Search This Blog

Monday, October 24, 2022

JAMANI ANTIII…NISHUSHE UNUNIO - 4

 







    Chombezo : Jamani Antiii...Nishushe Ununio

    Sehemu Ya Nne (4)



    “Nini tena mshikaji wetu? Nini kimekukuta wangu?” Darwin mmoja wa wafanyakazi wenzake na Bigambo ambaye kwa umri alikuwa mtu mzima licha ya mwili wake kuonekana kijana alimfariji kwa upendo mkubwa na kutoka moyoni mwake, hata Bigambo mwenyewe hakuwa na shaka na upendo wa Darwin.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/





    “Matatizo kaka, si unajua dunia hii, kuna jambo kubwa sana limenikumba na sijui nitalimaliza vipi lakini kwa kuwa Mungu ni mwema naamini kila kitu kitakwenda sawa kabisa,” Bigambo alisema lakini katika hali ya kushangaza kuna walioanza kumsema kwa maneno makali ya mafumbo huku wakimlaumu kwa kujiingiza kwenye mapenzi na mtu asiyemjua, wakiamini kabisa kwamba Bigambo analia kutokana na kukumbwa na matatizo ambayo yalisababishwa na Vivian.



    Kufumba na kufumbua, Vivian alijiweka sawa tayari kwa kuruhusu mechi ianze kuchezeka. Kuona hivyo, Bigambo alijiweka sawa na kumgeukia Vivian. Akanyoosha mikono na kuyaparamia maembe mawili na kufanya kama anayebonyeza ili kuona kama yameiva na yanafaaa kwa kuliwa.



    Vivian aliruka na kutoa kilio kilichomfanya Bigambo aangue kicheko cha nguvu.



    “Unacheka nini sasa jamani,” Vivian alilalamika huku akijinyonga kiaina, staili ya kumshika kwenye matunda aliyoitumia Bigambo ilikuwa ni ya kipekee mno, kiasi cha kumchanganya vilivyo Vivian, mwanamke kutoka Mbeya mwenye umbo na muonekano matata kabisa machoni kwa kila mwanaume rijali mwenye kujua matumizi sahihi ya watu wa aina hiyo.



    “Kwani kucheka ni dhambi jamani V?” Bigambo alijibu swali la kwa nini alikuwa akicheka, lakini hakuishia kwa kujibu swali pekee badala yake alipeleka tena mkono na awamu hii alizungusha hadi sehemu ya nyuma ya Vivian, juu kidogo ya lile eneo la kukalia na alitumia vizuri vidole vyake alijikuta akishika vitu vigumu vilivyopangwa kwenye mstari maalum.



    “Aaah, wewe B…!” Vivian alizidi kulalama akijitingisha palepale kitandani, wakati huo chupa za bia vinywaji vyao vilikuwa bado mikononi, kwa maana kwamba utundu wote aliokuwa akiufanya Bigambo kwa Vivian, alitumia mkono mmoja kuleta mateso hayo yote.



    Ikafika mahali Vivian akaanza kujisikia vibaya sana. Lile agano la kutofanya chochote pindi wakifika ndani lilianza kuyeyuka ubongoni na sasa mwili wake ulianza kuhitaji kushikwashikwa kwa maeneo yaliyohitajika kushikwa.



    “Lakini kumbuka ahadi yetu Bigambo,” Vivian alichombeza kutoka moyoni, maneno hayo hakumaanisha, bali ilikuwa ni ile hali ya kujitetea heshima yake asionekane kulegea kirahisi.



    “Ahadi gani tena…?” Bigambo aliuliza akiweka chupa ya kinywaji mezani na kumtazama mzimamzima Vivian ambaye naye aliweka chupa ya Savanna mezani na kubaki kimya akimtazama Bigambo kwa lile jicho la pembeni na kusindikiza kwa tabasamu laini na kuyaacha meno yake ya mbele yaliyoungua kidogo yaonekane sawia kwenye mboni za macho ya Bigambo.



    “Si hatufanyi?”



    “Nini?



    “Haa, jamani kwani wewe si unajua kabisa mwanaume na mwanamke hufanya nini wanapokutana chumbani wakiwa wawili na kama hawana undugu wowote?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Mimi sijui, kwani humu tumekuja kufanya nini?”



    “Bigambo bwana, hebu acha mambo yako…”



    “Mambo gani tena…?”



    “Wewe si umesema tunakuja kuzungumza kwa uhuru?”



    “Sasa si ndiyo hivi au kuna uhuru zaidi ya kuzungumza hivi?”



    “Sawa, lakini nasisitiza tu kwamba tusifanye chochote.”



    “Nimekuelewa, lakini tunaruhusiwa kugusana kwa maana ya kukushika mfano mkononi au kichwani…?”



    “Yaani wewe, sasa kunishika huko kichwani unatafuta nini kama siyo uchokozi wa kuamsha mambo mengine ya kuwekana majaribuni?”



    “Noo, si naweza mfano kuwa nasifia unadhifu wa nywele zako jinsi zilivyolala kwa mpangilio mzuri?”



    Hapo sasa Vivian alinyamaza lakini kunyamaza kwake kulikuwa ni kujiuliza mara mbilimbili kama akaze kikwelikweli au alegeze kiaina na mchezo baina ya Yanga na Singida United ichezwe na kila mmoja aondoke zake.



    “Haya bwana, siwezi kukuzuia maana una maneno mengi kama mbunge wa kuteuliwa…,” Vivian alianza kulegeza na kujiachia kiuhuru sasa, lakini hakuacha kusisitiza kutofanya mchezo wa maigizo wafanyao watoto wadogo wanapocheza.



    “Sibadili msimamo wangu, hatufanyi…,” alikazia Vivian huku akijiachia kwa kulala chali kitandani, ingawa hakuwa amevua nguo yoyote. Kitendo cha kulala chali kulisababisha eneo la mbele kuonekana vizuri kitendo kilichomfanya Bigambo alambe midomo kwa ubembe wa kimahaba na uchu.



    “Ila…,” Bigambo alisema na kuishia njiani.



    “Ila nini tena Bigambo…?”



    “Umependeza sana…”



    “Kwa lipi?”



    “Mfano hili hapa eneo la mbele…,” Bigambo alisema huku akiweka mkono wake wa kulia juu ya kisima cha burudani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Ooh, wewe Bigambo jamani…,” Vivian aligutuka na sasa aliinuka na kulegea zaidi, ambapo alilala tena na kunyoosha miguu yote, lakini Bigambo hakuondoa mkono wake eneo hilo na badala yake alianza kutumia utundu zaidi kwa kupapasa kwa mikogo, hali iliyomfanya Vivian arukwe na akili, mwisho wa siku aliamua liwalo na liwe.



    Sasa alimgeukia vizuri Bigambo na yeye kumrushia mashambulizi. Alianza kushika maeneo mbalimbali, hali iliyomfanya Bigambo kuanza kujikunja na kuwewesekea kitendo hicho. Ikafika mahali hakuna aliyewaamuru wachojoe magwanda yao lakini kila mmoja alijikuta akijiamrisha mwenyewe.



    Joto la miili yao lilikuwa limepanda na kufikia kiwango ambacho kama ni mgonjwa wa malaria hali ilikuwa mbaya sana. Wote walibaki kama walivyokuja duniani na Bigambo alimfuata Vivian.



    Bigambo alipeleka kinywa hadi kwenye papi za mdomo wa Vivian, ambaye midomo yake ilikuwa na lipsi nene na zenye kuvutia zaidi. Vivian alilala kwa mtindo wa kuhesabu mabati, Bigambo kuona hivyo, akiongozwa na mhemko wa kilevi alichokuwa ameshindilia, alianza kuyakabili matunda ya mwanamke huyo ambaye kwa wakati huo alikuwa akihema kama bata dume aliyetoka kupambana na mwenzake.



    Hakuishia hapo. Bigambo alitoa ulimi na kuanza kufanya utalii kwenye maeneo mbalimbali ya mwili wa Vivian aliyekuwa akiendelea kuhema huku akifumba na kufumbua macho. Ulimi wa Bigambo ulianza na eneo la juu ya kila tunda la Vivian, sasa ilikuwa ni zamu ya vile vikonyo viwili kabla ya kuhamia chini yake, mahali ambapo matunda mawili yalikuwa yamelalia.



    Vivian aliendela kujitikisa kwa kufuatisha msisimko uliotokana na utalii wa ulimi wa Bigambo mwilini mwake. Ikafika mahali ulimi ukavuka mipaka, kitendo kilichomfanya Vivian kuanza kuropoka.



    “Bigambo…”



    “Naam…”



    “Unajua sana jamani baba.”



    “Kufanya nini?”



    “Kunipa raha, unaniweza sana jamani…,” Vivian alijieleza kwa maneno yote matamu aliyoyajua lakini Bigambo hakusitisha suluba zake ambapo sasa alianza kutumia jembe lake kumuadhibu Vivian.



    Ikafika mahali alishika jembe lake na kuanza kulima kwa fujo zote kama vile kibarua aliyeoneshwa pesa na kuambiwa anza kulima na umalize ndani ya nusu saa, alianza na eneo la mgongo, kabla ya kushuka kiunoni na kuyagusa mapingili ya nyonga.



    Vivian alishindwa kuvumilia, bila kuamrishwa alijiweka sawa mwenyewe na kumtaka Bigambo aanze kulima shambani kwake kwani msimu wa mvua ulikuwa umeshaanza na maji yalikuwa ya kutosha kwa mpunga kustawi vizuri. Bigambo hakuona shida kufanya hivyo, sasa alijiweka mkao mzuri wa kulima kwa ustadi shambani kwa Vivian.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Mtanange ulikuwa wa kukata na shoka. Timu zote mbili zilikuwa zikishambulia lango la timu pinzani kwa nguvu na pasi za kushtukiza. Ikafika mahali Vivian alichoka na kuruhusu mashuti kadhaa yatikitise nyavu za golini kwake.



    Dakika 47 baadaye, wote wawili walijikuta wakitangaza kufika mwisho wa miti ya minazi na sasa walialikana kupasua madafu pamoja. Kwa upande wa Bigambo lilikuwa dafu lake la kwanza kupasua tangu waanze kazi ya kukwea minazi lakini kwa upande wa Vivian lilikuwa kama dafu la nne na viungo vyake vyote vilikuwa hoi hususan miguu ambayo hutumika zaidi kwenye zoezi la ukweaji wa minazi.



    “Nafika…,” Vivian alianza kutangaza kwa sauti ya kupayuka huku akihangaika mwili mzima ili ashike vizuri asije akaanguka na badala ya kuvunja dafu iwe stori nyingine.



    “Umefika wapi mama…?” Bigambo alihoji lakini kabla hajajibiwa naye alianza kusikia kitu cha tofauti na sasa alianza kukoroma huku akikunja sura na hapohapo alianza kuropoka kwa sauti yake ile mbaya.



    “Oooh, mama nami naelekea kupasua daaaafuuuu…,” Bigambo aligugumia na hapohapo alizidisha kasi ya ukweaji na kulishika dafu moja kabla ya kuliachilia na kulipasua kwa hasira kali, kitendo kilichomfanya Vivian naye apasue la kwake wote kwa pamoja walijikuta wakihitimisha safari kwa wakati mmoja, lakini kufumba na kufumbua Vivian alianza kuonesha jambo ambalo hata Bigambo lilimshangaza kwani hakulitegemeaa, lakini wakati huohuo mlango ukawa unagongwa kwa fujo kali sana.



    BIGAMBO alijivika ustaarabu ambao hakuwa nao na lengo likiwa ni kumpumbaza Vivian, ili atoe ushirikiano ambao ungeleta matokeo chanya kwa mpambanao huo wa watani wa jadi. Bigambo alimfuata Vivian mahali alipokuwa amelala na kuanza kumfanyia fujo zote ambazo hufanyiana wapendanao pindi wanapokutana kwenye eneo walilokuwepo Bigambo na Vivian. Vivian naye alimpokea na safari hii alimlalia kwa mtindo wa kawaida, aliweka kichwa maeneo ya kiuno na akawa kama anakibilingisha kichwa, hali iliyopelekea hali ya Bigambo kuanza kubadilika.











    Vivian hakuishia hapo, akajisogeza kwa mbele zaidi na wote wawili kujikuta wakitazamana usoni. “Baby…” aliita Vivian wakati huohuo mkono wake wa kushoto ukikiparamia kifua cha fundi kilichokuwa wazi na kuiacha bustani ionekane kwa uwazi na ukubwa wa kumezesha mafunda ya mate. Vivian hakuishia hapo, akakiruhusu kiganja kutembea bustanini kwa Bigambo huku vidole vyake laini vikitalii kwa umaridadi mkubwa kabisa kwenye vichuguu vifupi viwili, mahali ambapo marhani ya Bigambo yalikuwa.







    “Mmm…,” aliguna Bigambo kwa mtindo wa kufyonza muwa mtamu… “Oooh, yes baby…,” Vivian alichombeza kwa maneno laini na kuyafumba macho kwa maana ya kuhamasisha zaidi. Hali ya Bigambo ikazidi kuwa mbaya, kama ni kuharibikiwa sasa ilikuwa kwa kiwango cha kuhitaji msaada kamili na si maneno matupu. Kuona hivyo, Vivian akazidisha mbwembwe. Akafumba macho na kukisogeza kinywa karibu na kile cha Bigambo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/







    Bigambo naye akalegea kwa maana ya kumpokea Vivian kwa mtindo huo. Wakasogeleana na kuanza kushiriki pamoja kutafuna miwa ya Kilombero. Walizama kwenye kutafuna miwa kwa muda wa zaidi ya dakika kumi na tano, kila mmoja akionesha ufundi wa namna ambayo miwa mitamu huliwa. Vivian alizidisha manjonjo, akawa akajikunjakunja kwa kuweweseka kimahaba zaidi, ikawa mara akunje miguu na wakati mwingine ainyooshe kama anayejipima urefu, ilimradi kuonesha namna ambavyo alikuwa amekolea kwenye dimbwi la uhondo wa kilichokuwa kikiendelea. Bigambo hakuwa nyuma. Naye aliamua kupeleka mashambulizi kwa Vivian, tena yalikuwa yale ya kushtukiza kwa lengo la kumvizia adui akiwa amejisahau. Bigambo alipeleka mkono mmoja na kuyavamia maembe bolibo ya Vivian na kuyashika kama anataka kuhakikisha yameiva au la… Hakuishia hapo, akalishika embe moja na kumtupia mdomoni huku lile jingine akiendelea kulifanyia visa vya kichokozi…







    Vivian akashindwa kuvumilia.

    Sasa akajiachia kwa uhuru, akakaa mkao ambao ulimpa uhuru Bigambo kuonesha utundu wake zaidi ya huo. Kuona hivyo, Bigambo akaona isiwe tabu zaidi ya kupania kuonesha ufundi maridhawa, akamfuata Vivian na kumuweka vyema. Kufikia hapo, Vivian alikubali kutoka moyoni kabisa kwamba Bigambo ni mtaalam kwenye eneo la kusakata kabumbu hususan kama mechi yenyewe imewakutani







    sha watani wa jadi ambao kila mmoja hutazama sana ushindi wa pointi na si wingi wa vyenga kama ambavyo wengi hudhani. Walicheza gwaride hadi kila mmoja akaridhika na mwisho wa siku wakakubaliana kuondoka eneo hilo kwa kuwa Vivian alikuwa na ratiba ya kukutana na mtu nyumbani kwake, huku Bigambo akitarajia kwenda kufanya kazi zake binafsi. “Lakini baby,” Vivian alisema huku akitafuta mahali zilipokuwa nguo zake. “Vipi mama.” “Wewe ni kiboko.” “Kwa nini?” “Si kama hivi, kwanza sikuwa na mpango kabisa wa kufanya chochote lakini umetumia utundu wako wote kuhakikisha najikuta nikiingia mchezoni, hakika umeniweza.” “Kwa hiyo umecheza gemu kwa kulazimishwa?” “Sijamaanisha hivyo bwana.”







    “Sasa kumbe?” “Mwanzoni sikutaka kwa kweli, lakini ushawishi wako umesaidia sana hadi nikajikuta nikifurahia maandalizi na hatimaye namna ambavyo mchezo mzima ulivyokwenda,” Vivian alisema na hapohapo akawa anamalizia zoezi la kuvaa na kumsubiri Bigambo amalize ili waweze kutoka pamoja kabla ya kuachana na kila mmoja kuangalia njia na ratiba yake. “Sasa?” Bigambo alimuuliza

    Vivian ili kusikia kama kuna lolote anaweza kumueleza baada ya kumaliza kusakata mechi hiyo bora kabisa ya ghafla ambayo hakukuwa na mchezaji aliyekuwa akifikiria suala hilo zaidi ya makocha wa pande zote mbili ingawa nao hawakuwa na mawasiliano ya karibu juu ya mechi hiyo ambayo wengi hupenda kuiita kwa jina la Dabi. “Wala sina cha kusema labda kama nitapata nauli tu ya kunitoa hapa kwa pikipiki hadi nyumbani kwangu, mengine tutaongea kwenye simu nikifika, lakini kusema ule ukweli umenionesha mchezo bora kabisa kwa siku ya leo ambao sitausahau maishani mwangu,” Vivian alitiririka mfululizo na kumfanya Bigambo aishie kutabasamu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/







    Bigambo aliingiza mkono mfukoni na kutoa noti moja nyekundu, kisha kumpatia mkononi Vivian, lakini staili aliyotumia kumpatia ni ile ya kufumbata pesa na kumpenyezea kiganjani bila kumpa nafasi ya kutambua ni kiasi gani, kwa hiyo Vivian aliipokea na kuitia mkobani bila kujua ni kiasi gani, lakini moyoni aliamini ni pesa inayotosha kwenye nauli ya pikipiki kwani tangu wanafahamiana alimjua Bigambo si mtu wa kubabaisha na mhuni wa mjini na kama hana kitu huwa hawezi kudanganya na kujifanya mwenye nacho kama wafanyavyo vijana wengi wa mjini wakiwa na lengo la kumpata mwanamke wamtakaye. “Jamani wewe cha utundu sana,” Vivian alisema na kumkumbatia tena Bigambo ambaye alitumia nafasi hiyo kumchumu mashavuni huku mikono ikizunguka kwa kasi ya umeme na kulifumbata umbo zima la nyuma ikiwemo ile milima mikubwa miwili ambayo ndiyo silaha kuu ya Vivian kuwadatisha wanaume wengi wa mjini wapenda starehe ya kuruka uwanjani bila jezi.







    “Aaah, wewe jamani mbona hivyo B?” Vivian alilalamika kwa mtindo wa kudeka na kumfanya Bigambo atumie haraka sana kiganja chake kumminya eneo la nyuma ambapo alizidi kumpa uchizi tena Vivian aliyeanza kulegea macho na kusinzia kwa mbali,

    licha ya kwamba walikuwa kwenye maandalizi ya kuondoka chumbani humo ili waendelee na ratiba zingine. “Basi mama, pole sawa mrembo mzuri?” Bigambo alichombeza kwa maneno matamu na laini kisha kujiondoa mwilini mwa Vivian na kuufuata mlango ambapo aliufungua na kumpa ishara Vivian atangulie kutoka kabla yake. Walitoka, lakini kwa kuwa ilikuwa ni usiku, hawakuona tabu kushikana mikono na kuongozana hadi eneo la maegesho ya pikipiki. “Kiasi gani hadi Kibangu?”



    Bigambo aliuliza kwa niaba ya Vivian ambaye ndiye alikuwa mwenyeji wa huko, lakini kwa sababu Bigambo ni mwanaume alitaka kuonekana mwenye kujali zaidi kuhakikisha kila kitu kinakwenda kama kinavyotakiwa. “Kibangu ipi?” Kijana wa pikipiki aliuliza lakini badala ya kujibu, Bigambo alihamishia macho kwa Vivian ili ajibu swali hilo. “Karibu na kwa Mzee wa Upako…,” alitaja na hapohapo wakawa wameelewana.



    “Sasa Bae, mimi nakwenda maana usiku nao umeshaingia sana, nikifika tu nitakupigia kwa kuwa kuna jambo nataka nikusisitize ambalo ni muhimu sana kati yetu, sawa my…?” “Sawa, lakini unanipa kimuhemuhe kikubwa sana ni afadhali uniambie tu kabla ya kuondoka.” “Acha mambo yako bwana, ngoja niondoke,”



    Vivian alisema huku akikanyaga mguu kwenye kigingi cha kukanyagia kabla ya kukaa vyema kwenye kiti cha pikipiki, ambapo yule kijana hakuwa na muda wa kupoteza zaidi ya kutia gia na kuondoka kwa kasi na kumuacha Bigambo akikodoa macho huku akicheka na kujisifia moyoni kwa namna ambavyo ameweza kumpata Vivian kwa urahisi na wepesi wa namna hiyo. Kwa upande wa Vivian, kichwani alikuwa na maswali mengi ambayo hayakuwa na majibu kwa wakati huo.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    KICHWANI aliendelea kujiuliza bila kupata majibu juu ya namna ambavyo amekuwa akiyarahisisha maisha yake kwa wanaume. Ikafika mahali akaamua kwa dhati kabisa kubadili aina na mfumo wa maisha yake yote.



    “Hapana, lazima ifike mahali maisha yangu yabadilike. Haiwezekani niwe nakukuruka na wanaume kila kukicha namna hii,” Vivian alijisemea akiwa amejiinamia kwenye kiti chake. Hapohapo akachukua simu na kuamua kumpigia tena Bigambo, ili kumjulisha juu ya uamuzi wake wa kuachana na wanaume wote kwa wakati huo.



    “Eeeh, Bigambo uko wapi na unafanya nini?”



    “Hee, unauliza ninafanya nini kwani vipi tena na halafu ni tangu lini tukaanza kuulizana namna hiyo?” Bigambo naye akajibu kwa ukali lakini mwisho wa siku walielewana mahali pa kukutana ambapo dakika chache walikuwa pamoja waliendelea na zoezi la kugida ulabu. Kichwani mwa Vivian alishaondoa kabisa wazo la kuachana na Bigambo kama ambavyo alikuwa amedhamiria awali. Kila mmoja akaanza kuonesha ujalifu wa kupindukia kwa mwenzake.



    Walianza kusimuliana jinsi ambavyo wamekuwa wakipitia kwenye changamoto nyingi za penzi lao tangu wakutane kwa mara ya kwanza kazini. Lakini Vivian alijishangaa zaidi kwa namna ambavyyo amekuwa akijisikia kuwa na penzi zito kupindukia juu ya Bigambo, mwanaume ambaye hakuwa na mazoea naye zaidi ya kukutana naye kazini tu.



    Mapenzi yamekuwa yakimtesa kila mmoja wao. Vivian alimwaga siri zote na namna ambavyo huwa anajisikia raha pale anapokutana na Bigambo ambaye ameonekana ni mwanaume wa kuyaweza mambo. Kwa mara ya kwanza, Vivian alimwambia Bigambo kitu ambacho hakuwahi kukiweka wazi tangu waanza safari yao ya kutoka kimapenzi.



    “Unajua ni kwa nini nilikukubalia mapema sana baaada ya wewe kunitaka kimapenzi?” Vivian alimuuliza Bigambo akiwa amemuegemea mabegani, huku mkono mmoja ukiwa kwenye glasi ya kimiminika kizito chenye rangi ya njano.



    “Hapana,” Bigambo alijibu huku naye akinyanyua glasi yake na kugida maji hayo kabla ya kukunja ndita na kumtazama Vivian usoni akisubiri jibu kwa hamu kubwa sana.



    “Kwenye mahusiano yangu ya nyuma sikuwahi kabisa hata siku moja kufika mwisho wa safari wakati wa mechi ya kikubwa, sanasana ni kwamba wanaume wengi hujijali wao tu kufika mwisho wa safari na kumuacha mwanamke akitapatapa njia panda, sasa wewe uliponitongoza nikajisemea ngoja nijaribu,” Vivian alisema mfululizo na kuongeza;



    “Lakini tulipokutana kwa mara ya kwanza uliniweza kwelikweli, cha kushangaza nimekutana na wanaume kadhaa kwa kipindi hikihiki na sikuweza kufikia mwisho wa safari na leo ningependa sana nipate tiba tena,” Vivian alisema lakini moyoni akiwa anajiwazia ni kwa nini amekuwa mtu asiyekuwa na msimamo juu ya uamuzi wake maishani.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Mimi huwa najali sana kumwandaa mwanamke kabla mimi sijajiandaa, unajua raha ya tendo ni mwanamke kuanza kufika mwisho wa safari ndipo ampe sapoti mwanaume, hakika hilo huwa nalizingatia sana,” alianza kujinasibu Bigambo bila kujua anaanza kumpa wakati mgumu Vivian ambaye akinywa pombe hususan Reds huwa mwepesi kushinda maharage ya Mbeya.



    Hali ya Vivian ilianza kubadilika lakini alijisitiri sana asionekane kama ni dhaifu kwa kiasi hicho na pia hakuwaza kutoa penzi kwa wepesi namna hiyo ingawa Bigambo ni mwanaume wake wa siku nyingi. Kiasili, Vivian alikuwa na nyodo nyiye acheni tu. Hata huo uchangamfu aliouonesha kwa Bigambo ulitokana na ukweli kwamba jamaa alikuwa anamjulia vya kutosha.



    “Kwa hiyo wewe Bigambo ni tofauti kabisa na wanaume wengi ambao hujijali wenyewe tu? Lakini mbona inakuwa hivyo?” Vivian aliuliza swali ambalo lilikuwa wazi kabisa kwa maana ya jibu lake. Kufikia hapo, hali ya Vivian ilizidi kuwa mbaya, alianza kumtazama Bigambo kwa macho yenye kulegea kama mpishi aliyezidiwa na moshi wa kuni mbichi.



    “Kabisa, tena kuna wakati huwa najikuta naongeza na utaalam ambao nikiambiwa nirudie siwezi kabisa, yote hayo ni kuhakikisha najitoa ufahamu kwenye sita kwa sita, hapo sasa nitagusa na maeneo ambayo wanawake wengi huwa hawaguswi mara kwa mara,” alisema Bigambo na kuendelea;



    “Unajua kuna wanawake hawajawahi kupata raha ya tendo, ukiwaaambia habari za kufika mwisho wa safari hawajui inazungumzia nini na wao wanakuambia wanafurahia mapenzi na waume zao, lakini kifupi ni kwamba hakuna mwanamke ambaye hana uwezo wa kufika mwisho wa safari, mwanamke yeyote ni maandalizi, akipata mwandaaji mzuri kabla ya mechi, ni lazima afike ukingoni tena kwa shangwe na makelele ya fujo kama siyo nderemo,” alisema Bigambo huku akisukumizia maneno hayo na glasi ya nyagi kabla hajakunja sura yake yenye mikunjo mingi kadhaa.



    “Wewe B wewe jamani,” Vivian alisema na kuiweka mezani kabisa chupa ya Reds aliyokuwa ameishika mkononi, licha ya kwamba kabla hajaanza kunywa alikuwa mzima wa afya njema, awamu hii alianza kuhisi kama kuna kibaridi cha homa kali kinachoashiria malaria.



    “Sasa kwa hiyo unaweza kumtibu mwanamke ambaye ana tatizo la kutofika mwisho wa safari yake?” Vivian aliuliza lakini awamu hii alishindwa kujizuia na kuuweka mkono wa kulia begani kwa Bigambo na kisha kumnong’oneza masikioni kwamba wakachukue chumba tayari kwa mazungumzo binafsi zaidi, jambo ambalo lilitoa jibu la moja kwa moja kwa Bigambo ni nini ambacho Vivian alikusudia, zaidi sana akashika glasi yenye kinywaji na kuisukumizia mdomoni.



    “Eee, sana tu, mimi nimetibu sana wanawake ambao shida yao ni kutofurahia na kufika mwisho wa safari, lakini nawatibu kwa vitendo bila kufanya nao kikwelikweli,” alisema Bigambo na kuifakamia tena glasi yake ya kinywaji na kisha kumtamza usoni Vivian ambaye alikuwa kimya.



    “Mmh,” Vivian aliishia kuguna na kuikamata chupa yake ya Reds.



    “Vipi, mbona unaguna?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mmm, kawaida tu,” alisema Vivian na kuuondoa mkono wake begani kwa Bigambo.



    “Nikuombe kitu?” Vivian alianzisha tena mazungumzo.



    “Sema tu Vivian.”



    “Aaah, usiniite hivyo bwana,” Vivian alisema lakini sauti yake ilitoka kwa tabu na dalili za uchovu kwani pua zake zilikuwa zinabana kama mgonjwa wa mafua yenye kuambatana na malaria. Siku zote akiwa ameweka mambo yake, huwa hapendi kabisa kuitwa kwa jina la Vivian na mpenzi wake Bigambo, zaidi sana alipendelea kuitwa kwa jina la mpenzi, au sweetheart na majina mengine yenye kuashiria mapenzi.



    Walinyanyuka na kwenda kuchukua chumba. Mikononi hawakuacha vinywaji vyao ambapo kila mmoja alikuwa na hamu ya kutafuna tende za mwenzake.



    “Okey, samahani,” Bigambo alijitetea baada ya kumuita Vivian kwa jina.



    “Bigambo nataka uwe mwanaume wangu wa kweli lakini huwezi amini nilikuwa na mawazo ya kuachana na wewe,” Vivian alisema na kumtazama tena usoni Bigambo lakini pia akawa kama anayesikilizia jibu ambalo hakujua lingetokaje kwa wakati huo. Tayari walishaingia chumbani na kukaa kitandani ambapo walisogeza meza iliyokuwa chumbani humo na kuweka vinywaji vyao.



    Hata hivyo, kabla Bigambo hajasema chochote kutokana na kauli ya Vivian alimimina tena nyagi kwenye glasi na kuipiga yote kabla ya kumimina tena na kuiweka mezani bila kuinywa na hapohapo akanyanyuka kidogo na kukiweka sawa ambapo sasa aligeukiana na Vivian, alimtazama usoni na wote wakawa wametazamana bila kupepesa macho na Bigambo akapanua mdomo kama anayetaka kuuliza kitu kwa staili ya kipekee.



    “Sawa, tuendelee kuwa kwenye mahusiano na mimi kukufurahisha wewe ni sehemu ya kazi yangu,” Bigambo alisema huku akikamata glasi na kujimiminia kwa kasi huku akikunja ndita, uchungu wa nyagi uliendelea kulipa kazi ya ziada koromeo lake.



    Vivian alikaa kimya kwa muda. Kabla hajasema lolote, alikamata chupa ya Reds na kujimiminia kama alivyofanya Bigambo. Walikaa kimya kwa muda kabla ya kuendelea na mazungumzo.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kuona kama Bigambo anamchelewesha, Vivian alimsogelea na kuanza kumpa uchokozi wa wazi kabisa ulioashiria kwamba anataka dozi ya maana kwa wakati huo na siyo maneno mengi kama ilivyokuwa wakati wakiwa nje.



    “Baby,” Vivian aliita kwa sauti kavu lakini yenye kuelemewa na mahaba mazito sana.



    “Mmmh,” Bigambo aliitika lakini kabla hajafanya chochote alishangaa kumuona Vivian akichukua nguo na kuanza kuvaa huku akitokwa na machozi.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog