafundi hao wakizungumza hivyo, Doreen akiwa chumbani kwake mawazo yote yalikuwa kwa Dullah kwani kijana huyo alijua kumsisimua sana.

    “Huyu mkaka anavyoonekana mambo anayaweza, yaani hapa kaniacha mwili wote una ninyevuanyevua, asingeitwa na yule fundi saizi angekuwa kisha nipa raha, na nilivyomisi nanii da!” Doreen aliwaza.

    Baada ya Dullah kuwachekesha mafundi wake alitoka akiwa kashika soda yake ya kopo na kwenda kuendelea na kazi, ambapo aliiweka ile soda juu ya dirisha bila kujua kama Doreen alikuwa kasimama katika dirisha hilo kwa ndani akimwangalia.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dullah baada ya kuchota mchanga kama chepe kumi na kuzirushia eneo alililoelekezwa na Zakayo, akapozi kisha alijishika kiuno na kujinyoosha, kitendo hicho kilimhuzunisha sana Doreen.

    “Jamani huyu kaka anaumia bure tu, ngoja kama ataendelea kuja hapa lazima nifanye mpango wa kumpa sapoti yoyote,” Doreen aliwaza.

    Wakati Dullah akiendelea na kazi, Zakayo alifika kumwangalia, alivyomkuta akiwa kasimama akatabasamu na kujisemea moyoni ‘huyu kazi hii haiwezi na sijui kama kesho atakuja.’

    Zakayo aliwaza hivyo bila kujua kama Dullah alipanga kufika pale site kila siku kwa vile palikuwa na mtoto mkali Doreen ambaye wao walikuwa wakimwangalia tu kama dada yao.

    “Vipi, leo huu mchanga utaisha kweli?” Zakayo alimwuliza Dullah .

    Dullah bila kumficha alimwambia kwa siku ile alichoka sana hivyo angemalizia siku iliyofuata, kufuatia kauli hiyo, Zakayo akacheka na kuingia ndani kumweleza fundi Yassin.

    “Kwa kuwa ni mwanaume ataweza, si unajua hizi kazi unapoonza siku ya kwanza zinakuwa ngumu!” Fundi Yassin alimwambia Zakayo.

    Kufuatia kuelezwa hivyo, Zakayo alipinga na kumwambia Fundi Yassin kwamba Dullah akimaliza wiki pale site atampatia shilingi elfu kumi, fundi Yassin akaishia kucheka.

    Zakayo alipoingia ndani, Dullah alimalizia soda yake kisha akawafuata wenzake waliokuwa ndani na kushangaa jinsi walivyoweka marumaru katika vyumba viwili.

    “Da! Nyie mnapiga kazi sana, kazi hii yote mmeifanya leo?” Dullah aliwauliza.

    Fumdi Yassin amjibu kwamba mbona walifanya kazi kidogo sana siku hiyo, Dullah akabaki akishangaa, fundi Yassin alipomuuliza kama alimaliza kuhamisha mchanga, akacheka sana na kumwambia atamalizia kesho yake.

    Kwa kuwa fundi huyo alikuwa anauelewa usharobaro wa Dullah , hakumsema vibaya kwani alijua atazoea taratibu lakini kwa upande wa Zakayo alijisemea moyoni kwamba Dullah hakuwa mfanyakazi, sijui kwa nini hakumpenda kijana wa watu.

    Baada ya kufanya kazi hiyo, Dullah hakuendelea tena na kazi ya kuhamisha mchanga hadi wenzake walipomaliza kazi na baada kuoga kwenye bafu la nje, fundi Yassin alikwenda kuonana na Doreen ambaye alimpa bahasha iliyokuwa na hela.

    Baada ya kukabidhiwa alimpatia Zakayo shilingi 30,000 halikadhalika Haruni kisha akaiweka ile bahasha mfukoni, Dullah hakuwa na wasiwasi kwani alielewa kingeeleweka mbele ya safari.

    Hata hivyo, Dullah alipenda kabla ya kuondoka amuone Doreen akawa anaplani kuhakikisha anafanikisha hilo, fundi Yassin alipowaambia waondoke akamwambia alihisi kiu hivyo ngoja akaombe maji ya kunywa.

    “Wewe huna lolote, unataka umuone tu Doreen,” fundi Yassin alimwambia Dullah ambaye alicheka sana na kusema:

    “Siyo hivyo bro hayo ni mawazo yako tu mbona mimi nina demu wangu mkali kumpita sijui huyo Doreen halafu mimi mtoto wa kishua kama huyo nitampa nini?” Dullah aliwaambia wote wakacheka.

    “Jamani muda unakwenda, hayo maji nitaenda kununulia mbele ya safari, halafu kumbuka wewe hapa ni mgeni usije ukaleta picha mbaya bure,” fundi Yassin alimwambia Dullah bila kujua kama sharobaro huyo alibakia kiduchu kula tende tamu za mtoto huyo wa kishua.

    “Haya mkubwa nimekuelewa, twendeni jamani,” Dullah aliwaambia.

    Baada ya kutoa kauli hiyo, fundi Yassin aliwaambia waondoke wakatoka lakini wakiwa nje fundi Yassin aliyekuwa kamzoea sana Anne akamwita dada huyo wa kazi ili amuage.

    Licha ya kumwita Anne aliitika Doreen ambaye alitoka nje fasta, na kumwuliza fundi; “ Fundi ndiyo mnaondoka?”

    “Eh! Leo tumefanikiwa kuweka marumaru vyumba viwili kesho tutaendelea,” fundi Yassin alimwambia Doreen bila kujua msichana huyo alikuwa na furaha moyoni ya kumuona Dullah .

    “Hakuna shida, nawatakia safari njema,” Doreen ambaye alikuwa amevaa kama alivyovaa awali aliwaambia.

    Baada ya kumuaga msichana huyo, fundi Yassin, Zakayo na Haruni wakatangulia Dullah alibaki nyuma ambapo aligeuka na kumkonyeza Doreen aliyeachia tabasamu pana.

    Mafundi hao walipotoka getini walishika njia hadi ilipokuwa barabara kubwa ambapo Haruni ambaye alikuwa akiishi maeneo hayo aliwaaga wenzake kwamba wangekutana siku iliyofuata.

    Baada ya kuagana haukupita muda mrefu daladala iliyokea Kisauke mwisho lilifika ambapo wote watatu walipanda, kwa kuwa siti zilikuwa wazi fundi Yassin na Dullah waliketi pamoja.

    Kutokana na uchovu wa kazi, wakiwa kwenye daladala hilo hawakuwa na stori nyingi zaidi ya Dullah kuwatupia macho mademu wazuri aliowaona nje na wawili waliokuwa wamo ndani ya basi.

    Walipofika njia panda ya Wazo Hill maarufu kama Kibaoni, Zakayo aliyekuwa akiishia Bunju alimuaga Yassin na Dullah ambapo fundi Yassin alimsisitiza kuwahi kufika kazini siku iliyofuata.



    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa kuwa kituo cha mabasi ya Kisauke hakikuwa mbali walitumia kama dakika nne wakawa wamewasili ndipo fundi Yassin na Dullah walishuka wakaanza kuelekea Kituo cha daladala cha Kwa Ndevu kupanda gari la kwenda Mwenge ili wakaunganishe la Tandale.

    Wakiwa wanatembea Dullah alikuwa akijiuliza mbona fundi Yassin hakumpatia fedha kama alivyofanya kwa wenzake!

    Hata hivyo, kwa jinsi alivyokuwa akimfahamu fundi huyo alijua wakifika nyumbani angempatia ndipo akaanza kuifikiria safari yao tangu asubuhi alipokutana na yule mrembo kwenye DCM la kwenda Mwenge na wale wasichana waliopandia kituo cha Jogoo walioshukia njia panda ya kwenda Kunduchi.

    Kwa kuwa kichwani alikuwa na namba ya yule dada aliyekutana naye Mwenge, akazitamka kimoyomoyo, sifuri, saba, tano, nane, nne, mbili, arobaini, na kumalizia ya mwisho akaachia tabasamu lililoonwa na fundi Yassin.

    “Mwenzangu kimekufurahisha nini maana naona unatabasamu?” fundi Yassin alimwuliza Dullah .

    “Bro bwana, kwani hujamuona yule dada alivyotuangalia kisha kuanza kutikisa makalio yake?” Dullah alimchomokea fundi Yassin.

    “Hapana sijamuona, yupo wapi kwani?” fundi Yassin alimwuliza Dullah .

    Kufuatia kuulizwa hivyo, Dullah alimwambia alikwishaondoka ndipo wakaendelea na safari hadi walipofika kituoni ambapo walipanda gari la kwenda Mwenge.

    “Bro kweli kuna watu wapo vizuri sana duniani, wakati sisi tunafikiria hela ya kula wengine wanaporomosha majengo namna ile?” Dullah alimwambia fundi Yassin.

    Baada ya Dullah kuuliza hivyo, fundi Yassin alimweleza kwamba maisha ndivyo yalivyo na watu wote hatuwezi kufanana kauli ambayo iliungwa mkono na Dullah .

    Akiwa ameketi siti ya dirishani, Dullah akaanza kumkumbuka Doreen hasa alivyokuwa akizichezea embe bolibo zake, si mkuu wake wa kaya akaanza kuchangamka.

    Kijana huyo alipoangalia eneo la makazi ya mkuu wake wa kaya na kumuona alivyokuwa, akaachia tabasamu ambalo lilionwa na fundi Yassin ambaye alimwuliza alifurahishwa na nini!

    Kwa haraka Dullah alimuonesha fundi Yassin mzee mmoja aliyekuwa amekaa siti ya kushoto kwao aliyekuwa amepitiwa na usingizi na kuacha kinywa wazi, Yassin alipomwangalia mzee huyo naye akaachia tabasamu bila kujua Dullah alimpiga changa la macho.

    “Maisha dogo, unaweza kukuta tangu alipoondoka nyumbani kwake asubuhi hajanywa chai na huko alikokwenda hakijaeleweka hapo kajichokea mzee wa watu,” fundi Yassin alimwambia Dullah kwa kumnong’oneza.

    “Ni kweli bro nakubaliana nawe,” Dullah alimwambia fundi wake.

    Kama ilivyo kawaida ya mashorobaro kupenda mambo ya mademu na mambo mengine ya kivijana, wakati safari ikiendelea Dullah alikuwa akimtupia macho msichana mmoja denti aliyekuwa kabeba mkoba wake mkubwa mgongoni.

    Denti huyo ambaye alivyoonekana alikuwa kidato cha tano au sita kaumbika vizuri na licha ya kuwa ndani ya sare za shule sketi aliyovaa ilionesha namna alivyojazia.

    “Isingekuwa jela, mtoto mzuri kama huyu ni kulamba tu kwa kwenda mbele,” Dullah alijisemea moyoni baada ya kukitathmini kifua kitamu cha denti huyo kilichopambwa na viembe bolibo f’lani hivi.

    Gari lilipofika kituo cha Interchick, waliingia watu kibao akiwemo msichana mmoja mweupe aliyekuwa kava suruali ya jeans na kitop cha njano, Dullah alipomtupia macho moyo wake ukapiga paa!

    Wakati Dullah akiwa katika hali hiyo, fundi Yassin ambaye alikuwa akimfahamu vyema Dullah, alimbonyeza dogo huyo pajani, Dullah apomwangalia akamnong’oneza kwa kusema:

    “Umeyaona mambo yako hayo?”

    “Kaka nimeyaona, da mtoto kaumbika halafu mapigo kama haya ndiyo ugonjwa wangu mkubwa! Dullah alimwambia fundi Yassin.

    “Wewe si unajifanya mkali wa viumbe hawa, ukipata namba ya huyo dada au ukifanikiwa kuchonga naye nitakupa wekundu mmoja nje ya hela ya kazi,” fundi Yassin alimtania Dullah .

    “Bro, masihara hayo!” Dullah alimwambia fundi wake.

    “Siyo masihara, wewe fanya kama nilivyokuambia nikupe mpunga wako,” fundi Yassin alimwambia Dullah .

    Kauli ya fundi Yassin ilimuweka katika wakati mgumu sana Dullah ambaye hakuelewa ataanzaje kuzungumza na yule msichana kisha kuipata namba yake ya simu!

    “Sikubali nasema sikubali, kama mimi ndiye Dullah lazima nitaipata namba ya huyo mrembo kwanza hawa wapo duniani kwa ajili yetu,” Dullah aliwaza.

    Baada ya kuwaza hivyo, Dullah alimuomba fundi Yassin ahamie upande wa dirishani, fundi Yassin huku akicheka akahamia siti ya dirishani huku akisema alikuwa akijisikia vibaya hivyo kukaa dirishani ingemsaidia kupata hewa.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Fundi Yassin alitoa kauli hiyo kuwazuga abiria wengine wasiushtukie mpango wake na Dullah , kisha alimnong’oneza Dullah kwamba kama kweli alitaka teni ya fasta kazi ilibakia kwake.

    “Kabla ya kufika Mwenge ndiyo utabaini mimi ni Abdallah Nzamba a.k.a Dullah ,” Dullah alimwambia fundi Yassin kwa sauti ya kunong’ona.

    Basi likiwa limefika Tangi Bovu, Dullah alimgusa yule mrembo mgongoni ambaye wakati huo alikuwa kasimama pembeni yake na kumwambia aketi, kwa kuelewa Dullah alitaka kushikia kituo cha Bondeni yule mrembo aliketi na Dullah akasimama.

    “Asante kaka yangu!” mrembo alimwambia Dullah .

    “Usijali, ingawa bado sijafika mwisho wa safari nimeona nawe ukae japo kidogo,” Dullah alimwambia yule msichana.

    “Asante sana kaka kwa kunijali,” yule mrembo alimwambia Dullah bila kujua lengo la kijana huyo.

    Wakati Dullah akizungumza na mrembo huyo, fundi Yassin alikuwa kishamvulia kofia na kujisemea moyoni:

    “Kweli huyo dogo ni balaa hadi kufika Mwenge atakuwa kamuweka sawa huyu kiumbe,” fundi Yassin alijisemea moyoni.

    Gari lilipofika Makongo, Dullah alimtania yule dada kwamba jioni ile alikuwa akielekea wapi, mrembo akamwambia Keko.

    “Keko ndiyo unakoishi au unakwenda kazini?” Dullah akamwuliza.

    “Nyumbani!” mrembo akamjibu.

    Baada ya mrembo huyo kumfahamisha hivyo, Dullah alimwuliza alikuwa akiishi Keko ipi maana kuna Magurumbasi, Keko Mwanga, Keko Machungwa, Keko Madawa au Keko Akida?

    Kufuatilia Dullah kumtajia mrembo huyo vitongoji vya Keko akajikuta akicheka na kumwuliza kama kote huko alikuwa akikufahamu, Dullah akasema ndiyo maana kamtajia.

    Wakati maongezi yakiwa yamepamba moto, walishtukia gari limefika Mwenge ambapo wote walishuka na kwenda kupanda basi la Tandale uzuri liendalo Temeke ambalo lilikuwa likijaza abiria.

    Kwa kuwa basi hilo lilikuwa na viti vilivyokuwa wazi, Dullah alimpa ishala fundi Yassin akae siti iliyofuata ambapo yeye na yule mrembo wakaketi siti ya watu wawili.

    “Daa, leo imekuwa bahati tumepata usafiri kirahisi namna hii?” Yule msichana alimwambia Dullah .

    “Yaani huwezi kuamini kwa jinsi usafiri wa hapa unavyosumbua, mfano jana ilikuwa kasheshe tupu!” Dullah alimdanganya yule mrembo jambo lililomfanya fundi Yassin kutabasamu.

    “Kweli huyu dogo ni balaa, kisha mpiga changa la macho dada watu, kweli ukitaka kumpa mrembo yeyote lazima uongo utumike,” fundi Yassin aliwaza.

    Hawakukaa muda mrefu basi lilianza kuondoka, Dullah alifurahi sana kwani alijua mpaka kufika Keko atakuwa tayari kishamuweka sawa yule mrembo.

    Wakiwa wanaendelea na safari Dullah alimwuliza tena yule mrembo alikuwa akiishi Keko ipi kati ya alizomtajia, mrembo alitabasamu na kumwuliza mbona alihitaji sana kujua alikokuwa akiishi.

    “Jamani kwani kuna ubaya gani ukinifahamisha, halafu unaweza kushangaa kukuta wewe ni ndugu yangu au unaishi jirani na ndugu zangu,” Dullah alimwambia yule mrembo aliyeishia kucheka.

    “Haya bwana, mimi naishi Keko Juu ambayo hukuitaja,” yule mrembo alimwambia Dullah aliyeishia kucheka.

    “Keko Juu karibu na Twiga Hoteli au Shule ya Msingi Mgulani?” Dullah alimwuliza.

    “Du! Wewe kaka kweli unalifahamu hili jiji, mpaka Keko Juu unapafahamu?” yule mrembo alimwuliza.

    Dullah alimfahamisha kote huko anakufahamu ndipo yule mrembo akamwambia alikuwa akiishi karibu na Twiga Hoteli.

    Dullah alifurahi sana na kumwambia alikuwa akifika mara kwa mara katika uwanja wa mpira uliokuwa eneo lile kucheza mpira Wawili hao waliendelea na maongezi ambapo Dullah alimwomba yule dada kama hatajali ampatie namba yake ili siku atakayorudi hewani wawasiliane.

    “Kwani hauna simu?” yule mrembo alimwuliza.

    Kufuatia Dullah kupenda kujipaisha, alimwambia alikuwa na simu yake ya kisasa ‘smartphone’ ambayo aliibiwa na dogo mmoja aliyeingia chumbani kwake akiwa anaoga.

    Yule mrembo bila kujua akadanganywa, alimpa pole kisha alimwambia hata akimpa namba yake isingesaidia kitu kwa kuwa hakuwa na simu, Dullah akamwambia pale alikuwa na fedha za kununua simu na siku ilifuata angekuwa hewani.

    Kitendo cha mrembo kuambiwa na Dullah kwamba alikuwa na fedha za kununua simu nyingine akajua kumbe alikuwa mambo safi na kwamba kwa kama alihitaji kununua simu ya kisasa hakukosa laki mbili.

    “Kama ana laki mbili yupo vizuri ngoja nimpe namba yangu najua tukizoeana nitakuwa nampiga mizinga mpaka akome,” yule msichana akawaza.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Sasa hiyo namba utaindika wapi?” yule mrembo akamwuliza Dullah .

    Dullah alicheka na kumwambia amtajie ataikariri, ndipo mrembo akamwuliza kama kweli anaweza kuikariri Dullah akamwambia amtajie tu wala asihofu angeiweka kichwani.

    Baada ya yule msichana kumtajia Dullah alimwambia alishaidaka na asingeisahau, mrembo alipomwambia amtajie Dullah akaitaja bila kukosea, mrembo akaishia kumpongeza kwa kuwa na kichwa chepesi.

    Safari iliendelea ndipo fundi Yassin alibaini huko mbele ya safari dogo ambaye hakuwa na fedha kabisa angeumbuka, akageuka na kumwambia Dullah kwamba akifika Tandika atakwenda kumuona yule Mwarabu aliyemletea simu yake.

    Dullah alijua nini kilikuwa kikiendelea baina yake na fundi wake akamwambia sawa ndipo fundi akafungua pochi yake akachomoa wekundu watatu wa msimbazi na kumwambia aweke mfukoni.

    Dullah alichukua fedha hizo akiwa anatabasamu na kuzisunda mfukoni huku akimsifia sana fundi wake kwa kujiongeza, basi lilipofika taa za Veta yule mrembo alimwambia Dullah kwamba anasogea mbele kwani alikaribia kufika.

    Baada ya kusema hivyo, sharobaro Dullah alimwambia asiwe na wasiwasi naye atashukia hapo kwani alikuwa akihitaji kwenda kumuona rafiki yake mitaa ya Keko, fundi Yassin alipomsikia Dullah akitoa kauli hiyo akajisemea moyoni;

    “Mrembo kishaumia leo, sharobaro ana wekundu watatu mfukoni?”

    Kweli gari lilipofika kituo cha Keko Bora, Dullah alimuaga fundi Yassin kwamba anakwenda kumuona jamaa yake watakutana nyumbani kisha wakateremka na yule mrembo.

    Wakiwa wamesimama kituoni, Dullah alimwuliza yule mrembo kama alikuwa na haraka sana ya kwenda nyumbani, mrembo akamwambia siyo kivile kwa sababu dada yake alikuwa kasafiri.

    “Yap! Habari kama hizi ndiyo napenda kuzisikia,” Dullah alijisemea moyoni.

    “Kwa hiyo tunaweza kutafuta sehemu japo tupate kinywaji kisha kila mmoja aendelee na safari zake?” Dullah alimwuliza yule mrembo.

    Kufuatia yule mrembo kumuona Dullah alikuwa yupo vizuri kifedha, alimwambia hakukuwa na ubaya ndipo kijana huyo ambaye alikuwa na usongo wa yale mambo hasa baada ya kumkosa Doreen akamwambia amfuate.

    Wawili hao walivuka barabara na kuanza kurudi walikotokea kisha wakakata kulia na kuingia kibarabara cha mtaani ambapo hawakutembea umbali mrefu wakatuka baa, wakazama ndani.

    Msichana huyo ambaye mpaka muda huo Dullah hakulifahamu jina lake hakuelewa kama baa waliyoingia kwa nyuma ilikuwa na vyumba a.k.a machinjio, walipoketi tu mhudumu alifika na kuwauliza aliawahudumie nini!

    Dullah aliagiza kilevi yule mrembo aliagiza soda, kabla mhudumu hajaondoka Dullah alimwuliza kama alikuwa hatumii kilevi mrembo akamwambia huwa anatumia lakini kwa siku ile hakujisikia tu!

    “Kufuatia kauli hiyo, Dullah alimwambia anapojisikia vizuri anakunywa kilevi gani akamtajia ndipo akamwambia mhudumu amletee kilevi hicho na kuachana na soda.

    “Yaani best mimi ninywe kilevi wewe unywe soda wapi na wapi? Wewe leo kunywa tani yako suala la fedha siyo tatizo,” Dullah alimwambia yule mrembo kisha akamwita mhudumu wa jikoni.

    “Mimi niletee mchemsho wa kuku, wewe utapenda kula nini?” Dullah alimwagiza mhudu na wakati huo huo kumwuliza mrembo wake alihitaji kula nini.

    “Kama ulivyoagiza wewe,” mrembo akamwambia Dullah ambaye alifurahi sana kwani alijua jioni ile ya saa moja angemuua tembo kwa ubua.

    “Mimi nafikiri ungeagiza tofauti na mimi ili kila mtu aonje chakula cha mwenzake, unaonaje?” Dullah alimwuliza yule mrembo.

    “Oke, basi mimi niletee ulimi na ndizi mbili, ndimu na pilipili weka pembeni,” yule mrembo aliagiza.

    Baada ya kutoa oda hiyo Dullah alimwambia alifanya vizuri, wakaendelea kunywa pombe waliyoagiza na kuendelea na stori za hapa na pale ndipo mhumu wa jikoni akalea msosi.

    Alipowanawisha wakaanza kula na kupiga stori huko moyoni Dullah akisema: “Wewe leo lazima nikugaragaze kwani mla vya watu na vyake huliwa.”

    Dullah alikata kipande cha mnofu wa kuku na kutaka kumlisha yule mrembo ambaye alikwepesha mdomo na kumwambia ampe mkononi, kijana huyo akafanya hivyo.

    “Lakini unajua umenikosesha raha, mimi nilitaka kukulisha wewe umekwepesha mdomo,” Dullah alimwambia.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Sijapenda tu si unajua mambo hayo hufanyiana wapenzi na si kila mtu?” yule mrembo alimwambia Dullah bila kujua kama kauli yake ilimuumiza sana.

    “Najua sana ila sioni kama kuna tatizo mimi kukulisha si namna ya kupoteza mawazo baada ya kazi,” Dullah alimwambia.

    Wakati wawili hao wakizungumza, mhudumu wa vinywaji alifika na kuchunguza chupa zilizokuwa na kilevi na kubaini vilibaki kidogo akavimimina kwenye glasi na kumwuliza Dullah kama aongeze.

    “Hicho ndicho kilichotuleta hapa, kuepusha usumbufu leta mbili kwa kila mmoja na zote ziwe za moto kama za mwanzo,” Dullah alimwambia.







    Yule mrembo aliposikia Dullah kaagiza aletewe bia zingine mbili na kwa vile alikaa muda mrefu bila kupata ‘gambe’ akafurahi na kujisemea moyoni akimaliza kinywaji alichoagiza asingeendelea.

    Bia zilipoletwa wakaenda kula na kukata maji, kwa kuwa mlo walioagiza ulikuwa tofauti Dullah kila mmoja akawa anachanganya, Dullah akichukua kipande cha ulimi, yule mrembo naye akawa ananyofoa mnofu wa kuku, ikawa burudani ya aina yake.

    Walipomaliza kula, wakaendelea kukata maji ndipo bia za moto walizokuwa wakinywa zikaanza kupanda kichwani kwani mrembo akaongeza spidi ya maongezi na kuchekacheka hata kama Dullah hakuongea ishu ya kuchekesha.

    “Yapu! Chezea bia wewe, hivyo ndivyo nilikuwa nataka lazima ulipe fadhila za mfadhiliwa, mimi ndiyo Abdallah a.k.a Dullah ,” Dullah alijisemea moyoni.

    Kijana huyo alipobaini mrembo maji yameanza kuchanganya kichwani alimuomba asogeze kiti chake karibu yake kwani alitaka kumwambia jambo flani.

    “Wewe si niambie tu jamani hilo jambo kwani mpaka tusogeleane?” msichana huyo aliyeitwa Atuganile aliyependa kukatisha jina lake na kujiita Atu alimwambia Dullah kwa sauti iliyozidiwa kwa kilevi.

    “Kwani Atu kuna tatizo gani ukisogea hebu sogea bwana,” Dullah alimwambia msichna huyo mwenye shepu f’lani hivi ya kiuchozi.

    Atu alipoambiwa hivyo akasema isiwe tabu akasogeza kiti chake na kukigusanisha na cha Dullah ndipo Dullah akampiga kibao cha mahaba shavuni ambacho kilimfurahisha Atu.

    “Ila wewe unajua ni mchokozi sana, sawa tu!” Atu alimwambia Dullah .

    “Mimi wala siyo mchokozi ila ukitaka nikuchokoze nitakuchokoza, unaniruhusu?” Dullah alimwambia Atu.

    “Hebu nichokoze niuone huo uchozi wako,” Atu alimwambia Dullah na kuanza kucheka.

    Dullah aliyekuwa amebanwa na haja ndogo aliinuka na kumwambia ngoja akajisaidie kwanza akitoka huko ndiyo atajua uchokozi wake, akaenda uani.

    “Hana ujanja, ngoja nifanye fasta asije akatokea mtu akaenda kumsomesha nawaelewa sana wanaume wakaware wa hili jiji,” Dullah aliwaza.

    Baada ya kumaliza kupunguza maji alirejea walipokuwa wameketi na kusimama nyuma ya Atu aliyekuwa na kifua kilichobeba viembe bolibo vitamu sana, si akamwinamia mabegani na kuingiza mkono wake wa kulia ndani ya kitopu alichovaa Atu na kuishika embe bolibo ya kulia.

    Kutokana na embe hiyo kuwa ya moto, Atu alipata raha sana na kwa upande wa Dullah ilikuwa hivyo, kijana wa Kisukuma alilitumia vyema giza lililokuwepo kuichezea embe hiyo hasa ncha yake, Atu akaanza kutoa mhemko wa raha!

    Dullah alipogundua mashetani ya Atu yalikuwa eneo hilo, kwa akaingiza mikono yake yote kifuani kwa mrembo huyo ambapo kila mmoja ulishika embe bolibo ya upande wake akawa anazipekecha, mara kuzifinya na sijui kuzifanyaje bwana, Atu akapiga yowe!

    Kufuatia uyowe alioupiga Atu, Dullah aligundua kwamba mashetani ya dada huyo yalikuwa jirani hivyo kama angeendelea kumpagawisha, angweza hata kuangua kilio na watu kupigwa na butwaa!

    Alichokifanya kijana huyo sharobaro, alichomoa mikono yake kifuani kwa Atu ambaye licha ya kuwepo kigiza Dullah aliweza kuyaona macho yake yalivyokuwa yamelege na kwenda kukaa kwenye siti yake.

    Baada ya kukaa aliupitisha mkono wa kushoto maungoni mwa Atu na kumpa pole kwa alichomfanyia ndipo msichana huyo akamwambia muda ule alikuwa yupo katika hali mbaya.

    “Hali mbaya kivipi?” Dullah alimwuliza swali la kizushi.

    “Eti unaniuliza hali mbaya kivipi, kwani ulikuwa unafanyaje na kifua changu

    u?” Atu alimwuliza.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kufuatia dada huyo kutoa kauli hiyo, Dullah naye alimwambia hata yeye alikuwa katika wakati mgumu ndipo aliuchukua mkono wa Atu na kuupeleka kwenye makazi ya ‘mkuu wa kaya’.

    Mtoto wa kike alipomgusa mkuu huyo wa kaya, akapatwa na hali ambayo nashindwa kuilezea kwani alipitisha muda mrefu bila ya kukutana naye, akaishia kusema; “jamani wewe mbona mtundu namna hiyo.”

    Dullah alipigundua kwamba hata kwa namna gani kwa atua aliyofikia Atu asingeweza kumchomolea kama angehitaji mkomboti, alimuaga kwamba anakwenda msalani na kwenda moja kwa moja upande uliokuwa na vyumba a.k.a machinjio ambako alilipia rumu moja.

    Baada ya kufanya hivyo alimfuata Atu na kumuomba msamaha kwamba wahamie eneo la ndani ambalo lilikuwa tulivu kwa wao kufanyiana chochote kuliko pale walipokuwa wamekaa.

    Kutokana na pombe kumpanda kichwani, kujumilisha na jinsi mwili ulivyomchemka kihisia, dada wa watu hakubisha alinyanyuka na kumfuata nyuma Dullah kama mwanakondoo aliyekuwa akipelekwa malishoni.



    Baada ya kuingia chumbani Dullah aligundua kwamba alibaki na fedha kidogo ambazo zisingetosha kulipia chumba, akamuacha Atu akiwa kajibwaga kitandani akamfuata mhudumu wa pokezi.

    Alipofika aliomba amwazime simu yake akampigia simu fundi Yassin na kumuomba amuongezee shilingi elfu kumi na tano kwani bila kufanya hivyo angeumbuka mtoto wa kiume.

    Kufuatia ombi hilo, fundi Yassin aligundua Dullah alikuwa amepungikiwa na fedha ndipo akamwuliza hizo fedha angemtumiaje wakati hakuwa na simu akamwambia atume kupitia namba ile ya mhudumu wa gesti.

    Baada ya kuhakikishiwa atatumiwa fedha hizo, Dullah alifurahi na kupata nguvu za kwenda kumuumiza kiumbe wa watu, alipomaliza kuzungumza na fundi Yassin alimfahamisha mhudumu kwamba fedha hizo zikitumwa akate shilingi elfu saba ya rumu kisha zingine atazichukua akimaliza kazi iliyokuwa mbele yake.

    Alipotoa kauli hiyo, mhudumu aliishia kucheka ndipo sharobaro Abdallah a.k.a Dullah alikwenda chumbani alikomuacha mtoto mzuri Atu ambapo alimkuta akiwa kajibwaga kitandani akisubiri kukabiliana na chochote ambacho angeambiwa na Dullah .

    Kitendo cha sharobaro Dullah kumuona Atu akiwa kajibwaga kitandani kilimpa raha

    sana akajisemea moyoni:

    “Umekwisha kiumbe wewe, kumbe wala siyo msumbufu!”

    Kufuatia nafasi hiyo ya dhahabu aliyoipata Abdallah Nzamba a.k.a Dullah si naye akamfuata mtoto huyo wa kike, kwa utaalam wake akaanza kugusa kila eneo la hatari la Atu.

    Kutokana na mautundu aliyofanyiwa na Dullah , Atu alikosa utulivu akawa anahema, kijipinduapindua huku na kule kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa jambo lililompa burudani ya aina yake Dullah .

    Dullah alipomuona mtoto kisha lainika kama mlenda na anahema kwa fujo na yule hakuwa dada yake, akamnyonyoa manyoya yote naye akanyonyoa yake, akamchumu shavuni Atu kisha wakaanza kula mua a.k.a denda.

    Walikwenda sambamba na zoezi hilo na kujikuta wapo katika ulimwengu mwingine, si sharobaro Dullah mpenda sifa sijui alimbanaje bwana mtoto wa watu, Atu akajikuta akipiga kigelegele cha raha na kupasua dafu lake ndipo naye Dullah akapasua lake na kumnywesha dada wa watu maji matamu.

    “Ila wewe mkaka ni balaa!” Atu alimwambia Dullah .

    “Balaa la nini?” Dullah alimwuliza kwa kumtega.

    “Sijapata kuona, yaani mh!” Atu aliishia kuguna.

    “Kwani nimefanyaje si kawaida tu?” Dullah alimwuliza Atu.

    Msichana huyo ambaye tangu aanze malovee hakuwahi kukutana na mwanaume mtundu akama alivyo Dullah , alimfagilia kwa namna alivyomfanyia na jinsi alivyoweza kupasua madafu mawili kabla hata ya mtanange na la mwisho lililokwenda sambamba na la Dullah .

    Dullah aliishia kucheka na kumsifia msichana huyo kwamba naye alikuwa mjuvi wa malovee kisha akazivamia tena embe bolibo zake za mvilingo na ndogondogo akaanza kuziminya atakavyo na kumpagawisha kabisa mtoto wa watu akaibugia moja mdomoni na kuanza kuifyonza.

    Kufuatia Dullah kumfanyia hivyo Atu, msichana huyo alikosa utulivu kabisa akawa anahema na kuyazungusha macho yake pande zote za dunia huku kidole chake kimoja akiwa kaking’ata mdomoni kama mtu anyonyaye pipi ya kijiti.

    Sharobaro Dullah ambaye kitabia alikuwa hatofautiani na masharobaro wengine wanaopenda mambo ya mademu na kuvaa pamba za kijanja, alifurahishwa sana na mapozi ya Atu aliyekuwa kamdhibiti vilivyo.

    Kijana huyo alipogundua angeweza ‘kumuua’ mtoto wa watu aliyekuwa kazidiwa kupita kiasi kwa utaalam wake wa malovee sijui alifanyaje bwana, si Atu akajikuta akilia kufuatia mziki mnene aliopewa na Dullah .CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dullah ambaye alijua kulicheza kandanda kwa mwendo kasi na wa haraka alimpeleka Atu wa watu mpaka binti wa watu akajikuta akipasua dafu ndipo naye kalipasua lake na kumwenyesha maji matamu yaliyomfanya avute pumzi na kuzishusha kisha akajilaza huko baada ya kuishiwa nguvu.

    “Ila wewe mkaka mh!” Atu aliyekuwa kachoshwa kwa maji ya dafu aliyonyweshwa kitaalam na Dullah alimfungukia sharobaro huyo.

    “Kwa nini unasema hivyo?” Dullah alimwuliza Atu.

    “Da! Sijapata kuona, wewe ni balaa!” Atu alimwambia Dullah .

    Kufuatia kauli hiyo, Dullah alimwambia balaa lake lilikuwa nini ndipo Atu akamwambia alikuwa anayaweza bila kufafanua kuyaweza nini!

    “Jamani unaongea kwa mafumbo, kuyaweza nini?” Dullah alimwuliza Atu kwa kumtega.

    Alipoulizwa hivyo, Atu alimsifia jinsi alivyokuwa anajua kufanya maandalizi na alivyompelekesha puta na kumtegea mpaka wakafika pamoja mwisho wa safari tena mara zote mbili.

    “Kumbe umeinjoi eh?” Dullah alimwuliza Atu.

    “Sana tena sana, yaani tangu nilipoanza haya mambo wewe ni mtu wa pili kunipa raha hiyo, da! Unayweza kwa kweli,” Atu alizidi kumfagilia sharobaro Dullah .

    Kufuatia burudani aliyopewa alimuomba Dullah kama hatajali awe mtu wake wa kudumu ambapo sharobaro huyo alimwuliza itakuwaje kwa jamaa aliyekuwanaye.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog