Search This Blog

Monday, October 24, 2022

SEX MACHINE - 3

 







    Chombezo : Sex Machine

    Sehemu Ya Tatu (3)





    "SM, ni siku nyingine tena tunakutana na kuongea mimi nawe, kumbuka kuwa ukutanapo na mimi basi mbele yako kuna kazi kubwa na ngumu" ilisikika sauti mara baada ya kijana huyo kuingia ndani ya chumba cha mawasiliano. Sauti hiyo ambayo ilikuwa na kazi ya kumpa maelekezo ya nini cha kufanya, ilionekana dhahiri haikuwa ikiongea kimzaha mahali hapo bali ilikuwa ikionesha kuwa kuna jambo la msingi lilikuwa mbele ya kijana huyo.

    "kesho unatakiwa uwe Urusi na unakwenda kwa kazi moja tu ya kwenda kumuondoa duniani mfanya biashara mkubwa sana, huyu mfanya biashara ninasababu zangu binafsi za kumuua lakini kubwa zaidi ni kwamba, ndiye mfanya biashara pekee niliyenaye katika ushindani mkubwa sana wa kibiashara. Tazama ukutani" Sex machine akashusha pumzi nzito na kuelekeza macho yake kule alipoelekezwa. kukaonenekana picha kubwa ya kipande iliyomuonesha bwana mmoja mwenye asili ya kihindi kisha sauti ikaendelea.

    "huyo ndiye ninayetaka afe kabla hata haja ikaribia siku ya kesho kutwa kwani mtu huyo kwangu ni kero kubwa sana kumuona" alipo sema hayo, akauliza kwa shauku ya kutaka kujua kama aliyoyasema yameeleweka vema.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "tumeelewana?"

    "ndiyo, mkuu nimekuelewa"

    "vizuri, utapata ramani nzima na maelekezo ya wapi anapopatikana mtu huyo"

    "ok," alijibu Sex machine na baada ya hapo, alkkuja Joesan akatoka nae humo na kuelekea katika ofisi ya Joe na kumuonesha hiyo ramani ikiwa ni pamoja na kumkabidhi kila kinachohitajika. SM alitoka humo ndani na kuelekea ofisini kwake ambako hakukaa sana. Alilifuata tu koti lake la suti na kulitundika begani na kutoka mule ndani akichukuwa muelekeo wa kuelekea kwake. Hakufika katika nyumba ambayo ndiyo anayokaa laa!, alicuhukua uelekeo wa Kilakala ambao ulimpeleka hadi kilakala juu, pembezoni kabisa na milima, huko ndiko ambako alinunua nyumba yake ya siri, huko hakukuwa na mtu ambaye alikufahamu. Japo alikuwa na nyumba ambayo aliinunua akiwa na Sauda, hii pia aliinunua na ni baada ya mpenzi wake huyo kumwambia kuwa kuna nyumba mbili na zote zinauzwa. Hapo akacheza mchezo wa kijanja na kuamua moja iwe ya pamoja na nyingine iwe ya siri na isitambulike na mtu yeyote. Lilikuwa ni jumba lenye eneo kubwa sana kuanzia ndani hadi nje. Nje kulikuwa na bustani kubwa ya kupendeza na hapo ndipo ambapo alikuwa amekaa kijana huyo akijipatia matunda kwa ajili ya kujenga afya. Alikuwa akila taratibu sana hakutaka kutumia papara lakini akiwa bado anaendelea kula matunda hayo, ghafla aliamka na kuanza kurusha mikono hewani na hatimae akanogewa na mchezo huo na kuamua kuchukua mazoezi kabisana. Yalikuwa ni mazoezi makali mno na yaliyochukuwa muda mrefu. ilipomaliza, alielekea ndani moja kwa moja hakukumbuka hata kuingia na kile chombo kilichokuwa kimebeba matunda. Aliingia moja kwa moja hadi bafuni ambako alijipatia maji na kutoka bafuni humo akiwa na kijinguo kidogo chepesi. Akafikia sebuleni ambako alianza kuipitia vizuri ile ramani na kufikiria mbinu za kuweza kuifanya kazi ile kwa urahisi.

    "lazima niwepo kwenye hii hoteli ili nisiwe mbali na nyumba ya huyo muhindi" aliwaza Chriss alipokuwa akizidi kuipitia ile ramani. Hakupoteza muda sana aliingia chumbani na kujituliza.

    "nafikiri nimefanya jambo la maana sana kuchukuwa hii nyumba huku, sitaki mtu yeyote ajue kama nina nyumba ya maficho, hata mpenzi wangu simuamini na ndiyo maana sikumshirikisha kwenye hili. Usalama ni kitu cha msingi sana ukizingatia kwa sasa nimeshajua siri nyingi za mkuu kwa hiyo kunaweza kukawa na mageukano baadaye nikajikuta nakosa pa kujificha na kupanga mambo yangu kwa umakini" aliwaza namna hiyo kijana huyo na mara, Simu yake ikaunguruma, alipoangalia kwenye kioo cha simu hiyo, akagundua alikuwa ni Joesan. Akaiweka sikioni na kumruhusu bwana huyo kuongea.

    "kama unavyojua SM, Safari za mkuu ndizo zinazopelekea na mimi kuunganisha za kwangu. Baada ya kumaliza kazi ya Mkuu hiyo kesho sijui lini, ni lazima ubaki hapo hapo nchini Urusi huko nako utakutana na mtu anafahamika kwa jina la Chalcovich. Huyo atakupa maelekezo ya nini cha kufanya" alipewa maelekezo hayo na kisha simu hiyo .....................................





    akukuwa na muda wa kuuliza wala kuomba ushauri ni kazi tu. Kijana huyo hakutaka kuwaza sana kwani tayari ni kama alishayazoea maisha hayo tayari.



    URUSI NDANI YA UWANJA WA KIMATIFA. ASUBUHI YA SIKU YA JUMA TANO.



    Chriss alikuwa yupo ndani ya uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Taifa hilo kubwa, ambako alichukuwa ndege ndogo ya kukodi iliyotakiwa kumfikisha pembezoni kabisa mwa mji huo wa Moscow. Baada ya kupanda tu ndege hiyo, iliwasha injini zake na kuacha uwanja huo. Haikuchukua Muda mrefu sana kufika huko na moja kwa moja alichukuwa hoteli na kutulia kupanga mikakati yake ya kufanya kile kilichompeleka nchini humo. Alikaa kitandani na kufungua begi lake dogo na kutoa mazagazaga fulani ambayo aliyaweka vizuri kisha akatoka mule ndani akiwa amevaa nguo nyepesi chini na juu akiwa na fulana ya kawaida iliyombana. Hakujali baridi ya nchini hapo. Alipanda hadi juu kabisa ya ghorofa na kusimama juu kabisa na kulishangaa jiji hilo kwa uzuri. kisha akanyanyua darubini yake ndogo na kuiweka usoni na kuanza kuzunguuka kila kona huku akiendelea kuangaza.

    "vipi mbona sioni kitu inamaana siyo hoteli hii?" kilijiuliza kidume hicho na kuishusha ile darubini chini kabla ya kuipandisha tena usoni mwake.

    "shiit! Siwezi kufeli namna hii, itakuwa ramani imenidanganya lakini mbona ilisoma hapa" alijiuliza tena mawazoni kwa wakati huu akiwa haelewi.

    "hebu ngoja" alisema kwa sauti ndogo kisha akarudi tena chumbani.

    "ndiyo ni hapa kabisa, nyumba ya huyo muhindi hii hapa na hoteli yenyewe ni hii hapa" alisema akiwa anaitazama vizuri ile ramani aliyopewa.

    "kwahiyo mimi natakiwa kutazama sana hapa" akajishauri na kuchukua negi lake na kupanda kule juu.



    MASAA SITA NYUMA.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "sikilizeni kwa umakini, huyu mtu kwa sasa yupo nchini Urusi na yupo ndani ya mji wa Moscow. Huko amekwenda kutekeleza mauwaji ya mfanya biashara mmoja hivi mwenye asili ya India....!" alisema mama mmoja wa kizungu huko jijini London lakini sentensi yake ilikatishwa kwa mbele kabla mama huyo hajafikia lengo.

    "kwanini tusimchonganishe na serikali ya nchi hiyo ili akamatwe tu baada ya kufanya mauwaji hayo" ndivyo alivyodakia dada mmoja kwa kutoa wazo au kuchangia mada baada ya mama Doreen kuongea huko jijini London. Macho makali yalimuendea huyo dada na kutaka hata kumezwa kwa jinsi aliivyoonesha udhaifu mbele ya mwanamama huyo mwenye chuki mbaya dhidi ya wanaume.

    "Kekoo, unahamu ya kufa si ndiyo?"

    "hapana mama"

    "unahamu ya kufa wewe malaya. Hivi unajua sababu ya kuwachukia hawa wanume wewe au unaongea tu kama ujinga wako ulivyo kutuma. Ninashida sana na huyu kiumbe anayejiita Sex machine kabla hata hajaingia kwenye mikono ya hao warusi. Amenitia aibu sana huyo malaya wa kutengeneza au wewe hujui? hawa wanaume ni washenzi na unapoamua kuwapa moyo wako wanaweza hata kuunyofoa na kuupeleka kwenye uwanja wa vumbi na kuufanya moyo wako ni kama mpira wa makaratasi. Si watu hawa Kekoo" alisema mama huyo huku akiwa mwekundu kwa hasira zilivyomjaa, aliwageukia wale majemedari wake wa kike na kuwaambia kwa sauti kavu kabisa iliyokosa uwanamke alionao.

    "sikilizeni niwaambie kilichofanya hadi kuwachukia wanaume kwenye maisha yangu yote na kukataa kuingiliwa kimwili na wanaume japo kwa bahati mbaya sana nazinunua kwa gharama kubwa mbegu zao na kupandikiza na za kwangu ili kunipatia watoto. Wanaume walinifanya mimi nikazaliwa katika mazingira magumu na mama akapoteza maisha. Mama yangu alitokea kupendwa na tajiri mmoja mkubwa sana. Huyo alikuwa ni mmarekani na ilikuwa ni huko nchini Marekani. Pesa alikuwa nazo za kutosha huyu baba na alifanya anacho kitaka katika maisha yake. Alimpenda mama yangu akiwa ni binti kigoli, mrembo japo alitoka katika familia ya kawida lakini urembo wake haukubeba uhalisia wa maisha yake bali alionekana ni mtoto wa tajiri fulani hivi kutokana na kujua mwili wake unataka nini na kwa wakati gani. Baba huyo, akavutiwa na kutangaza mapenzi kwa mama yangu, mama hakupinga, kutokana na ugumu wa maisha na ukizingatia kuwa huyo baba alikuwa ni tajiri mkubwa, akakubali na kuingia katika penzi na mzee huyo. Baada ya mwaka mmoja wa mahusiano yao mama akapata ujauzito, hapa ndipo mama alipojuwa kuwa kumbe unaweza kuonekana una vingi na umekamilika kumbe umekosa kimoja na chenye thamani kubwa. Akakumbuka usemi uliowahi jusemwa zamani wa kuwa hakuna binadamu aliyekamilika. Baba huyo pamoja na mali, utajiri uliobeba utitiri wa pesa lakini upendo alinyimwa. Hakuwa na upendo yule mzee hata thumni, alikuwa ni katili na mnyanyasaji wa kutupwa, alikuwa ni mshenzi na mpenda ngono sijapata kusikia mwanaume anayependa ngono kwma huyo kwenye maisha yangu tangu nazaliwa hadi kuwa katika umri huu usiojua nini ladha ya penzi la mwanaume. Mama yangu hakujaliwa, akafukuzwa nyumbani na bwana huyo kikatili zaidi. Tendo hilo, mama lilimuumiza na kumtia wazimu. Mama yangu akachanganyikiwa hakujuwa ni wapi pa kupata msaada na nyumbani hakuweza kurudi tena na si kama labda kulikuwa mbali labda kungehitaji nauli au labda wazazi hawakumpenda laa! Mama hakupenda kurudi nyumbani na aibu ile, fedheha ambayo kama angeamua kuwapelekea wazazi wake nyumbani sidhani kama wangeishi hai. Ukizingatia baba yake kipindi hicho ambaye ndiye alikuwa ni babu yangu tayari alikuwa ni mzee na asiyejimudu tena, hakuwa na kipato wala mtoto wa kumsaidia, hawakuwa na kitu cha kujivunia zaidi ya numba ambayo ni mama ndiye aliyewajengea baada ya kuwa na mwanaume huyo. Ilikuwa ni nyumba nzuri na ya kisasa ambayo hata yeye na mimi kama ningezaliwa tungeweza kuishi. Aliogopa kuwaumiza wazazi wake mama yangu, aliogopa aibu na maneno ya majirani kuwa amechezewa na kupewa mimba na kutelekezwa. Unafikiri ni mama ndiye angeumia, laa! Wangeumia wazazi wake na hatimaye kuwafanya wasiishi kwa amani na kuumaliza umri wao wakiwa na furaha ya maisha. Mama akaishi kwa kudandia dandia na hatimaye akapata kwa kuishi japo si pazuri lakini hakutaka kujali kwani lengo na nia yake kubwa ilikuwa ni kuilea mimba yake. Hakupata mahitaji yoyote muhimu kutoka kwa mwanaume yule kama mjamzito.



    Siku nisiyopenda kuikumbuka ni hii hapa, siku ambayo baba yule aliyabadilisha kabisa maisha ya mama yangu kipenzi, siku iliyomfanya mama alee na kuituza mimba yake akiwa gerezani. Ni siku ambayo ilisababisha mimi kuzaliwa gerezani na kumsababishia mama yangu kifo kutokana na dharau za askari magereza.



    Siku hii mwanaume huyo alikuja nyumbani kwa mama akiwa amelewa kidogo lakini anajitambua, mbaya zaidi alikuja na malaya mmoja kama kuja kumkebehi mama. Matusi mazito na kashfa chafu zisizohimiliwa na sikio la binadamu yoyote yule mwenye akili timamu na kama siyo akili timamu basi sidhani kama binadamu yeyote mwenye nyongo, angeweza kuhimili kashfa, kejeli na maneno ya kuudhi kama hayo. Alikuja kimanyanyaso haswa lakini hayo yote mama aliyavumilia. Kitu kilichomkera ni yule malaya aliyekuja nae eneo hilo kutia neno na kumtukana mama yangu. Sikuwepo duniani kipindi hicho lakini kwa waliopata kuhadithiwa na mama, hawa wakiwa ni majirani zake waliokuwa wakimpa misaada mbalimbali ya hali na mali, walisema maneno hayo yalikuwa ni ya kuuma sana na yalikuwa hivi. Nanukuu.

    "kumbe malaya uliyekuwa ukiishi nae ndiyo huyu asiyejua hata kubadili nguo" mwisho wa kunukuu. Mama akamuangalia yule mwanaume ambaye alimpa ile mimba na kumtelekeza na pengine isingekuwa mimba hiyo, asingekuja kutukanwa na huyo mrembo wake. Baba huyo alifurahi kusikia maneno ya mwanamke huyo na kucheka kabisa. Mama alilia sana na kujiuliza moyoni mambo mengi sana. Lakini alisema maneno machache tu ambayo ndiyo yalikuwa ya mwisho kwa mwanaume huyo na hakuongea naye tena hadi hivi mimi leo nayarudia kwenu. Nanukuu kwa mujibu wa nilivyoelezwa.

    "kama si wewe hayawani kunipa hii mimba nisingekuwa hivi mimi" mwisho wa kunukuu. Kisha kilichofuata hapo ni damu kuruka kila pembe ya ukuta baada ya mama kunyanyuka na kipande kigumu cha ubao na kumshushia huyo mwanamke utosini. Yule baba macho yakamtoka baada ya kumshuhudia yule mwanamke wake akishuka chini taratibu huku sakafu ya eneo hilo ikimsubiri kwa hamu ya kutaka kumpokea na kuona ni jinsi gani ataweza kuparangana na kuipigania roho yake kwa suluba ya ubao ule uliotua kwa nguvu nyingi kichwani mwake. Mama hakuwa akilia bali mwili ulikuwa ukimtetemeka na kwa muda huo alikuwa akimfuata mwanaume huyo na kutaka kumtwanga na yeye pia lakini hakufanya hivyo ilionesha dhahiri mama alizidiwa na upendo juu ya mwanaume huyo na kama si upendo basi alitaka mimi nitakapozaliwa nimjue baba yangu maana alijua fika kuwa yeye si wa kuishi tena uraiani kwa kesi ile ya kuuwa ni lazima angeozea gerezani. Baba yule hakuamini kama amepona, alichoropoka na kutimua mbio huku mama akawa akimuangalia kwa uchungu mkubwa sana. Ni kama mtu aliyekuwa akisema kuwa, 'ni keeli unaniacha wewe mwanaume kisa tu nimekuulia huyu malaya wako, kwa nini unaniacha sasa na unajua kuwa mimi sikuuwa kwa makosa bali ni yeye aliyenilazimisha' nadhani alisema hivyo kutokana na jisi alivyokuwa akimuangalia, maaana unaambiwa alikuwa akimuangalia kwa huzuni na masononeko makubwa.



    Hakutaka kukimbia wala nini, ni kweli hakukimbia sijui labda ni kutokana na kuwa alikuwa tayari kwa lolote lile mbele yake. Muda haukuwa mrefu sana ndani hapo pakajaa askari polisi na mama akachukuliwa na kupelekwa mahabusu. Siku ya kutajwa na kusomwa kwa kesi yule baba alikuwepo na alikuwa ni shahidi namba moja wa kumuangamiza mama gerezani. Inamaana hakujua kuwa mama alikuwa na kiumbe tumboni mwake, hakujua kama kiumbe hicho msababishi ni yeye. Lakini yote ya yote, mama alikutwa na hatia na ....................................





    na hakuwa na mtetezi wala mwanasheria wa kusimamia kesi yake acha huyo shahidi wa kumfariji. Mama akahukumiwa kifungo cha maisha gerezani na adhabu kali mara baada ya kujifungua. Sinashaka mama baada ya kunizaa alijiuwa ili kuikwepa adhabu, adhabu iliyopo mbele yake. Hebu jiulize ni ukatili kiasi gani walionao wanaume na ni mapenzi kiasi gani waliyonayo wakina mama? Naamini mama alikuwa na uwezo mkubwa wa kujiangamiza ningali tumboni mwake lakini hakufanya hivyo hadi pale kipenzi chake nilipokuja duniani." alimaliza kuongea mama Doreen na kutulia akiwa na ghadhabu maradufu akasema.

    "sikutaka kuwauwa wanaume ila kwa huyu sex machine kwa jinsi alivyonionesha dharau, nimeapa kumuuwa na nitamuuwa kwa mikono yangu mwenyewe. Hivyo Kekoo wewe ni kiongozi na nakutegemea so sitahitaji mtu huyo awe mikononi mwa jeshi la polisi la nchi hiyo ya Urusi. Nataka awe mikononi mwangu. Hayo maneno yako ya eti, tumchonganishe na jeshi la polisi la urusi, futa tena futa kabisa ubongoni mwako."CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "nimekuelewa mama na pole sana sikuwa nikijua hayo yote" alijibu Kekoo, mwanadada mrefu kwenda juu na mwenye mwili wenye mvuto wa pekee sana. Waliendelea kumsikiliza Mama huyo na kupokea maelekezo yote.

    "nitawasubiri nje kabisa ya mji huo wa Moscow na gari kisha tuenda hadi katikati ya mji ambako kuna rafiki yangu yuko huko huyo atatusaidia ndege binafsi na kurudi hapa London." ndivyo walivyopokea maelekezo hayo.



    Sex machine alipopanda kule juu kwa mara ya pili, alizunguuka kuangalia usalama kisha akaweka darubini yake tena machoni kutazama kule ambako ramani ilimtaka awe makini napo. Ewalaaa! Nyumba ilionekana na alipoangalia vizuri alimuona tajiri huyo wa kihindi akiwa nyumbani kwake akizunguuka bustanini. Akaitoa darubini ile na kufunga silaha yake kwa ustadi wa hali ya juu sana, kwa muda mfupi tu akawa tayari amekamilisha zoezi hilo la kuifunga silaha hiyo ya kudungulia (Sniper rifle). akaseti lens vizuri ya kuonea mbali na kuelekea kule ambako nyumba hiyo ipo. Hakumuona pale bustanini. Utata.

    "yuko wapi?" akajiuliza.

    "mbona nilimuona hapa" akazidi kujiuliza maradufu huku akizidi kuangalia ni wapi mzee huyo yupo. Alipoangalia vizuri, alimuona maeneo ya chumbani kupitia dirisha la kioo akibadili nguo.

    "pole sana mzee najua ulitaka kutoka ili kunipa wakati mgumu wa kazi yangu. Hebu chukua mzigo huo uliopikwa kwa ajili yako" alinong'ona akiwa tayari amemuweka mzee huyo kwenye shabaha yake. Alimlenga kwenye paji la uso na kubonyeza trige na kuruhusu risasi iliyotoka kwenye mashine hiyo ya masafa marefu, kusafiri kwa kasi kubwa. Risasi hiyo ilionekana ikikimbia kwa kasi kubwa hadi kwenye paji la mzee huyo wa kihindi. ikapenya na kuacha alama ya nyota kwenye paji lake hilo huku akitoa mlio mdogo wa maumivu na kudondoka chini taratibu.

    "yess," alisema. Kijana huyo na kuifungua haraka haraka silaha ile na kuirudisha mule kwenye begi na kuweka kifaa kidogo kama kiberiti na kuliacha begi hilo hapohapo na yeye akashuka chini na kurudi chumbani kwake ambako alibadili nguo na kukamata brifcase yake na kutoka mule chumbani. Alipofika chumbani hapo tu, kule juu alikoacha lile begi lililobeba silaha ya kudungulia, kukatokea mlipuko mdogo ulioteketeza kila kitu na kuacha majivu ambayo yalikuwa yakisukumwa na upepo. Alikuwa ameiteketeza kabisa ile silaha kupoteza ushahidi. Alikmata korido ndefu kisha akakunja kushoto na kuingia kwenye kijichumba kijidogo kisha akatokea kwenye lifti na kujifungia. Akataka kubonyeza namba fulani zilizopo ukutani lakini ghafla akasikia sauti kutokea nyuma yake. Sauti tamu ya kike, sauti ambayo ilimuacha hoi na kumshangaza.

    "bonyeza namba nane hiyo itakuwa rahisi kukusaidia kutoka ndani ya jingo hili, ukieanda hadi flow namba moja, huko huwezi kutoka salama, askari wameshajaa huko chini" sauti hiyo ilimwambia namna hiyo tena kwa utaratibu mkubwa kabisa. Sex machine akaganda na kujifanya ile sauti haikuwa kwa ajili yake. Ni kama hakusikia, akaendelea na zoezi lake.

    "tukio la mauwaji ulilolifanya huko juu tayari habari zimefika kwa jeshi la polisi la nchi hii na wamejaa hapo chini hivyo kama huniamini toka" ikaendelea kumuambia sauti hiyo. Kijana huyo akaganda kwa muda lakini hakutaka kupuuza maneno ya msichana huyo japo hakumjua. Alichanganyikiwa sana kusikia kuwa kila kitu alichokifanya huko juu kimejulikana. Na nani? akajiuliza lakini jibu hakulipata. Akairuhusu lifti hiyo ishuke hadi flow namba nane kisha akamgeukia msichana huyo aliyekuwa akimsemesha. Alikuwa ni Kekoo. Binti mrefu ambaye hakuwa na tabasamu hata kidogo eneo hilo. Lakini urembo wake haukujificha hata kidogo ndani ya hiyo sura. Hakumsemesha hadi flow namba nane, mlango ukafunguka, akatoka mule ndani kabla ya binti hiyo kutoka. Kekoo hakuwa na haraka na mtu huyo, alijua ni jinsi gani atakavyomkamata kirahisi kijana huyo.

    "kama huamini chungulia kwenye hizo ngazi za kushuka huko chini" alisema Kekoo. Sex machine akaelekea upande wa hizo ngazi zilipo. Ghafla aligeuka na kurudi mbio. Alikutana na askari wa kirusi wakiwa wamebakisha hatua chache kuweza kufika hapo walipo, akarudi hadi aliko Kekoo.

    "nifuate faster" alisema kwa sauti ya juu Kekoo na kuingia ndani ya chumba kimoja huko wakakuta dirisha moja lililo wazi.

    "hakuna njia nyingine ya kutokea humu ndani zaidi ya hapa" aliongea tena binti huyo huku akimuonesha Sex machine kamba ikiyopo dirishani hapo.

    "tuna jump" aliongea huku akitangulia na kijana makini akimfuata kwa nyuma. Walishuka na hiyo kamba hadi chini kabisa. Wale askari walipofika ndani ya kile chumba, walikuta chumba kikiwa kitupu na hata walipochungulia dirishani ambako kulikuwa na kamba, hawakuambulia kitu zaidi ya kamba tupu. Kekoo na Sex machine walipofika chini, haraka sana binti huyo alizidi kumuelekeza kijana huyo amfuate na hakuleta ubishi kwani kila kona ya eneo hilo kulikwa tayari kumezingirwa na askari. Wakafika sehemu ambayo kulikuwa na pikipiki kubwa Kekoo akadandia na wakatokomea eneo hilo.



    Pembezoni mwa mji huo wa Moscow upande wa mashariki, kwa mbaliii, kunaonekana gari ndogo aina ya Subaru yenye rangi ya kibuluu ikiwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara moja tulivu. Muda mfupi mbele pikipiki kubwa lililokuwa limembeba Sex machine na yule binti liliwasili mahali hapo na kupaki pembeni ya ile gari.

    "hii ndiyo itatusaidia kututoa hapa hadi nje ya mji huu usioope ni msaada kwako, jeshi la nchi hii sio zuri kabisa na wakikukamata mateso yao huwa ni makali mno hadi unakufa, kuhusu mimi ni nani utanijua" alisema Kekoo na kumfunguli mlango wa gari hiyo kisha na yeye kuingia upande wa pili na kuliondoa gari hilo. Baada ya umbali mdogo alisimama na wakaingia wanawake wawili kwa haraka sana. Sex machine akashtuka baada ya kuona tukio hilo lililofanyika kwa haraka namna hiyo.

    "vipi mbona sielewi?" akauliza Sex machine.

    "utaelewa tu mpuuzi wewe" sauti ya nyuma ikamshtu na alipogeuka alikutana na kikosi ambacho hata hakukitegemea mahali hapo na wote wakiwa ni wanawake na hawana kabisa tabasamu. Alijiona mjinga sana kukamatika kipuuzi tena bila hata wakamataji kutoa jasho. Akataka kufanya kitu cha ghafla, alichelewa. Pigo moja la nguvu likatua kisogoni, alipigwa na kitako cha bastola hapo hapo giza likayavaa macho yake na kumfanya kupoteza fahamu.

    "chukua hiyo sindano hapo mdunge huyo ili asije kuleta shida" sauti ya dada mmoja humo ndani ilisema.

    "vipi hii gari ina mafuta ya kutosha?" Kekoo akauliza.

    "usitie shaka mamito kanyaga gia tairi zinung'unike, si unajua mama anatusubiri na hatupaswi kuchelewa"

    "nafahamu na ndiyo maana nimeuliza kama lina damu za kutosha maana nataka kukanyaga mafuta nianze kuendesha sasa maana naona mlikuwa mnaliendesha kirembo" alijibu Kekoo na kasi ya gari hiyo ikaongezeka maradufu. Dakika arobaini ziliwafikisha mahali ambako ndiko Mama Doreen alipo.

    "well done my doughters, kazi imekwenda vizuri. Ndege iko tayari kama mnavyoona mtoeni humo garini na mumuingize ndegeni. Wakafanya kama walivyoelezwa. Walimkokota na kumuingiza ndegeni kisha Kekoo binti hatari kabisa akakaa kwenye upande wa rubani na kuiondoa ndege hiyo safari ya kurudi London na kile walichokifuata ikaanza. Kekoo alipoiweka ndege sawa aliiacha ijiongoze yenyewe yeye akajumuika na wenzake.

    " umewezaje Kekoo kumkamata huyu jamaa?" aliuliza mama Doreen huku akimtazama Sex machine kwa hasira kali mno alitamani hata kumuangamiza kwa muda huo. Alizidi kuzidisha hasira zake dhidi ya wanaume, Alimchukia sana Sex machine kutokana na kitendo chake cha kuharibu future za binti yake. Mwenyewe alitaka siku moja binti yake huyo aje awe kama yeye lakini haikuwa hivyo, kijana aliyepo hapo ambaye hakuwa akijitambua kwa kuzidiwa na nguvu ya dawa ya usingizi, alizizima ndoto hizo.

    "ilikuwa ni kazi nyepesi sana mama, nilichokifanya baada ya kufika hotelini hapo ni kusubiri kwanza atekeleze kazi yake kisha mimi ndipo nilipotoa taarifa polisi na kuwaelekeza mahali ambapo mauwaji hayo yametokea kisha nikaingia ndani ya hoteli hiyo hadi mahali kilipo chumba cha lifti ambayo nilikuwa na imani kuwa ni lazima apitie hapo na kumueleza kuwa polisi walikuwa eneo hilo na wapo hapo kwa ajili yake, hapo nikamchanganya na alipohakikisha mwenyewe kwa macho yake kuwa kweli eneo hilo lilikuwa na askari, akajikuta akifuata tu kila nilichokuwa nikimuelekeza.

    " nakubali sana" alisema mama Doreen na kisha wote wakaanguwa kicheko cha kike na kugongeana mikono.



    Masaa sita baadae, ndege hiyo ndogo ilituwa katika uwanja mdogo wa jumba la dada huyo na kutembea kwa kasi sana kisha ikapunguza mwendo taratibu na kusimama kabisa. Gari ndogo ya ajabu iliyo wazi ilifika mahali hapo, wakamtoa Chriss humo ndani na kumuingiza ndani ya hiyo gari kisha gari hiyo ikaondoka na kuingia ndani ya jumba hilo la kifahari. Alitolewa na kwenda kufungwa kwenye chumba maalumu na kumuacha humo akiwa bado hajarudiwa na fahamu hata kidogo.........



    "muacheni hapo fahamu zikimrudia ndipo tutakapompa mateso hadi kifo." alisema mama Doreen.



    LOS ANGELES.



    Mwana dada mrembo alikuwa ametulia ndani ya nyumba yake ya kisasa akiwa mbele ya kompyuta yake mpakato akifuatilia kitu fulani lakini kadiri alivyokuwa akiendelea na kazi hiyo, ndipo alipoonekana kama mtu aliyechanganyikiwa mahali hapo.

    "inakuwaje hii, alisomeka Moscow na sasa London, hii nini maana yake? inamaana alikuwa na safari ya kwenda london?" alijiuliza dada huyo huku akigeukia upande mwingine kwa kuzunguusha kiti chake akachukua maji kwe glasi na kurudisha kiti chake pale kwenye kompyuta. Akaangalia kwenye kioo cha kompyuta hiyo na kupiga funda moja la maji na kuirudisha glasi yake pale mezani.

    "alitakiwa aende Urusi akafanye mauwaji kisha aende Ufaransa kwa ajili ya kuchukuwa mzigo wa madawa ya kulevya na baada ya hapo, alikuwa tena na safari ya Brazil, vipi tena Uingereza?" alizidi kujiuliza mwanadada huyo.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ooop!" alichoka. akajiegamiza kitini kisha akatulia kwa muda huku akikazia macho kidude fulani chenye rangi ya kijani ambacho kilikuwa kimetulia kabisa.

    "ngoja nijue yuko maeneo gani huko London" aliwaza tena kisha akaainamia tena ile kompyuta yake na kuanza kubonyeza bonyeza kicharazio cha kompyuta hiyo.

    "shiiit!" aling'aka dada huyo baada ya kujua mahali mtu huyo alipo. Ile alama ilisomeka kwenye jumba moja la thamani sana na aliwahi kufika ndani ya jumba hilo. Na siku ambayo aliingia ni siku ambayo kulikuwa na ibada ya siri ambayo ilikuwa ikiendeshwa na mmiliki wa nyumba hiyo.

    "hatari!" akasema kisha akanyanyuka na kuingia chumbani, alipotoka alikuwa amebadilika sana. alikuwa ndani ya suruali nyeusi ya jeans iliyombana sana. Juu alipiga kijitop cha rangi nyekundu huku akiwa na viatu vyekundu pia. Akatoka humo ndani kwa haraka sana na kuingia kwenye gari na kuondoka hapo nymbani kwake kwa mwendo wa kasi sana. Dakika chache alikuwa kwenye uwanja wa ndege. akatoka garini na kuingia ndani ya uwanja huo.



    Sex machine alifumbua mcho taratibu na kuangaza kila upande wa chumba hicho. Kilikuwa ni chumba kidogo sana chenye mwanga hafifu mno. Alijishangaa kuona yupo hapo na akiwa amefungwa kamba kwenye kiti. Alijivuta kutaka kujitoa lakini ni kama alikuwa akijisumbua, alifungwa madhubuti sana na hakuweza hata kutikisika.

    "niko wapi hapa na kwanini niko hapa? Nimefikaje?" alijiuliza maswali hayo kijana huyo huku akizidi kushangaa. Akaanza kuzivuta kumbukumbu nyuma na hapo akakumbuka kuwa kwa mara ya mwisho alikuwa mjini Moscow, akakumbuka alivyokuwa akiwakimbia polisi hadi kufanikiwa kuwatoka akiwa anaongozwa na binti mmoja. Mwisho akakumbuka akiwa kwenye gari na wanawake wengi kabla ya kupigwa na kitu kizito kichwani.

    "nimetekwa" akasema kwa sauti ya chini sana na kujituliza akisubiri kuwaona hao waliomteka na kumfikisha mahali hapo. Dakika chache mlango wa chumba hicho ulifunguliwa na mwanga mkali ukakipiga chumba hicho. Wakaingia watu wawili ambao walikuwa ni wanawake. Wakamsolea hadi karibu kabisa na alipo yeye.

    "Sex Machine, kijana hodari ambaye hukamatiki na ni mwenye uwezo wa kuvunja mitego iliyofungwa imara." akasema Mama wa Doreen. Sauti hiyo ikamfanya Sex machine ashtuke kutoka katika kisima cha mawazo. Aliikumbuka sauti hiyo, ni wapi alipata kuisikia. Hakukumbuka mapema hadi alipoinyanyua sura yake juu na kumtazama muongeaji.

    "kumbe umeamka!" alisema tena mwanamke huyo. Sura za wanawake wawili zilikuwa karibu kabisa na macho yake. Akaikumbuka sura hiyo ni sura ambayo aliiharibia binti yake siku kadhaa zilizopita.

    "nilitaka uamke ili nikupe mateso yatakayo kuuwa taratibu." alisema mama huyo huku akimkamata Sex machine kidevuni na kumnyanyua kichwa kwa nguvu. Makofi matatu ya nguvu yalituwa kwenye shavu la kulia la kijana huyo na kupelekea maumivu makali kisha akamsukuma nyuma na kumuacha. Akarudi nyuma.

    "kekoo hebu peleka kichapo kwa huyo mpuuzi hapo" alitoa amri mama huyo. Kekoo akasogea na makonde ya haja. alimpiga kijana huyo ngumi nyingi sana za uso, zilikuwa ni ngumi zisizo na idadi. Sex machine aligugumia kwa maumivu makali aliyokuwa akiyapokea mahali hapo. kichapo hakikoma hata kidogo. alipiga binti huyo hadi Sex machine akalegea kabisa kutokana na kichapo alichokuwa akikipokea.

    "usife sasa hivi wewe mwanaume unatakiwa ufe taratibu sana sasa ukiwa nyanya kiasi hicho utanishangaza." aliongea Kekoo huku akiwa amemkamata kichwa kijana huyo kisha akamtandika ngumi kali iliyomyumbisha. Kelele za maumivu zikamtoka huku damu zikimchuruzika mtindo mmoja.

    "ha ha ahaa! Vizuri sana hapo. Acha niendelee nae sasa" aliongea mama Doreen na kumuinamia kijana huyo ambaye alikuwa akipumuwa juu juu kama mtu mwenye presha ya kupanda.

    "oou! Yupo katika hali mbaya sana ngoja tumuache apumzike kisha baada ya nusu saa tutakuja tena" alisema mama huyo na kutoka mule ndani huku Kekoo akimfuata nyuma. Chriss alikaa mule ndani akiugulia maumivu makali sana aliyoyapata kutokana na kipigo.

    "inamaana mateso yote haya ni kwasababu nimemuingilia binti yake au kuna jingine?" alijiuliza kijana huyo huku akiwa amejiinamia. Aliendelea kukaa humo ndani pasipo kujua afanye nini ili aweze kutoka. Aliendeleza kuwaza hivyo hivyo hadi baada ya nusu saa wale wanawake walivyorudi tena. Walipoingia hapo hakukuwa na maongezi tena kilichofuata ni kipigo tu. Alipigika sana kijana huyo, alipigwa kupita kawaida, alipata maumivu makali sana Chriss hakujua kama anaweza kutoka mahali hapo. Aliamua kutulia tuli tu akiwapa nafasi ya kuweza kumpiga hadi watakaporidhika. Kipigo kikaendelea na wote walikuwa wakichangia. Ilikuwa ni kupokezana mahali hapo, akipiga mama Doreen, anapiga Kekoo lakini ghafla kishindo kikubwa kikasikika. Wote wakaacha zoezi walilokuwa wakilifanya kwa kijana huyo.

    "nini hicho" aliuliza mama Doreen.

    "hata sijui ni nini?"

    "hebu nenda kaangalie Kekoo huko si kawaida hiyo" akatoa amri mama huyo, Kekoo akaelekea huko yeye akaendelea kusubiri mahali hapo. Sex machine akamtazama mama huyo na kumuomba amfungue kamba. Hilo lilikuwa ni kama tusi kwa mama huyo, alifoka sana, alifoka kupita kiasi.

    "nani akufungulie mpuuzi wewe tena leo ndiyo nakuuwa kabisa, hivi unajua ni kiasi gani ulivyonichefua. Alimfuata akamkamata mabegani na kumtingisha, alimtingisha kwa nguvu sana huku akiongea maneno makali kwa uchungu mkubwa.

    " nyinyi wanaume hamna ubinadamu hata kidogo ni washenzi sana, mnaweza hata kumuangamiza mtu anayeonesha upendo kwenu, nyinyi ni wauwaji, nyinyi ni wanyama kabisa" alisema mama huyo huku akilia kwa uchungu. Chriss akajua hapo kuna zaidi ya hilo la kumuingilia binti yake. Akawaza ni nini kilichomtokea mama huyo wa kizungu hadi kuonekana kuwachukia wanaume kiasi hicho. Alichanganyikiwa kweli na alifikia hatua ya kuchomoa bastola kwenye kiuno chake na kumchapa risasi ya bega kijana huyo. Risasi hiyo ikapiga na kuchana nyama, maumivu makali yalimtambaa mwanaume huyo. Bastola ikahamia kwenye paji la uso kuashiria kuwa inayofuata inapigwa hapo. Alikuwa akitetemeka mwili mzima kwa ghadhabu alizokuwa nazo lakini hakuendelea kufanya hivyo, kishindo kikubwa kingine kikasikika. Akashtuka na kuishusha ile bastola chini, akaangalia mahali mlango wa chumba hicho ulipo. Kishindo kingine kikajirudia, akamgeukia Sex machine na kumwambia.

    "nakwenda kuangalia huko nijue kuna nini lakini nikirudi napasua kichwa chako" kisha akaelekea kunako kishindo hicho lakini kabla hajafika mlangoni, Sex machine akamuita kisha akamwambia.

    "ungefanya jambo la busara sana kama ungenifungu.......!" hajamaliza kuongea, risasi ikachimba ukutani na kumnyazisha kimya. Mama huyo akafungua mlango na kotokomea nje ya chumba hicho. Purukushani zikasikika huko nje ya hicho chumba Chriss akajua si kwema. Akaanza kuminyana kutaka kufungua kamba alizofungwa ili kuweza kutoka mahali hapo ikiwezekana aweze kwenda kutoa msaada kwani aliamini kabisa mama huyo hakuwa na makosa yoyote ila huwenda kuna jambo zito linalomtesa akilini mwake. Hakuweza hata kidogo alikuwa amefungwa imara sana mahali hapo na hakukuwa na uwezekano wa kuweza kujifungua. Akakata tamaa na akajua kwa vyovyote kuna wavamizi wamevamia na kama ni hivyo basi huwenda hata yeye akawa kwenye hatari ya kuuwawa. ghafka bin vuu, mlango wa chumba alichopo ukafunguliwa kwa kishindo kikubwa na alipoangalia vizuri, alimuona mwanamke akiwa amevaa kofia iliyoweza kumfunika uso hivyo hakumjua ni nani. Mwanadada huyo alikuja hapo na kisu kisha akakata kamba zilizotumika kumfungia na kumuacha hapo akiwa huru lakini dada huyo alikwenda hadi mlangoni na kusita kidogo kisha akageuka ni kama kuna jambo alitaka kulisema lakini alishindwa. Akafungua mlango na kupotea. Sex machine akajiuliza ni nani? Mbona amejiziba sura kwa kofia, inamaana hataki kujulikana? Au ndiyo wavamizi waliokuja kuvamia ndani ya jingo hilo? Hakupata jibu na badala yake akaamua kucha kufanya hivyo kwani hata kama angeendelea kujiuliza, ingekuwa ni kazi bure maana asingepata jibu kamwe. Akakumbuka kuhusu wale wanawake waliomteka akiwa nchini Urusi, akapata hofu na kuamua kutoka ndani ya chumba hicho alichokuwa kahifadhiwa, tena alitoka kwa uwangalifu wa hali ya juu sana. Kitendo cha yeye kufungua mlango tu, alikutana na damu mtindo mmoja. Sebule yote ilichafuka kwa damu, akawaza na kujiuliza hapo ni nini kimetokea. Akazidi kutafuta kwa kuingia chumba hiki na kile, hapa na pale. Alipofika kona moja akamkuta Kekoo akiwa anamalizia pumzi ya mwisho. Akamsogelea na kumuinamia na kuanza kumtingisha.

    "Kekoo nini kimekukuta? Yuko wapi mama?" aliuliza kwa kutumia majina aliyokuwa akiyasikia humo ndani wakiitana. Kekoo hakuwa na uwezo wa kuongea tena alinyanyua tu mikono juu kama mtu anayetaka kuomba jambo lakini haikuwezekana, Kekoo akaaga dunia.............





    Bila shaka alikutana na kipigo kikali na alipigana na fundi haswa maana Kekoo hakuwa akivuja damu sehemu hata moja lakini alipokata roho tu, damu zikaanza kumtoka mdomoni hii iliashiria kuwa aliumia sana ndani. Chriss akamuacha mtu huyo mahali hapo japo alimtesa lakini huruma juu ya wanawake ilimuingia sana, aliamini katika maisha yake yote kwamba mwanamke ni mtu muhimu sana katika maisha ya mwanaume na hakupaswa kuteseka hata kidogo. Hakujali mateso makali aliyoyapata, alichojali na kukifikiria ni kuhakikisha anajua mahali mama wa nyumba hiyo alipo. Akazidi kutafuta kila mahali, alitafuta kila kona hadi akachoka na kukata tamaa kabisa. Akajua labda baada ya kuzidiwa mama huyo alitafuta upenyo na kukimbia. Akawa anatoka taratibu akipita kona hii na kupitia ile. Mahali fulani akasikia sauti ya mwanamke aliyekuwa akinung'unika kuashiria kuwa alikuwa amefungwa kitu mdomoni. Alipoangalia vizuri, alimuona mama Doreen akiwa amefungwa mahali. Chriss alimuwahi kwa lengo la kutaka kumfungu lakini mama huyo alimpiga kikumbo, Chriss akayumba lakini akiwa amefanikiwa kutoka na gundi ambalo mama huyo alizibwa nalo mdomoni. Mama huyo alihema kwa nguvu na kumwambia kijana huyo kuwa aondoke eneo hilo. Chriss akagoma na kumwambia kuwa hawezi kuondoka hapo hadi ahakikishe amempa msaada. Mama huyo akamwambia kijana huyo aangalie kwenye pembe moja mahali hapo na alipoangalia, alikutana na bomu kubwa la saa lililokuwa limebakisha dakika mbili tu kuweza kulipuka. Chriss akamgeukia yule mama na kumfungua huku mama akionekana mbishi kusikia, Chriss alilivuta gundi alilokuwa amefungwa na kubana mikono ya mama huyo na kulitupa kando, mama huyo alipiga kelele huku akilia na kumwambia aondoke mahali hapo na amuache afe mwenyewe.

    "ni bora basi tufe wote lakini siwezi kukuacha ufe mwenye hauna hatia"

    "nimesema niache nife mwenyewe niacheeeeee.....!"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kimya we mwanamke, mimi siyo wa hivyo na siko tayari kumuona mwanamke anakufa kipumbavu. Najua ulinitesa lakini mateso yale siyo kwa sababu eti nilimuingilia mwanao tu. Kipo cha ziada juu ya wanaume sasa nataka kukuonesha kuwa si wote wenye roho za kishetani na kishenzi kama unavyodhani wewe. Ukitaka nikuache hapa basi hakikisha unanishika kwa nguvu zako zote na tunakufa wote" maneno hayo ya kijasiri yalimvunja kabisa mdomo mama yule, hakuamini kama mtu aliyempa mateso makali na kutaka hata kumuuwa angekuwa na moyo wa namana ile. Hakuwa na jipya tena hapo kilichobaki ni kuwa mpole na kuweza kufunguliwa kamba zilizo bakia. Chriss aliangalia saa na kugundua kuwa zimesalia sekunde thelathini tu ili bomu hilo liweze kulipuka. Akaongeza kasi ya kufungua kamba hizo hadi anamaliza kumfungua kamba zote, zilikuwa zinesalia sekunde kumi na tano pekee. Binti yule alichoropoka kutoka mikononi mwa Chriss na kuingia mahali Chriss akashangaa lakini punde akarejea na alipofika tu akamwambia kijana huyo kuwa yupo tayari kwa safari. Zilikuwa zimesalia sekunde kumi.

    "onesha njia ya siri itakayoweza kututoa nje" alisema na mama huyo akafanya kama alivyoelekezwa. Wakapita mahali huku mama huyo wa kizungu akiwa ni kiongozi wa kuelekeza njia. Walitokea nje ambako kulikuwa na uzio mkubwa, kwa mbali Chriss aliona mlango wa siri wa kuweza kuwatoa nje. Alimkamata mama huyo mkono na kukimbia nae kwa kasi kubwa wakafungua ule mlango, ile wanatoka tu nje ya ule uzio, Mlipuko mkubwa ukasikika. Chriss alimkamata yule mama mkono kwa nguvu sana na kuruka nae na kuangukia kwenye ngema fulani, kijana huyo akamfunika huyo mama kwa kumlalia kwa juu kuhakikisha hakuna madhara yoyote yanayomkuta. Mlipuko ule ulikuwa ni mkubwa sana hakuna kitu kilicho baki, nyumba yote iliteketea na kubaki kweupe kabisa ni moto pekee ndiyo ulikuwa ukiwaka. Mama yule aliamka kwa kilio kikali sana. Aliwalilia wafanya kazi wake wote huku akilitazama lile eneo ambalo eti, ndipo lilipokuwa jingo lake la thamani. Kilio kilikuwa kikubwa sana hadi Chriss/Sex machine akaja kwa nyuma na kumshika begani huku akimpiga piga mgongoni na kumwambia.

    "nilishindwa kutoka na Kekoo kwani nilimkuta akikata roho na alikufa nikiwa nashuhudia lakini wafanyakazi wako wengine wote hawakuuwawa na huu mlipuko bali walivamiwa na watu hatari na kuwauwa, huu mlipuko ulikuwa ni kwa ajili yako tu." akanyamaza Chriss na kuutazama ule moto uliokuwa unaendelea kuwaka kwa madaha na sifa ya kuweza kufanya ulichotumwa kisha akamshika yule mama vizuri ambae muda huo ni kama alipatwa na bumbuwazi maana alikuwa halii tena na badala yake alibaki akiukodolea macho moto ule.

    "roho imeniuma sana kuwaona watu wenye thamani kubwa na wasio na hatia wamepoteza maisha" alipokomea hapo Sex machine, macho ya mama huyo yote mawili yalikuwa yanamtazama yeye kwa mshangao mzito. Ni kama vile mtu aliyekuwa akijiuliza. Mbona vijana wangu ndiyo waliotaka kumteka mwanzo kule brazil, mbona hata hivyo huyo Kekoo ndiye aliita polisi na kufanikiwa kumteka kule Moscow na mbona ndiye aliyempa mateso na kutaka kumuuwa, iweje leo aseme kuwa ni watu wenye thamani na wasio na hatia." Alipokuwa katika mshangao huo mithili ya mtu anayejiuliza, macho yake yakashuka kwenye bega la kushoto la kijana huyo. Hapo alijikuta akiona aibu sana baada ya kukuta jeraha la risasi ambalo lilisababishwa na yeye, macho aliyashusha chini akiwa ni mwingi wa aibu, alipoyanyanyua juu, alimkuta kijana huyo ndiyo kwanza alikuwa akizidi kuushangaa ule moto. Akataka kunyanyua mkono ili kuweza kulishika lile jeraha lakini Chrisa akamkatisha zoezi lake hilo kwa kusema.

    "hatuwezi kuendelea kuwepo hapa kwani hatujui maadui zako wako upande gani na vile vile askari wanaweza kuja muda wowote kuanzia sasa kutokana na mlipuko huu mkubwa, tuondoke." akasema huku akimshika mkono na kumtoa eneo lile na kuondoka huku ving'ora vya gari za polisi vikisikika kwa mbali vikija eneo hilo la tukio.



    Walifika kwenye hoteli moja kubwa mjini hapo, ilikuwa ni hoteli ya nyota tatu, hoteli yenye kila kitu ndani. Walikuwa wamekaa chumbani humo mara baada ya kila mmoja kwenda kuoga kwa nafasi yake na muda huo yule mama alikuwa akimtibu majeraha mbalimbali kijana huyo.

    "pole sana najua unaumia" alibembeleza mama huyo kwa kiingereza safi kabisa.

    "hapana endelea tu mbona ni maumivu ya kawaida sana kwani ilipiga nyama tu ile risasi na haikuacha madhara makubwa" aliposema hivyo Chriss, mama huyo akakumbwa na unyonge mkubwa. Alitamani masaa yarudi nyuma na auone wema wa kijana huyo pasipo kumjeruhi popote pale.

    "naweza kufahamu jina lako sasa?" aliuza Chriss.

    "Moline, Moline ndilo jina langu." alijibu mama huyo akiwa na aibu.

    "waliovamia pale walikuwa ni wanaume au wanawake?"

    "walikuwa ni wanaume si wengi ni watatu tu lakini bila shaka walijipanga sana maana ni kwa dakika chache tu waliweza kuwamaliza walinzi wangu wote" alijibu dada huyo na kumfanya Chriss ashushe pumzi nzito. Hakushusha pumzi hizo kwa sababu eti, ya watu watatu kuweza kusambaratisha ulinzi wote na kutaka kumuangamiza Moline, laa! kilichomfanya kushusha pumzi hizo ni je, ni nani yule mwanamke aliyekwenda kumfungua yeye kule kwenye chumba cha mateso alikokuwa kafungwa. Hakutaka kuliweka bayana hapo kwa kuuliza lakini jambo hilo lilimuumiza sana moyo wake na kumfanya ajiulize kila wakati. Hiyo ikiwa ni mara ya pili kwake. Moja ilikuwa ni hapo hapo kwenye sherehe ya ibada ndani ya jingo hilo hilo kwa kukutana na mtu aliyekuwa akimtazama huku akitabasamu kila amtazamapo, pili ni siku hiyo. Alidata, lakini aliamini ipo siku isiyo na jina atamjua.

    "hukuwahi kufanya tukio lolote lile baya kwenye maisha yako?" akauliza Chriss baada ya kutafakari ya kwake. Moline akatikisa kichwa kukataa kuwa hajawahi kufanya tukio baya.

    "usipokuwa mkweli ni wazi utakuwa unaniongopea, haiwezekani watu wakutafute hadi ulipo na kuuwa walinzi wako wote kisha wewe kutaka kukuuwa kwa bomu, tena bomu la masaa" alisema Chriss na alivyosema tu bomu la masaa, Moline akakumbuka. alikumbuka mbali sana na alikumbuka jinsi ambavyo alimuangamiza mtu aliyesadikika kuwa ni baba yake. Ikabidi Moline ampe kila kitu kuhusu maisha yake ya kuwachukia wanaume. Alihadithia mwanzo mwisho kuanzia maisha ya mama yake hadi alipokuja kumuua baba yake.



    "niliapa kumuangamiza yule mwanaume aliyesababisha kifo cha mama yangu gerezani pindi tu nikitoka kwenye kituo kilichokuwa kikinilea kama mtoto yatima. Ndiyo, baada ya mama yangu kufa gerezani, mimi nilikabidhiwa kwenye kituo maalumu cha kulelea watoto yatima. Nikalelewa pale na kukulia pale. Kweli nilipotoka pale, hapo tayari nilikuwa na umri mkubwa japo si sana lakini nilikuwa ninakisasi nimekibeba kuliko hata umri wangu. Elimu niliyoipata nikiwa kituoni na kupita shule mbalimbali nilizosoma, zikanifanya nigundue vitu vingi hata kufunga na kufungua silaha nilijua kwa kasi sana kwa kusoma baadhi ya mambo yanayohusiana na silaha. Hivi nilivifanya kwa siri kubwa Kwasababu nilidhamiria kumuuwa baba yangu. Na nilipofanya uchunguzi, nikaambiwa kuwa baba yangu si mtu mdogo kwani ni mafia na anamiliki kikosi hatari na yeye mwenyewe akiwa ni muuwaji, ikanibidi kuingia kwenye mafunzo mbalimbali ya kijasusi lakini mafunzo hayo, ulikuwa ukijifunzia mtaani na mafunzo hayo yaliendeshwa kwa siri sana na serikali ya marekani ya kipindi hicho ilikuwa ikipiga marufuku sana mafunzo hayo kutokana na kwamba yalikuwa yakizalisha watu hatari na wenye uwezo mkubwa wa kufanya uhalifu wa silaha na kufanya mauwaji ya kutisha. Maslahi yakafanya vyuo hivyo vya siri kuendelea kuweka usiri mkubwa na hata wakitumwa wapelelezi kuja kupeleleza, waliishia kufa tena kifo kibaya sana. tukajifunza kwa kasi kubwa na wote tuliokuwa tukijifunza ni watoto na wengi tukiwa ni mabinti wenye kuhitaji kilipiza visasi, kwani kuna rafiki yangu mmoja alikuwa akiniambia kila wakati na alikuwa akisema. (namnukuu).



    "Moline kisasi kitaishi moyoni mwangu milele hadi siku nitakapolipa" mwisho wa kunukuu. Na alikuwa akisema kila wakati, akilala, akiamka na hata akila. Baada ya miaka miwili ...............

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    . Baada ya miaka miwili tukapewa jaribio la kuweza kufuzu kama tuko fiti na jaribio hilo lilikuwa ni la malipo



    tungefanikisha. Lilikuwa ni jaribio la kuuza roho. Tukalifanya kwa ari kubwa na tukafanikiwa kuteka mzigo mkubwa uliokuwa ukitoka bank ya kati na kwenda benki kuu ya Marekani. Mzigo ule tukaufikisha kambini lakini cha ajabu ni kwamba hakukuwa na malipo makubwa tulipewa pesa ndogo sana na tukaambiwa kuwa tumefaulu na tutakapozidi kufanya matukio makubwa kama hayo nabkufanikiwa, watakuwa wanatulipa pesa nyingi sana na kutufanya tuwe matajiri. mimi na wenzangu watano wa kike, tukaona ile haikuwa haki na tulidhulumiwa na si kutudhulumu tu bali walipanga kututumia kwenye uharamia na inasemekana ndiyo kazi ya chuo hicho cha siri kilichokuwa kikitufundisha. Tukapanga mbinu hatari za kutoroka kambini hapo. Haikuwa rahisi lakini kwa kuwa tulidhamiria, tukaamua kutokomea usiku wa saa saba. Tuliuwa walinzi wote wa usiku na kutoweka usiku huo. Kitu ambacho tulikipanga baada ya kufika mafichoni, ni kuweza kumchunguza mkuu wa ile kambi. baada kama ya miezi sita ya uchunguzi huku tukifanya matukio makubwa ya kutisha ili kuweza kupora na kuishi mjini. Tulifanikiwa. Mbaya zaidi ni kwamba mtu aliyekuwa akimiliki ile kambi alikuwa ndiye baba yangu. Roho iliniuma sana kujua jambo hilo, hapo ndipo nilipojua wanaume si watu kabisa na hawastahiki kuishi katika hii dunia. Tukapanga mikakati ya kufanya maangamizi ya kutisha. Hatukuwa wengi tulikuwa watano tu. Siku ilipofika tulielekea mahali ambapo mzee huyo anaishi na tulipofika hatukuuliza, tulifanya mashambulizi makubwa tuliteka pesa nyingi sana ambazo alikuwa akizihifarhi kwenye chumba chake cha siri na kwenda kuzificha mahali, baba hatukumuuwa yeye alikimbilia kambini. Wenzangu wakaniambia kuwa mzee huyo aliwanyanyasa ki ngono walipokuwepo kambini hapo hivyo hawato kubali kumuacha hai. Ikatubidi kuivamia kambi kwa kushtukiza. Huko kulikuwa na mapambano ambayo sikuwahi kuyaota wala kufikiria kama ningekuja kuyafanya katika maisha yangu. Nakumbuka tulipambana kwa muda wa masaa matatu na kisha kukimaliza kikosi chote akabaki baba pekee lakini kwa upande wetu tuliwapoteza marafiki zetu watatu na tukabaki wawili tu na huyu mwenzangu alikuwa na majeraha mwili mzima. Akajikaza tukaingia ndani ambako ndiko alikojificha huyo baba. tulipofika, rafiki yangu alimpa kichapo kikali sana. Nakumbuka alikuwa akimpiga huku akiwa analia kwa jinsi baba huyo alivyomfanya, alisema alimnyanyasa sana kijinsia na kumdhalilisha mno alikuwa akimlazimisha mapemzi na yeye hakupinga kwa sababu alikuwa kuna kitu alikuwa akikitafuta. Alimpiga hadi akaridhika ndipo nilipomwambia aniachie na mimi nifanye yangu. Aliponipisha mimi sikumpiga bali nilichukuwa bomu kubwa nikalitega karibu yake huku tukiwa tumemfunga kamba na kisha nikatega saa tena kwa muda wa masaa mawili. Hapo ndipo baba huyo aliporopoka na kusema nimuache nisimuue na kuanza kunihadithia kila kitu kilicho pita kuhusu maisha yangu akasema kuwa yeye ni baba yangu. Nikachukua hadithi yake na hadithi niliyowahi kuhadithiwa na majirani waliokuwa wakiishi na mama yangu kabla hajaenda gererzani na kupoteza maisha huko baada ya kunizaa, nikajua kweli alikuwa ni baba yangu. Kosa alilolifanya ni kusema kuwa yeye ni baba yangu na kunikumbusha machungu. Ni bora basi hata asingesema na kuniacha nijue mwenyewe kuwa yeye ni baba yangu kuliko hivyo alivyoamua kufungua domo lake na kutoa maneno hayo yaliyozidi kunichefua. Neno ninalolikumbuka ambalo nilimwambi ni.

    "nakupenda sana baba yangu na ndiyo maana nimekuwekea sauti nzuri hapo pembeni yako, hebu angalia basi jinsi spika hiyo inavyojitahidi kukuimbia" alipogeuka alilikuta ni lile lile bomu tena likiwa limebakisha sekunde za kuhesabika. Rafiki yangu alinishika na kunitoa mule ndani kwa nguvu sana hadi nje, huko tukapanda gari na kutoweka, tulipofika nje ya ile kambi, mlipuko mkubwa na wa kutisha ulisikika. Tukaongeza kasi na kutoweka. Tulikuwa na pesa nyingi sana ambazo zingetufanya kuwa matajiri hadi tunakufa. Tukapanga kila kitu baada ya kugawana pesa ile na mwenzangu akaelekea Brazil kuanzisha maisha yake na mimi kuhamia hapa uingereza. Na huyo mwenzangu alipokwenda Brazil, hakupenda maisha ya huko hivyo akahamia Urusi na ndiye aliyenipa ndege ambayo ilikufikisha wewe hapa baada ya kukuteka kule Moscow." alisema Moline. Ilikuwa ni story yenye kuumiza sana na ilimuweka kimya Chriss kwa muda kidogo huku akimuangalia dada huyo jinsi ambavyo yupo katika uchungu mkubwa. Ni wazi alikuwa na haki ya kufanya yote yale na alifanya hivyo kwa sababu hakuwa na mtu ambaye alimshauri kitu kizuri juu ya maamuzi yake. Lakini je, kama ni kweli amuzi hilo ni sahihi ni vipi atamaliza hasira zake au kama ameshamuua baba yake, kwa nini sasa aliamua kuendelea na kisasi. Kisasi huwa hakiishi na unapo kuwa na nadhiri ya kulipa kisasi basi ni wazi kisasi hakina mwisho na kizazi na kizazi kitakuwa kikiendeleza kisasi hicho.

    "Moline!" aliita Chriss. Moline akanyanyua kichwa kumtazama kijana huyo mpole kisha kijana huyo akasema.

    "ni kitu gani ambacho unaweza kufanya kwa sasa ili roho yako iachane na kisasi ulichokibeba moyoni mwako?" aliuliza Chriss. Moline alijiinamia na kuona aibu kubwa sana juu ya hayo maneno yaliyojenga swali kwake. Hakuwa na kitu cha kusema pia hakuwa na jibu zuri kwa mwanaume huyo.Akajikakamua na kujibu kuwa hakuna kitu kingine ambacho kitamfanya alipe kisasi. Aliposema hivyo alikumbana na swali jingine.

    "ninaimani bado hasira zako kwa wanaume wote duniani, hazijakwisha bado si ndiyo?" ki ukweli swali hili hakuwa na jibu nalo na badala yake alijivuta karibu na kumsogelea kijana huyo kisha akalishika lile bandeji ambalo lilikuwa limefunga kwenye jeraha la risasi, jeraha ambalo kama si yeye lisingekuwepo mahali hapo. Moyo ulimuuma sana. Kijana huyo hakustahili hata mchubuko kutoka kwake ni wazi kabisa alimkosea na kwa makosa hayo alipaswa kuomba msamaha. Chriss alichukua bastola na kuikoki vizuri kisha akamkabidhi na kumwambia.

    "timiza ile ahadi yako ya kutaka kunipasua kichwa, huu ndiyo muda pekee wa kufanya hivyo ili roho yako ipate kuridhika" Moline aliumizwa sana na hayo maneno, aliumia sana na kujikuta akikosa namna ya kufanya.

    "kama nimeweza kutibu jeraha nililolisababisha mwenyewe, ni wazi kabisa kuwa kwa sasa nimekuwa mpya wa nafsi. Hukustahili hata kuoneshewa kidole SM, hukustahili hata kupigwa kofi, hukustahili nasema hukustahili kabi........!" alishindwa kumalizia na machozi yakaanza kumtoka. Akayafuta na kuvuta kamasi nyembamba zilizokuwa zikimchuruzika kisha akarndelea.

    "nilidhani wanaume wote ni wakatili na wauwaji SM, baba yangu amenilisha sumu mbaya sana ambayo hata kama ingekuwaje nisingeweza kuitoa kwa kawaida. Sikutaka kuwauwa wanaume japo nilikuwa nikiwachukia sana ila nilichokiamua ni kuto kumruhusu mwanaume kuugusa mwili wangu kwa kuuingilia hadi pale nitakapokuwa marehmu. Kumbe nilikuwa nikikosea. Nilikosea sana kuliadhibu kundi kubwa la Ng'ombe kwa kutolipeleka malishoni, kwa kosa la Ng'ombe mmoja tu aliyeingia kwenye shamba la mkulima masikini. Nisamehe sana SM. Nasema nisamehe kwa sababu nakiri nimekosa na nimekukosea sana. Sikutegemea kama kipigo kile tulichokupa mule ndani, halafu eti upate ujasiri wa kuniokoa mimi." alimaliza kuongea Moline na kutulia kimya akisikiliza kama maneno yake na msamaha kwa mwanaume huyo kama umesikika na kukubalika.

    "nimefarijika sana Moline kwa kutambua wajibu wako na kile unachopaswa kukifanya. Huu sio muda tena wa kudili na kisasi japo kipo na kinakuzunguuka na wanaokizunguusha kisasi hicho ni wale ambao, wanataka wakilipe kwako kwa kile walicho kipoteza" alizungumza Chriss lakini kauli yake hiyo ikamfanya Moline kushtuka na kuamua kuuliza ni nani hao wanaotaka kulipa kisasi kwake. Chriss akatulia kidogo na kuvuta pumzi ndani ya mapafu yake kwa utaratibu kisha akageukia upande aliyoko mwana mama huyo ambaye alikuwa akimtazama kwa macho ya mshangao. Akasema.

    "wapo watu waliomuamini sana baba yako na kumheshimu na siyo kumheshimu tu bali walimtegemea pia. Hao walijua kuwa mtu huyo ameuwawa na mtu wa karibu na pengine ni kwa lengo la kulipiza kisasi. Bila shaka walitafuta kwa muda mrefu sana kumjua mtu huyo, sasa maisha yako ambayo uliamua kuishi ndiyo yaliyokukamatisha mapema sana kwa watu hao. Hupaswi kuishi maisha yale tena na pia hutakiwi kuonekana tena ndani ya ardhi hii ya London kwani wauwaji waliokuja kwa lengo la kukuuwa wanajua kuwa umesha kufa." maneno hayo yalimfanya ashushe pumzi nzito sana na kutulia kimya huku akimpa mwanya kijana huyo wa kuendelea kuongea.

    "unao utajiri wa kutosha, unazo pia pesa kama siyo mali. Hutakiwi kuwa na marafiki wale wa zamani tena, unatakiwa kuwa na marafiki wapya ndani ya taifa jipya huku ukiwa na maisha mapya yenye mtazamo mpya. Hapo utweza kishi kwa amani bila kuwaza kufuatiliwa tena. Waamini wanaume na waone ni binadamu ambao hawakuumbwa na ukamilifu lakini pia kama yupo anayekukwaza kwa makusudi, huna budi kumuepuka na siyo kufanya maamuzi mazito yatakayoongozwa na hasira zako" alikomea hapo na kutulia. Moline alimuangalia kijana huyo wa kiafrika mwenye uzuri na upole wa aina yake, akageuka pembeni. Akataka kumuuliza kwanini ameamua kuwa Sex Machine, akasita. Akaona atakuwa ni kama anamchimba.

    "nikaishi wapi tafadhali nichagulie taifa la kwenda kuishi" akasema.

    "nenda ukaishi Brazil huko naamini kutakubadilisha na kuwa mpya. Kwani yule binti yako yuko wapi?" akajibu kisha akauliza.

    "nilimpeleka nchini Urusi kwa rafiki yangu ili niweze kukamilisha mauwaji yako ndipo nimrudishe nyumbani, niliamua kumuachia huru na angeweza kufanya jambo lolote lile lakini sikutaka akutane na wewe tena. Nilikuchukia sana."

    "unanichukia tena?" akauliza Sex Machine huku akimtaza mama huyo kwa ukaribu zaidi. Mama huyo akatikisa kichwa kukataa kisha akauliza swali.

    "ulishawahi kusomea saikolojia labda?"

    "hapana sijawahi"

    "kweli!?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ndiyo sijawahi ni uwezo binafsi tu" alijibu Chriss na kupelekea Moline kuto kuamini. Lakini ni kweli kwamba kijana huyo hakuwahi kusomea saikojia hata kidogo. Moline alijikuta akijihisi raha sana kuwa karibu na kijana huyo. walizidi kupiga soga za kawaida hadi pale Chriss alipoomba akajimwagie maji kwa mara nyingine kwa ajili ya kutoa ile harufu ya dawa, hapo ndipo ukawa mwisho wa maongezi yao. Chriss alinyanyuka na kuchukua taulo kisha akaelekea bafuni akiwa na bukta tu mwilini mwake. Kwa mara ya kwanza Moline alijikuta akijihisi hali ya hatari sana. Moyo wake aliuona kama ulikuwa ukipotea njia

    [12/22, 5:40 PM] Ahmed Jiriwa: Riwaya: Sex machine 46.



    kwa jinsi ambavyo ulikuwa ukiongeza kasi ya mapigo yake. Hakuwahi kuwa na hisia hizo katika maisha yake na kama ziliwahi kumtokea, si kwa wingi kiasi hicho. Alijkuta akimtazama kijana huyo anavyopotelea kwenye mlango wa bafu hilo la kisasa kabisa, bafu la kioo, bafu ambalo aliyeko bafuni alimuona wa chumbani na aliyeko chumbani alimuona wa bafuni.

    "nimekuwaje hivi?" alijiuliza huku akishika titi zake ambazo hazikuwahi kukamatwa na mkono wa mwanaume zaidi ya mikono yake mwenyewe. Alihisi muwasho wa aina yake kwenye ncha za chuchu zake. Kila akifumba macho alikiona kifua cha SM kikiwa kimegawanyika na kujihisi kama amekilalia.

    "mbona leo hivi jamani, najihisije hali hii mbona haijawahi kutokea hata siku moja" alishtuka sana na kusogea hadi karibu kabisa ya koo na kuchungulia ndani ya bafu hilo. Hapo aliachia mdomo wazi baada ya kumuona kijana huyo akiwa amesimama katikati ya chumba cha bafu akiyaruhusu maji yauogeshe mwili wake. Mzigo wa haja ukiwa unanepa kwenda kushoto na kurudi kulia, alihisi hisia za ajabu sana zikiuvaa moyo wake, tayari pepo mbaya alikuwa akimtafuta kwenye kumi na nane zake. Aliduwaa hivyo hadi akawa hajui kama mwenzake alikuwa akimtazama tena kwa muda sana. Yaani bumbuwazi lililokuwa limemkata lilikuwa kubwa sana kiasi cha kutazamana na anayemchungulia humo bafuni lakini hamuoni. Alikuja kushtuka baada ya kumuona anayemchungulia ameacha zoezi la.kuoga, ndipo akaona jinsi wanavyotazamana, akageuza macho yake pembeni kwa haraka sana.

    "hivi atakuwa ameniona eeh? Oou jamani kaniona, aaa, sasa itakuwaje kama ameniona kuwa namchungulia?".....................





    alikuwa akizidi kujiuliza huku akikirudisha kichwa chake taratibu tena na kutaka kutazama kule bafuni kwa kuibia lakini alipoangalia tu akakutana na tabasamu huku kijana huyo akikimwagia maji kile kioo na kukifanya kisiweze kuonesha vizuri. Moline alitabasamu baada ya kuona mchezo ule.

    "jamani ametabasamu hadi raha. oh my God! mbona anamdudu mkubwa vile hadi ananisisimua, sasa kwanini amemwaga maji ili nisimuone? Na mimi namuendea huko huko sasa haiwezekani aoge peke yake kwani mimi sistahili kuoga. Naenda hivyo hivyo hata kama nimekwishaoga tayari" aliongea hapo kisha akapambua nguo zote na kulionesha umbo lake zuri na lenye mvuto wa aina yake. Matiti mazuri yaliyo tuna na kutengeneza mduara kama embe Bolibo. Chuchu zake za kuvutia akazishika kidogo na kuziminya kisha akacheka kidogo baada ya kuvuta hisia kali sana.

    "aaaaaaashhh!" akajitumbukiza ndani ya hilo bafu kwa ghafla. Sex machine alijua tu kuwa mwanamke huyo hawezi kuvumilia na ni lazima angelivamia bafu. Hakukuwa na wa kumsemesha mwenzake. Na alipoingia mule ndani ni moja kwa moja kumkumbatia kijana huyo na kumpa mdomo. ladha ya mate ikawafanya wagugumie na kuzidi kupapasana kwa hisia kali na sauti za mahaba kuchukua nafasi. Walizidi kushikana shikana hivyo na kuzidi kupeana ladha mbali mbali. Moline akili ilimruka mahali hapo alisahau au sijui alifanya makusudi. Inamaana kweli hakukumbuka kuwa yeye ndiye aliyekuwa akimsaka huyo kijana kwa kutaka kumuangamiza sababu ikiwa ni kuharibiwa binti yake? Itakuwaje kushiriki penzi na mwanaume aliyetembea na mtoto wako. Lakini mama huyo alizidi kufurahia mchezo huo tena akiwa anaonekana kuwa na hamu kubwa maana kwa jinsi alivyokuwa akiinyonya hiyo maiki ya SM, ni kama yuko kwenye mashindano ya jambo hilo. alikuwa akilalama mwanzo mwisho na kutoa sauti tamu yenye kuhamasisha. SM alikuwa akibweka kwa raha za aina yake kwani Moline alikuwa hanyonyi bali alikufuru. Inawezekana alijua kuwa kijana huyo ndiye aliyeivunja bikira ya binti yake ila ni kutokana na kutokujua uchungu halisi wa binti yule ambaye kumpata kwake ni kutokana na kuchanganya vinasaba vyake na vya mwanaume kwa kupitia mbegu za uzazi ambazo alizinunua kwa gharama kubwa na kuzipandikiza mbegu hizo kwenye maabara maalumu zinazohusika na kazi hiyo. Yai likaanguliwa kwenye Tube maalumu na kukuzwa humo hadi pale zilipounda kiumbe ambacho kilihamishiwa kwenye maabara nyingine kwa maendeleo zaidi. Pengine hili ndilo lililomfanya asiwaze juu ya kushiriki penzi la mwanaume huyo aliyetembea na binti yake. Kuzaa kwa uchungu kuna faida kubwa sana jamani. Kwa sbabu utakuwa unayajua maumivu ya kile unachokilea hivyo huto penda kufanya kitu ambacho kitautesa moyo wako kwa kuhisi utakuwa umemzulumu haki yake. Manung'uniko yalizidi na kwa muda huo tayari SM alikuwa amemkunja mama huyo kwa mtindo wa funga kamba za viatu na kumshindilia mpingo kwa nyuma. Alikuwa akilia kwa raha huku akijitukana mwenyewe kwa kosa la kutokuupa haki mwili wake kwa kipindi kirefu. alikuwa akijituma kwa nguvu sana na akimwambia kijana huyo amfanye kwa nguvu nyingi kwani raha anazozisikia hapo hazikuwa na kifano chake, hakupata kitu cha kufananisha raha hizo na zote alizokuwa akizipata duniani. SM alikuwa hapigiwi, alisukuma na kusukumiza ndani mara nyingine akawa anazamisha mpini wote ndani na kumng'ang'ania huku akiwa anamsugulia kwa ndani. Hapo ndipo palikuwa na kelele za kufa raia. Alilia hadi pale kijana huyo aliposhusha mzigo na kwa mara ya kwanza tangu kuwa Sex machine, anajikuta anakojolea ndani, mama huyo alitabasamu na kupumua pyuuuuuu! Bado mama huyo alikuwa akitaka mchezo uendelee, hivyo wakaamua kuoga na kuelekea chumbani kwa ajili ya mtanange mwingine ambao huo Moline angemtafutia SM jina la kumpa.



    %%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%



    Asunuhi kulipokucha Moline alikuwa hoi bin taabani. Mchezo haukuwa wa kitoto hata kidogo, alikesha kifuani kwa SM kwa usiku mzima akihema kwa pumzi za raha alizokuwa akipewa na kidume hicho. Alideka kama mtoto mdogo kwa kila alipotakiwa kudeka, penzi alilopewa lilikuwa la aina yake, alitamani sana kuanza mambo yale tangu akiwa mdogo lakini haikuwa hivyo, aliishi kifungoni kwa muda mrefu sana hivyo yote ya yote aliamua kumtupia marehemu baba yake kwa kumfanya aishi maisha ya kuwa mtumwa wa fikra. Aliamshwa kitandani hapo na kelekea bafuni ambako alioga na kurudi kisha akapewa nguo mpya kabisa za kuvaa ambazo hakujua kijana huyo alizitoa wapi, hakuhoji, alizichukua na kuzitia mwilini nguo zile zilimkaa kisawa sawa kabisa kama vile alipimwa. Alibaki kumuangalia tu kijana huyo na kuishia kutabasamu. Chrisa alikuwa ameshapiga lile vazi lake na kufuatiwa na suti safi nyeusi ambayo ilikwenda kulifunika lile jeraha. Wakatoka wote na kuelekea uwanja wa ndege. walipofika, Chriss akachukua ndege itakayompeleka Ufaransa na Moline alichukua ndege inayoelekea nchini Brazil.

    "naomba uwe unakuja kunitembelea SM, hata kama nitakuwa na mwanaume mwingine lakini wewe bado una nafasi yako tena kubwa mno na ya pekee sana" alisema hayo Moline alipokuwa amemkumbatia kijana huyo akiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa London, akiondoka na kwenda kutafuta maisha mapya akiwa katika taifa jingine. Alifumbua macho na kutazama pembeni ya kiti na kumuona dada mmoja akiwa amepakata mtoto mdogo wa kiume ambaye alifanana kila kitu na mtoto huyo. Alitabasamu kwa tabasamu la wazi kabisa, aliwaza mengi kubwa likiwa ni kutamani kuzaa mtoto ambaye naye pia atakwenda kufanana naye au hata asipofanana naye basi afanane na mtu wa pekee anayempenda, mtu aliyemrudisha kwenye maisha mapya anayopaswa kuishi binadamu wa kawaida.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "nakwenda kuzaa mwanangu wa kwanza kwa uchungu. Asante sana SM najua ipo siku utakuja na kumkuta mtoto wako akiwa amesha zaliwa" aliwaza hivyo Moline kwani anajua kwa vyovyote vile ni lazima ashike mimba kwani ameshiriki mapenzi na kijana huyo akiwa yu katika siku za hatari za kushika mimba. Nakwenda kusahau kila kitu kilichopita sasa, Doreen sitakutupa mwanangu najua nimefanikiwa sana hadi hapo ulipofikia na ninaimani utaweza kuwa na maisha yako huko huko Urusi" alizidi kuwaza na kulishika tumbo lake dogo ambalo aliamini baada ya muda litakuwa likiishi kiumbe cha thamani kwani hata mtu aliyempa mimba ni wa thamani sana kwake.

    Kwa upande wa Chriss yeye alikuwa na furaha tu kwa kuweza kumfanya mtu katili kurudi kwenye maisha ya kawaida na hakujua kwa nini furaha yake ilikuwa kubwa kila wakati. hakujua furaha hiyo ilisababishwa na nini hasa, lakini kikubwa na alichokuwa akikiwaza ni kuweza kumpa Moline maisha mapya.



    Alikwenda Ufaransa akachukua mzigo na kuusafirisha mzigo huo wa dawa za kulevya aina ya FD. Akausafirisha hadi nchini Brazil na kurudi zake Tanzania akiwa salama kabisa.



    Mambo yalizidi kuwa mambo, furaha ya Joesan ilikuwa ikizidi kila wakati lakini pia Chriss alikuwa akipata mafanikio makubwa sana kupitia kazi hiyo haramu huku akizidi kuwaingizia mamilioni ya shilingi mabosi zake.



    Kikao kikubwa kilikuwa kimekaliwa. kikao hiki kilikuwa ni cha watu wa nne. Alikuwepo Joesan kama mkurugenzi wa kampuni lakini pia alikuwepo Suzane. Binti mrembo na anayeaminiwa na bwana Joe. Alikuwepo mzee Rafael, mzee mstarabu asiye na makuu, mzee mkimya lakini mwenye talenti kubwa ya mapigano. Hawa watatu waliweza kujaza nafasi za viti vlivyokuwepo eneo hilo la siri. ulikuwa ni usiku wa saa sita na kilikuwa ni kikao cha siri kuliko siri yenyewe. Kikao hiki hakuna aliyekuwa anajua mzizi wake ni nini zaidi ya Joesan pekee. Mtu wa nne kwenye kikao hicho alikuwa ni mkuu, mr. Kim ambaye yeye aliwakilishwa na sauti yake kama kawaida. Na kikao kikaenda kuanza rasmi kwa sauti ya mkuu kusikika ikijikohoza kisha kuzungumza bila kusikika popote ila waliopo eneo hilo walisikia kutokana na sauti hiyo kuipata kupita vinasa sauti walivyokuwa wameviegesha kwenye masikio yao. Walikuwa wametulia kimya wakisiliza na hakuna hata mmoja ambaye alitia neno ama kuingiza swali, kila mmoja alikuwa ni msikilizaji kisha wakatazamana. Lakini wakati hayo yakiwa yanaendelea, kuna mtu alionekana kwenye kona moja karibu kabisa na ukuta wa jingo la kampuni ya Safaries Company. Alikuwa amevaa koti jeusi lililokuja hadi kichwani na pia alipiga na mawani nyeusi ambayo haikuwa mawani ya kawaida. Hiyo ilikuwa ni mawani ambayo ilikuwa inauwezo wa kupiga picha na vile vile kurekodi kitu chochote na pia yenye uwezo mkubwa wa kuona gizani. ..............................



    Tunamuona mtu huyo anaangalia saa yake ya mkononi na kuanza kutembea taratibu kwa kujiamini kisha anaruka ukuta wa jingo hilo, lenye ukuta ambao haukuwa mrefu sana wa kutisha. Wakati mtu huyo aliyejiziba kwa koti kubwa jeusi akiwa analikaribia lango la hilo jingo, umeme ukakatika mtaa mzima. Mtu huyo akafungua mlango kwa njia azijuazo mwenyewe na kuzama ndani. Muda huo kwa upande wa kule kwenye mkutano wa siri watu walikumbwa na mshtuko kila mmoja akawa anashangaa asijue nini cha kufanya.



    "Mkuu anasema kamera zote za kampuni zimezima ghafla" alisema joesan kwa sauti ya chini kana kwamba wakati huo mkuu wao anaongea, alisikia peke yake na wakati wote pale walikuwa na vifaa vya kunasa sauti. Alichanganyikiwa sana Joesan. Kitendo cha kamera za kampuni kizima ghafla wakati si kawaida, kilimchanganya yeye na mkuu wake wasijue nini tatizo.



    "inamaana mkuu hakuna hata kamera ya akiba ambayo inaonesha uhai?" aliuliza Joe.

    "hakuna Joe zote zimezima" alijibu kim akiwa haamini.

    "oh! Labda litakuwa ta......!"

    "sina hakika Joe kwa hilo unalosema na mimi vitu vyangu ninavipeleka kisasa sana, sasa hilo tatizo ulilotaka kulisema hapo ni la nini labda" Kim alimkatisha Joe akiwa hayupo katika hali ya kawaida kabisa.

    "fanya jitihada Joesan Tujue nini tatizo siyo kuniuliza maswali ya kipumbavu" alifoka Kim akiwa amechanganyikiwa kabisa.



    Hapo ndipo utakapojua kuwa mzee huyo anajali zaidi mali zake kuliko utu. Kwenye matatizo ya kampuni zake huwa hakuna boss wala na ni mtu mwenye hasira mbaya sana bwana huyo. Kampuni kama hiyo iliyobeba siri kubwa za maisha yake halafu kamera zote zizime, hiyo ni hatari sana na tukio kama hilo halikuwahi kutokea. Joesan alinyanyua mkonga wa simu na kuiweka sikioni kisha akabonyeza namba kadhaa na kusikilizia, simu ya upande wa pili, simu hiyo iliita kidogo kisha ikapokelewa na yeye kuanza kuongea.



    "Tai unanisikia!"

    "ndiyo nakusikia kiongozi" alijibu Tai mtaalamu huyo wa mambo ya teknolojia na mjenzi pia akiwa ni msimamizi wa mitambo yote ya hatari inayotumika kuathiri watu akili.

    "kamera za kampuni zote zimezima" alisema na wakati huo wakati Joe anaongea na simu, Mr. Kim alikuwa ameikazia macho luninga yake iliyokuwa ikiwaona watu wote waliopo kwenye hicho kikao na alikuwa ametega sikio kwa umakini sana kusikiliza nini kitajibiwa hapo.



    "itakuwa ni tatizo la umeme kiongozi" aliongea Tai.

    "usiseme itakuwa Tai tunataka uhakika, mkuu hayupo sawa na mimi ndiyo nimechanganyikiwa kwa asilimia kubwa sana" aliongea Joesan akiwa amepandisha sauti juu kabisa.

    "hivi ninavyoongea na wewe kiongozi ndiyo natoka hapa na pikipiki nikacheki" aliongea Tai.

    "ok, fanya hivyo na tupo hapa tunasubiri kitakachojiri huko, haiwezekani iwe ni umeme wakati kuna jenereta ambalo linajiendesha lenyewe umeme unapokatika" alisema Joe.

    "jenereta halijafanyiwa marekebisho si unajua" alisema Tai na simu ikakatika hewani. Tai akapanda kwenye pikipiki lake kubwa na kuingia barabarani kuelekea huko kunako tukio lililowachanganya vichwa mabosi hao.



    Lakini kwa upande wa kampuni tunamuona mtu huyo asiyefahamika akiwa anapita kila chumba na kufanya yake kwa haraka sana. Alihakikisha kila chumba anaingia tena akiwa makini sana na mara kwa mara alikuwa akiangalia mkono wake uliobeba saa. Haikujulikana alichokuwa anakifanya lakini hakuwa mtu wa kawaida hata kidogo, vitu vyake alifanya kwa kasi kubwa mno. Alionekana akipiga picha baadhi ya maeneo kwa kutumia ile mawani yake kitaalamu zaidi. Ni kitendo ya sekunde thelathini tu, alikuwa tayari amepita sehemu zote muhimu na kuweka alichopaswa kuweka na kutoka humo ndani huku mawani aliyovaa ikimsaidia kuona kwa ufasaha kabisa. Wakati yeye anatoka ndani ya lile jingo baada ya kufanya alichokikusudia, nje ya lile jingo upande wa mbele, Tai akafika na kupaki pikipiki lake kisha akapiga simu na kuiweka sikioni.



    "ndiyo!" ilipokelewa simu hiyo kwa haraka sana na mpokeaji akiwa ni Joe.

    "ni tatizo la umeme kweli kiongozi kama nilivyo hisi hakuna kitu kingine cha kuhisi zaidi ya umeme kwani mtaa wote huu hauna umeme" alisema Tai na kumfanya Joesan ashushe pumzi nzito akifuatiwa na Mkuu wake. Mkuu akaachia tusi zito kwenda kwa Tanesco kisha akasema.

    "hakikisha kesho ile plate ya kunyonya nguvu za jua inafungwa na tunaachana na jenereta hii ni hatari tutakuwa tunapata shinikizo la damu namna hii hadi lini" Tai akajibu.

    "umesomeka kiongozi"



    Tai akakaa kwa muda pale kwa takriban dakika tatu, umeme ukarudi naye akaondoka. Lakini wakati umeme unarudi, mtu mwenye koti alisharuka ukuta na kupita kwenye chochoro alilokuja nalo na kuzipita nyumba kadhaa na kuibukia mtaa mwingine. Akajizunguusha na kurukia pikipiki kubwa. Wakati anarukia hilo pikipiki, na kutokana na eneo hilo kuwa na mwanga kiasi, ndani ya lile koti jeusi ikaonekana bikini nyekundu. Hee! Inamaana huyo alikuwa ni bikini nyekundu? Ni nani sasa huyo dada na hapa napo amefuata nini ndani ya hiyo kampuni. Kizunguzungu.

    Aliitoa pikipiki hiyo kwa kasi kubwa hadi maeneo ya Forest usiku huohuo. Akatazama saa tena na kusogea karibu na lango moja kubwa kwenye jingo moja la kifahari sana hapa akatulia kidogo. Wakati huo kikao cha siri kikiwa kinaendelea kule kwa akina Joesan. Mtu yule mwenye koti akazama ndani ya ule uzio kama alivyoingia ndani ya jingo la kampuni na hapa napo umeme ukakatika mara tu baada ya kuukaribia mlango. Akaufungua na kuzama ndani taratibu, akapita sebuleni. Akaifuata korido ambayo ilikuwa kama inampeleka jikoni, hapa akatulia kwenye chumba kimoja kilichokuwa kimejitenga sana kisha akakifungua na kuzama ndani. Chumba hiki ndicho ambacho alikuwa akiishi Chriss kabla hajabadilishwa akili na kusahaulishwa ya nyuma. Akaangaza macho ndani ya kile chumba, kilikuwa ni chumba kisafi sana na inaonesha chumba hiki hakijawahi kuguswa ama kutumika tena tangu Chriss kutokuonekana. Akafungua mtoto wa meza mtu huyo na kukuta picha ya Chriss angali mdogo bado, hapo ilionekana akiwa na miaka kama mitatu hivi au miwili na ushee. Aliitazama kwa muda kidogo picha hiyo hadi machoziCHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    yakamdondoka kupitia mawani ile aliyovaa na kujenga njia shavuni mwake kisha chozi hilo likaporomoka na kuangukia juu ya ile picha tena kwenye paji la uso la kijana huyo. Alishtuka kidogo na kuifuta ile picha kisha akairudisha kama ilivyo akiiambatanisha na kidude kidogo sana kisha akaurudisha ule mtoto wa meza, akasogeza kidogo mawani yake pale machoni, akatoa kitambaa na kufuta machozi kisha kuuelekea mlango ili kutoka mule ndani. Ila wakati anatoka, ukutani akaona picha iliyomuonesha akiwepo yeye, mama wa Chrisa na baba wa Chriss kipindi hicho wakati yeye akiwa ni binti mdogo kabisa, wakiwa wamesimama. akatabasamu kuziona sura hizo kisha akatoka akiwa anafuta kamasi na kuurudisha huo mlango akaufunga kama alivyoukuta. Kichwani alikuwa akiiwazia sana ile picha, pengine Joesan alikuwa na nia mbaya zaidi ya kuzidi kumfanya kijana huyu zezeta, aliwaza hayo kutokana na ile picha pale ukutani lakini hakuishia kuwaza tu. Akaongoza moja kwa moja hadi kilipo chumba cha Joesan, hapa aliponyonga kitasa, mlango ukafunguka akaingia taratibu lakini mwanamke aliyemo humo ndani akashtuka na kuamka ghafla na kukamata simu ya mkononi. Alichelewa. Mtu huyo mwenye koti kwa kasi ya ajabu sana, aliruka na kuipiga teke ile simu ikaenda kuangukia ukutani huku simu hiyo ikipoteza uhalisia kwa kuchanguka baada ya kupiga vibaya ukutani. Mama huyo mwenye nyumba alibingilia na kuanguka chini ya kitanda kisha akachomoka na bastola ambayo nayo haikudumu mikononi mwake hata kwa sekunde tatu, ilipigwa kitaalamu sana kisha mama huyo akachotwa mtama na kujibwaga chini kwa kishindo. Wakati purukushani zikiwa zinaendelea, Mery alishtuka kutoka usingizini lakini mtu mwenye koti jeusi alimuona, akajirusha pale kitandani na kwenda kumgusa kidogo shingoni. Mtoto huyo akapoteza fahamu kisha akamnyanyua na kumtupia begani na kuchomoa bastola ndefu aliyokuwa ameihifadhi pajani mwake kwa kuifunga na mkanda maalumu na kumuelekezea mama huyo. Martha macho yalimtoka baada ya kuona kila jitihada za kujitetea zimegonga mwamba na sasa alikuwa akitazamana na mtutu wa bunduki.



    "Joesan!" aliita mtu huyo mwenye koti jeusi kwa kunong'oneza mithili ya mtu anayeongea jambo la siri kwenye sikio la mtu mwingine. Akaendelea.

    "ni muda wako sasa wa kuhisi maumivu. Ulilolipanga kwa huyu binti limefeli kuanzia sasa na najua ulikuwa umepanga kumuuwa kisaikolojia huyu pia kama ulivyomuuwa huyo liyempa jina lako unalotaka wewe ili tu umuondoe katikta kuutambua ukweli wa maisha yake na historia ya wazazi wake huku ukizidi kumzunguuka kwa kumwambia kuwa, jina la pili linaweza kuwa la kwanza. Kila wakati ulikuwa ukifurahi pale ulipokuwa ukilitaja jina la kijana huyo ulilolitunga mwenyewe kwa maslahi yako. Eti, Christiano Robin Isaya. F*ck Joesan" alimaliza kuongea kwa kumtukana tusi kubwa bwana Joesan kisha akaitoa usalama ile bastola na kuilekeza kwenye paji la uso la Martha ambaye alikuwa amefumba macho kukipokea kifo hicho. Alikubali kuolewa na mwanaume katili na muuwaji hivyo alijua fika ipo siku naye atakuja kuuwawa pindi mumewe akiwepo au kuto kuwepo, hivyo hakuwa akiogopa tena bali alichokuwa akikifanya hapo ni kumlaani mumewe mwanzo mwisho na alikuwa tayari kufa kwani hata hivyo hakuwa na cha kupoteza kama ni maisha alipokula panatosha. Faida yake hakuiona tena kwanza hakuwa mtu wa kuijaza dunia kama Mungu alivyoagiza na badala yake alikuwa akila tu bila kuleta faida. Mshahara wa dhambi ni mauti. Kweli ni hivyo lakini Martha alikuwa akihusishwa na kila baya kwa ...................................





    na badala yake alikuwa akila tu bila kuleta faida. Mshahara wa dhambi ni mauti. Kweli ni hivyo lakini Martha alikuwa akihusishwa na kila baya kwa kukubali kuishi na bwa huyo, alikuwa akishuhudia kila unyama aliokuwa akiufabya mumewe na hakuchukua hatua yoyote, hivyo ni kama alikuwa akiyashiriki hayo mabaya. Hata kama hakuwa na sauti kwa mumewe lakini pengine angeweza kwa na uwezo wa kufanya jambo na mumewe huyo kuchuuliwa hatua. Labda aliridhishwa na tabia ya mumewe. Yule mtu aliyemshikia bastola akasema sasa akiwa anasema kwa sauti ya juu kidogo.



    "fill pain Joesan" alipomaliza kusema hivyo akampiga risasi moja ya kwenye paji la uso. Risasi ambayo haikuweza kuacha alama yoyote pajini hapo, hakukuonesha kama alipigwa risasi maeneo hayo kwani hakukuwa na damu wala alama ya risasi yenyewe. Kisha mtu huyo mwenye koti akapotea na yule binti na kutokomea nae gizani.



    Asubuhi ya siku iliyofuata ndiyo mambo yalipobumbuluka pale Joesan alipoingia nyumbani kwake na kukuta kila kitu kiko tofauti. Alimkuta mkewe mpendwa amekauka akiwa wa baridi kabisa kuonesha kuwa kifo kilimkuta muda kidogo. Wazo la nini kilichomuuwa mkewe likakaa kichwani, alimgeuza kila kona lakini hakujua ni nini kimemsibu mkewe. Alipatwa na machungu makubwa bwana huyo, aliumia sana moyo. Hakuweza kufanya kitu chochote kwa wakati huo alijikuta nguvu zikimuishia na kukaa kabisa kitandani. Japo alikuwa akimfanyia vituko mwanamke huyo lakini ni wazi alikuwa na mapenzi naye makubwa sana. Mtima wake ulimuuma sana kwa tukio la kukuta mkewe akiwa amekufa. Machozi ya uchungu yalimtoka, alilia kiume kwa muda mrefu hadi pale dukuduku zito la uchungu lilipomtoka mtimani mwake, ndipo akapata wazo la kuchunguza nini hasa kilichopelekea mkewe kufa. Alikikagua chumba kile ndipo akaona simu ambayo ilikuwa imetawanyika vibaya sana pia aliona bastola ndogo ikiwa imeangukia kwenye pembe ya kitanda. Akajua mtu aliyemvamia mkewe hakuwa daraja dogo, ni mtaalamu na anaejua nini anafanya. Ni nani? Na kwa nini? Akabaki kujiuliza. Ni wazi mkewe alikuwa anampango wa kumpigia simu ili kumjulisha kuwa amevamiwa lakini adui kwa alivyo shapu akamuwahi na kuipiga teke simu. Mkewe akakimbilia kwenye silaha angalau aweze kujitetea nako adui akamuwahi na kuipiga silaha hiyo teke na kuanguka mbali kisha akamuuwa. Sasa alimuuwaje mbona sioni alama ya risasi wala alama yoyote inayoonesha kama kanyongwa? Alibaki kujipa maswali mfululizo huku akimjengea picha muuwaji alivyoingia na kutekeleza jambo hilo. Alijenga picha ya kuhisi kuwa muuwaji alinyata, alinyata hadi kwenye kitanda alichokuwa amelala mkewe kisha akataka kumkaba. Mkewe akashtuka na kukimbilia simu, simu ile akaipiga teke. Akawahi bastola, nayo akaibeta kwa guu lake alilolipiga kiufundi zaidi kisha akamuuwa. Kamuuwaje sasa mbona sijui hata kifo alichouliwa mkewangu? alijiuliza hivyohivyo mawazoni. Akaacha hapo na kugeukia jinsi muuwaji alivyoondoka. Alipofika kwenye muuwaji kuondoka, hapo akamkumbuka mtu ambaye alitaka kumsahau, mtu huyo hakuwa mwingine bali ni Mery.



    "yuko wapi mery mbona simuoni na mara nyingi amekuwa akilala na anti yake? Au leo hajalala humu?" alijiuliza na kutoka mule ndani na kuanza kutafuta kila kona ya ile nyumba. Masaa mawili ya kutafuta yaligonga ukuta. Alimkosa tena si kumkosa tu bali hata harufu ya binti yule mdogo hakuihisi. Mtu mzima alizidiwa ujanja. Joesan kilio kikaibuka upya, hapa sasa alilia kama mtoto. Alipoteza kila kitu sasa, amemkosa mke na pia amepoteza mtoto ambaye kwake alikuwa na faida kubwa kuliko kitu kingine. Alirudi chumbani kwake kwa kasi kubwa na kwenda kuuinua mwili wa mkewe na kuuweka kitandani kisha akatoka mbio sana mule ndani hata sijui kama alikumbuka kufunga mlango. Aliingia kwenye gari na kuliondoa kwa mwendo wa kasi sana, moyoni aliumia sana bwana huyo alikuwa na maumivu makubwa mno, kila wakati alikuwa akijiuliza ni nani anayemkanyaga paka mwenye njaa mkia. Alifika kwenye kampuni akiwa na hasira sana mwili wote ulikuwa ukimchemka. Kila aliyekuwa akipishana na yeye na kumsalimia, hakuna aliyejibu salamu yake kwa jinsi ambavyo ghadhabu ziliwamba kwenye kichwa chake hata mdomo wake kushindwa kunyanyuka. Alipitiliza hadi ilipo ofisi ya Suzane na kabla hata ya salamu akatoa amri kwa binti huyo kuwa atoe taarifa kwa dokta Emmy aagize wauguzi nyumbani kwake wakauchukue mwili wa mkewe kwa ajili ya kuufanyia uchunguzi kisha akamwambia akimaliza amfuate ofisini kwake. Suzane aliondoka hapo huku akiwa hamuelewi bosi wake. Baada ya muda Suzy aliingia kwenye ofisi ya bosi wake na kutwaa nafasi.



    "nini boss kimetukia?" aliuliza Suzy.



    Joesan hakuwa na hata nguvu ya kusema alimtazama mwanamke huyo na kuigamia kwenye kiti chake akiwa ameyaelekeza macho yake pembeni, akasema kwa upole mkubwa sana.



    "kuna mtu amevamia usiku bila shaka nyumbani kwangu na kufanya mauwaji ya mke wangu na wamemteka Mery pia"

    "boss! Unamaanisha Martha ameuwawa?"

    "ndiyo Suzane na muuwaji alikuwa na sababu za kufanya mauwaji yale, inaniuma sana Suzy, naumia moyoni kuliko kawaida, Suzy nauona moyo wangu kama unataka kutoka kwa jinsi ninavyoumia. Martha ni mwanamke wa maisha yangu, Martha alikuwa akifanana na mimi kwa kila kitu. Martha alikuwa hana kizazi kama mimi, nimemfanyi vituko vingi sana yule mwanamke lakini hakujali alisimama kwenye part yake kama mwanamke" machozi yalimtoka Joesan, muuwaji naye akalia ama kwa hakika ni zamu yake. Ameondolewa mtu muhimu sana kwenye maisha yake. Yule mtu mwenye koti jeusi hakukose pale aliposema 'Joesan fill pain'

    "wamempiga risasi au wamemuuwa kwa kifo cha namana gani?" aliuliza tena Suzy. Joesan aligeuka na kumtazama vizuri Msichana huyo na kusema.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "hicho ndicho kinacho nifanya nimlete huku ili daktari Emmy aje kuufanyi uchunguzi, mke wangu ameuwawa kitaalamu sana Suzy sijui hata muuwaji ametumia kifaa gani cha mauwaji, kama muuwaji anasababu za kufanya hayo, ni wazi vita yake hawata iweza nitahakikisha nampoteza mmoja baada ya mwingine, wauwaji ninao wa kutosha sana kabla hata sijamhusisha na Chriss" alisema Joesan huku akiwa yu katika majonzi mazito sana. Suzy akawa na kazi ya kumfariji bosi wake hadi pale mwili huo ulipoletwa ndipo Suzy alitoka na kuelekea kwenye chumba cha uchunguzi. Huko alikutana na Emmy ambaye alimuomba ampishe kwanza ili afanye kazi yake kisha atawaita. Suzy alitoka na kuelekea ofisini kwake. Ofisi nzima ilipata taarifa hizo na kwenda kumpa pole boss wao na kumtaka apige moyo konde kwani huo ndiyo uwanaume. Baada ya kama lisaa moja mbele, muuguzi alikuja na kumwambia Suzane kuwa yeye na boss wanahitajika ofisini kwa dokta Emmy. Wakanyanyuka kwa haraka sana na kukimbilia kwenye ofisi ya dokta, walipofika, walikaa kwenye nafasi zao na wote wakamtazama daktari huyo wa kike ambaye alianza kwa kutoa pole kwa bosi wake kisha akasema.



    "mkeo hajafa kwa mapenzi ya Mungu bali ameuwawa na ameuwawa kitaalamu sana. katika uchunguzi tulioufanya kwa kushirikiana na wenzangu, tumegundua kwamba kifo cha mkeo kimesababishwa na sumu na sumu hiyo imetokana na kupigwa na kitu chenye ncha kali kama sindano ambayo imepenya kwenye paji la uso na kutokea kisogoni. Ni vigumu sana kugundua kama kitu hicho kimepenya hapo kutokana na udogo wa kifaa hicho pia na sumu hiyo ambayo bado hatujaigundua ni sumu gani, kuwa na sifa ya kusimamisha mfumo wa upumuaji kwa haraka sana na kugandisha damu kwa kiasi kikubwa ndiyo maana sehemu iliyopata madhara haikuweza hata kutoa damu" akanyamaza dokta Emmy, kisha akaendelea tena.

    "tumeligundua hilo la kuchomwa na kitu chenye icha kali, baada ya kumgeuza upande wa nyuma ndipo tulipogungua kuwa amepigwa na kitu hicho na bila shaka ni kitu ambacho kimepata msukumo wa kasi sana, kama kasi ya usukumaji wa risasi kutoka kwenye chemba yake. Hatukuweza kuipata hiyo sindano, naamini hivyo kuwa ni sindano maana hakuna kitu kidogo vile halafu kisiwe sindano" alihitimisha maelezo yake dokta Emmy.

    "tofauti na hilo dokta?" akauliza tena Joesan.

    "tofauti na hilo hakuna zaidi ya hilo labda cha kuongezea ni kwamba anahitaji maziko ya haraka sana kabla ya kutokea mabadiliko mengine mwilini mwake kwa sababu hatujui hiyo sumu itkuwa na madhara gani mengine." aliposema hivyo Joesan aliomba ripoti hiyo ya daktari na kuondoka nayo kisha akawatangazia wafanya kazi wote kuwa siku inayofuata ndiyo maziko ya mkewe, akatoka na kuelekea chumba cha mawasiliano huko akaomba aonane na Mr. Kim. Bwana huyo akamwambia kuwa kwa muda huo itakuwa ngumu kuonana kwani yuko nje ya mji huo wa Morogoro ila anaweza kumueleza shida yake. Joesan akamueleza kila kitu. Mr. Kim alivyopokea hizo taarifa alishtuka sana alichofanya ni kumwambia Joesan kuwa alikuwa na muda kama wa siku tatu nne hivi za kuwa nje ya mji ila kwa hilo atakatisha siku na kesho baada ya mazishi ataomba wakutane mahali. Joesan akakubali na safari ya kwenda kutafuta mahali pa kujifariji ikaanza.



    **********************************************



    Siku ya pili, siku ambayo ilikuwa ni ya kihistoria sana kwa Joesan. Siku ambayo alikuwa akimpeleka mkewe kwenye nyumba yake ya milele. Hakuna siku yenye kuumiza kama hii, siku hii ndiyo siku pekee inayokupa imani kuwa sasa utabaki mwenyewe na yule uliye mpenda na akakupenda kwa dhati ameamua kwenda kuishi maisha mengine atakayoandaliwa na mola wake kama yapo huko aendako. Siku hii pia ni siku utakayojikuta ukitaka kumuomba msamaha uliyemkosea ili akusamehe kwa sababu unaamini hakuna siku utakuja kumuona tena. Lakini ndiyo hivyo tena, hakuna nafasi ya kufanya hivyo na hata kama utapewa nafasi ya kufanya hivyo si kama ile ambayo..



    Lakini ndiyo hivyo tena, hakuna nafasi ya kufanya hivyo na hata kama utapewa nafasi ya kufanya hivyo si kama ile ambayo muhusika akiwa hai. Hii wewe ndiye utakaye kuwa muongeaji mkubwa lakini hutapata jibu lolote kutoka kwa muombwaji msamaha huo. Siku ya huzuni ya kweli, siku ya kukuonesha uthamani wa yule aliyekutoka, siku yenye kuuma na kutesa moyo na pia ni siku ambayo hutaamini kama kweli ndiyo mwanzo wa kubaki mwenyewe. Joesan akiwa ndani ya suti nyeusi tii na mawani ya giza ambayo iliyaficha macho yake yanayotoa machozi kila wakati. Tendo hilo la utokaji wa machozi lilijidhihirisha kwa bwana huyo baada ya kuitoa mawani yake mara kwa mara na kupitisha kitambaa chake machoni ikiwa ni ishara ya kupangusa machozi hayo. Pembeni yake alikuwapo Suzane ambaye naye alibeba macho yenye majonzi mazito pia hakukosekana Merina pamoja na wafanya kazi wengine wa kampuni ya SC Company. Walikuwepo watu wengi sana. Watu hao wapo waliompenda Joesan na kumuamini kutokana na utoaji wake misaada kwa taasisi mbalimbali zisizojiweza, pia miongoni mwao wapo wale ambao huwa hawakosi msibani na walipenda kuhudhuria kila msiba huku wakiwa kipaumbele kwa kila jambo. Lakini pia walikuwapo watu maalumu waliokuwa wakisubiri amri ya 'haya fukieni'. Hawa nao walikuwa ni watu maalumu ambao ndiyo wameamua kujiajiri kwa kazi hiyo ya uchimbaji na uzikaji katika shughuli mbalimbali za mazishi ya watu wenye pesa zao kama Joesan. Katikati ya kundi lile kubwa la watu waliokuwa wamehudhuria mazikoni, alikuwepo mwanadada mrefu ambaye yeye muda wote alipenda kumuangalia Chriss. Chriss hakuweza kumuona mwanadada huyo kutokana na kuficha macho yake kwenye mawani ya jua.



    "kwa hakika tunao muda mrefu sana wa kuishi duniani lakini pia tunao muda wa kufa. Tunaijali dunia sana na kuisahau siku ambayo ndiyo siku inayokwenda kubadilisha historia nzima ya maisha yako. Kwa nini hamjui kuwa, hapa ndipo mahala pa kujiuliza, umemtendea nini bwana Mungu wako, hapa ndiyo pa kujiuliza ni yapi mabaya yasiyompendeza bwana na unayafanya kwa makusudi huku ukijua kuwa ipo siku utakuwa huna ujanja. Tunatakiwa tujifunze kila siku na kila wakati kuwa ipo siku tutarejea kwake bwana mungu wetu. Mwenzetu amekwenda kwa amani......!" alikuwa akisema mchungaji ambaye ndiye aliyekuwa akiongoza mazishi hayo. Alikatishwa na kilio Cha Joesan, kilio cha uchumgu sana, kilio kilichomfanya hadi mchungaji huyo kupatwa na huzuni ya aina yake. Merina na Suzane wakamkaribia na kumpigapiga mgongoni huku wakimliwaza kwa maneno ya kishujaa. Yule mwanamke aliyekuwa akimtazana Chriss kila wakati akawa anatabasamu kwa tabasamu la mbali sana ambalo si rahisi kuligundua kirahisi. Chriss alikuwa yu katika uchungu pia japo alikuwa hajui huyo anayemfanya bosi wake kulia ndiyo yule anti yake aliyekuwa akimpenda na kumjali. Joesan alitamani kumwambia Chriss kuwa huyo anayetaka kuzikwa hapo ni yule uliyekuwa ukimuita shangazi lakini angeanza vipi hadi kueleweka, akajikuta akizidi kulia maradufu. Kwa kweli tuliumbwa kwa mavumbi na tutarudi mavumbini pia. Ulifika ule muda wa Joesan kwenda kutupa mchanga juu ya sanduku lile lililo ndani ya shimo la kaburi ikiwa ni hatua za mwisho za kumzika Martha. Joesan aliukama mchanga kwa nguvu sana na kukunja ngumi kwa ghadhabu kubwa hadi mchungaji akaogopa kisha akaongea moyoni.



    "nenda kwa amani mke wangu ila naapa kuwa sitamuacha hai aliyesababisha haya kisha akatia mchanga ndani ya shimo lile na kugeuka kisha akaondoka mazima huku nyuma akiacha watu wakiendelea na shughuli za umaliziaji.



    Watu wakaanza kutawanyika mmoja mmoja. Chriss yeye alikuwa akiondoka taratibu eneo hilo na kuelekea mahali lilipo gari lake, akapanda na kutaka kuondoka. Mara pikipiki kubwa XLR, likapiga breaki kwenye upande ule alioko yeye kisha mtu aliyeko juu ya pikipiki hilo akafunua kofia lile la kijikinga na kuionesha sura yake kisha akatabasamu na kuliruhusu pikipiki hilo kuondoka kwa mwendo wa kasi mahali hapo. Chriss alibaki mdomo wazi. Sura ya mwanamke huyo hakuijua hata kidogo na hakuwahi kuiona mahali popote pale. Hakujiuliza sana ila kitu kilichomshangaza ni kwanini msichana huyo alitabasamu maeneo kama yale ya kuhuzunisha. Aliondika hapo kwa kasi pia huku akiangalia kama anaweza kujua uelekeo ambao msichana huyo ameuchukua lakini hakuuona ikabidi aachane nae. Akachukua uelekeo wa nyumbani kwake.



    Siku huyo hakukuwa na mtu aliyeingia kazini kila mtu alikuwa katika hali ya kimsiba msiba ni wafanya kazi wachache sana ndiyo walikwenda kazini mara baada ya kutoka msibani. Mzee Rafael yeye baada ya kutoka msibani, aliamua nusu siku hiyo akaimalizie nyumbani kwani hakuwa na kazi sana ofisini siku hiyo. Alikuwa ametulia Sebuleni kwake akiwa na tafakuli nyingi sana ubongoni mwake, aliukumbuka usiku wa siku ya tatu iliyopita. alikumbuka jinsi umeme ulivyokatika kiajabu ajabu na kamera zote za kampuni kuzima.



    "ni kweli lile lilikuwa ni tatizo la kawida la hitilafu ya umeme? Hapana hili jambo siliafiki hata kidogo. Mbona kwenye ofisi yangu nilikuta alama za viatu?" alizidi kujiuliza mzee huyo.



    "ninafanya jambo la maana sana kila ninapotoka ofisini kwangu kuiacha sakafu ikiwa na vumbi na sitaki ifanyiwe usafi hadi mwenyewe nifike kwanza. Kuna mtaalamu wa kazi ameingia humu kwenye kampuni na si bure kuna jambo alilifuata, hii inaweza kuwa hatari sana. Naweza kumwambia Boss hili swala, lakini hapana, hebu ngoja kwanza nilifikirie kwanza hili jambo, sitakiwi kukurupuka kusema lakini lile tukio halikuwa la kawaida na mtu aliyeingia humu ndani ndiye aliyetekeleza mauwaji ya mke wa boss na kama ni kweli basi ujue kazi imeanza" alizidi kuwaza mzee huyo hadi akapitiwa na usingizi hapo hapo sebuleni hadi alipokuja kushtuka muda ulikuwa umekwenda sana. Alijinyanyua na kuelekea kwenye chumba chake cha mazoezi hapo nyumbani kwake na kunyoosha mwili kidogo kabla ya kuingia jikoni na kujiandalia chakula. Hakuwa na mke mzee huyo, tangia mkewe alipopoteza maisha hakuhitaji tena kuoa japo watoto wake walimsihi sana kufanya hivyo lakini aligoma kwani maisha yake anayoishi ndiyo yaliyosababisha kifo cha mama yao, hivyo kuoa tena ni sawa na kuzidi kuleta matatizo kwenye familia yake. Akaona ni bora abaki mwenyewe kama ni kufa aje afe akiwa mwenyewe pia.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "pole sana kijana wangu kwa msiba mzito ulioupata." alitoa pole Mr. Kim mara baada ya Joesan kufika kwenye moja ya majumba yake ya siri.

    "nimesha poa mkuu ila nimeumia sana kwa pigo hili ni jambo lililokuja ghafla sana"

    "najua umeumia sana lakini ndiyo kanuni za maisha, maisha unayoishi yana kanuni zake na hiyo ni moja ya kanuni za maisha unayoishi. Ukumbuke kuna watu umewaumiza sana hadi hapo, sasa huo ni uchungu wa maumivu ya watu waliowahi kuumizwa na wewe"

    alisema Kim kwa utaratibu sana.

    "daah! Sijategemea kama nitakuja kuumia kama nilivyoumizwa na hiki kifo si.......!"

    "pole sana, hebu nipe hiyo ripoti ya uchunguzi wa dokta, Joesan" alikatishwa Joesan kwa kuombwa karatasi iliyobeba ripoti ya uchunguzi. Akampa mzee huyo. Kim akaipitia kisha akashtuka zaidi na zaidi kila alippkuwa akiisoma ripoti hiyo ya uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa Martha. Alishusha pumzi nzito na kuuangusha mgongo wake kwenye kiti na kutazama juu ya paa kabla ya kuunguruma kama dume la njiwa. Akageuka kwa upole sana akimtazama Joe aliyeweka utulivu wa hali ya juu. Bwana kim akajikohoza na kufinya macho yake madogo kabla ya kuunguruma tena, akasema.



    "huyu ni D.A"

    "nani!?" akauliza Joesan akiwa kama hajasikia vizuri. Mzee huyo akamtazama machoni na kumuangalia kwa muda mrefu kama anayemuuliza kwa macho kuwa kweli hujasikia au unaleta mchezo wa kuigiza. Au ni kweli hujaelewa. Lakini akarudia tena.



    "huyu ni D.A, anajiita jina hili likiwa na maana ya DEATH ADDERS. Huyu ni nyoka hatari sana, Joesan. Na amejiita hivi kwa sababu ni miongoni mwa nyoka hatari sana aliokuwa akiwapenda. Nilishawahi kuishi naye tempo moja huyu mzee huko nchini China na baada ya kumaliza mafunzo yetu ya awali tukahamia kwenye tempo jingine tofauti na lile la mwanzo. La mwanzo lilikuwa ni tempo la Budha. Tulijifunza imani za kibudha na mimi na yeye ndiyo tulikuwa ni watu wenye uwezo mkubwa sana kuliko wanafunzi wote. Tulipofuzu ndipo mimi nikaamua kuongeza ujuzi kwa kwenda kujifunza kwenye Tempo jingine hili lilikuwa la Mashaolin au Buda. Cha ajabu nilimkuta huko na akawa yeye ndiyo anauwezo mkubwa kuliko mimi. Kitendo hicho kilinikera sana, kwanini anipite wakati mwanzo tulikuwa ni watu wenye uwezo sawa. (hapo alificha kidogo lakini alitaka kusema, kwa nini apitwe na mtu mweusi wakati mapigano ni ya watu weupe tena kutoka huko China na Korea). Akazidi kuongea.

    "kila nilipojaribu kumfukuza, nilijikuta nikifeli. Lakini siku kata tamaa, nikaongeza juhudi hadi nikafanikiwa kuufikia uwezo wake. lakini hapo mimi na yeye tukawa hatupendani hata kidogo. Siku moja walimu wetu wakaweka shindano la kupambana. Tulijipanga wanafunzi wote, pambano likaanza kwa utangulizi wa wanafunzi wadogo kisha tukapangwa sisi mahasimu. Lilikuwa ni pambano gumu sana sitaki kudanganya na tulipambana kwa muda mrefu kwa kutumia silaha mbalimbali lakini alikuja kunishinda mwishoni kwenye mapigano ya bila kutumia silaha, alinipiga na kuniangusha vibaya sana hadi nikakubali kushindwa. Wanafunzi wote pamoja na walimu walimsifia sana, jambo hilo likazidi kunikera zaidi na kuweka chuki moyoni mwangu dhidi yake. Siku moja nyingine, tukapata tuwa ya kwenda Australia kama wanafunzi. Huko ndiko mimi na bwana huyo tulizidi kuchukiana mimi nilipenda vitu vyangu na yeye alipenda vyake huku akiwa na wafuasi wengi sana kuliko mimi. Tukaenda kutembelea kwenye pori lenye nyoka wakali na wanaosifika kuwa na sumu kali. yeye akatokea sana kumpenda huyo nyoka mwenuye meno makali na membamba sana anayekwenda kwa jina hilo la Death Adders. Huyo ni nyoka hatari sana na sumu yake ni hatari kupindukia. Tuliporudi kambini, mimi nikatengeneza silaha ambayo kama unakumbuka nilisema silaha hiyo imetengenezwa inchi Urusi lakini si kweli. Silaha hiyo niliitengeneza mimi kwa mikono yangu. Silaha hiyo ni ...............................





    Silaha hiyo niliitengeneza mimi kwa mikono yangu. Silaha hiyo ni bastola fupi na risasi zake ndio hizo zenye alama ya nyota ambazo nimezipa jina la Star Bullet. Hapo nikafarijika na kuamini ipo siku nitkuja kumuangamiza. Lakini D.A alikuwa kama shetani aisee, haikuwa vile nilivyofikiria, nilijidanganya. Kwa sababu na yeye alikuwa ni mtaalamu, akatengeneza silaha ya kwake ambayo nayo ilikuwa ni bastola lakini hiyo ilikuwa ndefu. yeye ya kwake ilikuwa ikitumia risasi nyembamba sana mfano wa meno ya huyo nyoka na kuziita Snake Pin Bullet (SPB) ambazo alizipika kwa mchanganyiko wa sumu kali ambazo sijui ni sumu gani na sumu gani. Hakutaka kusema mchanganyiko huo wa hizo sumu ni upi na upi lakini ukimuuliza sumu iliyopo kwenye risasi hizo, anasema ni sumu aina ya NEUROTOXINC. Kijana wangu hiyo si sumu ya mchezo ni sumu hatari mno ambayo inakuuwa kwa sekunde chache tu, inasifa ya kushambulia sana mfumo wa upumuaji na kuupa mshtuko moyo kwa ghafla sana. Nilipanga kumfanyia ubaya kwa sababu hakuwa mwema kwangu. Nilichelewa kwani alinishtaki kwenye uongozi wa kile chuo na mimi kufukuzwa kutokana na utengenezaji wa silaha hatari kinyume na imani za Mabuda. Nikaapa kulipa kwa kumtia hasara kisha kumuuwa taratibu. Nikapata habari kuwa amerudi kwao Tanzania na ameoa na anamtoto mmoja wa kiume. Nikapanga kuja Tanzania ili kumuangamiza niishi kwa amani, maana kuwepo hai mtu huyo kwangu niliona ni kama kulala ndani ya nyumba yako mwenyewe huku nje watu wakiwa wanilipua kwa moto. Kweli nikapanga safari na kuja huku kwa lengo la kuwekeza lakini ndani yake nilikuwa na kitu kingine. Na baada ya kumuuwa rafiki yako na kukuachia huyu kijana Chriss, nikasubiri ipite miaka mingine mingi ndipo nianze kumpa maumivu huyo mzee. Baada ya miaka kumi kupita huku tukiwa tumejiimaarisha angalau, ndipo nikakutuma umuuwe yule kijana ambaye binti yake ndiyo yule uliyekuwa ukiishi nae. Yule kijana alikuwa ni mtoto wa D.A. Yeye baada ya kuona ni mimi niliyesababisha mauwaji ya kijana wake, akakimbia kabisa hii nchi na sikuwahi kusikia habari zake tena hadi hii leo ambapo amekuja kumchukua mjukuu wake. Amejidhihirisha kwa silaha aliyoitumia pia amejidhihirisha kwa kuondoka na binti yake. Huu ni wakati wa kumtumia Chriss sasa kwani hata yeye anaonekana ana mpiganaji hatari na ndiye aliyekuja kutekeleza hayo mauwaji." historia hiyo ilimfanya Joesan kushusha pumzi nzito sana. Ilikuwa ni historia ya kusimumua sana na iliusisimua sana moyo wa bwana huyo. Kumbe kufanya mauwaji ya yule kijana alidhani anapora mali na kuongeza utajiri, kumbe ndani yake kulikuwa na kisasi. Alichoka aisee lakini alijipa imani kuwa ni bora amejua na kujua huko kutamfanya awe makini zaidi kuliko wakati akiwa hajui.



    "kile kikao" aliendelea mr. Kim.

    "kile kikao cha siri tulichokaa siku ile usiku, tulikuwa tuna mjadili huyu mzee na ndiye niliyetaka kumtuma Sex Machine akanitafutie huyo mzee popote duniani lakini niliona ingekuwa ni kazi kubwa sana kutokana sijui ni wapi amejificha. Sasa kwa hili tukio alilolifanya ni wazi ameanza kujitokeza kutoka mafichoni, acha aje itakuwa rahisi sisi kumnasa kuliko kama ningemtafuta mimi." aliongea Mr. Kim na kumalizia.

    "Sex machine ataanza kazi ya kufanya mapenzi kwa kuwaingilia wanaume kinyume na maumbile (mashoga). Akishamaliza hilo, sasa tunampeleka moja kwa moja kwenye hii vita aliyoinunua huyo mpuuzi D.A." alipo maliza kusema hivyo Kim, alipeana mkono na Joesan kisha akamwambia awe kawaida tu na ayachukulie maumivu ni sehemu ya maisha.



    SAA 22:08 USIKU.



    Maeneo fulani boma Road. Ndani ya jingo la orofa moja, ndani ya chumba kimoja. Muziki mwanana wa kitanzania ulikuwa ukimpa burudani binti mmoja mrembo, mwenye rangi ya chungwa. akiwa amevaa mavazi ya mazoea yaani mavazi penzi ya moyo wake. Alikuwa amevaa bikini nyekundu, juu akiwa amepiga kishati cha kibuluu ambacho alikuwa amefunga kifungo kimoja tu cha katikati na kuacha tumbo lake dogo wazi na sehemu kubwa ya matiti yake ikionekana. Mbele ya meza yake ya kioo iliyokuwa imebeba miguu yake mizuri minene ya kuvutia, miguu isiyojua shuruba kwa mtazamo, miguu ambayo inapendeza kuipapasa na kuishikashika. Pembeni ya hiyo miguu kulikuwa na Chupa kubwa ya mvinyo ambayo alishamimina kiasi fulani kwenye birauli. Alikuwa busy na kuangalia picha kwenye kompyuta yake mpakato aliyokuwa ameiweka mapajani. Kila picha alikuwa akiitazama kwa namna yake. Nyengine zilimfanya akunje sura nyingine zilimfanya atabasamu na nyingine zikamfanya asikitike. Mwisho aliruhusu video ya ngono akawa anaingalia huku machozi yakiwa yanamtoka. Hakuendelea sana kuitazama video hiyo, aliamua kuiweka kompyuta yake pembeni na kuizima kabisa. kisha akajilaza pale sofani na kutafakari hili na lile kabla ya kukaa vizuri na kuugida ule mvinyo wote ulioko kwenye birauli kisha akajinyanyua na kuaza kunengua. Umbo lake halisi likaonekana vizuri. Alikuwa na hipsi zilizotawanyika na kuufanya mlima mdogo wa makalio kusimama vizuri. mbele palijaa sana tukiachana na makalio mazuri.makubwa ya kuvutia na yanayopendeza kuyashika, pia alikuwa na paja za nguvu zilizo nona. Hakika alikuwa ni mrembo wa nguvu sana binti huyo. Alikuwa akicheza kwa maringo sana na alionekana kuujulia muziki wa kitazania. Alicheza sana na kumwagika jasho kabisa, alicheza kwa hisia mno. Bila shaka ilikuwa ni katika kupunguza wingi wa mawazo aliyokuwa nayo.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ushahidi wa kukupata ninao Sex machine." alisema maneno hayo tu na kuachana na

    kucheza kisha akaingia zake bafuni na kwenda kuchezea maji. Bado alama za viatu alizozikuta Rafael ofisini kwake, zilizidi kumpa mawazo sana. Hakutaka kuamini kabisa kuwa aliye kuja kuvamia usiku alikuwa ni mwema kwake au kwa kampuni lakini kila akitaka kuliweka wazi jambo lile moyo wake ulisita. Kitu kimoja kilichomfurahisha ni kwamba alikumbuka kuwa ndani ya ofisi yake hakukuwa na jambo lolote lililofanywa na mvamizi huyo pia hakukuwa na kitu kilichopotea. Hicho ndicho kilicho mfanya awe na imani kuwa mvamizi huyo wa usiku alikuwa na jambo la hatari kwa kampuni na lenye faida kwake.



    Mishe mishe zilikuwa nyingi sana katika kampuni hiyo, kila mfanyakazi alirudi kwenye nafasi yake na kuendelea na majukumu kama kawaida. Ofisi zote zilikuwa wazi hata ya Chriss pia ilikuwa wazi na kwa muda huo wa asubuhi, alikuwa akiminyaminya kicharazio cha kompyuta yake akifanya hiki na kile alimradi ni katika kuifurahisha nafsi yake. Joesan yeye alikuwa ni mtu mwenye mawazo mengi sana, hakuwa sawa kabisa, japo aliambiwa apige moyo konde na kupisha yaliyopita yapite, bado hakuonekana kuamini kama kweli yu peke yake kifamilia. Machozi yalitaka kumuanza kumtoka lakini roho ya kiume ikaziba nafasi na kuyafinya machozi yote yaliyokuwa yakiukaribia mlango wa kope zake za macho.



    "kama ni kweli haya yaliyotokea, basi ni wakati wa kuwa macho na huu ni wakati muafaka wa kuliinua jeshi langu. Vijana wangu ni lazima wawe imara zaidi na sitakiwi kuwa nao mbali" aliwaza Joesan.



    Ama kwa hakika waweza kufanya ubaya lakini usiwe na moyo mgumu wa kukabiliana na ubaya huo pindi tu ubaya utakapo pinduka na kukugeukia. Pigo moja la kuuwawa kwa mkewe, Joesan tayari alikuwa ni mwingi wa hofu sana. Aliona kuwa huo ndiyo wakati wa pekee kuhakikisha kuwa anafanya maandalizi ya kuweza kukabiliana na hao waliomuonesha kuwa hata wao wanaweza kumuweka roho juu. Alikuwa amesahau semi za wahenga kuwa 'unapozika wana wa wenzako, ukubali nawe siku moja kuja kuzikiwa wa kwako. Joesan aliona raha kuwajaza watu uchungu kwa kuwapoteza watu wawapendao akiamini yeye si wa kukutwa na uchungu huo. Hakujua kuwa mtenda naye hutendwa, alaye nyama ya mwenzake naye huliwa ya kwake, kama hakujua haya yote basi anatakiwa afahamu na ajipange.



    "nitahakikisha hakuna mtu anabaki hai, hata kama awe na nguvu kiasi gani lakini hapa wamechokoza sipo. Nituwaaaa nasemaaa!!" alikuwa akiongea kwa sauti ya chini hatimaye akaamua kupiga kelele kabisa kwa hasira alizokuwa nazo. Alijizunguusha pale kitini huku na huku kisha akakizunguusha na kumgeuza nyuma ambako alisimama na kukiacha kile kiti na kwenda hadi dirishani hapo akawa anaushangaa mji huo wa Morogoro kwa mapana zaidi. Aliwaza mengi hapo dirishani, tangu anauona mji huo wa Morogoro, hadi kupoteza kabisa taswira yake na kutokujua anaangalia nini, alikuwa ameduwaa tu na kama angetokea mtu wa kumshitua mahali hapo, basi angetoka na hicho kioo hadi chini. Mawazo yake yalikuwa mbali sana. Alipiga kite cha uchovu na kujitoa pale dirishani ambako hakujua alikuwa akitazama nini kisha akakamata simu yake na kuiweka sikioni baada ya kuwa ameingiza namba kadhaa kwenye simu hiyo na kubonyeza kitufe cha kupigia. Simu ikaita kwa muda mfupi na hatimae ikapokelewa.



    "bwana mkubwa" ilisema sauti ya upande wa pili namna hiyo.

    "Mpe taarifa Mandi, Sembugi, nawahitaji leo usiku na tukutane kwenye baa ndogo ya mafichoni kule Mriti mida ya saa tatu usiku leo."

    "sawa bwana mkubwa, hazita zidi hata sekunde tano tutakuwa tumekwishafika mahali hapo" akajibu mtu huyo ambaye alikuwa ni Sembugi. Joesan akamwambia powa na asikawie ni muhimu sana kisha akakata simu na kuiweka mfukoni halafu akatoka humo ofisini kwake hadi nje akataka kuelekea kwenye ofisi nyingine lakini akasita na kurudi tena ofini kwake. Alikuwa mithili ya mtu aliyechanganyikiwa sana. Alipofika mule ofisini, alichukua simu ya ofisi na kubofya namba mbili tatu na kuiweka sikioni.



    "Suzane, naomba uje na merina ofini kwangu muda huu" alitoa amri kisha akairudisha ile simu kwenye kikalio chake na kuigamia kwenye kiti chake. Dakika moja baadae, mlango wa ofisi hiyo ukafunguliwa na mabinti wawili wakaingia na kutafuta nafasi. Joesan alitulia .................



    Joesan alitulia kimya akiwa hawatazami ni kama hakuwaona mabinti hao. Sekunde kadhaa zikapita ndipo bwana huyo akasema.



    "Merina!" aliita kisha akaendelea.

    "nadhani unakumbuka nilikuuliza kama unakitu cha ziada ukaniambia kuwa unacho," akaweka koma na kumtazama Merina kama anayetaka kusikia kitu kutoka kwake na kuendelea.

    "ni muda wa kujua ni kitu gani kipo mwilini mwako. Nahitaji kuwa na timu imara na madhubuti na timu hiyo ninayoitegemea ni nyinyi mjue....., Suzane?!" akasema hayo kisha akaita jina hilo na huyo aliyeitwa akatikisa kichwa kuitika.

    "nataka tuongozane hadi kwenye uwanja wa mazoezi amabao unatumiwa na mzee Rafael ili nikajue ni kitu gani kipo mwilini mwa Merina kisha nitawaambia kwa nini ninataka iwe hivyo" alisema Joesan na kunyanyuka mahali hapo kisha kutoka pamoja humo ofisini. walielekea hadi ulipo uwanja huo wa mafunzo ambako walimkuta Rafael akiendelea na kazi ya kuwafua vijana. Mzee huyo alipomuona Joesan mahali hapo alisitisha alichokuwa akikifanya na kumgeukia Joesan.



    "boss nini tena mbona huku muda huu?" aliuliza mzee huyo ambaye ni mzee mpole sana asiye na papara katika mambo yake.

    "Rafael!" aliita Joesan kwa dharau kubwa kana kwamba anayemuita hapo ni mtu anayelingana nae ki umri. Akasema.

    "nataka unitafutie kijana unayemuamini katika mapambano na uniletee hapa mbele" maneno hayo yakamfanya Rafael kushtuka.

    "mtu ninayemuamini? anataka kumfanya nini huyu katili? Mbona sielewi?" alizidi kujiuliza mzee Rafael lakini hakuwa na jinsi mahali hapo zaidi ya kumtoa kijana huyo aliyeambiwa amtoe. Kijana akaitwa na kusogea hapo mbele na kusimama kwa heshima kubwa.

    "ndiyo huyu?" aliuliza Joesan kana kwmba hamuamini huyo aliyeletwa mahali yapo.

    "ndiyo boss, huyo ndiye kijana ninayemuamini sana" alijibu Rafael. Joesan akamsogelea kijana huyo na kumzunguuka zunguuka kisha akasimama mbele ya kijana huyo na kusema.

    "Merina huyu kijana ni mzuri katika nyanja za mapigano kama ulivyo msikia mwalimu wake alivyosema hivyo nataka nione uwezo wako leo hii mahali hapa, hebu pambana na huyu mtu tuone" alisema Joesan, Merina na yule kijana wakasimama tayari kabisa kuanza mapambano. Kila mmoja alikuwa kakaa mkao wa kupambana kweli, hakuna aliyeonesha tabasamu eneo hilo. Kijana yule akaja na mapigo ya karate lakini binti huyo akayatoka kwa utaalamu mkubwa sana. Alipotaka kumvamia kijana huyo, Joesan akasimamisha hilo pambano na kusema.



    "nilisahau kitu kimoja kukisema kwenu kama sheria ya hilo pambano, kila mmoja hapo ajue kuwa anatakiwa kuuwa yaani sitaki kuona wote mnatoka hapo mkiwa wazima bila mmoja kufa. Maneno yale yalimfanya kila mtu pale kuogopa si kwa wapiganaji pekee bali hata Suzane na mzee Rafael walishtuka.

    " wanatakiwa kuuwana? shit!" aliwaza mzee huyo akiwa anasikitika sana juu ya maneno hayo na hakujua kwanini bosi wake huyo ameamua kusema maneno hayo. Suzane alimtazama Merina na kumsikitikia sana, alijua hapo hawezi kuchomoka akiwa hai hata kidogo, ni lazima atalostishwa mahali hapo. Na kila akimuangalia kijana ambaye alikuwa akipambana nae, hofu ya moyo wa Suzane, ilizidi kuongezeka hatua kwa hatua. Maana kijana huyo alikuwa na mwili uliokubali mazoezi, hakuwa na sura ya kuonesha mzaha mahali hapo hata kidogo. Mpambano ulikuwa umesha ruhusiwa, kila mpambanaji alikuwa na muda mdogo tu wa kumsoma mwenzake na kujua atashinda kwa namna gani. Walizunguukana kama majogoo huku kila mmoja akiwa makini kumkabili mwenzake. Merina alikuwa kama si mtu wa kutaka kupambana kwa jinsi alivyokuwa amesimama na hakuwa pia amesimama katika tension yoyote ile. Yule kijana muda wote alikuwa akitabasamu na kumtisha binti huyo ambaye alikuwa hatishiki hata kidogo. Kijana huyo akaja kwa pigo kali la judo na kumshambulia Merina, Merina alirudi nyuma huku akikabiliana na mapigo ya mtu huyo kisha akayumba kidogo na kuikwepa ngumi iliyopigwa kitaalamu kabisa ambayo ilikuwa ikienda kuiharibu kabisa sura yake ya urembo. Alirudi juu kwa kunesa huku mashambulizi kwa upande wake yakiwa yanaendelea kwa kasi ya ajabu lakini ghafla ukelele wa uchungu na maumivu ulisijika hapo huku kijana huyo akionekana kushika mbavu zake baada ya msichana huyo kupiga pigo baya sana maeneo hayo. Pigo hilo lilimuweka Rafael katika mshangao mkubwa, lilikuwa ni pigo baya sana ambalo kitaalamu Rafael alijua kuwa mbavu changa za mwanafunzi wake hazikuwa salama. Uwanaume ndiwo uliyomfanya azidi kuoneshs ari ya kupambana lakini ki uhalisia kijana huyo alikuwa si wa kuendelea kupambana kabisa. Pigo lile lilikwenda kuharibu mbavu zake changa kwa kuzivunja vibaya sana. Alikuja kijana huyo huku akiwa ameinama upande mmoja, Merina alibadili mtindo wake wa kusimama na kumsubiri kijana huyo ambaye kwa namana yoyote ile alikuwa yu katika hali mbaya. Na laiti kama ingelikuwa ni majaribio ya kawaida ambayo hakutakiwa kufa mtu basi kijana huyo angenyanyua mikono juu kuonesha kuwa ameshindwa pambano hilo. Lakini hapo alikuwa ni lazima apambane hadi mwisho na ashindwe akiwa ni marehemu tayari. Alirusha makonde mawili huku akiwa anapiga kelele za hasira, makonde hayo hayakuwa na lengo, yalipiga hewa na kisha kupishwa kidogo akawa anakuja mzima mzima. Binti huyo aligeuka kwa kasi ya ajabu na kupiga pigo baya nyuma ya shingo la kijana huyo, hakuridhika hivyo bali aliruka juu Merina kwa mtindo wa ajabu sana na kukamata kchwa cha kijana huyo na kuzunguka nacho hadi kikatoa sauti ya mvunjiko mithili ya mti mkavu. Alipohakikisha amevunja shingo la kijana huyo, alirudi naye chini na kumpinda kwa nyuma kisha akapiga kweye koo la kijana huyo kwa nguvu sana akiwa amekiweka kijanja chake cha mkono mithili ya upanga kisha kumuacha akidondoka chini akiwa hana uhai tayari. Alimgeukia Joesan binti huyo na kumwambia kuwa kazi aliyompa amekwisha ikamilisha. Sura ya Merina haikuwa ile iliyokuwa ikitoa tabasamu kila wakati, hiyo ilikuwa ni sura nyingine kabisa, sura ambayo ilikuwa ni yenye kuhitaji mauwaji zaidi ya hayo aliyoyafanya hapo. Joesan kabla hajatoa jibu lolote, simu yake ya mkononi ikaita. Akaipokea na kuiweka sikioni.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "ongeza vijana wawili ili huyo binti auwe tena. Hapo sura yake na roho yake inahitaji zaidi ya mauwaji hivyo anaweza kuuwa wakati wowote, hebu fanya nilivyokuelekeza kwanza na haraka mno" sauti hiyo ikakoma. Ilikuwa ni namba ngeni japo sauti aliielewa. Akamtazama Merina, Merina alikuwa ameelekeza sura yake pembeni na alikuwa akitweta sana mithili ya kiumbe hatari anayejizuia kufanya ubaya. Joesan akamgeukia mwalimu Rafael na

    kumwambia kuwa aongeze vijana wengine wawili mahili. Vijana bila kupinga wakaongezwa na walikuja kwa kasi sana huku wakiwa na mori wa kupambana lakini walichokutana nacho hata muda wa kuhadithi hawakuupata. kilikuwa ni kichapo cha sekunde kama kumi na mbili tu kilichotukia mahali hapo. Suzane akabaki mdomo wazi. Hakutegemea kumuona Merina katika uhatari kiasi hicho. Alianza kumuogopa binti huyo, lilikuwa ni shambulio lililokwenda kuwaharibu mazima wale vijana walioongezwa. Merina aliruka juu na kubingilia hewani kisha akarudi chini ghafla akiwaacha maadui zake wakiwa hawelewi hata washambule namna gani. Mwanamke huyo alizunguka pale chini akiwa amesimama na kuleta muonekano wa kushangaza. Ghafla alijirusha kwa wale vijana na kutupa kucha zilizowararuwa wote na kuwauwa kwa kifo cha aina yake. Dada huyo ndipo alipoamka na kutabasamu akiwa amejaa damu mikononi mwake. Suzane na umafia wote hapo alijiona ni mtoto mdogo sana na hawezi hata kujaribu kugusa huo moto. Walitoka hapo hadi ofisini, huko akaawambia kuwa anahitaji kupumzika hivyo kila mmoja aelekee kwenye wajibu wake. Merina na Suzane wakaondoka hapo.



    "shost kumbe muda wote tuko wote hapa, hata huniambii kama unautaalamu mkubwa kiasi hicho?" alisema Suzy huku wakiwa wanatembea kwa mwendo wa haraka wakielekea mahali pao pa kazi maana Merina na Suzy walikuwa wapo ofisi moja.

    "kawaida tu shost na nilitakiwa kuwa kimya hivyohivyo sema sikuwa na uwezo wa kumpinga boss kwani sina sauti juu yake na nimeambiwa hivyo kuwa yeye ndiye atakuwa mwenye sauti ya mwisho kwangu" aliongea hivyo Merina huku akiwa anaosha mikono yake kwa maji na dawa fulani ya kuondoa uchafu wa kila aina kisha wakafungua mlango wa ofisi yao na kukaa kwenye viti kila mmoja. Suzy hakuwa na jingine la kusema, alijua labda mtu huyo atakuwa chini yake kiutendaji na hivyo ndivyo alivyoambiwa na Joesan lakini kwa kauli ya binti huyo kwa uchechefu tu inaonekana yuko juu zaidi yake na ameletwa ndani ya hii kampuni kwa kazi maalumu. Kazi ambayo oda yake imetoka kwa mkuu bila shaka maana hata boss wao mwenyewe hajui hilo.



    Kwa upande wa Joesan baada ya wale mabinti kutoka akapokea simu kupitia namba yake ya simu ya mkononi kama awali

    Akairuhusu na kuisikiliza, sauti ilikuwa ni ya mkuu, kitu kilichomshangaza Joesan ni kitendo cha mkuu kumpigia moja kwa moja kwenye simu yake ya mkononi na ikiwa hajawahi kumpa namba yake.



    "kijana wangu." ndivyo alivyoanza mazungumzo mkuu. Akaendelea.

    "binaadamu tunatakiwa kuishi kwa maandalizi ya baadae kwani hatujaumbwa tukakamilika, hivyo hupaswi kujiamini moja kwa moja hasa unapojua kuwa kwenye mafanikio yako, nyuma kuna lundo la maadui wasiyopenda mafanikio hayo. Nilijua kuwa itafika siku kama hii ya kuhitaji msaada, nilijua kuwa itafika siku kama hii ya kujiimarisha na wale wanaotaka kukunyima uhuru lakini pia nilijuwa pia utafika muda na siku kama hii ya kutakiwa kuitumia au kuyatumia maandalizi tuliokwisha kuyandaa kabla." akakohoa kidogo na kushusha pumzi.kiasi na kuendelea kusema.

    " huyo niliyekupa ni mtu atakayecheza pati nyingi sana kwako, kwanza ndiye atakayekuwa tulizo lako, namaanisha kuwa ndiye atakayekupa raha zote alizokuwa anakupa mkeo hadi  hadi zile ambazo mkeo alikuwa hakupi.................. ...........



    Pili, huyo ndiye atakayekuwa mlinzi wako wa karibu sana, hatatoka hata hatua kumi na tano kuanzia sasa hadi pale utakapomuambia wewe. Kwa sasa anasubiri kauli yako ili atekeleze hayo yote niliyokuambia. Merina ni wako kuanzia sasa kama unataka iwe hivyo na ni mlinzi wako pia." akamaliza mkuu na kukata simu hiyo. Joesan akabaki kapigwa na bumbuwazi kabisa asijue imekuwaje.



    "aisee mkuu ni mtu hatari sana, sikutegemea kama siku ile kunipa huyu mtoto wa kike aniburudishe, alikuwa yuko katika mpango wa kuniandalia kifaa cha kunilinda" aliwaza Joesan kisha akacheka kwa cheko dogo hadi kubwa na kucheka zaidi.

    "I'm Joesan!, I'm Joesannnnnnn!!!" alipiga kelele mahali hapo na sauti yake ikajaa mule chumbani na kujirudia rudia na kutengeza mwangwi mule ndani. Akachukua mkonga wa simu kisha kumpigia Suzy na kumwambia kuwa amwambie Merina afike kwenye ofisi yake muda huo. Kabla hata ya kuiweka ile simu chini, Merina alifika hapo na kusimama karibu kabisa na bwana huyo. Joesan akamwambia Merina akae, binti huyo akaketi na kumuangalia bosi wake usoni.



    "huu ndiyo ule muda wa kukaa kwenye nafasi yako sawa" alisema Joesan.

    "sawa boss lakini ukumbuke kuwa mimi na wewe tulishashiriki mapenzi, sasa sijajua ni nafasi zote ambazo natakiwa kukaa au moja?" aliongea Merina maneno ambayo mwisho yaliacha swali. Joesan akamtazama biti huyo ambaye alikuwa mrembo kweli kweli kisha akasema.

    "unatakiwa kunilinda muda wote hivyo na usiku pia ni muhimu sasa huoni kama unatakiwa kukava nafasi zote?"

    "hakuna shida boss nilitaka kuuliza tu maana ni wajibu wangu kuuliza kile nisichokijua ili nikijue" alisema Merina, Joe akatabasamu kwa faraja ya kupata mrithi wa mkewe tena mapema kupita kiasi hapo ndipo utakapojua kuwa utu wa Joe ni sawa na makalio ya Sokwe. anayaona yake yanathamani kuliko ayaonayo, kusahau kwa muda mfupi sana machungu.

    "badili mavazi kuanzia sasa, nenda kwenye chumba cha mavazi na ukija hapa uwe umebadilika na kuwa na muonekano sawa na mumeo sawa"

    "ok, sawa" Merina alijibu na kutabasamu kisha kunyanyuka na kuelekea huko alikoambiwa aende.



    "hali kwa sasa haiko shwari, kaeni tayari mtakapoiona simu yangu mjue ni kazi, Sembugi najua kuwa unajua kazi zetu ni kuuwa hivyo kuweni tayari kuanzia sasa kuna kuku wanataka kulala na Mwewe kitanda kimoja" alisema Joesan alipokuwa amekutana na vijana wake ndani ya mriti bar. Hakukuwa na maongezi mengine baada tu ya mazungumzo hayo kila mmoja akajua lake. Ni kama walikuwa hawajuani. Joesan alikuwa ni mtu wa kutabasamu muda wowote akiamini ufalme wa dunia na mbingu ni wake kwa jinsi anavyoabudiwa na kila aliye chini yake. Akaungurumisha injini ya gari na kutitia gizani.



    %%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%



    Asubuhi ya siku ya juma mosi ilikuwa tulivu sana, Merina alikuwa yupo katika vazi safi la suti. Alipendeza sana ndani ya vazi hilo, kila mmoja alikuwa akimtazama siku hiyo na alikuwa haamimini kama ipo siku wangekuja kumkuta Merina akiwa katika vazi hilo. Muda wote Merina alikuwa ni mtu wa kuvaa vijisketi vifupi vilivyoyaacha mapaja yake wazi

    Dokta Emmy na wafanyakazi wengine kama Suzy, walimchukulia kama Malaya fulani tu ndani ya kampuni hiyo na ukizingatia pia alitoka kwenye jumba la huduma za kuwahudumia wanaume kimwili, ndiyo kabisaa walimchukulia hivyo. Siku hiyo hiyo, wanaambiwa kuwa mwanadada huyo si wa kumkaribia na kwa muda huo ndiyo amekuwa Bod gad wa boss, walishangaa lakini kwa Suzy na Rafael walikubali na kuona kuwa dada huyo hiyo nafasi ni halali yake.



    "leo jioni ndiyo siku ambayo Sex machine anamalizia ile hatua ya mwisho ya kuanza kuwaingilia mashoga." Joesan alikuwa akiwapa taarifa hiyo wale watu muhimu tu mahali hapo huku kwa pembeni yake akiwepo Merina ambaye alikuwa kikazi kweli. Alikuwa yupo na vinasa sauti masikioni mwake pia alikuwa na mawani nyeusi ya giza.

    "Tai, kama tulivyokuwa tumeongea hii ni kazi makini sana na inayohitaji umakini mkubwa na uangalizi wa hali ya juu. Hapa ukikosea tu, ujue hautabaki hai. Hapa ndipo tunapokwenda kuwa matajiri wakubwa na nyinyi wafanya kazi muhimu kubadilisha maisha yenu." aliweka tuo. Akatulia kidogo na kuruhusu maneno yake yapenye kwenye ubongo wa Tai. Ukimya ulikuwa mkubwa kiasi cha kumfanya bwana huyo kuhitimisha.

    "ukimya unaoneaha kuwa tumeelewana hivyo basi kila mmoja ajue nini anatakiwa kufanya katika nafasi yake." watu wakatawanyika baada ya Joesan kuhitimisha.



    Saa kumi jioni ndiyo sex machine alitakiwa kuingia kwenye Happy Club kwa ajili ya kwenda kufanya wajibu wake, alikuwa amesha jiandaa kwa kazi hiyo na muda huo alikuwa tayari amepiga vazi lake la kazi (SMC). Muda ulipotimu, alikuwa yupo nje ya jingo hilo akipiga hatua taratibu kuelekea katika chumba ambacho shoga huyo aliyehitaji huduma hiyo ambaye alikuwa tayari amekwisha kuilipia kiasi kikubwa cha pesa, alikuwamo. Sex machine aliingia ndani kabisa ya Club hiyo, ambako huko hakukuwa kukusikika sauti yoyote ya muziki wala nini. Alikitazama chumba hicho na kushusha pumzi nzito sana huku akiwaza ni jinsi gani atakavyokwenda kumgeuza mwanaume mwenzake na kumla uroda, lilikuwa ni jambo gumu sana la kutokuaminika lakini ni kazi kwake hiyo na hakuwa na jinsi. Aliufungua mlango wa chumba hicho lakini hakutegemea alichokikuta humo ndani. Damu zilitapakaa na mwili wa mtu aliyetaka kumfanyia huo ushenzi alikuwa chini akiwa amechanguliwa kifua kwa risasi. Macho yakamtoka kwa mshangao mkubwa, lilikuwa ni jambo la kushangaza sana na hakulitegemea. Akausogelea huo mwili na kuutaza vizuri, alikuwa ni kidume kilichojaa misuli akionesha fika kuwa ni mchukuaji mzuri wa mazoezi lakini hakuamini kama alikuwa si riziki mwanaume huyo na laiti kama siyo kifo kumkuta, alitakiwa kumuingilia kama waingiliwavyo wanawake.



    "ni nani muuwaji?" alijiuliza Sex machine lakini jibu lilikuwa ni uwongo kupatikana kirahisi kwa muda huo. Akayainua macho yake na kuyazunguusha mule ndani, alizunguusha macho kwa muda hadi alipoyatuliza baada ya kuvutika na kitu alichokiona dirishani. Alisogea hadi dirishani hapo, na kugusa sehemu ambayo ilikuwa na tundu. Ndiyo ilikuwa ni tundu la risasi.

    "hapa ndipo ilipopenya risasi iliyoleta madhara kwa huyu bwabwa?" alijiuliza kisha akachungulia pale dirishani, hakuona kitu kilichompendezea. Lakini alipozidi kutazma kwa umakini aliona jingo refu kwa mbali kidoo ya jingo hilo.

    "ooh shit! Muuwaji alikaa pale kisha kufanya udunguaji wa mtu huyu, kwanini afe sasa?" alizidi kujiuliza bila mafanikio. Akarudi pale kwenye ule mwili na kutoa simu yake mfukoni.



    Kwenye upande wa ofisi ya Tai, kulikuwa na baadhi ya watu wakiwa wametulia kimya. Wote walikuwa wameyaelekeza macho yao kwenye luninga zilizokuwa zimeenea maeneo yote humo ndani, Joesan alikuwa ni miongoni mwa watu waliojaa humo kwenye hiyo ofisi ya Tai wakisubiri kuona ni jinsi gani Sex Machine atafanya ngono kinyume na maumbile tena kwa kumungilia mwanaume mwenzake. Muda ulikuwa ikienda kwa kasi kubwa na hakukuwa na kile walichokuwa wakikitegemea kutokea mahali hapo. Kila mmoja alikuwa akiitazama saa yake kila wakati.

    "mbona anachelewa sana vipi?" aliuliza Tai. Hakuna aliyemjibu wote waliokuwamo humo ndani walikuwa kimya kabisa. Pumzi nyingi zikamshuka Joesan, waliamini kuwa endapo Sex machine atakapo onesha hisia za mapenzi kwa mtu aliyemkuta huko na lile vazi lingeanza kurusha picha, lakini ukimya wa hadi muda huo, ukamtisha kidogo.

    "au hahitaji kumuingulia huyo shoga?" alijisemea moyoni Joesan. Lakini wakati akiwa anazidi kujiuliza, simu yake ikamtekenya mfukoni mwake. Akaitoa haraka haraka na kumtazama mpigaji, alikuwa ni Sex Machine.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mh!" akagumia kisha akaiweka sikioni na kukaa kimya akisikiliza kwa umakini mkubwa.

    "amekufa! Ameuwawa, kivipi sasa?" alishtuka sana baada ya kupokea hiyo simu, ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Sex machine ukimwambia kuwa huyo shoga ameuwawa. Joesan ikambidi kuuliza maswali ya kuchanganyikiwa na kikubwa alichotaka kujua ni jinsi huyo mtu alivyouwawa yaani kifo chake kikoje. Akaambiwa kuwa kifo chake kimesababishwa na kupigwa risasi ya kifua.

    "hakuna kazi Tai huyo shoga ameuwawa kwa kupigwa risasi sasa sijui........aaaghr!" alidata Joesan. Wakati huo akiwa tayari amekwisha kata hiyo simu na kutoka humo ofisini kwa kasi ya ajabu sana akifuatiwa na Merina nyuma. Taarifa hiyo haikumchanganya Joesan pekee bali ilimchanganya hata mkuu mwenyewe na kuamua kumuita Joesan, Rafael akiwapo na Merina kwenye chumba cha mikutano kwa ajili ya kujadili kifo hicho.

    "inavyoonekana hakuna kundi moja linalotuandama, hili ni kundi jingine lililojitokeza kwetu na kuharibu mipango yetu" sauti ya mkuu ilirindima mahali hapo.

    "hilo naliunga mkono mkuu kwani mtindo huu wa mauwaji umekuwa ni wa tofauti kwani hawa wametumia risasi za kawaida ikiwa ni tofauti na D.A." alisema Joesan kukubaliana na alichokiongea mkuu wao mahali hapo.

    "mkuu, kitu kinacho niumiza kichwa ni je, wamewezaje kufanya mauwaji hayo bila kuonekana na vyombo vyetu vya ulinzi hata mara moja? Lile jingo si linaulinzi wa kutosha lile?" mzee Rafael naye aliamua kuuliza.

    "ewaa! Hilo hata mimi linanichanganya lakini hiyo inanipa picha kuwa hatupambani na watu wadogo, hapa tunapambana na watu wenye weledi mkubwa. Joesan, hakikisha unakuwa macho na umfuate Sex Machine au ikiwezekana umuite ofisi kwako na .............................................................



    na umwambie kuwa kesho anatakiwa asafiri tena kwenda Nairobi kwa ajili ya kazi. Kuna shoga kule tumeshafanya nae mawasiliano hivyo kila kinachotakikana nitakupa umuwasilishie" aliongea mkuu huyo kisha kikao hicho kikavunjwa na kila mmoja kutakiwa kuwa makini na sekta yake kwani kazi inavyoonekana imeshaingiliwa na mdudu mbaya.



    NAIROBI KENYA.



    Saa nne juu ya alama, ndege kubwa ya shirika la Tanzania ilikuwa inakanya matairi yake ndani ya uwanja huo wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta. Dege hilo lilikimbia kwa kasi baada ya kuikanyaga sakafu ya uwanja huo hadi lilipokuja kutulia mahali ambapo ndipo lilipotakiwa kusimama. Mlango wa ndege hiyo ulifunguliwa na watu kuanza kushuka mmoja baada ya mwingine. Mtu wa nne kutoka ndani ya ndege hiyo alikuwa ni Sex machine akiwa amenyuka suti yake ya maana iliyomkaa vizuri kabisa huku nyuma alikuwa akifuatiwa na mwanamke mrembo aliyevaa kawaida sana. Mwanamke huyo machoni alipiga mawani ya kirembo. Alikuwa akishuka taratibu sana hadi alipofika chini. Wakaelekea mahali pa ukaguzi kisha wakatokea upande wa pili, huko Sex machine alichukua usafiri wa tax na kuomba apelekwe kwenye hoteli ambayo aliichagua. Huku nyuma yule mwanamke naye aliingia kwenye tax nyingine kisha akamuomba dereva wa tax aliyopanda aifuatilie tax ya mbele yake.

    "kuwa makini kaka yangu asijue kama kuna mtu anamfuatilia sawa" ndivyo alivyosema huyo dada ambaye bado jina lake halikujulikana ni nani.

    "usijali sister hizi kazi hatuzianza leo, vipi ni nani kwani yule?" alijitapa dereva huyo kisha akauliza swali la mtego.

    "usijali ni kifamilia zaidi yule ni mume wangu so nataka kujua ni wapi anaelekea maana hakuniambia kama leo ndiyo anaingia hapa nchini, sasa nashangaa kumkuta mahali hapa"

    "ohoo, basi haina shida ngoja tutajua, tu" alisema kaka huyo huku akiyaruhusu magari mawili yampite na yeye kuwa wa tatu ikiwa ni katika kumzuga mfuatiliwaji asijue kama anafuatiliwa lakini akiwa makini kuhakikisha gari aliyoilenga haimuachi. Gari iliyombeba Sex machine ilisimama nje ya hoteli moja kubwa mjini hapo. Iliegeshwa vizuri gari hiyo na Sex machine akashuka akiwa tayari amekwisha kufanya malipo kwa dereva tax, akapiga hatua ndogo ndogo hadi mahali ulipo mlango wa kuingilia ndani ya hoteli hiyo.

    "siamini kama huyu mwanaume anaingia hotelini yaani aaaah!" alistaajabu dada ambaye alikuwa yupo kwenye gari ya nyuma ambayo ilikuwa ikimfuatilia Sex machine. Aliongea kwa uchungu sana kiasi kwamba dereva wa gari hiyo, aliamini kabisa kuwa yule mwanaume aliyeingia ndani ya hoteli hiyo ni mume wa abiria wake aliyembeba.

    "tuondoke suka, haki ya manani nyie wanaume ni washenzi sana" alisema huyo dada akiwa anafuta machozi na kuzidi kumchanganya huyo dereva. Machozi na sauti ya kilio ilimdhihirishia kabisa huyo bwana. Ukimya kwake ndiyo ikawa kitu pekee, hakuongea chochote zaidi ya kumuuliza ni wapi waelekee.

    "twende na barabara hiyo ya mjini nitakuambia wapi nashukia" alisema na kutulia kimya kitini hadi mbele kidogo, ndipo akamwambia dereva huyo kuwa hapo ndipo anapo shukia. Dereva huyo aliegesha gari pembeni na dada huyo akashuka na kulipa kiasi alichotakiwa kulipa na kuondoka hapo kwa haraka sana. Alionekana kuwa ni mwenye haraka mno, alipokunja kona mbili tatu na kuhakikisha kuwa kutoka machoni mwa yule dereva tax ambaye alikuwa akimuangalia muda wote, alitoa simu ya kiganjani kwenye hand bagi yake, akabonyeza namba kadhaa na kuiweka sikioni.

    "ndiyo fadher nimeshaianza kazi na imekwenda vizuri. Yupo ndani ya jiji hili na nimeshajua kila kitu hadi mahali mchezo huo mchafu utakapo fanyika." alisema dada huyo baada ya kuiweka simu hiyo sikioni mwake.

    "uko wapi kwa sasa?" sauti nzito ilimuuliza.

    "nipo hapa mjini kwenye hii Super market kubwa sijui inaitwaje sijayasoma vizuri maandishi yake"

    "ok, nimeelewa, nenda mbele kidogo kisha kunja kulia na uchepukie kwenye nyumba mbili za hapo, halafu moja kwa moja ingia kwenye gari nyekundu" ilimaliza kutoa maelekezo, sauti hiyo nzito ya kiume, huyo dada akairudisha simu kwenye kibegi chake. Akafanya kama alivyoelekezwa na kuingia kwenye hiyo gari.

    "hongera kwa kazi nzuri, kuna mtoto hapo nyuma amelala, huyo ndiye atakayetumika kwa kazi ya leo" alisema mzee mmoja ambaye alikuwa akionekana upande wa mgongoni pekee na gari ikaingizwa barabarani kwa mwendo wa kasi sana ikichukua uelekeo wa mashariki. Huko ilizunguuka hadi kutokea upande mwingine kabisa wa hoteli aliyofikia Sex machine kisha gari hiyo ikasimama kwenye jingo la mbali kidogo na hiyo hoteli. Dada yule akakamata begi fulani akashika mlango wa gari na kuufungua kutaka kushuka, sauti ya yule mzee aliyekuwa akionekana mpongo ikamgutusha.

    "unajua chumba alichofikia ndugu yako?"

    "hapana huyo sina kazi naye leo nataka kumuuwa huyu shoga kabla hata ya kukutwa na Sex machine, zimebaki dakika mbili tu na sitakiwi kuchelewa, Sex machine si wa kufanya huo uharamu hata kidogo" alijibu huyo msichana na kushuka ndani ya hiyo gari. Alikimbia kwa hatua kubwa kubwa hadi kulikaribia jingo hilo ambalo bado lilikuwa katika ujenzi. Ni jingo ambalo kwa hapo lilipofikia tayari lilikuwa na orofa tano. Alifunua shati lake na kutoa kitu fulani alichokuwa amefunga kwenye mkanda wake wa suruali aliyokuwa ameivaa kisha akakibonyeza bonyeza vitufe vyake na kukirusha juu. Kifaa hicho kilijiendesha chenyewe kwenda juu yeye akawa ameshikilia kamba mbili ambazo aliipitisha moja kushoto na nyingine kuliani mwa kiuno chake kisha kuunganisha na loki fulani zilizopo kwenye mkanda wake wa suruali. Kifaa kile kilisafiri hadi orofa ya nne, kikaenda kukamata kwenye kingo ngumu za kule juu, yeye akaminya kitufe fulani ambacho alikuwa amekishika kwenye mkono wa kushoto huku akilitupia mgongoni lile begi aliloambiwa kuwa kuna mtoto wa kazi amelala. Kwakutumia gloves maalumu, alizikamata zile kamba mbili na kuanza kuvutwa kwa kasi kwenda juu. Lilikuwa ni tendo la haraka sana. Alipofika kule juu, alifyatua zile loki na kukiacha kile kifaa kikining'inia. Yeye akaelekea hadi kwenye dirisha moja ambalo lilikuwa likimuonesha ile hoteli aliyofikia Sex machine kwa mbali kidogo. Alifungua lile begi alilokuwa amelitupia mgongoni na kuanza kutoa bunduki kubwa isiyo na urefu wa kutisha. Akaifunga kiwambo cha kutokusafirisha sauti na kuikoki vizuri, akaiweka lenzi ya kuonea mbali kwa utaratibu mzuri kisha kuiweka jichoni akiwa amelifumba moja. Aliizungusha ile bunduki kila sehemu huku akiwa makini sana, akamuona mwanaume mwenye asili ya kihindi mwenye tumbo kubwa akiwa uchi hana hata nguo moja. Muhindi huyo alikuwa kwenye chumba kilichopo mkabala na chumba ambacho alimuona Sex machine akiwa ameiinamia kompyuta yake. Kwa jinsi ambavyo muhindi huyo alikuwa, ni wazi aliamini kuwa huyo ndiye aliyekuwa akisubiri huduma ya kuingiliwa kinyume na maumbile. Alijifananisha na meanamke kwa kila tendo. Mwanamke huyo akamuweka sawa mwanaume huyo asiye rijali, alama yake ya shabaha ikawa kwenye paji la uso la shoga huyo aliyetakiwa kuingiliwa na Sex machine. Akahesabu tatu mpaka moja kisha akavuta triger na risasi ikatoka kwa kasi kubwa, yule mwanaume akafumuliwa kisogo chake baada ya ile risasi kuchapa paji lake la uso. Alitupwa nyuma na kupigizwa ukutani akiwa mfu. Aliirudisha ile silaha kwenye begi lake na kwenda palepale

    alipoingilia akapenya pale dirisha na kuanza kushuka kwa kasi kubwa hadi chini na kurudi garini tena.

    "uko vizuri mno kuliko hata mimi sasa, ni dakika moja na nusu tu ulizotumia" alisema mzee huyo mara baada ya yule dada kukaa kwenye siti ya nyuma aliyokuwa amekaa awali.

    "lazima niwe hivi Father nina hasira sana za kumrudisha ndugu yangu nyumbani" alisema huyo dada na kunyamaza kimya asiseme kitu tena. Yule mzee naye hakujibu kitu bali alichokifanya ni kurudi barabarani na kuondoka eneo hilo. Ni nani hao? Huyo dada anataka kumrudisha ndugu yake nyumbani je, ndugu yake ni nani? Au ni sex machine?

    Duh!



    DAKIKA 30 ZILIZOPITA.



    Sex machine alipoingia pale hotelini, alichukua chumba ambacho hakikuwa mbali na ailpotakiwa kwenda kufanyia kazi yake. Kilikuwa ni chumba ambacho kilikuwa kikitazamana na chumba cha mwanaume aliyetakiwa kwenda kumuingili kimwili kwa lugha nyepesi tunaweza kusema kumlawiti, alishusha mizigo yake kitandani na kukaa kitako akiwa anatafakari. Hakujua kama huko nako kutatokea kama kule Morogoro au huku atafanikiwa kumla uroda mwanaume mwenzie. Kitendo hicho hakuwahi kukifanya hata mara moja lakini mwili wake ulikuwa uko katika uhitaji wa kutaka kujaribu huo mchezo japo hakuwa akijua nini madhara ya mchezo huo. Alitazama muda kwenye saa yake na kuona sasa limebaki lisaa limoja tu na muda huo akiwa tayari ameshafanya matusi kwenye ulinzi wa hoteli hiyo. hivyo alichokuwa akikisubiri hapo ni kutimia kwa muda tu na yeye kwenda kufanya yake. Dakika mbili ziliposalia ndipo kijana huyo akaanza kupunguza nguo na kutoka ndani ya chumba alichofikia na kuelekea chumba ambacho yupo huyo mteja wake. Ile anafungua mlango tu, alikuta huyo mwanaume aliye humo ndani akiruswa ukutani kwa kupigwa risasi huku kelele za kioo kumwagika zikifuata. Sex machine alikimbia hadi upande lilipo dirisha hilo kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha mdunguaji huyo hawezi kumuona. Alichelewa. Wakati yeye anaambaa na ukuta mwenzake, alikuwa akiteremka chini kwa kutumia kamba zile maalumu. Sex machine alipochungulia pale dirishani, aliliona lile jingo na kuona dirisha lililokuwa limeelekea upande huo. Akajua hapo ndipo mdunguaji huyo alipokuwa amekalia. Muuwaji ni mtu wa namna ya hatari sana, muda huo huo yeye anaingia ndiyo mteja anadunguliwa? Hofu ikamtanda moyoni, akajiuliza kwanini kila Shoga aliyetakiwa kukutana naye alikuwa akiuwawa? Alijiuliza sana lakini jibu lilikuwa hakuna kabisa. Akatoka humo ndani kwa haraka sana, akajua kuendelea kwake kukaa humo ni kujikamatisha kizembe kwa polisi ......................

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kwani aliamini huwenda muuwaji akaita polisi mahali hapo na likamtokea tukio baya. Alifanya kila kitu kwa haraka na kuondoka kabisa ndani ya hoteli hiyo na kwena moja kwa moja uwanja wa ndege kuangalia kama anaweza kupata usafiri wa ndege mida hiyo ya alasiri. Bahati ikawa kwake, akapata ndege iliyokuwa inaondoka mida hiyo ya saa kumi. Alipoingia tu kwenye ndege hiyo iliyokuwa inaelekea kilimanjaro, alituma ujumbe kwenda kwa Joesan kumtaarifu kile alichokikuta ndani ya chumba cha mteja.



    Joesan alichanganyikiwa zaidi baada ya kupata hizo taarifa. Ikabidi ampenna taarifa hiyo mkuu. Mkuu alivimba sana kwa ghadhabu. Nani aliyekuwa akitoa siri za hiyo mipango ya kibiashara? maswali hayo yote yalikuwa yakikigonga kichwa cha mzee huyo. Ni nani basi atakeyetaka kufanya hiyo biashara tena na bwana huyo ilihali mashoga wengi walikuwa wakiuwawa kwa mtindo huo. Hali ya sinto fahamu ikamkumba Mr. Kim. Hasira zikazidi kumpanda. Kila aliyekuwa akifanya naye mawasiliano kwa ajili ya kuingia naye katika makubaliano ya kibiashara, alikuwa akigoma na kuhofia uhai wake. Mashoga wengi duniani wwkajihami na kukataa kabisa biashara na huyo mzee wakiamini ni mkakati kwake wa kutaka kuwamaliza mashoga duniani. Kim akachanganyikiwa. Kikao kizito kikafanyika kwenye ukumbi wa mikutano. Mkutano huu wa dharula uliwahusisha watu watatu tu yaani Joesan, Sex machine na Mr. Kim akiwepo pia japo hakuonekana.



    "tumekutana hapa Sex machine kwa jambo moja tu, kila njia ya kufanya ili ufanye ngono na wanaume hao imeshindikana. Hebu tuambie njia ambayo sisi hatuja itumia labda ambayo inaweza kutusaidia" ilikuwa ni sauti ya Kim ikiunguruma nahali hapo. Sex machine alimtaza Joesan na kukiweka kile kinasa sauti vizuri na kujikohoza kisha akasema.

    "liwe ni tukio la kushtukiza, ninamaana ya kwamba asijue mtu yoyote zaidi ya sisi na mpango huo usifanyike ndani ya kampuni. Ninawasiwasi sana na usiri uliopo pale kwenye kampuni na sina imani nao kabisa, kama hakuna mtu anayevujisha hili, basi kuna vitu vimetegwa ambavyo vina safirisha sauti kwa hao watu" wazo hili likawafanya watu wale kuamini kuwa huwenda maneno yaliyoongelewa na kijana huyo yanaukweli ndani yake.

    "Joesan, nafanya maongezi na mtu moja hapa hapa na hili litafanyika ndani ya hoteli ya Urugulu. Nataka kuona je ni kweli alisemalo huyu kijana na kama hili likifanikiwa basi lazima kufanyike uchunguzi wa ndani nje kwenye ile kampuni ili tujue ni nini kinasababisha siri zetu kuwa uchi" alisema Kim na wote wakakubaliana huku sex machine akiambiwa akae mkao wa kula ndani ya siku mbili atapewa taarifa. Hali ilikuwa tete mshoga wote duniani waligomea biashara na huyo mzee hadi aweke hali ya usalama vizuri.



    Ndani ya jumba moja kubwa Nairobi, pembezoni kabisa mwa jiji hilo. Kunaonekana msichana akiwa amekaa kwenye kochi kubwa la gharama sana huku binti mdogo wa kike akiwa amekaa juu ya ki baiskeli cha matairi matatu akiwa ametulia tu bila kuendesha. Binti huyo mdogo hakuwa mwingine bali ni Mery, yule aliyekuwa akiishi na Joesan. Msichana huyo ambaye alikuwa mahali hapo, alikuwa ametulia kimya akiminyaminya simu yake kubwa. Uharakati huo wa kuminya minya simu uliendelea hadi pale alipotokea mzee mmoja mwenye mwili wa wastani, aliyeonekana yupo kimazoezi. Alifika hapo na kumbeba yule mtoto akafika nae hadi kwenye kochi na kuketi akiwa amembeba mtoto huyo.



    "hujambo Maria?" alimsalimia yule mtoto mzee yule.

    "sijambo babu"

    "kweli hujambo? Mbona unaonekana kama huna furaha sasa binti yangu?"

    "uliniambia kaka Chriss atakuja huku na kuishi na mimi lakini mbona haonekani au atakuwa kwa uncle Joe?" aliuliza binti huyo na kumfanya mzee huyo kuvuta pumzi nyingi ndani ya mapafu yake kisha kuzitoa kwa pupa. Akatulia na kumtazama binti huyo mdogo kisha akamwambia kwa sauti ya upole.

    "kaka Chriss hayuko kwa huyo anko wako bali yupo safarini, atakuja muda siyo mrefu. Nimeongea naye jana kwenye simu na ameniambia hivyo, amekumiss sana Maria"

    "kweli babu?" alisema Mery akiwa na furaha sana.

    "ndiyo" akijibu Mzee huyo na kumtazama binti aliyoko kwenye kochi la mbele yake ambaye kwa muda huo alikuwa ameacha kuichezea simu yake, wakajikuta wakitazamana.

    "Maria nenda chumbani ukalale, halafu hujalala kabisa leo kwanini?"

    "nilikuwa naendesha baskeli" alijibu Mery na kutoka mikoni mwa babu yake huyo kisha akakimbilia chumbani kwake. Mzee huyo akawa anamtazama binti yule mdogo huku tabasamu safi likiwa usoni mwake.

    "ninafuraha sasa kuishi karibu na binti huyu" alisema mzee huyo huku akirudisha macho yake kwa msichna aliyoko mbele yake.

    "woga umemuisha amezoea mazingira sasa" alisema binti huyo baada ya kuacha kumuangalia yule mtoto.

    "lazima azoee hapa kwani ndiyo nyumbani kwao, mwanzo ulikuwa ni ugeni unamsumbua" alisema yule mzee. Wote wakaangua kicheko cha nguvu na kupiga kimya cha muda kumruhusu shetani apite kisha mzee huyo akaendelea.

    "niambie Catherine, mtoto nadhani umemsikia mwenyewe hapa alivyosema. Anamtaka kaka yake na kazi hiyo ya kumleta kaka yake hapa unayo wewe"

    "najua father, najua na nimuahidi tu niko mbioni kumletea huyo kaka yake" alijibu huyo binti ambaye alikuwa akifahamika kwa jina la Catherine. Huyo ndiyo yule ambaye tulikuwa tukimfahamu kama bikini nyekundu.

    "ni wapi ulipofikia kwa sasa Catherine?" aliuliza tena huyo mzee.

    "sasa hivi nimeharibu kabisa biashara ya ushenzi ule aliokuwa akiufanya sidhani kama kuna shoga yoyote atakayejitokeza kukubali kushiriki mapaenzi yao ya kishetani tena. Na nimeapa mbele za Mungu, sitamuacha hai mwanaume yeyote yule atakayekuwa tayari kushiriki mapenzi hayo. Nitauwa" aliongea Catherine. Yule mzee alielekeza macho yake chini na alipokuja kuyainua juu, alishusha pumzi za kutosha kisha akamtazama tena binti huyo usoni. Akasema.

    "namjua yule mzee niliishi naye kwenye chuo kimoja cha mafunzo mwanzo mpaka mwisho hadi tulipokuja kutengana baada ya yeye kufukuzwa. Ni jeuri sana yule na huwa hakubali kushindwa hata mara moja. Ninaimani kwa sasa kama hajatafuta njia nyingine ya kufanikisha hilo jambo lake basi yuko mbioni kutafuta ufumbuzi"

    "father D.A nadhani unanijua mimi vizuri, si wa leo wala jana kwako, nimeishi nawe kwa kipindi kingi, unanijua nikiamua langu huwa halipingiki hata kidogo. Na kama yeye ni jeuri na mbishi, mimi ni kiburi fadha" akatamba binti huyo kwa ghadhabu sana. Alionesha kuwa hatanii hata kidogo lakini baada ya kusikilizwa sana na mzee huyo, cheko kubwa la nguvu likamtoka mzee huyo. Alicheka sana hadi huyo Catherine akashtuka.

    "kwanini unacheka hivyo Father?" aliuliza Catherine lakini pia bado kicheko cha father D.A hakikukoma. Alicheka hadi akawa anatoa machozi kabisa. Alipokuja kuacha kucheka, alimtazama kwa makini sana binti huyo akamwambia kwa utulivu mkubwa.

    "najua unahasira sana na mr. Kim lakini hasira zako haziwezi kumuangusha yule mzee hata kwa dakika moja. yule ni fundi na anajua kutumia mapigo ya maangamizi pia anauwezo wa kutumia silaha za siri na za dhahiri, sitakuruhusu umkaribie yule bwana ni katili mno."

    "hapana father lazima nihakikishe namdondosha yule mzee lazima, siwezi kumuacha hai hata kidogo."

    "hivi ulikuwa unajua kwanini nilikuwa nacheka?" akauliza.

    "hapana" akajibu Catherine.

    "nilikuwa nacheka kwa sababu moja tu ambayo ni hii. Nisikilize kwa umakini mkubwa. unahasira lakini weledi wako wa kupigana haufikii hata robo ya yule mzee"

    "what?" aling'aka Catherine.

    "ndiyo, hata robo humkuti yule. Wewe umejifunza Marsh arts kwenye Chuo kimoja tu huko China lakini Mr. Kim amejifunza mafunzo hayo kwa karibu vyuo vinne ndani ya nchi hiyo. viwili tulikuwa wote japo kimoja hakufuzu lakini viwili vya mwisho, alijifunza katika vyuo vingine yeye kama yeye, kwa hiyo yule ni mwalimu mwenye uwezo mkubwa wa kuweza kupewa dhamana na Taifa lolote duniani kufundisha ngumi" alisema Father D.A. Maneno hayo yakamchosha sana Catherine, alijihisi kukata tamaa kumuangusha mr. Lee Kim. D.A alijua kuwa binti huyo amevunjika moyo. Akamsogelea karibu na kumwambia kuwa asivunjike moyo kwani yupo mtu mmoja tu mwenye uwezo mkubwa wa kumupndoa kabisa duniani bwana Lee naye si mwingine bali ni.......! akaishia njiani. Hakutaka kumalizia kauli hiyo ambayo ilijenga maswali mengi kwa binti huyo. Catherine akataka kuuliza juu ya mtu huyo atakayeweza kumuangusha bwana Kim, akasita na kubaki kujiuliza mwenyewe tu. Ni yeye? Labda ni yeye kwasababu alishawahi kuniambia kuwa yeye alijifuza ngumi katika vyuo vitano huko huko nchini China na vyote vikiwa na aina zake na imani zake za kimafunzo. Sasa kama Kim amejifunza vyuo vinne, huwenda akawa ni yeye atakaye weza kumuangusha bwana huyo. Ndivyo alivyokuwa akijiuliza japo hakuwa na uhakika sana juu ya kujiuliza huko. Hakuwa na muda wa kumuuliza tena kwani kifaa chake cha kunasa sauti alichokiunganisha na ile simu yake kubwa, kikaleta mawimbi. Akanyanyuka na kumuacha mzee huyo mpole sana aliyeonekana kushiba imani kisha yeye akaelekea chumbani kwake ambako alichukua waya wa USB na kuchomeka kwenye ile simu akaiunganisha na kompyuta yake mpakato na kuanza kusikiliza sauti hizo. Alizisikiliza hadi sauti hizo zilipofika mwisho, akarekodi na kuzima kabisa Kompyuta yake. Alijitupa kitandani akiwa amechoka kiakiakili na kimwili, mawazo lukuki yakiwa yamekiandama kichwa chake.



    "wanampango wa kufanya biashara kubwa ya madawa ya kulevya, biashara ambayo itakwenda kuwaweka levo nyingine kimaisha" alikuwa akiwaza Catherine.

    "hapa ndipo wanapotaka pia kumgeuka Joesan hawa jamaa wawili, mh! akacheka kidogo na kuendelea...........................CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    " hawa wanataka kuleta vita na Joesan lakini kabla hiyo vita haijafika lazima kwanza niwe nimesha mteka Sex machine wao na kuwageuka wao. Hapa nitawachonganisha wote watatu ili kila mmoja amuone mwenzake hafai. Wao wakipigana sisi tunaingia kwenye ngome ya Mr. Lee." alizidi kuwaza mwanamke huyo akiwa amejilaza hapo kitandani na hiyo ni baada ya kusikiliza zile sauti zilizokuwa zimenaswa na kinasa sauti chake. Ambazo alinyaka kutoka kwa BC, mtu ambaye alikuwa akinyaka kila mawasiliano yake. Na hapo bwana huyo hakujulikana anaongea na nani. Lakini pia kuna kitu cha pekee hapo huwe amekipata.



    MOROGORO TANZANIA.



    Saa tatu juu ya alama usiku kila mtu ndani ya kampuni alikuwa busy. Huyu alifanya hiki na yule kufanya kile. Lilikuwa ni jambo la ajabu sana hadi kufikia muda huo, hakukuwa na dalili ya kufungwa kwa kampuni hiyo. Uchakalikaji ulikuwa ni mkubwa sana mahali hapo. Lakini wakati hizo mishemishe zikiwa zinaendelea, hapo hapo ndani ya ofisi ya mzee Rafael, kulikuwa kimya kabisa utadhani labda hakukuwa na mtu ndani humo. Rafael alikuwa amekaa humo ndani akiwa ameshika kitu kimoja kidogo sana mfano wa spika ya simu. Kidude hicho alikuwa akikizunguusha vidoleni mwake tarabu huku akiwa na mawazo sana.



    "hiki ni kinasa sauti, ni nani aliyefanya haya yote. Bila shaka mawazo yangu yalikuwa sawa kabisa. Hii inanipa picha ya yale makanyagio ya viatu niliyoyakuta siku ile ambapo kulitokea mzimiko wa umeme usiku" alizidi kuwaza Rafael. Kitu kile achokikuta chini ya meza yake kwa bahati mbaya, kilimpa picha ya kila kitu cha alama za viatu alizozikuta. Hakuamini kama eti, hiyo ni kwa ajili ya ulinzi wa Kim bali alichoamini ni kwamba kuna mtu au watu walikuwa wakifanya kazi hiyo kwa sababu maalumu. Hakutaka kusema kwa mtu yoyote yule kuwa amegundua hicho kitu, alitaka kuona nini hatima ya watu hao ila hakujua kuwa kufanya hivyo kwake ni hatari kwani huwenda ulinzi wa siri wa kimu ulikuwa ukimuona yeye bila kujua. Na alifanya hivyo makusudi kwani maisha ya kunyanyasika na kushuhudia mauwaji ya vijana anaowafundisha kwa kisingizio cha kuwapima majasusi wake, kilishamchosha. Alichokiona hapo ni yeye kuja kujaribiwa siku moja ili anekane anauwezo gani. Hilo jambo lilimuumiza sana na kumpa hofu kubwa moyoni mwake. Akaona ni bora asubirie kuona nini kinaweza kutukia.



    Usiku huo huo Suzane alimvamia Sex machine nyumbani kwake lakini hakumkuta, akampigia simu ilikumuuliza ni wapi alipo simu ikaita kisha ikakata. Akakumbwa na mshtuko, jambo hilo halijawahi kutukia kwa maisha ya Sex machine kupigiwa simu halafu ikate. Akawa anajiuliza ni nini kinatukia mahali hapo. Akataka kupiga tena lakini simu yake ikawahi kuita, mpigaji alikuwa ni sex machine.

    "uko wapi wewe na mbona nakupigia simu inaita halafu inakata" aliuliza kwa alama nyingi za kuuliza baada ya kupokea simu hiyo.

    "napata supu ya pweza kidogo, halafu ni bora umenitafuta maana nilitaka nikupigie simu nikitoka hapa" alijibu kijana huyo. Suzy akashtuka wewe unasema unapata nini?"

    "mbona unashtuka sana mtoto mzuri kwani mimi kunywa supu ya Pweza kuna ubaya?"

    "tena sana SM, wewe una nguvu za asili hivyo mambo hayo siyo mazuri"

    "nakutania Suzy, niko mjini nakuja sasa hivi hapo nyumbani so usiwaze."

    "ok, fanya haraka" alisema Suzy ma kujiegamiza kwenye gari ili kuendelea kumsubiri mwenyeji wake. Haukupita muda mrefu sana kijana huyo akawa anaingia hapo na pikipiki lake kubwa, akapiga breki na kushuka kisha akalivua kofia la usalama, akamfuata binti huyo ambaye alikuwa ametulia tu akimtazama kijana huyo jinsi alivyokuwa akimkaribia. Hakuna maongezi, salamu wala nini. Alimvamia na kuanza kumnyonya mate, alifanya hivyo kwa muda kidogo huku Suzy akitoa ushirikiano wa kutosha sana. Miguno ya maraha ikashika nafasi, binti huyo alikuwa akinungunika kila akishikwa na alikuwa akisikia raha za hatari sana.

    "kwa nini umesusa muda mrefu kunipa penzi Suzane?" aliuliza SM huku akiwa anampapasa kwa utaratibu sana juu ya kufuli lake kwa mbele.

    "mmmmh!, yaaaaa, aaaasssss!, si....si ulikuwa na mishemishe nyingi sana ya kikazi mpenzi wangu" aligumia hivyo Suzy huku akitoa jibu la swali aliloulizwa.

    "yaa, ni kweli lakini hata nikiwa free umekuwa hunikaribii"

    "acha lawama mpenzi huoni kuwa leo nipo kwa ajili yako, hebu twende ndani ukanitafune hadi niishe Joesan anitafute hadi akome" alisema binti huyo akiwa amejitoa kinywani mwa kijana huyo akimtazama usoni. Sex machine alimtitika binti huyo na kuelekea ndani, akamtupa kwenye kochi kubwa na kumpandia kwa juu. Alimvua nguo zote. Suzy akabakia bila nguo hata moja mwilini mwake. Mwili wake mtamu wa kuvutia ukaonekana ukiwa uko katika matamanio makubwa kabisa. SM alipambua za kwake na kuzitupia pembeni kisha akaanza purukushani na mbwembwe zake za kumuandaa mtoto huyo. Suyz kila akimuangalia kijana huyo, mashetani ya kikubwa, yalikuwa yakimpanda, mwili kumuwasha na kuhitaji mkuno wa kijana huyo. Mambo yakaiva, watu wakaingia kwenye maakuli. Shughuli ilikuwa si ndogo, shughuli ilikuwa pevu kweli kweli.

    "baby niambie kweli kama hukuwa ukipata Supu ya Pweza huko ulikokuwa maana naona unasugua kwa pupa sana kama uko kwenye riadha za mbio ndefu." alilalama binti huyo huku akiwa katika manung'uniko makubwa.

    "sijanywa kitu chochote baby nilikuwa nakutania tu"

    "sasa mbona leo unachelewa sana baby jamani, kwani roundi ya pili huwa unachukua muda gani kwa kawaida?"

    "nakaribia mpenzi" alimwambia huku akiwa anashuka na kupanda kama anaendeshwa na rimoti.

    "kwani nakuumiza?" aliuliza SM baada ya kuona Suzy analalamika sana.

    "hapana huniumizi ila naona unachelewa baby, aaangh, aaaaiii!" alipiga kelele mwishoni baada ya SM kuzama ndani mazima na kuhisi kama kizazi chake kimeguswa kwa jinsi kijana huko alivyogonga ukuta wa ndani ya tupu ya Suzy kisha akamwambia kuwa ngoja nikubadilishie dizaini. Aliposema hivyo akampindua na kumuweka mtindo ambao haaumizi na kuanza kumuendesha kwa taratibu na kwa ufundi mkubwa hadi Suzy akabadili milio, badala ya kulia kwa kumuomba amalize sasa akawa anaomba apewe zaidi ya hapo alipofikishwa na muda mwingine akawa anaomba apewe wote. Sex machine, hakufanya ajizi akaongeza speedi huku akiwa amezama hadi kunako mwisho. kelele za raha zikakijaza chumba hicho. Suzane akaanza kulalama.

    "asaaantee!, asante Chriss" akajikuta ametaja jina ambalo alionywa asilitaje. Hatari.



    **********************************************



    Kwa upande wa Joesan naye usiku huo alikuwa akipewa mambo adimu na matamu kabisa na Merina. Mtu ambaye kwa upande mwingine ni mlinzi wake wa karibu (Bodgad) lakini kwa upande mwingine alikuwa amechukua nafasi ya zaidi ya marehemu mke wake. Nasema zaidi kwa sababu, Joesan alikuwa akipewa vitu moto moto ambavyo mkewe



    alikuwa hampi. Usiku huo Joesa alikuwa akipiga kelele kama mtoto baada ya kulalishwa kitandani huku binti huyo aliyeharibiwa kimwili na Kim akiwa juu amekalia kipisi cha kiazi kitamu kwa kukikatikia kikiwa ndani ya njia haramu ya tundu la haja kubwa. Joesan alikuwa amefumba macho akiwa mdomo wazi kama mwehu kwa jinsi raha zilivyomzidia. Ilikuwa ni laana iliyokuwa ikifanyika mahali hapo lakini ilimfurahisha sana bwana huyo na kufikia hatua ya kumtukana matusi makubwa ya nguoni mkewe kwa kushindwa kumpa utamu huo. Aliona kama mkewe alikuwa anaujua utamu huo ila alikuwa hampi na aliwapa wengine. Alimtukana sana kila alipokuwa akiipata nafasi ya kufanya hivyo.

    "kwanini ulichelewa sasa kuja kunipa mambo haya we mwanamke, ona sasa ulivyokuwa mtamu hadi najikuta naota njozi nikiwa bado sijalala" alisema Joesan.

    "oouh! Shit, kila....kila jambo huja kwa wakati wake mume wangu. Huu ni wakati wake na ndiyo maana niko hapa leo kukupa haya mambo. Ngoja sasa nikufikishe mwisho wa safari ili tulale." alisema Merina kwa sauti ya puani huku akibana makalio yake na kuyaachia kwa utundu wa hali ya juu sana. Hali hiyo ilimfanya Joesana ahisi kitu cha hatari sana hadi akawa ananyanyuka na kutaka kukaa lakini hakuthubutu kufanya hivyo. Mikono laini ya Merina ilimrudisha pale kitandani. Alipiga kelele kubwa sana akiwa anamaliza haja zake huko huko kunako ushetani. Ama kwa hakika Merina alikuwa fundi na Mr. lee alifanikiwa kumharibu binti huyo kwa kiasi kikubwa sana. Walijikuta wakilala kila mmoja akiwa hoi.



    Kwa upande wa Suzane na SM, mambo yalikuwa tofauti kido japo walikuwa wamesha maliza mchezo wao wa raha lakini Suzy alikumbana na maswali ya kuwa Chriss ni nani. Kitu ambacho alikikosea binti huyo mahali hapo ni kujiumauma na ilikuwa ni lazima ajiume ume kwani swali hilo liliulizwa kipindi ambacho utamu ulimzidia na SM alifanya hivyo makusudi ili kupata ukweli wa jina hilo pia ukizingatia kuwa alikuwa katika upelelezi wa kujijua yeye ni nani. Kwani hakukubali kwa haraka kuwa eti, yeye ni Sex Machine na hilo ndilo jina lake.

    "samahani sana SM, sikuwa na maana ya kumtaja huyo mtu nikiwa na wewe hapa, ila kwa jinsi ulivyokuwa ukinifanyia hapa kitandani nimejikuta tu nikimtaja mtu huyo. Alikuwa ni mpenzi wangu na nilimpenda sana na yeye pekee ndiyo alikuwa akiweza kufanya utundu kama wako" alijitetea Suzy lakini kwa uelewa wa Chriss akawa anamashaka na majibu ya msichana huyo. Hakuwa na muda wa kuendelea kumuuliza maswali alichokifanya ni kufunika kombe mwanaharamu apite lakini ndani ya ubongo wake kukiwa na methali isemayo, ukitaka kumjua mchawi mpe mtoto au mpe mwana akulele. Kwani atakula nyama za wenzake ila ikifika zamu ya kutoa nyama yeye hapo ndipo utakapoona ........



    mapenzi kwa mtoto wako yatakapo zidi, hivyo alichokipanga Chriss ni kuzidisha utundu na ufundi kwenye mwili wa huyo msichana hadi atapike kilichokuwa siri. Na kwa ajuavyo vifua vya wanawake, hakuwa na shaka juu ya hilo kabisa. Wakaachana na hilo na kuhamia kwenye story nyingine huku Chriss akimsahaulisha kabisa huyo binti kuhusu hilo jina.

    "SM pamoja na kwamba nimekuja kuburudika na wewe mpenzi wangu, pia kuna kazi ambayo imenileta" akasema Suzane.

    "kazi gani?" akauliza SM. Suzane hakusema kitu bali alijiteremsha kitandani na kuchukua kibegi chake cha mkononi na kumgeukia na kumwambia kwa utulivu.

    "kesho jiandae. Nimeambiwa hivyo tu na boss sasa sijui ujiandae na nini" alipomaliza kusema hivyo, akatoka humo ndani na kupotea gizani usiku huo.



    Asubuhi baada ya kunyoosha mwili na kujimwagia maji, alichukua ulekeo hadi lilipo kabati lake akiwa uchi na kulifungua hilo kabati lililopo hapo ukutani. Akabonyeza kitufe kidogo kilichopo kwenye vazi hilo ambalo huwa halifuliwi hata kidogo. Akalipa mgongo kisha vazi hilo likajivika lenyewe mwilini mwa kijana huyo. Kilichofuatia hapo kilikuwa ni kutinga suti yake kisha akatoka akiwa na brifcase yake mkononi. Alipofika nje ya uzio wa nyumba hiyo, alikuta gari ndogo ikiwa inamsubiri, akaisogelea na kujiingiza garini. Safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza. Alitakiwa kufika uwanja wa ndege na bosi wake bila kujua kinachompeleka huko. Hawakuongea kitu chochote kingine humo ndani zaidi ya salamu. Ukimya ulidumu hivyo hadi walipofika uwanja wa ndege wa hapo Morogoro. Joesan na kampuni yake hawakuwa wakijua ni nani mvujishaji wa siri za kampuni hiyo, kitendo hicho cha kuto kujenga imani kwa kila kitu ndicho kilichopelekea Hata gari wanayosafiria wasiiamini. Ukimya huo ulikuja kuvunjika baada ya kushuka kutoka garini ndipo walipokaribiana na kuongea kwa sauti ya chini sana.

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Kuna kazi nne Sex machine, zote unatakiwa uzifanye ndipo urudi hapa nchini Tanzania. Moja utaifanya ndani ya V Ice Hotel, ambayo iko ndani ya jiji la Miami nchini marekani. Hapo utakwenda kukutana na tajiri mmoja lakini ni babu, namaanisha ni mzee sana huyo. Huyu ni shoga wa muda mrefu na kwa umri alionao ni kwamba kwa sasa anajishtukia kufanya shughuli hizo za kishoga na kuamua kuifanya kazi hiyo kwa siri sana kwa sababu tayari iko kwenye damu na kuiacha hawezi. Amekuwa akiikosa huduma hiyo kwa muda mrefu sana na amekuwa akijisikia vibaya kwa kukosa kusuguliwa kwa muda mrefu sasa. Amesema kuwa muda mwingi amekuwa akijichua mwenyewe sasa anahitaji kulipata joto halisi, hivyo kwa kukubali kwetu kumpa mtu wa kumhudumia, ameahidi kulipa mamilioni ya shilingi, Huo ni utajiri SM. Usiangalie mtu huyo alivyo, maana kama utamuangalia ni wazi mchezo unaweza kukushinda maana ni kikongwe siyo siri, pia anahiji usalama wa hali ya juu sana kutoka kwetu na ndiyo maana tumekuja kuongelea hapa sisi wawili. Kazi ya pili." akanyamaza kidogo Joesan na kuvuta pumzi kidogo kisha kujiminya pua kwa juu na kuendelea.

    "kazi ya pili ni ya mkuu, hii ni ya kumuondoa duniani mzee mmoja anayekwenda kwa jina la Milkao. Kama unavyojua kuwa vita ya mkuu ni kuhusu wafanya biashara. Kinacho nipa ugumu na wasiwasi wa kazi hii ni kwamba Hoteli utakayofikia kwa ajili ya kuifanya kazi hii ya kuuwa, ndiyo hoteli utajayoitumia kuifanya kazi ya tatu. Namaanisha nini? Ni kwamba kazi ya tatu ni kwenda kufanya mauwaji mengine ya meneja wa hiyo hoteli. Sasa sijui utaanza nani kati ya meneja na mzee Milkao japo haina uhakika sana kama huyo Milkao atafika katika hoteli hiyo akini wote wanatakiwa kufa. Kazi ya nne na ya mwisho ni yangu binafsi, hii inajulikana ni ya kwenda Ufaransa kuchukuwa nzigo na kuupeleka nchini Brazil kama kawaida. Mzigo ni uleule kilichoongezeka ni ukubwa tu wa mzigo huo. Huu ni mzigo mkuwa sana wa chupa hamsini za DF. Ni utajiri mkubwa pia. Nakuahidi SM, ukirudi salama ukiwa umefanikisha kusafirisha huo mzigo, kutembea na huyo shoga kikongwe pia kuuwa hao watu wote wawili, utajiri wa pesa nyingi sana unakuhusu na mkuu atakufanyia paty maalumu lakini pia kama moja kati ya hayo yatashindikana, pia utakuwa hujabadili kauli niliyoisema." Alimaliza kuongea bwana huyo na kumruhusu SM aondoke muda huo kuelekea ndani ya ndege ambayo ilikuwa tayari kuondoka kuelekea Dar es salaam. SM alijitia ndani ya ndege na ndege hiyo ikaanza kuchukua kasi. Ilikuwa ni ndege ndogo ya shirika la Emirates.



    Dakika chache zilitosha kumfikisha SM ndani ya uwanja wa kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere. Aliteremka na kubadilisha ndege. Hapo ndege kubwa ya kitanzania ikachukua kasi na kuingia katika barabara maalumu kwa ajili ya kuruka. Muda mfupi ndege hiyo ikawa inaiacha ardhi ya Tanzania na kulikamata anga la kimataifa. Alipokuwa angani, SM aliwaza mengi sana, alifikiri jinsi majukumu yanavyozidi kuongezeka hadi akafikiria kuwa sasa watu hao wanampango wa kumuuwa. Lakini wakati akiwa anawaza, Nairobi kenya kwenye mtaa wa Ruiru, ndani ya jumba lile la Father D.A, tunamuona Catherine akitoka mbio chumbani kwake akiwa amekamata simu yake mkononi na kwenda hadi sebulenu ambako alimkuta Father akiwa anacheza na Maria.

    "ooh, unashindwa hata kurusha mpira ili kuupiga, halafu unasema unataka kuwa mchezaji hodari wa tenes" alisema father alipokuwa anamuelekeza Maria jinsi ya kupiga mpira wa tenes.

    "hapana babu nilikose.......!" alishindwa kumalizia Maria, sentensi yake ikabaki kuelea hewani. Sauti ya Catherine iliyokuwa ikimuita father, ndiyo iliyokuwa imemkatisha majira hayo.



    "father hebu sikiliza hii sauti" aliongea Catherine huku akimkabidhi father D.A zile ear phone na kuziweka masikioni na kuanza kusikiliza. Alisikiliza kwa muda alipomaliza, akamfuata Maria na kumwambia aelekee ndani kwani muda huo muvi yake nzuri ya katuni ilikuwa imeanza. Maria alitoka hapo mbio na kuelekea ndani, alikuwa akihusudu sana katuni Maria na aliipenda kuliko michezo mingine hivyo hata kama yuko kwenye mazoezi ya kufundishwa Tenes lakini akiambiwa tu kuwa katuni imeanza ni lazima ataacha na kukimbilia ndani na mara nyingi akiikosa anaweza hata kulia.



    Walibaki wenyewe mahali hapo. Akiwa tayari ameshaisikiliza hiyo sauti na sauti hiyo ilikuwa ni yale maongezi ya Joesan akimpa SM pale uwanja wa ndege wa Morogoro ambayo yalisafirishwa kitaalamu sana kupitia lile vazi.

    "tunafanyaje sasa Catherine naona hii imekuwa too much aisee na kwa ulinzi ulivyo wa hapo Marekani na askari wa marekani walivyo makini Huyu kijana atakufa." alisema fadha mara baada ya kumuondoa Maria kijanja mahali hapo.

    "father, mimi naingia katika biashara na hawa wajinga...!"

    "kivipi?" akawahi father kwa swali.

    "naingia kwenye mtandao wao wa kibiashara na kuhitaji hiyo huduma najua watakataa kama nitaenda kwa dau dogo lakini kwa dau nitakalowatangazia na kuwalipa bakshishi, lazima wataingia mkenge. Ni dau kubwa sana father ambalo hawajawahi kulipata kwa huyo Sex machine kutembea na mwanamke. Mimi nitakuwa wa kwanza, na yule mzee anatamaa sana atakubali tu na kuingia kwenye hii biashara, akiingia tu basi kazi ni nyepesi"

    "itakuwa ni wapi sasa" akauliza tena father.

    "ni hapo hapo Marekani na ni kabla hajatekeleza mauwaji ya huyo Milkao na meneja wa hoteli" aliongea Catherine mamaa mipango, au waweza kumuita bikini nyekundu.

    "lakini unahakikisha hashiriki hata kazi moja ya mauwaji au?"

    "hapana hayo mauwaji ni lazima atekeleze na nitamsaidia mimi kufanya hayo mauwaji ili aniamini niweze kuondoka naye kiurahisi hadi shimoni huko atakwenda kubadilishwa na kuwa Roi na si Sex machine wala Chriss. Atarudi kwenye jina lake la zamani la Rajab Isihaq na kumpa jina la kulipiza kisasi cha baba yake na ndipo nitakapompa jina hilo la Revange Of Isihaq (ROI). Baada ya hapo anakwenda kumaliza kazi ya mwisho ya kuubeba mzigo wa Madawa ya kulevya ya FD na hapo ndipo tutakapokwenda kuanza kazi ya kuwachonganisha kisha Roi anarudi nyumbani kuja kumsalimia Mery madhani hata yeye atakuwa amemmiss" alipomaliza kusema hivyo, kicheko kikubwa kikaibuka kutoka kwa Father. Ilikuwa ni plan ambayo hakuitegemea kabisa katika maisha yake. Father alikubali kuwa anakichwa cha hatari na akimrudisha na Roi nyumbani, basi hapo atakuwa na vichwa vikali mno.

    "anza kazi Catherine muda umekwenda sana kumbuka unatakiwa uwahi kabla huyo ndugu yako hajafanya huo uharamu"

    "usiogope father leo ndiyo nitatumia zile ndege zinazokwenda kwa kasi sana ili kuwahi ndani ya Marekani kabla hata Chriss wao hajatua na atamkuta huyo kikongwe ni maiti tayari" alisema hivyo kisha akaingia chumbani kwake na kwenda kufanya mawasiliano na kampuni ya Joesan.

    "mr. Lee wewe ni mshenzi sana. Najua unatimu ya mpira uliyoiandaa ili siku moja uje kuniangamiza kwa magoli mengi bila mimi kupata kitu, nikupe salamu za hisia tu huko uliko Roi ni mwanangu nasema hivi kwa sababu Roi ni mtanzania na mimi pia ni mtanzania, kifo cha mtanzania mwenzangu lazima kilipwe na damu ya kijana wake. Sina shaka na Joesan kwani huyo ni mtoto mdogo sana na huyo mlinzi wake atamalizana na Catherine maana Roi ndio daraja lako wewe. Mimi hutaniona hadi siku unakufa wewe." aliwaza father na kufanya ishara fulani ikiwa ni imani za Ki Buda iliyochanganyikana na Budha Tempo kisha akafumba macho yake na kuipandisha mikono yake aliyoikutanisha pamoja hadi karibu kabisa na paji lake la uso. Ilikuwa ni nguvu njingi iliyokuwa ikitumika hapo na hisia kali za kiimani kutoka kwa father D.A akiwa anamtumia salamu mr. Lee Kim. Alitulia hivyo father kwa takriban dakika moja na sekunde tano. Muda huo huo kwa upande wa Mr. Lee ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi kidogo sebuleni kwake ndani ya 03 house, alishtuka kutoka ndani ya usingizi huo, alinyanyuka kabisa na kutoka pale kwenye kijigodoro alichokuwa amekitandika chini na kwenda kusimama kwenye dirisha kubwa la nyumba hiyo.

    "D.A nini unataka kufanya kwangu, unasema unataka kurudi Tanzania, ooh my God!" ............................



    aliwaza mr. Kim akiwa hapo dirishani.

    "umeamua kujitokeza sasa eenh! Mbona bado sijamaliza kazi yangu ya kuingiza utajiri mkubwa ili nikifika nchini kwangu niwe kama mfalme? D.A, hapana bado ni mapema sana na sitakubali nishindwe lazima niingize utajiri mkubwa kwa kuwatumia watanzani wenzako wajinga kama wewe" alizidi kuwaza mr. Lee.



    "ha ha haaa, aaha ha ha haa!" ni salamu tu hiyo mbona picha linaanza" alicheka sana Father na kusema maneno hayo mara baada ya kutoka kutuma salamu kwa imani za ki tempo. Alijua kuwa kwa salamu hiyo ni lazima mzee mwenzie atakuwa katika mashaka makubwa kabisa, haukuwa uwongo, Kim alijikuta akiongea mwenyewe mithili ya mwendawazimu. Alipokuwa anazidi kuwaza hapo na kucheka, alishtuliwa na sauti ya kushangilia na alipo geuka nyuma Father, alimuona Catherine akiwa tayari amependeza na kibegi chake cha kike mkononi. Father akaunguruma kama dume la njiwa na kusema.

    "mambo yameiva bila shaka maana nakuona uko ki mtoko?"

    "nilikuambia father kwa watu kama wale ambao hawajaridhika na pesa hawezi kukataa dola milioni moja kwa kazi ya kumnunua Sex machine na tayari wamekwisha kuwasiliana na mtu huyo kulingana na mashart yangu kuwa nafanya hiyo kazi kwa siku fulani kisha nikawaroga na dola laki tano ambazo tayari nimeshapiga simu bank na kutoa kontact zote hiyo pesa wahamishiwe kwenye akaunti yao, Wataishia hiyo hiyo na kupata pigo wasilolitarajia." alimaliza kusema Catherine kisha akatoa simu yake na kupiga mahali akaiweka sikioni.

    "nahitaji mtoto mzuri wa anga anipele Kwa Obama haraka sana" alisema na kutulia kidogo kisha akaishusha simu hiyo na kuiweka kwenye mfuko wake wa suruali ya jeans aliyovaa ambayo alikuwa ameunganisha na visikilizia maaikio, kisha akampa mkono wa kwahe mzee huyo na kumwanmbia ndege ya haraka imepatikana.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "kwa muda huu ninavyojua mwendo wa ndege hizo ni lazima utafika sawa na SM huko Marekani" aliongea father.

    "haitajalisha hata hivyo, mimi nitakuwa haraka zaidi kuliko yeye kwasababu ya kuwahi kuuwa kabla yake."

    "mwambie Roi nipo nyuma yake"

    "ubaki salama na umwambie Maria namletea kaka yake" alimaliza kusema hayo na kuingia kweye gari ambayo iliondoka hapo kwa kasi sana kuelekea kwenye uwanja wa ndege wa Kenyata. Dakika chache zilimfikisha hapo uwanjani na kuelekea moja kwa moja ambako kunahusika na usafiri binafsi, huko akaenda kukuta ndege kubwa ya kukodi yenye muundo kama wa air force. Akafanya kinachotakiwa kufanywa kisha akakwea pipa hilo na safari ikaanza. Ni mwendo wa kasi sana ilikuwa ikitembea kuelekea mahali ambapo ilitakiwa kupaa na sekunde kadhaa mbele, ndege hiyo ikainuka na kuelekea mawinguni.





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog