Search This Blog

Monday, October 24, 2022

KANGA MOJA KIUNONI...MBENGEMBENGE - 4

 







    Chombezo : Kanga Moja Kiunoni...Mbengembenge

    Sehemu Ya Nne (4)



    ILIPOISHIA I: Mara mlango wa mama Mei uligongwa kwa upole sana. Ilionekana mgongaji hakutaka kusikika na mtu mwingine... “Ngo ngo ngo ngo...” TAMBAA NAYO MWENYEWE... “Mh! Nani tena huyo?” aliuliza mama Mei akiwa ameegemea kifua cha mzee Hewa... “Kwani anagonga mlango gani?” mzee Hewa naye aliuliza... “Kwangu...” “Subiri niende nikamchungulie,” alisema mzee Hewa huku akitoka kitandani... “Uwe makini sana baby,” alisema mama Mei huku akiwa na wasiwasi mkubwa kwamba ni nani ingawa alijua si mume wake. Mzee Hewa alikwenda kusimama mlangoni kisha akachungulia nje kupitia tundu la funguo. Aliweza

    kumwona mtu aliyesimama kwenye mlango mkubwa wa kuingia ndani kwa mama Mei. Ni mwanaume lakini alionekana kwa tabu. Ilibidi mzee huyo atege macho vizuri ili aweze kumuona sawasa... “Haa! Si Mfaume yule?” alijihoji mzee huyo. Mfaume ni yule mpangaji aliyeshuhudia Jombi akiingia na kutoka asubuhi. Sasa alikuwa anataka nini kwa mama Mei labda ndiyo swali kuu lakini pia je, hakwenda kazini kwani? Hilo nalo lilikuwa swali la msingi... “Anataka nini kwa mama Mei?” alijiuliza mzee Hewa. Alirudi chumbani mbio... “Vipi, ni nani?” mama Mei aliwahi kumuuliza... “Mfaume...” “Mfaume! Ana shida gani na mimi?” “Sijui, mimi ndiyo nikuulize wewe,” alisema mzee Hewa akionesha kushangaa sana. Mama Mei alitaka kutoka kitandani, lakini mzee huyo akamzuia... “Sasa unataka kwenda wapi?” “Nataka nikahakikishe...” “Utahakikishaje?” “Si nitamchungulia.” Mama Mei alikwenda hadi sebuleni, akachungulia na kweli alimwona Mfaume amesimama bado mlangoni pake na anaendelea kugonga mlango

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wake kwa umakini sana. Alirudi chumbani kwa mzee Hewa... “Sasa huyu anataka nini?” aliuliza... “Mimi sijui, unajua wewe,” alisema mzee Hewa akiwa amelala kitandani. Mama Mei alifikia kukaa tu akiwa amepoteza muwashawasha wa kuwepo kitandani na mwaume huyo. Alifikiri mengi lakini alikosa majibu ya wazi. Ilifika mahali alitamani angekuwa ndani kwake ili atoke amsikilize lakini ilikuwa haiwezekani tena kutoka, angepita wapi! “Njoo basi mrembo,” mzee Hewa alisema huku akimshika mkono mama Mei na kumvutia kwake. Mama Mei alielekea kwa shingo upande maana mawazo hayakuwa pale. Mzee Hewa kwa ubishi hivyohivyo, alimshikashika mwanamke huyo huku akimbusubusu kiaina sehemu mbalimbali za mwili kwa lengo la kumuweka sawa waanze mchezo. Mama Mei alitekwa na ujanja wa mzee huyo, alisahau kabisa kama Mfaume amesimama mlangoni kwake akigonga, akalegea kwa mzee Hewa, shughuli ikaanza, wakaingia uwanjani. Mzee Hewa licha ya uzee wake bwana, alitumia uwezo wa akiba kummudu mama Mei. Alikumbuka mapozi mbalimbali na kumshirikisha ambapo mwanamke huyo alishangaa kupata kitu roho yake inapenda! Kelele zilikuwa nyingi akimkubali mzee Hewa na mambo yake yote huku lakini akimsisitiza kutoanika siri za penzi lao kwa mtu yeyote na

    kumuahidi kumlindia penzi kwamba, hakuna mwingine atakayelipata zaidi ya mume wake, baba Mei tu. Kwa upande wake, mzee Hewa kwa vile alijua kwamba alikoshwa na wowowo na umbo zima la mama Mei alikuwa akicheza huku akimwangalia kama mtafiti wa wanyama anavyokagua ili kupata tiba sahihi. Wakati wa kumaliza shoo, wote walipoteza akili na kuweweseka japo walijitahidi sana kuhakikisha sauti zao hazitoki ndani ya chumba walichokuwemo mpaka wote wakanyoosha mikono na miguu kwa pamoja..! Sasa walichoka, wakawa wamelala kwa mapumziko huku mama Mei akiwa na uso wa aibuaibu ya mbali maana walitoka kwenye tukio la historia. Mzee Hewa alijiona ni mshindi si wa mechi za mchangani, bali ligi kuu kabisa. *** Mama Mei na mzee Hewa walisimama mlangoni wakiangalia uwezekano wa kutoka kwani aliyekuwa akigonga mlango alikuwa kama ameondoka mlangoni hapo... “Ngoja nitoke mimi halafu wewe utafuatia ili nikaangalie mazingira kwanza,” alisema mzee Hewa...



    “POA.” Mzee Hewa alifungua mlango, akatoka kwenda chooni kisha akaenda mpaka nje, mbele ya nyumba yake hiyo, kote akaona kuko kimya, hakukuwa na dalili yoyote ya watu kuwepo eneo hilo. Hata nyumba za majirani pia zilipoa. Akapita mlango kwa mlango ndani kwake kuhakiki kama kuna mpangaji yumo ndani. Akafika kwenye mlango wa kuingia kwa Mfaume, akaona pia umefungwa tena na funguo, akarudi ndani kwake... “Toka haraka sana, hayupo wala hakuna mtu,” alimwambia mama Mei, naye alitoka. Aliingia ndani kwake, akafunga mlango na kwenda chumbani kulala. Alilala kwa muda, alikuja kushtuka kusikia mlango  wake mkubwa ukigongwa tena kama ulivyogongwa akiwa ndani kwa mzee Hewa... “Huyo sasa, acha nikamsikilize,” alisema mama Mei huku akitoka kitandani. Aliamini kuwa, aliyegonga ni Mfaume. Yeye dukuduku lake kubwa ni kutaka kujua, alikuwa ana shida gani... “Mambo?” alisalimia Mfaume baada ya mama Mei kufungua mlango na kusimama akiwa

    ameushikilia kwa juu... “Poa...karibu,” alisema mama Mei... “Asante sana...nataka kuongea na wewe...” “Kuhusu nini?” “Mambo fulanifulani...” Kama yapi?” “We niambie uko tayari au la!” “Mh!” aliguna mama Mei, kwani kusema hayuko tayari ni balaa maana hakujua Mfaume alikuwa na mazungumzo gani, akaona afadhali ayasikie kwanza... “Nipo tayari,” alisema mama Mei na kusikilizia... “Naomba tukae basi,” alisema Mfaume... “Wapi?” “Popote pale...” “Karibu,” mama Mei alimkaribisha sebuleni kwake. Aliona ni afadhali akae sebuleni kwake kama mgeni... “Pita tu,” alisisitiza karibu yake mama Mei. Baada tu ya kukaa, Mfaume akaanza kusema... “Anti mimi najua wewe ni mke wa mtu, nawe wajijua pia...” “Najijua ndiyo, vipi?” “Oke...vizuri sanasana...lakini mimi kuna jambo limeniumiza sana nikasema lazima nikwambie ulijue...”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    “Jambo gani hilo anko?” “Usiku wa kuamkia leo nani aliingia ndani kwako..?” “Hakuna aliyeingia...” “Anti usinidanganye, mimi ni mtu mzima...kijana mmoja wa mtaani, namjua vizuri sana, aliingia kwako. Nilimwona na ametoka saa kumi na moja alfajiri, pia nilimwona, unataka kukataa nini?” Mama Mei nusura presha impande, kwani aliyoambiwa ni ukweli...ukweli mtupu! Na alijua kama mume wake atakuja kuambiwa, ataamini kutokana na kumwonamwona Jombi nje ya nyumba hiyo. Kwa hiyo ataunga... “Mh! Anko sikia nikwambie... huenda ulifanya utafiti wa kutosha sana...ni kweli, siwezi kukataa. Kweli yule mtu alikuja ndani kwangu akaondoka muda huo, lakini si jamaa yangu...” “Jamaa wa nani sasa?” “Alikuja kuomba hifadhi ya kulala tu...” “Ni ndugu yako?” “Ndiyo...” “Baba Mei anamjua?” “Sina hakika,” alijibu mama Mei, jibu ambalo alijua lilimkera sana Mfaume kwani ukweli anaujua... “Kwa hiyo yule kijana alikuja kuomba hifadhi kwako licha ya kwamba ana kwake kule mbele?” aliuliza Mfaume akijifanya anamjua hata kwa sura kijana huyo kumbe alibahatisha tu... Maneno hayo ya Mfaume yakampa mwanga mpya mama Mei, alijua hana namna ya KUKIMBIA UKWELI huo ambao uliwekwa kama kivuli kwake



     kwake... “Nisamehe sana anko, naomba hilo liweke moyoni mwako. Namjua mume wangu...” “Kwa hiyo ni jamaa yako na si nduguyo?” “Ndiyo,” alijibu mama Mei kisha akaangalia chini kwa aibu ya kike, ya usaliti ilhali yeye ni mke wa mtu... “Da! Sasa anti, mimi kawaida yagu siwezi kukaa na dukuduku moyoni...itakuaje? Maana msema ukweli ni mpenzi wa Mungu, lazima nitamwambia mume wako, baba Mei. Mama Mei alishuka chini, akapiga magoti kwenye kapeti na kumwomba sana Mfaume... “Please anko, nifichie siri hiyo, naomba sana niko chini ya miguu yako, nitaachika mimi,” alisema akilia mama Mei. Mfaume alimkazia macho huku akimeza mate ya mahaba kwa namna ambavyo, mama Mei alikuwa akionekana muda huo. Mzigo ulikuwa mzigo kwelikweli, kiuno kiuno kwelikweli, paja paja paja hasa! Si mchezo..! “Utanipa zawadi gani ili nikutunzie siri hii?” aliuliza Mfaume kwa sauti ya kukoroma huku akilegeza macho...





    MAMA Mei alishtuka, akamwangalia kwa uso wa hamaki... “Anko, yaani kunitunzia siri hii tu unataka zawadi jamani?! Haya niambie wewe unataka zawadi gani?” “Mimi nimetokea kukupenda sana anti, hiyo ndiyo zawadi yangu pekee kwako,” alisema Mfaume akiangalia pembeni kwa aibu kwani kwa mwanamke kama mama Mei kumwambia nakupenda huku unamkazia macho ilihitaji uso wa kuchunwa! “Sasa na mimi nisemeje hapo? Sijajua,” alisema mama Mei huku akionekana kukasirikia tukio lile... “Ujibu, si umeshajua nina maana gani anti?” “Wala mimi sijajua maana yako...” “Sikia anti, nimesema nipe zawadi ili nikutunzie siri...sasa zawadi ninayoitaka mimi, nakupenda. Kwa hiyo naomba kuwa na wewe japo kwa siku moja tu, basi,” alisema Mfaume akijifanya ana uso wa mbuzi, hana aibu, anampa mtu shua... “Mh! Wapi! Siwezi kuwa na wewe hata kwa nusu siku mwenzangu... wewe kama unataka umwambie tu mume wangu, litakalotokea na litokee na kama ni kuachika niachike kwani naamini mimi sitakuwa wa kwanza kuachika hapa chini ya jua,” alibwabwaja mama Mei... “Haya, nashukuru sana,” alisema Mfaume akisimama na kutoka. Alitoka kwa uangalifu mpaka ndani kwake, akafikia kukaa kwenye kochi kubwa, akajilaza na kuanza kumfikiria mwanamke huyo, kwamba anapata wapi ujasiri wa kumwambia maneno kama yale kwamba, yu tayari kuachika... “Ina maana mimi sina sifa ya kuwa na yeye ila yule jamaa aliyemuingiza... “Lakini pia, ina maana ni mwanamke wa aina gani katika kizazi hiki ambaye haogopi ndoa, haogopi mwanaume, amuogopi mume wake?” alijiuliza Mfaume na kukosa raha. Moyoni alijiuliza, akirudi mume wake amwambie asimwambie? *** Jombi, akiwa kwenye shughuli zake, alimkumbuka mama Mei na jinsi alivyojidhalilisha mbele yake, akaamua kumpigia simu ili eti amwombe msamaha... “Halo,” alipokea mama Mei... “Vipi mzima mama?” alisalimia Jombi... “Mzima ndiyo, unasemaje?” “Nataka kukuomba msamaha kwa yaliyoto...” simu ikakatwa... “Daa!” aliumia Jombi baada ya kukatiwa simu, akajua imetoka hiyo, ikirudi ni pacha! Mama Mei alisonya mwenyewe kisha akasema moyoni...

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mimi sina haja ya wanaume suruali. Mwanaume unafika kitandani unalala kama mzoga bwana...lo!” Aliachana na huyo na kuanza kumuwaza Mfaume. Alikumbuka maneno waliyozungumza wakiwa wote sebuleni pale... “Ujibu, si umeshajua nina maana gani anti?” “Wala mimi sijajua maana yako...” “Sikia anti, nimesema nipe zawadi ili nikutunzie siri...sasa zawadi ninayoitaka mimi, nakupenda. Kwa hiyo naomba kuwa na wewe japo kwa siku moja tu, basi...” “Mh! Wapi! Siwezi kuwa na wewe hata kwa nusu siku mwenzangu... wewe kama unataka umwambie tu mume wangu, litakalotokea na litokee na kama ni kuachika niachike kwani naamini mimi sitakuwa wa kwanza kuachika hapa chini ya jua...”  “Haya, nashukuru sana...” “Potelea mbali, aseme asiseme atajua mwenyewe. Kwani ana ushahidi gani kwamba kuna mwanaume aliingia na kutoka ndani kwangu?” mama Mei alijipa moyo. *** Siku ile ilipita, muda mwingi mama Mei alikuwa ndani kwake, kwani kuna kila kitu, choo, bafu, stoo na vikorokoro vingine. Jioni ya siku hiyo, mumewe alimpigia simu na mazungumzo yao yalikuwa hivi... “Halo sweet...” “Mzima mama Mei..?” “Mi mzima baby, vipi wewe huko?” “Mzima...aa natarajia kuondoka huku kesho asubuhi, nitafika huko Dar usiku...” “Ah! Sawa darling, lakini nimekumisi kweli mwenzio...” “Ee! Sawasawa...poa basi,” alisema baba Mei na kukata simu. Mama Mei alianza kutetemeka, kwani mazungumzo ya mume wake yaliashiria kwamba, hakuwa sawa... “Kuna kitu, kwa vyovyote vile... baba Mei hawezi kuongea na mimi halafu asitumie jina la upendo...halafu namwambia nimemmsi anasema sawasawa badala ya kusema na mimi pia baby, lazima kuna jambo... “Au Mfaume ana namba yake ameamua kumwambia akiwa hukohuko Kenya?” aliwaza moyoni mama Mei, akakosa raha kabisa. Alijiongeza kwa mawazo mengi mpaka basi. Ilikuwa saa moja juu ya alama usiku, mama Mei akajitanda kanga juu na chini, akatoka kwa umakini hadi kwenye mlango mkubwa wa Mafume, akaushika, akausukuma, ukafunguka, akaingia na kumkuta Mfaume amakaa sebuleni kwake akiangalia tivii... “Karibu sana anti,” Mfaume alikaribisha kwa sauti ya chini ya kuibia wengine wasisikie...



    “ASANTE sana anko, nimekuja nina shida na wewe,” alisema mama Mei akikaa huku akimwangalia Mfaume kwa sura ya aibu. Baada ya mama Mei kukaa, ukimya mdogo ulipita, hakuna aliyeongea na mwenzake, matokeo yake kila mmoja alionekana anawaza jambo fulani. Mfaume alijua amefuatwa kutukanwa tena, ila aliondoa mawazo hayo baada ya kuiona sura ya mwanamke huyo umechangamka sana... “Anko,” mama Mei alianza kwa kuita... “Naam, niambie anti nakusikiliza.” Mama Mei kabla hajasema, alipeleka kidole kimoja kinywani na kung’ata kucha mara kadhaa huku akitema vipande ambavyo hata hivyo, havikuwepo..! “Unajua nimewaza sana...” “Kuhusu nini anti..?” “Kuhusu maneno yako kwamba, utamwambia mume wangu akirudi...” “Anhe, kwa hiyo?” “Mimi nimewaza sana, nimeona hakuna sababu ya kuharibiana maisha, nimekubaliana na wewe,” alisema mama Mei huku akimwangalia Mfaume kwa jicho la kuibia...

    “Kwa hiyo inakuaje sasa?” “Nakusikiliza wewe,” mama Mei alijibu. Mfaume alihisi anataniwa, hakuamini machoni pake. Alimwangalia tena mama Mei huku akijishikashika vidole vyake... “Mimi kusema kweli nimetokea kukupenda sana mama Mei, we hujui tu. Naumia kila siku ya Mungu ninapokuona na ninapokusikia sauti yako, ndiyo maana nikaweza kumwona yule kijana akitoka,” alisema Mfaume kwa sauti ya chini sana... “Mh! Kweli hata mimi nakupenda sana jamani, lakini naomba unitunzie siri asijue mtu mwingine yeyote yule.” Mfaume alimshika mama Mei, akamsimamisha, akamwingiza chumbani kwake huku akifumbafumba macho ya mahaba... “Umefunga chumbani kwako?” aliuliza Mfaume... “Ndiyo.” “Oke, ngoja na mimi sasa nikafunge mlango mkubwa,” alisema Mfaume akitoka. Usiku huo alikuwa ndani ya bukta tu. Mfaume aliufunga mlango huku mate yakimtoka. Alikuwa haamini kama kweli mama Mei amemkubalia...

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Daa! Leo hakuna kulala,” alisema moyoni huku akienda chumbani. Kwa upande wake, mama Mei yeye alichanganyikiwa. Alijua piga ua galagaza, kwa uamuzi wake kichwani asingekubali kumpa penzi Mfaume kwa jinsi anavyomjua yeye... “Da! Ni kwa nini ninapopenda hapawi sawa, ila nisipopenda. Kama mzee Hewa, yule ni kama alinibaka tu. huyu naye anatumia mwanya wa usaliti wangu ili anipate. Jombi ambaye nilikuwa na ridhaa naye, ndiyo hivyo tena, mwanaume suruali.” Mara, Mfaume aliingia huku akiachia tabasamu gumu ile mbaya... “Vipi anti, uko poa?” Mfaume alimuuliza... “Niko poa sana jamani,” alijibu mama Mei akiwa amejilaza kitandani tayari kwa mpambano ambao aliufuata mwenyewe uwanja wa ugenini. Mfaume alipanda kitandani kwani alishaoga, akalala upande wake. Bado moyo wake ulikuwa huamini kama kweli, pale kitandani alikuwa na mama Mei... “Mama Mei,” aliita Mfaume kwa sauti yenye kukwaruza sana... “Abee,” mama Mei aliitikia kwa sauti tamu, sauti ya kike, sauti yenye mvuto kwa mwanaume yeyote yule awe rijali au la! “Nakupenda sana “Hata mimi nakupenda sana.” Mfaume alipata nguvu, akamgeukia mama Mei na kumkumbatia, naye akakumbatiwa. Walishikana, wakahamasishana na kupeana joto la mahaba, mwishowe wakaingia kwenye uwanja kusakata mpira. Ilikuwa shughuli nzito, ilikuwa kazi sana. Mama Mei licha ya moyoni mwake kutokuwa tayari lakini hakuweza kuonesha kwamba hakuwa tayari, kwani ushirikiano wake ulikuwa wa asilimia mia moja huku akisema maneno mazuri ya mahaba kwa mwanaume huyo. Hali hiyo ilipandisha munkari kwa kila mmoja na kusababisha wote kuzama sawasawa kwenye mahaba mazito. Mfaume muda mwingi alikuwa akimwangalia mwanamke huyo kwa staili ya kumkagua kwa undani na umakini wa hali ya juu... “Anko...anko...anko,” aliita mama Mei kwa sauti iliyojaa haraka kama vile kuna jambo baya amelisikia au amelijua wakati huo wakiwa badi wanaendelea kucheza... “Mmm...mmm,” aliitikia Mfaume kwa sauti nzito ya kiume akisubiri kuambiwa alichoitiwa kwa haraka kiasi kile



    “UTANIACHA ANKO?” eti ndiyo lilikuwa swali la mama Mei... “Wewe tu anti...” “Mimi sitaki uniache,” alisema mama Mei akitoka kwenye kushinikizwa na kuwa hiari yake sasa na upendo juu. Sijui alikumbana na kitu gani kutoka kwenye mchezo wa Mfaume mpaka akaanza kubembeleza mahaba kiasi cha kuomba kujua kama ataachwa... “Sikuachi anti.” Mfaume akawa kama amechochewa sasa, alikimbiza ile mbaya mpaka mama Mei akawa anaguna tu na kusemasema maneno yake, alikuwa hoi, aliishiwa nguvu katika mchezo huo, akahisi ameingia katika maisha mengine mapya tofauti na aliyoyazoea kwenye eneo la mahaba. Walinyamaza, wakawa wanahangaika kila mmoja akiisakanya furaha yake ilipo mpaka ikafika mahali, mama Mei akajitoa kama anayesema liwalo na liwe, kwani mume ni kitu gani bwana! Wangapi wana waume zao lakini hawajatulia! Kwa Mfaume, ilikuwa ni historia nyingine kabisa kwani aliamini bahati ya kumpata mwanamke kama mama Mei, hasa kutokana na uzuri wake wa sura na umbo ni sawasawa na kufanikiwa kumpata malkia wa nchi yenye neema katika zama za dunia ya zamani zile. Chumba walichokuwemo, kwa upande wa dirisha, liliangalia eneo ambalo hakuna mtu aliyekuwa akiweza kupita, kwa hiyo kelele zozote zile, hakuna aliyekuwa na uwezo wa kuzisikia. Lakini mama Mei aliuliza kwanza kabla ya kuanza kuimba... “Baby kuna watu nje ya dirisha huko hawawezi kutusikia?” “Hakuna, kuna uchochoro hautumiwi, upande  wa pili ni godauni la mahindi,” alisema Mfaume kwa tabutabu kwani alikuwa kazini wakati huo. Kusikia vile, mama Mei alijichia kama mtu anayefukuza ndege kwenye shamba la mpunga, kila mara kelele, mara aende kona ile, mara arudi huku. Ikafika mahali akaachia ishara moja kwamba amemaliza safari yake ya upendo kwa mwanaume huyo, akapokelewa, wakapokeleana. Dakika nne nzima hakuna aliyekuwa akisema kitu, kila mmoja alikuwa akihema kwa kasi ya mchoko. Shughuli ilikuwa pevu

    sana. Mwishowe, ndiyo mama Mei akasema... “Asante sana baby, nimeinjoi, sijui wewe.” “Hata mimi pia sweet, nakushukuru sana. Nimefarijika sana kuwa na wewe, kwangu ni kama nimeota ndoto kwamba nimekuwa tajiri wakati ni maskini lakini baada ya kuamka nikakuta ni tajiri kweli,” alisema Mfaume huku akimshikashika mwanamke huyo sehemu mbalimbali za mwili wake... “Lakini nakuomba sana anko, usije ukaitoa siri hii kwa watu. Wa kujua anatakiwa kuwa wewe na mimi tu. Usirogwe hata siku moja, ukamwambia mzee mwenye nyumba,” aliomba sana mama Mei akiwa anamchezea kifua Mfaume.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haitatokea,” alijibu kwa kifupi Mfaume. Kwa mama Mei alijua mzee Hewa akipata habari, atapasuka na yake na lolote litaweza kutokea, hivyo akaona ni vyema akaziba mapema. Usiku huo, mama Mei ni kama alilala chumbani kwa Mfaume kwani baada ya mapumziko marefu, waliingia raundi nyingine na nyingine, hata walipopitiwa na usingizi, muda ulikuwa umekwenda na wakakoroma. Walishtuka saa kumi na moja na nusu alfajiri baada ya kusikia watu wakizungumzazungumza nje kwa sauti za haraka kuwahi makazini. Mfaume ndiye aliyemwamsha mama Mei ambaye aliamka, akatoka kitandani na kukaa kwanza. Mfaume alimshika mkono mpaka sebuleni, yeye akafungua mlango kuangalia mazingira kisha akamtoa alipoona kuko shwari. *** Kulipambazuka kabisa, jua lilianza kuchomoza, wapangaji wengine katika nyumba hiyo walianza kutoka nje, akiwemo mzee Hewa. Mama Mei tangu arudi kitandani kwake, hakuwahi kupata usingizi tena. Muda mwingi alijikuta akijiwazia mwenyewe na kujiona kama mjinga vile... “Sasa ina maana kwenye nyumba hii tu, nimeshatembea na wanaume wawili, mzee Hewa na Mfaume, ukimjumlisha na mume wangu, wanakuwa watatu, nyumba moja... “Mh! Huu sasa ni uhuni uliopitiliza. Kwa nini lakini? Inakuaje mpaka nafikia hatua hii mbaya,” aliwaza sana mama Mei akashindwa kupata majibu na kuamua kuamka kufanya mambo mengine. Akiwa ndani ya kanga moja na taulo kwa juu yake, mama Mei alitoka uani ambako alikutana na mzee mwenye nyumba, Hewa na mpangaji mwingine wakiwa wanazungumzia tukio la usiku, la mwizi kutimuliwa nyumba ya pili...



    HA! Kweli jamani?” aliuliza Mfaume aliyekuwa pembeni yao, maana yeye alikuwa ‘amepoteza fahamu’ baada ya kumaliza kazi na mama Mei. Mama Mei aliwasalimia huku akiwa mwenye aibu kubwa. Hata walipomsalimia, hakuwa mchangamfu. Maana hapo tayari, Mfaume anamfahamu kwa undani, mzee mweny

    nyumba pia... “Hujambo binti?” mzee mwenye nyumba alimsalimia... “Sijambo, shikamoo...” “Marhaba! Halafu usiku wa kuamkia leo nimegonga sana kwako, baadaye nikagundua hata funguo haipo ndani ya mlango, ulifungua ukatoka. Ikabidi nilale sebuleni kwangu kusikiliza labda umepata matatizo, nikakusikia asubuhi ukiingia, ulikuwa wapi?” aliuliza mzee Hewa bila kujali mazingira. Mama Mei alijiumauma kwa sana maana anajua muda huo alikuwa kwa Mfaume, sasa yeye ajibu nini na pale walikuwepo Mfaume na yeye mzee Hewa... “Mh! Labda sikusikia, mimi nikishafunga mlango nina tabia ya kuchomoa funguo naiweka mahali, kwani haitakiwi?” alijibu mama Mei na kuongeza na swali juu... “Ha! Mbaya sana binti... mbaya! Mtu akija na funguo yake malaya anaingiza, anafungua na kuingia ndani na wewe upo... “Faida za kuacha funguo kwenye mlango ni kwamba, atakayetaka kuingiza funguo zake zitakwama maana

    kutakuwa na funguo nyingine ndani.” “Ahaa! Basi nimejifunza,” alisema mama Mei huku akimwangalia Mfaume kwa macho ya kujiibaiba. Mama Mei alipitiliza hadi chooni, alipotoka alirudi ndani kwake na kukaa kitandani akijutia kwa kuwaza... “Yaani mimi ni mwanamke wa aina gani? Wanaume watatu kwenye nyumba moja wote nimelala nao, maana yake nini sasa? “Hivi nikiitwa maharage ya Mbeya au jamvi la wageni watakuwa wanakosea?” Mama Mei aliumia sana moyoni, lakini ilishatokea, akawa hana namna. Pia, kilichomuumiza kingine ni kubaini kuwa, kuachana na watu hao itakuwa ngumu sana. *** Ilikuwa saa kumi jioni, baba Mei aliingia nyumbani kwake na kulakiwa na mkewe kwa wao nyingi lakini zisizokuwa na nguvu kama inavyokuwa kawaida yake... “Vipi, za hapa mke wangu?” alisalimia baba Mei akipokewa mabegi...

    “Hapa salama tu, pole na safari mke wangu.” Baba Mei baada ya kupokelewa mabegi, aliingia moja kwa moja hadi chumbani na kukaa kitandani. Hali ikaanza kubadilika kwa mama Mei. “Vipi lakini, salama hapa!” aliuliza baba Mei huku akitaka kufungua vishikizo vya shati lake. Kabla hajajibiwa, mama Mei alijiinua taratibu pale kitandani na kumshika mkono baba Mei kwa maana ya kumsaidia kufungua vishikizo.” “Salama kabisa mume wangu,” alijibu mama Mei kwa sauti ya kimahaba. “Hivi mzee Hewa yupo?” aliuliza baba Mei kwa mshangao hali iliyomshtua mama Mei kwa dakika chake kisha akajibu. ”Yupo, aende wapi tena wakati ndiyo nyumba yake hii.” “Hajaulizia kodi yake?” alisema baba Mei kwa kutania. “Hajauliza jamani, mume wangu naomba nikakuandalie maji ya kuoga,” alisema mama Mei kisha akaondoka na kumuacha baba Mei akimalizia kubadilisha nguo. Muda wote huo hadi anatoka nje, akili ya mama Mei haikuwa sawa kabisa,

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

     mawazo yake yalikuwa yakifikiria ndani ya kipindi kifupi kutembea na wanaume wawili tena nyumba moja. “Sijui, maana Mfaume alivyoniambiaga kuwa akiwa na dukuduku lazima alitoe, ananitia wasiwasi kweli na ndoa yangu,” alijisemea mama Mei. Kitendo cha mama Mei kufika bafuni na kuweka ndoo, akakutana uso kwa uso na Mfaume akiwa anatokea chumbani kwake. “Mama Mei, mama Mei?” aliita Mfaume. Mama Mei alikaa kimya, alimsikia lakini hakutaka kupoteza muda wa kukaa naye kwa kuogopa huenda yakawa yaleyale. “Mama Mei jamani si nakuita,” aliendelea kuita Mfaume, safari hii alikuwa ameshamsogelea kwa ukaribu. Akamshika begani. “Mama Mei, unaonekana una mawazo sana, nini tena mpenzi nikusaidie,” alisema Mfaume kwa sauti legevu. “Shii! Ishia hapohapo, hivi hujui kama mume wangu amesharudi?” alisema mama Mei huku akiweka kanga yake vizuri na kuondoka. Mfaume alibaki akitoa macho na mdomo wazi huku akiangalia umbo lile la mama Mei, umbo alilolifaidi usiku kucha, hakumuamini hata kidogo maneno ya mama Mei kama kweli mumewe amesharudi. Je, nini kilitokea hapo?



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog